Simba wanaonesha utoto kwa Morrison na wachezaji wa kigeni

Simba wanaonesha utoto kwa Morrison na wachezaji wa kigeni

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Simba haionyeshi ukomavu kwenye soka hata baada ya kufikisha miaka zaidi ya 80 tangu kuanzishwa kwake.

Kila mtu waliwasikia viongozi wa Simba wakimuaga na kumtakia kheri Morrison huko aendako wakimaanisha kuwa aende mbele kwa mbele huko hata kabla ya msimu kumalizika kuonyesha kuwa hawana kazi nae tena.

Huu ni msimu wa usajili kwa wachezaji duniani kote hivyo Morrison alipaswa kupewa barua yake ili imsaidie kupata timu popote duniani.

Kitendo cha Simba kumnyima barua mchezaji ambae hawana kazi nae hata baada ya mchezaji kuiomba sio kitendo cha uungwana kwa Morrison aliyeitumikia Simba kwa mapenzi makubwa sana.

Kitendo hiki sio tu kwamba kitaipa Simba laana kubwa lakini kitawaohopesha na kiwatia hofu wachezaji wengine wa kigeni kwenye club ya Simba.

Uhasama wa Simba na Yanga usivuke viwango vya mpira. Mpira ni maisha ya wachezaji. Morrison asiposajiliwa hasara haiendi kwa Yanga bali kwa Morrison kwakuwa Yanga Ina wachezaji wengi wazuri kama au zaidi ya Morrison.

Hii itaitia Simba hasara, maana wachezaji wengi wa kigeni ipo siku Simba haitakuwa chaguo lao la kwanza kujiunga nayo.
 
Yani wewe una WENGE kweli kweli sijui umekula maharagwe ya wapi wewe..

Kanun zipo hivi... Timu ikimhitaji mchezaji inaandika barua kwa timu atokayo mchezaji then wakiridhiana kwenye terms mchezaji anapewa release leter anaondoka

Sasa kwa kuwa akili za mijitu ya yanga zimechakaa kama jengo lao wanalazimisha eti lazima smba wampe barua morisson

Narudia tena fuateni sheria waandikieni barua mabingwa mara nne "mfulilizo" waelezeni shida zenu za nyuma zitatatuliwa.

Kama Al-ahly walifanya hivyo kwa Luis, berkane walifanya hivyo kwa Chama, Tp mazembe walifanya hivyo kwa Sammata nyie vyura ni nani msifuate utaratibu pumbavvvvvv?
 
Yani wewe una WENGE kweli kweli sijui umekula maharagwe ya wapi wewe..

Kanun zipo hivi... Timu ikimhitaji mchezaji inaandika barua kwa timu atokayo mchezaji then wakiridhiana kwenye terms mchezaji anapewa release leter anaondoka...
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] umemkomeshaaa haswaaah.
 
wachezaji wa kigeni hawataiona SIMBA kama chaguo la kwanza maana mnajipaka matope WENYEWE ok ngoja tuone maana muda umesogezwa mbele na Morrison anajikia mshahara wake wa mwezi hadi mwezi wa nane
 
Huyo anajiita wakili msomi, ukimpa barua leo anawapeleka FIFA kudai malipo ya kuvunja mkataba.

Simba wakamatie hapohapo, haya majitu ya Africa magharibi mengi ni matapeli tu.

Siungi mkono Yanga kumchukuwa mchezaji asiyekuwa na nidhamu, huyo ni kama Baloteli muda wowote anakwenda kuigharimu timu.
 
Kama ikiwezekana huyo Morrison aendelee kuchezea kwenye timu yenu ya Makolo,aongezewe mkataba kabisa

Kwa kikosi tulichonacho kwasasa hata bila usajili tunajipigia tunavyotaka,tena kwa magoli ya kwenye video kabisa
 
Wewe kilaza kweli kweli, Morrison ni mchezaji wa Simba ndiyo maana anaendelea kulipwa mshahara hadi siku ya mwisho ya mkataba wake, kumpa barua hiyo nyie wapumbavu mnayodai tafsiri yake ni kuvunja mkataba. Ameambiwa timu inayomuhitaji iandike official letter ili wakae mezani wajadili nani atabeba gharama za kuvunja mkataba,haya ni mambo ya kisheria usiingize ushabiki oyaoya.

FB_IMG_1655579378566.jpg
 
Yani wewe una WENGE kweli kweli sijui umekula maharagwe ya wapi wewe..

Kanun zipo hivi... Timu ikimhitaji mchezaji inaandika barua kwa timu atokayo mchezaji then wakiridhiana kwenye terms mchezaji anapewa release leter anaondoka...
The fall of Simba has many colours!

mmefukuza kocha na wachezaji bado viongozi tu!

mwaka huu mnatukana sana kila comment kisa makombe yote ya bara yameenda Jangwani!! mfungaji bora mmekosa! kipa bora mmekosa, mchezaji bora mmekosa!!
 
... Morrison alipaswa kupewa barua yake ili imsaidie kupata timu popote duniani. Kitendo Cha Simba kumnyima barua mchezaji ambae hawana kazi nae hata baada ya mchezaji kuiomba sio kitendo Cha uungwana kwa Morrison aliyeitumikia Simba kwa mapenzi makubwa sana.
Kuna ishu za kisheria pia, inabidi usizichukulie poa. Unaweza ukampa barua ya kumuachia akaja kugeuza maneno kwamba umemvunjia mkataba, kwa hiyo umlipe mahela mengi mengi kadiri ya mkataba ulivyosema. Kumbuka kuwa Morrison ni wakili msomi 😁
 
Yani wewe una WENGE kweli kweli sijui umekula maharagwe ya wapi wewe....
mchezaji mmeshamtupia virago, mkataba wake umekwisha na msimu umekwisha, mpeni barua yake akahangaike huko aendako.

Ni sheria gani ya TFF/cecafa/caf/fifa inayokataza mchezaji aliyemaliza mkataba wake kupewa release letter yeye mwenyewe? Ndio maana mtapata taabu sana, maana hamkui, mmedumaa.
 
Huyo anajiita wakili msomi, ukimpa barua leo anawapeleka FIFA kudai malipo ya kuvunja mkataba...
Hiyo siyo kweli, kama shaka ndiyo hiyo basi Morrison angeambiwa aandike official letter ya kuomba kupewa release letter ili kuji commit na ushahidi kwamba yeye ndiye aliyekuwa initiator wa jambo hilo badala ya kusema timu yake ndiyo iombe hiyo barua.

Timu haiwezi kuomba release letter kwa mchezaji ambae mkataba wake umekwisha. Tunafahamu kuwa Simba imefilisika kifedha inataka ilipwe pesa na yanga kununua mkataba wa mwezi mmoja ipate pesa ya kufanya usajili. Inatia haibu walahi.
 
Et laana [emoji23][emoji23][emoji23]hapo kwanza ncheke.....laana atoe morison? Pole mtani
nimesikia wachezaji wazuri wote hawapendi kuja Simba, mmefilisika, mnataka kuuza mkataba wa Morrison wa siku 15 zilizobaki, shame on you. Hii ni sawa na mtu kufanya biashara ya kuuza maganda ya ndizi baada ya walaji kula ndizi na kutupa maganda.
 
Kama ikiwezekana huyo Morrison aendelee kuchezea kwenye timu yenu ya Makolo,aongezewe mkataba kabisa

Kwa kikosi tulichonacho kwasasa hata bila usajili tunajipigia tunavyotaka,tena kwa magoli ya kwenye video kabisa
Morrison sio kivileee kwa yanga ya sasa iliyochukua ubingwa kutoka kwa Simba yenye Morrison huyohuyo. Wanachofanya simba ni kumkomoa Morrison sio Yanga, yanga can do with or without Morrison.

Huu ni wakati wa usajili kwa vijana wapate riziki zao sio sawa kutaka kuuza mkataba wa siku 10 zilizobakia. Mnatia aibu kimataifa bila sababu ya maana.
 
The fall of Simba has many colours!

mmefukuza kocha na wachezaji bado viongozi tu!

mwaka huu mnatukana sana kila comment kisa makombe yote ya bara yameenda Jangwani!! mfungaji bora mmekosa! kipa bora mmekosa, mchezaji bora mmekosa!!
20b zimeyeyuka wanataka kuuza mkataba wa siku 10 kwa GSM. Wamesahau jasho na mchango wa Morrison kwao, wanaachana nae kihuni. Kumbukeni kuwa Morrison sio mchezaji mdogo Africa, caf na fifa wanamfahamu sana pia.
 
Simba haionyeshi ukomavu kwenye soka hata baada ya kufikisha miaka zaidi ya 80 tangu kuanzishwa kwake.

Kila mtu waliwasikia viongozi wa Simba wakimuaga na kumtakia kheri Morrison huko aendako wakimaanisha kuwa aende mbele kwa mbele huko hata kabla ya msimu kumalizika kuonyesha kuwa hawana kazi nae tena.

Huu ni msimu wa usajili kwa wachezaji duniani kote hivyo Morrison alipaswa kupewa barua yake ili imsaidie kupata timu popote duniani.

Kitendo cha Simba kumnyima barua mchezaji ambae hawana kazi nae hata baada ya mchezaji kuiomba sio kitendo cha uungwana kwa Morrison aliyeitumikia Simba kwa mapenzi makubwa sana.

Kitendo hiki sio tu kwamba kitaipa Simba laana kubwa lakini kitawaohopesha na kiwatia hofu wachezaji wengine wa kigeni kwenye club ya Simba.

Uhasama wa Simba na Yanga usivuke viwango vya mpira. Mpira ni maisha ya wachezaji. Morrison asiposajiliwa hasara haiendi kwa Yanga bali kwa Morrison kwakuwa Yanga Ina wachezaji wengi wazuri kama au zaidi ya Morrison.

Hii itaitia Simba hasara, maana wachezaji wengi wa kigeni ipo siku Simba haitakuwa chaguo lao la kwanza kujiunga nayo.
Hapa hoja siyo "utoto wa Simba" hapa hoja ni MKATABA! Hakuna ziada wala pungufu, hoja ni Mkataba. BM bado ana mkataba na SSC, hivyo wote - BM na SSC - lazima waendane na yalimo lkwenye Mkataba wao. Yeyote atakaye VUNJA huo Mkataba ni lazima AWAJIBIKE. SSC au BM hawawezi kufanya kosa hilo. Hivyo basi, cha kufanya ni kila upande kusubiri hadi mwisho wa Mkataba husika ili waachane vizuri.

SSC haiwezi kumpa BM hiyo barua, kufanya hivyo ni sawa na kuvunja Mkataba na BM na hivyo kuwajibika kumlipa BM mahela. Hili haliwezekani, vivyo kwa BM ambaye analijua sana hilo ndiyo maana anaomba SSC impe hiyo RELEASE LETTER kwa upole ili aende aendako badala ya kwenda huko aendako na kusaini nao Mkataba mpya kabla ya huu alionao SSC haujaisha. Akifanya hivyo, atawajibika kuwalipa SSC mihela kwa kuvunja Mkataba. Hilo BM hawezi kufanya, kwani anajua matokeo yake! Hivyo hapa hoja ni MKATABA! Siyo"utoto wa Simba".
 
Hapa hoja siyo "utoto wa Simba" hapa hoja ni MKATABA! Hakuna ziada wala pungufu, hoja ni Mkataba. BM bado ana mkataba na SSC, hivyo wote - BM na SSC - lazima waendane na yalimo lkwenye Mkataba wao. Yeyote atakaye VUNJA huo Mkataba ni lazima AWAJIBIKE. SSC au BM hawawezi kufanya kosa hilo. Hivyo basi, cha kufanya ni kila upande kusubiri hadi mwisho wa Mkataba husika ili waachane vizuri.

SSC haiwezi kumpa BM hiyo barua, kufanya hivyo ni sawa na kuvunja Mkataba na BM na hivyo kuwajibika kumlipa BM mahela. Hili haliwezekani, vivyo kwa BM ambaye analijua sana hilo ndiyo maana anaomba SSC impe hiyo RELEASE LETTER kwa upole ili aende aendako badala ya kwenda huko aendako na kusaini nao Mkataba mpya kabla ya huu alionao SSC haujaisha. Akifanya hivyo, atawajibika kuwalipa SSC mihela kwa kuvunja Mkataba. Hilo BM hawezi kufanya, kwani anajua matokeo yake! Hivyo hapa hoja ni MKATABA! Siyo"utoto wa Simba".
sio kweli, kama Morrison angekuwa anajiunga na timu ya Azam au namungo hadithi ingekuwa tofauti. Tunachosema sisi huku ni kusahau mchango wa morrison kizembe kabisa, lakini ni awaking call kwa wachezaji wenu wengine wa kigeni, maana wakati mwenzao Morrison akinyolewa wao wanajiandaa kwa kuweka maji nywele zao. Unajengea hofu wachezaji wenu bila sababu za msingi kabisa, maana Morrison ana marafiki wengi ndani ya wachezaji wa Simba waliobaki ambao hawapendi kuona Morrison anaharibiwa maisha na career yake kizembe hivyo.
 
Back
Top Bottom