Simbachawene: Ripoti zinaonesha zaidi ya 40% ya Watumishi wa Umma Tanzania hawafanyi kazi

Simbachawene: Ripoti zinaonesha zaidi ya 40% ya Watumishi wa Umma Tanzania hawafanyi kazi

Baba mwenye nyumba ana watoto kumi, anasema kati ya hao kumi ni sita pekee ndiyo wenye manufaa kwake, wanne waliobaki ni hasara.

Je hao wanne achukue hatua gani? Aendelee kuwalisha na kuwahudumia labda kuna siku watabadilika au awafukuze wakafie mbele ya safari?

Mpe ushauri baba mwenye nyumba.
Ajinyonge hadi afe ili akawe baba wa malaika waovu kuzimu.
 
Baba mwenye nyumba ana watoto kumi, anasema kati ya hao kumi ni sita pekee ndiyo wenye manufaa kwake, wanne waliobaki ni hasara.

Je hao wanne achukue hatua gani? Aendelee kuwalisha na kuwahudumia labda kuna siku watabadilika au awafukuze wakafie mbele ya safari?

Mpe ushauri baba mwenye nyumba.
Serikali huwa haizai inaajiri

Mwajiriwa akiwa mzigo inatupilia mbali huko inatafuta wengine
 
Waliosusiwa yani wamesusiwa na nani ? Nilishawahi kisikia stori za mkurugenzi wa Shirika la Uma fulani aliyesusiwa akapelekwa Dodoma makao makuu kazi yake ikawa kusoma magazeti...hii sikuamini sasa naanza kuona kuna ukweli 😂😂
 
Kuna mwalimu mwenzetu mkongwe alinishangaza kwa kutoa kauli kwamba tumeletwa shuleni kuja kula hela ya serikali bure! Ndio kwanza tulikuwa tumepangiwa kituo hapo kwa mara ya kwanza tukitokea vyuoni. Alidai kwamba hakuna kazi ya kufanya, tukaa wiki nne tu mshahara unatoka na kwenda benki kuuchukua na kuula bure bila kufanya kazi. Alihoji kwani kuna kazi gani hiyo ya kulipwa mshahara? Alizidi kunishangaza kwa kuuita mshahara wetu ni hela ya chai ya asubuhi ya mbunge mmoja!
 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene amesema zaidi ya asilimia 40 ya Watumishi wa Umma hawafanyi kazi licha ya kulipwa mshahara kila mwezi.

Amesema hiyo ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa hivi karibuni na Tume ya Utumishi wa Umma nchini

Mhe. Simbachawene amesema hayo leo jijini Arusha wakati akifunga Kikao kazi cha tano cha Serikali Mtandao ambapo amesema Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma wanawajibu wa kuhakikisha kila mtumishi anatekeleza majukumu yake ipasavyo.

‘’Watumishi ni lazima wafanye kazi kwani wasipofanya kazi wanakuangusha wewe Mkuu wa Taasisi, lazima tuwe na jamii inayoandaliwa kufanya kazi’’ amesisitiza Mhe. Simbachawene
Amefafanua kuwa kwa mujibu wa tafiti hiyo, wavivu, wazembe, wagonjwa pamoja na waliosusiwa kutokana na vipaji na uwezo wao ni asilimia 40 ya Watumishi wanaolipwa pasipo kufanya kazi

Amewataka Wakuu hao kuwatumia Watumishi wa Umma wenye vipaji na uwezo badala ya kuwafanyia fitina na hujuma hali inayopelekea kurudisha nyuma maendeleo ya nchi

Amesema hali hiyo imesababisha kutokuwepo kwa urithishanaji wa madaraka jambo ambalo limechangia kudhoofika kwa Taasisi pale kiongozi wa Taasisi anapostaafu au kuhama.

Aidha, Mhe. Simbachawene amesema kumeibuka tabia ya baadhi ya Watendaji wakuu hao pindi Mtumishi mwenye sifa za ziada anapohamia kwenye Taasisi anayoiongoza hupata hofu na kutompangia najukumu kwa hisia kuwa ametumwa kumchunguza a au kuchukua nafasi yake

Ameeleza kuwa tabia hiyo kwenye utumishi wa umma haikubaliki na wale wenye tabia hiyo wajirekebishe haraka kwani Taasisi hizo wanazoziongoza ni za umma na sio mali yao binafsi

Katika hatua nyingine, Kutokana na ongezeko la matumizi ya simu kwa wananchi, Mhe. Simbachawene amezitaka Taasisi za Umma kutoa huduma za kidijitali kutokana na fursa hiyo

Vilevile, Mhe. Simbachawene amezitaka Taasisi za Umma ambazo hazijaanza kutumia mfumo wa kidijitari wa e-Mrejesho ziingie mara moja la sivyo zitachukuliwa hatua kali na Ofisi anayoiongoza.

Awali Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao, ( e-GA) Mhandisi Benedict Ndomba aliwashukuru washiriki wa kikao hicho cha jumla 1526 ya ushiriki wao ambapo jumla ya mada 18 ziliwasilishwa ikiwa ni pamoja na kujiwekea mikakati ya kukabiliana na changamoto za usalama wa mtandao Serikalini.

Amesema kikao hicho kimejadili changamoto mbalimbali zinazoikabili Serikali Mtandao pamoja na kuweka mikakati madhubuti ya kuchangamkia fursa ya kujifunza teknolojia mpya zinazoibukia ili kuendana na mabadiliko yanayotokea duniani kote.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Mhe.Festo Kiswaga ameishukuru e-GA kwa kuendelea kuuamini Mkoa wa Arusha ikiwa ni mara ya tano sasa vikao hivyo vimekuwa vikifanyika Mkoani humo hali iliyopelekea Mkoa huo kuwa wanufaika wakubwa wa kiuchumi pamoja na kuwa wadau namba moja wa matumizi ya Serikali Mtandao.

Naye Katibu Mkuu-IKULU, Bw. Mululi Mahendeka amesema Ofisi yake itasimamia na kufanyia kazi maazimio yote yaliyowasilishwa leo na kuhakikisha utekelezaji wake unawasilishwa katika kikao kijacho

Pia, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya e-GA, Dkt. Jasmine Bunga amesema kikao kazi hicho kimekuwa muhimu kwa washiriki ambapo mbali ya kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili pia wamejiwekea mikakati ya kuendelea kujenga Serikali ya kidigitali.

Amesema lengo ya kujiwekea mikakati hiyo ni kuhakikisha Serikali inapiga hatua kubwa kwenye matumizi ya mifumo ya TEHAMA itakayoleta tija na ufanisi wa hali ya juu katika utoaji wa huduma bora za haraka na za uhakika kwa wananchi.
Yaani huyu Jamaa sijui Watumishi walishamfanya nini,hana tofauti na Mwendazake Kwa chuki na Watumishi.

Yeye anafanya kazi gani ya maana?
 
Hakuna Kazi inayofanyika nchi hii.
Naona hapo kuna bango kubwa la e-GA halafu watu wamekutana physically! yaani inaonesha jinsi gani hatufanyi kazi. One day travelling to, one day travelling back, many hours after meeting being idle in Arusha could be saved by video conferencing.
 
Nijambo la kustaajabu kama karibu nusu ya watumishi wa umma hawafanyi kazi. Pamoja na uhaba wa nguvu kazi ulipo bado kuna nguvu kazi inakula mshahara wa serikali na hawafanyi kazi inavyo takiwa. Ikumbukwe kuwa tanzania ina watu walio katika nguvu kazi takribani milioni 25 kati ya watanzania milion 65. Hii inamaana kuwa watanzania milion 49 niwategemezi sasa hawa wacache waliopo bado kuna watu hawatumii nguvu zao vizuri kutumikia Taifa hili. 😪 maendeleo yatatoka wapi? Yani nguvu kazi ya milion 25, ukitoa hapo hawa wavivu , ukitoa hapo jobless na wale wadangaji sijui maendeleo tutatoa wapi

"
#HABARI Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amesema zaidi ya asilimia 40 ya Watumishi wa Umma hawafanyi kazi licha ya kulipwa mshahara kila mwezi.

Amesema hiyo ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa hivi karibuni na Tume ya Utumishi wa Umma nchini

Mhe. Simbachawene amesema hayo leo jijini Arusha wakati akifunga Kikao kazi cha tano cha Serikali Mtandao ambapo amesema Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma wanawajibu wa kuhakikisha kila mtumishi anatekeleza majukumu yake ipasavyo.

‘’Watumishi ni lazima wafanye kazi kwani wasipofanya kazi wanakuangusha wewe Mkuu wa Taasisi, lazima tuwe na jamii inayoandaliwa kufanya kazi’’ amesisitiza Mhe. Simbachawene

Amefafanua kuwa kwa mujibu wa tafiti hiyo, wavivu, wazembe, wagonjwa pamoja na waliosusiwa kutokana na vipaji na uwezo wao ni asilimia 40 ya Watumishi wanaolipwa pasipo kufanya kazi

Amewataka Wakuu hao kuwatumia Watumishi wa Umma wenye vipaji na uwezo badala ya kuwafanyia fitina na hujuma hali inayopelekea kurudisha nyuma maendeleo ya nchi

Amesema hali hiyo imesababisha kutokuwepo kwa urithishanaji wa madaraka jambo ambalo limechangia kudhoofika kwa Taasisi pale kiongozi wa Taasisi anapostaafu au kuhama. #EastAfricaTV
 
40 percent is just too much of a burden to shoulder. How did they hire the employees who have no value addition.

Results ya employment ya watoto wa mjomba, shangazi etc Kama wanajuwa ni mzigo, basi wawatoe!!

Kiongozi huwezi kutoa kauli kama hiyo hadharani halafu na solution huna. Ni bora ukae KIMYA

Naona waziri ndio mzigo kama tatizo umeliona unaanza kulalamika bila kutoa maamuzi. You are the biggest problem
 
Back
Top Bottom