Simu yangu iliyoharibika nimeiweka ndani kwa miezi minne lakini kwa amani nayoipata sitamani tena kuitengeneza, peace of mind ni kitu muhimu sana

gearbox

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2024
Posts
563
Reaction score
1,768
Simu yangu iliharibika, gharama za kuifufua zilikuwa ni kubwa sana kwangu, nikasema nitulie kwanza nijichange nije kuifufa hapo baadae.

simu mpya nayotumia ina namba mpya ya whatsapp, ni wachache sana wanaijua. Namba yangu ya wharsapp iliyozoeleka sijaitumia miezi minne.

Kwa sasa amani ninayoipata ni kubwa sana, ni peace of mind, moyo na kichwa vimetulia, nimegundua ile namba yangu official ya whatsapp ambayo naitumia kwa muda mrefu ilikuwa inanifanya niwe bize sana mitandaoni
 
Hakuna ulichokiepuka mana bado una simu na utakuwa busy na mitandao ukitaka
 
Hakuna ulichokiepuka mana bado una simu na utakuwa busy na mitandao ukitaka
Ni kweli lakini naona kama nimeanza fresh start, ile namba yangu ya zamani ilikuwa na watu wengi sana tunaojuana kwa mabaya na mazuri, nikiingia sehemu ya status naweza nisizimalize
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…