Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 80
Siku ya leo hii Neema alitoka nyumbani kwake na kwenda kumtembelea rafiki yake, ambaye alimshangaa kwa mabadiliko ya muda mfupi,
“Mmmh nipe siri ya mafanikio shoga maana sio kwa kung’aa huko, halafu pale kwako mbona umehama bila kusema?”
“Ndiomana nimekuja nikuhadithie”
Kisha akamuelekeza jinsi yeye alivyokuta wameshahama na jinsi Ashura alivyomtumia ujumbe,
“Mmmh kumbe Yule mdogo wako ana upendo hivyo!”
“Ndio, nakushangaa tu wewe ulikuwa na mashaka nae”
“Kwakweli nisiwe mnafki, sijawahi kumuelewa Yule mdogo wako na sijawahi kumuamini kabisa. Yani kila alichokuwa akiongea nilikuwa nakitilia mashaka, eti leo hii ndio amekutafutia nyumba nyingine ya kukaa mmmh”
“Na zaidi ya yote baba yake Salome yani Yule alikuwaga mume wangu, amejirudi yani kawa mpole huyo balaa. Aminiomba msamaha na amesema yupo tayari kumlea mtoto wake”
“Ila wanaume bhana, kaona mtoto amekuwa ndio kujifanya yupo tayari kumlea mtoto wake. Ila napo ni vizuri, halafu kitu kingine, mbona Salome simuoni shule?”
“Na hilo ndio jambo lingine limenileta ili unipe ushauri, Salome hataki shule kwasasa, unaweza kuamini hilo? Salome amesema anataka kupumzika kwahiyo nimuombee ruhusa ya ugonjwa, kwa kifupi Salome wangu hataki shule kwasasa”
“Kheee makubwa hayo, utaniletea niongee nae”
“Sawa nitakuletea maana wewe ndio mshauri wangu, na wakina Pendo wako wapi?”
“Wameenda kanisani”
“Kheee watoto wale kwa kanisa loh!”
“Ila ndio vizuri, na hakika hata wakina Salome wangependa kusali sidhani kama angekataa shule”
“Basi saivi hizo ibada ndio kama kituo cha polisi, mtoto hataki kabisa kuongelea habari hizo”
Mara akafika mgeni mwingine pale kwa mama Pendo ila huyu mgeni baada ya salamu kama alionyesha kumfahamu kidogo Neema yani ilikuwa kama kuna tukio ambalo alilifanya Neema halafu yeye analijua.
“Mmh hivi sio wewe ambaye mwanao alitumbukia kwenye kaburi!”
Neema nae alishtuka kuona kuna mtu anagundua kuhusu hilo jambo kwani yeye na Sa
lome kwenye msiba ule hakujua kama kuna watu wangetokea kuwafahamu,
“Kwani na wewe ulikuwepo kwenye ule msiba?”
“Ndio nilikuwepo, na lile tukio lilikuwa la kushangaza sana. Nakukumbuka vizuri sababu mimi ndiye ulinikuta pale njiani na nikakwambieni tunaenda kwenye msiba wa Moza, mkashangaa pale kuwa Moza amekufa kisha tukaaanza kuongozana kuelekea makaburini’
Ndio Neema nae alipoanza kukumbuka hilo tukio na kuona ni kweli kabisa kama ni yeye lazima awe anamkumbuka vizuri,
“Vipi mwanao hali yake maana kila mtu alipigwa na bumbuwazi pale msibani”
“Mwanangu amepona wala sikutaka kurudi tena kule zaidi zaidi kwenda na mwanangu nyumbani”
“Hata mngerudi kule kuna kilichokuwa kinaeleweka basi! Yalitokea makubwa sana, mwili wa marehemu ulitoweka na hadi leo hakuna anayejua kilichoendelea labda ile familia tu. Ulitokea upepo wa gafla pale makaburini na kila mmoja akikimbia na lwake. Kwakweli hali ilikuwa mbaya sana”
“Duh poleni sana, kwahiyo marehemu hakuzikwa?”
“Azikwe vipi na hata mwili wake haujaonekana”
Mama Pendo ikabidi aingilie kati maana haya maelezo hata yeye yalimchanganya kabisa,
“Unataka kuniambia Salome alitumbukia kwenye kaburi”
“Ndio alitumbukia halafu akazimia”
“Yani Neema umekaa tu na mtoto na alipatwa na makubwa kiasi hiko, anakataa shule unakaa nae tu hujiulizi! Mlete nimpeleke kwenye maombi”
“Nitajaribu kumwambia kama atakubali”
“Wewe ni mama yake bhana, atakubali tu”
Neema aliitikia pale ila hakuwa na namna ingawa Salome alimwambia kuwa wafanye siri ila atafanyaje na mambo yameshakuwa kama hivyo yani kuna watu wanamkumbuka vyema. Aliaga muda huo na kuondoka zake.
Siku ya leo hii Neema alitoka nyumbani kwake na kwenda kumtembelea rafiki yake, ambaye alimshangaa kwa mabadiliko ya muda mfupi,
“Mmmh nipe siri ya mafanikio shoga maana sio kwa kung’aa huko, halafu pale kwako mbona umehama bila kusema?”
“Ndiomana nimekuja nikuhadithie”
Kisha akamuelekeza jinsi yeye alivyokuta wameshahama na jinsi Ashura alivyomtumia ujumbe,
“Mmmh kumbe Yule mdogo wako ana upendo hivyo!”
“Ndio, nakushangaa tu wewe ulikuwa na mashaka nae”
“Kwakweli nisiwe mnafki, sijawahi kumuelewa Yule mdogo wako na sijawahi kumuamini kabisa. Yani kila alichokuwa akiongea nilikuwa nakitilia mashaka, eti leo hii ndio amekutafutia nyumba nyingine ya kukaa mmmh”
“Na zaidi ya yote baba yake Salome yani Yule alikuwaga mume wangu, amejirudi yani kawa mpole huyo balaa. Aminiomba msamaha na amesema yupo tayari kumlea mtoto wake”
“Ila wanaume bhana, kaona mtoto amekuwa ndio kujifanya yupo tayari kumlea mtoto wake. Ila napo ni vizuri, halafu kitu kingine, mbona Salome simuoni shule?”
“Na hilo ndio jambo lingine limenileta ili unipe ushauri, Salome hataki shule kwasasa, unaweza kuamini hilo? Salome amesema anataka kupumzika kwahiyo nimuombee ruhusa ya ugonjwa, kwa kifupi Salome wangu hataki shule kwasasa”
“Kheee makubwa hayo, utaniletea niongee nae”
“Sawa nitakuletea maana wewe ndio mshauri wangu, na wakina Pendo wako wapi?”
“Wameenda kanisani”
“Kheee watoto wale kwa kanisa loh!”
“Ila ndio vizuri, na hakika hata wakina Salome wangependa kusali sidhani kama angekataa shule”
“Basi saivi hizo ibada ndio kama kituo cha polisi, mtoto hataki kabisa kuongelea habari hizo”
Mara akafika mgeni mwingine pale kwa mama Pendo ila huyu mgeni baada ya salamu kama alionyesha kumfahamu kidogo Neema yani ilikuwa kama kuna tukio ambalo alilifanya Neema halafu yeye analijua.
“Mmh hivi sio wewe ambaye mwanao alitumbukia kwenye kaburi!”
Neema nae alishtuka kuona kuna mtu anagundua kuhusu hilo jambo kwani yeye na Sa
lome kwenye msiba ule hakujua kama kuna watu wangetokea kuwafahamu,
“Kwani na wewe ulikuwepo kwenye ule msiba?”
“Ndio nilikuwepo, na lile tukio lilikuwa la kushangaza sana. Nakukumbuka vizuri sababu mimi ndiye ulinikuta pale njiani na nikakwambieni tunaenda kwenye msiba wa Moza, mkashangaa pale kuwa Moza amekufa kisha tukaaanza kuongozana kuelekea makaburini’
Ndio Neema nae alipoanza kukumbuka hilo tukio na kuona ni kweli kabisa kama ni yeye lazima awe anamkumbuka vizuri,
“Vipi mwanao hali yake maana kila mtu alipigwa na bumbuwazi pale msibani”
“Mwanangu amepona wala sikutaka kurudi tena kule zaidi zaidi kwenda na mwanangu nyumbani”
“Hata mngerudi kule kuna kilichokuwa kinaeleweka basi! Yalitokea makubwa sana, mwili wa marehemu ulitoweka na hadi leo hakuna anayejua kilichoendelea labda ile familia tu. Ulitokea upepo wa gafla pale makaburini na kila mmoja akikimbia na lwake. Kwakweli hali ilikuwa mbaya sana”
“Duh poleni sana, kwahiyo marehemu hakuzikwa?”
“Azikwe vipi na hata mwili wake haujaonekana”
Mama Pendo ikabidi aingilie kati maana haya maelezo hata yeye yalimchanganya kabisa,
“Unataka kuniambia Salome alitumbukia kwenye kaburi”
“Ndio alitumbukia halafu akazimia”
“Yani Neema umekaa tu na mtoto na alipatwa na makubwa kiasi hiko, anakataa shule unakaa nae tu hujiulizi! Mlete nimpeleke kwenye maombi”
“Nitajaribu kumwambia kama atakubali”
“Wewe ni mama yake bhana, atakubali tu”
Neema aliitikia pale ila hakuwa na namna ingawa Salome alimwambia kuwa wafanye siri ila atafanyaje na mambo yameshakuwa kama hivyo yani kuna watu wanamkumbuka vyema. Aliaga muda huo na kuondoka zake.