Simu gani inajaa chaji mapema zaidi ya hii

Simu gani inajaa chaji mapema zaidi ya hii

Hili panga linakata kote kote, maana battery nayo inakufa mapema, mwaka ama miaka 2 kama una matumizi makubwa kwisha kazi, battery inatakiwa ibadilishwe.
Battery ya simu ikikaa imara miaka miwili hiyo ni nzuri mbona
 
Hakuna haja yakuacha simu kwenye charge overnight...kama iphone(joking)
Unaamka asubuhi unaboost shorlty inakutosha kwa siku nzima.....
Pia uhitaji wa battery kubwa utapungua kwasababu hata ikikuishia chaji unaboost kwa muda mfupi sana

Mzee me najaza iphone yangu fasta tu na fast charge sasa ukitumia magsafe ndo balaaa
 
Battery ya simu ikikaa imara miaka miwili hiyo ni nzuri mbona
Hapana battery zinakaa miaka hadi mitano ukizitunza vizuri, ama Zaidi.

Hii simu ya 2017 Mwaka wa 4 huu ina 2700mah, now real capacity ni 2500mah imepoteza kama 10% tu,
Screenshot_20211015-000513.png
 
Hio ni xz1 compact
Sony hatari sana mi nina x compact ya 2016 ila battery yake ni sawa na hizi Samsung A series za 4000mah. Performance yake camera iko vizuri sana.Internet super speed inapanda mpaka4G+ nimecheki comparisons zake na flgship kama s8 plus bado iko faster japo ni 3gb ram na snapdragon 650.Xz1 compact itakuwa vizuri zaidi
 
Mkuu samahan ,hawa sony ni kampuni inayotengeneza simu kutokea wapi?Je kwa sasa kuna matoleo yapi ya midrange yanayoipiku redmi note 10 ambayo yanacheza kati ya 5 laki hadi 7 laki?
Ni Japan ila siku hizi wanatengeneza tu flagship na bei zao ni ndefu sana kusema kweli. Sisi wengine tunasubiria tu used za matoleo ya zamani.
 
Ni Japan ila siku hizi wanatengeneza tu flagship na bei zao ni ndefu sana kusema kweli. Sisi wengine tunasubiria tu used za matoleo ya zamani.
Duuh haya kiongozi na used zipi nikizipata now nitajiona poA kwa bajeti hio niliokuambia
 
Niliwahi kuandika humu, hii ni usb standard mpya ambayo inaenda hadi watts 240, hivyo tegemea simu kibao kuwa hivi, even infinix wana yao.

Hivyo mkuu soon unatoona simu kibao zinazojaa kwa robo saa tu.
Yangu inakanyaga masaa mawili na nusu [emoji124][emoji124] ntaendelea kuwa nayo maana pesa hazionekani .
 
Hili panga linakata kote kote, maana battery nayo inakufa mapema, mwaka ama miaka 2 kama una matumizi makubwa kwisha kazi, battery inatakiwa ibadilishwe.
Kumbe kila kitu kina madhara yake , na zile zinazokaa kwenye moto masaa mawili na nusu inakuwaje swala la betri ?
Mkuu mimi ninatumia oppo a3s tangu mwaka 2018 mwezi wa 11 mpaka leo , kwa sasa betri ndo limeanza kupungua makali maana zamani hata nipigeke mziki ilikuwa haitoi bar moja , lakini kwa sasa inakula kula nikiitoa kwenye chaji asubuhi kufikia jioni nikiingia na mtandaoni moto unakata.
Ila tangu nimemiliki simu zote kwa mikono yangu hii ndiyo simu niliyoiona bora , haijawahi nisaliti kama ilivyonisaliti Samsung J5 Prime , maana baada ya mwaka ilianza marue rue mengi tu ila hii tangia nimeinunua tena used sijawahi kurestore.
 
Kumbe kila kitu kina madhara yake , na zile zinazokaa kwenye moto masaa mawili na nusu inakuwaje swala la betri ?
Mkuu mimi ninatumia oppo a3s tangu mwaka 2018 mwezi wa 11 mpaka leo , kwa sasa betri ndo limeanza kupungua makali maana zamani hata nipigeke mziki ilikuwa haitoi bar moja , lakini kwa sasa inakula kula nikiitoa kwenye chaji asubuhi kufikia jioni nikiingia na mtandaoni moto unakata.
Ila tangu nimemiliki simu zote kwa mikono yangu hii ndiyo simu niliyoiona bora , haijawahi nisaliti kama ilivyonisaliti Samsung J5 Prime , maana baada ya mwaka ilianza marue rue mengi tu ila hii tangia nimeinunua tena used sijawahi kurestore.
Adui mkubwa wa Battery ni joto, mara nyingi charger zinazochaji haraka zinatengeneza joto, na zinazochaji taratibu joto linakuwa dogo sana. Hivyo kama huna haraka upo tu nyumbani bora usitumie fast charging.
 
Chifu sory kuna hizi rumours je hii simu ikiwa hivi ma note 10( redmi yupi kakalishwa) na pia hii na poco f3 Xiaomi Redmi Note 11, Note 11 Pro specs leak. Said to launch shortly.
Mkuu hizo simu note 11 na Note 11 pro sijazielewa ila tusubiri zaidi. Tetesi kuna Note 11 pro max itakuja na snapdragon 778.

Mwaka jana pia walitoa za China zenye specs tofauti ndio wakaja wakatoa international.

Redmi note 10 pro ya kichina ilikuwa ni dimensity 1100 sijui kwanini kwenye 11 wame downgrade.

Na poco F3 ni much better kuliko redmi note 10 ama 11 series, hazilinganishiki. Yenyewe hii ni Highend device.
 
Adui mkubwa wa Battery ni joto, mara nyingi charger zinazochaji haraka zinatengeneza joto, na zinazochaji taratibu joto linakuwa dogo sana. Hivyo kama huna haraka upo tu nyumbani bora usitumie fast charging.
Kumbe , shukrani sana mkuu , sasa kama zitakuja hizi simu za kutumia dakika 12 kuchaji siitakuwa balaa . Kuwa tunafanya replacement ya betri kila baada ya mwaka .
 
Back
Top Bottom