Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,147
- 14,699
- Thread starter
- #821
Haha![emoji23][emoji23]...ALISHANTO MBAGA leo kidigo apasuliwe korodani BAHARIA ANGEUMALIZA MWENDO ila bahati ilikua kwake
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Haha![emoji23][emoji23]...ALISHANTO MBAGA leo kidigo apasuliwe korodani BAHARIA ANGEUMALIZA MWENDO ila bahati ilikua kwake
Pamoja Sana bishopView attachment 2385020
320
“Vipi, kuna tatizo?” nilimuuliza Sharifa huku nikimtazama kwa umakini usoni.
“Hapana, nilikuwa naangalia saa,” Sharifa aliniambia huku akinyanyua bilauri yake ya mvinyo na kupiga funda kubwa. Nikashangaa iweje atazame saa kwenye simu wakati alikuwa amevaa saa ya mkononi! Hata hivyo nikapuuzia.
Muda huo huo simu yake ya mkononi ikaanza kuita, akaitazama kwa kitambo akionekana kama aliyekuwa akijishauri iwapo aipokee au aipotezee, kisha akabana taya zake na kuikata. Halafu akainua mkono wake wa kushoto kutazama saa yake ya mkononi na kukunja sura yake. Nikashangaa zaidi.
Kisha alichukua chupa ya Dodoma Wine na kumimina mvinyo katika bilauri yake japokuwa bilauri hiyo ilikuwa bado ina mvinyo nusu, alikuwa akimimina huku akiwa hatazami kwenye bilauri na alionekana kuwaza mbali. Bilauri ile ilijaa na mvinyo ukaanza kumwagika juu ya meza Sharifa akiwa hana habari. Nikamshtua, wakati huo mvinyo ulishaanza kulowesha kwenye suruali yake, akashtuka na kuruka huku akinitazama kwa aibu.
Kwa kuwa mvinyo ulimwagika na kuanza kusambaa juu ya meza Sharifa aliondoa haraka mkoba na simu yake toka juu ya meza huku akisonya, kisha huku akinitazama kwa jicho la wizi, akaondoka haraka kuelekea maliwato.
Hisia tofauti zilianza kuumbika kichwani mwangu, moyo wangu nao ulipiga kite kwa nguvu, hata hivyo niliendelea kutulia kwenye kiti changu nikimalizia chakula. Jambo moja nilikuwa na uhakika nalo, kuwa Sharifa alikuwa amemwaga ule mvinyo makusudi, kwa kuwa wakati ile bilauri ikiwa imejaa aliitupia jicho kisha akayahamisha macho yake akijifanya kutazama kando na kuendelea kumimina hadi nilipomshtua. Na hata mshtuko wake ulikuwa wa kuigiza.
Nilihisi kuwepo kwa hila fulani na hapo nikatamani kumfuatilia kule maliwato ili nijue nini kilikuwa kinaendelea lakini sikuweza kufanya hivyo. Nilipoyatupa macho yangu juu ya ile meza nikakiona kikaratasi kilichokunjwa vizuri, ambacho awali sikuweza kukiona kwa kuwa kilikuwa chini ya mkoba, nikashawishika kukichukua na kukifungua. Na hapo nikajikuta nikipigwa na butwaa. Karatasi ile ilikuwa na ujumbe ulioandikwa:
Jason Sizya, nakushauri uachane na upelelezi huu uliojiingiza na ufunge mdomo wako, la ukikaidi nakuhakikishia kwamba hatatuchukua siku moja kwa familia yako kuwa mikononi mwetu, tutawakata kiungo kimoja kimoja na watakufa taratibu lakini kwa maumivu makubwa. Hatukutishi ila tunakushauri zingatia ushauri huu na familia yako haitaguswa.
Kama kuna kitu ambacho sikukipenda maishani mwangu basi ni suala la kutishiwa maisha yangu au familia yangu. Sasa nilijikuta nikisisimkwa mwili wangu na damu ikaanza kunichemka na kukimbia kwenye mishipa yangu ya damu, vinyweleo mwilini na nywele kichwani zilinisisimka kwa hasira huku mapigo ya moyo yakianza kwenda mbio!
Sikusubiri, nikaikunja ile karatasi na kuinuka, nikaelekea kwenye maliwato ya wanawake alikokuwa ameelekea Sharifa, lakini nikiwa na tahadhari zote kichwani. Nilipofika nikasimama kwa muda pale katika mlango wa kuingilia huku nikisikiliza kwa makini, baada ya kuhakikisha hali ni shwari nikaingia nikiwa na nia moja tu, kumbana Sharifa anieleze ukweli.
Nilipoingia nikajikuta nimetokea kwenye ukumbi mpana na msafi wa maliwato uliokuwa na masinki kadhaa ya kunawia mikono. Nikayazungusha macho yangu kutazama eneo lile na kuiona milango kadhaa ya vyoo. Nikaanza kutembea kwa tahadhari nikiwa makini kutafuta ni choo kipi alichokuwa ameingia Sharifa. Wanawake wawili waliingia mle ndani na waliponiona wakashtuka, nikawapa ishara kuwa wasiwe na wasiwasi, nikaendelea kumtafuta Sharifa. Hata hivyo hakuwemo mle vyooni.
Nilipochunguza vizuri nikagundua kioo cha dirisha moja kilikuwa kimeondolewa na Sharifa alikwisha toweka. Sikutaka kusubiri, nikatoka mbio na kuelekea ukumbini kisha nikaufuata mlango mkubwa wa kutokea nje nikiwa sitaki kumpoteza Sharifa.
Kule nje manyunyu yalikuwa yamekata lakini kulikuwa na wingu zito lililoashiria kuwa mvua kubwa ilikuwa mbioni kunyesha. Bado hakukuwa na dalili za uwepo wa Sharifa, nikaamua kutoka kabisa katika eneo lile na kuvuka barabara kisha nikaelekea upande wa pili uliotazamana na ile Club, ambako kulikuwa na kijiwe cha madereva wa teksi waliokuwa wakisubiria abiria. Baadhi ya madereva hao walianza kunichangamkia, sikuwajali.
Nikaangaza macho yangu huku na huko lakini hakukuwa na dalili yoyote ya Sharifa. Kwa mwendo wa miguu, nikaanza kuondoka eneo lile nikiifuata Barabara ya Mwinjuma, sikutaka kuchukua teksi eneo lile kwa kuogopa kujiingiza kwenye hatari. Sikuwa nikimwamini mtu.
Wakati nikiwa natembea taratibu kando ya barabara, nyuma yangu kulikuwa na watu wawili waliokuwa wakija upande ule ule niliokuwepo na walikuwa wametokea katika Club ile ile. Niliporudisha uso wangu mbele nikamwona mtu mmoja akija upande niliokuwepo, sikuonesha kugwaya, nikapeleka mkono wangu kiunoni na kuipapasa bastola yangu na hapo mwili ukanisisimka, nikaendelea kutembea kwa mwendo ule ule.
Nilipofika katikati, wa nyuma na wa mbele wakiwa umbali sawa, nikasimama na kuinama nikijifanya kufunga vizuri kamba za viatu vyangu na wakati huo nikisubiri nione watu hao wangechukua hatua gani. Nilisubiri kuona kama wangesita basi ningeng’amua kuwa walikuwa watu wabaya kwangu lakini kama si watu wabaya wangepita na hamsini zao.
Yule aliyekuwa akija mbele yangu aliendelea na hamsini zake lakini wale watu wawili waliokuwa wakija nyuma yangu walisita kidogo, wakawa kama wanaojiuliza jambo huku mmoja akijifanya kutoa simu yake na kuanza kuongea, kwa vitendo hivyo nikajua wazi kuwa nilikuwa nawindwa. Nilichoamua ni kugeuza na kuanza kurudi kule kwa wale watu wawili, na hapo nikawaona wakiingiwa na woga fulani, nikaongeza mwendo kuwaendea.
Haraka sana nikamwona mmoja wao akipeleka mkono wake kiunoni huku akiniamuru nisimame. Nikakaidi amri yake na kuanza kuwapita kwa mwendo ule ule. Nilipowapita kwa hatua mbili tu wakageuka na mmoja wao tayari alishatoa bastola na kuanza kuielekeza kwangu. Jambo hilo nililitegemea tangu mwanzo nikageuka haraka kwa teke maridadi la karate na kuupiga mkono wake wenye bastola, ikamtoka na kuanguka chini.
Akiwa bado hajakaa sawa nikampiga konde moja lililotua shavuni, akaenda chini. Yule wa pili akarusha ngumi nikaudaka mkono wake na kuuzungusha haraka, halafu nikauvunja. Akapiga yowe kali la uchungu huku macho yakimtoka pima kama mjusi kabanwa na mlango. Kabla hajakaa sawa nikaachia ngumi kali kwenye shingo na kuvunja taya lake, akaanguka chini akiwa hana fahamu.
Yule wa kwanza alikuwa ameshainuka, akanijia na kurusha mapigo matatu ya haraka haraka, nikayaona na kuyakwepa, na kwa haraka akanipiga teke kali la tumboni, nikahisi kichefuchefu cha ghafla huku maumivu makali yasiyo na mfano yakisambaa mwilini.
Kabla sijakaa sawa akanitandika teke la nguvu kwenye korodani. Maumivu niliyoyasikia hapo yalifanya nigande kama sanamu. Alipoleta ngumi ya usoni nikajibetua nyuma na kusimama. Mapigo mengine mawili ya karate yaliponijia shingoni nikayakinga katika namna ya kuyapunguza nguvu kisha kwa nguvu zangu zote nikapeleka ngumi moja matata na kuuvunja mwamba wa pua ya yule mtu, akapepesuka na kupoteza mhimili.
Sikusubiri atulie, nikamuwahi kwa mapigo mengine mawili lakini yule mtu alikuwa makini sana, akayapangua mapigo yale kama mchezo na kunikwepa. Nguvu nyingi nilizowekeza kwenye mapigo yale na kumkosa zikanifanya nipepesuke kama mlevi. Yule mtu akaruka teke la kuzunguka na kunishindilia teke mgongoni nikaanguka chini bila kupenda huku maumivu makali yakisambaa mgongoni mwangu. Hakika yule mtu alikuwa mpambanaji matata mwenye mwili ulioshiba.
Pigo jingine la teke lilipokuja nikawahi kuliona na kuinama chini kidogo kulikwepa na hapo pigo lile likakata upepo bila mafanikio. Nikajipinda na kumchota mtama wa nguvu, akapaa hewani huku akiweweseka, nikamsubiri atue ili nimwadhibu lakini yule mtu alikuwa mjanja na kutua chini kama paka kwa miguu yake miwili na mkono mmoja chini huku akinitazama kwa hasira.
Kisha akanyanyuka tayari kwa mpambano, kabla hajaamua afanye nini nikainua mguu wangu wa kulia kama niliyetaka kumpiga teke akakinga mikono yake, nikazunguka kwa kasi ya ajabu na kuachia teke mzunguko la mguu wa kushoto lililotua kifuani kwake, akaanguka chini, na hapo mapigo matatu makini yakavunja mbavu zake na kumfanya apige yowe kali la maumivu huku damu ikianza kumtoka mdomoni.
Muda huo watu walishaanza kujaa eneo lile, sikutaka kuendelea kupoteza muda kwa kuhofia wenzao wangefika na mambo kuwa magumu zaidi, hivyo nikaondoka haraka na kuvuka barabara kisha nikaingia kwenye kichochoro fulani, nikapotelea kizani.
* * *
Harakati za Jason Sizya bado zinaendelea, na sasa mambo yanazidi kunoga, endelea kufuatilia hadi mwisho...
[emoji23][emoji23]...Nimesoma nae huyo Alishanto bin Mbaga hahahaa.
Mungu akituamsha salama, kesho nitatupia baada ya kutoka kwenye majukumu...bishoooop tukumbuke mkuu