Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 26
"Asalaam Aleykum" sauti yenye ukarimu ya kijana Hassan Tembo ilimjulia hali Rehema.
"Aaleykum-salaam" Alijibu kwa nidhamu ya hali ya juu kwa lafudhi nzuri ya kiswahili iliyochanganyikana na upemba na uarabu kwa mbali. Sauti hiyo ikampa ladha Fulani Tembo, akatoa tabasamu hafifu.
“Khaifa….” Tembo akaupima ujuzi wa Rehema kama alikuwa kweli ameiva kidini ama alikuwa anarashia rashia. Rehema akashindwa kujibu, Tembo akajipa majibu yake kichwani.
Robert alimtanguliza Tembo akaifikia sofa nyekundu iliyoanza kupoteza ubora wake wa awali. Laiti kama kingekuwa kipindi cha nyuma basi huenda sofa hii ingekuwa ya kuitazama mara mbili. Huenda aliinunua kwa mtu ambaye alikuwa ameanza kuichoka au alikuwa katika kununua sofa nyingine akaamua kuiuza hii.
"Roby mambo?!"
"Poa ndugu za siku kadhaa, hatuonani" Rehema hakujibu badala yake akacheka kwa kujilazimisha. Sura yake ilitangaza dhiki ya hali ya juu.
“Naona upo na mtu mkubwa sana kama shehe vile, kaka umependeza sio siri” Rehema alimsifia Hassan kupitia mazungunmzo yake na Robert.
“Huyu Mufti kabisa mbona…” Roby alikolezea kikatoka kicheko kidogo kutoka kwa Rehema, safari hii aliufumbua mdomo wake, Tembo akauona mwanya. Moyo ukamdunda sana kana kwamba ameona kitu cha kutisha ama kushangaza sana.
"Kaka unatumia kinywaji gani?" Rehema alimuhoji Tembo huku akiwa wima wima, akajibiwa kwa kichwa. Tembo hakuhitaji kinywaji.
“Jamani kaka, hata maji tu…”
Anazuga huyu hana pesa wala nini! Tembo aliwaza kisha akausimamia msimamo wake ili asije kumwaibisha Rehema.
"Mimi niletee maji yanatosha" Robert aliomba. Rehema akatoka nje, Tembo hakuona dalili ya pesa katka mikono ya Rehema.
Akaduwaa!
"Oya kaka, mzigo wenyewe ndo huo hapo sasa,..ona!" Robert alimnong'oneza Tembo. Tembo hakujibu kitu zaidi ya kuitazama subwoofer iliyoketi kipweke katika stuli ndogo yenye mguu mmoja mbovu. Ilikuwa inavutia sana, lakini kwa Tembo ilivutia zaidi, sio kuwa hakuwa na uwezo wa kununua mpya tena yenye ubora kupita ile bali aliiona kama vile ni chambo ya kumnasa Rehema. Tayari Hassan Tembo alikuwa amevutiwa na mwanya wa Rehema pamoja na ile mitikisiko aliyoishuhudia ikipenyeza kutoka katika kanga moja nyepesi.
Kabla Tembo hajajibu lolote, aliingia msichana mwingine bila kugonga mlango. Bila shaka yalikuwa ni mazoea yake kufanya hivyo!!
Au huenda alijisahau!! Nani anajua?
"Rehema yuko wapi?" Aliuliza kibabe huku akiwa amekunja ndita. Hakuna aliyemjibu bila shaka wote walikuwa wamekereka na kitendo hicho cha kuingia bila hodi pale ndani halafu mbaya zaidi hata salamu pekee hakukumbuka pia!!!
"Asalaam Aleykum" sauti yenye ukarimu ya kijana Hassan Tembo ilimjulia hali Rehema.
"Aaleykum-salaam" Alijibu kwa nidhamu ya hali ya juu kwa lafudhi nzuri ya kiswahili iliyochanganyikana na upemba na uarabu kwa mbali. Sauti hiyo ikampa ladha Fulani Tembo, akatoa tabasamu hafifu.
“Khaifa….” Tembo akaupima ujuzi wa Rehema kama alikuwa kweli ameiva kidini ama alikuwa anarashia rashia. Rehema akashindwa kujibu, Tembo akajipa majibu yake kichwani.
Robert alimtanguliza Tembo akaifikia sofa nyekundu iliyoanza kupoteza ubora wake wa awali. Laiti kama kingekuwa kipindi cha nyuma basi huenda sofa hii ingekuwa ya kuitazama mara mbili. Huenda aliinunua kwa mtu ambaye alikuwa ameanza kuichoka au alikuwa katika kununua sofa nyingine akaamua kuiuza hii.
"Roby mambo?!"
"Poa ndugu za siku kadhaa, hatuonani" Rehema hakujibu badala yake akacheka kwa kujilazimisha. Sura yake ilitangaza dhiki ya hali ya juu.
“Naona upo na mtu mkubwa sana kama shehe vile, kaka umependeza sio siri” Rehema alimsifia Hassan kupitia mazungunmzo yake na Robert.
“Huyu Mufti kabisa mbona…” Roby alikolezea kikatoka kicheko kidogo kutoka kwa Rehema, safari hii aliufumbua mdomo wake, Tembo akauona mwanya. Moyo ukamdunda sana kana kwamba ameona kitu cha kutisha ama kushangaza sana.
"Kaka unatumia kinywaji gani?" Rehema alimuhoji Tembo huku akiwa wima wima, akajibiwa kwa kichwa. Tembo hakuhitaji kinywaji.
“Jamani kaka, hata maji tu…”
Anazuga huyu hana pesa wala nini! Tembo aliwaza kisha akausimamia msimamo wake ili asije kumwaibisha Rehema.
"Mimi niletee maji yanatosha" Robert aliomba. Rehema akatoka nje, Tembo hakuona dalili ya pesa katka mikono ya Rehema.
Akaduwaa!
"Oya kaka, mzigo wenyewe ndo huo hapo sasa,..ona!" Robert alimnong'oneza Tembo. Tembo hakujibu kitu zaidi ya kuitazama subwoofer iliyoketi kipweke katika stuli ndogo yenye mguu mmoja mbovu. Ilikuwa inavutia sana, lakini kwa Tembo ilivutia zaidi, sio kuwa hakuwa na uwezo wa kununua mpya tena yenye ubora kupita ile bali aliiona kama vile ni chambo ya kumnasa Rehema. Tayari Hassan Tembo alikuwa amevutiwa na mwanya wa Rehema pamoja na ile mitikisiko aliyoishuhudia ikipenyeza kutoka katika kanga moja nyepesi.
Kabla Tembo hajajibu lolote, aliingia msichana mwingine bila kugonga mlango. Bila shaka yalikuwa ni mazoea yake kufanya hivyo!!
Au huenda alijisahau!! Nani anajua?
"Rehema yuko wapi?" Aliuliza kibabe huku akiwa amekunja ndita. Hakuna aliyemjibu bila shaka wote walikuwa wamekereka na kitendo hicho cha kuingia bila hodi pale ndani halafu mbaya zaidi hata salamu pekee hakukumbuka pia!!!