Simulizi: Ajira Toka Kuzimu

Simulizi: Ajira Toka Kuzimu

Abdallahking

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2018
Posts
3,985
Reaction score
10,840
891903_578916088831669_1315917485_o.jpg


Simulizi: AJIRA TOKA KUZIMU
Mwandishi: GEORGE IRON MOSENYA
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES


SEHEMU YA 1

Aliitazama nchi hii kwa mbali sana, aliyekuwa mkuu wake alimuonyesha kwa kutumia kidole kimoja. Ilikuwa ina rangi ya bluu hii ndio ilikuwa nchi kubwa aliyokuwa ameagizwa kumfanyia kazi yake ambayo hakuwa ameshurutishwa kuifanya bali kwa hiari yake mwenyewe. Baada ya kuelekezwa vyema katika nchi hii sasa alimuelekeza vi-nchi vingine vidogo vidogo ambavyo havikuwa na ukubwa wa kutisha. Majina yake mengi yalikuwa ya kigeni lakini yalieleweka na kukaa vyema katika kichwa cha kijana huyu aliyekuwa anaelekezwa. Alitikisa kichwa juu na chini kuashiria kuwa anaelewa somo alilokuwa anapewa.
Mkuu wake aliyefahamika kwa jina la Tuntufye Kanyenye ama kwa kifupi Tuntu alitoa tabasamu ambalo kwake lilikuwa bora lakini linatia karaha ukilitazama. Tabasamu hili lilimaanisha kuwa alikuwa na imani kubwa na kijana huyu aliyekuwa anaagizwa katika nchi hii ya bluu na nyingine ndogo ndogo.
“Nakutakia safari njema yenye mafanikio….” Tuntu alimtamkia kijana wake huku akimpapasa kichwa chake katika hali ya kubariki. Baada ya hapo akampulizia marashi fulani katika nguo zake. Halafu akamtwaa na kumnyanyua juu juu tayari kwa kumrusha katika dunia hiyo. Hofu ikaanza kumtawala kijana huyu akawa anatetemeka ujasiri aliokuwanao ukaanza kuyeyuka akawa anatweta kwa hofu lakini tayari alikuwa katika mikono hii mibaya yenye nguvu. Akiwa bado katika uoga mara alirushwa kwa nguvu zote akauacha ule ulimwengu akawa anaelekea katika ulimwengu mwingine. Alikuwa anarusha miguu huku na kule lakini aliishia kuipatia majeraha hewa ambayo ilikuwa katika kila sehemu.
Kwa takribani dakika tano nzima alikuwa hewani na sasa alikuwa anakaribia kutua katika nchi hii ya bluu. Uoga ukamzidi akajikunyata akauziba uso wake kisha akapiga kelele kubwa sana za uoga huku akijaribu kukwepa asitue eneo lile aliloliona kuwa la hatari sana.
Jasho kali lilikuwa linamtoka, alikuwa peke yake chumbani alikuwa amekaa kitako katika kitanda chake cha futi tano kwa sita. Alikuwa anatetemeka. Taa ilikuwa imezimwa akasimama aweze kwenda kuiwasha lakini akajihisi kuwa alikuwa katika kutetemeka, akarudi akaketi tena. Alikuwa ametoka kuota ndoto mbaya sana ambayo hajawahi kuiota kabla. Alijaribu kupikichapikicha macho yake ili aweze kuona kama aliyoyaota yalikuwa ndani ya chumba kile lakini hapakuwa na mfano wa kitu kama hicho pale ndani. Kwa unyonge akarejea kitandani akauchapa usingizi tena.
Palipokucha hakuwa na kumbukumbu tena kama usiku ule alikuwa ameota ndoto mbaya. Aliamka akiwa na amani tele. Alijisikia mwenye nguvu za kustaajabisha!!
Hakujua kama alikuwa ameingia katika utumwa
Utumwa wa bila kujua.

****

Hassan alikuwa anazipitia post za hapa na pale katika mtandao wa kijamii wa facebook katika namna ambayo hakuwahi kuifanya hapo kabla. Alizitazama post za mapenzi hasa hasa za wasichana, hakujalisha kama ni warembo ama la. Hakuwahi kufikiria kuwa siku moja anaweza kuwa kama alivyo.
“Beatrice Cosmas” alilisoma jina hilo na kulirudia mara kwa mara, “Saint Augustine Mwanza” akakisoma na hicho chuo alichokuwa anasoma dada huyu.
“Nipo njiani nakuja Dar yeyote aje kunipokea jamani” hatimaye akaikariri na ile post aliyoweka dada huyu mnene katika picha akiwa na mwanya na macho ya kuvutia.
Hassan aliingia katika inbox ya dada huyu akamkaribisha Dar huku akimwomba ampe nafasi ya kumpokea mara atakapofika. Beatrrice akazuga kujizungusha zungusha na kumwomba Hassan namba yake ya simu na kuahidi kumpa taarifa baada ya kufika. Hassan bila kinyongo alimpatia namba yake ya simu huku akitoa tabasamu.
Hassan aliingia katika shughuli zake huku akiwa ameanza kusahau kama alikuwa na ahadi ya kupokea simu yoyote ile mpya. Ilikuwa kama bahati ya kipekee baada ya kuwa amepokea malipo baada ya mauzo ya mzigo wake wa samaki.
Wakati anaingia katika gari lake aina ya GX 100 alikutana na mlio wa simu yake, ilikuwa namba mpya, aliitazama kisha akabonyeza kitufe cha kupiga. Simu ikaita kidogo ikapokelewa na sauti nyembamba ya kike.
 
SEHEMU YA 2


“Hassan jamani…nimekupigia simu muda mrefu kweli!!!”

“we nani??”

“Jamani mi Beaty!!!”

“Beaty yupi tena”

“Wa facebook…”

“aaah!! Beatrice wa Mwanza eeeh!!”

“Ndio mimi, tupo Mbezi vipi unakuja kunipokea kweli?”

“Poa nakuja!!” alijibu Hassan upesi. Kisha akafanya upesi akakabidhi biashara yake kwa vijana wake akaingia garini akawasha gari na kutokomea kwa kupitia njia za panya hadi akafika Ubungo stendi.

Zilikuwa zimepita dakika tano tangu gari la Zuberi kutoka Mwanza liingie hapo stendi na kushusha abiria. Beatrice hakuwa na uhakika kama Hassan atakuja kweli ama la!!! Aliposhuka akajaribu kuipiga simu ya Hassan haikupokelewa, akajaribu tena haikupokelewa akaanza kukata tamaa. Akiwa anatafuta uwezekano mwingine wa kutoka pale stendi mara simu yake ikamwonyesha kuwa Hassan alikuwa anapiga. Akapokea haraka haraka. Kabla hajaongea simu ikakatwa, akahisi Hassan amebip, akapiga kite cha karaha, akatazama salio kisha akataka kupiga. Akashtukia ameguswa begani, alipogeuka akakutana na sura ngeni kabisa ikamtupia tabasamu, hakujibu lile tabasamu badala yake akashangaa.
“Hassan Tembo…..” akajitambulisha kwa jina lake analotumia kule facebook.
“Mambo!!!” alisalimiwa katika hali ambayo ilionyesha kuwa Beatrice bado alikuwa katika mshangao.
“Poa…vipi za safari pole sana na karibu Dar”
“Asante mh!! Yaani kule facebook unaonekana mkubwa kweli mh!! Facebook ina mambo” Beatrice aliyasema hayo kwa kebehi. Maneno hayo yakamuumiza Tembo, akahisi amedharauliwa sana, lakini kabla ya kujibu chochote alimtazama kwa kuibia ibia Beatrice kuanzia chini, akakutana na viatu vyenye mtindo wa kisasa lakini vikiwa vimechakaa kutokana na kuikanyaga sana lami na kuvaliwa mara kwa mara, bila shaka hakuwa na viatu vingi, gauni lake kwa mahesabu ya haraka haraka lilikuwa halifiki hata shilingi elfu kumi na tano, kichwani alikuwa na wigi huku nywele zake halisi zikichungulia kwa mbali na kuutangaza uchakavu wake.
Mkononi alikuwa na mabangili ya bei chee huku akiwa amevaa na kicheni kilichopauka kikiwa na maneno I LOVE U…usoni hakuwa na mng’aro wa utajiri huku mkoba wake uliochakaa ukiutangaza umasikini wake kama sio ubahili.
“Mh!! Hana lolote huyu hebu ngoja…sijui na yeye nimwambie kuwa picha zake za facebook anaonekana mrembo?? Yaani anaonekana ana pesa kumbe hana maana yoyote” alijisemea Tembo huku usoni akizuga kutabasamu.

“Kwa hiyo unaelekea wapi sasa hivi, twende basi”

“Mh!! Asante Hassan usijali na asante kwa kuja mi nishafika hivyo, tutaonana facebook baadaye basi!!” Beatrice alijaribu kumkwepa Tembo, naye akaligundua hilo. Moyoni mwake aliitambua dharau ya Beatrice akaahidi kumkomesha na kumkata kidomo domo.

“Wapi sasa unaelekea sasa hivi!!” Tembo aliuliza huku akijua fika kuwa yule binti hakuwa na pa kwenda.
“Nitaenda hapo Magomeni ila kuna mtu namsubiri”:.alijibu.
“Basi twende nikusindikize!!”

“Asante Hassan..usijali hata” alizidi kukwepa Beaty.

“Poa basi ngoja mi nirejee maskani yangu” alisema Tembo.
 
SEHEMU YA 3


“Poa basi ngoja nikusindikize kidogo” Beaty akawa amejibu bila kujua kuwa amefanya kosa kubwa sana. Walisogea mbele kidogo, Hassan mtoto Mama Tembo akatoa funguo za gari akabonyeza. Gx 100 ikapiga kelele za kujitoa loki, akafika akaegemea ile gari akaanza kuagana na Beaty tena. Wakati huu sasa Beaty akatoa tabasamu la ukweli. Mara akawa muongeaji sana. Tembo akajua tayari amemuingiza kwenye kumi na nane.
Wasichana kwa tamaa!!!
Lakini hakujua Beaty anajiingiza katika domo baya wakati huu!!

“Mh!! Huyu shoga yangu mwenyewe sijui haji??” Beaty akaanza kujiongelesha ilimradi tu kufikisha ujumbe. Tembo akamwambia kuwa kama haji waondoke naye, binti akaingia mkenge akakubali, milango ikafunguliwa, akakutana na marashi ya aina yake huku mziki ukisikika kwa mbali sana kutoka katika santuri iliyokuwa katika redio, hiyo ni baada ya gari kuwashwa. Beaty akabweteka katika siti ya nyuma, Tembo akakataa kuendesha gari hadi alipohamia siti ya mbele. Safari ya kutoka ikaanza.

Tayari Beaty alikuwa amesahau kuwa alisema kuwa Tembo ni mdogo sana, sasa alikuwa anamwona kuwa ni mkubwa tena mtanashati. Tembo alikuwa kimya sana huku akitikisa kichwa kufuatana na mdundo wa mziki uliokuwa unaendelea.

“B twende tukapate msosi kwanza au vipi”

“Poa tu twende” alikubali haraka haraka Beaty. Tembo akafurahi na nafsi yake.

“Atanikoma na hatanisahau!!!” aliapa kimya kimya Tembo huku akiiendesha gari kuitafuta Kinondoni. Na hatimaye akaifikia Best Bite, akapaki gari wakaingia katika mgahawa ule maarufu jijini Dar es salaam.
“Chipsi mayai….” Akaagiza B, muhudumu akamwambia hakuna orodha hiyo ya chakula. Tembo akacheka kimoyo moyo akagundua kuwa Beatrice alikuwa na ujanja wa facebook tu, wala kimaisha halisi hakuwa na ujanja wowote. Hata chakula kilivyoletwa Beatrice hakujua jinsi ya kutumia uma na kisu , kuzitumbua chipsi na paja la kuku lilokuwa mbele yake.
Kwa mara nyingine tena Tembo akausoma ushamba wa Beatrice!!!!
Kwisha habari yake!!!!!! Akajisemea huku akistaajabu huo ujasiri alikuwa ameutoa wapi.

**Nani ni mwajiriwa kutoka kuzimu????
**Je? Hassan Tembo atafanikiwa azma yake na kwanini anasema kuwa atamkomesha Beatrice.
**Nchi ya bluu ni ipi???
 
SEHEMU YA 4


“Atanikoma na hatanisahau!!!” aliapa kimya kimya Tembo huku akiiendesha gari kuitafuta Kinondoni. Na hatimaye akaifikia Best Bite, akapaki gari wakaingia katika mgahawa ule maarufu jijini Dar es salaam.
“Chipsi mayai….” Akaagiza B, muhudumu akamwambia hakuna orodha hiyo ya chakula. Tembo akacheka kimoyo moyo akagundua kuwa Beatrice alikuwa na ujanja wa facebook tu, wala kimaisha halisi hakuwa na ujanja wowote. Hata chakula kilivyoletwa Beatrice hakujua jinsi ya kutumia uma na kisu ,kuzitumbua chipsi na paja la kuku lilokuwa mbele yake. Kwa mara nyingine tena Tembo akausoma ushamba wa Beatrice!!!!
Kwisha habari yake!!!!!! Akajisemea

****

Baada ya kutafuna mifupa ya kuku wa kisasa wanaokuzwa kwa kutumia madawa makali lakini ikatiwa viungo na kuonekana kuwa bora kwa mwanadamu. Tembo alikuwa akimsikiliza Beaty atasema nini, na tayari ilikuwa saa nne na dakika kadhaa usiku.
“Kwa hiyo twende Magomeni au sio..ni Magomeni ipi kwani??” aliuliza Hassan Tembo huku akijichokonoa na kijiti katika meno yake.
“Mh!! Sijui watafungua geti sasa hivi maana mh!!” alizungumza kama anajisemea vile Beaty. Tembo akajichekesha kwa kulazimisha.
“Kwani wewe unaenda wapi sasa hivi??” aliuliza huku akizungusha funguo za gari lake huku na huko.
“Naelekea nyumbani pande za Mbagala hivi”
“Dah!! Vipi anakusubiri mke nini??” aliuliza huku akijichekesha
“Hapana nipo na mwanangu mmoja tu sijaoa bado” alijibu kwa kujiamini.
“Mhh!! Kumbe una mtoto Hassan…” alihoji Beatrice..
“Hapana mwanangu yaani rafiki yangu mmoja hivi… mi sina mtoto wala!”
“Mh!! Afadhali maana presha ishaanza kunipanda” Beaty akatokwa na kauli iliyomfanya Tembo atabasamu.
“Kwani wewe ni lazima uende nyumbani leo???” akamhoji
“Mh!! Wala sio lazima maana hawajui kama nimefika..sasa nisipoenda nitaenda wapi?” alijibu na kujiuliza. Tembo hakusema lolote akaingia garini na Beaty akaingia. Tembo akawasha gari hadi Kinondoni kwa Manyanya, gari yake ilipolifikia geti la CHICHI HOTEL geti lilifunguka bila msaada wa mlinzi. Beaty akaduwaa, Tembo akashuhudia hali hiyo, akajiaminisha moyoni kuwa tayari amemteka Beaty na ushamba wake.
“Elfu hamsini Deluxe” alitajiwa bei ya chumba akazama mfukoni akahesabu hizo noti akamkabidhi binti mweupe wa haja aliyekuwa na tabasamu muda wote pale mapokezi.
Kisha kwa ishara akamwita Beaty, kama msukule Beaty akamfuata hadi chumba namba kumi na nane. Tembo akachomeka kikadi akaufungua mlango. Beatrice hakuwa na ujanja wowote, Tembo akawa kiongozi Beaty akawa mfuasi.
 
SEHEMU YA 5



“Mh!! Siamini kama nalala na wewe leo, yaani mh! Umevunja rekodi kabisa, sijawahi kulala na mwanaume sehemu kama hizi… yaani tumekutana mara ya kwanza tu dah..” Beaty alizungumza huku akikishangaa kile chumba. Tembo hakumjibu badala yake akapenyeza mkono wake kiunoni mwa Beaty na kisha akamtekenya kidogo, Beaty akaanza kujichekesha kama bwege.
Kwisha habari yake!! Akajisemea Tembo, kisha akamrusha kitandani.

Bila kutegemea walioga wote, walicheza wote na mwisho wa siku wakajikuta wamefanya mapenzi nani aliyejiuliza kuhusu mimba na maambukizi ya magonjwa, jibu lilikuwa jepesi tu HAKUNA.

Palipokucha Tembo alimsindikiza Beaty hadi nyumbani kwao. Ile kushuka kwenye gari na kuambiana kwaheri huo ndo ulikuwa mwisho wa Tembo kuonana na Beaty japo walikuwa wanawasiliana. Hadi Beaty anarejea chuoni hakuwahi kumtia tena Tembo machoni. Kule facebook hakujibiwa chochote alichouliza, hatimaye akachoka akajiweka pembeni.
Na huo ukawa mwanzo wa Tembo Hassan kujielewa kwamba alikuwa amefanya jambo ambalo hakuwahi kulitegemea.
Hakuwa na wasiwasi!!!
Beatrice akajipa moyo kuwa mambo yameishia pale, kuwa amedanganywa tu na mwanaume na bahati mbaya wamefanya mapenzi… hakujua Tembo yu kazini hakujua balaa aliloachiwa!!!

*****

Tembo Hassan aliitazama kwa dharau picha ya msichana mmoja akiwa yupo pamoja na mpenzi wake, walikuwa wamekumbatiana kimahaba huku wote wakiwa na tabasamu halisi kutoka moyoni.
“I love my husband jamani” picha ile iliandikwa hivyo kwa juu. Tembo akakereka sana kuona maneno yale, akamtazama vyema yule msichana. Paja jeupe la kuvutia, macho mazuri!!

“Clara Clara Clara!!!!” aliita kwa sauti ya chini ile picha kana kwamba ilikuwa inamsikiliza, halafu akamaliza akaihifadhi katika simu yake. Kabla ya kuifunga simu yake aliamua kufungua profile ya Clara akaanza kuipitia hatua kwa hatua.
“Reading novles” alikuta maneno haya katika vitu ambavyo vinamvutia Clara mojawapo likiwa hilo la kusoma riwaya.
Tembo kwa akili ya haraka haraka akamkumbuka mdau mmoja wa facebook kwa jina la Ibarahim Gama. Huyu alikuwa ni mtunzi mahiri ambaye mara chache Tembo huwa anapata nafasi ya kupitia simulizi zake zinazopendwa na watu wengi katika mtandao wa kijamii. Tembo alizikumbuka kichwani mwake jinsi simulizi hizo ambavyo huwa zinaiteka akili yake.
Ghafla bila kujua anachokifanya aliingia katika mtandao wa kijamii wa facebook, akaingia katika kundi la simulizi moja baada ya jingine. Kona ya riwaya, Uwanja wa simulizi, Stori za mapenzi na sitosahau, Tungo zetu kisha akamalizia na kurasa ya George wa hadithi stories. Huko kote akakuta kuwa Clara ni mdau na anazifuatilia simulizi kwa ukaribu.
Hapahapa! Akajisemea Tembo kisha akaandika “Kaa mkao wa kula kusoma simulizi zangu kuanzia kesho” watu wengi waliitazama kama utani na hawakuamini kabisa kuwa Hassani Tembo alikuwa na uwezo wa kuandika simulizi. Lakini wakamjibu kuwa wanangoja simulizi hizo.
 
SEHEMU YA 6


Tembo alipofika nyumbani alifungua maboksi kadhaa akakutana na vitabu vya simulizi vya kiingereza na Kiswahili. Akavichukua vyote viwili akavilinganisha. Akachagua cha kiingereza, akakisoma kikamvutia sana. Akatulia tuli akaanza kukitafsiri katika lugha ya Kiswahili, siku iliyofuata akadondosha katika makundi simulizi hii. Maoni yakawa mengi, sifa zikamiminika, wanawake walikuwa wengi waliomsifia Tembo kwa mwanzo mzuri, wanaume walikuwa wachache, jambo hilo lilimvutia sana. Alikuwa katika mawindo, Hassan Tembo!!
Hakuwa na shida na wanaume. Lengo lake lilikuwa ni hao hao wanawake na mawindo yake yalikuwa kwa Clara. Hadi inafika sehemu ya sita ya simulizi yake hii ya kuiba kutoka katika kitabu cha kiingereza na kuitafsiri kuwa ya Kiswahili bado Clara alikuwa hajajitokeza lakini tayari mawindo yake yalikuwa na wateja wengi sana ambao walikuwa wamejiingiza katika kutaka kumjua sana zaidi ya pale facebook.
Huku Tembo akidhania kuwa Clara hakuwa akifuatilia simulizi zake, haikuwa hivyo Clara alikuwa naye bega kwa bega. Siku hii Tembo akaamua kumtag Clara katika simulizi zake.
“Asante Tembo kwa kunitag hadithi yako yaani imenigusa kweli hii simulizi yaani haya mapenzi acheni yaitwe mapenzi” Clara alimuandika meseji Tembo. Kabla ya kuijibu Hassan alitabasamu kidogo halafu akafikiria nini cha kumjibu.

Tembo:Usijali dear….imewagusa wengi sana!! Na ndiyo nia yangu mimi
Clara:Ikiwa inaendelea uwe unanitaarifu basi
Tembo:Usijali….ntakuwa nakutaarifu
Clara:Mh!!!!natamani uimalize yote nijue mwisho wa huyu mkaka maana dah!! Sipati picha.
Tembo: Mambo mengi sana ujue natamani kuwa naandika sana sema muda tu
Clara: Haya kaka hongera kwa kipaji sipati picha wifi si atakuwa anafurahia sana, kila siku unamuhadithia, nikija Dar nitakutafuta unisimulie au unipe kitabu nijisomee.
Tembo: aah!! Wala hapendi hadithi, kwani we upo wapi? Halafu kitabu sijatoa bado ila nitatoa.
Clara: Mwanza nipo chuoni huku lakini Dar ndo nyumbani.
Tembo: Huwa nakuja Mwanza mara kadhaa siku nikija nitakutafuta.
Clara: Nitafurahi sana yaani sana tu…pliz usiache kunitafuta kama kweli ukija.
Tembo: usijali dadangu sitaacha nipatie namba yako kama hutajali…maana facebook sio pa kuamini sana unaweza uingie au usiingie.
Tembo akapewa namba ya simu!!!
Mtego unaelekea kunasa!!

*****

Basi liliiliwaza stendi ya Mwanza iliyokuwa katika upweke mkubwa kutokana na kukosa mabasi mengi katika muda huo wa usiku.
Abiria mmoja baada ya mwingine walishuka kutoka katika basi lile. Walipomalizika kabisa alisimama abiria ambaye huenda ni maksudi ama kukwepa vurumai aliamua kuwa wa mwisho kushuka. Alikuwa hana dalili ya nywele katika kichwa chake kilichofanana rangi na uso wake mweusi. Mgongoni alikuwa na kibegi kidogo cheupe kilichorandana na kiatu chake mguuni, hakuonekana kuwa mgeni sana wala mwenyeji sana, usoni alikuwa na miwani kubwa nyeupe iliyomkaa vyema.
Alipofika chini aliusabahi mji huu kwa kuvua miwani yake na kufanya mfano wa toba ya kiislam. Kisha alipiga hatua kadhaa mbele hadi akakifikia kibanda cha chipsi.
“Zege na mishkaki mitatu!!” aliagiza kwa sauti ya wastani lakini yenye amri ndani yake.
“Poa braza”
Baada ya dakika kumi na tano Hassan Tembo alikuwa akifanya mashambulizi ya hatari katika viazi mviringo vyenye mayai pamoja na mishkaki.
“Nipatie na Fanta baridi”
 
SEHEMU YA 7


Punde aliletewa akaigida kwa fujo zote kisha akalipa kilichostahili akasimama na kuondoka bila kuaga.
Alitembea haraka haraka kama mwenyeji hadi katika kituo cha mabasi, kulikuwa na baridi kali sana kutokana na msimu wa mvua uliokuwa ukiendelea, kila mtu alikuwa na koti ama sweta lakini Tembo hakuwa na chochote kile zaidi ya fulana yake. Baridi lilianza kuushambulia mwili wake kwa fujo akajihisi kama hana hata hiyo fulana.
Taratibu akiwa katika kujikunyata akaichukua simu yake akaingia katika orodha ya majina akaligusa jina la Clara, akabonyeza kitufe cha kupiga simu ikaanza kuita iliita mara tatu ikapokelewa.
“Nani wewe??” sauti ile ilihoji.
“Aaah!! Jamani si tunasalimiana kwanza au??”
“Bwana eeh!! Sema wewe nani??” ilitoa karipio sauti ile iliyokuwa katika usingizi.
“Hassani hapa…”
“Yupi?”
“Tembo…”
“Aaah!! Jamani Tembo samahani jamani….nisamehe bure miee” sauti ya Clara ikabadilika ikawa katika kubembeleza. Tembo akakenua meno.
“Usijali nimeona kuondoka kimya kimya sio ishu….nipo hapa Mwanza kesho naweza kuondoka kurejea Dar es salaam….”
“Jamani Tembo wewe tabia mbaya upo wapi kwani njoo basi kwangu walau nikuone tu”
Tembo aliunda tabasamu jingine maridhawa kisha akamuuliza Clara ni wapi anapoishi.
“Huku panaitwa Nyamalango sijui unapajua. Karibu na chuo kikuu cha mtakatifu Augustino”
“Hapana nielekeze labda naweza kuja”
Clara akamuelekeza Tembo, hadi akaelewa.
Akabaki kusubiri kama atakuja ama laa.

Ile hali ya Clara kuzungumza na Tembo ilimsababisha ajikute akizifikiria simulizi baadhi za Tembo ambazo amewahi kuzisoma. Nyingi zikiwa za mapenzi motomoto. Ile baridi ikaamsha mshawasha katika mwili wa Clara, kifua chake kipana kikaanza kuwasha alijaribu kuzikuna nyonyo zake lakini haikusaidia kitu alikuwa anazifanya zizidi kuwasha. Mwili ukawa unamsisimka bila kujua sababu haikuwa kawaida yake kabisa kukumbwa na hali kama hii. Baridi likazidi kujikusanya na kuutesa mwili wake. Alikuwa peke yake kitandani.
Mara simu ikaita hakutaka kuipuuzia alipokea. Alikuwa ni Hassan Tembo tayari akiwa maeneo jirani na chumba cha Clara.
“Nakuja bab….aaa!! Hassan” alijiumauma Clara huku ule muwasho ukizidi.
Muwasho ulihitaji mkunaji!!!
Haya yalikuwa maajabu ambayo hakuwahi kuyapata hapo zamani. Kuzungumza na mtu kwenye simu kisha anakuwa katika hali ile???
Ilistaajabisha!!

**BEATY… Kaachwa njia panda asijue la kufanya….. nini kitajiri upande wa Beaty…
**Ni zamu ya Clara sasa… anawashwa kunako na anahitaji mkunaji… Tembo ndani ya jiji la Mwanza
 
SEHEMU YA 8


****

KITU cha kwanza baada ya Tembo kuingia katika chumba cha Clara. Binti alilalamika kuwa ana kiu ya kumsikiliza Tembo akimsimulia mojawapo ya hadithi zake za mapenzi. Tembo akatabasamu kisha akamtazama Clara usoni, akamkazia macho kwa sekunde kadhaa, macho ya Clara yalikuwa yamejirembua tayari, lakini ile kutazamwa na Tembo yalikaribia kufumba kabisa, Clara akajikuta anachukua kidole chake kimoja na kukitumbukiza mdomoni akaanza kukimung’unya kama pipi.
Tembo akajikoholesha, macho ya Clara yakafumbuka. Tembo alitaka kumkabili binti yule pale kitandani lakini alikuwa ana hofu moyoni mwake.
“Nisogee ama utanisikia nikiwa nasimulia nikiwa huku!!” Tembo akauingiza mtego.
Clara naye akatumia nafasi ile kujifaidisha.
“Hassan!! Usiku huu bwana…sogea unisimulie nifaidike mwenyewe!! Peke yangu yaani…” alijibu kwa sauti nyororo. Tembo akajikuta anatabasamu tena, akasimama na kuelekea mahali alipokuwa ameketi Clara.
Kitandani kwake!!
Tembo akachukua simu yake akafungua sehemu ya picha, akaitafuta ile picha ya Clara kutoka facebook akiwa amemkumbatia mpoenzi wake na kisha kujisifu kuwa anampenda sana. Tembo akaamua kumchokonoa.
“Mumeo akinikuta humu si itakuwa msala?”
“Tembo ulihudhuria ndoa yangu ama…. Please!! Mi nd’o mwenye hiki chumba na nimekukaribisha….” Alijibu Clara huku akionyesha kukereka na wasiwasi wa Tembo. Lakini wakati huo huo aliushangaa moyo wake!!
Deniss alikuwa kila kitu katika maisha yake, alikuwa rafiki, mpenzi na mume mtarajiwa!! Hakuwahi kutarajia kuwa ipo siku atakutanisha macho yake na kisha kuanguka katika hisia na mwanaume mwingine, lakini sasa amenasa kwa Tembo. Hawana hata saa zima tangu waonane lakini mwili wa Clara umechemka, unawasha na unahitaji huduma.
Kazi kwelikweli!!
Hassan akiwa pembeni ya Clara alianza kusimulia simulizi yake moja ambayo aliiba kutoka lugha ya kiingereza na kuileta katika Kiswahili. Hata kabla hajafika mbali Clara akaingilia kati.
“Mhh!! We Hassani wewe mjanja kuna mahali unasoma, ndio kuna mahali unasoma nd’o unanisimulia….” Clara alilalamika ilhali kiuhalisia kabisa Tembo hakuwa akisoma mahali popote.
“Aaah!! Wala sisomi Clara..”
 
SEHEMU YA 9



“Kama kweli hausomi ngoja nikubambe sasa…” clara akasimama na kupiga hatua kuiendea swichi ya kuzima na kuwa sha taa, wakati anatembea, upesi Tembo akamtazama na kubaini kuwa Clara alikuwa ameumbika haswa!! Na mbaya zaidi alikuwa amevaa kanga moja tu!!
Wanawake!!!!
Clara akaizima taa, kwamba Tembo asimulie wakati wakiwa gizani.
Ile simulizi ikabadilika baada ya Clara kurejea pale kitandani…. Ilikuwa ni simulizi ya binti wa kitajiri alivyoangukia katika penzi la mtoto wa kimaskini. Vikwazo vingi vikataka kuliua penzi lao lakini uimara wao ukalisimamisha tena…..
Kadri Tembo alivyosimulia Clara naye akazidi kuwashwa….
Unawashwa halafu hausemi!! Clara usiwe mjinga, usiwe mjinga!! Sauti ya ndani ikamwambia Clara…
Kweli akajiona mjinga sana, akamwangukia Tembo huku akiitoa kanga yake mwilini. Kanga ikaanguka, akavua na blauzi yake.
Na hapo likamtoka neno moja
“TEMBO NIKUNE!!”
Clara alikuwa katika hisia ambazo hajawahi kuzipata maishani akiwa na mwanaume yeyote yule
Hisia kali za kimapenzi!!!

Bila kujijua labda ama kwa kuzidiwa na hisia Clara alijikuta akiuvaa uhusika wa yule binti wa kwenye simulizi aliyeitwa Sarah akamkumbatia Hassan kwa nguvu sana, Hassan naye akajikuta amevaa uhusika wa yule mtoto wa kimaskini wa kwenye simulizi aliyekuwa na jina la George. Clara akajikuta anatokwa na machozi, machozi hayo yakatambaa katika mabega ya Hassan, mara bila kunong'onezana wakajikuta wanatazamana, kila jicho lilikuwa kama aidha linaanza kuupata uhai ama linaupoteza uhai wake, Clara na Tembo walikuwa katika hali ya mahaba. Maajabu kweli!!! Mahaba ya siku moja tena dakika kadhaa!! Ilikuwa inashangaza.

Tembo akawa wa kwanza kuusogeza mdomo wake katika shavu la Clara lakini ghafla Clara kama vile kuna ugomvi alikwepesha shavu na kuziruhusu papi za mdomo wake zichukue hadhi hiyo. Papi zilipokutana na ndimi zikachomoza zikaanza kugombana kwa sekunde kadhaa kabla ya kuachana bila kuachanishwa. Ni wakati huo ambao ndimi zilikuwa katika ugomvi wa kusisimua ndio Tembo alipata nafasi ya kuzitomasa chuchu nzuri kubwa zilizojaa vyema kifuani mwa za Clara.
Mpapaso huo wa Hassan Tembo ukazua kizaa zaa sasa walikuwa wameachiana lakini Clara alikuwa katika muwasho wa aina yake na sasa alihitaji kukunwa, na kweli alihitaji kukunwa sio kwa kutumia gunzi ama kucha zake yeye mwenyewe maana kweli alitegemea kucha zake zitakidhi haja lakini zilikuwa zimeshindwa. Clara akamtumbulia Tembo jicho la haja, haja ya mapenzi. Tembo akalitambua hilo.
Mwanga ungeweza kuwa shuhuda pekee wa tukio hili la aina yake, lakini tayari Clara alishaufukuza mwanga chumbani. Basi giza likabaki kutazama yatokeayo, uzuri wa giza ni kwamba likiona mambo halimwambii mtu yeyote!!.
 
SEHEMU YA 10


Kitanda kikatwaliwa na watu wawili, chaga zikahimili uzito na sasa ulikuwa unasubiriwa ujasiri wa hizi hizi chaga kuwazuia wawili hawa wasiangukie uvunguni iwapo wataanza kutingishika!!!
Kweli wakaanza kutingishika kwa fujo!!
Zilifanikiwa kuhimili na zilistahili pongezi.

Asubuhi sana Tembo alikuwa yupo macho siku hii ilikuwa ni jumatatu hiyo ikimaanisha kuwa jumapili Clara na Tembo walikesha. Clara alipoamka Tembo alikuwa ameoga na kuvaa tayari kwa kuondoka. Clara alimwonea Tembo aibu lakini Tembo alijidai hajalishtukia hilo akazuga kuchangamka, hatimaye Clara naye akawa na furaha akaungana na Tembo kufurahia madhambi waliyofanya usiku uliopita
Laiti kama Clara angejua madhara ambayo yangetokea baada ya tukio hili, hakika asingemkaribisha Tembo chumbani kwake na kulala naye kama wapenzi wa siku nyingi!!!
Hilo lilikuwa kosa kubwa lililoyabadili maisha yake!!

****

Wiki nzima ilikuwa inakamilishwa na siku hii ya jumapili, siku hii ilikuwa ya saba tangu Clara alale na Tembo bila Deniss ambaye ni mpenzi wake kushtukia mchezo huu. Chaga za kitanda zingekuwa na uwezo wa kusema zingekuwa za kwanza kumshtaki Clara kwa Deniss kwani zilikesha zikipiga mayowe siku hiyo ya tukio.

Siku hii ilianza kama jumapili nyingine, tofauti ilikuwa moja. Clara hakuwa na ari ya kwenda kanisani siku hiyo, basi hakutaka kujilazimisha akaghairisha kwenda, kingine ni kwamba alichelewa kuamka tofauti na kawaida, hilo halikumpa shida kwa kuwa hakuwa na mambo mengi ya kufanya hapo chumbani kwake. Saa nne kasorobo ilimkutia Clara akiwa bado kitandani alihisi njaa kwa mbali hilo pia halikumsumbua.
Mkojo ndo kitu ambacho baada ya kujizuia sana sasa alikuwa amesalimu amri alikuwa ameamua kwenda msalani.
Aliporejea ndo mkanda huu hapa ukaanza, ni kama simulizi na ilikuwa hivi. ….Clara alijirudisha tena kitandani kumalizia makombo ya usingizi wake, safari hii hakupata nafasi ya kusinzia akaanza kupata muwasho kwa mbali sana, muwasho huu katika ncha za matiti yake ulikuwa mtamu na wa kipekee, alikuna kwa pozi huku akiviringisha viringisha katika viganja vyake ncha za chuchu zake, hali kama ile ikatambaa hadi katikati ya miguu na penyewe alisogeza kidole kimoja mara viwili hatimaye vitatu mwasho ulikuwa umeongezeka.
 
SEHEMU YA 11


Alizidi kujikuna kwa juhudi zote lakini ikashindikana, Clara alitaka kuusingizia ugonjwa wa U.T.I lakini alighailisha baada ya kugundua kitu flani cha tofauti, mara taratibu zikamvaa hisia za kufanya mapenzi, alijikuta katika hisia zilizomfanya Tembo ajilie vitu bila gharama yoyote. Clara alipalangana kuzishinda lakini ilishindikana. Deniss mpenzi wake alikuwa anasoma huko Dodoma, Tembo aliyekata kiu yake siku saba zilizopita tayari alikuwa Dar es Salaam, machozi ya uhitaji yakaanza kumtoka Clara, alikuwa anahitaji huduma kwa udi na uvumba!!!!
Muwasho ule haukujali kilio chake, ukazidi kumhangaisha!!
Clara akaanza kutetemeka mwili wake hasahasa sehemu za mapaja.
“Nini hiki jamani….nini hiki…” alilalamika akiwa anajiviringisha huku na kule pale kitandani.
Clara alikuwa anazidi kujifaragua huku na huko akihangaika mithili ya kuku anayetaka kutaga na mahali pake pa kutagia kuna kitu mithili ya kunguru. Hakujua atafanya nini. Alitamani kupiga kelele lakini kelele hizo zingesaidia nini?? Akagundua hazina maana akatulia akijaribu kujikaza. Lakini hakufanikiwa. Aliyaunganisha meno yake akayaumanisha kujaribu kupambana na hali ile lakini bado hali ilikuwa tete. Akarusha rusha miguu, akaikanyaga kanyaga shuka lakini wapi ilikuwa kazi bure!!!

Clara akajilazimisha kusimama akafanikiwa, akahisi kutetemeka, mikono yake ikawa inatetemeka, Hakuwa katika hali ya kuanguka lakini alikuwa kama mtoto mdogo anayejifunza kutembea akiwa katika hatua za awali kabisa. Hakujua anaelekea wapi lakini ni kama alikuwa anaufuata mlango, alipoufikia akakishusha kitasa ukafunguka, hakukumbuka kuufunga wakati anapiga hatua moja baada ya nyingine kutoka nje. Alipofika nje alitazama huku na huko akavutiwa na mlango uliokuwa nusu wazi nusu umefungwa, akili yake ikamwagiza kwa amri kali kuufuata mlango ule, akajikongoja sasa alikuwa kama bibi kizee kwa jinsi alivyoukunja uso wake, alipoufikia mlango alijifikiria kwa nusu dakika, alitaka kubisha hodi lakini akahisi anachelewa. Akausukuma na kuzama ndani.
KILICHOTOKEA HUKO!!!!...........

Usikose tena kesho asubuhi mwendelezo wa simulizi hii…..
TOA MAONI YAKO……
 
Nishaliamsha dude................... kazi kwenu


 
Back
Top Bottom