Simba yatangaza mkataba wa TSH Bilioni 26.1 kuanzia leo Agosti 1, 2022

Simba yatangaza mkataba wa TSH Bilioni 26.1 kuanzia leo Agosti 1, 2022

TUNATAKA TUCHANGANYE NA HIZI 26 ZA M BET ILI TUENDESHEE CLUB YETU
Utaolewa bila mahari. Yaani Club yenu unataka wanaume wengine ndo wakuchangie? Kesho ukipata Ujauzito utamlalamikia nani kama unapenda kuchangiwa?😂
 
Wrong move, na kama TMO hukustahili kuwa afisa hata kidogo.

Sadaka haitozwi kodi popote pale, rudi kasome upya sheria au omba aindikwe kwa kiswahili labda utaelewa.

Sheria inakutaka kusubmit vitabu vya hesabu, na sio kukutoza kodi. Vitabu vya hesabu vitaonesha shughuli zako unazofanya ambapo huwezi tozwa Corporate tax hata kidogo.

NGOs wachopaswa kilipa ni PAYE na labda SDL.

Wakiagiza magari wanasamehewa kodi, wakiagiza vifaa vya hospitali zao wanasamehewa kodi nk.

Hali kadhalika kwenye hizo timu hazina hizo kodi na ndio maana matajiri wengi hutumia mgongo huo kujifanya wanawekeza.

Ingekuwa hivyo SIMBA au YANGA ndio zingekuwa zinalipa wachezaji wao, lkn amini nakwambia wachezaji wengi wanalipwa na watu tofauti tofauti na sio Klabu kama klabu.

Usisome kitu kwa kukariri mkuu, najua unataka kujua zaidi ila nakuomba kakae chini soma tena. Kasome MISAMAHA YA KODI ndio uje hapa ueleze hicho unachofikiria.
Umechanganya sana mambo, ndiyo maana hamuelewani.
Simba na Yanga zinalipa kodi. VAT kwenye mikataba, PAYE kwa wafanyakazi wao n.k ...
 
Ndio maana nimeona huna unalojua. We ulivyopimbi kwani shule zao wakipata pesa wanafanyia nini kama sio kuendeshea hayo hayo makanisa?? Wewe mzima kichwani lkn??

Au unadhani mapato ya hospitali zao wanagawana waumini???

Umeongea kindezi sana. Msingi wa kodi ni FAIDA. Kodi ambazo haziko generated na faida ni WTH Taxes, SDL, PAYE (Hii unakusanya kwa niaba ya watumishi/wafanyakazi) SDL, BED NIGHT nk.

Hizo PIT na CORPORATE TAXES msingi wake ni FAIDA except kwa wale PRESUMPTIVE.

Haya tuendelee hizo bil 26 za SIMBA, TRA watatoza KODI gani?? Jibu hilo swali acha wenge.
Watatoza 18% VAT
 

"Zile zama za kuwa na mkataba sare sare maua zimepita. Kwa miaka ya hivi karibuni Simba tumewekeza vya kutosha ili kuhakikisha brand yetu inakua,"- Meneja wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano, Ahmed Ally.

“Process ya mdhamini mpya tulianza tangu mwaka jana. Tumepokea boss nyingi za kutaka kuwa main sponsor, lakini M-Bet ndio wamekidhi vigezo vyetu vyote,” - CEO wa Simba, Barbara Gonzalez.

"Kwa ukubwa wa Simba ni lazima kujihusisha na kampuni ambayo inaongoza kwenye biashara ambayo wanafanya. Mkiangalia takwimu M-Bet wanaongoza kwa ukubwa Tanzania."- Barbara

"Hii ni mara ya kwanza mdhamini mkubwa anakuwa na senior team pekee, huko nyuma mdhamini mkuu alikuwa kwa timu zote lakini sasa timu zingine tunaweza kuzitafutia mdhamini wake,"- CEO

Mkurugenzi wa Masoko wa M-Bet, Allen Mushi ametaja mchanganuo wa udhamini mpya wa Klabu ya Simba:

Mwaka wa kwanza - Bil 4.670
Mwaka wa pili - Bil 4.925
Mwaka wa tatu - Bil 5.205
Mwaka wa nne - Bil 5.514
Mwaka wa tano - Bil 5.853
Jumla ni Bilioni 26, Milioni 168 na Tsh. 5,000.

=================================

TUJIKUMBUSHE MKATABA WA YANGA
Yanga SC ilisaini mkataba mpya wa Udhamini Mkuu na Kampuni ya kubashiri ya Sportpesa Tanzania, wenye thamani ya Tsh 12.3B kwa miaka mitatu (3), ambayo ni sawa na 4.1B kwa kila mwaka.

Mkataba huo ni ongezeko la Tsh bilioni 2 kwa mwaka kutoka kwenye mkataba awali wa bilioni moja kwa mwaka mmoja.

Pia soma:
Yanga FC yaingia mkataba mpya na SportsPesa wa miaka 3 wenye thamani ya Tsh Bilioni 12
Wa Cuba wanajua
 
Umechanganya sana mambo, ndiyo maana hamuelewani.
Simba na Yanga zinalipa kodi. VAT kwenye mikataba, PAYE kwa wafanyakazi wao n.k ...
Mkuu najua hilo, nikichosema mm ni ile CORPORATE TAX
 
Back
Top Bottom