66
“Kama hakuna tatizo mbona huongei? Naona umenywea ghafla au eneo hili linakuboa?” Rehema aliniuliza tena huku akiniangalia kwa umakini.
“Wala hapajaniboa, na-
enjoy chakula kitamu ingawa hawakufikii, mpenzi wangu,” nilijibu Rehema huku nikiachia tabasamu.
“Haya bwana,” Rehema aliongea kwa sauti tulivu iliyobeba uchovu. Lakini sikuona tashwishwi yoyote usoni kwake.
Muda huo nilijifanya kuzungusha macho yangu kuyatazama mandhari ya ukumbi ule lakini lengo langu lilikuwa kumwangalia Amanda. Katika uchunguzi wangu macho yangu yalianza kutua kwenye ile meza ya jirani iliyokuwa na wale akina dada wawili warembo na mwanamume mmoja, rafiki zake Rehema.
Hapo hayakukaa sana, niliyapeleka moja kwa moja kwenye meza aliyoketi Amanda na mwanamume wake, nikamwona akiinamisha kichwa chake chini kama aliyeona kitu kwenye miguu yake, aliangalia chini kwa kitambo kisha aliinua uso wake taratibu kwa madaha kana kwamba alikuwa anaigiza filamu, mara macho yetu yakakutana. Kwa nukta kadhaa macho yetu yalitulia yakitizamana kisha Amanda aliyahamisha macho yake na kutazama kando.
Muda huo huo nikamwona akiyashusha macho yake kuitazama simu yake ya mkononi ambayo ilikuwa inatoa mwanga na hapo nikatambua kuwa ilikuwa inaita. Aliitazama ile simu kwa kitambo akionekana kama aliyekuwa akijishauri jambo, akabana taya zake na kumnong’oneza jambo yule mwanamume aliyekuwa naye kisha akainuka na kusogea kando, sehemu isiyo na kelele za muziki na kuipokea kisha akaipeleka moja kwa moja sikioni.
Alionekana kuwa mtulivu sana alipokuwa akiongea na simu na muda wote alikuwa ananitupia jicho la wizi. Baada ya mazungumzo ya takriban dakika tatu huku sura yake ikibadilika kisha alikata simu na kuonekana akishusha pumzi kisha akarudi pale kwenye meza.
Nilihisi kuwepo jambo maana nilimwona akiongea jambo na yule mwanamume aliyekaa naye kisha akachukua chupa ya bia iliyokuwa juu ya meza na kuimiminia bia yote iliyokuwemo katika bilauri huku akinitupia jicho la wizi, kisha alinyanyua na kuigida bia yote na kuikita ile bilauri juu ya meza. Kisha alitupia tena jicho la wizi akionekana mwenye wasiwasi kabla hajanyanyua mkono wake kuitazama saa yake ya mkononi.
Niliendelea kumchora tu nikajisahau kuwa Rehema alikuwa ameketi pembeni yangu na alikuwa akiniangalia kwa umakini kila nilichokifanya. Amanda alinong’ona tena jambo kwa yule mwanamume aliyekuwa naye na kunyanyuka huku akinitupia jicho la wizi. Macho yetu yakagongana. Amanda akajifanya kutazama tazama huku na kule mle ukumbini kama aliyekuwa akitafuta kitu kisha nikamwona akiondoka haraka eneo lile, akaelekea kwenye vyumba vya maliwato.
Sikutaka kusubiri maana nilikuwa nahisi kuchanganyikiwa kadiri muda ulivyosonga, nikamwomba Rehema anielekeze vilipo vyumba vya maliwato, bila ajizi akanielekeza. Nilisimama nikaelekea huko na nilipomtupia jicho la wizi yule mwanamume aliyekuwa ameketi na Amanda nikagundua kuwa alikuwa akiniangalia kwa mashaka, lakini sikumjali. Nilisonga na hatimaye nikajikuta nipo mahala ambako kulikuwa na ukumbi mpana uliokuwa na picha mbili za kuchorwa zilielekeza vyoo vya wanawake upande wa kushoto na vyoo vya wanaume upande wa kulia.
Nikasimama katika eneo ambalo ningeweza kumwona kila aliyetoka katika vyoo vya wanawake nikiwa na nia ya kumsubiri Amanda ili nimbane hadi anieleze ukweli kuhusu yule mwanamume aliyekuwa naye na kwa nini alikuja Ushirombo bila kuniambia.
Mara nikamwona Amanda akitokea kwenye vyumba vya maliwato ya wanawake na aliponiona alishtuka sana akataka kurudi chooni lakini akasita, jasho lilikuwa linamtiririka na alikuwa na wasiwasi mwingi. Alijongea taratibu mahala nilipokuwa nimesimama huku akilazimisha tabasamu, alijifanya kutokuwa na shaka yoyote. Niliendelea kumwangalia kwa umakini nikiwa nimekunja uso wangu.
Aliponifikia tu nikamkamata kwa nguvu na kumvutia kwenye vyoo vya wanaume, na hapo tukajikuta tumetokea kwenye ukumbi mpana na msafi wa vyoo uliokuwa na masinki kadhaa ya kunawia mikono na kando kulikuwa na sehemu za kujisaidia haja ndogo. Niliyazungusha haraka macho yangu kutazama eneo lile huku nikiwa makini, sikumwona mtu yeyote zaidi yetu, nikaiona milango kadhaa ya vyumba vya maliwato. Sikusubiri, nikamshika mkono Amanda na kumpeleka kwenye chumba kimojawapo pasipo mtu mwingine kutuona.
Ni kama mwili wa Amanda ulikuwa umeingiwa na ganzi, hakuweza kunigomea wala kuzungumza chochote bali alifuata kila nilichomtaka kufanya na muda wote alikuwa ananiangalia kwa wasiwasi mkubwa huku jasho likimtoka. Tulipoingia mle chooni nikambana kwenye ukuta huku nikimkabili. Tukabaki tumetazamana.
Macho yake legevu yalinitazama kwa wasiwasi kama mtu ambaye alikuwa akijutia kosa fulani alilolifanya. Hisia zangu zilianza kuwa taabani na macho yangu yakaanza kufanya ziara ya kushtukiza kifuani pake na hapo kupitia kivazi chake nikaziona chuchu zake laini zilivyosimama kwa utulivu juu ya milima miwili kama zilizokuwa zikinidhihaki.
Macho yangu yakatambaa kuuangalia mwili wake na yalishuka hadi kiunoni na hapo nikaiona nyonga yake laini yenye mifupa miteke iliyopakana na mzigo imara wa makalio yaliyotuama vema. Wakati nikiwa katika hali ile ya mduwao mara nikakumbuka kuwa nilimfuata kule chooni kwa ajili ya kumuhoji na si kufanya mapenzi.
“Unafanya nini hapa Ushirombo?” nilimuuliza kwa hasira huku nikimkazia macho.
“Na wewe unafanya nini, kwani hapa ndo Tabora?” Amanda akaniuliza huku akikunja sura yake.
“Kwa hiyo tunashindana, siyo? Mimi nikifanya hivi na wewe unafanya vile?” nilimuuliza kwa hamaki huku nikimkazia macho, akabaki kimya akiwa ameinamisha uso wake. “Nitakutandika makofi sasa hivi.”
Amanda alibaki kimya akiniangalia kwa woga, alikuwa anapumua kwa shida na niliweza kuona jinsi mapigo ya moyo wake yalivyokuwa yakienda kasi isivyo kawaida.
“Niambie, yule mwanamume ni nani?” nilimuuliza kwa hasira lakini Amanda akaendela kubaki kimya huku akionekana kupumua kwa shida.
“Nakuuliza, yule mwanamume ni nani?” nililirudia tena swali langu.
“Naomba unisamehe mpenzi wangu,” Amanda alinisihi kwa sauti ya kunong’ona.
“Nikusamehe kwa lipi, naomba kwanza uniambie yule ni nani?” niliuliza kwa ukali huku nikimminya kwa nguvu pale ukutani. Amanda akaanza kutetemeka kwa hofu.
“Yule nii… nii… Jason naomba unisamehe, tutazungumza…” Amanda alitaka kusema lakini akaonekana kusita sana na kuinamisha uso wake chini. Alishindwa kuvumilia na sasa machozi yalikuwa yanamtoka.
Nilimtazama nikaona asingeweza kunijibu, na sikuwa na muda wa kuendelea kubembelezana kwani sikutaka kabisa Rehema ashtukie jambo lile baada ya kuona nimechukua muda mrefu kule chooni. Niliinua mkono wa kulia nikataka kumzaba kofi usoni, nikamwona akijikunja kwa hofu huku akitoa yowe hafifu la woga.
“Nakuuliza kwa mara ya mwisho, yule ni…” kabla sijamaliza Amanda alianza kulia na haraka akaipitisha mikono yake nyuma ya shingo yangu na kunikumbatia kwa nguvu kitendo kilichofanya chuchu za matiti yake kukitekenya kifua changu, nikahisi joto kali la mwili wake likitambaa kwa kasi mwilini kwangu na kufanya nijisikie faraja ya aina yake.
Ingawa nilikuwa nimekasirika sana lakini mbele ya Amanda nilijikuta nimekuwa kama mbwa muoga mbele ya chatu mwenye njaa kali. Bila kujua, kwa kiganja changu taratibu nikaanza kumfuta machozi lakini aliuondoa mkono wangu machoni mwake kisha akanisogezea mdomo wake kisha akaanza kuniporomoshea mabusu mfululizo mdomoni na hapo ndimi zetu zikakutana.
Kabla sijajua nini nifanye nikajikuta nikiishiwa nguvu na hapo tukaanza kubadilishana ndimi na kuufanya mwili wangu kusisimka kwa raha. Nilichoweza kusikia baada ya pale ilikuwa ni sauti nyepesi ya pumzi yake iliyokuwa ikipenya kwa fujo kwenye matundu ya pua yake. Nilitaka kuleta pingamizi lakini sikufanikiwa kwani sikuwa na ujasiri wa kupingana na hisia zangu.
Mikono yangu ikaanza kutambaa taratibu kwenye mwili wa Amanda huku kila mmoja akionekana kuwa na hamu na mwenzake japo mazingira hayakuruhusu. Nikaanza kulipandisha gauni lake juu haraka nikiwa nimedhamiria kumaliza mchezo humo humo chooni.
Mara nikahisi mlango mkubwa wa kuingilia maliwato ukifunguliwa na kisha nyayo za mtu au watu ziliingia na kusimama, kumbe hata Amanda alikuwa amezisikia lakini akazipuuzia. Mikono yangu ikaendelea kutambaa, kwa tahadhari, katika mwili wa Amanda na kumfanya azidi kulegea. Mara nikahisi kuwa zile nyayo za mtu zikija hadi pale kwenye mlango wa choo tulichokuwemo.
Kabla sijajua nifanye nini nikahisi mtu huyo akigusa kitasa cha mlango wa choo tulichopo na kukinyonga huku akiusukuma mlango kwa pupa, ukafunguka na hapo tukakatisha zoezi letu baada ya kumwona mwanamume akisimama pale mlangoni.
Niligeuka haraka kumwangalia kwa umakini nikiwa nimekasirishwa sana na kitendo chake cha kuvamia starehe za watu wengine lakini nilipomwona nikajikuta nikinywea. Alikuwa ni yule mwanamume aliyekuwa na Amanda, na alisimama akituangalia katika hali ya kutoamini kile alichokiona.
Amanda alishtuka sana, alimwangalia mara moja kisha akayarudisha macho yake kwangu kabla hajainamisha uso wake chini akionekana kutetemeka huku akiliweka vizuri gauni lake. Mapigo ya moyo wangu yakaanza kunienda mbio, si kwa sababu ya kumwogopa yule mwanamume ila kwa sababu ya ukweli kwamba kama yule mwanamume angeleta matata habari zingemfikia Rehema, na sikupenda kumuudhi.
“Amanda!” yule mwanamume alimaka kwa mshangao. “Nooo! Nooo…” alipiga kelele na taratibu nikamwona akilegea kabla hajaanguka na kupiga kichwa chake sakafuni, akapoteza fahamu. Amanda akachanganyikiwa.
Nami nilipatwa mshtuko mkubwa sana. Hata hivyo, akili yangu ilikuwa inafanya kazi haraka haraka sana.
“Sikia Amanda, nataka kesho urudi Kahama na mambo yote tutakwenda kuyamaliza huko, mchana nikukute umeshafika, sawa?” nilimwambia Amanda, akabetua kichwa chake kukubali na hapo nikatoka nje haraka nikimwacha ametaharuki asijue la kufanya.
Nilimkuta Rehema akiwa ameketi kitini kwa utulivu kama nilivyomwacha, niliketi kando yake huku nikilazimisha tabasamu ingawa uso wangu haukuweza kuficha wasiwasi niliokuwa nao, sikujua nini kingefuata baada ya yule mwanamume kuzinduka. Rehema alikuwa ananiangalia kwa umakini lakini aliendelea kuwa mtulivu sana. Sikujua alikuwa ananiwazia nini.
“Tuondoke, nimeshachoka kukaa hapa,” nilimwambia Rehema huku nikizungusha kichwa changu kuangalia upande ule wa kuelekea maliwato.
“Vipi, kuna tatizo lolote?” Rehema aliniuliza kwa sauti tulivu huku akiendelea kuniangalia kwa umakini sana.
“Hakuna tatizo, nimechoka tu kukaa hapa, nahitaji tukapumzike. Au kuna ubaya?” nilimuuliza huku nikiendelea kutabasamu. Hata hivyo moyoni nilikuwa na wasiwasi mkubwa nikiogopa kuumbuka.
“
Okay, as you wish!” Rehema alisema na kumwita mhudumu kisha akalipia kile chakula na vinywaji. Tukainuka na kutoka nje huku akimpigia simu dereva wa teksi iliyotuleta akimtaka atufuate.
* * *
Itaendelea...