Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #121
SEHEMU YA 104
Wakina Sara walifikishwa na Jesca kwa mkaka ambaye anasadikika kuwa alimbeba Salome wakati ameanguka kaburini, waliweza kufika baada ya Yule Jesca kuwaunganisha na Yule ambaye alikuwa akimjua vizuri Yule dereva.
Walifika na kusalimiana kisha wakaanza maongezi ya hapa na pale na haswa ni kuulizia kuhusu Salome,
“Jamani hata mimi mwenyewe sielewi, Yule mtoto alikuwa na mama yake kwenye gari na mama yake alikuwa akilia sana, gafla nilisikia akiongea na mama yake na muda kidogo mama yake akaniambia kuwa tusiende tena hospitali bali twende nyumbani kwao. Basi nilifanya hivyo kwa kuwapeleka nyumbani kwao”
“Mmmh kwahiyo hujui alizindukaje zindukaje. Wewe si ulimbeba na uliiona hali yake?”
“Ni kweli nilimbeba na alikuwa kama mtu aliyepigwa na shoti ya umeme tena nilijua amekufa yani nilikuwa naenda nao tu hospitali ila nilikuwa najua lazima tutaambiwa kuwa amekufa. Hata mimi nilipomsikia anaongea tena akiwa mzima kabisa nilishtuka sana”
“Mmmh inabidi tukaongee na mama yake, lazima kuna kitu anakijua. Unapajua kwao?”
“Napakumbuka vizuri sana, kwa tukio kama lile lazima nikumbuke kwao ni wapi”
Basi wale kaka wa Sara wakamuomba huyu dereva awapeleke kwao na Salome ili wakaongee na mama yake kwani kuna kitu walianza kuhisi kuwa hakipo sawa na Salome na walihisi kuwa wakiongea na mama yake wataujua ukweli wa mambo yote.
Basi safari ikaanza ya kuelekea kwakina Salome, na kweli walifika ila kwa bahati mbaya ilikuwa ni kwakina Salome kwa zamani na hakuna hata mmoja pale mtaani aliyejua nyumba mpya waliohamia wakina Salome, na waliambiwa ni kitambo sana wamehama. Ikabidi waachane pale na kila mmoja kuelekea sehemu yake, ambapo wale mapacha na dada yao waliamua kurudi tu nyumbani kwani siku ya leo hakuna walichofanya zaidi ya kufatilia mambo hayo.
“Ila mnakumbuka kuwa mama alisema tusirudi mpaka atupigie simu”
“Sasa mpaka saa hizi jamani, saa mbili hii labda mama kasahau. Tumpigie tu simu sisi wenyewe”
Wakaamua kumpigia simu mama yao ila simu ya mama yao iliita bila ya kupokelewa ikabidi wakubaliane tu kurudi nyumbani.
Wakina Sara walifikishwa na Jesca kwa mkaka ambaye anasadikika kuwa alimbeba Salome wakati ameanguka kaburini, waliweza kufika baada ya Yule Jesca kuwaunganisha na Yule ambaye alikuwa akimjua vizuri Yule dereva.
Walifika na kusalimiana kisha wakaanza maongezi ya hapa na pale na haswa ni kuulizia kuhusu Salome,
“Jamani hata mimi mwenyewe sielewi, Yule mtoto alikuwa na mama yake kwenye gari na mama yake alikuwa akilia sana, gafla nilisikia akiongea na mama yake na muda kidogo mama yake akaniambia kuwa tusiende tena hospitali bali twende nyumbani kwao. Basi nilifanya hivyo kwa kuwapeleka nyumbani kwao”
“Mmmh kwahiyo hujui alizindukaje zindukaje. Wewe si ulimbeba na uliiona hali yake?”
“Ni kweli nilimbeba na alikuwa kama mtu aliyepigwa na shoti ya umeme tena nilijua amekufa yani nilikuwa naenda nao tu hospitali ila nilikuwa najua lazima tutaambiwa kuwa amekufa. Hata mimi nilipomsikia anaongea tena akiwa mzima kabisa nilishtuka sana”
“Mmmh inabidi tukaongee na mama yake, lazima kuna kitu anakijua. Unapajua kwao?”
“Napakumbuka vizuri sana, kwa tukio kama lile lazima nikumbuke kwao ni wapi”
Basi wale kaka wa Sara wakamuomba huyu dereva awapeleke kwao na Salome ili wakaongee na mama yake kwani kuna kitu walianza kuhisi kuwa hakipo sawa na Salome na walihisi kuwa wakiongea na mama yake wataujua ukweli wa mambo yote.
Basi safari ikaanza ya kuelekea kwakina Salome, na kweli walifika ila kwa bahati mbaya ilikuwa ni kwakina Salome kwa zamani na hakuna hata mmoja pale mtaani aliyejua nyumba mpya waliohamia wakina Salome, na waliambiwa ni kitambo sana wamehama. Ikabidi waachane pale na kila mmoja kuelekea sehemu yake, ambapo wale mapacha na dada yao waliamua kurudi tu nyumbani kwani siku ya leo hakuna walichofanya zaidi ya kufatilia mambo hayo.
“Ila mnakumbuka kuwa mama alisema tusirudi mpaka atupigie simu”
“Sasa mpaka saa hizi jamani, saa mbili hii labda mama kasahau. Tumpigie tu simu sisi wenyewe”
Wakaamua kumpigia simu mama yao ila simu ya mama yao iliita bila ya kupokelewa ikabidi wakubaliane tu kurudi nyumbani.