Simulizi: Lisa

Simulizi: Lisa

Kama siyo kwa nini unatuwekea namba zake hapa halafu mtu mwenyewe hajui customer care ni nn?

Maana mnatualika twende fb ilhali story mliileta jf, unakela, anakela, mnakela nyote 😎😎

Mbaya zaidi huyo jamaa unayechapisha namba yake hapa anadai kuwa hiyo story haijakamilika, wakati huo huo wewe unatuambia kuwa sehemu iliyobaki ipo pdf 😁😁

Sijui nimuamini nani kati yenu 😎
 
Aisee nipo page ya 30 kudadeki sijawah soma hadithi nkawa mlevi kuisoma kila saa kila mahali kama hii ..Kudos kwa mwandishi naendelea kusoma kimya kimya [emoji1614]
 
LISA KITABU CHA SABA
SIMULIZI........................LISA
KURASA....301 MPAKA 305
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY WHATSAPP NO: +255628924768
SHUKA CHINI SOMA SASA

Sura ya: 301
Lisa alikuwa ametoka tu kumpumzisha Pamela wakati Sarah alipokimbilia wodini na kupiga magoti chini, akiegemea kitanda alicholala Pamela huku macho yake yakiwa yamezama kwenye dimbwi la machozi. “Lisa, Bi. Masanja, samahanini. Naomba msamaha kwenu kwa niaba ya kaka yangu.”
Sarah aliinamisha kichwa chini kwa nguvu na paji la uso wake liligonga chini kwa nguvu, na punde, likawa limevimba.
Mara Alvin naye akaingia. Baada ya kuona tukio hilo, mara moja alimvuta Sarah na kumyanyua.“Sarah, inuka.”
Hata hivyo, Sara alikataa kuinuka. Alisema katikati ya kwikwi, “Alvinic, usinizuie. Ni kosa la kaka yangu...”
"Inatosha. Uso wako umetoka kuumia juzijuzi tu, kwanini unauumiza tena kwa kuubamiza chini? Sitakuruhusu upige magoti,” Alvin aliamuru kwa nguvu.
"Alvinic, si sahihi alichokifanya kaka yangu kwa Bi. Masanja. Hata kama kichwa changu kitapasuka, ni sawa tu mradi amsamehe...” Sarah alimshika mkono na ghafla akajitupa mikononi mwake. "Alvinic, ninamuonea

huruma sana."
“Usilie.” Alvin aliinamisha kichwa chini na kumshika.
Wakati huo huo, Lisa alisimama tu kando akiwa kimya na kutazama tukio hilo likiendelea. Mumewe alikuwa amemshika mwanamke mwingine aliyemchukia na kumwonyesha mapenzi mazito mbele yake. Alikuwa amekufa ganzi kabisa. Kwake, ilikuwa kama anatazama kichekesho cha Futuhi tu. Alipochoka na kuchoshwa nayo, alisema kwa upole, “Je, show imekamilika? Kama mmemaliza ondokeni tafadhari. Ni usiku wa manane, na mgonjwa anahitaji kupumzika.” Alvin alikunja uso, lakini Sarah alimsukuma kando na kusema huku akitokwa na machozi, “Nipo hapa kuomba msamaha kwa dhati. Natumaini unaweza kumsamehe kaka yangu, nakuomba sana. Nitakubali masharti yoyote utakayotoa, hata... hata kama utataka nimwache Alvinic.”
“Sarah...” Uso mzuri wa Alvin ukazama. Alionyesha kuwa na hasira kali. “Unawezaje kusema hivyo? Ina maana hunipendi?” "Hapana, Alvinic. Ninakupenda sana.” Sarah akasonga. “Lakini sina jinsi. Nahitaji tu msamaha wa kaka yangu kwa gharama yoyote, lakini upendo wangu kwako

hautabadilika kamwe. Siku zote nitakupenda hata kama...”
“Nyamaza, huwezi kufanya hivyo.” Alvin akamkatisha. Kulikuwa na hisia ya kina ya mapenzi machoni pake. “Usiseme hivyo tena. Niachie mimi jambo hili.”
"Kweli Alvinic?" Sarah na Alvin walitazamana kwa upendo.
Akiwatazama, Lisa alihisi kama yeye ndiye mvamizi tu katika uhusiano huo. Hata hivyo, ni yeye mwenyewe tu ndiye aliyejua kwamba wakati mwingine moyo wa mtu unaweza kufa ganzi kiasi cha kutosikia maumivu yoyote. Alichohisi ni kitu kikimjia kooni. Haraka alilikimbilia pipa la taka na kuliachamia. Alichukizwa sana hadi akajisikia kutapika.
Lisa alikuwa hajawahi kutapika kiasi hicho hapo awali. Alitapika kuanzia chakula chote alichokula hadi nyongo yote, na machozi yakatoka. Alijua kwamba lazima Alvin alikuwa akimchukia sana, lakini hakuwa na la kufanya kurejesha upendo wake uliopokonywa kwa njia za hila.
"Uko salama?" Akiwa amekunja uso, Alvin alimtazama kwa mshtuko. Sarah kwa haraka akachukua rundo la tishu na kumkabidhi pia. Lisa aliutoa tu mkono wake na kucheka kidogo huku mwili wake ukiwa umeinama. “Niko sawa,

bila shaka. Nilitapika kwa sababu nilichukizwa nanyi, enyi wapenzi msio na haya.”
Uso wa Alvin ulibadilika sana. "Lisa Jones, bora uchunge mdomo wako."
“Nimesema kitu kibaya?” Lisa alitazama juu huku macho yakiwa yana machozi. Sarah, ulikuja hapa kuomba msamaha au kunifanyia show?” Kisha akamgeukia Alvin na kusema, “najua hunipendi, lakini kisheria, mimi bado ni mke wako. Huwezi kunionyeshea dharau na mchepuko wako kiasi hiki.” Alimtazama tena Sarah. “Kwa upande wako, umekuwa ukilia na kupiga magoti kuomba msamaha tangu ulipoingia mlangoni. Nilikuambia upige magoti? Unafikiri tunaweza kupuuzia kila kitu kilichotokea kwa sababu tu ulipiga magoti? Alichokifanya Thomas ni uhalifu. Alimchoma kisu na kumshambulia , na kumtilia Pamela dawa za kulevya, na pia kufanya uhalifu mwingine mwingi tu. Unafikiri kupiga magoti na kusema maneno machche tu kama samahani kunaweza kutatua yote? Ikiwa nitamuua Thomas na kupiga magoti mbele yako, unaweza kunisamehe?"
Midomo ya Sarah ilitetemeka. "Hiyo sio ninamaanisha ..."
"Toka nje." Lisa alielekeza mlango.

“Hatutasuluhisha suala hili faraghani. Uhalifu wowote aliofanya utashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.”
Mdomo wa Sarah ulisogea na alipotaka kuzungumza, Lisa akaendelea, “Usinipige magoti wala usiombe msamaha. Hata ukigonga kichwa hadi kipasuke, ni bure. Mimi sio Alvin Kimaro, kwa hivyo sitajisikia vibaya.” “Lisa Jones,” Alvin alimuonya. Alikuwa mwisho wa subira yake.
“Nimesema kitu kibaya? Yaani kaka yake atufanyie ubaya na bado sisi ndiyo tuwe wanyonge kwenu, kweli? Anafanya kana kwamba yupo juu ya sheria, lakini badala yake sisi ndiyo tumegeuka kuwa wabaya.” Lisa alicheka. “Ondokeni machoni mwangu. Nikiwaona tena, naogopa ninaweza hata kutapika mpaka utumbo. Ninahofia ninaweza kuwatapika hata watoto...”
Alvin alikasirika, lakini kwa kuzingatia watoto tumboni mwake, alimkumbatia Sarah na kuondoka.
Lisa alifunga mlango kwa nguvu na kuuegemea mlango kabla hajashuka taratibu. Alizika uso wake katika magoti yake. Alikuwa na maumivu, kiakili na kimwili. Mwanaume aliyempenda hakuwa naye tena moyoni mwake. Angeweza kufanya nini ili asiumizwe

tena na watu hao wawili?
•••
Saa moja asubuhi, Lisa alienda kumuona Kelvin kwenye wodi ya jirani kabla ya kwenda kununua kifungua kinywa. Alipokuwa anelekea kwenye mlango wa wodi ya Pamela baada ya kununua kifungua kinywa, alisikia sauti ya Pamela akirusha vitu huku na kule. “Wewe b*star, hivi Lisa alimpendaje mwanaume kama wewe? Hapana, wewe si mwanaume. Wewe ni shetani.”
“Pamela...” Lisa aliingia ndani haraka, na kumuona Pamela akiwa ameegemea kitanda cha hospitali kama mnyama aliyejeruhiwa aliyepandwa na hasira. Hata hivyo, hakuwa na nguvu na punde si punde alianguka kwa kutetemeka kwenye mto.
Kwa upande wa Alvin, alisimama mbele ya kitanda huku uso wake ukiwa umekunja sura ngumu.
“Ulimwambia nini jamani?” Lisa alimsukuma Alvin kwa hasira. “Angalia jinsi alivyomnyonge! Kwanini bado hutaki kumwacha?”
Alvin aliwatazama wale wanawake wawili wenye hasira na kukunja ngumi zake kwa nguvu. "Nilisema nitampa yeye na
Kelvin milioni 300 kila mmoja, kisha waachane kabisa na suala hili."

"Sawa, nimekubali," Pamela ghafla alisema kwa upole.
“Pamela, una kichaa?” Lisa aliuliza huku akiwa haamini. “Alvin, kakutishia kitu? Najua wewe na Kelvin msingekubali hivhivi tu hata kama mgekuwa na shida na pesa. Lazima kuna kitu amekutishia, ni kipi hicho? Ikiwa Thomas Njau hataenda jela, ataendelea kukusumbua tena na tena. Yeye haogopi chochote katika ulimwengu huu.”
"Lisa, hapana." Pamela aliinua kichwa chake na kumtazama kwa kusihi. “Sitaki mambo haya yafike mbali na kuwaumiza watu wengine...”
“Pamela, usiseme hivyo. Wewe ni jasiri kuliko maneno unayoongea.” Lisa alimkazia macho Alvin. "Sema! Umemtishia nini? Kwanini usinitishie mimi basi badala yake?”
Akiwa amekereka, Alvin akalegeza tai yake. "Lisa Jones, ikiwa utaendelea kufuatilia suala hili, nitamzuia Daktari Angelo kuponya ugonjwa wa baba yako."
Lisa alihisi ngurumo kwenye ubongo wake. Alimtazama Pamela. “Ndivyo alivyokutishia hivyo?”
Pamela alisema kwa uchungu, “Lisa, una baba mmoja tu. Sitaki umpoteze.”
“Ndiyo, nyie wote mnajua jinsi baba yangu

alivyo muhimu kwangu kwa sababu ninaye mmoja tu. Ndiyo maana ananitisha na baba yangu tena na tena.” Lisa alimtazama Alvin kwa ukali. "Mara ya mwisho, ilikuwa ni kwa ajili ya sifa ya Sarah ukanilazimisha kutangaza kwamba tumeachana, na watu kwenye mtandao bado wananikosoa hadi leo. Sasa unanitishia maisha ya baba yangu kwa sababu ya huyo fisadi Thomas?”
Sura ya: 302
Alvin aliuma midomo yake myembamba kimya kimya. Lisa alikosa subira na kumkimbilia kumsukuma. “Alvin Kimaro, mbona unanifanyia Ukatili sana? Wewe ni binadamu kweli? Kwa sababu ya Sarah, umeniumiza mimi na watu walio karibu na mimi tena na tena. Kukutana na wewe lilikuwa kosa kubwa.”
Hakuweza tena kuyazuia machozi yake huku akiinama chini. Alvin alihisi uvimbe kooni. Kwa sababu fulani, moyo wake ulihisi kama unakandamizwa na mkono, na kufanya iwe vigumu kwake kupumua.
"Lisa, usilie." Pamela alijaribu kuinuka na kumfariji. Lakini, mara tu aliposogea, alianguka kitandani.
"Pamela, usisimame, bado hauna nguvu." Lisa

alimsaidia kwa haraka kurudi nyuma.
“Lisa nisikilize. Mimi nimekubali tu kuachana na hii kesi. Usiifuatilie. Kwa vyovyote vile... sikulazimishwa.” Pamela alimshika mkono na kulazimisha tabasamu.
"Hapana." Lisa akatikisa kichwa. "Ikiwa Thomas Njau hatahukumiwa wakati huu, atavuka mipaka zaidi wakati ujao. Sitaki upatane kwa ajili yangu. Nataka aende jela.” Alimtazama Alvin na kuuma mdomo. “Sawa. Mwambie Daktari Angelo aondoke. Kwa kiwango kikubwa, nafasi ya baba yangu kuweza kupona ni ndogo sana.”
"Lisa Jones, kwanini unataka kulazimisha hasira yangu?" Uso wa Alvin haukuonekana kupendeza.
Lisa aliangua kicheko. "Ni nani aliyelazimishwa hapa?"
“Bwana Kimaro, Lisa siye aliyevamiwa, ni mimi. Hawezi kuniamulia,” Pamela alisema kwa haraka. “Nilisema sitafuatilia suala hilo, kwa hiyo tuachane nalo. We ondoka kwa amani tu. Hii ni kauli yangu ya mwisho." “Pamela...”
“Usiseme chochote Lisa.” Macho ya Pamela yalijawa na dhamira. “Sisi ni marafiki. Hata kama ungekuwa ni wewe kwa ajili yangu, ungefanya vivyo hivyo.”

Macho ya Lisa yakawa mekundu mara moja. Uhusiano wake ulikuwa umejaa fujo, lakini kwa bahati nzuri, alikuwa na rafiki ambaye asingemwacha. Lisa alisimama na kuinua kichwa chake kwa ukaidi. "Hata kama Pamela atakubali, kuna mwathirika mwingine. Hata...” “Ninakubali pia.” Sauti ya Kelvin ilisikika ghafla kutoka mlangoni.
Lisa aligeuka na kumwona Kelvin akiwa ameshikwa mkono na msaidizi wake. Alikuwa amesimama pale muda mrefu sana lakini kwa kuwa walikuwa kwenye zogo hawakuweza kutambua uwepo wake. Mkono wake bado ulikuwa kwenye banzi. Kelvin akasogea kuinga chumbani, kila hatua aliyopiga ilikuwa ya uchungu sana. “Endelea kumtibu baba yake. Suala hili litaishia hapahapa.”
“Kelvin...” Lisa aliuma midomo yake, lakini machozi yalikuwa bado yakitiririka mashavuni mwake.
Kelvin hakumtazama. Badala yake, alimtazama Alvin kwa huzuni na chuki. "Hujui jinsi ya kumtunza mwanamke huyu na unaishia tu kumuumiza mara kwa mara. Alvin Kimaro, kama wewe bado ni mwanamume, basi mtaliki. Acha kumuumiza kwa mwanamke mwingine. Tayari amefunikwa na makovu chungu mzima kwa sababu yako.”

Alvin alimtazama Lisa mwenye machozi, na kisha akamtazama Kelvin, ambaye alikuwa akimlinda. Mlipuko wa hasira ukapanda moyoni mwake. "Ni uamuzi wangu ikiwa nitaachana naye au la. Kwa kuwa mwanzoni alinitongoza bila aibu, haya yote ni yake mwenyewe.”
“Nani alikutongoza? Ni wewe uliyempokonya kutoka kwangu kwa ndoana au kwa hila. Alikuwa mchumba wangu.” Kelvin alikasirika. "Kwa hivyo kama angekuwa mchumba wako?" Alvin alitabasamu huku akionyesha ujeuri machoni mwake, jambo ambalo hakulitambua. "Mbona alikubali kulala na mimi na kubeba watoto wangu tumboni mwake, na hata sasa bado ananisumbua na kunibembeleza?”
Lisa hakuweza kuvumilia tena. “Nani anakusumbua? Maadamu uko tayari kunitaliki, nitaondoka mara moja.”
"Nini? Je, ulifikiri kwamba ungeweza kunitongoza tu na kuniacha muda wowote unaotaka, ndiyo maana ukaamua kuwa na Kelvin kama mpango wako mbadala?” Alvin alibana kidevu chake kikatili. "Lisa Jones, sitaruhusu watoto walio tumboni mwako kumwita mtu mwingine baba yao. Hata ukitaka talaka, itabidi uzae watoto kwanza. Itakuwa wakati muafaka kwako kumfungulia Sarah

nafasi.”
Maneno yake yalikuwa kama visu vinavyouchoma moyoni mwa Lisa tena na tena. Yalikuwa machungu sana hadi yakamzuia kupumua vizuri.
“Kwa kuwa unampenda sana Sara, kwanini usimzalishe watoto wako? Nendeni mkazae watoto wenu wenyewe. Kwanini ukae na mwanamke mwingine kisha uwatolee macho watoto wangu?” Alisihi huku akitokwa na machozi. “Alvin nakuomba sana. Niache na watoto wangu, sawa?"
Macho ya Alvin yalimtoka. Kisha, akageuza uso wake uliojaa jeuri. “Hapana, kuzaa ni uchungu sana. Siwezi kuvumilia kwa Sarah kupata uchungu wa uzazi. Anachopaswa kufanya ni kuwa Bibi Kimaro na kulea watoto wangu tu, basi!”
“Alvin Kimaro, wewe b*star. Wewe si binadamu.” Lisa hakuvumilia tena kumsikiliza. Sarah hakustahili maumivu, hivyo uchungu wa kuzaa watoto ukasukumwa kwa Lisa badala yake. Bado alikuwa binadamu kweli?
Wakati huo, alikimbia kwenda kumpiga na kumng'ata kama mnyama. Ni kana kwamba alikuwa amesahau kwamba alikuwa mjamzito. Akiwa ameshtuka, Alvin aliumwa kwenye

mkono wake. Lakini, alijaribu kila awezalo kujizuia asimsukume.
"Njoo mumshike haraka." Alvin akaamuru na walinzi kadhaa waliingia ndani kwa sauti yake. Sekunde chache tu, wakamkandamiza Lisa chini.
“Alvin Kimaro, unafanya nini? Achana naye.” Kelvin alivumilia maumivu ya majeraha yake na kusonga mbele. Pamoja na hayo, harakaharaka alisukumwa pembeni na mlinzi mmoja. Ilimuuma sana hata akashindwa kuamka tena.
"Alvin, unaweza kunifanya utakavyokavyo, lakini usiwadhuru watu wasio na hatia." Macho ya Lisa ya wasiwasi yalijaa chuki.
“Usijali. Sitamlemaza, lakini ili kuepusha usiendelee kunipandisha hasira ukiwa mjamzito, hutaruhusiwa kwenda popote ukiwa mjamzito.” Uso wa Alvin uligeuka kuwa mbaya alipoona jinsi Lisa alivyokuwa na wasiwasi juu ya Kelvin. Baada ya hapo, alimnyanyua kwa nguvu na kutoka nje ya chumba hicho.
“Niache niende.” Haijalishi jinsi Lisa alimpiga sana njiani na kuchana mikwaruzo michache kwenye uso wake, haikuwa na maana. Wakiwa ndani ya gari, Alvin alimfunga kamba.
“Alvin Kimaro, kwanini unanifanyia hivi? Niache niende.” Lisa alijitahidi sana, lakini

Alvin akafumbia macho.
Gari lilimpeleka moja kwa moja hadi New Metropolis Park. Alimbeba hadi chumbani na kumuonya kwa uso wa huzuni, “Kwa kuwa hutabaki kwenye nyumba ya Mzee Kimaro tena, basi utakaa hapa kuanzia sasa. Huruhusiwi kwenda popote bila idhini yangu. Kaa tu hapa kama msichana mzuri hadi watoto watakapozaliwa.
"Unanifungia?" Lisa alihisi kana kwamba anapandisha kichaa. Sio tu kwamba Alvin angempa Sarah watoto ambao Lisa alingezaa, lakini pia alikuwa akimfungia. Je, bado alikuwa binadamu? “Unawezaje kufanya hivyo? Hii ni kinyume cha sheria. Napiga simu polisi.”
Lisa alichukua simu yake, lakini Alvin alimpokonya na kuivunja kwa kuibamiza chini. “Lisa Jones, nilishawahi kukupa nafasi. Ni kosa lako kujihusisha na Kelvin Mushi.” Alvin alishindwa kujua kwanini yeye mwenyewe alikuwa amekasirika hivyo. Labda ndiyo yale wahenga walisema ‘mkuki kwa nguruwe!?’. “Una haki gani ya kuniambia hivyo? Wewe ndiye unayeendekeza uhusiano wa kimapenzi na Sarah ukiwa bado kwenye ndoa. Usifikiri sijui kuwa tayari umeshalala naye.”
“Kwahiyo kama nimelala naye itakuwaje? Angalia jinsi unavyoonekana kuwa mbaya na

mwendawazimu. Unawezaje kujilinganisha na Sarah?" Kadiri alivyozidi kusema ndivyo maneno yake yalivyokuwa makali na makali zaidi.
Lisa alipigwa na butwaa. Alipougusa uso wake usio sawa, moyo wake ulimuuma zaidi. Ni nani aliyesema hajali kuharibika kwake? Lakini sasa, alisema kwamba alikuwa mbaya.
Uso wake uliharibika kwa sababu gani hapo mwanzo? Je, hakukumbuka hilo hata kidogo? "Alvin, ikiwa utatoa watoto wangu kwa Sarah, ni bora niruke kutoka kwenye jengo hili." Lisa alisema kwa uthabiti na uso wa kumaanisha. “Ruka, fanya haraka. Ukithubutu kuwaumiza wanangu, nitawazika rafiki zako na baba yako ambaye amelazwa hospitalini,” Alvin alisema kwa ukali. Kisha akaufunga mlango kwa nguvu na kuondoka zake.
Sura ya: 303
Lisa alikimbia, lakini alisikia sauti ya mlango ukifungwa kwa nje. Alijaribu kuvuta mlango, lakini haijalishi aliuvuta vipi, haukutikisika hata kidogo. Alikuwa mfungwa kwa mara nyingine tena. Hakuweza kwenda popote. Alikaa chini kama mdoli aliyevunjika.
Zamani, hata kama Alvin alimtendea ukatili kiasi gani, hakuwahi kumchukia kabisa. Ni kwa

sababu alijiambia kuwa hakukusudia kufanya hivyo. Alilemazwa tu na Sarah. Lakini, sasa alimchukia sana.
Alimchukia Thomas Njau. Alimchukia Sarah Njau. Alimchukia Alvin Kimaro. Alimchukia Rodney Shangwe na kila mtu mwingine aliyekuwa karibu naye.
Ikiwa si kwa Alvin na ujinga wao, je Sarah angewadanganya? Mwisho wa siku, Alvin alistahili. Mapenzi yake yasiyoisha kwa Sarah ndiyo yaliyomfikisha hadi hapo.
Ni yeye pia aliyemruhusu Thomas kuwaumiza Pamela na Kelvin. Sasa, Thomaso hakulazimika kuteseka na vikwazo vya sheria. Na yeye, alikuwa amefungwa. Hakupata picha jinsi Thomas, ambaye aliruhusiwa kutoka katika kituo cha polisi, angezidisha jitihada zake za kuwaumiza marafiki zake hata zaidi. Alimchukia Alvin Kimaro. Kwenye mawazo yake, alimwinua hadi juu angani kisha akamrusha na kumkanyaga vibaya sana ardhini. Siku moja, angewafanya wateseke kwa ajili ya maumivu waliyowasababisha kina Pamela, Charity, Kelvin na yeye.
Mchana. Mwanamke asiyemfahamu alitumwa kwenda kumhudumia. Aunty Yasmine na Shani, watu wawili waliomtunza hapo awali, walihamishwa.

Lisa alifungiwa katika nyumba hiyo ya ghorofa mbili kila siku bila mahali popote ambapo angeweza kwenda. Ilikuwa inachosha sana. Angeweza tu kutazama televisheni au kupata hewa safi kwenye kibaraza. Wakati mwingine alipotazama chini kutokea kwenye kibaraza, alikuwa na hamu ya kujirusha. Hata hivyo, kwa mawazo ya watoto tumboni mwake, aliamua kuwa mgumu.
Aliendelea kukaa humo kwa wiki nzima bila kutoka hadi Hans alipokuja kumchukua ili kumpeleka hospitali kwa uchunguzi wa uzazi. “Alvin yuko wapi?” Lisa aliuliza. Hans alikuwa kimya sana.
Lisa alicheka. “Najua. Lazima awe pamoja na Sara. Hakuna kitu muhimu zaidi kwake kuliko Sarah kwa sasa."
"Bibi mdogo, usiwe hivyo." Macho ya Hans yalikuwa yamejaa huruma. "Nitaongozana na wewe hadi hospitali." Lisa alikuwa anataka kusema kitu, lakini alipowaona walinzi wawili wasiowafahamu, alinyamaza.
Njiani kuelekea hospitali, Hans aliendesha gari huku Lisa akiwa amekaa kwenye siti ya nyuma. Hans alisema, “Siku hizi, nimekuwa makini hasa kwa Sarah Njau. Ni kwa hilo tu ndipo Bwana Mkubwa ameanza kuamini kwamba mimi ni mwaminifu kwake kabisa.”

"Lazima iwe ngumu kwako." Lisa hakutarajia kwamba Alvin angekuwa mwangalifu na Hans. "Inaweza kuwa ni kwa sababu nilikutetea mara ka mara sana mbele ya Bwana Mkubwa hapo awali, kwa hivyo hakuniamini sana," Hans alisema kwa sauti ya chini. "Hapo awali uliniomba nikusaidie kutafuta mtu akutengenezee mchongo ili kufanya mimba ionekane kama imeharibika ..."
“Haiwezekani sasa. Alvin alisema kwamba ikiwa watoto wake watapata madhara yoyote, hatawaacha Pamela na baba yangu. Nina wasiwasi sana kuhusu Pamela sasa.” Lisa alisema, “Thomas Njau bila shaka atalipiza kisasi kwa Pamela, lakini Pamela hataondoka Nairobi ikiwa hawezi kuwasiliana nami. Unaweza kumtumia ujumbe ili aondoke nchini mara moja?”
“Bila shaka, lakini wewe...”
“Nisaidie kuwasiliana na mtu. Jack Kimaro," Lisa alisema ghafla.
Hans alishtuka. "Jack atakusaidia?"
"Sina hakika, lakini katika Nairobi yote, ni nyinyi wawili tu mnaoweza kunisaidia kutoroka." Lisa hakuwahi kutarajia kwamba angetafuta msaada wa Jack siku moja. Ingawa alimnyanyasa mara kwa mara, alikuwa na hisia kwamba Jack angemsaidia. Aliweza kuhisi

msamaha machoni pake kila alipomkabili... “Sawa.”
Wakati gari lilipopita kwenye makutano ya barabara iliyochangamka na yenye hekaheka na shughuli nyingi, skrini kubwa iliyokuwa kando ya duka kubwa ilikuwa ikitangaza harusi ya Melanie na Jerome.
Alitazama skrini. Melanie alionekana mrembo kama binti wa kifalme. Hapo awali, Lisa alipanga kufichua utambulisho wa Melanie siku ya harusi yao. Kwa bahati mbaya, alikuwa chini ya kizuizi cha nyumbani.
Hans alipumua. “Sasa kwa vile familia za Campos na Ngosha zimeunganishwa kwa ndoa, thamani ya Melanie Ngosha imepanda sana. Sio tu kwamba yeye ni makamu wa Mkurugenzi wa Ngosha Corporation, lakini pia ni mke wa Jerome Campos. Familia za Campos na Ngosha zimeshirikiana kwenye mradi mkubwa. Sasa, thamani ya Jerome ni karibu juu kama ya Bwana Mkubwa Alvin.” Lisa alifunga macho yake na kuzuia chuki chini ya macho yake. Melanie Ngosha hakuwa binti wa Joel hata kidogo, hata hivyo alirithi kila kitu kutoka kwa Joel, vyote vilipaswa kuwa vya Lisa. Kwa upande wa Lisa, sasa alikuwa kama panya wa mitaani. Melanie Ngosha, Nina

Mahewa. Walikuwa wanasubiri muda wao tu! Alimradi bado alikuwa anapumua, angefichua rangi zao halisi kwa walimwengu!
Walifika katika hospitali binafsi ya Dokta Choka. Lisa alitazamwa na walinzi kadhaa wakati akipanda juu kwa uchunguzi wake wa uzazi.
Njiani, alimwona Cindy Tambwe, ambaye alikuwa amevaa vazi la kipepeo la manjano lililofichua nusu ya mapaja yake. Alishikilia mkoba wa kifahari mkononi mwake, na mkufu wa almasi wa karati kumi ukining'inia shingoni mwake.
Lisa alikuwa mfuatiliaji mzuri wa mambo ya mitindo, kwa hiyo aliweza kusema kwa jicho moja kwamba vazi hilo lilikuwa na thamani ya pesa nyingi, ambapo bei yake ingeweza kuwa ya juu hadi tarakimu nane. Cindy Tambwe aliyepita bila shaka hakuwa na pesa, lakini mambo yalikuwa tofauti tangu alipopatana na Chester.
“Lisa, ni bahati mbaya hapa tunakutana tena. Nimemaliza kurekodi kipindi leo na nimekuja hapa kumtafuta Chester.” Cindy alitazama juu na kuinua pete ya almasi kwenye kidole chake huku akitabasamu. “Inaonekana vizuri? Chester alinipa.”
“Inaonekana vizuri, lakini Dokta Choka ni

malaya maarufu. Kila mwanamke aliyelala naye lazima awe nazo angalau kumi au ishirini kati ya hizo,” Lisa alisema kwa unyonge. "Ni kawaida yake kuwanunulia wanawake pete kama hizo, lakini pia lazima wavumilie unyanyasaji mkubwa kitandani. Hapo ulipo sijui kama una marinda..."
Midomo ya Cindy iliganda kabla hajadhihaki. "Huenda na wewe alishakufumua eti, ungejuaje yote hayo?”
Lisa alicheka. “Labda hujui kila msichana anachangua pale anapotaka kuwekeza thamani yake. Thamani yangu niliwekeza kichwani, ndiyo maana hutaniona nikidhalilika. Wewe umechagua kuwekeza katikati ya mapaja yako ili uweze kupata maisha unayoyataka. Kwa hiyo mimi na wewe tupo anga mbili tofauti kabisa.”
Cindy akacheka kwa dharau. “Bado mimi ni bora zaidi kuliko wewe! Tizama jinsi unavyotia huruma! Mume wako alikudanganya wakati wa ndoa yako. Halooo! Nilikuwa nakuonea wivu, lakini haikuchukua muda Alvin Kimaro akakutelekeza. Sasa, anaongozana na Sarah tu popote anapoenda...” Cindy alinyamaza na kumtazama Lisa. "Ulikuwa unalijua hilo? Sasa, kila wakati Chester ananipeleka kwenye bata zao na marafiki zake, Sarah huwa yuko

pamoja na Alvin kila mara. Sitataja jinsi walivyo karibu sana, lakini siku zote atalala kwa Sarah baada ya kula bata.”
“Bi. Tambwe...” Hans alionya.
"Kaka, kwani nasema uongo? Si hata wewe pia huwa unakuwepo?” Cindy akapepesa macho yake makubwa na kusema. "Hata niliona lovebites nyingi kwenye shingo ya Sarah mara ya mwisho. Teh...teh..teh...." Uso wa Lisa ulikuwa umepoa sana. "Kumbe ndio hivyo? Basi wanapendezana. Yeye ni kipande tu cha takataka ambacho sitaki kukiona tena. Nadhani anafaa kabisa
kuwa hata marafaiki na mtu kama wewe.” “Haya, acha kujifanya. Najua
imekuuma sana.” Cindy akatoa kioo na kupaka lipstick nyekundu kwenye midomo yake. "Hata hivyo, Sarah alinialika kwenda kwenye jumba lake la baharini huko Mombasa siku chache zilizopita. Ni kipande ghali zaidi cha ardhi ya pwani huko Mombasa. Unaweza kuona bahari ya bluu mara tu unaposukuma mlango wa chumba cha kulala.”
Sura ya: 304
Uso wa Lisa hatimaye ulizama. Yeye, bila shaka, alikumbuka jumba hilo la baharini.

Ilikuwa ni nyumba ambayo aliwahi kuishi na Alvin, alikokuwa ameongozana na Alvin kwenda kuuguza ugonjwa wake na kupata nafuu. Pia ndipo walipoweka nadhiri zao nyingi za maisha, wakaishi kwa mapenzi mazito na hata kutunga mimba ya watoto wao. Lakini sasa, alimpa Sara? Mwanaume huyo angewezaje kuwa mkatili kiasi hicho? Kwa kweli alikuwa ... hana moyo.
Alipomwona akiwa ameduwaa, Cindy alicheka. Alimkaribia Lisa na kushusha sauti yake. "Wewe na Pamela Masanja mlikuwa
mabinti wenye fahari sana. Nani angefikiria kwamba Pamela angevunjwa na kuharibiwa sifa yake, na wewe? Mumeo alikutupa. Kwa kweli, nyakati zimebadilika sana.”
"Umesema nini?" Lisa alinyanyuka ghafla na kumkazia macho kwa macho. “Pamela hakufanywa lolote na Thomas...”
“Ina maana hujaona jinsi habari za Pamela zilivyoenea kila kona mtandaoni? Koneksheni yake imevuja akifanyiwa vitendo vibaya na Thomas. Binti wa thamani wa familia ya Masanja kutoka Dar es Salaam ametiwa unajisi. Haha, kila mtu anasema kwamba anastahili kwa sababu alijitongozesha kimakusudi kwa Thomas Njau. Nani atamtaka katika siku zijazo? Hata mimi siwezi kuvumilia

kuwatazama nyinyi wawili tena.” Cindy alimuangalia kwa mbwembwe kisha akageuka. Lisa alipigwa na butwaa. Hakuwahi kufikiria kuwa tukio la Pamela lingefichuliwa na kugeuzwa kimakusudi. Hata kama hakufanyiwa chochote, mitandao ingeeneza kana kwamba alifanyiwa mambo fulani. Hii ndiyo nguvu ya mitandao ya kijaminii bwana! Habari kama hii ilikuwa pigo kubwa kwa mwanamke. Hakuweza kuamini.
Alizunguka kumtazama Hans. "Tukio la Pamela ni la kweli kwenye mitandao?"
Hans alisita, lakini mwishowe, aliinamisha kichwa chake kwa uchungu. “Ndiyo.” “Imekuwaje? Yeye ndiye mwathirika, lakini kwanini kila mtu anamsema vibaya kwa kujirahisha kwa Thomas Njau?” Lisa alimfokea bila kujizuia. “Ni nani aliyegeuza mambo ya kuyafanya yawe tofauti?”
"Samahani. Ni picha za sura ya Pamela ndiyo zimesambaa, zikiwa na maneno ya ‘Connection ya Mkemia Mkuu wa Zamani wa Osher yavuja. Video sijaziona lakini watu wanatumiana chini kwa chini. Lakini kwa kuwa Bi. Masanja hakufuatilia suala hilo, kila mtu alifikiri huenda ikawa ni kweli,” Hans alieleza kwa huruma.
“Nipe simu. Nataka kuona habari.” Lisa

akampokonya simu mkononi.
Mlinzi aliyekuwa pembeni akamvuta mara moja. “Bi. Jones, tafadhali twende haraka kwenye uchunguzi."
"Hapana, nataka kuwasiliana na Pamela," Lisa alipiga kelele na kujitahidi kupinga. Hata hivyo, walinzi walimpuuza na kumpeleka kwa nguvu kwenye chumba cha uchunguzi wa ultrasound. Haijalishi alikuwa akifanya fujo kiasi gani, hakuna aliyemjali.
Baada ya uchunguzi kukamilika, alirudishwa tena kwenye jumba la baridi la New Metropolis Park.
Lisa alivunjavunja kila kitu ndani ya nyumba, na kumtishia mtumishi wake mpya wa ndani. Hadi jioni ndipo Alvin alipoingia pale. Aliitazama ile nyumba iliyoharibika, lakini kabla hajauliza chochote, kisu kikamjia. Akarudi nyuma na kumshika Lisa mkono ambao ulikuwa umekamata kisu, akakichukua kisu na kukitupa pembeni. Akamgeukia na kumwangalia yule mwanamke mwenye nywele ndefu na mkali aliyekuwa mbele yake. “Unataka kuniua?”
"Nilikosea. Ni afadhali uwe mpumbavu, na bado ungekuwa bora kuliko ulivyo sasa.” Lisa alimtazama kwa chuki. “Kwanini upo huru? Chizi kama wewe alipaswa kuwa umefungwa

kwenye hospitali ya vichaa. Nilidanganyika kufikiria kuwa naweza kukuponya mwenyewe. Haha, lazima nilikuwa mwendawazimu." "Nyamaza. Nadhani wewe ndiye chizi hapa." Alvin alimkokota hadi bafuni na kukiegemeza kichwa chake kwenye kioo. “Tazama sasa. Kuna tofauti gani kati yako na kichaa?”
“Mimi ni kichaa. Nimesababishwa kuwa kichaa na wewe." Uso wa Lisa ulikuwa na michirizi ya machozi. “Alvin, kwanini unamfanyia hivi rafiki yangu? Unajua kuwa Pamela alikuwa karibu kubakwa. Naweza kuachana na ukweli kwamba ulimwokoa Thomas, lakini kwanini alilidhalilisha jina la Pamela alipotoka? Je! Unajua jinsi gani sifa ilivyo ni muhimu kwa msichana? Je, wanawake wengine wote isipokuwa Sara hawana thamani machoni pako?”
Mshipa kwenye paji la uso wa Alvin ulivimba. “Umemaliza? Watu kwenye mitandao ya kijamii hawana makosa. Rafiki yako ndiye aliyejipendekeza kwa Thomas. Nasikia alikuwa anataka gari kama nililokununulia.”
"Ulisema nini?" Lisa alimkazia macho huku akimtumbulia macho kana kwamba haamini alichotoka kukisikia.
“Ni Pamela Masanja aliyeokuwa akimsumbua

Thomas na kujaribu kila njia kumtongoza. Baada ya kukubaliana naye, aligundua kwamba sifa yake ilikuwa mbaya, hivyo alitaka kujiepusha naye. Hakuna kitu katika ulimwengu huu kinachokuja bila gharama." Sarah alisema kwa uso mkavu.
“Nani kakuambia ufanye hivyo? Sarah?” Lisa alimgeukia na kumuuliza Alvin, “Unaamini kila kitu anachosema?"
“Ningemwamini nani nisipomuamini Sarah? Wewe?” Alvin alikoroma na kusema kwa dharau, “Pamela Masanja na wewe ni watu wa aina moja. Ndege wenye kufanana huruka pamoja. Familia ya Masanja ina ushawishi huko Dar es Salaam, lakini hawana thamani huku Nairobi. Bila shaka, alitaka kulazimisha kuolewa na Thomas kwa sababu familia ya Njau ina ushawishi hapa.”
Uso safi wa Lisa ulibadilika rangi kama karatasi. Aliitazama midomo myembamba ya Alvin, ambayo alikuwa ameibusu mara nyingi hapo awali. Kiasi kwamba alisahau kwamba jinsi midomo hiyo ilivyokuwa myembamba, ndivyo mwanaume huyo alivyokuwa jeuri na mkatili zaidi.
Je, angemuamini nani kama si Sarah? Kila kitu ambacho Sarah alisema kilikuwa sawa. Hakukuwa na haja ya kuchunguza na kamwe

haja ya kuwa na shaka. Lisa aliumia sana hata asijue la kusema.
Maneno yote yaliyokuwa yakimtoka Alvin kooni yalikuwa ni fimbo ya kumuadhibu. Hakuweza hata kusogea kwa sababu alikuwa ameshikwa na kukandamizwa kwa nguvu na Alvin.
Wakati huo Alvin alihisi yule mwanamke aliyekuwa chini yake amepatwa na kichaa ghafla. Alikuwa kama mnyama mdogo aliyejeruhiwa. Alipopotea katika mawazo kwa sekunde kadhaa, mkono wake ukalegea.
Lisa alijifungua na kunyakua chupa ya losheni kwenye sehemu ya kuoshea uso kabla ya kuipasulia kichwani mwa Alvin. Damu safi mara moja ilidondoka kutoka kwenye paji la uso wake.
Alvin alipatwa na wazimu, na yeye alinyoosha mkono kumsukuma. Lisa alijigonga ukutani mara moja, na damu ikaanza kutoka mapajani mwake. Aliteleza ukutani taratibu huku akiwa ameshika tumbo lake huku akilia kwa uchungu asiweze kuongea.
Alvin aliingiwa na hofu tena. Hakujali jeraha lililokuwa kichwani mwake, alimnyanyua kwa haraka na kutoka nje ya chumba kile. Kwa mwendo wa dakika ishirini, Lisa alikuwa amezidiwa na maumivu kiasi kwamba hakuweza kuongea kabisa. Alishika tu upindo

wa sketi yake iliyotapakaa damu.
Milipuko ya maumivu ilimpata Lisa tumboni. Alijiwazia kwa huzuni, jinsi Alvin na yeye waliwahi kutazamia kupata watoto. Kwa kuwa wote wawili walitoka katika malezi ya bahati mbaya, walitamani kwamba watoto hao wangewapa familia kamili. Aliwahi kumshukuru Mungu kwa kumpa mapacha.
Hata hivyo, baadaye, kila siku alikuwa na wasiwasi kuhusu jinsi angeweza kuwalinda watoto wake akiwa kama mama. Ingemlazimu kufanya nini ili kuwazuia wasiumizwe na Sara? Labda pengine ingekuwa afadhari kwamba watoto walikuwa wameamua kwenda. Angalau wasingeteseka. Labda hiyo ndiyo ingekuwa ahueni kwao.
Sura ya: 305
"Lisa Jones, bora uendelee kukaa. Hakuna kinachopaswa kutokea kwa watoto." Alvin alimnyanyua na kukimbilia hospitalini. Mwanamke mikononi mwake alikuwa na mimba ya miezi mitatu, lakini alikuwa mwepesi kama manyoya. Ni kana kwamba angeweza kuelea wakati wowote.
Moyo wake ulihisi kama kuna kitu kinaubana. Hakuweza kujua ni nini, lakini ilionekana kama

hofu na kwamba alikuwa akipoteza kitu chake cha tahamani zaidi. Hata hivyo, Lisa alifumba taratibu macho yake yaliyochoka kana kwamba hakumsikia.
Punde si punde, Lisa alisukumwa kuingia Emergrncy Room. Alvin alitembea huku na kule nje ya mlango huku damu zikimtiririka kwenye paji la uso wake.
Hans alionekana kukosa amani. "Bwana Mkubwa, kwanini usifunge paji la uso wako kwanza?"
"Achana nao tu." Mikono ya Alvin iliyotapakaa damu ilikuwa ikitetemeka bila kukoma. Alionyesha uwepo wa hasira na kuchanganyikiwa.
Haikuchukua muda mlango wa chumba cha upasuaji kufunguliwa. Daktari akatoka. “Bwana Alvin, watoto wawili wa mgonjwa hawawezi kuokolewa. Ni lazima utie sahihi hii mara moja ili atoe mimba. Vinginevyo, hata maisha ya mama yatakuwa hatarini.”
"Unasema nini?” Alvin alishikwa na bumbuwazi. “Watoto hawawezi kuokolewa? Wewe ni bure kabisa. Umesomea wapi udaktari wako?" Alvin alimshika dokta kola kwa hasira huku macho yakiwa mekundu.
Hao walikuwa watoto wake. Laiti si kwa wakati huu, asingejua ni kiasi gani aliwajali wale

watoto wawili.
“Bwana Kimaro, kwa kweli hata kama angepelekwa wapi bado haitakuwa na masaada wowote. Itakuwa sawa na daktari yeyote,” daktari alieleza kwa woga. “Vitoto tumboni mwa mama yao vilikuwa tayari vimeyumba sana alipokuwa na ujauzito wa mwezi mmoja, na hajawa katika hali nzuri siku hizi pia kutokana na kiwewe. Tayari kulikuwa na dalili za kuharibika kwa mimba hapo awali, na alikuwa amebeba mapacha. Kwa kweli nimejaribu niwezavyo.”
Mapacha! Mapacha wake walikuwa wamekwenda. Alikuwa amewasukuma kwa mikono yake mwenyewe. Alvin kwa unyonge akamuachia daktari. Uso wake mzuri ulionekana kuvunjika moyo katika mwanga uliofifia. Tayari alikuwa amepoteza damu nyingi, na wakati huo, alihisi kizunguzungu cha ghafla ambacho kilimuumiza sana kichwa. "Alvinic, umepoteza damu nyingi." Sarah alimkimbilia ghafla na kumnyanyua kwa haraka. “Wacha nikufunge jeraha lako.” Alvin kwa hali ya kawaida alitaka kukataa, lakini maneno ya Sarah yalikuwa kama kamba iliyomvuta kwa nguvu. Akili yake ilikwenda tupu, na akamfuata bila kujua.
Daktari alisema kwa wasiwasi, “Bwana Kimaro,

hii saini ya...”
“Hans, nitakuachia hili.” Alvin akamwambia Hans. Sarah akamvuta Alvin harakaharaka hadi kwenye chumba cha matibabu.
Akiwa amekunja uso, Hans alitia sahihi haraka karatasi za daktari. “Si lazima
useme... Kuwaokoa mama na watoto ni muhimu zaidi."
“Bila shaka.” Daktari alikimbia tena ndani ya ER ili kumuokoa Lisa.
Macho ya Lisa yalikuwa na uchungu sana hata hakuweza kuyafungua. Hata hivyo, hakuwa amepoteza fahamu kabisa. Masikio yake yangeweza kusikiliza mazungumzo ya madaktari.
“Nilisikia Bwana Kimaro amepata penzi jipya, lakini sikuamini mpaka nilipojionea leo. Nimeshtushwa sana."
“Ndiyo, inasikitisha sana. Mkewe yuko hatarini, lakini hakutia sahihi hata karatasi. Hajali iwapo mke wake ataishi au kufa.”
“Je, hiyo ni kweli?"
“Nawezaje kusema uongo? Ikiwa Msaidizi wake hakutia saini, sidhani kama kuna mtu angemjali.”
“Pia nilimwona Bwana Kimaro na yule mwanamke wakiondoka wakiwa wamekumbatiana."

Lisa alipumua kwa nguvu! Chozi lilidondoka kwenye kona ya macho yake. Ha! Alvin Kimaro, wewe ni mkatili sana! Ilibainika kuwa alikataa hata kusaini jina lake wakati maisha yake yalikuwa hatarini. Kwake, thamani ya maisha yake kwa Alvin ilikuwa ndogo kuliko hata ya ombaomba wa mitaani. Hata wakati huo, kulikuwa na Sara tu moyoni mwake. Mapenzi yoyote aliyokuwa nayo kwake yalionekana kugeuka mavumbi na kutoweka kabisa. Kuanzia muda huo na kuendelea, maadamu bado alikuwa hai na anapumua, alikuwa na chuki tu na wapenzi hao wadanganyifu.
Katika wodi, Lisa alifungua macho yake. Sarah alikuwa amesimama wodini peke yake, akitabasamu na kucheza na ufunguo wa gari mkononi mwake. “Unaona hii? Hili ndilo gari la kifahari la kipee nchini ambalo Alvinic alikupa mara ya mwisho, lakini pleti namba yake imebadilishwa hadi AKLSN. ‘Alvin Kimaro Loves Sarah Njau’. Imekaa vizuri, eeh?"
Lisa aliitambua kwa haraka. Alvin aliwahi kumpa funguo hizo za gari, na plate namba ya kipekee ya gari wakati huo ikawa mada moto kwenye Mtandao. Iliwafanya wanawake wengi kuwa na wivu.

Lisa alitabasamu kwa utulivu. “Unapenda tu kuokota mabaki ya watu. Magari, majengo ya kifahari, wanaume. Hakika, wachukue wote. hata hivyo sijali.”
"Kwa hivyo ikiwa unajali? Mimi ndiye pekee katika moyo wa Alvin.” Sarah akasogea hadi kitandani na kumtazama kwa unyonge kutoka juu. “Angalia. Nilichofanya ni kusema neno moja tu. Kwa hivyo vipi ikiwa rafiki yako wa karibu angebakwa? Ndugu yangu alitoka bila dhamana, lakini rafiki yako wa karibu hakuwa na bahati. Amedhalilishwa na kuwa kama panya wa mitaani. Sifa yake imeharibiwa, lakini anastahili. Ni kosa lake kunitukana hospitali hapo awali.”
"Ulijua kuwa Thomas atamdhuru?" Macho mekundu ya Lisa yalimtoka.
“Duh.” Sarah akainama huku tabasamu likiwa limejikunja kwenye kona za mdomo wake. "Ni aibu iliyoje kwamba hatua ya mwisho haikufaulu, lakini haijalishi. Hata hivyo hakuna mwanaume atakayemtaka tena.”
Lisa alikasirika sana hadi kifua kilimvimba. Akiwa ametoka tu kwenye upasuaji, alitetemeka kwa maumivu. “Wewe b*tch...” Sarah alitazama sura yake ya uchungu na kutabasamu kwa ushindi zaidi. “Nilisahau kukuambia, lakini nilimuua Jennifer Musyoka

pia. Ni huruma kwamba polisi hawatawahi kupata ushahidi.”
“Ni wewe?...” Lisa hakuweza kujizuia kunyakua kikombe cha maji ya moto pembeni na kumwagia Sarah.
Mara Sarah akapiga kelele na kukwepa haraka, Alvin akaingia ndani kwa kasi, alikasirika sana baada ya kuona maji kwenye nguo za Sarah.
“Wewe kichaa. Sara alikutunza kutokana na wema wa moyo wake lakini bado huthamini wema wake. Nadhani unapaswa kupelekwa katika hospitali ya magonjwa ya akili." Sauti na macho ya Alvin yalikuwa yamejaa chuki. “Nakushukuru sana kwa wema wako. Unapaswa kumruhusu akutunze badala yake. Sitaki kamwe kuwaona nyinyi wawili maishani mwangu.” Lisa alifunga macho yake. Alikuwa na wasiwasi kwamba kweli angepandwa na hasira ikiwa angewatazama kwa muda mrefu zaidi.
"Alvinic, kulingana na uzoefu wangu wa miaka mingi, nadhani anaweza kuwa amepata unyogovu wa moyo. La sivyo, asingetuumiza mimi na wewe. Haijalishi ataniumiza, lakini ninaogopa kwamba kwa hali yake ya sasa, anaweza kuwaumiza wengine pia,” Sarah alisema kwa wasiwasi.

Alvin aliganda. Kikumbusho hicho kilimfanya atambue kwamba kweli Lisa alikuwa akipatwa na kichaa sana tangu alivyoonekana siku za karibuni. Kwanza, alijaribu kumchoma kisu na kumpiga kwa chupa ya glasi. Sasa, hata alimmwagia Sarah maji ya moto. Kwa kuzingatia hayo, pamoja na ukweli kwamba Sarah alikuwa mwanasaikolojia maarufu, vilimfanya awe na shaka pia.
TUKUTANE KURASA 306-310
ONYO: Si ruhusa kusambaza wala kukopi kazi hii mahali popote,ukibainika sharia itachukua mkondo wake(By:Official Dully)
 
SIMULIZI......................LISA
KURASA....306 MPAKA 310
PRESENTS: SIMULIZI ZA DULLY WHATSAPP: +255628924768

Sura ya 306
“Sarah Njau, usifanye mzaha. Mimi si mgonjwa.
Hali yangu ya akili ni timamu sana.” Lisa alipoona
jinsi Alvin alivyokuwa kimya, ghafla alihisi kukosa
amani. Kwa hiyo, alieleza kwa haraka, “Msitake
kuniudhi zaidi.”
Sarah alimtazama kwa macho ya huruma. “Hakuna
kichaa yoyote ambaye amewahi kukubali ugonjwa
wake. Isitoshe, ulipata mimba pia ukiwa na hali
hiyo. Nakushauri upate matibabu haraka
iwezekanavyo.”
Lisa hakutaka kitu zaidi ya kuinuka na kumpasua
Sarah usoni kwa pumzi yake ya mwisho. Hata
hivyo, alijua kwamba Alvin angemwamini zaidi
Sarah ikiwa angepandisha hasira zaidi. “Sarah
Njau, Alvin tayari ni wako, na unaweza kuchukua
nafasi ya Bibi Kimaro pia. Lakini kwanini huwezi
kuniacha niende? Ninawaomba nyote wawili
mniruhusu niende, sawa? Ninaahidi kwamba
nitakuepuka kila wakati nikikuona katika siku
zijazo.”
Alvin alikunja uso bila fahamu. Kimantiki,
alimchukia Lisa, lakini wazo la kumkwepa
lilimfanya akose furaha isiyoelezeka.

Sarah alitabasamu kwa uchungu. “Nawezaje
kukufanya uelewe hili? Huenda usijitambue, lakini
itaharibu maisha yako yote ikiwa hautatibiwa. Mbali
na hilo, wewe bado ni mke wa zamani wa Alvinic.
Ikiwa habari itaenea, wengine wangemwonaje?”
Uso wa Alvin ullilegea ghafla. “Inatosha. Kwanini
hutaki kuamini kama wewe ni mgonjwa?”
Lisa karibu kupasuka kwa hasira kwa sababu ya
Sarah. Alilia kwa uchungu. “Nini nilikukosea katika
maisha yangu ya nyuma? Kupoteza watoto wangu
tayari kumenisikitisha sana, lakini sasa unataka
kuniweka katika hospitali ya magonjwa ya akili?
Alvin Kimaro, sijali kama hunipendi, lakini tafadhali
nichukulie kama binadamu.”
"Si lazima uende kwenye hospitali ya wagonjwa wa
akili, lakini huwezi kuondoka kwa sasa. Itabidi
unywe dawa kila siku,” Sarah alimfariji kwa upole.
“Mimi ni mzima wa afya. Sihitaji dawa hata kidogo.”
Lisa alijitetea.
“Ni kupoteza muda kujaribu kuzungumza na
wewe.” Sarah kisha akamgeukia Alvin. "Alvinic,
tunapaswa kuchukua hatua kabla hali yake haijawa
mbaya. Tunapaswa kumsaidia. Wewe pia umewahi
kuwa na ugonjwa huu hapo awali. Unapaswa kujua
jinsi ugonjwa wa akili unavyoweza kuwa na
madhara.”

Lisa aliitazama sura ya mwanaume huyo na ghafla
aliingiwa na hali ya kutokuwa na utulivu.
“Basi, hebu tumtendee wema kwa sasa. Mkabidhi
kwa wataalam wa magonjwa ya akili kwa muda.
Ikiwa hali itakuwa mbaya, tutamhamisha hadi
hospitali ya magonjwa ya akili." Baada ya hapo,
Alvin aliondoka.
“Alvin Kimaro, simama hapo ulipo...” Lisa
hakuweza kukubaliana na hali hiyo, hivyo akainuka
haraka kitandani. Hata hivyo, mara tu miguu yake
ilipotua chini, maumivu makali kwenye sehemu ya
chini ya mwili wake yalimfanya aanguke tena.
Alitazama juu tu na kuona mwonekano wa Alvin
ukiondoka.
Sarah akainama na kunong’ona, “Nitazungumza na
madaktari hapa. Ugonjwa wako utakuwa mbaya
zaidi na hatari zaidi. Hatima yako itakuwa tu
kwenda hospitali ya magonjwa ya akili."
"Sarah Njau, nenda kuzimu ukafe." Wakati huo,
kuna kitu katika akili ya Lisa kikaingia. Kwa vile
hakuweza kuinuka, alirukwa na akili na kumng'ata
Sarah paja.
Hata hivyo, alimuacha baada ya kusikia sauti ya
Sarah. Ni wakati huo Alvin aliporudi na kujiona
tukio hilo. Kwa hivyo, mara moja alimkimbilia na
kumpiga teke. Mguu wake ukampiga begani.

Kichwa cha Lisa kisha kikagonga fremu ya kitanda
cha chuma nyuma yake. Ilikuwa inamuma sana
kiasi kwamba karibu hakuweza kuvumilia.
Ilionekana kana kwamba alikuwa karibu kuzimia
wakati wowote.
Aliuma meno na kutazama juu huku akihangaika,
ila alichokiona ni Alvin akiuangalia mguu wa Sarah
kwa huruma. "Uko salama?"
“Sijambo. Asante Mungu umewahi kurudi." Sarah
akaikumbatia shingo yake kwa nguvu.
“Usijali, nipo hapa kwa ajli yako." Alvin alimbusu
paji la uso wake kwa upole. Alipomtazama Lisa,
mara moja sura yake nzuri ikabadilishwa na sura
ya kuchukizwa.
“Ulisema huumwi wewe? Nadhani ugonjwa wako ni
mbaya ya tunavyofikiria. Usipopona, utafungiwa
ndani milele. Kwa njia hiyo, huwezi kumuumiza
yeyote.” Baada ya Alvin kumuonya, alimbeba
Sarah kuelekea mlangoni na kuondoka bila
kuangalia nyuma.
“Mimi si mgonjwa. Mimi si mgonjwa...” Lisa
alitambaa hadi mlangoni, akijaribu kutoroka, lakini,
mlinzi aliingia haraka na kumpeleka kwenye wodi
ya wagonjwa wa akili.
Kulikuwa na kitanda kimoja tu kwenye kona na

dirisha dogo na la juu sana hivi kwamba mtu
asingeweza kupanda kutoka humo. Mlango wa
chuma nje pia ulikuwa umefungwa. Lisa alibisha
mlango kwa muda mrefu, lakini hakuna mtu
aliyeufungua. Baadaye, alichoka sana na akalala
kwenye kitanda cha hospitali, akijipinda na
kujikunja kama mapira.
Hali ya hewa ilibadilika na kuwa joto kali. Ni kana
kwamba joto liliongezwa makusudi. Punde,
alianguka kwenye joto kutokana na joto kuzidi.
Akiwa amepoteza fahamu, kuna mtu aliingia
kumchoma sindano. Alitumia nguvu zake zote
kumzuia. Hata hivyo, mtu huyo aalikuwa
amemkandamiza kwa nguvu kitandani. Sindano
ililazimishwa kupenya kwenye ngozi yake. Machozi
ya moto yalitiririka kwenye kona za macho yake.
Kwa muda mfupi tu, alihisi kizunguzungu. Alihisi
kwamba alikuwa akipandisha wazimu kweli.
Alichukia sana. Je, alikosea nini katika maisha
yake ya nyuma hadi kumfanya anyanyaswe hivyo
na Alvin Kimaro, shetani? Ha! Aliwahi kutaka
kubaki na kumsaidia Alvin ili apate nafuu ili
asipelekwe hospitali ya wagonjwa wa akili.
Alimpigania Alvin asipelekwe huko, lakini yeye
ndiye aliyempeleka huko badala yake!
'Alvin Kimaro. Sarah Njau. Hata kama nitakuwa

mzimu, sitawaacha kamwe'. Lisa alijipiza.
•••
Usiku sana. Katika Jumba la Klabu, Alvin alikuwa
amekaa kwenye sofa la ngozi akiwa na glasi ya
mvinyo mwekundu mkononi mwake. Alikuwa
amevalia shati jeusi lenye mistari na vifungo
vichache vya juu vikiwa vimefunguliwa. Uso wake
uliokuwa umekunjamana ulionekana hatari sana.
Sarah, ambaye alikuwa akiimba na Cindy,
alinyamaza na kumtazama tena. Midomo yake
ikakunjua tabasamu zito. Kuanzia wakati huo na
kuendelea, mwanamume huyu angekuwa wake na
wake peke yake!
Kisha, mlango ukafunguliwa kwa nguvu. Sam
akaingia ndani akiwa na hasira machoni pake.
“Alvin, unawezaje kumfungia Lisa kama mgonjwa
wa akili? Unajaribu kumfanya awe kichaa?”
“Sam, huelewi. Lisa ana wazimu kweli.” Rodney
alisimama kivivu na kuweka mkono wake begani
kwa Sam.
Lakini, Sam alitupa mkono wake mbali. “Bullsh*t.
Alikuwa sawa kabisa nilipomwona mara ya
mwisho. Ninamjua. Amepitia vikwazo vingi huko
Dar es Salaam, kwa hivyo yeye si mtu ambaye
atashindwa kirahisi hivyo.”
“Unamfahamu? Je, unamfahamu kuliko mimi?”

Alvin alikodoa macho na kusimama taratibu.
“Alvin, unamfahamu pia, lakini umesahau mambo
mengi.” Sam hakuelewa kwanini Alvin alionekana
kuwa mtu tofauti sasa. “Mruhusu atoke. Ikiwa
humpendi tena, basi mwache aende zake. Yeye
hatakusumbua. Ukimweka mahali kama humo,
hata mtu wa kawaida atarukwa na akili, achilia
mbali mwanamke aliyefiwa na watoto wake.”
Sarah alisema kimya kimya, “Bwana Harrison, Lisa
kweli alipatwa na wazimu. Ikiwa huniamini, karibu
amchome Alvin na kisu. Yeye pia ndiye
aliyemjeruhi Alvinic kichwani...”
“Funga mdomo wako.” Sam hakuwahi kumpenda
Sarah, lakini sasa alikuwa na chuki isiyoeleweka.
"Sam Harrison, ndivyo unavyozungumza na
Sarah?" Rodney alikunja uso bila furaha. "Sarah
ana nia nzuri tu."
Sura ya: 307
Sam alimtazama Rodney, kisha akawatazama
Chester na Alvin waliokuwa kimya. Hakuweza
kuelewa ni kwanini walionekana kana kwamba
wamevurugwa akili. Ilianza lini? Ilionekana kama
kila kitu kilibadilika tangu Sarah atokee.
“Chester, Rodney, ni sawa kwa vile Alvin ni

mgonjwa, lakini nyinyi wawili ni watu wa kawaida.
Ugonjwa wa Alvin ulipoanza, Lisa alikataa
kumuacha. Unajua jinsi alivyoharibika na kufungwa
kwenye jela ya Kimaro, na nyinyi wawili hata
mlimsifu hapo awali. Ndiyo, hujamfahamu kwa
muda mrefu, lakini unapaswa kumuelewa kidogo.”
Sam alinguruma kwa hasira. "Wakati huo, ni yeye
aliyemchukua Alvin na kuzuia familia ya Kimaro
kumtupa katika hospitali ya magonjwa ya akili.
Bado sasa, mnamtumpa yeye moja kwa moja.
Bado nyinyi ni wanaume?"
Alvin alikunja uso sana. Maneno ya Sam
yalionekana kufahamika kwake kidogo. Alijaribu
kukumbuka kumbukumbu hizo, lakini kichwa
kilimvurugika ghafla, na hakukumbuka chochote
tena.
Rodney naye alikunja uso. Sam alimfokea.
“Rodney, najua unamlaumu Lisa kwa kumchukua
Alvin, lakini alipokutana na Alvin, hakujua kama
Alvin aliwahi kuwa na Sarah. Alipojua, aliamini pia
kwamba Sara alikuwa amekufa. Ni mke wa Alvin,
lakini baada ya kurudi kwa Sarah ulidai aondoke
kwa sababu nyie mna uhusiano mzuri na Sarah.
Lakini umewahi kujiweka katika viatu vyake?
Alipoteza watoto wake na mumewe. Yeye hana
chochote alichobakiza. Vipi kuhusu Sarah? Ana

wewe. Ana Alvin. Ana wakati ujao mkamilifu.”
Rodney alishangazwa na maneno yake. Macho ya
Chester yaliganda kidogo huku akiwasha sigara.
Ndiyo, wakati fulani alifikiri kwamba Lisa alikuwa
anastahili kuwa na Alvin, lakini, Lisa alipokutana na
Charity mara kwa mara alimuudhi sana. Kisha, ni
baada ya kifo cha Maurine na kurudi kwa Sarah
ambako kulimfanya asahau kwamba alikuwa
amemsifu Lisa hapo awali.
“Sam, kwa kawaida sitamruhusu atoke hadi
atakapopata nafuu,” Alvin alieleza. Kwa kweli,
alikuwa amechanganyikiwa sana.
Sam alipokuwa anataka kuzungumza, mara ghafla
simu ya Chester ikaita. Aliijibu, na muda mfupi
baadaye, sigara mdomoni ikaanguka kwenye
suruali yake na kuchoma tundu ndani yake bila
yeye kutambua.
Ni hadi Cindy alipomfagilia sigara hiyo kwa haraka
ndipo alipoweka simu yake chini na kusema kwa
sauti nzito, “Hospitalini wananitafuta. Lisa Jones
amekufa...”
Chumba kilikaa kimya kwa zaidi ya sekunde kumi.
Alvin alimtazama Chester na kupata shida
kupumua. Ni kana kwamba kilindi cha moyo wake
kilichomwa na kisu kikali. "Umesema nini?"
Macho yake yalimtazama Chester. Chester

alifungua kinywa chake kwa uso mgumu. "Wauguzi
hospitalini walipoenda kumchoma sindano,
waligundua kuwa alikuwa amepasua shuka
vipande vipande na kujinyonga."
Alvin kichwa kilimshtuka. Kila kitu kilichomzunguka
kiligeuka kuwa cheusi. Lisa alikuwa amekufa? Hiyo
ingewezaje kutokea?
Alitazama saa yake kujua kama ilikuwa ni Aprili ya
Wajinga na kuna mtu alikuwa akimchezea. Lisa
alikuwa bado mdogo sana. Kwanini alijinyonga?
Hakuamini. Hakuamini kuwa Lisa amekufa.
Alvin alitoka haraka chumbani. Alikimbia hadi
hospitali na kumshika mmoja wa madaktari wa
idara ya magonjwa ya akili. "Wadi ya Lisa Jones ni
chumba gani?"
"Amepelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia
maiti."
“Chumba cha kuhifadhia maiti?” Alvin alishusha
pumzi, na mng'aro wa hasira ukamtoka machoni.
“Kwanini ulimpeleka kwenye chumba cha
kuhifadhia maiti?”
Daktari aliogopa sana kwa sura yake ya ukali kiasi
kwamba miguu yake ilitetemeka. “Yeye... Alikufa.
Ni utaratibu wa kawaida wa hospitali kumpeleka
mtu aliyekufa katika chumba cha kuhifadhi maiti.”
Alvin alimtupa pembeni na kukimbilia chumba cha

maiti. Alvin aliinua kitambaa cheupe huku mikono
yake ikitetemeka, na kumuona Lisa akiwa amelala
kimya kimya. Kama asingekuwa na jeraha la kijani
kibichi kwenye shingo yake, angeonekana kama
alikuwa amelala tu.
Aliweka mkono wake unaotetemeka kwenye pua
yake ili kuona kama alikuwa akipumua. Kulikuwa
na barafu. Je, alikuwa amekufa kweli? Kisha
akapiga kichwa chake kwa nguvu. Ilibidi awe
anaota. Hii haikuwa kweli. Mara ya mwisho
walipokutana, hata alikuwa akiwakosoa na
kuwauma watu. Alikufaje ghafla hivyo?
“Potelea mbali, Alvin.” Nguvu kali ilimvuta kwa
nyuma na kumsukumia mbali. Pamela alikimbia
kando ya kitanda. Baada ya kuona maiti ya Lisa,
alimtazama Alvin kwa hasira. “Yote ni sababu
yako, b*star! Wewe ndiye ulimnyanyasa Lisa hadi
kifo chake, muuaji wewe!”
“Sikufanya hivyo. Yeye... alikuwa mgonjwa.” Alvin
hakutupa hata macho yake yake meusi kwa
Pamela. Alibaki palepale huku akimtazama Lisa.
Bado hakuweza kukubali kilichokuwa mbele yake.
Hakuweza kujielewa. Hakumpenda Lisa hata
kidogo. Hata hivyo, kwanini alihisi kana kwamba
nafsi yake ilikuwa imetolewa? Ni kana kwamba

alikuwa amepoteza mtu muhimu katika maisha
yake? Machozi hata yalimtoka bila kujizuia na
kumfanya asione vizuri.
"Wewe ndiye mgonjwa." Huku akiwa na kwikwi,
Pamela alimfokea na kumkosoa, "Lisa alikuwa
sawa. Wewe ndiye uliyekuwa ukimtesa na
kumnyanyasa bila sababu. Ulimsukuma kwa
makusudi na kumfanya apoteze watoto wake.
Ulimfunga hata katika hospitali ya magonjwa ya
akili na kumwondolea uhuru wake wote. Ni wewe
na Sarah ndiyo mlimfanya aonekane kichaa.
Haijalishi kama hukuwa na hisia kwake. Ungeweza
tu kuachana naye. Lakini kwanini ulilazimika
kumtelekezana ujauzito wa watoto wako na kisha
wewe ukarudi kwa Sara? Kwanini hukumwacha
aende zake? Hata hivyo ni sawa. Sasa kwa kuwa
amekufa, hatimaye ameachiliwa. Ameachiliwa
kutokana na kuteswa na nyie. Nitamchukua.
Sitawaruhusu ninyi wanandoa wasio na aibu
kuhifadhi maiti yake.” Pamela akashusha pumzi
ndefu na kumuomba muuguzi amsogeze Lisa.
"Unafanya nini?" Alvin bila fahamu alishika mkono
wake. “Ni mke wangu, kwa hiyo nitashughulikia
mazishi yake. Hili halikuhusu.”
“Umewahi kumchukulia kama mke wako? Ni nini
kinakupa haki ya kumzika? Mpuuzi wewe!” Pamela

akatoa kitambaa kilichokuwa na damu na kukiweka
kifuani mwake. “Itazame kwa makini. Lisa aliandika
maneno yake ya mwisho juu yake kwa kutumia
damu yake mwenyewe. Hataki umzike, na hataki
kuzikwa chini ya familia ya Kimaro pia. Anataka tu
kukaa mbali nawe.”
Alvin aliduwaa baada ya kuona maneno yale
yaliyoandikwa kwa damu. Ina maana, alimchukia
sana? Labda ingembidi amwache aende zake.
Hata hivyo, hakuweza kufanya hivyo alipomtazama
usoni. Hakuweza kuzuia macho yake kutoka
kwake. Hakuweza kukubali ukweli kwamba
asingemuona tena katika maisha yake.
"Hapana. Huwezi kumuondoa.” Alvin alimzuia
Pamela kwa dhamira.
"Alvin, acha tu amchukue Lisa." Ghafla, Bibi
Kimaro ilisikika mlangoni.
Ghafla Alvin akageuza kichwa chake na kumuona
Mzee Kimaro, Bibi Kimaro, na Jack wamesimama
pale. Hakujua walipotokea. Jack alipomuona Lisa
alishindwa kujizuia kumpiga Alvin usoni. “Jinsi gani
huna aibu kufikiria hata kumzika binti wa watu.
Hukumchukulia kama binadamu alipokuwa hai,
kwa kuwa sasa amekufa, kwanini usimwachie?”
“Kwa sababu tu sikuingilia mambo yako, uliishia

kumsukuma Lisa na kuwaua mapacha. Niligundua
tukio hili siku mbili tu zilizopita,” Mzee Kimaro
alisema kwa hasira. “Unawezaje kuwa mkatili
hivyo? Unaweza kuwa mpenzi kigeugeu, lakini
huwezi kumtendea mke wako na watoto kwa njia
hii. Hata mama yako hakufika hatua kama hii.”
Sura ya: 308
"Kweli," Bibi Kimaro alisema kwa kukata tamaa.
“Mkeo alipokuwa mjamzito, ulimsumbua Sara
mchana kutwa na usiku kucha. Sio tu kwamba
ulimpuuza, lakini pia ulimfunga na kumsababishia
kuishia katika hospitali ya magonjwa ya akili.
Umepitia hospitali ya magonjwa ya akili ulipokuwa
mdogo pia. Unawezaje kufanya jambo lisilo la
moyo kama hilo? Tayari amekufa, lakini unakataa
kumwachilia. Unapanga kumwonyesha jinsi
unavyopendana na Sarah kwenye mazishi yake
mwenyewe?"
“Tafadhali, nakuomba, mwache aende zake."
Pamela ghafla alipiga magoti na kulia kwa
uchungu. "Hakuwa na furaha na wakati wake wote
hapa Nairobi. Ningependa kumrudisha Dar es
Salaam, kule alikotoka.”
“Mwondoe.” Mzee Kimaro alitikisa mkono wake.

Huenda hakumpenda Lisa hapo mwanzo, lakini
wakati wa muda wao pamoja siku za mwishoni
mwishoni, alianza kumpenda kwa utii wake.
“Ulimtesa sana binti wa watu alipokuwa hai. Kwa
kuwa sasa amekufa, mwacheni tu, mwache aende
kwa amani.”
Bibi Kimaro alisema kwa uchungu, "Alvin, sielewi
kwanini umekuwa mkatili hivi siku za karibuni."
Hapo hapo, kifua cha Alvin kikamshikana. Je,
alikuwa mkatili? Je, alikosea?Hakuwa na maana ya
kumfungia Lisa. Alikuwa chini ya hisia kwamba
alikuwa na huzuni.
Hapo awali alikuwa amefikiria kumpa kiasi cha
pesa ambacho kilimtosha kutumia maishani mwake
na kumfanya aondoke baada ya kujifungua watoto.
Lakini, kwanini alikufa vibaya hivyo? Alvin alikuwa
ameganda palepale. Mwishowe, Pamela
alimchukua Lisa.
Tukio la kukutana kwa mara ya kwanza na Lisa
lilimpita akilini na kuendelea kujirudia kichwani
mwa Alvin.
“Kweli mimi ni mgonjwa, nina kichaa. Ninaumwa
kichaa cha mapenzi!”
"Mvulana mzuri, unaonekana kupendeza sana
huku macho yako yakiwa yamefumbwa hivi
kwamba unawafanya wanawake washindwe

kujizuia."
"Nataka kukuoa."
“Naapa kuanzia sasa nitakutendea mema tu, na
nitakuahidi kila nilichosema. ..
Kwa kweli, aliwahi kuwa mrembo sana na mrembo
kama vixen mdogo. Kwa hiyo alianza lini
kumchukia, hasa alipomwona? Je, yeye ndiye
aliyemsababisha ajinyonge? Wakati huo, Alvin
alichanganyikiwa mpaka mwisho wa akili zake.
Hakukumbuka hata jinsi alivyotoka hospitalini.
Hapo ndipo Sara alipotokea mbele yake, na macho
yake mekundu yakajawa na hatia. "Ni kosa langu.
Nilifikiri alikuwa anaugua mshuko wa moyo kidogo.
Sikujua kuwa hali yake ilikuwa mbaya sana.
Asilimia 15 ya watu wanaopatikana na unyogovu
wa moyo huishia kujiua. Nilipaswa kumtendea
vyema. Samahani."
Hata hivyo, Alvin moja kwa moja alimpita Sarah
kana kwamba hakumsikia. Alichokuwa nacho
akilini mwake ni sura ya Lisa iliyokufa huku macho
yake yakiwa yamefumba. Alikuwa akifanya nini
alipokufa?
“Alvinic...” Sarah alinyoosha mkono wake
kumshika.
Alvin aliinua mkono wake kwa nguvu ili kujinasua
kutoka kwenye mshiko wake. Alimtazama kwa

hasira na kusema, “Imetosha. Baada ya yote, yote
yamesababishwa na Thomas. Ikiwa asingefanya
hivyo, Pamela asingejiingiza kwenye matatizo, na
nisingemfunga Lisa. Ugonjwa wa Lisa usingekuwa
mbaya zaidi, na asingefikiria kuniua. Watoto
wasingepoteza maisha yao pia. Sikupaswa
kumsaidia.”
Ilikuwa ni kwa sababu ya Thomas kwamba
alipoteza mapacha pamoja na Lisa. Ghafla, alianza
kutilia shaka. Je, Mungu alikuwa akimuadhibu Alvin
kwa kumsaidia Thomas?
“Samahani. Sikutarajia ingekuwa hivi.” Sarah
aliogopa kuona sura yake ya hasira. Hakuwahi
kumuona Alvin akionekana kutisha kiasi hicho.
Ikiwa hilo lingetokea kabla ya hapo, angehisi hatia
mara moja kwa kuwa mkali kwake. Lakini,
hakuweza kuvumilia kifo cha Lisa. “Ndio.
Hukutarajia kwa sababu unachofikiria ni
kumwendekeza Thomas tu. Ameua watu wangapi
kwa miaka yote?"
Lisa alikuwa sahihi. Alvin aliona maisha ya kila mtu
hayana thamani isipokuwa ya Sarah. Hata alivuka
msingi wake wa maadili kwa ajili yake tena na tena.
"Alvinic, mimi ndiye wa kulaumiwa kwa hilo. Ni
kosa langu." Sarah alipiga magoti na kulia kwa
jazba. "Kwa kweli sikutarajia mambo kuwa hivi."

“Naomba uondoke sasa. Nataka kutumia muda
wangu peke yangu.” Alvin aliingia kwenye gari
mara moja bila hata kumtazama. Hii ilikuwa mara
yake ya kwanza kumtendea Sarah bila kujali tangu
arudi.
Sarah aliinua kichwa chake taratibu na kulitazama
gari hilo likitokomea kwa mbali. Akasaga meno na
kukunja ngumi. Hakuwahi kufikiria kwamba Alvin
angepoteza utulivu wake kwa sababu ya kifo cha
Lisa. Ikizingatiwa kuwa alimlawiti Alvin kisaikolojia,
hakupaswa kuwa na hisia na Lisa. Kwa
mwonekano wake, alikuwa amedharau upendo wa
Lisa kwake. Kwa bahati nzuri, Lisa alikuwa
amekufa. Kusingekuwa na mtu ambaye angeweza
kuchukua nafasi yake tena!
Ghafla, Thomas akampigia simu. "Sarah, kweli Lisa
amekufa?"
“Ndiyo.”
“Hiyo ni ajabu. Kwa hiyo hivi karibuni, utakuwa Bi
Kimaro halali?” Thomas alifurahi. Huku Sarah
akiwa tegemeo lake, angeweza kuomba na
kupewa chochote katika siku zijazo.
"Afadhali ujiangalie mwenyewe," Sarah alijibu kwa
ukali, "Alvinic anakulaumu kwa kifo cha Lisa.
Nadhani hatajisumbua kuhusu wewe tena.”

"Nini? Lazima utakuwa unatania.” Baada ya kuhisi
wasiwasi kwa muda, Thomas alitabasamu na
kusema, “Bwana Kimaro anakujali zaidi. Jitahidi tu
kumpa mahaba mazito, na muda si muda atasahau
jambo hilo.”
Sarah kichwa kilimuuma. Kwanini alikuwa na kaka
asiyejitambua kiasi hicho? Kama si kaka yake wa
tumbo moja, asingemjali. "Ninakuonya, chunga
tabia yako kuanzia sasa. Siku moja utajikuta huna
msaada."
Baada ya kukata simu, Sarah aliendesha gari hadi
jela moja kwa moja.
Punde, Charity akatoka nje. Sarah alikuwa
amewaomba baadhi ya watu waliokuwa jela
kumshughulikia Charity, lakini alikuwa mgumu na
mcheza karate mzuri kiasi kwamba hawakuweza
kumfanya chochote. Kwa hivyo, alikuwa akiishi
maisha mazuri gerezani. Ingawa alikuwa
amekonda, alionekana bora zaidi.
Ndani ya moyo wake, Sarah alikuwa akihema kwa
hasira. Hata hivyo, alipompiga picha Charity na
kuhisi kuwa alikuwa amegundua mawazo yake,
alitabasamu. "Inaonekana umekuwa ukiishi vizuri
gerezani."
"Unajaribu kufanya nini tena?" Sura ya Charity
ikaonekana kukasirika. Kama angejua ni Sara,

asingetoka nje.
“Hakuna aliyekutembelea hivi karibuni, sivyo? Kwa
hiyo nimekuja kukuambia jambo fulani kutokana na
wema wa moyo wangu.” Sarah alitabasamu na
kusema, “Rafiki yako mkubwa, Lisa, amefariki leo.
Charity alitetemeka, lakini muda mfupi baadaye,
alicheka na kusema, “Acha kuongea upuuzi. Lisa
yuko sawa. Alikuja tu na kunitembelea muda si
mrefu uliopita.”
“Sisemi uongo. Amekufa kweli. Alijiua.” Sarah
alikuwa akichezea kucha zake, ambazo zilikuwa
zimetoka kubandikwa. "Hivi karibuni nitakuwa mke
mpya wa Alvin."
“Sitakuamini.” Charity akatikisa kichwa. Lisa
alikuwa mwanamke mzuri na mwenye afya njema,
kwanini angejiua? Alichosema Sarah kilionekana ni
ujinga tu kwake.
Sura ya: 309
Sarah alibofya ulimi wake na kusema, “Kwanini
nikudanganye? Lisa hakuweza kukubali ukweli
Zaidi ya hayo, kaka yangu pia alitaka kumbaka
Pamela. Lakini Alvinic hakuweza kuvumilia
kumuona akiwa kwenye matatizo, hivyo akamtoa
kwamba mimi na Alvinic tuko kwenye uhusiano.

kaka yangu jela na kumzuia Pamela asichunguze
suala hilo. Lisa alikasirika sana hivi kwamba
alikuwa na ugomvi na Alvinic. Alvinic alimsukuma,
na akawapoteza watoto tumboni mwake. Kwa
kuwa alikuwa na kiwewe, nilimwambia Alvinic
ampeleke hospitali ya magonjwa ya akili kwa
matibabu. Pamoja na sindano na dawa zote
alizopewa, alijiua mwishowe.”
Alitamka kila neno kwa kawaida sana. Hata hivyo,
maneno hayo yalisikika masikioni mwa Charity
kama bomu.
Thomas alitaka kumbaka Pamela? Lisa alijiua?
Ingawa Charity hakuwajua Pamela na Lisa kwa
muda mrefu, aliweza kutambua kwamba ni watu
pekee waliomwamini kwa dhati pindi anapopata
matatizo. Lakini, angalia jinsi walivyoishia.
"Sarah, kwanini unakuwa mkatili kiasi hiki?" Charity
alikasirika sana hadi macho yake yakawa
mekundu, na mwili wake ukatetemeka. Kama
kusingekuwa na dirisha la nondo lililowatenganisha
wawili hao, angetoka nje na kumchukua Sarah na
kumfanyia kitu kibaya sana.
"Mimi ni mkatili zaidi kuliko unayoweza kunifikiria."
Sarah aliridhishwa na jinsi Charity alivyoonekana
kuwa na wasiwasi sasa. “Lisa alipokutembelea
mara ya mwisho, hakukuambia kuwa wazazi wako

wamekufa?”
Bam! Habari hizo zilikuja kama pigo jingine kwa
Charity. Alitikisa kichwa kwa nguvu. "Lazima
utakuwa unanidanganya!"
"Nilimweka mama yako chini ya ‘hypnosis’ nyepesi.
Baada ya mimi kuondoka, alianguka kwenye sinki
la kuogea na akafa kwa kupoteza damu nyingi kwa
sababu hakuna aliyemuokoa. Baba yako alipojua
kuhusu hilo, alipata mshtuko wa moyo na akafa.
Usitarajie kama watakutembelea maisha yako
yote.”
Sara aliangaza vibaya. Aliongea kwa upole kiasi
kwamba ni wawili tu waliweza kumsikia. "Lakini
ilipofika wakati wa mazishi ya mama yako, niliutoa
mwili wa mama yako kwenye jeneza na
kuubalidilisha kuwa wa mbwa."
"Sarah, wewe si binadamu." Damu ya Charity
ilikuwa ikichemka.
Aliendelea kupiga nondo za dirisha mithili ya
mwendawazimu, akitaka kumuua Sarah vibaya
sana. Hata hivyo, upesi polisi walimzuia.
Charity alipiga kelele kama mnyama wa porini, na
uso wake ulijaa machozi. Kwanini Mungu alikuwa
akimpendea hivyo?
Alichoishia ni kuwa gerezani, na rafiki na wazazi
wake walikuwa wamekufa. Sasa, alikuwa peke

yake kabisa. Hata hivyo, muuaji alikuwa huko nje
akiwa huru kaisa. Katika kipindi chote alichokuwa
gerezani, Charity hakuwahi kulia kwa huzuni hivyo
bila tumaini na bila kufarijiwa. Polisi hawakuwa na
la kufanya zaidi ya kumwangusha na kupoteza
fahamu.
Charity alipozinduka alijikuta amelala kwenye
kitanda cha magereza. Macho yake ya kupendeza
yalibadilishwa na kuwa kama shimo la giza lisilo na
mwisho. Alitaka kulipiza kisasi. Alitaka kulipiza
kisasi dhidi ya kila mtu aliyemkosea.
Sarah Njau, Alvin Kimaro, Chester Choka, Thomas
Njau... Alichokuwa akingoja ni muda tu!
•••Nusu mwaka baadaye•••
Mara tu Chester alipomaliza upasuaji wa saa tatu,
msaidizi wake alimsogelea ghafla. "Nilipokea
habari kwamba Charity aliruka baharini na
kukimbia wakati wafungwa walipokuwa wakilima
shamba lao huko Bagamoyo. Polisi wamejaribu
kumtafuta baharini kwa siku tatu, lakini bado
hawajampata.”
Chester alijitenga kwa muda. Kisha, taratibu
akavua miwani yake na kugeuka kuelekea
dirishani. Akawasha sigara.
"Charity hawezi kuogelea."
"Unashuku kuwa amekufa?"

"Unafikiri nini kitatokea kwa mtu ambaye hawezi
kuogelea, anarukia baharini?" Chester akavuta
sigara yake.
Ghafla, alikumbuka sura ya Charity wakati
alipokutana naye kwa mara ya kwanza akiwa na
umri wa miaka kumi na saba. Alikuwa amesimama
chini ya jua na sare za shule, shati jeupu na sketi
damu ya mzee. Ngozi yake ilikuwa laini. Charity
alikuwa kidato cha sita wakati huo na Chester
tayari alikuwa mwanafunzi wa udaktari akitokea
familia tajiri jijini Nairobi.
Siku hizo, wasichana walikuwa na haya sana
walipomwona. Charity pekee alimtazama kimya na
kwa mbali kwa macho yake safi. Wakati huo,
Chester alikuwa na hamu kubwa ya kuvunja
usichana wa binti huyo. Charity alikuwa mpole na
alionekana kumpenda sana Chester.
Lakini nyuma yao kulikuwa na mtu ambaye
hakuufurahia hata kidogo uhusiano wao huo. Mtu
huyo alikuwa Sarah Langa. Sarah alimchukia
Charity kwa sababu tu alikuwa binti wa mama yake
wa kambo. Chuki yake alihakikisha inasambaa
hadi kwa Alvin, ambaye alikuwa ni mpenzi wake
kipindi hicho. Na Alvin, bila kujua nia na makusudi
ya Sarah, akameza chambo na kueneza chuki

hiyo hadi kwenye genge lote la marafiki zake,
Rodney na Chester, ambao walijikuta wote
wakimchukia Charity kwa sababu ya chuki
zilizoenezwa na Sarah.
Hatimaye Charity akamkosa Chester aliyempenda
sana. Tangu wakati huo Chaster hakumpenda tena
Charity na alimchukia kila alipomuona. Kila
alipopata mafanikio, walimchukulia kama mafanikio
hayo yalikuwa ni haki ya Sarah. Charity
alipambana kwa juhudi zake lakini
vikwazoalivyokutana navyo kwa sababu ya Sarah
havihesabiki.
Sura ya: 310
•••Miaka mitatu baadaye. Marekani•••
Lisa aliondoa bendeji usoni mwake polepole mbele
ya kioo, akionyesha sura yake ndogo na ya
kupendeza. Kisha akagusa ngozi yake maridadi.
Baada ya kupitia miaka michache ya matibabu,
ngozi yake iliyoonekana mara chache iligeuka
kuwa laini na nyororo.
Isingekuwa rahisi kusema kwamba alionekana
kama msichana mwenye umri wa miaka 18 pia.
Sura yake, japo ilibadilika kidogo, Daktari
Ramoskutoka Cuba aliyesimamia upasuaji wake,

alijitahidi sana kuirejesha katika mwonekano wake
wa awali.
"Wow, wewe ni mzuri sana, mama." Lisa
alimwambia maneno hayo msichana mdogo
mrembo aliyeinama kwenye mapaja yake na
kumtazama kwa furaha, kisha akamgeukia na
mvulana mdogo aliyekuwa akikimbia kimbia mbele
yake. "Duh, angalia ni nani aliyepita na sura yake
ya kuvutia mbele yangu?" Mvulana yule akakimbilia
nyuma yake alionekana mwenye furaha. "Hakuna
mtu anayeweza kuzaa mvulana mzuri kama mimi."
Lisa akasugua uso wake. Kutokana na sura yake
changa na yenye kupendeza, hakuna mtu ambaye
angeamini kwamba tayari alikuwa amepitia
matatizo makubwa huko nyuma, na sasa ana sura
mpya, na watoto wawili wazuri wenye afya.
“Lakini mimi sifanani na Mama hata kidogo. Lazima
nionekane kama baba yangu mchafu.” Msichana
mrembo alitabasamu.
Lisa naye akanyamaza. Kulikuwa na msemo
kwamba binti atafanana na baba wakati mwana
atafanana na mama.
Hakika ilikuwa sahihi. Ingawa Suzie na Lucas
walikuwa mapacha, hawakufanana hata kidogo.
“Uko sahihi. Unafanana na baba yako mchafu,
lakini wewe ni mrembo zaidi." Pamela akainama na

kuzipapasa nywele za msichana huyo mrembo.
“Pamela...” Lisa alimtazama. “Niko tayari kurudi
nyumbani. Na wewe je?"
Pamela aliinamisha macho yake chini. “Nitarudi
wakati fulani baadaye. Bado nina mradi wa
kushughulikia."
Lisa alimtazama kwa huzuni. "Ni sawa. Nyie wote
ni Wamarekani sasa. Watoto wangu ni kwa
kuzaliwa na wewe ni kwa Green Card. Wakati huu,
nitarudi mimi binafsi...”
“Hakuna haja. Tutashungulikia na wewe upate
Green Card.” Pamela ghafla akatazama juu na
kusema, "Mimi sioni faida ya wewe kurudi iwe
Tanzania ama Kenya. Unaweza kupata maisha
mazuri hapa hapa kwa uwezo ulio nao. Marekani
inawapenda sana watu wenye akili kama wewe."
"Hiyo ni sawa. Lakini lazima nirudi kumalizia kazi
niliyoianzisha ya kumlipizia mama yangu kisasi."
Lisa alificha sura ngumu machoni pake. “Ofcourse
kuna wengine wamejitokeza pia kwenye mkumbo.
Sarah na Alvin, lazima warudishe kila kitu
kilichochangu."
“Sawa.” Pamela alikubali. “Kuhusu Thomas,
nitakuja kudili naye mimi binafsi. Kwa sasa mimi si
mnyonge kiasi hicho.”
“Sitaweza kuondoka na watoto hawa wawili pamoja

nami wakati huu, kwa hivyo nahitaji uwatunze kwa
sasa." Lisa alimsihi Pamela.
“Usijali. Sisi ni marafiki bora.” Pamela aliweka
mkono wake kwenye bega la Lisa huku
akitabasamu. “Zaidi ya hayo, mimi ni godmother
wao."
“Mama, naweza kwenda nawe.” Lucas aliinua
kichwa chake na kusema, “Naweza kukusaidia.”
"Mtoto mzuri. Mama anajua unaweza kumsaidia,
lakini unahitaji kumtunza Suzie.” Lisa
akampigapiga kichwani. "Mbali na hilo, ikiwa familia
ya Kimaro itawaona nyinyi wawili,
watawang’angania."
“Ndio. Mama yako amejitahidi sana kukulinda.”
Pamela aliinamisha kichwa chake na kusema kwa
uzito, “Hasa ni kwa sababu baba yako ataoana na
mama yako wa kambo mwovu. Mwanamke huyo ni
mbaya zaidi kuliko mama wa kambo wa Snow
White. Ikiwa atajua kuwapo kwako, atakuiba na
kukupeleka kwa mama yako wa kambo akulee kwa
mateso.”
Suzie aliogopa sana hadi akakumbatia paja la
Pamela. “Basi mimi sitaki kwenda na mama. Sitaki
huyo mama wa kambo.”
Lucas alikunja uso. “Sawa. Nitakaa hapa kwa sasa,

lakini lazima urudi haraka na kutuchukua."
“Sawa.” Lisa aliitikia kwa tabasamu mwanana.
Licha ya kwamba angewa’miss sana watoto wake,
ilimbidi arudi.
•••Siku mbili baadaye•••
Aliposhuka tu kwenye ndege wa Jomo Kenyatta,
Kelvin Mushi alimwendea mara moja. "Karibu tena,
Lisa." Kelvin alikuchukua masanduku yake huku
akitabasamu. “Hukuwachukua Lucas na Suzie
pamoja nawe?”
“Nimemwomba Pamela kuwatunza. Kelvin...” Lisa
alimjibu kwa uchangamfu.
“Ghorofa iko tayari. Ngoja nikupeleke huko sasa.”
Kwa hayo, Kelvin na Lisa wakaingia kwenye gari.
Redio kwenye gari ilikuwa ikitangaza habari za
ndani. “Kulingana na chanzo cha habari,
Mwenyekiti Kimaro, mtu tajiri zaidi nchini Kenya,
ametumia dola milioni 20 kununua gauni la harusi
la mchumba wake. Inavyoonekana, Mwenyekiti
Kimaro ametayarisha vazi hilo kwa miaka miwili.
Wawili hao wamekuwa kwenye uhusiano kwa
miaka minne na hatimaye wanafunga ndoa.”
Kelvin alimtupia jicho Lisa. Alipoona hali yake ya
utulivu ndipo akashusha pumzi ya raha. “Nimesikia
habari zake pia. Inaonekana kwamba wanafunga
ndoa.”

“Ndiyo hivyo.” Lisa alionekana kutojali lakini
hakukasirika hata kidogo. Tangu alipopelekwa
katika hospitali ya magonjwa ya akili kwa matibabu,
alikuwa ameacha kumpenda Alvin. "Nilikuwa
nadhani kwamba wangekuwa wamefunga ndoa
kwa muda mrefu."
Kelvin alisema, “Wameishi pamoja kwa muda,
jambo linalofanya ionekane kama wamefunga
ndoa.”
Lisa alitabasamu. "Hilo halishangazi."
Alvin alikuwa tayari na Sarah kabla ya kuachana
na Lisa. Zaidi ya hayo, kwa kuwa alidhani kwamba
Lisa amekufa, kwa kawaida angekutana na Sarah.
Kuangalia sura yake, midomo ya Kelvin
ilitetemeka, na akashikilia ulimi wake.
Saa moja baadaye, gari liliingia katika kitongoji
ambapo Karen Estate ilikuwa. Nyumba
aliyomnunulia ilikuwa kwenye ghorofa ya nane.
Ilikuwa na vyumba vinne vya kulala, kumbi mbili za
kuishi, na kibaraza kikubwa. Pia kulikuwa na
vyumba viwili vya watoto - chumba chenye
mandhari ya bluu-anga kwa mvulana na chumba
chenye mandhari ya waridi kwa msichana.
Matandiko katika chumba cha bluu yalikuwa na
Spiderman, ambayo Lucas aliipenda zaidi, ilhali
chumba cha waridi kilikuwa na wanasesere

mbalimbali wa Barbie.
Lisa alipigwa na butwaa. Kelvin alimweleza,
“Nilifikiri ungekuja na watoto pia. Sikufikiri Lucas na
Suzie wangeishi nje ya nchi maisha yao yote.
Utavirudisha hivi karibuni au baadaye, kwa hivyo
nimeunda vyumba vyao kulingana na mapendeleo
yao. Kuna chekechea katika kitongoji hiki, na
mazingira ya hapa ni mazuri kabisa. Pia kuna shule
ya msingi, shule ya sekondari, na chuo karibu na
kitongoji hiki. Zote ni taasisi bora za elimu hapa
Nairobi.”
Lisa alikaa kimya kwa muda mrefu baada ya
kusikia alichosema Kelvin. Bila kusema chochote,
aliguswa. Isingekuwa kwa usaidizi wa Kelvin, Jack,
na Hans miaka mitatu iliyopita, angeweza kuwa na
wazimu kwa kudungwa sindano za kila siku wodini.
Angeweza kugeuka kuwa kweli kichaa na kuishia
katika hospitali ya magonjwa ya akili miaka yote.
Hansa, akishirikiana na Sam Harrison, Jack Kimaro
na Kelvin Mushi ndiyo waliofeki kifo cha Lisa wakati
huo ili kumnusuru yeye na watoto. Baada ya
kwenda nje ya nchi, Kelvin aliendelea kumsaidia
Lisa na watoto wake.
Angeweza kusema kwa waziwazi kwamba
asingekuwa vile alivyokuwa siku hiyo bila yeye.
Sasa kwa kuwa alikuwa amerudi, bado alikuwa

akimjali na kumfikiria sana.
“Lisa, usifikirie sana. Ninafanya hivi kwa hiari
yangu,” Kelvin alisema huku akitabasamu. "Tangu
nilipokutana nawe huko Dar es Salaam, moyo
wangu hauna mtu mwingine ila wewe. Endelea na
unachotaka kufanya, lakini siku zote nitakusubiri
wewe pekee.”
"Kelvin, mimi tu ... sidhani kama ninastahili kuwa
na wewe." Moyoni, Lisa alihisi hatia sana.
“Ni kwa sababu ya Lucas na Suzie?” Kelvin aliuliza
kwa sauti nyepesi. "Machoni mwangu, hao ni
malaika wa kupendeza zaidi ambao nimewahi
kukutana nao. Hawajawahi kuwa mzigo. Ingekuwa
furaha yangu kama ningekuwa baba yao.”
Kwa mara nyingine tena, Lisa aliguswa.
Kila alipokuwa katika hali kama hii, alijikuta
akisaidiwa na Kelvin badala ya Alvin. Alijuta
kumwangukia Alvin badala ya yeye. Kelvin ndiye
alipaswa kumthamini.
“Samahani, Kelvin. Siwezi kukuahidi chochote
sasa. Nilirudi safari hii kwa nia moja tu ya kulipiza
kisasi,” Lisa alisema kwa ukali.
“Najua. Nimengoja kwa miaka mitatu, na sijali
kusubiri tena hata kama itakuwa milele.” Kelvin
alipapasa kichwa cha Lisa. "Nenda na ujitayarishe

kwa sherehe ya kuadhimisha miaka 30 ya Ngosha
Corporation usiku wa leo."
TUKUTANE KURASA 311-315
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA SABA
SIMULIZI........................LISA KURASA......311 MPAKA 315
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY WHATSAPP: +255628924768

Sura ya: 311
Hoteli ya Pavilion Intercontinental. Mombasa. Sherehe kubwa ilikuwa ikiendelea. Mambo mengi sana yalikuwa yametokea kwa familia ya Ngosha katika miaka michache iliyopita. Miaka mitatu iliyopita, Joel alizinduka ghafla kutoka kwenye coma, baada ya hapo akasisitiza kuachana na Nina, lakini Nina alipinga wazo hilo. Baadaye, masharti ya talaka yao yaliamuliwa na mahakama. Hata hivyo, bado walikuwa na daraka la kumtunza binti yao, Melanie.
Tangu Melanie aolewe na Jerome, hali yake ilikuwa imeboreka sana. Sio tu kwamba alikua Makamu Mkurugenzi wa Ngosha Corporation, lakini pia alikuwa ameanzisha kampuni ya umeme kwa ushirikiano na Campos Corporation. Iliaminika kuwa Kampuni ya Ngosha lilikuwa na thamani ya zaidi ya dola bilioni sita.
Siku hii iliadhimisha mwaka wa 30 tangu Ngosha Corporations ianzishwe, hivyo kampuni hiyo ilifanya sherehe kubwa zaidi kuwahi kutokea. Ilihudhuriwa na watu mashuhuri na familia tajiri zaidi katika sekta ya biashara kote ndani na nje ya Kenya.

Katika ukumbi wa sherehe, baada ya kuwahudumia wageni wachache, Joel aligeuka na kumkuta Damien akiwa amezungukwa na watu wazito na wenye ushawishi, hisia ngumu ikaangaza juu yake.
Tangu Joel apate fahamu miaka mitatu iliyopita, mambo mengi yalionekana kubadilika. Lisa alikuwa amejiua, na Damien akawa Mwenyekiti mpya wa Ngosha Corporation licha ya kwamba hakuwahi kuvutiwa kabisa na mambo ya biashara hapo awali.
Damien aliyemjua leo alikuwa mtu tofauti kabisa. Alikuwa na moyo wa hali ya juu na mwenye mikakati mingi japo alilazimika kutegemea kiti cha magurudumu. Pia alikuwa amewafuta kazi wasaidizi wengi walioaminika wa Joel.
Hata hivyo, Joel alipuuza hali hiyo alipoona kwamba Damien alikuwa kaka yake wa damu na kwamba alijitolea kumlea Melanie. Kwa bahati nzuri, Melanie alikuwa mwenye busara na mwenye bidii katika miaka hii yote. Hata hivyo, Joel hakuweza kujizuia kuhisi hatia kuhusu kumlipa Lisa deni kubwa sana kila alipomwona Melanie.
“Uko hapa, Joel.” Nina alimwendea na kusema kwa wasiwasi, “Unapanga kutangaza lini kwamba Melanie ndiye Mkurugenzi Mtendaji

rasmi wa kampuni na ubia wake na Campos Corporation?”
Ishara ya chuki ikaangaza machoni mwa Joel. “Nani alikuruhusu kuingia?”
“Haya, kwanini siwezi kuja? Mimi ndiye mama mzazi wa Melanie,” Nina alijibu kwa jeuri. “Angalia binti yetu alivyo na uwezo. Baada ya miaka mingi, bado una wasiwasi juu ya kumruhusu kusimamia Ngosha Corporation?" Joel hakuweza kuwa na wasiwasi juu yake. Kuonekana kwake kulimfanya ajisikie kucheka. "Halo, shemeji na kaka." Damien alitabasamu alipowakaribia akiwa kwenye kiti cha magurudumu.
“Nimekuambia mara nyingi kuwa yeye si shemeji yako tena,” Joel alimuonya kwa sauti nzito.
“Najua, najua. Ilikuwa ni mtelezo wa ulimi,” Damien alisema na kucheka. “Kaka, kuona jinsi Melanie anavyofanya vizuri leo kunanikumbusha kwamba kweli mimi ni mzee. Sasa ni wakati wa vijana kuangaza. Baadhi ya wageni wamekuwa wakikusifu kwa kuwa na binti bora kama huyo na ni baraka iliyoje kwako.”
Joel aliitikia kwa kichwa. "Kwa kweli, Melanie amefanya vizuri zaidi katika miaka miwili

iliyopita. Ana uwezo wa kuwa Mkurugenzi Mtendaji. Nitatangaza habari hiyo jukwaani baadaye.”
"Kaka, ninaogopa kuwa ni vigumu kushawishi umma kuhusu nafasi ya Melanie kama Mkurugenzi Mtendaji kwa kuwa hana hisa zozote," Damien alisema kwa sauti ya chini. “Nilisikia baadhi ya wanahisa hawajafurahishwa nayo. Baada ya yote, mimi ndiye Mwenyekiti, na Mkurugenzi Mtendaji ni mtu anayetakiwa kutoka kwenye familia yetu.” Joel akamtupia jicho la ajabu. "Damien, nikihamisha hisa zangu kwa Melanie, itathibitisha kwamba atakuwa msimamizi wa mustakabali wa Ngosha Corporation. Uko tayari kumsaidia?”
“Kaka wewe ni kaka yangu wa damu. Umekuwa ukinitunza tangu nilipokuwa mdogo, kwa hivyo, bila shaka, sitajali kufanya hivyo. Zaidi ya hayo, sina mtoto. Siku zote nimemtendea Melanie kama binti yangu.” Damien aliachia tabasamu hafifu. "Nitajitahidi niwezavyo kumsaidia ili Ngosha Corporation iweze kufika mbali."
“Asante.” Joel alimpiga Damien begani. Alikuwa amesukumwa sana na maneno yake. “Kusema kweli, afya yangu si nzuri tena kama ilivyokuwa hapo awali, kwa hiyo nitakuachia

wewe na Melanie kazi ya kuendesha kampuni ya Ngosha.”
"Ni kweli, kwa sasa zingatia hali yako tu kaka." Mara tu Damien aliposema hivyo, zogo likazuka mlangoni. Kuna watu walikuwa wakipiga kelele, "Mwenyekiti Kimaro yuko hapa."
Alvin kwa sasa alikuwa mkuu wa familia ya Kimaro. Alikuwa amevalia suti nyeusi yenye heshima, shati la bluu na tai. Mavazi hayo yalimfanya aonekane mwenye kuvutia ndani ya umbo lake refu na jembamba. Akiwa na sifa zake mashuhuri na uso mzuri, kila mtu hakuweza kujizuia kushangaa mvuto wake. Taa za chumba cha kulia zilimulika. Umri wake haukujalisha. Kwa kweli, mtu huyu alikuwa kama divai - kadiri inavyozeeka, ndivyo ilivyokuwa na ladha nzuri. Sio tu kwamba alikuwa mtanashati zaidi, lakini pia alidhihirisha hisia kali za umaridadi na mamlaka. Akiwa amevutiwa na uwepo wake, Melanie alimtazama kwa mshangao kwa mbali. Asingeweza kamwe kuchoshwa na sura ya mtu huyo.
Kisha, akamtazama Jerome, ambaye pia alikuwa amevalia suti nyeusi. Ingawa hadhi yake ilikuwa imeboreka sana kwa miaka hii, hali yake ya heshima ilikuwa mbali na ya Alvin.

“Mpenzi wangu, unamtazama nani?” Jerome aliinua uso wake kwa tabasamu baya. Alikuwa amejitahidi sana kwa miaka mingi kupambana na Alvin, lakini, Alvin alikuwa mfanyabiashara mzaliwa wa asili, na Jerome alichukia jinsi alivyoyumbayumba kila wakati ukilinganisha na Alvin. Haijalishi alikuwa wapi, Alvin ndiye aliyekuwa akishika nafasi ya kwanza. "Nashangaa tu kwanini yuko hapa." Melanie alimshika mkono huku akitabasamu.
Jerome alikaza macho yake. "Labda inahusiana na Lisa. Baada ya yote, Lisa ni mke wake wa zamani. Pia alihudhuria siku ya kuzaliwa ya 70 ya babu yako mara ya mwisho."
"Ah, baba yangu hakufurahishwa na sura yake hata kidogo. Nilisikia kuwa ni Alvin na Sarah ndio walimtesa Lisa hadi kifo chake.” Kwa kufikiria tukio hilo, Melanie alishtuka. Alijiona mwenye bahati kwamba hakuolewa naye. “Ndio. Ninashangazwa na jinsi anavyokosa aibu.” Jerome alikunja midomo yake kwa tabasamu la kejeli. Akizungumzia kuwafanyia wanawake ukatili, Jerome hakuwa karibu na Alvin.
Upande wa pili, uso wa Joel ukaingia giza baada ya kumuona Alvin. Hata hivyo, Alvin alijifanya kana kwamba hakutambua

mabadiliko ya uso wa Joel. Alimsogelea na kusema kwa sauti nzito, “Mjomba Joel, nimekuja hapa leo kukupongeza kwa kuadhimisha miaka 30 ya kampuni yako. Hapa kuna zawadi kwa ajili yako." Kwa hayo, Hans akamkabidhi Joel zawadi ya gharama kubwa. Hisia nyingi zilimpanda Joel huku akimwangalia Alvin. “Ondoka, Alvin.”
"Hans, mpe." Alvin alimtupia jicho Hans huku akijifanya kuwa hakusikia maneno ya Joel. “Alvin, unataka nini tena?” Joel alimshutumu kwa hasira. “Ulimuua binti yangu, na sasa unakuwa mkali hata kwangu. Unahisi hatia na unajaribu kujifanya nijisikie vizuri kwako kwa vijizawadi kama hivi?"
Alvin alikunja uso wake huku akibetua midomo yake bila kujua. Ingawa hakuhusika moja kwa moja na kifo cha Lisa, bila shaka lilikuwa kosa lake.
Joel alizidi kupandwa na hasira baada ya kumuona Alvin. "Niliulenga mti usiofaa wakati huo. Potelea mbali, sitaki kukuona tena.” “Kaka, ndiye mgeni wetu mashuhuri siku ya leo. Si vizuri kumfukuza mbele ya watu.” Damien alitabasamu na kuongea ili kupunguza mvutano ule.

Sura ya: 312
Ilikuwa ni saa mbili usiku. Sherehe ilikuwa imeanza rasmi. Kwa hivyo, mwenyeji alimwalika Joel jukwaani kwa hotuba yake. Kadiri Joel alivyokuwa akimwangalia Alvin, ndivyo alivyozidi kuudhika. Kwa hivyo, alizuia macho yake na akapanda jukwaa mara moja. Alichukua kipaza sauti na kusema, “Mabibi na mabwana, karibu kwenye sherehe ya maadhimisho ya miaka 30 ya Ngosha Corporation. Pamoja na maadhimisho haya, ningependa kutoa tangazo muhimu hapa leo. Katika miaka hii yote, Damien na Melanie wamekuwa wakishughulikia mambo mengi katika kampuni kwa kuwa hali yangu haikuniruhusu kufanya hivyo. Kwa hilo, ningependa kuchukua fursa hii kutangaza kwamba kuanzia leo na kuendelea, Melanie atachukua nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa ...”
“Sikubaliani." Ghafla mtu alisukuma mlango wa jumba la karamu lililokuwa limefungwa.
Kila mtu alitazama upande huo. Mwanamke mmoja aliingia ukumbini akiwa amevalia vazi jekundu la lenye mpasuo hadi magotini, akionyesha miguu yake iliyosimama kwenye viatu vya visigino virefu. Nywele zake ndefu

zenye kustaajabisha, zenye mawimbi, za kahawia zilianguka kwenye pande zote za mabega yake. Chini ya mwanga wa taa, alionekana kama malaika mzuri. Kila harakati zake zilitoa hisia ya haiba na mvuto.
Bila shaka, alikuwa mwanamke mrembo zaidi kwenye sherehe usiku huo. Wengi wa wageni walipigwa na butwaa kumwona mwanamke huyo. Uzuri wake ulikuwa wa aina yake huko Nairobi. Hata hivyo, wageni waliona upesi kufanana kati ya mwanamke aliyevalia gauni jekundu na Melanie. Baada ya kulinganisha sura zao, waligundua kuwa Melanie hakuwa mrembo karibu na yule mwanamke aliyevalia gauni jekundu.
Bam! Joel, aliyekuwa amesimama jukwaani, alidondosha kipaza sauti kwenye sakafu. Alimtazama yule mwanamke aliyevalia gauni jekundu kwa mshtuko. Alitetemeka, karibu na kuanguka chini. “Lisa!”
Melanie kisha akapiga kelele. "Lisa, si umekufa?" Alipigwa na bumbuwazi kiasi kwamba karibu aingiwe na wazimu.
Baada ya miaka mitatu ya kusubiri, hatimaye angeweza kuchukua Ngosha Corporation. Hata hivyo, mwanamke aliyefanana kabisa na Lisa alijitokeza ghafula. Alikuwa anaota au aliona mambo kwa uhalisia wake?

Nina alikuwa wa kwanza kupata fahamu zake, na mara moja akamkemea mwanamke huyo, “Tapeli gani huyu? Usalama, fanya haraka na mmchukue. Msimruhusu avuruge sherehe yetu.”
Walinzi wachache walitembea haraka hadi kwa mwanamke yule. Yule mwanamke aliinua uso wake mzuri kidogo, na sura ya dharau ilionekana kwenye uso wake wa kifahari. "Bi. Mahewa, ni miaka miwili tangu bwana Ngosha akupe talaka. Wewe ni nani ili utoe maelekezo ya nini cha kufanya wakati wa hafla muhimu ya Ngosha Corporation? Niko sawa, baba?" Kisha akamkazia macho Joel.
Machozi yalitiririka mashavuni mwa Joel. Alimpa Nina mwanga wa hasira kabla ya kukimbilia kwa maafisa wa usalama. “Usithubutu kumgusa. Kwa hayo, alishuka jukwaani kwa fujo.
“Tulia kaka. Lisa alikufa miaka mitatu iliyopita.” Damien akamsimamisha Joel haraka. Hakuwa na hisia nzuri kuhusu hili.
Silika zake zote zilimwambia kwamba alilazimika kumfukuza mwanamke huyu bila kujali kama yeye ndiye Lisa halisi.
"Naweza kumtambua binti yangu mwenyewe." Joel alimsukuma Damien kwa mkono mmoja.

Joel alipozidi kumsogelea yule mwanamke, alizidi kuwa na uhakika kuwa ni Lisa.
"Bado uko hai, Lisa." Joel alitokwa na machozi. “Samahani, Baba. Hapo zamani, ilinibidi kudanganya kifo changu na kuondoka kwa sababu ambazo siwezi kusema. Hata hivyo, nimerudi sasa,” Lisa alisema huku akiwa amelia. Alimsogelea na kumkumbatia baba yake kwa upole.
“Ni sawa. Nimefurahia kwamba umerudi. Nina deni kubwa kwako. Kuanzia sasa na kuendelea, nitakupa kilicho bora zaidi ya kila kitu.”
Wageni wote pale ukumbini walisikia alichokisema Joel. Kisha, wakaanza kunong'ona juu yake.
“Tangu lini Joel akawa na binti wa haramu?”
"Nilisikia juu yake miaka mitatu iliyopita. Joel alimrudisha binti huyu kutoka Dar es Salaam ili kumtambua kama sehemu ya familia ya Ngosha.”
“Sasa kwa kuwa umetaja, naweza kukumbuka. Nilisikia binti huyu wa haramu aliolewa na Bwana Kimaro baada ya hapo.”
“Seriously? Je, huyo ni Lisa... ni mke wa zamani wa Bwana Kimaro?”
"Ndio, yeye ndiye."

Kila mtu kwa siri akahamishia macho yake kwa Alvin. Wakati huu, uso mzuri wa Alvin ulikuwa umesinyaa na kupooza. Macho yake ya ndani yalikuwa na giza. Hakuna aliyejua kilichokuwa akilini mwake.
Alichokifanya ni kutoa sigara taratibu na kuiwasha. Alipuliza moshi kwa fujo na moshi huo ulificha sifa zake mashuhuri.
“Baba, usimruhusu mwanamke huyu akudanganye.” Melanie alimsogelea ghafla na kusema kwa upole, “Mtu aliyekufa anawezaje kufufuka? Nadhani anafanana na Lisa tu. Kwa namna fulani alipata sura ya zamani ya Lisa na akaja kutudanganya. Zaidi ya hayo, uso wa Lisa ulikuwa umeharibika.”
“Kweli, kaka. Bado unakumbuka jinsi Lisa alivyoonekana kabla hajajinyonga, sivyo? Hata daktari wa juu wa urembo alisema kuwa haiwezekani kurejesha sura yake ya uso. Unapaswa kukumbuka hili, Bwana Kimaro...” Damien ghafla akamtazama Alvin aliyekuwa amekaa kwenye kiti.
Alvin alitoa majivu kwenye sigara kabla hajasimama. Kisha, akamwendea Lisa huku mkono wake mmoja kauingiza kwenye mfuko wa suruali yake. Uso laini wa Lisa ulizidi kumdhihirikia alipokuwa akimsogelea. Aligundua kwamba kwa miaka mingi, kila mara

alikuwa akiona sura yake yenye ulemavu alipomfikiria, hivi kwamba alikuwa amesahau jinsi alivyokuwa anaonekana mwanzoni.
Sasa alipomwona tena, alipokelewa na hali ya kufahamiana na mshangao. Ilibidi akubali kwamba hakuna mtu huko Nairobi ambaye angeweza kulinganishwa na uzuri wake wa kipekee.
“Inatosha, acha kumuuliza Alvin. Kila mtu anajua kwamba hajawahi kunipenda. Hata msaidizi wake ananielewa kuliko yeye.” Lisa alitabasamu kabla ya kumnong'oneza Joel sikioni. “Baba, kabla hujapata ajali, uliahidi kunihamishia asilimia 35 ya hisa za kampuni.” Kwa hayo, wazo dogo la kusitasita katika macho ya Joel likatoweka. Mbali na Lisa, mtu pekee ambaye alijua juu ya suala hili alikuwa wakili wa Joel anayeaminika zaidi.
“Sawa. Mnaweza kuacha kuuliza. Nimethibitisha kwamba kweli ni binti yangu wa damu, Lisa,” Joel alisema kwa dhamira. Melanie alianza kuogopa. “Baba amefanya nini kukuroga?”
"Nimemwambia baba siri yetu ndogo," Lisa alisema kwa tabasmu. "Hiyo ni sawa. Daktari mkuu wa urembo alidai kuwa hakukuwa na tiba ya uso wangu, lakini hiyo haimaanishi kuwa kila daktari ulimwenguni asingeweza

kuutibu. Pamoja na ukuaji wa upasuaji wa plastiki, nimetumia miaka michache iliyopita nje ya nchi kupokea matibabu ya uso. Ilinichukua miaka mitatu kupona.”
Damien alisema bila kujali, “Ndugu yangu anampenda sana binti yake, hivyo kumpumbaza ni rahisi sana. Lakini familia ya Ngosha ni familia yenye heshima, na hatutamruhusu mtu yeyote asiye na asili ya damu yetu kujiunga nasi. Nadhani tunapaswa kuchukua kipimo cha DNA."
“Ndiyo.” Mara moja Nina alienda sambamba na wazo lake. “Hata kama yeye ndiye Lisa halisi, bado ni binti wa haramu mwenye aibu. Hana haki ya kuhudhuria hafla kama hiyo." "Usalama, mpeleke nje." Melanie alimfukuza moja kwa moja.
Ikizingatiwa kuwa Melanie alikuwa mke wa Jerome na mrithi wa hivi karibuni wa Ngosha Corporation, maafisa wa usalama walikimbia kwa haraka kwenda kumtoa Lisa.
"Harakisha. Usipomfukuza, familia za Campos na Ngosha zitaifungia hotel hii. Haitopokea tena sherehe za watu mashuhuri,” Jerome aliagiza upesi.
“Usithubutu.” Kwa hasira, Joel hakuweza kuacha kukohoa.

Sura ya: 313
"Baba, tafadhali tulia." Lisa alipapasa mgongo wa baba yake kwa wasiwasi kabla ya kumtazama Damien kwa ghafla.
“Bam’dogo, bado huna urafiki nami kama ulivyokuwa hapo awali. Mimi pia ni binti wa kaka yako, lakini unapendelea Melanie.” Damien alimtazama kwa ujeurii. “Kama nilivyosema. Nitakubali kuwa wewe ni binti wa kaka yangu na ripoti ya kipimo cha DNA. Vinginevyo, sitaamini neno ulilosema.” "Nadhani sio kama unaniamini. Hutaki tu nirudi kwa kuhofia kuwa uwepo wangu utatisha kwa Melanie.” Lisa alitabasamu licha ya ukali uliokuwa ukitanda machoni mwake.
“Bila shaka uwepo wako utamwathiri binti yangu. Wewe ni binti wa haramu, bado unatarajia kupata sehemu ya Kampuni ya Ngosha,” Nina alisema kwa sauti. "Binti yangu Melanie amefanya mengi kwa kampuni katika miaka ya hivi karibuni. Ipo kwa kila mtu kuona." "Hiyo ni sawa." Baadhi ya wenye hisa wa kampuni hiyo walitikisa kichwa, na mmoja wao akageuka na kumtazama Mzee Ngosha. "Nini unadhani; unafikiria nini?"
Mzee Ngosha akakunja uso. "Melanie kweli ana uwezo wa kuwa mrithi wa kampuni ya

Ngosha. Joel, maliza tangazo la kumfanya Melanie kuwa Mkurugenzi Mtendaji. Tunahitaji kufanya uchunguzi wa DNA kabla ya kubaini kama kweli mwanamke huyu ni Lisa.”
“Babu umenielewa vibaya.” Lisa alieleza taratibu. “Sikujitokeza leo kuwania urithi wa Kampuni. Niko hapa tu kufunua ukweli - kwamba Melanie si binti wa kuzaliwa wa baba yangu."
Maneno ya Lisa yalizua taharuki miongoni mwa hadhira. Joel, hasa, alipigwa na butwaa. Nina, ambaye alikua na wasiwasi zaidi, alifoka, “Siamini kama una jeuri ya kusema hauko hapa kuwania mrithi wa Kampuni. Ili kumuondoa Melanie, hata ulifikia hatua ya kutoa shtaka hili. Je, huoni kufanana kati ya hayo mawili?”
"Unasema ujinga!" Macho ya Melanie yalikuwa mekundu kwa hasira.
“Mjinga! Mwondoe hapa!” Damien alipiga mkono wake chini kwenye mpini wa kiti cha magurudumu. Uso wake ulikuwa umetanda kwa hasira.
"Baba Mdogo, kwanini una haraka?" Tabasamu la ajabu lilienea kwenye uso wa Lisa. "Unaogopa kuwa nitaharibu mipango yako?"

“Hukunisikia? Sitaki mwanamke huyu anayeeneza uongo hapa.” Damien aliwakodolea macho wana usalama. Hawakuwa na la kufanya zaidi ya kumsogelea tena Lisa.
"Nimekuja na ripoti mbili hapa leo." Aliinua mkono wake juu. “Ripoti moja inaonyesha kwamba baba yangu na Melanie wao si baba na binti. Ripoti nyingine inathibitisha kwamba baba mdogo na Melanie wana uhusiano wa baba na binti.”
Baada ya kusikia hivyo wanausalama walishindwa cha kufanya. Joel akampokonya nyaraka zile mikononi mwake na kuanza kuzisoma zile taarifa. Alikuwa amechanganyikiwa, na mwili wake ulikuwa ukitetemeka kiasi kwamba alionekana kuwa karibu kuzimia. Aliinua kichwa chake kumwangalia Nina kabla ya kumtazama Damien kwa hasira. “Nyinyi wawili ni wazazi wa Melanie?”
Wasiwasi ulitanda machoni mwa Nina na Melanie lakini kwa sekunde moja tu ya haraka. Nina alikanyaga miguu yake chini na kupiga kelele, “Joel, wewe nyoka. Unaamini chochote kinachotoka kinywani mwake. Ni rahisi sana kughushi mambo siku hizi. Ninaapa kwamba Melanie ni binti yako wa kuzaliwa.”

Rangi zilitoka kwenye uso wa Melanie. “Baba, unawezaje kusema kwamba baba mdogo Damien ni baba yangu? Hiyo haiaminiki. Wewe ni baba yangu.”
Damien pia alionekana kuhuzunika na kukasirika. "Kaka, tulikua pamoja, lakini unanishuku kwa sababu ya ripoti ya kughushi?"
Bibi Ngosha na Mzee Ngosha walitazamana huku wakionekana kutokuamini. “Joel, ninaamini Damien hawezi kufanya kitu kama hiki.”
Joel alianza kusita baada ya kusikia hivyo. Kumtoa Nina nje ya mlinganyo, kwa kweli aliona ni vigumu kuamini kuwa huu ni ukweli. Baada ya yote, alimlea Melanie tangu alipokuwa mtoto, na Damien alikuwa ndugu yake mpendwa.
“Ninaelewa kwamba mnaweza msiamini ripoti za uchunguzi. Kwa bahati nzuri, nilikuja na mpango mbadala. Lisa alipiga makofi mara moja kwa utulivu na ujasiri.
Skrini kubwa iliyokuwa mbele iliwaka ghafla, na kuonyesha klipu isiyofaa yenye msongamano mkubwa. Damien alikuwa amelala kitandani na Nina akiwa juu yake. Wawili hao walikuwa wakifanya jambo la faragha sana.

"Mpenzi, angalia, kaka yangu asiye na maana anawezaje kujilinganisha na mimi?"
“Uko sahihi. Najuta sana sasa. Nilipaswa kukuruhusu kunioa tangu mwanzo. Damien, wewe ni wa ajabu.”
Nina alipoteza akili baada ya kuona tukio hilo la shauku. Alikimbia mbele, huku akipiga kelele kwa mshangao, “Acha kuicheza. Acha!"
Picha ilibadilika kwenye skrini. Nina alionekana akiwa amelala mikononi mwa Damien. Nguo zake zilikuwa zimevurugika.
“Damien, ni lini Joel mjinga huyo atakabidhi hisa kwa binti yetu, Melanie?”
“Usijali. Nitajaribu kumshawishi afanye hivyo katika maadhimisho ya miaka 30 ya Kampuni.” “Hapo ni sawa. Kufikia wakati huo, Melanie atachukua Kampuni yote ya Ngosha.”
Chini ya jukwaa, uso wa hasira wa Damien ulibadilishwa na aibu. Hapo awali alikuwa amepanga kujiweka wazi kwa Joel baada ya Melanie kuchukua Kampuni. Hata hivyo, hakutarajia itokee hadharani, kwa njia ya kutisha zaidi iwezekanavyo. Picha aliyotumia miaka mitatu kujijengea ilibomoka ndani ya sekunde chache. Kila mtu alikuwa akimshutumu Damien, Nina, na Melanie.

“Mungu wangu, hii ni mbaya sana. Mdogo mtu kula shemeji yake? Ndiyo haya sasa! Nilidhani mambo kama haya yanatokea kwenye tamthiliya za kina Irene Uwoya pekee.” “Uchumba? Haya, tayari walilala na kila mmoja miaka ishirini iliyopita na hata mtoto wao wa nje alilazimishwa kuwa binti wa Joel. Haya yote ili tu kuiba hisa za mtu huyo?”
"Damien ana hila. Nakumbuka Joel amekuwa mwema kwake kila wakati.”
"Bila kumtaja Nina, ambaye kila mara hujifanya kuwa mtukufu. Sikutarajia angekuwa na tabia mbaya kiasi hicho.”
“Hasa. Ninahisi kutapika nikifikiria tu kwamba mke wangu huenda naye dukani mara kwa mara.”
"Kwa bahati nzuri, kila kitu kiko tayari. Vinginevyo, Joel angetoa hisa zake kwa Damien kwa sababu zisizo sahihi.”
Kupumua kwa Joel kulienda kasi aliposikia porojo na shutuma hizo. Lakini, kwa wazo la pili, alijisikitikia sana. Ikawa, alikuwa amewaacha Lisa na Sheryl kwa msingi wa uwongo ambao Nina alimsadikisha kuuamini. Alikuwa amejinyima familia yenye furaha ambayo angekuwa nayo kwa sababu ya uwongo huo. Miaka yote hiyo, alikuwa amemlea binti wa mtu mwingine kama kipenzi

cha thamani huku Lisa akiwa amepitia mateso mengi.
Alifanya nini duniani?! “Wewe b*tch!” Uso mzuri wa Joel haujawahi kutisha kama ilivyokuwa sasa. Akasogea kumpiga kofi kali Nina usoni. “Nitakulipa!”
"D-Damien, nisaidie." Akiwa ametishwa na uso uliopinda wa Joel, Nina alijificha haraka nyuma ya Damien.
Joel aligeuka nyuma kumtazama kaka yake. “Damien, sikutarajia haya kutoka kwako. Inavunja moyo. Sisi ni ndugu! Nimekupa kila ulichotaka tangu tukiwa wadogo, na hivi ndivyo unavyonilipa? Wewe ni jini!”
"We ndumilakuwili! Unathubutuje kufanya jambo la aibu kama hili? Huna aibu?” Mzee Ngosha aligonga glasi chini kwa hasira. Familia ya Ngosha ilikuwa kichekesho kwenye jumuiya ile nzima ya wafanyabiashara. “Damien, umenikatisha tamaa sana,” Bibi Ngosha alisema kwa uchungu. “Nina, nilikuelewa vibaya. Nisingemruhusu Joel kukuoa kama ningejua.”
Sura ya: 314
Nina alijibu kwa uchungu, “Nilimpenda Joel kuliko mtu yeyote angeweza kufikiria, kiasi

kwamba sikuwa na jinsi zaidi ya kufanya hivi ili niolewe naye...”
“Unaonyesha upendo wako... kwa kubeba mtoto wa ndugu yangu, ili nikuoe?” Joel alianza kucheka sana hadi machozi yakamtoka. "Ni bahati mbaya sana kwangu kukutana na wewe. Ondoka mbele yangu! Wewe na binti yako wote wawili!”
“Baba...” Uso wa Melanie ulikuwa umepauka kama mzimu.
Alikuwa karibu kutwaa Kampuni la Ngosha sekunde chache zilizopita, lakini kila kitu kilibadilika kwa kufumba na kufumbua tu. “Baba, sijui kuhusu hili. Siku zote nimekuchukulia kama baba yangu. Tafadhali usiniache.”
“Una uhakika ulikuwa hujui?” Lisa alimsogelea yule mwanamke mwingine huku akitabasamu. “Miaka mitatu iliyopita, baba alipozirai baada ya ajali, wewe na mama yako hamkumtembelea hata mara moja. Hata Dk. Angelo, aliyekuwa akimtibu Baba wakati huo, karibu afe kutokana na moto. Ikiwa nisingemwomba daktari amtibu Baba kwa siri, huenda angali amepoteza fahamu hadi sasa au ameshakufa kabisa.”

Akiwa amechanganyikiwa, Melanie akatikisa kichwa haraka. “Hapana, nilimtembelea. Mimi...”
“Ulikuwa busy na michakato ya kuolewa na Jerome.” Lisa akakatiza, “Hata ulinicheka usoni mwangu wakati habari za kifo cha Dk. Angelo zilipotangazwa. Ulinidhihaki kwa kutarajia baba asingepata fahamu. Naamini ulikuwa umeshajua kwa wakati huo.” “Unadanganya, nilikuwa sifahamu chochote.” Melanie alisema huku midomo ikitetemeka. Lisa alinyoosha mikono yake bila huruma. "Nyinyi watatu mlidhani mngeweza kuchukua udhibiti kamili juu ya Kampuni ya Ngosha. Mlikuwa mnasubiri baba yangu afe, ili Nina aweze kurithi mali yake yote kihalali. Hata hivyo, hamkutarajia kwamba baba yangu angetoka katika hali ya kukosa fahamu katika kipindi cha chini ya nusu mwaka. Muda ulikuwa unaenda hivyo mkaendelea kumdanganya. Nisingetokea leo, mngekosana na baba yangu baada ya kumdanganya awape hisa. Hilo lingetokea, angekuwa amepoteza kila kitu alichojenga kwa ajili ya familia ya Ngosha.”
Miguu ya Melanie karibu kutoweka. Hii ilikuwa kwa sababu kila kitu ambacho Lisa alisema kilikuwa ukweli.

"Baradhuri wakubwa!" Joel akatetemeka. Asingeujua ukweli kama si Lisa. Kadiri alivyozidi kuwaza juu ya hili, ndivyo alivyozidi kuwaogopa wale watatu. “Ondokeni mbele yangu! Sasa hivi!" Joel aliwatazama kwa chuki na macho yake ya kutoboa.
Kifua cha Damien kilikuwa kikichemka kwa hasira. Lakini, alielewa kuwa hakukuwa na maana ya kuendelea kujifanya wakati huo. Nusu ya sekunde baadaye, aliinua kichwa chake na tabasamu la kejeli usoni mwake. “Huna mamlaka ya kufanya hivyo. Mimi ndiye Mwenyekiti na mbia wa Ngosha Corporation.” “Hiyo ni sawa." Nina aliunganisha silaha na Damien bila woga. “Damien anamiliki 20% ya hisa za Ngosha Corporation. Si wewe pekee mwenye mamlaka hapa.”
“Wewe...Wewe...” Damu ya Joel ilichemka. Hakuwahi kuona watu wasio na haya hapo awali. "Melanie, tuambie maoni yako."
Melanie aligugumia. “Ingawa mimi si binti yako, Mwenyekiti Ngosha ni baba yangu. Kando na hilo, Ngosha Corporation haingepata nafasi ya kushirikiana na Campos Corporation kama usingekuwa mchango wangu. Mpendwa, unaonaje?"

Jerome aliona aibu kabisa, lakini aliachwa bila njia mbadala. “Melanie ni mke wangu. Kampuni la Campos halitasalia ikiwa hatabaki.” Wanahisa wa Kampuni ya Ngosha walifadhaika waliposikia hivyo. Bwana Ngugi ndiye aliyekuwa wa kwanza kusogea mbele. “Mwenyekiti Ngosha, haya ni mambo yako binafsi ya familia yako. Hakuna haja ya kupeperusha nguo zako chafu kwenye maadhimisho ya miaka 30 ya Kampuni.”
“Hiyo ni sawa. Melanie amechangia sana Kampuni katika miaka ya hivi majuzi,” wanahisa wengine waliunga mkono.
Joel alikata tamaa sana. Watu hawa wote walikuwa wakifanya kazi naye tangu mwanzo wa wakati, lakini sasa waliungana na Damien kwa ajili ya manufaa fulani ya kibinafsi.
"Baba, usifadhaike." Lisa alimpiga bega huku akitabasamu kabla hajageuka kuwatazama wanahisa. "Vema, ina maana kwamba nyote mnamuunga mkono Damien na Melanie kama Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Ngosha Corporation?"
Kundi la wanaume likanyamaza. Walikuwa wamepokea manufaa mengi kutoka kwa Damien katika miaka ya hivi majuzi, ambayo

yaliwaweka wote kwenye mashua sawa na zilizotajwa hapo juu.
“Sawa baba. Tutaondoka kama hawataondoka.” Lisa aliunganisha mikono yake na ya Joel.
“Lisa...” Mwisho Joel alionekana kuwa na wasiwasi. Kampuni la Ngosha ndilo pekee alilokuwa amemuachia.
Alinong'ona sikioni mwake, “Baba, kumbuka kwamba Kampuni ya Ngosha imealika wanahabari kutoka karibu kila mchapishaji mkuu nchini Kenya usiku wa leo. Waandishi wa habari siku hizi wako kwenye utiririshaji wa moja kwa moja.
Sura ya mshangao ilitanda usoni mwake alipogundua kuwa kashfa za usiku huo zingekuwa zimemfikia karibu kila mtu nchini. Kiongozi wa Kampuni alikuwa amefungwa kwa karibu na sura na sifa ya kampuni. Wanahisa hawa waliomuunga mkono Damien na wengine wote bila shaka wangetukanwa na umma.
“Hivi karibuni, watakuja kuomba msaada wako,” Lisa alimkumbusha baba yake.
Aliitikia kwa kichwa akijua. “Hakika. Hakuna haja ya kukaa katika eneo hili la kuchukiza pia. Haya, twende mahali pengine tukazungumze.”

Wote wawili waliondoka kwenye jumba la sherehe ndani ya dakika chache. Hakuna aliyetarajia mwenyekiti huyo wa zamani wa Kampuni angekuwa wa kwanza kuiaga sherehe. Kila mtu alibadilisha sura iliyochanganyikiwa. Dakika chache baada ya wawili hao kuondoka, Alvin naye akaondoka. Nina na Melanie walipumua. Walifurahi kwa siri.
Basi vipi ikiwa Joel aliujua ukweli? Asingekuwa na la kufanya hata hivyo. Wasaidizi wake aliowatumainia walikuwa tayari wamefukuzwa kwenye nafasi zao. Damien kimsingi ndiye aliyekuwa msimamizi wa Kampuni hiyo. Mwongozaji wa sherehe alimtazama Damien kwa kuchanganyikiwa. “Um... Mwenyekiti Ngosha, vipi kuhusu sasa...”
Pembe za midomo ya Damien zilibadilika na kuwa tabasamu hafifu. Alikuwa karibu kutoa hotuba wakati mke wa mfanyabiashara mmoja alipopaza sauti, “Hakuna haja ya kuendelea na sherehe. Watu wamechachamaa wanatukana hovyo kwenye mtandao, wakimwita Mwenyekiti wa Ngosha Corporation ni dhaifu, asiye na haya, na mnafiki. Wanahisa wa Kampuni pia hawana maadili. Wamemdanganya Joel Ngosha, kwa zaidi ya miaka ishirini, hata hakuwa na budi ila kuondoka eneo la tukio.”

“Hiyo ni sawa. Majukwaa kadhaa ya media yanatiririsha habari moja kwa moja usiku wa leo. "Jukwaa hili ambalo niko nalo limepata maoni zaidi ya elfu kumi. Ni aibu iliyoje.” Rangi zote zilimtoka kwenye uso wa Damien. Wanahisa na watendaji wa Kampuni hiyo walikagua haraka simu zao. Katika dakika chache, kashfa za Kampuni ya Ngosha zilikuwa zimeenea.
[Habari zinazochipuka!: Mwenyekiti wa Ngosha Corporation alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na shemeji yake. Mtoto wa nje ya ndoa ni chombo cha kuiba mali ya kaka mkubwa.] [Siaminika. Nilitazama mkondo wa moja kwa moja hapo awali. Mtaalamu kama Damien Ngosha hata alipata usaidizi kutoka kwa wakuu wa kampuni. Lazima amewahonga sana. Nafikiri hili linapaswa kuangaliwa.] [Haha, ndege wa manyoya ya aina moja huruka pamoja. Labda hawafikirii kuwa jambo hilo ni tatizo.]
[Siku zote watu husema kwamba watu matajiri sana ni wagonjwa kiakili. Ninaamini hivyo sasa.]
[What's wrong with wale waliobaki nyuma kwenye sherehe?Kuonyesha support yao kwa Damien?]

[La hasha! Inanikera nikitazama bidhaa za Kampuni ya Ngosha. Jiunge nami kuzisusia kuanzia leo]
Sura ya: 315
Wageni wengi hawakuweza kujiletea kubaki baada ya kusoma maoni haya.. “Um... nafikiri ni bora tuondoke.”
“Ah, ghafla nilikumbuka nina mkutano wa kuhudhuria usiku wa leo, itabidi niondoke kwanza.”
Wageni waliondoka mmoja baada ya mwingine. watendaji wa Ngosha Corporation waliona aibu sana hivi kwamba walitamani wangeweza wajizike kwenye shimo moja kwa moja sekunde hiyo.
"Damien, wewe na binti yako ni aibu sana." Wanahisa wote sasa walijutia uchaguzi wao. Waliwafokea watendaji waliokuwa nyuma, “Mbona nyote bado mko hapa? Rudi kwa kampuni kwa mikutano na idara ya PR sasa.” Ukumbi wa sherehe ulikuwa tupu kwa dakika chache.
Mzee Ngosha alimrushia fimbo yake Damien. "Wewe ni aibu kwa familia!" Kisha, akaondoka eneo lile akiwa na Bibi Ngosha.

Akiwa amekasirika, Damien akavunjilia mbali glasi zote zilizokuwa juu ya meza. Nina alishtuka sana hivi kwamba alikimbia haraka kumkumbatia bintiye. “Kwanini Lisa mjinga huyo hakufa pamoja na mama yake miaka hiyo yote iliyopita?”
“Baba... tufanye nini sasa?” Midomo ya Melanie ilitetemeka huku akihoji. Macho yake machozi yalijaa hasira.
Mng'aro uliangaza machoni mwa Jerome huku akitabasamu kwa ujanja na kusema, "Kuna kitu tunaweza kufanya. Je, Lisa hakukiri wazi kuwa yeye ni binti wa haramu wa Joel mapema? Aunty Nina, unaweza kugeuza hili na kusema ni Joel ndiye aliyekulaghai kwanza. Ulitafuta tu msaada kutoka kwa ndugu yake kama kulipiza kisasi.”
“Ndiyo, uko sawa.” Macho ya Melanie yalipepesa. "Sio tu kwamba watu wataacha kututukana, lakini pia watetezi wa haki za wanawake watatuonyesha msaada wao." Damien aliitikia kwa kichwa. “Jerome, hilo ni wazo zuri.”
"Sawa, nitafanya maandalizi mara moja kwa mkutano na waandishi wa habari."
Hata hivyo, mara tu sauti ya Nina ilipopungua, sekretari wa Damien akawakaribia kwa ghafula. “Mwenyekiti Campos, ninaogopa hilo

halitafanya kazi. Lisa alichapisha haya kwenye Facebook yake kama dakika tatu zilizopita. Angalia.”
Akawapa simu yake.
Akaunti ya Facebook ya Lisa ambayo ilikuwa haijatumika kwa miaka mitatu ilikuwa ime’updetiwa. [Halo watu wote, jina langu ni Lisa Jones, binti ya Sheryl Masawe na Joel Ngosha. Kwa bahati mbaya, mimi ni mtoto wa nje. Miaka 28 iliyopita, wazazi wangu walipendana. Lakini kwa sababu ya malezi tofauti ya familia, babu na babi yangu hawakuwaruhusu kuwa pamoja na kumlazimisha kuoana na Nina Mahewa badala yake. Mwaka huo huo, Bw. Ngosha na Bibi Mahewa walilewa na kuwa na mahaba ya usiku mmoja.
Alidai kuwa alikuwa na ujauzito wa mtoto wake na kumlazimisha kubeba jukumu hilo. Mama yangu hakumwambia Bwana Ngosha juu ya uwepo wangu, kwa hivyo Bwana Ngosha, kama mtu anayewajibika, alimuoa Bibi Mahewa. Nililelewa na mama yangu mzazi. Nilichotaka kusema ni kwamba bwana Ngosha asingemuoa Miss Mahewa kama asingemlaghai na mtoto. Cha kufurahisha zaidi, mtoto hata si wa Bwana Ngosha, na

mama yangu alifariki muda mfupi baada ya kunizaa...]
Chapisho lilipata maoni mengi ndani ya dakika chache.
[Nilikuwa karibu kusema kwamba Joel Ngosha hana tofauti na Nina Mahewa. Mmoja wao alikuwa na binti wa haramu, ambapo mwingine alimdanganya mumewe. Kama ilivyotokea, alikuwa mtu wa tatu.]
[Alijilazimisha kuingia katika familia tajiri akiwa na mtoto ambaye hata si mali yake. Ajabu.] [Kinachoshangaza zaidi ni kwamba inaonekana, Joel Ngosha alimpa Nina Mahewa zaidi ya shilingi bilioni 30 walipotalikiana miaka michache iliyopita.]
[Ningekufa kwa hasira kama ningekuwa Joel Ngosha.]
[Sielewi. Nina alilala na Damien kwanza kwanini alisisitiza kuolewa na Joel baadaye? To ruin his life?]
[Sina hakika. Damien ni mlemavu na hana urithi mwingi katika familia. Joel amekuwa Mwenyekiti wa Ngosha Corporation kila wakati. Familia ya Mahewa haikujulikana huko Nairobi kabla ya Nina kuolewa na Joel. Leo, wao ni mojawapo ya familia tajiri zaidi jijini.]
[Nilisikia kwamba Joel alianguka katika hali ya kukosa fahamu baada ya ajali miaka mitatu

iliyopita na nusura apoteze maisha yake. Niliweka dau kwamba Nina na Damien walikuwa nyuma ya hilo pia.]
[Nilitaja miaka mitatu iliyopita kwamba Nina angeweza kuwa mpangaji mkuu lakini hakuna aliyeniamini.]
“Ahh, Lisa you b*tch!” Nina alifoka kwa hasira bila kujali adabu zake.
Jerome alikuwa amebana taya pia. Ilionekana kuwa Lisa alikuwa tayari mbele ya wakati wao na alikuwa anatarajia hii kutokea.
Kusema kweli, Jerome asingemwoa Melanie ikiwa angejua kuwa ni binti ya Damien. Alikuwa amefikiria kuchukua polepole Ngosha Corporation baada ya kupandishwa cheo. Kurudi kwa Lisa bila kutarajiwa kulivuruga mpango wake.
•••
Sauti za nyayo zilisikika katika eneo kubwa la maegesho. Lisa alichukua ufunguo wa gari lake ili kufungua gari jeupe lililokuwa mbele yake.
"Lisa Jones." Sauti nzito ya Alvin isiyojali ilisikika nyuma yake.
Joel aligeuka mara moja na kujiweka mbele ya Lisa. "Alvin, tafadhali kaa mbali na binti

yangu." Alvin aliendelea kumsogelea kana kwamba hamsikii mtu huyo.
Alikuwa ameshangazwa na utulivu wake katika jumba la karamu hapo awali alipokuwa akishughulika na watu matajiri na wenye nguvu nchini humo. Ilikuwa dhahiri kwamba alikuwa amepanga hili kwa uangalifu. Alikuwa amefaulu kufichua rangi halisi za Damien, Nina, na Melanie mbele ya watu mashuhuri zaidi wa Kenya.
Labda wale watu wenye akili za polepole walikuwa bado hawajatambua kwamba wanahabari waliokuwepo usiku huo wangetiririsha hafla nzima kwa wakati halisi. Yeyote aliyejali sifa yake bila shaka angejiweka mbali na watatu hao mara tu walipofikia utambuzi huo. Kuwa na uhusiano mzuri ilikuwa muhimu zaidi kuliko kitu chochote kwa mfanyabiashara.
Lakini, Lisa alikuwa ameharibu yote hayo kwa watatu wale bila juhudi kubwa. Hilo bila shaka lilivutia. Alvin alimkumbuka tu kama mwanamke msumbufu na mkali kutoka miaka mitatu iliyopita. Siku hiyo, alikuwa amerudi mrembo na mwenye nguvu zaidi kuliko hapo awali, kana kwamba alikuwa mtu tofauti kabisa.

Ilionekana kuwa alikuwa akiishi vizuri katika miaka ya hivi majuzi. Kwa upande mwingine, alikuwa amedanganywa naye miaka hii yote kama mpumbavu. Hata alihisi hatia kwa yale yaliyompata. Hakuwa amelala vizuri katika kipindi cha usiku elfu moja au zaidi kwa sababu yake.
“Ulinidanganya. Hujafa.” Macho meusi ya Alvin yalijaa hasira ndani ya sekunde chache.
Kana kwamba alishindwa kujizuia, Joel alinyoosha mkono kumshika lakini alizuiwa mara moja. “Mjomba Joel, sogea.” Alvin alionya kwa ukali.
Akiwa na hasira, Joel alikuwa karibu kujibu wakati Lisa alipomvuta pembeni kwa upole. Alimtazama Alvin usoni mwake bila huruma. “Uko sahihi. Nilikudanganya.”
"Vizuri sana. Nani pia alikuwa ndani yake? Pamela? Au watu wa hospitali?" Alvin alijiona mjinga kadri alivyozidi kuwaza jinsi alivyomdanganya kwa miaka mitatu iliyopita. Aliinamisha kichwa chake kabla ya kugeuza midomo yake kwa tabasamu. "Mwenyekiti Kimaro, kama sikuwa nimejifanya kuwa nimekufa wakati huo, ninaogopa ningechomwa na kuwa majivu."
"Unamaanisha nini?" Licha ya tabasamu la kupendeza lililoning'inia usoni mwake, kejeli

iliyofichwa chini ilijaza macho yake yaliyojifinya.
TUKUTANE KURASA 316-320
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini ba
 
LISA KITABU CHA SABA
SIMULIZI........................LISA KURASA......316 MPAKA 320
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY WHATSAPP: +255628924768

Sura ya 316
“Hakika unajua ninachomaanisha.” Lisa alitabasamu kabla ya kutoa miwani kwenye mkoba wake na kuivaa. Mara moja alionekana mrembo zaidi na jasiri. "Nilikuwa mtu wa kawaida tu lakini ulinitupa katika hospitali ya magonjwa ya akili. Kila siku nilidungwa sindano kwa nguvu na kulishwa dawa za wagonjwa wa kichaa. Kabla ya hapo ulifungia ndani ya nyumba, niliishi maisha ya kubanwa zaidi kuliko mfungwa gerezani. Ninyi nyote mngenitia wazimu wa kweli muda si mrefu.” Uvimbe ukatokea kwenye koo la Alvin huku akiongea kwa sauti ya kizaazaa, “Hukuwa sawa kiakili wakati huo...”
“Unajua tofauti kati ya kichaa na matatizo ya akili yanayoletelezwa na hasira kali?” Lisa aliuliza. "Nilikuwa mjamzito na wewe ukanifungia ndani peke yangu huku wewe ukitanua na mpenzi wako bora wa muda wote. Baabaye ukanisukuma kwa mikono yako na kunisababisha kupoteza watoto wangu. Hiyo haikutosha, wewe na mpenzi wako mkanipakazia ugonjwa wa kichaa na kunilazimisha fungiwa ndani ya wodi kama mgongwa wa kichaa. Lakini wewe ulikuwa na mpenzi wako wa muda wote Sarah mbele na

nje ya macho yangu kila siku. Ningewezaje kukosa kuwa na mfadhaiko wa hasira kali? Ningewezaje kuwa mtulivu na mwenye adabu na wewe wakati huo?"
“Alvin, ungewezaje kumtendea hivyo binti yangu?” Joel aliumia moyoni aliposikia hivyo. Alipotoka kwenye hali ya kukosa fahamu, pia alifikiri kwamba Lisa alikuwa na tatizo la akili. Hakujua yote ni kwa sababu ya Alvin. “Wewe nyoka!” Joel alishindwa kushikilia tena akajaribu kumpiga ngumi ya uso.
Alvin alizuia ngumi ya mwanaume huyo bila juhudi na hata kuirudisha nyuma kwa nguvu. “Achana naye baba.” Macho mazuri ya Lisa yakawa makali mara moja. "Ulinitishia na baba yangu mara nyingi sana miaka mitatu iliyopita na sasa unajaribu hila ile ile ya zamani?" Mkono wa Alvin ukaganda mara moja. Akaminya midomo yake myembamba kabla ya kulegeza kamba taratibu kwa Joel. Sura ya mshangao iliosha juu ya uso wake. “Nilikutishaje?”
Alvin alibaki kimya. Lisa aliinua kichwa kumtazama huku akitabasamu. “Bwana Kimaro, mbona unajifanya? Je, hukujiamini kabisa katika kunitisha wakati huo?”
Kuliona tabasamu lake la kupendeza kulimfadhaisha. Alikumbuka aliwahi kumchukia

kwa kufanya hivyo. Lakini, sasa angeweza kuzungumza juu ya siku za nyuma bila kujali na tabasamu la dhihaka.
"Kila mtu alifanya makosa wakati huo. Marafiki zako pia hawakuwa na hatia.” Hatimaye alijibu kwa sauti nzito.
"Ndio, kaka mkubwa wa mpenzi wako ndiye mtu pekee asiye na hatia." Lisa aligeuka na kutabasamu mbele ya Joel. “Baba, waandishi walimkamata akinisaliti na Sarah wakati yuko kwenye ndoa na mimi. Hakuwa tayari kukiri makosa yake kwa mwanamke huyo licha ya kwamba kila mtu alikuwa akimtukana hivyo akanilazimisha niuambie umma kuwa mimi na yeye tayari tumetalikiana. Vinginevyo, angemkataza Dk. Angelo kukutibu. Mwishowe, kaka mkubwa wa Sarah alivamia ndani ya nyumba ya rafiki yangu na kutaka kumbaka bila huruma. Rafiki yangu mmoja alidungwa kisu na mwingine karibu kubakwa. Baada ya hapo akatishia kumwondoa Dokta Anjelo asikutibu tena ili kunishinikiza niachane na habari za kumfikisha mahakamani kaka wa mpenzi wake.”
Joel aliogopa kusikia hivyo. Binti yake aliteseka kiasi gani kwa ajili yake? Alijiona kama mtu aliyeshindwa kabisa kumlinda kadiri alivyofikiria zaidi juu ya hili. Macho yake

yalikuwa yamejaa hasira. Alijichukia kwa kuwa mzee na dhaifu sana kupigana na mtu huyo.“Alvin, wewe mnyama! Hapana, wewe ni mbaya kuliko mnyama!”
Alvin alikunja uso. Ni lini aliahidi kumtunza vizuri Lisa, hata hivyo? Hata hivyo, aliona aibu alipofikiria kuhusu siku za nyuma. Hii ndiyo sababu hakuweza kumsahau Lisa miaka yote hii. Ilikuwa nje ya hatia. “Baba, sahau. Yote ni ya zamani.”
Lisa alimsukuma kidogo Joel kuelekea kwenye gari huku akitabasamu kwa unyonge. “Twende. Hakuna sababu ya kupoteza pumzi zetu na mtu kama yeye.
“Lisa, usijali. Nitalipiza kisasi kwa ajili yako,” Joel alisema kwa hasira.
Alvin alikunja uso wake huku Lisa akicheka kabla ya kumwambia baba yake, “Achana na visasi baba. Sitaki afikirie kuwa nina wazimu na kunitega tena katika hospitali ya magonjwa ya akili. Pengine itakuwa vizuri zaidi kama tutakaa mbali naye katika siku zijazo.” Kisha, akazunguka na kuingia kwenye kiti cha dereva. Alvin alikuwa bado amesimama mbele ya gari. Lisa alitoa kichwa chake nje ya dirisha. "Mwenyekiti Kimaro, hutaki kupisha njia?"
Alvin akasimama tu akimtazama kama

sanamu. Miwani ya jua ya mwanamke ilikaa kwa uzuri kwenye pua yake nzuri. Akageuza macho yake kuelekea chini kuitazama midomo yake yenye majivuno lakini tete. Ilikuwa ni kama mwanamke huyu alikuwa amebadilika kabisa. Alihisi kutomfahamu lakini hakuweza kujizuia kuondoa macho yake. Alvin hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, kwani hakuwa mtu wa kuvutiwa kirahisi na urembo wa wanawake. Sekunde chache baadaye, hatimaye alipisha kando.
Gari jeupe la Lisa lilimpita kwa kasi. Hans akamshatua kwenye safari yake ya mawazo. "Bwana Mkubwa, ni wakati wa kwenda." "Angalia jinsi alivyodanganya kifo chake na kuondoka nchini. Nataka kujua ni nani aliyemsaidia.” Alvin aligeuka na kumwangalia msaidizi wake ghafla. Hans alitetemeka kwa mbali na haraka akaitikia kwa kichwa.
Alvin alisoma post ya Lisa kwenye Facebook baada ya kuingia kwenye gari. Alvin alitabasamu bila kupenda. Aliduwaa baada ya kugundua kilichokuwa kikiendelea.
Jamani! Alipaswa kukasirishwa kwa kudanganywa naye miaka mitatu iliyopita lakini alikuwa akitabasamu? "Hans, unafikiri hakuwa mgonjwa wakati huo?"
“Um... sina uhakika,” Hans alijibu kwa

kusitasita, “Lakini Bi Njau ni mtaalamu. Pengine... asingetudanganya?” Alinyamaza kwa muda mfupi mwishoni na kuonekana mwenye wasiwasi.
Alvin alishikwa na butwaa. Ndiyo, alikuwa amemwamini Sarah aliposema kwamba Lisa alikuwa mgonjwa wa akili miaka mitatu iliyopita. Hata hivyo, vipi ikiwa alikuwa akisema uwongo?
Alisugua kichwa chake kwa upole. Hapana, Sara asingemdanganya.
Sarah alimpigia simu wakati akiwaza hayo. "Alvinic, unakuja nyumbani?"
"Ndio, niko njiani."
Sarah alinyamaza kwa muda mfupi kabla ya kuongea tena. "Niliona habari kwamba Lisa amerudi. Inaonekana...”
“Ndio.” Alijibu haraka haraka na picha za urembo wa Lisa zikapita akilini mwake. "Alvinic, mimi ..." Sarah alicheka vibaya. “Naona amekuwa mrembo kuliko mimi na inanitia wasiwasi. Naogopa utarudiana naye.” “Usifikirie kupita kiasi. Sikuwa hata na mpango naye kabisa hapo awali. Niko nyumbani." Akakata simu na kujisemea kuacha kumfikiria Lisa.
Aliporudi kwenye jumba la kifahari la baharini usiku huo, Sarah alitoka nje kumlaki akiwa

amevalia gauni jekundu la kulalia lenye kuvutia. Ghafla, Alvin alikumbushwa jinsi Lisa alivyokuwa amevaa nguo yake nyekundu siku hiyo.
"Kuna nini? Sionekani vizuri?” Sarah aliona kuwa amevurugwa na kumtikisa begani huku akipiga kelele.
“Nitakwenda kuoga." Alvin akaelekea kwenye ngazi.
Sarah aliuma mdomo. Alvin alipotoka kuoga baadaye, alienda mbele kumkumbatia kwa nyuma na kusema kwa sauti ya kutongoza, “Alvinic, hebu... tujaribu tena usiku wa leo.” Alvin alisimama pale, bila kutikisika. Dakika chache baadaye, Alvin alimsukuma Sarah mbali kwa upole. "Nitaenda kwenye maktaba." "Alvinic, kwa nini? Tutapataje watoto namna hii?" Sarah aliuliza kwa wasiwasi, “Au unachukizwa na mimi kwa sababu ya kile kilichonitokea nilipotekwa na magaidi...” “Hapana, sivyo. Mimi ndiye mwenye tatizo.” Sura ya kuchanganyikiwa ilimwangazia usoni mwake. Hakujua ni nini kilikuwa kibaya. Katika muda wa miaka mitatu iliyopita, alijua wazi kwamba anampenda Sara lakini alikuwa akifeli kila alipokuwa akijumuika naye kwenye tendo la faragha!

Sura ya: 317
Wakati fulani, hata alifikiri kwamba alikuwa na aina fulani ya ugonjwa ambao ulimzuia kuwa karibu na wanawake. Sarah alikuwa amejaribu kutibu tatizo hili kupitia vipindi vyake kadhaa vya matibabu ya kisaikolojia lakini havikufaulu. Uso wa Sarah ulikuwa umesinyaa kwa karaha na kuchanganyikiwa. “Kwanini...kwanini usiende kupata uchunguzi wa madaktari? Kwa kweli siwezi kuvumilia tena. Nakutaka...” Alivua gauni lake na kujitupa kwa hasira. Katika sekunde hiyo ya mgawanyiko, Alvin alimsukuma mbali mara moja bila kupenda. Mwanamke ambaye hakutarajia hilo alianguka chini. Alianza kulia kwa sauti ya juu.
Alvin alimwonea huruma alipomfikiria juu ya unyonge wake. "Samahani." Akavua koti lake na kumfunga. Akambeba mpaka kitandani na hatimaye akatoka chumbani.
Alipotoka tu chumbani, Sarah alipiga ngumi kitandani kwa hasira. Hakutarajia kwamba hata baada ya kutumia mbinu chafu za kisaikolojia kumlawiti mwanamume huyo ili apendane naye miaka mitatu iliyopita, bado alishindwa kufaulu kwenye mbinu za mahaba. Wakati fulani, hata alijisikia kuumwa wakati alijaribu

kujilazimisha juu yake.
Ilikuwa ni miaka mitatu na nusu. Alikuwa karibu kupoteza akili yake kuishi maisha haya ya kuvumilia. Wakati mwingine, alitamani sana kuburudika na kuachilia hisia zake zilizozikwa ndani yake kabisa na mwanamume mwingine. Ghafla, namba isiyojulikana ilikuwa ikimpigia. Alipuuza mara moja.
Ndani ya sekunde chache, nambari hiyohiyo ilimtumia picha. Sarah alikuwa amevalia bikini kwenye picha hiyo na ameketi juu ya mwanamume wa makamo. Mwanamume huyo alikuwa na ndevu nyingi zilizochafuka huku mwili na mikono yake ikiwa imechorwa tattoo. Alikuwa akitabasamu kwa utamu huku akikaa kwenye tumbo lake kubwa.
Mshtuko ulimpitia. Hii ilikuwa ndoto yake kubwa iliyomtesa zaidi. Alijibu simu ilipoita tena. Sauti potovu ya mtu ilisikika kutoka kwenye simu. “Hehe, Sarah, sikufikiri kwamba ungeolewa na tajiri mkubwa zaidi wa Kenya baada ya kukukusaidia kutoroka kwenye kambi ya Al-Shabaab. Unafikiri Alvin Kimaro angefanya nini akigundua kuwa tulikubaka na kukulawiti siku za nyuma?”
Rangi zote zilimtoka usoni. "Hisan, uko hai?" “Haha, bila shaka, niko hai. La sivyo, hakuna mtu katika ulimwengu huu atakayejua jinsi

ulivyokuwa mwanamke wa bei nafuu,” alisema kwa kuuma meno, “Wewe ni mkatili sana. Uliniahidi kwamba nikusaidie kutorokea Ulaya ukatafute maisha, na baadaye tungeanzisha familia. Kwanini ulinidanganya?”
“Sijui unazungumzia nini,” alijibu huku akijitahidi kadiri awezavyo kuficha woga wake. “Hukumbuki?” Mtu huyo alicheka vibaya. “Sawa, nadhani sina chaguo ila kuzungumza na Alvin basi. Nitamjulisha jinsi bila aibu ulivyochagua kutufurahisha sisi watatu tulipokuteka siku za nyuma. Tulikupa chaguo, kufa au ukubali kufanya mapenzi na sisi wote watatu kwa wakati mmoja na ukachagua kufanya mapenzi. Unakumbuka?...Sitasahau tukio hilo. Nina picha za kumwaga. Nimtumie ili ajue mpenzi wake ni mwanamke gani?” "Nyamaza! Unataka nini?" Sarah hakuthubutu kufikiria hilo.
"Si mengi. Nahitaji pesa tu...”
“Ngapi?” Sarah alikosa uvumilivu.
"Hmm, vipi kuhusu dola milioni 1?" Hisan alicheka. “Mbali na hilo, nimeboreka sana hapa Mombasa tangu nifike hivi majuzi. Nahitaji uje nikumbushie enzi zetu kidogo.”
Sarah alikuwa akitetemeka wakati huo. "Acha. Usiniharibie. Mimi sasa ni mke wa mtu...” “Haha, si kama mimi nitaondoka nacho. Sawa,

Sarah, acha kujifanya. Najua ulivyo mjanja kuliko mtu mwingine yeyote.” Akacheka vibaya tena. “Njoo huku nakuahidi kukufurahisha. Usithubutu kufanya ujanja na mimi. Picha zitaangukia mikononi mwa Alvin endapo utajaribu kufanya ujanja wowote.”
"Basi usifanye hivyo, nakuja." Akiachwa bila njia mbadala, Sarah alifumba macho na kukubali. Kamwe katika miaka milioni hakuweza kutarajia kwamba Hisan alikuwa bado hai. Alifikiri hakuna mtu ambaye angewahi kujua kuhusu maisha yake ya nyuma.
“Nitakungoja."
Baada ya kumaliza kuongea na simu, Sarah alivaa na kushuka ngazi. Alvin alikuwa amesimama mbele ya madirisha ya maktaba akiwa na tafakari zake. Vidole vyake vyembamba vilikuwa vimezungushwa kwenye glasi ya divai nyekundu. Dirisha lilionyesha wazi uso wake mzuri. Mwanaume mwenye sura nzuri angemfanya mwanamke yeyote kutaka kumfanyia mambo ya kitandani usiku kama huo. Hali ya kuchanganyikiwa ikaangaza usoni mwa Sarah. Alvin alikuwa mwanaume mzuri kuliko wote ambao aliwahi kuwaona na bado alikuwa na matatizo katika idara hiyo.

“Unaenda nje?” Alvin akautazama mkoba wake.
"Ndio, nitakutana na marafiki zangu. Nachoka na hali hii.” Aliweka nywele zake nyuma ya sikio ili kudhihirisha uso wake wenye huzuni. Uso wake ulikuwa umeoshwa na aibu. “Samahani. Ninaahidi... nitamuona daktari.” “Um... hakika.” Alikuwa na shughuli nyingi sana akifikiria kushughulika na Hisan hivi kwamba aligugumia tu jibu na kuondoka haraka kwenye jumba hilo.
Kimya cha pin-tone kilianguka kwenye chumba. Alvin aliinamisha kichwa chini na kuumaliza ule mvinyo kwa mkupuo. Paka mnene alikuja karibu na miguu yake na kuanza kulia. Akainama kumpapasa Charlie kichwani. "Nifanye nini ikiwa nitaendelea kushindwa?" alijiuliza kimya kimya.
•••
Jumba la familia ya Ngosha.
Simu ya Lisa iliita na kwenda bustanini kabla ya kujibu. Sauti ya mtu mwingine ilisikika kutoka kwa simu. “Bibi, Sarah Njau alienda kwenye nyumba ya kibinafsi aliyoinunua kwa siri chini ya jina lake. Hisan yupo pia. Kamera za uchunguzi tulizopitia juhudi zote za kusakinisha huenda hazitakuwa na manufaa kwa sasa.”

Lisa alihisi kukata tamaa baada ya kusikia hivyo. “Nilifikiri angekutana na Hisan hotelini. Inaonekana yuko makini kuliko nilivyofikiria.” “Ni sawa. Hawataishia mara moja tu, lazima wataendelea. Cha muhimu ni kwamba kaingia mtegoni.”
“Uko sahihi. Endelea kuwaangalia kwa karibu. Nijulishe akiondoka.”
“Sawa.” Baada ya kuiweka simu, Joel alionekana kuwa na wasiwasi.
"Lisa, wenye hisa wengi wa Ngosha Corporation walinipigia simu mapema. Wanataka nirudi kwenye nafasi yangu kesho. Inaonekana wamekubali kumfukuza kwa muda Damien na Melanie kwenye nyadhifa zao.” "Kwa muda? Wanataka wakutumie kurekebisha hali hiyo kisha wakuteme tena.” Lisa alikuwa na wasiwasi. “Baba, ni bora kusubiri bei ya hisa ya Ngosha Corporation ishuke zaidi."
“Hakika,” alikubali bila kusita.
“Baba, umenielewa lakini?” Lisa aliuliza huku akitabasamu. “Tunazungumza kuhusu mabilioni ya dola hapa.”
“Haijalishi. Furaha yako ndio kipaumbele changu kikuu." Alipomaliza kusema hivyo, alijikongoja kurudi nyuma kidogo.
Lisa akamshika mara moja. “Baba, kuna nini?”

“Pumzi, pengine ni uzee tu. Ninaendelea kupata shida ya kupumua tangu hivi majuzi. Nadhani ajali hiyo imeathiri sana afya yangu. Ninaanza kuhema kwa nguvu baada ya kutembea hatua chache tu.” Alitabasamu kwa uchungu. “Ndiyo maana nilitaka kumkabidhi Melanie Kampuni hilo mapema lakini ni aibu iliyoje...”
Lisa alikunja uso. “Baba nitakupeleka hospitalini kwa uchunguzi kesho.” “Hakuna haja ya hilo. Ninafanya hivyo kila mwaka.”
"Lazima unisikilize la sivyo sitakuwa na raha." Lisa alikuwa amedhamiria.
Machozi yalianza kumtoka huku akimtazama. “Lisa, nina deni kubwa sana kwako na mama yako. Sina maana kabisa!”
"Baba, kusema kweli, mimi huchukia wakati mwingine lakini oh, mimi bado ni binti yako mwisho wa siku."
Joel alikuwa akijipiga teke. Licha ya kufanya kazi katika tasnia ya biashara kwa miaka mingi, bado aliishia kubweka kwa mti mbaya. Alihisi haja ya kurekebisha kwa Lisa katika siku zijazo. Ni lazima asimwache ateseke.
Sura ya: 318

•••Siku inayofuata•••
Lisa alimpeleka Joel katika hospitali mpya iliyofunguliwa lakini yenye sifa nzuri huko Nairobi kwa uchunguzi wa kimatibabu. Matokeo ya uchunguzi yalitoka asubuhi hiyohiyo.
Daktari alikunja uso baada ya kuitazama ripoti hiyo. "Bwana. Ngosha, kuna sumu kwenye damu yako."
"Nini?" Joel alishtuka sana, “Lakini uchunguzi nilioufanya miezi mitatu iliyopita ulionyesha kuwa nilikuwa sawa.”
Daktari akatikisa kichwa “Ni sumu ya muda mrefu, ambayo ilianza kutokea angalau miaka miwili iliyopita. Je, unapata kikohozi, maumivu ya kichwa na kifua kubana kila mara?” “Ndiyo.” Joel aliitikia kwa kichwa haraka, "Nilienda kumuona daktari mapema. Baada ya kunifanyia uchunguzi wa mwili, daktari alidai kuwa inaweza kuwa ni kutokana na madhara ya ajali na umri wangu..."
"Sijui kwanini daktari ambaye alikutibu hapo awali alisema hivyo. Naam, unaweza kutofautisha kwa uwazi kutokana na matokeo sasa. Kama usingefahamishwa mapema, afya yako ingedhoofika ndani ya mwaka mmoja. Huenda ungeeanguka au kupata mshtuko wa

moyo na kupoteza maisha." Daktari alimtazama Joeli kwa huruma huku akiongea. Watu walisema jamii ya watu matajiri na waliofanikiwa imejaa shida na matatizo kwa ndani. Sasa daktari aliposhuhudia mwenyewe aligundua kuwa kauli ile ilikuwa sahihi. Joel alizama katika hali ya kukata tamaa.
“Dokta inawezekana kuondoa sumu katika mwili wa baba yangu?" Lisa aliuliza.
Daktari akamjibu, “Inawezekana, lakini hatakuwa sawa kama hapo awali, nashauri afanyiwe matibabu haraka iwezekanavyo.” "Asante."
Baada ya kutoa shukrani zake kwa daktari, Lisa alimshika Joel na kutoka naye nje huku akiwa ameduwaa. Huku akimtazama Joel alivyokuwa amechanganyikiwa alisema kwa unyonge, “Kuhusu sumu ni lazima kuna mtu karibu yako amekuwa akikuchomekea kwenye chakula. aidha yuko katika kampuni au kwenye nyumba yako. Nina uhakika daktari uliyemwona kabla ya hii pia alikuwa amehongwa, ndiyo maana alidai kuwa hauna tatizo."
“Ni Melanie ndiye aliyenipeleka huko kila mara,” Joel alisema kwa huzuni huku akionyesha dhihaka, “Sikutarajia jambo hilo kutokea hata katika ndoto tu.” Kwa kweli,

nilitumia zaidi ya miaka 20 kumlea, na kumpa kilicho bora zaidi. Hata sikuwahi kufikiri kwamba Damien ndiye baba yake mzazi. Kuhusu Nina, nilimpa dola milioni chache baada ya kuachana naye. Nina na Melanie wanatisha sana. Tukio hili bila shaka linahusiana nao."
Lisa alishika midomo yake, alikuwa sahihi, kwa bahati nzuri alikuwa amerudi, kama angechelewa kurdi baadaye Joel angekuwa tayari ameshapoteza maisha,
“Nahitaji kutoa taarifa polisi,” Joel alisema kwa hasira.
“Baba acha. Kama utafanya hivyo, Nina na Melanie hakika watampachika mtu ambaye amekuwa akinyunyiza sumu chakula chako. Kwa kuwa walikuwa na ujasiri wa kufanya kitendo kama hicho, nina hakika wamekuja na mpango wa kujinasua."
Lisa alikodoa macho kabla ya kuendelea, “Unatakiwa mwili wako utolewe sumu kwa siri huku ukijifanya hujui lolote kuhusu hilo, weka macho kwa yaya na watumishi katika jumba lako na sekretari wako ili kujua ni nani amekuwa akichoma chakula chako. Kisha, unaweza kumshika mtu huyo na kuwafanya Nina na Melanie waungame.”
Hatimaye Joel alielewa na kumtazama binti

yake kwa kumshangaa. “Lisa, una akili zaidi kuliko mimi.”
"Baba, wewe ni mkarimu sana na unaamini watu kwa urahisi sana." Uso mzima wa Lisa uliwasilisha hali ya huzuni. Baada ya kupitia misukosuko mingi, alielewa kanuni kwamba kuwa mkarimu kwa maadui zake kungemaanisha kujifanyia ukatili yeye mwenyewe.
“Umesema kweli. Joel alishusha pumzi na kutikisa kichwa kwa huruma. Kama asingekuwa mwema sana, asingemwoa Nina na hivyo kumuumiza sana Sheryl wakati ule. Mawazo ya Sheryl yalimfanya ashushe pumzi kwa maumivu. Akatabasamu kwa uchungu. Joel aliingia kwenye kitengo kingine kwa ajili ya kuanza matibabu ya kuondolewa sumu, na Lisa ilibidi ashughulikie malipo ya matibabu yake. Baada ya kuachana na Joel, Lisa alipokea simu nyingine.
“Sarah ameondoka nyumbani kwa Alvin asubuhi hii tena.” Lisa alitazama saa iliyosomeka saa tano asubuhi “Unahisi anaweza kuwa anelekea kwa Hisan, huh?”
“Ndiyo.” Mtu wa upande mwingine alicheka na kusema, "Sijui kama Alvin anaweza kumridhisha."

Lisa alipotaka kujibu mara ghafla lifti ilisimama kwenye ghorofa ya tatu. Alvin ambaye alikuwa amejengeka kwa nguvu alionekana akiwa na Hans wakitokea kwenye jengo la huduma za matatizo ya kiume. Alikuwa akitoa hisia zisizopingika za utu uzima wa kiume. Watatu hao walipotazamana, Alvin aliganda. Lisa uligeuka kuwa wa ajabu baada ya kutazama ubao ulio nyuma yake uliosomeka 'kitengo cha andrology'.”
"Pengine hawezi kumridhisha. Nina jambo la kushughulika nalo sasa. Bye." Lisa alimalizia maneno yake na kubonyeza kitufe cha kukata simu.
Mara tu Alvin aliposikia neno 'kumridhisha', uso wa Alvin ulibadilika kwa huzuni. “Unamtumbulia macho nani? Nimekuja hapa tu kumsindikiza Hans!”
Alipoona amegeuzwa mbuzi wa kafara, Hans hakusema lolote. Alihisi kumwaga machozi. Hakujali kufanywa mbuzi wa kafara kwa mambo mengine, lakini hili? Asingeweza kukubali. Ni jambo la kudhalilisha sana.
Mara Hans alipokea ishara ya jicho kutoka kwa Alvin. Hakuwa na jinsi zaidi ya kutikisa kichwa. kwa kusitasita huku akikuna kichwa kwa aibu, “aaah! Ni kweli, nina tatizo la kuwahi kufika kileleni. Nashindwa kumridhisha mama

watoto...”
“Ni ajabu basi!” Lisa akashangaa. “Inakuaje bosi amsindikize msaidizi wake kwa daktari kwa jambo kama hili? Hahaa! Nina suluhisho kwa jambo hili Hans!”
“Suluhisho gani? Kwani wewe ni daktari?" Alvin alijawa na msisitizo na dharau. “Naongea na Hans, siyo wewe. Hans mwaya tumia vumbi la kongo!" Lisa aliinua kichwa chake kwa tabasamu. Hans hakuweza kujizuia ila kucheka.
Alvin alimtazama kwa huzuni na mara Hans akasema kwa uchungu, "Nimejaribu, lakini haikufanya kazi."
“Oh kweli?” Lisa alimkazia macho Alvin. “Basi fanya mazoezi ya kegel. Labda misuli ya mashine haikazi...”
"Mbona unanitazama mimi, si kasema haijawahi kumsaidia?" Alvin alitamani angemfukuza kutoka kwenye lifti.
“Hans pole, ungekuwa mpenzi wangu ningekusaidia. Kuna staili nyingisana za kumasidiamwanamume mwenye tatizo hilo. Ni jambo dogo sana." Tabasamu la kupendeza likaonekana kwenye kona za macho ya Lisa. Alvin alivutiwa na sura yake. Uso wake uliokuwa na makovu ulipita akilini mwake bila kujua. Ikabidi akubali kwamba mwanamume

yeyote angevutiwa na uzuri wake sasa. Kama angetabasamu kama muda huo hapo awali, huenda asingemchukia kabisa.
Muda mfupi baadaye, Lisa aliongeza, "Hans, unahitaji kuponya huu ugonjwa haraka iwezekanavyo. Vinginevyo, mpenzi wako atalazimika kutafuta mtu mwingine ili kukidhi matamanio yake." Akiwa anaongea hayo alicheka huku macho yake yakiwa yamemtazama Alvin.
“Unadhani wanawake wote hawajiheshimu kama wewe?” Alvin alikasirishwa na macho yake, alishindwa kuzuia hisia zake.
“Kwa hiyo mimi sijiheshimu?” Lisa alijinyooshea kidole na kucheka. “Sawa. Siwezi kuwa na faida yoyote kwa kubishana na wewe!” Aliamua kuachana na maongezi hayo mara moja. Hivi ndivyo Alvin alivyokuwa akimuona kama mtu asiyejiheshimu wakati yeye ndiye aliyemsaliti.
Lifti ilipofika, Lisa alitoka moja kwa moja. Baada ya kumtazama akitembea kwa mbali, Alvin aligeuka na kumwambia Hans kwa sura ya huzuni, “Kati ya hospitali nyingi sana za Nairobi, kwa nini ulinileta hapa?”
Hans alijihisi mnyonge. "Nilikuleta hapa kwa sababu ulikataa kwenda kwenye hospitali ya Dokta Choka. Hospitali hii ilifunguliwa hivi

majuzi na daktari wa andrology hapa ni maarufu sana nchini Kenya."
"Toka." Alvin alimuangalia Hans kwa ukali kabla hajatoka kwenye lifti. Hakukuwa na kitu cha aibu zaidi ya kukutana na mke wake wa zamani alipotembelea kitengo cha andrology, ama magonjwa ya kiume. Damn it!
Sura ya 319
Lisa aliendesha gari hadi makao makuu ya Mawenzi Investments mara baada ya kutoka hospitali. Makao makuu sasa yalikuwa yamehamia Nairobi kutokea Dar es Salaam. Baada ya miaka mitatu, Sura zinazofahamika kwenye dawati la mbele zilikuwa tayari zimebadilishwa na sura mpya.
Lisa alipoingia tu, mhudumu wa mapokezi akamzuia. "Wewe ni nani? Umeshapanga miadi?"
"Hapana." Lisa akavua miwani yake ya jua, akidhihirisha uso wake mzuri sana. "Lakini ningependa kukutana na Mwenyekiti wako." Mhudumu wa mapokezi alipigwa na butwaa kwa muda kabla ya kudhihaki.“Wewe ni nani kukutana na Mwenyekiti wetu bila kufanya miadi mapema? Je, unafikiri kwamba Mwenyekiti wetu atakutana na mtu yeyote

ambaye amevaa vizuri? Wewe si mtu mashuhuri kama Cindy Tambwe. ”
"Cindy Tambwe?" Lisa aliinua uso wake, "Cindy ndiye balozi mpya wa kampuni yetu. Toka nje," mhudumu wa mapokezi alijibu kwa hasira.
Tabasamu la Lisa likawa gumu kidogo. "Kwa hiyo Mwenyekiti wako ni nani sasa?"
"Unataka kukutana na Mwenyekiti wetu lakini hata humjui yeye ni nani? Naam, Mwenyekiti wetu ni Sarah Langa Njau. Miss Njau ni mchumba wa Alvin Kimaro ambaye anaongoza KIM International."
Maneno ya mhudumu wa mapokezi yalifanya macho ya Lisa yawe na huzuni. Huku hali ya mamlaka isiyoonekana ikimtoka, mhudumu wa mapokezi aliingiwa na hofu.
Wakati huo, mtu aliyekuwa nyuma yake akapiga kelele. "Mwenyekiti J-Jones?"
Lisa aligeuka na kumkazia macho yule mwanamume aliyekuwa nyuma yake ambaye alionekana kana kwamba alikuwa na umri wa miaka 40. Alionekana kudorora kwa uso dhaifu kidogo. Mwanamume huyo hapo awali alikuwa meneja wa Mawenzi huko Nairobi. Macho ya kupendeza ya Lisa yalimtoka, na akatabasamu kwa mshangao.
“Ni wewe, Mwenyekiti Jones! Habari ambazo

watu wamekuwa wakieneza mtandaoni kuhusu wewe ni za kweli? Bado uko hai?" Meneja wa zamani alimtazama kwa msisimko, macho yake yakiwa mekundu,
“Ndio, bado niko hai.” Lisa aliitazama ile tagi iliyokuwa mbele ya kifua chake na kukunja uso. Sasa alikuwa ni mesenja tu wa kusafirisha mafaili kutoka ofisi moja moja hadi nyingine. Mwanamume yule aliyeitwa Amba alijibu kwa huzuni, "Mwenyekiti Jones, labda hujui kwamba ulipotangazwa kuwa umekufa miaka mitatu iliyopita, umiliki wa kampuni ulihamishiwa kwa Mumeo, Alvin Kimaro. Baada ya yote, Bwana Kimaro alikuwa mume wako halali. Bila kusema, wanahisa wote isipokuwa Chris Maganga walimuunga mkono Bwana Kimaro. Kwa kweli, Mawenzi Investments imekuwa ikifanya vizuri sana chini ya uongozi wa Mwenyekiti Kimaro miaka hii michache. Hata thamani ya kampuni hii imeongezeka maradufu. Hata hivyo, Alvin alimteua Sarah kuwa Mwenyekiti mpya wa kampuni. Miaka miwili iliyopita nilipewa nafasi ya chini. Hali ya Meneja Mkuu Ngololo ni ya kusikitisha zaidi kwani yeye ni msimamizi tu sasa. Hata hivyo, kwa wale waliofanya kazi hapo awali chini yako, nyadhifa zao zote zimeshushwa.

“Vipi kuhusu Chris Maganga?”
"Bwana Maganga amerejea Mwanza. Sarah anajua mlikuwa na mahusiano ya kirafiki naye, hivyo hakumruhusu kujihusisha na masuala ya kampuni. Nilisikia kwamba hata bonasi yake ilikatwa."
Uso wa Lisa ukaingiwa simanzi nzito. Hakutarajai hata kidogo kwamba Alvin angemkabidhi Sarah kumiiki kampuni ya Mawenzi, kampuni aliyoipigiania kwa damu na jasho kwa miaka mingi, na urithi pekee kutoka kwa mama yake. ‘Alvin, oooh! Alvin! Sasa kwa kuwa nimerejea, tutapambana jino kwa jino!’
'Alvin oh! Alvin, sasa nimerudi, nitasuluhisha matokeo haya na wewe."
"Yeye ni nani, Ambah?" Mhudumu wa mapokezi alichanganyikiwa baada ya kumsikia akimwita Lisa kama Mwenyekiti Jones.
“Hujui chochote. Yeye ni Lisa Jones, mwenyekiti halisi wa kampuni hii. Amerudi sasa,” Amba akajibu kwa hasira, “Kampuni hii ni yake.”
Mhudumu wa mapokezi alikuwa ameduwaa. Wakati huu, sauti ya afisa wa usalama ilisikika kutoka kwa mlango. "Halo, Mkurugenzi Njau." Umati uligeuza macho kwa Sarah ambaye alikuwa amevalia mavazi ya kuvutia ya kiofisi.

Alivaa tabasamu la upole akiingia ofisini. Nyuma yake kulikuwa na mwanamke aliyevalia nguo nyeusi ambaye alifanana na mlinzi wake.
Sarah alipomwona Lisa, uso wake uliojipamba vizuri ukaganda. Kwa kweli, tayari alikuwa amemwona Lisa kwenye video jana yake usiku. Lakini, hakutarajia kwamba angeonekana mrembo zaidi baada ya kumuona ana kwa ana. Ikiwa mtu angedai kwamba Lisa alikuwa na umri wa miaka 20, hakuna mtu angebisha.
Sarah alijilinganisha na Lisa bila fahamu. Haijalishi ni juhudi kiasi gani alizoweka katika kutunza ngozi yake, mikunjo michache tayari ilikuwa ikionekana chini ya pembe za macho yake ikizingatiwa kwamba alikuwa anatimiza miaka 30 hivi karibuni. Hatimaye alielewa kwanini Alvin alikuwa amemwangukia Lisa wakati huo.
Alikuwa amejiuliza kuhusu mahali alipo Lisa siku chache zilizopita. Alishtuka baada ya kugundua kuwa uso wa Lisa ulikuwa umetibiwa.
Baada ya kusema hivyo, ilikuwa na maana gani? Alikuwa na udhibiti kamili juu ya Alvin muda huo, kwa hivyo Lisa hakuchukuliwa kuwa kitu.

Alipofikiria hilo, Sarah alikunja mdomo wake na kutabasamu. Alijifanya kuwa hakumuona Lisa na moja kwa moja akaelekea kwenye lifti. “Unaenda wapi Sarah? Hii ni ofisi yangu, sivyo?” Lisa alimvuta Sarah nywele zake ndefu ghafla.
Jambo la kushangaza ni kwamba Lisa alikuwa akimkokota Sarah hadi sakafuni bila kuwa na wasiwasi kuhusu sura yake. Kwa hayo, Sarah alipiga kelele kwa uchungu.
"Unafanya nini?" Yule mwanamke aliyevalia nguo nyeusi alisogea kwa upole na kumshambulia Lisa mara moja.
“Lo! Ilikuwa ni ajali. Sikutarajia kwamba angeweza kuanguka kwa kumvuta tu kidogo hivyo.” Lisa alirudi nyuma na kulegeza mshiko wake kwenye nywele za Sarah. Nywele zilizokuwa mkononi mwake kisha zikadondoka chini. "Nilikuwa nikivutiwa na nywele zako nene lakini kumbe ni za bandia?"
“Lisa, umefanya makusudi kabisa! Mkamate sasa, Maya.” Sarah alikasirika sana hivi kwamba sifa zake za kawaida za kifahari zilidhalilishwa.
Kwa sababu ya nywele zake nyembamba, fupi na nyepesi kama manyoya, Sarah alikuwa ametembelea kwenye saluni ya gharama kubwa zaidi ili kupandikizwa nywele bandia

ndefu na nene. Sasa baada ya Lisa kuzinyofoa, alipandwa na hasira.
“Mbona unanishika? Sikufanya kwa makusudi.” Lisa alipambana na Maya. Muda mfupi baadaye, Maya naye alijikuta akiburutwa chini kwenye sakafu.
Hali hiyo ilimuacha Sarah akiwa na mashaka. Maya alikuwa mlinzi ambaye Alvin alikuwa amemkabidhi kumlinda Sarah. Ilionekana kwamba kwa miaka hiyo michache, Lisa alikuwa amepata ujuzi fulani, na kufanya iwe vigumu kushughulika naye.
"Wewe ni kweli ni memba wa ONA?" Lisa aliinamisha uso wake na kumwangalia Maya ambaye alisimama haraka haraka. “Unamfahamu Shani?”
“Shani?” Maya alisaga meno yake na akajibu kwa dharau, “Bwana Kimaro amempanga kufanya kazi mahali pengine kwa muda mrefu. Ni miaka kadhaa imepita tangu arudi.”
Ilimgusa Lisa kwamba Alvin alimpa Maya jukumu la kumlinda Sarah, kama vile alivyomwomba Shani amlinde. Linapokuja suala la kushughulika na wanawake, hakuwa amebadilika hata kidogo.
Akimtazama mlinzi mwenye uwezo wa Sarah akikandamizwa, mhudumu wa mapokezi aliuliza kwa butwaa, “Mwenyekiti Njau, unataka

niwaite polisi?”
"Endelea." Lisa mara moja alienda sambamba na wazo hilo. "Pia ningependa kuwafahamisha polisi kwamba kuna mtu anamiliki kampuni yangu kinyume cha sheria."
“Kumiliki?” Sarah alimdhihaki na kumkosoa Lisa, “Mawenzi Investments sasa ni mali ya Alvin na ameniteua mimi binafsi kama mwenyekiti. Kusema kweli, wewe ni mtu mfu, Lisa.”
Lisa akapepesa macho. “Nimekufa vipi? Kwa kuwa serikali haijatoa hata cheti cha kifo changu, ninastahili kudai mali yangu. Hata hivyo, Alvin bado ni mme wangu kwa mujibu wa sheria, hivyo kimsingi unamiliki kampuni ya mke wake halali."
"Uko sahihi kabisa, Mwenyekiti Jones." Amba alipiga makofi mara moja. "Kwa kweli, yeye ndiye mwanamke mshenzi zaidi ambaye nimewahi kukutana naye."
“Hiyo inaonyesha jinsi gani alivyo mjinga. Hapo awali, mwanamke huyu pia alidai kuwa nilikuwa mgonjwa wa akili na kumfanya Alvin anipeleke katika hospitali ya magonjwa ya akili,” Lisa alisema huku akihema.
Sura ya: 320

Ilikuwa karibu saa sita mchana. Wafanyakazi walikuwa wameanza kukusanyika katika jumba la kulia chakula. Baada ya kusikia maneno ya Lisa, kila mtu alishtuka na kumtazama Sarah kwa namna ya ajabu.
“Oh! Jamani. Huo ni ukatili sana!”
“Sikutarajia hilo pia. Kwa kawaida anaonekana mwenye heshima, mkarimu, na mpole hivi kwamba nilimtendea kama mungu wa kike.” “Haya, usiseme kwa sauti. Yeye ni mwenyekiti wetu. Atatufuta kazi akisikia haya.”
Uso wa Sarah uligeuka kuwa mbaya. Tangu alipojulikana hadharani kuwa ni mpenzi wa Alvin, kila mtu alikuwa akijikombakomba kwake na kumchukulia kama mungu wa kike. Hakuwa amepitia unyonge wa namna hii. "Lisa, nitakushtaki kwa kunisdhalilsha ikiwa utatoa maneno yako ya uzushi zaidi."
“Utajua mwenyewe. Mimi nimekuja hapa leo kuangalia kampuni yangu. Nitaandaa mkutano mkuu kesho. Nitawakusanya wanahisa wote wa kampuni hapa na kuwajulisha kila mmoja wao kuhusu hilo.” Lisa alimnyooshea Sarah kwa kidole chake cha shahada, ukucha wake ukiwa umepakwa rangi nyekundu ya kucha. "Na wewe, utakuwa mtu wa kwanza nitakayemfukuza."
Sarah aliitikia kana kwamba amesikia mzaha.

Aliinama na kuangua kicheko huku machozi yakikaribia kumtoka. "Lisa, unafikiri kwamba una nafasi yoyote hapa? Mawenzi Investments sasa ni tofauti na ilivyokuwa miaka mitatu iliyopita. Ni sawa. Unaweza kwenda mbele na kuwajulisha. Ngoja tuone nani atahudhuria mkutano mkuu. Ikiwa unafikiria kunifukuza kazi, endelea kuota."
“Tusubiri tuone.” Lisa alipogeuka, alivuta tagi ya mfanyakazi wa Amba. “Wewe siyo mesenja tena. Fuatana na mimi.”
“Sawa.” Amba alimfuata kwa furaha.
Lakini, Amba alianza kuogopa mara tu baada ya kutoka nje ya mlango wa kampuni. “Mwenyekiti Jones, sina uhakika kama nikuambie hili... Usikasirike baada ya kusikia...”
“Unapanga kuniambia kuwa sina nafasi kubwa kwa sababu Alvin anampenda Sarah?” Lisa alimtazama huku akitabasamu.
Amba alimtazama kwa aibu, akisema, “Mwenyekiti Jones, unastaajabisha. Unafikiri sawasawa na mawazo yangu."
“Ni sawa. Sina hisia tena na Alvin. Hata kama anampenda, iltamsaidia nini? Mimi ndiye mbia mkuu zaidi katika Mawenzi Investments mradi niko hai. Hayuko juu ya sheria.” Lisa alitoa tabasamu hafifu.

Kule ofisini, Sarah alimpiga Maya jicho, akitaka ampigie Alvin mara moja. “BwanaKimaro, Bi Jones alikuja kwenye ofisi za Mawenzi Investments sasa hivi.
Mara alipowasili... alishika nywele za BMwenyekiti Njau na kuzinyofoa, na kusababisha uharibifu wa ngozi ya kichwa.” “Huyu mwanamke aliyelaaniwa! Si nilikuambia umlinde Sarah?” Punde Alvin alipandwa na hasira.
“Nilikuwa namlinda, lakini kabla sijapata fahamu, Bi Jones alikuwa tayari amemshambulia Bi. Njau. Alipomnyanyasa Bi. Njau tena baadaye, nilianza kushughulika naye, lakini... alionyesha ujuzi wa ajabu sana. Miss Jones amekuwa na nguvu sana,” Maya alisema kwa hatia.
Alvin alishangaa kusikia hivyo. Ingawa Maya hakuwa memba wa juu wa ONA, bado alikuwa mpiganaji bora nchini Kenya. Hakutarajia kwamba Lisa angeweza kumshinda Maya. Je, alikuwa amepitia nini miaka michache iliyopita? Maya kisha akaongeza, “Bi Jones anafikiri... Anafikiri kwamba unajaribu kumnyang’anya kampuni yake.”
"Najaribu kuchukua kampuni yake?" Alvin alicheka. “Ni mwanamke wa ajabu kiasi gani. Sina mpango wowote na kampuni ndogo kama

Mawenzi Investments.”
"Bi Njau alisema hivyo pia, lakini Bi Jones haonekani kuamini. Anataka hata kuandaa mkutano mkuu na kukufukuza wewe na Bi Njau.”
"Anauma zaidi ya anachoweza kutafuna." Ni wazi kwamba Alvin alikuwa amekasirika kwa hasira. “Mpeleke Sarah hospitalini wamuangalie ngozi ya kichwa.”
“Sawa, nitafanya hivyo. Hata hivyo, ninakupigia simu bila Bi Njau kujua. Aliniambia nisikuambie,” Maya alinong’ona, “Amekuwa akimhurumia kwa kutoweka kwake miaka mitatu iliyopita. Anaelewa kuwa Bi Jones alipitia wakati mgumu.
“Yeye ni mkarimu sana,” Alvin alisema kwa huzuni. Mara tu alipokumbuka akishuku kwamba Sarah alimdanganya kuhusu mshuko wa moyo wa Lisa, alihisi hatia.
"Baada ya kusema hivyo, Bi Njau amekuwa hana raha tangu alipokutana na Miss Jones. Nadhani ni kwa sababu Bi Jones alidai kuwa wewe ni mume wake kwani amerudi sasa. Hata alimwita Bi Njau hawara.”
“Nitazungumza na Sarah baadaye.” Alvin alikasirishwa na tabia ya Lisa ya kukosa aibu. Baada tu ya Maya kukata simu ndipo

akarudisha macho yake kwa Sarah. "Umefanya vizuri," Sarah alishika mikono ya Maya na kusema kwa huzuni, "Asante kwa kunisaidia wakati wote, Maya."
"Hapana, Bi Njau. Nilipofanya makosa wakati huo, ulinisaidia kuficha. Kama si wewe, Bwana Kimaro angenifukuza kutoka ONA na nisingekuwa hivi nilivyo leo,” Maya alisema kwa shukrani, “Mimi si mpumbavu kama Shani ambaye alianza kumhurumia Lisa baada ya kumlinda kwa muda mfupi tu. Lisa ni hawara tu ambaye aliingilia uhusiano wako na Bwana Kimaro. Yeye alitamba naye tu wakati wewe hukuwa karibu. Nafikiri tu kwamba Alvin ni haki yako.”
“Hapana, lilikuwa kosa langu... niliingia kwenye matatizo mapema...” Sura ya huzuni iliufunika uso wa Sarah. "Ikiwa Lisa ataendelea kushikamana na Alvinic, sidhani kama naweza kuendelea kuwa naye."
“Usiseme hivyo. Nina hakika unaweza, na nitakusaidia,” Maya aliuma mdomo na kujibu. Sarah akaitikia kwa kichwa. Simu yake iliita, alikuwa ni Alvin anayepiga.
Haraka alipapasa pua yake na kutoa sauti ya upole ya puani kabla hajabonyeza kitufe cha kujibu. "Alvinic. ..”
“Sauti yako ina tatizo gani?” Alvin mara moja

aligundua jambo la kushangaza.
“Ni sawa. Labda... Labda koo langu haliko sawa,” Sarah alijibu huku akilazimisha tabasamu.
“Sawa, najua kila kitu. Lisa alikuja kukutafuta na kukusababishia matatizo, sivyo?” Sarah alipojaribu kuficha jambo hilo, Alvin aliona Lisa kuwa mwanamke asiye na maana na asiye na huruma. Lazima alikuwa kipofu alipokuwa akiongea na mwanamke kama huyo hospitalini asubuhi siku hiyo.
“Hapana, naweza kuelewa hilo. Amenichukia tangu mwanzo. Kwa kawaida, alipoteza utulivu alipogundua kwamba nimekuwa mwenyekiti wa Mawenzi Investments.
"Umeweka moyo wako na roho yako kwa Mawenzi Investments katika miaka hii miwili na ninajua. Nitamfundisha somo baadaye.” "Alvinic, alidai kwamba ... wewe bado ni mume wake. Ni ukweli?" Sarah ghafla alikuwa na uvimbe kwenye koo lake. “Bado utanioa mimi?”
“Nitakuoa mpenzi. ''nimeahidi kukuoa na nitafanya hivyo kwa uhakika.'' Baada ya Alvin kukata simu, alijikunyata kwa hasira.
Kwa kweli, hakuwa amefikiria juu ya suala hilo hapo awali. Sio yeye ambaye alikuwa amebeba maiti ya Lisa wala kuangalia

uthibitisho wa kifo chake. Kwa hivyo ndoa yake na Lisa haikubatilishwa na kifo chake cha kugushi. Katika kesi hii, Alvin na Lisa bado walizingatiwa kama wenzi wa kila mmoja. “Nenda ufuatilie ujue Lisa anaishi wapi,” Alvin aligeuza kichwa chake na kumwambia Hans. Hans alirejea baadaye kidogo akiwa na jibu. “Karen Estate”
TUKUTANE KURASA 321-325
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA SABA
SIMULIZI........................LISA KURASA......316 MPAKA 320
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY WHATSAPP: +255628924768

Sura ya 316
“Hakika unajua ninachomaanisha.” Lisa alitabasamu kabla ya kutoa miwani kwenye mkoba wake na kuivaa. Mara moja alionekana mrembo zaidi na jasiri. "Nilikuwa mtu wa kawaida tu lakini ulinitupa katika hospitali ya magonjwa ya akili. Kila siku nilidungwa sindano kwa nguvu na kulishwa dawa za wagonjwa wa kichaa. Kabla ya hapo ulifungia ndani ya nyumba, niliishi maisha ya kubanwa zaidi kuliko mfungwa gerezani. Ninyi nyote mngenitia wazimu wa kweli muda si mrefu.” Uvimbe ukatokea kwenye koo la Alvin huku akiongea kwa sauti ya kizaazaa, “Hukuwa sawa kiakili wakati huo...”
“Unajua tofauti kati ya kichaa na matatizo ya akili yanayoletelezwa na hasira kali?” Lisa aliuliza. "Nilikuwa mjamzito na wewe ukanifungia ndani peke yangu huku wewe ukitanua na mpenzi wako bora wa muda wote. Baabaye ukanisukuma kwa mikono yako na kunisababisha kupoteza watoto wangu. Hiyo haikutosha, wewe na mpenzi wako mkanipakazia ugonjwa wa kichaa na kunilazimisha fungiwa ndani ya wodi kama mgongwa wa kichaa. Lakini wewe ulikuwa na mpenzi wako wa muda wote Sarah mbele na

nje ya macho yangu kila siku. Ningewezaje kukosa kuwa na mfadhaiko wa hasira kali? Ningewezaje kuwa mtulivu na mwenye adabu na wewe wakati huo?"
“Alvin, ungewezaje kumtendea hivyo binti yangu?” Joel aliumia moyoni aliposikia hivyo. Alipotoka kwenye hali ya kukosa fahamu, pia alifikiri kwamba Lisa alikuwa na tatizo la akili. Hakujua yote ni kwa sababu ya Alvin. “Wewe nyoka!” Joel alishindwa kushikilia tena akajaribu kumpiga ngumi ya uso.
Alvin alizuia ngumi ya mwanaume huyo bila juhudi na hata kuirudisha nyuma kwa nguvu. “Achana naye baba.” Macho mazuri ya Lisa yakawa makali mara moja. "Ulinitishia na baba yangu mara nyingi sana miaka mitatu iliyopita na sasa unajaribu hila ile ile ya zamani?" Mkono wa Alvin ukaganda mara moja. Akaminya midomo yake myembamba kabla ya kulegeza kamba taratibu kwa Joel. Sura ya mshangao iliosha juu ya uso wake. “Nilikutishaje?”
Alvin alibaki kimya. Lisa aliinua kichwa kumtazama huku akitabasamu. “Bwana Kimaro, mbona unajifanya? Je, hukujiamini kabisa katika kunitisha wakati huo?”
Kuliona tabasamu lake la kupendeza kulimfadhaisha. Alikumbuka aliwahi kumchukia

kwa kufanya hivyo. Lakini, sasa angeweza kuzungumza juu ya siku za nyuma bila kujali na tabasamu la dhihaka.
"Kila mtu alifanya makosa wakati huo. Marafiki zako pia hawakuwa na hatia.” Hatimaye alijibu kwa sauti nzito.
"Ndio, kaka mkubwa wa mpenzi wako ndiye mtu pekee asiye na hatia." Lisa aligeuka na kutabasamu mbele ya Joel. “Baba, waandishi walimkamata akinisaliti na Sarah wakati yuko kwenye ndoa na mimi. Hakuwa tayari kukiri makosa yake kwa mwanamke huyo licha ya kwamba kila mtu alikuwa akimtukana hivyo akanilazimisha niuambie umma kuwa mimi na yeye tayari tumetalikiana. Vinginevyo, angemkataza Dk. Angelo kukutibu. Mwishowe, kaka mkubwa wa Sarah alivamia ndani ya nyumba ya rafiki yangu na kutaka kumbaka bila huruma. Rafiki yangu mmoja alidungwa kisu na mwingine karibu kubakwa. Baada ya hapo akatishia kumwondoa Dokta Anjelo asikutibu tena ili kunishinikiza niachane na habari za kumfikisha mahakamani kaka wa mpenzi wake.”
Joel aliogopa kusikia hivyo. Binti yake aliteseka kiasi gani kwa ajili yake? Alijiona kama mtu aliyeshindwa kabisa kumlinda kadiri alivyofikiria zaidi juu ya hili. Macho yake

yalikuwa yamejaa hasira. Alijichukia kwa kuwa mzee na dhaifu sana kupigana na mtu huyo.“Alvin, wewe mnyama! Hapana, wewe ni mbaya kuliko mnyama!”
Alvin alikunja uso. Ni lini aliahidi kumtunza vizuri Lisa, hata hivyo? Hata hivyo, aliona aibu alipofikiria kuhusu siku za nyuma. Hii ndiyo sababu hakuweza kumsahau Lisa miaka yote hii. Ilikuwa nje ya hatia. “Baba, sahau. Yote ni ya zamani.”
Lisa alimsukuma kidogo Joel kuelekea kwenye gari huku akitabasamu kwa unyonge. “Twende. Hakuna sababu ya kupoteza pumzi zetu na mtu kama yeye.
“Lisa, usijali. Nitalipiza kisasi kwa ajili yako,” Joel alisema kwa hasira.
Alvin alikunja uso wake huku Lisa akicheka kabla ya kumwambia baba yake, “Achana na visasi baba. Sitaki afikirie kuwa nina wazimu na kunitega tena katika hospitali ya magonjwa ya akili. Pengine itakuwa vizuri zaidi kama tutakaa mbali naye katika siku zijazo.” Kisha, akazunguka na kuingia kwenye kiti cha dereva. Alvin alikuwa bado amesimama mbele ya gari. Lisa alitoa kichwa chake nje ya dirisha. "Mwenyekiti Kimaro, hutaki kupisha njia?"
Alvin akasimama tu akimtazama kama

sanamu. Miwani ya jua ya mwanamke ilikaa kwa uzuri kwenye pua yake nzuri. Akageuza macho yake kuelekea chini kuitazama midomo yake yenye majivuno lakini tete. Ilikuwa ni kama mwanamke huyu alikuwa amebadilika kabisa. Alihisi kutomfahamu lakini hakuweza kujizuia kuondoa macho yake. Alvin hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, kwani hakuwa mtu wa kuvutiwa kirahisi na urembo wa wanawake. Sekunde chache baadaye, hatimaye alipisha kando.
Gari jeupe la Lisa lilimpita kwa kasi. Hans akamshatua kwenye safari yake ya mawazo. "Bwana Mkubwa, ni wakati wa kwenda." "Angalia jinsi alivyodanganya kifo chake na kuondoka nchini. Nataka kujua ni nani aliyemsaidia.” Alvin aligeuka na kumwangalia msaidizi wake ghafla. Hans alitetemeka kwa mbali na haraka akaitikia kwa kichwa.
Alvin alisoma post ya Lisa kwenye Facebook baada ya kuingia kwenye gari. Alvin alitabasamu bila kupenda. Aliduwaa baada ya kugundua kilichokuwa kikiendelea.
Jamani! Alipaswa kukasirishwa kwa kudanganywa naye miaka mitatu iliyopita lakini alikuwa akitabasamu? "Hans, unafikiri hakuwa mgonjwa wakati huo?"
“Um... sina uhakika,” Hans alijibu kwa

kusitasita, “Lakini Bi Njau ni mtaalamu. Pengine... asingetudanganya?” Alinyamaza kwa muda mfupi mwishoni na kuonekana mwenye wasiwasi.
Alvin alishikwa na butwaa. Ndiyo, alikuwa amemwamini Sarah aliposema kwamba Lisa alikuwa mgonjwa wa akili miaka mitatu iliyopita. Hata hivyo, vipi ikiwa alikuwa akisema uwongo?
Alisugua kichwa chake kwa upole. Hapana, Sara asingemdanganya.
Sarah alimpigia simu wakati akiwaza hayo. "Alvinic, unakuja nyumbani?"
"Ndio, niko njiani."
Sarah alinyamaza kwa muda mfupi kabla ya kuongea tena. "Niliona habari kwamba Lisa amerudi. Inaonekana...”
“Ndio.” Alijibu haraka haraka na picha za urembo wa Lisa zikapita akilini mwake. "Alvinic, mimi ..." Sarah alicheka vibaya. “Naona amekuwa mrembo kuliko mimi na inanitia wasiwasi. Naogopa utarudiana naye.” “Usifikirie kupita kiasi. Sikuwa hata na mpango naye kabisa hapo awali. Niko nyumbani." Akakata simu na kujisemea kuacha kumfikiria Lisa.
Aliporudi kwenye jumba la kifahari la baharini usiku huo, Sarah alitoka nje kumlaki akiwa

amevalia gauni jekundu la kulalia lenye kuvutia. Ghafla, Alvin alikumbushwa jinsi Lisa alivyokuwa amevaa nguo yake nyekundu siku hiyo.
"Kuna nini? Sionekani vizuri?” Sarah aliona kuwa amevurugwa na kumtikisa begani huku akipiga kelele.
“Nitakwenda kuoga." Alvin akaelekea kwenye ngazi.
Sarah aliuma mdomo. Alvin alipotoka kuoga baadaye, alienda mbele kumkumbatia kwa nyuma na kusema kwa sauti ya kutongoza, “Alvinic, hebu... tujaribu tena usiku wa leo.” Alvin alisimama pale, bila kutikisika. Dakika chache baadaye, Alvin alimsukuma Sarah mbali kwa upole. "Nitaenda kwenye maktaba." "Alvinic, kwa nini? Tutapataje watoto namna hii?" Sarah aliuliza kwa wasiwasi, “Au unachukizwa na mimi kwa sababu ya kile kilichonitokea nilipotekwa na magaidi...” “Hapana, sivyo. Mimi ndiye mwenye tatizo.” Sura ya kuchanganyikiwa ilimwangazia usoni mwake. Hakujua ni nini kilikuwa kibaya. Katika muda wa miaka mitatu iliyopita, alijua wazi kwamba anampenda Sara lakini alikuwa akifeli kila alipokuwa akijumuika naye kwenye tendo la faragha!

Sura ya: 317
Wakati fulani, hata alifikiri kwamba alikuwa na aina fulani ya ugonjwa ambao ulimzuia kuwa karibu na wanawake. Sarah alikuwa amejaribu kutibu tatizo hili kupitia vipindi vyake kadhaa vya matibabu ya kisaikolojia lakini havikufaulu. Uso wa Sarah ulikuwa umesinyaa kwa karaha na kuchanganyikiwa. “Kwanini...kwanini usiende kupata uchunguzi wa madaktari? Kwa kweli siwezi kuvumilia tena. Nakutaka...” Alivua gauni lake na kujitupa kwa hasira. Katika sekunde hiyo ya mgawanyiko, Alvin alimsukuma mbali mara moja bila kupenda. Mwanamke ambaye hakutarajia hilo alianguka chini. Alianza kulia kwa sauti ya juu.
Alvin alimwonea huruma alipomfikiria juu ya unyonge wake. "Samahani." Akavua koti lake na kumfunga. Akambeba mpaka kitandani na hatimaye akatoka chumbani.
Alipotoka tu chumbani, Sarah alipiga ngumi kitandani kwa hasira. Hakutarajia kwamba hata baada ya kutumia mbinu chafu za kisaikolojia kumlawiti mwanamume huyo ili apendane naye miaka mitatu iliyopita, bado alishindwa kufaulu kwenye mbinu za mahaba. Wakati fulani, hata alijisikia kuumwa wakati alijaribu

kujilazimisha juu yake.
Ilikuwa ni miaka mitatu na nusu. Alikuwa karibu kupoteza akili yake kuishi maisha haya ya kuvumilia. Wakati mwingine, alitamani sana kuburudika na kuachilia hisia zake zilizozikwa ndani yake kabisa na mwanamume mwingine. Ghafla, namba isiyojulikana ilikuwa ikimpigia. Alipuuza mara moja.
Ndani ya sekunde chache, nambari hiyohiyo ilimtumia picha. Sarah alikuwa amevalia bikini kwenye picha hiyo na ameketi juu ya mwanamume wa makamo. Mwanamume huyo alikuwa na ndevu nyingi zilizochafuka huku mwili na mikono yake ikiwa imechorwa tattoo. Alikuwa akitabasamu kwa utamu huku akikaa kwenye tumbo lake kubwa.
Mshtuko ulimpitia. Hii ilikuwa ndoto yake kubwa iliyomtesa zaidi. Alijibu simu ilipoita tena. Sauti potovu ya mtu ilisikika kutoka kwenye simu. “Hehe, Sarah, sikufikiri kwamba ungeolewa na tajiri mkubwa zaidi wa Kenya baada ya kukukusaidia kutoroka kwenye kambi ya Al-Shabaab. Unafikiri Alvin Kimaro angefanya nini akigundua kuwa tulikubaka na kukulawiti siku za nyuma?”
Rangi zote zilimtoka usoni. "Hisan, uko hai?" “Haha, bila shaka, niko hai. La sivyo, hakuna mtu katika ulimwengu huu atakayejua jinsi

ulivyokuwa mwanamke wa bei nafuu,” alisema kwa kuuma meno, “Wewe ni mkatili sana. Uliniahidi kwamba nikusaidie kutorokea Ulaya ukatafute maisha, na baadaye tungeanzisha familia. Kwanini ulinidanganya?”
“Sijui unazungumzia nini,” alijibu huku akijitahidi kadiri awezavyo kuficha woga wake. “Hukumbuki?” Mtu huyo alicheka vibaya. “Sawa, nadhani sina chaguo ila kuzungumza na Alvin basi. Nitamjulisha jinsi bila aibu ulivyochagua kutufurahisha sisi watatu tulipokuteka siku za nyuma. Tulikupa chaguo, kufa au ukubali kufanya mapenzi na sisi wote watatu kwa wakati mmoja na ukachagua kufanya mapenzi. Unakumbuka?...Sitasahau tukio hilo. Nina picha za kumwaga. Nimtumie ili ajue mpenzi wake ni mwanamke gani?” "Nyamaza! Unataka nini?" Sarah hakuthubutu kufikiria hilo.
"Si mengi. Nahitaji pesa tu...”
“Ngapi?” Sarah alikosa uvumilivu.
"Hmm, vipi kuhusu dola milioni 1?" Hisan alicheka. “Mbali na hilo, nimeboreka sana hapa Mombasa tangu nifike hivi majuzi. Nahitaji uje nikumbushie enzi zetu kidogo.”
Sarah alikuwa akitetemeka wakati huo. "Acha. Usiniharibie. Mimi sasa ni mke wa mtu...” “Haha, si kama mimi nitaondoka nacho. Sawa,

Sarah, acha kujifanya. Najua ulivyo mjanja kuliko mtu mwingine yeyote.” Akacheka vibaya tena. “Njoo huku nakuahidi kukufurahisha. Usithubutu kufanya ujanja na mimi. Picha zitaangukia mikononi mwa Alvin endapo utajaribu kufanya ujanja wowote.”
"Basi usifanye hivyo, nakuja." Akiachwa bila njia mbadala, Sarah alifumba macho na kukubali. Kamwe katika miaka milioni hakuweza kutarajia kwamba Hisan alikuwa bado hai. Alifikiri hakuna mtu ambaye angewahi kujua kuhusu maisha yake ya nyuma.
“Nitakungoja."
Baada ya kumaliza kuongea na simu, Sarah alivaa na kushuka ngazi. Alvin alikuwa amesimama mbele ya madirisha ya maktaba akiwa na tafakari zake. Vidole vyake vyembamba vilikuwa vimezungushwa kwenye glasi ya divai nyekundu. Dirisha lilionyesha wazi uso wake mzuri. Mwanaume mwenye sura nzuri angemfanya mwanamke yeyote kutaka kumfanyia mambo ya kitandani usiku kama huo. Hali ya kuchanganyikiwa ikaangaza usoni mwa Sarah. Alvin alikuwa mwanaume mzuri kuliko wote ambao aliwahi kuwaona na bado alikuwa na matatizo katika idara hiyo.

“Unaenda nje?” Alvin akautazama mkoba wake.
"Ndio, nitakutana na marafiki zangu. Nachoka na hali hii.” Aliweka nywele zake nyuma ya sikio ili kudhihirisha uso wake wenye huzuni. Uso wake ulikuwa umeoshwa na aibu. “Samahani. Ninaahidi... nitamuona daktari.” “Um... hakika.” Alikuwa na shughuli nyingi sana akifikiria kushughulika na Hisan hivi kwamba aligugumia tu jibu na kuondoka haraka kwenye jumba hilo.
Kimya cha pin-tone kilianguka kwenye chumba. Alvin aliinamisha kichwa chini na kuumaliza ule mvinyo kwa mkupuo. Paka mnene alikuja karibu na miguu yake na kuanza kulia. Akainama kumpapasa Charlie kichwani. "Nifanye nini ikiwa nitaendelea kushindwa?" alijiuliza kimya kimya.
•••
Jumba la familia ya Ngosha.
Simu ya Lisa iliita na kwenda bustanini kabla ya kujibu. Sauti ya mtu mwingine ilisikika kutoka kwa simu. “Bibi, Sarah Njau alienda kwenye nyumba ya kibinafsi aliyoinunua kwa siri chini ya jina lake. Hisan yupo pia. Kamera za uchunguzi tulizopitia juhudi zote za kusakinisha huenda hazitakuwa na manufaa kwa sasa.”

Lisa alihisi kukata tamaa baada ya kusikia hivyo. “Nilifikiri angekutana na Hisan hotelini. Inaonekana yuko makini kuliko nilivyofikiria.” “Ni sawa. Hawataishia mara moja tu, lazima wataendelea. Cha muhimu ni kwamba kaingia mtegoni.”
“Uko sahihi. Endelea kuwaangalia kwa karibu. Nijulishe akiondoka.”
“Sawa.” Baada ya kuiweka simu, Joel alionekana kuwa na wasiwasi.
"Lisa, wenye hisa wengi wa Ngosha Corporation walinipigia simu mapema. Wanataka nirudi kwenye nafasi yangu kesho. Inaonekana wamekubali kumfukuza kwa muda Damien na Melanie kwenye nyadhifa zao.” "Kwa muda? Wanataka wakutumie kurekebisha hali hiyo kisha wakuteme tena.” Lisa alikuwa na wasiwasi. “Baba, ni bora kusubiri bei ya hisa ya Ngosha Corporation ishuke zaidi."
“Hakika,” alikubali bila kusita.
“Baba, umenielewa lakini?” Lisa aliuliza huku akitabasamu. “Tunazungumza kuhusu mabilioni ya dola hapa.”
“Haijalishi. Furaha yako ndio kipaumbele changu kikuu." Alipomaliza kusema hivyo, alijikongoja kurudi nyuma kidogo.
Lisa akamshika mara moja. “Baba, kuna nini?”

“Pumzi, pengine ni uzee tu. Ninaendelea kupata shida ya kupumua tangu hivi majuzi. Nadhani ajali hiyo imeathiri sana afya yangu. Ninaanza kuhema kwa nguvu baada ya kutembea hatua chache tu.” Alitabasamu kwa uchungu. “Ndiyo maana nilitaka kumkabidhi Melanie Kampuni hilo mapema lakini ni aibu iliyoje...”
Lisa alikunja uso. “Baba nitakupeleka hospitalini kwa uchunguzi kesho.” “Hakuna haja ya hilo. Ninafanya hivyo kila mwaka.”
"Lazima unisikilize la sivyo sitakuwa na raha." Lisa alikuwa amedhamiria.
Machozi yalianza kumtoka huku akimtazama. “Lisa, nina deni kubwa sana kwako na mama yako. Sina maana kabisa!”
"Baba, kusema kweli, mimi huchukia wakati mwingine lakini oh, mimi bado ni binti yako mwisho wa siku."
Joel alikuwa akijipiga teke. Licha ya kufanya kazi katika tasnia ya biashara kwa miaka mingi, bado aliishia kubweka kwa mti mbaya. Alihisi haja ya kurekebisha kwa Lisa katika siku zijazo. Ni lazima asimwache ateseke.
Sura ya: 318

•••Siku inayofuata•••
Lisa alimpeleka Joel katika hospitali mpya iliyofunguliwa lakini yenye sifa nzuri huko Nairobi kwa uchunguzi wa kimatibabu. Matokeo ya uchunguzi yalitoka asubuhi hiyohiyo.
Daktari alikunja uso baada ya kuitazama ripoti hiyo. "Bwana. Ngosha, kuna sumu kwenye damu yako."
"Nini?" Joel alishtuka sana, “Lakini uchunguzi nilioufanya miezi mitatu iliyopita ulionyesha kuwa nilikuwa sawa.”
Daktari akatikisa kichwa “Ni sumu ya muda mrefu, ambayo ilianza kutokea angalau miaka miwili iliyopita. Je, unapata kikohozi, maumivu ya kichwa na kifua kubana kila mara?” “Ndiyo.” Joel aliitikia kwa kichwa haraka, "Nilienda kumuona daktari mapema. Baada ya kunifanyia uchunguzi wa mwili, daktari alidai kuwa inaweza kuwa ni kutokana na madhara ya ajali na umri wangu..."
"Sijui kwanini daktari ambaye alikutibu hapo awali alisema hivyo. Naam, unaweza kutofautisha kwa uwazi kutokana na matokeo sasa. Kama usingefahamishwa mapema, afya yako ingedhoofika ndani ya mwaka mmoja. Huenda ungeeanguka au kupata mshtuko wa

moyo na kupoteza maisha." Daktari alimtazama Joeli kwa huruma huku akiongea. Watu walisema jamii ya watu matajiri na waliofanikiwa imejaa shida na matatizo kwa ndani. Sasa daktari aliposhuhudia mwenyewe aligundua kuwa kauli ile ilikuwa sahihi. Joel alizama katika hali ya kukata tamaa.
“Dokta inawezekana kuondoa sumu katika mwili wa baba yangu?" Lisa aliuliza.
Daktari akamjibu, “Inawezekana, lakini hatakuwa sawa kama hapo awali, nashauri afanyiwe matibabu haraka iwezekanavyo.” "Asante."
Baada ya kutoa shukrani zake kwa daktari, Lisa alimshika Joel na kutoka naye nje huku akiwa ameduwaa. Huku akimtazama Joel alivyokuwa amechanganyikiwa alisema kwa unyonge, “Kuhusu sumu ni lazima kuna mtu karibu yako amekuwa akikuchomekea kwenye chakula. aidha yuko katika kampuni au kwenye nyumba yako. Nina uhakika daktari uliyemwona kabla ya hii pia alikuwa amehongwa, ndiyo maana alidai kuwa hauna tatizo."
“Ni Melanie ndiye aliyenipeleka huko kila mara,” Joel alisema kwa huzuni huku akionyesha dhihaka, “Sikutarajia jambo hilo kutokea hata katika ndoto tu.” Kwa kweli,

nilitumia zaidi ya miaka 20 kumlea, na kumpa kilicho bora zaidi. Hata sikuwahi kufikiri kwamba Damien ndiye baba yake mzazi. Kuhusu Nina, nilimpa dola milioni chache baada ya kuachana naye. Nina na Melanie wanatisha sana. Tukio hili bila shaka linahusiana nao."
Lisa alishika midomo yake, alikuwa sahihi, kwa bahati nzuri alikuwa amerudi, kama angechelewa kurdi baadaye Joel angekuwa tayari ameshapoteza maisha,
“Nahitaji kutoa taarifa polisi,” Joel alisema kwa hasira.
“Baba acha. Kama utafanya hivyo, Nina na Melanie hakika watampachika mtu ambaye amekuwa akinyunyiza sumu chakula chako. Kwa kuwa walikuwa na ujasiri wa kufanya kitendo kama hicho, nina hakika wamekuja na mpango wa kujinasua."
Lisa alikodoa macho kabla ya kuendelea, “Unatakiwa mwili wako utolewe sumu kwa siri huku ukijifanya hujui lolote kuhusu hilo, weka macho kwa yaya na watumishi katika jumba lako na sekretari wako ili kujua ni nani amekuwa akichoma chakula chako. Kisha, unaweza kumshika mtu huyo na kuwafanya Nina na Melanie waungame.”
Hatimaye Joel alielewa na kumtazama binti

yake kwa kumshangaa. “Lisa, una akili zaidi kuliko mimi.”
"Baba, wewe ni mkarimu sana na unaamini watu kwa urahisi sana." Uso mzima wa Lisa uliwasilisha hali ya huzuni. Baada ya kupitia misukosuko mingi, alielewa kanuni kwamba kuwa mkarimu kwa maadui zake kungemaanisha kujifanyia ukatili yeye mwenyewe.
“Umesema kweli. Joel alishusha pumzi na kutikisa kichwa kwa huruma. Kama asingekuwa mwema sana, asingemwoa Nina na hivyo kumuumiza sana Sheryl wakati ule. Mawazo ya Sheryl yalimfanya ashushe pumzi kwa maumivu. Akatabasamu kwa uchungu. Joel aliingia kwenye kitengo kingine kwa ajili ya kuanza matibabu ya kuondolewa sumu, na Lisa ilibidi ashughulikie malipo ya matibabu yake. Baada ya kuachana na Joel, Lisa alipokea simu nyingine.
“Sarah ameondoka nyumbani kwa Alvin asubuhi hii tena.” Lisa alitazama saa iliyosomeka saa tano asubuhi “Unahisi anaweza kuwa anelekea kwa Hisan, huh?”
“Ndiyo.” Mtu wa upande mwingine alicheka na kusema, "Sijui kama Alvin anaweza kumridhisha."

Lisa alipotaka kujibu mara ghafla lifti ilisimama kwenye ghorofa ya tatu. Alvin ambaye alikuwa amejengeka kwa nguvu alionekana akiwa na Hans wakitokea kwenye jengo la huduma za matatizo ya kiume. Alikuwa akitoa hisia zisizopingika za utu uzima wa kiume. Watatu hao walipotazamana, Alvin aliganda. Lisa uligeuka kuwa wa ajabu baada ya kutazama ubao ulio nyuma yake uliosomeka 'kitengo cha andrology'.”
"Pengine hawezi kumridhisha. Nina jambo la kushughulika nalo sasa. Bye." Lisa alimalizia maneno yake na kubonyeza kitufe cha kukata simu.
Mara tu Alvin aliposikia neno 'kumridhisha', uso wa Alvin ulibadilika kwa huzuni. “Unamtumbulia macho nani? Nimekuja hapa tu kumsindikiza Hans!”
Alipoona amegeuzwa mbuzi wa kafara, Hans hakusema lolote. Alihisi kumwaga machozi. Hakujali kufanywa mbuzi wa kafara kwa mambo mengine, lakini hili? Asingeweza kukubali. Ni jambo la kudhalilisha sana.
Mara Hans alipokea ishara ya jicho kutoka kwa Alvin. Hakuwa na jinsi zaidi ya kutikisa kichwa. kwa kusitasita huku akikuna kichwa kwa aibu, “aaah! Ni kweli, nina tatizo la kuwahi kufika kileleni. Nashindwa kumridhisha mama

watoto...”
“Ni ajabu basi!” Lisa akashangaa. “Inakuaje bosi amsindikize msaidizi wake kwa daktari kwa jambo kama hili? Hahaa! Nina suluhisho kwa jambo hili Hans!”
“Suluhisho gani? Kwani wewe ni daktari?" Alvin alijawa na msisitizo na dharau. “Naongea na Hans, siyo wewe. Hans mwaya tumia vumbi la kongo!" Lisa aliinua kichwa chake kwa tabasamu. Hans hakuweza kujizuia ila kucheka.
Alvin alimtazama kwa huzuni na mara Hans akasema kwa uchungu, "Nimejaribu, lakini haikufanya kazi."
“Oh kweli?” Lisa alimkazia macho Alvin. “Basi fanya mazoezi ya kegel. Labda misuli ya mashine haikazi...”
"Mbona unanitazama mimi, si kasema haijawahi kumsaidia?" Alvin alitamani angemfukuza kutoka kwenye lifti.
“Hans pole, ungekuwa mpenzi wangu ningekusaidia. Kuna staili nyingisana za kumasidiamwanamume mwenye tatizo hilo. Ni jambo dogo sana." Tabasamu la kupendeza likaonekana kwenye kona za macho ya Lisa. Alvin alivutiwa na sura yake. Uso wake uliokuwa na makovu ulipita akilini mwake bila kujua. Ikabidi akubali kwamba mwanamume

yeyote angevutiwa na uzuri wake sasa. Kama angetabasamu kama muda huo hapo awali, huenda asingemchukia kabisa.
Muda mfupi baadaye, Lisa aliongeza, "Hans, unahitaji kuponya huu ugonjwa haraka iwezekanavyo. Vinginevyo, mpenzi wako atalazimika kutafuta mtu mwingine ili kukidhi matamanio yake." Akiwa anaongea hayo alicheka huku macho yake yakiwa yamemtazama Alvin.
“Unadhani wanawake wote hawajiheshimu kama wewe?” Alvin alikasirishwa na macho yake, alishindwa kuzuia hisia zake.
“Kwa hiyo mimi sijiheshimu?” Lisa alijinyooshea kidole na kucheka. “Sawa. Siwezi kuwa na faida yoyote kwa kubishana na wewe!” Aliamua kuachana na maongezi hayo mara moja. Hivi ndivyo Alvin alivyokuwa akimuona kama mtu asiyejiheshimu wakati yeye ndiye aliyemsaliti.
Lifti ilipofika, Lisa alitoka moja kwa moja. Baada ya kumtazama akitembea kwa mbali, Alvin aligeuka na kumwambia Hans kwa sura ya huzuni, “Kati ya hospitali nyingi sana za Nairobi, kwa nini ulinileta hapa?”
Hans alijihisi mnyonge. "Nilikuleta hapa kwa sababu ulikataa kwenda kwenye hospitali ya Dokta Choka. Hospitali hii ilifunguliwa hivi

majuzi na daktari wa andrology hapa ni maarufu sana nchini Kenya."
"Toka." Alvin alimuangalia Hans kwa ukali kabla hajatoka kwenye lifti. Hakukuwa na kitu cha aibu zaidi ya kukutana na mke wake wa zamani alipotembelea kitengo cha andrology, ama magonjwa ya kiume. Damn it!
Sura ya 319
Lisa aliendesha gari hadi makao makuu ya Mawenzi Investments mara baada ya kutoka hospitali. Makao makuu sasa yalikuwa yamehamia Nairobi kutokea Dar es Salaam. Baada ya miaka mitatu, Sura zinazofahamika kwenye dawati la mbele zilikuwa tayari zimebadilishwa na sura mpya.
Lisa alipoingia tu, mhudumu wa mapokezi akamzuia. "Wewe ni nani? Umeshapanga miadi?"
"Hapana." Lisa akavua miwani yake ya jua, akidhihirisha uso wake mzuri sana. "Lakini ningependa kukutana na Mwenyekiti wako." Mhudumu wa mapokezi alipigwa na butwaa kwa muda kabla ya kudhihaki.“Wewe ni nani kukutana na Mwenyekiti wetu bila kufanya miadi mapema? Je, unafikiri kwamba Mwenyekiti wetu atakutana na mtu yeyote

ambaye amevaa vizuri? Wewe si mtu mashuhuri kama Cindy Tambwe. ”
"Cindy Tambwe?" Lisa aliinua uso wake, "Cindy ndiye balozi mpya wa kampuni yetu. Toka nje," mhudumu wa mapokezi alijibu kwa hasira.
Tabasamu la Lisa likawa gumu kidogo. "Kwa hiyo Mwenyekiti wako ni nani sasa?"
"Unataka kukutana na Mwenyekiti wetu lakini hata humjui yeye ni nani? Naam, Mwenyekiti wetu ni Sarah Langa Njau. Miss Njau ni mchumba wa Alvin Kimaro ambaye anaongoza KIM International."
Maneno ya mhudumu wa mapokezi yalifanya macho ya Lisa yawe na huzuni. Huku hali ya mamlaka isiyoonekana ikimtoka, mhudumu wa mapokezi aliingiwa na hofu.
Wakati huo, mtu aliyekuwa nyuma yake akapiga kelele. "Mwenyekiti J-Jones?"
Lisa aligeuka na kumkazia macho yule mwanamume aliyekuwa nyuma yake ambaye alionekana kana kwamba alikuwa na umri wa miaka 40. Alionekana kudorora kwa uso dhaifu kidogo. Mwanamume huyo hapo awali alikuwa meneja wa Mawenzi huko Nairobi. Macho ya kupendeza ya Lisa yalimtoka, na akatabasamu kwa mshangao.
“Ni wewe, Mwenyekiti Jones! Habari ambazo

watu wamekuwa wakieneza mtandaoni kuhusu wewe ni za kweli? Bado uko hai?" Meneja wa zamani alimtazama kwa msisimko, macho yake yakiwa mekundu,
“Ndio, bado niko hai.” Lisa aliitazama ile tagi iliyokuwa mbele ya kifua chake na kukunja uso. Sasa alikuwa ni mesenja tu wa kusafirisha mafaili kutoka ofisi moja moja hadi nyingine. Mwanamume yule aliyeitwa Amba alijibu kwa huzuni, "Mwenyekiti Jones, labda hujui kwamba ulipotangazwa kuwa umekufa miaka mitatu iliyopita, umiliki wa kampuni ulihamishiwa kwa Mumeo, Alvin Kimaro. Baada ya yote, Bwana Kimaro alikuwa mume wako halali. Bila kusema, wanahisa wote isipokuwa Chris Maganga walimuunga mkono Bwana Kimaro. Kwa kweli, Mawenzi Investments imekuwa ikifanya vizuri sana chini ya uongozi wa Mwenyekiti Kimaro miaka hii michache. Hata thamani ya kampuni hii imeongezeka maradufu. Hata hivyo, Alvin alimteua Sarah kuwa Mwenyekiti mpya wa kampuni. Miaka miwili iliyopita nilipewa nafasi ya chini. Hali ya Meneja Mkuu Ngololo ni ya kusikitisha zaidi kwani yeye ni msimamizi tu sasa. Hata hivyo, kwa wale waliofanya kazi hapo awali chini yako, nyadhifa zao zote zimeshushwa.

“Vipi kuhusu Chris Maganga?”
"Bwana Maganga amerejea Mwanza. Sarah anajua mlikuwa na mahusiano ya kirafiki naye, hivyo hakumruhusu kujihusisha na masuala ya kampuni. Nilisikia kwamba hata bonasi yake ilikatwa."
Uso wa Lisa ukaingiwa simanzi nzito. Hakutarajai hata kidogo kwamba Alvin angemkabidhi Sarah kumiiki kampuni ya Mawenzi, kampuni aliyoipigiania kwa damu na jasho kwa miaka mingi, na urithi pekee kutoka kwa mama yake. ‘Alvin, oooh! Alvin! Sasa kwa kuwa nimerejea, tutapambana jino kwa jino!’
'Alvin oh! Alvin, sasa nimerudi, nitasuluhisha matokeo haya na wewe."
"Yeye ni nani, Ambah?" Mhudumu wa mapokezi alichanganyikiwa baada ya kumsikia akimwita Lisa kama Mwenyekiti Jones.
“Hujui chochote. Yeye ni Lisa Jones, mwenyekiti halisi wa kampuni hii. Amerudi sasa,” Amba akajibu kwa hasira, “Kampuni hii ni yake.”
Mhudumu wa mapokezi alikuwa ameduwaa. Wakati huu, sauti ya afisa wa usalama ilisikika kutoka kwa mlango. "Halo, Mkurugenzi Njau." Umati uligeuza macho kwa Sarah ambaye alikuwa amevalia mavazi ya kuvutia ya kiofisi.

Alivaa tabasamu la upole akiingia ofisini. Nyuma yake kulikuwa na mwanamke aliyevalia nguo nyeusi ambaye alifanana na mlinzi wake.
Sarah alipomwona Lisa, uso wake uliojipamba vizuri ukaganda. Kwa kweli, tayari alikuwa amemwona Lisa kwenye video jana yake usiku. Lakini, hakutarajia kwamba angeonekana mrembo zaidi baada ya kumuona ana kwa ana. Ikiwa mtu angedai kwamba Lisa alikuwa na umri wa miaka 20, hakuna mtu angebisha.
Sarah alijilinganisha na Lisa bila fahamu. Haijalishi ni juhudi kiasi gani alizoweka katika kutunza ngozi yake, mikunjo michache tayari ilikuwa ikionekana chini ya pembe za macho yake ikizingatiwa kwamba alikuwa anatimiza miaka 30 hivi karibuni. Hatimaye alielewa kwanini Alvin alikuwa amemwangukia Lisa wakati huo.
Alikuwa amejiuliza kuhusu mahali alipo Lisa siku chache zilizopita. Alishtuka baada ya kugundua kuwa uso wa Lisa ulikuwa umetibiwa.
Baada ya kusema hivyo, ilikuwa na maana gani? Alikuwa na udhibiti kamili juu ya Alvin muda huo, kwa hivyo Lisa hakuchukuliwa kuwa kitu.

Alipofikiria hilo, Sarah alikunja mdomo wake na kutabasamu. Alijifanya kuwa hakumuona Lisa na moja kwa moja akaelekea kwenye lifti. “Unaenda wapi Sarah? Hii ni ofisi yangu, sivyo?” Lisa alimvuta Sarah nywele zake ndefu ghafla.
Jambo la kushangaza ni kwamba Lisa alikuwa akimkokota Sarah hadi sakafuni bila kuwa na wasiwasi kuhusu sura yake. Kwa hayo, Sarah alipiga kelele kwa uchungu.
"Unafanya nini?" Yule mwanamke aliyevalia nguo nyeusi alisogea kwa upole na kumshambulia Lisa mara moja.
“Lo! Ilikuwa ni ajali. Sikutarajia kwamba angeweza kuanguka kwa kumvuta tu kidogo hivyo.” Lisa alirudi nyuma na kulegeza mshiko wake kwenye nywele za Sarah. Nywele zilizokuwa mkononi mwake kisha zikadondoka chini. "Nilikuwa nikivutiwa na nywele zako nene lakini kumbe ni za bandia?"
“Lisa, umefanya makusudi kabisa! Mkamate sasa, Maya.” Sarah alikasirika sana hivi kwamba sifa zake za kawaida za kifahari zilidhalilishwa.
Kwa sababu ya nywele zake nyembamba, fupi na nyepesi kama manyoya, Sarah alikuwa ametembelea kwenye saluni ya gharama kubwa zaidi ili kupandikizwa nywele bandia

ndefu na nene. Sasa baada ya Lisa kuzinyofoa, alipandwa na hasira.
“Mbona unanishika? Sikufanya kwa makusudi.” Lisa alipambana na Maya. Muda mfupi baadaye, Maya naye alijikuta akiburutwa chini kwenye sakafu.
Hali hiyo ilimuacha Sarah akiwa na mashaka. Maya alikuwa mlinzi ambaye Alvin alikuwa amemkabidhi kumlinda Sarah. Ilionekana kwamba kwa miaka hiyo michache, Lisa alikuwa amepata ujuzi fulani, na kufanya iwe vigumu kushughulika naye.
"Wewe ni kweli ni memba wa ONA?" Lisa aliinamisha uso wake na kumwangalia Maya ambaye alisimama haraka haraka. “Unamfahamu Shani?”
“Shani?” Maya alisaga meno yake na akajibu kwa dharau, “Bwana Kimaro amempanga kufanya kazi mahali pengine kwa muda mrefu. Ni miaka kadhaa imepita tangu arudi.”
Ilimgusa Lisa kwamba Alvin alimpa Maya jukumu la kumlinda Sarah, kama vile alivyomwomba Shani amlinde. Linapokuja suala la kushughulika na wanawake, hakuwa amebadilika hata kidogo.
Akimtazama mlinzi mwenye uwezo wa Sarah akikandamizwa, mhudumu wa mapokezi aliuliza kwa butwaa, “Mwenyekiti Njau, unataka

niwaite polisi?”
"Endelea." Lisa mara moja alienda sambamba na wazo hilo. "Pia ningependa kuwafahamisha polisi kwamba kuna mtu anamiliki kampuni yangu kinyume cha sheria."
“Kumiliki?” Sarah alimdhihaki na kumkosoa Lisa, “Mawenzi Investments sasa ni mali ya Alvin na ameniteua mimi binafsi kama mwenyekiti. Kusema kweli, wewe ni mtu mfu, Lisa.”
Lisa akapepesa macho. “Nimekufa vipi? Kwa kuwa serikali haijatoa hata cheti cha kifo changu, ninastahili kudai mali yangu. Hata hivyo, Alvin bado ni mme wangu kwa mujibu wa sheria, hivyo kimsingi unamiliki kampuni ya mke wake halali."
"Uko sahihi kabisa, Mwenyekiti Jones." Amba alipiga makofi mara moja. "Kwa kweli, yeye ndiye mwanamke mshenzi zaidi ambaye nimewahi kukutana naye."
“Hiyo inaonyesha jinsi gani alivyo mjinga. Hapo awali, mwanamke huyu pia alidai kuwa nilikuwa mgonjwa wa akili na kumfanya Alvin anipeleke katika hospitali ya magonjwa ya akili,” Lisa alisema huku akihema.
Sura ya: 320

Ilikuwa karibu saa sita mchana. Wafanyakazi walikuwa wameanza kukusanyika katika jumba la kulia chakula. Baada ya kusikia maneno ya Lisa, kila mtu alishtuka na kumtazama Sarah kwa namna ya ajabu.
“Oh! Jamani. Huo ni ukatili sana!”
“Sikutarajia hilo pia. Kwa kawaida anaonekana mwenye heshima, mkarimu, na mpole hivi kwamba nilimtendea kama mungu wa kike.” “Haya, usiseme kwa sauti. Yeye ni mwenyekiti wetu. Atatufuta kazi akisikia haya.”
Uso wa Sarah uligeuka kuwa mbaya. Tangu alipojulikana hadharani kuwa ni mpenzi wa Alvin, kila mtu alikuwa akijikombakomba kwake na kumchukulia kama mungu wa kike. Hakuwa amepitia unyonge wa namna hii. "Lisa, nitakushtaki kwa kunisdhalilsha ikiwa utatoa maneno yako ya uzushi zaidi."
“Utajua mwenyewe. Mimi nimekuja hapa leo kuangalia kampuni yangu. Nitaandaa mkutano mkuu kesho. Nitawakusanya wanahisa wote wa kampuni hapa na kuwajulisha kila mmoja wao kuhusu hilo.” Lisa alimnyooshea Sarah kwa kidole chake cha shahada, ukucha wake ukiwa umepakwa rangi nyekundu ya kucha. "Na wewe, utakuwa mtu wa kwanza nitakayemfukuza."
Sarah aliitikia kana kwamba amesikia mzaha.

Aliinama na kuangua kicheko huku machozi yakikaribia kumtoka. "Lisa, unafikiri kwamba una nafasi yoyote hapa? Mawenzi Investments sasa ni tofauti na ilivyokuwa miaka mitatu iliyopita. Ni sawa. Unaweza kwenda mbele na kuwajulisha. Ngoja tuone nani atahudhuria mkutano mkuu. Ikiwa unafikiria kunifukuza kazi, endelea kuota."
“Tusubiri tuone.” Lisa alipogeuka, alivuta tagi ya mfanyakazi wa Amba. “Wewe siyo mesenja tena. Fuatana na mimi.”
“Sawa.” Amba alimfuata kwa furaha.
Lakini, Amba alianza kuogopa mara tu baada ya kutoka nje ya mlango wa kampuni. “Mwenyekiti Jones, sina uhakika kama nikuambie hili... Usikasirike baada ya kusikia...”
“Unapanga kuniambia kuwa sina nafasi kubwa kwa sababu Alvin anampenda Sarah?” Lisa alimtazama huku akitabasamu.
Amba alimtazama kwa aibu, akisema, “Mwenyekiti Jones, unastaajabisha. Unafikiri sawasawa na mawazo yangu."
“Ni sawa. Sina hisia tena na Alvin. Hata kama anampenda, iltamsaidia nini? Mimi ndiye mbia mkuu zaidi katika Mawenzi Investments mradi niko hai. Hayuko juu ya sheria.” Lisa alitoa tabasamu hafifu.

Kule ofisini, Sarah alimpiga Maya jicho, akitaka ampigie Alvin mara moja. “BwanaKimaro, Bi Jones alikuja kwenye ofisi za Mawenzi Investments sasa hivi.
Mara alipowasili... alishika nywele za BMwenyekiti Njau na kuzinyofoa, na kusababisha uharibifu wa ngozi ya kichwa.” “Huyu mwanamke aliyelaaniwa! Si nilikuambia umlinde Sarah?” Punde Alvin alipandwa na hasira.
“Nilikuwa namlinda, lakini kabla sijapata fahamu, Bi Jones alikuwa tayari amemshambulia Bi. Njau. Alipomnyanyasa Bi. Njau tena baadaye, nilianza kushughulika naye, lakini... alionyesha ujuzi wa ajabu sana. Miss Jones amekuwa na nguvu sana,” Maya alisema kwa hatia.
Alvin alishangaa kusikia hivyo. Ingawa Maya hakuwa memba wa juu wa ONA, bado alikuwa mpiganaji bora nchini Kenya. Hakutarajia kwamba Lisa angeweza kumshinda Maya. Je, alikuwa amepitia nini miaka michache iliyopita? Maya kisha akaongeza, “Bi Jones anafikiri... Anafikiri kwamba unajaribu kumnyang’anya kampuni yake.”
"Najaribu kuchukua kampuni yake?" Alvin alicheka. “Ni mwanamke wa ajabu kiasi gani. Sina mpango wowote na kampuni ndogo kama

Mawenzi Investments.”
"Bi Njau alisema hivyo pia, lakini Bi Jones haonekani kuamini. Anataka hata kuandaa mkutano mkuu na kukufukuza wewe na Bi Njau.”
"Anauma zaidi ya anachoweza kutafuna." Ni wazi kwamba Alvin alikuwa amekasirika kwa hasira. “Mpeleke Sarah hospitalini wamuangalie ngozi ya kichwa.”
“Sawa, nitafanya hivyo. Hata hivyo, ninakupigia simu bila Bi Njau kujua. Aliniambia nisikuambie,” Maya alinong’ona, “Amekuwa akimhurumia kwa kutoweka kwake miaka mitatu iliyopita. Anaelewa kuwa Bi Jones alipitia wakati mgumu.
“Yeye ni mkarimu sana,” Alvin alisema kwa huzuni. Mara tu alipokumbuka akishuku kwamba Sarah alimdanganya kuhusu mshuko wa moyo wa Lisa, alihisi hatia.
"Baada ya kusema hivyo, Bi Njau amekuwa hana raha tangu alipokutana na Miss Jones. Nadhani ni kwa sababu Bi Jones alidai kuwa wewe ni mume wake kwani amerudi sasa. Hata alimwita Bi Njau hawara.”
“Nitazungumza na Sarah baadaye.” Alvin alikasirishwa na tabia ya Lisa ya kukosa aibu. Baada tu ya Maya kukata simu ndipo

akarudisha macho yake kwa Sarah. "Umefanya vizuri," Sarah alishika mikono ya Maya na kusema kwa huzuni, "Asante kwa kunisaidia wakati wote, Maya."
"Hapana, Bi Njau. Nilipofanya makosa wakati huo, ulinisaidia kuficha. Kama si wewe, Bwana Kimaro angenifukuza kutoka ONA na nisingekuwa hivi nilivyo leo,” Maya alisema kwa shukrani, “Mimi si mpumbavu kama Shani ambaye alianza kumhurumia Lisa baada ya kumlinda kwa muda mfupi tu. Lisa ni hawara tu ambaye aliingilia uhusiano wako na Bwana Kimaro. Yeye alitamba naye tu wakati wewe hukuwa karibu. Nafikiri tu kwamba Alvin ni haki yako.”
“Hapana, lilikuwa kosa langu... niliingia kwenye matatizo mapema...” Sura ya huzuni iliufunika uso wa Sarah. "Ikiwa Lisa ataendelea kushikamana na Alvinic, sidhani kama naweza kuendelea kuwa naye."
“Usiseme hivyo. Nina hakika unaweza, na nitakusaidia,” Maya aliuma mdomo na kujibu. Sarah akaitikia kwa kichwa. Simu yake iliita, alikuwa ni Alvin anayepiga.
Haraka alipapasa pua yake na kutoa sauti ya upole ya puani kabla hajabonyeza kitufe cha kujibu. "Alvinic. ..”
“Sauti yako ina tatizo gani?” Alvin mara moja

aligundua jambo la kushangaza.
“Ni sawa. Labda... Labda koo langu haliko sawa,” Sarah alijibu huku akilazimisha tabasamu.
“Sawa, najua kila kitu. Lisa alikuja kukutafuta na kukusababishia matatizo, sivyo?” Sarah alipojaribu kuficha jambo hilo, Alvin aliona Lisa kuwa mwanamke asiye na maana na asiye na huruma. Lazima alikuwa kipofu alipokuwa akiongea na mwanamke kama huyo hospitalini asubuhi siku hiyo.
“Hapana, naweza kuelewa hilo. Amenichukia tangu mwanzo. Kwa kawaida, alipoteza utulivu alipogundua kwamba nimekuwa mwenyekiti wa Mawenzi Investments.
"Umeweka moyo wako na roho yako kwa Mawenzi Investments katika miaka hii miwili na ninajua. Nitamfundisha somo baadaye.” "Alvinic, alidai kwamba ... wewe bado ni mume wake. Ni ukweli?" Sarah ghafla alikuwa na uvimbe kwenye koo lake. “Bado utanioa mimi?”
“Nitakuoa mpenzi. ''nimeahidi kukuoa na nitafanya hivyo kwa uhakika.'' Baada ya Alvin kukata simu, alijikunyata kwa hasira.
Kwa kweli, hakuwa amefikiria juu ya suala hilo hapo awali. Sio yeye ambaye alikuwa amebeba maiti ya Lisa wala kuangalia

uthibitisho wa kifo chake. Kwa hivyo ndoa yake na Lisa haikubatilishwa na kifo chake cha kugushi. Katika kesi hii, Alvin na Lisa bado walizingatiwa kama wenzi wa kila mmoja. “Nenda ufuatilie ujue Lisa anaishi wapi,” Alvin aligeuza kichwa chake na kumwambia Hans. Hans alirejea baadaye kidogo akiwa na jibu. “Karen Estate”
TUKUTANE KURASA 321-325
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
[emoji120][emoji7]
 
LISA KITABU CHA SABA
SIMULIZI........................LISA KURASA......321 MPAKA 325
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY WHATSAPP: +255628924768

Sura ya 321
Baada ya Amba kuwapigia simu wahahisa kadhaa wa Mawenzi, alimgeukia Lisa akiwa amekasirika kwa huzuni. “Mwenyekiti Jones, wakurugenzi wa Mawenzi Investments hata hawakupokea simu zangu. Wapo waliojibu lakini walikata simu kabla sijamaliza kuongea. Ninasikitika kusema kuwa Chris Maganga ndiye pekee atakayehudhuria mkutano huo.” "Mjomba Chris bado ni yule yule, sivyo?" Lisa alicheka huku akimwagilia maua kwenye kibaraza.
"Haujakasirishwa na hilo, Mwenyekiti Jones?" “Usijali. Mkutano mkuu utaendelea kama kawaida. Unaweza kwenda nyumbani sasa. Kuna mgeni atatembelea nyumbani kwangu baada ya muda mfupi.” Lisa alimkonyeza kwa namna ya kinyonge.
Kwa mtazamo wa Lisa wa kujiamini, Amba aliondoka kwa mashaka.
Muda mfupi baada ya Amba kuondoka, Lisa alipiga simu ya video ili kuzungumza na watoto wake wawili nchini Marekani. “Nimekukumbuka, Mama.” Suzie alionyesha sura yenye machozi kwenye uso wake mzuri wa mviringo. Hata hivyo, Lisa alipandwa na

hasira mara tu alipoona chokoleti mdomoni mwa Suzie.
“Susan Jones, ulimshawishi ma’mdogo akununulie chokoleti tena, sivyo?” Suzie akapepesa macho yake yasiyo na hatia. “Hapana, Mama. Unanisingizia!”
“Huna akili Suzie.” Lucas alimtizama dada yake na kusema. “Ona. Hukusafisha chokoleti pembeni mwa mdomo wako.”
Kwa mshtuko, Suzie alilamba chokoleti kwenye ukingo wa mdomo wake haraka. Muda si muda alikuwa msafi na kusema bila hatia, “Sikula. Godmother alikula chokoleti na kunibusu baadaye.”
Lisa alijipapasa paji la uso wake, akacheka huku akishangaa kwanini amezaa na mtoto wa aina hiyo ambaye alikuwa mjuzi wa kusema uongo.
Lucas alisema, “Unafikiri Mama atakuamini tena, mjinga wewe!”
“Nani mjinga sasa? Sichezi na wewe tena.” Suzie alikoroma. Aligeuka na kumpuuza Lucas.
Lucas alishusha pumzi na kumuuliza, “Mama unaendeleaje huko? Baba alikuletea shida? Unaweza kupambana na kila kitu? Unahitaji nije nikusaidie?”

Lisa alishindwa cha kusema. Mtoto wake alikuwa na maswali kama polisi.
Wakati huu, mtu alikuwa akipiga hodi mlango kwa teke.
“Mpenzi, nina jambo la kufanya sasa. Tutaendelea usiku wa leo. Muah!”
Lisa akakata simu. Alipokaribia tu mlangoni, mlango ulipigwa teke kwa nguvu. Alvin aliingia ndani huku uso wake ukiwa na huzuni, macho yake yakionyesha ukali.
“Lisa unathubutu vipi kumsababishia Sarah matatizo?! Unabipu kifo, huh?" Alvin alinyoosha mkono wake mkubwa kuibana shingo yake bila kusita.
Lakini, Lisa alikuwa tofauti na hapo awali. Alimpanchi kwa uangalifu kabla hajamfanyia chochote.
Alipogundua umachachari wake, Alvin alitania, "Inaonekana kama Maya yuko sahihi. Umepata ujuzi fulani kwa miaka hii michache, lakini uwezo wako si lolote kwangu.”
"Siku zote nimekuwa nikifahamu ujuzi huu na hakuna ubaya kuuweka katika vitendo kwa ajili ya kujilinda sasa hivi." Lisa aliinua uso wake mzuri wa umbo la mviringo. Alipepesa macho yake mazuri na kutabasamu kwa busara. “Hubby, umekuwa si mwaminifu baada ya kuachana na mimi kwa miaka michache. Una

mawazo ya kumuua mkeo mchana kweupe, huh?"
“Uliniita nani?” Uso mzuri wa Alvin ulikaribia kubadilika. “Nani anakupa haki ya kuniita hivyo? unaota?.”
“Nasema ukweli tu. Tazama, hiki ndicho cheti chetu cha ndoa.” Lisa akakitoa na kukizungusha.
“Una wazimu, Lisa? Kwanini unanionyesha vitu vya aina hii?” Alvin alimkaripia vikali. Tabasamu gumu lilienea kwenye uso wa Lisa. Maneno hayo yaligonga kengele kwenye kichwa chake. Hapo awali Alvin alikuwa amezoea kumtishia kwa cheti cha ndoa kila alipotaka kudai talaka. Kwa bahati mbaya, kila kitu kilikuwa kimebadilika tangu wakati huo. "Wewe si mke wangu." Alvin alimkubusha.
Lisa alicheka ghafla. “Alvin, ingawa ndoa yetu ilikuwa ni makubaliano tu, lakini nilishawahi kukuomba hata senti? Mawenzi Investments ndicho kitu pekee ambacho mama yangu aliniachia na ndicho kitu muhimu zaidi kwangu, hata hivyo ulimpa Sarah. Unaongeza mafuta kwenye moto. Ikiwa ulitaka kumpa kitu, ulipaswa kumpa kitu ambacho kilikuwa chako wakati huo. Kwanini umpe kilicho changu?”

Kadiri Lisa alivyozidi kuongea, ndivyo alivyokasirika zaidi. Licha ya kujifunza kudhibiti hisia zake kwa miaka hii michache, bado hakuweza kujizuia lakini kupoteza utulivu wake wakati huo.
Alvin ambaye tayari alikuwa amefura kwa hasira, alishindwa kujibu swali lake. "Ningejuaje kuwa kampuni hiyo ndiyo urithi ulioachiwa na mama yako?"
Lisa alitabasamu. "Ni kweli. Hukujua kuhusu hilo. Hujui lolote.”
Alijua kweli. Ni kwamba tu alikuwa amesahau kutokana na kuharibiwa kumbukumbu muhimu. Hata hivyo, asingemsamehe kwa sababu tu alikuwa amesahau.
“Ni sawa ikiwa umeisahau, lakini huwezi kuchukua kilicho changu na kumpa mwanamke wako.” Lisa alifoka.
“Hata hivyo, hukupaswa kumshambulia Sarah,” Alvin alisema kwa uchungu, “Ni kosa lako kwamba ulighushi kifo chako. Sarah alijitahidi sana kuisimamia Mawenzi Investments na ameboresha utendaji wa kampuni kwa kiasi kikubwa.”
"Kwani hakuna watu wengine katika Mawenzi Investments? Hapo awali, Meneja Mkuu Ngololo alifanya kazi nzuri katika kusimamia kampuni. Kwanini mlimshusha cheo?” Lisa

alichukizwa sana. “Sarah alisomea saikolojia na sio usimamizi wa biashara. Ikiwa anataka kusimamia kampuni, anaweza kusimamia New Era Advertisings, hiyo ndiyo inayomhusu. Kwanini anang’ang’ana na Mawenzi Investments?"
Lisa alitabasamu ghafla bila furaha na kujibu, “Anataka tu kuninyang’anya vitu vyangu vyote, sivyo? Anaweza pia kunyakua Ngosha Corporation ya baba yangu pia?”
“Inatosha. Sarah si mtu wa aina hiyo.” Alvin alishindwa kujizuia kumkatisha. "Mwanzoni, alipendezwa na biashara ya uwekezaji. Sikuwa na kampuni zozote za uwekezaji, hivyo nilimwacha amchukue Mawenzi Investments.” “Naam, basi niwashukuru ninyi wawili kwa kuisimamia vizuri Mawenzi Investments kwa niaba yangu.” Lisa alikunja midomo yake bila kutarajia. “Nimpe thawabu gani kwa ajili ya kazi yake ngumu?”
“Lisa, nimekerwa sana na utani wako. Unachukiza.” Macho ya Alvin yalidhihirisha chuki yake kwake.
“Sawa. Ikiwa hutaki kuona upande wangu wa kuchukiza, ni bora uirudishe Mawenzi Investments kwangu haraka iwezekanavyo na kumfukuza Sarah. Nitarudi kwenye kampuni na kupanga upya kila kitu kesho.” Lisa hakuwa na

wasiwasi kabisa juu ya jinsi alivyokuwa akimchukulia.
Alvin alijawa na hasira. Lisa alimfanya aonekane kama alikuwa na hamu ya kumiliki kampuni yake. "Sina haja kabisa kampuni mbaya kama Mawenzi Investments. Baada ya kusema hivyo, ni lazima umuombe msamaha Sarah hadharani kesho.”
Lisa alichimba masikio yake kwa kidole na kusema. “Unataka nimuombe msamaha? Endelea kuota."
"Sitakurudishia kampuni hiyo." Alvin alitoa kicheko jeuri. "Wanahisa wa Mawenzi Investments ni wajanja. Hata ukiitisha mkutano hawatakujali kwa sababu wanapokea maagizo yangu.”
“Sawa basi.” Lisa hakuwa na wasiwasi hata kidogo. Alipeperusha cheti cha ndoa na kuongeza, “Katika hali hii, nitapiga picha na kuposti cheti hiki mtandaoni. Nitadai kwamba bado tumeoana. Miaka mitatu iliyopita, ilibidi niuambie umma kwamba tuliachana kwa sababu ulinitishia na baba. Unadhani watu wataacha kumshambulia Sarah baada ya kipande hiki cha habari kufichuliwa? Nadhani hakuna mtu ambaye amezungumza kuhusu

uhusiano wenu katika miaka michache iliyopita.”
“Usithubutu,” kauli ya Alvin ikabadilika huku akimwonya kwa uchungu.
"Bila shaka, sitaogopa hata kidogo kufanya hivyo." Lisa aliinua kichwa chake huku akifichua uso wa dharau.
Alvin alimtupia jicho na kukamata cheti cha ndoa ghafla. Mara Lisa akageuka na kuking’angania.
Kifua cha Alvin kilimgonga Lisa mgongoni. Huku nywele zake ndefu zikining’inia chini, aliweza kunusa kwa urahisi harufu hafifu ya kama ya maua alipoinamisha kichwa chake. Hakuweza kukumbuka ilikuwa harufu ya maua gani, lakini lilikuwa na harufu nzuri sana. Sio tu kwamba alipendezwa na harufu, lakini pia alitulizwa nayo na kuliwazwa kabisa. Alinukia vizuri zaidi kuliko Sarah.
Alvin alipokuwa akitoka nje kwa muda, Lisa alimsukuma na kukimbilia chumbani kwake mara moja. Akiogopa kwamba angekimbia, bila fahamu alimvuta mkono wake laini na mwembamba kumwelekea. Kutokana na nguvu nyingi za Alvin, aliishia kujigonga

mikononi mwake. Kwa wakati huu, mgongo wake ulikuwa umekwama kwenye kifua chake. Huku akiuma meno alitumia mkono mmoja kumshika Lisa na mwingine kujaribu kumpokonya cheti cha ndoa mkononi.
Sura ya: 322
Lisa alijitahidi kujinasua kutoka kwa Alvin bila kutambua kwamba alikuwa akizunguka katika mikono yake. Akiwa amegundua mabadiliko ndani yake, uso wake ulikuwa tayari umejawa na aibu. "Alvin, wewe ni mtu wa ajabu sana."
Alvin naye alionekana kuwa na aibu na mshtuko sana. Siku zote alikuwa akidhani kwamba asingesisimka tena kwa mwanamke kwa sababu kila alipokutana na Sarah, bila fahamu alihisi kuchukizwa naye. Hata alishuku kuwa hakuwa na uwezo tena wa kumridhisha. Hakutarajia kwamba angesisimka tu kwa kumkumbatia Lisa. Hisia hii ilimfanya adhalilike hasa, na kwa namna fulani alipoteza udhibiti pia.
Akiwa amekasirishwa na matamshi ya Lisa, alisema, “Ni nini kinanifanya niwe mtu wa

ajabu? Wewe ndiye wa ajabu. Mimi ni mwanaume wa kawaida.”
“Kwanini ulitembelea kitengo cha andrology hospitalini asubuhi ya leo,” Lisa alifoka.
Alvin aliona aibu hata uso wake ukatepeta ghafla. Kama angekuwa na uwezo angeyeyuka tu na kupotelea hewani. "Nimekuambia kwamba nilienda huko kumsindikiza Hans."
“Unanichukulia kama mjinga? Kwanini bosi amsindikize mfanyakazi wake huko?” Lisa alimsukumia mbali. Alimuonyesha mlango wa kutokea na kusema kwa hasira, "Toka nje."
Alvin aliutazama uso wake uliokuwa umekunjamana mithili ya waridi zuri lililokaribia kuchanua. Alihisi usumbufu fulani. “Kwanini nitoke?”
"Hakuna uhusiano wowote kati yangu na wewe." Lisa alijitahidi kumkumbusha ukweli ambao hata hivyo Alvin hakuwa tayari kuukubali.

“Nina uhakika bado nina uhusiano na wewe. Bado una cheti cha ndoa yetu kwa hivyo kishria wewe bado ni mke wangu.” Alvin alifoka ghafla na kumsogelea taratibu.
Lisa alishangazwa na tabia yake ya kukosa aibu. “Alvin, kwanini unakosa adabu? Umekiri kuwa mwaminifu kwa Sara. Hata kama hutaki kuniheshimu mimi, kwanini hutaki kumheshimu Sarah basi?”
Jina 'Sarah' lilionekana kama ndoo ya maji baridi iliyomwagiwa juu yake. Alikunja uso kwa hatia na kukodoa macho ghafla. Ni lazima alirogwa atoe maneno ya kipuuzi kama yale. “Nilikuwa nakukebehi tu. Sura yako tu kwanza inanichukiza sana”
Kwa hayo, Alvin alikoroma na kuelekea bafuni. Lisa alitoa kicheko cha dharau. Alidai kuwa sura yake ilimchukiza kwanini sasa anatumia bafu lake? Huenda mwanamume huyu alitaka kwenda kujidhuru tena bafuni mwake ili kupunguza hasira. Ugonjwa wake ulionekana kuwa haujamwisha.

Baada ya kusubiri na kuona kimya kwa dakika kama kumi hivi, Lisa aliamua kwenda kuchungulia. Alvin alikuwa bado yupo ndani. Kwa hali aliyomkuta nayo, alihitaji kweli hata kutembelea kitengo cha andrology? Alvin alikuwa anajaribu kupoza msisimko wake wa mapenzi kwa kujichua, na mtambo ulikuwa umesimama vizuri tu. Sasa kwanini kulikuwa na tatizo la unyumba kwenye uhusiano wake na Sarah? Alikuwa akikwama wapi, au ni kwa sababu Sara alikuwa mgumu kuridhika? Lisa alitoa mshtuko.
Wakati huo, Lisa alihisi njaa ghafla. Hakuwa amekula chakula cha mchana, kwa hiyo alielekea jikoni kupika makaroni, akaweka na jibini, kisha akaongeza na soseji. Dakika ambayo Alvin alitoka bafuni kwa unyonge, harufu ya makaroni na jibini na soseji ikitoka jikoni mara moja ikajaza pua yake. Harufu ya ajabu mara moja ilimfanya awe na njaa.
Alitembea hadi jikoni na kumwona Lisa ambaye alikuwa amevaa kitop tu chepesi sana na kipensi kifupi sana, akiwa anakata soseji. Alionekana kupendeza huku nywele zake zikibembea kama mkia wa farasi. Hisia

ambazo alikuwa ametoka kuzituliza bafuni zilibubujika tena ndani yake.
Alvin aliuma meno yake na kwenda kwa Lisa. Kisha, akasema bila chuki, “Unajaribu kunitega?”
“Huh?” Lisa alishikwa na mshangao kabisa. Macho yake meusi ya kupendeza yalifichua hali ya kutokuwa na wasiwasi na kujiamini. Hakutambua jinsi alivyoonekana kuwa mwenye kuvutia wakati huo. "Nikutege kwa lipi?"
"Unanifahamu vizuri kuliko mtu mwingine yeyote." Alvin alikazia macho yake kwenye uso mzuri wa Lisa na kumdhihaki kabisa. Alitamani hata ayashike matiti yake yaliyotuna na kukinyanyua kile kitop chepesi kifuani
kwake. Midomo yake nayo ilikuwa kama inamualika kwa busu zito.
Lisa alitazama chini bila kumjali. “Hatimaye umemaliza kumwaga wazungu wako bafuni kwangu, huh?”

Alvin alimtazama kwa ukali, uso wake ukawa mbaya bila yeye kujitambua. “Lisa Jones, una mawazo gani? Huna aibu?”
Lisa aliinua macho yake. Kimsingi hakuwa akimpenda, lakini kwanini alikuwa akipandsha hisia baada ya kumuona? Alikuwa akijaribu kupoteza uvumilivu wake kidogokidogo? “Nilikuwa nawaza tu kwamba kwa hali hiyo, huna haja ya kutembelea kitengo cha andrology! Sarah ndiye anapaswa kumuona daktari. Kama mwanamke, hakuna haja ya kutamani sana. Kwa hali yako, anapaswa kuridhika.”
“Sarah hafanani na wewe,” Alvin alimdhihaki kwa hasira licha ya kuufahamu ujumbe wake.
Lisa hakuwa na neno. Alvin alikuwa ameishi naye kwa muda kabla hajaondoka na hata akapata watoto pamoja. Aliijua hamu yake na uwezo wake. Wote wawili hawakuwa wamezowea mbio za marathoni kitandani. Huenda Sarah alikuwa ni mtu aliyependa kuzama kina kirefu kwenye bahari ya mahaba kabla hajaibuka nchi kavu na Alvin hakuwa na uzoefu huo. Lisa alianza kutilia shaka hilo

lakini hakuwa tayari kulijadili akilini mwake, akabadili mada.
“Umeamuaje?” Lisa aliuliza ghafla.
Alvin alipigwa na butwaa kwa muda, huku uso wake ukiwa umekunjamana. "Unazungumza juu ya Mawenzi?"
"Ni juu yako ikiwa utanirudishia, lakini haiwezekani kwangu kuomba msamaha kwa Sarah," Lisa alisema bila kujali, "Baada ya kusema hivyo, uvumilivu wangu una mipaka yake. Unapaswa kuamua kesho. Vinginevyo, ninaogopa sitaweza kudhibiti mikono yangu na kuishia kufichua maovu mliyoyafanya.”
“Lisa Jones, unafahamu hata mipaka yako? Unathubutuje kunitisha?!” Alvin alipandwa na hasira, macho yake yakiwa yamejawa na huzuni.
“Kwanini? Unapanga kuniua, huh?” Lisa hakuwa na woga.
Uso mzuri wa Alvin ukaingia hasira. Machoni mwake, je, alikuwa kichaa tu aliyeua watu

kinyama? “Unafikiri sitaweza kufanya hivyo?” alimuonya vikali.
“Najua unaweza kufanya hivyo. Hakika sitatilia shaka, lakini huwezi kuninyonga kwa urahisi sasa.” Lisa alitabasamu. "Labda mimi si mkubwa kama wewe, lakini tukianza kushambuliana, itawatahadharisha majirani na mtaa mzima. Zaidi ya hayo, tangu ulipoingia katika mtaa huu, mienendo yako yote imerekodiwa kwenye kamera za uchunguzi. Nikifa, hakika hutaweza kuondoka salama. Mwenyekiti Kimaro, hata kama unapanga kuficha ukweli kupitia hongo, tukio hili bila shaka litapiga kengele. Kwa mfano, familia ya Campos, ambayo imekuwa ikipanga njama na kugombea kuwa Mtanzania mahiri zaidi nchini Kenya, pengine itachukua fursa hiyo kuharibu sifa yako na hata... kukuweka kuzimu.”
"Ni uchambuzi gani wa kina umetoa." Alvin alikasirika sana. Ina maana alikuwa na mawazo kwamba angemuua? Ingawa hakuwahi kufikiria kufanya jambo lolote lisilo halali, nia yake ilikuwa nini kumkasirisha?
"Asante." Lisa aliinamisha kichwa chake na kuendelea kukata soseji. "Hapo awali, uliweza

kunitisha na baba yangu na Pamela. Lakini sasa kwa kuwa baba yangu amepata nafuu na Pamela hayupo, niko peke yangu. Sina cha kupoteza.”
Alvin alimkazia macho mgongoni. Hakuwa na udanganyifu kwamba maneno yake yalikuwa ya kweli. Hakika, hakuna kitu tena ambacho angeweza kutumia kumtishia mwanamke huyu.
Walikaa kimya kwa nusu dakika kabla ya Alvin kusema, "Ninaweza kuahidi kuirudisha Mawenzi kwako, lakini lazima tupeane talaka."
"Hapana." Lisa alimkataa kabisa bila kuinua kichwa chake.
Alvin alilipuka kwa hasira. “Kuwa na shukrani, tayari nimeshafanya makubaliano.”
Lisa aligeuza kichwa chake na kuinua macho yake. "Kama usingemteua Sarah kama Mwenyekiti wa Mawenzi, ningekubali talaka. Lakini ulinikasirisha, haswa leo nilipojua kuwa ulimfanya Cindy kuwa balozi wa Mawenzi. Una maana gani kukusanya watu hao ninaowachukia na kuwaweka kwenye kampuni

yangu? Kwanini usimwombe Lina ajiunge pia? Kwa kuwakusanya hao wanafiki watatu, unaweza kutimiza matakwa yako yote.”
Akiwa ameudhishwa na shutuma zake, Alvin alidhihaki, “Kwa hiyo sasa unamchukia kila mtu niliyemteua? Ulikuwa umekufa, unategemea kampuni ingeongozwa na nani?"
Sura ya: 323
Kusikia dhihaka za Alvin kunaweza kumfanya Lisa akasirike sana. Kwa hiyo, aliamua kumpuuza na kuzingatia kuandaa chakula chake.
Alvin akaendela. “Ninaweza kukata rufaa kwa mahakama ukikataa kutia sahihi hati za talaka. Wenzi wa ndoa wanaweza kukata rufaa kwa hakimu baada ya kuishi tofauti kwa miaka miwili.”
“Hakika tukutane mahakamani. Lakini mambo yatapendeza iwapo wanahabari watagundua kuwa bado tumefunga ndoa. Sitakuwa na jukumu la kulinda sifa ya mpenzi wako tena.” Lisa alijibu bila kujali.

Jambo hili lilimkasirisha Alvin. "Lisa, nifanye nini ili utie sahihi kwenye karatasi?"
"Hmm, bado sijafikiria juu yake." Alimsukuma nje ya njia na kuanza kupasha moto sufuria.
Mara baada ya mafuta kuwashwa, aliweka madikodiko ndani yake, na harufu ya kupendeza ilijaa nyumba nzima. Ghafla, tumbo la Alvin lilianza kunung'unika.Lisa alimuangazia tabasamu la fumbo na akalirudisha kwa mng'ao wa aibu.
"Sikula chakula cha mchana kwa sababu nilikuja hapa kuzungumza nawe." Alvin alilalamika.
“Oh.” Lisa aliguna tu. Aliweka viazi kwenye sahani, akasafisha sufuria, na kuanza kupika samaki wa kukaanga.
Hisia za Alvin zilishambuliwa na harufu nzuri kwa mara nyingine. “Ongeza nyingine zaidi. Nina njaa."
"Hiyo sio kazi yangu." Hakuwa na la kusema.

“Mimi ni mume wako kisheria. Bila shaka, ni kazi yako.” Ilikuwa ni muda mrefu sana tangu awe na hamu ya kula hivyo akajitetea bila haya. "Kuhakikisha mume wako amelishwa vizuri ni moja ya majukumu yako."
"Na hiyo ni sheria gani, Wakili Kimaro?" Lisa hakuweza kumvumilia tena. Aligeuka na kupiga tai yake kwa mkono wake mdogo. Macho yake yasiyopendeza lakini mazuri ghafla yalionekana kuvutia. “Wakili Kimaro, usisahau kwamba ulikuwa unajadili kunitaliki sekunde moja iliyopita,” alimkumbusha kwa fadhili.
"Na haikufaulu, sivyo?" Alichagua kutokuwa na haya hadi mwisho.
Lisa alimtazama kwa jicho kali kabla ya kuanza tena kupika. Hakupika zaidi ya kawaida kwa ajili yake tu. Baada ya kupika aina nyingine mbili ya chakula, alivitoa vyote kwenye meza ya chakula.
“Mbona chakula hakitoshi?” Alvin alionekana kutofurahishwa.

"Kwani nilisema ni kwa ajili yako?" Lisa alichukua sahani na kuanza kufurahia chakula chake. Ingawa alikuwa amepika sana nyumbani alipokuwa akiishi nje ya nchi, viungo vya huko vilikuwa vichache na havikuwa ladha nzuri kama vile ambavyo angeweza kupata kutoka nyumbani. Soseji hii ya kienyeji, haswa, ilimpa hamu kubwa.
Alvin akamkazia macho yule mwanamke aliyekuwa akifurahia chakula kile. Akiwa amechanganyikiwa, alikwenda kwenye kabati na kuchukua sahani kubwa. Lisa nusura akiteme chakula kinywani mwake alipoinua kichwa chake na kuona ukubwa wa sahani mikononi mwake.
Kwa umakini?
Je, Alvin alikuwa amejinyima njaa katika miaka mitatu iliyopita? Je, alikuwa na njaa hivi kwamba akachagua sahani kubwa zaidi jikoni mwake? Hatimaye Lisa alielewa Suzie alipata wapi hamu yake kubwa ya kula.
“Unapanga kula chakula changu chote?” Lisa alikasirishwa sana na mzaha huo wa Alvin.

“Hukupika cha kutosha,” Alvin alisema kabla ya kujisaidia chipsi na kipande kikubwa kabisa cha samaki bila kusahau soseji za kutosha. Ilikuwa imepita muda mrefu sana tangu apate chakula chenye ladha ya kumshibisha.
Kwa kawaida Alvin hakuwa na hamu ya kula. Pia alikuwa mchaguzi sana kwa vyakula ambaye hakuweza hata kuridhika na wapishi maarufu. Hata hivyo, chakula cha Lisa kilipopikwa nyumbani kilikuwa kitamu sana.
Chipsi zilizokauka kidogo zilipendeza sana. Bila kusahau soseji zilizochomwa kwa viungo anuai. Alijiuliza alinunua wapi viungo hivyo. Muda si muda, alimaliza kila kitu kwenye sahani yake—pamoja na sahani nyingine kwenye meza.
Lisa alikasirika. “Kwa hiyo umeamua kula mpaka chakula cha mpishi, sivyo?”
“Nilikuambia uongeze zaidi lakini hukusikiliza. Baada ya kuweka kipande cha mwisho cha chipsi kinywani mwake, alishika kitambaa ili kufuta midomo yake maridadi kwa maringo. “Hata hivyo bado sijashiba.”

Lisa alihisi kifua chake kikidunda kwa nguvu huku wazo la kupindua meza likiingia akilini mwake.
Alvin alimtazama yule mwanamke kwa ukimya. “Ili kukushukuru kwa chakula hiki, nitairudishia Mawenzi Investment kesho. Lakini naomba niweke wazi kwamba sitishiwi na wewe.”
"Ha." Lisa alidhihaki, bila shaka hakushawishika. Hakuridhika na tabasamu lake la kejeli.
“Mbali na hilo, nakuonya usiwe mkorofi tena kesho. Sitakuwa mwema nikigundua kuwa unamnyanyasa Sarah tena.”
Kisha akainuka na kuelekea mlangoni. Alipokaribia tu kuufikia mlango, aligeuka na kutazama nyuma. "Lakini ninaogopa kusema kwamba Mawenzi Investments hivi karibuni itaporomoka kutoka kwenye nafasi yake ya juu bila msaada wangu. Nitakusubiri uniombe msaada.”
"Haitatokea." Lisa alibisha kwa tabasamu tulivu.

Kidokezo cha kejeli kiliangaza machoni pa Alvin kabla ya kuondoka kwenye nyumba hiyo. Aliondoka akiwa ameshiba kabisa na kuridhika kwa chakula kilichopikwa na mpishi wake mkubwa duniani.
Hata hivyo, Lisa hakuwa na wasiwasi. Alikuwa amekata tamaa juu yake kwa muda mrefu. Baadaye, alipiga simu kwa Meneja Mkuu. "Kikao cha bodi ya kesho kinafanyika kama ilivyopangwa."
•••Nje ya jengo•••
Hadley aligeuka kuongea mara baada ya Alvin kurudi kwenye gari. "Niligundua kilichotokea miaka mitatu iliyopita. Ilikuwa ni Jack Kimaro ndiye aliyewahonga wafanyakazi wa hospitali ili kughushi kifo cha Lisa Jones.”
“Ni kweli alikuwa yeye?” Hasira kali ilijaza macho ya Alvin. Si ajabu aliona ni ajabu kwamba Jack alikuwa ameambatana na Mzee Kimaro pamoja na Bibi Kimaro hospitalini siku hiyo.
"Nipeleke kwenye kampuni." Alvin alimwamuru Hans.

Sura ya: 324
Hans akampeleka Alvin moja kwa moja kwenye ofisi za KIM International.
Bang! Mlango ulifunguliwa nje ya bluu. Jack, ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye dawati, alitazama juu. Muda si mrefu alipata utulivu baada ya kuona hali ya mawingu usoni mwa Alvin.
“Mwenyekiti Kimaro, kuna kitu—”
Alvin alimpiga ngumi ya uso kabla hajamaliza sentensi. Jack alishikwa na machozi. Pembe za midomo yake zilianza kuvuja damu. Katibu wa mlango haraka akampigia simu Makamu Mkurugenzi Lea Kimaro kwa siri.
“Alvin, usifikiri nakuogopa kwa sababu tu una mamlaka kamili juu ya Kampuni hii. Mimi pia ni sehemu ya familia.” Jack alikuwa akitetemeka kwa hasira.
“Unadhani kwanini nilikupiga?” Alvin alimshika kola Jack kwa fujo. “Ulinidanganya kwa kufeki kifo cha Lisa miaka mitatu iliyopita. Jack,

nimekuwa mkarimu kupita kiasi kwako sivyo? Nimekusamehe kwa mambo magapi na bado unanifanyia haya?”
Jack aligeuza midomo yake kuwa tabasamu la kijeuri. “Una jeuri hata ya kusema hivyo? Kama nisingeingilia kati ungekua umeua mtu miaka mitatu iliyopita...”
“Nilikuwa nikimtibu lakini wewe ulisaidia kughushi kifo chake. Kwanini? Ulikuwa na mpango gani wakati huu? Jack, unavutiwa naye?"
Kwa sababu fulani, wazo la kaka yake wa kambo kuwa na hisia kwa Lisa lilifanya damu yake ichemke. Alihisi kumwangamiza mtu huyo sekunde hiyo hiyo.
“Kumtibu! Hivyo ndivyo ulikuwa unamtibu?” Jack alimkazia macho. “Huna aibu? Je, unajua hali aliyokuwa nayo nilipomuokoa kutoka hospitalini? Alikuwa amechanganyikiwa sana hata mimi sikuweza kumtambua. Nilimleta ili kuchunguzwa na daktari mwingine na niliambiwa kuwa hali yake ya akili haikuwa sawa kwa sababu alikuwa ametumia dawa nyingi za akili bila mpangilio. Hali yake hatimaye iliimarika baada ya matibabu ya nusu

mwaka. Daktari alisema hakuwa mgonjwa hata kidogo. Je! unajua kuwa mtu wa kawaida anaweza kupata wazimu baada ya kutumia dawa za akili? Huenda angepagawa ikiwa hilo lingeendelea tena.”
Hilo lilimshangaza Alvin. “Hili haliwezekani. Unanidanganya tena. Huu hauwezi kuwa ukweli kamwe." Alikataa kuamini kwamba Sara angemdanganya. Ikiwa hii ilikuwa kweli... Alitetemeka kwa mawazo ya uso mzuri na usio na hatia wa Sara.
"Hakuna ninachoweza kufanya ikiwa huniamini." Jack alichanganyikiwa kweli. Alvin alikuwa mwenye kipaji kwa kushughulika na mambo ya biashara lakini alionekana kuwa mburura kabisa katika masuala ya mahusiano. "Hata hivyo, nilichagua kumwokoa miaka mitatu iliyopita kwa sababu kwanza kabisa, nilihisi vibaya kwamba ulimfungia ndani kila wakati. Pili, nilijihisi kuwa na hatia kwa kumsababishia kuharibiwa uso kwa njia isiyo ya moja kwa moja.”
"Ninakumbuka ghafla kuwa mara nyingi ulisafiri nje ya nchi katika miaka ya hivi karibuni. Ulikuwa ukimtembelea kwa siri, huh?” Alvin

alimkazia macho Jack. "Kweli huna hisia naye?"
"Kwa hivyo ikiwa nina hisia naye?" Jack alitabasamu kwa ujeuri na kuinua macho yake. “Wewe inakuhusu nini? Huridhiki na Sarah? Au, inawezekana kwamba wewe—”
“Hapana. Sitaki kuonekana kuwa tumechangia mwanamke pamoja na ndugu yangu.” Alvin alitema maneno hayo makali kupitia midomo yake myembamba. "Familia ya Kimaro pia haitaruhusu hilo kutokea."
“Mambo yangu binafsi hayakuhusu wewe,” Jack alisema, bila kupendezwa na jambo hilo.
"Jack usinijaribu." Alvin alimpiga Jack kifuani. Mwisho alikasirishwa na tabia yake ya kijeuri.
“Kuna nini nyie wawili?” Sauti ya juu ya Lea ilijaa chumbani. Aliwasogelea na kuona damu kwenye midomo ya Jack. Kwa hasira, alinyosha mkono kumpiga Alvin usoni.
Alvin akamshika mkono mara moja na kumkazia macho. "Unapaswa kutumia wakati wako wa bure kumtia adabu mume wako."

Lea akatetemeka. Ni kweli, alishangazwa sana na jinsi familia ya Campos ilivyokuwa imeongezeka kwa thamani zaidi ndani ya miaka kadhaa. Hata hivyo, hakuamini kuwa Mason ndiye aliyekuwa nyuma yake. Alikuwa akimpenda mwanaume huyo tangu enzi zao za chuo kikuu! "Yeye hahusiki katika chochote kinachotokea na Kampuni la Campos. Kwanini usimwache peke yake?”
“Bado huoni ukweli baada ya miaka yote hii? Sielewi ni vipi niliweza kuzaliwa na mtu mjinga kama wewe.” Alvin alitikisa kichwa bila kujali kabla ya kuondoka.
“Fedhuli wewe!” Lea alikuwa akitetemeka kwa hasira.
“Jack, uko sawa? nyie wawili mmegombaniia nini?” alihoji kwa wasiwasi.
“Ni sawa, Mama, usijali kuhusu hilo. Hataniletea matatizo tena.” Jack alilazimisha tabasamu. "Unaweza kuenda tu."
Baada ya Lea kuondoka, Jack alishusha macho yake chini, karibu kuivunja kalamu

iliyokuwa mkononi mwake. Kwa kweli, alikasirika sana kwamba Alvin aliweza kupata ushindi juu yake kila wakati. Aliwaza juu ya sura ya usoni na ya kiburi ya Alvin wakati anaingia ndani ili kumpiga leo.
Ilikuwa ni wakati wa kutoka kazini. Jerome akampigia ghafla. "Jack, pole, nilisikia umepigwa ngumi."
“Umesikia kutoka kwa nani?” Jack alikodoa macho.
Jerome akapumua. “Sio mimi tu. Watu wengi maarufu hapa Nairobi wamesikia jinsi Alvin alivyingia ofisini kwako na kukupiga. Hakuna kitu kama siri mahali hapa."
Jack alikunja vidole vyake kwenye simu. Huko Nairobi, kila mtu alimchukulia Jack kama mzaha.
"Pamoja na kwamba wewe ni mdogo wake, lakini alivuka mpaka alipokupiga. Kwanini hakuweza tu kuzungumza na wewe mambo kwa utulivu? Haonyeshi heshima yoyote kwako hata kidogo. Jack, uko tayari kukaa chini yake maisha yako yote? Kwa kweli... wewe ndiye

autakayefuata katika familia ya Kimaro ikiwa Alvin atashindwa.”
“Unajaribu kusema nini hasa?” Jack aliuliza kwa wasiwasi.
“Sisi ni ndugu! Na tunaweza kufanya kazi pamoja,” Jerome akajibu, “Angalia, nimepata sapoti kubwa kutoka kwako hapo awali na familia ya Campos imeongezeka na kuwa familia ya pili tajiri zaidi nchini Kenya katika miaka michache tu. Msimamo wangu katika jamii hii umebadilika.
Je, hutaki kuwa kama mimi?”
“Uko sahihi. Hakika nilikudharau zamani,” Jack alisema kwa dhihaka, “Niambie ukweli. Unataka nini toka kwangu?"
"Wewe ni mtu mwerevu, Jack, kwa hivyo sitakuwa na hila na wewe. Je, unaweza kunipatia nyaraka za kihandisi za Cement mpya ya Oceanic ambayo Maabara ya KIM International inaunda kwa sasa? Niamini, hii ndiyo nafasi nzuri ya kumwangamiza Alvin kama hutaki kuonewa naye maisha yako yote?”

“Unaniwazia sana. Alvin hajawahi kunipa nafasi ya kuingilia masuala ya uvumbuzi miaka hii ya hivi karibuni. Amekuwa akinilinda sana.” Jack akainama nyuma kwenye kiti cha ngozi.
"Unaweza kufikiria njia, Jack. Tunaweza kujitengenezea nafasi,” Jerome aliendelea kushawishi.
Jack aligusa jeraha karibu na midomo yake, giza likaangaza machoni pake.
Saa kumi na mbili jioni, Alvin alirudi kwenye jumba lake la baharini. Alisikia harufu ya nyama ikipikwa jikoni. Sarah alitoka jikoni akiwa amevalia aproni nyepesi ya pinki iliyokuwa na katuni ya paka. Gauni jeupe alilokuwa amevaa chini yake lilionekana safi na lla kupendeza.
Lakini, mwanamume huyo alifikiria bila kujua juu ya Lisa ambaye alikuwa akipika jikoni mapema siku hiyo. Nywele zake nadhifu mithili ya mkia wa farasi na nguo za kupumzikia alizovaa, na jinsi alivyokuwa anafanana na mama mwenye nyumba ambaye alikuwa akipika...vilimfanya Alvin apotelee kwenye mawazo ghafla.

“Unafikiria nini? Unaonekana umechanganyikiwa.” Sarah alimwendea na kumpiga kifua chake kwa mahaba.
"Nilikuwa nikishangaa kwanini umeamua kupika usiku wa leo." Alishangaa kwani Sarah hakuwa na utaratibu wa kupika nyumbani.
"Kwanini isiwe hivyo? Imekuwa muda mrefu sana tangu tuwe na chakula cha jioni kilichopikwa nyumbani. Nilipika nyama ya nguruwe usiku wa leo. Tutakula na kushushia na mvinyo mwekundu baadaye, sawa?” Alisema akitabasamu.
Sura ya: 325
“Hakika.” Maneno ya Jack yalimjia akilini mwake huku akiitazama sura ya Sarah. Lisa hakuwa na huzuni miaka mitatu iliyopita. Akili yake iliyumba tu kwa sababu ya dawa zote za akili alizolazimika kutumia.
Kama huu ulikuwa ukweli...
Kisha Sarah alimdanganya Alvin kuhusu mfadhaiko wa Lisa alipomshawishi kumpeleka

mwanamke huyo kwenye hospitali ya wagonjwa wa akili.
Kama Lisa 'asingekufa' miaka mitatu iliyopita, angeweza kumrudisha kwenye hospitali ya magonjwa ya akili na hilo lingemfanya awe na wazimu. Kuwaza juu ya hili kulitosha kumfanya ashtuke.
"Kuna nini? Mbona unanitazama hivyo?" Sarah alihisi wasiwasi alipomtazama.
“Sarah, je, kweli Lisa alishuka moyo miaka mitatu iliyopita?” Ghafla alimtazama kwa umakini. Mwanamke huyo alifadhaika lakini alidumisha utulivu.
“Huniamini? Akainamisha macho yake
chini. Alitingisha midomo yake na kusema. “Ni kweli, alipokwenda hospitali miaka mitatu iliyopita nilifikiria kumfanyia uchunguzi sahihi lakini sikuthubutu kumsogelea baada ya kunimwagia maji ya moto, siwezi kukuambia. uhakika kwamba kwa hakika alikuwa ameshuka moyo lakini alionyesha dalili zinazofaa. Nina hakika wafanyakazi katika hospitali ya magonjwa ya akili wasingempokea

isipokuwa wangekuwa na uhakika wa hali yake. Haikuwa juu yangu tu."
Alvin alinyamaza baada ya hapo. Hatimaye Sarah alijisikia ahueni sasa baada ya kuonekana amejiamini. Hata hivyo ilimbidi kuwa makini baada ya kuulizwa swali hili bila kutarajia. “Isitoshe, hakuna mtu mwenye ugonjwa wa akili ambaye angetaka kukiri. Ulikuwa hivyo... ”
“Sawa, wacha tule,” akakatiza. “Hakika, nitakutengea chakula.”
Muda si mrefu alijitokeza tena kutoka jikoni, alikuwa ametia bidii kwenye chakula, hata kupamba meza kwa vikorombwezo mbalimbali. Hata hivyo, Alvin alijikuta hataki kula tena baada ya kuonja mara moja tu. Si kwamba chakula kilikuwa cha kutisha. lakini kwa namna fulani, chakula cha mchana kilichoandaliwa na Lisa mchana wa siku hiyo kilikuwa cha kupendeza zaidi kwa kulinganisha na cha Sarah. Sarah alimtazama kwa macho ya kuuliza.

"Bado kichwa chako kinauma?" Alvin alibadilisha mada ya mazungumzo.
Tabasamu la aibu lilienea usoni mwake huku akigusa nywele zake bila fahamu. “Najisikia vizuri...”
“Samahani kukuweka katika hilo,” alisema kwa hatia, “Tayari nimewajulisha wanahisa wa Mawenzi Investments kwamba Lisa atakuwa anachukua nafasi yake, anaweza akakutaka uondoke baada ya kupata mamlaka tena kesho na usibishane naye. Ukipenda kuendelea kufanya biashara ya majengo, naweza kukuanzishia kampuni nyingine kesho."
Tabasamu likaganda usoni mwake. “Mbona... ghafla sana?”
"Kampuni hilo ni yake hata hivyo. Nilichukua tu madaraka nikifikiria kwamba amekufa. Sitaki usumbufu zaidi kutoka kwa wanawake yule. Natumai hautajali." Alvin alimtazama Sarah kwa jicho la kikauzu.
"Hapana." Sarah alionekana kutokuwa na wasiwasi ila kiukweli alikuwa amepandwa na

hasira. Hakutegemea Alvin angeachana na Kampuni hilo haraka kiasi hicho. Je ni biashara ya nyumba aliyokuwa anaitaka? Sivyo hata kidogo. Alichokuwa anakitaka ni kila kitu cha Lisa. Alifurahia tu hisia za kupokonya kila kitu alichokuwa nacho yule mwanamke.
Sarah alimtupia jicho Alvin ambaye alionekana kuwa Seriuos kuhusu hilo.
"Babe, ninasikitika kuwa Bi Jones atafurahi sana. Alinionyeshea dharau mbele ya kila mtu leo," Sarah alisema mara moja akionyesha masikitiko makubwa.
Alvin alijisikia vibaya lakini haraka akaeleza, "Sina jinsi, ananitishia na cheti cha ndoa. Nisipomkabidhi. Kampuni kwake, atatangaza ukweli kwamba nilimlazimisha kutangaza hadharani kwamba tuliachana wakati huo ilihali haikuwa kweli. Sifa yako itaathiriwa zaidi kama hilo likitokea."
"Sawa, haijalishi," Sarah alijibu huku akihema.
“Sikuwa na wazo kwamba ulikuwa ukinifanyia hivi. Pole.”

Sarah alionekana kuguswa lakin bado alikuwa amechanganyikiwa.
Kwa kweli, alikasirika.
Kamwe hakutarajia uamuzi wake miaka mitatu iliyopita wa kumlazimisha Lisa kuuambia umma kwamba alikuwa ameachana na Alvin angerudi kumng'ata mwishowe.
“Sawa... ataendelea kukutisha kwa hili mpaka lini? Atakupa talaka kweli?” Machozi yalitiririka ghafla mashavuni mwake. “Mimi na wewe tumefahamiana kwa zaidi ya miaka 20 na tumekuwa wapenzi pamoja kwa zaidi ya miaka kumi. Ni lini hatimaye... utanioa?”
“Nitajaribu niwezavyo kumtaliki. Alvin akamkabidhi kitambaa cha kujifutia machozi huku akijisikia hatia sana. "Tayari nina mipango, kwa hivyo hupaswi kufikiria kupita kiasi." “Sawa. Kweli, imekuwaje leo ... hospitalini?" alihoji kimya kimya.
Uso wake mzuri ulianguka ndani ya sekunde chache huku akiweka kichwa chake chini. "Ninatumia dawa za kutuliza maumivu."
"Basi sawa."

Furaha ilikuwa imeandikwa usoni mwa Sarah lakini Alvin alikula chakula kidogo sana haraka kabla ya kupanda juu. Sarah alikunja sura yake, akitazama kipande kikubwa cha nyama iliyobaki.
•••
Siku iliyofuata katika Kampuni ya Mawenzi.
Lisa alipita kwenye lango kuu la kuingilia akiwa amevalia suti nadhifu ya biashara. Aligonga dawati la ofisi ya mapkezi huku akipita. Mhudumu wa mapokezi toka jana yake alitetemeka huku akiinua kichwa
chake. "Mwenyekiti Jones."
“Umeikumbuka sura yangu? Natumai sihitaji kuweka miadi kabla ya kuja tena wakati ujao.” Alitabasamu kabla ya kuelekea kwenye lifti.
Mhudumu wa mapokezi alihisi miguu yake ikiishiwa nguvu. Alikuwa na hofu ya kuachishwa kazi alipopata habari asubuhi ya siku hiyo kwamba Lisa ndiye angekuwa mwenyekiti mpya. Kwa bahati nzuri, haikutokea.

Baada ya kuingia kwenye chumba cha mikutano, Lisa aligundua kuwa wanahisa wote walikuwa wamefika. Sarah alikuwa ameketi kwenye kiti cha kwanza upande wa kulia. Wanahisa wengi walikuwa wamekusanyika wakijikombakomba kwake.
"Mwenyekiti Njau, nilipoenda kwa safari ya kikazi nje ya nchi mara ya mwisho, niliona mkoba huu ambao nilifikiri ungekufaa sana."
"Mwenyekiti Njau, huu ni mchoro halisi kutoka kwa mchoraji maarufu Hilton Johan. Inavyoonekana, kazi zake za sanaa zinagharimu mamilioni ya shilingi na ni ngumu sana kuzipata. Ninafahamiana naye kibinafsi, kwa hivyo hapa kuna zawadi kidogo kwa ajili yako."
“Mwenyekiti Njau, nilinunua chupa hii ya mvinyo mwekundu kutoka nje ya nchi. Inakaribia miaka 40.”
Lisa aliketi kwenye kiti cha ngozi. Alijimiminia kahawa na kurudisha chupa kwenye meza kwa sauti kubwa. Clang!

Kila mtu katika chumba cha mkutano aligeuzia mwelekeo wake kwake.
“Haya nyie. Acheni kukusanyika karibu yangu. Tuna mkutano wa bodi leo. Tukukaribishe kurejea kwa Mwenyekiti Jones.” Sarah alijisemesha kwa tahadhari.
Lisa alimtazama mwanamke huyo kwa kero. "Tuna mkutano wa bodi leo. Wewe uko hata kwenye bodi? Nani alikupa ruhusa ya kuwa hapa?"
"Nilikuwa na wasiwasi kwamba usingefahamu kinachoendelea katika kampuni baada ya kuwa nje kwa miaka michache, hivyo nilikuja kukuongeza kasi." Sarah alionekana kufadhaika na kuhuzunika.
Mkurugenzi Gumbo alimtetea, “Miss Jones, ninaelewa kuwa kuna mzozo wa kibinafsi kati yenu lakini hakuna sababu ya kuzungumza juu ya hilo kwenye kampuni. Tunamshukuru sana Mwenyekiti Njau na Mwenyekiti Kimaro kwa kuongeza faida ya kampuni katika miaka ya hivi majuzi. Bei yetu ya hisa ina thamani kubwa sana tunapozungumza.”

"Hiyo ni sawa. Tuliambiwa ghafla kuwa umekufa. Kampuni isingeweza kujiendesha bila kuwa na mwenyekiti mwenye uwezo. Tulimwona Bi. Njau anafaa na kweli ametufaa. Kwa hiyo ni nyema akaendelea kupewa nafasi." Mwanahisa mwingine alisema.
Sarah alizungumza huku kukiwa na furaha ya kujilazimisha usoni mwake, "Mwenyekiti Jones lazima alikuwa na sababu zake."
"Mwenyekiti Njau, wewe ni mkarimu sana kwa kumtetea licha ya jinsi anavyokuchukulia," mwanahisa mwingine alisema. “Baada ya yote, kila mtu alijua kwamba siku moja Sarah atakuja kuwa Bi Kimaro. Kwa upande wa Lisa, ilikuwa ni kosa lake kumwachia Alvin.”
"Hiyo ni sawa. Si ajabu kwamba Bwana Kimaro alikuchagua mwishowe. Wanaume hupenda mwanamke anayejielewa.”
Lisa alimtazama kwa ukali mtu ambaye alitoa maoni hayo. Cha kufurahisha zaidi, alikuwa mwanahisa wa kike anayeitwa Wande.

"Mkurugenzi Wande, maneno yako hayaendani kabisa na jina lako," alisema kwa kejeli.
Mkurugenzi Wande alikasirika alipoelewa maana ya maneno ya Lisa. “Mwenyekiti Jones, unamaanisha nini? Nina makosa kusema kwamba wanaume wanapenda mwanamke anayejitambua?"
“Nimeondoka kwa miaka mitatu tu lakini kila mtu anadhani anaweza kunidharau sasa kwa kuwa mimi siye mwenyekiti, huh? Msisahau ni nani ndiye aliyewaagiza kuwa hapa kwa ajili ya kikao hiki cha bodi,” Lisa alikikumbusha kile chumba ambacho kilikuwa kimejaa watu.
Kila mtu alinyamaza kwa sababu kila mtu alidhani aliyeitisha mkutano huo alikuwa ni Alvin.
“Sarah, ninapendekeza uondoke sasa au nitawaambia wana usalama wakutoe nje,” Lisa alionya kwa upole. “Isitoshe, Alvin si amekuambia? Au nikukumbushe tena wadhifa wangu?”

Uso mzuri wa Sarah ulipauka papo hapo. Alijua kwamba wawili hao hawakuachana, kwa hivyo angeonekana kuwa ni kmada tu ikiwa Lisa angemwambia kila mtu ukweli.
"Hakika, nitaondoka." Aliinuka na kusimama huku akionekana kuwa na huzuni.
Lisa hakusumbuliwa na sura ya chuki iliyotupwa kwake na bodi ya wakurugenzi. "Sawa, kama mwenyekiti wa Mawenzi Investments, ninakuondoa kwenye nafasi yako. Unaweza kutoka hapa baada ya kukabidhi kila kitu.”
"Unakwenda mbali sana," Mkurugenzi Gumbo alisema kwa wasiwasi, "Tunapinga uamuzi huo."
"Hiyo ni sawa. Wanahisa wana haki ya kumpigia kura mwenyekiti,” wengine waliunga mkono.
"Nyinyi nyote mnaonekana kufikiria kuwa mtasamehewa kwa hili kwa msaada wa Alvin, huh?" Macho ya Lisa yalitazama chumba chote.

Wote wakanyamaza. “Sawa, basi nitampigia simu.”
Lisa alimpigia simu Alvin. Katika sekunde chache, sauti yake ya kijeuri ilisikika kupitia spika.
"Huyu ni nani?" Wanahisa walidhihaki. “Mume wake wa zamani hata hakuwa amehifadhi mawasiliano yake. Namna alivyomtendea ilikuwa tofauti kabisa na jinsi alivyomjali Sarah.”
Sarah, ambaye alikuwa karibu kuufikia mlango, alisimama na kutabasamu kwa hasira.
Lisa hakukasirika. Aliongea kwa utulivu kwenye simu, "Ni mimi, Lisa."
“Unajaribu—”
“Bwana Kimaro, uko kwenye kipaza sauti,” alimkatiza, “Sikufikiri kwamba ingechukua miaka mitatu tu kwa wenyehisa wa shirika langu kunikosea heshima. Sina hata mamlaka ya kumfukuza Sarah sasa.”

Alvin aliyekuwa upande wa pili wa simu alihisi damu ikichemka baada ya kusikia maneno ya Lisa. Alikuwa karibu kubishana wakati Lisa aliendelea, “Hey, ni kitu gani hiki kwenye mkoba wangu? Inahisi kama cheti cha aina fulani."
Sarah aliyekuwa akiingia kwenye lifti nusura apige teke mlango wa lifti uliokuwa mbele yake.
‘Cheti gani? Cheti chao cha ndoa?’ Alvin alijiwazia. ‘Mwanamke huyu alikuwa akimtishia tena. Jamani!’ Aliuma meno na kujilazimisha sauti ya upole huku akisema, “Endelea basi. Unapaswa kuendesha mambo ya kampuni yako jinsi unavyotaka kwa kuwa umerudi. Itakuwa bora ikiwa kampuni itakufia chini ya uongozi wako.”
Lisa alicheza na kalamu kwenye vidole vyake na kuhema kabla ya kuzungumza kama mtoto anayedeka kwa baba yake, “Lakini wanahisa wanamjali Sarah tu sasa. Nimechanganyikiwa na nimekatishwa tamaa kidogo, kusema ukweli. Hii inaniwia vigumu sana."

Alvin alihisi butwaa mwili mzima lakini akabaki hana njia mbadala. “Kampuni ni yako tangu mwanzo, hivyo unapaswa kuwa na mamlaka kamili. Nitamtuma mtu azungumze kidogo na mtu yeyote ambaye hatakusikiliza.”
“Asante. Kwaheri!” Akakata simu.
Kimya cha pin-tone kilitanda kwenye chumba cha mkutano. Kutokana na mazungumzo ya Alvin, ilionekana kama alikuwa akimpa Lisa mamlaka maalum. Je! ni kwa sababu alikuwa mke wake wa zamani? Isitoshe, jinsi alivyozungumza naye ilionekana kana kwamba bado kuna kitu kati yao.
Ndani ya dakika chache, wanahisa walichanganyikiwa na kujuta kumtetea Sarah. Pia, ingekuwa mbaya sana kama wangeletewa mtu na Alvin kwa ajili ya 'mazungumzo kidogo'.
Mkurugenzi Gumbo alikohoa kinafiki na kugeuza maamuzi ghafla. "Um... Tutaheshimu uamuzi wa Bwana Kimaro."
"Hiyo ni kweli, tutafuatana na chochote ambacho Bwana Kimaro anasema," wengine

wote waliunga mkono na kutikisa kichwa mara moja.
Sarah aligeuka rangi mara moja. Alikuwa akingoja mbele ya mlango wa lifti kuona Lisa akifedheheshwa, lakini sasa ilionekana kuwa yeye ndiye aliyeona aibu badala yake.
“Mbona bado uko hapa?” Lisa aligeuka ghafla na kumpungia simu mwanamke huyo. “Hujasikia alichosema Alvin? Fanya haraka kukabidhi vitu vyako. Sitaki kabisa kukuona katika kampuni yangu.”
Sarah alikasirika kabisa. Macho yake yalimtoka machozi lakini aliinamisha kichwa na kuondoka mara moja.
Wanahisa wote hawakujua la kufanya. Yote yalikuwa makosa ya Bwana Kimaro kwa kumweka mke wake wa zamani na mpenzi wake wa sasa mahali pamoja.
"Sawa, turudi kwenye biashara." Maneno ya ukali yalimjia Lisa usoni. “Hiyo ilikuwa ina maanisha nini? 'Tutaheshimu uamuzi wa Bwana Kimaro?' Ana uhusiano gani na kampuni hii? Ikiwa nyote mnapenda

kumsujudia sana, basi nendeni mkamfanyie kazi kwenye kampuni yake.”
Alipiga kiganja chake juu ya meza, macho yake yakiwa yamefurika kwa hasira. "Kumbukeni kuwa kampuni hii ilijengwa na mama yangu na alikuwa anatokea kwa Masawe, siyo Kimaro. Ikiwa hamuwezi kukubali hilo, basi ondokeni tu na msubiri kufurahia bonasi zenu za kila mwaka nyumbani. Watoto zenu, binti zenu, na watu wa jamaa zenu wanaofanya kazi hapa watabeba mizigo na kwenda pamoja nanyi.” Mkutano huo hatimaye ulimalizika.
Amba alimtazama Lisa kwa heshima. “Mwenyekiti Jones, ulikuwa unavutia sana kwenye mkutano. Ulipokuwa unasimamia hapo awali, bado ulionyesha heshima kubwa kwa wanahisa hao. Lakini mapema, uwepo wako mkuu uliwaambia nani ni bosi. Wewe ni mzuri.”
Lisa alikosa la kusema kwa maneno yake na kukohoa kwa nguvu. "Watu hubadilika. Nilikuwa nikiwaheshimu na kuwachukulia kama wazee na kama wandugu ambao wangepigana vitani pamoja nami. Lakini nimegundua kuwa hisia sio ya pande zote.

Watu hao wanajali tu faida na manufaa yao binafsi.
"Watu wengi wako hivyo." Amba ghafla akatazama mbele.
Lisa alimkazia macho, akamuona Sarah akimsogelea huku akiwa amebeba sanduku lililojaa vitu. Alikuwa ameongozana na Maya aliyekuwa akimwangalia Lisa kwa unyonge.
"Lisa, usijione mjanja sana." Maya alimkazia macho. “Unamtishia Bwana Kimaro kwa cheti cha ndoa? Sote tunajua kwamba hajali kabisa kuhusu wewe.”
“Wewe ni mlinzi tu. Usifanye kana kwamba Alvin ni mume wako.”
Lisa alipiga kelele. "Kuna mengi unaweza kujifunza kutoka kwa neema ya Shani."
“Wewe...”
“Sawa,” Sarah alimkatisha Maya. “Sawa, kwanini usiachane tu na Alvin na kuwa na mwanzo mpya na mwanaume mwingine? Wanachukia kutishiwa zaidi. Unaweza

kuachwa bila chochote ikiwa utamchokoza zaidi.”
Lisa alitabasamu kabla ya kunong'ona karibu na sikio la Sarah, “Acha kujifanya. Unakumbuka jinsi ulivyoharibu kila kitu nilichokuwa nacho? Nitakulipa pole pole kwa hilo.”
Sarah alikodoa macho na kucheka. “Unafikiri unaweza kushindana na mimi? Endelea kuota. Ninaweza kukusagasaga kwa urahisi kama biskuti.”
"Ndio unavyowaza hivyo? Tutaona basi.” Lisa alijiweka sawa na kumpita yule mwanamke.
“Lisa, wewe ni mjinga sana,” Sarah akamwambia Lisa aliyekuwa akitoweka kwenye macho yake, “Makampuni mengi yanayofanya kazi na Mawenzi kwa sasa yanafanya hivyo kwa sababu ya kuniheshimu mimi na Alvin. Watasimamisha ushirikiano wao mara nitakapoondoka. Hivi karibuni, Hudson itapoteza uwezo wa kujiendesha. Nitasubiri kuona ni nini unaweza kufanya wakati huo."

“Usijali kuhusu hilo. Fanya haraka upotee,” Lisa alijibu bila adabu.
Hasira ilikuwa imeandikwa usoni mwa Sarah. Baada ya kutoka nje ya jengo hilo, alipiga simu. "Meneja Howard, tengeneza habari kwamba Lisa ametuudhi mimi na Alvin. Hatuna mpango kuhusu Mawenzi Investments tena.”
“Sikuwa na wazo kwamba ulikuwa ukinifanyia hivi. Pole.”
Sarah alionekana kuguswa lakin bado alikuwa amechanganyikiwa.
Kwa kweli, alikasirika.
Kamwe hakutarajia uamuzi wake miaka mitatu iliyopita wa kumlazimisha Lisa kuuambia umma kwamba alikuwa ameachana na Alvin angerudi kumng'ata mwishowe.
“Sawa... ataendelea kukutisha kwa hili mpaka lini? Atakupa talaka kweli?” Machozi yalitiririka ghafla mashavuni mwake. “Mimi na wewe tumefahamiana kwa zaidi ya miaka 20 na tumekuwa wapenzi pamoja kwa zaidi ya miaka kumi. Ni lini hatimaye... utanioa?”

“Nitajaribu niwezavyo kumtaliki. Alvin akamkabidhi kitambaa cha kujifutia machozi huku akijisikia hatia sana. "Tayari nina mipango, kwa hivyo hupaswi kufikiria kupita kiasi." “Sawa. Kweli, imekuwaje leo ... hospitalini?" alihoji kimya kimya.
Uso wake mzuri ulianguka ndani ya sekunde chache huku akiweka kichwa chake chini. "Ninatumia dawa za kutuliza maumivu."
"Basi sawa."
Furaha ilikuwa imeandikwa usoni mwa Sarah lakini Alvin alikula chakula kidogo sana haraka kabla ya kupanda juu. Sarah alikunja sura yake, akitazama kipande kikubwa cha nyama iliyobaki.
•••
Siku iliyofuata katika Kampuni ya Mawenzi.
Lisa alipita kwenye lango kuu la kuingilia akiwa amevalia suti nadhifu ya biashara. Aligonga dawati la ofisi ya mapkezi huku akipita. Mhudumu wa mapokezi toka jana yake

alitetemeka huku akiinua kichwa chake. "Mwenyekiti Jones."
“Umeikumbuka sura yangu? Natumai sihitaji kuweka miadi kabla ya kuja tena wakati ujao.” Alitabasamu kabla ya kuelekea kwenye lifti.
Mhudumu wa mapokezi alihisi miguu yake ikiishiwa nguvu. Alikuwa na hofu ya kuachishwa kazi alipopata habari asubuhi ya siku hiyo kwamba Lisa ndiye angekuwa mwenyekiti mpya. Kwa bahati nzuri, haikutokea.
Baada ya kuingia kwenye chumba cha mikutano, Lisa aligundua kuwa wanahisa wote walikuwa wamefika. Sarah alikuwa ameketi kwenye kiti cha kwanza upande wa kulia. Wanahisa wengi walikuwa wamekusanyika wakijikombakomba kwake.
"Mwenyekiti Njau, nilipoenda kwa safari ya kikazi nje ya nchi mara ya mwisho, niliona mkoba huu ambao nilifikiri ungekufaa sana."
"Mwenyekiti Njau, huu ni mchoro halisi kutoka kwa mchoraji maarufu Hilton Johan. Inavyoonekana, kazi zake za sanaa

zinagharimu mamilioni ya shilingi na ni ngumu sana kuzipata. Ninafahamiana naye kibinafsi, kwa hivyo hapa kuna zawadi kidogo kwa ajili yako."
“Mwenyekiti Njau, nilinunua chupa hii ya mvinyo mwekundu kutoka nje ya nchi. Inakaribia miaka 40.”
Lisa aliketi kwenye kiti cha ngozi. Alijimiminia kahawa na kurudisha chupa kwenye meza kwa sauti kubwa. Clang!
Kila mtu katika chumba cha mkutano aligeuzia mwelekeo wake kwake.
“Haya nyie. Acheni kukusanyika karibu yangu. Tuna mkutano wa bodi leo. Tukukaribishe kurejea kwa Mwenyekiti Jones.” Sarah alijisemesha kwa tahadhari.
Lisa alimtazama mwanamke huyo kwa kero. "Tuna mkutano wa bodi leo. Wewe uko hata kwenye bodi? Nani alikupa ruhusa ya kuwa hapa?"
"Nilikuwa na wasiwasi kwamba usingefahamu kinachoendelea katika kampuni baada ya

kuwa nje kwa miaka michache, hivyo nilikuja kukuongeza kasi." Sarah alionekana kufadhaika na kuhuzunika.
Mkurugenzi Gumbo alimtetea, “Miss Jones, ninaelewa kuwa kuna mzozo wa kibinafsi kati yenu lakini hakuna sababu ya kuzungumza juu ya hilo kwenye kampuni. Tunamshukuru sana Mwenyekiti Njau na Mwenyekiti Kimaro kwa kuongeza faida ya kampuni katika miaka ya hivi majuzi. Bei yetu ya hisa ina thamani kubwa sana tunapozungumza.”
"Hiyo ni sawa. Tuliambiwa ghafla kuwa umekufa. Kampuni isingeweza kujiendesha bila kuwa na mwenyekiti mwenye uwezo. Tulimwona Bi. Njau anafaa na kweli ametufaa. Kwa hiyo ni nyema akaendelea kupewa nafasi." Mwanahisa mwingine alisema.
Sarah alizungumza huku kukiwa na furaha ya kujilazimisha usoni mwake, "Mwenyekiti Jones lazima alikuwa na sababu zake."
"Mwenyekiti Njau, wewe ni mkarimu sana kwa kumtetea licha ya jinsi anavyokuchukulia," mwanahisa mwingine alisema. “Baada ya yote, kila mtu alijua kwamba siku moja Sarah

atakuja kuwa Bi Kimaro. Kwa upande wa Lisa, ilikuwa ni kosa lake kumwachia Alvin.”
"Hiyo ni sawa. Si ajabu kwamba Bwana Kimaro alikuchagua mwishowe. Wanaume hupenda mwanamke anayejielewa.” MMoja wa wanahisa alinong’ona.
TUKUTANE KURASA 326-330
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA SABA
SIMULIZI........................LISA KURASA......326 MPAKA 330
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY WHATSAPP: +255628924768

Sura ya: 326
Lisa alimtazama kwa ukali mtu ambaye alitoa maoni hayo. Cha kufurahisha zaidi, alikuwa mwanahisa wa kike anayeitwa Wande.
"Mkurugenzi Wande, maneno yako hayaendani kabisa na jina lako," alisema kwa kejeli.
Mkurugenzi Wande alikasirika alipoelewa maana ya maneno ya Lisa. “Mwenyekiti Jones, unamaanisha nini? Nina makosa kusema kwamba wanaume wanapenda mwanamke anayejitambua?"
“Nimeondoka kwa miaka mitatu tu lakini kila mtu anadhani anaweza kunidharau sasa kwa kuwa mimi siye mwenyekiti, huh? Msisahau ni nani ndiye aliyewaagiza kuwa hapa kwa ajili ya kikao hiki cha bodi,” Lisa alikikumbusha kile chumba ambacho kilikuwa kimejaa watu.

Kila mtu alinyamaza kwa sababu kila mtu alidhani aliyeitisha mkutano huo alikuwa ni Alvin.
“Sarah, ninapendekeza uondoke sasa au nitawaambia wana usalama wakutoe nje,” Lisa alionya kwa upole. “Isitoshe, Alvin si amekuambia? Au nikukumbushe tena wadhifa wangu?”
Uso mzuri wa Sarah ulipauka papo hapo. Alijua kwamba wawili hao hawakuachana, kwa hivyo angeonekana kuwa ni kmada tu ikiwa Lisa angemwambia kila mtu ukweli.
"Hakika, nitaondoka." Aliinuka na kusimama huku akionekana kuwa na huzuni.
Lisa hakusumbuliwa na sura ya chuki iliyotupwa kwake na bodi ya wakurugenzi. "Sawa, kama mwenyekiti wa Mawenzi Investments, ninakuondoa kwenye nafasi yako. Unaweza kutoka hapa baada ya kukabidhi kila kitu.”

"Unakwenda mbali sana," Mkurugenzi Gumbo alisema kwa wasiwasi, "Tunapinga uamuzi huo."
"Hiyo ni sawa. Wanahisa wana haki ya kumpigia kura mwenyekiti,” wengine waliunga mkono.
"Nyinyi nyote mnaonekana kufikiria kuwa mtasamehewa kwa hili kwa msaada wa Alvin, huh?" Macho ya Lisa yalitazama chumba chote.
Wote wakanyamaza. “Sawa, basi nitampigia simu.”
Lisa alimpigia simu Alvin. Katika sekunde chache, sauti yake ya kijeuri ilisikika kupitia spika.
"Huyu ni nani?" Wanahisa walidhihaki. “Mume wake wa zamani hata hakuwa amehifadhi mawasiliano yake. Namna alivyomtendea ilikuwa tofauti kabisa na jinsi alivyomjali

Sarah.”
Sarah, ambaye alikuwa karibu kuufikia mlango, alisimama na kutabasamu kwa hasira.
Lisa hakukasirika. Aliongea kwa utulivu kwenye simu, "Ni mimi, Lisa."
“Unajaribu—”
“Bwana Kimaro, uko kwenye kipaza sauti,” alimkatiza, “Sikufikiri kwamba ingechukua miaka mitatu tu kwa wenyehisa wa shirika langu kunikosea heshima. Sina hata mamlaka ya kumfukuza Sarah sasa.”
Alvin aliyekuwa upande wa pili wa simu alihisi damu ikichemka baada ya kusikia maneno ya Lisa. Alikuwa karibu kubishana wakati Lisa aliendelea, “Hey, ni kitu gani hiki kwenye mkoba wangu? Inahisi kama cheti cha aina fulani."
Sarah aliyekuwa akiingia kwenye lifti nusura

apige teke mlango wa lifti uliokuwa mbele yake.
‘Cheti gani? Cheti chao cha ndoa?’ Alvin alijiwazia. ‘Mwanamke huyu alikuwa akimtishia tena. Jamani!’ Aliuma meno na kujilazimisha sauti ya upole huku akisema, “Endelea basi. Unapaswa kuendesha mambo ya kampuni yako jinsi unavyotaka kwa kuwa umerudi. Itakuwa bora ikiwa kampuni itakufia chini ya uongozi wako.”
Lisa alicheza na kalamu kwenye vidole vyake na kuhema kabla ya kuzungumza kama mtoto anayedeka kwa baba yake, “Lakini wanahisa wanamjali Sarah tu sasa. Nimechanganyikiwa na nimekatishwa tamaa kidogo, kusema ukweli. Hii inaniwia vigumu sana."
Alvin alihisi butwaa mwili mzima lakini akabaki hana njia mbadala. “Kampuni ni yako tangu mwanzo, hivyo unapaswa kuwa na mamlaka kamili. Nitamtuma mtu azungumze kidogo na mtu yeyote ambaye hatakusikiliza.”

“Asante. Kwaheri!” Akakata simu.
Kimya cha pin-tone kilitanda kwenye chumba cha mkutano. Kutokana na mazungumzo ya Alvin, ilionekana kama alikuwa akimpa Lisa mamlaka maalum. Je! ni kwa sababu alikuwa mke wake wa zamani? Isitoshe, jinsi alivyozungumza naye ilionekana kana kwamba bado kuna kitu kati yao.
Ndani ya dakika chache, wanahisa walichanganyikiwa na kujuta kumtetea Sarah. Pia, ingekuwa mbaya sana kama wangeletewa mtu na Alvin kwa ajili ya 'mazungumzo kidogo'.
Mkurugenzi Gumbo alikohoa kinafiki na kugeuza maamuzi ghafla. "Um... Tutaheshimu uamuzi wa Bwana Kimaro."
"Hiyo ni kweli, tutafuatana na chochote ambacho Bwana Kimaro anasema," wengine wote waliunga mkono na kutikisa kichwa mara moja.

Sarah aligeuka rangi mara moja. Alikuwa akingoja mbele ya mlango wa lifti kuona Lisa akifedheheshwa, lakini sasa ilionekana kuwa yeye ndiye aliyeona aibu badala yake.
“Mbona bado uko hapa?” Lisa aligeuka ghafla na kumpungia simu mwanamke huyo. “Hujasikia alichosema Alvin? Fanya haraka kukabidhi vitu vyako. Sitaki kabisa kukuona katika kampuni yangu.”
Sarah alikasirika kabisa. Macho yake yalimtoka machozi lakini aliinamisha kichwa na kuondoka mara moja.
Wanahisa wote hawakujua la kufanya. Yote yalikuwa makosa ya Bwana Kimaro kwa kumweka mke wake wa zamani na mpenzi wake wa sasa mahali pamoja.
"Sawa, turudi kwenye biashara." Maneno ya ukali yalimjia Lisa usoni. “Hiyo ilikuwa ina maanisha nini? 'Tutaheshimu uamuzi wa

Bwana Kimaro?' Ana uhusiano gani na kampuni hii? Ikiwa nyote mnapenda kumsujudia sana, basi nendeni mkamfanyie kazi kwenye kampuni yake.”
Alipiga kiganja chake juu ya meza, macho yake yakiwa yamefurika kwa hasira. "Kumbukeni kuwa kampuni hii ilijengwa na mama yangu na alikuwa anatokea kwa Masawe, siyo Kimaro. Ikiwa hamuwezi kukubali hilo, basi ondokeni tu na msubiri kufurahia bonasi zenu za kila mwaka nyumbani. Watoto zenu, binti zenu, na watu wa jamaa zenu wanaofanya kazi hapa watabeba mizigo na kwenda pamoja nanyi.” Mkutano huo hatimaye ulimalizika.
Amba alimtazama Lisa kwa heshima. “Mwenyekiti Jones, ulikuwa unavutia sana kwenye mkutano. Ulipokuwa unasimamia hapo awali, bado ulionyesha heshima kubwa kwa wanahisa hao. Lakini mapema, uwepo wako mkuu uliwaambia nani ni bosi. Wewe ni mzuri.”
Lisa alikosa la kusema kwa maneno yake na

kukohoa kwa nguvu. "Watu hubadilika. Nilikuwa nikiwaheshimu na kuwachukulia kama wazee na kama wandugu ambao wangepigana vitani pamoja nami. Lakini nimegundua kuwa hisia sio ya pande zote. Watu hao wanajali tu faida na manufaa yao binafsi.
"Watu wengi wako hivyo." Amba ghafla akatazama mbele.
Lisa alimkazia macho, akamuona Sarah akimsogelea huku akiwa amebeba sanduku lililojaa vitu. Alikuwa ameongozana na Maya aliyekuwa akimwangalia Lisa kwa unyonge.
"Lisa, usijione mjanja sana." Maya alimkazia macho. “Unamtishia Bwana Kimaro kwa cheti cha ndoa? Sote tunajua kwamba hajali kabisa kuhusu wewe.”
“Wewe ni mlinzi tu. Usifanye kana kwamba Alvin ni mume wako.”
Lisa alipiga kelele. "Kuna mengi unaweza

kujifunza kutoka kwa neema ya Shani." “Wewe...”
“Sawa,” Sarah alimkatisha Maya. “Sawa, kwanini usiachane tu na Alvin na kuwa na mwanzo mpya na mwanaume mwingine? Wanachukia kutishiwa zaidi. Unaweza kuachwa bila chochote ikiwa utamchokoza zaidi.”
Lisa alitabasamu kabla ya kunong'ona karibu na sikio la Sarah, “Acha kujifanya. Unakumbuka jinsi ulivyoharibu kila kitu nilichokuwa nacho? Nitakulipa pole pole kwa hilo.”
Sarah alikodoa macho na kucheka. “Unafikiri unaweza kushindana na mimi? Endelea kuota. Ninaweza kukusagasaga kwa urahisi kama biskuti.”
"Ndio unavyowaza hivyo? Tutaona basi.” Lisa alijiweka sawa na kumpita yule mwanamke.

“Lisa, wewe ni mjinga sana,” Sarah akamwambia Lisa aliyekuwa akitoweka kwenye macho yake, “Makampuni mengi yanayofanya kazi na Mawenzi kwa sasa yanafanya hivyo kwa sababu ya kuniheshimu mimi na Alvin. Watasimamisha ushirikiano wao mara nitakapoondoka. Hivi karibuni, Hudson itapoteza uwezo wa kujiendesha. Nitasubiri kuona ni nini unaweza kufanya wakati huo."
“Usijali kuhusu hilo. Fanya haraka upotee,” Lisa alijibu bila adabu.
Hasira ilikuwa imeandikwa usoni mwa Sarah. Baada ya kutoka nje ya jengo hilo, alipiga simu. "Meneja Howard, tengeneza habari kwamba Lisa ametuudhi mimi na Alvin. Hatuna mpango kuhusu Mawenzi Investments tena.”
Sura ya: 327
Lisa alifunga kompyuta yake ndogo, tayari

kuelekea nyumbani. Miaka mitatu ilikuwa imepita tangu aachane na kampuni hiyo lakini ilimchukua siku moja tu kupata kasi ya kubadilisha mambo.
Alikuwa karibu kufungua mlango wa mbele wa nyumba yake wakati kivuli cheusi kilimfunika ghafla. Kwa haraka, aliinua mguu na kurudi nyuma ili kupiga teke. Mkono mkubwa ukaushika mguu huo mara moja. Uso mzuri wa Alvin ulionekana kuwa wa baridi kama barafu.
“Ulikuwa unapanga kunipiga teke wapi?”
Lisa alipepesa nyuma kwa macho yake mazuri kabla ya kuelekeza macho yake kwenye sehemu yake ya chini ya kitovu. “Ikulu”
"Nadhani unahamu ya kifo." Alikuwa karibu sana kupasuka kwa hasira.
Baada ya kuzima hasira iliyompanda, aliupiga mguu wa Lisa aliokuwa ameushikilia.
Lisa, ambaye alikuwa amesimama kwa mguu

mmoja, alipoteza usawa wake na haraka akashika tai ya Alvin kwa msaada. Alvin alishikwa na butwaa na akaanguka mbele pia. Alianguka nyuma chini na kwenye zulia. Midomo yake ilitua kwenye midomo ya Lisa kwa bahati alipoanguka mbele.
Midomo ya mwanamke ilikuwa nyororo kama jeli. Lipstick yenye ladha ya machungwa aliyokuwa amepakaa ilikuwa ya kuvutia sana. Ilimfanya atamani kuinyonya bila fahamu.
Wakati huo huo, taa za moja kwa moja kwenye korido zilizimika kwa sababu zilikuwa zikitumia sensa. Alvin aliguna. Aliweza kuhisi pumzi yake kwenye ngozi yake katika giza na ghafla akawa na hamu ya kuonja midomo yake.
Lakini, wakati huo huo, mlango wa lifti ulifunguliwa na taa zilizosensi harakati ya lifti zikawaka tena. Alitoka mama na binti yake. Msichana huyo alikuwa na umri wa miaka saba au minane tu.
Yule mama ambaye alishtuka baada ya kuona

kile kitu mbele yao, haraka akamfunika bintiye macho.
Lisa alihisi mashavu yake yakiungua na mara moja akamsukuma mtu huyo kutoka kwake. “Um...”
“Samahani kwa kukatiza. Tafadhali endeleeni.” Mama alifungua mlango wa nyumba yao kwa haraka na kumwingiza bintiye ndani. Kisha akafunga mlango kwa nguvu nyuma yake.
Sauti zao bado zilisikika kutoka upande wa pili wa mlango. “Mama kwanini unanisukuma? Niliona walikuwa wakibusiana.”
"Nyamaza." Mama alionya.
"Mama, kwanini wasibusuane ndani ya nyumba?" Binti alizidi kusmbua.
"Kuna baadhi ya mambo kuhusu mapenzi ambayo huyajui."

"Kama yale? Niliiona kwenye TV hapo awali. Hawawezi kujizuia kupendana, sivyo?”
Uso mzuri wa Alvin ulikuwa umetanda. Hakuweza kuvumilia lakini kuangukia kwenye mapenzi? Yeye na Lisa? Pfft, haikuwa kweli.
Lisa, kwa upande mwingine, alikuwa na aibu sana hivi kwamba alitamani kutoweka kwenye hewa nyembamba. Akamkazia macho mwanaume huyo. “Ondoka nje.” Kisha, akajaribu kufunga mlango nyuma yake.
Akiusimamisha mlango kwa mkono wake, Alvin akausukuma na kuingia ndani ya nyumba. Nyumba ilikuwa pana lakini umbo lake refu lilifanya nafasi hiyo kuonekana ndogo kuliko ilivyokuwa.
“Alvin, unataka nini? Kwanini usiende nyumbani kwa Sara wakati huu wa usiku?”
“Hata hapa nimekuja kwa sababu ya Sarah. Baada ya simu yako uliyopiga leo asubuhi...

Lisa, wewe ni mwanamke mlaghai sana. Ulimuaibisha Sarah mbele ya watu wote na hata ukamfanya alie.”
Alvin alikuwa amekasirika tangu simu hiyo ilipopigiwa, hasa baada ya mmoja wa wanahisa kumpigia simu kumjulisha kuwa Sarah ametoka nje ya mkutano huku akitokwa na machozi baada ya kudhalilishwa na Lisa. Alitamani sana kumnyonga mwanamke huyu hadi afe.
“Oh, unamuonea huruma?” Lisa aliweka mikono yake mbele ya kifua chake. "Sijakulazmisha useme maneno hayo."
“Wewe... Usifikiri kuwa naogopa kwa sababu tu umeshikilia cheti chetu cha ndoa.” Macho yake meusi yaliganda. "Mtu wa mwisho aliyenikasirisha alishatoweka kutoka kwa ulimwengu huu."
“Unazungumzia Charity?” Alisema ghafla. Alvin alionekana kupigwa na butwaa, lakini

aliondoa mshangao wake haraka haraka. "Alistahili kwa sababu alijaribu kutoroka kifungo chake kwa kuruka ndani ya bahari. Ni kawaida kwamba samaki wangemla.”
Lisa aligeuka kimya kimya ili aweze kuona dhamira ya mauaji machoni mwa Alvin. Alijua kwamba watu hao wasingejihisi kuwa na hatia kuhusu matendo yao. Kama ilivyotokea, alikuwa sahihi.
Alvin Kimaro, kumbuka jinsi unavyojitapa kuhusu hili na nitahakikisha unateseka siku zijazo.' “Haya, toka.”
Akiwa amechanganyikiwa na ujeuri wake, akamshika mabega. "Nataka tuwe tumeachana ifikapo kesho."
"Haiwezekani." Lisa aligoma kijeuri.
Akiwa amekasirika, Alvin akapiga teke juu ya pipa la takataka. "Lisa, usinilazimishe nikufanye kitu kibaya!"

"Kweli, wacha nione kile unachotaka kufanya." Tabasamu la fumbo lilimwangazia usoni mwake. Uso wake mzuri ulianguka.
Baada ya kufanya kazi kwa siku nzima, Lisa alichokuwa akitaka sasa ni kuoga kwa muda mrefu na kupiga simu ya video kwa wapenzi wake wawili waliokuwa Marekani. Hata hivyo, hakuweza kufanya hivyo huku mwanaume huyo akimsumbua. “Unaweza kuondoka? Naenda kuoga."
“Nitaondoka baada ya kukubali kusaini hati za talaka." Alvin alijilaza kwenye kochi na kunyoosha miguu yake. Mtu huyu alijulikana kwa sura yake ya kifahari, lakini wakati huo huo, alikuwa akiishi kama asiye na makazi.
“Unataka pesa? Nitakupa dola bilioni moja hiyo inaweza kukufanya uishi maisha yako yote bila kufanya kazi. Huo ndiyo wema ninaoweza kukufanyia. Wewe ni wa thamani hii tu, baada ya yote.” Alvin aliwambia.

"Unaweza kukaa hapa usiku kucha ikiwa ndivyo unavyotaka." Lisa alimpuuza akaingia chumbani kwake.
Uso wa Alvin ulianguka. Mara akainuka na kumkimbilia yule mwanamke. Kwa bahati mbaya, alimwona akimalizia kuvua chupi nyeusi ya kuvutia kutoka chumbani.
Kitu kiliangaza machoni pake. “Lisa, hiyo ni ya nini? Unajaribu kunitega?” Aliitikisa kichwa chake.
“Una wazimu? Nimtege nani na nipo nyumbani kwangu? ” Lisa alijibu bila wasiwasi huku akiendelea kuvua. Akachukua upande wa kanga na kujitupia mwilini.
"Hivi ndivyo unavyovaa ukiwa nyumbani? Kanga moja tu" Alihisi kuudhika bila sababu. “Huoni hata kama una mgeni?”
"Utajiju. Kwanini nishindwe kujiachia nikiwa

nyumbani kwangu?” Mwanamke anapaswa kupata hewa kila wakati." Lisa alitoka kuelekea bafuni.
Alipokuwa akimpita Alvin aliyekuwa kasimama njiani, alimpiga kikumbo.
“Una shida gani?” Lisa alichukia.
"Kama bado hutaki kusaini hizi hati za talaka, wewe bado ni mke wangu kitaalam, kwa hiyo nitadai haki yangu ya ndoa usiku huu." Baada ya kusema hivyo akajibwaga kitandani bila wasiwasi.
“Ni nini jamani...” Lisa alijisikia kulaani sana. Ni siku chache tu zilikuwa zimepita tangu arudi na hivyo ndivyo alivyokuwa akimtendea. Ilivyoonekana hakuwahi kumsahau kabisa.
"Alvin, usipoondoka nitapiga simu polisi." Lisa alimtisha.
“Polisi ni nani wa kunizuia mimi kulala na mke

wangu kihalali?”
Alvin akaanza kutoa nguo moja moja. Baada ya Lisa akumaliza kuoga, alimkuta akiwa uchi wa mnyama.
“We Alvin una matatizo gani jamani?” Lisa moyo ulimripuka kwa hofu.
“Naenda kuoga nije kulala na mke
wangu.” Alvin alijibu, alivuta upande wa kanga kutoka mwilini mwa Lisa. Lisa naye akabaki mtupu vilevile, lakini kwa aibu tu akaziba baadhi ya maeneo yake kwa mikono.
Alvin hakuchukua muda bafuni, na alipotoka alimkuta Lisa akiwa kajilaza na pajama zake nyepesi. Sasa Alvin hakuwa na nguo za kulalia, angelala uchi au angefanyaje?
Alinyamaza kwa sekunde kadhaa na kufikiria kumpigia Hans ili amnunulie mpya na kumpelekea usiku huohuo.

Sura ya: 328
“Alvin vaa nguo zako na uondoke, sitaki ndani ya nyumba yangu.” Kabla Alvin hajachukua simu kumpigia Hans, Lisa alikurupuka na kuanza kumsambulia kwa hasira. Alitumia kila alichoona kinafaa kumpigia Alvin lakini haswa yalikuwa makopo na chupa za rosheni na vipodozi vingine.
Baadhi ya chupa za rosheni zilikuwa zimefunguka hivyo kumfanya Alvin atapakae vimiminika vizito vyenye harufu kali mwilini mwake na usni pia. Aliparamia kabati la nguo na kuanza kujifuta mwili kwa kila nguo aliyogusa. Bahati mbaya nguo nyingi alizojifutia zilikuwa ni za ndani.
“Alvin, unachafua nguo zangu zote, nitavaa nini kesho?” Lisa alilalamika baada ya kuona nguo zake za ndani zikiharibiwa kwa mafuta ya rosheni. Nyingi zilikuwa nyeupe na rangi angavu hivyo zisingetakata hata kama angezifua usiku huo.

“Nitakununulia zingine.” Alvin alijibu kijeuri. Alitaka kumwambia Hans anunue na nguo za ndani za Lisa pia lakini kwa mawazo ya pili, alijisikia aibu kumruhusu mtu mwingine kugusa vitu hivyo vya ndani na vya faragha.”
“Twende mjini tukanunue mpya sasa hivi." Alvin aliamuru na kuanza kuvaa nguo zake.
"Hivi una muda mwingi wa kuchezea, eeh? Nimechoka na nataka kupumzika tu nyumbani.” Lisa alijisikia kulia.
Alvin alikunja uso kabla ya kusema kwa huzuni, “Basi wewe pumzika, niitakwenda kukuletea mimi mwenyewe.”
Jambo hili lilimshangaza Lisa na kumtazama kwa ajabu. “Usifikirie sana kuhusu hilo. Sivutiwi nawe. Sitaki kabisa unifedheheshe kwa kuwa na uhusiano wa nje wa kimapenzi wakati bado upo kwenye ndoa yangu.”

Alvin aligeuka ili kuondoka lakini ghafla akageuka na kumtazama tena Lisa. “Oh, sawa, ninahisi njaa sana. Nikute chakula kimeiva nikirudi.” Kisha, hatimaye akaondoka.
Lisa akamtolea macho. Hivi kweli alifikiri yeye amekuwa mpishi wake binafsi? Endelea kuota! •••
Dakika 20 baadaye, Alvin aliibukia katika duka la nguo za ndani lililokuwa karibu. Aibu ilikuwa imemjaa. Ni nini kilimpata hadi akawa anamnunulia Lisa chupi mida hiyo? Hakuwahi hata kumnunulia Sara kabla.
"Bosi, unatafuta chupi za wanaume?" Mwanamke muuzaji akamfuata. Macho yake yalimtoka baada ya kumtazama kwa karibu uso wake mzuri. Mtu huyo alikuwa na sura nzuri kuliko watu mashuhuri wengi.
Hata alihisi sura yake haikuwa ngeni kwenye macho yake.
“Umh, hapana. Natafuta nguo za ndani za kike,” Alvin alijibu kwa jazba.

“Oh, ni kwa ajili ya mpenzi wako. Naelewa." Muuzaji alimuonea wivu sana mpenzi wake ingawa hakumjua. “Hizi hapa ndizo zilizo kwenye chati sana kwa upande wa wanawake. Unapenda zipi?"
Alvin aliutupia jicho upesi mkusanyo huo na kugundua zote zilikuwa za kuvutia sana. Alihisi joto ghafla huku akiwaza jinsi Lisa angeonekana akiwa amezivaa. "Nipe kitu cha kizamani kidogo, chenye kuhifadhi vyema mazingira muhimu, pamba kwa asilimia mia."
Muuzaji hatimaye alielewa alichokuwa akitafuta. “Naona. Hutaki mpenzi wako avae nguo za ndani zinazoonyesha wazi. Bosi, wewe unaelewa kweli. Kwa kweli, pamba ni salama zaidi kwa ngozi yetu kwa sababu zinanyonya jasho.”
“Kweli?”Ghafla alifikiri Lisa hajali sana afya yake kwani alikuwa anamiliki tu zile za lace nyeusi.

“Bosi, nikufungie ngapi?”
Alvin alifikiria jambo hilo kwa sekunde kadhaa. "30. Hizo zitamtosha kwa mwaka mzima mwaka .Nipatie sidiria 30 pia." Hatimaye, alifanya malipo na kuondoka dukani akiwa amebeba mifuko kadhaa ya shopping.
Kwa bahati mbaya ama nzuri, rafiki mmoja wa Sarah aitwaye Joan Halua, msichana mdogo wa familia ya Halua, alikuwa akinunua bidhaa karibu na akampiga picha ili kumtumia Sarah kupitia WhatsApp. “Angalia vitu ambavyo Alvin amekununulia usiku huu kutoka kwenye duka la nguo za ndani. nakuonea wivu sana.”
Wakati huo, Sarah alikuwa akinyanduliwa na Hisan katika nyumba yake binafsi. Dakika 20 baadaye, aliamka kuangalia simu yake. Uso wake ulibadilika kwa tabasamu la furaha baada ya kusoma ujumbe wa Joan.
Alvin hakuwahi kumfanyia kitu kama hicho

hapo awali. Ilionekana kana kwamba alikuwa akijaribu kumfariji kwa kudhalilishwa na Lisa asubuhi ya siku hiyo.
"Unaangalia nini? Bado, sijaridhika. Leo hakuna kulala. Njoo tuendelee.” Hisan alisema kabla ya kumvuta tena mikononi mwake.
"Hapana, rafiki yangu alinitumia ujumbe kwamba Alvin anarudi nyumbani." Alikataa kwa sauti iliyochoka kwa kilio cha kupelekewa moto. "Atakuwa na shaka ikiwa nitachelewa kurudi nyumbani. Sitaweza kukupatia pesa akiniacha.”
“Hakika. Lakini anajua wewe ni mkali sana kitandani?" Alikibana kidevu chake kwa kuchezeacheza. "Yeye na mimi nani anakukuna zaidi?"
“Wewe ni mnoma sana. Hakufikii hata kidogo.” Sarah alimsifia mwanaume huyo huku akitabasamu.

“Wewe mtamu sana. Vitu vyako haviishi hamu ndiyo maana bado napenda kulala na wewe baada ya miaka hii yote.” Hisan alicheka kwa sauti. Kuonekana kwa tumbo lake kubwa karibu kumfanye Sarah kuwa mgonjwa lakini hakuwa na chaguo ila kucheka pamoja.
Baada ya kuondoka kwenye ghorofa, sura ya SArah ilianguka tena. Ingawa Hisan aliweza kumridhisha jinsi Alvin alivyoshindwa, mtu huyo alikuwa bomu lililosubiri muda tu ili kuripuka. Alihitaji kufanya mbinu kupata picha zote na kuachana naye kabla ya mambo hayajaharibika.
•••
Alvin aligonga kengele ya mlango. Lisa alipigwa na butwaa baada ya kuona idadi ya mabegi aliyokuwa ameyabeba. Alinunua kiasi gani?
"Seti 30 kwa jumla." Akayatupia yale mafurushi kwenye kochi. Tumbo lake lilianza kunung'unika baada ya kusikia harufu ya chakula kitamu kutoka jikoni. "Chakula changu

kiko tayari?" Macho yake yaling'aa kama mbwa anayesubiri kulishwa.
Bila kusema, Lisa aliashiria bakuli la chakula mezani.
Alvin alitembea akitarajia tu kupata mlo wa kuvutia. Upishi ulikuwa mzuri. Ubwabwa kwa nyama ya kuku iliyorostiwa vyema, na hata alikuwa amenyunyiza vikorombwezo kadhaa juu ya ubwabwa. Hata hivyo, aligusa sahani na kugundua tayari kilikuwa kimepoa.
“Hakuna kingine? Mbona hiki kimepoa?" Alvin alikasirika. Alikuwa ameenda kumnunulia chupi kwa wema na hayo ndiyo aliambulia kama malipo?
"Ni kosa lako kuchukua muda mrefu," Lisa alijibu kwa uvivu.
“Si nilitoka kwenda kununua vitu kwa ajili yako lakini”
"Niilikulazimisha uchafue nguo zangu zote?"

Alijibu. "Ni juu yako ikiwa unataka kula au uache. Kuna microwave jikoni ikiwa unataka kuitumia."
Akamkazia macho lakini hakuwa na wasiwasi. Alichukua mifuko ya shopping na kuelekea bafuni. Pamoja na kwamba nguo zilikuwa mpya, alitakiwa kuzifua na kuzikausha kwanza kabla ya kuzivaa.
Hatimaye, Alvin alienda kupasha chakula kwenye microwave kabla ya kula. Chakula kilikuwa na ladha nzuri zaidi kuliko nyama ambayo Sarah alikuwa ametayarisha usiku wa jana yake.
Sura ya: 329
Alvin alikula chakula chote kwa muda mfupi lakini bado alikuwa akihisi njaa. Alienda bafuni na kumkuta Lisa akiwa anafua nguo zake kwenye sinki. Bila hata kumuaga, aliamua kuondoka.

Mwanamume huyo aliendesha gari kupita barabara yenye shughuli nyingi na kuona mgahawa maalumu kwa pasta. Aliingia na kuagiza pasta kutoka kwenye menyu lakini alitema chakula baada ya kuonja mara moja tu. “Pasta unayotengeneza ina ladha ya kutisha,” alifoka kwa hasira.
"Umekuja hapa kwa ajili ya kula au kufoka?" Mmiliki wa mgahawa akaruka kwa hasira. "Nimekuwa nikiendesha mgahawa wangu kwa zaidi ya miaka kumi na kila mtu hapa anazipenda pasta zangu. Wewe ndiye wa kwanza kulalamika.”
"Hiyo ni sawa. Pasta za hapa ni bora zaidi katika mtaa mzima." Mmoja wa wateja hakuweza kujizuia kusema.
Alvin hakujua la kusema. Lisa alikuwa amemroga kwenye vyakula alivyompikia? Haikuwa na umuhimu wowote hata kama ingekuwa mmiliki huyo amekuwa akiendesha mgahawa huo kwa zaidi ya karne nzima.

Ukweli ulibaki kuwa chakula alichotengeneza Lisa kilikuwa na ladha nzuri zaidi.
•••
Kufika nyumbani, Sarah alimsalimia huku akiwa amevalia nguo za ndani za kuvutia. Alionekana kushangaa kumuona Alvin akirudi nyumbani mikono mitupu.
“Mbona umechelewa nyumbani hivi?” Sarah alihoji huku uso wake ukiwa umemshuka. Kwanza alikuwa amechoshwa na shuruba za Hisan, pili alichoka kwa kuona Alvin akija akiwa mikono mitupu.
"Nilikuwa nikifanya kazi kwa muda wa ziada," Alvin alisema bila kutarajia alipokumbuka kila kitu kilichotokea nyumbani kwa Lisa hapo awali.
“Pole.” Sarah alihisi moyo wake kuzama.
"Lisa alikutishia kwenye mkutano asubuhi ya leo?" Alvin alimuuliza ghafla.

"Ndio." Sarah alijibu huku akikunja sura yake kwa madeko.
Alvin alikumbushwa kitu ghafla. Alikuwa ameenda kumtafuta Lisa ili kumuonya kuhusu tukio hilo lakini bado alisahau kila kitu baada ya kuingia nyumbani kwake.
Hisia ya hatia iliosha juu yake. “Sarah, samahani, mimi—”
“Acha. Najua ulimkubalia Lisa achukue kampuni kwa ajili ya yangu mwenyewe.” Sarah alijitupa mikononi mwake. “Ila nina wasiwasi kwamba Lisa atakuiba. Mkutano wa leo ulipoisha, aliniambia kuwa ataharibu kila kitu ninachojivunia.”
"Kuharibu kila kitu?" Macho ya Alvin yalionyesha kubadilika. "Anafikiri yeye ni nani?"
Sarah akashusha pumzi. “Nilimshauri aachane na mambo hayo lakini hakutaka kunisikiliza.

Kuna umuhimu gani wa kukosana na kila mtu? Anahitaji kujua kwamba makampuni mengi yanashirikiana na Mawenzi kwa sababu ya kukuheshimu.”
Wazo likamjia Alvin kichwani huku akimpigapiga Sarah kichwani. “Uko sahihi. Itakuwa majanga kwa Mawenzi Investments ikiwa kampuni zitakataa kufanya kazi naye. Ni juu yake kuamua kama anataka kusaini hati za talaka ili kuokoa kampuni.”
“Alvinic, unafikiria...” Sarah aliuma mdomo wake. "Hii haitakuwa sawa."
"Acha ujinga wewe, kila mtu anajua kwamba tunafunga ndoa mwaka huu. Itakuwaje kwako nisipomtaliki?” Akamkumbatia kwa upole. Mwanamke huyo alitabasamu kwa ujanja mikononi mwake.
Baada ya kuelekea ghorofani, Sarah alimuuliza kwa mtego wakati akibadilisha nguo chumbani. “Alvinic, ni lini utapata muda wa kwenda

shopping na mimi? Nataka kununua nguo mpya za ndani."
“Si nilikupa kadi yako ya benki hapo awali? Tumia tu kwa chochote unachotaka." Alvin alimjibu na moja kwa moja akaelekea bafuni.
Sarah alihisi kukosa raha ghafla. Joan alikuwa amekosea, au? Alvin alikuwa akinunua nguo za ndani kwa ajili ya nani kama si yeye mwenyewe? Lisa? Au alikuwa na mwanamke mwingine?
Alfajiri iliyofuata, Sarah alichukua ufunguo wa gari la Alvin kwa siri na kuingia ndani ili kuangalia picha za dashcam. Ndani ya sekunde chache, aligundua kuwa Alvin alikuwa ameendesha gari kwenda mahali fulani paitwapo Karen Estate mara mbili jana yake usiku.
Asubuhi hiyohiyo, Sarah aliendesha gari hadi sehemu ile ile na akashtuka baada ya kumuona Lisa akitoka pale. Ni kweli alikuwa

Lisa. Hii ilikuwa nje ya matarajio yake.
Tatizo lilikuwa nini? Tayari Sarah alikuwa amemvuruga Alvin ili amdharau Lisa. Ni lazima angekuwa ni Lisa ambaye alikuwa akimg’ang’ania Alvin. Huyo b*tch! Lazima angemtambua.
•••
Saa mbili na nusu asubuhi, Lisa aliingia kwenye kampuni na kuwakuta baadhi ya wanahisa na wajumbe wengine wa bodi ya wakurugenzi wakimsubiri. Meneja Mkuu Ngololo aliyekuwa amerejeshwa kwenye nafasi yake alionekana kukosa subira akiwa amesimama kando.
"Leo mbona mapema?" Lisa aliwauliza kwa mshangao.
Mkurugenzi Gumbo alisema baada ya kuketi kwenye meza yake, "Unafikiri bado tunaweza kulala vizuri? Makampuni matatu makubwa ya

ujenzi ambayo yameshirikiana nasi kwa miaka mingi ghafla yalighairi ushirikiano wao mara moja. Zaidi ya saiti kumi za ujenzi kote nchini Tanzania na Kenya haziwezi kuendelea kufanya kazi leo. Mwenyekiti Jones, ulionekana kana kwamba ulikuwa karibu sana na Bwana Kimaro hivi majuzi, lakini kwanini ghafla hakuna mtu anataka kushirikiana nawe?”
"Ninaamini ni kwa sababu alimkosea Miss Njau jana," Mkurugenzi Williams alisema kwa hasira, "Kampuni hizo za ujenzi zilifanya kazi nasi tu kwa heshima ya Miss Njau na Bwana Kimaro. Lazima walisikia kwamba kuna kitu kibaya kati yenu."
"Tunapaswa kufanya nini? Kampuni imepoteza zaidi ya dola milioni kumi baada ya maeneo ya ujenzi kulazimika kuacha kazi kwa siku moja tu, itakuweje baada ya wiki?” Mkurugenzi Wande aliuliza kwa wasiwasi.
“Hilo si tatizo letu kubwa. Suala ni kwamba

wanataka kuacha kushirikiana nasi.” Mkurugenzi Gumbo alionekana kufadhaika.
“Siku zote tunaweza kushirikiana na washirika wengine,” Lisa alijibu.
"Unajua nini?" Mkurugenzi Gumbo alisema bila subira, "Wateja walinunua tu mali zetu kwa sababu ya sifa nzuri za kampuni tunazoshirikiana nazo. Hao ndio njia bora zaidi ya kufanya biashara katika nchi hii. Wateja walinunua mali hizi kutoka kwetu kwa sababu wanaziamini. Kwa hakika watatukimbia ikiwa kampuni zitabadilishwa. Sifa ya kampuni yetu itaharibika wakati hilo litatokea.”
“Hiyo ni sawa. Suluhisho pekee sasa ni kutafuta msaada kutoka kwa Bwana Kimaro au kumwomba Bi Njau msamaha. Mkurugenzi Williams alisema, "Lazima utatue tatizo hili uliloanzisha. Usituhusishe wajumbe wa bodi.”
"Usitulaumu kwa kuchukua nafasi yako usipotatua jambo hili," Mkurugenzi Gumbo

akaingilia. "Huwezi kutukasirikia. Tunafikiria tu faida za kampuni. Mwenyekiti mzuri hatazuia ukuaji wa kampuni.”
Lisa aliwatazama tu kwa utulivu. "Nilisema siwezi kushughulikia hili?"
“Una uhakika unaweza?” Mkurugenzi Gumbo hakuonekana kushawishika.
Mkurugenzi Williams alisita kabla ya kusema, "Labda kuna nafasi. Bwana Kimaro anaonekana kama bado anamjali Mwenyekiti Jones.”
"Natumai hautoi ahadi tupu," Mkurugenzi Wande alisema kwa sauti ya kushangaza. "Maeneo ya ujenzi yanaweza kuacha kufanya kazi kwa siku tatu tu."
“Hakika.” Lisa aliitikia kwa kichwa.
“Basi tutakupa nafasi. Ikiwa kampuni za ujenzi hazitaanza tena kufanya kazi baada ya siku

tatu, basi tutachukua nafasi yako kama mwenyekiti wa kampuni.” Mzee Gumbo alitoa angalizo.
Baada ya kuondoka kwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi, Meneja Mkuu hakuweza kujizuia kuuliza kwa wasiwasi, “Mwenyekiti Jones, unaweza kweli kushughulikia hili? Hali ni tata sana wakati huu."
Sura ya: 330
“Rudi kazini. Nitalishughulikia hili.” Lisa alifungua laptop yake. Amba alimtazama kwa ajabu bosi wake ambaye safari hii alionekana kujiamini isivyo kawaida.
Ndani ya muda mfupi, kila mtu alisikia habari za kampuni tatu kubwa zaidi za ujenzi za Kenya na Tanzania kughairi ushirikiano wao na Mawenzi Investments. Siku iliyofuata, hisa za kampuni hiyo zilishuka kwa pointi nane.
Alasiri hiyo, Lisa alikuwa anakula chakula cha

mchana kantini wakati Alvin alipompigia simu. Sauti ya Alvin ilipambwa na kiburi. “Unatakiwa uniombe msaada. Nitasuluhisha suala hilo na kampuni za ujenzi ikiwa utakubali kunitaliki.”
“Usijali. Nitalitatua mwenyewe.” Lisa alimkata stimu kabisa.
Tabasamu la kijeuri lilienea usoni mwake. "Thubutu, hata kama utawaita mabosi wa kampuni hizo na kuwapa rushwa ya ngono hutaweza kutatua jambo hili."
Mwanamke akacheka. “Kweli umedhamilia kunitaliki kwa nguvu zote? Maana si nguvu hizi unazotumia kubadilisha mawazo ya watu.” "Umejitakia mwenyewe hili." Sauti yake haikuwa ya kirafiki. “Nisingefika mbali kama hukumkosea Sarah na kuendelea kuburudisha ndoto zako hizo nzuri. Ninakushauri usaini hati hizi mapema na kwa utulivu wa akili au sitajali kupoteza wakati wangu kuendelea kucheza mchezo huu na wewe.”

"Inaonekana kama mpenzi wako wa maisha yako amekuwa akikushinikiza sana nikutaliki ili umuoe," Lisa alijibu bila kujali. "Unaweza kuendelea kufanya chochote unachotaka."
Sauti yake isiyo na hasira ilimkera sana Alvin hivi kwamba akakaribia kutupa simu yake chumbani. Hakika, angeweza kuwa mkaidi na kujidai yote aliyotaka kwa muda huo lakini hakuweza kusubiri kuona majuto usoni mwake baada ya siku tatu.
Ilikuwa ni mida ya saa kumi jioni ambapo Lisa alimkuta Meneja Halua kutoka Idara ya Masoko akipapasana na Sarah alipotoka kwenye lifti.
Sarah haraka alisema alipomkaribia, “Lisa, usielewe vibaya. Meneja Halua na mimi tunajadili kazi tu.”
Meneja Halua aliinua macho yake kwa aibu. “Bi Njau, huna haja ya kujieleza. Kwa maana, leo inaweza kuwa siku ya mwisho ya Mwenyekiti Jones katika kampuni hii.”

Lisa alimtupia jicho meneja huyo bila kujali. Kujiamini kwake na uwepo wake wa kutawala ulijaza chumba. Meneja alihisi wasiwasi kwa sekunde ya haraka kabla ya kujifanya ana utulivu wa kutosha.
“Lisa, tulikuwa tunazungumza tu. Usifanye mambo kuwa magumu kwake kwa sababu tu una kinyongo dhidi yangu.” Sarah alijiweka mbele ya meneja.
“Bado unafanya nini hapa Sarah?” Lisa alijibu kwa upole, "Huwezi kuishi siku hata moja bila kuja kufanya show mbele yangu, huh?"
"Sii ... sikuwa..." Sarah alionekana mwenye huzuni ghafla kana kwamba anataka kulia. “Nilisahau kukabidhi baadhi ya nyaraka kwa Meneja Halua nilipoondoka jana. Ndiyo maana niko hapa leo.”
"Meneja Halua, chukua hizo nyaraka na urudi kazini haraka. Bado ni saa za kazi. Sijali kama ungependa kuzungumza na Sarah, lakini una

wakati wote wa kuzungumza naye baada ya saa za kazi.”
Lisa hakuweza kujisumbua kushughulika na watu hao na akageuka kwa nia ya kuondoka. Bila kutarajia, ghafla Sarah akablock
kwa mbele ili kujigongesha kwenye mabega yake. Mara Sara akajikongoja hatua chache nyuma na kuanguka chini.
“Sarah.” Kivuli kirefu kilikimbia kumsaidia mwanamke huyo asianguke chini. Lisa alielewa kila kitu ndani ya sekunde chache. Alikasirishwa na ulaghai huo wa uwongo kupita kiasi.
“Alvinic, sikujua kama upo hapa,” Sarah alisema mara moja, “Usielewe vibaya. Lisa hakufanya hivi makusudi.”
“Acha kumtetea. Niliona kwa macho yangu kwamba alikugonga kimakusudi.” Alimtazama Lisa kwa hasira. “Hujabadilika hata kidogo baada ya miaka mitatu. Bado ni mkatili kama

hapo awali. Fanya haraka na kuomba msamaha, la sivyo?"
“La sivyo nini?” Lisa alikosa la kusema. Miaka mitatu iliyopita, ni yeye ndiye aliyekuwa akinyanyasika bila huruma. Ilikuaje akawa mkatili sasa? Hakukuwa na kitu kingine ambacho angeweza kusema. Lakini, alipitia matukio kama hayo mara nyingi sana kwake kuwa na hasira juu yake tena.
“Alvin, umewahi kusikia kuhusu kitu kinachoitwa kamera za uchunguzi? Unaweza kuangalia ni nani aliye na makosa kwanza kabla ya kutoa shutuma?” Lisa alisema kwa utulivu.
Sarah alionekana kufadhaika lakini Alvin hakuliona hilo hata kidogo. Muda wote alikuwa akimwangalia Lisa kwa hasira. "Unamaanisha kwamba nisiamini macho yangu mwenyewe lakini niamini kamera za uchunguzi ambazo zinaonyesha mtazamo tofauti kutoka kwa pembe tofauti?"

Lisa alisugua kichwa chake. Alitamani sana kumfokea na kumwambia kwamba mtu anaweza kuona mambo kwa macho yake kutoka pembe tofauti pia. Alijiuliza ikiwa huenda Sarah alimlaza akili ili asiwe na akili hata kidogo kila anapokuwa mbele ake.
“Alvinic, achana naye. Twende,” Sarah alimuomba huku akimvuta mkono mwanaume huyo.
Meneja Halua alisema kwa haraka, “Bwana KImaro, hakika unapaswa kumtetea Bi Njau wakati huu. Alikuwa hapa kunikabidhi nyaraka fulani. Alikuwa akinikumbusha maelezo ya ziada wakati Mwenyekiti Jones alikuja kusema kwamba Miss Njau alikuwa akifanya show na kuanza kumkaripia. Bila kutaja alikuwa akimaanisha kuwa tulikuwa tunapoteza muda kwa kupiga gumzo. Yeye hata... Yeye hata...”
“Ongea.” Macho ya Alvin yaliyokuwa yamemkodoa yalijawa na hatari.

Meneja Halua alisema kwa kusaga meno, "Hata alijisifu kuwa nguo za ndani alizovaa leo zilinunuliwa na wewe."
Sarah aliinamisha kichwa huku machozi yakimlenga lenga.
“Naweza kueleza hilo. Sarah, si unajua jinsi ninavyojisikia kuhusu wewe kwa sasa? Ninajisikia vibaya hata nikimtazama tena mwanamke huyu sasa.” Alvin alifadhaika, bila kutarajia kwamba uamuzi wake wa jana usiku ungemuumiza Sarah.
Ghafla, akampa Lisa jicho la kutoboa ngozi. Wafanyakazi waliokuwa wamekusanyika kuangalia zogo hilo walionekana kushangaa.
Kama ilivyotokea, Bwana KImaro hakuwa na hisia kwa Mwenyekiti Jones tena. Hata alichukizwa naye. La hasha, walipaswa kujaribu zaidi kumfurahisha Sarah badala ya kumuunga mkono Lisa. Baadhi yao walijutia sana uchaguzi wao wa kumuunga mkono Lisa.

Lisa hakuwa na neno la kujibu. Sio tu kwamba alikuwa hana la kusema, lakini pia alijisikia kucheka kwa upuuzi ule. Alijiona mjinga kwa kutorekodi mazungumzo yao mapema. Tazama, watendaji wa kampuni yake walikuwa wakishirikiana na Sarah kumshtaki.
“Lisa, hata mimi nilifikiria kukusaidia kwenye tukio la kampuni za ujenzi zilizokususia kwani zamani tulikuwa mke na mume. Lakini sitafanya hivyo tena.” Sauti ya Alvin ilikuwa baridi kama barafu. “Kuanzia leo na kuendelea, nitahakikisha watu wote wanajua kuwa sina uhusiano tena na Mawenzi Investments. Isitoshe, yeyote ambaye atathubutu kukusaidia atakuwa akipambana na mimi moja kwa moja.” Kisha, akatoka nje ya kampuni bila kuangalia nyuma huku akiwa amemshikilia Sarah kwa karibu.
"Bwana KImaro, tafadhali subiri." Mkurugenzi Gumbo na wengine haraka walimfuata. Hata hivyo, Alvin aliwapuuza kabisa na kuingia kwa kasi kwenye gari lake.

Wajumbe wa bodi walikasirika na kurudi mbio kumkaripia Lisa, “Sijui unataka kufanya nini lakini kwanini uishushe kampuni pamoja nawe? Angalia ulichofanya! Neno moja tu kutoka kwa Bwana KImaro na hakuna mtu atakayethubutu kufanya biashara nasi tena."
“Mtu kama wewe hastahili kuwa mwenyekiti. Ondoka hapa!” Mkurugenzi Wande alipiga kelele.
Wafanyakazi na wanahisa wengine pia walianza kuzungumza nyuma yake. “Anafanya nini hapa? Kampuni ilikuwa ikipanda chini ya uongozi wa Mwenyekiti Njau. Hata nilipata mamia ya maelfu ya dola katika bonasi za mwisho wa mwaka katika miaka ya hivi karibuni.”
"Ni bahati mbaya sana kwamba tumekwama na mwenyekiti wa aina hii."
"Sawa, tunapaswa kuuza hisa zetu hivi karibuni na kuwekeza mahali pengine kabla

hatujachelewa."
“Sasa kwa vile umesema, basi lazima nijitayarishe pia.”
TUKUTANE KURASA 331-335
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA SABA
SIMULIZI........................LISA KURASA......331 MPAKA 335
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY WHATSAPP: +255628924768

Sura ya: 331
Lisa alichokonoa masikio yake kwa vidole na kuhema. "Ninasikitika sana kwa kila mtu pia. Sikujua kwamba kurudi kwangu kungedhuru watu wengi, nitarudi na kufikiria njia zingine."
“Potelea mbali. Usirudi tena.” Mkurugenzi Gumbo alikasirika sana hata hakutaka kumuonyesha adabu yoyote. "Bila shaka, tunaweza kukupa nafasi ikiwa utapiga magoti na kuomba msamaha wa Bwana Kimaro na Bi. Njau."
"Hiyo haiwezekani. Ni afadhali kampuni isambaratike kuliko kuinamisha kichwa changu kwa wapenzi hao wasio na haya.” Lisa kwa ukaidi alisema hivyo na kuondoka huku kukiwa na shutuma za kila mtu.
Alipofika nyumbani, polepole alianza kutengeneza kikombe cha kahawa. Amba alikuwa kwenye hatihati ya kupiga magoti na kumlilia kumsihi ili akamwombe Alvin msamaha.

"Mwenyekiti Jones, makampuni ambayo yalikuwa yanaendelea kufanya kazi pamoja na kampuni yetu yanatishia kuvunja ushirikiano wao. Tafadhali fikiria kumuomba msamaha Bwana Kimaro...”
“Usiwe na haraka.” Lisa alikoroga kahawa yake. "Amba, ninakupa nafasi ya kuruka hadi kileleni sasa."
“Nafasi gani? Una uhakika haitanifanya niporomoke badala yake?” Amba alikuwa karibu kuachia machozi.
Lisa alimpiga jicho kali. Akatoa kadi nyeusi kwenye pochi yake na kumtupia. "Kuna shilingi bilioni sabini ndani yake. Baada ya siku mbili, nunua hisa zote kutoka kwa wanahisa wa Mawenzi Investments.”
Amba karibu adondoke magotini. "Mwenyekiti Jones, kwanini una pesa nyingi kiasi hiki?" Ilikuwa ya ajabu. Ni nini hasa kilikuwa kimempata katika miaka hiyo mitatu?
“Unataka kuchukua nafasi hii, au unataka kuniuliza maswali tu?” Lisa aliuliza.

"Ndio ndio ndio..." Amba alivutiwa kabisa.
"Kwa wakati huu, wanahisa lazima wawe na hofu. Ikiwa kuna mtu aliye tayari kununua hisa, bila shaka ataziuza kwa bei ya chini. Shilingi bilioni sabini za Kenya ni zaidi ya pesa za kutosha.” Lisa alimfafanulia.
“Lakini Bi. Jones, tukinunua hisa, utakuwa mwenye hisa pekee kwenye kampuni. Utakuwa na udhibiti kamili, ndiyo, lakini pindi Kimaro akikandamiza kampuni, Mawenzi Investments haitakuwa na mustakabali. Kwanini unataka kupoteza pesa hizi?”
“Nani alisema hakutakuwa na mustakabali?” Lisa alimtazama kwa pembeni. “Tayari nimewasiliana na kampuni za ujenzi. Ninachukua tu fursa hii kubadilisha muundo wa kampuni. Kuanzia sasa na kuendelea, sitaki kumsikiliza mtu yeyote ambaye anataka kwenda kinyume na mimi katika kampuni.”
Amba alishangaa. Hii ilikuwa mara ya kwanza kuhisi kwamba Lisa alikuwa tofauti na hapo awali.
•••

Usiku, wanaume kadhaa walikusanyika kucheza poker kwenye chumba cha hoteli ya nyota tano. Rodney alicheza kadi ya Mfalme, kisha akaanzisha mada. "Nilisikia kwamba wanahisa wa Mawenzi Investments wanauza hisa zao kwa bei ya kutupa."
Alvin alikuwa akigonga meza bila kujali. "Kuziuza ndio njia pekee ya wao kuzuia hasara zao zaidi. Kampuni hiyo ni lazima ifilisike kabisa. Hakuna mtu anayeweza kumuokoa Lisa wakati huu.
Chester aliwasha sigara. “Hebu fikiria, si umekuwa ukihisi hatia tangu alipokufa kwa miaka hii mitatu? Amefanya nini tena kukukasirisha?”
Vidole vya Alvin vikawa ngumu. Baada ya muda, alisema, “Alinitishia kwa kutumia cheti cha ndoa. Ana hamu ya kifo."
“Huogopi kwamba akikutishia tena, Sarah ata...”
“Haina maana. Hakika ninampa somo muda huu,” Alvin alisema. “Na hana pa kutokea ila

kwa kunidondokea na kuniomba msaada wangu.”
"Nilisikia kwamba maeneo muhimu ya ujenzi chini ya Mawenzi Investments yameacha kufanya kazi kwa siku tano. Wamepoteza zaidi ya dola bilioni. Watu wengi walionunua nyumba hizo wanadai kurejeshewa fedha.” Rodney alicheka na kucheza karata yake ya mwisho. "Nimeshinda. Lipa."
Wakati Alvin akitoa pesa zake nje, alitazama simu yake iliyokuwa kando yake bila fahamu. Je, mwanamke huyo hakuwa tayari kupiga simu kuomba msamaha na kukubali makosa yake bado? Hata hivyo, kuomba msamaha ingekuwa bure sasa. Lisa hakupaswa kamwe kumuumiza Sarah.
•••
Kesho yake asubuhi, nyumbani kwa Alvin, wajakazi walitoa kifungua kinywa kwenye meza. Sarah alimimina glasi ya maziwa ya moto kwa Alvin kwa furaha, kisha akasema kwa kusitasita, “Tayari ni siku ya sita. Nadhani Mawenzi Investments inapaswa tu uisamehe Hubby.”

Macho meusi ya Alvin yalimtazama. "Wewe ni mtu mpole sana."
Sarah alicheka kwa uchungu. "Nimefanya kazi huko kwa miaka miwili, baada ya yote."
"Wacha tupate kifungua kinywa." Alvin alimenya yai lililochemshwa kwa ajili yake.
“Alvinic,” Sarah alisema kwa hisia tofauti, “Je, kweli huna hisia na Lisa? Hujawahi kunisindikiza kwenda kununua chupi hapo awali. Nimekuwa nikijaribu kujishawishi siku hizi lakini bado ni ngumu kwangu kukubali. Kila nikifikiria jambo hilo, moyo wangu unauma sana hivi kwamba nashindwa kupumua.”
“Hapana.” Alvin alikanusha waziwazi. "Samahani. Sitafanya tena jambo lolote la kukuudhi.”
“Sawa,” Sarah alijibu huku akitabasamu kwa lazima.
Alvin alikuwa na hisia za huzuni moyoni mwake. Aliapa kumpa adhabu kali zaidi Lisa na kumtendea vyema Sarah.

"Bwana Kimaro, Hisa za Mawenzi Investments zilifikia kikomo mara tu soko la hisa lilipofunguliwa asubuhi ya leo," Hans aliingia ghafla na kusema kwa sauti ya chini.
“Ni nini kinaendelea?” Alvin alimtupia jicho kali.
Hans akapepesa macho. "Saa 7:00 asubuhi ya leo, Kilimani Group ilitangaza ushirikiano na Mawenzi Investments kwenye tovuti yake ya kimataifa."
Sarah alikuwa na hisia mbaya. "Kampuni ya Kilimani Group ni maarufu sana?"
Hans alielezea, "Kilimani Group sio maarufu tu, historia yao inarudi nyuma zaidi. Zaidi ya wasanifu mia moja wa juu kutoka kote Afrika Mashariki wamekusanyika hapo. Kampuni hii ndiyo kampuni ya ujenzi yenye mapato makubwa zaidi Afrika Mashariki na wana sifa kubwa. Kilimani Group imeshiriki katika takriban kila mradi wa kitambo ambao umesifiwa na watu kote hapa nchini na Afrika Mashariki kwa ujumla. Wakati huo huo, wasanifu wa Kilimani Group wamepokea tuzo zote za kimataifa kwa miaka kumi mfululizo.”

Mkono wa Sarah uliokuwa umeshika uma ulikaza, na yeye mwenyewe hakujitambua. "Kwanini kampuni kama hiyo ifanye kazi na Lisa? Hawaiogopi KIM International?"
Hans akatikisa kichwa. "Kilimani Group mara nyingi hufanya kazi na serikali kwenye nchi hizi za Afrika Mashariki. Hawaogopi mtu wala kampuni yoyote.” Alisita na kusema tena, “Zaidi ya hayo, kampuni ya Ruta Design, inayoongoza huko Uganda na yenye tawi lake Tanzania na hapa Kenya pia imetangaza kuwa wametia saini ushirikiano wa miaka kumi na Mawenzi Investments. Timu ya ujenzi ya Ruta Design iliwekwa kwenye saiti ya ujenzi ya Mawenzi Investments jana usiku.
“Ruta Design?” Sarah alishikwa na hamu ya kupiga kelele. "Hiyo ni kampuni gani ya uwongo? Sijawahi kusikia kabla.”
Hans alimtazama kwa kina. "Ingawa mkurugenzi wa Ruta Design, Joseph Ruta, ni kijana, aliwahi kuwa mmoja wa wasanifu watatu bora huko Uganda. Yeye binafsi alibuni hoteli moja na pekee ya nyota saba huko Uganda. Baada ya hapo, alianzisha kampuni ya usanifu. matawi ya kampuni yake yanaweza

kupatikana karibu miji yote mikubwa nchini Uganda, Tanzania na Kenya, na yanaendelea kwa kasi miaka hii. Lazima uwe umesikia kuhusu Mradi wa Kigamboni Satelite City huko Tanzania miaka miwili iliyopita. Ilifanyika kwa ushirikiano na Ruta Design, na likawa eneo la makazi lenye gharama kubwa zaidi nchini Tanzania. Bei yake ni shilingi 140,000 kwa kila futi ya mraba, na watu hata waliingia wazimu kuinunua.”
"Joseph Ruta ... Inaonekana hanifikii kwa chochote." Alvin alicheka, lakini sauti yake ilikuwa ya kujilazimisha kana kwamba chuki ilikuwa ikipita ndani yake. Wale waliokuwa wanamfahamu walijua ni ishara kwamba alikuwa na hasira.
Hans alimkumbusha kwa kuchanganyikiwa, “Bwana Mkubwa, hukumbuki huyu jamaa?”
“Unakumbuka nini?” Alvin aliuliza kwa ukali.
Hans alipumua. “Bi. Lisa alikuwa mfanyakazi katika Ruta Design hapo awali. Joseph alikuwa mwandamizi wake.”
Sura ya: 332

Alvin alipigwa na butwaa. Hakuwa na kumbukumbu yake hata kidogo.
Hata hivyo, kutokana na ugonjwa wake mara ya mwisho, alikuwa amesahau mambo mengi. Ilikuwa kawaida kwamba hakuweza kukumbuka.
"Sijawahi kujua ... Lisa alikuwa na mwandamizi kama huyo." Sarah alikasirika kiasi cha kutaka kutema damu. Hapo awali alifikiria kuwa angeweza kumwangamiza kabisa Lisa wakati huu. Hakutarajia kamwe Lisa kuhusishwa na kampuni kubwa kama hizo za ujenzi.
Mwangaza ulipita machoni pa Sarah. Alifanya kama alikuwa na wasiwasi na akasema, "Hata kama Joseph alikuwa mkuu wa Lisa ... hana uwezo wa kwenda kinyume na Alvinic. Angalia hadhi ya Alvinic.”
Uso wa Alvin ulibadilika sana. Hiyo ilikuwa sawa. Kwanini mtu asiyefahamika kama huyo aende kinyume naye kwa ajili ya Lisa?
“Lisa asingeweza kuuza mwili wake, sivyo?” Sarha alichombeza. Alvin alipomfikiria Lisa

kuwa karibu na mwanaume mwingine, alihisi wimbi la hasira isiyoelezeka.
Hans alikosa la kusema. Sarah alikuwa amebobea kabisa katika ustadi wa kuchomekea uchochezi kati ya watu. Hakupaswa kusema chochote.
“Chunguza ni nani hasa alinunua hisa za Mawenzi Investments kwa bei ya chini." Alvin ghafla akakumbuka kitu na kumuamuru Hans.
“Sawa.” Hans akaitikia kwa kichwa. Ilikuwa kazi rahisi. Alitakiwa tu apige simu idara husika ili kupata taarifa hizo. Muda mfupi baadaye, alirudi kwenye chumba cha kulia akiwa na habari kamili. "Watu waliokuwa nyuma ya pazia ambao walikuwa wakinunua hisa walikuwa Lisa na Chris Masunga."
“Ah!” Sarah akatoa macho. Haraka akawa ameelewa kitu. "Lisa alikuwa amepanga tangu mwanzo. Kwa makusudi aliwafanya wanahisa wa Mawenzi Investments kuingiwa na hofu na kisha akanunua hisa zao kwa bei ya chini. Sasa, Mawenzi Investments ni mali ya Chris na yeye. Chris anafanya kazi chini yake."

Mshindo ukasikika! Kijiko kilitupwa kwenye sahani na kikatoa sauti ya wazi na ya kutoboa masikio. Alvin alisimama mara moja na kukipiga teke kiti kilichokuwa mbele yake. Hah! Alikuwa amemchukulia poa kabisa mwanamke huyo. Hapo awali alikusudia kumwangusha bila huruma. Alvin hakuwahi kufikiria kwamba njia zake alizokuwa akizitumia kumwangusha Lisa ndizo zilizomnyanyua mwishowe.
Kabla ya hili, Alvin alikuwa amepoteza mabilioni kadhaa kuwahonga wanahisa wa Mawenzi ili wawe upande wake. Lakini, iliibuka kuwa Lisa alikuwa akinunua hisa za wanahisa hao wasimotii kimya kimya. Aliwaondoa watu kwenye kampuni hiyo ambao hawakufuata maagizo yake na akafanikiwa kuwa mtu pekee aliye madarakani. Thamani ya soko ya kampuni ingepaa kwa urahisi hadi kufikia makumi ya mabilioni kwa kuweza pia kupata ushirikiano wa makampuni yenye sifa nzuri. Lisa, oh Lisa! Alimshangaza sana!
Sarah alikasirika kwa siri kiasi kwamba alikaribia kusaga meno hadi yakavunjika. Hapo awali, alidhani angeweza tu kumfanya Lisa afe, kama miaka mitatu iliyopita. Hata hivyo, hakuthubutu tena kumdharau Lisa.

•••
10:00 asubuhi, Ofisi ya mwenyekiti wa Mawenzi Investments ilikuwa katika machafuko. Mkurugenzi Gumbo alivunja chombo kwa hasira. "Lisa Jones, unacheza na sisi? Kwanini hukutuambia kuwa tayari ulikuwa kwenye mazungumzo na Kilimani Group na Ruta Design tangu mwanzo? Umetutia hofu bila sababu na hata hisa zetu tukauza kwa bei ndogo. Matokeo yake, ulinunua hisa kwa bei nafuu. Wewe ni mkatili sana! Je, Sheryl alizaaje binti mpuuzi kama wewe?”
“Lazima uturudishe hisa zetu. Kama sivyo, haya hayatakuwa na mwisho.” Mkurugenzi Williams alipiga meza kwa nguvu.
“Nimeona sehemu yangu ya watu waovu, lakini sijawahi kukutana na mtu mbaya kama wewe. Mawenzi Investments ilianzishwa na sisi sote. Badala yake, unafanya chochote kinachohitajika ili kutuhadaa. Kama mtu, unapaswa kuwa na mapungufu fulani ya kimaadili.”
“Bibi mdogo, wewe bado kijana. Usiwe mkatili sana na usichome madaraja yako. La sivyo, ungekuwa umekufa kabla hujajua.”

Akiwa amekabiliwa na karipio na ukosoaji wa wanahisa wale waroho waliouza hisa zao, Lisa alikunywa kahawa polepole kabla ya kukiweka kikombe mezani kwa kishindo kikubwa.
Ofisi ilinyamaza kimya. Lisa aliinua kichwa chake. “Kila mtu anielewe, sikutaka kuwa mtu asiye na huruma lakini wakati wa mkutano wa kwanza niliporudi, niliwaambia nyote kwamba kampuni hii haikupewa jina la familia ya Kimaro. Hata hivyo, nyie bado mliwaabudu Alvin na Sarah kana kwamba ni mababu zenu. Siku chache zilizopita, Alvin na Sarah walikuwa wakinitusi kwenye ukumbi wa kampuni. Ninyi nyote wenye hisa mlikuwa kama mbwa wanaolamba miguuni mwao ili kuwafurahisha. Mliniambia hata nipotee. Kwa kuwa nyote mnapenda kuwalambalamba hao wawili, nendeni mkawatafute basi.”
“Tulifanya hivyo kwa sababu hatukutaka kuwaudhi na kupoteza nguvu ya kampuni. Ilikuwa ni kwa ajili ya kampuni,” Mkurugenzi Gumbo alisema kwa unyonge, “Kama ningejua kwamba tayari ulikuwa umepata kampuni za ujenzi, je, ningekosa aibu hivyo? Nilifanya hivyo kwa ajili ya kampuni."

"Hiyo ni sawa. Tumeifanyia kampuni mengi miaka hii mitatu. Ulikuwa wapi wakati huo?”
"Ikiwa hautaturudishia hisa zetu leo, usifikirie hata kutoka nje ya mlango huu."
“Kweli? Nataka kuona jinsi utakavyonizuia kuondoka.” Lisa alicheka. Ghafla, walinzi zaidi ya 20 waliingia na kuwazunguka wanahisa. Walipoona hali hii, zaidi ya nusu ya kiburi chao kilipungua.
Mkurugenzi Wande alifikiria kitu na kupiga magoti mara moja. "Lisa, tupe wanahisa huruma yako. Sisi ni wazee, tunataka tu kupata bonasi ili kujikimu.”
"Ndio, tutakusikiliza kuanzia leo."
"Tunapaswa kila mmoja kuchukua hatua nyuma na kuweka kipaumbele katika kuleta amani."
Lisa akasugua macho yake. Ilionekana kana kwamba walikuwa wakifanya hivyo kwa njia laini kwa sababu njia ngumu haikufanya kazi.

“Inatosha. Mkurugenzi Wande, ulienda hata kumpa Sarah zawadi jana. Na Mkurugenzi Williams, tayari wewe ni mzee sana, lakini hukuchoka kumfuatafuata nyuma Sarah kama mkia. Sijawahi hata kukusikia ukiiombea kampuni. Ulikuwa ukinifokea tu mbele ya Sarah muda mwingi.
“Si hivyo tu. Mkurugenzi Gumbo, nilikuwa nimeshachukua nafasi hii lakini kwa nini bado ulikuwa unaripoti mambo ya kampuni kwa Alvin kila siku bila kuacha chochote?” Lisa alimfichua kila mmoja wao. Nyuso zao zilikuwa na rangi nyekundu kwa aibu.Hakuna aliyetarajia Lisa kujua kuhusu mienendo yao waziwazi.
“Nimewafukuza nyinyi kutoka kwa bodi ya wakurugenzi kwa sababu mioyo yenu haipo hapa tena. Unataka tu kupata samaki wakubwa kama Alvin na Sarah. Unafikiri kila kitu kitaenda sawa mradi tu unawategemea, sivyo?" Lisa alisema kwa huzuni, "Kwenu, mimi ni mtu asiye na uaminifu wowote. Mnafanya jambo moja mbele yangu na jingine nyuma ya mgongo wangu. Sitaki kuwa na sauti nyingi katika kampuni. Nataka tu sauti yangu mwenyewe isikike. Kuanzia leo na kuendelea,

nyinyi hamtakuwa na uhusiano wowote na Mawenzi Investments. Usalama, wafukuzeni wote na msiwaruhusu tena katika siku zijazo."
Walinzi hao walichukua hatua haraka na kuwafukuza wanahisa wote.
Ofisi ikawa tupu mara moja. Chris alisema kwa hisia, “Lisa, unazidi kuwa mwenyekiti sasa. Una nguvu zaidi kuliko mama yako alivyokuwa wakati huo. Najiona duni ikilinganishwa na wewe sasa.”
"Mjomba Chris, kampuni itategemea mimi na wewe kuanzia sasa." Lisa alitabasamu.
Sura ya: 333
Wakati wa ukaguzi jioni, Lisa alipofika tu katika Idara ya Masoko, alimwona mwanamume akigeuka na kuondoka alipomwona.
"Meneja Halua, si vizuri kumkwepa mwenyekiti wa kampuni unapomuona, sawa?" Lisa alimwita kwa tabasamu la uwongo.
“Mwenyekiti... Mwenyekiti Jones, samahani. Kwa kweli sikukuona.” Meneja Halua alijikaza na kurudi nyuma kuomba msamaha.

"Macho yangu hayako vizuri sana."
"Nadhani sio macho yako tu ambayo hayako vizuri sana lakini mdomo wako pia." Lisa alitabasamu kwa kucheza na kusema, “Kwa mfano...
unajua sana kusema mambo ambayo ni ya uzushi.”
Miguu ya Meneja Halua ilikuwa ikitetemeka kidogo. Alikuwa amefikiria kweli kwamba Mawenzi Investments ingesambaratika au Lisa angefukuzwa nje ya kampuni. Lakini ikatokea ndivyo sivyo.
“Meneja Halua, umefukuzwa kazi. Ondoka mara moja. Ninaamini hutatilia shaka uamuzi wangu kwani tayari umeshapata mtu wa kukuunga mkono. Kampuni inayofuata hakika itakukaribisha." Baada ya Lisa kumnong'oneza sikioni, alipiga hatua za kifahari na kuendelea kuelekea Idara ya Masoko.
Meneja Halua aliuma meno. Aligeuka nyuma na kusema kwa sauti kubwa, “Kuna shida gani hata kama nikiondoka? Bi. Njau anakaribia kuwa mke wa mtu tajiri zaidi nchini Kenya.

Baada ya kuondoka mahali hapa, atanipanga kuingia KIM International.”
Wakati msaidizi wa Lisa, Amba alipokuwa karibu kumkemea, Lisa alimgonga begani na kumzuia. "Usipoteze nguvu na muda wako!"
Baada ya wao kuondoka, Amba alisema kwa hasira, “Mwenyekiti Jones, kwanini hukumfundisha somo?”
“Hakuna haja, nimeshafanya hivyo,” Lisa alisema kwa utulivu.
Nusu saa baadaye. Meneja Halua alikuwa karibu kuondoka baada ya kufunga. Hata hivyo, alipofika kwenye milango, kulikuwa na polisi wa kumkamata. “Kampuni yako imetoa ripoti polisi. Unashukiwa kufanya ubadhirifu. Tufuate kituo cha polisi.”
“Sikufanya hivyo! sitaki!” Meneja Halua alipiga kelele. Hapo awali wakati Sarah akiwa ni mwenyekiti, wale ambao walikuwa na msimamo kama wake wangeiba pesa, na kila mtu alifumbia macho. Katika kipindi hicho alipochukua upande wa Sarah, alikuwa ametapeli pesa nyingi sana kwa jina la

kampuni. Baada ya Lisa kuingia iliripotiwa kama kesi ya uchunguzi. Angelazimika kwenda jela.
“Acha kukurupuka. Tayari tuna ushahidi thabiti. Twende zetu.”
Meneja Halua alichukuliwa na polisi. Habari zilienea katika kampuni.
Amba alipojua jambo hilo, alikumbuka lile somo alilomaanisha Lisa.
•••
Jioni, gari la kifahari la lilisimama mbele ya jengo la kampuni ya Mawenzi. Lisa akaingia kwenye gari. Alipouona uso wa Joseph Ruta, ambao hakuwa ameuona kwa muda mrefu, alitoa tabasamu la kirafiki.
"Joseph, muda umepita."
Asingesahau kamwe kwamba alikuwa ni Joseph ambaye alimpa kazi wakati alipofungiwa na tasnia ya usanifu wa majengo huko Dar es Salaam wakati huo kutokana na hila za Jones Masawe. Hakutarajia kwamba wangefanya kazi pamoja tena baada ya miaka mitatu.
“Lisa, umekuwa mrembo zaidi. Ninakuona kwa mtazamo mpya.” Joseph alicheka. “Twende. Ili

kusherehekea ushirikiano wetu, nitakuandalia chakula.”
“Joseph, mimi ndiye ninayepaswa kukuhudumia. Kampuni yako ndiyo pekee nchini Kenya ambayo ingejitokeza kuniunga mkono,” Lisa alisema kwa unyoofu, “Wewe ndiye mfadhili wangu.”
"Watu wa nje hawajui utambulisho wako kama mkurugenzi wa muundo wa Kilimani Group." Joseph alitania.
"Tuendelee kuweka wasifu wa chini tu." Lisa alisukuma kidole kwenye midomo yake na kufanya sura ya kushangaza. Vicheko vilisikika ndani ya gari.
Saa moja baadaye, gari liliingia uani kwenye hoteli kubwa. Magari machache ya kifahari yalikuwa yameegeshwa uani. Lisa alifahamu hoteli chache zilizotoa huduma nzuri za chakula kama ile. Japo ilikuwa katika eneo lililojitenga, chakula chake kilikuwa na ladha nzuri.

Waliposhuka kwenye gari, kuna mtu alikuja kuwapokea. Alikuwa ni Sam Harrison. Lisa alishangaa kumuona pale maana kumuona Sam maeneo hayo pia ilimaanisha kuwa Alvin na genge lake wangekuwepo pia. Alijikuta anakosa raha ghafla maana kila alipokuwa na wakati mzuri basi Alvin angekuwepo tu ili kumharibia.
“Lisa nilikukumbuka sana. Njoo, nikukumbatie.” Sam alimlaki kwa furaha.
“Bwana Harrison...” Lisa alikunja uso kuonyesha kutofurahishwa kwake.
“Usinifikirie sana Lisa. Najua unahofia kukutana na Alvin na wengine,” Sam akaeleza haraka ili kusafisha hali ya hewa, “nilikuja Nairobi nna Bwana Joseph na hivyo nilimwalika kwa chakula hapa na marafiki zangu. Sikuwa naelewa kama nyie tayati mmekutana na angekuja na wewe hapa!”
“Basi itabidi niondoke, wewe mwenyewe unajua namna mambo yanavyokuwaga nikikutana na genge la Alvin.” Lisa alitoa wasiwasi wake.

“Usijali, mimi nipo nitasuluhisha hilo.” Sama alimtoa wasiwasi.
“Kwani....” Joseph alitaka kuongea kitu lakini kabla hata hajamaliza usemi wake, sauti kali ilisikika.
“Nyie...” Alvin akageuka. Alishangaa kumuona Lisa akitoka na kijana mtanashati. Mwanaume huyo alikuwa amevaa suruali ya jeans na shati la khaki. Nywele zake fupi zilikuwa zimekunjamana kidogo, na alionekana kama mtu mashuhuri—aliyekuwa na mvuto mzuri!
Kwenye mkono wa kijana huyo kulikuwa na mkoba wa wanawake wa rangi ya zambarau, na ni wazi ulikuwa wa Lisa.
Mwanamke huyo... Hawakuwa wametalikiana bado lakini tayari alikuwa akishirikiana na wanaume wengine. Ubaridi ulitanda kwenye macho meusi ya Alvin. Wakati huo, Lisa aliona kundi la watu pia. Alipepesa macho na kumtazama Sam bila la kusema neno. Sama aligusa pua yake kwa unyonge.
Sarah ghafla akasema, “Sam, marafiki uliosema unakuja kuwapokea sasa hivi walikuwa... ndo hawa?”

“Ndiyo.” Sam aliitikia kwa kichwa tu. "Lisa anafahamiana na Bwana Joseph Ruta. Nilikuwa nimepanga nikutane naye kwa chakula. Lakini najua wewe na Lisa hamna maelewano mazuri, kwa hiyo tutaondoka sehemu nyingine.” Akapunga mkono na kuelekea upande wa Lisa.
Cindy alisema kwa kusitasita, “Kwa kuwa kila mtu anamjua mwenzake, hakutakuwa na shida. Kwanini tusiende pamoja kwenye jumba la klabu? Tukiwa wengi zaidi ndivyo inavyopendeza zaidi.”
Macho ya kila mtu mara moja yalitua kwake. Chester alikunja uso huku Alvin akitabasamu. “Siyo jambo lisilowezekana. Inatokea kwamba nina kitu nataka kujifunza kutoka kwa Mkurugenzi Jones. Ulianza lini kupanga hila hiyo ya biashara ili kufufua kampuni licha ya kuwa katika hali isiyo na matumaini? Nadhani tukijumuika pamoja itakuwa vizuri zaidi.”
Lisa aliinua macho yake kwa uvivu. Alipotaka kuongea, ghafla alifoka. “Samahani, sikukusikia vizuri, ulikuwa unasema?"

Wakati kila mtu alipofikiri kwamba Alvin alikuwa karibu kuachia hasira yake kwa Lisa, ghafla alitabasamu. "Unafikiri kwamba hali yako itabadilika kwa sababu tu thamani ya soko ya Mawenzi Investments imeongezeka? Lisa, kukuangamiza ni rahisi kama vile kumkanyaga sisimizi chini ya miguu yangu.”
Lisa alisafisha sikio lake kwa kidole. "Nadhani sasa nimeelewa maneno yako, na ninakushukuru sana kwa kweli. Bila wewe kunipa changamoto nisingepata akili hii. Ningekuandalia chakula cha jioni ukipendacho kama shukrani lakini naogopa kundi hili la watu ulilofuatana nalo. Je, ninahitaji kuwahudumia pia? Hata nikiwa na pesa nyingi, hazikuanguka kutoka angani.”
Sarah, Chester, Rodney, na Cindy walichukulia maneno ya Lisa kama dhihaka kwao. Nyuso zao zilibadilika.
Chester alisema kwa sauti isiyo ya kirafiki kabisa. “Lisa, ni miaka mitatu imepita bado haujaonyesha maboresho. Umeuchoka ulimi wako?”
“Kwa kweli siwezi kuthubutu kuwaudhi nyie. Kazi yenu ni kuharibu tu makampuni ya watu wengine na kutishia kukata ndimi zao." Lisa

alishtuka na kutikisa kichwa. Akamgeukia Joseph na kusema, “Joseph, twende zetu.”
Joseph? Alvin alimtazama kwa ujeuri. "Wewe ni Mkurugenzi wa Ruta Design?"
Joseph alitabasamu kwa unyonge. Hakukubali wala kukanusha.
Alvin alitikisa kichwa na kusema kwa ukali, “Vema sana, wewe ndiye mtu pekee ambaye unathubutu kwenda kinyume na mimi katika Kenya yote.”
“Lisa nimetoka naye mbali. Kwake, siogopi vitisho vyovyote.” Joseph alitabasamu na kumgeukia Lisa ambaye alishikwa na butwaa. “Twende zetu.”
“Sawa.” Lisa aliondoka naye wakitembea sambamba.
Sura ya: 334
Wakiwa wanatembea kuelekea kwenye gari, mwanga wa mwezi uliwaangazia kana kwamba walikuwa wanandoa wakamilifu. Kifua cha Alvin kilihisi kana kwamba kuna mtu

amewasha moto ndani yake. Alikasirika. Sarah alimtazama na kukunja ngumi kwa siri.
“Um...mimi naondoka pia. Tuliahidina na Joseph kuwa na chakula cha jioni pamoja.” Sam aliondoka haraka baada ya kusema. "Sam hasomeki kabisa siku hizi," Rodney alisema kwa hasira na kuwageukia wenzake, "Bado tunaenda kwenye jumba la klabu kujiburudisha?"
"Inachosha kwenda kwenye jumba la kilabu kila wakati. Sarah, twende zetu nyumbani.” Alvin alifoka na kuingia ndani ya gari.
Muda mfupi baadaye, gari lilisimama mbele ya jumba la kifahari. “Unaweza kutangulia ndani. Nina miadi na mtu mwingine kujadili mambo kadhaa ya kikazi sasa hivi."
“Mbona sikusikia kuwa ulikuwa na miadi hapo awali?” Sarah aliuliza, nusu-utani.
"Nilisahau kukuambia kuhusu hilo hapo awali." Alvin aliwasha sigara. Alionekana kutokuwa na raha kabisa. “Usinisubiri usiku huu. Lala mapema.”

Sarah akauma meno na kujilazimisha kushuka kwenye gari. Alitaka kusema maneno machache zaidi lakini alichosikia ni exhaust ya gari tu.
Alikanyaga miguu kwa kufadhaika. Hakujua ni kwanini, lakini alikuwa na hisia kali kwamba Alvin alikuwa anaenda kumtafuta Lisa.
Nusu saa baadaye, gari la Alvin lilifika kwenye Hoteli ya Silverland.
Sam ndiye aliyependekeza waende hapo. Sam aliipenda baa hii zaidi katika Nairobi nzima ndiyo maana Alvin alijua kulikuwa na nafasi kubwa sana ya kuwakuta hapo.
Alipousukuma mlango na kuingia ndani, sauti ya kupasua anga ilisikika ikiimba.
'"Ingawa rohoni nimekwisha....
Namuomba Mola anisaidie... Niweze kukusahau kabisaaa ...
Nipate mwingine kushinda weweee "

Alvin akatazama katikati ya ukumbi wa baa. Mwanamke kijana mwenye nywele ndefu zilizomwagika alikuwa ameketi kwenye kiti kirefu. Kichwa chake kilikuwa chini na alikuwa akiimba kwenye kipaza sauti. Alikuwa amevaa suruali ya jeans ya buluu. Mguu wake mmoja uliegemea kwenye kiti kirefu huku mguu wake mwingine ukigusa chini. Alikuwa amevaa jozi ya viatu vya turubai vyenye rangi nyeusi na nyeupe ambavyo vilifichua sehemu ya vifundo vyake vya mguu vilivyo maridadi.
Mwangaza hafifu wa taa za rangi ulioanguka juu yake ulikuwa kama maua ya waridi yaliyochanua usiku. Alishika gitaa la acoustic na kutekenya nyuzi zake kwa vidole vyake vyembamba.
Wanaume walivutiwa na uzuri wake. Wanawake walipiga mayowe kwa sauti nzuri iliyomtoka.
"Kila mtu, wacha tuimbe pamoja." Lisa alisimama kutoka kwenye kiti kirefu. Kasi aliyokuwa akiipiga gitaa ilikuwa inaendana na kasi ya wimbo. Ujuzi wake haukuwa mkubwa sana na wala si duni sana, lakini wimbo ulivutia sana.

Banio la nywele lilitoka nyuma ya sikio lake na nywele zikasambaa kufunika uso wake mzima. Alizirudisha nyuma kwa kutingisha kichwa chake, akifunua uso wake wa kushangaza na wa kuvutia. Uso huo mdogo uling'aa chini ya mwanga hafifu wa rangi, na ilikuwa kana kwamba nyota bilioni zilikuwa zikimulika machoni pake.
Miguu ya Alvin ilikuwa imekwama palepale. Lisa alionekana kama amesimama kwenye jukwaa la tamasha. Mwili wake mzima ulionekana kung'aa. Hakujua kuwa uimbaji wake ulikuwa wa sauti na ustadi zaidi kuliko hata baadhi ya wasanii maarufu. Hakujua kuwa Lisa ndiye alikuwa mwalimu wa Cindy enzi hizo wakiwa shule ya sekondari, akimfundisha kuimba na kumtungia nyimbo pia. Hakujua kuwa angeweza kucheza gitaa pia. Hakuwahi kugundua kuwa anaonekana mrembo sana alipotkuwa akiimba na kucheza jukwaani huku akitabasamu.
Moyo wake ulipiga kwa nguvu. Wimbo ulipoisha, akabaki akitamani zaidi. Sio yeye tu, bali watazamaji wote walihisi vivyo hivyo.

"Msichana mzuri, uimbaji wako ni mzuri sana. Imba wimbo mmoja zaidi!”
"Ni kweli, unaimba vizuri zaidi kuliko hata wale waimbaji kwenye matamasha ya moja kwa moja."
“Msichana mzuri, mimi ni meneja katika kampuni ya muziki. Unataka kusaini mkataba na sisi?"
“Hakuna haja, naimba kwa ajili ya kujifurahisha tu. Nimechoka, hivyo nitapumzika kwanza.” Lisa alishuka kutoka jukwaani. Ngazi za jukwaa zilikuwa za juu sana, na Joseph akaenda mara moja ili kumsaidia kushuka.
Tukio hilo lilimchoma macho vibaya sana Alvin. Watu waliokuwa karibu nao walianza kunong'ona.
“Huyo lazima awe mpenzi wake. Ninamuonea wivu sana kwa kuwa na pisi kali kama hii, utasema ni mungu wa kike!”
"Ndio, sura yake inaonekana nzuri sijawahi kuona! Kwanini sina bahati kama hiyo?"

Alvin akakunja uso. Alitembea kwa hatua ndefu. Wakati Lisa, ambaye ndo kwanza alikuwa ameketi tu anainua glasi yake ili kunywa mvinyo wake, nguvu kali ilimrudisha nyuma kwa ghafla. Mvinyo mwekundu kwenye glasi ulimwagika kote kwenye fulana nyeupe kifuani mwake.
Sehemu ya shati lake iliyolowa sana ilinasa kifuani mwake, ikionyesha mikunjo yake ya kuvutia na mistari iliyofifia chini.
Lisa alipiga kelele. Aligeuka nyuma kwa hasira na kumuona Alvin akiwa na sura yenye hasira na nyororo. "Alvin, una wazimu?"
Baada ya kumkazia macho, kwa haraka Lisa alichukua kitambaa ili kufuta madoa kwenye shati lake. Hata hivyo, haijalishi aliifuta kwa bidii kiasi gani, bado ilishikamana na kifua chake kwa nguvu. Ilifanya hata matiti yake kuonekana kwa mbali kupitia kitambaa laini cha fulana kilicholowa.
"Vaa hii." Mara moja Joseph alivua shati lake la khaki na yeye akabaki kwenye fulana ya ndani. Alitaka kumfunika Lisa, lakini mikono mikubwa ya Alvin ilimzuia kufanya hivyo. Macho ya kina Alvin yalikuwa yakimtazama kwa onyo.

“Bwana Kimaro, si tayari una mpenzi wako? Unaingilia mambo mengine ambayo hayakuhusu kwanin?” Joseph alitabasamu kwa utulivu.
"Unapaswa kumuuliza Lisa kwanini ninaingilia mambo yake." Alvin akalishika lile shati la Joseph na kulitupa huko. "Tuondoke!"
Alipokuwa akiongea, macho yalimtoka Lisa na kuyafanya macho ya Alvin yakawa na joto. Hakuwahi kutarajia kuwa Lisa angekuwa mrembo kiasi hicho. Akikumbuka kuwa ni yeye ndiye aliyenunua nguo za ndani alizovaa chini, hisia zisizoelezeka zilijaa moyoni mwake.
"Ni bahati mbaya gani niliyopata katika maisha yangu ya mwisho kwamba nililazimika kukutana nawe katika maisha haya?" Sauti yake ya kiburi ilimfanya Lisa kuhisi hasira kali.
"Hilo ndilo ninalotamani pia kujua." Alvin aligundua kuwa mikunjo ya kifua cha Lisa bado inaweza kuonekana kwani fulana yake ilikuwa bado imeshikama na mwili.

Alivua shati lake badala yake na kumlazimisha alivae. Lisa aligoma. Ghafla Alvin alihisi kukasirika na kumsaidia kumvalisha kwa nguvu. Ulaini aliouhisi chini ya mkono wake ulikuwa kama unyoya unaoufurahisha moyo wake.
Sura ya: 335
"Alvin, kwa nini umekuja?" Wakati Sam, ambaye alikwenda kujaza sahani nyingine ya nyama, aliporudi, macho yake karibu yadondoke kutoka kwenye soketi zake alipoona tukio hilo. Alitazama huku na kule kwa pupa na kushusha pumzi baada ya kuona yupo Alvin tu. Hakutaka kugongana na Rodney, Sarah, na wengine. Kulikuwa na kejeli zisizoisha kila walipokutana.
“Si nyie mlikuwa mkienda clubhouse? Si unaandamana na Sarah?” Sama aliongeza aliongeza maswali mawili zaidi.
Hilo lilifanya uso wa Alvin kuwa mweusi. “Kwanini uniulize hivyo? Ina maana Lisa hajakwambia japo mmekuwa kwenye ‘hangout’ kwa muda mrefu tayari?” Akageuza kichwa kuelekea kwa Lisa na kuinua macho yake. “Cheti chako cha ndoa kiko wapi? Si huwa

unatembea nacho kila mahali ili kunitishia? Kitoe na uwaonyeshe."
Lisa kidogo akose la kusema. “Huoni hata aibu unaposema hivi kwa sauti? Huoni aibu kwa kutamba na kuringa na mwanamke mwingine wakati kumbe unajua bado kwenye ndoa! Mbaya zaidi unafanya kazi pamoja naye ili kuniangamiza mimi na kampuni yangu. Aibu kwako."
“Unajua wazi kwamba sina hisia na wewe. Ni wewe ndiye unayening'ang'ania. Ulijaribu hata kumuumiza Sarah. Unastahili hayo yote! " Alvin hakuonyesha kujali maneno yake hata kidogo.
Sam alikuwa amemzoea, lakini Joseph alishangaa kusikia maneno yake. "Sikujua kwamba maneno ya mtu tajiri zaidi wa Kenya, Bwana Kimaro ambaye kila mtu anamheshimu, yangekuwa ya ajabu kiasi hiki."
“Unafikiri wewe ni nani wa kuninyooshea kidole?” Midomo myembamba ya Alvin ilionyesha tabasamu la kejeli. "Au unampenda?"

Joseph alisema kwa upole, “Kwani kuna shida gani nikimpenda? Lisa ni mzuri na mrembo. Maadamu yuko tayari na yuko huru kuolewa nami, ninaweza kumkubali wakati wowote, tofauti na mtu fulani ambaye ni kama mbwa kwenye hori.”
Lisa alishangaa, lakini alielewa mara moja alipomwona Joseph akipepesa macho kwa siri. Moyo wake ukapata joto.
Alvin alikunja ngumi. Hasira yake ilimfanya Sam ashuku kwamba angemrukia mtu sekunde yoyote.
Sam ilikwenda kati ya watu hao wawili haraka. “Alvin, tulia. Joseph anatania tu.”
"Sikuwa na mzaha hata kidogo." Joseph alifoka.
Alvin, ambaye alikuwa akichokozwa tena, alipunguza macho yake. Alidhihaki, “Mimi sina shida naye, ila ni yeye ndiye hataki. Ni yeye ambaye sasa anakataa kuachwa.” Baada ya kuongea alimvuta Lisa kwake na kumtazama kwa ukali. “Sema mawazo yako. Uko tayari kunitaliki?”

Lisa alitabasamu. “Niko tayari!”
Uso wa Alvin ukawa mgumu ghafla. Macho yake makali yalionekana kana kwamba alitaka kumla akiwa hai. Alikuwa amekataa kabisa kutiasaini hati za talaka siku chache zilizopita. Hata hivyo, kwa kuwa sasa alikuwa na mwanamume mwingine, alitaka kumwacha mara moja.
“Lakini si sasa,” Lisa aliendelea kusema, “Wewe na Sarah mlinitesa na kuyafanya maisha yangu kuwa magumu. Nimeirudi baada ya miaka mitatu, lakini bado Sarah ananifanyia mambo mengi ya kijinga. Mwambie aendelee kuota ikiwa anafikiri nitasalimisha cheo cha Bi Kimaro kwa urahisi hivyo.”
Joseph mara moja akammiminia glasi ya mvinyo na kumpa kwa hisia ya upendo. “Nitakuunga mkono hata ufanye nini, nitakusubiri."
"Asante." Lisa alikuwa karibu kupokea glasi ya mvinyo. Hata hivyo, alishushwa kutoka kwenye kiti na Alvin kabla hata hajaigusa.

“Tunaondoka sasa hivi.” Alvin aliamuru.
“Hilo halitawezekana. Maisha ya usiku ndiyo kwanza yanaanza." Joseph akamshika mkono mwingine Lisa.
“Muachie twende. Ukinisumbua, bado ninaweza kusababisha madhara kwa Ruta Design hata kama siwezi kuiharibu. Haijalishi uko katika biashara tofauti,” Alvin alionya.
Macho ya watu hao wawili yaligongana. Lisa alimgeukia Joseph kinyonge na kusema kwa sauti nyororo, “Joseph samahani. Nitakuhudumia kwa chakula kingine wakati ujao.”
“Hauruhusiwi kula naye tena,” Alvin alitamka onyo lingine.
Joseph alicheka na kupuuza maneno ya Alvin. “Sawa, wakati ujao. Kuwa mwangalifu na unipigie ikiwa chochote kitatokea. Nitakuwa kando yako daima.”
“Asante—” Lisa alikuwa bado hajamaliza kuongea aliponyanyuliwa na kuwekwa kwenye mabega ya Alvin na kutoka nje.

Sam alimpa Joseph ishara ya dole gumba. “Unashangaza. Unathubutu kwenda kinyume na Alvin waziwazi. Huna hofu naye?”
“Niko kwenye biashara ya huduma na yeye yuko kwenye biashara za bidhaa. Hata kama anataka kuniangamiza, itachukua mipango fulani na muda mrefu. Haitakuwa rahisi hivyo.” Joseph aliinua mabega yake kwa utulivu.
"Ni mbaya sana kama utakuwa unamwigizia tu?" Sam alionyesha wasiwasi.
“Kwanini unasema naigiza? Sionekani kuwa serious kuhusu hilo?” Joseph aliinua nyusi zake kwa namna ya kutania.
Sam alishikwa na butwaa. “Hapana... Ina maana uko serious kabisa?”
"Wanaume siku zote hutamani wanawake warembo," Joseph alisema huku akitabasamu, "Ingawa najua kuwa siwezi kuwa naye, haibadilishi ukweli kwamba anaweza kuwa mpenzi wangu."
•••

Lisa alitupwa ndani ya gari na Alvin. Alipoanguka, ni kana kwamba viungo vyake vilikuwa karibu kuvunjika pia. Kiatu kimoja kwenye mguu wake kilianguka nje ya gari alipotupwa kama furushi.
“Kiatu changu...” Lisa alinyanyuka kukichukua lakini alimsikia tu Alvin akifunga mlango kwa nguvu. Mlango ulifungwa haraka, na hakuweza kuufungua hata alipojaribu kiasi gani.
Alvin akaketi kwenye kiti cha dereva. Akakanyaga moto na kuondoka kwa kasi.
“Alvin, simamisha gari. Kiatu changu kilianguka." Lisa alimsogelea na kumvuta.
“Usijaribu kunihadaa. Najua unataka tu kurudi kumtafuta Joseph, sivyo?” Alvin alikuwa na moto mkali ndani yake."Lisa Jones, kwanini wewe ni mtu mbaya hivi? Nilikuwa nikishangaa jinsi ulivyoweza kusaini ushirikiano na Kilimani Group na Ruta Design, na ikawa kwamba ulitegemea sura na mwili wako. Huna aibu?”
"Unasema nini?" Lisa alikodoa macho.

Alvin alidhihaki, “Unahitaji maelezo ya wazi kutoka kwangu? Kwa uwezo wako ninaoujua mimi, Kilimani Group ingeweza kufikiria hata Mawenzi Investments ikiwa hukuwa na maelewano yaliyo kinyume na maadili? Kweli una ujanja fulani juu ya mkono wako. Umemfanya Joseph akuangukie na hata hafikirii kuwa wewe ni mchafu.”
Lisa akashusha pumzi ndefu. Ingawa alijua kwamba hakuna maneno mazuri yanayoweza kutoka katika kinywa chake kibaya, alitaka kumpiga na kiatu chake hadi kufa kwa kumfikiria kwa mawazo hayo machafu.
Kwa kweli, alifanya hivyo. Haraka akavua kiatu kilichobaki kwenye mguu wake na kumpiga usoni bila kusita.
Alvin, ambaye hakufikiria kwamba Lisa angethubutu kufanya hivyo, aligongwa moja kwa moja usoni na soli ya kiatu chake. Gari hata lilitikisika kidogo kwa kukosa udhibiti kwa muda
"Lisa, nadhani lazima uwe umechoka kuishi." Alinyakua kiatu na kukitupa nje ya dirisha kwa

hasira. Ikiwa asingekuwa akiendesha gari wakati huo, bila shaka angemfundisha somo.
"Nani alikuambia uniambie maneno machafu kama hayo?" Lisa alijisikia kuridhika ajabu alipoona alama ya kiatu kwenye uso wake mzuri. “Alvin, umepoteza viatu vyangu. Lazima unifidie kwa jozi nyingine."
Alvin alidhihaki, “Kwanini? Unataka nikufidie pea ya viatu uvae mbele ya Sarah na kusema nimekununulia ili umuumize? Lisa, una mipango mzuri sana ya kuudhi."
"Ikiwa hutaki kumuumiza, unapaswa kuniacha niende na usisumbuane nami hapa katikati ya usiku." Lisa alitazama mbele, na haikuonekana kama ilikuwa njia ya kurudi nyumbani kwake.
"Alvin, unanipeleka wapi?"
"Wanawake wasiofaa kama wewe ni afadhali wafungiwe tu ili usiniaibishe na kunidanganya." Lisa alihisi baridi ikifika kwenye mifupa yake. “Unanifungia tena?”
"Umejitakia hili," Alvin alijibu.

TUKUTANE KURASA 336-340
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] aiseeee mbona mpo fasta hivoo
 
LISA KITABU CHA NANE (8) SIMULIZI........................LISA KURASA..................351 - 355
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 351
Baada ya Joel kujionea ‘live’ usaliti wa Nina, alishindwa kuvumilia na kupata mshtuko wa moyo. Lisa alimpeleka baba yake haraka hospitali kuingiziwa dripu ya IV. Ingawa kuona Nina akikamatwa kulimfanya Joel kupumua, afya yake ilidhoofika tena kwa sababu alikuwa amechanganyikiwa.
Haikuchukua muda Mzee Ngosha na Bibi Ngosha wakakimbilia hospitali. Mara baada ya Bibi Ngosha kuiona hali ya Joel, machozi yakaanza kumlenga lenga. "Nina hana akili. Tulimtendea vizuri sana kwa miaka mingi. Ajali uliyokutana nayo miaka mitatu iliyopita lazima inahusiana naye. Kwa bahati nzuri, mimi na baba yako tulimwomba Lisa akutunze. Vinginevyo...”

Maneno hayo yalipelekea mtetemo kwenye uti wa mgongo wa Mzee Ngosha. Sasa alipofikiria jambo hilo, alitoa shukrani zake za dhati kwa Lisa. "Tuna deni kubwa kwako, mjukuu wangu..."
Lisa alitabasamu na kukaa kimya kwa muda. “Usijali kuhusu hilo, babu. Sikuwahi kutarajia mengi kutoka kwa familia ya Ngosha, kwa hiyo sijavunjika moyo.”
“Wewe...” Mzee Ngosha aliona aibu ghafla.
Bibi Ngosha akamvuta. “Lisa yuko sahihi. Kwa kweli tabia yetu ilimkatisha tamaa tangu mwanzo. Ni kosa langu. Sikupaswa kumzuia Joel kumuoa mama yako. Samahani sana."

Mzee Ngosha alikunja ngumi na kukohoa kwa aibu. “Nakubaliana na bibi yako. Kuanzia sasa jisikie huru kabisa. Unakaribishwa nyumbani muda wowote utakao. Baada ya yote, hiyo ni nyumba yako."
Lisa alipigwa na butwaa kwa muda na kujawa na hisia mseto. Kwa kweli, alitamani kwamba babu na bibi yake wangemwambia hivyo alipofika Nairobi kwa mara ya kwanza. Hata hivyo, walimzingua pindi tu walipomuona. Siku zote alilazimika kupambana peke yake ndani ya jiji hilo, jambo ambalo lilimfanya ajisikie kama mgeni.
Wakati huo, kuna mtu aligonga mlango, ambapo Melanie aliingia akimsukuma Damien, ambaye alikuwa ameketi kwenye kiti cha magurudumu.

“Mnatafuta nini hapa?” Joeli alipowaona, alianza kupandwa na hasira na kukohoa kwa nguvu.
“Joel, usifadhaike. Ni mbaya kwa afya yako.” Mzee Ngosha kisha akawanyooshea kidole Damien na Melanie, na kusema, “Tokeni nje.”
“Babu tumekuja kukuomba msamaha. Kwa kweli sikujua kwamba Mama alifanya mambo hayo.” Melanie aliinua kichwa chake na kujibu kwa uchungu. Macho yake yalikuwa mekundu.
“Ulikuwa hujui kweli?” Lisa alidhihaki, “Wewe ndiye uliyempeleka Baba kwa uchunguzi wa kimatibabu kila mara. Wewe na Nina mlipanga njama hizi zote pamoja, lakini una bahati kwamba mama yako ndiye aliyebeba lawama zote.”

Baada ya ukimya wa muda, Lisa alihamishia macho yake kwa Damien. “Baba mdogo, ninazungumza na wewe hivi kwa sababu mimi ni mtu mstaarabu sana. Kama ningekuwa wewe, ningeona aibu kujitokeza hapa. Ikiwa baba yangu angekufa kwa sumu, Kampuni ya Ngosha ingeenda kwako na Melanie. Nyote wawili mngefaidika zaidi, na Nina aliyeenda gerezani kwa niaba yenu.”
Uso mzuri wa Damien ulilegea kabla ya kujibu, “Siku zote nimemchukulia kaka yangu kama baba yangu, kwa hiyo ningewezaje kujaribu kumuua kaka yangu? Kaka nitapiga magoti nakuomba msamaha sasa. Kwa miaka hii yote, nilipumbazwa na Nina na nimefanya mambo mengi mabaya dhidi yako, lakini sikupanga kukuua hata kidogo.”

Damien alipokuwa akizungumza, alijilazimisha kutoka kwenye kiti cha magurudumu na kupiga magoti sakafuni. Hata hivyo, miguu yake ilikuwa dhaifu sana kuweza kusimama. Mara miguu yake ikageuka kuwa mlenda, alianguka sakafuni vibaya.
“Baba.” Melanie alilia na kwenda kumshika kwa haraka.
“Melanie, nishike nipige magoti.” Damien aliendelea.
Kwa kuwa Damien alikuwa mwanae wa kumzaa, Bibi Ngosha alishindwa kuvumilia kumuona akipiga magoti. “Miguu yako imelemaa. Utapiga magoti vipi? Fanya haraka ukae kwenye kiti chako.”
"Ndio, miguu yangu imelemaa." Damien

aliinamisha kichwa chini na kububujikwa na machozi. “Tangu nilipozaliwa, watu wengi wamekuwa wakinidharau kwa sababu tu ya ulemavu wangu. Ninamshukuru Kaka, lakini wakati huo huo, ninamwonea wivu. Nampenda Nina, lakini hakuwa anavutiwa nami. Zaidi ya miaka ishirini iliyopita, sijawahi kumpenda mtu mwingine yeyote isipokuwa yeye. Nilimfanyia kila kitu bila kulalamika. Nilidhani angeniangukia hatimaye baada ya kupata Ngosha Corporation, lakini nilikosea. Ni sasa tu ndio nimeelewa utu wake. Baba, Mama, Kaka, ni kosa langu...”
Bibi Ngosha alikuwa kwenye hatihati ya kulia. Hakuweza kupinga kusema, “Yote ni makosa yangu. Sikupaswa kukuzaa na kukufanya uteseke sana na kujidharau.”

“Baba, Mama, mnaweza kunilaumu mimi. Ni sawa. Lakini natumaini hamtamchukia Melanie.” Damien aliinua kichwa chake na kuomba. "Melanie hana hatia. Sijawahi kuoa, na yeye ni binti yangu wa pekee. Yeye pia ni mjukuu wako wa damu.”
“Babu, Bibi, samahani. Nimekuwa mbali nanyi kwa muda mrefu, na imenisikitisha sana. Bado mnakumbuka jinsi mlivyokuwa mkinijali?" Melanie mara moja akapiga magoti karibu na Damien. Alitazama juu na kugeuza nywele zake kuelekea nyuma, akionyesha uso uliopigwa na kuvimba.
"Ni nini kilitokea kwenye uso wako?" Mzee Ngosha aliuliza kwa sauti nzito.
Melanie akasonga na kuuma mdomo. Kisha, Damien akasema kwa huzuni,

“Ni Jerome aliyempiga.”
"Ni mpuuzi sana huyo mwanamume." Mzee Ngosha alipandwa na hasira. "Familia ya Campos ina kiburi sana. Nitakutana na babu yake.
Familia yetu imewanyanyua sana mafukara wale wasio na shukrani, hawakuwa na kitu chochote!”
“Ni sawa, babu. Tayari wewe ni mzee. Hakuna haja ya kusimama kwa ajili yangu, na sitaki wewe kuwa upset kwa sababu yangu. Familia ya Campos sio sawa na ilivyokuwa hapo awali. Jerome alisema kwamba alinioa kwa sababu tu alifikiri nilikuwa...Binti wa Joel. Alichagua kuwa nami kwa sababu ya familia ya Ngosha.” Tabasamu la uchungu likapita usoni mwa Melanie.
“Ni dharau kiasi gani?” Damien alisema

kwa uchungu huku akimpapasa Melanie sehemu ya nyuma ya mkono wake. “Ni kosa langu, sio lako. Ananidharau kwa sababu mimi ni mlemavu na siwezi kumsaidia chochote”
“Inatosha!” Bibi Ngosha hakuweza kuvumilia tena kusikia hivyo. "Sasa kwa kuwa Nina yuko jela, acha yaliyopita yawe yamepita. Damien, bora usiishi peke yako huko nje. Rudi nyumbani. Uwe mtu mzuri na ulete sifa njema kwa familia ya Ngosha pamoja na kaka yako.”
“Naweza kweli kufanya hivyo?” Damien kwa tahadhari akahamishia macho yake kwa Joel aliyekuwa amejilaza kitandani. “Baba, ni sawa. Sitaki Kaka anielewe vibaya.”
Midomo ya Joel ilicheza, lakini kabla

hajazungumza, Melanie alisema, “Baba, msikilize babu. Mimi nakaa katika nyumba ya familia ya Campos. Nina wasiwasi kuhusu wewe kuwa peke yako katika hali yako. Je, ukianguka? Hata iweje, mtumishi wako si sehemu ya familia yetu kamwe.”
“Rudi tu.” Maneno ya Melanie yalimfanya Bibi Ngosha kukosa raha. "Hamia nyumbani leo."
Joel akafumba macho. Muda si mrefu, Mzee Ngosha na Bibi Ngosha waliondoka wakiwa na Damien na Melanie. Lisa alikuwa akitazama tukio zima kimyakimya. Hakuwahi kufikiria kwamba Damien na Melanie bado wangepokea hisani nzuri kwa wazee hao baada ya Nina kufungwa gerezani. Ukiachana na Melanie, Damien hakuwa na haya kama mwanaume.

“Unawaza nini baba?” Macho ya Lisa yakatua kwa baba yake. Ikiwa baba yake naye alifikiria sawa na babu na bibi yake, Lisa angejuta kujiingiza kwenye sakata hilo.
“Unafikiri kwamba mimi bado ni mjinga kama hapo awali? Baada ya kupitia mengi, nimeshajifunza somo langu.” Joel alilalamika. "Damien anatisha zaidi kuliko hata Nina. Anajua kabisa kwamba babu na bibi yako watamhurumia na kumbembeleza.”
“Najua." Lisa akahema. Babu na bibi yake walionekana kuwa wazee, lakini walikuwa na mali nyingi. Ingawa Mzee Ngosha alikuwa amestaafu kufanya kazi, bado alikuwa na nguvu katika Ngosha Corporation na ushawishi katika jiji la Nairobi. Mara baada ya Melanie na

Damien kupata kampuni ya Ngosha Corporation, wangemtumia tena.
Sura ya: 352
“Lisa, kwa kuwa niko hospitalini, nitakuomba unishughulikie mambo fulani kwa sasa.” Joel ghafla akampiga piga Lisa nyuma ya mkono wake. "Nitamwambia msaidizi wangu kuripoti kwako mambo yote ya kampuni kuanzia sasa."
Kichwa cha Lisa kilianza kumuuma. "Baba, unanilazimisha kijanja kusimamia Kampuni ya Ngosha?"
“Ninakulazimisha vipi?” Joel alimkazia macho. "Kama binti yangu na mrithi wa Ngosha Corporation, hutaitwa tena binti haramu. Unastahili kuwa na mwanmke

bora kabisa katika Kenya nzima. Hata Sarah pia hawezi kufananishwa na wewe.”
Nia ya Joel hatimaye ikamwingia Lisa. Hisia ya joto ikaenena ndani yake. Bila kusema, Joel lazima aligundua kuwa Alvin alikuwa akienda kufunga ndoa na Sarah, hivyo alitaka asihizunike. Kwa kuzingatia kwamba Lisa alikuwa mmiliki wa Mawenzi Investments, binti pekee na mrithi wa Ngosha Corporation, Sarah asingeweza kumshinda kwa heshima na hadhi. Haidhuru Sarah alikuwa na jeuri kiasi gani, yeye alikuwa mwanasaikolojia tu. New Era Advertisings, kampuni ya familia yao, ingekuwa imeanguka kwa muda mrefu bila usaidizi wa Alvin, na Thomas angekuwa jela kama si kukingiwa kifua na Alvin.

“Usijisumbue na mambo hayo mwanangu. Utaweza kupata mtu bora zaidi anayekustahili. Binti yangu ni mrembo sana, mwenye uwezo, na tajiri. Hakuna mtu yeyote katika Kenya anayeweza kukuzidi,” Joel alimtia moyo huku akitabasamu.
“Asante, Baba. Ninajiamini kila wakati. Kwa wale ambao hawakunichagua, ni hasara yao.”
"Safi sana." Joel alitabasamu.
Saa kumi jioni, Lisa alipanga foleni kwenye chumba cha pharmacy kilichokuwa chini ili kuchukua dawa. Alipomaliza, alirudi juu na kumuona Maya akitoka nje ya kitengo cha uzazi na magonjwa ya uzazi ya wanawake akiwa na Sarah.

Akiwa amevalia nguo nyeupe, Sarah alionekana kama malaika kiasi kwamba kila mtu hospitalini alimtazama mara mbili mbili. Kwa upande mwingine, Lisa alikuwa rafu kidogo kwani siku nzima tangu jana yake alikuwa akimuuguza Joel hospitalini. Hakuwa hata na chembe ya kipodozi usoni na nywele zake zilikuwa zimetimka kidogo, na alionekana amechoka.
Sarah alilinganisha sura yake ya nje na ya Lisa, akafurahi sana, na akapata nguvu ya kuongea mbele yake. "Hi, Lisa. Nini kinakuleta hapa? Nini tatizo? Hujisikii vizuri?”
Lisa akatoa macho yake na kuendelea kwenda mbele bila kumjali Sarah. Alihisi kuchoka sana baada ya kumtunza Joel kwa siku moja. Hakuwa na nguvu ya kupoteza kuongea upuuzi na

mwanamke yule.
“We mwanamke, mbona huna adabu hivyo?” Maya alipiga kelele, “Bi Njau alikuwa anakusemesha, ina maana hujamsikia?”
“Bi Njau ni nani na kwanini nijibu swali lake?” Lisa aliwageukia kwa jazba na kusimama kwenye korido. Aliwatupia macho wawili hao kwa hasira.
“Wewe...” Maya alikuwa amekasirika kwa hasira.
Sarah alimsimamisha Maya na kusema kwa upole, “Lisa, najua unanichukia, lakini nimejitayarisha kukukubali. Kwa kweli ninampenda Alvin sana, na wewe najua unampenda, kwa hivyo tunaweza tu kushea. Naweza kukubali hilo.”

Lisa alichukizwa. “Oh, asante. Lakini sina mpango wa kushea mume na mtu yeyote. Ninaogopa kuambukizwa maradhi.”
Sura ya Sarah ilibadilika kidogo, kisha akainamisha kichwa chake. “Unathubutuje kutoa maneno ya dharau hivyo? Unapolala naye kila siku haimaanishi kwamba unampenda?” Aligusa tumbo lake huku akisema, “Sawa, unaweza kukaa kando basi uniachie mume wangu. Nimepanga kuzaa watoto wengi kwa Alvinic. Nilikuja hospitalini leo kuangalia jinsi ya kupata mapacha au mapacha watatu kwa njia ya urutubishaji katika mfumo wa uzazi.”
Maya alitabasamu na kusema, “Ni Bw. Kimaro ambaye alipendekeza kufanya urutubishaji kwa vitro aliposikia kwamba Sarah alitaka kupata angalau watoto

wawili. Aliogopa kwamba angekuwa na wakati mgumu kuwa mjamzito mara mbili. Tayari amemuomba Dokta Choka kuajiri timu bora zaidi ya madaktari wa uzazi nchini kwa ajili yake.”
“Maya...” Sarah alimtazama kwa aibu na kudhihaki.
Macho ya Lisa yalitangatanga na kutua kwenye tumbo la Sarah kabla ya kucheka ghafla. "Ni bora kuwa mwanaume. Ni rahisi kwao kusema kwa vile wana kazi ya kutoa manii tu kwa ajili ya kuingizwa kwenye hiyo ‘artificial insemination’. Lakini wanawake wana kazi kubwa ya kupitia kila aina ya shida. Katika hatua za mwanzo, wanawake wanatakiwa kuchukua sindano na madawa. Nilisikia kwamba mchakato wa kuingizwa mbegu ni mchungu sana pia. Nakushangaa sana. Upendo wangu

kwa Alvin si kama wako.”
Uso wa Sarah ukabadilika ghafla. Kwa kweli, alijua kila kitu ambacho Lisa alikuwa ametaja. Yeye pia alikuwa hataki, lakini hakuwa na jinsi kwa sababu Alvin hakuweza kumgusa hata kidogo.
“Umemaliza? Una wivu tu.” Maya alimshutumu Lisa kwa hasira.
"Nina wivu?" Lisa aliinua mabega yake. “Nina wivu gani? Nimepata mimba ya mapacha hapo awali, kwa hivyo sihitaji kupitia shida hizi zote. Inaonekana nimeweka kiwango cha juu sana kwa Alvin kwamba mtoto mmoja hawezi kumtosha tena.”
“Umezidi sasa Lisa.” Sarah aliuma mdomo wake kwa huzuni, na machozi yakaanza kumlenga lenga.

Lisa alitazama pembeni, na hakika Alvin alikuwa akielekea kwao. Kulikuwa na viongozi wachache wa hospitali pamoja naye.
Alipofika juu na kumuona Sarah analia, alimwangalia Lisa mara moja. “Ulimfanya nini tena? Si tayari tumeachana, kwanini unaendelea kutusumbua?”
Lisa aliongea kwanza kabla Sarah hajafungua mdomo wake. "Nilikuwa nashangaa tu kusikia kwamba umemwambia Sarah akuzalie watoto kwa njia ya upandikizi wa bandia. Kwanini usimruhusu apate mimba kwa njia ya kawaida? Unajua kwamba ni lazima atumie sindano na dawa kila siku kabla ya kuingizwa mimba kwa njia ya bandia? Bi. Njau, sisemi uwongo, sivyo?”

Sarah, ambaye mwanzoni alitaka kulalamika huku akitokwa na machozi, alipigwa na butwaa. Lisa hapo awali alikuwa akimnanga Sarah, lakini sauti yake mbele ya Alvin ilimfanya aonekane kana kwamba alimwonea huruma Sarah. Sarah alipoona hali ya kutofurahi ya Alvin, alieleza upesi, “Alvinic ana wasiwasi kwamba nitakuwa nimechoka sana ikiwa nitaendelea kubeba mimba mara kwa mara.”
"Ikiwa una wasiwasi kuhusu kumchosha, basi inatosha tu hata kubeba mimba mara moja. Hakuna haja ya kuwachukulia wanawake kama mashine za kutengeneza watoto,” Lisa alisema huku akiachia tabasamu. “Kawaida wanandoa wanapoenda kwa ajili ya upandishaji mbegu kwa njia ya bandia, ni aidha hawana uwezo wa

kuzaa au hawawezi kufanya ngono. Lakini ninafahamu wazi kama una uwezo au la. Haiwezekani kuwa ni Bi. Njau ambaye hana uwezo wa kuzaa...” Aliziba mdomo kwa mshangao. “Nakumbuka sasa. Nyote wawili mmekuwa pamoja kwa muda mrefu, lakini bado hana ujauzito.”
Uso mdogo wa Sarah ulibadilika rangi kwa hasira. Kwa hakika angeweza kupata mimba, lakini Alvin ndiye ambaye hakutaka kumgusa. Lakini, hakuweza kusema hivyo waziwazi, kwa hivyo aliweza kukubali tu macho ya kushangaza kutoka kwa viongozi wa hospitali. Alifadhaika sana hadi machozi yakaanza kumdondoka.
"Lisa, nitakuchana mdomo ikiwa utaendelea kuongea upuuzi." Alvin alimvuta Sarah kwenye kumbatio lake.

Kisha, akasema kwa hasira kwa viongozi wa hospitali, “Mfukuzeni hapa. Sitaki kumuona.”
Akiwekwa katika hali ngumu, mkurugenzi wa hospitali alisema, “Bwana Kimaro, Lisa ni binti wa Bwana Ngosha. Bwana Ngosha kwa sasa amelazwa katika hospitali yetu...”
“Nataka familia ya Ngosha ihamie hospitali nyingine. Sitaki kumuona hapa,” Alvin alifoka na kuondoka huku akiwa amemkumbatia Sarah.
"Alvinic, yote ni makosa yangu. Nilikutia aibu.” Sarah alinung'unika mikononi mwake.
“Sio tatizo lako. Mimi ndiye nina makosa kukuacha uende kupandishwa mbegu kwa njia ya bandia.” Alvin

alichanganyikiwa pia. Maneno ya Lisa yaligusa udhaifu wake, na kumfanya ajisikie fedheha.
“Ni sawa. Ilimradi niweze kuzaa mtoto wako, niko tayari kufanya hivyo,” Sarah alisema kwa utulivu. Alvin akahema. Alijisikia vibaya kwa ajili ya unyonge wa Sarah.
Dakika 15 baadaye, Lisa alipokea taarifa kutoka hospitalini kuwaamuru wabadili hospitali. Joel alikuwa katikati ya matibabu yake, lakini alikasirika aliposikia kuhusu hilo. “Alvin ana kiburi sana. Kwani familia yetu ilikuwa na chuki dhidi yake katika maisha yetu ya zamani? Au, matibabu yangu yalimsumbua kwa namna yoyote?” “Baba si wewe uliyemsumbua, ni mimi.” Mapigo ya moyo wa Lisa yalikuwa chini. Angekumbuka kila kitu ambacho Alvin alikuwa amewafanyia.

“Lisa, usiwe na huzuni. Ni tatizo langu. Sikupaswa kuja katika hospitali ya familia ya Choka. Familia ya Choka na familia ya Kimaro zimetiwa lami kwa brashi sawa. Hebu tuondoke. Nitakumbuka ukatili huu wa leo. Sisi akina Ngosha tutarudisha walichotufanyia huko mbeleni,” Joel alisema huku akitulia.
“Ndiyo. Tutarudisha walichotufanyia.” Lisa aliitikia kwa kichwa.
Sura ya: 353
Siku iliyofuata baada ya Nina kuhukumiwa, Joel alitangaza hadharani kwamba amemfanya Lisa kikamilifu

kama mrithi wake na mrithi wa urithi wake. Zaidi ya hayo, Lisa angekuwa msimamizi wa kila jambo, liwe kubwa au dogo, alipokuwa amelazwa hospitalini.
Hapo ndipo watumiaji wa mtandao walipogundua kwamba utajiri wa Joel ulifikia kiasi cha dola za Marekani bilioni tatu. Pamoja na thamani ya soko la kampuni ya Mawenzi Investments, ilimaanisha kwamba Lisa angekuwa mwanamke tajiri zaidi nchini Kenya.
Si hivyo tu, lakini mitandao pia ilisheheni picha mbalimbali za urembo wake na sifa zake za elimu ya juu. Mamia ya maoni yalitiririka kufuatia habari hiyo kusambaa kama upepo mitamdaoni;
[Nimekuwa mmoja wa mashabiki wake. Ni mwanamume gani atastahili mwanamke tajiri, mrembo, na mwenye

kipaji kama yeye?]
[Hivi, hata anahitaji mwanaume kweli? Si bora kwake kuwa single? Anaweza hata kubadili kati ya wavulana wachache na wazuri wakati wowote anaotaka.]
[Ni ukumbusho tu kwamba yeye ndiye mke wa zamani wa Alvin Kimaro.]
[Hivi Alvin Kimaro ni kipofu? Lisa ni dhahiri kuwa ni bora kuliko Sarah kwa sura, thamani halisi na urembo.] Mashabiki wa Sarah ambao hawakuridhika walionekana kumtetea pia.
[Sarah ana shida gani? Yeye ni mwanasaikolojia maarufu. Ana kipaji na mzuri pia. Kando na hilo, yeye ndiye mmiliki wa New Era Advertisings.]

[Kwani ni nini ikiwa yeye ni mwanasaikolojia? Lisa pia ni miongozi mwa wabunifu bora wa Kilimani Group, na mkurugenzi mkuu wa ubunifu wa kampuni hiyo]
[Kilimani Group ni nini? Sijawahi kusikia.]
[Jibu mbele yangu. Ni sawa kama hujui, lakini tafadhali usifichue ujinga wako. Utaiona mara tu unapotafuta kwenye mtandao. Kilimani Group ni kampuni ya ujenzi maarufu na yenye mapato ya juu zaidi Afrika. Watu wengi wenye vipaji katika Kilimani Group ni wasanifu mashuhuri wa kimataifa ambao wamepokea tuzo nyingi, na mapato yao ya kila mwaka yanazidi makumi ya mabilioni kwa urahisi. Ili kuwa afisa mkuu wa kubuni wa Kilimani Group,

lazima awe mmoja wa wasanifu watano bora Afrika, angalau. Lisa alishinda tuzo kadhaa huko Tanzania na hapa Kenya kama vile Grand-Prix award ya Lexus Crowns]
[Hiyo haiwezekani. Lisa bado mdogo sana. Acha kukuza mambo.]
[Naweza kuthibitisha hilo. Siyo ya kujisemea tu. Baada ya kuhitimu kutoka chuo kikuu, nilipata fursa ya kufanya mafunzo yangu katika Kilimani Group mwaka jana. Nilitokea kukutana na Lisa, na wakati huo, hata Lorenzo alikuwa akimheshimu.]
[Lorenzo. Unazungumza juu ya mbunifu, Lorenzo, ambaye alichukua Tuzo la ‘AAK Duracoat Awards of Excellence in Architecture’ mwaka jana?]

[Ndiyo, huyo ni yeye.]
Huku kukiwa na mjadala mzito kwenye mtandao, Kilimani Group ilichapisha kimataifa picha ya Lisa: [Bi Lisa Jones, afisa mtendaji mkuu wa kampuni yetu, ambaye alichukua nafasi hiyo mwaka jana.]
Habari hizo zilishangaza Kenya nzima. Watu wengi walitoa maoni kwenye akaunti ya Facebook ya KIM International.
[Bwana Kimaro, hadhi ya mke wako wa zamani imekuwa juu sana. Unajuta?]
[Haha, Alvin Kimaro, asante kwa kumtaliki Lisa wetu. La sivyo, asingekuwa hapa alipo leo.]
[Bwana Kimaro, tafadhali usijute na uje

kumtafuta Lisa wetu siku zijazo.]
Kwa siku moja nzima, mratibu wa ukurasa wa Facebook wa KIM International alikuwa na kazi ya kufuta ujumbe mmoja baada ya mwingine, lakini maoni hayakuwa na mwisho, kadri alivyoyafuta ndivyo yalivyozidi kuingia. Jambo hilo lilimfanya aingiwe na wasiwasi kiasi cha kutokwa na jasho.
Wakati huo, mkutano wa ndani wa ngazi ya juu wa KIM International ulikuwa ukiendelea. Jack alikuwa akitazama chini kwenye simu yake wakati ghafla alifoka. Chumba cha mikutano, ambacho kilisikika sauti ya Alvin pekee, kilikuwa kimya sana. Kila mtu alitazama kuelekea Jack.
Umbo la Alvin la kifahari liliegemea nyuma, na kalamu iliyokuwa mikononi

mwake akaitupa mezani. Macho yake makali yalikuwa ya hasira kali. “Meneja Mkuu Kimaro unajishughulisha na nini? Kwanini haupo pamoja nasi kwenye mkutano?”
Jack aligusa pua yake. “Unataka kujua kweli?” Wasimamizi wakuu walishusha pumzi zao. Waliweza kuhisi hali ya hewa ikiwa imeanza kuchafuka. Wawili hao walipokaa pamoja haikupita hata dakika tano bila chumba kugeuka kama Urusi na Ukraine.
“Ninaangalia akaunti rasmi ya Facebook ya kampuni. Inakaribia kulipuka.” Jack alitabasamu bila kufafanua. "Inahusiana na wewe, Mkurugenzi Kimaro."
Meneja mmoja alicheka na kusema, “Lazima ni watu wanaompongeza Mkurugenzi Kimaro na Bi. Njau kwa harusi yao.”

"Hiyo ni sawa. Hivi majuzi, watu wengi walikuja kwenye kampuni kutoa baraka zao. Mkurugenzi Kimaro ndiye mtu tajiri zaidi wa Kenya.”
Alvin alibaki kutojali, lakini alikubaliana na kile wasimamizi wakuu walisema. Hata hivyo, hakupendezwa na mambo hayo hata kidogo. "Kwa hivyo ... hiyo ndiyo sababu umakini wako ulizunguka kwenye simu yako katika mkutano muhimu wa kampuni?"
“Hapana, umeelewa vibaya. Inahusu... mke wako wa zamani.” Jack aliinua mabega yake. "Huenda hujui kuhusu hilo bado, lakini Joel tayari amemfanya Lisa kuwa mrithi wake. Wanamtandao wanajadili thamani halisi ya Lisa, na kuna mtu hata akafichua madili yake yaliyofichwa. Kumbe yeye ni

mkurugenzi wa ubunifu wa Kilimani Group. Kilimani Group tayari imethibitisha hilo.”
"Kilimani Group?" Baadhi ya wasimamizi wakuu walishangaa. "Ni ukweli? Hiyo ndiyo kampuni ya juu zaidi ya ujenzi Afrika. Wanaofanya kazi huko wote ni magwiji katika uwanja wao. Ni lazima awe gwiji kwa kuwa na cheo kama hicho.”
“Sisemi uongo. Unaweza kujiangalia mwenyewe ikiwa huniamini.” Jack alimtazama Alvin kwa kuchekacheka. “Kaka, ulijua hilo? Hata hukuniambia.”
Alvin alikosa la kusema. Hakujua jambo lolote kati ya hayo. Haishangazi Kilimani Group ilikuwa ya kwanza kushirikiana na Lisa. Mwanamke huyo... alikuwa na uwezo mkubwa, jambo ambalo

hakulitarajia.
Tayari alishangazwa na kazi nzuri aliyoifanya kuwaondoa wanahisa wasiotii wa Mawenzi Investments mara ya mwisho, lakini, hakutarajia kwamba angemshangaza tena.
Alvin alikodoa macho. Hakuweza kujizuia kupendezwa na mwanamke huyo kwa mara nyingine tena. Akivunga hamu ya kuitoa simu yake na kutazama umbea, Alvin alisema kwa ukali, “Tuko katikati ya mkutano. Ondoka kama unataka kujadili mambo mengine."
Kila mtu katika chumba cha mkutano akanyamaza. Jack aliinamisha kichwa chake na hakuongea zaidi.
Mkutano ulipelekwa haraka haraka huku

mada zikipitiwa juujuu tu. Takriban dakika 10 baadaye, mkutano ulikuwa umekamilika. Kitu cha kwanza alichofanya Alvin ni kuitazama simu yake. Alipoona habari kuhusu Lisa, karibu apige namba yake, bila kujua lengo lake ni kumpongeza au kumdhihaki, lakini sekunde moja baadaye, akakumbuka kwamba alikuwa mwanamume aliyeoa.
Alijizuia na kuwasha sigara. Alipitia kila habari hadi mwishowe, macho yake yakatua kwenye picha nzuri ya Lisa. Alipigwa na butwaa kwa muda na hakuweza kupinga kuhifadhi picha hiyo. •••
Mawenzi Investments.
Wakati Lisa alipopita kuelekea ofisini kwake, nusura azime kwa kelele za pongezi kutoka kwa wafanyakazi wake.

"Mkurugenzi Jones, wewe ni wa kushangaza sana."
Kwa kustaajabishwa, Amba alikuwa akihaha kwa kugonga mikono na magoti yake. "Vyombo vya habari vingi vimepiga simu kuomba mahojiano ya kipekee na wewe asubuhi ya leo. Ulifanya nini hasa kubadilisha hali yako katika miaka mitatu?"
'Nilitegemea kitu pekee cha thamani alichonipa Mungu, akili, bila shaka.” Lisa alisema kwa utulivu. “Tafadhali kataa mahojiano yote ya kipekee. Niko busy,”
“Sawa, lakini umealikwa kuhudhuria Starlight Gala na Times Media kesho usiku. Bwana Ngosha awali alitakiwa kuhudhuria, lakini amelazwa, kwa hiyo mwaliko ulikuja kwako.”

Sura ya: 354
Lisa alipokea kadi ya mwaliko na kuichezea mikononi mwake. "Je, kuna maana yoyote kwa aina hii ya mialiko?"
"Watu mashuhuri kutoka kila tasnia watakuwepo. Nilisikia kwamba Cindy, mwimbaji mashuhuri wa kike unayemchukia zaidi, atatumbuiza pia.” Amba alimchombeza Lisa kwani aliogopa asingehudhuria mwaliko huo. “Ikiwa huna shughuli nyingi, unaweza kwenda kumpa wakati mgumu kidogo, si unakumbuka wakati ule alivyokuwa anachonga sana akiwa na Sarah?”
Sekunde chache baadaye, Lisa alicheka. “Wow, Msaidizi wa miye, unazidi kuwa mkorofi zaidi kama bosi wako. Cindy ni mpenzi wa Chester.

Huogopi kwamba nitaingia kwenye matatizo?”
Amba alisema huku akitabasamu, “Wewe ni mrithi wa kampuni ya Ngosha na mbunifu mkuu wa Kilimani Group sasa. Thamani ya kampuni ya Mawenzi Investments imepanda hata maradufu. Watu wengi sana wanajaribu kukufahamu. Ingawa familia ya Chokaina nguvu, wewe pia si haba. Ni lazima wajiulize mara mbili kwa sasa kabla ya kukufanyia ujinga wowote.”
“Una hoja hapo. Kwa bahati nzuri, nina jambo langu na Chester pia.” Lisa alifunga kadi ya mwaliko. Lisa alikuwa bado na kinyongo kwamba hospitali ya familia ya Choka ilimfukuza Joel mara ya mwisho.
•••
Usiku. Kwenye lango kuu la ukumbi wa

mikusanyiko, Ssafu na safu za magari ya kifahari yaliingia. Kwenye zulia jekundu refu, Lisa alishuka kutoka kwenye gari nyeusi aina ya Rolls-Royce Ghost. Alivalia mavazi ya nguva yenye matundu ya almasi, ambayo yalionyesha kikamilifu mikunjo yake yenye umbo la S. Iliyolingana na sifa zake maridadi na rangi ya korosho iliyokoza, alionekana kama binti wa kifalme moja kwa moja kutoka kwenye jumba la malikia. Alikuwa wa kisasa, wakifahari, mzuri, na asiye na mbwembwe. Angeweza kuelezewa kwa kila kivumishi cha sifa.
Wanawake wasomi na watu mashuhuri waliovalia mavazi ya kifahari usiku huo walipauka kwa kulinganisha na Lisa. Si nyuma ya Lisa, Cindy alishuka kutoka kwenye gari aina ya Bentley Bentayga. na kumshika mkono Chester. Hata

hivyo, Lisa alivutia macho sana hivi kwamba hakuna mtu aliyemwona Cindy pindi anaingia.
Cindy akasaga meno kwa chuki. Times Media ilikuwa moja ya makampuni makubwa ya Kenya, kwa hivyo hapo awali alikuwa amepanga kuwa bora usiku huo. Hata vazi alilovaa lilibuniwa na mbunifu wa hali ya juu, ambaye alikuwa ameombwa na Chester kwa muda mrefu. Kamwe hakutarajia kwamba Lisa angemwibia umaarufu tena. Hata alipata nafasi ya kusaini mkataba na Mawenzi Investments kama balozi wao, lakini Lisa aliuvunja.
Kwanini hakufa miaka mitatu iliyopita? Ikiwa angefanya hivyo, Cindy asingekuwa mtu wa kudharauliwa sana. Ilisikitisha zaidi kwamba Lisa alikuwa sasa mrithi wa Ngosha Corporation.

Hakuna kinachomkera mwanadamu zaidi ya mafanikio ya mwanadamu mwingine.
"Chester, sikuwahi kufikiria kwamba Lisa angezingatiwa sana. Ulikuwa unaangaziwa popote ulipoenda." Cindy alificha wivu wake na kumtania yule mtu mashuhuri kando yake.
Chester akarekebisha miwani yake yenye fremu ya dhahabu na kumtazama kwa mawazo. “Kwanini? Unamwonea wivu?”
Cindy alishangaa, lakini hakuthubutu kufsema ujinga wowote mbele ya Chester. “Hilo ni hakika. Ni nani hapa ambaye hatamuonea wivu? Ana bahati sana.”
“Una bahati pia. Unapaswa kujifunza

kuridhika na ulicho nacho.” Sauti ya Chester ilikuwa ya kubembeleza, lakini ilikuwa ya kutisha.
Cindy alitabasamu huku akisema, “Nimeridhika sana kukutana na wewe. Lakini... Alvin Kimaro na Sarah watakuwa hapa usiku wa leo pia. nina wasiwasi sana...”
“Hakuna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu watu wengine. Kila mtu yuko ndani ya jumuiya moja nchini Kenya na hatimaye tutagongana tu. Sarah lazima azoee.”
Baada ya Chester kusema kwa utulivu, Cindy aliweza tu kuinamisha kichwa chake na kunyamaza.
Lisa alipoingia kwenye jumba la karamu, aligundua kuwa kulikuwa na

watu wengi waliofahamiana naye usiku huo, kama vile Jerome na Melanie, Lea na Mason. Pia kulikuwa na Jack, Kelvin, Rodney...
Lisa akacheka. Hata damu katika mwili wake alihisi ikikimbia kwa kasi.
Usiku huo ulikuwa unaenda kuwa wa kuvutia. Baada ya miaka mitatu, watu waliofahamiana wote walikusanyika mahali pamoja.
Kelvin aliinua glasi yake kuelekea kwake kutoka mbali. Punde, alipokea ujumbe wa WhatsApp kutoka kwake: [Ninajua unalenga nini, kwa hivyo sikukukaribia. Lakini nitakuwa nikikutazama.] Moyo wa Lisa ukapata joto.
Jack, ambaye alivalia suti nyeupe, alimwendea kwa furaha na kumpa glasi

ya mvinyo. “Sikutaka kuhudhuria mara ya kwanza, lakini niliamua kuja mara moja niliposikia kwamba na wewe ungehudhuria. Usiku wa leo utapendeza sana.”
“Pamechangamka kweli kweli. Nimependa sana.” Lisa alikunywa mvinyo kabla ya mdomo wake kuinua tabasamu la kuvutia.
Mwangaza uliangaza machoni pa Jack. Ghafla akahema kwa majuto. “Usingeolewa na Alvin kwanza, hakika ningekuoa. Lakini nikikutongoza sasa hivi, wanafamilia wa Kimaro bila shaka watanisema vibaya. Hakuna mtu ambaye angeweza kukubali ndugu wawili kuoa mwanamke mmoja.”
“Kwa bahati nzuri, hukunitongoza. ningekubali.”

“Kwa nini?”
"Kwa sababu nina wachumba wengi sana." Lisa aliwatupia macho wanaume waliokuwa wakimtazama kwa pembeni. "Angalia, kuna watu wengi ambao wanajaribu kumrithi kaka yako."
“Ni kawaida. Sasa wewe ndiye mwanamke mrembo, mwenye kipaji, na mwenye thamani ya juu nchini Kenya.” Jack alinyoosha mkono wake kwake. "Unaweza kucheza na mimi? Ninataka kuwa mtu anayeonewa wivu sana usiku wa leo. Nipe furaha hii."
“Sawa.” Lisa aliweka mkono wake kwenye kiganja chake kikubwa, na wote wawili wakatembea kwenye uwanja wa muziki.

Walichukua nafasi kama wanandoa wakamilifu. Mara moja walivutia wivu na porojo za watu wengi, lakini wote wawili walipuuza yote na badala yake wakaanza mazungumzo.
“Sema, kwa nini umekuja leo? Kuharibu sherehe?" Jack aliuliza kwa utani.
Lisa akatumbua macho. "Ni tamasha la Times Media, kwanini niharibu? Nimekuja tu kucheza gitaa na kufurahi na kujumuika na marafiki.”
"Unajua kucheza gitaa?" Jack akakohoa. “Walimwalika Cindy kutumbuiza usiku wa leo. Yeye ni mtaalamu.”
“Ni vizuri. Nataka kutumbuiza baada yake.” Lisa alidhamiria. "Niliandika wimbo mpya, na nahisi watu

wataupenda sana. Unaweza kuusikiliza kidogo?”
Jack nusura apoteze stepbaada ya Lisa kumwimbia sikiono kipande cha wimbo huo. “Lisa, unataka kumchokoza Cindy? Huu wimbo ameuachia hivi karibuni na unafanya vizuri...”
“Ni wimbo wangu.” Lisa alimnong’oneza huku akitabasamu.
“Toka lini umekuwa mwanamuziki?"
“Huniamini?” Lisa alimkazia macho. “Mimi ndiye niliyeandika nyimbo maarufu za Cindy. Nilikuwa nikicheza gitaa na piano kabla hata Cindy hajajifunza kuimba. Ndoto yangu ya kwanza ilikuwa kuwa mwanamuziki lakini mazingira yalinibadilisha kuwa injinia. In fact ni kwamba Cindy alivutika

kuwa muimbaji kupitia mimi.”
Mshangao ulikuwa umeandikwa usoni mwa Jack. “Kwa hiyo huu wimbo mpya ni wewe pia uliuandika?”
“Sio huo tu, hata ule uliomtoa kwenye gemu niliuandika mimi. Ni vile tu kwamba amesahau kushukuru. Ni lazima nimfundishe hilo leo.” Lisa alilalamika.
"Una ujuzi gani mwingine ambao siujui?" Jack alikosa la kusema.
“Mimi ni hazina. Maisha yangu ya utotoni yalikuwa magumu sana hapo awali, na kipaji changu kilizuiwa na wengine. Sasa, ni wakati wangu wa kuangaza.” Lisa aliongea kwa kujiamini. Jack hakuweza kujizuia kuangua kicheko.

Sura ya: 355
Alvin na Sarah walipoingia, mara wakawaona Jack na Lisa wakiwa katikati ya ukumbi wa ngoma. Walikuwa wakicheza pamoja kama wanandoa waliokuwa na ‘chemistry’ nyingi. Mmoja alikuwa mrembo kama binti wa kifalme, wakati mwingine alikuwa amevaa suti nyeupe kama mtoto wa mfalme.
Chini ya mwanga, walizungumza na kucheka. Mara kwa mara, Lisa alikuwa akisema jambo ambalo lililomfanya Jack acheke kwa sauti. Pia alikuwa na tabasamu la kupendeza na tulivu usoni mwake. Tukio lile liliuumiza sana moyo wa Alvin. Wakati huo, alikuwa na hamu ya kukimbilia na kuwatenganisha wote wawili.
Kile Alvin alichohisi kilimfanya amkaze

kwa nguvu mkono Sarah. Sarah akashusha pumzi na kugugumia kwa sauti ya chini. "Alvinic, unaniumiza ..."
“Samahani.” Alvin aliachia mshiko wake kwa maneno ya kuomba msamaha, lakini macho yake hayakutoka katikati ya sakafu ya dansi.
Sarah alikunja ngumi kwa hasira.
Harusi yake na Alvin ilipaswa kuzungumziwa zaidi wakati huu, lakini Lisa alionekana kutawala kila mahali na kuiba umaarufu wake. Si hivyo tu, watu wengi walikuwa wakimlinganisha na Lisa kwenye mitandao. Ingawa alikuwa ameitangaza harusi yake hadi kwenye mabngo ya barabarani, bado alishindwa kabisa kupambana na Lisa.
Hatimaye alipata kuhudhuria hafla hiyo na Alvin, lakini Lisa alionekana kama

mzimu unaowasumbua. Kilichomfanya azidi kuchanganyikiwa ni kuona wivu machoni mwa Alvin. Ilikuwa ni aina ya wivu ambayo mwanaume angekuwa nayo kwa mwanaume mwingine.
“Alvinic, Aunty Lea yuko pale. Twende tukasalimie,” Sarah alisema kwa sauti nyororo ili kumpotezea mawazo ya Lisa.
“Sawa.” Walikuwa familia, baada ya yote, kwa hiyo walipaswa kutendeana vizuri hadharani.
Wote wawili walitembea kuelekea kwa Lea. Lea alikuwa akibadilishana maneno na rafiki wa zamani. Rafiki yake wa zamani alimtania, “Binti-mkwe wako na mwana wako wako hapa.”
“Habari yako, Aunty Lea,” Sarah aliwasalimia wale wanawake wawili.

"Ah, ana tabia nzuri sana." Rafiki wa zamani wa Lea alipoona kwamba familia ya Lea imeingia, alipata kisingizio na akaondoka kwenda kuzungumza na watu wengine.
Lea alimpa Sarah mtazamo wa chuki. Alimchukia sana Sarah, hasa pale kila Mzee Kimaro na Bibi Kimaro walipotaja kuharibika kwa mimba ya Lisa enzi hizo alipokuwa amebeba mapacha. Wanandoa hao wazee wangeizungumzia kila alipoenda kuwasalimia katika miaka hii michache. Kama si Sarah, Lisa asingepoteza ujauzito wake na angekuwa ni Bi. Kimaro zamani sana.
Ingawa Lea hakumpenda sana Lisa hapo awali, alifikiri kwamba Sarah alikuwa mkatili sana. Sarah aliweza hata kujihusisha na mwanaume ambaye

alikuwa ameoa na alikuwa akitarajia kupata watoto. Mwishowe, alisababisha mke halali apoteze mimba. Ilikuwa wazi kwamba Sara hakuwa na hisia zozote za maadili.
Sarah alionekana kuwa na huzuni baada ya kuona Lea anampuuza.
Alvin aliona ni vigumu sana kuvumilia na akasema, “Mama, salamu ya Sarah.”
“Najua. Mimi si kiziwi,” Lea alijibu bila kujali.
Sarah alilazimisha tabasamu na kusema, “Aunty Lea, nitakuletea chakula.” Hakutaka kujaribu kupata kibali cha Lea ili tu kukwepa asikutane na karipio kali.
Alipoona Sarah anaondoka kwa huzuni, Alvin alikasirika. “Inaonekana sikupaswa

kuja kukusalimia. Na kwanini hukumtupia jicho kali kama hilo Jack na kumwacha acheze na Lisa? Shemeji wa zamani na shemeji yake, ni aibu sana.”
Hapo awali Lea alifikiri kwamba haikuwa sawa pia, lakini kwa silika alienda kinyume na maneno ya Alvin aliposikia sauti yake. “Wewe na Lisa tayari mmeachana. Ni muziki tu wanacheza na sio mapenzi. Watu wengine hata hawasemi chochote. Ni wewe tu unayenyoosha vidole hapa. Unajiingiza sana katika mambo ya wengine.”
“Hata ikiwa watu wengine wanasema jambo fulani, hawatalisema mbele yako,” Alvin alijibu kwa ukali.
“Umekosea. Wanafikiria tu njia za kufahamiana na Lisa sasa. Yeye ndiye mrithi wa Ngosha Corporation na mkurugenzi mkuu wa muundo wa

Kilimani Group. Kwa utambulisho huu, hakuna mtu atakayetaka kupitisha nafasi hii ili kumjua. Kutakuwa na manufaa na hakuna hasara iwapo Jack atajenga uhusiano mzuri na Lisa.” Lea alisema kwa hisia ngumu, “Alvin, lazima uelewe kwamba Lisa si Lisa tena wa zamani. Ana uwezo wa kuongeza thamani ya soko la Mawenzi Investments kwa urahisi na kuifanya iingie kwenye orodha 100 bora za Kenya.
"Mbali na hilo, yeye ndiye binti pekee wa Joel Ngosha na mwanamke wa kweli wa familia ya Ngosha. Ingawa alikuwa ameolewa hapo awali, bado kuna wanaume wengi bora kutoka kwa familia tajiri ambao wanataka kumuoa na kufahamiana naye. Ikiwa huamini, jionee mwenyewe.”

Alvin alitazama tena ulingo wa muziki. Lisa alikuwa tayari amemaliza kucheza wimbo na Jack. Baada ya hapo, alialikwa kwa nyimbo nyingine na Erick Malugu mwenye uwezo na mwonekano mzuri, aliyekuwa mkurugenzi wa S.E Group. Alvin alikunja ngumi bila fahamu.
Lea akahema. "Wakati mwingine, huwezi kuwadharau wengine. Wewe unajiona ndiyo mwenye kujua kila kitu? Uvumi niliousikia zaidi leo haukuwa juu ya watu kumcheka Jack, lakini wanazungumza juu ya jinsi ulivyoachana na Lisa na kumuoa na Sarah! Atakuletea kitu gani kizuri? Kila mtu katika jamii ya juu anamuepuka Thomas Njau. Ikiwa sio wewe kuisaidia New Era Advertisings, hakuna mtu ambaye angekuwa tayari kushirikiana nao.”

“Imetosha, usiseme tena.” Alvin tayari alihisi kuudhika, na alizidi kukosa raha kusikiliza maneno ya Lea. “Nilipona kutokana na ugonjwa wangu kutokana na matibabu ya Sarah. Kama si kutiwa moyo na Sarah wakati huo katika hospitali ya magonjwa ya akili, ningekuwa tayari nimekufa.”
“Lisa aliwahi kukutia moyo pia. Ungeniua wakati ule isingekuwa yeye,” Lea alifoka.
Alvin alipigwa na butwaa, akahisi uvimbe kooni. "Je! kitu kama hicho kilitokea hapo awali?"
Lea alikosa la kusema. “Hivi ndivyo Sarah alivyoutibu ugonjwa wako? Umesahau kila kitu kizuri kuhusu Lisa."
Alvin alikuwa ameduwaa kutokana na maneno yake. Hata hivyo, alipojaribu

kutafakari kwa kina, ghafla kichwa kilianza kumuuma. Aliegemeza kichwa chake kwenye mikono yake.
Alvin alipoona kwamba Mason na Jerome walikuwa katika mazungumzo ya kina si mbali naye, alisema kwa upole, “Mtazame Mason. Alisema hakuwa na hatia, lakini bado ana uhusiano wa karibu na familia ya Campos. Bado unamwamini?”
Lea akatazama juu, na sura yake ikageuka kuwa mbaya mara moja. Aligeuka na kuelekea kwa Mason. "Mason, njoo hapa kwa sekunde."
Lakini, alingoja kwa dakika tatu kamili kabla ya Mason kumjia na tabasamu usoni mwake. “Lea, kuna nini?”
Lea akamtazama. Alihisi kwamba

alikuwa akizidi kumsoma vizuri. "Mason, si nilikuambia toka mwanzo kuweka umbali kati yako na familia ya Campos? Hasa Jerome—”
“Lea, jina langu la mwisho ni Campos. Pia ni familia ya wazazi wangu. Siwezi... kutowasiliana na familia ya Campos kwa sababu tu ya mpasuko kati ya familia ya Campos na familia ya Kimaro.” Mason alinyoosha mikono yake. "Mbali na hilo, maendeleo ya familia ya Campos miaka hii hayajazuia familia ya Kimaro kwa njia yoyote ile. Huoni kwamba familia hizo mbili zinaendelea kukua pamoja katika miaka ya hivi karibuni?”
Baada ya mshangao wa muda, Lea alisema kwa hasira, “Haijaizuiaje familia ya Kimaro? Baadhi ya kampuni tanzu za KIM International zilinyonywa faida

mara kwa mara na kampuni ya Campos. Si hivyo tu, kama isingekuwa msaada wa KIM International wakati huo, familia ya Campos—”
”Kwamba Familia ya Campos ingekuwa kama ilivyo leo? Nilijua ungesema hivyo tena,” Mason alimkatisha. "Familia ya Campos ipo kama ilivyo leo kupitia umoja wa wafanyikazi wote katika kampuni ya Campos. Isitoshe, kwani hatuendelei vizuri hata bila msaada wa KIM International miaka hii mitatu?”
"Kama nisingekupa makumi ya mabilioni hapo awali, unafikiri siku hii ingefika kwa Campos Corporation-"
“Sitaki kugombana na wewe, Lea.” Mason alimkatisha. “Siku zote ni sisi, familia ya Campos, ambao tunashutumiwa kwa kupanga njama na

kula njama kila tunapopambana kutoka kwenye dhiki. Ni kana kwamba familia ya Campos inapaswa kuwa na shukrani kwa familia ya Kimaro milele,” Mason alisema kwa kuudhika. Akageuka na kuondoka.
Lea alihisi ubaridi moyoni mwake. Mason hakuwa hivyo hapo zamani. Hata hivyo, alikuwa akizidi kukosa subira naye kadiri muda ulivyopita.
TUKUTANE KURASA 356-360
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (8) SIMULIZI........................LISA KURASA..................356 - 360
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 356
Baada ya Mason kuondoka, alienda moja kwa moja kwenye bustani iliyokuwa nje. Nyuma ya kitalu cha maua gizani, mwanamke alionekana na kushika mikono yake shingoni
mwake. "Kwanini ulitoka peke yako na kumwacha yule mwanamke mzee, Lea?"
“Kwa sababu nilikukumbuka. Hakika Lea ni mzee ukilinganisha na wewe." Mason alizunguka kiuno cha mwanamke huyo. Walianza kubusuana na kubadilishana joto.
“Mpenzi, hapa tutakutwa, ninapafahamu mahali ambapo pamejificha zaidi. Twende huko.” mwanamke alisema kwa utamu.

"Sweety babe, twende huko sasa.” Mason alitembea kuelekea nyuma huku akiwa amemkumbatia yule mwanamke. Walipeana peksi kadhaa huku wakitembea.
Hata hivyo, hawakutambua kwamba Lisa alikuwa ametoka nyuma ya mti wa kijani kibichi ili kuongea na wanaye kwa njia ya video. Aliwafumania wakati wanaondoka. Simu ambayo aliishika ilikuwa ikirekodi video. Alipotaka tu kuwafuata, mkono ukatoka nyuma na kumpokonya simu yake. Aligeuka nyuma kutazama. Alimuona Alvin akiwa ameshika simu yake na kuitazama ile video. Mara moja naye akaishiwa pozi.
"Huoni aibu kama mwanamke kwa kurekodi mambo haya?" Alvin alivunga. Baada ya muda, alimtazama Lisa kwa sura isiyo na furaha.

Lisa hakuwa na la kusema. Alifikiri kwamba Alvin hakuwa na furaha kwa sababu aliona tu video ya baba yake wa kambo akiwa na uhusiano wa kimapenzi na kibinti kidogo, lakini hakutarajia angezungumza naye.
“Kwanini nione aibu? Wewe ndo wa kuona aibu.” Lisa alitabasamu huku akisema. “Angalia jinsi baba yako wa kambo alivyo wa ajabu. Ana zaidi ya miaka 50 lakini bado anaweza kujihusisha kimapenzi na mwanamke huyo mdogo sawa na binti yake.”
"Futa video hiyo kutoka kwenye simu yako." Alvin alihisi kuudhika ajabu.
"Unafikiri mimi ni kompyuta ambapo unaweza kufuta chochote upendavyo?" Lisa akairudisha simu yake. Aligeuka,

akitaka kuondoka.
Alvin alimshika huku macho yake yakionekana kuwa makali. "Nitumie video hiyo."
Lisa alimnyooshea mkono. Chini ya mwanga wa mwezi, mikono yake midogo midogo ilionekana mizuri sana. Alivaa bangili ya almasi mkononi mwake. Ilikuwa rahisi, lakini ngozi yake nzuri ilifanya ionekane ya kifahari.
Moyo wa Alvin ulirukaruka. "Unataka nini?"
"Nilipe kwa uhamisho wa hakimiliki." Lisa alipepesa macho yake mazuri kana kwamba ni jambo la kawaida. "Video ya Mason itakuwa na thamani kubwa. Ni mkwe wa familia ya Kimaro na mtoto wa kiume mkubwa wa familia ya Campos.

Taarifa hizi lazima ziwe na thamani ya angalau milioni 80."
Alvin alimpiga jicho kali. “Milioni 80? Kwanini usiibe benki tu?”
“Alvin Kimaro, usinifikirie kuwa mimi ni mtu asiye na uzoefu na asiyeelewa soko. Paparazi yeyote anaweza kupata makumi ya mamilioni ya shilingi kwa urahisi kwa kashfa ya mtu Mashuhuri. Ikiwa hauko tayari kulipa, ninaweza tu kuuza video kwa vyombo vya habari. Lazima kuna watu watapigania kulipia, haswa familia ya Campos. Hata wataizika kwa mabilioni ya shilingi, nadhani.” Lisa aligeuka na kuondoka kwa utulivu.
Alvin alihisi anaumwa na tumbo kutokana na kumkasirikia Lisa. Alitakiwa kuhamisha video hiyo kwenye simu

yake wakati alikuwa amempokonya simu mapema. “Sawa, nitalipia. Nihamishie video hiyo.”
“Nipe pesa kwanza ndo nikuhamishie video. Wakati wa kufanya biashara, mimi huwa mwaminifu kwa wateja wakubwa na wadogo.” Lisa aliinua nyusi zake.
Mdomo wa Alvin ulitetemeka. Akatoa simu yake na kumhamishia pesa mara moja. Macho ya Lisa yalikuwa yamepinda huku akitabasamu alipoona kiasi hicho cha pesa. Tabasamu lile tamu liliujaza moyo wa Alvin hadi ukingoni.
Bado alikuwa na hasira kidogo mwanzoni, lakini ilikuwa ni kana kwamba hasira yake ilitulizwa kwa ghafula. Milioni 80 tu? Angeweza

kuirejesha kwa sekunde chache tu. Kwa thamani ya biashara zake kama mtu tajiri kabisa, alikuwa akiingiza angalau milioni 500 kwa saa, awe mamcho au amelala! Milioni 80 ilikuwa psa ndogo tu. Akiwa na huzuni, alipokea video hiyo kwenye simu yake.
“Kwaheri. Ilikuwa ni furaha kufanya biashara na wewe wakati huu." Lisa akageuka na kuondoka. Alikuwa ametoka nje kwa muda tu na kupata milioni 80. Jamani, alitaka kuhudhuria karamu nyingi zaidi kama hiyo.
“Subiri...” Alvin alifoka bila fahamu alipomuona akiondoka.
“Kuna kitu kingine chochote?” Lisa alitazama nyuma. Sehemu ya nywele zake ndefu za rangi ya korosho zilipeperushwa na upepo wa usiku,

ukifichua uso wake wenye kustaajabisha na shingo yake kama ya swala.
Koo la Alvin likamkauka. Hakuweza kujizuia kusema, “Usicheze na Jack tena kuanzia sasa. Inatia aibu.”
"Nicheze naye, nisicheze naye, hiyo haikuhusu. Wewe povu linakutoka la nini? Mwanamume hapendezi kuwa mbea"
Alvin alikunja uso. "Kwa hiyo mimi ni mmbea?"
“Kwa sababu unaendelea kujiingiza katika mambo ya watu wengine,” Lisa alijibu kwa kejeli.
Alvin alicheka. “Wewe ni mke wangu wa zamani. Jack ni kaka yangu. Je, watu watasema nini ikiwa nyinyi mtakuwa

pamoja? Nyinyi wawili hamna aibu, lakini mimi najali heshima yangu.”
“Unamchukulia Jack kama kaka yako? Ulimpiga upendavyo katika kampuni na kumfanya awe kicheko Nairobi nzima,” Lisa alimkaripia, “Sijawahi kuona mtu mbabe na mbinafsi kama wewe.”
"Kwa hivyo unajisikia vibaya kwa Jack sasa?" Alvin alikodoa macho. Hasira ilimtoka machoni pake.
“Aliokoa maisha yangu. Kwa hivyo ni lazima niwe upande wake?” Lisa alitabasamu aliposema, “Hata hivyo sisi sote tupo single. Kuna tatizo gani hata tukiamua kuwa wapenzi? Jack pia ni handsome kuzidi hata mtu fulani.”
“Thubutu!” Macho ya hasira ya Alvin yalionekana kana kwamba yanataka

kumrukia. "Familia ya Kimaro haitakubali hili."
“Haijalishi hata kama hukubaliani, kwa sababu Jack ametelekezwa katika Kampuni ya KIM. Anyway, hata mkimtimua kabisa, anaweza tu kufanya kazi katika kampuni yangu. Inaweza kutokea kwamba nina kampuni nyingi sana ambazo siwezi kuzisimamia zote. Nani anajua? Huenda utaniita 'shemeji' siku zijazo." Lisa alimtazama. "Hujui kwamba maisha yamejaa mshangao?"
Kifua cha Alvin kilidunda hadi kichwa kilimuuma. Aligundua kuwa asingeweza kufanya mazungumzo na Lisa. Kila mara alikuwa akikasirika sana hivi kwamba alihisi kama alikuwa karibu kupata mshtuko wa moyo.
"Lisa, ningependa kukuangamiza kuliko kukuacha wewe na Jack kuniingiza

katika aibu."
“Usijali, nilikuwa najisemea tu hata hivyo. Kuna watu wengi sana wanajaribu kunitongoza sasa. Jack ni chaguo moja wapo tu. Bado sijachagua mmoja.” Lisa aliondoka huku akionyesha dharau baada ya kusema hivyo.
Alvin aliupiga mti kwa hasira. Walikuwa wametalikiana, lakini kwa nini hisia zake bado zingeweza kutawaliwa na mwanamke huyo? Alitamani hata kumficha alipomwona akicheza na mwanaume mwingine.
Aliporudi kwenye jumba la karamu, Cindy alikuwa akicheza piano.
Sauti tamu na laini ya kuimba kucheza kwake ilisikika katika jumba la karamu. Wageni walifurahia onyesho hilo kwa

kuwa watu wengi katika familia za matawi ya juu walikuwa na mapenzi fulani na piano na muziki.
Watu walikuwa wakizungumza kumsifia;
"Cindy sio diva wa tasnia ya muziki bure. Anaweza kuimba noti za chini na za juu huku akicheza piano bila kuhitaji kuvuta pumzi.”
"Hiyo ni kweli. Uwezo wake sio wa maonyesho tu. Si ajabu Dokta Choka amekuwa akimsaidia miaka hii michache.”
"Sio tu kwamba anamuunga mkono, lakini pia anamdekeza sana. Chester humpa chochote anachotaka. Hata alimsaidia alipofanya mabadiliko kutoka kuwa mwimbaji hadi kuwa nyota wa filamu.”

"Ulienda wapi? Nilikutafuta kila mahali. Jack alikimbilia upande wa Lisa kwa haraka na kusema. “Unafuata baada ya Cindy...”
"Nimetoka tu kutafuta pesa kidogo." Lisa alimwonyesha milioni 80 ambazo alipata.
Jack alishtuka. "Ni nini, umepata wapi?"
"Ndugu yako." Lisa alimn”yooshea kidole Alvin ambaye aliingia kwa nyuma huku akionyesha giza totoro.
Jack alimpa dole gumba. “Nimevutiwa. Ninunulie dinner ya laki baadaye.”
“Siwezi. Bwana Malugu alisema atanirudisha nyumbani baadaye.” Lisa alipofikiria jinsi alivyokuwa amepata pesa hizo kupitia video ya baba yake,

hakuweza kujizuia kumuonea huruma Jack. Ilimsumbua kwa muda na kujikuta anashikwa na hatia. "Ili kufidia masikitiko yako ya kunikosa, nitahamisha milioni 40 kwako."
Jack alikuwa ameduwaa kutokana na mshtuko. "Wewe ... wewe ni mkarimu sana?"
“Sisi ni marafiki! Ni milioni 40 tu.” Lisa alimhamisha zile pesa bila mpangilio na kuondoka zake.
Sura ya: 357
Punde, Alvin alikuja upande wa Jack. Aliuliza kwa sura ya huzuni, "Lisa kakuambia nini?"

Jack alimulika simu yake kwa Alvin huku akitabasamu. "Hawezi kula chakula cha jioni na mimi kwa sababu anaenda kwenye miadi yake na
Bwana Malugu usiku wa leo, kwa hivyo amenihamishia milioni 40."
Wakati huo, Alvin alijionea huruma mwenyewe jinsi alivyokuwa amekasirika, kukasirika na kukasirika. Lisa alipata pesa hizo kutoka kwake na akamgawia Jack mara moja. Je, alimchukulia kuwa boya?
Subiri, alikuwa ana miadi na Erick Malugu baadaye? Alvin hakuweza kutulia tena.
Baada ya Cindy kumaliza wimbo wake, alisimama taratibu. Alitoka nyuma ya piano na kuinama. Kulikuwa na duru ya makofi ya radi katika ukumbi wa karamu. Wakati huo, Cindy alifurahi

sana. Alijua kuwa machoni pa watu hao kutoka jamii ya hali ya juu, alikuwa mtu mdogotu ambaye haonekani. Lakini, alijulikana kwa kila mtu kuwa alikuwa na kipaji adimu usiku huo.
Muda huohuo, alimuona Lisa akielekea kwake taratibu. Ni wawili tu ndio walikuwa wamesimama katika eneo ambalo vyombo vya muziki viliwekwa. Kwa wakati huo, kila mtu alikuwa amemtazama Lisa mrembo na mlimbwebde. Tabasamu la Cindy likalegea.
"Lisa, umekuja mahali pabaya? Hapa ni mahali pa kucheza piano." Cindy alilazimisha tabasamu na kusema kwa sauti ya upole.
“Sikjakosea hata kidogo. Wewe si umemaliza kucheza wimbo wako?

Nimezungumza na mratibu. Nataka kujaribu ujuzi wangu.” Nguo ya Lisa iliyojaa almasi ilifuata nyuma yake alipokuwa akiiendea piano na kuketi mbele yake.
Mwili mzima wa Cindy ukakakamaa. Aligeuka nyuma kwa haraka na kusema, “Lisa, watu ambao wako hapa leo si watu wa kawaida tu. Hata mwanamuziki maarufu, Nandy, yuko hapa pia. Si mahali ambapo unaweza kufanya mzaha wako. Ikiwa unataka kucheza piano... unaweza kucheza ukirudi nyumbani.”
“Unadhani nitajiaibisha?” Lisa alitabasamu bila kufafanua.
Cindy akabaki amebana midomo. Hiyo ilipaswa kuwa kinyume chake. Yeye pia alikuwa anamfahamu vizuri Lisa. Lisa

alikuwa na talanta ya kipekee katika muziki hapo awali. Walikuwa wamesoma piano na gitaa pamoja wakiwa shule ya sekondari. Wote walisoma kwenye shule ya ‘Dar es Salaam Independent Schools’ kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita. Lisa aliweza kujifunza kila kitu haraka na mara nyingi alisifiwa na walimu.
Lisa alikuwa akivutiwa sana na muziki kipindi hicho. Ni vile tu alitegemea kuwa mrithi wa kampuni ya familia yao Kibo Group, iliyojihusisha na mambo ya ujenzi, ndipo ilimlazimu kwenda kusomea Uinjinia wa mambo ya kubuni majengo, alipomaliza kidato cha sita. Vinginevyo angekuwa msanii mkubwa tu kwa kipaji chake. Na hata alitunga nyimbo na kumwandikia Cindy baada ya hapo. Lakini, Cindy hakuweza kupima ujuzi wake wa sasa.

Lakini Lisa asingeweza kufanya jambo lisilowezekana mbele ya umati ule wa watu maarufu. Cindy alihisi kutokuwa na utulivu moyoni mwake.
Wakati huo, wageni walianza kuzungumza juu yake pia. Macho yao yaliweka alama ya dhihaka huku wakimtazama Lisa.
Baada ya yote, Cindy alikuwa amemaliza kufunika kwa show kali. Ikiwa Lisa angeimba baada yake, bila shaka angeonekana mzaha.
Melanie alijifanya kana kwamba ana wasiwasi na kusema, “Dada, hii si karamu ya familia ya Ngosha ambapo unaweza kufanya chochote unachotaka. Isitoshe wewe ndiye mrithi aliyeteuliwa wa familia ya Ngosha sasa. Unapaswa kutunza heshima ya familia ya Ngosha.”

"Hiyo ni sawa." Joan Halua alichukua nafasi hiyo na kuunga mkono maneno ya Melanie.
Sarah alipoona kwamba kila mtu amezungumza, alisema kwa upole, “Hii ni kuhusu kucheza piano. Ni tofauti na kubuni majengo, baada ya yote. Una maoni gani, Alvinic?" Alimvuta mwanamume yule mrefu na mtanashati kando yake.
Alvin alikunja uso. Alikuwa amemsikia Lisa akiimba na kucheza gitaa hapo awali. Kwa kweli alikuwa mzuri sana. Angempoteza Cindy, na sauti yake ilisikika vizuri zaidi kuliko ya Cindy alipocheza gitaa. Lakini, hakuwa na uhakika kama ingekuwa hivyohivyo pia ikiwa Lisa angeimba huku akicheza piano. Baada ya yote, kwa kweli

hakuwa na uhakika na uwezo wa mapafu ya Lisa na uzoefu wake. Ikiwa mambo yangeenda ndivyosivyo, Lisa angejidhalilihsa kabisa.
"Sina uhakika." Alikaza midomo baada ya kusema hivyo. "Ni suala lake mwenyewe."
“Mwache ajiaibishe ikiwa anataka,” Rodney alisema kwa kejeli, “Nafikiri anajaribu tu kujionyesha baada ya kusifiwasifiwa na wengine kwa siku chache. Anadhani yeye ni mzuri kwa kila kitu.”
'”Namhurumia kweli. Anafikiri kwamba anaweza kumshinda Cindy? Cindy ndiye diva wa Afro-pop."
"Usijali. Mwache afanye kama anataka. Yeye ndiye mrithi wa Ngosha

Corporation, kwa hivyo umwacheni avurunde ili tupate sababu ya kumnanga hapo baadaye. Tutamsema hadi atamani kufa.”
Mbele ya maongezi ya umati, Lisa alitabasamu kwa unyonge na kukandamiza key ya piano, na kufanya jumba la karamu litulie.
Alirekebisha kipaza sauti na kusema kwa sauti ya kupendeza, “Huu ni wimbo mpya niliotunga. Leo itakuwa mara yangu ya kwanza kuucheza na kuumba, hivyo natumai kila mmoja atausikiliza.”
“Ana kichaa? Hata alitunga wimbo wake mwenyewe.”
"Labda anamuonea wivu Cindy na anataka kumshinda, lakini Cindy ni mwimbaji haswa."

"Siku hizi, kila mwanamke kijana kutoka kwa familia tajiri anataka kutengeneza nyimbo yake. Muziki umevamiwa kwa kweli.”
Kila mtu aliponong'ona masikioni mwa mwenzake, mlio wa muziki wa furaha ukiambatana na sauti ya key za piano ulisikika polepole.
"Nakuambia, 'simama hapo',
“Ndege inaruka juu ya anga ya buluu, "Ninakwenda safari,
"Ninakwenda safari ya mbali. "Machozi yananidondoka kifuani mwangu,
"Mahusiano haya hayataisha, "Tunafuatilia ndoto zetu za siku zijazo pamoja,
"Huu sio mwisho, ni mwanzo mpya."
Umati ulitulia taratibu na kusikiliza kwa

makini wimbo huo mpya. Wimbo huo wa furaha ulikuwa na kidokezo cha huzuni ambacho kilirejelea kuagana. Mara moja uliwakumbusha watu miaka yao ya chuo kikuu ambapo walilazimika kuwaaga wapendwa wao ili waweze kufuata ndoto zao wenyewe. Ilikuwa huzuni kidogo iliyochochea mioyo yao.
Alvin alimtazama yule mwanamke aliyekuwa anang'aa pale jukwaani huku akiwa haamini. Kichwa chake kilikuwa kimeinama chini, lakini mwili wake ulitoa mwanga ambao hakuna mtu angeweza kuuzuia.
Siku zote alikuwa hivi, akimshangaza mara kwa mara. Haishangazi alikuwa amepanda jukwaani akiwa na ujasiri kama huo. Ustadi wake wa piano na sauti vilikuwa bora zaidi kuliko za Cindy. Sarah aliyaona macho ya Alvin ya

kutamanika na nusura aingiwe na wazimu. Alifikiri kwamba Lisa angejifanya mjinga. Hii ilitokeaje? Miaka mitatu iliyopita, alikuwa amemponda Lisa kwa urahisi kama mchwa.
Miaka mitatu baadaye, wanaume wote nchini walikuwa wakimwona Lisa kwa sura mpya.
Cindy aliyekuwa amesimama pembeni ya Lisa alifedheheka sana hadi uso ukabadilika na kuwa mweupe. Hakuna aliyemjua Lisa kuliko yeye kwenye muziki. Ndio, hii ndiyo aina ambayo Lisa alikuwa amefanya vyema. Baadaye, wimbo uliisha kwa noti ya mwisho.
"Ajabu!" Msanii Nandy akiwa ameambatana na mumewe, alitangulia kupiga makofi. Wimbo huo uliimbwa vizuri, ulichezwa vyema, na hata kupangwa vizuri.

"Bi Jones, ni kweli ulitunga wimbo huu?" Bwana Lojas kutoka Times Media aliuliza kwa mshangao.
"Niliandika muziki na maneno mwenyewe." Lisa alisimama na kumuinamia Nandy. "Bi. Mfinanga, hongera, nimesikia mengi kuhusu wewe.”
”Nandy alijawa na sifa tele kwake. "Inasikitisha kwamba kipaji chako hakisikiki tena, Bi Jones. Tunaweza kurekodi nyimbo moja pamoja? Najuana na watu wengi katika tasnia ya muziki na wanaweza—”
“Asante kwa wema wako, Bi. Mfinanga, lakini muziki sio ndoto yangu. Ni hobby yangu tu,” Lisa alikataa kwa upole. "Kwa kawaida huwa na mambo mengi na nina

shughuli nyingi sana."
Bwana Lojas alicheka. "Bi. Nandy, hujui hili, lakini Miss Jones pia ni mbunifu maarufu wa majengo.”
“Hiyo ni ajabu." Nandy alifichua sura ya kupendeza.
Wakati huo, Joan ghafla alisema, “Bi Jones, ulinakili wimbo wa Cindy? Wimbo wako unafanana sana na 'Pepo Ya Ndoto’, wimbo maarufu wa Cindy."
Kila mtu alishtuka, na mtu mwingine akaongezea, "Ni kweli hata mimi nimekumbuka..."
“Bi Jones, haiwezekani kuwa umeiba, sivyo?” Jerome alidhihaki kwa nia mbaya.

Sura ya: 358
Mara tu kauli hiyo ilipotolewa, macho ya kila mtu yakatua kwa Lisa.
Cindy alionyesha uvumilivu na usemi wa ukarimu, akisema, "Kwa kweli, sio kweli. Ukisikiliza kwa makini, wimbo aliotunga Lisa una mahadhi mepesi kuliko wimbo wangu, 'Pepo Ya Ndoto'. Ina mtindo tofauti pia."
Lisa alimtazama Cindy. Kila mtu aliweza kusikia maana iliyojificha katika maneno ya Cindy. Ilikuwa ni kukiri kwa njia isiyo ya moja kwa moja kwamba Lisa alikuwa amenakili Cindy, lakini ni mtindo wa wimbo tu ndio ulikuwa tofauti. Kwa maneno aliyosema, alijionyesha kuwa mkarimu sana huku akimponda

chinichini.
Kwa hakika, wakati uliofuata, Joan alisema, “Bi Tambwe, unaweza kuwa mkarimu, lakini hupaswi kuendekeza wizi. Ukibadilisha na kupanga upya nyimbo chache za kigeni na kusema kuwa umeunda wimbo huo mwenyewe, si itakuwa dhuluma kwa waundaji asilia?”
Melanie naye alionyesha sura ya aibu. "Lisa, ingawa sisi sote ni washiriki wa familia ya Ngosha, huwezi kukosa akili." Kabla Sarah hajazungumza, tayari kila mtu alikuwa akimlenga Lisa. Moyo wake ulikuwa na furaha sana aliponong'ona masikioni mwa Alvin, "Alvin, ni kweli aliiba?"
Uso mzuri wa Alvin ulikuwa umepoa sana. Hakuna aliyeweza kukisia

alichokuwa akifikiria.
Rodney hakuweza kujizuia na kusema, “Haijaibiwa kabisa, lakini inafanana kwa angalau 60%. Ni kama nilivyosema. Hawezi kutunga. Mwishowe, bado alinakili kutoka kwa Cindy. Sijui ni nani aliyempa jeuri ya kupanda jukwaani na kujaribu kumwaibisha Cindy. Anamchukulia kila mtu hapa kama mjinga?"
Sara alifurahi aliposikia maoni hayo. Ingawa sura yake ilikuwa ya wasiwasi, moyo wake ulikuwa na furaha.
Mbele ya shutuma zote, Lisa alitabasamu na kucheza kwa starehe wimbo mwingine ambao hakuna mtu aliyewahi kuusikia hapo awali. Wimbo huu ulikuwa wa kutuliza zaidi. Lakini, sauti yake kama ya mbinguni ilisikika

kwa mtindo wa kitamaduni.
Wimbo ulipoisha, alicheza wimbo mwingine. Nyimbo hizi zilikuwa na mitindo tofauti na hakuna mtu aliyewahi kuzisikia hapo awali. Baada ya kucheza na kuimba nyimbo hizo, umati ulibadilisha tena mawazo yao na kuanza kumwangalia Lisa kwa jicho la kitofauti.
.
Cindy alihisi wasiwasi moyoni mwake ukizidi kuwa na nguvu.
Joan alifoka, “Kila mtu anazungumza kuhusu wizi wako. Mbona unacheza nyimbo tena? Haijalishi unacheza vizuri kiasi gani, haiwezi kuficha ukweli kwamba umeiba.”
Lisa alimpuuza na badala yake akamtazama Nandy. “Una maoni gani kuhusu nyimbo mbili za mwisho? Je,

zinafanana na nyimbo zozote huko nje?”
Nandy akatikisa kichwa. "Ni si msanii tu, bali mfuatiliaji mzuri wa muziki pia. Nyimbo hizi sijawahi kuzisikia popote. Ni nyimbo mpya kabisa."
“Bw. Campos, unaonaje?” Lisa aliwatazama wale watu waliozungumza kwa ukali zaidi hapo awali.
Jerome alisema kwa upole, “Tulikuwa tunazungumza kuhusu wimbo wako wa kwanza. Ingawa nyimbo zinazofuata hazijafahamika, ni nani anayeweza kuwa na uhakika kwamba hujanakili nyimbo za kigeni?”
“Ndiyo maana nilimuuliza Nandy kwanza. Unafikiri yeye asingeweza kuthibitisha hili kwa hadhi yake?” Lisa alirudi kwa utulivu.

Hadhi ya Nandy katika tasnia ya muziki iliheshimiwa. Haijalishi nafasi ya Jerome katika ulimwengu wa biashara ilikuwa ya juu kiasi gani, hakuthubutu kumkanusha waziwazi Bi. Nandy. Jerome akanyamaza kimya.
Lisa alisimama taratibu na kuyahamishia macho yake mazuri kwa Cindy. Alitabasamu ghafla, akauliza, "Unaonaje, Cindy?"
Cindy alishangazwa sana na swali la Lisa. “Unacheza vizuri sana. Endelea na kazi nzuri.”
Lisa akaachia mkoromo wa kicheko na kufinya macho huku akitabasamu. “Hata sasa hutaki kueleza kwanini wimbo wa kwanza ulifanana na wimbo wako, ‘Pepo Ya Ndoto’? Ni kwa sababu

nyimbo zote katika albamu ya 'Pepo Ya Ndoto', iwe mashairi au mahadhi yake, zote ziliandikwa na mimi."
Kwa tamko hilo, watu wote waliingia katika ghasia. Umati wa watu ulitupa macho yao kwa Chester bila kujua. Kila mtu alijua kwamba Cindy alikuwa mpenzi wa Chester. Alikuwa akimlinda kwenye duara miaka yote hii, akimdekeza kama yai kwenye kiganja cha mikono yake. Kwa Lisa kumwiaibisha Cindy sasa, hiyo ilikuwa ni sawa na kumpiga Chester usoni. Chester aliwasha sigara na kukunja uso sana.
Cindy alichanganyikiwa. "Unasema nini?"
Rodney alifoka mara moja, “Lisa Jones, nadhani umepandisha wazimu kweli! Nyimbo hizo ziliandikwa na Cindy, sio

wewe! Unawezaje kukosa aibu?"
“Ndio, unajua Cindy ana kipaji gani? Kwanini akuhitaji kumwandikia nyimbo?” Joan naye alipiga kelele.
Lisa alipuuza shutuma hizo na kusema, “Wimbo wa kwanza katika albamu ya 'Pepo Ya Ndoto', uliitwa 'Watatu Pamoja'. Ulihusu urafiki wangu na Cindy, na mtu mwingine wa tatu. Tulikuwa marafiki wazuri wakati huo. Mwaka huo, ndoto ya Cindy ilikuwa kuwa mwimbaji, kwa hiyo nilitoa nyimbo zangu nane bora nilizotunga mimi mwenyewe na kumpa Cindy bila mkataba. Kwanini nilicheza nyimbo mbili za mwisho mapema? Nyimbo hizo mbili ndizo nyimbo zangu za hivi punde zaidi. Nilitaka tu kuonyesha kila mtu uwezo wangu. Sikuwa na nia ya kumchafua Cindy hata kidogo.”

Uso wa Cindy ulikuwa umepauka, na alionekana kama anakaribia kulia. "Lisa, ni kwa sababu unataka kuwa mwimbaji? Ni sawa, ninaweza kukutambulisha kwa wanamuziki, lakini hutakiwi kukanyaga sifa yangu.”
Lisa alitabasamu na hata hakumtazama. “Hamkutakiwa kuwa na haraka ya kunishtaki. Kwa bahati nzuri, kitabu changu cha nyimbo bado kipo. Baadaye, nitapiga picha zake na kuziweka kwenye mtandao. Hata hivyo, kuna zaidi ya nyimbo nane katika kitabu changu cha nyimbo. Kuna nyimbo 18. Wale wanaojua muziki wanaweza kufurahia polepole. Unaweza pia kuja kwangu kununua hakimiliki ya nyimbo zangu zingine, lakini sitazitoa bure wakati huu, kwani...” Baada ya kunyamaza, alimkazia macho Cindy.

“...baadhi ya watu hawashukuru kwa vitu ambavyo wamepewa kwa nia njema. Kuna watu wengi wasio na shukrani duniani.”
Cindy karibu kuanguka. Alijua kabisa mtunzi wa nyimbo hizo ni nani.
Hata hivyo, hakuwahi kujali kuhusu hilo. Ilikuwa ni kwa sababu, wakati huo, Lisa hakuwa tishio kwake. Ilikuwa tu kitabu cha nyimbo, kwa hiyo kila mtu angefikiri kwamba Lisa alikuwa akimwonea wivu. Hata hivyo, kwa msimamo wa Lisa kulikuwa na haja ya kumuonea wivu Cindy? Lisa alikuwa binti wa kifalme wa familia ya Ngosha, familia iliyomiliki ardhi nyingi zaidi nchini Kenya. Sambamba na utukufu wake kama mbunifu mashuhuri wa kimataifa, bila shaka wengine wangeamini maneno yake zaidi.

Lisa alimaliza kuongea na kuinama. "Nilicheza tu piano kwa leo ili kufanya karamu iwe ya kupendeza zaidi kwa Times Media, lakini sikutarajia kusababisha usumbufu mwingi. Samahani zangu za dhati, Bwana Lojas.”
“Ni sawa, Miss. Jones. Ulicheza vizuri sana, haswa nyimbo mbili za mwisho. Mabosi wengi kutoka kwenye kampuni za muziki wapo usiku wa leo, kwa hivyo ninaamini kwamba wapo watakaojitokeza ili kununua hakimiliki ya nyimbo hizo hivi karibuni.” Lojas alikuwa mwerevu na alikuwa ameona mambo mengi ya aina hii kwenye tasnia hapo awali.
Hapo awali alimthamini Cindy, lakini alibadilishwa kabisa na maneno ya Lisa.Hata hivyo, bado alipaswa

kuzingatia sifa ya Chester. Alisema huku akitabasamu, “Kila mtu ajisevie chakula. Utapata nguvu ya kusikiliza hotuba yangu jukwaani ikiwa utakula vya kutosha.” Umati ulitawanyika taratibu.
Kulikuwa na watu wengi ambao walikuwa bado wanajadili kile kilichotokea.
“Oh, Bwana Cedo Kadenyi, wewe ni mtayarishaji wa muziki. Nini unadhani; unafikiria nini?"
"Kile Lisa Jones alisema kina uwezekano mkubwa kuwa kweli. Angalia tu nyimbo zake mbili. Ni nzuri sana. Akiachia moja anaweza ku pata tuzo ya muziki kwa urahisi."
Sura ya: 359

Chester akakaa kwenye sofa lililopo mkabala na Lisa. Kulikuwa na tabasamu angavu usoni mwake, lakini macho yake yalitoa mchomo mkali wa hasira. “Nipe kitabu asilia cha nyimbo.”
"Inaonekana Cindy alikuja kulalamika kwako." Lisa alitabasamu kwa utulivu. "Ni nini kizuri unakipata kwa mwanamke mnafiki kama huyo?"
"Ana mapungufu mengi, lakini bado ni mwanamke wangu," Chester alisema, "Lisa Jones, usiende kinyume nami. Familia yako ya Ngosha haiwezi kumudu matokeo ya kumkasirisha tajiri namba tatu wa nchi hii. Hujatosheka tu kwa kusharirisha nyuso za watu wengine usiku huu?”

Lisa alitabasamu kwa dhihaka. "Chester Choka, kama kijana tajiri namba tatu wa nchi, macho yako ni mabaya sana. Unapaswa kubadilisha miwani yako."
Macho ya Chester yaliangaza kwa ukali. "Uvumilivu wangu una mipaka yake, Lisa."
“Suala kati yangu na Cindy linaweza kuchukuliwa kuwa chuki ya zamani. Sikutaka kueleza yaliyopita, lakini... ni kosa lako kwa kuwa mkali sana, Dokta Choka.” Lisa alitabasamu kwa ujeuri. "Kwa neno moja tu, ulimfukuza baba yangu katika hospitali yako."
Chester aliganda na kukunja uso. "Sikujua kuhusu hilo."
“Hata ungejua, ungemruhusu Alvin

afanye hivyo. Inaeleweka kwamba nyinyi watatu ni ndege wa manyoya yanayofanana.” Lisa alisimama, macho yake mazuri yakionekana kuwaka kwa hasira. “Unataka nikupe kitabu cha nyimbo asilia? Dokta Choka, lazima uwe unaota. Unafikiri mimi ni mmoja wa wafanyakazi wako? Hakika, ikiwa unataka kuiondoa familia ya Ngosha, endelea. Sitajali hata kidogo. Sio kama sina pesa hata hivyo. Hata hivyo, ngoja nikukumbushe. Usiende kutafuta mchawi na kurudi nyumbani ukiwa umerogwa. Mtazame Alvin sasa.”
Chester, ambaye hakuwahi kamwe kushindwa waziwazi hapo awali, alikasirika sana hivi kwamba akavuta sigara mfululizo.
“Chester Choka, miaka mitatu iliyopita, nilishukuru sana kwamba ulipata daktari

wa kumuokoa baba yangu, lakini baada ya kugundua kuwa Charity aliruka baharini na kufa, nilipoteza kila sehemu ya shukrani niliyokuwa nayo kwa ajili yako. Ulimchukia mwanamke asiye na hatia na bado unamchukulia mwanamke kama Cindy kama hazina. Lazima kuna shimo kwenye ubongo wako." Baada ya Lisa kumaliza kuongea, alitoka bila kugeuka nyuma.
Nyuma yake, Chester alipiga mkono wake kwa hasira na glasi ya mvinyo ikaanguka chini. Uso wake ulikuwa umekakamaa kwa hasira.
Rodney akapigwa na butwaa. Kati ya hao watatu, ni Chester pekee ndiye angetabasamu na kuficha machungu yake moyoni mwake. Kwa kawaida hakuwahi kuonyesha kama alikuwa na furaha au hasira. "Hapana, Lisa alisema

nini kilichokukasirisha?" Rodney aliuliza swali lililoambulia ukimya tu.
Hata hivyo, Alvin alicheka na kutabasamu kidogo. “Angalau sasa unajua kwanini mimi hukasirishwa sana na huyo mwanamke.”
"Chester, usiwe na wazimu." Rodney alimfariji. "Kwa neno moja tu, sio shida kwako kuangusha familia ya Ngosha na Mawenzi Investments."
“Unadhani familia ya Ngosha ni kuku kwenye soko la mbogamboga? Hawawezi kuuawa kwa neno moja tu.” Chester alimtazama kwa ukali. “Si rahisi kihivyo. Lisa Jones wa sasa hana doa dhaifu.”
Alvin alipigwa na butwaa, Rodney akasema, “Hilo haliwezekani. Mtu anawezaje kutokuwa na doa dhaifu?"

"Labda mtu hatakuwa tena na maeneo dhaifu baada ya kupoteza kila kitu," Chester alisema kwa kufikiria.
Alvin alikunja uso. Moyo wake ghafla ukahisi kukosa raha. Aligeuka nyuma kwa umati wa watu na kumtafuta Lisa bila kujua, lakini alimuona tu akiondoka pamoja na bwana mdogo wa familia ya Malugu.
Kupitia madirisha ya sakafu hadi dari, aliweza kuwaona watu hao wawili wakizungumza na kucheka huku wakitoka pamoja. Alikaribia kuisaga kwa mikono glasi ya mvinyo mikononi mwake.
Dakika tano baadaye, hakuweza kukaa tena. Alimwambia Rodney amrudishe Sarah baada ya karamu na akatoa

udhuru wa kuondoka mapema. Alilifuata gari la Bwana Malugu mpaka waliposimama kwenye sehemu ya kuegesha magari mbele ya majumba ya Karen Estate. Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa nusu saa, bado hakumuona Lisa akishuka kwenye gari.
Taa za gari zilikuwa zimewaka, lakini hakujua walikuwa wanafanya nini. Walikuwa na mazungumzo gani kwa muda mrefu hivyo? Inaweza kuwa...
Alvin alipofikiria kuwa Lisa na Erick Malugu wanaweza kuwa wanafanya jambo lile lile lililotokea kati yao siku kadhaa zilizopita kwenye gari, moyo wake ulianza kumuuma papo hapo. Alishindwa kuvumilia akatoa simu yake ili apige.
Hazikupita hata dakika kumi, polisi

mmoja aliendesha gari na kugonga kioo cha gari la Bwana Malugu.
“Kuna jambo?” Erick alishusha dirisha.
Ofisa huyo aliwatazama mwanamume na mwanamke waliokuwa ndani ya gari, akisema kwa mshangao, “Mtu fulani aliripoti kwamba mnafanya biashara isiyofaa kwenye gari.”
Ni aina gani ya biashara zisizofaa ambazo mwanamume na mwanamke pekee wanaweza kufanya ndani ya gari? Maneno ya Erick na Lisa yakawa mazito kutoka vinywani mwao.
Lisa aliuliza kwa mshangao. "Haya umeona kuna biashara gani inayoendelea hapa?"
"Samahani." Afisa huyo alimlaani mtu

aliyewaripoti. Mtu huyo lazima awe mwendawazimu.
Afisa huyo alipoondoka na Erick akijiandaa kuendelea na mazungumzo, gari la maji lilipita ghafla likimwaga maji kwa fujo. Kwa vile dirisha lilikuwa limeachwa wazi, Erick, aliyekuwa ameketi upande huo, alilowa maji. Alikasirika sana hata uso wake ukawa mbaya ghafla.
Lisa alizuia kicheko chake na kusema.“Samahani, naona bora urudi nyumbani ukaoge,”
"Ndio, labda kuegesha gari langu hapa kumemkwaza mtu." Erick alitabasamu kwa jazba. Alikuwa mtu mwerevu. Lisa alikuwa na wafuatiliaji wengi usiku huo, lakini ni yeye tu ndiye aliyepata nafasi ya kumpeleka nyumbani, kwa hivyo

lazima kulikuwa na wanaume wengi waliomwonea wivu.
“Hapana, lazima nimemkosea mtu. Huenda kuna mtu ambaye atakuja kunisababishia matatizo baadaye.” Lisa alimkabidhi kitambaa na kutoka kwenye gari kuelekea kwake.
Akiwa anakaribia kubonyeza lifti, ghafla mkono mkubwa uliibuka kutoka nyuma na kuzuia kitufe cha lifti. Kisha, harufu ya kupendeza ya mtu aliyemzoea ilimfunika kutoka nyuma.
Lisa hakutazama juu na akasema kwa kawaida, "Baada ya shida uliyotuletea, bado haujatosheka tu?"
“Nimewaletea shida gani?” Kicheko cha kejeli cha mtu huyo kilisikika juu yake. Ilionekana kana kwamba hakukubaliana

kabisa.
Lisa akageuka na kuinamisha kichwa chake. "Uliripoti polisi kwamba nilikuwa na 'biashara zisizofaa' kwenye gari na ukatuma mtu wa kummwagia maji Bwana Malugu. Usiseme kuwa si wewe.”
"Kwanini nifanye mambo ya kipumbavu hivyo?" Alvin alijifanya kama amesikia mzaha na kuvaa tabasamu la kejeli. Asingekubali kufanya jambo kama hilo hata kama angepigwa hadi kufa. Ingekuwa ni kujifedhehesha sana.
"Lazima kuna mtu aliwaona mmekaa kwenye gari muda mrefu na akaripoti kwa polisi kwa nia njema." Macho ya Alvin yalipita kwenye sehemu kubwa ya kifua chake iliyo wazi. “Jiangalie. Umevaa hivi na unakaa kwenye gari na

kijana mhuni kama Erick Malugu. Huogopi kwamba watu watakuita hujiheshimu?”
"Kwa hiyo ikiwa mimi sijiheshimu? Tayari tumeachana, kwa hivyo hayakuhusu, ndiyo maana ninakuita mmbea." Lisa aliunyosha mkono wake na kubonyeza kitufe cha lifti.
Alvin aliutazama mgongo wake mzuri na kuhisi moyo wake ukimuuma kwa chuki. “Unafikiri Bwana Malugu atafanya nini akijua kwamba tulilala kwenye gari langu siku chache zilizopita?”
“Labda atanionea huruma zaidi. Baada ya yote, wewe ndiye unakaribia kutulia na kuanzisha familia.” Uso wa Lisa ulikuwa umejaa dhihaka. “Alvin Kimaro, huoni kuwa wewe ni msumbufu? Tayari tumeachana, na ni wewe

uliyenilazimisha kusaini talaka. Sarah na wewe mnafanya taratibu za kupandikiza mimba, lakini bado unaendelea kunifuatilia. Usiniambie kwamba huwezi kuniacha niende, au labda...Unamtaka Sarah, lakini unanitaka na mimi pia.” Alimsogelea ghafla. Sauti yake ya kuroga ilikuwa kama sumaku.
Alvin alimsukumia mbali kwa nguvu na kumdhihaki, lakini umahiri wake wa kucheza piano na uimbaji wake wa ajabu usiku huo uliangaza akilini mwake ghafla—pamoja na kumwona akicheza na wanaume wengine na kumwona akiongea na kucheka na wanaume wengine...Ghafla aligundua kuwa alikuwa ametumia zaidi ya usiku huo kumwangalia.
Walikuwa wametia saini karatasi za talaka. Lisa alikuwa huru kabisa.

Angeweza kuwa na yeyote anayetaka kuwa naye. Hata hivyo, wakati Bwana Malugu na yeye walipokuwa ndani ya gari kwa muda wa nusu saa tu, alitaka kukwaruza moyo na mapafu yake na kuyatoa nje! Alijua kuwa hakutakiwa kuendelea kuwa hivyo. Ingemuumiza Sarah, na haikuwa haki kwake pia. Hata hivyo, Alvin hakuweza kujizuia.
Sura ya: 360
"Kwani kuna ubaya kuwa na nyie wote?" Alimshika Lisa mabegani na kumkandamiza ukutani, macho yake yakiwa yanawaka moto. “Lisa, lazima nikubali kwamba wewe ni mwanamke wa kuvutia sana. Ni mimi ambaye sikukufahamu vya kutosha hapo awali.”
Kisha, akalazimisha kumbusu Lisa

mdomoni, lakini, Lisa aligeuza kichwa chake na kukwepa. Midomo yake iliangukia kwenye shavu lake na harufu nzuri ya mwili wake ikamshika na kumfanya ashindwe kujiondoa.
“Alvin Kimaro, unakumbuka jinsi ulivyowaagiza kwa hasira walinzi wako kunikandamiza chini na kunilazimisha kutoa cheti cha ndoa wiki iliyopita? Unakumbuka jinsi ulivyonilazimisha kusaini karatasi za talaka? Bado unakumbuka jinsi ulivyokuwa jeuri wakati huo?"
Lisa alisema kwa upole huku akionyesha huzuni. “Kweli uliponibeba siku ile kutoka kwenye gari sikuwa nimelala. Nilihisi tu kama ni ndoto na sikuthubutu kuamka. Baada ya wewe kuondoka, nilifikiri juu ya mambo mengi na kuhisi kuwa labda bado kulikuwa na

nafasi kwa ajili yetu. Lakini siku iliyofuata, ulikuja kwangu kutoa talaka. Hukuniachia hata chembe ya heshima. Wewe...” Karibu na mwisho, sauti yake iligoma, lakini bado alijifanya kuwa na nguvu.
Mwili wa Alvin ulikuwa mgumu. Mwili wake ulionekana kuwa na kikomo, na kumfanya ashindwe kujisogeza.
Lisa alimsukumia mbali. "Baada ya hapo, nilikuona na Sarah ulipokwenda kufanya upandikizaji wa mimba hospitalini. Kwa vile umeamua kuwa naye, kwanini huwa unarudi kuniumiza? Kati yangu na Sarah, mimi ndiye jalala la hasira zako na tamaa zako za ngono. Ulisema unanitaka, lakini kati yetu sisi watatu, ni lazima nikubali tena na tena kwamba ni mimi pekee ndiye ninayeumia zaidi. Hakuna anayeweza

kujifanya kana kwamba hana wivu, sivyo? Lakini nikimuumiza Sarah, unanipiga na kunikaripia tena.”
Lisa alijiinamia na kulia ghafla bila kujizuia. Alvin alimtazama na ghafla akahisi uchungu ukimjaa kifuani. Kwa kweli, alijua pia kwamba alikuwa akimtendea kinyume na haki. Hata hivyo, alikuwa alishikilia sana msimamo wake na kudharau ushawishi wa mwanamke huyo kwake.
"Simama." Alvin alinyoosha mkono kumshika, lakini, Lisa alimsukumia mbali kana kwamba alikuwa na wazimu. “Ondoka. Sitaki kukuona. Niache na maisha yngu, sawa? Sitaki kujihusisha na wewe na mkeo tena.” Aliangua kilio cha uchungu tena na tena.
Mwili wa Alvin ulijhisi kuganda. “Sawa,

nitaenda.”
Aligeuka taratibu na kutoka nje ya mtaa huo hatua moja baada ya nyingine. Hapo awali, alikuwa akifikiri kwamba anachukizwa na Lisa. Hakuwahi kufikiria kwamba hata siku moja angeweza kuguswa naye.
Wakati mwingine, alimchukia sana hadi akakosa raha kabisa, lakini kwa sababu fulani, kamba za moyo wake zilipigwa kwa namna fulani. Ilikuwa ni huruma kwamba alikuwa amechelewa kukutana naye.
Alvin alikaa kwenye gari na kuwasha simu yake. Kwenye skrini kulikuwa na picha ya Lisa ambayo alikuwa ameihifadhi kutoka kwenye mtandao siku chache zilizopita. Aliificha mahali fulani kimya kimya.
Usiku kucha, Alvin alikaa kwenye

maegesho ya magari ya Karen Estate na kuvuta sigara. Hakujua kuwa wakati huo tasnia ya burudani ilikuwa imetikisika.
Saa saba usiku, menejimenti ya Cindy ilifanya mkutano wa dharura na hatimaye wakatoa tangazo rasmi kwa umma. [Bila kujua, imepita miaka mitano tangu niingie kwenye tasnia ya burudani. Mwaka huo, 'Pepo ya Ndoto' ilinifanya kuwa maarufu kote Afrika Mashariki. Kwa kweli, kwa miaka mingi, nimekuwa nikimshukuru kimya kimya mtu mmoja moyoni mwangu na huyo ni rafiki yangu mzuri, Lisa Jones. Yeye ndiye aliyeniandikia album nzima ya 'Pepo ya Ndoto'. Ninashukuru sana kukutana na rafiki kama yeye katika maisha yangu. Alikuwa akijiweka kimya na hakutaka kujionyesha, lakini kwa kuwa sasa anajulikana kwa umma,

sitaki kuficha kipaji chake tena. Ninataka kumpa zawadi ambayo nilitunukiwa wakati huo. Hii ni tuzo yake. Lisa, nakupenda.]
Baadaye, Cindy alichapisha tuzo kadhaa na picha aliyokuwa amepiga akiwa na Lisa shuleni. Katika picha, wawili hao walikuwa wakitabasamu sana na wakionekana kuwa na urafiki wa ajabu.
Wanamtandao walilipuka.
[Kwa hiyo Lisa na Cindy walikuwa marafiki wakubwa. Tizama toka wakiwa shuleni walikuwa warembo kweli!]
[Si hivyo tu. Aliandika hata nyimbo za Cindy. Ni zaidi ya urafiki!]
[Hakuna mtu atakayezungumza kuhusu

kipaji cha muziki cha Lisa? Hivi, kuna jambo lolote ambalo hawezi kufanya? Kwa kweli, Lisa shikamoo!]
[Cindy ni mkarimu sana. Amemkumbuka rafiki yake wa karibu na kuelezea alivyomsaidia?]
Lisa alipoamka asubuhi na kuona maoni ya wanamtandao, alitabasamu.
Kama alivyotarajia, Cindy angefanya kitu haraka ili kulinda hadhi yake ndogo iliyokuwa imebaki isije ikapotea yote. Alitoa simu yake bila haraka na kumpigia Sam. "Sam, umemaliza nilichokuomba ufanye?"
“Bila shaka. Unadhani mimi ni nani? Ninatawala Dar Es Salaam. Ni kazi ndogo sana kupata kitu chochote kutoka kwa Janet Kileo. Kwa jinsi familia ya Kileo ilivyo dhaifu sasa, Janet

ananitazama kama anamtazama babu yake—”
“Unaweza kunitumia sasa hivi?” Lisa alikatiza majigambo yake.
“Hakika. Una akili sana. Huenda Cindy alisahau kwamba aliacha mambo mengi mabaya alipokuwa akijaribu kuwalambalamba Lina na Janet huku Dar Es Salaam.” Sam alimtumia rekodi.
Lisa mara moja aliipachika chini ya chapisho la Cindy kwenye Facebook.
[Asante kwa kufunua ukweli, Cindy Tambwe, lakini nilikuwa mdogo
na mjinga nilipokuwa pamoja nanyi zamani. Sikujua jinsi ya kuwasoma watu wakati huo. Baada ya mambo mengi kutokea, sithubutu kukuchukulia kama rafiki tena.]

Wanamtandao walipakua na kusikiliza rekodi ambayo Lisa alichapisha kwa udadisi.
Kwenye rekodi hiyo ya simu, sauti ya Janet ilisikika ikisema, “Huogopi kwamba Lisa atagundua unakula chakula cha jioni na mimi? Sisi ni maadui wakubwa."
Sauti ya Cindy kisha ikajibu, “Kwa hiyo ikiwa atagundua? Kwa hali yake ya sasa, hatoki katika ulimwengu sawa na mimi.”
Janet akajibu, “Hiyo ni kweli. Nilisikia kutoka kwa Lina kwamba familia ya Jones ilimfukuza na hana hata mahali pa kukaa sasa. Alikuomba msaada?"
"Alinipigia simu, lakini sikuipokea."

"Haha, vizuri. Hivyo ndivyo inavyopaswa kuwa. Akikuomba kumkopesha pesa, usifanye hivyo.”
“Bila shaka, sitafanya hivyo. Lakini Pamela huyo mjinga hakika atafanya hivyo.”
Rekodi iliisha ghafla. Hata hivyo, ilitosha kwa wanamtandao kujua rangi halisi za Cindy.
[Hiyo ni sauti ya Cindy kweli?]
[Ni hakika. Ni sawa kabisa na uimbaji wake wa kawaida na sauti yake kwenye vipindi vya Runinga.]
[Kwa hivyo rekodi ilikuwa baada ya Cindy kuwa maarufu. Alimdharau Lisa na kukataa kupokea simu za Lisa au kumkopesha pesa wakati alihitaji

msaada zaidi? Ooh! My God, hata yeye ni binadamu? Alichapisha post yake na kusema kwamba Lisa na yeye walikuwa kama dada usiku wa manane. Huo ni unafiki mkubwa!]
[Bora na nyie watu mmegundua kuwa yeye ni mnafiki. Nimekuwa nikisema mara kadhaa hapo awali kwamba Cindy ana nyodo sana. Hana maana na anadharau watu, anajifanya kama yeye ni mungu wa kike.]
[Hata aliwaita wengine wajinga kwa kumkopesha Lisa pesa. Ana utu kweli? Ikiwa Lisa asingemwandikia nyimbo, angekuwa hapo alipo leo?]
TUKUTANE KURASA 361-365

ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo
wake (By: Official Dully)
 
Back
Top Bottom