Simba yamuuza Cloutous Chama RS Berkane kwa Bilioni 1.5 na mshahara wake wapanda kwa 400%

Simba yamuuza Cloutous Chama RS Berkane kwa Bilioni 1.5 na mshahara wake wapanda kwa 400%

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Picha ikimuonyesha Clatous Chama na Tuisila Kisinda wakiwa katika jezi za mazoezi za RS Berkane muda mchache kabla ya kuanza mazoezi hiyo jana!

Picha kwa hisani ya majasusi wetu waliopo huko Morocco, wana Simba mjiandae kupokea tangazo la kuuzwa kwa Chama muda wowote kuanzia sasa!

Neno moja kwa Chama
=========

Kaimu Afisa habari wa Simba SC Ezekiel Kamwaga amethibitisha kuwa Kiungo wa kimataifa wa Zambia Cloutous Chama (30) amejiunga na Club ya RS Berkane ya Morocco akisaini mkataba wa miaka mitatu.

Chama amesaini mkataba huo unaotajwa kuwa umeigharimu RS Berkane ada ya uhamisho ya Tsh Bilioni 1.5 kwenda Simba SC na kuongezewa mshahara mara nne ya aliokuwa analipwa Simba SC.

Chama ambae ameonekana kwenye mazoezi ya RS Berkane akiwa na Tuisila Kisinda wa Yanga, alijiunga na Simba SC mwaka 2018 akitokea Lusaka Dynamos ya Zambia.

FEC319FE-7AF8-48E2-A918-3536179D4F75.jpeg
 
Back
Top Bottom