CHANGE
Story by Elton Tonny
Urafiki, Familia, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Ukatili, Mauaji, Mambo yasiyotazamiwa, Mambo yenye kuhofisha
R-rated 18+
Enjoy!
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
SEHEMU YA THELATHINI
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
Tayari Namouih alikuwa amemaliza kushughulika na mambo mengi ya kikazi ilipofika mida ya saa nane mchana, na hakuwa amepumzika mpaka muda huo hata mara moja. Blandina alikuwa pamoja naye kumsaidia, na baadhi ya watu walihitaji huduma ya mwanasheria mkuu walipatiwa tarehe za kupewa suluhu zao walizohitaji na wengine kukabidhiwa kwa wanasheria wengine ndani ya kampuni hiyo kwa sababu hangeweza kushughulika nao wote kwa kipindi kifupi sana cha wakati. Ingawa Blandina alikuwa mkono muhimu sana wa Namouih katika kazi, zamu hii Namouih hakujihisi amani ya asilimia zote kuwa naye sambamba kutokana na kujua alimfanyia unafiki. Na tangu walipoagana jana na mpenzi wa rafiki yake, Namouih hakuwa amemtafuta Draxton wala Draxton kumtafuta yeye. Ilikuwa wazi kwamba wote walifanya mambo kwa umakini, ingawa Namouih hakudhani ikiwa mwanaume yule alijua kwamba mume wake amerudi.
Basi, imefika mida ya saa tisa, Namouih akamwambia Blandina kwamba sasa ndiyo anakwenda kule alikopanga kwenda leo, na bila shaka hangechelewa kurudi. Blandina alikuwa anataka watoke wote kama huko alikotaka kwenda ilikuwa ni kwenda kupata chakula lakini Namouih akasema haikuwa hivyo, bali alipanga kukutana na mtu fulani wa muhimu. Blandina akawa anataka kujua ni nani, ila Namouih akamjibu kwa njia ya kejeli kwamba ni siri na hangetakiwa kumwambia yeyote. Blandina mdada wa watu aliachwa gizani kabisa, naye akamwambia rafiki yake awe na safari njema na asichelewe kurudi ili wajumuike pamoja baadaye kule walikopenda kukaa kupata vinywaji kama kawaida yao, ingawa mara ya mwisho Blandina alipigwa kwa chupa huko.
Mwanasheria mrembo sana Namouih akaondoka kutoka kwenye kampuni hiyo, na sasa akawa mwendoni kuelekea kule msituni bila ya kuwasiliana na Draxton hata mara moja. Alijua tu kwamba ni lazima mwanaume huyo angekuwa huko, hivyo kufika kwake tu kulitosha maana alielewana naye kutokea usiku wa jana. Lakini pia akikumbukia kwamba asubuhi hii mume wake alikuwa ameishika simu yake, Namouih alihisi kwamba huenda Efraim alikuwa amefanya kitu fulani, labda kuweka mfumo wa ufatiliaji kwenye simu yake wa kukamata sms au vinginevyo, lakini hakudhani sana kwamba hiyo ilikuwa ndiyo ukweli wa mambo, na kuona kama ni yeye tu ndiyo alikuwa akepandwa na presha kutokana na aliyofanya. Hivyo akamtumia ujumbe mume wake akisema kwamba alikuwa amekwenda kuonana na yule rafiki yake daktari, yaani Salome, kama njia ya kujihami mapema. Hangetambua namna alivyokuwa anajipeleka katika hatari ya kuukamatisha mchezo wake na Draxton, kwa sababu gari lake lilikuwa limewekewa kifaa cha ufatiliaji, na mpaka sasa mume wake alikuwa akitazama kule ambako mke wake alikuwa akielekea akiwa kule kule kazini kwake!
Mwanamke huyu akafanikiwa kufika huko msituni kwa kuwa mwangalifu sana ili kuhakikisha hakuna yeyote aliyemfatilia, naye akalikuta gari la Draxton nje ya ile nyumba yake. Aliingiwa na msisimko mzuri sana kwa kutazamia mengi, naye akashuka na kuanza kuelekea upande wa mbele. Sehemu ya ardhi kuizunguka nyumba ilikuwa imesafishwa vizuri kutokana na uchafu mwingi uliosababishwa na mvua iliyoonyesha siku ya jana, na hata sasa wingu la mvua lilikuwa limeanza kutanda angani. Namouih akaenda moja kwa moja mpaka sehemu ya mlangoni na kuingia ndani, naye akatabasamu kwa furaha baada ya kukuta aina fulani ya mazingira ambayo hakuwa ametarajia.
Sehemu hiyo ya sebule ilikuwa imeachwa nafasi pana kwa masofa na meza kusogezwa pembeni zaidi kwenye usawa wa madirisha, na chini hapo katikati aliketi Draxton huku akimtazama mwanamke huyu kwa njia ya kawaida tu. Alikuwa amekaa kwenye kitu kama zulia (carpet) nene sana jekundu, lililokuwa na muundo kama godoro laini, na katikati kulikuwa na vyombo kadhaa vilivyofunikwa; bila shaka kukiwa na chakula kwa ndani. Namouih alipendezwa sana na jambo hilo, kwa sababu ilikuwa ni kama Draxton ameandaa mlo wa pekee kwa ajili yao, kwa njia fulani ya wapendanao. Mwanaume huyo akamwonyesha kwa ishara ya macho kuwa akaribie hapo, na Namouih akaanza kuelekea sehemu hiyo taratibu na kuchuchumaa, kisha akavua viatu vyake na kuketi huku anatabasamu kwa hisia.
"Hii yote ni nini?" Namouih akauliza kwa sauti ya chini bila kumwangalia usoni.
"Lunch," Draxton akajibu.
"Mmmm..."
"Yeah. Nimetimiza ahadi yangu," Draxton akasema.
"Ahahah... Ingekuwa vizuri kama ningekuona ulivyopika kabisa. Au hujapika?"
"Nimepika."
"Mmmm... kweli? Siyo kwamba umenunua halafu unazuga tu hapa?"
"Ni ngumu sana kukushawishi mpaka uuone ushahidi eti?"
"Ndiyo."
"Nimeungua hapa hivi wakati nakaanga nyanya," Draxton akasema hivyo huku akimwonyesha mkono wake usiokuwa na alama yoyote.
"Em' kwenda huko!" Namouih akasema hivyo, na wawili hawa wakacheka pamoja.
Ukafata utizami fulani mzuri sana baina yao, kisha Draxton akasema, "Karibu Namouih."
"Asante," Namouih akajibu kwa sauti nyororo.
Draxton akanyanyuka na kuvuta jagi lenye maji na kibeseni kidogo, naye akamsogelea ili aanze kumnawisha mwanamke huyu kiganja chake. "Samahani ila huwa situmii vijiko hapa," akamwambia.
Namouih akatabasamu na kusema, "Usijali. Napenda kula kwa mikono pia."
Wakaendelea kuangaliana kwa sekunde chache, kisha mwanaume akaanza kumnawisha mkono. Namouih akawa anayaangalia macho ya Draxton kwa upendezi mwingi mno, na baada ya kumaliza kumnawisha Namouih, mwanaume huyo akachukua taulo ndogo na safi iliyokuwa pembeni na kuanza kuufuta mkono wa Namouih taratibu. Wakati Draxton anafanya hivi, Namouih akawa ametambua kwamba mwanaume huyu alikuwa anafanya mambo taratibu akiwa karibu yake ili aivute vyema harufu yake ambayo alionyesha kuipenda mara nyingi sana, na jambo hilo likampa Namouih hisi ya kujidai. Draxton akamaliza kumfuta na kurudi upande wake ili aketi, kisha akamwambia Namouih ajisikie huru kufunua na kujichukulia chakula.
Namouih akawa anatabasamu tu na kuanza kufunua vyakula, na kiukweli alivutiwa sana na mapishi ya Draxton kwa kuvuta harufu nzuri sana iliyotokana navyo. Kulikuwa na nyama za kukaangwa, kupikwa, chips kavu, wali kiasi, na dagaa fulani wa baharini waliokaangwa pia (dagaa mchele). Draxton alikuwa amenunua na mtindi mweupe pakti mbili pia, hivyo akampatia Namouih moja, nao wakaanza kula taratibu. Namouih alimtania sana Draxton kwa kusema hajui kupika, naye Draxton akawa anacheka tu kwa sababu jinsi Namouih alivyokichangamkia chakula ilipingana na kauli zake za kimasihara kukielekea. Kiukweli Namouih alikifurahia sana chakula cha Draxton, na wawili hawa wakaendelea kula taratibu huku wakiongelea masuala ya kazi. Ilikuwa ni kama hawakutaka kuzungumza kuhusu jambo lao lile, lakini akili zao kwa pamoja zililifikiria sana na kufanya iwe ni kama wanasubirishiana.
Namouih akawa ameshiba kwanza, na Draxton alipotaka kumnawisha mkono, akakataa, akimwambia amalize kula chake kwanza, na yeye angenawa mwenyewe. Akaanza kunawa huku anamwangalia kwa macho yenye upendezi sana, kisha akajifuta mikono na kukaa sawa tena. Draxton akamalizia kula na kutaka kuvuta jagi lenye maji ili anawe, lakini Namouih akajinyanyua na kulichukua jagi kisha kupiga magoti karibu yake, akionyesha kwamba anataka kumnawisha, lakini Draxton akawa anamwambia hiyo si sahihi kwa kuwa Namouih alikuwa mgeni hapo. Akawa anasisitiza kwamba angenawa yeye mwenyewe, lakini Namouih akaweka uso wa kununa huku akimwangalia kwa njia hiyo ya kudeka, naye Draxton akaweka mikono yake mbele ili anawishwe kwa kutotaka kumuudhi mtoto. Namouih akaanza kumnawisha huku akiangalia chini na kuibana midomo yake kwa njia ya shau, naye Draxton akawa anautathmini tu urembo wake.
Namouih alipomaliza kumnawisha, akatoa na kuweka vyombo vyote pembeni, kisha akaketi tena chini hapo; wakati huu akiwa karibu zaidi na Draxton. "Asante kwa chakula kizuri sana Max," akamwambia huku akimwangalia kwa hisia.
"Oooh sa'hivi ndiyo kimekuwa kizuri eh?" Draxton akauliza.
Namouih akacheka kidogo, kisha akasema, "Tokea mwanzo. Una style nzuri sana."
"Siyo kama wewe. Chako ni kitamu kupitiliza," Draxton akamwambia.
"Ulishawahi kula chakula changu?"
"Umeshahau mara ya kwanza nimekuja kwako?"
"Aaaa... kweli! Eh... ahahahah... ni muda. Angalau sa'hivi wote tumejua ladha ya vyakula vyetu. Hata we' chako ni kitamu mno yaani, siwezi kuacha kusifia," Namouih akasema.
"Ahah... asante. Natamani tu kama... all of this would've been on a different note."
"Unamaanisha kwamba...?"
"Kama tu ulivyoniambia siku ile. Huwa nawaza pia... ingekuwa vipi kama mimi na wewe tungekutana chini ya hali tofauti na tulizonazo sasa," Draxton akasema.
Namouih akaanza kutembeza kiganja chake mkononi kwa Draxton taratibu, naye akasema, "Unahisi kuwa na majuto kwa sababu ya hili jambo linaloendelea baina yetu."
"Siyo rahisi Namouih... unajua... kutoka hapa... kurudi kwa Blandina na kuigiza kana kwamba mambo yako shwari... ina...."
"Inakufanya ujione kama mtu anayetia kinyaa sana. Kutoka na rafiki ya mpenzi wako..."
"No, Namouih, sijamaanisha hivyo. Unaelewa tu kwamba... kwamba..."
"Ninaelewa Max, usijali. Lakini mimi.... sijui ni kwa nini ila ni kama hisia hizo naziweka tu pembeni kwanza na kuamua kufurahia wakati huu pamoja nawe... hivyo yaani," Namouih akamwambia hivyo na kukishika kifua cha Draxton.
"I don't know Namouih. Bado nahisi kama utaumia sana kwa sababu ya haya yote," Draxton akasema.
"Mhm... napenda sana unavyoonyesha kunijali. Unajua... Blandina ameniambia jinsi mlivyokuwa wote jana," Namouih akasema.
Draxton akamwangalia kwa njia ya kuelewa kile alichomaanisha.
"Ni jambo zuri kwamba angalau umemtuliza kidogo... ijapokuwa bado anakuhitaji. Usiwaze kuhusu mimi kuumia kwa sababu hata mimi pia nakuwa narudi kwa mume wangu... ni jambo zito... lakini Max... bado ninataka kuendelea kuwa nawe... haitajalisha kama ni kwa kipindi kifupi cha kukusaidia wala nini... I just wanna be here... with you," Namouih akasema kwa hisia.
"Kwa nini imegeuka kuwa namna hii Namouih? Kwa nini... kwa nini ilipaswa kuwa wewe?" Draxton akauliza.
Namouih akakipandisha kiganja chake mpaka shingoni kwa Draxton na kusema, "Kwa sababu umeshanipenda Max."
Draxton akaangalia chini kidogo.
"Unakumbuka ulichoniambia jana?" Namouih akauliza.
Draxton akamtazama.
"Ulinishika ghafla halafu... ukasema 'I love you.' Ahah... nataka kujua ikiwa ilikuwa ni akili yako au ya upande wa pili iliyosema hivyo Max..." Namouih akasema.
"Ni... haikuwa akili Namouih. Nafikiri kuna kitu tu kutoka hapa... kilichonisukuma kusema hayo maneno," Draxton akamwambia huku akijinyooshea kidole usawa wa moyo wake.
Namouih akatabasamu kwa hisia sana, naye akamwinamia karibu zaidi na uso wake kama anaelekea kumbusu.
Draxton akafumba macho na kuivuta harufu tamu ya bibie kwa hisia, kisha akasema, "Uhakika ulio nao... unanivutia. Ila tu wazo la mume wako likija akilini naona...."
"Efraim hajawahi kunipa kile nilichokipata kutoka kwako Max... hata mara moja," Namouih akasema.
"Nini?" Draxton akauliza kwa sauti ya chini.
"Toka amenioa... hatujawahi," Namouih akamwambia.
"Kwa nini?" Draxton akauliza.
"Sijui. Hanipi sababu kila mara nikijaribu kumwomba tushiriki... iko tu kama jinsi ilivyo kwako na Blandina, lakini si kama yeye ana tatizo kubwa namna ilivyo kwako... ni kama tu hataki," Namouih akasema.
Draxton akabaki kumtazama tu kwa hisia.
"Imepita miaka zaidi ya sita Max... miaka sita bila ya mimi kufanya tulichofanya jana... na ninaweza kusema ni moja ya penzi ambalo sijawahi kupewa na mwanaume yeyote... kwa sababu wewe siyo wa nchi hii," Namouih akasema.
Draxton akatabasamu, naye Namouih akacheka kidogo.
"Kwa hiyo... mume wako anakuacha tu... kama mimi navyofanya kwa Blandina?" Draxton akauliza.
"Angalau unaweza hata kumpa Blandina kidogo Max... Efraim hanigusi kabisa. Huwa inanivunja sana moyo kwa sababu sielewi ana maana gani... ndiyo maana ninathamini sana unachofanya kwa ajili yangu..."
"Hapana Namouih... wewe ndiyo unanisaidia mimi... na inaumiza tu fikira kwamba mambo mengi yako kwa mvurugo lakini ninathamini sana ulichofanya kwa ajili yangu. Natamani hali zingekuwa tofauti... ila kwa sababu unataka kuendelea kunisaidia ingawa kuna vizuizi, nitajitahidi pia kukupa unachohitaji. Ila unapaswa tu kukumbuka kwamba...."
Namouih akamkatisha Draxton kwa kukifata kinywa kumbusu moja kwa moja kwa hisia sana, kisha akauachia mdomo wake na kusema kwa sauti yenye deko, "Achana na mawazo hayo... ninahitaji tu penzi lako Max."
"Namouih..." Draxton akaita kwa sauti ya chini huku akikishika kiuno chake.
"Please.... nimeshalemewa mno... siwezi tena kusubiri..." Namouih akaongea kwa sauti yenye deko na hamu kubwa sana.
Wawili hawa walikuwa wamekaribiana sana, Draxton akiwa amekaa kwa kuitandaza miguu chini, na Namouih akiwa ameketi katikati yake huku akiishika shingo ya jamaa na nyuso zao zikiwa karibu mno. Ingawa bado Draxton hakujiamini vya kutosha, alikumbuka vizuri kuwa upande wake wa pili ulivutiwa na Namouih, na hivyo yeye alichotakiwa kufanya ilikuwa kumwamini mwanamke huyu ili asitawaliwe na fikira za kumuumiza na hivyo afanikiwe kumpatia penzi kwa kujiendesha vyema. Aliuhitaji sana msaada huu kutoka kwa Namouih, lakini haikuwa tu kwa sababu ya msaada, alikuwa anahitaji pia penzi la mwanamke huyu mrembo.
(........).
Namouih akauachia mdomo wa Draxton taratibu na kumwangalia, na sasa mwanaume huyu alikuwa ameinamisha uso wake kidogo huku amefumba macho yake. Namouih hangehitaji kumwambia la kufanya, kwa sababu aliona tayari Draxton alikuwa akilifanya, yaani, kuuacha upande wake wa pili utoke. Nywele za Draxton zikaanza kukua na kuwa nyeupe, hata ngozi yake pia, kisha akafumbua macho yake na kumtazama Namouih usoni. Yalikuwa yale macho ya blue, lakini wakati huu hakumtazama mwanamke huyo kwa njia ya kinyama, bali ilikuwa kwa njia yenye umakini wa kawaida. Kuanzia hapo, Namouih akawa ametambua kwamba mwanaume huyu alikuwa anajitahidi sana kujiendesha vyema, naye akaishika shingo yake tena na kutabasamu kidogo.
Sasa Draxton akawa katikati ya badiliko lake, na ilikuwa ni kama tayari upande huu ulikuwa umeshamzoea Namouih hasa baada ya kilichotokea siku ya jana baina yao, kwa hiyo akawa ametulia tu. Namouih akaanza kuifata tena midomo ya Draxton, lakini Mnyama-Draxton akamkwepa kiasi. Mwanamke akawa anamwangalia kwa kushangaa kidogo, naye Draxton akafungua kinywa chake kumwonyesha meno kwa njia iliyomwambia Namouih kwamba alikuwa anakwepa kumbusu kinywani kwa kuhofia kumuumiza kwa yale meno yake makali, kitu kilichomfanya Namouih atambue kwamba upande huu ulionyesha hisia ya kumjali kwa mara nyingine tena. Lakini kama jana waliweza kupeana mapenzi bila Namouih kuumia sana, mwanamke huyu alitaka kumhakikishia kwamba hakuhitaji kuhofia hilo, hivyo akamsogelea mdomoni zaidi na kusema kwa kunon'goneza, "Trust me."
Draxton akatulia, kisha Namouih akamfata mdomoni tena na kumbusu mara tatu. Mwanamke huyu alikuwa anajitahidi kupeleka mambo taratibu, lakini tayari Draxton alikuwa amezidiwa na hisia za kimahaba zenye nguvu zaidi akiwa namna hiyo, hivyo ghafla akakishika kiuno cha Namouih na kukiminya kwa nguvu, kitu kilichomuumiza sana Namouih kutokana na makucha marefu ya jamaa kumkandamiza. Akatoa sauti ya kuumia kidogo, kisha naye akamkandamiza Draxton kwa makucha yake marefu ya urembo shingoni kwake, lakini haikuonekana kama Draxton aliumia. Namouih akawa anamwangalia kwa uso ulioonyesha maumivu kiasi, na ndiyo Draxton akaacha kukikandamiza kiuno chake polepole.
Namouih akajirudisha nyuma taratibu na kugeuza mwili wake pembeni kujituliza kwa sababu hakuwa ametarajia jambo hilo tofauti na ilivyokuwa jana, na katikati ya sekunde chache alizogeuka ili kutuliza maumivu, akahisi pumzi za moto za Draxton nyuma ya shingo yake, na hapo hapo nguo yake ikachanwa kutokea mgongoni! Alishtuka, lakini hakuwa hata na muda wa kujisawazisha na tayari Draxton akawa ameushika mwili wake na kuuvuta karibu naye kwa nguvu; yaani Namouih akiwa amempa mgongo kwa ukaribu sana, kisha mwana-mnyama akaivuta nguo yake yote kwa fujo na kuirusha pembeni. Namouih alikuwa amesisimuliwa sana na jambo hilo, hata mawazo ya angevaa nini baada ya hapo hayakuingia akilini kabisa, na sasa akawa amebaki na sidiria nyeupe na chupi laini nyeupe pia.
Draxton akawa amekaa nyuma yake, akiwa ameishika shingo ya Namouih kama ameikaba kutokea nyuma na kumfanya mwanamke huyu aelekeze uso wake juu huku akipumua kimahaba, kisha mwanaume akaivuta sidiria hiyo na kuirusha pembeni pia. Namouih alikuwa amemwachia tu mwanaume huyo mwili wake autendee kwa njia aliyotaka, kwa sababu tayari moyo wake ulikuwa umeridhia aina ya penzi ambalo angelipata kutoka kwake. (........).
(........).
(........).
(........).
(........).
(........).
(........).
Namouih akacheka kidogo huku akipumua na kumwangalia kwa ulegevu, kisha akamwambia kwa kunong'oneza, "I want you inside of me Max."
Ilionekana kwamba Draxton akiwa katikati ya badiliko lake hakuweza kuzungumza kama mtu wa kawaida, lakini alichokisikia alikielewa. Baada tu ya Namouih kumwambia hivyo, mwanaume akararua T-shirt lake kwa mikono yake na kuivuta bukta yake yote mpaka ikachanika, na sasa yeye pia akawa mtupu mbele ya Namouih. (........). Ingawa hali hii ilikuwa mpya na tata, bado Namouih aliifurahia, na ndiyo maana alimwachia aendelee kumpa penzi kwa njia aliyoona kuwa sahihi. Kama ni kupewa mapenzi kwa njia ya mnyama, basi na yeye angetakiwa kujifunza kuyapokea kama mnyama tu.
(........).
(........).
Ilikuwa kama ndoto vile kwa Draxton. Ingawa alikuwa katikati ya badiliko lake, akili yake ilielewa vizuri kabisa kwamba jambo alilokuwa akilifanya ni jambo ambalo hakuwahi kufikiri angekuja kuweza kufanikiwa kufanya, na sasa alikuwa akilifanya kwa mara ya pili bila kupitiliza mpaka kuwa mnyama kabisa na hata kumuumiza mwanamke huyo sana. Yeye pia alifurahia mno joto la mwanamke huyu, na akili yake ilikubali kwamba alikuwa mtamu balaa!
(........).
(........).
Namouih akabaki kupumua kwa uchovu sana kama vile alikuwa ametoka kutua zigo zito mno, kisha Draxton akamvuta kidogo na kupiga magoti ili amwingie tena.
Namouih akanyanyua uso kilegevu na kusema, "Hapana... Max... that's enooough... hhh... you'll kill me!"
Draxton, akiwa mnyama pia, hakuelewa hii kauli, naye akaupiga mkono wa Namouih uliokuwa unataka kumzuia kuingia ndani tena na kisha akapenya ndani.
"Ahsss.... maamaahh...."
Namouih akalia kwa deko ya hali ya juu, kwa kuwa alielewa hapa habari yake ilikuwa imekwisha. Mwanaume hakutaka kumwacha hata kidogo, na kama wangeendelea hivyo kwa muda mrefu basi angechelewa sana kutoka hapo; tena akiwa hoi bin taaban.
(........).
(........). Hiyo ilikuwa ni ni safari ndefu, siyo mchezo!
Draxton akaiachia miguu ya Namouih na kujirudisha nyuma, akiwa ameitoa mashine yake ndani ya hekalu la mwanamke huyo na kubaki anapumua kwa nguvu. Namouih alikuwa ndiyo kama hajitambui vile. Mwili wake ulikuwa umeiva joto la ajabu kutokana na mahaba aliyopata hapo, naye akabaki akipumua kwa njia iliyoonyesha uchovu na mridhiko wa hali ya juu. Kuna sehemu za mwili wake alizohisi zikiuma sana, lakini bado moyo wake ulikuwa umeridhika sana na penzi alilolipata siku hii, naye akawa anatabasamu kilegevu katikati ya pumzi zake za uchovu. Draxton akawa anamwangalia sana, jinsi alivyolala hapo chini kwa kujiachia, naye akanyanyuka na kutambaa kumwelekea mpaka alipomfikia usawa wa uso wake.
Nywele za Namouih zilikuwa zimelowana kutokana na jasho tele lililomjaa, naye akamtazama Draxton machoni kwa hisia. Mnyama-Draxton akapitisha kiganja chake kifuani kwa Namouih mpaka usoni, na hisia ya kusisimua mwili wake ikampata mwanamke huyu. Yeye pia akanyanyua kiganja chake na kuushika uso wa Draxton, kisha akasema, "I love you Max."
Inaonekana maneno hayo yalimgusa sana mwana-mnyama Draxton, kwa sababu alifumba macho yake kidogo, kisha alipoyafumbua, yakawa yamerudi katika hali ya ukawaida bila kuwa na lenzi za blue. Namouih akatabasamu kidogo, akiwa amestaajabishwa na jambo hilo kwa kutambua kwamba Draxton aliweza kuji-control vizuri kurudia hali ya kawaida, na taratibu ngozi yake ikaanza kurudi kuwa ya kawaida na kuiacha ya uzungu.
Draxton sasa akawa anamwangalia Namouih kwa hisia sana, nywele zake zikiwa nyeupe bado, naye akasema, "I love you too, Namouih."
Hii ilishangaza kiasi, lakini Namouih akatabasamu kwa furaha sana baada ya kusikia hivyo, naye akakishika kichwa cha Draxton na kumvutia kwake ili wapeane busu. Wakalambana ndimi pamoja taratibu, nao wakaivunja taratibu na kutazamana machoni kwa ukaribu.
"Sijui ni kwa nini... lakini nimetokea kukupenda sana..." Namouih akasema.
"Umenipenda kama Draxton... au Max?" Draxton akauliza.
"Wewe ni yule yule kwangu..." Namouih akamwambia.
"Hhh... hii imefika mbali sana Namouih... sana," Draxton akasema.
"Najua. Lakini bado sitaki ifikie tamati," Namouih akasema kwa hisia.
Draxton akashusha pumzi, kisha akasema, "Ninaweza kuhisi jinsi ambavyo mwili wako umekuwa wa moto sana... ni kwa sababu nimekuumiza kwa kadiri kubwa. Wacha nikupake damu yangu."
Namouih akamwangalia tu machoni na kisha kutikisa kichwa kukubali.
Draxton akatoka usawa wa uso wa mwanamke huyo na kunyanyuka kabisa, naye akaenda pembeni kwanza. Ni kweli Namouih alikuwa ameumizwa sehemu za nyonga yake kwa makucha ya Draxton, pamoja na kifua na kalio lake kutokana na meno ya Draxton, na hata kuchubuka sehemu ya kitoweo chake, hivyo mwanaume huyo akaenda kuchukua kisu na kujikata kiganjani, halafu akarejea kwa mrembo na kuketi karibu na mwili wake uliolala bado. Akaanza kumpaka damu yake taratibu kwenye sehemu hizo, na Namouih akajinyanyua na kugeuka ili apakwe na nyuma pia. Walikuwa kimya kwa muda huu wote mpaka Draxton alipomaliza kumpa tiba hiyo isiyoeleweka vizuri, na ile tu Draxton alipotaka kunyanyuka tena, Namouih akakishika kichwa chake na kuanza kumpiga denda taratibu. Draxton akarudisha busu hiyo kwa upendo pia, halafu akamwacha chini hapo na kuelekea sehemu ya chumba.
Namouih akawa anajitazama mwilini mwake na kuona jinsi ngozi yake ilivyokuwa nyekundu kutokana na mchezo wenye rafu nyingi sana kutoka kwa mwanaume yule, naye akaichukua simu yake na kuangalia muda. Ilikuwa ni saa kumi na mbili jioni sasa, na kwa makadirio ya haraka angeweza kusema yeye na Draxton walipeana mapenzi kwa masaa mawili mfululizo kama siyo zaidi! Kuona namna ambavyo muda ulisonga kulimfanya atambue kwamba hangetakiwa kuendelea kukaa hapo kwa muda mrefu, lakini angevaa nini wakati Draxton alikuwa amezirarua nguo zake zote? Ni hapo ndipo akaanza kusikia mvua ikinyesha huko nje, naye akacheka kidogo kwa kutoamini hilo maana ilizidi kuongezeka tu.
Draxton akarejea kwa mrembo hatimaye, akiwa ameshika nguo fulani mikononi na yeye akivaa bukta nyingine tena. Namouih akawa anauangalia mwili wa mwanaume huyo, jinsi ulivyokuwa umejikata kiume haswa, naye akatabasamu na kuendelea kumtazama tu kwa uvutio. Mwanaume akaketi karibu yake na kumpatia T-shirt nyeupe yenye mikono mirefu, pamoja na bukta nyingine ngumu. Namouih akamwangalia na kuachia tabasamu, naye Draxton akatabasamu pia.
"Samahani kukuchania nguo... nitakununulia zingine," Draxton akasema.
"Asante. Kwa hiyo... natakiwa kurudi nyumbani nikiwa nimevaa hizi?" Namouih akauliza.
"La. Vipi ukipita kwa duka fulani kuchukua zingine zitakazokufaa?" Draxton akasema.
"Halafu hizi unazonipa?"
"Ukipenda zitupe tu."
"Kwa nini nizitupe?"
"Namouih..."
Namouih akatabasamu kidogo.
"Bila shaka Efraim amesharudi," Draxton akasema.
Namouih akatikisa kichwa kukubali.
"Itabidi uwahi... mvua inaweza kuendelea mpaka usiku," Draxton akamwambia.
Namouih akamsogelea mdomoni taratibu na kusema, "Hauoni kwamba hicho ndiyo kisingizio kizuri cha kunifanya nichelewe?"
"Lakini...."
"Efraim anajua niko na rafiki... usijali," Namouih akasema.
Draxton akatazama pembeni.
"Na wewe? Blandina hatakwazika tena maana uko mbali naye kwa mara nyingine?" Namouih akauliza.
"Nimemwambia nimeondoka kwenda nje ya jiji kwa muda mfupi..." Draxton akasema.
"Ahaaa... ndiyo maana hakuwa na mchecheto leo," Namouih akasema na kutabasamu.
Bado mwanamke huyu hakuwa amevaa chochote, hivyo ukaribu aliouweka kwa Draxton ukamsisimua sana mwanaume huyo.
"Unajua... unanifanya nitake kuku... kukushika tena..." Draxton akamwambia.
"Kuna kitu kinakuzuia kwani?" Namouih akaongea kwa njia ya madaha.
"Haitakuwa jambo zuri nikiwa nakupaka damu yangu kila mara Namouih... unaelewa nachomaanisha," Draxton akasema.
"Ndiyo naelewa."
"Yeah. Unanifanya nihisi kama... njaa... kila mara... ila ni muhimu sana nijizuie maana hata kama hautakubali, ninajua huwa unaumia. Sema tu una king'ang'anizi sana," Draxton akasema.
Namouih akatabasamu kwa hisia na kutazama chini.
Mvua bado ilikuwa inanyesha, hata sauti za ngurumo za radi zilisikika. Draxton akachukua T-shirt lile na kuanza kumvalisha Namouih, kisha akafanya hivyo hivyo na ile bukta. Alikuwa anamvalisha huku akimwangalia usoni kwa umakini, na mwanamke huyo alikuwa anamwangalia tu kwa uvutio mwingi. Kisha mwanaume akanyanyuka na kwenda kufata chupa za maji ya kunywa zilizokuwa pembeni, na ni hapa ndiyo Namouih akaanza kujishika sehemu zile zilizokuwa na maumivu na kuhisi akiwa amepona kabisa. Ilikuwa ni kama hakuumia kabisa, naye akamtazama Draxton baada ya mwanaume huyo kufika hapo tena na kumpa maji anywe.
Namouih akayafungua maji huku akisema, "Kuna kitu fulani huwa nafikiria sijui kama kilishawahi hata kupita kwenye akili yako."
"Kitu gani?" Draxton akauliza.
"Hivi unavyonipaka damu halafu... napona tu... ngozi inajishikiza yenyewe tu yaani... ingekuwa kama msaada mkubwa kwa watu wanaojeruhiwa vibaya labda... kama kwenye ajali...."
"Ndiyo tunarudi kule kule kwenye mimi kutumiwa kama kifaa cha experiment endapo kama ingefahamika damu yangu inaweza kuponya. Baba alikuwa anajaribu kunitengeneza kwa njia ya pekee, kwa ajili yangu mwenyewe, niwe tofauti tu... lakini jinsi watu wanavyoona mambo kwa njia mbaya ndiyo sababu aliamua kunificha... maana aliona ningekuwa hatari kwa wengi katika njia ambazo hata yeye hakufikiria..." Draxton akasema.
"Napenda unavyoongea Max. Ila bado huwa ni ngumu kiasi kukuelewa..." Namouih akamwambia.
Draxton akatabasamu.
"Miaka 95 ni mingi sana. Halafu hivi ulisomea wapi sheria? Ulihitimu wapi?" Namouih akauliza.
"Nilisoma sheria nikiwa Venezuela. Nilichukua madarasa kwa miaka mingi... huku nikijitahidi kuendelea kuficha siri yangu. Nili-pass bar exam vizuri sana, tena level ya juu..." Draxton akajisifia.
"Wow!" Namouih akamwambia na kumpigia makofi laini.
"Ahahahah... yeah. Baada ya kilichompata Ramona... sikuhitaji... yaani, nilikuja tu Tanzania kuendelea, au niseme kutafuta maisha mapya. Nilijifunza lugha yenu kwa miaka miwili tu."
"Yote?"
"Yote."
"Una kichwa chepesi."
"Ahah... mwanzoni nilikaa mwenyewe sana... ila ilipita kipindi kirefu pia bila ya mimi kubadilika kwa hiyo niliweza tena kujiamini na hata kutafuta uraia wa huku huku... angalau nijipe utambulisho mpya... na... nikarudia miaka ya uanasheria kwa huku pia ili niwe na mambo ya kufanya na siyo kukaa tu."
"Kuhama sehemu tofauti na kuishi muda wote huo... ulikuwa unatoa wapi pesa ya...."
"Oh, baba alikuwa pesa. Aliniachia urithi mwingi chini ya mwongozo wa mama na hata mama pia alikuwa akifanya kazi za hapa na pale kunipa support. Over the years... ziliendelea kuongezeka... na siyo kwamba me nilikuwa mtu wa kukaa tu... nilifanya kazi pia nilipokuwa Venezuela... na angalau huku thamani ya pesa ilikuwa ndogo kwa hiyo nilizokuwa nazo zilinisukuma kwa kipindi kirefu sana."
"Okay. It's touching. Halafu... hiyo tattoo... uliyonayo mgongoni... alikuchora nani?" Namouih akauliza.
"Ramona," Draxton.
"Oh kumbe! Alikuwa artist eeh?"
"Yeah."
"Hayo maneno huwa yanamaanisha nini? Kwa nini ulimwambia aandike... living in my heart you are, so you aren't dead? Au ilikuwa idea yake?" Namouih akauliza.
"Kuna siku nitakuelezea," Draxton akasema.
Namouih akatulia kidogo, kisha akasema, "Sawa. Uliniambia umekuja huku 90' eeh?"
"Yeah... we' ndiyo unazaliwa."
"Ahahah... ni miaka yangu ya kuishi we' ndiyo umekaa Tanzania. That's so cool. Umejitahidi sana kukaa muda wote huo bila kuumiza mtu yeyote Max... miaka 32! Umejitahidi sana," Namouih akamwambia kwa shauku.
Draxton akaangalia chini kwa njia iliyoonyesha huzuni.
Namouih alipogundua hilo, akamuuliza, "Max, uko sawa?"
Draxton akatikisa kichwa kukubali na kusema, "Yeah, niko sawa."
"Mbona hivyo?"
"Nilijitahidi ndiyo... kutoumiza watu... lakini kuna kipindi nilishindwa Namouih..." Draxton akasema na kumwangalia.
"Unamaanisha umeshaumiza mtu fulani ukiwa huku Tanzania?"
Draxton akatikisa kichwa kukubali na kusema, "Yeah. Ni... ni jambo lililoniumiza sana yaani... nilijichukia mno."
Namouih akakishika kiganja chake na kumwambia, "Pole Max. Unajua siyo jambo zuri lakini naweza kusema ulijitahidi sana... miaka mingi kupita ukiwa umeshaweza kuji...."
"Hakuna kitu kizuri Namouih. Yaani mimi ndiyo definition sahihi ya neno ubaya!" Draxton akamkatisha.
"Max...."
"Alikuwa mtoto, Namouih," Draxton akasema.
Namouih akatulia.
"Sikumbuki mambo vizuri lakini najua niliua mtoto. Ni kitu kilichoitesa conscious yangu sana... mpaka leo," Draxton akasema na kuinamisha uso wake.
Namouih akamwangalia kwa huruma, kisha akauliza, "Mtoto... alikuwa mtoto wa miaka mingapi?"
"Sikujua. Ila najua alikuwa mdogo sana... ninakumbuka walikuwa wawili na mwenzake mdogo pia ila yeye alikimbia... bila shaka wazazi wake walikuwa wanamtafuta alipoingia msituni na ndugu yake... na mimi nikapitiliza, nika... hhh... iliniuma sana..."
Namouih akaweka umakini wake zaidi, kisha akaushika uso wa Draxton na kumtazamisha usoni kwake. "Huyo mtoto... alikuwa wa kiume?" akamuuliza.
Draxton akatulia kidogo, kisha akatikisa kichwa kukubali.
"Alikuwa... mweupe... mdogo kama miaka 6 hivi... alikuwa na ndugu yake mwingine wa kike mdogo mdogo, si ndiyo?" Namouih akauliza huku pumzi zake zikianza kutetemeka.
Draxton akavishika viganja vya Namouih huku akimwangalia kwa umakini, kisha akamuuliza, "Kwa nini unauliza hivyo?"
"Nijibu kwanza Max. Hilo tukio... ulipomuua huyo mvulana... ilikuwa 2013?" Namouih akauliza tena.
Draxton hakuelewa ni jinsi gani Namouih aliweza kujua hilo, lakini akatikisa kichwa chake kukubali.
Namouih akauachia uso wa Draxton na kuweka kiganja chake mdomoni, naye akaanza kulengwa na machozi kwa sababu alikuwa ameshaelewa hilo lilimaanisha nini.
Draxton akamshika mabegani na kuuliza, "Vipi Namouih? Kuna tatizo gani?"
Namouih akainamisha uso wake na kuanza kulia bila kutoa sauti, na ni kitu kilichomfanya Draxton akose amani.
"Namouih..."
Draxton akamwita hivyo, lakini Namouih akajitoa mikononi mwake na kwenda pembeni kwanza. Draxton akanyanyuka pia akiwa haelewi mwanamke huyo alikuwa amepatwa na nini, na hivyo akamsogelea karibu na kuugeuzia mwili wake kwake. Namouih alikuwa anadondosha tu machozi huku ameangalia chini, naye Draxton akaanza kumfuta huku akijihisi vibaya sana moyoni kumwona analia.
"Namouih what's wrong?" Draxton akamuuliza huku akiwa ameshika uso wa mwanamke huyo kwa wororo.
Namouih akamwangalia machoni kwa huzuni, kisha akasema, "Huyo... mvulana... alikuwa mdogo wangu Max."
Uso wa Draxton ukatoa umakini wake wenye kujali na kubaki akimwangalia Namouih kwa njia ya kawaida, lakini akiwa ameshangazwa sana na kauli hiyo.
"Itakuwa upande wako wa pili ulimuua Nasri.... alikuwa mdogo wangu... hhh... Max...." Namouih akaanza tena kulia.
Draxton alikosa hata cha kusema. Macho yake yakaanza kutangatanga tu, kwa sababu zile hisia za kujiona kuwa mbaya kutokana na kuua mtoto mdogo zilikuwa zimeongezwa maradufu baada ya kujua aliua mdogo wa mtu muhimu sana kwake kwa wakati huu. Akautoa mkono wake usoni kwa Namouih na kurudi nyuma, akiwa ameshindwa afanye nini sasa.
Namouih akashusha pumzi na kujifuta machozi upesi, kisha akasema, "I need to go."
"Namouih..." Draxton akaita kwa huzuni.
"Nina... nahitaji... nahitaji kwenda Max... nahitaji kutuliza akili."
"Samahani... Namouih...."
Draxton akiwa anataka kuongea maneno kidogo, Namouih akampita na kuifata simu yake, kisha akavichukua viatu vyake na kuvishikilia tu mkononi. naye akaanza kuondoka kuelekea nje.
Draxton akaanza kumfata huku akisema, "Namouih... tafadhali just...."
Namouih akasimama na kumgeukia huku amenyanyua kiganja chake kumzuia asimfate, naye Draxton akasimama. "Please... nina... ninahitaji muda wa kuwa mwenyewe hiki ni... kitu kizito sana kwangu..."
Draxton hakuwa na namna ila kumwelewa tu, kwa sababu hata yeye alikuwa ameshtushwa sana na utambuzi wa jambo hilo ambalo hakuwahi kufikiri lingekuja kuleta mvurugiko mkubwa zaidi ya ilivyokuwa kwake mwanzoni. Namouih akatoka ndani hapo na kuelekea nje, mvua bado ikiwa inanyesha na giza likiwa limeanza kuingia, naye akaenda mpaka kwenye gari lake na kuingia. Akatulia kwa muda mfupi ndani hapo, akiwa anamwona Draxton sehemu ya mlangoni kwenye ile nyumba, naye akaligeuza gari upesi na kuondoka msituni huko.
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
ITAENDELEA
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
β
Usikose sehemu za mwendelezo wa hadithi hii kali ya CHANGE. Ni story nzuri na ndefu sana. Waweza ipata nakala yote kwa gharama nafuu sana. Karibu WhatsApp au kwa E-mail yangu.
WhatsApp no: +255 678 017 280