Simulizi, Mikasa, Vitimbi na Visa vya wasanii wa zamani wa bongo fleva - A special thread

Simulizi, Mikasa, Vitimbi na Visa vya wasanii wa zamani wa bongo fleva - A special thread

Kwa watoto wa 2000.... Jide na Ray C waliwahi kuwa na beef la kimuziki kama Nandi na Zuchu au Mondi na Kiba... Pia Hadija Kopa mamake Zuchu aliwahi kuwa na beef na Nasma Hamisi Kidogo huyu ni Almareuhum Kwa Sasa.........
 
View attachment 3211241

Taji Liundi mtoto wa kishua ambaye alinisurika kifo baada ya kunyweshwa sumu na mama yake mzazi.

Ndio mtangazaji wa kwanza kupiga nyimbo za wasanii wa Bongo kwenye radio mwaka 1994 akiwa Radio One.

Neno “Bongo Flava” lilitajwa kwa mara ya kwanza na Mike Mhagama 1996 kupitia kipindi cha “DJ Show” ili kutofautisha harakati za wana hip-hop na RnB wa Bongo, na wale wa Marekani.


Respect kwa Master T

View attachment 3211241

Taji Liundi mtoto wa kishua ambaye alinisurika kifo baada ya kunyweshwa sumu na mama yake mzazi.

Ndio mtangazaji wa kwanza kupiga nyimbo za wasanii wa Bongo kwenye radio mwaka 1994 akiwa Radio One.

Neno “Bongo Flava” lilitajwa kwa mara ya kwanza na Mike Mhagama 1996 kupitia kipindi cha “DJ Show” ili kutofautisha harakati za wana hip-hop na RnB wa Bongo, na wale wa Marekani.


Respect kwa Master T
Mtu wa kwanza kulitumia neno bongo fleva anaitwa SANDE SINGO SHOMALI. Ktk kipindi Cha radio one dj show, hapo studio alikuwepo yeye (Sande shomali) na SEBASTIANI MAGANGA.
Na haswa baada ya kuucheza wimbo wa UNIQUE SISTERS, wakaulizana huu muziki wa wasanii was Tanzania tuuitaje? Ndipo wakalipata jina BONGO FLEVA.
NA muziki wa kwanza wa bongo fleva kusikika redioni, NI ngoma ya TWO PROUD (Mr 2) inayoitwa NI Mimi, kiitikio chake kipo hivi ; nipo KWENYE maikrofoni, hata unipe Nini sitamani sioni, NI Mimi.
Dj aliyeucheza huo wimbo simkumbuki, kipindi hicho mzee JULIUS NYAISANGA alikuwa NI mkurugenzi wa vipindi pale redio one, anko J aliingia studio na kumzuia huyo dj asiucheze huo wimbo. Dj akaukatisha huo muziki
Baada ya hapo simu za wasikilizaji zilikuwa NI nyingi wakiuomba huo wimbo
 
View attachment 3211245

Mwaka 2001 kundi la Gangwe Mob kutokea Temeke wanazindua brand yao ya nguo, iliyoitwa Gangwe Gear. Walitengeneza T-shirts, full jeans na kofia zenye chapa yao.

Gangwe Mob iliundwa na wasanii wawili Inspecta Harun na Luteni Kalama na wimbo wao wa kwanza kuwatambulisha kwenye game ni Mtu Bee kabla hawajatoa Ngangari wimbo uliokuwa hit mtaani.

Gangwe Mob ni kundi lililopata bahati ya kuwa na management nzuri ya Sebastian Maganga ambae kwa sasa ni mfanyakazi kwenye Clouds Media.

Waliuza album yao Simulizi la Ufasaha kwa MAMU shilling Million 30 na ilibidi wapokee cash sababu hawakuwa na akaunti ya benki wakabeba pesa kwenye kikapu na wakatembea peku kuofia kuvamiwa.

Pia Gangwe Mob wana historia ya kukataliwa Mpwapwa kwa kuwa mashabiki walihisi ni Gangwe Mob feki walifanyiwa fujo na show yao iliharibika, zamani wasanii hawakuwa na video hivyo usipotokea kwenye magazeti inakuwa ni ngumu mashabiki kukufahamu.
Hii story hadi leo ukienda mkoani Dodoma pale wilayani Mpwapwa ipo. Siku nilihadithiwa nilicheka sana kwa maana zamani mtu ulikuwa unaweza kwenda mkoani ukaandaa show na kusema mimi nifulani na ukumbi ukaitika.
 
images (17).jpeg


Mtoko wa Juma Nature

Mara ya kwanza kabisa Juma Kassim Nature anaingia studio ilikuwa ni studio za Sound Crafters kwa Enrico, alikwenda kurekodi wimbo wa kundi alilokuwa anaunda yeye na swahiba wake Dollo. Kundi ili liliitwa FSG lilikuwa na wasanii wawili tu yeye Juma na Dollo.

Wimbo waliorekodi uliitwa ‘Wimbi la Njaa’

Chorus yake inaenda, ‘’Wimbi la njaa matatizo umasikini, Chanzo cha nguo kupwaya kufunga na pini’’.


Baada ya hapo Juma Nature akawa maarufu mitaani kwa sababu ya kushirikishwa na makundi mbalimbali ya Temeke kama Wandava ya King Sepeto, Joint Mobb ya Rich One, Manduli, ZigZag Crew etc na kila aliposhirikishwa aliua sana.

Nature akakutana na P Funk na P akaonesha interest ya kumsaini Bongo Records/Sound Solutions ila ikawa nenda rudi kwa kuwa P alikuwa bado na mashaka haswa kuhusu style ya Nature kama inaweza kuwa biashara maana P alikuwa anapata shida sana kuelewa Kiswahili anachotumia Nature kwenye mistari yake. Kama mnavyojua P kalelewa maisha ya kizungu na kipindi hicho anatoka mtoni bado wamoto.

Siku moja Nature alienda Bongo Records kurekodi wimbo alioshirikishwa na Mabaga Fresh kundi lililoundwa na DJ Snox na JB Mkuu wa Majaji aka Mbuzi wa Al badir. Studio walikuwepo Mabaga, yeye, P Funk na alikuwepo Bon Luv kama prodyuza mualikwa.

Hii ndio siku ambayo P alifanya maamuzi rasmi ya kumsaini Juma Nature kama msanii wa Bongo Records na mipango yote ya album ilianzia hapa.

Ilikuwaje?? Bon Luv baada ya kumsikia Nature anaingiza verse yake kwenye ‘Mtulize’ alipagawa ikabidi amuulize mara mbili mbili P Funk kama anaelewa hii talent ilivyo kubwa na anampango nae gani. Ndio Majani akafanya maamuzi ya mwisho na kilichofata baada ya hapo ni historia.
 
20250130_163955.jpg


Solo Thang AKA Ulamaa anatekwa na Kikosi cha Mizinga


Kuna wimbo wa Solothang unaitwa Ndugu Zangu, Solo anasema, ‘’Nishatekwa na Kikosi na sitolipa kisasi’’.

Ni stori ya kweli, Solo alitekwa na kundi la Kikosi cha Mizinga lilikokuwa linaonngozwa na rapa mbabe Kalapina.

Unaweza kuwa unajiuliza ilikuwaje Kikosi cha Mizinga wakamteka Solo? Tumezoea siku hizi kusikia stori za wasiojulikana ndio wanafanya utekaji.

Lakini enzi hizo ubabe, undava, uhuni na vurugu zote ilikuwa ni jambo la kawaida kwa makundi ya wasanii wa rap.

Sababu haswa ya Solo kutekwa ni bifu alilokuwa nalo P Funk na Kikosi cha Mizinga na chanzo cha bifu ni ubabe tu hakukuwa na sababu ya maana sana iliyofanya Kikosi wapishane na Majani.

Solo alikuwa ni msanii wa Bongo Records ya P Funk Majani na alikuja na style iliyokuwa inafanana na Hashim Dogo member wa Kikosi.

Mtaani kukazuka maneno kwamba P anamtengeneza Solo kama replacement ya Hashim Dogo aka Mwendawazimu.

Wakati huo Hashim alikuwa ni rapa anayeheshimika sana mtaani na anakubalika na mashabiki wa gangsta rap ila hakuwa anatambulika sana kwenye mainstream.

Bongo records waliachia wimbo unaitwa ‘Bongo Chelea pia’ ambao ndani ya huo wimbo kuna mistari Solo Thang anasema ‘Tunasonga kama Dogo na Pina’.
Huu mstari ndio ulikuja kuleta tafarani ya kutafutana mtaani mpaka kutekwa kwa Solo.

Kwa nini? Kalapina na Hashim walikuwa na wimbo wamerekodi muda mrefu kwa Majani unaitwa Tunasonga.

Huu wimbo P Funk aliuzuia kutoka sababu ya mgogoro wake na Kikosi.

Sasa Solo kutumia wimbo wao ambao haujatoka kwenye mistari yake, Kikosi walitafsiri anafanya kusudi ku-pre empty wimbo wao na kuondoa exclusiveness.

Walichukulia hii kama vita na Bongo Records na Solo ndio anatumika kuwashambulia.

Hii bifu ilikuwa mbaya ila ilikuja kumalizwa kindugu. Baadae katika kutunishiana misuli Solo na Pina walikuja kugundua wao ni ndugu kabisa na wakaitwa kupatanishwa na familia.
 
20250130_170016.jpg

Albert Mangwea

Albert Mangwea rapa mkali kabisa kuwai kutokea kwenye hii ardhi ya Tanzania.

Mangwea kipindi cha uhai wake alipendwa sana sababu ya ukubwa wa kipaji chake, alikuwa anaweza kuchana, kuimba na ku-free style na alifanya haya kwa lugha zote Kiswahili na Kinyamwezi.

Mangwea alipendwa na mashabiki wa muziki lakini alipendwa zaidi na wasanii wenzie wa bongofleva sababu ya lifestyle yake, mtu poa, rafiki, mcheshi na anaependa kufurahi muda wote.

Tulimpoteza Ngwea kwa matumizi wa kupitiliza ya madawa ya kulevya ‘overdose’. Mungu Amlaze Pema.

Ilikuwaje Mangwea akaingia kwenye maisha ya ulevi wa kupindukia na mwishoni akaangukia kwenye madawa ya kulevya?

Ngwea kwa muda mrefu sana alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kukosa usingizi. Huu ugonjwa ulimsumbua sana kwa muda mrefu, licha kuangaika huku na kule kutafuta tiba lakini akufanikiwa.

Ilikuwa ni kawaida Ngwea kukata wiki au zaidi hajapata usingizi, yani ni asinzii kabisa hata afanye nini, huu ni ugonjwa unaosumbua wasanii wengi hata msanii fulani mkubwa sana nchini analo hili tatizo (stori ya siku nyingine).

Mangwea alikuwa alali na alikalala unaweza kusema amekata roho anapotea kabisa ulimwenguni.

Hivyo ili kupata usingizi akajikuta ameingia kwenye matumizi makubwa ya pombe na ikampelekea kuingia kwenye kula nyeupe.

Rest in Peace Alberto!
 
FB_IMG_1737997422253.jpg


Yamenikuta, yamenikuta, yamenikuta mzee mwenzangu

‘Yamenikuta’ ni moja ya nyimbo kubwa kuwai kutokea kwenye kiwanda cha muziki Tanzania.

Huu wimbo ulikuwa hit mitaani bila msaada wa social media wala promo ya radio. Ulilia kila kona ya nchi vijana walikuwa wanaimba mashairi yake.

Wimbo ni wa kundi la GWM lililohasisiwa na masela watatu kutoka Temeke, Easy Dope, D Chief na KR. Kundi hili lilianza rasmi mwaka 1993 likiwa na ndugu wawili ambao ni mapacha Richard Makala [Easy Dope] na Robert Makala [D Chief]. KR alikuja kuongezeka baadae .

Yamenikuta ni wimbo wao maarufu Zaidi ambao walimshirikisha 2 Proud kwa sasa Mr II aka Sugu ulirekodiwa na Bon Luv. Ila wana nyimbo nyingi zilizokuwa maarufu kitaa na mainstream kama ‘Cheza mbali na kasheshe’ na ‘Kamua’.
Lilikuwa ni kundi lenye exposure kubwa ya muziki kuanzia kwenye kuandaa catalog, videos na shows.

Kama waswahili wanavyosema maneno uwa yanaumba, inawezekana yameumba kwa vijana awa wa GWM, Easy D na D Chief maana kwa sasa wote wamepatwa na ugonjwa wa kurukwa akili.

Inasikitisha sana story yao maana wanavyosema mtaani ni kuwa chanzo cha matatizo yao ni ugomvi wa nyumba ya urithi iliyopo Temeke hivyo kuna ndugu zao wamewachezea.
 
Back
Top Bottom