SEHEMU YA THELATHINI NA SABA
Siku inayofuata baada ya kupunguza baadhi ya kazi zangu ofisini , niliamua kupiga simu kwa ndugu yeyote wa Jastini ili tupange namna ya kumsaidia,akili ikaniambia kumpigia simu mkewe ni kujitengenezea mazingira mabaya hasa ukizingatia jamaa yupo jela.
Nikakumbuka nina namba ya mtu ambaye nilikuwa nakwaruzana naye muda mwingi ambaye alidai ni dada yake ambaye hatujawahi kuonana ,kiufupi simfahamu na huenda hata yeye ananifahamu.
Nikampigia huku moyo ukinienda mbio maana nilijua natonesha vidonda vya watu na pia yule mdada sijui mmama hakuwa na lugha nzuri sana anaonekana ni mkali mkali,lakini nikalivaa tu lile jambo nikaweka simu sikioni.
Hello nani mwenzangu!
aliuliza upande wa pili mara baada ya kusalimiana.
Naitwa Daniel,mwezi uliopita ulinipigia kwaajili ya masuala ya ndugu yako Jastini.nilijitambulisha.
Oooh sawa nimekukumbuka,
Unasemaje? au unataka nini ?
aliuliza.
Nimepata taarifa za rafiki yangu Jastini kuwa yule gerezani,kifupi nimesikitika sana ila nina wazo fulani dada yangu.niliongea kwa tahadhari huku nikimsikilizia kwa umakini.
(Huku akitoa kicheko hafifu)
Mdogo wangu yupo jela ndiyo,lakini nikushangae wewe,kwani unataka nini kwetu?
Kwanza ulisema huhusiki na masuala ya Jastini ukidai tukuache na tulikuacha kweli licha ya Jastini kushindwa kukuhusisha moja kwa moja lakini ndugu tunatambua kuwa huenda mna kiapo mlichojipangia kuwa kama mmoja akikamatwa basi msitajane,ni kweli hakukutaja licha ya kupewa kibano kikali ataje wahusika na hakutaka kutaja yeyote.sasa ni biashara gani isiyo na washirika?
Ni kwamba ndugu yangu ni mjinga sana.aliweka kituo.
Samahani mama tunaweza kuonana tuongee kirefu ? niliuliza .
Inawezekana!
Lakini kwani unataka nini kwetu wewe,maana nahofia usalama wangu.aliongea akionesha ni mwenye wasiwasi kidogo.
Kuwa na amani dada ,mimi sina nia mbaya ni kwamba nahitaji tujadili hatima ya rafiki yangu Jastini kuwa usiogope.
Sawa mimi nipo maeneo ya mahakama ya (akiitaja mahakama ilipo)
Najaribu kuonana na watu fulani tujue namna ya kushughulikia haya masuala.alijibu.
Sasa dada kama upo hapo nadhani ni jambo jema kwanini tusionane tupange kabisa,eeeh ndani ya dakika chache nitakuwa hapo . niliongea kwa pupa .
Basi subiri nimalize mambo yangu kisha nitakupigia simu maana kuna mtu namsubiri hapa niongee naye . aliweka kituo.
Mida ya saa saba mchana tulionana yule mama ambaye kiukweli alikuwa ni mtu mzima tofauti na nilivyodhani huku akiwa na wenzake watatu , wanawake watatu akiwemo na yeye na mwanaume mmoja.walikuwa makini sana huku wakinitazama kwa hofu huenda walijua mimi si mtu mwema.
Nilijitambulisha kwa mara nyingine huku tukiingia kwenye mgahawa mmoja hivi,lakini hata mimi nilikuwa makini nao maana ni kama tunawindana.
Naitwa Lydia kama nilivyokuelekeza kwa siku ya kwanza,huyu ni mtoto wangu ,akimuonesha yule mwanaume ambaye ni kama umri tulilingana tu.na hawa ni ndugu wa mke wa jastini.alinitambulisha kwa wale watu huku akiniangalia pasi na kupepesa macho,sijui alijua labda nina manati nitamdhuru!!
Mimi kama nilivyowaeleza mwanzo ni kwamba sihusiki na habari za Jastini na mnavyosema hakunitaka huko kituoni licha ya kupewa mateso ,ni kweli kwakuwa asingeongea uongo kwakuwa sihusiki ila ni kwamba ni rafiki wa karibu,siyo kikazi ama kibiashara bali maisha ndivyo yalivyo.niliongea huku wakionesha wanakubali.
Kwanza bro mimi nikushukuru sana,kwa kuweza kutaka kushirikiana na sisi kumnusuru Jastini ambaye mimi ni mjomba wangu,na tangu mwanzo ,mama yangu na ndugu wote niliwaeleza kuwa wasihangaike kutafuta nani ama nani ,kifupi uncle wangu alishakuwa kwenye matatizo hivyo hakukuwa na haja ya kutaka kuwaumiza na watu wengine tusiokuwa na ushahidi nao.
Lakini kwa kufupisha maelezo ni kwamba Jastini anakabiliwa na kesi kubwa ya kufanya biashara ya nyara za serikali (madini)bila. Vibali huku akitambua kuwa kufanya hivyo ni kosa kisheria.hivyo yupo jela kwa shitaka hilo na si vinginevyo.maana wale wadai wake walishamsamehe.alifafanua yule niliyetambulishwa kuwa ni mtoto wa dada yake Jastini.
Kwanza nilipenda maelezo yake lakini pia huenda tabia ya Jastini alikuwa anaijua siku nyingi hivyo hakushtuka hata kusikia mjomba wake yupo lockup . Baada ya hapo nilimuita tuongelee kwenye gari nikiwaacha wale wanawake wanakula.
Kwanza nikushukuru kwa kunifahamisha vizuri maana mama yako alikuwa anaongea kwa vitisho sana kiasi cha kumuogopa .niliongea huku nikijichangamsha.
Sikia bro,mimi Jastini namjua vizuri sana,mimi mwenyewe kashachukua hela zangu nyingi sana huku akijaribu kunishirikisha kwenye biashara zake lakini nikawa nagoma,pia si mimi tu wapo wengi ambao kawatapeli ,huku wengine wakisamehe na wenye madeni makubwa makubwa ndiyo hao wanakuja.hivyo bro usiwe na shaka na mimi ndiye niliyemtuliza mama kuwa asikusumbue kwani nilijua moja kwa moja utakuwa huhusiki maana kwanza mjomba wangu kwenye biashara hiyo yupo kitambo sana,na kilichomfanya arudi nyuma kimaisha ni baada ya kutamani kununua kuliko kuwa mchimbaji.aliongea yule jamaa huku nikifurahi angalau nitapumua maana Dah mwezi mzima hata bia sinywi,zitashukaje na nina mawazo.
Tulibadilishana contacts zetu huku nikiona sasa yule ndiye mtu sahihi ambaye nitaongea naye jambo likaeleweka kuliko wanawake.
Naitwa Pastor Lewis unaweza kusave hivyo ndiyo utanikumbuka vizuri,pia karibu sana kanisani kwetu.aliongea huku akitabasamu.
Kwanza nilimuangaliaaa kisha nikamuuliza.
Kwani wewe ni mchungaji,maana nilikuwa nawaza tukitoka hapa upige hata mbili tatu japo mimi bado niko kazini nisingekunywa.niliongea nikiwa namshangaa maana hakufanania na uchungaji,
Ndugu yangu hakuna jipya chini ya jua ,sisi binadamu ni wakosefu na ipo njia impendezayo mwenyezi Mungu ambayo ukiifuata hutatetereka.hata mjomba wangu nilikuwa namwambia mara kwa mara lakini labda aliniona mpuuzi.kumbuka yanayofanyika yote leo yalishafanyika,na kwanza nikushukuru kwa hicho ulichotaka kunipa ,na nikushauri tu kuwa kwani ukinywa hizo bia bro unapata faida gani? sisemi unakosea ila waweza kunipa faida hata mbili tatu ili nijue.aliweka kituo.
Hapana ni mazoea tu hivi vitu vina faida basi,ni kwamba tulijikuta tunashawishika tu kuvitumia.niliongea kwa aibu fulani hivi maana kutangaza ulevi mbele ya hawa wachungaji huwa sipendi.
Daniel,una jina zuri la nabii mkubwa sana kwa mujibu wa biblia ,okoka sasa hujachelewa ,ukisoma kitabu cha Muinjili Marko,anatuonesha ni jinsi gani tunapaswa tutubu na kuiamini Injili, wakati ni sasa Danieli.
aliweka kituo.kisha nikaenda kuwaaga wale akina mama ambao imani ilirudi tuliagana kwa furaha kisha nikarudi ofisini huku nikiwaza vitu vingi ila tayari nikushukuru kuona wameamini kuwa sihusiki na msala wa ndugu yao.
Nilirudi nyumbani mapema ,kumbuka mwezi mzima na tangu nitoke kule kwa mganga sikuwahi kugusa pombe,kwanza bado sikuwa na imani ya moja kwa moja kuwa matatizo yangu yameisha nilijua naweza kukamatwa muda wowote na maaskari hivyo nikajiweka mbali na vyombo kwa muda ili nijue mbivu na mbichi kwanza.
Nikiwa barabarani katikati ya foleni kuna jamaa alikuwa anauza vitabu vingi sana,na mimi ni mpenzi wa vitabu nikaamua kumuita huku nikichukua kitabu fulani kinachohusu masuala ya uchumi kikiandikwa na mhadhiri fulani wa moja ya chuo kikuu bora Duniani Havard ,nikasema hiki kitanisaidia kuzugazuga ili nisiwe natoka ndani,kwanza mchungaji Lewis kaniongezea kitu pombe siyo ya kuendekeza.
Jifunze,
Elimika
Burudika.
Inaendelea......................