Simulizi - DYLAN

Simulizi - DYLAN

DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI

★★★★★★★★★★★★


Dylan alifumbua macho, akitambua Leila alichofanya, lakini akatulia asikilizie jambo hilo lingeelekea wapi. Leila alishindwa kuendelea kuzuia hisia zake, naye akaibusu kwa mara ya pili shingo ya Dylan. Dylan akalegeza mikono yake kutoka kiunoni kwa binti, naye Leila akawa kama amerudiwa na fahamu na kutambua alichofanya.

Wakaachiana taratibu na kuangaliana usoni. Leila alionyesha dhahiri kwamba alikuwa anamhitaji Dylan, na hapa ndipo Dylan alipoweza kuzielewa hisia za mwanamke huyu bila kuelezewa chochote. Leila alikuwa akisogeza uso wake kuelekea wa Dylan, kama anasita-sita, kila mara akiiangalia midomo ya jamaa na macho yake haraka-haraka. Ijapokuwa hii ilikuws ni mara ya kwanza kwa Dylan aliyepoteza kumbukumbu kuwa karibu namna hii na mwanamke aliyemwonyesha hulka ya kimahaba, hakuwa na wasiwasi hata kidogo. Kwa mpigo mmoja wa mapigo ya moyo, Dylan akaifata midomo ya Leila na kuibusu kwa wororo sana.

Misisimko mingi iliivaa miili ya wawili hawa, na sasa Leila akawa amepata kibali cha kuonyesha upendo wake kwa Dylan. Busu zao laini ziligeuka na kuwa denda zilizojaa huba nzito sana, nao wakashikana miili na kuendelea kudodosana kiaina.

Lakini Dylan akaivunja denda hiyo taratibu, huku Leila akipumua kwa hamu kubwa baada ya kupatiwa penzi kwenye midomo yake. Dylan akamtazama machoni, na ikawa wazi kwake kuwa binti alitaka mambo mengi zaidi, ila sehemu na wakati havikufaa.

"Leila..."

"Bee..."

"Baba na mama watapatwa na wasiwasi tukichelewa sana...nafikiri itakuwa vyema tukiwahi," Dylan akamkumbusha.

Leila akaibana midomo yake na kutikisa kichwa chake kukubali, huku anamwangalia jamaa kwa hamu nyingi sana. Dylan akatabasamu na kujitoa karibu yake, kisha akaanza kumwongoza waelekee nyumbani. Walitembea miili yao ikiwa karibu, na mara kwa mara wangeangaliana na kutabasamu. Dylan akakishika kiganja cha Leila na kuingiza vidole vyake kwenye vidole vya binti, naye Leila akavibana vyema, wakiendelea kutembea wameshikana mkono namna hiyo.

Hawakusemeshana kitu chochote tena mpaka wanaikaribia nyumba. Walipofika usawa wa mti fulani, Dylan akamvuta Leila na kumsimamisha hapo, akiwa ameuweka mgongo wake kwenye mti. Mapigo ya moyo wa Leila yalikimbia sana, huku akiwa anamwangalia Dylan kwa hamu kubwa, akisubiria afanye alichotaka kufanya. Dylan alimwangalia machoni kwa hisia nyingi za uvutio, naye akatabasamu kwa furaha kutokana na hisia hizi mpya zilizomsisimua sana.

Dylan akaisogelea midomo ya Leila taratibu, naye Leila akaifungua yake na kuipokea ya jamaa. Walianza kudendeshana kimahaba sana, huku Leila akivuta-vuta nywele za Dylan. Ijapokuwa kumbukumbu za Dylan zilikuwa mbali, hakuweza kusahau jinsi ya kupinga denda mwanamke hata kidogo! Aliinyonya midomo ya Leila kwa hamu kubwa, kisha akaiachia na kuweka paji lake la uso kwenye paji la binti. Wote wakawa wameyaelekeza macho yao chini, kisha Dylan akasogeza uso wake nyuma kidogo.

"Kwenye upande wako sing'oki."

Akasema Dylan na kumfanya Leila acheke kidogo kwa hisia. Kisha wakaachiana na kuanza kuelekea kwenye nyumba. Walipofika, Leila aliongea na mama yake kuhusu mambo yaliyotokea kwa mama Theodota, naye Dylan akatumia muda wake pamoja na Baraka. Mara kwa mara, wawili hao wangetazamana kwa kuibia-ibia, na Leila angetabasamu kwa njia yenye haya na shauku kiasi. Dylan pia alifurahia alichokuwa ameanzisha na mtoto wa kike, naye alitazamia mambo mengi mazuri kwenye uhusiano wao huu mpya.

Asubuhi iliyofuata, wanafunzi waliwahi shuleni, na sasa wakawa wamebaki wazazi, Leila, na Dylan. Shani alikuwa anasaidizana na Leila kuandaa vitu, naye Baraka alikuwa anaoga. Dylan alipokuwa sebuleni akimsubiri Baraka, Leila aliketi kwenye kochi baada ya Shani kwenda chumbani. Wakawa wanaangaliana kwa njia ya kichokozi. Dylan akapandisha nyusi zake mara mbili kumwelekea Leila kwa utundu, naye Leila akamwonyesha ishara ya busu kwa mdomo wake. Dylan akachekea kwa chini, huku Leila akitabasamu kwa furaha.

"Ethan..."

Dylan akageuka baada ya Shani kumwita. Alikuwa ameshika nguo fulani kubwa mikononi.

"Naam..." Dylan akaitika.

"...nitolee hilo pazia dirishani halafu uniwekee hili hapa," Shani akamwambia.

"Aaa...sawa."

Dylan akaenda upande wa dirisha na kulitoa pazia kutokea juu, akiwa amesimama tu chini kutokana na kuwa mrefu. Kisha akampatia pazia hilo na kuchukua lile alilotakiwa kuweka, naye Shani akaelekea chumbani. Wakati ameanza kuliweka kule juu, alimtazama kidogo Leila, aliyekuwa ameketi kwenye kochi huku ameiinua miguu na kuikunjia juu alipokaa. Alikuwa amevaa dera kama kawaida yake, naye akampa Dylan tabasamu hafifu huku akimwangalia kwa macho fulani hivi...wanajua wanawake tu wanavyofanyaga!

Dylan akatabasamu pia, na hapo hapo Leila akafanya jambo fulani lililoukamata umakini wake. Alishika pindo ya dera lake iliyofunika miguu, kisha akaanza kuipandisha juu huku anamwangalia Dylan kilegevu. Tabasamu la Dylan likafifia na sura yake ikawa makini kuangalia binti alichoelekea kukifanya. Leila alipandisha nguo yake taratibu, mpaka ikafikia sehemu ya paja.

Dylan alizubaa! Ni hapa ndipo Leila akalifunika paja lake haraka ili kumshtua Dylan. Alimpatia kwa kuwa kweli macho ya Dylan yalishtuka na kumwangalia Leila usoni, aliyekuwa anamcheka kwa kuweza kucheza vizuri na akili yake.

"Ethan...mbona bado hujaliweka tu?"

Sauti ya Shani ikamshtua nyuma yake na kufanya mikono yake ikurupuke na kuanza kuliweka pazia hapo juu. Alipompiga Leila jicho la wizi, alimwona jinsi alivyomcheka kichini-chini, naye akatikisa kichwa chake kwa kutambua jinsi gani Leila alimfanya awe kituko.

Baraka aliingia ndani kutoka bafuni na kwenda chumbani, naye Dylan akawa amemaliza kuliweka pazia. Shani akamshukuru, kisha akaenda kubeba vitu vyake pamoja na Leila. Wakati Shani ametangulia kutoka nje, Dylan akamsogelea karibu Leila na kumwambia, "Subiri na wewe zamu yako..." na kumfanya Leila acheke kidogo. Kisha binti akatoka nje ili ajiunge na mama yake kuelekea kwenye kazi zao.


★★★


Ilifika mida ya saa 4 asubuhi Baraka na Dylan wakiwa kwenye ofisi yao, pale mvulana mdogo alipokuja anakimbia na kumwambia Baraka kwamba Leila anagombana na watu fulani kule mgahawani kwao. Alichosema ilikuwa ni kwamba kuna watu fulani walitaka kumpiga Leila, na ugomvi huo ukawa mkubwa kwa sababu watu wengi walikuja kuuangalia. Dylan na Baraka wakatoka hapo upesi na kwenda kule ili kujua ni nini hasa kilichotokea.

Walipofika, walikuta watu wakiwa wamechanganyikana mbele ya mgahawa wa mama Conso, huku Leila akitukanana na mwanamke fulani mwenye umri mkubwa kidogo kumzidi. Waliposogea karibu zaidi, Baraka alimshika Leila na kumuuliza nini kinaendelea, na kwa hasira binti akajibu kwamba hao washenzi wanataka eti kumpiga kwa sababu alisababisha Fabian apigwe jana. Baraka akashangaa kwa sababu jambo hilo lilikuwa geni kwake, lakini Dylan alielewa vizuri jambo hilo.

Huyo mwanamke aliyekuwa akitukanana na Leila, alikuwa ni mama yake mdogo Fabian, naye alikuwa amekuja na kaka yake Fabian, ambaye alikuwa na umri wa miaka 35. Walikuwa wanataka kumpiga Leila kwa sababu hakuwaambia ni nani aliyempiga Fabian jana na kumuumza vibaya. Kwa kuwa kaka yake Fabian alikuwa mwenye mwili mkubwa, alitaka kulipiza kisasi kwa mtu aliyemuumiza mdogo wake.

"Lazaro...nisikilize. Kufanya hivi haifai..huyu ni mtoto. Kwa nini tusi..." Baraka akajaribu kumtuliza huyo kaka.

"Mtoto? Mtoto huyo? Umesikia kila kitu alichokuwa ananiambia?" mama mdogo akapayuka.

"Ndiyo mwanao mshenzi! Akitaka kunibaka, lazima akung'utwe!" Leila akasema kwa hasira.

"Halafu nitakuzibua wewe ******* zako wewe!" Lazaro akamwambia Leila huku amemsonta.

"Leila hebu tulia. Lazaro, kwani hatuwezi kukaa chini tukazungumza kistaarabu?" Baraka akamwomba.

"Kistaarabu? Mpaka aseme kwa nini wamemchangia na bwana wake mwingine kumpiga Fabian! Na atuambie ni nani huyo!" akasema mama mdogo.

"Yaani leo huondoki hapa mpaka useme...la sivyo nitakufumua kama mlivyomfanya mdogo wangu," Lazaro akatoa kitisho.

Watu wengi wa eneo hili walimhofu Lazaro kwa sababu walijua alikuwa mwenye fujo nyingi sana, na mara zote ambazo alizinguana na mtu ilikuwa lazima ampige. Hata mke wake alipewa sana upendo huo wa vipigo mara kwa mara, na ni kama sikuzote yeye na ndugu zake walitafuta sababu za kugombana na watu kwa kuwa walijua kaka mkubwa angewanyooshea mambo kwa mtindo huo.

"Huyu ndiyo Lazaro aliyemfanyia fujo Baraka kipindi kile?"

Dylan akamuuliza mama Conso hivyo kwa sauti ya chini, ambaye alikuwa amesimama pembeni yake huku akimtazama Lazaro kwa makini.

"Ndiyo huyo," akajibu mama Conso kwa uhakikisho.

"Wewe malaya wewe! Ninakupa dakika tano haki ya Mungu usiponiambia ni nani..."

"Ni mimi," Dylan akamkatisha.

Watu wote waliokuwa eneo hilo wakamtazama Dylan (Ethan) kwa makini baada ya yeye kujisema. Dylan, akiwa ameudhika, akasogea mbele kumwelekea Lazaro, huku Baraka na Leila wakihofia sana. Jamaa akasimama katikati akiwatazama mama mdogo na kaka mtu, huku wawili hao wakimwangalia kwa hasira.

"Mimi ndiyo nilimpiga," Dylan akasema kwa ujasiri.

"Kwa nini ulimpiga?" Lazaro akauliza kwa kupandisha besi.

"Alifanya kitu ambacho ikiwa dada yako angefanyiwa, basi usingemwacha salama huyo mpumbavu," Dylan akamibu kwa utulivu.

"Nimekuuliza swali...jibu swali!" Lazaro akasema huku amemnyooshea kidole.

"Kwani nimejibu tako lako au?" Dylan akauliza kwa kejeli.

"Nini? Unasemaje (...)nge wewe?!" Lazaro akauliza huku amekunja sura.

Kufikia hapa, watu wote waliokuwa eneo hilo wamewazunguka, walitulia kimya wakiangalia tukio hili. Wote wenye biashara zao waliziacha ili kushuhudia mambo ambayo yangetokea hapo, huku wengi wakihofia usalama wa Ethan (Dylan) kwa kuwa walifikiri hakumjua Lazaro.

"Umetoa miguu yako kutoka kote huko ili kuja kupiga mwanamke...unajitambua?" Dylan akamuuliza kwa hisia kali.

"(....)mae zako wewe!"

Lazaro akamtukana na kuanza kupiga hatua kumwelekea.

"Subiri..."

Dylan akanyoosha kiganja chake juu ili kumsimamisha. Lazaro akatulia kidogo huku anamwangalia kikatili. Dylan akawageukia watu wote huku amenyoosha kidole chake cha shahada juu.

"...ninaomba mtu YEYOTE yule asije kuingia hapa katikati! Baraka msogeze Leila nyuma..." Dylan akasema kwa sauti ya juu.

"Ethan..." Baraka akaita.

"Ethan!" Leila akaita kwa sauti ya kutaadharisha.

Wakati huu Dylan alikuwa anawaangalia Baraka na Leila, hivyo Lazaro alikuwa anamfata Dylan kwa kasi ili aanze kumshambulia kabla hajageuka. Lakini Dylan alikuwa anatambua jambo hilo vizuri sana, naye alipohisi Lazaro amemkaribia zaidi, aligeuka upesi na kuuwahi mkono wake aliokuwa anauleta moja kwa moja ili ampige Dylan ngumi ya shingo. Aliukwepa na kuushika kwa kasi, kisha kuigeuza nguvu ya Lazaro ilipoelekea kwa kuutega mguu wake mmoja. Hii ilifanya upande mmoja wa Lazaro uangukie mgongoni kwake, kwa hiyo akatumia bega kumnyanyua na kumtupia kwa mbele kama anashusha gunia kubwa la mchele kutokea begani.

Watu walianza kusikika wakiongea ovyo ovyo, naye Lazaro akanyanyuka kwa hasira akiwa anahisi maumivu mgongoni. Akamfata Dylan kwa kasi, lakini Dylan akamkwepa kwa ufundi sana na kuzungukia nyuma yake, kisha akampiga kwa kalio nyuma yake na kumfanya Lazaro aangukie mbele kwa kukosa muhimili (balance). Watu wengi walicheka baada ya Dylan kumfanya Lazaro aonekane kama mtu duni sana.

Faida kubwa aliyokuwa nayo Dylan ni kwamba, alijua mwanaume huyo alitegemea sifa zake za kuogopwa na baadhi ya watu kwa sababu alijiona kuwa hashikiki, na ni kujiamini huko kupita kiasi ndiyo kungekuwa jambo la kumwangusha kwa sababu alitegemea zaidi nguvu badala ya kutumia akili. Dylan hakujua ni kwa nini, lakini kuna kitu moyoni mwake kilimwambia angeweza kumdhibiti huyo mpuuzi.

Baada ya kusikia watu wamemcheka, Lazaro alinyanyuka kwa mara nyingine tena akiwa na hasira kali sana, naye alikuwa amechukua jiwe kubwa na kulirusha kwa nguvu kumwelekea Dylan. Kwa kasi, Dylan aliweza kukwepa, lakini kwa tukio baya jiwe hilo likampiga kifuani msichana mdogo aliyekuwa amesimama hapo karibu. Watu walihuzunika sana kwa kuwa msichana huyo alianguka na kuzimia, na baadhi wakaanza kumhudumia haraka.

Dylan alikasirika sana! Alimgeukia Lazaro akimtazama kwa hasira sana, ambaye hakuonyesha kujali kilichompata msichana yule. Watu wengi walipiga kelele kuwaambia waache ugomvi huo, lakini Lazaro akamfata Dylan tena akijaribu kumpiga. Dylan alikuwa ametulia akimwangalia kwa hasira, na Lazaro alipomfikia akarusha ngumi ambayo Dylan aliizuia kwa kuupiga mkono wake kwa kiwiko.

Papo hapo Dylan alitumia mkono mwingine kumpiga tumbo, kisha mguu mmoja kuupiga uso wake alipoinama, na alipounyanyua akaushika mkono wake na kuuvuta kwa nguvu huku akiugeuzia mgongo wake kwake, na hapo akauvunja kwa kuukunjia kwa nguvu kwenye bega lake kwa kasi ya ajabu!

"Aaaagh!"

Yowe hilo la maumivu lilitoka kinywani mwa Lazaro, aliyehisi maumivu makali sana. Lakini Dylan wa wakati huu hakuwa na huruma hata kidogo baada ya kuona msichana yule ameumia. Hapo hapo alimgeukia Lazaro kwa kumpiga kiwiko shingoni, kisha teke la usoni lenye nguvu sana lililofanya Lazaro aangukie chini huku akisikilizia maumivu ya mkono.

Wahuni walishangilia sana. Sauti nyingi zilisikika zikisema 'mpige huyoo' ili kumhamasisha Dylan aendelee kumshushia mpuuzi huyo kichapo. Akamfata hapo chini na kuanza kumpiga ngumi za usoni, huku watu wakisogea karibu zaidi na kuendelea kushangilia. Ijapokuwa Lazaro alijitahidi kufurukuta, Dylan alimdhibiti kisawasawa, na sasa akawa amelegea zaidi.

Baraka alimfata Dylan na kumwambia aache, na kijana huyu akatulia huku anapumua kwa hasira. Hapo hapo wakaja askari watatu, ambao walikuwa wa kituo kidogo cha eneo hilo, na kufanya watu wasambae kwa kuhofia. Kihalisi, walikuwa wamefika tokea Dylan alipoanza kumsumbua Lazaro, lakini wakabaki kutazama tu kwa umbali fulani. Sasa wakamnyanyua Lazaro, ambaye alikuwa amedebweda haswa, nao wakasema yeye pamoja na Dylan waende kituoni.

Ijapokuwa baadhi ya watu walijaribu kutetea upande wa Dylan, kijana huyo akatii tu na kuongozana nao mpaka kituoni kwenye ofisi ya kituo chao. Mmoja wao alikuwa ameshika bunduki kubwa, hivyo kwa kiasi fulani watu waliogopa. Baraka, mama Conso, na Leila walikuwa wameambatana nao, huku askari wawili wakiwa wamemshikilia Lazaro kwa kuwa aliyumba-yumba sana huku damu zikivujia usoni. Mama mdogo wa Lazaro alikuwepo pia, akilalamika njia nzima, na watu wengi njiani waliwaangalia sana mpaka wanafika kwenye kituo kile.

"Hakuna! Hawa ndiyo wametuanza sisi! Wamempiga mwanangu mpaka wamemvunja kidole...na sasa hivi wamemvunja mkono kaka yake...afungwe tu huyu mbwa!" mama mdogo akaendelea kulalamika.

"Punguza jazba Sofia. Wewe kijana...ni kwa nini unachukua sheria mikononi na kuvunja mtu mkono?" akauliza askari mkuu wa kituo hicho.

"Masoud...kama mama Conso alivyokuelezea, hawa ndiyo walioanzisha fujo. Walitaka kumpiga Leila ndiyo Ethan akaingilia kati..." Baraka akasema kwa ustaarabu.

"Alikuwa hakuulizi wewe, alikuwa anamuuliza huyu..." mama mdogo akadakia.

"We naye vipi? Linakuuma tu kwamba mdebwedo wako amegalagazwa...funga tako lako!" Leila akamwambia.

Lazaro alikuwa pembeni akiendelea kusikilizia maumivu tu, naye Dylan alikuwa ameketi kimya kwenye benchi.

"Nyie hebu tulieni," akasema afande mmoja.

"Tako lako mwenyewe mshenzi wewe! Umekalia kuuza k*** tu malaya uliyekubuhu mpaka majalalani wewe!" mama mdogo akamtukana Leila.

Leila akasimama kwa shari na kumtemea mate usoni. Mama mdogo aliponyanyuka ili agombane naye, askari wawili pamoja na Baraka wakawatenganisha huku wakiwaambia watulie, na wanawake hawa wakaendelea kusimama huku wanaangaliana kwa hasira.

"Masoud...huyu bwege afungwe miaka 30 kwa hiki alichokifanya..." mama mdogo akamwambia mkuu wa askari.

"Nyoo! Miaka 30 ya maisha yako uliyotumia kutafuta wa kukubebesha mimba ila ukashindwa au?" Leila akamwambia kwa dharau.

"Binti nimesema kaa chini!" askari mmoja akamwambia Leila, huku amemnyooshea kirungu.

"Chonde! Usininyooshee jiti lako hilo..." Leila akamwambia kwa ujasiri.

"Leila!" Baraka akamzuia binti yake.

"Unasemaje wewe?" askari akamuuliza kwa ukali.

"Nyie hamna lolote. We na wenzako mlikuwepo muda wote hadi mtoto wa watu anapigwa jiwe lakini mkakaa tu. Mlivyoona Ethan amemkalisha huyu fala ndiyo mkajifanya mnajua kuamua sana ugomvi..." Leila akawaambia ukweli.

"Shenzi wewe ngoja nikuonyeshe!"

Askari huyo akasema hivyo kwa kuudhika na kuanza kumfata Leila. Dylan alinyanyuka na kusimama mbele ya Leila, akimzibia njia askari huyo ili asimfikie Leila. Askari alisimama na kumtazama Dylan usoni akiwa amekunja sura.

"Ah-aaah jamani mambo haya yasiende hivi! Eeh...Masoud..." Baraka akajaribu kutuliza hali.

"Nipishe..." askari akamwamrisha Dylan.

Dylan akasimama hapo hapo huku anamwangalia tu.

"Nimesema toka! Nitakuumiza!" akamfokea.

"Kama vipi twende hapo nje, lakini siwezi kukuacha upige mwanamke," Dylan akamwambia kwa sauti thabiti.

"Ethan...Masoud mbona husemi kitu jamani?" mama Conso akamwambia askari mkuu.

"Ethan...kaa chini," Masoud akamwambia Dylan kwa ustaarabu.

Maaskari hawa walifahamiana vizuri sana na familia ya Baraka na Dylan mwenyewe (waliyemjua kama Ethan), hivyo Masoud alijua Ethan huyu ndiye yule kijana anayejulikana kuwasaidia watu wengi wa hapo kutengeneza upya daraja lao. Alijua pia kuhusu tabia za Lazaro, lakini kuna sababu iliyomfanya yeye pamoja na askari wengine wawe kama...wanamhofu. Kwa hiyo kuona kwamba Dylan aliweza kumnyamazisha jamaa kiaina, kuliwafanya askari hawa waone aibu, na hasa kwa sababu Masoud alikuwa anamheshimu kijana huyu.

Baada ya askari Masoud kumwambia Dylan akae, kijana huyu aliendelea tu kusimama huku anamwangalia afande aliyetaka kumpiga Leila. Masoud akamwambia afande wake awaache, naye akarudi nyuma kidogo na kumsonta Dylan kwa kirungu chake, akijifanya mbabe. Angetoka naye nje kweli ndiyo angeona!

"Masoud, Lazaro anahitaji matibabu, hapaswi kuendelea kukaa hapa. Tuachie tuondoke," mama mdogo akasema.

"Kwa nini awaachie wakati shida mmeanzisha nyie wenyewe?" Leila akasema.

"Aah yaani we msichana wewe! Hivi unashindwa kufunga mdomo wako?" yule afande akamwambia Leila.

"Mbona huyu akiongea humwambii? Tena hadi amenitukana lakini unaniona mimi tu!" Leila akasema kwa ukali.

"Leila...nyamaza!," Baraka akamfokea binti yake.

"Ni kweli. Lazaro atapaswa kwenda hospitali, lakini bado siwezi kuwaacha hawa bila kuwaadhibu," Masoud akasema kwa uthabiti.

"Kwa nini umwadhibu Ethan wakati hana kosa?" Leila akauliza.

"Hana kosa?" mama mdogo akadakia.

"Kosa gani? Ni nini kilichomtoa huyo mtu wako kule kwenu kote mpaka kwenye mgahawa wetu? Si ili ampige Leila? Halafu alipopigwa yeye ndiyo amegeuka malaika," mama Conso akamwambia mama mdogo.

"Kwenda huko na wewe hayakuhusu!" mama mdogo akamwambia mama Conso.

"Wewe ndiyo hayakuhusu. Kiherehere tu kunusanusa boxer za haya majitu unayoyaita matoto. Unaniambia mimi nauza k(...), ulishaniona? Wakati we unaiuza ya kwako hadi kwa afande mtu hapa, unafikiri hatujui?" Leila akamwambia mama mdogo.

"Wewe binti wewe! Unamaanisha nini?" yule afande akadakia.

"Hee..baba tulia...sijakutaja. Mbona unajishtukia?" Leila akamwambia kwa kejeli.

"Lakini Leila mbona husikii?" Baraka akamnyamazisha binti yake.

Afande huyo akaanza tena kumfata Leila, lakini Dylan akamzibia njia kwa mara nyingine. Akalishika shati lake kwenye kola na kufanya kama anamvuta, naye Dylan akaitoa mikono yake kwa nguvu sana. Jambo hilo lilifanya askari wengine waingilie kati na kuwaachanisha.

"...mjinga huyu, niacheni nimwonyeshe!" afande akasema kwa kujitutumua.

"Beba rungu lako, twende hapo nje!" Dylan akamwambia kwa hisia kali pia.

Jambo hilo lilikuwa limegeuka kuwa la kibinafsi baina ya askari huyo Na Dylan. Damu ya Dylan ilikuwa ya moto sana, naye alikuwa tayari kupambania kile alichoona ni sawa, haijalishi aliyembana naye alikuwa "askari."

"Inatosha jamani. Haina haja ya kugombana."

Wote waligeukia upande wa mlangoni baada kusikia sauti hiyo. Walikutana uso kwa uso na mwanamke fulani aliyekuwa mgeni kabisa kwenye macho yao. Alianza kutembea kuelekea sehemu hiyo waliyokuwepo, kisha akasimama usawa wa Dylan na kumwangalia machoni. Walitazamana kwa sekunde kadhaa, kisha mwanamke huyo akampita na kusogea mpaka kwenye meza ya Masoud.

"Habari, naitwa Grace. Nimekuja kumtolea dhamana kijana huyu."

Akamwambia maneno hayo Masoud kwa ufupi sana huku akimwelekezea Dylan mkono. Kwanza kabisa, wote walikuwa wakiangalia mwonekano wake. Alivalia gauni fupi iliyoishia magotini yenye rangi ya maroon, nayo ililichora umbo lake vizuri sana. Alikuwa na kalio kubwa kwa nyuma, na alikuwa mrefu kumfikia Dylan. Macho yake yalikuwa makubwa kiasi, na nywele zake zilikuwa zimechanwa juu na kunyolewa pembeni kidogo kwa mtindo wa kiduku. Alinukia vizuri mno, na kuingia kwake kwenye kituo hicho kuliisambaza harufu ya marashi ya mwili wake.

Baraka, mama Conso, Leila, wote waliangaliana wakiwa hawajui mtu huyu ni nani, naye Dylan alikuwa anamtazama kwa makini pia. Kabla Masoud hajamjibu lolote, mwanamke huyo, Grace, akafungua mkoba wake mdogo aliobeba na kutoa pesa nyingi zilizofungwa kwenye 'rubber band.' Wote walimshangaa, naye akamnyooshea Masoud mkono uliozishika huku anatabasamu.

"Umesema huwezi kumwacha bila adhabu. Chukua...milioni moja hiyo, nafikiri ni adhabu tosha," Grace akasema.

Wote walibaki wakiwa wamepigwa na butwaa. Mwanamke huyo alikuwa nani? Na ni nini kilichopelekea mpaka atoe kiasi kikubwa hivyo cha pesa kwa ajili ya mtu ambaye hakumfahamu?


★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

WhatsApp +255 787 604 893
 
DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA

★★★★★★★★★★★★★★★★★

Masoud akazipokea pesa hizo kimaswali sana, naye Grace akatoa tabasamu la kuridhika. Kisha akageuka na kuwaonyeshea Baraka, Leila, mama Conso na Dylan kwa kiganja chake kuwa wamfate nyuma yake. Waliangaliana kwa mshangao, naye Masoud akamuuliza Dylan ikiwa alimjua mwanamke huyo. Baada ya Dylan kukanusha, Masoud alisema wako huru kuondoka, hivyo wakatoka pamoja na kumfata mwanamke huyo, wakiwaacha mama mdogo na Lazaro mule kituoni.

Baada ya kutoka nje, walimwona Grace akiwa amesimama kando ya gari lake, akiwasubiria. Wakamfata hapo, naye akasalimiana nao. Leila alipoanza maswali, Grace akawaambia waingie ndani ya gari ili aweze kuwarudisha sehemu zao, na kwa hiyo angewaelezea mambo wakiwa wanaelekea huko. Ijapokuwa waliingiwa na mashaka, wanne hao walikubali kupanda kwenye gari, na safari ya kurudi ikaanza.

"Kwa hiyo wewe siyo wa huku?" Baraka akaendelea kumuuliza wakiwa mwendoni.

"Hapana. Kampuni yangu iko nje ya jiji hili. Nilikuwa nimekuja huku kwa ajili ya likizo fupi..." Grace akaeleza.

"Kwa hiyo kumbe haumfahamu Ethan hata kidogo? Kwa nini umetoa pesa kubwa sana kwa ajili yake?" Leila akauliza kwa udadisi.

"Kwa sababu nataka kumsaidia," Grace akajibu.

"Kunisaidia na nini?" Dylan akauliza.

"Nilipokuwa huku, nilipata kusikia kuhusu ustadi wa engineer fulani kwenye ujenzi wa daraja lile. Nilipoenda kujionea, nilipendezwa nalo sana. Kwa hiyo, nikaamua kumtafuta engineer huyo aliyehusika hapo," Grace akaeleza.

"Engineer?" mama Conso akauliza.

"Mimi siyo..."

Dylan alikuwa kidogo aseme yeye siyo mkandarasi, pale Baraka alipomkandamiza mkono na kumtikisia kichwa kumzuia. Dylan akakunja uso wake kimaswali.

"Kwa nini ulimtafuta?" Baraka akauliza.

"Aam...niliona ana kipawa cha hali ya juu kwenye miundo ya construction, hivyo nilitaka kufanya maongezi naye ili nione kama angeweza kufanya kazi nami kwenye kampuni yangu," Grace akasema.

Baraka akamwangalia Dylan huku akiwa anatabasamu, huku Dylan akimwangalia kwa njia yenye maswali.

Walifika eneo la mgahawa wa mama Conso, naye akashuka. Leila hakushuka kwa kuwa hangeendelea na kazi siku hiyo baada ya vurugu zilizotokea, hivyo alikuwa ameamua tu kurudi nyumbani. Grace aliendesha gari mpaka eneo la ofisi ya Baraka, naye Baraka akamwambia Ethan (Dylan) atangulie na binti yake nyumbani kwa kuwa aliiacha ofisi muda ule bila kuifunga, hivyo akasema angekaa kidogo kusikilizia mambo, kisha angekuja nyuma yao ili aweze kuzungumza na Leila. Akamshukuru Grace kwa kumpa lifti, kisha Grace akaliondoa gari hapo na kuanza kuwapeleka wawili hao nyumbani.

Njiani alimwelezea Dylan kuhusu kampuni yake kwa ufupi, kuwa ilijihusisha na masuala ya ukandarasi pia. Alihitaji kina kipya cha ujuzi na ubunifu wa hali ya juu, na aliona mambo hayo ndani yake Dylan. Dylan hakuwa hata na uhakika ikiwa angeweza kufanya kazi rasmi za kampuni ya ukandarasi, kwa kuwa hata suala la kujenga daraja lilikuja bila kutarajia.

Grace alimwambia walikuwa na mambo mengi ya kuzungumzia, lakini kutokana na hali za siku hiyo, aliamua tu kumwachia Dylan kadi ya mawasiliano na kumwambia akipata nafasi angekuja kesho kumwona. Baada ya kuwafikisha eneo la nyumba yao, aliwaaga na kugeuza gari ili arudi alikotoka. Dylan alibaki amesimama akitafakari mambo mengi sana, huku Leila akitangulia nyumbani kwa kuwa bado alikuwa ameudhika.

Dylan alipofika ndani pia, alimkuta Leila amejishika kiuno huku anaongea na rafiki yake kwenye simu, akimwambia kuhusu mambo yaliyotokea kituoni na jinsi mama mdogo wa Fabian alivyomuudhi sana. Dylan akabaki kumtazama tu jinsi alivyoongea kwa jazba, lakini siyo jazba yake aliyokazia fikira, bali ni uzuri wake. Alipomaliza kuongea na simu, akaiweka mezani huku akipumua kwa hasira, naye akamtazama Dylan.

"Ethan... yaani bora usingemvunja yule mshenzi mkono tu, ungemvunja pu(...) kabisa!" Leila akamwambia.

"Punguza ukali wa maneno Leila..." Dylan akasema kwa sauti tulivu.

"Hakuna cha maneno! Yaani wamenikera mimi wale watu mpaka kunako! Halafu lijinga lile likampiga jiwe Marietta, masikini mtoto wa watu! Isingekuwa ya kibwana uchwara chake yule Sophia pale kituoni yaani ningemkunja-kunja mpaka angejua kwamba...."

Dylan aliendelea kumwangalia tu Leila alivyoendelea kuitoa kero yake. Aliongea sana mpaka ikawa inachosha kumsikiliza. Hivyo Dylan akamsogelea karibu zaidi huku anamwambia 'basi inatosha.' Lakini mwanamke hakuwa ameridhika bado.

"....eti likanivuta nje, wakaanza kunitishia eti watanipiga! Nikasema nyooo... mumpige nani? Hako kabibi kakaanza kuleta za kimalaya... nikakaonyesha jinsi ninavyojua kutoa za ki..."

Dylan akamkatisha kwa kuupiga busu mdomo wake na kufanya maneno yake yaishie mdomoni mwa jamaa. Alikishika kiuno chake na kuubana mwili wa Leila kwenye wake, huku sasa akiibusu midomo yake kimahaba. Leila hakuendelea tena kuleta fujo, kwa kuwa alilegea kwa hisia nyingi za kimahaba zilizouvamia mwili wake upesi.

Dylan akaivunja denda hiyo na kumwangalia machoni, na hapo hapo Leila akaishika shingo ya Dylan na kumvutia mdomoni mwake tena. Wakaendelea kupeana busu, na wakati huu Leila alionekana kutaka mambo mengi zaidi ya busu tu, kwa kuwa mkono wake mmoja ukashuka mpaka sehemu ya mbele ya suruali ya Dylan, na kuanza kuisugua-sugua kwa juu. Dylan akiwa anajua vizuri Leila alipotaka jambo hili lielekee, akijitoa kinywani mwake kifupi.

"Leila..."

"...mmm..."

"Nafurahi kuona unanihitaji... Lakini hapa... nyumbani..."

"...wengine hawarudi mpaka baadae..." Leila akasema kwa deko.

"Hatuwezi kuwa na uhakika..."

"...me nakuhitaji Ethan... naomba uniondolee stress zote za leo mpenzi..."

Dylan aliona kweli Leila alihitaji penzi lake, na ijapokuwa alihofia usalama wao ikiwa wangekutwa, hakutaka pia kutoa sababu ya kumkwaza mwanamke wake. Leila akaanza kuifungua suruali ya Dylan huku anamwangalia kimahaba sana, naye Dylan akaweka kiganja chake usoni kwa Leila huku anamwangalia kwa hisia za upendo. (........).

(........)

(........)

(........)

(........)

(........)

Mapenzi yao motomoto yaliwatoa sebuleni mpaka chumbani, na huko mambo yalipamba moto zaidi mpaka Leila alipofikishwa sehemu ya kuridhika. Lakini akawa bado anataka waendelee.

"...mmmm... tuendelee..." Leila akasema kwa sauti iliyojaa huba nzito.

"Ningependa...lakini tatizo muda Leila..." Dylan akasema.

"Me nataka tenaahh..." Leila akasema kwa mideko.

"Ahah... usijali... utapata tu tena..." Dylan akamwambia

Kisha Dylan akambusu kwenye paji lake la uso, huku Leila akionyesha dhahiri kwamba alitaka sana waendelee. Dylan alijua vizuri kwamba Baraka angefika muda wowote ule kwa kuwa alisema angekaa ofisini kidogo kisha angefunga na kuja nyumbani, hivyo alitaka kuhakikisha wanakuwa waangalifu ili baba wa watu asiwakamate wakifanya yao kwenye nyumba yake. Baada ya hapo Dylan alinyanyuka na kumsisitiza Leila waanze kurekebisha vitu ndani vizuri zaidi.

Hawakuwa wametambua kuwa, wakati wakiendelea kupeana mapenzi motomoto, Emilia alikuwa amesimama nje ya mlango wa kuingilia chumbani hapo. Alikuwa amewahi kuondoka shule baada ya mtihani wa kwanza kuisha kwa kuwa mtihani wa pili hakutakiwa kufanya; wa somo la biashara. Alikuwa amefika muda ule Dylan alipompeleka Leila chumbani, hivyo alipofika karibu na mlango wa kuingilia kwenye nyumba aliweza kusikia sauti za miguno ya Leila. Kwa hiyo aliingia ndani kwa kunyata na kufikia kwenye mlango wa chumbani, na hapo ndiyo akaweza kuona mambo vizuri.

Aliona vizuri sana jinsi Dylan alivyoingiza mashine yake ndani ya kitoweo cha dada yake huku miguu ya Leila ikiwa imenyanyuka kwa kusambaa hewani. Kwa kuiangalia mashine ya Dylan, na tendo lote kwa ujumla, ilimsisimua sana binti huyo ambaye hakuwahi kufikiria angepata kumwona Dylan bila nguo zozote siku moja.

Emilia alianza kujawa na hisia nyingi za kimahaba; kumwelekea Dylan. Siyo kwamba tu kwa kuwa alimwona namna hiyo, ila hisia zake zilifikia hatua hiyo kwa sababu tayari alikuwa anavutiwa na kijana huyo, lakini kwa kuwa Dylan alimheshimu kama mdogo wake, Emilia alimpa heshima hiyo pia. Lakini sasa hisia zake kwake zikawa zimepitiliza, naye akawa akitamani kupata kile ambacho dada yake alikuwa anafurahia wakati huu.

Aliendelea kusimama hapo mpaka wakati ambao Dylan na Leila walionekana kufikia mwishoni na kuanza kuongeleshana, naye akatoka nje bila kuwashtua wawili hao na kwenda mbali kidogo ili awaache wamalizie mambo yao. Akiwa anasubiri, aliendelea kukumbukia jinsi mashine ya Dylan ilivyokuwa yenye kutamanisha sana macho yake kila mara alipoiona inapanda na kuingia kwenye kitoweo cha dada yake.

Dakika chache baada ya hapo, Steven akawa amefika sehemu hiyo akitokea shuleni na kumwona dada yake hapo. Steven akamuuliza Emilia mbona amewahi sana leo, naye akamweleza kuwa mtihani wake ni mpaka kesho baada ya kumaliza wa asubuhi. Steven aliposema waelekee nyumbani sasa, Emilia alisita kidogo na kutaka kumzuia, lakini hakuwa na sababu ya kumpatia mdogo wake. Asingeweza kumwambia kuhusu jambo alilokuta likiendelea nyumbani, hivyo akaamua tu kuanza kuelekea tena nyumbani pamoja na Steven, akiombea wawili wale wawe wamemaliza na kupasafisha ndani.

Walipofika nje ya nyumba, walimkuta Dylan (Ethan) akiwa anachota maji kwa ajili ya kuoga, huku akiwa kifua wazi. Steven akamkimbilia na kumkumbatia kwa furaha, naye Dylan akampokea kwa furaha pia. Emilia alikuwa amesimama tu, akitazama mwonekano wa Dylan akiwa kifua wazi, na hisia zake zikawa zinapanda tu kumwelekea jamaa. Dylan akamsalimu Emilia, akiwa hana wazo la ni nini kilichotembea kwenye akili ya msichana huyo, naye Emilia akaitikia huku akitoa tabasamu bandia. Dylan akawaambia waingie ndani ili waweze kupumzika, kisha akabeba ndoo yake yenye maji na kuelekea bafuni, huku Emilia akiendelea tu kumwangalia.

Emilia alipofika ndani, alimkuta Leila akiwa ameketi kwenye kochi huku anakula. Yeye na Steven wakamsalimia, naye Leila akawaambia wabadili nguo ili waje kula; ikiwa walikuwa na njaa, maana mara nyingi walikula huko huko shuleni. Steven akaondoka, lakini Emilia akabaki akimtazama tu dada yake. Leila akamuuliza vipi, naye binti akakanusha kwa kusema hakuna jambo lolote, kisha akaelekea chumbani. Alikuta chumba kikiwa safi, kitanda kama hakijaguswa vile! Akakaa akimwaza sana Dylan, na kushindwa kujua aanze vipi kumweleza hisia zake, kwa kuwa sasa alitambua wazi kwamba dada yake ndiye alikuwa mmiliki.

★★★

Baadae, wazazi wa vijana hawa watatu wakawa wamerejea nyumbani. Leila aliwaelezea kila kitu kuanzia wakati ambao Fabian alijaribu kumlazimisha afanye naye mapenzi usiku ule, na ndipo Ethan akamsaidia. Aliwaeleza pia kuhusu jinsi Lazaro alivyomfanyia fujo, lakini alificha ukweli wa kwamba alikuwa anatoka kimapenzi na Fabian, ijapokuwa mama yake alilijua hilo. Kwa kiasi kikubwa Shani alishangaa kujua kwamba Ethan (Dylan) aliweza kumpiga mwanaume yule. Wote hawakujua kwa nini, lakini Shani hakuwepo maeneo ya kazini kwake muda ule ugomvi huo unaendelea, la sivyo angesikia na kwenda pale.

Dylan alitambua kuwa Emilia alikuwa akimtazama sana. Mwanzoni alifikiri ni kawaida tu, lakini kadiri muda ulivyopita msichana huyo aliendelea kumwangalia tu na kumfanya jamaa ajiulize ni kwa nini. Baada ya maongezi hayo, Baraka alimsihi sana Leila awe makini na asifanye mambo ambayo yanaweza kumsababishia shida, kama jinsi alivyokuwa akiongea na askari. Dylan akaomba radhi kwa kutenda kwa njia ile, na kusema alipandwa tu na hasira kwa mambo aliyofanya Lazaro. Baraka akamhakikishia kuwa ilikuwa ni sawa, na akatania kidogo kwa kusema hata yeye alifurahia kuona yule bwege anakalishwa chini.

Emilia na Steven wakaondoka na kuelekea vyumbani kwao, wakiwaacha wazazi wao pamoja na Leila na Dylan.

"Yule mwanamke alisemaje?" Baraka akamuuliza Dylan.

"Mwanamke gani?" Shani akauliza.

"Kuna mwanamke fulani alikuja pale polisi akamtolea Ethan dhamana... eti milioni moja!" akasema Leila.

"Ati?! Milioni moja?" Shani akashangaa.

"Ndiyo," akajibu Leila.

"Wa wapi?" Shani akauliza.

"Anatokea nje ya huu mji. Ethan... alipowaleta nyumbani mliongea nini?" Baraka akamuuliza Dylan.

"Aliniachia namba ya mawasiliano...akasema ikiwezekana atapita kesho," Dylan akasema.

"Anataka nini kutoka kwako mpaka atoe milioni moja?" Shani akamuuliza.

"Eti anataka kumsaidia Ethan kwa sababu alijenga daraja. Me simwamini huyo mwanamke, anatoa vibe za kichawi sana," Leila akasema.

"Wewe naye!" Baraka akamwambia Leila.

"Kwa hiyo ukamwambiaje?" Shani akamuuliza Dylan.

"Ndiyo mpaka tuje kuongea. Sikuweza kumwambia kwamba sina simu, kwa hiyo nafikiri tukionana tena tutaongea vizuri," Dylan akajibu.

"Ni mkubwa?" Shani akaendelea tu kuuliza.

"Kwa kumwangalia ana kama miaka 30 na kitu hivi...sema ana hela sana kwa hiyo anaonekana mdogo...au labda ni mdogo sina uhakika," akasema Baraka.

"Ni mbibi huyo. Hela tu. Ethan... akijaribu kukurubuni kwa lolote usikubali," Leila akasema.

"Hee! Jamani we mtoto kwa wivu!" Shani akasema.

"Siyo wivu. Hao ndiyo wale wanakuchekea usoni afu' ukiwafata tu wanakuingiza mtegoni... tunakuja kusikia oooh fulani katolewa kafara..." Leila akaongea kwa mkazo.

"Hebu kaa kimya! Wewe hauna mawazo mazuri, kila wakati unafikiria mambo hasi tu! Em' kwanza nenda chumbani," Baraka akamwambia Leila kiukali.

Binti akanyanyuka akiwa amenuna na kumtazama Dylan machoni, ambaye alikuwa anamwangalia kwa hisia, kisha akaondoka na kuingia chumbani kwake.

"Usimsikilize huyo Ethan. Hii ni nafasi nzuri sana kwako," Baraka akasema.

"Kwa nini unasema hivyo?" Dylan akamuuliza kwa umakini.

"Wewe kijana wangu una kipawa cha hali ya juu sana. Ni wakati ukitumie sasa kikupe faida kubwa," Baraka akamwambia kwa kutia moyo.

"Lakini....sina uhakika Baraka. Mambo yote niliyoyafanya..."

"Uliweza kuyafanya ukiwa bado hukumbuki mambo vizuri. Piga picha tu ni mambo gani mengi unaweza kufanya kumbukumbu yako ikiwepo...na itakaporudi..."

"...lakini ndiyo hicho Baraka. Sina uhakika kama mambo ambayo yule dada anaweza kutarajia nifanye nitaweza kuyafanya..."

"Utaweza bwana. Mambo mengi sana unaweza," Shani akamwambia.

"Ethan..." Baraka akamwita.

"Naam..."

"...nina imani utaweza. Huyo mwanamke amekutolea milioni 1! Siyo mchezo! Anaiona kama shilingi mia tu, kwa kuwa anajua akikupata ataingiza mamilioni zaidi... Wewe jiamini na ninakutia moyo uongee naye...akisema anataka kukuajiri kwenye kampuni yake, kubali. Hii itakuwa nafasi nzuri kwako kupiga hatua mbele zaidi, na najua utafanikiwa tu," Baraka akamtia moyo.

"Ni kweli. Na angalau ukifanya hivyo sisi tutaacha hizi kazi za vichochoro; we uwe unaleta vitu vizuri tu hapa," Shani akasema.

"Mama Leila!" Baraka akamshangaa.

"Ahahahah...namtania tu. Ethan fanya yote unayoweza ukubali kazi kwa huyo mwanamke. Hata akitaka vitu vitamu kutoka kwako we mpe," akasema Shani.

"Lakini mama Leila..."

"Niiini? Milioni moja siyo mchezo baba Leila, huwezi ukasema tu huyo mwanamke anamtaka Ethan kwa ajili ya kazi...anataka hadi hiyo naniliu..." Shani akatania huku ananyanyuka.

Dylan akacheka kidogo huku Baraka akitikisa kichwa. Shani akaelekea zake chumbani na kuwaacha wawili hao hapo.

"Kwa hiyo ndiyo maana ulinizuia nisimwambie kwamba sina uhakika kama mimi ni engineer?" Dylan akamuuliza Baraka.

"Ndiyo. Kwanza ingemchanganya maana anajua umelitengeneza daraja kwa hiyo haingeingia akilini kusema wewe siyo engineer. Inawezekana ulikuwa engineer kabla... kwa sababu usingeweza kufanya yale yote uliyofanya Ethan.." Baraka akamwambia.

Dylan akashusha pumzi ndefu.

"Kwa hiyo...umeamuaje?" Baraka akauliza.

"Wacha tuone jinsi mambo yatakavyokuwa. Sijui anataka kunisaidia vipi, na ninahitaji kujua kwa nini ANATAKA kunisaidia. Tukishaongea itakuwa rahisi kupangilia mambo mengine zaidi," Dylan akajibu kwa unyoofu.

"Sawa kabisa," Baraka akamwambia kwa uelewa.

Waliendelea kuongelea mambo mengi hapo, kutia ndani hali ya yule msichana, Marietta, ambaye alipelekwa hospitali baada ya kupigwa jiwe na Lazaro kifuani. Dylan alifikiria kwenda kesho kumwona, naye Baraka akamwambia ingekuwa busara kufanya hivyo na lilikuwa jambo zuri. Kisha baada ya muda fulani wakafunga vizuri nyumba na wote kwenda kupumzika kwa ajili ya kesho.

★★★

Asubuhi kama kawaida wanafunzi waliwahi kwenda shule, naye Baraka alikuwa amewahi kutangulia kazini, akimwacha Dylan, Leila na Shani wakijiandaa pia. Ilikuwa ni wakati Dylan anavaa T-shirt yake chumbani, pale Leila alipoingia na kumkumbatia kwa nyuma. Dylan alishtuka, na kuanza kumsisitiza kwa sauti ya chini aondoke haraka kwa kuwa haikuwa busara kuingia ndani hapo wakati wazazi bado wapo.

Leila alikuwa amevaa khanga moja tu kutokea kifuani mpaka usawa wa magoti yake, akiwa na lengo la kwenda kuoga. Lakini alipomwona Dylan kupitia uwazi mdogo wa mlangoni kwenye chumba, akapenya na kuingia ili kumwonyesha upendo. Akawa anakataa kutoka na kung'ang'ania Dylan ambusu, na ndipo hapo Dylan akamwacha na kwenda kuufunga mlango. Ile anageuka, akakuta Leila ameidondosha khanga yake chini, na sasa mwili wake wote ukawa wazi mbele ya jamaa.

Dylan alipandwa na hisia za kimahaba zilizomtaka amfate binti huyo na kumwonyesha nini maana ya penzi, lakini alijua huu haukuwa wakati mzuri, na Leila alikuwa akihatarisha taswira yao mbele ya wazazi wake. Binti akamsogelea mwanaume karibu na kuishika sehemu yake ya siri, kisha akaishika shingo yake na kuanza kumpiga denda laini. Dylan hakuwa na cha kufanya zaidi ya kuendelea kuibusu midomo ya Leila pia, huku mkono wake mmoja ukikishika kiuno cha binti kwa wororo.

Leila alipotaka kuifungua suruali ya Dylan, jamaa akajitoa mdomoni mwake na kumzuia.

"Leila..." akamnong'oneza.

"Nini..." Leila akajibu kwa kukwazika.

"Wazazi wako hapa...hatuwezikuendelea..."

"Agh...achana nao bwana. Tuendelee na mambo yetu..." Leila akajibu kwa kutojali.

"Nini? Hivi hau..."

"Leilaaa!"

Wote wakashtuliwa na sauti ya Shani, akimuita binti yake kutokea nje ya chumba hiki. Dylan akafumba macho huku akihisi hapa lazima kivumbi kingeanza tu. Leila akawa ametulia huku anamwangalia Dylan machoni. Wakatulia kusikilizia nini kingefuata, nao wakamsikia Shani akiendelea kumwita Leila mara kadhaa.

Ghafla hapo hapo mlango wa chumba hicho ukagongwa. Leila akaziba mdomo wake, naye Dylan akamwonyesha kwa ishara ya kidole kuwa atulie tuli.

★★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★★

WhatsApp +255 787 604 893
 
DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI

★★★★★★★★★★★★★★★★★

Ethan..." sauti ya Shani ikasikika akimwita Dylan.

"Naam..." Dylan akaitika, huku akivua T-shirt yake haraka sana.

Leila alishangaa kwa nini anafanya hivyo, na hapo hapo Dylan akamsogeza pembeni ya mlango ili ajibanze. Kisha akaufungua mlango kiasi na kutoa kichwa na sehemu ya kifua chake nje kuchungulia, akijifanya anavaa.

"Umemwona Leila?" Shani akamuuliza.

"Ndiyo nimemwona," Dylan akajibu kiukweli.

Leila akakunja sura akishangaa.

"Yuko wapi?" Shani akamuuliza Dylan.

"Nimemwona hii asubuhi...lakini si..jui yuko wapi," Dylan akasema.

Leila akatikisa kichwa huku anazungusha macho yake kwa kutambua Ethan alikuwa tu anamrusha roho tu.

"Simwoni ndani kote na nje..." Shani akasema.

"Labda ametangulia?" Dylan akauliza huku akijua jibu vizuri.

"Aagh... atatanguliaje sasa wakati hata hajanisaidia kubeba vitu? Yaani huyu mtoto me hata simwelewi..."

"Yaani... kana papara mno!" Dylan akasema kikejeli ili Leila amsikie.

Leila akamwangalia sana, kisha akaona amkomeshe. Akachuchumaa polepole na kuishusha suruali ya Dylan. Dylan alihisi jambo hilo, lakini akajitahidi kuweka utulivu ili Shani asihisi kitu chochote. Shani alikuwa bado amesimama hapo hapo akionekana kufikiria sana.

"..aa... namalizia kuvaa sasa hivi, nitakuja kukusaidia kubeba..." Dylan akasema.

Ni wakati huu ndipo Leila akaiweka mashine ya Dylan mdomoni mwake. Dylan akajikaza sana asionyeshe hisia zozote zile. Leila alikuwa akimfanyia makusudi, naye Dylan alilitambua hilo.

"Aaaa unavaa? Sawa basi... ngoja nitangulie... utanibebea vitu nitakavyoacha uje navyo... yaani huyu atanitambua leo..." Shani akasema kwa njia ya kuudhika.

"...ssawa..." Dylan akajibu.

Baada ya Shani kuanza kuelekea sebuleni, Dylan akaufunga mlango na kujiachia ili aihisi raha aliyoipata kutokana na mdomo wa Leila. Mwanamke aliendelea tu kuinyonya huku anamwangalia machoni, naye Dylan akawa anamwangalia huku anatikisa kichwa.

"...haya Ethan natangulia," Shani akasikika akisema hivyo.

"...haya niko nyuma yako..." Dylan akajibu.

Ijapokuwa Dylan alijihisi vizuri sana kutokana na jinsi Leila alivyomwonyesha upendo, alijua ni muhimu kuwa na usawaziko na kiasi kuhusu jinsi walivyotakiwa kufanya mambo. Ikabidi asubirie mpaka wakati ambapo Leila angetosheka kumpatia penzi hilo la mdomo ili aweze kumwambia alichofikiria. Leila akanyanyuka baada ya sekunde kadhaa, akimwangalia Dylan kwa macho yaliyojaa hamu kubwa. Kisha akamfata mdomoni na kuanza kumpiga busu ili waendeleze mahaba yao. Lakini alipoanza kumvuta Dylan ili waelekee kwenye godoro pale chini, jamaa akamsimamisha kwanza.

"Leila..."

"Vipi?"

"Nafikiri tunapaswa kuongea kuhu..."

"Agh Ethan, hebu acha hizo bwana! Mbona unaanza kuboa?"

"Leila hapa ni nyumbani. Ulivyofanya muda huu ni..."

"Kwa hiyo haunitaki au?"

"Siyo hivyo... nisikilize. Umeona jinsi mama yako alivyoudhika kwa sababu..."

Dylan hakuwa hata amemaliza kuongea, naye Leila akageuka na kuifata khanga yake akiwa ameudhika. Akajifunga na kuanza kuuelekea mlango ili atoke nje, naye Dylan akamsimamisha.

"Leila sikia..."

"Nipishe... si unadengua?" Leila akasema kwa mkazo.

"Usiwe hivyo Leila... tafadhali," Dylan akambembeleza.

Leila akaangalia pembeni kwa njia ya kukereka, naye Dylan akamsogelea karibu zaidi.

"Ninakuhitaji pia... ila hali Leila. Haitakuwa jambo lenye kupendeza kama siku moja Baraka ananikuta nawe humu... tukiwa hivi. Hebu fikiria tu katika njia ya kawaida, unafikiri atahisije?" Dylan akazungumza kwa hisia.

Leila akamwangalia kwa ufupi, kisha akaweka mikono yake kwenye kiuno cha Dylan.

"Kwa hiyo... hatutakuwa pamoja tena kwa sababu tu tuko nyumbani? Me siwezi kusubiri Ethan..." akasema kwa kudeka.

Dylan akatabasamu na kumwambia, "Usijali. Nenda ukaoge halafu... ndiyo tutapanga mambo vizuri."

Leila akatikisa kichwa taratibu kukubali, kisha akampiga Dylan busu laini.

Baada ya hapo, binti akatoka na kwenda kuoga. Dylan alitoka chumbani kwake baada ya kumaliza kuvaa, na sasa akawa anasubiri Leila atoke bafuni ili amuage kuwa anatangulia. Lakini baada ya binti kurudi akamwambia kwamba wangeenda pamoja, na ijapokuwa Dylan alisema alipaswa awahi kwa kuwa bila shaka Shani angehitaji vitu vile mapema, Leila alisisitiza amsubirie tu. Hivyo akakaa mpaka binti alipomaliza kuvaa, kisha wote wakaondoka kuelekea sehemu zao za kazi.

★★★

Ilifika mida ya saa 8 hivi mchana, wakati Dylan akiwa na Baraka kwenye ofisi yake, pale gari la Grace lilipofika. Dylan hakutarajia kwamba Grace angekuja hapo na leo, lakini ujio wa mara nyingine wa mwanamke huyu ulimtaarifu Dylan kuwa bila shaka mwanamke huyo alimhitaji sana. Grace akashuka kutoka ndani ya gari, naye akaanza kuielekea ofisi ya Baraka. Watu, hasa wanaume vijana, walimtazama sana mpaka alipofika karibu na Baraka. Akawasalimu vizuri, kisha akamwambia Dylan kuwa alimfata ili waweze kuongea.

Dylan alikubali na kumwambia angemfatia kiti, lakini Grace akakanusha na kumwambia alihitaji wazungumze sehemu tulivu zaidi, hivyo angempeleka mahali pengine palipofaa. Dylan, kwa kushauriwa na Baraka kuwa akubali, akaridhia na kuondoka pamoja naye; ijapokuwa alijiona kuwa wa hali ya chini kiasi ukilinganisha na mwanamke huyo aliyemtolea dhamana ya milioni moja siku iliyotangulia.

Basi, baada ya muda fulani, wawili hawa wakawa pamoja sehemu iliyokuwa na hoteli fulani ya kisasa, nao wakawa wameketi kwenye viti chini ya kivuli kilichojengwa kwa mtindo wa nyumba ya nyasi, wakiongea huku wanapata chakula na vinywaji alivyoagiza mwanamke huyu. Grace alikuwa anamwelezea kuhusiana na kampuni yake; kwamba aliona kijana huyu alifaa kabisa kwenye kitengo cha mipango ya uendeshaji wa masuala ya ujenzi, na alikuwa na uhakika angefika mbali.

Dylan aliona awe mnyoofu kwa kumwambia ukweli kuhusu tatizo lake la kupoteza kumbukumbu, hivyo alitaka kujua ikiwa bado ingewezekana yeye kufanya kazi chini ya hali zake. Grace akamhakikishia kuwa hilo halikuwa na shida kabisa, na kwamba alikuwa na imani katika akili nyingi ya kijana huyu, hivyo alichotakiwa tu kufanya ilikuwa ni kukubali.

Dylan akikumbuka vizuri ushauri wa Baraka usiku wa jana, akakubali kuchukua nafasi hiyo ya kazi kwenye kampuni ya mwanamke huyu, naye Grace akafurahi sana na kumwambia angeanza kufanya mipango ili Dylan ahamie kule; kwa kuwa ilikuwa mbali kutokea huku. Waliendelea kukaa hapo mpaka kwenye mida ya saa 1 jioni, kisha Grace akamrudisha Dylan nyumbani kwa Baraka.

Dylan alipendezwa sana na utu ambao mwanamke huyo alionyesha. Alikuwa mwenye aina fulani ya umakini na utulivu wa hali ya juu, vitu ambavyo vilimwambia Dylan kuwa Grace alikuwa mtu wa kazi zaidi. Wakati amefikishwa eneo la nyumba ya Baraka, Dylan alimweleza Grace kwamba hakuwa na simu, hivyo hangeweza kumpigia. Kwa kushangaza, Grace akasema asijali kuhusu hilo kwa kuwa angemtafutia. Mpaka jamaa akashangaa! Yaani jinsi mwanamke huyu alivyomtendea ilikuwa ni kama walifahamiana kwa kitambo kirefu kumbe walikutana jana tu. Dylan akashukuru kwa hilo, kisha Grace akageuza gari na kuondoka eneo hilo.

Dylan akawa anaelekea nyumbani sasa ili aweze kumpa story nzima Baraka, pale aliposikia sauti za juu za kufokeana kutokea ndani mule. Akasogea upesi ili ajue kwa uhakika ni nini kilikuwa kinaendelea, na baada ya kuufikia mlango, akakuta ni Baraka akiwa anamfokea Leila, ambaye pia alikuwa anamjibu baba yake kwa ukali sana. Dylan hakujua ni kwa nini walikuwa wanagombana hivyo, lakini Leila alikuwa mkali kupita maelezo.

"....shida ni nini? Kwa hiyo nisingekuwepo ungekuwa anafanyaje?" Leila akaendelea kulalamika.

"Funga mdomo wako Leila! Unaongeaje na mama yako hivyo? Kwa hiyo tusikwambie ukweli kisa nini? Umekuwa nani wewe?" Baraka akamwambia kwa ukali.

"Agh yaani nyie mnaweza kufanya mtu hata akachukua maamuzi mabaya kwa sababu mnajua sana kutia hasira! Kitu kidogo eti wote mnanivaa kwa shari..."

"Leila funga bakuli lako nitakuwasha sasa hivi!" Shani akamkatisha.

"Niwashe tu! Si ndiyo fani yako? Eti siruhusiwi kuwa na mambo yangu kwa kuwa ninaishi tu hapa bado... ndiyo sababu mnanisengeeenya..." Leila akalalama.

"Lini tumekusengenya wewe? Nani hapa alishawahi kukwambia kwamba unafanya vitu kwa sababu tu unaishi kwenye hii nyumba? Mbona unakuwa na tabia za ajabu wewe!" Baraka akamwambia.

"Na ndiyo maana haishi kusemwa vibaya huko mitaani! Limekalia kutikisa mitako tu kichwani hakuna kitu! Unasema tunakusengenya kwa kuwa unakaa hapa, basi tafuta nyumba bora zaidi ya hii ukae mama..." Shani akamwambia kwa ukali.

"Nitatafuta tu. Mnaniandama kweli eti kisa naishi hapa... nawabana sana inaonekana. Nitaondoka tu, haijalishi... maana nimechoka kuishi majalalani," Leila akasema kwa jazba.

"Majalalani?!" Shani akauliza kwa mshangao.

Dylan, kutoka alipokuwa amesimama, alishangazwa sana na maneno yasiyo ya heshima kutoka kwa Leila. Ijapokuwa hakujua kisa cha ugomvi huu kilikuwa nini, alijua kuwa hiyo siyo njia nzuri ya kuzungumza na wakubwa.

"Majalalani? Unamaanisha nini? Leila... unamaanisha unajiona kama takataka kuishi na sisi? Ndiyo tunakufanya uhisi hivyo?" Baraka akauliza kwa hisia.

"Sijui. Naenda kulala," Leila akajibu hivyo na kuanza kuondoka.

Lakini Baraka akamzuia na kumuuliza tena kama walimfanya ajihisi kuwa takataka.

"Ndiyo! Hamnipi faida yoyote mimi hapa! Ni maneno, maneno, maneno tu... ni bora kuishi hata kaburini siyo hapa!" Leila akasema kwa sauti ya juu.

Baraka alishikwa na hasira kali sana na kumwasha binti yake kofi zito la usoni. Leila alidondokea chini huku akilia, na sasa Baraka akawa anaufungua na kuuvuta mkanda wake kutoka kwenye suruali aliyovaa. Dylan kuona hivyo, akaingia upesi na kujaribu kumwambia Baraka asitende kwa hasira, lakini baba wa watu hakutaka kusikiliza lolote tena. Akanyanyua mkono ulioshika mkanda juu ili aanze kumtandika Leila, lakini Dylan akamkinga Leila kwa mwili wake hapo chini, hivyo Baraka alipoanza kupiga mikanda akawa anaupiga mgongo wa Dylan. Aliendelea kuishusha mikanda ya nguvu sana, akiwa kama amerukwa na akili kutokana na kuhisi hasira kali.

Shani alitambua wazi kwamba mume wake hakuwa kwenye akili sawa wakati huu, kwa kuwa aliendelea tu kuupiga mgongo wa Dylan bila kuacha; kwake yeye akiwa anazitoa hasira zilizowaka kumwelekea Leila. Shani akafanikiwa kumzuia Baraka asiendelee, na baba huyu akarudi nyuma kidogo huku akipumua kwa kasi. Dylan alihisi maumivu mgongoni, kwa sababu sehemu ya chuma ndogo kwenye mkanda ule ndiyo iliyokuwa inaupiga mgongo wake sana. Leila akawa anamwangalia huku analia, naye Dylan akageuka na kumtazama Baraka.

Baraka alipoanza kutulia, alitambua kwamba hakufanya jambo sahihi kwa kuruhusu hasira yake imtawale namna hiyo, kwa sababu angeweza kumuumiza vibaya sana Leila. Akaudondosha mkanda chini na kutoka nje akiwa ameghafilika sana. Shani alimwangalia Dylan kwa huruma nyingi, kwa sababu nguo aliyokuwa amevaa iliraruka na alama za uvimbe zilionekana. Lakini kijana akanyanyuka tu polepole na kumsaidia Leila asimame pia.

"Ethan... uko sawa?" Shani akamuuliza.

"Ndiyo. Niko sawa," akajibu.

"Yaani wewe mtoto wewe!" Shani akamwambia Leila huku amemsonta kwa kidole.

Leila alikuwa analia tu kwa hasira huku amejishika shavu alilopigwa na Baraka. Dylan akaanza kumfuta machozi na kumkumbatia ili kumbembeleza, akimwacha Shani anashangazwa na njia yake ya kumbembeleza binti yake. Dylan aliweza kuwaona Emilia na Steven upande wa kuelekea vyumbani, bila shaka wakiwa hapo muda wote ambao ugomvi ule ulikuwa unaendelea. Akamwomba Shani aongee na binti yake kwa utulivu na kumsihi Leila asiwe mgomvi, ili yeye atoke nje kwenda kuongea na Baraka.

Dylan alipotoka ndani, alimkosa Baraka sehemu yote nje ya nyumba yao, hivyo akatambua huenda alikuwa amekwenda mbali kidogo. Akaamua kumfata huko huko, naye akamkuta mwanzoni mwa lile daraja akiwa amesimama hapo. Akamfata na kumpa pole kutokana na mkazo wake. Baraka akaomba samahani pia kwa kuwa hasira yake ilisababisha amuumize Dylan, lakini mwanaume akamwambia haikuwa na shida kabisa.

Baraka alimwambia sababu ya kugombana na Leila vile kwa leo ilikuwa ni suala la Leila kutomsaidia mama yake leo asubuhi na kufanya mambo yake tu huko alikojua yeye. Alisema walianza kumsemesha kwa njia ya kawaida lakini binti akaja juu kama kawaida yake. Dylan alijihisi hatia kiasi kwa kuwa alijua ni yeye ndiyo alichangia sababu iliyofanya Leila asimsaidie mama yake ijapokuwa alijitahidi kumdhibiti asubuhi hiyo.

Baraka alipomuuliza kwa nini alijiweka apigwe badala ya Leila, Dylan alitaka kusema kabisa kwamba sababu likuwa ni hisia zake kumwelekea Leila, lakini akaona huu haukuwa wakati mzuri kuzusha suala hilo, hivyo akasema tu alifanya vile ili binti asiumie maana kama angemtoa jicho hakuna ambaye angemtaka kabisa. Baraka akafurahishwa na utani wa kijana huyu, naye akafunguka mengi kuhusiana na Leila.

Alimweleza kuwa Leila ni mwanamke ambaye ni dhaifu kihisia, na analijua hilo, hivyo njia yake ya kushughulika na watu mara nyingi ni mbaya kwa sababu ANALAZIMISHA kuwafikirisha kuwa yeye ni imara sana. Alimsimulia kuhusu pindi nyingi ambazo amegombana naye, lakini bado alimpenda sana na kujitahidi kumwelewa, ijapokuwa kama nyakati za namna ya leo zingefanya Baraka akose subira ya jinsi ya kushughulika naye.

Kutokana na maoni ya Baraka, Dylan akawa ametambua ni kweli kabisa, na hicho ndiyo hata kilichofanya yeye pia na Leila wakaribie kugombana leo asubuhi kwa sababu ana kawaida ya kulazimisha mambo yaende kwa njia yake. Akampa pole tena baba huyu, kisha wote wakarejea nyumbani baada ya muda fulani.

Wakiwa njiani kurudi, Dylan alimwambia yaliyojiri leo pamoja na yule mwanamke, Grace, kwamba alikubali ofa yake ya kufanya kazi kwenye kampuni yake, na kwamba mipango ya yeye kuanza kule alikuwa amekwenda kuianzisha. Baraka alifurahi sana kwa ajili ya kijana huyu, naye akammwagia 'baraka' zake zote ili mambo atakayofanya huko yafanikiwe.

Walipofika, Leila alikuwa sebuleni na mama yake, naye akawafata na kupiga magoti chini; akimwomba baba yake msamaha kwa kuongea maneno mabaya sana. Alikuwa analia, akisema anastahili hata kufukuzwa kwa kitendo kile, lakini Baraka akamnyanyua na kumtuliza, kisha akamsihi sana asirudie kufanya mambo ambayo yaliwavunja moyo. Akamhakikishia kwamba yeye ni wa muhimu sana kwao, hivyo alipaswa kuacha kuhisi kana kwamba hakutosha ndani ya familia hii. Dylan akafarijika sana moyoni baada ya kuona wamenyoosha mambo baina yao.

★★★

Zilipita siku mbili baada ya hapo, na sasa hali nyumbani kwa Baraka ikawa imetulia. Kupitia kwa simu ya rafiki yake, yaani Fred, Dylan alikuwa ameongea na Grace ambaye alimjulisha kuwa siku iliyofuata angekuja kumchukua ili ampeleke kule jijini kwao kwa ajili ya kuanza kazi. Dylan aliona ni kama vile mambo yalikuwa yanakwenda haraka sana, hivyo akamwomba ushauri Baraka kuhusiana na hilo, naye akafurahia sana kwa ajili ya kijana huyu na kusema Mungu alikuwa amemnyooshea mkono wa baraka hivyo alipaswa kuchangamkia nafasi hii. Kwa hiyo Dylan akaongea tena na Grace kumfahamisha kwamba alikuwa tayari, hivyo angekuja kumpitia asubuhi.

Taarifa ya Dylan (Ethan) kuondoka nyumbani kwa Baraka iliwahuzunisha sana watoto wake, ambao walikuwa wamekwishamzoea sana kufikia wakati huu. Aliongea nao usiku walipokuwa pamoja, na hasa Steven ndiye alionyesha kwa maneno mengi kwamba hakutaka Dylan aondoke. Lakini akawahakikishia kwamba kuondoka kwake kusingekuwa jumla, bali angekuwa akija kuwasalimu mara kwa mara nyakati ambazo angepata nafasi. Akamwahidi Steven kuwa angemletea zawadi nyingi pia.

Ijapokuwa Leila na Emilia hawakuzungumza sana kuhusu jinsi walivyohuzunishwa na jambo hili, mioyoni mwao walijihisi vibaya mno. Leila alihisi ni kama angetenganishwa na penzi lake jipya lililokuwa limeanza kuiva sana, hasa kwa sababu alihisi ni kama Dylan angeibiwa na wanawake wengine huko aendako. Na upande wa Emilia, binti huyu alihuzunika kwa kuwa nafasi aliyokuwa anaitafuta ya kumwambia hisia zake haikupatikana, na kwa sababu ya kumzoea sana pia alihisi ingekuwa ndiyo kumpoteza. Shani alimtia moyo Dylan kupiga kazi kwa bidii na kumtania kama kawaida yake kwamba asiwasahau.

Leila alihitaji sana nafasi ya kuwa peke yake pamoja na Dylan kwa kuwa kesho angeondoka, hivyo ilipofika mida ya saa 3 walipokuwa wamemaliza kupata chakula, kwa ujanja akasema kuna kitu fulani cha muhimu alihitaji kufata dukani, na kwa sababu ilikuwa usiku akaomba Dylan amsindikize. Mama yake aliona ni kama analeta usumbufu, lakini binti akasisitiza sana kwa kusema kitu hicho kilikuwa muhimu sana. Dylan akakubali na kuwahakikishia wazazi wa binti kurudi haraka, kisha wawili hawa wakatoka pamoja na kwenda mpaka usawa wa daraja lile; lakini hawakulifikia.

Walikuwa wamefika usawa wa kichaka kimoja, pale Leila alipomvuta Dylan mpaka kwa ndani na kuanza kumpiga denda kwa hamu kubwa. Kulikuwa na giza, naye Leila akawa anafungua suruali ya Dylan haraka haraka ili wapeane mapenzi hapo hapo. Dylan kwa kujua hili lingeelekea wapi, akajitoa mdomoni mwake ili amsemeshe.

"Leila..."

"Usianze mambo yako Ethan..."

"Ahahah... unajua tunatakiwa kuwahi... halafu... me sidhani kuwa nawe sehemu kama hii ni vizuri..."

"Me sijali bwana. Unaondoka kesho Ethan... nakuhitaji sana na wewe unalijua hilo... nipe mapenzi ninayohitaji..." Leila akasema kwa deko.

"Kwenye majani?" Dylan akauliza.

"Ndiyoo..."

"Leila..."

Bila kujali kwamba wako kichakani, binti akaitoa mashine ya Dylan na kuanza kuisugua-sugua kwa kiganja chake. (.........).

(.........).

(.........).

(.........).

(.........).

(.........).

(.........).

(.........). Kisha wakaachiana, naye Leila akaomba waendelee, lakini Dylan akamwambia haingewezekana. Alimhakikishia kuwa hii haingekuwa mara ya mwisho kwa kuwa kuondoka kwake hakukumaanisha ndiyo angeachana naye, hivyo hakupaswa kuogopa. Akamkumbatia kwa upendo, kisha wote wakajitengeneza vizuri baada ya penzi lao la kificho, nao wakarejea nyumbani.

Hakukuhitajika maelezo mengi sana kwa kuwa Leila alisema walicheleweshwa na wateja kuwa wengi kwenye duka walilokwenda baada ya kutafuta sana kitu alichohitaji kwenye maduka mengi ambayo hayakuwa nacho. Baada ya hayo, Dylan akaendelea kukaa na Baraka hapo wakiongea mambo kadhaa kuhusu safari yake kesho, kisha baadae wote wakaingia kulala.

★★★

Asubuhi na mapema, Dylan aliagana na Emilia pamoja na Steven ambao walielekea shule, kisha Shani na Leila ambao walielekea makazini kwao, na Baraka pia. Yeye alibaki hapo kwa kuwa Grace angekuja kumpitia na kwenda naye kule; ndivyo mipango yao ilivyokuwa. Kwa kawaida kama nyumba yote ilifungwa halafu mtu mwingine wa hapo angekuja, funguo walizikuta sehemu fulani ya siri waliyoijua wenyewe tu, hivyo kabla ya Dylan kuondoka angeziweka mahali hapo.

Lakini ilipofika saa 2 hivi, Dylan akiwa bado ndani, Leila akawa amerudi tena. Dylan hakuwa ametarajia hilo, kwa kuwa inaonekana ni kama binti alilipangia jambo hilo namna hii. Bila kuchelewa, Leila akamfata Dylan na kuanza kuinyonya midomo yake kimahaba sana.

"Mbona umerudi?" Dylan akamuuliza baada ya kuachia midomo yake.

"Ulifikiri ningekuacha uondoke bila kukuaga?" akasema Leila kimapozi.

"Hhahah... lakini si tumeshaagana?"

"Sijatosheka."

"Vipi... kazini je?"

"Nimewaambia nimesahau simu nyumbani ndo' nmeifata."

"Leila..."

Kabla Dylan hajasema lolote zaidi, Leila akamsukuma kwenye kochi, kitu kilichofanya Dylan akae bila kupenda. Kisha Leila akamkalia katikati ya mapaja yake huku amemsogezea kifua chake usoni, naye Dylan akawa anamwangalia machoni kwa uvutio.

"Leila unajua muda hautaruhusu."

"Basi tuchaplishe," akamjibu kwa maringo.

Bila kukawia, binti akaanza kuinyonya midomo ya jamaa huku anaunyonga-nyonga mwili wake taratibu juu ya mwili wa Dylan kama anacheza muziki kwa 'slow motion.' Dylan akawa amekishika kiuno chake na pia (........). Dylan hakuwa na jinsi ila kuacha tu Leila afanye vitu vyake, kwa kuwa binti kweli alikuwa amelewa penzi la Dylan.

(........).

(........).

Leila alianza kupagawa sana na kujing'atang'ata midomo yake huku amekunja uso kimahaba, na hapa ndipo wote wakasikia 'horn' ya gari nje iliyopigwa mara mbili. Dylan akaacha kuyanyonya matiti ya mtoto na kutazama nje kupitia dirishani, na hapo akawa ameliona gari la Grace likiwa kwenye eneo hilo la nje. Akamtazama Leila, ambaye alikuwa ameshajawa na hamu kubwa ya kimapenzi hapo, kisha akamwambia muda wa kuondoka umefika sasa. Kama ilivyo kawaida ya Leila alianza kulalamika kwa kusema angemwambia Grace asubiri ili wamalize mambo yao kwanza, lakini Dylan akasema hilo halingewezekana pia.

Dylan akanyanyuka akiwa amembeba Leila, kisha akambusu kwa upendo na kumwachia asimame, naye akampa dera lake ili avae. Leila alikerwa sana na Grace kwa sababu alikuja wakati ambao alikuwa ameanza kuonja utamu kutoka kwa Dylan na kuukatisha. Hivyo akavaa dera lake akiwa ameudhika huku Dylan akivaa viatu vyake haraka.

Lakini kabla hajamaliza, mlango wao ukagongwa hapo nje, naye Dylan akajua bila shaka ni Grace ndiye ameugonga; huenda aliona asogee ili kumtoa ndani. Leila akaenda mlangoni hapo na kuufungua mlango, naye akamkuta Grace akiwa amesimama nje hapo na mwonekano wake mzuri kama kawaida.

"Za asubuhi?" Grace akamsalimu.

"Ni nzuri," Leila akajibu kibaridi-baridi.

"Amm... nimekuja kumchukua Ethan, sijui yupo ndani?" Grace akauliza.

"Hayupo."

Jibu la Leila lilisikiwa vyema na Dylan pale ndani. Alikuwa ameshamaliza kuvaa viatu na kubeba begi lake dogo ili aelekee mlangoni pale alipomsikia Leila anamjibu Grace hivyo, na jambo hilo likamshangaza sana.

★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

WhatsApp +255 787 604 893
 
DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU

★★★★★★★★★★★★★★★★


"Grace akashangaa kiasi.

"Hayupo? Lakini...tulikubaliana kukutana hapa..."

"Grace habari yako?" Dylan akakatiza maongezi yao na kutoka nje.

Grace akatabasamu kidogo baada ya kumwona, naye Leila akazungusha macho yake kwa kukerwa.

"Ni nzuri. Uko tayari?" Grace akamuuliza Dylan.

"Ndiyo niko tayari, tunaweza kwenda," Dylan akajibu kwa unyoofu.

Grace akamwangalia Leila, ambaye alikuwa anamtazama Dylan sana. Dylan akamtazama Leila pia kwa hisia.

"Leila....ninaenda sasa. Wafikishie tena wengine salamu zangu za heri eeh? Tutawasiliana..." Dylan akamwambia kwa hisia.

Leila akatikisa kichwa taratibu kukubali, kisha Dylan akamwangalia Grace tena.

"Okay, let's go," Grace akamwambia Dylan.

Ile tu wameanza kupiga hatua, Leila akamvuta Dylan mkono na kuanza kumpiga denda ya kimahaba sana mbele ya Grace. Aliunyonya mdomo wa Dylan huku anampiga jicho la pembeni Grace, na mwanamke huyu akawa ameelewa kuwa binti alifanya makusudi ili kumwonyeshea kwamba Ethan (Dylan) ni wake. Walipoivunja busu hiyo, Dylan alimwangalia Leila kwa kutomwelewa kabisa, kisha Leila akatoa tabasamu la ushindi na kuanza kuzivuta-vuta nywele za Dylan huku anamwambia wataonana.

Grace akaona atangulie tu kwenye gari, naye Dylan, akiwa amekerwa kiasi na kitendo alichofanya Leila, akamuaga kwa mara nyingine tena na kulielekea gari pia. Leila alibaki kuwatazama mpaka Grace alipoliondoa gari hapo, naye akasema kwa kejeli 'nimekuja kumchukua Ethan' na kusonya akiwa amekerwa na Grace sana. Kisha akarejea ndani na kuingia zake chumbani, akihisi upweke baada ya Dylan kumwacha.


★★★


Mambo upande wa Dylan yalikwenda kwa njia ambayo hakuwa ametarajia kabisa. Kwanza, sehemu ambayo angeishi isingekuwa sehemu yoyote tu, ilikuwa kwenye nyumba ya Grace mwenyewe. Pili, aliajiriwa kama kiongozi wa kitengo cha masuala ya mipango ya ukandarasi kwenye kampuni yake Grace, na hili kwa kiasi kikubwa lilimshangaza kwa kuwa ndiyo alikuwa amefika tu. Lakini imani ambayo Grace alikuwa nayo kumwelekea Dylan ilipita ukawaida, na jinsi alivyomtendea vizuri sana kulimfanya atie bidii zaidi ili kumletea mafanikio zaidi mwanamke huyu. Tatu, pesa ambayo Dylan alilipwa kwenye mwezi wake wa kwanza tu hapo ilikuwa kubwa sana mpaka akawa anashangaa mno na kuhisi labda kuna makosa yalijitokeza, lakini Grace akamhakikishia kwamba hiyo ilikuwa ni pesa stahili yake.

Kwa kadiri fulani, ilionekana ni kama Grace alifanya mambo hayo yote akiwa na nia fulani, lakini Dylan hangeweza kutambua ni nini. Ijapokuwa hivyo, bado kijana huyu alimwamini sana Grace kwa sababu alimsaidia na kumtendea kama dada anavyomtendea mdogo wake kwa upendo. Kumleta Dylan kwake moja kwa moja ilikuwa ni jambo la kipekee kwa kuwa Grace hakuwa na kawaida hiyo; na hakuwahi kuleta mtu yeyote aishi kwake hata mara moja (tofauti na msaidizi wa kazi na mlinzi ambaye aliwahi kuwa jasusi serikalini).

Grace alikuwa na umri wa miaka 34, naye alikuwa mwanamke mwenye pesa SANA. Nyumba yake tu ilikuwa kubwa na pana sana, yenye vitu vingi vya kisasa, na iliyokuwa imejengewa mambo mengi kwa mitindo ya wazungu. Mwanamke huyu alikuwa mwenye akili na thabiti; yaani hakupenda michezo ya kijinga-kijinga ilipokuja kwenye masuala ya kazi. Na kama ni kitu alichokuwa anachukia, ilikuwa ni uonevu. Wafanyakazi wake wengi kwenye kampuni, hasa wanawake, walimpenda kwa kuwa hakuonyesha ubaguzi wala upendeleo kwa yeyote yule, naye alishughulika nao mmoja mmoja endapo kulikuwa na tatizo lolote. Hakuwa na mwanaume yeyote kimahusiano, naye aliyaweka maisha yake kuwa binafsi sana kiasi kwamba wengi walichojua zaidi kumhusu ni kazi tu; hata rafiki zake wachache wenye pesa hakuwashirikisha sana kwenye maisha yake ya kibinafsi.

Kwa kuwa sasa Dylan alikuwa ametumia mwezi kama mmoja na nusu huku, alizoeana na Grace kwa kiasi fulani, kama yale mazoea waliyonayo kaka na dada. Baada tu ya kuhalalishiwa mshahara wake wa kwanza, alikwenda kumtembelea Baraka kifupi kule alikoishi na kuwatoa "out" familia yake yote. Walifurahia sana kumwona tena, na sasa waliona alikuwa na mwonekano uliopendeza sana. Aliwasimulia mambo mengi aliyoyafanya huko kwenye kampuni, nao pia wakamsimulia mengi yaliyotokea wakati akiwa kazini.

Aliweza kupata nafasi ya kuongea na Leila kidogo, ambaye kwa maringo alimweleza jinsi alivyom-miss sana na jinsi alivyohisi upweke mwingi baada ya yeye kuondoka, lakini Dylan akamwambia kuwa alitaka kutengeneza mazingira mazuri ili naye pia ampeleke kule siku moja waweze kujivinjari pamoja. Kwa kuwa sasa Leila alijua Dylan analipwa, alimwomba pesa kiasi ya kutumia, naye Dylan akampatia mrembo wake. Ni kweli kabisa kwamba Dylan alikuwa anatengeneza mazingira mazuri ili kumtoa Leila siku moja ili wawe pamoja, lakini pia alitaka kuja kuyaweka wazi mahusiano yao kwa baba yake, na alitaka kufanya hivyo bila kumwambia Leila ili iwe 'surprise' kwake endapo angemwambia baadae.

Baadae aliongea na Baraka pia, kisha akampatia kiasi fulani na kumtania awe anatoka kula nje pasipo Shani kujua, naye Baraka akashukuru sana hasa kwa sababu ilikuwa ni pesa nyingi. Kwa kuwa sasa Dylan alikuwa ana simu, alikuwa na kawaida ya kuwasiliana na rafiki zake wa huku. Hivyo aliwaacha na kurejea jijini kwao alikoishi, akijihisi furaha sana moyoni.


★★★


Grace alikwenda pamoja Dylan kwenye party ya rafiki zake siku kadhaa baadae, ambao walimfahamu Dylan pia. Ilikuwa ni kama sherehe ndogo tu ya kujitumbuiza, na waliokuwa hapo walikuwa wanawake na wanaume wenye pesa ambao walijuana na Grace kwa muda mrefu hasa kutokana na masuala ya kikazi. Wengi wao walikuwa wenye miaka 30 kwenda mbele, hivyo ni Dylan pekee ndiye aliyekuwa mwenye miaka ya chini kuzidi wote. Lakini kutokana na akili yake nyingi, kujichanganya kwake pamoja nao kulimfanya aonekane kuwa mkubwa sana kutokana na jinsi alivyoweza kuchangamana nao vizuri.

Walifanyia party hii kwenye nyumba ya rafiki yake Grace aliyeitwa Nasma, ambaye ndiye aligharamia kila jambo lililofanyika hapo. Walikuwa wakila nyama za kuchomwa, wakinywa vinywaji, wakicheza muziki, na wanawake hao walivaa kwa kujiachia; vigauni vilivyoishia mapajani na kuibana miili yao sana, blauzi zilizoonyesha sehemu kubwa ya matiti yao, na wachache hata walikuwa wamevaa sidiria na chupi tu kama wazungu vile.

Ni Grace pekee ndiye ambaye alivaa nguo iliyositiri mwili wake; nguo fulani laini iliyounganika mpaka chini kufikia miguuni, yenye mtindo wa suruali, iliyoonyesha umbo lake vizuri lakini ikificha mgongo wake. SIKUZOTE alivaa nguo zilizofunika mgongo wake, na hata wengine walipoanza kuogelea na kumwita ajiunge nao, jibu lake lilikuwa ni hapana kama ilivyokuwa pindi nyingi za nyuma.

Ilifika hadi mida ya saa sita usiku wakiwa nje hapo; baadhi ya rafiki zake Grace wakiwa ndani ya swimming pool, na wengine wakiwa pembezoni wamekaa huku wakifurahia maongezi.

"Mwanamke mweusi ana raha yake achana na haya makuku ya kizungu! Yaani wanawake weupe wamepoa kama vipolo vya uji!" akawa anasema rafiki yao aliyeitwa Sebastian, akimtania Nasma kwa kuwa alikuwa mweupe.

"Kwenda huko wewe, hauna lolote! Hapo ukilambishwa nyeupe hiyo nyeusi hutaitamani hata chembe!" Nasma akamjibu pia.

"Nimezipitia hizo kama review na zote zinakuwa za baridiii...sijui wanafugaga friji humo ndani?" akasema Sebastian.

"Hahaaaa...huo ndiyo utamu wa mirinda nyeusi, lazima iwe ya baridi babu we! Sisi weupe tuna mambo yetu kwa weusi adimu. Yaani hadi maji ya kuoga yanaonjwa unafikiri mchezo? Utaipata hiyo kwa cheusi wako?" Nasma akamwambia Sebastian, na wote hapo wakacheka sana.

Wawili hawa walikuwa wenye ukaribu sana hivyo walipenda kutaniana.

"Ndiyo maana ndoa mnazisikia kwa Chereko ya TBC tu," akasema Sebastian.

"Pesa kwanza baba, ndoa mpaka miaka 60 huko," akasema mwanamke aliyeitwa Hamisa.

"Nyie ndiyo wa kuolewa? Hahahaaa...yaani siku Hamisa, Sarah, Nasma, na Asia mkiolewa nahudhuria hizo ndoa nikiwa uchi! Hapa wa kuolewa ni Grace tu," akatania Sebastian.

Wote wakacheka sana.

"We hujaona kwamba ni wanawake wenye sura, au umbo la kawaida na tabia pole tu ndiyo huwa wanaolewa? Hawana makuu kama hili hapa ndiyo maana lipo lipo tu!" akasema Sebastian, akimtania Nasma.

"Huna lolote wewe. We ndiyo wale...aah-ahhh subiri...yaani wewe ndiyo wale mnaopenda vipya tu halafu mnasahau mlivyoanza navyo maisha tuhela tukishaanza kuingia...au nadanganya?" Asia akamwambia Sebastian.

"Kwani kuna mtu amewakataza kuanza na vipya? Suala siyo vipya wala vikuukuu, haya makolo-ubweche yamejaa tamaa tu hata kama ni vipya yakienda navyo kidogo tu yanachoka, yanataka vingine," akasema Nasma.

"Lakini siyo na mimi. Sebastian tu ndiyo kolo-ubweche," akatania Dylan, nao wote wakacheka.

"Sisi hapa tunajua pesa...eeh...hatuna time na visumbua fikira. Kwa hiyo hata kama ni ndoa ikifika mbona tunajua kutulia...na tunatenda haki kisawasawa," akasema Sarah.

"Aa wapi! Mnakuwa mnariiinga sana...mara ooh leo naumwa...mara eti sijisikii kupiga pachu pachu... Unafikiri nikitoka hapo nikakutana na barmaid ametutumka ntamwacha salama?" Sebastian akasema kiutani.

Wanawake wakaanza kumpondea maneno Sebastian na yeye akawa akijaribu kubishana nao huku wanacheka. Kwa asilimia kubwa ni Grace na Dylan ndiyo waliokuwa wanawasikiliza tu na kuchangia maongezi yao kidogo mno kwa kuwa walikuwa watulivu.

"Kwa hiyo Grace ndo' chaguo lako?" Sarah akamuuliza Sebastian.

"Haswaa! Toto limetuliaaa...em' licheki kwanza! Yaani kwa wewe Grace sijui tunafanyaje tu ku-win!" Sebastian akasema.

Grace akacheka kisha akasema, "Sahau."

"Dah! Yaani mpaka huwa najiuliza unatakaga kiwango gani mtoto? Yaani ni kama hakuna jamaa yeyote anayeweza kufika hapo, eti Ethan?" Sebastian akasema.

"Ahahahah... hamna bwana. Grace, unaona ameanza kukusema sasa? Anaona unazeeka, acha kujibania sana utafute mtu mzuri umwonyeshe huyu pimbi," Dylan akatania.

Wote wakacheka, lakini Grace akaangalia chini akitafakari maneno yake.

"Seb unajishaua tu. We mwambie kama unamtaka maana ngozi tu hiyo imeshakupagawisha hapo, ukiachilia mbali kalio," Asia akamtania Sebastian.

"Grace angekuwa na papara angeumiza wengi sana, ila baby wangu ametulia mno huyu, tena usije nyanyua dole lako sisi wote hapa tutakuua," Nasma akamwambia Sebastian.

"Aaah...sisi wanaume hatunaga hizo dhambi kabisa. Tukipenda tumependa. Yaani unakuta wanaume tunaoa mwanamke ana watoto watano kabisa na tunawahudumia wote! Tunaendaga peponi kabisa sisi au siyo Ethan? akasema Sebastian.

"Hapo unakuwa unayapa matatizo massage," akasema Dylan, na wote wakacheka sana.

Ijapokuwa maongezi yao yalikuwa yana utani mwingi, lakini kwa Grace yaliacha jambo fulani moyoni mwake lililomkumbusha vitu vingi vilivyofanya ahisi kukosa amani; bila yeyote kujua.

Baada ya muda fulani, wawili hawa waliagana na rafiki zao na kuanza kuelekea nyumbani. Njia nzima kurudi wakiwa kwenye gari, Dylan alimsemesha sana Grace kirafiki, lakini akatambua ni kama Grace alizama sana kwenye mawazo ya kitu fulani kilichofanya jinsi alivyoitikia kusiwe kuzuri. Hivyo aliona amwache tu na kubaki kimya mpaka walipofika nyumbani. Grace akaegesha gari tu na kuelekea ndani, bila kusema lolote akionekana kama mtu aliyekwazwa, akimwacha Dylan anajiuliza ni nini kilikuwa kimempata mwanamke huyu ghafla. Lakini kwa haraka akafikia mkataa tu kuwa huenda alikuwa amechoka, hivyo naye akaelekea ndani kwenda kupumzika.


★★★


Dylan aliendelea kuendesha mambo kwenye kitengo alichopewa ndani ya kampuni yake Grace, na sasa wengi walikuwa wakiona matokeo mazuri kutokana na njia yake ya kufanya mambo. Kazi zote alizoongoza na kusaidia kufanya zilileta mafanikio na uradhi mwingi kwa wafanyakazi wa hapo, nao wakazidi kumpenda.

Siku kadhaa zilipita, naye Dylan alitaka kufanya mpango wa kumleta Leila upande huu wa jiji ili kumtembeza, kwa sababu alim-miss sana mrembo wake huyo. Alitaka kumfanyia 'surprise' kwa kumpeleka sehemu nzuri ambayo alijua ingemfurahisha sana. Lakini kwa sababu fulani, Leila hakuwa akipokea au kujibu jumbe zake, na hata alipopata nafasi ya kumjibu, alisema tu alikuwa bize na mambo mengi hivyo hakuwa hata na muda wa kushika simu. Akampa pole, naye Leila akamwambia angemtafuta baadae. Dylan hakuona ubaya wowote kwenye hilo, hivyo akaendelea na kazi zake.

Baada ya kumaliza kazi kwenye mida ya jioni, alianza kuelekea nyumbani sasa kwa ajili ya kupumzika. Mara nyingi alichukua usafiri wa kulipia uliompeleka mpaka nje ya geti la nyumba ya Grace. Alipofika alianza kulielekea geti, lakini kabla hajalifikia, akatoka mwanaume fulani ndani hapo ambaye hakumtambua kwa haraka. Alikuwa amevaa kofia iliyoficha uso wake kiasi, na nguo zake zilikuwa nadhifu tu kama wafanyakazi wa kwenye kampuni yao. Alipopishana naye, mwanaume huyo akamtazama Dylan kifupi machoni na kumtikisia kichwa mara moja kama salamu, naye Dylan akaitikia kwa njia hiyo hiyo, kisha akaondoka hapo.

Ni baada ya Dylan kuitafakari sana sura ya mwanaume huyu kwa kifupi ndipo akahisi ni kama alimfahamu, lakini hakujua ni kutokea wapi. Akaingia ndani ya nyumba akiwa bado anamtafakari, akijaribu kuvuta taswira ya ni wapi ambapo aliwahi kumwona, na sasa akaweza kukumbuka kikamili alipomfahamia mwanaume huyo.

Kipindi kile baada ya kumaliza ujenzi wa daraja, alikumbuka kuna mwanaume alionekana kama anamwangalia sana wakati yuko saluni, na hata siku ile alipocheza mpira alimwona. Ilikuwa ndiyo huyu huyu aliyetoka hapa sasa hivi. Alijiuliza kidogo mwanaume huyu angefahamiana vipi na Grace mpaka kuja kwake, na hata tu jinsi alivyojiweka ungedhani anaficha kitu fulani. Alilikuta gari la Grace ndani hapo sehemu ya kuegeshea, hivyo ni wazi mwanaume huyo alikuwa ni mgeni wake aliyetoka kuonana naye.

Alienda moja kwa moja mpaka chumbani na kujisafisha, kisha akatoka ili aende sehemu ya sebule. Chumba chake kilikuwa kwenye ghorofa ya pili ya nyumba hii, hivyo aliposhuka ngazi na kufika chini, alimwona Grace akiwa anatokea kule juu pia akija chini, kwa hiyo akasimama hapo ili kumsubiri afike chini. Kufikia wakati huu, Grace alikuwa amesuka nywele ndefu na laini zilizomfikia mgongoni, na alivaa blauzi ya mikono mirefu, suruali laini nyeupe, na viatu virefu kwa chini. Alikuwa anatembea taratibu huku akiongea na mtu fulani kwenye simu yake.

Dylan alianza kumwangalia kwa uvutio mwingi. Hangeweza kujizuia kumwangalia kwa matamanio ilhali alitambua kabisa kwamba kuwa naye isingewezekana kwa sababu uhusiano wao ulikuwa na mipaka kama ya kaka na dada, na yeye tayari alikuwa na uhusiano na Leila. Hivyo akajitahidi kutoyaruhusu mawazo yake yafike mbali mno. Akaendelea kumtazama mpaka alipofika ngazi ya tatu chini na kusimama; akimalizia kuongea na simu. Baada ya kukata, akamwangalia Dylan na kutabasamu, naye Dylan akatabasamu pia.

"Ndiyo umerudi?" Grace akauliza.

"Yeah. We umefika zamani eeh?" Dylan akamuuliza pia.

"Siyo sana. Ninataka kuto...oow!"

Grace alikuwa ameanza kupiga hatua kuja chini na kutaka kusema alikuwa anataka kutoka tena, lakini akaukwaa mguu wake mmoja na kukaribia kuanguka. Dylan alimwahi na kumdaka ili aziangukie mwili wake vibaya sana, kwa kuushika mwili wake kama amemkumbatia, huku Grace akionyesha uso wa maumivu akiangalia chini.

"Pole..." Dylan akasema akiwa bado kamshikilia.

"Anhh...ssss..." Grace akatoa sauti iliyoonyesha alihisi maumivu.

"Mguu? Unauma?" Dylan akauliza.

Grace akatikisa kichwa taratibu kukubali.

"Okay, come on. Twende ukae," Dylan akasema.

Akaanza kumsaidia kwa kumpa egamio kutembea polepole kuelekea upande wenye masofa, kisha akamketisha hapo na kumvua viatu. Akaushika mguu wa Grace ulioumia na kuugeuza, naye Grace akatoa sauti ya maumivu na kumwambia aache. Msaidizi wa kazi kwenye nyumba hii, aliyeitwa Matilda, alifika hapo na kuuliza kwa kujali ni nini kilikuwa kimetokea, naye Grace akamwambia ametegua mguu wake hivyo angehitaji dawa.

"Dawa ya nini?" Dylan akauliza.

"Ya kuchua," akasema Matilda.

"Hakuna haja, acha tu nikunyooshe," Dylan akasema huku anauchukua mguu wa Grace.

"Wewe! Hapana! Nitaumia," Grace akamzuia.

"Ni kidogo tu lakini..baada ya hapo utapoa. Ona umetegukia kwa hapa..."

"Hapana Ethan...no. Matilda..."

"Sawa dada, nakuletea," Matilda akasema na kuelekea juu.

"Grace, unadeka wewe!" Dylan akamtania.

"Siyo kudeka bwana. Aagh...sasa hapa nitaondokaje na mguu huu?" Grace akasema.

"Ulikuwa unaenda wapi?"

"Kwa....rafiki. Ila itabidi niahirishe," Grace akasema.

"Kama ilikuwa muhimu nenda mguu ukishapoa kidogo."

"Hapana yaani...hii kitu yote imeniondolea mood kabisa."

"Pole."

Ni wakati huu ndipo Matilda akawa amerejea na dawa ya kuchua mishipa na misuli. Akaanza kumpaka Grace taratibu kwenye mguu huo, huku Dylan akimwangalia Grace kwa kujali. Baada ya Matilda kumaliza, Grace akanyanyuka na kusema angerudi tu chumbani kupumzika, hivyo akamwambia msaidizi wake ampelekee chakula kiasi baadae huko huko chumbani. Dylan alipotaka kumsaidia kwenda, Grace akasema haikuwa na shida kwa kuwa angeweza kwenda mwenyewe. Lakini akiwa anatembea kuzielekea ngazi, alijivuta sana na kufanya Dylan atambue kuwa mguu huo uliumia zaidi ya alivyofikiria. Hata tu jinsi alivyokunja sura yake ilimdhihirishia mwanaume kuwa kweli maumivu aliyohisi Grace yalikuwa mengi. Hivyo, akaamua kwenda kumsaidia hivyo hivyo tu.

Grace alikuwa ameanza kupanda ngazi lakini kwa shida, hivyo Dylan akafika kando yake na kuuweka mkono wake mmoja kiunoni kwa Grace kisha kuushika wa bibie na kuuzungushia kwenye bega lake. Grace akaweka kipingamizi, huku Dylan akiendelea kusisitiza tu amsaidie, lakini mwishowe Grace akamzuia kabisa kwa uthabiti kuwa angeweza kwenda mwenyewe.

Dylan alimshangaa kwa kiasi fulani, akijiuliza ni kwa nini ilikuwa kama Grace alijisogeza mbali sana na wanaume. Sikuzote alikuwa makini sana kutokuwa na mazoea yenye ukaribu ulipita kiasi na mwanaume yeyote, lakini Dylan kama Dylan hakutaka kujali hilo wakati huu. Alitaka kumsaidia hata kama angemkasirikia kwa kufanya hivyo. Akamfata tena na kupitisha mkono mmoja ubavuni kwake na mwingine kwenye miguu yake, kisha akamnyanyua na kumbeba. Ilihitaji nguvu sana kwa kuwa Grace alijazika haswa, lakini kwa Dylan hilo halikuwa na shida.

"Hey Ethan! What are you..." Grace akauliza akiwa hajatarajia jambo hilo.

"Acha kuwa mbishi...twende nikupelek..."

"Nishushe bwana...usini..."

"Grace, usiwe na matata kama Grace ma..."

*Acha masihara Dylan, em' nishush...!"

Grace akatulia kidogo baada ya kutambua alifanya jambo ambalo hakutakiwa kufanya. Akabaki kumwangalia tu Dylan usoni, ambaye pia alikuwa anamtazama kwa kuchanganywa na maneno yake.



★★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★★

WhatsApp +255 787 604 893
 
DYLAN

Story by Elton Tonny

Familia, Kazi, Urafiki, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Unyanyasaji, Usaliti, Visasi, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

(R-rated 18+)

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE

★★★★★★★★★★★★★★★★★


Lakini hapo hapo Dylan akaanza kucheka kwa kufurahishwa na Grace, huku yeye Grace akiendelea kumtazama kwa wasiwasi kiasi.

"Ahahahah... inaeleweka ukijikwaa miguuni lakini hadi na ulimi pia? Dylan ndiyo nani?" Dylan akauliza bila kutambua kihalisi alikuwa anajiulizia yeye.

Grace akaendelea tu kumwangalia.

"Wewe ni mzito Grace. Kwa hiyo tulia nikufikishe kwanza ndiyo ulalamike vizuri," Dylan akasema kiutani.

Dylan akaanza kupanda ngazi polepole akiwa amembeba mwanamke huyu hodari. Grace alipata hisia fulani mpya ambazo alijitahidi sana kuzizuia zisikite mizizi ndani yake, kwa sababu alizozijua yeye tu. Dylan angemwangalia mara kwa mara na kutabasamu tu, naye Grace angetikisa kichwa chake akijifanya amekwazwa na jambo hilo.

Baada ya Dylan kumfikisha chumbani, alimpeleka moja kwa moja mpaka kitandani na kumweka taratibu. Akiwa anamwachia, Dylan alimwangalia Grace usoni kwa ufupi, naye Grace akamtazama vilevile. Utizami waliopeana ulikuwa wa ajabu kidogo kwa sababu ni kama kuna hisia fulani zilizofichika zilionekana kwa mmoja na mwenzake baada ya kutazamana kwa ukaribu huo. Lakini Dylan akaachia tu tabasamu la kirafiki na kumuaga, kisha akaenda zake kule chini.

Grace alibaki hapo akitafakari mambo mengi sana. Alikuwa na mzigo mzito mno kwenye akili yake ambao alipaswa kuutua kwa wakati uliofaa na kwa njia aliyokuwa amepangia, hivyo alijua alihitaji kuwa makini zaidi na kila jambo alilofanya au kusema.


★★★


Siku iliyofuata, Dylan alikuwa kwenye kampuni kama kawaida akiendelea na kazi. Kulikuwa na mwanamke fulani aliyefanyia kazi hapo, aliyeitwa Loreen, ambaye alivutiwa sana na Dylan (Ethan). Alikuwa ameshamwambia mwanaume kuwa alimpenda, lakini kwa unyoofu Dylan akamwambia tayari alikuwa kwenye uhusiano. Ijapokuwa hivyo, bado Loreen aliendelea kuonyesha kupitia vitendo vya kichokozi kuwa alimhitaji sana, na hili likawa linasababisha asikazie fikra kazi zake zaidi.

Kwa sababu hiyo, ilibidi Dylan akae naye siku hii ili wazungumze vizuri, na akamweka wazi kwamba ikiwa angeendeleza uzembe kwa sababu za kibinafsi basi angefutwa kazi siku moja. Lakini Loreen alianza kumbembeleza Dylan kwa njia ya kimahaba, na hapa Dylan akatambua kweli mwanamke huyu alikuwa mbinafsi. Walikuwa wakizungumza ofisini kwake, na Dylan alipomwambia aache kwa mara nyingine, Loreen alimfata na kumpiga denda kwa lazima. Ni wakati huu ndipo Grace akawa ameingia ofisini humo na kukutana na picha hiyo ambayo hakuwa ameitarajia.

Dylan akamsukuma nyuma Loreen, ambaye alianza tena kujisogeza-sogeza mwilini kwake kwa mitindo ya kumzuzua, na hapo hapo Grace akamwita Loreen kwa sauti ya juu, kitu kilichofanya wawili hao washtuke. Dylan alijua bila shaka Grace alikasirishwa na jambo hili, naye Loreen akajiinamia akionekana kuogopa sana. Grace akamwita Loreen na kumwambia amfate ofisini kwake, kisha akampa Dylan utizami wenye kuonyesha ukali kiasi na kuondoka. Dylan akajua hapo lazima kingenuka haswa!

Baadae Dylan akaanza ofisini kwa Grace kumweleza kuhusu kile kilichotokea hasa na siyo kile ambacho huenda alifikiri. Alipokaribishwa kuingia ofisini kwake Grace, alimkuta bibie akiwa ameketi kwenye kiti chake huku anamtazama sawia.

"Grace...kwanza kabisa, naomba samahani kwa sababu..."

"Kwa sababu nimekuta unabusu mwanamke ofisini?" Grace akamkatisha.

"Aaaa..."

"Eeeee...ndo' umeanza kujifunza kuongea au?" Grace akamwambia kikejeli.

"Siyo unavyofikiria Grace," Dylan akasema.

"Ninafikiria nini?"

"Najua hujapenda ulichoona...na..."

"Ethan, hauhitaji kuomba samahani. Ninajua vizuri tokea mwanzo kwamba Loreen anakutaka na amekuwa akikusumbua kwa muda sasa," Grace akasema kwa uhakika.

"U..ulijuaje hilo?"

"Naijua kampuni yangu vizuri Ethan, na wewe uko ndani yake. Kwa hiyo skip all this nonsense and just get back to work (...achana na huu upuuzi wote urudi kuendelea na kazi)," Grace akasema.

Dylan akamtazama kwa njia yenye mashaka kiasi. Alitegemea angekuta amefura lakini kwa kushangaza alimtendea vizuri.

"Okay. Asante kwa uelewa wako Grace," akamwambia.

"Your welcome," Grace akajibu.

"Aam...vipi kuhusu Loreen?"

"Nimemwonya. The next time nikimkuta anachezea time, namfukuza."

"Samahani sana tena Grace..."

"Aaagh...Ethan bwana.... Nimekwambia achana nayo, relax, and just go," Grace akasema.

Dylan akatabasamu kidogo.

"Okay. Vipi mguu?" akauliza.

"Unapoa. Asante pia kwa...kunisaidia jana," Grace akasema.

"Ahahah... sasa je! Nisingefanya vile ungekuja unatambaa leo," Dylan akatania na kumfanya Grace atabasamu pia.

Waliangaliana kifupi kwa njia fulani ambayo ilikuwa...mpya. Yaani ilikuwa ni kama kila mmoja wao alisubiri mwenzake aseme jambo fulani, na utizami huo ukavunjwa baada ya simu yake Dylan kuanza kuita. Akaitoa mfukoni na kuangalia mpigaji, kisha akamuaga Grace na kutoka ofisini kwake. Grace akachukua simu yake na kumpigia mtu fulani, na mtu huyo alipopokea, Grace akaanza na maneno haya, "Jafari, nisikilize kwa makini...."


★★★


"Oy vipi?" akasema Dylan baada ya kupokea simu alipotoka kwenye ofisi ya Grace.

"Safi tu. Umetutupa sana mhuni," akajibu rafiki yake kwenye simu, yaani Fred.

"Hamna kaka. Sema mambo yanakuwa mengi kidogo ila tuko pamoja," Dylan akasema.

"Poa. Hivi ulisikia mama yake Oswadi alivyofumaniwa anadonyoana na Omari?"

"Wewe! Wapi?"

"Kule Bayi Guest. Alipigwa siyo mchezo."

"Aliyewafumania alikuwa mume wake?"

"Hamna, ilikuwa ni Oswadi. Sema inaonekana alikuwa ameshawajua kutokea kitambo kwo' akasubirishia wajibane kwa sababu alienda na wasela wengine pale mpaka chumbani na kumpa jamaa kipondo."

"Dah! Kwa hiyo Omari yuko wapi sasa?"

"Omari alikimbia, mpaka leo hatujui ameenda wapi. Wamemtafuta sana lakini jamaa kapotea. Ahahahah mwanangu usije kujaribu, mke wa mtu sumu."

"Ila hapo aliyeonyesha uchungu ni mwanae. Usaliti siyo kitu kizuri kabisa," Dylan akasema.

"Eeee. Halafu unajua, kuna kitu nimekumbuka boy. Huyo demu....Leila...simwelewi mwanangu," Fred akasema.

"Unamaanisha nini?" Dylan akauliza.

"Nilikuwa nataka kukuuliza ka' bado unatoka naye."

"Ndiyo, bado ni mtu wangu."

"Dah!"

"Kwani vipi?"

"Yaani, unaweza ukaona kama vile nachonga uwongo mwanangu lakini lazima nikwambie ukweli. Huyo demu siyo," Fred akasema.

Dylan akaweka umakini wake vizuri zaidi.

"Kwani amefanyaje?"

"Juzi kati hapa nilimwona mida ya saa 2 hivi usiku amebananizwa gizani kwenye kona na jamaa fulani hivi...walikuwa wamekumbatiana yaani...kimapenzi mwana."

Dylan hakuamini alichosikia. Akabaki amezubaa asijue cha kusema.

"Uko sure kabisa na unachosema Fred?" Dylan akauliza.

"Sikutanii mwanangu. Tena nikafikiri labda niliona vibaya, ila baadae nikamwona kwa mbali kama anaagana na huyo jamaa, af' ana gari, ndiyo akarudi upande wetu akielekea kwenda nyumbani. Nikajiuliza labda mlikuwa mmeshaachana au vipi? Sasa hapo inakuwaje?" Fred akasema.

Dylan akashusha pumzi ndefu na kutikisa kichwa kwa kusikitika. Alihisi ni kama hii haingeweza kuwa kweli mpaka ajihakikishie mwenyewe.

"Okay. Fred...nitahitaji kuhakikisha jambo hilo. Nataka uwe unaniangalizia Leila, na ukiona kitu suspicious namna hiyo, unishtue...hata ukitaka nitakulipa," Dylan akasema.

"Dah, kwo' niwe kama spy wako au siyo?"

"Nisaidie tu kwa hill kwa sababu niko mbali. Na, ujitahidi kuwa makini, sitaki ahisi anafatiliwa."

"Usikonde mwanangu, tuko pamoja. Nikimdaka tu tena nakushtua."

Dylan akainamisha uso wake kwa huzuni.

"Oya, mechi ya sisi na town inachezwa Jumamosi hii. Kama vipi ukuje maana tunaenda kule kwenye uwanja wao," Fred akamtaarifu.

"Aaaa...sawa nitaangalia, then nitakwambia," Dylan akasema, akiwa ameishiwa pozi kabisa.

Baada ya wawili hawa kuagana, Dylan aliketi chini kutafakari mambo yote aliyosema Fred kumhusu Leila. Hakutaka kukubali kabisa kwamba mwanamke wake angemtendea namna hiyo ukitegemea na mambo waliyopitia pamoja, hata ingawa hawakuwa na mahusiano ya muda mrefu sana. Lakini alijua pia kwamba angehitaji kuthibitisha, na kama ingekuwa ni kweli basi angeamua la kufanya. Kwa wakati huu alichotakiwa kufanya ilikuwa ni kuhakikisha hamwonyeshi Leila kama amepata taarifa hiyo mbaya sana kumhusu, ili aweze kumkamata kwenye tendo lenyewe.


★★★


Ilipofika Jumamosi, Dylan aliongea na Baraka kupitia simu na kumuuliza kama angekwenda kutazama mechi baina ya timu ya kwao na ya mjini kwao kule. Baraka akasema aliona ingekuwa mbali na gharama ingekuwa kubwa pia, lakini Dylan akasema angemsaidia kwa jambo hilo na hata ikiwezekana aende na familia nzima kupata burudani hiyo. Baraka alifurahi sana na kusema angekuwa tayari kwa hilo, hivyo akaanza kufanya maandalizi ya kwenda pamoja na familia. Baadae, Baraka akamjulisha Dylan kwamba ambao wangeenda ilikuwa ni yeye, Shani, Emilia na Steven, hasa kwa kuwa walitamani sana kuitumia nafasi hiyo kufanya matembezi, lakini Leila alisema hangeweza kwa kuwa alijisikia vibaya.

Jambo hilo liligonga taa nyekundu ya hatari kwenye akili ya Dylan, na hata ijapokuwa alijitahidi kutofikiri labda ana-panick, hakutaka kupuuzia uwezekano wa kwamba Leila alidanganya ili afanye mambo yake mengine. Kwa hizi siku chache zilizopita, alikuwa amewasiliana naye mara chache tu na kila wakati walipoongea Dylan angeweza kuhisi utofauti wa jinsi Leila alivyomwitikia; yaani haikuwa kama zamani. Kuna wakati alimtania kwamba anaogopa kwa sababu ya kuwa mbali naye basi atakuta amechukuliwa na mtu mwingine, lakini Leila akamuahidi kwamba hiyo haingeweza kutokea.

Waliokuwa wanajua kuhusu uhusiano wake na Leila walikuwa ni Fred, Grace, Pili na Sada (rafiki zake Leila), na Emilia, ijapokuwa hakuna yeyote aliyedhani binti huyo alijua. Dylan alikuwa anataka kumwambia Baraka kwanza kwamba anampenda binti yake, lakini kutokana na taarifa aliyopewa na Fred kuhusu Leila, akaona asubiri kwanza maana mambo yalikuwa yanaelekea kuvurugika.

Kwenye mechi hiyo Fred angekuwepo kama mchezaji pia, hivyo Dylan alijua wazi kwamba hakungekuwa na mtu wa kumwangalizia ikiwa Leila angetenda mambo kisiri. Kwa hiyo alichofanya ilikuwa ni kumtumia pesa Baraka kwa ajili ya familia yake kwenda kwenye mechi, kisha yeye akamwomba Grace gari lake moja kwa kusema kuna sehemu alihitaji kwenda mara moja, ili YEYE MWENYEWE aende kule kwao Leila kumfatilia.

Dylan alifikia hatua hii kwa sababu kutoka ndani kabisa ya moyo wake hakupenda usaliti, kwa hiyo ijapokuwa bado hakuwa na kumbukumbu zake zilizopotea, utu wake haukuwa umebadilika kwa asilimia zote. Aliona hii huenda ingekuwa nafasi ya kuthibitisha uaminifu wa mpenzi wake huyo, na angefanya hivyo bila yeyote kujua.

Ilipofika mida ya saa 7 mchana, aliondoka na gari moja la Grace kuelekea kule kwenye mji wa Baraka. Ingemchukua masaa mawili kufika huko, na kwa kuwa mechi ilitakiwa kuchezwa saa kumi na nusu, kufikia muda ambao angekuwa amefika bila shaka Baraka na familia yake wangekuwa wameondoka. Ikiwa kweli Leila alikuwa ana nia mbili, basi kusema alikuwa anaumwa kulikuwa kisingizio kibaya sana. Hiyo ingemaanisha alipaswa kukaa nyumbani mpaka wengine waondoke, ndiyo angeweza kufanya mambo yake. Dylan kwa kutambua jambo hilo ndiyo kulimfanya achukue uamuzi huu, na sasa angeweza kusubiri tu aone jinsi ambavyo mambo yangekwenda.

Alifika kule kwenye saa tisa na nusu hivi, naye akaliegesha gari sehemu ambayo ilikuwa na mti mkubwa. Aliliweka gari sehemu sahihi kabisa ambayo ilikuwa ni pembezoni mwa mwingilio wa daraja lile kuelekea upande wa pili wa eneo la kina Baraka, na hii ilikuwa kwa sababu mbili. Kwanza, alikaa hapo ili kama Leila angetoka kule kwao basi angeweza kumwona. Na pili, Fred alimwambia kwamba siku ile alipomwona Leila na yule mwanaume, alikuwa na gari, hivyo ikiwa mwanaume huyu angemfata Leila basi angekuja na gari eneo hilo amsubirie aje au moja kwa moja mpaka nyumbani kwao Leila ili amchukue huko. Sehemu hii aliyoegesha gari ilimruhusu kuona kufikia upande wa pili wa daraja, kwa hiyo kama gari la huyo mwanaume lingepita huko, basi angeliona.

Eneo hilo lilikuwa kama tu jinsi alivyolikumbuka, na watu kadha wa kadha walipita na kufanya shuguli zao. Haikuwa kufikia kule kwenye soko, bali sehemu yenye nyumba chache na maduka madogo ya bidhaa. Dylan aliendelea kukaa humo humo ndani ya gari lake mpaka inafika saa 10 jioni, na hapo akaiona familia ya Baraka wakitokea darajani, kisha wakachukua usafiri wa pamoja na kuondoka. Alijua bila shaka walikuwa ndiyo wanaelekea kufurahia mechi na matembezi, hivyo akampigia simu Baraka na kumuuliza kama walikuwa wameshaondoka, na kama Leila alikuwa nyumbani bado. Baraka alijibu ndiyo kwa yote, na sasa Dylan alichohitaji tu kufanya ni kuendelea kusubiri hapo na kutazama viashiria vyovyote vile kwa umakini.

Hakukutokea jambo lililovuta umakini wake mpaka ilipofika saa 11 kasoro, pale alipomwona Leila akitokea upande ule wa daraja. Mapigo ya moyo wa Dylan yalianza kwenda mbio kiasi kwa kuwa ilikuwa ni kama alichofikiria kilikuwa karibu kutokea, lakini akajitahidi kujipa moyo kuwa huenda angekuwa anatoka kwenda tu sehemu nyingine; kama kujifariji. Leila alipendeza sana kwa kuvalia T-shirt nyeupe na suruali nyeupe pia zilizombana na kuchora umbo lake vizuri, naye akachukua bodaboda na kuanza kuondoka eneo hilo. Bila kuchelewa, Dylan aliwahisha gari nyuma yake na kuanza kumfatilia, akijitahidi kutoachwa na bodaboda ile kutokana na kwenda kwa kasi.

Walifika mpaka eneo la mjini kwenye mji wao, na hii ilikuwa ajabu kwa sababu Leila alikataa kwenda kuangalia mechi mjini kwa kusema anaumwa halafu baada ya familia yake kuondoka yeye akachukua bodaboda na kuelekea huko huko. Dylan alizidi kupatwa na hofu lakini akajikaza tu na kuangalia haya yote yangempeleka wapi. Binti akashuka eneo fulani lililokuwa na maduka mengi mjini na wanaharakati wakipiga kazi mbalimbali, na baada ya kumlipa bodaboda akaanza kuelekea upande mwingine kwa kutembea. Yote haya Dylan aliyaona, na ili kutaka kujihakikishia mambo zaidi, akampigia simu Leila.

Kutoka alipokuwa amesimamisha gari, aliweza kumwona Leila akisimama na kutoa simu yake mfukoni, kisha akapokea. Dylan akamsalimu kwa kumuuliza anaendeleaje, naye Leila akasema bado hakujisikia vizuri kabisa, na kutania kwamba alihitaji kula kuku mzima kabisa hivyo Dylan (Ethan) amtumie hela. Kwa ujanja, Dylan akasema angeituma lakini akamuuliza angenunuaje sasa wakati alikuwa nyumbani, mgonjwa, na hakukuwa na mtu mwingine pale. Leila akasema angeagiza mtu wa jirani kwa hiyo haingekuwa na shida. Hii ikawa ni uthibitisho mwingine wa uwongo wa Leila kwa kuwa Dylan alijua vizuri kabisa kwamba hakuwa nyumbani. Hivyo akamwambia asijali; angemtumia pesa hiyo. Kisha wakaagana, naye Leila akaendelea kutembea.

Dylan aliendelea kusogeza gari taratibu kwa upande wa barabara, na hatimaye akamwona Leila anaingia ndani ya gari lingine jeusi, aina ya Mark X. Alibaki kuangalia tu jambo hilo bila kujua ni gari la nani, lakini wazo alilopewa na Fred halikuwa mbali sana kutoka kwenye akili yake. Akakaza viganja vyake kwenye usukani akihisi hasira kiasi, lakini akajitahidi kuwa mtulivu.

Gari hilo lilianza kuondoka eneo hilo, naye Dylan akaanza kulifatilia taratibu. Ilikuwa ni pindi yenye kumsumbua sana moyoni kwa sababu hakufikiria ingefika siku ambayo angehitaji kutumia njia hii kuhakikisha uaminifu wa mtu aliyemwamini. Gari hilo lilifika nje ya hoteli fulani kubwa yenye ghorofa 8, iliyoitwa TeX Palace Hotel, nalo likaegeshwa sehemu ya maegesho. Dylan alikuja kutokea nyuma yao na kuliegesha gari lake upande wa pili wa barabara kutokea kwenye hoteli ile, na alipoangalia usawa ule wa maegesho, akamwona Leila akitoka pamoja na mwanaume fulani mweusi, mwenye mwili mkubwa wa mazoezi. Alivalia miwani nyeusi machoni na nguo nadhifu zilizomfanya Dylan ajue alikuwa mwenye pesa.

Wawili hao wakaelekea ndani ya hoteli ile, naye Dylan akashuka upesi na kuelekea huko pia. Alipofika mwanzoni mwa milango ya kuingilia kwenye jengo, aliwaona wakiwa wanaelekea upande uliokuwa na lifti (elevator) na kuingia humo, hivyo akaingia upesi na kupiga jicho la haraka juu ya milango ya lifti hiyo. Aliona namba iliyoandikwa juu hapo inabadilika kutoka 0 kuwa 5, hivyo upesi akatoka hapo na kuanza kupanda ngazi kuelekea ghorofa ya tano. Alikuwa anaharakisha sana kupanda ngazi mpaka watu aliopishana nao wakawa wanamshangaa, lakini hakujali hilo.

Kutokana na kasi yake, alifika juu huko haraka na kutazama upande wa lifti ile, na hapo akawaona wawili hao wakiwa wameshatoka na kuelekea upande wa mbele pamoja; wakiwa wanatembea huku wameshikana viuno. Dylan alivunjika moyo sana, lakini hata hapo bado hakutaka iwe kweli kabisa. Akawafata taratibu mpaka walipoingia kwenye chumba kimoja, kisha akasogea mpaka hapo polepole. Akili yake ilimwambia ageuke tu na kuondoka kwa kuwa mpaka kufikia hatua hiyo alikuwa amekwishathibitisha kwamba Leila hakuwa mwaminifu, lakini moyo wake bado ulimzuia.

Akakishika kitasa na kukikunja kimkono taratibu, akitumaini hawakufunga kwa funguo ndani, na tukio zuri likawa kwamba hawakuwa wamefunga. Mlango ukafunguka, naye Dylan akausukuma taratibu na kuingia ndani humo. Alipofika mbele, alibaki amezubaa baada ya kuona jambo lililopasua vipande-vipande hisia zake. Leila, alikuwa amemkalia mwanaume huyo kitandani, huku akiwa kifua wazi tayari, na jamaa akinyonya titi lake la kulia. Mikono ya huyo mwanaume ilikuwa inalitomasa kalio la Leila huku binti akiwa ameelekeza uso wake juu akihema kimahaba na kiuno chake akikinyonga-nyonga.

Dylan akatokwa na chozi kisha akalifuta taratibu, akiwa hapo kimya kimya bila wawili hao kuwa wamemwona. Ni wakati jamaa alipotoa titi la Leila mdomoni mwake ili ambusu mdomoni, pale alipomwona Dylan akiwa amesimama hapo anawaangalia. Alishtuka sana na kukunja uso kimaswali asijue mtu huyu chumbani hapo alikuwa ni nani.

"Wewe! Unafanya nini hapa?" mwanaume huyo akafoka.

Ile Leila anageuka pia, akatoa macho yake kwa mshangao na kuanza kuogopa sana. Dylan akawa anamwangalia kwa njia ya kawaida tu, naye Leila akajitoa mapajani mwa jamaa na kuketi upande wa pili wa kitanda; akijifunika na shuka haraka huku akipumua kwa hofu kubwa sana.



★★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★★

WhatsApp +255 787 604 893
 
Back
Top Bottom