323
Tukiwa pale nyumbani kwa Lister, suala la vinywaji vikali halikuwa la kutusumbua vichwa, tulikuwa na uwezo wa kunywa mpaka jioni na pale tulipotaka pombe zitutoke kichwani basi zingetutoka, tulijua ni kitu gani tungefanya ambacho kingetufaya turudi haraka katika hali yetu ya kawaida.
Ukiwa usiku mwingi na upepo mwanana ukitupepea toka baharini, kama mwanamume rijali nilijikuta nikishindwa kabisa kuvumilia kumtazama Pamela, nikawa natamani kumsogelea kisha nimkumbatie na kumbusu. Sikuwa tena na uwezo wa kustahimili. Tayari nilikuwa nimemaliza chupa nzima ya whisky na sasa akili yangu ilinituma kufanya jambo.
Japokuwa kazi ndo kwanza ilikuwa imeanza, ilikuwa bado mbichi, na Pamela alikuwa jasusi aliyezoea mikikimikiki kiasi cha kutokuwa na hisia za ngono, lakini akili yangu iliniambia si kila wakati ni wakati wa hatari. Si kweli kuwa kila chui huvaa ngozi ya kondoo! Pamela alikuwa msichana wa kawaida kabisa na pia alikuwa na matamanio kama wasichana wengine.
“Mbona hunywi?” Pamela alinizindua toka kwenye mawazo ya ngono yaliyoanza kuniteka.
“Dah, kinywaji kama hiki na upweke hakipandi kabisa. Ingekuwa tupo wawili tu hapa, na hayo macho yako mazuri yakiendelea kuniloga, ningekuwa tayari nimeshaku… ah, au basi!” nilisema kwa utani.
Kauli hiyo ilimfanya Pamela aangue kicheko kisha akapiga funda la pombe. “Nina nini miye hata uchanganyikiwe kiasi hicho!”
“Hujui una nini!” nilimuuliza huku nikijisogeza karibu yake, kauli ambayo ilimfanya Pamela azidi kucheka. Shingo yake ndefu aliilaza upande kidogo, macho yake kiasi yakilainika huku vidole vikiitua glasi ya pombe na kuanza kutekenyana.
Nikapitisha mkono wangu kwenye kiuno chake. Pamela akatulia huku akinitazama usoni kwa mshangao. Ilikuwa picha ya kusisimua, picha ya kuvutia, picha ambayo, kwa muda ilizifanya fikra zangu zichukue likizo na nafasi yake kuchukuliwa na hisia za ajabu, hisia za kimaumbile zilizonifanya niwaze kumtoa nguo moja moja kisha nimkumbatie akiwa kama alivyozaliwa! Dah, nilianza kujishangaa kwani haikuwa akili yangu bali akili ya pombe!
“Ni nini unawaza wewe?” Pamela aliniuliza huku akinitazama kwa macho yaliyorembua. Kabla sijamjibu, kwanza nilimtupia jicho Luteni Lister na kumwona amejiegemeza kwenye kiti na macho ameyafumba, huenda alikuwa amepitiwa na usingizi au alikuwa ametopea kwenye lindi la mawazo yaliyomfanya kimwili awepo pale lakini kimawazo awe mbali. Nikashusha pumzi ndefu.
“Kuna kitu kinanitatiza hapa,” nilisema nikiwa namtazama Pamela kwa macho yaliyojaa ubembe wa huba.
“Najua… ila pumzisha kichwa sasa. Au nikupatie ndimu ukate kilevi?” Pamela aliniuliza.
“Kwa nini nikate kilevi?” nilimuuliza kwa mshangao.
“Maana naona unaanza kuingiwa ana mawazo ya… au basi!” alisema kwa utani na kuangua kicheko.
“Unaonaje tukajipa mapumziko kidogo na kuburudisha mioyo yetu baada ya kazi hii?” nilimuuliza Pamela huku nikiendelea kumtazama kwa matamanio. “Naona kazi hii imekuwa ngumu kuliko nilivyotarajia, na hatujui itatupeleka mpaka wapi!”
Pamela aliachia tabasamu kisha akauliza, “Niambie wewe unafikiria nini?”
“Unajua napenda sana maeneo yaliyotulia sana kama sehemu za ufukweni hivi,” nilisema kisha nikatabasamu na kunywa pombe. “Ninapokuwa huko akili yangu hutulia kabisa kwa kuwa upepo ule hufukuza matatizo yangu kichwani.”
Pamela alinitumbulia macho kwa kitambo kidogo, kimya, kama aliyekuwa anatafakari jambo ambalo hakulielewa.
“Vipi, Pamela?” nikamuuliza. “Ni nini unawaza? Au haujapenda wazo langu?”
‘Hapana,” Pamela alijibu akitazama chini kwa muda kisha alitazama bilauri yake ya pombe halafu akayahamishia macho yake kwangu na macho yake yakagongana na ya kwangu. na hapo nikagundua kuwa siku zote nilipokutana naye sikuwa nikimchanganyia macho kwani sikuwa kugundua kama alikuwa na macho yake laini yanayobembeleza, macho ambayo si kwamba yalikuwa yanabembeleza tu, bali pia yalikuwa yanashawishi na kushurutisha. Wakati tukitazama, mara Pamela akacheka.
“Nini kimekufurahisha hivyo?” nilimuuliza nikiwa nimekunja ndita na kutabasamu kwa wakati mmoja.
“Jason, nimegundua kuwa mbali na uwezo mkubwa wa kishushushu ulio nao sikuwa najua kama uko
charming na una vituko namna hii!” Pamela alisema.
“Vituko?” nilimuuliza kwa mshangao.
“Hujioni ulivyo! Napenda sana jinsi ulivyo maana wajua kufikiria haraka nini cha kufanya. Nadhani hiyo ni talanta uliyobarikiwa na Mungu mbali na mafunzo,” Pamela alisema kisha akagida pombe yote iliyokuwemo kwenye bilauri yake. “Nakubaliana na wewe, ni kweli tunahitaji mapumziko kidogo na kuburudisha mioyo yetu.”
Kwa kuwa pombe ilikuwa imenikolea na ilinishawishi kufanya jambo, maneno ya Pamela kwangu ilikuwa ndiyo ruhusu ya kufanya jambo langu, hivyo nikashusha pumzi ndefu kisha nikamkumbatia kwa nguvu na kumbusu mdomoni huku mkono wangu mmoja ukikiminya kiuno chake, kisha nikamsogeza karibu yangu na kukamtazama machoni.
“Jason, kwani nini shida?” Pamela aliniuliza akinitazama machoni. Alikuwa amelegeza macho yake na kinywa.
“Unataka kujua shida yangu?” nilimuuliza huku nikiendelea kumtazama machoni.
“Ndiyo. Shida yako nini?” Pamela alisema huku akitabasamu kwa mbali.
“Nikikwambia utakubali au…?” nilimuuliza na kumkonyeza kilevi huku nikiendelea kukiminya minya kiuno chake chenye mifupa miteke.
“Itategemea,” Pamela alisema na kuachia kicheko hafifu. Muda huo alikuwa anapumua kwa nguvu.
“Unaonaje tukiumalizia usiku huu kwa kupongezana kwa hatua nzuri tuliyofikia?” nilimuuliza huku nikimkazia macho. Na hapo nikamwona akiyakwepa macho yangu na kutazama kando akiwa kimya kidogo.
“Niwe mkweli tu, ningependa iwe hivyo lakini sitaki kumsaliti mkeo…” Pamela alisema kwa sauti ya chini huku akionekana kupumua kwa shida kidogo, “Namheshimu Rehema, sitaki kugombana naye na pia najua ukionja asali utataka kuchonga mzinga kabisa jambo ambalo sitaki litokee.”
Niliachia tabasamu kabla ya tabasamu hilo halijaunda kicheko kidogo, kisha nikamminya tena kiunoni kabla sijamvuta na kumbusu shingoni, halafu kwenye shavu kabla ya mdomo wangu kuhamia kwenye mdomo wake.
“Basi fanya hivi… nipe mara moja tu halafu uniambie koma! Nitakuelewa,” nilimnong’oneza sikioni. Sauti yangu ikaonekana kuusisimua sana mwili wake. Niligundua kuwa chuchu zake zilikuwa zimesimama na kuwa ngumu.
“Mh! Yana ukweli hayo? Maana nyie wanaume mkitaka jambo lenu…” Pamela alisema kwa sauti ya chini ya mahaba halafu akaiachia sentensi yake hewani pasipo kuimalizia. Mwili wake ulikuwa unatetemeka kwa ashki na alikuwa ananitazama machoni kisha akaachia tabasamu kwa mbali. Halafu akageuka kumtazama Luteni Lister, aliporidhika akanikonyeza na kuinuka akaelekea maliwato huku akigeuka kunitazama kwa macho ya mahaba yaliyokuwa yakinialika.
Nikataka kuinuka ili nimfuate, na hapo nikamwona Luteni Lister akiyafumbua macho yake na kunitazama huku akitabasamu. Tabasamu lake lilikuwa pana na kisha alikunja na kutikisa ngumi, “Safi sana!” Alinong’ona. “Nakwaminia jembe langu! Kaza hivyo hivyo mpaka kieleweke.”
Nikashangaa sana. Kumbe muda wote Luteni Lister alikuwa akiyasikia maongezi yetu wakati tukiongea!
“Sasa sikiliza… usilaze damu sasa, nyanyuka umfuate huko huko ukamalize mchezo,” Luteni Lister alinisisitiza kwa sauti ya chini huku akigeuka kutazama kule alikokuwa ameelekea Pamela.
Sikutaka kujivunga, nikanyanyuka na kupiga hatua za haraka kuelekea kule bafuni. Huku nyuma nikamsikia Luteni Lister akisema, “Nakukubali sana, mwanangu!”
* * *
Harakati za Jason Sizya bado zinaendelea, kwa kuwa wamechukua mapumziko kidogo nasi tuchukue mapumziko vile vile😀... tukirudi tena mambo yatakuwa byee!😀