Simba yampa mwaliko Rais wa CAF, Patrice Motsepe kuwa mgeni rasmi Simba Day 2022

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607

Klabu ya Simba imetuma maombi kwa Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Patrice Motsepe kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Simba Day ambapo wanatarajiwa kucheza dhidi ya Saint George ya Ethiopia, kwenye Uwanja wa Mkapa, Jumatatu Agosti 8, 2022.

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Wallace Karia amesema Simba walituma maombi hayo lakini bado hajajua majibu kutoka kwa kiongozi huyo wa soka la Afrika.

“Yanga wao watakuwa na kocha mkubwa Pitso Mosimane, Simba bado wanasubiri majibu ya Motsepe,” - Karia.
 
Hajafika bado hata hajathibitisha
 
Ni Jambo jema kwa mustakhabar wa soka la Tanzania
 
Haya ndo mambo tunayataka kusikia na kuona kwenye medani ya soka

Nadhani Simba SC imeamua kujitenga na wanasiasa kama awali
 
Huo ndiyo utofauti wa timu ndogo na timu kubwa.

We are Unstoppable 💪
 
Lkni hatuna uhakika wa jezi mpya.....

Kweli sisi Ni MAKOLO
 
Karia ni msanii tu, subiri Simba wenyewe wakishapata Jezi MPYA, watamtangaza Mgeni Rasmi...

Kassimu Majaliwa Huenda....
 
Mwaka jana alikuwa Spika wa Bunge, mwaka huu tumwalike Spika wa Bunge sababu wakiwa wageni rasmi uwa wanakirudi Bungeni akili zinakuwa fyatu wanajitumbua wenyewe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…