Simba yatoa angalizo mashabiki wake kutowafanyia fujo mashabiki wa timu nyingine uwanjani

Jambo jema maana Simba hatunaga ubaya na mtu.
 
Pamoja ya yote hayo uzalendo ni lazma upewe kipaumbele

Kama Simba ama Yanga mojawapo anafakiwa kimataifa

Heshima ya kwanza inaliendea taifa

Watanzania tuweni wazalendo kwa maswala ya kitaifa
Huu U - Simba na U - Yanga
Tuiachie derby iamue
 
Waliopiga wenzao wachukuliwa hatua za kisheria,mpira ni burudani na sio vita au uhasama.
 
Waliopiga wenzao wachukuliwa hatua za kisheria,mpira ni burudani na sio vita au uhasama.
Hata ungekuwepo wewe lazima wale vyura ungewachapa za uso walikua wanapiga makelele yasiyo na maaaana sasa unategemea umeandaaa Sherehe yako halafu mgeni tena aje awe kerro?? Siku moja moja ngoja watiwe adabu kama hiyo ya jana ili wawe na nidhamu
 
Japo imeandikwa kishabiki na si kwa kukemea vitendo hivyo......
 
Sidhani kama wapigaji walikurupuka tu wakashusha kipigo. Lazima kuna chanzo .

Hata hivyo hawa watani zetu nao wapunguze ulimbukeni . Wewe unaona mwenzio keshapigwa goli anamaumivu moyoni halafu unajisogeza karibu nae unamzomea ,unategemea akuache salama?
 
Para ya mwisho ndo msingi wa barua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…