Simulizi: Harakati za maisha

Poor you.
 
Mtu umejoi juzi af unaninukishia mdomo legend naeweza kukuzaa huku napigana gaza sometimes sio must kuonesha ushamba
Wanasema mjinga mpuuze yaani Kuna maneno mtu akiongea namcheka namdharau namuona mpuuzi wa mwisho. Umeona majibu ya Jack Daniel ndo mwanaume wa kisawasawa anavyo jibu una type eti we mavi 😂🤣 eti legend,legend my foot.
 
Wanasema mjinga mpuuze yaani Kuna maneno mtu akiongea namcheka namdharau namuona mpuuzi wa mwisho. Umeona majibu ya Jack Daniel ndo mwanaume wa kisawasawa anavyo jibu una type eti we mavi 😂🤣 eti legend,legend my foot.
ACha kusifia wanaume utafikwa na koni endelea kusugua vuzi la shemej hapo ushenzini ugeni wako wa jf usituletee umama na ushamba kaa kimya when men talks kifusi fool
 
Ni stor tu inawafanya mnaburuzana hv??? [emoji1787][emoji1787][emoji1787]nmecheka balaa
JF uwanja wa Fujo,halafu nakumbuka marehemu leadermoe aliniambia humu JF Kuna watu wa kila aina washenzi na waungwana muhimu wale washenzi kuwaepuka.halafu mtu utasikia sie ma legend JF wewe mgeni unaishia kucheka maana JF Niko miaka kwa ID nyingine ambayo nilisahau password ikabidi nifungue hii mpya.
 
SEHEMU YA SITINI NA NNE

Asubuhi na mapema niliamka huku kitu cha kwanza ikiwa ni kupiga simu ili nijue familia inaendeleaje,lakini kubwa zaidi ni kuhusu maendeleo ya Jane kuhusu afya yake.

Pole na safari mume wangu ,vipi ulifika muda gani? Maana mkoa ulioenda ni mbali sana.
mke wangu aliniuliza.

Mimi nilifika salama tu,
Ila naomba kujua vipi hali ya Jane anaendeleaje?na vipi kuhusu vitisho vya mume wake pamoja na ndugu zake wamefikia wapi?
Niliuliza.

Jamani mume wangu mbona unaulizia familia za watu badala ya familia yako,
Kwanza naomba ujue kuwa kijana wetu haonekani tangu jana Mida ya saa tano usiku jana.
Kabla hajamaliza maneno yake nikadakia.....

Alienda wapi na ilikuwaje akawa hayupo,na pia wewe ulijuaje kama hayupo? niliuliza maswali mfululizo.

Wote tukiwa na hofu haswa baada ya wewe kuondoka ghafla bila kujiandaa kama nilivyozoea na mbaya zaidi ukaniachia msala,wote tulipooza sana siyo mimi ,siyo dada wa kazi wala kijana wetu kila mtu alikuwa na mawazo.

Baada ya kupata chakula cha usiku ndipo nilipo mwambia kuhusu maagizo uliyotoa kuwa akiwa kama mtoto wa kiume anapaswa kuhakikisha ulinzi ndani ya nyumba kutokana na vitisho tulivyopata mchana kutoka kwa ndugu wa Jane.
Na kijana alinielewa vizuri sana huku akitoka ili akafunge geti vizuri lakini tulishangaa kuona harudi ndani licha ya dakika kadhaa kukatika.

Mimi na dada wa kazi tuliamua kutoka nje ili tujiridhishe nini kinakwamisha mwenzetu ashindwe kurudi,cha ajabu tulikuta geti lipo wazi na yeye hayupo huku tukigundua huenda katekwa na mtu kwani hata viatu vyake (sendoz)
Vilikuwa pale pale nje.
Ikabidi turudi ndani haraka baada ya kubaini uwepo wa watu wabaya.

Lakini hatukuwa na namna ikabidi turudi kufunga geti huku tukihakikisha sehemu zote haswa ndani kama huenda mtu yeyote mwenye nia ovu akajificha humu ndani lakini hatukuona mtu.

Nikaamua kupiga simu polisi kwenye kituo chetu cha karibu hapa lakini nikaambiwa niende leo asubuhi kwani kwa usiku ule hakuna askari atanisaidia . maana muda ulienda
Nikaamua kukupigia wewe niombe ushauri lakini hukupatikana nikajua labda uko njiani bado na network inasumbua.

Na kijana wako hata simu aliiacha sebuleni maana alikuwa anaenda tu akafunge geti vizuri kisha arudi lakini ndipo alipotoweka jumla ,sasa hapa nakuomba mume wangu fanya hima wasiliana na maaskari ili tujue mtoto wa watu anapatikana vipi na kumbuka namna wazazi wake walikuwa wanamkataza asiwe na mazoea na wewe wakikuona kama gangster la mjini

Daniel mume wangu fanya hima nisaidie mwenzio najua upo kwenye majukumu yako lakini ni vyema tukalitanguliza mbele hili kabla wenye mtoto wao hawajaingilia kati fanya chochote niokoe umeniachia mizigo mizito haya ya Jane hayajapoa,limejitokeza lingine.
aliweka kituo mke wangu baada ya kuongea muda mrefu sana.

Sawa mke wangu nakupigia baada ya muda mfupi usijali kisha nikakata simu.

Niliamua kukata simu ili kuyatafakari yale maneno yake huku moyo ukiniuma sana,lakini pia hasira zilianza kuninyemelea niligundua familia ya Jane inahusika kwa asilimia nyingi juu ya upotevu wa kijana wangu, kijana ninayemkubali kinoma,akiwa hana jeuri wala kiburi.
Huku akiwa na adabu zote.
Huku nikiwa mbioni kumuandalia mazingira mengi ili awe kwenye ramani fulani ikiwa ni sehemu ya shukurani zangu kwake kutokana na mengi anayofanya nyumbani kwangu.

Sasa kwanini wapuuzi wachache wameamua kuhamishia matatizo kwa kijana wa watu masikini.
Ni mpole ,ni mtu asiyejua mambo mengi ,ni mchamungu haswa.
Sasa kwanini wamteke?
Kwani wasingenisaka mwenyewe?
nilijiuliza maswali mengi nikiwa nishakasirika kwa zaidi ya asilimia sabini.

Nilikumbuka kuwa jana Mida ya saa nne walinipigia simu wale ndugu wa Jane wakiendelea kunipa vitisho vyao ndipo nilipoizima simu na nadhani ndiyo maana mke wangu hakunipata kwenye simu.niliwaza sana.

Niliingia bafuni nikajiswafi kisha nikarudi huku nikiwaza kumwambia mke wangu ukweli kuwa nipo mjini sipo mkoa kama nilivyodanganya ili nirudi tumtafute kijana wetu lakini kuna akili iliniambia hakuna haja.

Kama kawaida niliripoti kazini nikiwa natokea lodge ambapo kwanza nilianza kujiona muoga sana why nijifiche lodge huku nikiiacha familia?
Je kama wangetekwa wote Ningejuaje?niliwaza kwa dakika kadhaa huku nikijiona mjinga na sikuwaza mbali kwasababu niliziba uso huku mwili mzima ukionekana.

Nikiwa nalazimisha tabasamu kwa wafanyakazi wenzangu,huku nikiwa nimepanga nisijulikane na yeyote kama nina matatizo na sikuwa tayari kumsimulia yeyote .
Niliendelea na kazi huku nikiwa na hasira nyingi sana nilitamani nione yeyote kutoka kwenye familia ya Jane wakinipigia ili nijibizane nao kiume lakini hakuna aliyepiga nikaishia kupokea simu zingine tu .

Baada ya muda fulani nilipokea simu kutoka kwa mke wangu.........

Mbona uliniambia utanipigia baada ya muda mfupi lakini hujapiga,ina maana haya mambo huoni kama ni mazito?

Huoni kama ni tuna janga kubwa sana mume wangu haswa kuhusu kijana wa watu?
Hata huyu dada leo sitaki hata atoke nje ya nyumba achilia mbali nje ya geti hili na pia kuna simu nimepokea kutoka kwa wale jamaa zake na Jane wanakuulizia na wametoa vitisho zaidi ya jana.sasa huoni kama nipo hatarini baba.
akilalamika mke wangu kwa sauti tulivu na ya chini kama vile alikuwa ananinong'oneza eti.

Nilikata simu kisha nikaenda kwa boss wangu yaani meneja mdogo,
Nilimwambia nina matatizo nikiwa naomba ruhusa huku nikiwa mnyenyekevu mno muda ule.

Danieli ndugu yangu unajua nafasi yako kwenye taasisi hii ni kubwa sana,yaani tunakuhitaji sana,
Hatuhitaji suti na huo muonekano wako,bali kile kilicho ndani yako.
Halafu sihitaji uniambie matatizo yako ila nakuruhusu uende nakupa siku tatu na pia kumbuka nikikuhitaji basi uje mara moja.
Pia nikutakie mema kwenye utatuzi wa changamoto zako.na utamuona
(Jina kapuni) ili umuage na yeye .
Ni maneno ya meneja akitaka nimpitie mtu mmoja ambaye huhusika na masuala ya nauli n.k.

Mpaka saa sita mchana nilikuwa natoka pale ofisini huku nikiliacha jengo na kuingia njia ielekeayo lodge.

Lazima niiokoe familia yangu,lazima nirudi nyumbani,wanaume tumeumbwa mateso,tumeumbiwa shida na matatizo si kuyakimbia bali ni kukabiliana nayo.
Nilijiwazia huku nikiwa nimeshafika lodge kuchukua vitu vyangu.

Niliangalia kwenye mkoba wa kazini nikakuta manati yangu iko full ,na haikuwahi kutumika kizembe nikaisunda Chemba kisha nikatoka huku nikichukua usafiri binafsi na kuikamata njia ya nyumbani kwangu nikiwa siogopi chochote wala lolote.

Jifunze,
Elimika,
Burudika.

Itaendelea.......................
 
Ndugu wapenzi na wafuatiliaji wa simulizi hii kwanza niwaombe radhi kwa kuchelewesha ni majukumu yanabana.

Pili mimi naandika simulizi inayonihusu (code nazingatia)
si kwa kuuza bali ni kushare ili watu wajifunze na pia waburudike.

Tatu ningeomba tuishi kama marafiki na ndugu kwenye hii simulizi,kuna comments nimesoma kiukweli zimenisikitisha sana.
Ni vyema kubadilika.

Kwani ukitukana unapata faida gani?
Acheni utoto basi.badilikeni
 
Sawa mkuu tuko pamoja .....Wanaojibu vibaya ww achana nao"Asiyejua maana haambiwi maana"
Usivunjike moyo tuko pamoja mkuu tukielimika na kujifunza mengi
 
Sasa kama ulishauriwa uwapuuze mbona unashindwa kitu kidogo kama hiko we mrembo,.tatizo ushamba ungekua na id ya zamani ni rahis kujua kuwa hii ni mpya ila kwa vile wewe ni zero huwez jua aya fuata ushauri wa marehemu kuku mgeni wewe
 
Tuko pamoja Samson Mzee wa misala 😄
 
Leo nimieshia hapa
 

Niombe radhi kwa niaba ya wanaokutusi,binafisi nimejifunza kuhusu Pombe kupitiliza na hasira vina madhara sana kwa familia.Mungu anisaidie
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…