LGE2024 Simiyu: Mch. Msigwa adai CHADEMA hawana uhalali wa kumkosoa Rais Samia

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mchungaji Peter Msigwa ametema cheche katika mkutano uliofanyika Simiyu, akitoa kauli kali dhidi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Amesema kuwa CHADEMA hakina uhalali wa kukikosoa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwani chama hicho kimekosa uhai na timu yake imeonekana kuchoka. Msigwa ameongeza kuwa Chadema hawana mipango madhubuti na nyuso zao zimekosa nuru.

Aidha, alimsifu Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuitekeleza miradi iliyokuwa imeachwa na aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, akidai kuwa Rais Samia amenyang'anya ajenda zote za CHADEMA kwa ufanisi wake.

Your browser is not able to display this video.
Soma, Pia:
Mchungaji Msigwa alitaka wagombea wawili nafasi ya Mwenyekiti Taifa
Mchungaji Msigwa Mbona hasikiki au amerudi CHADEMA Kimya Kimya?
Mchungaji Msigwa: Mbowe amezungukwa na Wahuni halafu anasema atachukua Nchi!
 
June 2024 yeye alikuwa na uhalali? Kama ametubu tumuone akigaragara mbele ya Rais Samia vyenginevyo itakuwa usanii wa kisiasa
 
 
Mbona ameacha kumtukana Mbowe
 
Huyo houseboy wa Kasisi wa kizungu ndiye mnamuita Mchungaji?
 

Attachments

  • FB_IMG_1721892194992.jpg
    53.1 KB · Views: 5
  • FB_IMG_1721892194992.jpg
    53.1 KB · Views: 5
  • IMG-20200403-WA0003~2.jpg
    18.8 KB · Views: 5
  • Screenshot_2024-07-21-09-14-46-163_com.whatsapp~2.jpg
    244.5 KB · Views: 5
  • FB_IMG_1719903252490.jpg
    26.2 KB · Views: 5
  • FB_IMG_1719903155204.jpg
    51.5 KB · Views: 5
  • downloadfile-21~2.jpg
    141.1 KB · Views: 5
Mchngaji msigwa amekua akieleza ukweli sana kuhusu Chadema,

na ukitazama unaona bayana kwamba hawana uelekeo kabisa na wala hawana hoja..

na wengine imefikia mahali kutumia kukitumia chama kwa masuala yao binafsi dah 🐒
 
Na wewe umeamini aliyoyaongea?! Katema cheche au kaharisha cheche?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…