Simulizi: Lisa

Simulizi: Lisa

LISA KITABU CHA NANE (10) SIMULIZI...........................LISA
KURASA.....................481- 485
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 481
"Acha kuongea ujinga." Rodney alifadhaishwa kidogo na alichosema Pamela.
“Nasema ukweli tu. ” Wakati huo, Pamela aligeuka na kusimamisha teksi.
“Hutaki nikurudishe?” Rodney alifoka.
“Nisingethubutu. Wewe ni mkorofi sana. Ninaogopa kwamba utnaweza kunitupa barabarani. ” Mara moja Pamela aliingia kwenye teksi bila kutazama nyuma.
Rodney alikuwa ameduwaa kwa muda mrefu. Hii haikwenda kama alivyofikiria. Alidhani kwamba Pamela bila shaka angemsumbua. Baada ya yote, asilimia 10 ya hisa za Shangwe Corporation zilimuuma sana.

Subiri! Alikuwa amesahau kumkumbusha kuchukua vidonge vya kuzuia mimba.
Dakika hamsini baadaye, Pamela alishuka kwenye gari na kumuona Rodney akitokea kwenye gari nyuma yake, alikuwa akimfukuzia kwa nyuma tangu uwanja wa ndege.
“Unataka nini tena?” Hali ya Pamela ilizidi kuwa mbaya mara tu alipomwona yule mjinga.
"Kunywa hii." Rodney alimkabidhi boksi la vidonge vya kuzuia mimba kwa macho ya kukwepa. "Siwezi kukuacha uwe na mimba ya mtoto wangu."
Moyo wa Pamela ukatulia. Kwanini hakuwa na bahati katika maisha yake? Kwanza, alikutana na Patrick, na sasa, alikuwa Rodney, wote ni watu wa ajabu tu!

“Usijali. Nilikunywa mara moja nilipotoka hotelini jana. Ningechelewa sana kama ningesubiri uniletee.” Pamela alizuia hasira yake alipomkaribia hatua kwa hatua. “Rodney Shangwe, usiende mbali sana. Mimi ndiye mhanga hapa. Tafadhali kumbuka kwamba kama si kwa sababu nilijiunga na Osher, ubikira wangu usingeharibiwa na wewe. Unaweza kunichukia, lakini unapaswa kunithamini.”
Rodney alishindwa kujizuia kurudi nyuma kutokana na hasira iliyokuwa machoni mwake, mwili wake ukahisi kuishiwa nguvu kidogo.
“Nafanya hivyo kwa manufaa yako, sikupendi! Hata ukiishia mimba ya mtoto wangu utakuwa single mother. Hata hivyo, usifikiri hadhi yako itabadilika kwa sababu tu una mtoto wangu.”
“Usijali. Sitaki kueneza jeni zako duni,

lakini hii ilinitokea kwenye mkutano wako na waandishi wa habari. Si unipe maelezo ni nani aliniwekea?” Pamela aliuliza kwa ukali.
Rodney alishangazwa na swali hilo. Bila shaka, alijua ni Thomas. Hata hivyo, Thomas alikuwa kaka ya Sarah, na Sarah tayari alikuwa amefanya mambo mengi kwa ajili yake. Ikiwa angemwambia, Tomaso angeweza kuingia matatani na hivyokumsononesha Sarah.
“Mimi... Ningejuaje? Lazima uliwachokoza nyuki wa porini kwa kuvaa vile. Nilikwambia ukabadilishe ukajifanya mjanja.” Rodney alitazama pembeni kwa hatia, hakuthubutu kukutana na macho yake.
Lakini, macho yake hayakuweza kukwepa macho ya Pamela. Ilionekana kuwa mawazo ya Lisa yalikuwa sahihi.

Alikuwa ni Thomas Njau usiku huo, na Rodney aliijua, lakini alikuwa akimfichia Sara.
Athari kubwa ya kukata tamaa ilimwangazia machoni mwake. Ingawa hakumpenda, bado alimkubali mtu huyu. Alifikiri tu alikuwa kipofu kumpenda Sarah.
Ilikuwa sawa ikiwa macho yake yangekuwa kipofu, lakini moyo wake ulikuwa kipofu pia, kiasi kwamba asingeweza kutofautisha mema na mabaya. Kulikuwa hakuna kitu cha kuthamini juu ya mtu kama huyo. Bila kumtazama tena, Pamela aligeuka na kuondoka.
"Hey, unaondoka hivyo hivyo tu?" Rodney alipigwa na butwaa kwa muda lakini bila fahamu akamzuia.
"Nini? Utaniambia kuwa alikuwa Thomas? Je, utanisaidia kumkamata?

Ulimsaidia hata kuficha ushahidi.” Pamela alicheka kwa unyonge. "Rodney Shangwe, usinichukulie kama mjinga. Usiku huo, Thomas pekee ndiye angethubutu kufanya jambo kama hilo, akizingatia jinsi alivyothubutu kuingia ndani ya nyumba yangu, kunipiga, na kunishambulia miaka mitatu iliyopita.
“Miaka mitatu baadaye, ana wewe wa kumlinda, kwa hiyo hawezi kufanya nini? Ana maisha mazuri sana. Hata kama hana Alvin pembeni yake, bado ana Rodney Shangwe.”
Kisha, akainamisha macho yake ili kuficha chuki machoni mwake na kuondoka bila kuangalia nyuma.
Rodney alimtazama akiondoka kwa mwendo wake wa madaha, na uso wake mzuri ukawaka kwa aibu. Hakufikiri Pamela angejua kila kitu. •••

Usiku, karamu ya biashara ilikuwa ikiendelea. Alvin alisimama kwenye kibaraza cha wazi, chini ya anga ya usiku, akiwa na glasi ya divai mkononi mwake. Macho yake ya kina na ya huzuni yalitazama kupitia dirishani kwenye sherehe nzuri na ya kuvutia ndani.
Asingeenda kwenye karamu hiyo ikiwa mwenyeji wake hakuwa mshirika wake wa biashara kwa miaka mingi. Hakupendezwa kabisa na matukio kama haya. Ikiwa asingekuwa na ugomvi na Lisa, angeandamana naye kwenye karamu hiyo. Pamoja naye, karamu isingekuwa ya kuchosha sana.
Labda ni kwa sababu alikuwa amelewa kidogo, lakini akili ya Alvin ilijawa na mawazo yasiyo na huruma. Alim’mis sana Lisa. Alitaka kumvuta mikononi mwake kwa nguvu na kumbusu kwa nguvu.

Ghafla, mwanamume na mwanamke walitoka nje. "Hubby, kwanini umeniuliza habari za mawasiliano ya Nebula sasa hivi?"
“Ni kwa sababu ya Kelvin Mushi kutoka Golden Corporation." Mwanamume huyo alieleza, “Alifikiri kwamba nguo uliyovaa wakati wa harusi yetu ilikuwa nzuri, kwa hiyo akaniomba niwasiliane na Nebula.”
“Mbona mwanaume kama yeye anaulizia gauni la harusi? Je, amepata mpenzi? Lakini sikuwahi kusikia kuwa alikuwa na rafiki wa kike hapo awali. Halo, ulimweleza wazi? Nebula hasa hutengeneza nguo bora kabisa za harusi.”
"Nilimweleza. Hakunijibu nilipomuuliza ikiwa anafunga ndoa, lakini nilisikia kwamba familia yake huko Dar es

Salaam ilikuwa imempangia ndoa, na aliridhika sana nayo.”
“Labda kweli anaoa. Itabidi tuhudhurie harusi hiyo.”
"Alisema haitakuwa harusi ya kifahari, na sherehe itafanyika Dar es Salaam, lakini tayari nimempa baraka zangu."
Kelvin Mushi! Macho ya giza ya Alvin yalijawa na mwanga ghafla, yakatumbuka kama yanataka kuanguka. Ikiwa mtu huyo asingetaja, alikuwa kishalisahau jina hilo.
Miaka mitatu iliyopita, Kelvin aliendelea kumsumbua Lisa na kumtazama kwa kumtamani, lakini sasa alikuwa anaoa. Baada ya yote, miaka mitatu ilikuwa imepita. Hakuweza kumngoja Lisa milele, na umri haurudi nyuma, kwa hiyo ilikuwa kawaida kwake kuoa.

Hata hivyo, kulikuwa na hali isiyoelezeka ya wasiwasi moyoni mwake.
Akiwa amekasirika, akanywa mvinyo. Aliyekuwa akiolewa na Kelvin bila shaka hakuwa Lisa, kwanini alikuwa anawaza sana?
Saa tatu usiku alipokuwa akijiandaa kuondoka, ilitokea tu bahati kumwona Kelvin akitoka kwenye korido ya chumba cha maliwato. Ilikuwa wazi kwamba Kelvin alikuwa katika hali nzuri. Tabasamu tulivu lilining'inia kwenye kingo za midomo yake, na alikuwa amevalia suti na fulana nzuri nyeusi iliyomfanya aonekane mzuri na maridadi.
Alvin alikunja uso na bila fahamu akajihisi kama mtu anayeumwa macho. "Bwana Kimaro." Kelvin alimpa kwa heshima salamu.

“Mh.” Alvin akanyanyua miguu yake mirefu na kuondoka.
Jamaa huyo mwenye kiburi alipoondoka, tabasamu la kejeli lilitanda mdomoni mwa Kelvin, akajiwazia moyoni mwake. 'Alvin Kimaro, wacha tuone ni muda gani unaweza kujivunia! Hivi karibuni, utaanguka kutoka kwenye mawingu, na mwanamke wako nitamuoa. Inasikitisha kwamba bado haujui chochote.’
Baada ya kutoka kwenye karamu hiyo ya biashara, Alvin alimtaka dereva ampeleke kwenye jumba la familia ya Ngosha.
Sura ya: 482
Kwenye dirisha la ghorofa ya pili la jumba la Joel Ngosha, mwili mdogo wa Lucas ulipanda hadi dirishani na kuchungulia nje. "Mama, baba mchafu

yuko mlangoni tena."
Kwa siku kadhaa, Alvin alikuwa akisimamisha gari lake kwenye mlango wa jumba la familia ya Ngosha, na wakati mwingine, alikuwa akiondoka tu baada ya Lisa kuondoka kwenda kazini. Lisa alikuwa tayari ameshazoea.
“Usimjali. Nenda kalale." Lisa alimtoa Lucas kwenye kiti na kuvuta vifunga dirisha huku akihofia macho makali ya Alvin yangemuona Lucas.
"Mama, ikiwa siku zote yuko hapa, itakuwaje akigundua kuwa unafunga ndoa na Anko Kelvin?" Lucas aliuliza kwa wasiwasi.
“Hatajua. Muda ukifika, nitaiambia kampuni itangaze kuwa niko kwenye safari ya kikazi na nitaondoka kwa siku chache.” Lisa alikisugua kichwa chake kidogo kumliwaza. "Lucas, utajali kuwa

mama anaolewa?"
"Hapana. Nimefurahi kwamba mama hatimaye amepata mtu ambaye atakutendea mema,” Lucas alisema kwa umakini. “Na Anko Kelvin ni mzuri sana kwangu na Suzie. Hakika akikutendea ubaya siku moja nitamfundisha somo. Mimi nitajifunza kungfu, na nikiwa mkubwa nataka niwe mwanajeshi. Nitakuwa na nguvu sana hivi kwamba hakuna mtu atakayeweza kumdhulumu Mama tena.”
"Kijana mzuri." Lisa akambusu paji la uso wake.
Siku iliyofuata, Lisa alitoka nje ya Jumba asubuhi. Alipotoka nje ya geti, aliendesha gari moja kwa moja kana kwamba hakugundua uwepo wa Alvin. Alvin alilitazama gari lake kwa mbali kwa uso uliojaa uchungu.

Zamani, alipokuwa akingoja getini, bado alikuwa akitoka kuongea naye asubuhi. Lakini sasa, hakumpa hata nafasi ya kukutana naye. Kwa kuwa Lisa alienda kazini, hakukuwa na haja ya yeye kukaa hapa tena.
Jioni, Alvin akiwa anajiandaa kwenda kwa akina Lisa tena, ghafla Bibi Kimaro alimpigia simu na kumtaka arudi.
Ilikuwa tayari saa kumi na mbili jioni, na Suzie alikuwa akila na Mzee na Bibi Kimaro. Alipomuona Alvin akiingia ndani, moyo ulimchanika kusikoelezeka huku akiuma kijiko. Ingawa alikuwa bado mchanga, aliweza kuona kuwa baba yake mchafu alikuwa amedhoofu na amechoka zaidi. Nywele zake fupi zilizokuwa safi na nadhifu zilikuwa zimekua kidogo na kukosa matunzo. Bado alikuwa mzuri na anavutia, lakini pia alikuwa na huzuni zaidi.

"Kula chakula cha jioni kisha upande ghorofani ukapate usingizi mzuri, nahisi una mwaka mzima hujala wala kulala." Bibi Kimaro alihema. Hata iweje, bado alikuwa ni mjukuu wake, hivyo kumuona hivyo moyo wake ulimuuma sana. “Acha kusubiri kwenye lango la akina Ngosha kila siku. Umemaliza upasuaji juzijuzi hapa. Utaharibu mwili wako tu bure."
“Niko busy. Ikiwa hakuna kitu kingine unachohitaji, nitaondoka."
Alvin alipokaribia kugeuka ili aondoke, Mzee Kimaro alishindwa kujizuia. “Usifikiri kuwa sijui unaenda kwa akina Ngosha tena. Kila mtu hapa Sherman Mountain tayari anajua kukuhusu kusubiri huko kila usiku, na yeye anataka kuondoka. Zamani, sote tulikushawishi umuoe, lakini hukutusikiliza. Sasa kwa kuwa unajuta, unataka kurudi kwake tena. Unafikiri unaweza kumtupa na kurudiana naye

muda wowote unapotaka?”
“Ndiyo, Alvin. Mwache Lisa aendelee na maisha yake, na wewe mwenyewe uendelee na yako. Bado wewe ni mdogo, una safari ndefu mbele yako. Lisa sio mwanamke pekee katika ulimwengu huu." Bibi Kimaro akatikisa kichwa. Alikuwa mzee sana kuelewa mambo ya mapenzi ya kizazi kipya, lakini alihisi kuwa Lisa asingeweza kumsamehe mjukuu wake.
"Sitaki mtu mwingine ila yeye." Alvin alikunja ngumi kwa ukaidi na kwenda mbele.
Suzie alikimbia na kumshika mkono ghafla. “Anko usiende. Unaweza kulala nami usiku wa leo? Baba harudi nyumbani, na sitaki kulala na yaya.” Msichana mdogo akamtazama kwa macho malegevu na ya kusihi, na moyo wa Alvin ukalegea. Hakuweza kuvumilia

kumkataa.
Angeweza kusema kwa wengine, lakini kamwe hakuweza kusema 'hapana' kwa Suzie.
“Baki na Suzie.” Bibi Kimaro mara moja alimshawishi alipoona amesita kuondoka. "Haujarudi kwa muda mrefu, kwa hivyo anaku’miss."
“Sawa.” Alvin alikubali.
Usiku, baada ya yaya kumuogesha Suzie, Alvin alimkumbatia ili alale. Ingawa hakuwa amelala sana katika siku chache zilizopita, hakuweza kupata usingizi alipokuwa amelala kitandani.
Hata hivyo, hakutarajia Suzie angejirusha na kugeuza kifua chake, asipate usingizi pia. “Anko...”
“Mh? Nini tatizo?" Alvin alimtazama kwa upole.

Moyo wa Suzie ulihisi uchungu. Alijua kwamba ndiye baba yake halisi, lakini hakuweza kumwambia kwamba mama yake alikuwa karibu kuolewa na Kelvin baada ya wiki moja. Kelvin alikuwa mzuri, lakini baba yake mchafu alionekana mwenye huzuni sana. Alimchukia wazi siku chache zilizopita, lakini moyo wake ulikuwa umebadilika siku chache zilizopita pia. Alikuwa mnyonge sana!
“Anko, wiki ijayo... Baba atanipeleka safarini kwa siku chache.” Mwishowe, Suzie alishindwa kuvumilia.
“Hiyo ni nzuri. Jack anapaswa kukupeleka nje kucheza. Nitampa siku mbili za mapumziko.” Alvin hakufikiria sana juu yake.
Moyo wa Suzie ulimuuma, akatoa dokezo lingine. “Rafiki ya baba anaoa,

kwa hiyo atanipeleka kwenye harusi."
"Loo, kuna chokoleti nyingi za kula kwenye harusi, lakini usile nyingi sana," Alvin alimkumbusha kwa sauti ya chini.
Ndani ya moyo wake, Suzie alihema bila msaada. Hivyo ndivyo vidokezo pekee ambavyo angeweza kutoa kwa Alvin. Ikiwa angekuwa wazi sana, Mama yake na Lucas bila shaka wangekasirika.
'Baba, ni juu yako kuigundua mapema. Ikiwa huwezi, basi ndivyo hivyo.' Suzie alijisemea kimoyo. Alitamani sana baba yake aingie kwenye kichwa chake na kuyasoma mawazo yake moja kwa moja.
Siku chache zilizofuata, Alvin alikuwa na kazi ya kwenda na kurudi kati ya Jumba la familia ya Ngosha, na kampuni ya Mawenzi. Kwa kupepesa macho, siku sita zilikuwa zimepita.

Alasiri hiyo, kichwa chake kilihisi kizunguzungu kidogo, labda kwa sababu alikuwa hajapumzika vizuri. Katibu alipomkumbusha kwamba kulikuwa na mkutano wa kimataifa kwa njia ya video uliofanyika saa tisa kamili.
Alvin alikasirika na kusema, “Usije kwangu kwa kila jambo dogo. Jack si yupo? Anaweza kushughulikia mambo haya. ”
"Hapana, Bwana Mkubwa Kimaro. Bosi Jack yuko likizo leo na kesho,” katibu huyo alisema.
Alvin aliduwaa na ghafla akamkumbuka Suzie akisema kuwa Jack anaenda kuhudhuria harusi. “Sawa, nimekumbuka.”
Usiku uliofuata, aliendesha gari hadi kwenye mlango wa jumba la Ngosha.

Alisubiri getini hadi saa sita usiku, lakini hakuona gari lolote likitoka wala kuingia getini. Kwa sababu fulani, hali ya wasiwasi ilimpanda, na hakuweza kujizuia kumpigia Hans simu.
“Peleleza ujue Lisa alienda wapi na kwanini hajarudi mpaka usiku huu.”
Hans hakutaka kufanya hivyo, lakini alikuwa chini ya Alvin. Kwa hivyo, alitafuta mtu wa kumuuliza huko Mawenzi Investments na akajibu haraka, "Bi. Jones ameenda Uganda kwa safari ya kikazi.”
Kama bosi wa kampuni kubwa, ilikuwa kawaida kusafiri kwa biashara. Moyo wa Alvin ulishuka ghafla, akiogopa kwamba huenda amepata mpenzi mpya. Ingawa alijua kwamba asingepata hivi karibuni, bado aliogopa.
"Peleleza alipofikia anaishi hoteli gani. Pia, niwekee tiketi ya ndege ya kwenda

Uganda." Alvin mara moja alisema.
Kichwa cha Hans kilianza kumuuma. "Bwana Mkubwa, kampuni ina shughuli nyingi ..."
"Hakuna kitu muhimu zaidi kuliko yeye. Suzie alisema kuwa wanawake wanapaswa kulindwa. Kwa hali hiyo, nitamfuata popote atakapokwenda. Ninaamini kwamba ataelewa unyoofu wangu,” Alvin alisema kwa sauti ya chini.
Sura ya: 483
Hans alikosa la kusema na akajiwazia kwa siri kuwa mtoto Suzie alijua kweli kuwachanganya wazazi wake. Ikiwa Lisa angedundua kuhusu hila za Suzie, angeweza kupandwa wazimu.
“Sawa, nitashughulikia.” Hans hakuwa na chaguo ila kuwapigia watu wa

Uganda. Hata hivyo, alipata habari kwamba hakukuwa na rekodi ya Lisa katika hoteli yoyote ya Uganda. Je, Lisa alikuwa na nyumba ibinafsi huko? Alipiga simu kwenye uwanja wa ndege uliofuata na kugundua kuwa hapakuwa na rekodi ya ndege ya Lisa kuruka hadi Uganda. Badala yake, alifahamu kuwa Lisa na Pamela walisafiri kwa ndege hadi Dar es Salaam jana.
Kichwa chake ghafla kilihisi ganzi kidogo. Kwa nini Lisa alienda Dar es Salaam wakati huo lakini akadai kwamba alikuwa Uganda kwa safari ya kikazi? Je! ni kwa sababu alikuwa akifanya jambo kwa siri huko Dar es Salaam, na sababu ilikuwa ni kumficha Alvin?
Kufikiria juu yake, kulikuwa na uwezekano mkubwa. Akiwa anawaza tu, Alvin alimpigia. “Umeshakata tiketi?” “Hapana, mimi... sikujua ni wapi Bi

Jones anakaa Uganda. Anaweza kuwa na nyumba binafsi huko. ” Hans alifanya uamuzi mara moja. Kwa kuwa Lisa alikuwa akijaribu kujificha, angemsaidia. “Bwana Mkubwa, usiende. Jamaa kutoka Mawenzi alisema kuwa Bi Jones atakuwa nje kwa siku mbili hadi tatu pekee. Anaweza kurudi kesho.”
“Basi naweza kurudi naye. Ngoja nitafute watu wa kumfuatilia.”
Mara Alvin alimpigia Master Ganja kutoka ONA baada ya kukata simu. Kwani, ONA ilikuwa na macho kila mahali.
Takriban nusu saa baadaye, Ganja alipiga akiwa na habari njema. “Bwana Mkubwa, taarifa za ndege zilionyesha kuwa Bi Jones hakwenda Uganda kwa safari ya kikazi. Alikwenda Dar es Salaam na Pamela Masanja.”

"Anafanya nini huko Dar es Salaam? ” Macho ya Alvin yalififia. "Hans aliangalia na kusema kwamba alikwenda Uganda."
"Aliiambia kampuni kwamba alikwenda Uganda, lakini hakwenda," Ganja alisema. "Hakuna rekodi inayoonyesha hoteli anayokaa huko Dar es Salaam, lakini Dar es Salaam ni nyumbani kwao, kwa hivyo anaweza kuwa anakaa katika nyumba yake ya zamani.”
Alvin akazidi kuwa na mashaka. Kwanini Lisa alilazimika kusema uwongo ikiwa anarudi Dar es Salaam na Pamela? Kweli, Jack alichukua siku ya kupumzika siku hiyo pia. Je, ilikuwa ni bahati tu? Watu hao watatu waliondoka Nairobi kwa wakati mmoja, na ilionekana kana kwamba Joel hayupo nyumbani kwake pia.
“Peleleza pia Jack na Joel Ngosha

walienda wapi.” Aliamuru ghafla.
Punde, Ganja aligundua mahali alipo Jack. “Bwana Mkubwa, Jack na Joel pia wamekwenda Dar es Salaam.”
Suzie alisema kwamba Jack alikuwa akimpeleka kwenye harusi ya rafiki yake. Watoto hawakusema uwongo. Jack, Pamela, Lisa, na Joel. Je, walikuwa na rafiki gani wa kufanana kwamba wangehudhuria harusi pamoja? Haikuwa na maana.
Subiri... Ghafla akakumbuka kwamba alipohudhuria karamu siku kadhaa nyuma, alisikia kwamba Kelvin Mushi alikuwa akioa, bibi-arusi alikuwa ni nani? Hata hivyo, Jack na Joel hawakulazimika kuhudhuria harusi ya Kelvin. Hawakumjua Kelvin vizuri, isipokuwa kama Bi harusi alikuwa ni mtu waliyemfahamu kabisa, lakini ...

Wazo hilo lilipojitokeza, mwili wake wote ulitetemeka. “Niandalie helkpota yangu mara moja. Ninataka kwenda Dar es Salaam. Sasa hivi.”
Ganja alishtuka. "Lakini Dar es Salaam iko mbali kidogo, na utahitaji kutuma maombi ya njia ya ndege kwenda Dar es Salaam..."
“Sijali. Tumia njia yoyote ya haraka iwezekanavyo. Sijali ni pesa ngapi inachukua kuhonga watu wa uwanja wa ndege. Fanya hivyo sasa.”
Alvin alikuwa akichanganyikiwa kutokana na wasiwasi. Alitumai kuwa huo ulikuwa ni uvumi tu na kwamba haikuwa kweli. Je, ikiwa mtu ambaye Kelvin alikuwa anamuoa alikuwa ni Lisa kweli?
Alvin alishikwa na mshikemshike kabisa akidhani Lisa anaenda kuolewa na mtu

mwingine ghafla. Wakati huo huo, moyo wake ulionekana kushikwa kwa nguvu na nguvu isiyoonekana, iliuma sana akatamani kufa. Ikawa kwamba hisia zake kwa mwanamke huyo zilikuwa za kina kuliko vile alivyowazia. Afadhali kumwangamiza kila mtu kuliko kumwacha aolewe na mwanaume mwingine. Alipokuwa akiwaza hayo, aliendelea kumpigia simu Lisa, lakini hakuweza kumpata.
Upande wa pili, huko KIM International, Hans aliposikia kwamba Alvin alikuwa akiandaa helkopta yake kibinafsi haraka, alisita kwa muda mrefu kabla ya kupiga nambari ya Lisa bila raha.
"Hans, kuna nini?"
Hans alitabasamu kwa uchungu wakati sauti ya Lisa ilipotoka. “Bi. Jones, kwanini ulitoroka kwenda Dar es Salaam? Alvin aliogopa na kuamua kukufuata.”

“Baaasi.” Pamela, ambaye alikuwa kama kijakazi kando ya Lisa, alishtuka sana hivi kwamba viatu virefu mikononi mwake vilianguka chini.
"Hans, ninafunga ndoa leo." Lisa alisema kwa sauti ya chini.
"Nini?" Hans aliruka kutoka kwenye kiti chake kwa mshtuko. “Wewe ... unaolewa na nani? Kwanini hapakuwa na habari yoyote kuhusu hili?” Alipiga uso wake kwa nguvu, akishuku kuwa ni ndoto mbaya.
"Kelvin Mushi.” Sauti ya Lisa ilikuwa laini. “Nimeteswa sana na Alvin kwa miaka mingi sana. Baada ya tukio la mwisho, hatimaye nilielewa kuwa Kelvin ndiye bora kwangu. Nataka kumuenzi, lakini naogopa Alvin angegundua, kwa hivyo tulipanga kwanza harusi ya hali ya chini. Nadhani huenda Alvin ameona

kitu. Hata asipofika, atajua akifika.”
Hans alikosa la kusema kabisa na habari hizo za kulipuka. “Bi. Jones, unafanya jambo kubwa huku ukimzuia jamaa asijue?” Alitabasamu kwa uchungu. "Ikiwa Bwana Mkubwa atagundua, hakika atachukia. Anaweza hata kufanya jambo la ajabu sana.”
Wazo la kugundulika na alvin lilimfanya Lisa ashtuke na kutaka kughairi harusi.
“Bi. Jones, ninakadiria kwamba itachukua saa mbili na nusu kufika Dar es Salaam kwa mwendo wa kasi zaidi.” Hans angeweza tu kumkumbusha.
Ilikuwa ni ukweli kwamba Lisa na Alvin hawakuweza tena kurudiana pamoja, hivyo hakuweza kumshawishi. Mbali na hilo, Bi Jones alikuwa ameteseka sana miaka hiyo michache.
"Asante kwa kuniambia, Hans." Lisa

alimshukuru kwa dhati. Kama si Hans alimsaidia kwa siri miaka yote hiyo, asingekuwa mahali alipokuwa muda huo.
"Sitamwambia Bwana Mkubwa kuhusu hili, lakini nadhani atajua mara tu atakapowasili Dar es Salaam." Hans alisema na kukata simu.
Katika chumba cha hoteli, Pamela alimtazama Lisa kwa wasiwasi. "Tunapaswa kufanya nini? Masaa mawili na nusu itakuwa karibu saa saba na nusu machana atakapofika Alvin. Ikiwa atafanya haraka, sherehe ya harusi inaweza kuwa bado haijaisha.”
“Basi tutaiwahisha mapema. ” Kelvin akaingia ghafla. “Nitaarifu hoteli kwamba itafanyika saa tano na nusu asubuhi.”
Lisa alishtuka. "Lakini wageni bado

hawajafika."
“Ndugu zetu wote wanakaa katika hoteli hii, kwa hiyo tunaweza kupiga simu na kuwaomba waje mapema. ” Kelvin alikandamiza mikono yake kwa upole begani mwake, akimhakikishia, “Pia nitapanga baadhi ya waandishi wa habari waje. Hapo awali nilipanga kuiweka chini ya rada, lakini Alvin anaweza kuwa amegundua kitu, kwa hivyo ni bora kuiweka hadharani. Siamini kwamba atampokonya mke wa mtu mwingine bila kujali sifa yake.”
Lisa aliitikia kwa kichwa. Kusema ukweli, Alvin alikuwa mtu wa kutisha. Hakujua kama angevumilia jambo kama hilo.
Pamela alikuwa na huzuni. “Ulitaka kusubiri hadi upate ujauzito ndio utangaze. Habari zilivuja wapi hasa? Oh, nakuonea huruma sana.

Ulimchokoza mtu tajiri zaidi nchini.” Pamela alipumua.
Karaha kubwa ilitanda machoni mwa Lisa huku akisikiliza. Alichukia wanaume ambao hawakujua jinsi ya kuthamini wengine kama Alvin Kimaro zaidi. Ikiwa angeweza kufanya hivyo tena, hakutaka kukutana naye tena.
Sura ya: 484
Saa tano asubuhi,
Ndugu wa familia ya Mushi walikuja mmoja baada ya mwingine kumuona bibi harusi. Lisa alivaa viatu vyake virefu na kusimama, na kuwaona Sonya Mushi, Ethan Lowe, na Tracy Laizer wakiingia pamoja.
Akiwaza hayo, ilikuwa imepita miaka kadhaa tangu Ethan na yeye kuonana. Mwaka huo, alipoondoka Dar es

Salaam, Ethan alilazimika kumfanya Tracy Laizer, mtoto wa Bilionea wa madini, kuwa mpenzi wake ili kusaidia familia ya Lowe, na walikuwa pamoja tangu wakati huo.
"Lisa, ni muda mrefu." Ethan alimtazama kwa macho magumu. Baada ya kutomuona kwa miaka mitatu, alizidi kuwa mrembo, haswa leo. Akiwa na vazi la harusi lenye weupe wa theluji na uso wake mdogo wa kushangaza ulioguswa na mpambaji kwa usanii mkubwa, alionekana mrembo kama wa kwenye hadithi. Alipokuwa mdogo, alizoea kufikiria mara nyingi kuhusu kuolewa naye, lakini hakufikiri kwamba angeolewa na mjomba wake hata siku moja.
“Ethan, huyu ni mkeo, sivyo? Yeye ni mrembo sana. ” Lisa alitabasamu kwa unyonge na kumsalimia Tracy.

“Habari, Bibi.” Tracy aliitikia kwa kichwa. Bila shaka, alijua kwamba mumewe alikuwa ameshikamana na mpenzi wake wa zamani, lakini kwa bahati mbaya, Lisa alikuwa karibu kuolewa na Kelvin. Hakuwa na maoni mazuri ya Lisa, lakini hakukuwa na kinyongo pia.
Lisa alipigwa na butwaa katika salamu hiyo. Hakuweza kujizuia kufikiria mawazo yake ya zamani. Mara nyingi alifikiria kuhusu Lina kumwita Shangazi, lakini bila kutarajia, Lina na Ethan walitengana.
“Sonya, huyu ndiye bibi harusi, sivyo? Ni mzuri." Baadhi ya jamaa wa familia ya Mushi walikusanyika ghafla karibu na Sonya na kuzungumza.
Sonya alimtazama Lisa kwa dharau kidogo. "Kweli yeye ni mrembo, lakini ni aibu kwamba yeye ni bidhaa ya mtumba."

Maneno ya jamaa zake yalikuwa tofauti. “Kwanini Kelvin anaoa mtu ambaye aliolewa hapo awali? Kelvin wetu ni mmoja wa wajasiriamali wa juu nchini na kijana mashuhuri. Wanawake kama yeye hawastahili.”
“Oh, haikuweza kusaidia. Kelvin alirogwa naye.” Sonya alipumua kwa muda mrefu na kwa nguvu.
Baadhi ya jamaa wa familia ya Mushi mara moja walimtupia Lisa macho kwa dharau. Lisa alikunja uso kidogo aliposikia. Sonya alikuwa hampendi na bado hakumpenda.
Pamela alikasirika na kutaka kuongea wakati Ethan alipomtazama mama yake bila furaha, akisema, "Mama, kwanini Lisa hastahili kuwa na mjomba? Yeye ni mwenyekiti wa Mawenzi Investments na ana utajiri wa mabilioni, bila kusahau

hadhi yake kama mbunifu bora, na babake ni Bw. Joel, miongoni mwa watu mashuhurinchini Kenya na watanzania waliofanikiwa zaidi nje ya nchi. Kwa mawazo yangu, ni Mjomba ndiye anayepata daraja la kijamii kwa kumuoa.”
“Wow, huyu bibi harusi ni wa ajabu sana. ” Macho ya wale jamaa walipomtazama Lisa yalibadilika tena ghafla.
"Hakuna mtu atakayefikiri wewe ni bubu ikiwa hauongei." Sonya alimtazama Ethan kwa ukali.
“Mama, fanya haraka uende kuwasalimia wageni. Kuna jamaa wengine nje.” Ethan alimkumbusha bila kujali, akimfukuza mwanamke huyo kijanja.
"Mwishowe, amani na utulivu. Ethan

Lowe, hatimaye uligundua jinsi ya kufanya kitu kizuri.” Pamela akacheka.
Uso wa Ethan ulipooza kidogo kwa maneno hayo lakini alihuzunika alipofikiria mambo ya nyuma. “Hapo zamani, nilitapeliwa na Lina. Hata hivyo, mmemwona Lina hivi karibuni?"
Moyo wa Lisa yalizama baada ya kutajwa kwa mtu huyo. "Miaka mitatu iliyopita, alikuwa Nairobi baada ya kufanyiwa upasuaji wa plastiki ili kubadilisha sura yake ili kupata mwonekano mpya, na akatoweka baada ya kugundulika. Siku zote nilihisi kwamba kulikuwa na mtu mwenye nguvu sana anayemsaidia kutoka nyuma yake.”
Ethan alionyesha kutoridhika na maneno yake. "Natumai hataonekana tena."

“Naam, ndiyo.” Pamela alidakia. “Sarah peke yake anatosha kutuumiza kichwa. Itakuwa shida ikiwa Lina atatokea pia."
Lisa alikunja uso. Siku zote alifikiri kwamba Lina alikuwa mjanja zaidi kuliko Sarah, na alikuwa na hisia kwamba bila shaka Lina angetokea tena.
“Lisa, hii ndiyo namba ya mawasiliano yangu. Katika siku zijazo, tutakuwa jamaa tuliounganishwa kwa ndoa ya mjomba.” Ethan alimkabidhi kadi ya biashara kwa uchungu. "Nilifanya makosa hapo awali na niliyarudia kila wakati na kukuumiza. Katika siku zijazo, ikiwa Mjomba atakuonea, au ikiwa mama yangu anakukashifu, unaweza kuja kwangu wakati wowote. Hata kama sina uwezo, nitakuwa ndugu yako kila wakati. Zaidi ya hayo, nitakuja Nairobi baada ya siku chache.”
Lisa alipigwa na butwaa. Je! Kampuni

ya Lowe itapanuka hadi Kenya?"
“Hapana, niliachana Lowe Enterprises?” Ethan alisema huku akitikisa kichwa. "Nilijiunga na kampuni ya mjomba, Golden Corporation Kwa sasa inapanuka na tayari ndiyo kampuni inayoongoza ya dawa, kwa hivyo mama yangu aliniambia nitengeneze kampuni hiyo na Mjomba katika siku zijazo."
"Kila la kheri." Lisa alichukua kadi ya biashara.
Baada ya Ethan kuondoka, Pamela alitikisa kichwa chake. “Kabla ya hili, ulitaka kuwa shangazi yake. Sasa, si wewe ni shangazi yake, hata anafanya kazi kwa ajili ya mumeo.”
"Sahau. Imekuwa miaka mingi sana. Haijalishi tena.” Lisa alitabasamu kwa unyonge.

Baadaye kidogo, sherehe ya harusi ilianza. Wakati wa matembezi ya kujongea, Joel alimshika mkono Lisa na kumsogelea Kelvin taratibu. Nyuma yao, Suzie na Lucas wakarusha maua kutoka kwenye kikapu. Ingawa harusi ilikuwa ndogo, ilikuwa ya kifahari na ya gharama, na kila ua lililorushwa lilinunuliwa kutoka nje ya nchi.
Harufu ya maua ilijaza chumba. Lisa alimtazama Kelvin mbele yake. Akiwa amevalia suti nyeupe, alionekana mzuri na mpole kama mwana mfalme. Hapo awali, alifikiria juu ya harusi ya kimapenzi na Alvin, lakini mtu huyo alishindwa mara kwa mara. Katika maisha haya, kuna mtu hatimaye alimpa harusi nzuri. Alijisikia furaha kweli.
"Kelvin, mtunze binti yangu vizuri siku zijazo." Joel akamkabidhi Kelvin mkono wake.

“Nitafanya, Baba.” Kelvin aliushika mkono wa Lisa.
Punde, Padri alianza ibada ya ndoa. "Bwana. Kelvin Mushi, je, unamchukua Lisa Jones kuwa mke wako, katika hali nzuri au mbaya zaidi, katika ugonjwa na afya, wakati wa furaha na wakati wa huzuni, kumpenda bila kipingamizi na kuwa mwaminifu kwake milele?”
Kelvin alisema kwa upendo, "Ndiyo, nakubali."
Padri akatabasamu na kumgeukia Lisa. “Bi. Lisa Jones, je, unamchukulia Kelvin Mushi kuwa mume wako, katika hali nzuri au mbaya zaidi, katika ugonjwa na afya, nyakati za furaha na huzuni, kumpenda bila kipingamizi na kuwa mwaminifu kwake milele?”
Lisa alitikisa kichwa na kunong'ona, "Ndiyo, nakubali."

Padri akasema, “Kisha, tafadhali badilishaneni pete zenu, na bwana arusi anaweza kumbusu bibi arusi.”
Baada ya wanandoa kubadilishana pete zao za harusi, Kelvin alibusu midomo ya Lisa kwa upole kupitia pazia la shela. Wakati huo, waandishi wa habari mara moja walichukua picha.
Sura ya: 485
Suzie aliuma midomo yake na hakuweza kujizuia kulia. Lucas alimtazama, na uso wake wa baridi ulionyesha ulaini adimu. "Nini tatizo? Huwezi kuvumilia kumuacha mama aolewe? Usijali, mama bado atatupenda kama zamani.”
“Usinidanganye. Mama na Anko Kelvin hakika watatuletea wadogo zetu katika siku zijazo. Mama hatatupenda sana

wakati huo.”
Suzie alifuta machozi na kunung'unika kwa sauti ya chini, akijisikia vibaya sana.
Ingawa Kelvin alikuwa mzuri sana kwake, hakuwa Baba yake halisi.
Yote hayo yalikuwa makosa ya baba yake. Kwanini alikuwa mjinga sana? Tayari alimuashiria, lakini bado alikuwa hajafika.
Sasa, mama yake alikuwa tayari ameolewa. Ilibidi akubali ukweli.
“Hilo halitaftokea.” Lucas aliminya midomo yake myembamba na kumshika mkono wake mdogo. “Mama si mtu wa aina hiyo na utakuwa dada yangu mdogo sikuzote nitakunza."
“Lucas...” Suzie alilia tena. Baada ya kuishi kwa miaka mitatu, hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Lucas kusema maneno ya joto kama hayo.

Baada ya sherehe hiyo, wanahabari walichapisha picha hizo nzuri za harusi mtandaoni. Kelvin naye alimshika mkono Lisa na kupiga picha wakiwa wamevalia pete zao za ndoa, na kuiweka kwenye Facebook.
[Kushika mkono wako, mpaka kifo kitakapotutenganisha. Nimekuwa nikikusubiri tangu siku ya kwanza nilipokutana nawe. Siku 1257. Ninafurahi kwamba sikukata tamaa.]
Kama bosi wa Golden Corporation, mara chache alichapisha mambo yake kwenye mitandao ya kijamii. Siku zote amekuwa mtu wa faragha machoni pa umma, kwa hivyo chapisho hili adimu lilizua hisia.
[Oh Mungu wangu, Bwana Mushi! Sijawahi kumwona kabisa akitupia vitu

mtandaoni, leo ni ajabu, inaonekana kweli amefurahi!]
[Mke wa Bwana Mushi lazima atakuwa na bahati ya upendeleo katika maisha haya. Amebarikiwa sana. Bwana Mushi ni kiongozi wa biashara ambaye ni mzuri na tajiri na wa chinichini. Wanaume kama yeye ni vigumu kuwapata.]
[Je, hujui bado? Vyombo vya habari tayari vilitoa picha za bibi harusi hapo awali. Bibi harusi wa Kelvin Mushi ni Lisa Jones.]
[Lisa Jones? Hiyo haiwezi kuwa.]
[Ni yeye, mke wa zamani wa Alvin Kimaro na mpenzi wake wa zamani.]
[Kelvin alimalizana vipi na Lisa? Mbona wamefunga ndoa kwa ghafla?]

[Hakika ni kweli. Waandishi wengi tayari walichukua picha kwenye harusi. Lisa ni kweli mshindi katika maisha. Alvin Kimaro alimfanyia ujinga, lakini aligeuka na kuolewa na tajiri mwingine mkubwa, mfanyabiashara wa dawa za binadamu. Inashangaza.]
[Ni ajabu gani kuhusu hilo? Lisa ni mrembo na mwenye kipaji. Nani hataki kumuoa? Anastahili kupendwa.]
[Si ajabu Kelvin hajawahi kuwa na kashfa na wanawake hapo awali, na sijawahi kusikia kuwa ana mpenzi. Kwa hivyo ni kwa sababu amekuwa akimngojea mtu ambaye amekuwa akikaa moyoni mwake. Wanaume wazuri kama yeye ni wachache.]
[Lisa anaweza kuwa aliumizwa sana na Alvin na akageuka na kuona kwamba Kelvin amekuwa akimngoja kimyakimya kila wakati.

Lazima hatimaye aliguswa.]
[Nashangaa kama Alvin Kimaro anajua kuhusu jambo hili. Hata alichapisha kwenye Facebook kwamba atamsubiri Lisa maisha yake yote.]
[Pengine amejificha kwenye kona na analia sasa hivi. Ni kosa lake kwa kutojua jinsi ya kumtunza.]
Majadiliano motomoto kati ya wanamtandao yalisukuma papo hapo sherehe hii ndogo ya harusi hadi kilele cha habari zinazovuma.
•••
Katika helkopta kibinafsi.
Alvin aliendelea kuangalia muda kwenye simu yake. Ilikuwa tayari saa sita mchana Moyo wake ulionekana kushikwa muda wote, ikabidi ashushe pumzi ndefu kila mara. Aliendelea kujipa

moyo kuwa ni mawazo yake tu. Lisa angeolewa vipi na Kelvin? Hawakuwa wameonana tangu miaka mitatu iliyopita, na tangu Lisa arudi, hakuwahi kuwaona pamoja hapo awali. Ilikuwa haiwezekani wao kuoana ghafla.
Alichukua funda kubwa la maji, na kugundua kuwa mkono wake ulikuwa ukitetemeka vibaya.
Chester alimpigia simu ghafla, akajibu kwa hasira.
"Ikiwa una jambo la kusema basi liteme haraka."
"...Uko wapi sasa?" Chester aliuliza baada ya kimya cha muda.
"Kwenye helkopta kwenda Dar." Chester akahema. “Bado hujasikia?” "Nimesikia kuhusu nini?" Moyo wa Alvin

uligonga kwa hofu na sauti ya Chester.
Ndiyo, aliogopa. Ilikuwa ni mara ya pili akipata tena aina hiyo ya hofu. Mara ya kwanza ni pale alipomsukuma chini Lisa ambaye wakati huo alikuwa mjamzito. Ni uoga uleule alioupata alipompeleka hospitali.
Ni kana kwamba alikuwa akipoteza polepole kitu cha thamani kwake.
"Lisa na Kelvin walifunga ndoa huko Dar es Salaam," Chester alisema kwa unyonge. “Harusi imekamilika. Kelvin tayari amekiri hadharani na waandishi tayari wamepiga picha za tukio hilo. Ikiwa huniamini, tafuta tu habari zinazovuma sasa hivi mitandaoni. Kila mtu tayari anajua."
Alvin akasugua kichwa chake na kucheka kwa uchungu. “Unanidanganya. Leo ni Aprili Fools, sivyo?"

"Hapana, Alvin. Lisa aliolewa kweli. Nenda kwenye hisi zako na urudi. Mimi na Rodney tutakunywa pamoja sasa hivi, tunahudhunika pamoja nawe.”
"Nyamaza. Hawezi kuolewa. Haijafika hata saa sita sasa.” Alipiga kelele, akikataa kuamini ukweli.
"Hakuna mtu anayesema kwamba ndoa lazima iwe baada yas saa sita." Chester alimkumbusha. "Tulia. Ni wewe mwenyewe ulilazimisha talaka na kuachana na Lisa hapo awali. Kwa kweli, makosa yote ni ya kwako...”
“Bam.” Alvin akakata simu.
Bado alimpenda Lisa na hakuwa na hamu ya kusikia kuwa ameolewa. Ingawa upendo huu ulikuja kwa kuchelewa sana na ghafla, alimpenda tu. Alitaka kupata watoto naye. Alitaka

kuwa naye maisha yake yote. Ndiyo, aliwahi kumuumiza, lakini alijuta. Tangu waachane tena, yote aliyofanya ni kujuta tu. Hakuweza hata kulala usiku kwa sababu ya majuto yake. Kichwa chake kilikuwa kitupu kwa muda mrefu hadi hatimaye akawasha simu yake na kugusa habari hiyo.
Hakuhitaji kutafuta hata kidogo. Habari za harusi ya Lisa na Kelvin zilijadiliwa na watumiaji wa mtandao kote nchini. Mtandao ulikuwa umejaa picha za harusi yao. Alivaa mavazi ya meupe ya harusi na tabasamu tamu. Alijua kwamba alikuwa mrembo, lakini hakutarajia kwamba angekuwa mrembo zaidi katika vazi la harusi.
Akasogea chini. Kulikuwa na picha za Kelvin na Lisa wakibadilishana pete zake za harusi, na picha za Kelvin akimbusu.
Kila picha ilikuwa kama kisu moyoni

mwake. Maumivu yake yalikuwa yanashindikana. Mwili wake mzima uliganda na macho yake yakibubujikwa na machozi yasiyozuilika. Angewezaje kufanya hivyo? Walikuwa wameachana kwa siku chache tu, lakini aliolewa na mtu mwingine kwa kufumba na kufumbua? Alijua alikuwa katika makosa, lakini kwanini hakumpa nafasi? Macho yake yakawa mekundu ghafla, kama mnyama anayekaribia kupoteza udhibiti.
Hapana. Hapana, alikuwa mwanamke wake. Asingemruhusu kamwe awe mali ya mtu mwingine. Kwa hivyo ikiwa alikuwa ameolewa? Asingeweza kukubali. Lisa angeweza tu kuwa wake. Angemfanya yeyote aliyethubutu kumchukua kutoka kwake aishi maisha mabaya zaidi kuliko kifo.
Alitazama juu kwa kasi na kumfokea rubani. "Tutafika Dar es Salaam lini?"

Hakuweza tena kusubiri.
“T... Dakika kumi.” Nahodha alitetemeka kwa hofu kwa kuangalia kwake.
“Nipeleke hotelini kwa mwendo wa kasi zaidi.” Kisha akapiga namba ya Ganja. "Mtaarifu kila mtu wa ONA anayepatikana Dar es Salaam haraka iwezekanavyo."
Kwa hivyo ikiwa Lisa alikuwa ameolewa? Kwa vile alikuwa amemfuata, angemchukua hata iweje.
TUKUTANE KURASA 486-490
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (10) SIMULIZI...........................LISA
KURASA.....................486- 490
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 486
Kwenye karamu ya harusi.
Lisa alibadilisha shela lake na kuvaa gauni jekundu. Nguo hiyo ilisisitiza mikunjo yote yote ya mwili wake na mkufu mzuri wa almasi ulipamba shingo yake. Hakukuwa na shaka kwamba kama bibi-arusi siku hiyo, alikuwa mzuri zaidi kuliko wote.
“Anko, Aunty. Hongereni sana.” Katika meza nyingine ya marafiki na familia, Ethan aliinua toast na hisia mchanganyiko.
"Asante." Lisa alikuwa anakaribia kunywa pale Kelvin alipomkumbusha kwa upole. “Usinywe sana. Kunywa kidogo ni sawa."

"Wow, bwana harusi anamjali sana bibi arusi." Mtu fulani kutoka kwa familia ya Mushi alipiga kelele kwa tabasamu. "Bibi arusi anaweza kunywa kidogo, lakini bwana harusi lazima anywe glasi tatu."
"Anko, usimpe Kelvin wakati mgumu." Lisa alitabasamu kinyonge. "Tuna safari ya ndege ya alasiri kwa ajili ya fungate baadaye alasiri hii."
“Kelvin, angalia jinsi bibi arusi wako anavyokuwasha, Je, hatupaswi kunywa zaidi?” Mwanaume huyo hakurudi nyuma badala yake alizidi kuwa mkali. “Sawa.” Kelvin alimtazama Lisa kwa upendo. "Usijali, naweza kushikilia kinywaji changu, nitakuwa sawa."
“Lakini...”
“Tayari nina furaha sana kwamba unanijali sana. ” Kelvin alifurahi kutoka

ndani ya moyo wake.
Lisa alimtazama akitabasamu kama mtoto, na moyo wake ulijaa maumivu kidogo. Aliapa kwamba angemtendea vyema katika maisha yake yote.
Wakati huo, sauti nzito ya ghafla ilisikika kutoka nje. Mtu fulani akapiga kelele, “Ni nani? Kwa kweli walirusha helikopta hapa."
"Lazima atakuwa ni mtu mkubwa."
Sura ya Lisa ilibadilika kidogo. Alikumbuka kwamba Alvin alikuwa na helkopta binafsi, na Hans alisema kwamba alitarajiwa kufika wakati huo. Cha ajabu bado alikuwa na ujasiri wa kuja hata baada ya habari za harusi yake kujulikana na kila mtu.
Kelvin pia aliliona hilo na bila fahamu akamshika mkono wake. “Usijali,

nilipanga watu walinde nje. Dar es Salaam ni jiji letu. Siamini kuwa Alvin atathubutu kuiba mke wa mtu mbele ya watu wengine wote.”
Midomo myembamba ya Lisa ilitetemeka. Ingewa ni mtu mwingine, asingekuwa na wasiwasi, lakini Alvin hakuwa mtu wa kawaida. Alikuwa kichaa. Hakuna aliyejua angefanya nini.
"Kelvin, nadhani afadhali tuondoke kwanza." Alisema kwa wasiwasi.
“Sawa.” Kelvin alikunja uso. Haukuwa wakati wa kushindana nguvu na Alvin bado.
Hata hivyo, alipoushika mkono wa Lisa na kutaka kuondoka, mtu mmoja mrefu na mkubwa akaingia kutoka kwenye lango kuu la kuingilia ukumbi wa

karamu. Mwanaume huyo alikuwa na sura nzuri isiyo na kifani, na hata ikiwa alikuwa amevaa shati jeusi la kawaida, sura yake isiyo na kifani na ya kiungwana ilitosha kuwatetemesha watu waliokuwapo.
Upepo ulipeperusha shati lake, na wakati huo, kishindo cha mtu huyo kilikuwa kama pepo kutoka kuzimu. Macho yake yalikuwa mekundu na ya damu, na hata uso wake mzuri ulijaa hasira mbaya. Kila mtu akavuta pumzi ya hofu. Uadui uliotoka kwa kijana huyo ulijaza jumba hilo kwa hofu kubwa.
Jack alipiga paji la uso wake. Ilionekana hakuna jinsi mlo huu ungeweza kuendelea kwa amani tena.
“Anko...” Suzie alisimama kwa furaha, lakini nuru machoni mwake ikatoweka haraka. Hata hivyo hakuwa na cha

kufanya. Baba yake mchafu alikuwa amechelewa sana. Kelvin na Mama yake walikuwa tayari wameoana.
“Alvin Kimaro...” Ethan alikunja uso na kufichua utambulisho wa mtu huyo.
Umati ulikuwa katika ghasia. Alikuwa ni yeye? Mtu mashuhuri zaidi, tajiri mkuu nchini Kenya, Alvin Kimaro?
“Mamaaa, huyo ndo Alvin Kimaro? Yeye ni mzuri sana. Yeye ni mtanashati kuliko picha za mtandaoni.”
"Nilidhani kwamba Kelvin alikuwa mzuri, lakini ikilinganishwa na Alvin, Alvin ni mzuri zaidi."
“Kwa kweli Lisa ana bahati ya kuoendwa na vijana wazuri.”
Kundi la mabinti lilipiga soga, na uso mzuri wa Kelvin haukuweza kujizuia

kuzama. Kwa silika alisimama mbele ya Lisa.
Alvin alimtazama Lisa kwenye umati wa watu. Alijitokeza kwa urahisi katika umati akiwa na gauni jekundu lililomfanya aonekane wa kupendeza. Huyo alikuwa ni mwanamke wake!
Hata hivyo, wakati huo, Kelvin alikuwa amemshika mkono, naye akajificha nyuma ya Kelvin kama mwanamke mdogo.
Hofu na hofu ikatanda.
Kwa hatua kubwa, Alvin alielekea
kwao.
Uso wake wenye huzuni ulikuwa kama
na mishale ya moto machoni pake, na hakuna mtu ambaye angefikiri kwamba amekuja kuwapongeza.
“Bwana Kimaro, ikiwa upo hapa kwa ajili ya kutupongeza, basi nakukaribisha, lakini ikiwa upo hapa kuharibu harusi

naweza kukuambia kuwa umechelewa. Lisa sasa ni mke wangu.” Kelvin alimtazama Alvin kwa umakini. “Tafadhali acha kumsumbua mke wangu.”
“Mke wako?” Alvin aliachia kicheko cha chinichini, lakini kicheko kilikuwa cha ukiwa na cha kusikitisha.
Wakati fulani, kweli alikuwa ni mke wake. Yeye ndiye ambaye alimlazimisha kutia sahihi hati za talaka. Ikiwa tu kulikuwa na mashine ya kurudisha nyuma wakati, ikiwa tu kungekuwa na dawa ya majuto,
alitamani kurudi nyuma na kurekebisha makosa yake ya zamani. Je, alipoteza mwanamke wa aina gani kwa sababu ya Sarah Njau? Ilimuuma sana hata akatamani kufa.
“Ni sherehe ya harusi tu. Mmejiandikisha?" Akadhihaki.

Kelvin alimuangalia bila kubadilika hata kidogo. "Tayari. Tulijiandikisha jana saa sita mchana. Alvin Kimaro, mimi ni tofauti na wewe. Nikitaka kuoa mwanamke, nitasajili ndoa, na pia nitampa harusi. "
Mwale wa mwisho wa matumaini machoni mwa Alvin uliangamizwa kabisa. Ilionekana kuwa kuna kitu kisichoweza kuvumilika kikija kooni mwake, na karibu hakuweza kusimama wima. Hakutarajia kwamba baada ya siku chache tu, tayari Lisa alikuwa amesajili ndoa yake na mwanamume mwingine.
Alvin alitazama ukumbi wa harusi. Joel, Suzie, Jack, na wengine wote walijua. Ni yeye tu aliyewekwa gizani.
"Alvin, nenda." Lisa aliutazama uso wake wenye huzuni na kukunja uso. “Nimeweka wazi kati yangu na wewe.

Tulimalizana muda mrefu uliopita.”
"Tulimalizana muda mrefu uliopita?" Alvin alitoa kicheko cha chinichini hadi machozi yakamtoka. "Nakumbuka ni siku chache tu zimepita nililala na wewe kitanda kimoja, sasa tumemalizana vipi muda mrefu?”
Sauti yake ilikuwa ya juu sana, wageni wakaanza kuzungumza, wakimtazama Lisa kwa macho yaliyojaa dharau.
Wazazi wa Kelvin walikasirika sana na nyuso zao zilibadilika. Baada ya yote, mtoto wao alimpenda mwanamke huyo.
Macho ya Lisa yalikuwa yamejaa hasira. “Ndiyo, nilikuwa na wewe. Lakini nilipokuwa na wewe, sikuwahi kufanya chochote na Kelvin. Nimeona tu na Kelvin baada ya kuachana na wewe kabisa.”
"Alvin Kimaro, hauitaji kuleta shida."

Kelvin alimshika bega Lisa huku macho yakiwa yamezama. “Nimeshajua kuhusu wewe na Lisa. Bila shaka, sina budi kukushukuru. Kama usingefanya vile, Lisa asingenikubali haraka hivyo.”
Alvin alichomwa kisu kikali tena. Hiyo ilimaanisha nini? Alikuwa amemuumiza kwa kumsaidia Sarah, hivyo akakata tamaa kabisa juu yakena kuwaza kuwa Kelvin alikuwa bora zaidi yake?
Sura ya: 487
Kila mtu kwenye harusi alikuwa akimwangalia Alvin. Alikuwa mtu mashuhuri zaidi miongoni mwa wafanyabiashara wa Afrika, lakini wakati huo, alionekana mnyonge kama mvulana mdogo aliyepoteza mpenzi. Uso wake ulitoa ishara ya kutokuwa na uhakika na kutokuwa na msaada.
Hata hivyo, muda mfupi baadaye,

alicheka kwa uchungu. Kilikuwa ni kicheko cha kijeuri, cha kutisha, na cha kibabe.
“Kelvin Mushi, si unajua mimi ni mtu wa aina gani? Yeye ni mwanamke wangu. Yeye ni wangu kwa maisha. Basi vipi ikiwa ameolewa? Ni kipande cha karatasi tu.” Alvin alisogea mbele kwa ukaidi, uso wake mzuri ukiwa umeandikwa hatari.
Kelvin na Lisa waliogopa sana. Walionekana kudharau unyonge wa Alvin.
"Alvin Kimaro, ondoka. Niliacha kukupenda zamani.” Lisa hakuweza kujizuia kupiga kelele. Alikuwa amemwambia hivyo mara nyingi tayari.
"Haijalishi maadamu ninakupenda." Alvin alinyoosha mkono kumshika mkono, lakini Kelvin alimpiga ngumi mara moja.

Baada ya kubadilishana ngumi chache, Alvin hakuwa katika hali ya kuweza kupigana kutokana na operesheni ya utumbo, hivyo akamsakizia Master Ganja. Kelvin alikuwa katika hali mbaya baada ya kukabiliana na Master Ganja kwa muda mfupi tu.
“Anko, nitakusaidia.” Ethan aliruka juu mara moja, na wanaume wengine kutoka kwa familia ya Mushi pia walikusanyika haraka kumsaidia.
Master Ganja aliwashusha wote na walikuwa wakijikunja kwa maumivu na hawakuweza kunyanyuka.
“Walinzi!” Kelvin alijishika kifua na kupiga kelele hadi nje ya ukumbi huku akihangaika kuinuka.
Wito wake wa kuomba msaada ukaanguka kwenye masikio ya viziwi. Watu walioingia walikuwa kundi la watu

wasiojulikana.
"Bwana kubwa, watu wote nje wamesafishwa." Yule mtu anayeongoza wenzake kutoka ONA waliokusanywa kutoka Dar es Salaam alimwambia Alvin kwa heshima.
"Kazi nzuri." Alvin aliitikia kwa kichwa kushukuru.
Lisa alimtazama Alvin kana kwamba ni shetani. Joel hakuweza kujizuia na kuonya kwa hasira, “Alvin Kimaro, inatosha. Ndio, kwa uwezo wako, unaweza kumchukua Lisa, lakini umefikiria juu ya sifa ya familia yako na KIM International? Majina yao yataharibiwa. Unaiba mke wa mtu mbele ya waandishi wa habari? Tabia yako imekithiri sana. Habari zikienea, familia yako na wewe mwenyewe mtachukiwa na watu wote.”
"Ndio, Alvin, acha, tayari Lisa

ameshaolewa." Jack naye alisimama kwa haraka ili kumkatisha tamaa. "Babu na Bibi watazimia kwa hasira."
'Nimesema hivi kabla. Hakuna anayeweza kunizuia leo. ” Hakukuwa na chembe ya utani machoni pa Alvin. Alimtazama Lisa tu.
Lisa alimtazama na kukimbia kuelekea mlango wa nyuma. Hata hivyo, alikuwa amevaa gauni na viatu virefu, na Alvin akamshika haraka. Akamtoa nje na kumnyanyua.
“Lisa...” Kelvin alikimbia haraka, lakini mwanachama wa ONA alimzuia na kuanza kupigana naye.
Alipowapita wazazi wa Kelvin, Alvin alitoa onyo la kutisha. "Iwapo yeyote kati yenu atathubutu kupiga simu polisi kuhusu suala hili, nitaifanya Golden Corporation, kampuni kuu ya dawa

nchini Kenya, kutoweka kabisa."
Baada ya onyo hilo, akambeba Lisa na kwenda moja kwa moja hadi kwenye helikopta iliyokuwa kwenye nyasi, akaingia naye ndani na kuondoka.
Wazazi wa Kelvin hawakuweza kujizuia kutetemeka wakifikiria juu ya hali ya kutisha iliyokuwa machoni mwake hapo awali.
Mzee Mushi alikosa hasira kwa Kelvin. “Nilikuambia usioe huyo mwanamke, lakini ulisisitiza. Tazama sasa. Umeoa hivi punde, lakini mkeo amechukuliwa.”
Uso mpole wa Kelvin ulipotoshwa kwa hasira. Hakutarajia kuwa Alvin angekithiri kiasi cha kumpokonya mke wake hadharani. Hiyo ilikuwa ni sawa na kukanyaga uso wake chini. Kila alipokuwa akikabiliana na Alvin, siku zote alikuwa kama sisimizi. Usiku huo, ulitakiwa kuwa usiku wa harusi

yake, lakini Lisa aliishia kuwa na Alvin.
Alipofikiria nini kinaweza kutokea kati ya wawili hao, alikasirika sana na akatamani kutapika damu.
'Alvin Kimaro, sitakuacha kamwe.' Kwa hasira akatoa simu yake.
Sonya akaikamata. “Wewe ni wazimu? Hukusikia onyo lake? Huwezi kuwaita polisi. Familia yetu ya Mushi hailingani na Alvin Kimaro.
"Ndio, huwezi kuwaita polisi." Mzee Mushi alisema kwa hasira. “Huwezi kuwa na huyo mwanamke pia. Mtaliki mara tu atakaporudi.”
“Hii ni kazi yangu. Jiepushe nayo.” Kelvin aliondoka akiwa amekunja uso.
Suzie na Lucas wakatazamana, wote wawili wakamtazama Jack kwa kukosa la kusema.

“Anko tufanye nini? Baba mchafu kwa kweli alimchukua mama yetu." Suzie alitetemeka.
“Baba mchafu alikuwa anatisha sana sasa hivi.
” Lucas pia alikuwa na wasiwasi. "Anko, mama atakuwa sawa?”
“Usijali. Alvin hataki tu mama yako awe na Kelvin.”
Ingawa ndivyo Jack alisema, moyo wake ulitetemeka. Alvin hakuwa mtu wa kawaida. Alikuwa mgonjwa wa akili. Nani alijua nini kingetokea kwa Lisa? Haikuwa kama hakuwahi kumuumiza Lisa siku za nyuma. Kwa matumaini, angeweza tu kuwatuliza watoto wale wawili wakati huo.
‘Madhara ya jambo hili ni makubwa mno. Lazima nirudi haraka kwa familia

ya Kimaro.’ Jack akajisemea. Vitendo vya Alvin vingeharibu kabisa jina la familia ya Kimaro. Katika siku zijazo, familia ya Kimaro ingedharauliwa popote walipoenda.
Wakiwa wamerudi kwenye chumba cha hoteli, Kelvin alipiga namba fulani kwa haraka. “Hamishia watu kwangu. Nataka Alvin Kimaro afe."
"Sio kwa sasa." Mtu huyo alisema kwa sauti ya chini. "Tulia. Ikiwa unataka kufikia mambo makubwa, basi unapaswa kuvumilia. Tayari umevumilia kwa miaka mingi sana. Bado kidogo tu.”
"Lakini mke wangu alichukuliwa." Kelvin aliunguruma. "Nani anajua Alvin atamfanyia nini."
"Basi, umewahi kufikiria jinsi Lisa Jones atakutazama ikiwa utapeleka watu wengi? Atakushuku, na Alvin Kimaro pia

atakuwa na shaka. Mtu huyo alisema kwa upole, "Ikiwa Lisa Jones atagundua kuwa ulikuwa injinia wa kile kilichompata Logan Law, hufikirii kwamba atakuchukia?"
Kelvin alihisi kama ndoo ya maji baridi inamwagiwa juu yake. Hakuweza kusema chochote kwa muda mrefu. Alijikaza tu kwenye simu na mishipa ilionekana ikituna juu ya mkono wake.
Mtu huyo akaendelea, “Isitoshe, si mara ya kwanza Alvin kulala naye. Vumilia tu kwa muda kidogo. Baada ya hapo, nitakuruhusu umshughulikie Alvin upendavyo. Wakati huo unakuja, unaweza kumponda mpaka kufa kama mchwa. Mfanye ateseke kama vile alivyokusababishia wewe mateso leo.” Mtu huyo kisha akakata simu.
Kelvin aliipiga chini simu hapohapo. Sawa. Angevumilia. Angevumilia kwa

mwezi mmoja zaidi. ‘Alvin Kimaro, katika mwezi mmoja, utasalimiwa na lango la kuzimu.’ Uso wake wa kikatili ulionekana kwenye kioo kilichokuwa ukutani.
Katika helikopta. Alvin kwa pupa aliutazama uso dhaifu na wenye kunga’aa wa Lisa. Alimgusa kwa upole uso wake mdogo. Alionekana mtulivu na mpole baada ya kuzirai. Laiti angekuwa hivyo milele! Kwanini maneno mengi ya kuumiza yalilazimika kutoka kinywani mwake?
“Samahani, nisamehe. Nitatumia maisha yangu yote kukufadhili.”
Alvin akaifuta lipstick kwenye midomo yake kwa nguvu. Kelvin alikuwa amembusu hivyo hapo awali, kwa hiyo alitaka kufuta alama zake zote.
Baada ya kuifuta, aliinamisha kichwa chake na kumbusu midomo yake yenye unyevu.

Lea, Mzee Kimaro, na Bibi Kimaro walibadilishana kumpigia simu lakini hakupokea. Baada ya busu refu, akapiga namba ya Hans "Ninampeleka Lisa kwenye jumba la kifahari kwenye kisiwa changu cha kibinafsi. Walete watu huko ili kupanga karamu ndogo ya harusi mara moja. Nitafanya harusi na Lisa usiku wa leo.”
Sura ya: 488
Hans alikuwa mwisho wa akili yake. Hata alikuwa na hamu kubwa ya kujiua.
Habari kwamba Alvin alimteka Lisa zilienea kote nchini. Alikuwa akipokea shutuma nzito kwenye mtandao kwa wakati huu. Wanamtandao hao walikuwa wakimzomea Alvin kwenye mtandao rasmi wa KIM International, lakini bado alisisitiza kufanya harusi.
Hans alijisikia kumkumbusha kuwa

mwanamke ambaye alitaka kumuoa tayari alikuwa ameolewa na mtu mwingine.
'Bwana Mkubwa Kimaro, je ugonjwa wako umeibuka tena?' Kwa ajili ya hadhi ya Alvin Kimaro, Hans hakuthubutu kusema hivyo. Alikubaliana na wazo la mtu huyo bila kupenda.
Saa tano baadaye.
Helikopta ilitua kwenye kisiwa cha kibinafsi kwenye bahari ya Hindi. Katikati ya kisiwa kizima kulikuwa na nyumba ya kifahari. Kwa wakati huo, watumishi katika jumba hilo walikuwa busy kupamba kwa mapambo na waridi.
Alvin alimweka Lisa kitandani kwa upole kwenye chumba cha kulala.
Nje ya dirisha kulionekana na bahari siyo na mwisho iliyoenea hadi upeo wa macho. Mahali hapo palikuwa tulivu sana hivi kwamba Alvin alikuwa na amani sana kuliko hapo awali. Aliweza

hata kumtazama Lisa kimya kama vile ni mke wake kipenzi. Hakuna mtu angefika hapo kuharibu uhusiano wao.
Macho yake yalipotua kwenye vazi la harusi la Lisa, yaliganda kwa hasira. "Butler, lete gauni jipya la arusi hapa."
Vazi jipya la harusi jeupe lililetwa haraka kwa Alvin. Yeye binafsi alibamdilishia mavazi yake.
Muda mfupi baadaye, Lisa aliketi huku akiikandamiza shingo yake iliyokuwa inamuuma. Alitazama kuzunguka chumba cha ajabu, akihisi kupigwa na butwaa.
Alipoinamisha kichwa chini, alijikuta amevaa nguo ya harusi ambayo hajawahi kuiona. Ilikuwa imepachikwa na vipande vidogo vingi vya lulu. Kwa mtazamo wa kwanza, alifikiri alikuwa amegeuka kuwa nguva.

Hata hivyo, kwanini alikuwa hapo? Mahali hapa palikuwa wapi? Alikumbuka Alvin aliingia ndani ya ukumbi wa harusi yake na Kelvin na hata kumfanya apoteze fahamu.
Uso wake ulibadilika. Alitazama nje ya dirisha na kugundua kuwa anga lilikuwa giza.
Wakati huo Alvin aliingia na trei. Alikuwa amevalia suruali nyeusi na shati jeupe na fulana nyeusi. Nywele ndefu kwenye kichwa chake zilichanwa vizuri, zikifunua paji la uso wake mkali. Alionekana mzuri na mtanashati wa kuvutia.
“Umeamka. Pata vitafunwa kidogo." Alvin kwa upole akaweka trei kwenye meza ya kando ya kitanda.
“Alvin we mwendawazimu, hapa ni wapi? ” Lisa alijitahidi kuinuka. Akiwa hana viatu, alikimbilia mlangoni bila

kujali alikuwa wapi.
Hata hivyo, kabla hajatoka nje, Alvin alimshika mkono. Alichukua jozi ya slippers safi na kuweka mbele yake. “Vaa hizi.”
"Sitavaa." Lisa akazipiga teke zile slippers.
"Usipovaa, sitakutoa nje." Alvin alimshika mkono, lakini sauti yake ilibaki laini. "Vaa, au utaumiza miguu yako."
Kwa namna fulani, kubembelezwa na Alvin ambaye siku zote alikuwa na tabia kama hii hakukumpa Lisa chochote zaidi ya hasira. Je, angewezaje kutisha wakati wa harusi mapema lakini akamtendea tofauti kabisa wakati huu? Je, alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wake tena?

Lisa alifikiri kwamba isingefaa kwake kuwa mkaidi ikiwa angetaka kukimbia baadaye. Baada ya kusitasita kwa muda, alivaa slippers. Mara Alvin akamwachia, alitoka nje kwa kasi kama mwanamke mwendawazimu.
Ilikuwa ni sehemu ya ajabu ambayo ilikuwa kubwa kama ngome. Kuta zikiwa zimepambwa kwa waridi, utepe, na maua mengine ya kuvutia, eneo hilo lilitoa hali ya furaha. Ilivyoonekana, ilikuwa ni kama harusi kubwa ilikuwa imefanywa na sasa ulikuwa wakati wa wanandoa kutumia usiku wao wa kwanza pamoja, yaani fungate.
Watumishi waliopita mbele ya Lisa walikuwa weusi na weupe. Wote walimkodolea macho na kumsalimia mara kwa mara, “Habari, Madam.” Lisa aliona inatisha, kwa hiyo alikimbia haraka zaidi.

Lakini, alipotoka nje ya jumba hilo hakuona nyumba nyingine nje. Baada ya kukimbia kwa muda mrefu, alijikuta anaingia kwenye msitu wa ajabu. Hata hivyo, alichoweza kuona baadaye ni bahari isiyo na mipaka.
Alipigwa na butwaa. Je, hakuwa Kenya au Tanzania tena? Alikuwa wapi? Pia hakuwa na simu yake. Hisia ya hofu ambayo hakuwa nayo kwa muda mrefu ikaingia akilini mwake.
Alisikia baadhi ya hatua nyuma yake. Alipogeuka, Alvin alikuwa akielekea kwake ufukweni. Macho yake yalikuwa tulivu kama anga kubwa juu yake.
Lisa alipandwa kichaa kabisa. “Alvin, wewe ni kichaa sana! Umenileta wapi huku? Unaelewa kuwa nimeolewa na Kelvin na ni kinyume cha sheria kumpokonya mke wa mtu mwingine?”
“Itachukuliwa kuwa haramu ikiwa Kelvin

atawaita polisi. Kwa vile hatapiga simu polisi, huwezi kuiita kuwa ni kinyume cha sheria.” Alvin aliingiza mikono yake kwenye mifuko ya suruali yake, midomo yake myembamba ikijipinda na kufanya tabasamu la kawaida.
Lisa alipigwa na butwaa. Je, Kelvin hakupiga simu polisi baada ya Alvin kumchukua? “Ulimtishia Kelvin tena?” Lisa aliinua kichwa chake na kumtazama kwa macho ya moto.
“Kwa kuwa alikubali kutishika, inaonyesha kwamba wewe si muhimu sana kwake.”
Alvin aliinamisha kichwa chini na kumtazama. Upepo ulikuwa umezitimuatimua nywele zake ndefu nene na zinazotiririka. Hakuweza kujizuia kunyoosha mkono wake ili kuweka nywele zake vizuri. Hata hivyo, kabla hajamgusa, Lisa aliuvuta mkono

wake.
Lisa alitoa kicheko cha dharau na kumtazama. Ni nini kingine ambacho ungeweza kutumia kumtishia kando na kampuni yake? Kama ungekuwa katika viatu vyake, usingeachana na kampuni yako pia.”
"Naelewa," Alvin akajibu bila kuchelewa. Labda asingefanya hivyo wakati huo, lakini alikuwa amekuja kutambua kwamba alikuwa mtu wa maana zaidi kwake sasa.
"Lisa, bado ninaweza kupata pesa nikipoteza, lakini itakuwa ngumu sana kupata mwanamke kama wewe baada ya kukupoteza.”
"Nyamaza." Lisa hakumuamini hata kidogo. Alianguka katika hali ya kufadhaika na akasema, “Siku zote uko hivi! Maneno yako huwa matamu sana, lakini ni nani aliyeniumiza zaidi katika

miaka michache iliyopita? Alvin Kimaro, nilimchagua Kelvin kwa sababu sitaki kuishi aina ya maisha ambayo nitawekezamatumaini kwako na bado yatavunjwa dakika inayofuata. Inachosha. Siwezi hata kuwa na imani na wewe. Hatutakuwa na furaha kwa njia hii.”
“Tutakuwa na furaha. Nitaamini chochote utakachosema kuanzia sasa." Alvin aliweka mkono wake begani kwa uchungu. "Hatimaye iliniuma sana kwamba nilipaswa kumpenda na kumvumilia mtu ninayempenda bila masharti bila kujali kama yeye ni mwovu, mbaya au mzuri."
“Ha! Umejua hili kwa muda mrefu kutoka kwa Sarah. Haijalishi ni mwovu kiasi gani, bado unampenda,” Lisa alimfokea.
"Mimi sikujua." Alvin alitoa tabasamu la

uchungu. “Nilimfahamu tangu nilipokuwa mdogo, na sikujua alipobadilika. Lisa, sina uhusiano naye tena. Nimezuia mawasiliano na namba yake ya WhatsApp. Ikiwa chochote kitamtokea kuanzia sasa, sitajisumbua tena— ”
“Inatosha. Nyamaza tu. Hatuwezi kamwe kurudiana pamoja. Kwa muda mrefu nimeacha kukupenda. Ninataka tu kuishi maisha ya kawaida na Kelvin kuanzia sasa. Tafadhali niruhusu niende.” Lisa akatikisa kichwa. “Kwa kweli sikupendi tena. Huna nafasi tena moyoni mwangu. Vinginevyo, nisingekubali kuolewa na Kelvin.”
Sura ya: 490
Saa kumi alfajiri. Dar es Salaam.
Kelvin hakuwa amelala bali amesimama kwenye kibaraza kama sanamu. Macho

yake yalikuwa mekundu yakiwa na damu kutokana na kukaa macho usiku kucha. Trei ya majivu iliyokuwa kando yake ilikuwa tayari imejaa virungu vya sigara.
Nyuma yake kulikuwa na kitanda. Ilitakiwa kuwa Lisa na yeye wawe na
usiku wao wa kwanza ndani ya chumba hicho baada ya harusi yao, lakini Alvin alikuwa amemnyakua.
Alikuwa wapi? Alikuwa anafanya nini sasa? Kelvin alifadhaika sana hata hakuweza kutuliza akili yake.
Ghafla, sauti ilisikika kutoka kwenye simu yake. Akapokea ujumbe wa ajabu.
Akabonyeza fungua na kulikuwa na video fupi. Katika video hiyo, taa hazikuwashwa lakini aliweza kuona vizuri vivuli viwili kitandani. Aliitambua sauti ya kilio iliyokuwa ya Lisa.
Ghafla, alihisi kama kifua chake

kimepasuka. Kelvin hakuwa mpumbavu. Aliweza kujua walichokuwa wakifanya. Hata hivyo, hakutaka kuamini. Aliogopa kufikiria juu yake ...
Usiku huo ulipaswa kuwa usiku wake wa kwanza na yeye. Alikuwa ameutarajia siku nyingi kwa kile kilichoonekana kama umilele.
Tangu alipokutana na Lisa huko Dar es Salaam, alikuwa amempenda. Alipokubali pendekezo lake, kwa kweli alikuwa amefurahi. Ingawa walifanya harusi ndogo tu, alikuwa ameweka juhudi nyingi katika mapambo. Hakutarajia kuwa mwanamke wake angeishia kuwa na Alvin usiku huo.
"Alvin Kimaro, nitakufanya uteseke kuzimu hivi karibuni au baadaye." Kelvin alipiga teke meza ya kahawa iliyokuwa mbele yake. Uso wake wa kifahari na mzuri uligeuka kuwa mbaya sana.

"Pia, Lisa Jones, kwanini ... kwa nini unanitendea hivi?"
Mtazamo wake ulibeba alama za hasira. Alikuwa akimwekea kinyongo, lakini upendo wake kwake ulikuwa na nguvu zaidi. Alipaswa kuwa mchumba wake miaka mitatu iliyopita. Hata hivyo, alijua kwamba alipanga tu kuolewa naye kwa sababu tu alikuwa amemuokoa.
Baada ya kurudi kutoka Marekani miaka mitatu baadaye, aligundua kwamba Lisa alitaka kumrudisha Alvin. Bado alivumilia tabia yake kwa uchungu. Baada ya yote, yeye
alikuwa hajamuahidi kuwa naye, lakini ilikuwa hadithi tofauti sasa. Kama mke wake wa ndoa, alilala mikononi mwa mwanamume mwingine usiku wa harusi yao?!
'Lisa Jones, huna aibu hata kidogo? Hata kama Alvin angekulazimisha, si ungemtishia maisha yako?' Kelvin

alikunja ngumi. Aliwachukia wote Alvin na Lisa.
Macho yake yalikuwa na hasira kali kwa muda mrefu. Mara akampigia simu sekretari wake. “Regina, umelala? Njoo chumbani kwangu sasa hivi."
“Bwana Mushi...” Regina Gwakisa alifurahi na kushangaa. Alishangaa kwanini Bwana Mushi alikuwa akimwita chumbani kwake muda huo. Haikuwezekana kwamba alitaka kuzungumza naye juu ya kazi. Alikuwa akifanya kila awezalo ili kumtongoza Kelvin, lakini siku zote alikuwa akijiweka mbali naye.
Endapo Lisa asingenyakuliwa na Alvin, Kelvin asingekuwa katika hali mbaya na kumtaka aaende chumbani kwake. Hakika, ilikuwa fursa nzuri kwa Regina kumfanya asogee kwake usiku huo.

“Sawa, Bwana Mushi. nakuja sasa hivi.”
Dakika kumi baadaye, Regina alionekana katika chumba cha Kelvin. Alikuwa kavaa tu nightdress fupi. Kwa makusudi, alifunua paja lake.
Kelvin alimwendea akiwa na uso wa huzuni na mzuri. Regina aliinua kichwa chake na kumtazama, mapigo ya moyo yakimuenda mbio sana.
Alikuwa amempenda kwa muda mrefu. Sio tu kwamba mtu huyu alikuwa mzuri na mtanashati lakini pia alikuwa kijana na mwenye uwezo. Angekuwa karibu naye angefaidika sana. Angekubali hata angeombwa afanye naye jambo la aibu.
“Bwana Mushi...” Alipepesa macho yake kwa upendo. Kabla hajapata fahamu zake, Kelvin alimvuta kwa karibu mikononi mwake na kumbusu kwa mapenzi.

Baada ya kupigwa na butwaa kwa muda, Regina alifurahi sana.
Hakutarajia hili. Kwa kweli ilikuwa zaidi ya matarajio yake.
Fungate ya Lisa usiku huo iligeuka kuwa ya kwake.
•••
Katika kisiwa.
Jua la rangi ya machungwa lilipanda polepole juu ya upeo wa macho juu ya bahari. Ilipofika saa sita mchana Lisa alifumbua macho yake ya uchovu taratibu. Alipoinuka, alikuwa peke yake kwenye kitanda kilichochafuka na maua ya rose.
Upepo wa baharini ulipovuma, mapazia kwenye madirisha yalisogea.
Macho yake yalikuwa yameduwaa. Hakuwahi kufikiria kwamba angemsaliti Kelvin japo hakupenda. Alijaribu kumpinga Alvin kwa nguvu zake zote jana usiku, lakini mtu huyo alikuwa

mkaidi na alijifanya mwendawazimu. Mwili wake ulikuwa bado unauma hata sasa.
Aliinua blanketi na kujificha chini yake. Alikuwa amejikunja ndani kama mpira. Hakuthubutu kujiwazia angekabiliana vipi na Kelvin wake mpendwa hata kama angeweza kukimbia kutoka mahali hapo. Hakustahili tena kuwa na yeye. Kwa kweli hakustahili.
Ghafla, mlango wa chumba hicho ukasukumwa. Mwanamke mwenye umri wa miaka 40 aliingia akiwa na rundo la nguo nadhifu. “Bi Mkubwa, umeamka. Hapa kuna nguo ambazo unaweza kubadilisha. Unataka kuoga—”
“Potelea mbali!” Lisa alifagia kila kitu kutoka kwenye sinia iliyokuwa kwenye meza ya kando ya kitanda kama kichaa. Alizungusha mikono yake kichwani kwa sura ya kutisha, huku nywele zake

zilizotibuka zikianguka juu ya mabega yake.
Mwanamke huyo alishtuka sana hadi akarudi nyuma na kugongana na mtu.
Alipogeuka na kuangalia, aliita kwa woga, "Bwana Mkubwa..."
"Nipe nguo na uende nje." Alvin alielekea kitandani huku akiwa ameshika nguo.
Lisa alipomwona tu, alichukua maua na kumtupia usoni. Uso wake mzuri ulikuwa mzito kwa chuki.
“Umemaliza?” Macho ya Alvin yalibaki ya upole. “Una uhakika unataka nipotee? Hutaki kuvaa nguo? Au unapanga kukaa kitandani milele?"
Baada ya kukumbushwa, Lisa aligundua kuwa alikuwa uchi. Pia, vazi la harusi alilovaa jana yake lilichanika. Ikiwa angekataa nguo hizo, asingekuwa na

chochote cha kuvaa.
"Kwa kuwa hutaki nguo, ni sawa." Alvin aliinua uso wake. Alijifanya mnyonge na akashusha pumzi. "Kwa kweli, napenda sana jinsi unavyoonekana ukiwa uchi."
Huyu mhuni mbaya...Lisa alikasirika sana hadi uso wake ukakunjamana. Alipoona kwamba angeondoka, hakuwa na la kufanya ila kusema kwa kuudhika, “Simama hapo hapo. Nipe nguo.”
“Sawa mke wangu.” Alvin alitoa tabasamu kidogo. Aligeuka na kumpitishia nguo mara moja.
“Mke wako ni nani? Umekosea. Mimi ni mke wa Kelvin.” Lisa alicheka kwa kuudhika.
Mtazamo wa upole wa Alvin uliganda kwa muda kabla haujawa laini tena. “Lisa, sina hasira. Nilikuwa nakutesa,

kwa hiyo sasa ni zamu yako kunitesa. Maadamu una furaha na unaweza kutoa hasira yako, ni sawa."
Lisa hakuweza kujizuia kuruka kwa hasira. “Sitaki kukutesa. Ninataka tu kukaa mbali kutoka kwako. Nakuchukia.”
"Ndio, unanichukia, lakini nashangaa ni nani aliyekufurahisha jana usiku?" Alvin alikodoa macho.
Uso mzuri wa Lisa ukabadilika na kuwa wa kutisha mara moja. Alitamani angemchuna usoni.
“Lisa hata ukinichukia na kutonipenda tena, mwili wako bado umenizoea.” Alvin aliinamisha kichwa chake na kumbusu kwenye midomo yake myembamba.
Lisa hakukwepa lakini alisema bila kujali, “Ni mahitaji yangu tu ya kimwili.

Nina tabia kama hii ninapokuwa na wewe. Zaidi ya hayo, nadhani huwezi kulinganishwa na Kelvin...”
"Jaribu na useme tena." Alvin akayaminya mashavu yake, macho yake yakidhihirisha hisia kali za kuudhika. Punde, uso wake ukawa mbaya.
Lisa alimuangalia kwa makusudi. “Nimekuwa naye kwenye uhusiano kwa muda sasa. Si ni kawaida tu hata tukilala pamoja kwa sasa?”
“Lisa kwanini unilazimishe kuchukia? sitaki kukuumiza.” Alvin alihisi hasira zake zikimpanda.
Jinsi Alvin alivyokuwa akifanya kwa wakati huo ilimtia hofu tena Lisa. Ghafla, alijuta kidogo. Wakati fulani alimuumiza sana hivi kwamba

alipelekwa hospitali katikati ya usiku. Tukio hilo lilikuwa bado ni ndoto mbaya
inayomsumbua.
“Alvin... Alvin Kimaro, umesema kwamba hutaniumiza tena. Je, utarudi kwenye neno lako?” Lisa alisema kwa wasiwasi, "Vema, hujawahi kutimiza ahadi yako hata hivyo."
TUKUTANE KURASA 491-495
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (10) SIMULIZI...........................LISA
KURASA.....................491- 495
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 491
Ghafla, sura ya Alvin yenye hasira iliganda kana kwamba amepooza.
Akashusha macho chini huku Lisa akimtazama kwa kejeli.
"Mimi huwa sirudi nyuma kwa neno langu." Sekunde tatu baadaye, alijiweka sawa mwili wake. Moyo wake ulijawa na taabu na uchungu.
“Lisa, usinichokoze. Ninakuchukulia kama mwanamke wangu. Ingawa nilikuwa kwenye uhusiano na Sarah, sijawahi kumgusa mwanamke mwingine isipokuwa wewe tu.”
Lisa alipigwa na butwaa kabla ya kudhihaki, “Usinidanganye kwa kunichukulia kama mjinga. Umekuwa kwenye uhusiano na Sarah kwa zaidi ya miaka kumi. Haiwezekani kwamba

hujawahi kulala naye hata kidogo. Siamini, ukizingatia kwamba wote wawili mmekuwa pamoja kwa muda mrefu.”
"Bado alikuwa mdogo wakati huo. Baadaye, nilikuwa na shughuli nyingi za kusimamia KIM International, kwa hivyo sikujihusisha na aina hiyo ya mambo kwa sababu ya ubize. Baada ya hapo, alijinga na chuokikuu huko Garisa na akapotea baada ya kutekwa na magaidi wa Al-Shabaab, sikuonana naye tena mpaka aliporudi miaka mitatu iliyopita. Amini usiamini, niimefanya mapenzi na wewe tu.” Alvin mwenyewe aliona ni muujiza pia baada ya kumaliza kuongea.
Kwa kweli, hakuwa amemwambia Lisa jambo lolote—yaani kwamba hakuwa na tamaa zozote za ngono wala msisimko alipokuwa na Sarah.
Hakuelewa hapo zamani, lakini sasa, polepole aliielewa.

Alipoendelea kumlinda Sara bila kujali mengine yote, haikumaanisha kwamba alimpenda. Alimchukulia tu kama familia yake au mwangaza pekee wa gizani. Alikuwa akiamini kwamba Sarah alikuwa mwema na wa ajabu, akisahau ukweli kwamba watu hubadilika.
Ni pale tu alipokutana na Lisa ndipo alipogundua mapenzi yasiyosahaulika ni nini. Kuwa naye kulimfanya ajisikie mtulivu sana, mtamu na mwenye furaha. Asipomuona, angemkumbuka sana. Alipokula chakula alichotengeneza, kilikuwa na ladha ya chakula kitamu zaidi duniani.
Haijalishi alikuwa katika hali gani, bado angeendelea kufikiria kwamba alikuwa mtu mzuri zaidi.
“Nguo zipo hapa. Baada ya kuvaa, nitakuandalia kifungua kinywa.” Kwa hayo, Alvin aligeuka. Akafunga

mlango na kuondoka.
Baada ya kuachana kitandani kwa muda, Lisa alijikokota nje taratibu na kuoga. Maji ya moto yalipomwagika mwilini mwake, bado hakuamini. Yeye ni mwanamke wa kwanza kwa Alvin kuwa naye? Ilikuwa haiaminiki.
Baada ya kuoga, alivaa jozi mpya ya jeans na T-shati nyeupe. Ingawa nguo hizo hazikutoka kwenye brand za kifahari, ilikuwa ya kustarehesha sana. Lakini, hakuweza kuficha alama za mabusu ya Alvin kwenye shingo yake. Baada ya kufikiria kidogo, hakujali kuhusu alama hizo kwani hakumjua mtu mwingine yeyote kwenye kisiwa hicho zaidi ya Alvin.
Katika hali ya kukata tamaa kama hii, ilibidi ajue mahali alipokuwa na kuwasiliana na mtu wa nje.
Alikuwa na aibu sana kuwasiliana na

Kelvin, kwa hiyo angeweza tu kuwasiliana na Logan na Austin. Baada ya kutoka nje ya chumba hicho, akakutana na mtumishi wa kike mweusi ambaye alikuwa akielekea kwake. Alijaribu kuazima simu kutoka kwake, lakini aligundua kuwa kulikuwa na kizuizi cha lugha kati yao. Kwa kuzingatia kwamba mtumishi huyo hakuweza kuzungumza Kiswahili wala Kiingereza, Lisa alihisi ajabu sana hivi kwamba alitumia ishara kuwasiliana.
Hatimaye mtumishi huyo alipotoa simu yake mfukoni, Lisa alipigwa na butwaa. Kulikuwa na watu ambao bado walitumia simu za zamani kama hizo? Kwenye skrini kulikuwa na maneno ambayo hajawahi kuona hapo awali. Hakuweza kuelewa chochote, na wala hakuweza kupakua programu zozote za mitandao ya kijamii alizokuwa anazifahamu. Aliuliza watumishi wengine wachache baadaye lakini yote

yalikuwa sawa.
Hatimaye alizama katika kukata tamaa.
Hii ilikuwa wapi jamani?
Baada ya kushuka ngazi kwa huzuni, Alvin alitoa kifungua kinywa nje ya jiko akiwa amevaa aproni. Alitazama kwenye kifungua kinywa. Kulikuwa na mayai yaliyokaangwa, maziwa fresh, sandwichi, juisi ya parachichi, na aina mbalimbali za matunda mapya kwenye meza.
"Ulikuwa unakamata tumbo na moyo wangu kwa kupika kwako, kwa hivyo sasa nitatumia upishi wangu kushinda moyo wako tena." Alvin aliondoa apron na kuiweka kando. Siku hiyo, alivaa fulana nyeupe iliyofanana na ya Lisa na jozi ya jeans pia.
Akiwa amepunguza kabisa nywele kichwani mwake, alionekana kama mvulana mdogo.
Lisa alishindwa cha kusema. Je,

alikuwa amevaa mavazi yanayofanana naye kwa makusudi? Ikiwa angekuwa na seti nyingine ya nguo, angevua nguo zake zote mara moja.
“Sahau kuhusu hilo. Kwa upikaji wako mbovu, siamini kwamba ulitengeneza vyakula hivi vyote wewe mwenyewe.” Lisa alikoroma.
'Kwa kweli nilifanya mwenyewe. Siku chache zilizopita, nilijifunza jinsi ya kupika kutoka kwa mpishi. Kwa vile wewe ndio ulinipikia enzi zile, nitakupikia kuanzia sasa. Ikiwa huamini, unaweza kutazama mikono yangu... ” Alvin alinyoosha vidole vyake vyote. Vidole vyake vilivyokuwa nadhifu sasa vilikuwa na makovu. Pia kulikuwa na mikunjo kwenye viganja vyake.
"Inauma." Alvin alimtazama kwa macho yake meusi. Sambamba na uso wake mzuri wa kuvutia, mwanamke yeyote

labda angeyumba kwa kumtazama. Lakini, Lisa hakuyumba hata kidogo.
“Kama mwanaume, unanung’unika kuhusu maumivu kidogo hivyo. Huna aibu? Kelvin asingefanya hivi.”
Alvin alikosa la kusema.
Hali yake nzuri iliharibiwa kabisa baada
ya kusikia neno 'Kelvin'.
Mara Lisa alianza kula kifungua kinywa bila kujisumbua kutazama sura yake ngumu. Licha ya kuwa na kinyongo dhidi yake, asingetesa tumbo lake kwa njaa. Ikiwa angepata ugonjwa wa tumbo uliosababishwa na njaa, asingeweza kufurahia chakula kitamu tena.
“Kina ladha nzuri?” Mara Alvin aliuliza huku akionekana kutarajia jibu la kupendeza.
Lisa bila huruma alitazama pembeni. "Ni

wastani tu. Sio nzuri kama upishi wa Kelvin.”
Uso wa Alvin ukatiwa karaha, na akaonya vikali, “Sitaki kusikia neno ‘Kelvin’ likitoka kinywani mwako tena. Nisemaje?”
Lisa alimdhihaki. “Kwanini? Unataka kuniumiza tena, huh? Hakika, ahadi zako ni rundo la bullsh*t."
Alvin akasaga meno. Alikuwa akitumia udhaifu wake kumshinikiza kupita kiasi.
“Sitakuumiza.” Macho yake makali kama tai yalitua mdomoni mwake. "Lakini ukiendelea kumtaja Kelvin, sina la kufanya ila kuifunga midomo yako."
Alipomaliza tu kuongea, ghafla aliuegemeza mwili wake na kumbusu midomoni akiwa bado amezama kwenye mawazo.
Akiwa amemaliza tu kunywa maziwa,

harufu hafifu ya maziwa na utamu bado ilitanda kwenye midomo yake.
Hapo awali, alitaka tu kumfanya afunge mdomo wake, lakini hakuweza kupinga kumbusu baada ya hapo.
Kwa hasira, Lisa alijaribu kumsukuma kwa nguvu, lakini hakusogea hata sentimeta moja. Kwa hasira kali, alishika uma juu ya meza na kumchoma mgongoni.
Alihisi mwili wake kutetemeka kwa muda. Baadaye, alikutana na busu la mapenzi zaidi. Busu hilo lilidumu hadi akakaribia kukosa hewa.
"Hebu tuone kama utathubutu kumtaja tena mtu huyo." Alvin aliinuka na kumkazia macho mdomo wake uliokuwa umevimba.
Lisa alijifuta mdomo kwa nguvu kabla hajamkazia macho. Lakini, hakuthubutu

kusema chochote kingine kwa kuogopa kwamba angembusu tena.
"Unaweza kula kwanza." Kwa hayo, akageuka.
Hapo ndipo Lisa alipoona dimbwi la damu nyuma ya fulana nyeupe ya Alvin karibu na bega lake.
Aliinamisha kichwa chini na kutazama kwenye uma mkononi mwake. Uma ulikuwa umetapakaa damu nyingi.
Akashtuka.
Alikuwa kichaa gani! Ingawa alikuwa amemchoma kisu mwilini, angeweza kuendelea kumbusu kwa muda mrefu. Je, maumivu hayakuwa kitu kwake?
Alvin akavua fulana yake pale juu. Alipogeuka na kujitazama kwenye kioo, aliona matundu manne nyuma ya bega lake ambapo damu ilikuwa ikitoka.

Sura ya: 492
Mtazamo wa mjakazi mkuu ulibadilika alipoingia na kifaa cha huduma ya kwanza. “Bwana Mkubwa umejeruhiwa vibaya sana. Ni lazima utafute daktari wa kitaalamu akuhudumie.”
“Ni sawa. Nipatie tu bandeji na nitajifunga jeraha langu mwenyewe.” Alvin aliongea kwa kina na kutojali.
Baada ya jeraha lake kufungwa bandeji, alishuka na kukuta Lisa hayupo tena. Baada ya kumuuliza mtumishi fulani, alipata habari kwamba alikuwa ameenda kwenye maktaba.
Alielekea kwenye maktaba na kugundua kuwa alikuwa akijaribu kuwasha kompyuta.
Lisa aliposikia nyayo zake, alimtazama kwa macho ya kusitasita.

“Usijisumbue kuiwasha. Nimeondoa nyaya zote za mtandao. ” Alvin alimsogelea kwa utulivu. "Huhitaji kuazima simu za watumishi pia. Wao hata si Wakenya wala Watanzania. Kizuizi cha lugha ni jambo moja, lakini simu zao zinaweza zitatumika tu kuwasiliana na watu kutoka nchi zao wenyewe."
"Hivii ni wapi hapa jamani?" Lisa alizama katika kukata tamaa baada ya kumsikia Alvin akijigamba kwa maneno hayo. "Alvin, ikiwa una ujasiri, unaweza kunifunga milele. Uliniondoa hadharani, kwa hivyo inachukuliwa kuwa uliniteka nyara. Baba yangu anaweza kuripoti kwa polisi na kuwaamuru wakukamate.”
“Nimezungumza na baba yako. Nilimwambia asipige simu polisi ikiwa anajali usalama wako. ” Alvin aliubembeleza uso wake kimahaba. Wale ambao hawakujua hali hiyo

wangefikiri kwamba walikuwa wanandoa wenye upendo.
“Hata hivyo, mimi ni mgonjwa wa akili. Nikikata tamaa, ninaweza kufanya jambo lolote la kichaa.”
Kwa sauti ya upole zaidi, alimwambia Lisa jinsi alivyomtishia baba yake. Alishtuka na kuutupa mkono wake.
Alvin kisha akatabasamu na kusema, “Bila shaka, siwezi kumzuia kukuona milele. Baada ya yote, baba yako bado anaweza kufanya jambo kuhusu hilo. Nilimwambia kwamba nitakuruhusu urudi mwezi mmoja baadaye ili kumfanya ajisikie vizuri. Ninataka tu kutumia muda fulani na wewe katika ulimwengu wetu mdogo na kukufanya uniangukie tena.”
“Sitamwangukia mtu aliyeniteka nyara. Endelea kuota!" Lisa alifoka kwa hasira, "Nitahakikisha kwamba tunatengana

mara tu nitakapoondoka mahali hapa."
"Una uhakika unaweza kuftengana na mimi baada ya kupata mapumziko safi kutoka kwangu?" Alvin aliuma mdomo kwa mawazo.
Lisa aliona jambo la kushangaza mwanzoni, lakini alielewa maana yake haraka na akashtuka. Kwanini angetaka kumfanya akae naye hapo kwa muda wa mwezi mmoja? Ikiwa walngelala pamoja kwa mwezi huo mmoja, angeweza kupata mimba ya mtoto wake.
“Alvin Kimaro, wewe ni mtu
mbaya sana! Ni afadhali nife kuliko kupata mimba ya mtoto wako,” alimfokea kwa hasira.
“Lisa, uliwahi kuwa na ujauzito wa watoto wangu, maana yake miili yetu bado iko sawa. Nikilala nawe kila usiku

kwa mwezi huu mmoja, kuna uwezekano kwamba utapata mimba.”
Alvin alipokuwa akiongea hayo, damu iliyokuwa ndani yake ilianza kumchemka. Watoto wao hawakufaulu kuishi wakati huo, sivyo? Lakini wakati huu, angehakikisha kwamba wangezaliwa salama.
“Suzie ni mrembo sana, sivyo? Hakika tunaweza kuzaa mtoto mzuri kama Suzie.”
"Siwezi kujisumbua kukuburudisha."
Lisa alikuwa karibu kupandisha kichaa kwa sababu yake. “Acha kuota! Hata nikipata mimba ya mtoto wako nitaitoa.”
“Ukisisitiza kutoa mimba, sitakuwa na budi ila kukuweka hapa hadi utakapojifungua mtoto wetu.” Alvin alimtazama bila kujali. "Niamini,

ninaweza kumudu kufanya hivi. Hivi karibuni, KIM International itavumbua aina mpya ya smartphone ambayo italeta mabadiliko katika soko la kimataifa wakati huu. Sio tu kwamba KIM International itaendelea kuwa kampuni bora zaidi nchini Kenya, lakini pia nitakuwa mmoja wa wajasiriamali mia moja bora ulimwenguni. Hakuna mtu katika Kenya nzima anayeweza kunizuia."
Lisa alishangaa.
Hajawahi kufikiria kuwa maendeleo ya
KIM International yangefikia kiwango hicho.
Ikiwa alichosema Alvin ni kweli, hata Rais asingeweza kumfanya chochote.
"Maadamu utazaa mtoto wetu, bila kujali ni binti au mvulana, mali zangu zote zitakuwa zao." Alvin aliukunja uso wake kwa upole. "Lisa, nilikuwa nikishughulika na maendeleo yangu ya kazi kabla ya

hii ili kufanya KIM International kupanda juu.
Lakini tangu nilipoanguka kwa ajili yako, nilitambua kwamba ni bure kabisa kupata pesa nyingi. Nataka tu kuwa na wewe. Wacha tufurahie wakati mzuri pamoja hapa katika kipindi hiki." Akambusu kwa upole kwenye midomo.
Lisa alionekana kuduwaa.
Alikuwa amemdharau Alvin. Alijuta
kurudi Kenya kwa lengo la kulipiza kisasi kwa Alvin.
Wakati huo, alikuwa amekazia akili yake kulipiza kisasi kwa Sara. Lakini, alipuuza jinsi Alvin angeweza kuwa mjanja dhidi yake.
'Kisiwa hiki ni kizuri. Acha nikupeleke nje tutembee.” Alvin aliukumbatia mwili wake uliokuwa mgumu huku akitoka nje.
Alvin alipokaribia kufika langoni, mjakazi mkuu alimsogelea akiwa na kidonge na

glasi ya maji.
'Chukua." Alvin akampa Lisa kidonge.
"Hii ni nini?" Lisa alitetemeka sana. Yeye hakuthubutu kuichukua.
“Kidonge cha kuzuia mimba,” Alvin alieleza kwa macho yaliyotkaza kidogo, “nililala nawe jana usiku, lakini ulikuwa Dar es Salaam siku chache zilizopita, kwa hivyo unaweza kuwa umefanya hivyo na Kelvin. Lazima nihakikishe kwamba hutapata mimba ya mtoto wa Kelvin.”
Lisa hakujua la kusema. Hakuwa amefanya chochote na Kelvin, lakini kidonge hicho kingeweza kumzuia kupata mimba baada ya kufanya na Alvin jana yake usiku. Kwa hivyo, alichukua kidonge bila kusita.
Baada ya kukimeza, alizama kwenye mawazo mazito. Kwa kuzingatia kwamba kuna uwezekano mkubwa

angepata mimba katika siku chache zijazo, ilimbidi afikirie njia ya kuepukana nayo.
Baada ya Lisa kuoga usiku, alijikata mguu wa nyuma kwa kitu chenye ncha kali.
Kisha, alipaka chupi yake kwa damu.
Mara tu alipomaliza kufanya hivyo, alimwambia Alvin, “Je, una pedi? Niko kwenye kipindi changu.”
"Ni bahati mbaya." Alvin aliinua kichwa chake. Ni wazi kwamba hakumwamini hata kidogo. "Unajaribu kutafuta kisingizio cha kuzuia kupata mimba, huh?"
“Sisemi uongo. Ikiwa huamini, unaweza kuangalia mwenyewe.”
Lisa alipomaliza sentensi yake, Alvin alimsukuma kitandani.
Alvin alikagua na kugundua kuwa kweli alikuwa anavuja damu.

Alikunja uso kwa huzuni, lakini uso wake ulififia muda mfupi baadaye.
Kwa kuwa alipanga kumweka hapo kwa muda wa mwezi mmoja, bado angepata hedhi. Ilikuwa haiepukiki.
“Nitamwomba mtumishi akuchukulie pedi.” Muda mfupi baadaye, mtumishi alimpitishia pedi.
Baada ya Lisa kuvaa pedi ya usafi, Alvin alimpeleka kitandani. Alikuwa amefungwa mikononi mwake usiku mzima.
Siku iliyofuata, aliamka kwa busu yake, ambayo ikawa utaratibu wa kila siku. Lisa bado alipaswa kuwa mwangalifu sana. Kila siku, alikamua damu kutoka kwenye jeraha lake na kuchafua pedi kwa damu. Alikuwa na wasiwasi kwamba mtumishi aliyetoa takataka angeona jambo lisilo la kawaida.

Siku ya saba. Alvin alichukua bikini na kwenda kwa Lisa. “Babe, hedhi yako imeisha sasa. Nitakupeleka ufukweni ili uende kuogelea leo.”
Lisa alitazama bikini ya waridi, ambayo ilikuwa nzuri na ya kuvutia.
Ikiwa angeivaa, Alvin bila shaka angeona jeraha kwenye mguu wake wa nyuma. Alikuwa na hisia kwamba hakika Alvin angelala naye usiku huo. Kwa hivyo, ilimbidi kuficha jeraha haraka au angemshuku.
"Hapana, sipendi kuogelea." Akatazama pembeni. "Nenda mwenyewe kama unataka lakini mimi sitajiunga."
“Kama hauogelei, kuna faida gani mimi kuogelea peke yangu? ” Alvin alimkumbatia na kumweka kwenye mapaja yake.
Lisa hakumpinga. Baada ya yote,

haijalishi alijaribu sana kumpinga katika kipindi hicho, hakuwa na nguvu kama yeye. Kadiri muda ulivyopita, hakuweza kuhangaika kupoteza nguvu zake tena.
“Sawa basi. Nitatembea kando ya bahari pamoja nawe.” Alimfariji kwa upole. Akiwa amepigwa na wazo, Lisa alitikisa kichwa muda mfupi baadaye.
"Sawa, lakini nataka kupanda juu na kuvaa nguo ndefu."
Sura ya: 493
Baada ya kusikia haya, uso mzuri wa Alvin ukawa mpole.
Wiki nzima iliyopita, Lisa kila wakati alionekana kutojali na mwenye chuki bila kujali jinsi alivyojaribu kumfurahisha. Sasa, alikuwa tayari kubadili nguo na kutembea kando ya bahari pamoja naye. Je, hilo lilimaanisha kwamba polepole alikubali hali halisi?

"Endelea." Baada ya kumsihi kirahisi, ghafla alijuta kumletea nguo chache. Alimpigia Hans mara moja. "Chagua nguo nyingi zaidi za Lisa na uzitume hapa. Nataka zile zinazofaa kuvaliwa ufukweni na saizi ya mke wangu.”
Pembe za mdomo wa Hans zilitetemeka. 'Mke wako? Huna aibu? Kweli yeye ni mke wa Kelvin.' Aliwaza tu lakini maneno hayo bila shaka yasingejaribu kuvuka kinywa chake, vinginevyo...
"Bwana Mkubwa, tafadhali rudi ofisini ikiwa unapatikana." Hans aliongea kwa msisitizo, "Hivi karibuni, KIM International imekuwa ikipokea shutuma nyingi. Mzee Kimaro na Bibi Kimaro wamekasirika sana hivi kwamba wanakaribia kuugua. Na wanahisa wa kampuni huja ofisini kila siku kunitafuta. Umma umekuwa ukitushambulia, na bei

za hisa za KIM International zinaendelea kushuka.”
"Je, si kawaida kwa bei ya hisa kupanda na kushuka?" Alvin alijibu kwa njia nyepesi, “Mwambie Chester atoe habari kuhusu kashfa za maadili ya baadhi ya watu mashuhuri. Kila mtu atasahau polepole kuhusu tukio hili."
Hans alikosa la kusema. 'Je, si unamweka Chester katika hali ngumu kwa kufanya hivi? Katika suala la kuzorota kwa maadili, hakuna mtu anayeweza kukushinda.' Hayo maneno pia yalibaki kwenye mawazo ya Hans, yangemponyoka mdomoni bila shaka matokeo yake yangekuwa hayaelezeki.
"Kuhusu Mzee Kimaro na Bibi Kimaro, wakiuliza kunihusu, waambie tu kwamba ninasaidia familia ya Kimaro kuzalisha wajukuu. Waambie wasiwe na wasiwasi juu yangu. Wanahisa hao

hawatasumbuka juu ya kampuni mradi tu wanapata pesa za kutosha za kutumia. Mimi ndiye mfanya maamuzi wa KIM International. Yeyote ambaye hafurahii uamuzi niliofanya anaweza kupotea.” Alvin alipomaliza kuongea tu, akakata simu.
Aliinua kichwa chake baada ya kumuona Lisa akishuka kwenye ngazi akiwa amevalia gauni refu jekundu lililokuwa na mchoro wa alama za kizamani. Licha ya kuwa hakuwa amejipodoa, alionekana kama mrembo mwenye sura nzuri na ngozi yenye kuwaka.
Alvin akaenda mbele. Kisha, akafunga mikono yake kiunoni mwake na kumkumbatia. Kwa sauti ya kicheko, alisema, "Unaonekana mrembo."
Lisa aliweza kuhisi mara moja mabadiliko ndani yake. Mwili wake

ulipozidi kuwa na msisimko, alijiuliza sana ikiwa mtu huyu alikuwa kweli kazaliwa na binadamua alikuwa tolewa kutoka kwa mnyama wa porini. Kwanini badiliko kama hilo ndani yake lilitokea wakati alikuwa amebadilika tu kwa mavazi, je angekuwa mtupu muda huo ingekuaje?
"Inaonekana hutawahi kuwa na ngozi mbaya hata utajiweka kwenye jua vipi." Alvin alimpigapiga mabega yake. Mara chache walitoka nje kwa siku chache zilizopita, na jua kali kando ya bahari lilikuwa limechoma sana ngozi yake. Lakini, bado alikuwa mng’avu kama hapo awali.
Lisa alitazama chini na kumpuuza. Alvin hakujali. Alitoka nje ya nyumba ya kifahari huku mikono yake ikiwa imezunguka kiunoni mwake.
Pwani ya bahari ilikuwa safi sana. Lisa aliinua kichwa chake na kutazama kwa

mbali. Laiti Alvin asingemleta hapo kwa njia ya mateka, angefikiri kwamba eneo hili lilikuwa kivutio cha ajabu cha watalii.
“Nimechoka." Baada ya kutembea kwa muda, Lisa alikaa chini ya mnazi ufukweni. "Ninakiu. Nataka kunywa maji ya madafu.”
“Sawa.” Alvin alifurahi sana kwamba alikuwa akitoa ombi kwa hiari yake mwenyewe. “Nisubiri hapa. Nitakuletea.”
Hakuwa na wasiwasi hata kidogo kwamba Lisa angekimbia, kutokana na bahari kubwa na kutokuwepo kwa boti hapo. Hakuna hata mgeni mmoja aliyeweza kupatikana kwenye kisiwa hicho.
Baada ya Lisa kugundua kuwa ameondoka, alisimama na kupanda kwenye mwamba karibu na bahari. Alijiumiza kwa makusudi kwenye

mwamba mahali ambapo jeraha lake lilikuwepo. Alipomuona Alvin anakuja, alijifanya kuteleza kutoka kwenye mwamba na kutumbukia baharini.
“Lisa...” Alvin alitokea kuona tukio hili. Alishtuka sana hadi akaruka baharini bila kusita. Aliogelea kuelekea kwake na kumwinua upesi kutoka baharini. "Uko salama?"
“Niko sawa...” Baada ya Lisa kumaliza sentensi yake akiwa amekunja uso, sauti ya kugugumia maumivu ilisikika.
Alvin alimchukua haraka hadi ufukweni na kuangalia jeraha lake. Aligundua kuwa sehemu ya nyuma ya mguu wake ilikuwa imefugwa.
Inavyoonekana, kulikuwa na sehemu ya ngozi yake iliyokatwa na mwamba mkali na kusababisha jeraha kubwa.
Alvin akambeba Lisa na kukimbilia

ndani ya jumba lile bila kufikiria tena. Mjakazi mkuu haraka akamleta sanduku la huduma ya kwanza Kwa kuzingatia jeraha lake la kina, Lisa alihitaji kupigwa sindano ili kupunguza uvimbe.
Lisa aliendelea kuvumilia maumivu. Maumivu hayakuwa kitu ilimradi Alvin asijue asili ya jeraha hilo.
Kwa upande mwingine, Alvin aliumia moyoni na kujilaumu. "Ukienda kando ya bahari wakati ujao, nitahakikisha kuwa na wewe wakati wote ili usifanye jambo lolote la hatari tena."
Lisa hakuongea neno lolote. Alikuwa akiishi maisha kana kwamba yuko jela siku zote. Ikiwa alikuwa akimwangalia au la, haikujalisha.
Usiku, Lisa alijikunja kwenye kochi la kibarazani na kujitenga. Alikuwa kachoka kimawazo hadi kufa. Hapo, hakuweza kucheza na simu yake, kutazama runinga, au kufanya

shopping. Hakujua mtu mwingine yeyote hapo pia. Ukiachna na kusoma vitabu maktaba, aliweza tu kutazama angani kila siku.
"Umeboreka?" Alvin akatoka bafuni. Moyo wake uliumia sana baada ya kuona sura yake dhoofu.
"Lala na mimi kwa sababu umechoka."
Alipomaliza tu sentensi yake, alimchukua hadi chumba chake cha kulala na kumuweka kitandani. Kisha akanyoosha mikono yake kumvua nguo za kulalia.
Akijua nia yake, Lisa alimpinga kwa kawaida. “Alvin, mguu wangu umeumia na unauma. Huwezi kuniacha nipumzike?”
Macho ya Alvin yalimtoka kwa hatia, akasema bila kupenda, “Nimemuuliza daktari. Alisema kuwa wanawake wana

uwezekano mkubwa wa kupata mimba siku chache baada ya kipindi chao kuisha. Siwezi kukosa fursa ya siku hizi. Hata hivyo, usijali, sitakigusa kidonda chako.”
Pamoja na hayo, alifunga midomo yake na midomo yake kwa njia ya ujasiri lakini ya upole.
Lisa alikuwa dhaifu sana kumshinda hata kabla ya kujeruhiwa. Sasa kwa kuwa alikuwa ameumia, hakuna angeweza kufanya ili kumzuia. Alijua ya kwamba mtu huyo alikuwa ameazimia kufanya hivyo. Ingawa siku hizo uwezekano wa kupata mimba haukuwa juu, haikuwa na maana kwamba alikuwa salama kabisa.
Dakika aliyojiwazia kuwa ana mimba ya mtoto wake, moyo wake uliingiwa na hofu.
“Alvlisa, tafadhali usinitendee hivi.” Alimsihi ghafla huku akimshika mkono.

Mwili wa Alvin uliganda. Kwa kadiri alivyokumbuka, hakuwahi kumwita Alvlisa kwa muda mrefu sana. Hata hivyo, neno hilo kwa namna fulani liligonga kengele lilipotoka kinywani mwake. Ilionekana tu kuwa jambo la kweli wakati alipozungumza naye kwa njia hii.
“Lisa, unaweza kunilaumu na kunichukia kwa ninachotaka kufanya sasa. Lakini sijali. Nataka tu kukupa mimba ya mtoto wangu.” Alirudia kumbusu midomo yake kwa huzuni lakini kwa ujasiri wakati huo huo. "Ninaapa kwamba nitakutendea wewe na mtoto vizuri katika siku zijazo. Samahani, Lisa, sijui jinsi ya kukuzuia ubaki upande wangu. Ninakubali kwamba mimi ni mtu mbaya kwako, lakini nitapandwa kichaa ikiwa nitakupoteza.”

Sura ya: 494 Nairobi.
Jack aliingia kwenye nyumba ya kahawa iliyoundwa kipekee.
"Bwana Jack, baba yako anakungoja juu." Mhudumu alimpeleka kwenye ghorofa ya tatu.
Jack alipousukuma mlango, aligundua kuwa, mbali na Mason, Jerome na baba mdogo wake wa pili, Maurice Campos, walikuwapo pia.
“Baba, nilifikiri umeniita hapa wewe tu. Sikujua kuwa Anko na Jerome wako hapa pia. ” Jack aliona ajabu.
Hata hivyo, bado alipata kiti na kuketi juu yake. “Baba kwanini umeniomba nije huku? Kuna nini?"
Mason alionekana kulipuuzia swali lake na kujikita katika kumimina kahawa.

Baada ya Maurice na Jerome kutazamana, Maurice aliuliza huku akitabasamu, “Unajua kilichompata Alvin?”
“Sijui. Hajawasiliana nasi.” Jack alikunja uso. "Anko, wewe sema ttu."
Tabasamu la maana likapita usoni mwa Maurice. "Nilisikia Kimaro Electronics, wakishirikiana na kampuni kutoka China, iko karibu kufanikiwa kutengeneza Kilimanjaro Smartphones."
Macho ya Jack yalimkazia na kusema. 'Hakika...”
Jerome alikuwa amegusia jambo hilo Jack mara chache, lakini Jack hakutarajia kwamba Maurice angejitokeza ana kwa ana wakati huu.
Hata Mason.

Mtazamo wa Jack ulidhihirisha hisia tofauti. Alikuwa akifikiria kwamba Mason alikuwa mtu wa kifahari ambaye alijikita tu kwenye sanaa bila kuwa na wasiwasi juu ya kile kinachoendelea katika ulimwengu wa biashara. Alikuwa akiamini kwamba Mason alifichua ugonjwa wa akili wa Alvin miaka mitatu iliyopita kwa ajili ya familia ya Campos.
Kwa mtazamo wa mambo sasa, hata hivyo, Jack alihisi kuwa baba yake hakuwa mtu rahisi.
"Anko, nilimwambia Jerome hapo awali kwamba Alvin haniruhusu kuhusika katika masuala ya electronics, maabara hiyo inasimamiwa na Wachina." Jack alieleza kwa sauti ya chini.
“Hiyo ilikuwa hapo awali,” Jerome alisema huku akitabasamu, “Sasa, ni tofauti kwani Alvin hayupo Kenya. Mara bidhaa inapotengenezwa, kila aina ya

matangazo yanahitajika kufanywa. Kama meneja mkuu wa KIM International, ambayo ni kampuni mama ya Kimaro Electronics, unafaa kuidhinisha taratibu zote za uundwaji wa simu hizo. Kwa hivyo, unaweza kupata habari kuhusu data za simu hizo kwa urahisi."
Jack alichukua kikombe cha kahawa. Akainamisha kichwa chake na kukinywa kidogo. Matendo yake yalificha mwangaza machoni pake.
Kwa kusema ukweli, alikatishwa tamaa sana katika familia ya Campos.
Kwa kuzingatia ukweli kwamba familia ya Campos imekuwa ikimchukulia kama mtu wa nje siku zote, walikuwa na tamaa sana. Kama familia ya pili yenye ushawishi mkubwa nchini Kenya, Campos walikuwa wakijaribu kutafuta njia ya kuiba bidhaa ambayo mtu mwingine alikuwa ametumia pesa nyingi

na juhudi badala ya kuboresha bidhaa za kampuni yao kwa uwezo wao wenyewe. Tabia yao ilikuwa ya aibu kama nini!
Kwa kweli, Jack alikiri kwamba hakuwa mtu mzuri pia. Hapo awali, alikuwa ametumia njia za chinichini kupata nafasi yake katika kampuni ya KIM International. Hata hivyo, alikuwa na mipaka yake.
Baada ya kugundua kuwa Jack hasemi neno lolote, Maurice alisema kwa upole, “Jack, jina lako la mwisho linaweza kuwa Kimaro, lakini jina la mwisho la baba yako ni Campos. Wewe ni mtoto wa familia ya Campos. Ni suala la jina la mwisho tu. Baada ya yote, Kimaro wananachukulia kuwa mtot wa nje. Fikiria jinsi familia ya Kimaro imekuwa ikikutendea miaka hii. Alvin alipata kila kitu ingawa wewe ni mtoto wa Lea pia.

"Unaweza kuwa meneja mkuu wa KIM International, lakini unasimamia tu sehemu katika kampuni ambayo haikulipi vizuri. Je, umeridhika na hili? Je, unapanga kuendelea kuishi katika hali ya sintofahamu? Hapa kuna nafasi kwako kuifanya iwe kubwa."
“Baba...” Jack alielekeza macho yake kwa Mason. Hakuyaamini maneno ya Maurice. Baada ya yote, Campos mara nyingi walitoa ahadi za uwongo.
Mason aliegemea nyuma kidogo, macho yake yakiwa meusi. “Jack, kuna jambo moja ambalo nimekuwa nikikuweka gizani. Nina asilimia 60 ya hisa katika Kampuni ya Campos.”
Jack alishikwa na butwaa. Hakuwahi kufikiria kwamba baba yake angeficha ukweli huu vizuri. Asilimia 60 ya hisa ilikuwa sawa na kiasi kikubwa cha utajiri. Lakini, watu hawakujua. Huenda

mama yake pia hakujua hilo.
Jack alipokuwa akiwaza jambo hilo,
aliona baba yake akitisha sana.
Wakati huo huo, Jerome akaongeza kahawa ya Jack. "Kwa kweli, niliamua kujizuia mbele ya umma hapo awali ili kuepuka familia ya Kimaro kugundua kuhusu hili. Fikiri juu yake. Wewe ni mtoto wa pekee wa Anko Mason. Nani mwingine atachukua hisa za Campos Corporation isipokuwa wewe? Kampuni ya Campos itakuwa yetu mapema au baadaye.”
Jack alichanganyikiwa kabisa. Hakusema lolote kwa muda.
Hakika, ikiwa Mason anamiliki asilimia 60 ya hisa, hisa hizo zingeenda kwa Jack kwa vile alikuwa mtoto wa Mason.
Ikiwa familia ya Campos ingekuwa familia yenye ushawishi mkubwa katika siku zijazo, Jack angeshindwa kumwangamiza Alvin?

Mason alimtazama kwa kina na kusema kwa upole, “Jack, najua unashangaa sana. Lakini kama mtoto mkubwa wa familia ya Campos, sina budi kujiandaa na mambo fulani. Nisipofanya hivyo, akina Campos wasingekuwa kama walivyo leo. Kama mwanaume, hutaki kujenga kazi yenye mafanikio? Haijalishi jinsi mama yako ni mke mzuri kwangu, lakini KIM International bado inachukuliwa kuwa nguvu ya jitihada zake mwenyewe. Siwezi kamwe kuwa na mkono ndani yake.
Zaidi ya hayo, Kimaro wamenidharau tangu mwanzo. Kila nikikuona unakandamizwa na Alvin, huwa najistukia kama baba yako. Kweli, nilipitia hali hiyo hiyo pia. Ukiisha kustahimili dhoruba, nitakupa kila kitu nilicho nacho.”
Jack alishtuka. Baada ya muda, alijibu kwa hisia tofauti, “Acha nifikirie jambo

hilo, Baba.”
“Hakuna cha kufikiria—'” Jerome akaruka ghafla huku akihema.
"Jerome, mpe muda," Mason alimkatisha kwa sauti ya kuonya. "Fikiria kwa makini, Jack. Mara tu kifaa hiki cha KIM International kitakapozinduliwa kwenye soko kwa ufanisi, KIM International itakuwa biashara yenye nguvu zaidi Afrika. Alvin atapokea utukufu wote, wakati wewe bado utakuwa meneja mkuu maskini. Huna hata hisa zozote katika KIM International na inabidi umtegemee mama yako akupe hisa siku zijazo.”
"Zaidi ya hayo, uhusiano wa mama yako na Alvin unaonekana kuimarika sana siku hizi," Maurice aliongeza kwa huzuni, "Nashangaa ni hisa ngapi ambazo Lea atakupa wakati huo? Lakini baba yako ni tofauti. Wewe ni mwanawe

wa pekee.”
Macho ya Jack yaliangaza kwa hisia ngumu. Kwa muda mrefu, alikaa kimya.
Mason alimtazama na kucheka. “Nasubiri kusikia habari njema kutoka kwako.” Mara tu Mason alipomaliza sentensi yake, alikuwa tayari kuondoka.
“Baba...” Jack aligeuka ghafla na kuuliza, “Huogopi kwamba... Mama atafadhaika baada ya kujua?”
Lea alikuwa amejitolea sana kwa ajili ya Mason, lakini lengo kuu la Mason lilikuwa kuharibu KIM International. Lea angeshuka moyo jinsi gani ikiwa angegundua kuhusu hilo?
Sura ya mshtuko ikapita kwenye uso wa Mason. “Usijali, nitamsaidia mama yako baada ya hapo. Wakati mwingine, unapewa nafasi moja tu kwenye njia

yako ya mafanikio. Isitoshe, mama yako asingekuwa kama alivyo leo bila usaidizi wa familia ya Kimaro. Hata atakapomtegemea mume kama mimi na mwana kama wewe katika siku zijazo, hadhi yake ya utukufu itabaki.”
“Jack, kama ningekuwa wewe, nisingesita hata kidogo. Kumbuka kwamba kila mtoto huchukua jina la mwisho la baba yake, kwa hivyo Campos linapaswa kuwa jina lako la mwisho,” Jerome alimkumbusha Jack kwa ukali.
Jack alikunja uso wake kwa kina huku akihisi kuchanganyikiwa. Hata hakuona kwamba Jerome na wengine walikuwa wameondoka.
Mason, Maurice, na Jerome waliingia kwenye gari jeusi baada ya kufika chini.
Jerome aliuliza, “Baba Mkubwa, unafikiri Jack atatusaidia?”

"Haijalishi." Ule usemi wa upole wa Mason toka alipokuwa juu ulitoweka. Aliwasha sigara huku akionekana kutofanya lolote.
Maurice alicheka. “Kaka, huna huruma hata na mwanao wa kumzaa?”
Akikazia macho, Mason aliendelea kuwasha sigara. Hana moyo? Ha! Angeweza kuwa na moyo wakati Jack hakuwa mtoto wake? Alifahamu fika kuwa Jack alikuwa mtoto wa Lea na Mike Tikisa. Jack alikuwa ni mdogo wa damu wa Alvin!
Usiku alipokutana na Lea, Lea alikuwa amelewa na alikuwa amelala na Mike badala ya Mason. Mason alikuja baada ya Mike kuondoka.
Lea alitokea kuwa mjamzito wakati huo, kwa hivyo Mason alimkaushia tu na

kumuoa, kwa sababu alikuwa na pesa, sabuni ya roho!
Kwa miaka mingi, alikuwa akiwavumilia Lea na Jack, wapumbavu hawa. Kuhusu Jack na Alvin, Mason hakuweza kusubiri kuona hawa ndugu wawili wa kdamu wakipigana wao kwa wao. Wasingegundua ukweli kamwe! Ingawa ni kweli Mason alikuwa na asilimia 60 ya hisa katika Kampuni ya Campos, asingeweza kamwe kumpa Jack.
Sura ya: 495
Jack alikaa ghorofani kwa muda mrefu. Hakika maneno ya Mason yalikuja kama pigo kubwa kwake.
Alikuwa akitetemeka, lakini Lea angeshuka moyo sana ikiwa angemsaidia Mason. Hata babu na bibi zake wangekatishwa tamaa naye.
Mara nyingi aliwakuta wakimtendea haki

na hakuridhika nao, lakini wakati mwingine, ilibidi akubali kuwa Alvin alikuwa na uwezo zaidi yake. Baada ya kusema hivyo, hakutaka kucheza mchezo wa pili kwa Alvin milele. Kwa macho ya Alvin, Jack alikuwa mtu ambaye angeweza kumfukuza wakati wowote.
Akiwa katika hali ya kutatanisha, Suzie alimpigia simu ghafla.
“Baba mbona hujaja kunichukua? Watoto wengi tayari wameondoka.”
Ghafla alirudiwa na fahamu, na kugundua kwamba ilikuwa karibu saa saa kumi na moja jioni.
“Sawa, nitawasili baada ya muda mfupi.”
Akiwa njiani alipokea simu kutoka kwa Bibi Campos.

Wakati anafika shule ya awali, tayari ilikuwa saa kumi na moja nanusu jioni. Akiwa na kizunguzungu, Suzie aliingia kwenye gari lake.
“Anko Jack, Mama bado hajawasiliana nami. Baba yangu mchafu alimpeleka wapi? Sitaenda kumuona Mama tena? Namkumbuka sana.” Mtoto mdogo alikuwa karibu kulia huku akisema.
"Hapana. Alvin lazima amemchukua mama yako ili kuishi katika ulimwengu wao mdogo.” Jack hakuweza kujizuia kulifikiria jambo hilo na kuendelea, “Labda mama yako atarudi na kaka au dada mchanga kwa ajili yako.”
“Hilo haliwezekani.” Suzie alishtuka kusikia hivyo. "Mama yangu tayari ameolewa na Anko Kelvin. Ikiwa atakuja na mimba ya watoto wa baba yangu mchafu... haitakuwa vizuri.”

Jack alikohoa kidogo. Bila shaka, hilo halingekuwa jambo zuri. Hata hivyo, iliwezekana kwa Alvin kufanya vile kwa kuzingatia ugonjwa wake wa akili. Hata hivyo, usijali. Alvin anampenda mama yako, hivyo hatamuumiza.”
Hapo ndipo Suzie alihisi raha. “Anko Jack, wapi tunakwenda? Hii haionekani kama njia ya kurudi nyumbani.”
"Tutakula chakula cha jioni katika nyumba ya familia ya Campos," Jack alieleza, "bibi yako alinipigia simu na kuniambia kwamba anataka tule chakula cha jioni huko."
“Ah, sitaki!” Suzie akatikisa kichwa mara moja. “Sitaki kwenda huko. Tafadhali nirudishe kwa Bibi Kimaro kwanza
."
“Suzie, utakuwa sawa. Wote wanafikiri kwamba wewe ni binti yangu. Pia, babu na babu yako wapo.” Jack alimtuliza

kwa sauti ya upole.
"Hapana." Suzie alipiga kelele. “Hawanipendi. Kila nikienda huko wananipuuza. Mara ya mwisho, ni Jill ambaye alinisukuma kwanza, lakini Bibi- Mkubwa alinikaripia na akambembeleza Jill, wala hakumkaripia yeye hata kidogo. Hata alisema kuwa
Kimaro haikunifundisha vizuri na kuniita mgonjwa.”
Jack aliona kuwa haiaminiki. Jill alikuwa binti wa binamu wa Mason, na kila mara alicheza katika nyumba ya familia ya Campos. Ilifahamika kwamba Suzie alikuwa binti wa Jack, hivyo alishiriki uhusiano wa karibu na familia ya Campos. Hata hivyo, kwa nini Bibi Campos alimpendelea mjukuu wa jamaa yake badala yake? Yeye alienda mbali sana na maneno hayo.
"Suzie, kunaweza kuwa na

kutokuelewana?"
"Hakuna kutokuelewana. Hata nilimsikia Jill akiwaambia watoto wengine katika familia ya Campos wasicheze nami. Wanapenda kucheza na Benny. Hata walisema kwamba ninaudhi.” Suzie alisema kwa hasira, “Walifikiri sikusikia, lakini nina usikivu mzuri. Nilisikia yote.”
“Benny ni nani?” Maneno ya Suzie yalizidi kumchanganya Jack. Kulikuwa na jamaa, watumishi, na watoto wengi katika familia ya Campos. Hata hivyo, hakuwahi kusikia mtu yeyote anayeitwa Benny.
“Sijui. Sijawahi kumuona.” Suzie akatikisa kichwa. “Pia, wakati wowote ninapoenda kwenye nyumba ya familia ya Campos, Bibi mkubwa hataniruhusu kugusa vitu vya huko. Ninaweza kuhisi kwamba hawanipendi.”

Jack alipokuwa akisikiliza alichokisema Suzie, alizidi kukasirika.
Hakuwa na hasira na Suzie bali na watu wa Campos.
Ingawa Suzie hakuwa binti yake wa kumzaa, alikuwa mwanaye, hata hivyo. Alikuwa akimpenda kwa sababu alikuwa mwerevu na mjanja. Alipojua kwamba bibi yake alimtendea Suzie hivyo, alikata tamaa. Maneno ya Suzie yalionekana kama ndoo ya maji baridi aliyomwagiwa kichwani.
Ilikuwa ni ajabu. Katika miaka hii yote, mapokeo ambayo familia ya Campos ilimpa Jack hayakuwa mazuri ikilinganishwa na jinsi walivyowatendea watoto wao wengine. Walikuwa wakimtendea Suzie vivyo hivyo.
Ingawa Mason alisema asilimia 60 ya hisa za Campos Corporation zingekuwa

zake mapema au baadaye, ilikuwa dhahiri kupitia mtazamo wa familia ya Campos kwake na kwa Suzie kwamba hawakumpenda sana. Je, inaweza kuwa...
Je, Mason alisema tu maneno hayo ili kumdanganya?
Alipofikiria kwa makini, Mason hakuwa akimjali hata kidogo katika miaka hii yote. Hakumjali mjukuu wake, Suzie pia. Je, kweli Mason angempa hisa hizo? Jack alianza kuwa na mashaka makubwa, hasa kwa sababu Mason alionekana kuwa hodari sana katika kuficha mambo. Nani alijua kama angekuwa na wanawake wengine nje ya familia katika siku zijazo au mtoto wa nje pia?
Benny? Hata hivyo, Benny alikuwa nani hasa? Jack hakuwahi kusikia habari zake hapo awali.
Kadiri alivyozidi kuwaza, ndivyo moyo wake ulivyozidi kuwa na mashaka.

“Suzie, unaweza kunifanyia upendeleo?” Jack alisema kwa sauti ya chini, “Wewe ni mwerevu sana, kwa hiyo ukienda kwa familia ya Campos baadaye, nisaidie kujua Benny ni nani kupitia Jill. Nitakununulia chokoleti usiku wa leo."
"Sawa, nitafanya kwa ajili ya chokoleti. ” Suzie aliitikia kwa kusitasita.
“Lakini usiruhusu watu wazima wakutambue,” Jack alimkumbusha.
“Sawa, najua. Ni jambo dogo. Kwa akili ndogo ya Jill hawezi hata kunificha hata kidogo.” Suzie alikuwa na sura ya kiburi.
Walipofika kwa familia ya Campos, Jack alienda kuzungumza na babu yake na bibi yake huku Suzie akienda kucheza

na Jill. Ingawa Jill alikuwa mjukuu wa dada mdogo wa Mzee Campos, mageti ya nyumba zao mbili yaliunganishwa.
Suzie alipoenda kumtafuta Jill, Jill alikasirika alipomwona.
“Mbona umekuja tena? Nilisema sikupendi na sitaki kucheza na wewe.”
Suzie akatazama huku na kule. Aliona hakuna watu wazima karibu, hivyo akanong'ona, “Lakini nimechoka sana. Je, unaweza kucheza nami kwa muda kidogo? Dada Jill, wewe ndiye fundi wa kucheza huu mchezo wa jigsaw? Unashangaza!”
Jill alikuwa na umri wa miaka minne kama Suzie, hata hivyo. Alikuwa kalewa baada ya kupongezwa na Suzie. “Bila shaka. ”
“Dada Jill, mbona leo uko peke yako?

Yuko wapi... Benny?' Suzie alijifanya kuuliza ovyo.
“Kaka Benny inabidi asome. Yuko katika shule ya msingi,” Jill alisema huku akiendelea kutatua fumbo lake la jigsaw kwa umakini.
“Wow, yeye ni mzuri sana. Bado niko shule ya awali. ” Suzie alisema, “Lakini kwanini sijakutana naye hapo awali? Je, anaishi karibu? Dada Jill, una bahati sana kwamba una kaka wa kucheza na wewe. Sina mtoto wa kucheza naye nyumbani na ninachoka sana kuwa peke yangu.”
“Kaka Benny alikuja jana pia. Yeye ndiye aliyenifundisha jinsi ya kufumbua mafumbo ya jigsaw.” Jill alikasirika baada ya kusikia maneno ya Suzie. “Mm, ni kweli. Anaishi tu karibu na

hapa. ”
“Wee, kumbe ni mtoto wa jirani?” Suzie alitenda kwa furaha na kuuliza.
"Hapana, ni mtoto wa mjomba ..." Jill alifunika mdomo wake ghafla baada ya kuropoka hivyo.
"Nini tatizo?" Suzie alijifanya hajui na kumtazama huku akipepesa macho.
"Yote ni makosa yako." Jill alimtazama Suzie kwa hasira. "Mama yangu aliniambia kuwa jambo hili nisimwambie mtu yeyote."
“Kwanini usimwambie mtu yeyote? Kuna tatizo?” Suzie alijieleza kwa mshangao.
“Hata mimi sijui.” Jill alikuwa na sura ya majuto usoni mwake. “Lakini baba na mama yangu waliniambia kwamba kaka

Benny ni siri.”
"Lo, itakuwa sawa mradi tu sitasema chochote juu yake?" Suzie alijifanya mtiifu na asiye na hatia. “Dada Jill, nitakusikiliza kuanzia sasa mradi tu uwe tayari kucheza nami.”
"Sawa, sina marafiki sasa, kwa hivyo naweza kucheza na wewe." Jill aliitikia kwa kichwa. Alifikiri Suzie alikuwa mjinga na anaweza kuwa kibaraka wake.
TUKUTANE KURASA 496-500
ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
LISA KITABU CHA NANE (10) SIMULIZI...........................LISA
KURASA.....................496- 500
PRESENT: SIMULIZI ZA DULLY

Sura ya: 496
Hata hivyo, Jill hakujua kwamba mara
Suzie alipomaliza chakula chake cha
jioni na kutoka nje ya mlango wa familia
ya Campos, mara moja alimwambia
Jack habari zote alizopata kutoka
kwake.
“Mtoto wa Anko wake...”
uso wa Jack ulibadilika mara tu
aliposikia hivyo. Anko ambaye Jill
alizungumza juu yake angeweza tu
kuwa Maurice au Mason. Maurice
alikuwa na watoto wawili, mkubwa
akiwa Jerome na mdogo akiwa Meddie.
Meddie alikuwa anasoma nje ya nchi
muda huo.
Kwa hivyo, Benny labda alikuwa mtoto
wa nje wa baba yake au Maurice.

Hata hivyo, mke wa Maurice alikuwa
mwanamke mkali. Ikiwa mume wake
angekuwa na mtoto wa kiume wa nje,
bila shaka asingemvumilia Maurice
kumpeleka kwenye familia ya
Campos.Kuna uwezekano mkubwa
kwamba Benny alikuwa mtoto wa nje
wa Mason Campos.
Moyo wa Jack ulihisi unyonge ghafla.
Haishangazi Mason hakujali sana juu
yake. Ni kwa sababu alikuwa na mtoto
mwingine nje. Mason alikuwa hata
akisema kuwa yeye ndiye mwanawe wa
pekee siku hiyo na karibu ashindwe na
maneno yake. Baba yake alionekana
kutisha zaidi alipofikiria jambo hilo.
Lea alikuwa amejitolea sana kwa ajili ya
Mason. Hata alichukua makumi ya
mabilioni ya pesa kama msaada kwa
ajili ya Kampuni ya Campos miaka
mitatu iliyopita, lakini Mason alikuwa na
mwanamke mwingine na mtoto wa

kiume nje?
Lea angeweza kushikwa wazimu
kutokana na hasira ikiwa angejua
kuhusu hilo.
Kwa bahati nzuri, maneno ya Suzie
yalimfanya Jack atulie. Ikiwa kweli
angevujisha data za Kiimanjaro
Smartphone ya Kimaro Electronics
kutoka KIM International, familia ya
Campos ingeweza kuwa familia yenye
nguvu zaidi nchini Kenya, lakini yeye
angekuwa tu jiwe la kukanyagia la
Mason. Ishu ilikuwa ni kwamba,
alitakiwa kumwambiaje Lea kuhusu
hilo?
“Suzie, usimwambie mtu yeyote kuhusu
hili kwa sasa,” Jack alimkumbusha.
Aliogopa Lea asingeweza kuhimili
mshtuko wake.
Usiku, Jack alimpigia Mason simu.
“Baba siwezi kufanya ulichoniomba jioni

hii. Nadhani tunapaswa kutumia njia
sahihi ili kushindana. Kwa kweli,
Kampuni ya Campos tayari inaendelea
vizuri. Kwanini unataka kujiweka
kwenye viwango vya KIM International?"
"Jack, unanivunja moyo sana." Sauti ya
chini ya Mason ilikuwa na athari ya
kutkata tamaa.
"Baba, kama binadamu, lazima tujue
mipaka yetu." Licha ya kuhuzunika,
Jack alijaribu kumzuia. "Tayari una tajiri
wa kutosha.
Mbali na hilo, kama si msaada wa KIM
International, familia ya Campos
isingefikia hatua hii— ”
"Funga mdomo wako! Haiwezekani
kufanikiwa ikiwa una moyo mpole. Si
ajabu hutaweza kushindana dhidi ya
Alvin katika maisha yako yote. Unaweza
kuwa hivihivi milele tu.” Mason akakata
simu moja kwa moja.

Jack alijawa na uchungu. Alikuwa na
hisia kwamba Mason angejaribu mbinu
nyingine baada ya kushindwa
kumtumia. Alilazimika kuwaangalia
wafanyikazi wa kampuni.
•••
Mbali katika kisiwa nje ya nchi.
Lisa alikuwa akihesabu siku. Kabla
hajajua, nusu ya mwezi tayari ilikuwa
imepita. Japokuwa hakutakiwa kufanya
lolote kwani Alvin alikuwa akimhudumia
vyema kwa kumpatia chakula kizuri na
vinywaji, bado alikonda baada ya nusu
mwezi.
Ilikuwa hasa kwa sababu siku zake
zilikuwa za huzuni sana. Sababu
nyingine ni kwamba alikuwa tayari
ameolewa, lakini alikuwa pamoja na
Alvin kila siku. Alijisikia hatia kwa ajili ya
Kelvin.
Siku hiyo, Alvin alimpeleka baharini

kuvua samaki.
“Lisa, ona samaki aina ya kodre
niliowakamata. Nitakutengenezea
samaki wa kukaanga kwa ajili yako
usiku wa leo, sawa?" Alvin alileta
samaki aliyenona na mwororo. Uso
wake ulikuwa umejaa tabasamu huku
akijaribu kumfurahisha.
“Sipendezwi na chochote.” Lisa alijibu
kinyonge.
Lisa alisimama na kwenda upande
mwingine. Mtazamo wake ulikuwa wa
kinyonge sana.
Alvin alihema huku akimwangalia kwa
nyuma. Wakati huo simu yake iliita Liun
Xiuan, injinia wa Kichina kutoka Kimaro
Electronics ndiye aliyepiga simu. Sauti
yake ilikuwa ikitetemeka kwa msisimko
aliposema, "Bwana Kimaro, utafiti na
utengenezaji wa Kilimanjaro

Smartphone umefaulu."
“Kweli?” Alvin aliitikia kwa utulivu.
“Umefanya vizuri.”
Liun Xiuan alishtuka. “Bwana Kimaro,
mbona hujaonyesha furaha hata
kidogo? Umewekeza zaidi ya dola
bilioni kumi kwenye utengenezaji wa
simu hii. Aidha, simu hii ni teknolojia ya
juu zaidi duniani, itaweza kushindana
mpaka kwenye masoko ya Ulaya. Hii
itakuwa kampuni ya kwanza Afrika
kutengeneza Smartphone bila
kutegemea vifaa kutoka nje. Nadhani
thamani ya soko ya KIM International
itaongezeka mara tatu angalau.”
"Sawa," Alvin alijibu kwa utulivu,
"Unaweza kutangaza habari kwamba
simu itazinduliwa hivi karibuni na kualika
waandishi wa habari kwa ajii ya
mkutano nusu mwezi baadaye.
Nitahudhuria muda ukifika.”

“Unarudi lini?” Liun Xiuan alisema kwa
haraka, “Habari zinapotolewa, hakika
zitavutia kampuni kubwa katika sekta za
mawasiliano kushirikiana nasi. Kampuni
inahitaji sana uwepo wako. Isitoshe, hili
ni jambo muhimu sana. Ni bora kwako
kuhusika katika kila kitu kuanzia uuzaji
hadi ushirikiano.”
Alvin alimtazama Lisa ambaye alikuwa
kashikwa na hisia ngumu. Alipunguza
sauti yake na kusema, “Sina muda
sasa.
Kampuni ilitumia pesa nyingi sana
kuajiri mameneja hao wakuu. Ni wakati
wao wa kufanya kazi zao.”
“Sawa.” Liun Xiuan hakuwa na chaguo.
Bosi wake alikuwa mtu katika upendo,
baada ya yote.
Baada ya kukata simu na Liun Xiuan,
Alvin alimpigia Master Ganja simu.

“Imarisheni ulinzi kwenye kampuni
kipindi hiki ambacho tunaenda
kutangaza ujio wa smartphone yetu
mpya. Hasa mainjinia hao wa Kichina
wote wapewe ulinzi mzito. Hatujui ni
watu wangapi wenye nia mbaya na sisi,
ambao watajaribu kuzima ndoto zetu
zilizo mbioni kutimia.”
Hakujificha kwa makusudi kutoka kwa
Lisa. Kulikuwa na wao wawili tu kando
ya bahari. Akitoa maagizo ya Ganja,
sauti yake ilisafiri hadi masikioni mwa
Lisa pia. Alizidi kushtuka huku
akiendelea kusikiliza.
Hakufikiri kwamba smartphone ya hali
ya juu ya KIM International
ingetengenezwa hivi karibuni. Hakujua
ni kiasi gani bei ya soko ya KIM
International ingeongezeka baada ya
simu hii kuzinduliwa. Hakuna mtu katika
Kenya, au hata katika Afrika nzima,
ambaye angeweza kushindana dhidi ya

Alvin wakati huo. Moyo wake ulikata
tamaa.
Je, angeweza kutoroka au kujificha kwa
mtu huyu milele?
“Lisa, unakaribia kuwa mke wa mtu tajiri
zaidi Afrika, hivi karibuni nitampita hadi
Dangote. ” Alvin alimkumbatia kwa
nyuma ghafla. Mkono wake ulikaa
kwenye tumbo la chini. "Watoto wetu
watakuwa wakuu kuliko wakuu na
wafalme."
Lisa alimtazama kwa unyonge.
“Unadhani ninajali haya yote?”
“Lisa, nataka kukuambia tu kwamba
kuniacha na kurejea upande wa Kelvin
ni jambo lisilowezekana. Kelvin ana nini
cha kushindana na mimi? Kumponda ni
rahisi kama kumponda mchwa mguuni
mwangu.”
Alvin akageuza mabega yake kwa
nguvu. Aliinamisha kichwa chake na

kuuma kwenye mdomo wake laini wa
chini.
Lisa hakuwa na neno. Wakati fulani,
alifikiri labda angekubali tu hatima yake.
Kwa uwezo wake, hakuweza kumtoroka
mtu huyu hata hivyo. Hata hivyo, bado
alihisi kinyongo.
Kwa kupepesa macho, siku nyingine
kumi zilipita. Juu ya kitanda kikubwa
cha kifahari, hakuna staili ya mapenzi
ambayo haikutumika.
Alvin alikuwa anajichagulia tu, mara
‘leo nataka popo kanyea mbingu’... Mh!
Kuna muda Lisa naye alikuwa
ananogewa kwelikweli hadi ‘anaifinyia
kwa ndani’. Kwa kila njia, Alvin
alihakikisha kuwa Lisa lazima aondoke
akiwa mama kijacho ndani ya mwezi
huo mmoja.
Sura ya: 497
Asubuhi hiyo Alvin aliamka kwanza.

Mwanamke aliyekuwa kando yake bado
alikuwa amelala fofofo. Shughuli ya jana
yake usiku ilikuwa imemfanya achoke.
Akamfunika vizuri na blanketi.
Alipoinuka, aligundua kuwa mguu wake
ulikuwa na madoa ya damu!
Mwanzoni, Alvin alifikiri aliumia mahali
fulani. Hata hivyo, aliingiwa na hofu
baada ya kukuta hakuna majeraha
kwenye mguu wake. Ikiwa haikuwa
damu yake, basi ilikuwa ya Lisa.
Aliinua blanketi kwa uangalifu.
Aligundua kuwa nyuma ya nguo yake ya
ndani kulikuwa na madoa. Ingawa
aliwahi kupata hedhi hapo awali, alijua
kwamba kwa hakika Lisa alikuwa
kwenye kipindi chake.
Hata hivyo, je, hakuwa na hedhi chini ya
siku 20 zilizopita? Kwanini alikuwa

kwenye hedhi tena? Aligundua kitu
mara moja. Ikiwa angekuwa na hedhi
siku kadhaa zilizopita, basi kulingana na
makadirio, angekuwa kwenye siku za
hatari katika kipindi hicho.
Je, inawezekana kwamba hahakuwa
na hedhi hapo awali? Damu ilitoka wapi,
basi?
Ghafla alikumbuka kwamba kati ya
majeraha aliyoyapata alipoanguka
kutoka kwenye mwamba kando ya
bahari mara ya mwisho, jeraha moja
wapo lilionekana kuwa la muda mrefu
kwani lilikuwa na kina kirefu na damu
yake haikuwa ‘fresh’.
Alielewa kila kitu mara moja. Alikuwa
akimdanganya muda wote.
Baada ya Lisa kuzinduka, haraka
haraka aliona usumbufu uliokuwa nao
mwilini. Hedhi yake ya kweli ilikuja.
Kulingana na tarehe, ulikuwa ni muda
muafaka. Aliweza kuhisi kuwa nguo

yake ya ndani ilikuwa na unyevu.
Alitarajia Alvin asingegundua. Lakini,
hilo lisingeweza kufichwa kwa muda
mrefu. Angewezaje kumweleza jambo
hilo? Je, aseme kwamba hedhi yake
ilikuja mapema kwa sababu alikuwa na
stress nyingi? Sahau! Aliamua kuoga
kwanza.
Akaketi. Ghafla, aliona umbo refu likiwa
limekaa kwenye sofa ndani ya chumba
hicho huku miguu yake mirefu ikiwa
imenyooshwa kwa umaridadi. Kulikuwa
na sigara kati ya vidole vya mtu huyo.
Moshi ulitia ukungu chumba kizima.
Hata hivyo, moyo wa Lisa ulirukaruka.
Alikuwa na hisia mbaya. Alimtazama, na
Alvin akaizima sigara. Macho yake safi
yalikuwa kama vipande vya barafu.
“Ulikata mguu wako ili ujifanye una
hedhi. Ili kuficha jeraha, ulianguka kwa
makusudi kutoka kwenye mwamba.
Umeweka juhudi nyingi kwa hili."

Kope nene za Lisa zilikuwa chini. Kwa
kuwa alikuwa amepatia kila kitu,
hakukuwa na haja ya yeye kujitetea.
"Lisa, unachukua fursa ya upendo
wangu kunitesa kweli?" Alvin alisimama
na kuelekea pembeni ya kitanda.
“Unaamini kuwa kuanzia sasa nitafanya
mapenzi na wewe hata kama uko
kwenye kipindi chako?”
Lisa alitetemeka. Baada ya muda,
alidhihaki. “Usinichekeshe. Asilimia ya
kubwa ya wanaume katika ulimwengu
huu hawafanyi ngono na wanawake
wakati wa kipindi chao.
Kwanza, ni uchafu na hatari kwa afya
zao. Pili, wanaogopa kuumiza mwili wa
mwanamke. Alvin, hili ni jambo ambalo
wanaume wote wanaliheshimu.
Usinifanye nikuone kama wewe ni
mkatili sana.
“Sijui hata yatakuwa ni mapenzi gani

haya. Unachofanya sasa ni kunichukulia
kama chombo chako cha starehe. Sina
uhuru hata kidogo. Siwezi hata kupanga
wakati gani nipate mimba, na unaweza
kufanya mapenzi na mimi upendavyo.”
Akiendelea kuongea alianza
kutetemeka kwa hasira.
Aliweza kuwa anapoteza udhibiti wa
hisia zake kwa sababu ya kipindi chake,
au labda kufadhaika kulikuwa kumeingia
ndani yake kwa muda mrefu sana.
Alimfokea kwa hasira huku akilia,
“Mapenzi yako haya yanatisha sana!
Nisingependa kuwa na upendo wako
hata kidogo. Kwanini hukumtendea
Sara hivi kama unavyonitendea mimi
sasa? Unajua siku kama hizi kweli
zinanifanya nijisikie ninaishi kuzimu?
Kila mara huwa nafikiria kuruka tu
baharini ili nizame.”
Kama si Lucas na Suzie, angeweza

kujitosa baharini muda mrefu uliopita.
Mwishowe, bado alijisikia vibaya kwa
watoto hao wawili. Wangehuzunika
sana ikiwa wangempoteza mama yao.
“Usithubutu.” Alvin aliuma meno na
kumuonya Lisa kwa ukali. Kulikuwa na
unyonge, kuchanganyikiwa, na hisia ya
kukata tamaa machoni pake.
Maneno yake yalikuwa kama kisu.
Alipofikiria uwezekano wa yeye
kuondoka katika dunia hii, akili yake
ilitawaliwa na hofu. Hakufikiria hata
kabla ya kuzungumza.
"Lisa Jones, ikiwa utathubutu kujimaliza,
nitawafanya marafiki na familia yako
wote kufa pamoja nawe."
“Wewe mwendawazimu! Wewe ni
pepo!” Lisa alilaani vikali, "Nakulaani
kwamba hivi karibuni au baadaye,
marafiki na familia yako yote

watakuacha. Hakutakuwa na mtu kando
yako. Kila mtu atakuchukia na
kukudharau. Kampuni yako itafilisika, na
utabaki bila chochote.”
“Nikemee vyovyote unavyotaka. Hata
unitukane kwa ukali kiasi gani,
sitakuacha kamwe.” Alvin aliuvumilia
uchungu moyoni mwake. Alionya, “ Kwa
kuwa hukupata mimba wakati huu, basi
tutajaribu tena. Ikiwa mwezi mmoja
hautoshi, basi miezi miwili...
nitahakikisha unakaa hapa hadi unapata
mimba. Nina muda wa kutosha.” Alitoka
kwa hatua ndefu baada ya kusema
hayo.
Alipotoka alisikia sauti ya vitu
vinavyovunjwa na kilio cha mwanamke
huyo.
Alijawa na uchungu, na hata machozi
yakamtoka. Mwanamke aliyempenda
alikuwa amemlaani. Hah! Alikuwa
amefikiria kumwacha pia. Lakini, kila

alipomwona pamoja Kelvin, alishindwa
kuvumilia. Ingekuwa afadhali aende
kuzimu pamoja naye.
Alvin aliketi juu ya meza na kuangusha
glasi baada ya glasi ya divai. Hapo
awali, hakupenda kunywa pombe na
kuvuta sigara. Hata hivyo, ni mambo
hayo tu yanayoweza kumtia ganzi na
kusahau maumivu kwa muda.
Simu yake iliita. Alipoipokea, sauti ya
wasiwasi ya Hans ilisikika. “Bwana
Mkubwa, kuna shida. Landell Group
imetangaza kabla yetu na ilizindua
smartphone yao mpya zaidi leo. Hata
hivyo, data ya simu yao ni sawa kabisa
na data ya Kilimanjaro Smartphone
yetu. Mbaya zaidi ni kwamba data ya
simu yetu kwenye maabara imetoweka.”
"Unasema nini?" Alvin alisimama ghafla.
Alivunja glasi ya divai kwa mikono yake,

akipiga kelele, “Si
niliwaambia wanachama wa ONA
kulinda maabara? Je, data ilipoteaje? Ni
kundi gani la wajinga! ”
“Hatujui. Tuko katikati ya kuchunguza,”
Hans alinong’ona, “Hata hivyo, maabara
kwa kweli imekuwa na ulinzi mkali siku
hizi. Ni wasimamizi wachache tu wa
KIM International walioweza kuingia
kwenye maabara.
“Bwana Mkubwa, kampuni ndogo ya
Landell Group imezinduliwa asubuhi ya
leo na kutangaza simu yao leoleo, ni
ajabu sana. Tunakadiria kuwa hisa za
kampuni yetu zitaporomoka.
Tunaweza kupapata hasara ya dola
bilioni 20. Nadhani hata inaweza kuwa
zaidi ya hapo. Hali itakuwa mbaya ikiwa
hii itaendelea. Kampuni iko kwenye hali
mbaya sasa. Lazima urudi mara moja."
"Sawa, nitarudi mara moja." Alvin

alikata simu huku moyo wake ukiwa
mzito. Haraka akaelekea chumba cha
kulala.
Lisa alikuwa anaoga ndani. Ghafla,
mlango wa bafuni ukasukumwa.
Alikaribia kupiga kelele baada ya kuona
Alvin akiwa amesimama mlangoni.
"Unafanya nini? Ninaoga sasa. Toka
nje!” Ingawa alifanya ngono naye mara
nyingi, bado hakuweza kumkubali
amwangalie akioga.
Alvin alimtazama kwa kuchanganyikiwa.
Hapo awali, alifikiri angeweza kuongoza
KIM International kuwa juu zaidi kwa
ujio wa smartphone. Kwa njia hiyo,
hakuna mtu ambaye angeweza
kumchukua Lisa kutoka kwake.
Lakini, KIM International ilikuwa chini ya
shambulio ambalo halijawahi kutokea.
Walikuwa wameshikwa na tahadhari.

Alvin alikuwa na hisia kwamba huu
ungekuwa wakati mgumu zaidi katika
maisha yake yote. Hakujua kama
alikuwa na ujasiri wa kumuweka wazi au
la.
“Lisa...” Alienda chini ya bafu na
kumbusu midomo yake yenye
unyevunyevu kwa nguvu.
Maji yakamwagika juu yao wote wawili.
Lisa hakuweza kufungua macho yake,
lakini bado alimsukuma mbali kwa
hasira.
"Alvin, potelea mbali! Huwezi hata
kuniacha peke yangu ninapokuwa
kwenye kipindi changu?”
Ni kana kwamba Alvin alikuwa hamsikii
Lisa. Aliendelea kumbusu kwa pupa
kana kwamba lilikuwa busu lao la
mwisho kabla ya kutengana.
Lisa aliogopa, na alikuwa amepotea
kutokana na busu hilo. Alimuacha

aende pale tu alipokaribia kuzidiwa na
kisha kumsukuma kwa nguvu.
"Lisa, lazima niondoke kwa sababu ya
mambo kadhaa," Alvin alisema kwa
sauti ya sikioni.
Lisa alipigwa na butwaa. Mwili wake
wote ulilegea, na sauti yake ilikuwa kali.
“Sawa, ondoka haraka. Hata hivyo sitaki
kukuona kila siku.”
"Nitarudi haraka iwezekanavyo." Alvin
aliuma sikio lake kidogo.
Lisa alihisi kana kwamba umeme
ulikuwa unapita ndani yake, lakini
hakuweza kumsukuma mbali hata
kidogo.
"Nisubiri." Alvin akamuacha. Baada ya
kumtazama kwa kina kwa zaidi ya
sekunde kumi, akageuka na kutoka
bafuni.

Lisa alisimama chini ya bafu, bado
amepigwa na butwaa. Hakujua ni nini
kinamsumbua mwanaume huyo.
Sura ya: 498
Saa sita baadaye, helkopta ya Alvin
ilitua Nairobi.
Mara moja alikimbia kuelekea KIM
International. Ingawa ilikuwa tayari saa
tatu usiku, hakuna hata mwanahisa
mmoja wa KIM International aliyekuwa
ameondoka. Kilichotokea siku hiyo ndio
mzozo mkubwa zaidi tangu KIM
International kuanzishwa.
Mzee Kimaro, Lea Kimaro, Spencer
Kimaro, Jack Kimaro, na wengine
walikuwa wakingoja kwenye chumba
cha mikutano. Mlango wa chumba cha
mkutano ulipofunguliwa, kila mtu alijaa.

“Alvin, lazima utupe maelezo ya jambo
hili. KIM International imepoteza pesa
nyingi sana kuwekeza kwenye huu
mradi wa smartphone. Hata kampuni
zilizosaini mkataba nasi hapo awali
zinatushitaki kwa kuvunja mkataba.
Wanataka fidia ya juu sana kutoka
kwetu."
"Hiyo ni sawa. Kampuni yetu iliapa
kwamba hii itakuwa smartphone ya
teknolojia ya juu zaidi ulimwenguni
wakati tunatia saini kandarasi.
Lakini, baada ya mkataba kusainiwa,
Landell Group ilizindua smartphone
sawa na yetu. Shida ni kwamba, ingawa
tunataka kuishtaki Landell Group kwa
kuiba Data zetu, taarifa zote
zinazohusiana kwenye maabara
zimefutwa."
“Kama suala hili halitatatuliwa, kampuni
nzima italazimika kuacha kufanya kazi
baada ya kulazimika kulipa kiasi

kikubwa cha fidia kwa kukiuka mkataba.
Aidha, fedha nyingi za kampuni
zimetumika kuwekeza katika utafiti na
maendeleo ya maabara. Kampuni
inaweza kufilisika."
Wanahisa katika bodi ya wakurugenzi
walionyesha huzuni na hasira zao.
Waliposikia kwamba kampuni hiyo
inaweza kufilisika, baadhi ya wanahisa
walianza kukemea kwa sauti kubwa.
"Alvin, hili ni kosa lako! Wewe ndiye
ulisisitiza kupoteza pesa nyingi
kutengeneza simu. Sasa,
umetudanganya sote.”
“Hiyo ni sawa. Unapaswa kubeba
jukumu kubwa zaidi katika suala hili!
Isitoshe, sifa ya kampuni imeharibiwa
kabisa kwa sababu ulimpokonya mke
wa Kelvin. Sio tu hautoki kutatua tatizo,
lakini hata ulijificha wakati wa nyakati
muhimu za kampuni. Kama Mwenyekiti
wa kampuni, ulipaswa kushughulikia

uzinduzi wa smartphone wewe
mwenyewe.”
"Mzee Kimaro, familia ya Kimaro lazima
watupe sisi, wanahisa, maelezo leo."
Uso wa Mzee Kimaro ulibadilika
kutokana na kuzungukwa na wanahisa.
Valerie kisha akaongea kwa hasira.
“Mbona nyie nyote
mnazungukazunguka na baba yangu?
Baba yangu tayari ni mzee sana na ana
wasiwasi juu ya jambo hili pia. Isitoshe,
mnafikiri ninyi pekee mna wasiwasi?
Tunapoteza nafasi yetu pia kama familia
yenye nguvu zaidi."
“Acheni ugomvi. ” Lea akapaza sauti
yake na kuwazuia kwa utulivu. "Jambo
muhimu zaidi sasa ni kupata suluhu
kwenye kampuni. Lazima tujue ni nani
aliyevujisha data za maabara.”

“Kuna faida gani hata tukikamata
mwizi? Hata tukimshika mtu huyo, sifa
ya KIM International bado itaharibika.”
Mwanahisa alisema kwa uchungu,
“Wakubwa wa kampuni zilizosaini
mikataba nasi watatutafuta na mikataba
hiyo mkononi kesho asubuhi. Hatuwezi
kuepuka kuwafidia. Tusipolipa, itabidi
tupeleke hili mahakamani. Kufanya
hivyo kutasababisha sifa ya kampuni
kugonga mwamba. Nani atathubutu
kushirikiana nasi katika siku zijazo? Nini
kitatokea kwa kampuni baada ya kufidia
pesa? Tutafilisika?”
“Umemaliza kuzungumza?” Alvin
alienda mbele kwa hatua ndefu. Taa
nyeupe zilizokuwa juu zilimulika kwenye
mwili wake mzuri na ulio wima. Sura
yake tulivu ilijazwa na hali ya utawala
wa mtu ambaye alikuwa ameketi katika
nafasi ya juu kwa muda mrefu.
“KIM International haitafilisika.

Nitachunguza kwa kina suala la data
zilizovuja. Kuanzia sasa, kila meneja
mkuu katika kampuni anatakiwa
kuwajibika. Nikijua mvujishaji ni nani,
nitafanya maisha ya mtu huyo kuwa
kuzimu hai.”
Mkurugenzi Owens ghafla alidhihaki na
kusema, "Nafikiri Jack lazima awe ndiye
mvujishaji."
Nyuso za Lea na Jack zilibadilika. Lea
alisema kwa hasira, “Mkurugenzi
Owens, tafadhali usiwashtaki wengine
tu. Jack ni mwanangu.
Jina lake la mwisho ni Kimaro pia.
Hatawahi kufanya lolote kusaliti familia
ya Kimaro.”
“Ha! Jina lake la mwisho linaweza kuwa
Kimaro, lakini jina la mwisho la baba
yake ni Campos," Mkurugenzi Owens
alisema kwa hasira, "Takriban nusu
mwezi uliopita, mke wangu alimuoona

Jack, Mason, Maurice, na Jerome
kwenye nyumba ya kahawa."
Moyo wa Jack ulishuka. Alikuwa na
hisia mbaya. Hakufikiri kwamba kuna
mtu alikuwa amemwona wakati huo.
“Mkurugenzi Owens, ni kawaida kabisa
kwangu kunywa kahawa na baba na
Anko wangu. Tunakutana mara kwa
mara wakati wowote ninapoenda kwa
familia ya Campos— ”
"Sahau, Jack. Acha kujitetea.”
Mkurugenzi Owens alisema kwa hasira,
“Leo tu, nimepata taarifa fulani. Mwenye
hisa wa ajabu ambaye ana asilimia 60
ya hisa za Campos Corporation ni baba
yako, Mason Campos.
“Na hapa kuna jambo lingine. Saa moja
tu iliyopita, Landell Group ilitoa taarifa.
Tayari wanashirikiana na Campos
Corporation na kuwakabidhi hakimiliki

ya data za simu kwa Campos. Kwa
maneno mengine, ikiwa kampuni yoyote
nchini Kenya inataka kutumia
smartphone ya Landell Group, itabidi
iwatafute Kampuni ya Campos.”
"Hiyo haiwezekani." Wanahisa wengi
walishtuka.
Wanafamilia wa Kimaro walishtuka pia.
Lea, haswa, alishtuka kabisa.
“Hii haiwezekani! Mason anawezaje
kuwa mwenyehisa mkubwa zaidi katika
Kampuni ya Campos?”
“Nyinyi nyote ni wajinga sana! ”
Mkurugenzi Owens alifoka. "Mason ni
mtu mwenye tamaa. Yeye ni mzuri
katika kujificha kuliko kaka yake
Maurice na Jerome. Yeye ndiye mtu
mkubwa nyuma ya pazia. Atajidhihirisha
tu muda si mrefu kwa sababu familia ya
Campos inakaribia kuchukua nafasi ya
familia ya Kimaro kama yenye nguvu

zaidi hapa Kenya. Hana cha kuwa na
wasiwasi tena.”
"Huyo Mason anatisha sana." Valerie
alijisemea moyoni.
Spencer alivuta pumzi pia, akisema,
"Zaidi ya miaka 20 iliyopita, familia ya
Campos ilikuwa familia ndogo tu
ambayo haikujulikana sana hapa
Nairobi. Hawakuwa zaidi ya mchwa
machoni pa familia ya Kimaro. Kwa
kweli wanaipita familia ya Kimaro
sasa?”
Mzee Kimaro alifumba macho.
Alishusha pumzi ndefu baada ya
kugundua kuwa walikuwa
wamechelewa kufanya lolote sasa.
Familia ya Campos ilikuwa tayari
imeinuka wakati huo, na walikuwa
wameweka mipango yao kwa uangalifu
katika miaka kadhaa iliyopita.

“Jack ni mtoto wa Mason. Hisa za
Campos Corporation zitakuwa zake
katika siku zijazo. Kumsaidia Mason ni
sawa na kujisaidia mwenyewe.” Valerie
alimtazama Jack kwa hasira. “Jack,
ulivujisha data za siri za kampuni.
Unajaribu kuharibu familia ya Kimaro?"
“Sikufanya.” Jack akatikisa kichwa.
Alimtazama kila mtu, akishangaa.
Lakini, aliona tu kila mtu katika chumba
cha mkutano akimtazama kwa hasira na
kutomwamini. Macho yao yanaonekana
kana kwamba wanataka kumnyonga.
"Sikusaliti KIM International," Jack
alieleza tena, "Ndiyo, baba yangu
alinitafuta hapo awali, lakini
nilimkatalia."
Mwili wa Lea ulitetemeka. "Baba yako
alikuomba umvujishie data ya mradi wa
simu ya kampuni?"

Akiwa ametazamana na macho ya
mama yake ya kutokuamini, Jack
aliweza kutikisa kichwa tu. "Ndiyo,
aliniambia yeye ndiye mwanahisa
mkubwa zaidi katika Kampuni ya
Campos. Pia alijaribu kunishawishi kwa
kusema Campos Corporation itakuwa
yangu katika siku zijazo, lakini
sikukubali.”
Lea karibu kupoteza mwelekeo wake.
Ingawa tayari alihisi kwamba Mason
alianza kuwa tofauti kwake na mara
nyingi hakurudi nyumbani, hakuwahi
kufikiria kuwa mtu anayelala karibu
naye angekuwa wa kutisha kiasi hicho.
Miaka mitatu iliyopita, alimpa pesa
nyingi sana kusaidia kampuni ya
Campos. Baada ya kugundua kuwa
alidanganywa, alichukia. Hasa
alipokumbuka nyakati zote alizoisaidia
Campos Corporation katika makumi ya
miaka, Hakuwahi kufikiria hata siku

moja kwamba mume wake angekuwa
mtu wa tamaa sana. Watu wanaweza
kuwa na tamaa, lakini wanapaswa kuwa
na dhamiri na kujua mipaka yao pia. Ni
mwanaume wa aina gani alipendana
naye? Je, Mason hakuwahi kuwa mtu
mpole na mnyenyekevu? Je, alikuwa
ameficha rangi zake za kweli kwa kiasi
gani?
Sura ya: 499
"Dada, ulimpenda mwanaume wa aina
gani?" Valerie alikemea, “Kwa sababu
ya mtu huyu, ulisisitiza kumtaliki Mike
Tikisa wakati huo. Umealika shida kwa
kusaidia Campos Corporation.
Umesababisha hata mtoto wa Mason
aibe data ya simu! ”
Uso wa Lea ulikuwa umepauka, na
hakuweza kusema neno lolote. Alikuwa
fahari ya familia ya Kimaro, lakini sasa
alikuwa na jukumu la kubeba lawama za

uharibifu wa KIM International. Ndiyo,
alikuwa mjinga. Alikuwa mjinga wa
ajabu kwa kumpenda mtu mbaya kiasi
kile. Alikuwa kipofu!
“Aunty Valerie, ngoja nirudie hili.
sikufanya hivyo.” Jack alisisitiza.
“Hukufanya hivyo?” Valerie alimtazama
kwa dharau. “Jack, wewe ni mwanangu.
Sitaki kukushuku pia, lakini siamini
kuwa huna hatia. Hujawahi kuridhika
kumzunguka Alvin. Baba yako ndiye
mwenyehisa mkuu wa Campos
Corporation. Kwanini usichukue hatua
kwa kipande kikubwa cha keki?
Kampuni ya Campos itakuwa yako
mapema au baadaye.”
“Hiyo ni kweli, Jack. Usituchukulie
wajinga. Wewe ni meneja mkuu tu
katika KIM International. Bado kuna
Alvin juu yako. Kwa upande mwingine,
katika Campos Corporation, wewe ni

mtoto wa pekee wa Mason. Una future
kubwa huko. Zaidi ya hayo, Alvin
hakuwepo kwenye kampuni siku hizi.
Wewe, kama meneja mkuu,
unasimamia masuala yote ya uongozi
katika KIM International. Pia uliingia na
kutoka kwenye maabara. Haiwezi kuwa
mtu mwingine yeyote kama si wewe.”
"Usiseme zaidi. Piga simu polisi."
Jinsi Wanahisa walivyojadili, ndivyo
walivyozidi kumchukia Jack. Mtu
mmojahata akaenda mbele na
kumsukuma.
Makamu mkuu wa meneja alisimama
vilevile, akisema, “Jack, nimekuwa
nikikushuku kwa muda mrefu. Ulikuwa
na shauku kubwa ya kuchukua jukumu
la taratibu zote za kutia saini mradi wa
Kilimanjaro Smartphone. Hukuturuhusu
kuingilia mambo mengi pia. Ulisema
unataka kuifanya mwenyewe na hata

ukatukumbusha kuwatupia macho watu
wanaofanya kazi chini yetu ili kuepusha
data za kampuni hiyo kuvuja. Kwa kweli,
ulikuwa unajaribu tu kuficha matendo
yako kwa kusukuma lawama kwa
wengine, sivyo?”
"Makamu Meneja Mkuu, ulichosema ni
kweli?" Alvin alimtupia jicho kali mtu
huyo.
"Mkurugenzi Kimaro, ni kweli kabisa,"
Makamu wa Meneja Mkuu alisema,
"Jack hakuturuhusu sisi wasimamizi
wakuu kushughulikia masuala
yanayohusiana na simu siku hizi.
Alisema ni yeye ndiye anayesimamia
kwa vile haukuwepo.”
Uso wa Jack ulibadilika sana. Alipotaka
kusema kitu, kofi kali lilimtua usoni.
Aligeuza kichwa chake na kuona uso
wa hasira wa Spencer. Moyo wake
ulihisi uchungu. “Mjomba — ”

"Jack, wewe ni mwenye dhambi wa
familia ya Kimaro." Spencer
alimuelekezea kidole huku akitetemeka.
“Wewe ni sawa na baba yako, siku zote
unafikiria kuwadhuru wengine. Ikiwa
kweli unajisikia hatia kwa hili, tangaza
jambo hili kwa umma."
“Ninawezaje kutangaza ikiwa
sikuifanya?" Jack alifoka kwa hasira.
Alimtazama kila mtu, na wote walikuwa
wakimtazama kwa macho ya kutoamini.
Hata Mzee Kimaro, Valerie, Alvin, na
Lea walikuwa na mashaka naye.
“Mama, hata wewe huniamini?” Jack
alikuwa na uso wa kukata tamaa. "Mimi
ni sehemu ya familia ya Kimaro.
Sitafanya lolote kusaliti KIM
International.”
“Jack...” Lea alimtazama. Aligundua
kuwa asingeweza kumtetea mtu yeyote
kwa hisia zake pekee. Hapo awali

alisema kwa ujasiri kwamba Mason
hakuwa na hatia, lakini ukweli ulimpiga
usoni.
“Mpeleke kituo cha polisi. ” Alvin ghafla
alimuamuru Ganja aliyekuwa
amesimama nyuma yake kwa ukali.
“Jack, nitalichunguza suala hili hadi
mwisho. Nikigundua kuwa wewe ndiye
uliyefanya hivi, nitafanya maisha yako
kuwa jehanamu hai.”
Jack alihisi baridi mwili mzima. Kabla
hajajua, Ganja na wanachama
wachache wa ONA walikuwa wakimtoa
nje. Hatimaye fujo hiyo ilifikia mwisho.
Lakini, maneno ya kila mtu bado
yalikuwa chini.
Alvin aliwatazama na kusema kwa sauti
kavu, “Ni usiku sana. Ninyi nyote
mnapaswa kurudi mkapumzike.”
Mkurugenzi Owens alitabasamu kwa

uchungu. "Tunawezaje kulala wakati
jambo zito limetokea?"
Alvin alisisitiza midomo yake pamoja.
“Miaka yote, KIM International imepata
misukosuko na misukosuko pamoja na
changamoto nyingi.
Lakini, KIM International daima
imesisitiza uaminifu. Kwa kuwa KIM
International imekiuka mikataba, nitalipa
fidia kwa washirika wetu wa biashara.
Ikiwa hakuna pesa za kutosha, nitalipa
kiasi kilichobaki mwenyewe.
Ikishindikana, nitachukua lawama zote
na kujiuzulu.”
Aligeuka na kuondoka baada ya
kusema.
Hata hivyo, hakuondoka kwenye
kampuni hiyo. Alienda ofisini kwenye
ghorofa ya juu moja kwa moja.
Muda mfupi baada ya kuketi, Hans
aliingia ndani haraka na kusema,
"Bwana Mkubwa, Mzee Kimaro alizimia

baada ya kutoka nje ya chumba cha
mkutano."
Alvin alichanganyikiwa. Mara
akasimama na kwenda hospitali.
Hospitalini, baada ya kumuokoa Mzee
Kimaro, daktari alisema mzee huyo
alikuwa overstimulated, ambayo
ilisababisha thrombosis ya venous ya
ubongo. Angepooza katika siku chache
baadaye. Hii bila shaka ilikuwa sawa na
kuongeza tusi kwa jeraha kwa familia ya
Kimaro.
Valerie alikasirika na kuanza kupigana
na Lea hapohapo. “Yote ni makosa
yako, Lea! Angalia ulichofanya.
Mwanzoni, ulipata mume msaliti. Halafu
hao wana wawili uliozaa nao wana
matatizo. Mmoja wao aliiba siri za
kampuni, huku mwingine
akimnyang'anya mke wa mtu mwingine.
Baba siku hizi hana hali nzuri.
Alipoenda kuvua samaki, alikejeliwa na

wengine waliosema familia ya Kimaro
haina maadili. Sasa hata amepooza
baada ya kuwakasirikia nyie.”
Spencer alijiinamia pembeni kama mtu
aliyekosa uhai. Aliwaacha wapigane
walivyotaka, huku akiwa ameduwaa.
Lea alimruhusu Valerie ampige pia. Akili
yake ilikuwa inamzunguka. Karipio la
Valerie lilikuwa kama mijeledi ikitua juu
yake, na alihisi kana kwamba maisha
yake yote ni mzaha. Kama mke,
alichagua mume asiyefaa na kuidhuru
familia ya Kimaro. Akiwa mama,
hakuwafunda wanawe ipasavyo.
Alifunika uso wake na kulia kwa
uchungu.
Alvin akaunyosha mkono wake na
kuusimamisha mkono wa Valerie. "
Inatosha, hii ni hospitali. Ukiendelea
kuwa na fujo na kelele, ninaweza
kuwaambia walinzi wakutoe hapa.”

“Alvin, una haki gani ya kuingilia kati?
Unakaribia kuwa si chochote tena. Mtu
tajiri zaidi wa Kenya? Haha, punde
itakuwa hadithi tu. Jack anakaribia
kuchukua nafasi yako. Lo,, anaweza
kubadilisha jina lake kuwa Jack
Campos, haha!”
Valerie alianza kulia na kukemea. Alvin
alibana midomo yake kwa nguvu.
Ghafla, Yvette alikimbia huku akilia.
"Jamani, hali ni mbaya sana. Willie naye
alikamatwa! ”
Spencer aliposikia hivyo alishtuka. “Ni
nini kimetokea kwa Willie?”
Yvette alilia huku akisema, “Alienda baa
kunywa usiku na kukutana na mke wa
Given Campos. Alilewa na kujaribu
kumnyanyasa. Matokeo yake,
alichukuliwa na Given.”

Spencer alijikwaa hatua chache nyuma.
Willie alikuwa mwanawe wa pekee.
Valerie alikemea, “Kaka umemdekeza
vipi mwanao? Tatizo kubwa limetokea
katika familia ya Kimaro, lakini Willie
alikuwa kwenye baa kumdhalilisha mke
wa mtu mwingine?”
Spencer alikuwa katika hali mbaya
kimawazo. “Hili haliwezekani. Ni kweli
kwamba Willie alikuwa mjinga hapo
awali na alifanya mambo mengi
mabaya. Lakini, baada ya kurudi kutoka
Dar es Salaam miaka mitatu iliyopita,
amebadilika sana. Hata alikuwa na rafiki
wa kike anayefaa wakati fulani uliopita.”
“Ni familia ya Campos,” Yvette alisema
kwa hasira, "Lazima uwe mtego wa
familia ya Campos. Vinginevyo, Willie
angewezaje kukutana na mke wa Given
Campos kwa bahati mbaya hivyo?”

Maneno yake yalimkumbusha kila mtu
wa Kimaro kilichokuwa kinaendelea.
Given alikuwa binamu wa Jerome.
Sura ya: 500
“Je! Familia ya Campos ina kinyongo
nasi?" Spencer alikasirika. "Sio tu
kwamba waliiba data ya simu ya KIM
International, lakini hata wanataka
kumdhuru mwanangu sasa. Huku si
kutokuwa na shukrani tu, bali ni unyama
uliopindukia.”
“Acha kupiga kelele! Kumuokoa Willie
ndio kipaumbele sasa. ” Yvette alibanwa
na machozi. “Willie alikuwa amelowa
damu kutokana na kupigwa.
Amejeruhiwa sana. Nina wasiwasi
hataweza kuvumilia ikiwa tutachelewa
sana. Alvin, nakuomba. Kwa haraka
waambie wanachama wa ONA
kuangalia mahali Willie alikopelekwa.”

“Aunty Yvette, usijali. Nitaomba mtu
ashughulikie sasa hivi.” Kichwa cha
Alvin kilikuwa kinakaribia kupasuka.
Shida za kampuni bado hazijatatuliwa
na Mzee Kimaro alikuwa na hatihati ya
kupooza na alikuwa hajatoka kwenye
chumba cha dharura bado, lakini kuna
kitu kilikuwa kimetokea kwa Willie!
Mambo yalikuwa yakitokea moja baada
ya jingine kana kwamba kulikuwa na
nguvu isiyoonekana ikilenga familia ya
Kimaro nyuma ya pazia.
Alvin aliishiwa nguvu. Lakini, alijua
kuwa yeye pekee ndiye angeweza
kusaidia familia ya Kimaro wakati huo.
Punde, wanachama wa ONA
waligundua kwamba Willie alikuwa
amelpelekwa kwenye jumba la kifahari
la Given Campos.
Alvin aliandamana na baadhi ya watu
wa ONA kwenda huko. Walipofika
kwenye jumba hilo la kifahari, Willie

alikuwa tayari amelala chini na kupoteza
fahamu.
Kichwa chake kizima na uso wake
ulikuwa umejaa damu.
“Samahani, Bwana Mkubwa Kimaro.
Umechelewa sana kuja.” Given
alitabasamu kwa fujo huku akichukua
rundo la pesa na kuzitupa kwenye mwili
wa Willie. "Halo, hii ni kwa ajili ya ada ya
matibabu. Sikutaka kukufidia mwanzoni,
lakini mimi ni mtu anayetii sheria.
Ninajua kwamba lazima nifidie kwa
kumpiga mtu.
Dola 20,000 zinapaswa kutosha
kumtibu.”
"Ivan, unawezaje kuthubutu kuongea na
Bwana Kimaro kwa njia hii? Lazima uwe
na hamu ya kifo." Ganja akamshika
Given kwa nguvu.
Hata hivyo, kundi kubwa la watu liliingia
kwa haraka kutoka nje na kuwazunguka

Alvin, Ganja, na wengine.
"Bwana Kimaro, huwezi kumpiga
binamu yangu." Jerome aliingia kutoka
nje. Alikuwa na sura ya kiburi aliposema
hivyo, “ Willie ndiye aliyemnyanyasa
shemeji yangu kwanza.
Isitoshe, Willie hakuwachafua
wanawake wengi wazuri hapo awali
hhapa Nairobi? Anastahili hata kama
atakuwa amekufa."
"Willie alibadilika kitambo. Ni lazima tu
ziwe ni njama zenu za makusudi hizi. ”
Alvin alisema kwa utulivu.
Hapo zamani, Jerome hakuwa chochote
ila mzaha tu kwa Alvin. Given alikuwa
hata mtu ambaye Alvin asingeweza
hata kuzungumza naye. Sasa, watu
hawa walikuwa wanaanza kuwaonea
watu wa familia ya Kimaro?
“Unasema tumemfanyia njama lakini

una ushahidi?” Jerome aliuliza huku
akitabasamu, “Kila mtu anajua kwamba
ninyi, watu wa familia ya Kimaro, mna
tabia mbaya ya kuwanyanyasa
wanawake. Je, wewe si hivyo pia,
Bwana Kimaro? Ulimpokonya mke wa
mtu kwa nguvu. Tsk, mke wa mtu
mtamu eeh? Hakika hii ni tabia mbaya
sana.”
"Lisa amekuwa mwanamke wangu kila
wakati." Umbo kubwa la Alvin lilitembea
kuelekea kwa Jerome hatua kwa hatua.
Macho yake meusi yalijawa na kiza.
Wakati huo huo, sura ya ukali ilimfunika.
Baadhi ya watu walizaliwa na heshima,
kama Alvin. Jerome hakuwa na sifa aina
hiyo ya sura.
Alvin alipopita, Jerome alipiga hatua
mbili nyuma. Akawaacha wanausalama
wake wamkinge mbele.
“Alvin, unajaribu kufanya nini?

Ninakuonya, familia ya Kimaro sivyo
ilivyokuwa. Kuanzia sasa na kuendelea,
familia kuu nchini Kenya itakuwa ni sisi,
familia ya Campos. Familia ya Kimaro
hata haitashika nafasi ya pili au ya tatu.
Hah, mnaweza hata kuwa familia duni
zaidi hapa Kenya. Je, kweli unafikiri
wewe bado ni bwana mdogo tajiri zaidi
ambaye unaweza kufanya lolote
upendavyo?” Jerome alimdhihaki kwa
sauti kubwa, “Mbali na hilo, ukweli
kwamba ulimpokonya mke wa mtu
mwingine ni kinyume cha sheria.
Unafikiri unaweza kusimama hapa na
kuendelea kuwa na kiburi hadi lini?”
Mwili mzima wa Alvin ulitetemeka kwa
hasira.
Wakati huo kundi kubwa la polisi liliingia
mlangoni. Afisa wa polisi alichunguza
hali katika nyumba hiyo. Baada ya
hapo, alienda moja kwa moja kwa Alvin.
“Alvin, Kelvin na Joel wamekuripoti kwa

utekaji nyara wa Lisa Jones. Tafadhali
twende kituo cha polisi pamoja nasi kwa
uchunguzi."
"Hah, nilichosema kinageuka kuwa
kweli, huh?" Jerome alifurahishwa na
hali ya Alvin. “Bwana mdogo tajiri wa
Kenya? Hili pia litabadilika hivi karibuni.”
Alvin alimtazama Jerome bila kujieleza.
Ghafla, alielewa kitu. “Una uhusiano
gani na Kelvin?”
"Hakuna uhusiano mkubwa kati yetu. Ni
kwamba tunashiriki adui mmoja.”
Jerome aliinua uso zake. "Mbali na hilo,
ikiwa hatachukua nafasi hii kumrudisha
mke wake, basi yeye ni mjinga."
Alvin alisisitiza midomo yake pamoja.
Ingawa kile Jerome alisema kilikuwa na
mantiki, alihisi kwamba haikuwa rahisi
hivyo. Kwa wakati huu, ni kana kwamba
alikuwa ameanguka kwenye kimbunga.

"Alvin, tufuate." Polisi wakamfunga
pingu. “Ulimteka nyara Lisa hadharani
pale hotelini na hakuna mtu aliyeweza
kuwasiliana na Lisa baada ya hapo.
Kuna mashahidi na ushahidi wa
kutosha. Unapaswa kufika kituo cha
polisi mara moja na kutuambia kuhusu
mahali alipo Lisa.”
“Bwana Mkubwa...” Ganja alimtazama
Alvin kwa wasiwasi.
"Mpeleke Willie hospitali mara moja."
Alvin alimtazama Willie aliyekuwa
amelala kwenye dimbwi la damu.
Alikuwa na wasiwasi kwamba Willie
asingekuwa kama kawaida kwa damu
zote alizopoteza hata baada ya kuamka.
Alvin alipompita Jerome, alimpiga jicho
kali sana. "Jerome Campos, mtu nyuma
yako ni Mason, sawa? Sitawaacha ninyi
nyote kutoka kwenye ndoano.”

Mtazamo huo ulimfanya Jerome
aogope, lakini upesi akahisi kutulia.
Familia ya Kimaro ilikuwa imekwisha
kabisa. Hakukuwa na jinsi ya
kubadilisha hali hiyo hata kama Alvin
binafsi angechukua hatua. Kisha, familia
ya Campos ilihitaji tu kushindana dhidi
ya ONA.
Ganja haraka akampeleka Willie katika
hospitali ya familia ya Choka. Spencer
na mkewe walikimbia kwa haraka.
Baada ya Willie kuokolewa, daktari
alisema, “Mgonjwa hayuko tena katika
hali mbaya. Hata hivyo, kichwa chake
kilijeruhiwa vibaya na kupoteza damu
nyingi. Pia aliletwa hospitali akiwa
amechelewa. Atakuwa... amedumaa
kiakili siku zijazo. ”
"Ulemavu wa akili?" Yvette alizimia
mara moja kutokana na mshtuko.

Spencer naye alipigwa na butwaa.
Hakutarajia mwanawe wa pekee
angekuja kuwa taahira siku za usoni.
Moyo wa Lea ulikuwa mnyonge pia.
“Spencer—”
“Funga mdomo wako!” Spencer
alimpiga kofi kali usoni mwake. Alikuwa
Karibu kupandisha kichaa kutokana na
hasira. “Ni kosa lako. Wewe ndiye
ulisisitiza kusaidia familia ya Campos
wakati huo. Wewe ndiye uliyetaka
kuolewa na Mason. Wewe ndiye
uliyesaidia familia hiyo ya wasaliti hadi
leo. Umesababisha Willie wetu adhurike
pia! Sina dada kama wewe.”
ITAENDELEA LISA KITABU CHA 11

ONYO: Ni marufuku kusambaza, kukopi wala kuuza kazi hii kwani endapo kama tutakubaini basi sheria itachukua mkondo wake (By: Official Dully)
 
Dah Kimaro family imeingia cha kike kwa wahuni compos ngoja tuone geneous Alvin akipindua meza...... Me nawaangalia tu nipo paleee.........[emoji190]
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] sema me namkubali sana alvin[emoji16][emoji119] eniweeii mwandishii yupo vizurii sanaa
 
Ngojaa huko mbelee utaona show yake jamaa ni falaa ila ana roho mbayaa aiseee mali na madaraka ni vitu vibaya sana[emoji119][emoji174]
Atakutana na watoto wa kihuni wenye Kenya yao mpaka sasa hivi kapigwa KO kwa kuchukuliwa mke mchana kweupe
 
Hii kambi inakalika kweli waungwana! Nisije nikakaa nikaanza kupata majaka ya moyo maana hua hazikamiliki
 
Back
Top Bottom