Simba yatangaza mkataba wa TSH Bilioni 26.1 kuanzia leo Agosti 1, 2022

Simba yatangaza mkataba wa TSH Bilioni 26.1 kuanzia leo Agosti 1, 2022


"Zile zama za kuwa na mkataba sare sare maua zimepita. Kwa miaka ya hivi karibuni Simba tumewekeza vya kutosha ili kuhakikisha brand yetu inakua,"- Meneja wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano, Ahmed Ally.

“Process ya mdhamini mpya tulianza tangu mwaka jana. Tumepokea boss nyingi za kutaka kuwa main sponsor, lakini M-Bet ndio wamekidhi vigezo vyetu vyote,” - CEO wa Simba, Barbara Gonzalez.

"Kwa ukubwa wa Simba ni lazima kujihusisha na kampuni ambayo inaongoza kwenye biashara ambayo wanafanya. Mkiangalia takwimu M-Bet wanaongoza kwa ukubwa Tanzania."- Barbara

"Hii ni mara ya kwanza mdhamini mkubwa anakuwa na senior team pekee, huko nyuma mdhamini mkuu alikuwa kwa timu zote lakini sasa timu zingine tunaweza kuzitafutia mdhamini wake,"- CEO

Mkurugenzi wa Masoko wa M-Bet, Allen Mushi ametaja mchanganuo wa udhamini mpya wa Klabu ya Simba:

Mwaka wa kwanza - Bil 4.670
Mwaka wa pili - Bil 4.925
Mwaka wa tatu - Bil 5.205
Mwaka wa nne - Bil 5.514
Mwaka wa tano - Bil 5.853
Jumla ni Bilioni 26, Milioni 168 na Tsh. 5,000.

=================================

TUJIKUMBUSHE MKATABA WA YANGA
Yanga SC ilisaini mkataba mpya wa Udhamini Mkuu na Kampuni ya kubashiri ya Sportpesa Tanzania, wenye thamani ya Tsh 12.3B kwa miaka mitatu (3), ambayo ni sawa na 4.1B kwa kila mwaka.

Mkataba huo ni ongezeko la Tsh bilioni 2 kwa mwaka kutoka kwenye mkataba awali wa bilioni moja kwa mwaka mmoja.



Pia soma:
Yanga FC yaingia mkataba mpya na SportsPesa wa miaka 3 wenye thamani ya Tsh Bilioni 12

Vipi zile 20B za Mo alishatoa? Maana na zenyewe ziliitwa nono
 
Mo alijichanganya sana kumleta huyu malaya wake Simba Sc
IMG-20220801-WA0007.jpg

Mkuu ebu changanya na zako hapo kidogo 😂
 
Ni kwasababu hujui kuwa kodi inakusanywa na hao TRA na kwamba kodi itakadiriwa kwa kuangalia vitu vingi(ikiwemo pesa kama hizi), au umeamua tu kutaka ligi ya mabishano mkuu?

Linapokuja swala la uwekezaji ambao upo wazi kitaifa ujue pua za TRA hazikosi, na kudanganya ni kazi unless iwe serikali yenyewe.

Kwahiyo kama unahisi Simba Sc aliingia mkataba wa 3B per year kama mlivyolishwa matango pori halafu katangaza 5B hadharani, ni kitu ambacho hakiwezi kutokea.
SIMBA ni KAMPUNI??? Umewahi kuona Financial statements za Simba Sports Club??
Kwako wewe hapo kodi itatozwa kwa nani?? Unadhani TRA wanasikiliza maneno badala ya ushahidi wa kimaandishi??

Sikia, TRA wao wataangalia Statements za pande zote mbili kwa M-Bet itaonekana kwenye Comprehensive Income upande wa Expenses kwa maana Advertisement expns na Simba as a Revenue (Sponsorship).

Mkataba wa Miaka 5 na Sheria ya kodi haitozi kodi kwa miaka kadhaa mbele, hutoza katika mwaka husika wa Kodi au Mkuu wangu umesahau hili leo??

Ukiangalia Mapato ya M-bet na matumizi yao maana yake watagenerate Loss katika miaka hii ya karibuni.

Financial Statements za M-bet haziko stable sana kiasi cha kumudu hizo gharama.

Nilichokuwa nawaza hapa ni kwamba ni ngumu mno kwa M-bet kuhandle huo mkataba, ni moja ya makampuni madogo hapa Tz pamoja na ukongwe wake.

Nakuomba tafuta vitabu vya mahesabu ya M-bet ndio utakuja kuelewa ninashosema hapa.
 
@CARDLESS anakwambia TRA hawahusiki kabisa hapo, mimi sitaki kuamini kama hajui ila ni katika hali ya kupanick( yeye kama shabiki wa utopolo)[emoji23]
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] Unanichafua kaka, nimeuliza wanahusika vipi hapa?? Ulipaswa kusema namna wanavyohusika hapa maana tunajua hakuna WITHHOLDING TAXES HAPO si ndio wajameni??

Kodi hatutozi kwa miaka kadhaa mbele bali kwa mwaka husika wa fedha [emoji2][emoji2][emoji2]

Naanza mdogo mdogo najua tutakubalia huko mbele, uzuri nakujua. [emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
 
Inaonekana watu wanaliwa vibaya sana hizo pesa ni mingi sana.
Hivi hakuna sheria zinazoyabana makampuni ya betting kutoa Audited and Detailed Financial statements kila mwaka?
Ikiwekwa hii sheria tutajua mbivu na mbichi inaonekana Market share ni kubwa sana
Medieval mindset


Mmekaa kubana Bana watu Tu
 
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] Unanichafua kaka, nimeuliza wanahusika vipi hapa?? Ulipaswa kusema namna wanavyohusika hapa maana tunajua hakuna WITHHOLDING TAXES HAPO si ndio wajameni??

Kodi hatutozi kwa miaka kadhaa mbele bali kwa mwaka husika wa fedha [emoji2][emoji2][emoji2]

Naanza mdogo mdogo najua tutakubalia huko mbele, uzuri nakujua. [emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
Ni kweli mkuu, kodi hatutozi kwa miaka kadhaa mbele bali ni kwa mwaka husika wa fedha ndiomaana hata hizo 26B hazotolewi kwa mkupuo bali kwa kipindi (kila mwaka).
 
SIMBA ni KAMPUNI??? Umewahi kuona Financial statements za Simba Sports Club??
Kwako wewe hapo kodi itatozwa kwa nani?? Unadhani TRA wanasikiliza maneno badala ya ushahidi wa kimaandishi??

Sikia, TRA wao wataangalia Statements za pande zote mbili kwa M-Bet itaonekana kwenye Comprehensive Income upande wa Expenses kwa maana Advertisement expns na Simba as a Revenue (Sponsorship).

Mkataba wa Miaka 5 na Sheria ya kodi haitozi kodi kwa miaka kadhaa mbele, hutoza katika mwaka husika wa Kodi au Mkuu wangu umesahau hili leo??

Ukiangalia Mapato ya M-bet na matumizi yao maana yake watagenerate Loss katika miaka hii ya karibuni.

Financial Statements za M-bet haziko stable sana kiasi cha kumudu hizo gharama.

Nilichokuwa nawaza hapa ni kwamba ni ngumu mno kwa M-bet kuhandle huo mkataba, ni moja ya makampuni madogo hapa Tz pamoja na ukongwe wake.

Nakuomba tafuta vitabu vya mahesabu ya M-bet ndio utakuja kuelewa ninashosema hapa.
Kumaanisha kodi huwa inatozwa na TRA kwa makampini pekee?

Sitaki kujibu hoja nyingine yoyote katika hiyo comment yako, acha nikomae na hapa.
 
Ni kweli mkuu, kodi hatutozi kwa miaka kadhaa mbele bali ni kwa mwaka husika wa fedha ndiomaana hata hizo 26B hazotolewi kwa mkupuo bali kwa kipindi (kila mwaka).
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] haya sasa twende mbele kidogo, eeh TRA wanasikiliza porojo au detailed documents???
 
Back
Top Bottom