Elton Tonny
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 396
- 2,976
- Thread starter
-
- #421
MIMI NA MIMI 2
A Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA KUMI NA TISA
★★★★★★★★★★★★★★★★★
Ukimya ukaendelea kuijaza sehemu hiyo ya sebule kana kwamba hakukuwa na watu, maana mimi na Festo tuliendelea kuangaliana na kisha kubadilishana macho na bibie Miryam pia, ikiwa kama vile sote tunasubiri mmoja wetu ndiyo aseme kitu fulani. Na Miryam ndiye akaona avunje hali hiyo yenye utata.
"Karibu Festo," akamwambia hivyo na kutoa tabasamu nililoona lilikuwa la kujilazimisha.
Festo akatabasamu kiasi na kusema, "Asante. Nimefikia pazuri leo, mambo yako moto."
Miryam akatabasamu kiasi pia na kuangalia chini.
"Nani anazaliwa?" Festo akamuuliza hivyo.
"Ni mama," Miryam akamjibu.
"Oh, ni nzuri... sema sikuwa nimepata mwaliko, ningekuja kwa utayari ahah..." Festo akasema hivyo.
"Haina shida. Tayari umeshafika," Miryam akamwambia hivyo.
Jamaa akatabasamu tu, na yeye Miryam akawa ameweka uso ulioonyesha hisia za uajabu-ajabu tu.
Festo akanitazama na kusema, "Habari yako?"
"Safi. Karibu," nikasema hivyo kiutulivu.
"Asante," akaniambia hivyo, huku akikaza macho yake kwangu kama kunipa maana fulani ambayo sikuielewa, ila kama ananiambia 'ondoka.'
Nikamtazama Miryam, yeye akiwa anasogelea sofa ili akae, nami nikasema, "Miryam, me naenda."
Miryam akasitisha kuketi kwanza na kunitazama tu usoni.
"Nitarudi baadaye kidogo, ngoja nikupishe we' na mgeni," nikamwambia hivyo.
Miryam akatikisa kichwa kukubali na kutazama pembeni tena, bado akionekana kutatizika yaani, naye akamwambia Festo, "Karibu ukae Festo."
Nikamtazama Festo, naye akakaa kwa raha zote pamoja na bibie hapo sofani kwa kilichoonekana kuwa maongezi ambayo yangeenda vizuri baina yao, nami nikaamua kujiondokea hapo tu kama sina maana yaani. Kumwona jamaa hapa kulikuwa kumenizidishia hisia mbaya zaidi ya ile iliyokuwa imeniingia muda mfupi nyuma, lakini sikutaka kujiumiza mno kwa kuwaza juu yake, sema ni ile tu kujua kuhusu mambo mengi kumwelekea ndiyo kuliipa akili yangu mkereketo kiasi ulioendelea... yaani kunikereketa. Ilikuwa nje ya uwezo.
Nikafika ndani kwa Ankia na kukaa tu sofani, nikijaribu kujituliza kiakili na kihisia, lakini fikira zikawa zinalazimisha niwaze kuhusu nini ambacho mwanaume huyo angekuwa amekuja kuzungumza na bibie. Maana hakuwa amealikwa. Hata kale kahisia ka wivu kalikuwepo kabisa, nikitamani nirudi huko kujipitisha tu ili nijue ama nione yaliyoendelea, lakini huo ungekuwa ni upuuzi kwangu.
Nikaona tu nifanye mambo mengine ili kupisha muda kwanza, na jambo la mwanzo ikawa kuchukua simu yangu na kumpigia mama.
★★
Baada ya dakika kadhaa za kuongea na mzazi wangu, nikaona ni busara nikiingia bafuni kujimwagia kidogo, shauri tu ya kuhisi joto mno. Katika maongezi niliyofanya na mama nilikuwa nimemjulisha kwamba kesho ndiyo ningekwenda huko nyumbani ili kumsalimia, na ningeambatana na Mariam pamoja na kaka yake. Kwa hilo mama akakubali, na bila shaka angejiandaa kutupokea vizuri maana alikuwa mpenda wageni sana.
Nilipotoka bafuni na kurudi ndani nikakuta Ankia akiwa amerejea hapa kwake tayari. Tena alikuwa pamoja na rafiki yake mwingine aliyetoka naye huko Mzinga, mwanamke mtu mzima kama mama Chande tu aliyependeza kweli kwa namna ambavyo alivaa, nami nikawasalimu vizuri na kwenda kuvaa nguo safi na kujiweka vizuri zaidi. Katikati ya muda huo Ankia pia akawa ameenda kuoga ili ajiandae vizuri kwenda kwa kina Miryam.
Mimi nilipomaliza kujiweka fresh nikarudi tu kukaa sebuleni pamoja na huyo rafiki yake Ankia, akiwa anamsubiri mwenziye amalize kujiandaa. Haikuchukua dakika nyingi sana nasi tukaanza kusikia muziki mnene ukipigwa kutokea hapo kwa kina Miryam, na Ankia akatoka chumbani huku akiwa anacheza taratibu na kuja kunielekea. Nikawa namwangalia tu kwa umakini, naye akaja mpaka nilipokaa na kumwonyeshea rafiki yake jinsi ambavyo alikuwa na ukaribu nami kwa kutikisa kalio lake karibu na mapaja yangu.
Wanawake hawa wakacheka kidogo, nami nikaendelea kutulia tu kama vile sitaki yaani. Ndiyo Ankia akaniuliza ikiwa alikuwa amependeza, na alivalia kawaida tu; gauni fupi la kitenge, yaani fupi sana, na miguuni ndiyo alivaa suruali nyeusi ya skinny iliyobana umbo lake tenteme vizuri mno. Nikamwambia yuko poa, na yeye akaniasa tuelekee hapo kwa Miryam maana mida ya kupachangamsha ndiyo ilikuwa hii, lakini nikamwambia atangulie tu kwanza.
Ilikuwa imeshaingia saa kumi kuelekea saa kumi na moja. Ankia na mwenzake wakaondoka haraka huku akiniambia nisikawie kwenda, nami nikakubali. Alikuwa amekosa kufika mapema kusaidiana na wenzao kutengeneza nini na nini, ndiyo maana alitaka kuwahi hapo kwa ajili ya mengine yaliyokuwa yamebaki. Mimi bado nilikuwa nafikiria kuhusu Festo, sijui kama bado alikuwepo ama la, na sikutaka kwenda tena yaani mpaka niwe na uhakika ikiwa ningekwenda na kumkuta ama kutomkuta.
Siyo kwamba niliogopa. Ni ile tu kuwa na utayari wa kiakili kushughulika na hali tata kama hiyo ndiyo nilichokuwa nahitaji. Naona bado jamaa alikuwa akininyima amani sana kichwani, hata kama ningempuuzia vipi, kuwa kwake huru tu na kuendeleza ukaribu na Miryam japo alikuwa amekataliwa ni mambo yaliyonitatiza sana kichwani. Ni kama vile pamoja na yote niliyokuwa nimefanya, bado jamaa alikuwa amenishinda kwa asilimia kubwa, kwa hiyo ningeendelea kumwona kama mshindani wangu mkuu zaidi aliyebaki haijalishi alikuwa ameniambia nini kuhusu yeye kutaka kubadilika.
Inaonekana shamra hapo nje ilizidi kupanda, maana sauti za watu wakifurahia zilizidi kuongezeka. Nikiwa nimetulia tu, Tesha akanipigia simu kuuliza nilikuwa wapi, mbona siendi wakati watu walikuwa wameanza kuongezeka, nami nikamwambia nilikuwa nimetulia kwanza ila ningefika tu hapo kwao si muda mrefu sana. Akasisitiza niende, kwamba Bi Zawadi alikuwa amesharudi, na yule Doris alikuwa amefika pia pamoja na Dina. Akaniambia mambo yalikuwa yameanza kuiva, na mimi tu ndiye niliyekuwa nimebaki kufika hapo ili yapakuliwe.
Dina pia akaanza kunitumia jumbe za kuuliza mbona sitokei huko, lakini sikujibu hata moja. Yaani nikaendelea tu kukaa sofani kama mtu aliyeishiwa raha, ama labda ungesema walikuwa wamenifukuza. Nilikuwa natamani ninyanyuke tu niende, lakini miguu ikawa kama imeng'ang'ania sakafu la hapo ndani. Nikaanza hadi kujiona kama mtoto aliyezira kula bila sababu yoyote, tena kwenye siku ambayo mapilau na makuku ndiyo yalipikwa sasa, ila haikuchukua muda mrefu sana kwa hilo kuweza kubadilika.
Tesha akawa amekuja hapa kabisa, pamoja na Bobo, wakifikiri kwamba kuna kitu kilikuwa kinanisumbua yaani labda niliumwa, ila nikawaambia nilikuwa poa tu sema kuna jambo lilinivuruga kidogo. Tesha alikuwa mwepesi kunielewa, na bila kumhusisha Bobo, akawa ameniambia kwamba "yule" jamaa alikuwa ameshaondoka, akimaanisha Festo, kwa sababu nadhani aliona kwamba uwepo wa Festo pale kwao ndiyo uliofanya nikaamua kujiweka pembeni.
Taarifa hiyo ilinipa ahueni kidogo ingawa haikuwa sababu pekee iliyofanya niendelee kujichimbia huku kwa muda huo wote, maana hata kama Festo angekuwa hajaondoka bado, nisingeahirisha kabisa kwenda kusherehekea na Bi Zawadi. Kwa hiyo baada ya wana kuwa wameniomba tukajumuike huko, nikajiweka vizuri tena, kisha kwa pamoja tukaenda. Na sasa saa moja ilikuwa inavizia kuingia.
★★
Ile tumeingia tu hapo getini kwao Tesha, nikakuta watu wakiwa wengi-wengi, wadada wale sanasana waliopendelea kuvaa madera wakiwa kwa huku nje pamoja na wanaume vijana, na hapo varandani kulikuwa na ile meza yao Tesha ya dining, kiti kimoja ambacho alikalia rafiki mwingine wa Bobo, huku spika ya muziki ikiwa imewekwa kwa hapo juu ikishusha muziki mnene. Jamaa alikuwa ameunganisha tu simu yake kwa Bluetooth ya sabufa yao wakina Tesha, ambayo ndiyo iliungwa kwenye spika hiyo ili muziki uliotoka kwenye simu yake udundie hapo.
Milango yote ilikuwa wazi, mapazia pia yaliachanishwa ili ndani paonekane vizuri, nasi tukaelekea mpaka hapo ndani. Bobo akabaki nje hapo kwa mwenzake kwa ufupi, na sisi tulipoingia tukawakuta wenyeji na wageni wakiwa wamekaa sebuleni pamoja na watoto wengi wa majirani wa mtaani waliokuwa wamekaa kwenye uwazi ulioachwa pale sehemu ya dining.
Yaani sebule ilipanuliwa kwa kulisogeza pembeni sofa lililoukinga upande huo wa dining, kwa hiyo palionekana kama ukumbi mdogo uliopambwa kwa njia nyeupe na nyekundu, pamoja na watu waliopendeza pia. Baada tu ya mimi kuingia, mama Chande akatoa kama sauti za shangwe kunielekea mimi na wakina Tesha, na mashosti zake waliotufahamu wakaiga. Hizo ndiyo shobo nilizokuwa sifagilii, basi tu. Tesha naye akaanza kuongea kama MC fulani hivi kwa kusema mwarabu na mchina wa kitaa nimefika.
Nikawa nimetuliza tu hisia nikionekana kuchukulia hayo kuwa kawaida, na umakini wangu ukavutwa na Doris, Dina, pamoja na wanawake wengine wawili watu wazima waliokuwa wamekaa pamoja nao. Doris aliniangalia kwa shauku ya kirafiki, na mimi nikamfata hapo na kumsalimia kirafiki pia. Alifanya hadi kusimama na kunikumbatia, na Dina naye akafanya hivyo hivyo, kisha ndiyo wakawa wamenitambulisha kwa mwanamke mmojawapo hapo kuwa mama yao mzazi.
Nikamsalimu pia kwa heshima, huyu akiwa kama vile mama mdogo wake Miryam maana ndiye aliyekua pamoja na marehemu mama yake, na alionekana kuwa aina ya mwanamke aliyependa kuhukumu vitu yaani, kwa kumwangalia tu, saikolojia ya kidaktari ikawa imeniambia hivyo. Kwa hiyo nikaona niachane naye na kwenda kumsalimu Bi Jamila pamoja Ankia, waliokuwa hapo sebuleni pia.
Yaani hii sehemu yote ilionekana kubanana kabisa kutokana na jinsi palivyojaa watu, hapo chini watoto walikaa huku wakinywa juice na biskuti walizopewa, kule jikoni kukiwa na wanawake baadhi walioshughulika na msosi na kuja tena sebuleni, na sikuwa nimemwona Mariam, Bi Zawadi, wala Miryam; bila shaka wakiwa huko chumbani. Inaonekana Tesha alikuwa anataka kumkaribisha mama mkubwa wake kiaina, kwa hiyo akaelekea huko chumbani kama kuwashtua, kisha akarejea akiwa pamoja na Miryam. Ah!
Malkia wa moyo wangu alikuwa amevalia kwa njia ya kawaida tu, lakini alipendeza sana. Sikuwahi kumwona akiwa amevaa nguo yenye rangi ya maroon, na kiukweli hili gauni alilolokuwa amevaa sasa lilimfanya atamanishe mno macho na hisia zangu. Yaani alikuwa kama chakula ambacho hakikuwahi kuguswa, kumwangalia tu kulinisahaulisha shida zote za kichwani maana alinifanya nifikiri ni mimi tu ndiye niliyepaswa kuja kula hicho chakula!
Bibie mwenyewe akawa anajitahidi kuwatendea watu vizuri tu hapo, na inaonekana wakati niko kule kwa Ankia walikuwa wameleta na makreti kama matatu ya bia, bila shaka likiwa ni wazo la Tesha na Bobo, lakini yaliwekwa tu huko chumbani kwa Tesha na hakukuwa na wengine waliokunywa bia taratibu isipokuwa mama yake Doris, rafiki yake, Doris mwenyewe, Ankia, mama Chande, na wanawake wengineo hapo. Najua Miryam asingekunywa, kwa hiyo Ankia aliponipa ofa ya kufata moja ili nipoze koo, nikawa nimekataa. Leo ningeenda kwa mabiti ya bibie.
★★
Baada ya dakika kadhaa, Bi Zawadi, Shadya, na Mariam wakawa wametoka huko chumbani, kwa pamoja wakija sebuleni taaratibu kama vile mwanamke huyo alikuwa kimwanaharusi. Alipendeza kweli kwa kuvaa gauni refu jekundu lenye mistari myeupe hapa na pale, likiwa na muundo kama wa batiki, lakini ikiwa ni kitambaa kizito tu, na mtindo wa nywele za rasta zilizobanwa juu ya kichwa ulimpendezesha hata zaidi.
Alionekana vizuri sana, yaani alipendeza mno, na najua Shadya ndiye aliyekuwa amehusika kumpendezesha namna hiyo yeye na Mariam pia. Binti alivalia gauni la blue-bahari lisilo refu sana, na alikuwa amesuka nywele za kizungu za mawimbi zenye rangi ya brown, huku mbele ya mwanzo wa nywele zake akivaa tiara nyeupe. Walipendeza kama vile wasingekuja kupendeza tena!
Tukaanza na kuwapigia makofi, Tesha akiendelea kufanya u-MC kuwakaribisha na kumtambulisha Bi Zawadi kuwa kama "birthday girl," na Miryam alikuwa akichukua video kwa ajili ya kutunza kumbukumbu ya mambo mengi yaliyotokea hapa. Haikuwa ajabu kwangu kutambua kuwa wanawake waliokuwepo hapo, hasa ambao hawakunifahamu, walionyesha kuvutwa zaidi na uwepo wangu, wakinitazama sana na hata mara nyingine kusimama karibu nami nilipokuwa nimetulia tu kuwaangalia wapendwa wangu.
Lakini sikujishughulisha nao. Yaani nilitulia. Nilitulia kweli. Dina alikuwa akinitumia jumbe fupi kwenye simu na kutarajia tufanye ile kuchat ya kisiri, lakini nikampiga chini kama vile simjali. Yaani mpaka wakina Ankia, Bobo, mama Chande walinifuata kuniuliza vipi, mbona sichangamki bwana, na mimi nikawa natabasamu tu kwa kuwa niliamua kuitathmini kwanza furaha ya wote niliokuwa nawapenda sehemu hii. Hasa Miryam.
Kila mara nilipomwona akitabasamu pale wengine walipokuwa wakiburudika aidha kwa muziki, ama utani wa Tesha, nilihisi amani zaidi ya vile ambavyo nilikuwa kabla ya Festo kuja hapa muda ule. Ikawa wazi zaidi kwangu kuwa hiki ndiyo kitu nilichokuwa nahitaji zaidi ili kuepuka kujishusha moyo kisa huyo jamaa, na haingejalisha tena alikuja hapa kuongea na Miryam kuhusu nini; nisingeacha kuendelea kumwonyesha mwanamke huyo upendo wangu kamwe.
Kila mara ambayo Miryam angetazama upande wangu na kukuta namwangalia tu, angeacha kutabasamu na kufanya aidha shughuli nyingine ama kwenda jikoni, au wapi, akiwa bado analazimisha kuniepuka eti. Nikawa najikuta natabasamu mwenyewe tu kwa sababu hali hii nilikuwa nimeshaanza kuizoea, na ilifurahisha, kwa sababu najua ingeendelea kunizidishia motisha ya mbio zangu za kuufikia moyo wake mpaka kuukamata. Na matumaini ya kuwa pamoja naye bado yalikuwa chanya, kwa hiyo nisingekata tamaa.
Sherehe ikaendelea. Nikapata na juice ya embe ambayo nilimiminiwa na bibie mwenyewe kwenye glasi, na alifanya hivyo mbele yangu kama hataki yaani. Kwa muda huu nilikuwa nimeamua kutulia ndiyo, lakini jambo fulani likafanya niamue kwamba kuchangamka zaidi ingefaa, hasa kwa ajili yake Miryam. Kuna mara ambazo nilikuwa nikimwona mama yake Doris alipokuwa akimtazama Miryam, yaani, alimwangalia kwa njia isiyo rafiki. Miryam angepita hapo mara kwa mara na kusemeshana pamoja na watu wengine kirafiki, hata Doris pia, lakini huyo mama alimwangalia vibaya tu kana kwamba walikuwa na ugomvi.
Mpaka ikafikia hatua nikaona Miryam alipotaka kumwongezea kinywaji, mwanamke huyo akakataa, lakini Shadya alipotaka kumwongezea kinywaji hicho hicho, akakubali. Wengine hawakuwa wakitambua jambo hili, lakini niliona likimnyima Miryam amani kiasi. Huyo mwanamke alitakiwa kuwa kama mzazi kwake pia maana alikuwa na uhusiano wa karibu pamoja na marehemu mama yao wakina Miryam, sasa sijui alikuwa na shida gani mpaka akaona amtendee bibie namna hiyo.
Ikafika muda wa kukata keki sasa, nayo ikaletwa na kuwekwa hapo mezani, lakini haikufunguliwa kwanza. Yaani ilikuwa ndani ya kifaa kama boksi lakini lenye muundo mzito kama ubao, au hizi bodi za dari zinavyokuwaga ngumu (ceiling board), likiwa jeupe na lenye kishikio kwa juu ambacho kikivutwa ndiyo lote linafunguka na kuiachia keki iwe wazi.
Ikiwa imewekwa hapo, Tesha akasema, "Sawa sawa. Sasa... unajua... birthday girl wetu hapa anatimiza miaka 62, na amezaliwa kwenye tarahe 11 ya leo hii, mwezi wa 11 huu, na mwaka wa 61 ule. Lakini hebu mchekini kwanza! Sura na mwanya uoneokanao kama vile binti mbichi mbichi ambaye bado yuko kwenye miaka ishirini vile!"
Tesha akampamba Bi Zawadi namna hiyo.
Sote kwa pamoja tukacheka kidogo, naye Bi Zawadi akasema kwa maringo, "Jamani, me mwanya nimeutoa woopi..."
Tukafurahishwa zaidi na utani wake wa kuigiza kama mwanadada mdogo, naye Tesha akasema, "Upo kwenye loading huo mwanya, maana leo utakula keki mpaka meno ya mbele yatayeyuka!"
Bi Zawadi akacheka kidogo.
Tesha akasema, "Okay, okay. Sasa... umefika wakati maalumu wa bibi wetu kushika kisu na kuchinja keki. Jamani, fungua keki hiyo... watoto msiangalie nyuma, hakuna yai bovu huko, keki safi hii hapa, kwa hiyo macho yote yawe mbele..."
Ankia alikuwa karibu yake Bi Zawadi, kwa hiyo akamsaidia kukivuta kishikio cha boksi la keki, nayo ikawa imefunguliwa. Kweli ni keki moja nzuri sana ikawa amefunuliwa hapo mezani, ikiwa kubwa, yenye rangi nyeupe kwa nyekundu, ambayo mimi na Tesha tuliagiza ipambiwe na kamdoli ka mwanamke aliyeshika namba 62 wakati ule tumeenda kuitafuta. Vyote vilikuwa ni keki.
Miryam, Doris, Shadya, na wengine baadhi walikuwa wakichukua video kwenye simu zao, huku Ankia akimsaidia Bi Zawadi kuweka flare ndogo juu ya keki (vimshumaa vinavyowakaga kwa kutoa cheche kama fataki vile), tayari kwa kuwasha ili tumwimbie Bi Zawadi wimbo wa 'birthday' kwa pamoja kabla ya kuikata. Huu ndiyo ukawa wakati sahihi wa mimi kuanza kuchangamka.
Tesha akasema, "Sawa, sasa tunawasha hapo, simameni jamani watoto na watu wazima ili tumwimbie birthday girl wimbo wake mtamu sana wa...."
"Tesha, ngoja kwanza," nikamkatisha.
Watu wakaniangalia.
"Enhe, JC ana neno. Leta mambo handsome wa Kijiji..." Tesha akaongea hivyo.
"Ahah... wa kuleta mambo ni Mamu. Ana zawadi special kwa ajili ya birthday girl," nikasema hivyo.
"Wooow! Mamu jamani!" Bi Zawadi akasema hivyo na kuanza kumpigia makofi Mariam, ambaye alikuwa pembeni yake.
Akiwa na tabasamu mwanana usoni, Mariam akaniangalia na kunitikisia kichwa chake kama kuuliza kitu, nami nikamtikisia nyusi kukubali. Akatoka hapo upesi na kwenda chumbani huko kwanza, kisha akarudi akiwa na kile kinanda chake mkononi. Watu wakahisi binti alikuwa amekuja kujaribu kumpigia muziki Bi Zawadi, na hawakukosea. Akakaa kitini na kukunja mguu wake huku kinanda kikiwa katikati, nasi sote tukawa tunamwangalia kwa subira.
Mariam akaanza kupiga kinanda, yeye mwenyewe, akipiga ile midundo iliyotokeza sauti ambayo sote tuliifahamu kuwa ya wimbo maarufu utumiwao kwenye sikukuu za kuzaliwa. Yaani kinanda kilitengeneza melody ya 'happy birthday to you, happy birthday to you,' na hakukosea hata mara moja! Kwa waliokuwa wanafahamu juu ya tatizo alilokuwa nalo, walionekana kushangaa sana. Mama yake Doris akajisogeza mbele zaidi kwenye sofa ili asikilize kwa makini, na Mariam akaendelea kupiga kinanda tu kwa utaalamu wa hali ya juu sana.
Nikamtazama Miryam na kuona jinsi ambavyo alimwangalia mdogo wake kwa hisia sana, kisha akaniangalia usoni kwa umakini. Nikampa tabasamu hafifu huku nikimwangalia kwa hisia, naye akarudisha umakini wake kwa mdogo wake tena. Tesha akaanza kumsifia kweli Mariam na watu hapo kupiga makofi. Ankia akamwambia binti arudie tena kupiga midundo hiyo, halafu watu wote wafatishe na kuanza kumwimbia Bi Zawadi wakati ambao flare ingewashwa ili apulize na kutoa ombi lake kwa Mungu. Ikawa hivyo.
Mariam akaanza tena kupiga kinanda, nasi tukawa tunaimba kwa kufatisha sauti hiyo, na tukipiga makofi pia. Bi Zawadi alionekana kufurahi sana, akiwa amefunika mdomo wake kwa viganja huku akimtazama Mariam kwa hisia, naye Tesha akazidisha mbwembwe za maneno ili wimbo uendelee kuimbwa tu. Ankia akawasha mshumaa wa kwenye keki, huku bado tukiendelea kuimba, na Miryam alikuwa akichukua video tu kwenye simu yake huku akitabasamu kwa furaha sana.
Bi Zawadi akaendelea kuenjoy kwanza muziki aliopigiwa na Mariam kabla ya kuinama na kupuliza mshumaa wa keki kwa nguvu, nasi sote tukampigia makofi na wakina mama Chande kutoa sauti kwa shangwe. Ankia akampatia kisu laini Bi Zawadi ili aanze kukata keki, na mama huyu akajitahidi kukata vizuri vipande vya mwanzo, halafu Ankia akachukua kikopo cha stiki na kuanza kuzichomekea keki kipande kimoja-kimoja.
Bi Zawadi akataka wa kwanza kabisa kumlisha iwe ni Mariam, naye binti akanyanyuka na kwenda kula keki kwa furaha, kisha naye akamlisha mama mkubwa wake na kumkumbatia kwa upendo. Akafata Bi Jamila, kisha Miryam, ambaye alikumbatiwa na Bi Zawadi kwa karibia dakika nzima kabisa. Baada ya hapo akafuata mama yake Doris, Doris mwenyewe, Dina, Tesha, Ankia, Shadya, Bobo, mama Chande, na karibia wote walikuwa na kitu kizuri cha kumpa mama huyu kama zawadi, iwe ni kaelfu kumi, mkufu, kitenge kizuri, ama zingine zilizotiwa ndani ya maboksi, halafu ndiyo nikaja mimi sasa.
Bi Zawadi alikuwa ananiita kwa shauku sana kuwa niende kulishwa naye, nami nikamfikia na kula keki yangu, kisha nikamlisha yake pia. Halafu, nikaingiza mkono mfukoni na kuchomoa wallet yangu iliyokuwa imetuna, nami nikaanza kutoa elfu kumi moja baada ya nyingine. Nilikuwa nazitoa kwa madoido yaani, nikiziachia karibu na kichwa cha Bi Zawadi zimmwagikie tu kama mvua, na wanawake wakawa wanatoa sauti za shangwe kunishabikia yaani.
Bi Zawadi akawa amefumba mdomo huku akicheka kwa aibu, Bi Jamila naye akishangilia eti, nami nikamtazama Miryam kutokea pale alipokuwa amesimama. Aliniangalia kwa jicho makini sana, kama hataki eti, nami nikamtikisia nyusi kiuchokozi, na yeye akazungusha jicho na kuangalia pembeni, kitu ambacho kikanifanya nicheke kidogo na kumalizia kummiminia cheupe wangu pesa ya zawadi. Hapo nilikuwa nimemmwagia laki mbili kamili, wanawake wakiwa wamehesabu na kumshangilia cheupe wangu, naye akanikumbatia kwa furaha sana.
Nikaenda pembeni tena na kusimama karibu yake Mariam zamu hii, na ndiyo watu wengine wakaendelea kulishwa keki, na Tesha kuchangamsha sherehe kama ilivyotakiwa baada ya Bi Zawadi kuokotewa pesa zake na Ankia. Angekuja kujinunulia tuvitu tuzuri mwenyewe ahisi raha hata zaidi, cheupe wangu huyo. Ilikuwa siku yake!
Nilijikuta napenda sana hii kitu. Ilikuwa sherehe ya kawaida tu, mambo yasiwe mengi wala ya gharama za ajabu, lakini ushirika wa hawa watu na jinsi walivyoonyeshana upendo ulipatajirisha sana hapa. Halafu pia nikaanza kuona kwamba mama yake Doris alinifatilia sana baada ya hako kakitendo kangu muda mfupi nyuma, yaani aliniangalia mno mara kwa mara, nafikiri akiwa ameona kitu fulani ndani yangu kilichomfanya agundue mi' wa maana. Chezea!
Mariam akawa amemwomba Bi Zawadi alishwe keki tena, kale kamdoli eti, nasi kwa pamoja tukacheka kidogo. Bi Zawadi akamwita na kumlisha taratibu huku watoto wakimkodolea, halafu na yeye akamwomba Mariam ampigie kinanda kwa mara nyingine tena. Mariam akafurahi kufanya hivyo. Akaanza kumpigia kinanda tena, na watu wakaungana naye kuimba wimbo wa birthday kwa kufatisha sauti. Wakina Ankia na mama Chande walikuwa wameelekea jikoni pamoja na wadada wengine, nafikiri kuweka mambo ya msosi sawa zaidi.
Nikamwangalia Miryam. Alikuwa amesimama pembeni tu, akiwatazama Bi Zawadi na Mariam kwa hisia sana, nami nikasogea upande wake na kusimama karibu naye bila yeye kutambua kwamba nilikuwa nyuma yake. Doris, Dina, na wageni wengine walikuwepo hapo sebuleni pia, na niliona umakini wao ukielekea kwangu mara kwa mara, lakini sikuwajali sana wakati huu.
Nikamwambia Miryam kutokea pembeni, "Hiyo hapo."
Akageuza shingo yake kuelekea upande wangu, lakini hakunitazama kabisa.
Nikasema, "Unakumbuka tulivyoongea siku ile? Kuhusu Mamu?"
Akionekana makini zaidi sasa, akamtazama tena mdogo wake.
"Nilikwambia kuna ishara zingejionyesha Mamu akianza kuwa imara zaidi kiufahamu. Hiyo hapo moja, Miryam. Kumbukumbu yake inazidi kuwa imara. ASD inaondoka hivyo," nikamwambia.
Akaniangalia machoni kwa hisia makini.
Nikampa tabasamu hafifu la uhakikisho, naye akaacha kuniangalia na kumtazama Mariam tena, kisha akashusha pumzi na kunipita kuelekea jikoni bila kusema asante wala nini. Lakini najua kutoka ndani ya moyo wake kwamba alikuwa amefurahi sana kusikia hivyo, ni basi tu eti hakutaka nione hilo moja kwa moja.
Nikajisogeza tu pembeni tena baada ya hapo, na Mariam alipomaliza kupiga kinanda chake, Tesha kama MC akasema, "Haya, umefika wakati wa kuhalalisha rasmi kabisa umri wa bibi wetu mrembo. Mko tayari?"
Wanawake na watoto wakasema 'ndiyoo' bila hata ya kuelewa alichomaanisha, na Tesha aliponiangalia, tukajikuta tunacheka kidogo kwa kuwa ni mimi na yeye tu ndiyo tuliokuwa tunaelewa kilichokuwa karibu kutokea. Miryam akawa amerejea tena. Tesha akaomba kiti ili aweze kupanda usawa huo hapo katikati, na baada ya kufanya hivyo, akayafikia maputo huko juu na kuichukua kwa uangalifu ile kamba iliyobaki mwishoni, kisha ndiyo akashuka. Halafu akamvuta Bi Zawadi usawa wake na kusimama karibu yake.
"Hii ni zawadi nyingine kwa mrembo wetu Zawadi. Makofi kwake na vilegelege kwa kutimiza miaka 62!" Tesha akaongea hivyo kwa shauku.
Watu wakacheka na wakina mama Chande kupiga hivyo "vilegelege," halafu Tesha akaniangalia huku akijikaza asicheke. Nikamtikisia kichwa kama kumwambia aache tu, naye Miryam akaniangalia kwa macho yaliyoonyesha alikuwa ameshashtukia dili. Tesha akaivuta hiyo kamba na kumkimbia mama mkubwa wake ghafla, na yale maputo hapo juu yakaanza kupasuka moja baada ya lingine. Kila moja lililopasuka lilitoa vikaratasi vingi vidogo-vidogo vilivyomeremeta, halafu maputo mawili ya mwisho yakamwaga maji!
Miryam akafunika mdomo wake kwa kiganja. Bi Zawadi alikuwa bado amesimama hapo kati, kwa hiyo hivyo vikaratasi na maji yakawa yamemwagikia. Wakati maputo yalipokuwa yanapasuka na kutoa hivyo vikaratasi, watu walikuwa wanashabikia eeeeh, lakini maji yalipommwagikia Bi Zawadi, wengine wakaonekana kushangaa na kubaki kimya. Tesha akaanza kucheka, Mariam pia, huku Bi Zawadi akiwa amefumba macho, kisha naye akaanza kucheka.
Watu wengine wakaanza kucheka pia, Bi Jamila ndiyo alikufa mbavu yaani, naye Tesha akasema, "Maji ya baraka ya sikukuu ya kuzaliwa! Ulifikiri tungekuacha salama ma' mkubwa?"
Bi Zawadi akasonya kidogo na kusema, "Shenzi wewe!"
Wengine ndiyo wakazidisha vicheko, na maongezi kuhusu hicho kitendo yaanza hapa na pale. Nilikuwa nikijizuia nisicheke, lakini nilipomwona Miryam anatabasamu huku akitikisa kichwa chake, nikashindwa kujizuia tena. Ankia akaja karibu na kunilalia begani huku akicheka, na Doris akawa amemsogelea Miryam kumnon'goneza jambo fulani lililofanya kwa pamoja wacheke kwa furaha sana.
Bi Zawadi alipouliza nani aliweka hayo maputo yenye maji huko juu, mimi na Tesha tukanyoosheana vidole kama kulaumiana, naye Bi Zawadi akatikisa tu kichwa na kuanza kuelekea chumbani ili akajikaushe. Miryam akanikata jicho kali kweli eti kama vile hakupenda, maana alijua ni mimi ndiye niliyekuwa nimeyafunga maputo huko juu, nami nikabana tu tabasamu langu na kuamua kwenda uani kwanza kabla hajanitafuna. Lakini naelewa alikuwa ameburudika sana. Ilikuwa wakati wenye kiburudisha kwa kweli!
DJ Bobo pale varandani akawasha muziki tena. Tukawa tumemwomba Bi Zawadi samahani ya kummwagia maji bila kumwandaa baada ya yeye kurudi tena sebuleni, na alituvuta masikio mimi na Tesha, lakini akasema alikuwa ameburudika sana leo kwa kweli.
Akatushukuru sisi wote kwa kuifanya siku hii iwe murua mno kwake, na akaombea uzima wetu sote ili tuendelee kuwa pamoja kwa mazuri na magumu yote ya maisha. Na alimshukuru mno Miryam kwa kuwatunza wote vizuri kwa upendo, akimwombea mafanikio zaidi kwenye maisha yake. Na huyu mama alikuwa na maneno mazuri sana yaliyogusa hisia, mpaka nikajikuta nampigia makofi na wengine kufanya hivyo pia.
Baada ya hayo ndiyo wanawake wakaanza kusambaza upendo wa misosi kwetu sisi wote. Kwa watoto waliokuwepo, waliketi sehemu ya chini pale dining na kuwekewa kwenye masinia, wanawake wakila pamoja hapo sebuleni, na sisi wanaume tukawa kwa huku varandani tukila na kunywa pia taratibu. Wakina Bobo na Tesha walipiga bia mbili tatu, lakini mie sikunywa hata kidogo. Tesha ndiyo akawa ameniambia kuwa yule mpenzi wake, Happy, alibanwa na kazi hata kwa siku hii, ndiyo maana hakuweza kuja kujiunga nasi leo.
Kwa hiyo muda ukaendelea kusonga tu. Hakukuwa na nafasi ya fujo hapo, kila kitu kilikwenda kwa utulivu na utaratibu mzuri kabisa mpaka sote tulipomaliza kula na kunywa, kisha tukamalizia muda wa masaa machache kwa kuoiga story na nini, na watu wengi waliokuwepo wakawa wanaaga na kurudi makwao.
★★
Ikiwa imeshaingia mida ya saa tano, umati ukawa umepungua, hapo kwa Miryam tukabaki siye tu tuliokuwa na ukaribu zaidi na familia hii, yaani hata wanaume tuliokuwepo ilikuwa mimi, Tesha, Bobo, na jamaa wengine wawili waliokuwa na ukaribu na Tesha. Basi. Kule ndani walikuwepo wanawake, Doris na familia yake wangelala hapa leo, na ili wapate nafasi ya kutoshea ya vyumba, Tesha angekuja kulala pamoja nami pale kwa Ankia, na hata Shadya angelala pamoja na Ankia huku kwake. Haikuwa na noma.
Wakati huu nikawa tu hapa varandani pamoja na Bobo na hao jamaa wawili, muziki ukiwa umeshushwa sauti, na Bobo tayari alikuwa ameshaniambia kwamba alimtokea Ankia kimapenzi, na mwanamke huyo alimkubalia lakini alitaka jambo lao liwe la chini-chini kwanza; wengine wasijue. Zilikuwa ni taarifa nzuri, kujua kwamba Ankia alipata mtu wa kumpenda aliyetaka kutulia naye, nami nikampa pongezi Bobo na kuahidi kutunza siri yake.
Tesha alikuwa ameenda huko ndani ili arudi pamoja na chupa zingine za bia, na hata wakina Doris na Dina hapo sebuleni walikuwa wakinywa huku wanapiga story na Miryam, Bi Zawadi, Ankia na mama Chande. Inaonekana Bi Jamila na Mariam walikuwa vyumbani, na hata mama yake Doris na yule mwanamke waliyekuja naye hawakuwepo sebuleni pia.
Nikiwa nimeegamia tu ukuta huku nakula story za kuchorwa tattoo na nini kutoka kwa hawa wasela, Miryam akawa ametoka ndani na kuja hapo varandani pia, nami nikamwangalia kwa umakini. Akasemeshana na Bobo kiurafiki na kisha kuvaa ndala na kutupita sote kuelekea ule upande wa nyuma ya nyumba uliokuwa na stoo. Inaonekana alitaka kwenda kuchukua kitu fulani huko. Kwa hiyo kwa kuzuga, nikajivuta-vuta tu na kuelekea upande huo pia ili nikajaribu kumchokoza kidogo.
Uzuri hakukuwa na watu wakati huu ambao wangekuja kwa huku maana na sherehe ilikuwa inaelekea kuzimika hapo mbele, na nilipofika huko kwenye chumba cha stoo, nikamkuta bibie akiwa ndiyo anatoka humo na kutaka kurudi tena huku tulikotoka. Lakini akasitisha hatua zake baada ya kuniona nimefika mbele yake, naye akanishusha na kunipandisha kwa mtazamo wa kawaida tu. Ile 'na huyu naye vipi?'
Hakuonekana kuwa amechukua chombo wala kitu chochote kutokea humo stoo, kwa hiyo kwa sauti ya chini nikamuuliza, "Ulikuwa unatafuta nini?"
Akaendelea tu kuniangalia kimkazo kiasi.
Nikatabasamu na kusema kimchezo, "Hakuna kilichokuleta kuchukua, eti? Ulikuwa tu unataka nikufate..."
Bila kunijibu, akageuka tu na kuanza kuelekea huko nyuma zaidi, nadhani ili akapitie kwenye mlango wa huko nyuma ili kuniepuka. Nikatabasamu zaidi na kumwahi ili nimsimamishe kwanza.
"Miryam, sikia... usikimbi...."
Nilikuwa nimeanza kumfata huku nikisema hivyo kwa sauti ya chini sana, na yeye kusimama ghafla ndiyo kukafanya maneno yangu yakatike. Alikuwa amefikia kwenye kile kikona chenye nafasi nyembamba, pale pale ambapo nilimnyuka Dina siku ile, na kutokana na yeye kusimama ghafla yaani ikawa imefanya nikaribie kabisa kumgusa kutokea nyuma, na kabla sijajirudisha, nikatambua upesi kwa nini alisitisha kuelekea mbele zaidi.
"Kumbe?"
"Eeh, zilikuwaga za nondo, sa'hivi naona wameweka na chupa-chupa. Ni vizuri, hapa wezi hawaruki ukuta. Nimekuja sana hapa kipindi cha nyuma..."
Nikasikia sauti mbili za wanawake zikisema maneno hayo kutokea huko nyuma, na upesi nikatambua kwamba moja ilikuwa ni ya mama yake Doris pamoja na yule rafiki yake aliyekuja naye, ndiyo waliokuwa wakiongea hivyo. Inaonekana walikuwa wamekuja kwa huku nyuma ili kupaona, na labda kuzungumza kidogo.
Miryam akageuka na kutaka kurudi tena kwa upande wangu, sijui ili awaepuke, lakini nilikuwa karibu zaidi na yeye kwa hiyo akaishia kuniangalia usoni kwa kutotarajia niwe karibu naye namna hiyo. Kisha ndiyo akaashiria kutaka kunipita kwa kulazimisha mwili wake upite kwa kujibana sana hapo ukutani, na mimi nikajikuta natulia tu na kumwangalia alivyokuwa anahangaika kutaka kupita kwa lazima.
Hii ikafanya nyuso zetu ziwe karibu zaidi, na kwa makusudi nikakaza mwili wangu ili kuzuia yeye asisonge mbele zaidi, yaani abaki hapo hapo. Miryam akanitazama usoni kwa ile njia yake ya kuudhika, akiwa anajua nimemfanyia makusudi kabisa, nami nikajitahidi kubana tabasamu langu na kuamua kulegeza mwili ili apite, mwishowe angenimeza kweli!
Maongezi ya wanawake wale yakaendelea.
"Hivi ni kweli kabisa ulivyosema kuhusu huyo dada?"
"Nikudanganye kwa lipi sasa?"
"Hmm... basi ana lake jambo..."
"Siyo siri, me nakwambia. Na tena... hiyo siyo tangu Maimuna alipofariki tu, wala kwa sababu ya vurugu za Joshua na nini hapo juzi... ni tokea muda sana, mpaka me huwa nashangaa...."
Sauti ya mama yake Doris akisema hivyo ikasikika vizuri sana kwetu, na mkazo uliokuwepo usoni mwake Miryam ukafifia baada ya jambo hilo lililosemwa kuonekana kuteka zaidi umakini wake, na hakuacha kunitazama usoni. Mimi pia nikaendelea kumwangalia Miryam usoni kwa utulivu, nikiwa nimeweka umakini wangu kwake kwa sababu ya jambo hilo.
"Kwani tayari alikuwa ameshakuja huku?"
"A-aah, huku amekuja wazazi wake walipofariki... Maimuna alipofariki nimekwambia," mama Doris akasema hivyo.
"Ahaa, sawa. Eh! Mbona sasa anachelewa jamani? Mwanamke mwenyewe mzuri kweli, shida itakuwa wapi?"
"Ndo' maana nakwambia nashangaa. Tumeshamshauri sana, mimi na Shadya tumeshamtafutia wachumba wenye hela, lakini wote kawakataa. Mwanamke heshima ndoa, kuzaa, uwe na kwako na familia yako... yeye mpaka anataka kuzeeka ndo' aje kushtuka eti! Yaani sijui amekuwaje jamani..." mama Doris akaongea hivyo kwa sauti ya chini.
Ilieleweka kwamba wanawake hao walikuwa wanamwongelea Miryam, naye bibie akashusha macho yake kutazama chini huku akionekana kuanza kuhuzunishwa na jambo hilo. Kwa mara ya kwanza leo nikawa nimetambua kuwa marehemu mama yake na Miryam aliitwa Maimuna, na mama Doris kumsema hivyo bila shaka kulimtia simanzi kuu Miryam. Nikawa namtazama kwa hisia.
"Hakuwaga hivyo? Alikuwa na wanaume?"
"Ndiyo, alikuwaga tena anatoka na mtu wa maana nakwambia. Eti akaachana naye, kisa nini sijui. Sasa hivi amekuwa mfungwa kwa hii familia, Doris ni mdogo kwake lakini anatangulia kuolewa.... nakwambia ataendelea kukaa hivyo hivyo hadi huyu mdogo wake wa kike ataolewa ye' anakodoa tu. Sijui anafikiri atakuja kuazima ndoa ya mtu? Labda kwa sababu tu ya huo uzuri?" mama Doris akasema hivyo.
Miryam akafumba macho yake na kutikisa kichwa taratibu, akionekana kutoamini.
"Usiseme hivyo ila, tusimwombee mabaya. Ni vizuri ametulia, labda uje tu ujaribu tena kuongea naye. Atakusikiliza," rafiki akaongea hivyo.
"Ah, me nilishachoka. Ameshakuwa mtu mzima, tumemjali mno, imetosha. Sa'hivi tunajali hawa makinda waliobaki. Yeye kama kaamua kujilaani eti kisa ameachiwa familia ya kutunza... ni yeye. Atakapokuja kujuta baadaye lakini, atakuwa ameshachelewa. Na amechelewa mno. Yaani hataolewa huyu. Ndoa isimame kabisa? Haipo. Me nakwambia, atabaki kudandia ndoa za watu kama siyo kutumiwa na wanaume ambao watamwacha na mamichango tu..." mama Doris akasema hayo.
Aisee!
Rafiki yake akasikika akisema, "Basi turudi ndani, tukikutwa hapa tunapiga umbea!"
"Ahahahah... siongei kwa ubaya, ni ukweli tu. Tushamshindwa. Loh! Twende tukale tu keki tena..." mama Doris akaongea hivyo.
Inaonekana wanawake hao wakawa wamerudi ndani tena, bila kujua kuwa sehemu ndogo ya maongezi yao kumhusu mwanamke mwenzao ilikuwa imemwachia hisia mbaya na nzito sana maana aliwasikia. Najua Miryam aliumizwa na maneno ya mama yake Doris. Yaani mtu aliyemwona kama mama mdogo ama shangazi yake, ndiye aliyekuwa akimsema namna hiyo kabisa, tena hapa hapa nyumbani kwake? Lazima iliuma.
Miryam akawa bado ameinamisha uso wake kiasi, akionekana kuhuzunishwa na utambuzi wa jambo hilo, nami nikapatwa na hisia ya simanzi kumwona namna hii. Nikaweka tu kiganja changu kimoja usawa wa shavu lake na kuligusa, kisha nikalishika lote kwa njia yenye kumpatia faraja ya bila maneno. Akapandisha macho yake na kunitazama usoni kwa macho yaliyojaa hisia zilizovurigika kiasi, na najua aliweza kuiona hisia yangu ya uelewa wa hali yake ndani ya macho yangu kwa jinsi nilivyomtazama pia.
Nikataka nimwambie kitu chenye kufariji ili asiwazie sana kuhusu maneno ya mama yake Doris, nami nikasema, "Miryam... hayo yote siyo kweli. Sawa? Haujajilaani popote. Hawa hawakujui, hawawezi kuelewa kwa nini una...."
Akaacha kuniangalia na kuweka kiganja chake kwenye kifua changu kama kunizuia nisiendelee, kisha taratibu akautoa mkono wangu kutoka usoni kwake na kuondoka hapo; akielekea kule mbele tulikowaacha wakina Bobo. Nikajihisi vibaya kweli.
Sasa ndiyo ikaeleweka vizuri zaidi kwangu kwa nini mama yake Doris alimtendea Miryam kwa njia fulani ya masengenyo. Lilikuwa tu ni suala la mwanamke huyu kukataa wanaume wengi waliokuwa wametafutwa kwa ajili yake ili aolewe, yaani ile tu kwamba aliwapiga chini ndugu zake katika harakati zao za kujaribu kumshurutisha aolewe. Walikuwa wanataka kumpeleka sana, lakini yeye kuendelea kuwa na msimamo ndiyo kitu kilichowafanya wakerwe naye mno. Si wanaukoo ndiyo huwa wako hivyo?
Kwa sekunde chache nikabaki tu sehemu hiyo nikimfikiria kidogo, maana ilikuwa wazi kwamba alibeba mambo mengi mazito moyoni yaliyomsumbua mno kihisia. Ilikuwa ni vita kwake akiwa kama mwanamke kupambana na jinsi jamii ilivyomchukulia, ingawa najua haikuwa lazima kujali hilo, lakini matokeo ya maamuzi yake yaliathiri kwa njia nzuri au mbaya jinsi ambavyo alionwa na jamii nzima mpaka kufikia kwenye familia yake, na watu aliowajali.
Katika hilo pia, ningetakiwa kumsaidia. Najua nisingeweza kubadili jinsi ambavyo watu walimfikiria, lakini ningeweza kufanya jambo fulani ili kubadili jinsi mambo yalivyokuwa kwake yeye. Hapo mbele naelewa kungekuwa na mengi magumu kwenye uhusiano wangu pamoja naye kuendana na yote yaliyokuwa yakimzunguka, lakini ningehakikisha anaipata heshima aliyokuwa akiistahili kutoka kwa watu wote waliokuwa wameishusha. Na huyo mama yake Doris angeisoma!
★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★
Full Story WhatsApp or inbox
Whatsapp +255 678 017 280
A Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA KUMI NA TISA
★★★★★★★★★★★★★★★★★
Ukimya ukaendelea kuijaza sehemu hiyo ya sebule kana kwamba hakukuwa na watu, maana mimi na Festo tuliendelea kuangaliana na kisha kubadilishana macho na bibie Miryam pia, ikiwa kama vile sote tunasubiri mmoja wetu ndiyo aseme kitu fulani. Na Miryam ndiye akaona avunje hali hiyo yenye utata.
"Karibu Festo," akamwambia hivyo na kutoa tabasamu nililoona lilikuwa la kujilazimisha.
Festo akatabasamu kiasi na kusema, "Asante. Nimefikia pazuri leo, mambo yako moto."
Miryam akatabasamu kiasi pia na kuangalia chini.
"Nani anazaliwa?" Festo akamuuliza hivyo.
"Ni mama," Miryam akamjibu.
"Oh, ni nzuri... sema sikuwa nimepata mwaliko, ningekuja kwa utayari ahah..." Festo akasema hivyo.
"Haina shida. Tayari umeshafika," Miryam akamwambia hivyo.
Jamaa akatabasamu tu, na yeye Miryam akawa ameweka uso ulioonyesha hisia za uajabu-ajabu tu.
Festo akanitazama na kusema, "Habari yako?"
"Safi. Karibu," nikasema hivyo kiutulivu.
"Asante," akaniambia hivyo, huku akikaza macho yake kwangu kama kunipa maana fulani ambayo sikuielewa, ila kama ananiambia 'ondoka.'
Nikamtazama Miryam, yeye akiwa anasogelea sofa ili akae, nami nikasema, "Miryam, me naenda."
Miryam akasitisha kuketi kwanza na kunitazama tu usoni.
"Nitarudi baadaye kidogo, ngoja nikupishe we' na mgeni," nikamwambia hivyo.
Miryam akatikisa kichwa kukubali na kutazama pembeni tena, bado akionekana kutatizika yaani, naye akamwambia Festo, "Karibu ukae Festo."
Nikamtazama Festo, naye akakaa kwa raha zote pamoja na bibie hapo sofani kwa kilichoonekana kuwa maongezi ambayo yangeenda vizuri baina yao, nami nikaamua kujiondokea hapo tu kama sina maana yaani. Kumwona jamaa hapa kulikuwa kumenizidishia hisia mbaya zaidi ya ile iliyokuwa imeniingia muda mfupi nyuma, lakini sikutaka kujiumiza mno kwa kuwaza juu yake, sema ni ile tu kujua kuhusu mambo mengi kumwelekea ndiyo kuliipa akili yangu mkereketo kiasi ulioendelea... yaani kunikereketa. Ilikuwa nje ya uwezo.
Nikafika ndani kwa Ankia na kukaa tu sofani, nikijaribu kujituliza kiakili na kihisia, lakini fikira zikawa zinalazimisha niwaze kuhusu nini ambacho mwanaume huyo angekuwa amekuja kuzungumza na bibie. Maana hakuwa amealikwa. Hata kale kahisia ka wivu kalikuwepo kabisa, nikitamani nirudi huko kujipitisha tu ili nijue ama nione yaliyoendelea, lakini huo ungekuwa ni upuuzi kwangu.
Nikaona tu nifanye mambo mengine ili kupisha muda kwanza, na jambo la mwanzo ikawa kuchukua simu yangu na kumpigia mama.
★★
Baada ya dakika kadhaa za kuongea na mzazi wangu, nikaona ni busara nikiingia bafuni kujimwagia kidogo, shauri tu ya kuhisi joto mno. Katika maongezi niliyofanya na mama nilikuwa nimemjulisha kwamba kesho ndiyo ningekwenda huko nyumbani ili kumsalimia, na ningeambatana na Mariam pamoja na kaka yake. Kwa hilo mama akakubali, na bila shaka angejiandaa kutupokea vizuri maana alikuwa mpenda wageni sana.
Nilipotoka bafuni na kurudi ndani nikakuta Ankia akiwa amerejea hapa kwake tayari. Tena alikuwa pamoja na rafiki yake mwingine aliyetoka naye huko Mzinga, mwanamke mtu mzima kama mama Chande tu aliyependeza kweli kwa namna ambavyo alivaa, nami nikawasalimu vizuri na kwenda kuvaa nguo safi na kujiweka vizuri zaidi. Katikati ya muda huo Ankia pia akawa ameenda kuoga ili ajiandae vizuri kwenda kwa kina Miryam.
Mimi nilipomaliza kujiweka fresh nikarudi tu kukaa sebuleni pamoja na huyo rafiki yake Ankia, akiwa anamsubiri mwenziye amalize kujiandaa. Haikuchukua dakika nyingi sana nasi tukaanza kusikia muziki mnene ukipigwa kutokea hapo kwa kina Miryam, na Ankia akatoka chumbani huku akiwa anacheza taratibu na kuja kunielekea. Nikawa namwangalia tu kwa umakini, naye akaja mpaka nilipokaa na kumwonyeshea rafiki yake jinsi ambavyo alikuwa na ukaribu nami kwa kutikisa kalio lake karibu na mapaja yangu.
Wanawake hawa wakacheka kidogo, nami nikaendelea kutulia tu kama vile sitaki yaani. Ndiyo Ankia akaniuliza ikiwa alikuwa amependeza, na alivalia kawaida tu; gauni fupi la kitenge, yaani fupi sana, na miguuni ndiyo alivaa suruali nyeusi ya skinny iliyobana umbo lake tenteme vizuri mno. Nikamwambia yuko poa, na yeye akaniasa tuelekee hapo kwa Miryam maana mida ya kupachangamsha ndiyo ilikuwa hii, lakini nikamwambia atangulie tu kwanza.
Ilikuwa imeshaingia saa kumi kuelekea saa kumi na moja. Ankia na mwenzake wakaondoka haraka huku akiniambia nisikawie kwenda, nami nikakubali. Alikuwa amekosa kufika mapema kusaidiana na wenzao kutengeneza nini na nini, ndiyo maana alitaka kuwahi hapo kwa ajili ya mengine yaliyokuwa yamebaki. Mimi bado nilikuwa nafikiria kuhusu Festo, sijui kama bado alikuwepo ama la, na sikutaka kwenda tena yaani mpaka niwe na uhakika ikiwa ningekwenda na kumkuta ama kutomkuta.
Siyo kwamba niliogopa. Ni ile tu kuwa na utayari wa kiakili kushughulika na hali tata kama hiyo ndiyo nilichokuwa nahitaji. Naona bado jamaa alikuwa akininyima amani sana kichwani, hata kama ningempuuzia vipi, kuwa kwake huru tu na kuendeleza ukaribu na Miryam japo alikuwa amekataliwa ni mambo yaliyonitatiza sana kichwani. Ni kama vile pamoja na yote niliyokuwa nimefanya, bado jamaa alikuwa amenishinda kwa asilimia kubwa, kwa hiyo ningeendelea kumwona kama mshindani wangu mkuu zaidi aliyebaki haijalishi alikuwa ameniambia nini kuhusu yeye kutaka kubadilika.
Inaonekana shamra hapo nje ilizidi kupanda, maana sauti za watu wakifurahia zilizidi kuongezeka. Nikiwa nimetulia tu, Tesha akanipigia simu kuuliza nilikuwa wapi, mbona siendi wakati watu walikuwa wameanza kuongezeka, nami nikamwambia nilikuwa nimetulia kwanza ila ningefika tu hapo kwao si muda mrefu sana. Akasisitiza niende, kwamba Bi Zawadi alikuwa amesharudi, na yule Doris alikuwa amefika pia pamoja na Dina. Akaniambia mambo yalikuwa yameanza kuiva, na mimi tu ndiye niliyekuwa nimebaki kufika hapo ili yapakuliwe.
Dina pia akaanza kunitumia jumbe za kuuliza mbona sitokei huko, lakini sikujibu hata moja. Yaani nikaendelea tu kukaa sofani kama mtu aliyeishiwa raha, ama labda ungesema walikuwa wamenifukuza. Nilikuwa natamani ninyanyuke tu niende, lakini miguu ikawa kama imeng'ang'ania sakafu la hapo ndani. Nikaanza hadi kujiona kama mtoto aliyezira kula bila sababu yoyote, tena kwenye siku ambayo mapilau na makuku ndiyo yalipikwa sasa, ila haikuchukua muda mrefu sana kwa hilo kuweza kubadilika.
Tesha akawa amekuja hapa kabisa, pamoja na Bobo, wakifikiri kwamba kuna kitu kilikuwa kinanisumbua yaani labda niliumwa, ila nikawaambia nilikuwa poa tu sema kuna jambo lilinivuruga kidogo. Tesha alikuwa mwepesi kunielewa, na bila kumhusisha Bobo, akawa ameniambia kwamba "yule" jamaa alikuwa ameshaondoka, akimaanisha Festo, kwa sababu nadhani aliona kwamba uwepo wa Festo pale kwao ndiyo uliofanya nikaamua kujiweka pembeni.
Taarifa hiyo ilinipa ahueni kidogo ingawa haikuwa sababu pekee iliyofanya niendelee kujichimbia huku kwa muda huo wote, maana hata kama Festo angekuwa hajaondoka bado, nisingeahirisha kabisa kwenda kusherehekea na Bi Zawadi. Kwa hiyo baada ya wana kuwa wameniomba tukajumuike huko, nikajiweka vizuri tena, kisha kwa pamoja tukaenda. Na sasa saa moja ilikuwa inavizia kuingia.
★★
Ile tumeingia tu hapo getini kwao Tesha, nikakuta watu wakiwa wengi-wengi, wadada wale sanasana waliopendelea kuvaa madera wakiwa kwa huku nje pamoja na wanaume vijana, na hapo varandani kulikuwa na ile meza yao Tesha ya dining, kiti kimoja ambacho alikalia rafiki mwingine wa Bobo, huku spika ya muziki ikiwa imewekwa kwa hapo juu ikishusha muziki mnene. Jamaa alikuwa ameunganisha tu simu yake kwa Bluetooth ya sabufa yao wakina Tesha, ambayo ndiyo iliungwa kwenye spika hiyo ili muziki uliotoka kwenye simu yake udundie hapo.
Milango yote ilikuwa wazi, mapazia pia yaliachanishwa ili ndani paonekane vizuri, nasi tukaelekea mpaka hapo ndani. Bobo akabaki nje hapo kwa mwenzake kwa ufupi, na sisi tulipoingia tukawakuta wenyeji na wageni wakiwa wamekaa sebuleni pamoja na watoto wengi wa majirani wa mtaani waliokuwa wamekaa kwenye uwazi ulioachwa pale sehemu ya dining.
Yaani sebule ilipanuliwa kwa kulisogeza pembeni sofa lililoukinga upande huo wa dining, kwa hiyo palionekana kama ukumbi mdogo uliopambwa kwa njia nyeupe na nyekundu, pamoja na watu waliopendeza pia. Baada tu ya mimi kuingia, mama Chande akatoa kama sauti za shangwe kunielekea mimi na wakina Tesha, na mashosti zake waliotufahamu wakaiga. Hizo ndiyo shobo nilizokuwa sifagilii, basi tu. Tesha naye akaanza kuongea kama MC fulani hivi kwa kusema mwarabu na mchina wa kitaa nimefika.
Nikawa nimetuliza tu hisia nikionekana kuchukulia hayo kuwa kawaida, na umakini wangu ukavutwa na Doris, Dina, pamoja na wanawake wengine wawili watu wazima waliokuwa wamekaa pamoja nao. Doris aliniangalia kwa shauku ya kirafiki, na mimi nikamfata hapo na kumsalimia kirafiki pia. Alifanya hadi kusimama na kunikumbatia, na Dina naye akafanya hivyo hivyo, kisha ndiyo wakawa wamenitambulisha kwa mwanamke mmojawapo hapo kuwa mama yao mzazi.
Nikamsalimu pia kwa heshima, huyu akiwa kama vile mama mdogo wake Miryam maana ndiye aliyekua pamoja na marehemu mama yake, na alionekana kuwa aina ya mwanamke aliyependa kuhukumu vitu yaani, kwa kumwangalia tu, saikolojia ya kidaktari ikawa imeniambia hivyo. Kwa hiyo nikaona niachane naye na kwenda kumsalimu Bi Jamila pamoja Ankia, waliokuwa hapo sebuleni pia.
Yaani hii sehemu yote ilionekana kubanana kabisa kutokana na jinsi palivyojaa watu, hapo chini watoto walikaa huku wakinywa juice na biskuti walizopewa, kule jikoni kukiwa na wanawake baadhi walioshughulika na msosi na kuja tena sebuleni, na sikuwa nimemwona Mariam, Bi Zawadi, wala Miryam; bila shaka wakiwa huko chumbani. Inaonekana Tesha alikuwa anataka kumkaribisha mama mkubwa wake kiaina, kwa hiyo akaelekea huko chumbani kama kuwashtua, kisha akarejea akiwa pamoja na Miryam. Ah!
Malkia wa moyo wangu alikuwa amevalia kwa njia ya kawaida tu, lakini alipendeza sana. Sikuwahi kumwona akiwa amevaa nguo yenye rangi ya maroon, na kiukweli hili gauni alilolokuwa amevaa sasa lilimfanya atamanishe mno macho na hisia zangu. Yaani alikuwa kama chakula ambacho hakikuwahi kuguswa, kumwangalia tu kulinisahaulisha shida zote za kichwani maana alinifanya nifikiri ni mimi tu ndiye niliyepaswa kuja kula hicho chakula!
Bibie mwenyewe akawa anajitahidi kuwatendea watu vizuri tu hapo, na inaonekana wakati niko kule kwa Ankia walikuwa wameleta na makreti kama matatu ya bia, bila shaka likiwa ni wazo la Tesha na Bobo, lakini yaliwekwa tu huko chumbani kwa Tesha na hakukuwa na wengine waliokunywa bia taratibu isipokuwa mama yake Doris, rafiki yake, Doris mwenyewe, Ankia, mama Chande, na wanawake wengineo hapo. Najua Miryam asingekunywa, kwa hiyo Ankia aliponipa ofa ya kufata moja ili nipoze koo, nikawa nimekataa. Leo ningeenda kwa mabiti ya bibie.
★★
Baada ya dakika kadhaa, Bi Zawadi, Shadya, na Mariam wakawa wametoka huko chumbani, kwa pamoja wakija sebuleni taaratibu kama vile mwanamke huyo alikuwa kimwanaharusi. Alipendeza kweli kwa kuvaa gauni refu jekundu lenye mistari myeupe hapa na pale, likiwa na muundo kama wa batiki, lakini ikiwa ni kitambaa kizito tu, na mtindo wa nywele za rasta zilizobanwa juu ya kichwa ulimpendezesha hata zaidi.
Alionekana vizuri sana, yaani alipendeza mno, na najua Shadya ndiye aliyekuwa amehusika kumpendezesha namna hiyo yeye na Mariam pia. Binti alivalia gauni la blue-bahari lisilo refu sana, na alikuwa amesuka nywele za kizungu za mawimbi zenye rangi ya brown, huku mbele ya mwanzo wa nywele zake akivaa tiara nyeupe. Walipendeza kama vile wasingekuja kupendeza tena!
Tukaanza na kuwapigia makofi, Tesha akiendelea kufanya u-MC kuwakaribisha na kumtambulisha Bi Zawadi kuwa kama "birthday girl," na Miryam alikuwa akichukua video kwa ajili ya kutunza kumbukumbu ya mambo mengi yaliyotokea hapa. Haikuwa ajabu kwangu kutambua kuwa wanawake waliokuwepo hapo, hasa ambao hawakunifahamu, walionyesha kuvutwa zaidi na uwepo wangu, wakinitazama sana na hata mara nyingine kusimama karibu nami nilipokuwa nimetulia tu kuwaangalia wapendwa wangu.
Lakini sikujishughulisha nao. Yaani nilitulia. Nilitulia kweli. Dina alikuwa akinitumia jumbe fupi kwenye simu na kutarajia tufanye ile kuchat ya kisiri, lakini nikampiga chini kama vile simjali. Yaani mpaka wakina Ankia, Bobo, mama Chande walinifuata kuniuliza vipi, mbona sichangamki bwana, na mimi nikawa natabasamu tu kwa kuwa niliamua kuitathmini kwanza furaha ya wote niliokuwa nawapenda sehemu hii. Hasa Miryam.
Kila mara nilipomwona akitabasamu pale wengine walipokuwa wakiburudika aidha kwa muziki, ama utani wa Tesha, nilihisi amani zaidi ya vile ambavyo nilikuwa kabla ya Festo kuja hapa muda ule. Ikawa wazi zaidi kwangu kuwa hiki ndiyo kitu nilichokuwa nahitaji zaidi ili kuepuka kujishusha moyo kisa huyo jamaa, na haingejalisha tena alikuja hapa kuongea na Miryam kuhusu nini; nisingeacha kuendelea kumwonyesha mwanamke huyo upendo wangu kamwe.
Kila mara ambayo Miryam angetazama upande wangu na kukuta namwangalia tu, angeacha kutabasamu na kufanya aidha shughuli nyingine ama kwenda jikoni, au wapi, akiwa bado analazimisha kuniepuka eti. Nikawa najikuta natabasamu mwenyewe tu kwa sababu hali hii nilikuwa nimeshaanza kuizoea, na ilifurahisha, kwa sababu najua ingeendelea kunizidishia motisha ya mbio zangu za kuufikia moyo wake mpaka kuukamata. Na matumaini ya kuwa pamoja naye bado yalikuwa chanya, kwa hiyo nisingekata tamaa.
Sherehe ikaendelea. Nikapata na juice ya embe ambayo nilimiminiwa na bibie mwenyewe kwenye glasi, na alifanya hivyo mbele yangu kama hataki yaani. Kwa muda huu nilikuwa nimeamua kutulia ndiyo, lakini jambo fulani likafanya niamue kwamba kuchangamka zaidi ingefaa, hasa kwa ajili yake Miryam. Kuna mara ambazo nilikuwa nikimwona mama yake Doris alipokuwa akimtazama Miryam, yaani, alimwangalia kwa njia isiyo rafiki. Miryam angepita hapo mara kwa mara na kusemeshana pamoja na watu wengine kirafiki, hata Doris pia, lakini huyo mama alimwangalia vibaya tu kana kwamba walikuwa na ugomvi.
Mpaka ikafikia hatua nikaona Miryam alipotaka kumwongezea kinywaji, mwanamke huyo akakataa, lakini Shadya alipotaka kumwongezea kinywaji hicho hicho, akakubali. Wengine hawakuwa wakitambua jambo hili, lakini niliona likimnyima Miryam amani kiasi. Huyo mwanamke alitakiwa kuwa kama mzazi kwake pia maana alikuwa na uhusiano wa karibu pamoja na marehemu mama yao wakina Miryam, sasa sijui alikuwa na shida gani mpaka akaona amtendee bibie namna hiyo.
Ikafika muda wa kukata keki sasa, nayo ikaletwa na kuwekwa hapo mezani, lakini haikufunguliwa kwanza. Yaani ilikuwa ndani ya kifaa kama boksi lakini lenye muundo mzito kama ubao, au hizi bodi za dari zinavyokuwaga ngumu (ceiling board), likiwa jeupe na lenye kishikio kwa juu ambacho kikivutwa ndiyo lote linafunguka na kuiachia keki iwe wazi.
Ikiwa imewekwa hapo, Tesha akasema, "Sawa sawa. Sasa... unajua... birthday girl wetu hapa anatimiza miaka 62, na amezaliwa kwenye tarahe 11 ya leo hii, mwezi wa 11 huu, na mwaka wa 61 ule. Lakini hebu mchekini kwanza! Sura na mwanya uoneokanao kama vile binti mbichi mbichi ambaye bado yuko kwenye miaka ishirini vile!"
Tesha akampamba Bi Zawadi namna hiyo.
Sote kwa pamoja tukacheka kidogo, naye Bi Zawadi akasema kwa maringo, "Jamani, me mwanya nimeutoa woopi..."
Tukafurahishwa zaidi na utani wake wa kuigiza kama mwanadada mdogo, naye Tesha akasema, "Upo kwenye loading huo mwanya, maana leo utakula keki mpaka meno ya mbele yatayeyuka!"
Bi Zawadi akacheka kidogo.
Tesha akasema, "Okay, okay. Sasa... umefika wakati maalumu wa bibi wetu kushika kisu na kuchinja keki. Jamani, fungua keki hiyo... watoto msiangalie nyuma, hakuna yai bovu huko, keki safi hii hapa, kwa hiyo macho yote yawe mbele..."
Ankia alikuwa karibu yake Bi Zawadi, kwa hiyo akamsaidia kukivuta kishikio cha boksi la keki, nayo ikawa imefunguliwa. Kweli ni keki moja nzuri sana ikawa amefunuliwa hapo mezani, ikiwa kubwa, yenye rangi nyeupe kwa nyekundu, ambayo mimi na Tesha tuliagiza ipambiwe na kamdoli ka mwanamke aliyeshika namba 62 wakati ule tumeenda kuitafuta. Vyote vilikuwa ni keki.
Miryam, Doris, Shadya, na wengine baadhi walikuwa wakichukua video kwenye simu zao, huku Ankia akimsaidia Bi Zawadi kuweka flare ndogo juu ya keki (vimshumaa vinavyowakaga kwa kutoa cheche kama fataki vile), tayari kwa kuwasha ili tumwimbie Bi Zawadi wimbo wa 'birthday' kwa pamoja kabla ya kuikata. Huu ndiyo ukawa wakati sahihi wa mimi kuanza kuchangamka.
Tesha akasema, "Sawa, sasa tunawasha hapo, simameni jamani watoto na watu wazima ili tumwimbie birthday girl wimbo wake mtamu sana wa...."
"Tesha, ngoja kwanza," nikamkatisha.
Watu wakaniangalia.
"Enhe, JC ana neno. Leta mambo handsome wa Kijiji..." Tesha akaongea hivyo.
"Ahah... wa kuleta mambo ni Mamu. Ana zawadi special kwa ajili ya birthday girl," nikasema hivyo.
"Wooow! Mamu jamani!" Bi Zawadi akasema hivyo na kuanza kumpigia makofi Mariam, ambaye alikuwa pembeni yake.
Akiwa na tabasamu mwanana usoni, Mariam akaniangalia na kunitikisia kichwa chake kama kuuliza kitu, nami nikamtikisia nyusi kukubali. Akatoka hapo upesi na kwenda chumbani huko kwanza, kisha akarudi akiwa na kile kinanda chake mkononi. Watu wakahisi binti alikuwa amekuja kujaribu kumpigia muziki Bi Zawadi, na hawakukosea. Akakaa kitini na kukunja mguu wake huku kinanda kikiwa katikati, nasi sote tukawa tunamwangalia kwa subira.
Mariam akaanza kupiga kinanda, yeye mwenyewe, akipiga ile midundo iliyotokeza sauti ambayo sote tuliifahamu kuwa ya wimbo maarufu utumiwao kwenye sikukuu za kuzaliwa. Yaani kinanda kilitengeneza melody ya 'happy birthday to you, happy birthday to you,' na hakukosea hata mara moja! Kwa waliokuwa wanafahamu juu ya tatizo alilokuwa nalo, walionekana kushangaa sana. Mama yake Doris akajisogeza mbele zaidi kwenye sofa ili asikilize kwa makini, na Mariam akaendelea kupiga kinanda tu kwa utaalamu wa hali ya juu sana.
Nikamtazama Miryam na kuona jinsi ambavyo alimwangalia mdogo wake kwa hisia sana, kisha akaniangalia usoni kwa umakini. Nikampa tabasamu hafifu huku nikimwangalia kwa hisia, naye akarudisha umakini wake kwa mdogo wake tena. Tesha akaanza kumsifia kweli Mariam na watu hapo kupiga makofi. Ankia akamwambia binti arudie tena kupiga midundo hiyo, halafu watu wote wafatishe na kuanza kumwimbia Bi Zawadi wakati ambao flare ingewashwa ili apulize na kutoa ombi lake kwa Mungu. Ikawa hivyo.
Mariam akaanza tena kupiga kinanda, nasi tukawa tunaimba kwa kufatisha sauti hiyo, na tukipiga makofi pia. Bi Zawadi alionekana kufurahi sana, akiwa amefunika mdomo wake kwa viganja huku akimtazama Mariam kwa hisia, naye Tesha akazidisha mbwembwe za maneno ili wimbo uendelee kuimbwa tu. Ankia akawasha mshumaa wa kwenye keki, huku bado tukiendelea kuimba, na Miryam alikuwa akichukua video tu kwenye simu yake huku akitabasamu kwa furaha sana.
Bi Zawadi akaendelea kuenjoy kwanza muziki aliopigiwa na Mariam kabla ya kuinama na kupuliza mshumaa wa keki kwa nguvu, nasi sote tukampigia makofi na wakina mama Chande kutoa sauti kwa shangwe. Ankia akampatia kisu laini Bi Zawadi ili aanze kukata keki, na mama huyu akajitahidi kukata vizuri vipande vya mwanzo, halafu Ankia akachukua kikopo cha stiki na kuanza kuzichomekea keki kipande kimoja-kimoja.
Bi Zawadi akataka wa kwanza kabisa kumlisha iwe ni Mariam, naye binti akanyanyuka na kwenda kula keki kwa furaha, kisha naye akamlisha mama mkubwa wake na kumkumbatia kwa upendo. Akafata Bi Jamila, kisha Miryam, ambaye alikumbatiwa na Bi Zawadi kwa karibia dakika nzima kabisa. Baada ya hapo akafuata mama yake Doris, Doris mwenyewe, Dina, Tesha, Ankia, Shadya, Bobo, mama Chande, na karibia wote walikuwa na kitu kizuri cha kumpa mama huyu kama zawadi, iwe ni kaelfu kumi, mkufu, kitenge kizuri, ama zingine zilizotiwa ndani ya maboksi, halafu ndiyo nikaja mimi sasa.
Bi Zawadi alikuwa ananiita kwa shauku sana kuwa niende kulishwa naye, nami nikamfikia na kula keki yangu, kisha nikamlisha yake pia. Halafu, nikaingiza mkono mfukoni na kuchomoa wallet yangu iliyokuwa imetuna, nami nikaanza kutoa elfu kumi moja baada ya nyingine. Nilikuwa nazitoa kwa madoido yaani, nikiziachia karibu na kichwa cha Bi Zawadi zimmwagikie tu kama mvua, na wanawake wakawa wanatoa sauti za shangwe kunishabikia yaani.
Bi Zawadi akawa amefumba mdomo huku akicheka kwa aibu, Bi Jamila naye akishangilia eti, nami nikamtazama Miryam kutokea pale alipokuwa amesimama. Aliniangalia kwa jicho makini sana, kama hataki eti, nami nikamtikisia nyusi kiuchokozi, na yeye akazungusha jicho na kuangalia pembeni, kitu ambacho kikanifanya nicheke kidogo na kumalizia kummiminia cheupe wangu pesa ya zawadi. Hapo nilikuwa nimemmwagia laki mbili kamili, wanawake wakiwa wamehesabu na kumshangilia cheupe wangu, naye akanikumbatia kwa furaha sana.
Nikaenda pembeni tena na kusimama karibu yake Mariam zamu hii, na ndiyo watu wengine wakaendelea kulishwa keki, na Tesha kuchangamsha sherehe kama ilivyotakiwa baada ya Bi Zawadi kuokotewa pesa zake na Ankia. Angekuja kujinunulia tuvitu tuzuri mwenyewe ahisi raha hata zaidi, cheupe wangu huyo. Ilikuwa siku yake!
Nilijikuta napenda sana hii kitu. Ilikuwa sherehe ya kawaida tu, mambo yasiwe mengi wala ya gharama za ajabu, lakini ushirika wa hawa watu na jinsi walivyoonyeshana upendo ulipatajirisha sana hapa. Halafu pia nikaanza kuona kwamba mama yake Doris alinifatilia sana baada ya hako kakitendo kangu muda mfupi nyuma, yaani aliniangalia mno mara kwa mara, nafikiri akiwa ameona kitu fulani ndani yangu kilichomfanya agundue mi' wa maana. Chezea!
Mariam akawa amemwomba Bi Zawadi alishwe keki tena, kale kamdoli eti, nasi kwa pamoja tukacheka kidogo. Bi Zawadi akamwita na kumlisha taratibu huku watoto wakimkodolea, halafu na yeye akamwomba Mariam ampigie kinanda kwa mara nyingine tena. Mariam akafurahi kufanya hivyo. Akaanza kumpigia kinanda tena, na watu wakaungana naye kuimba wimbo wa birthday kwa kufatisha sauti. Wakina Ankia na mama Chande walikuwa wameelekea jikoni pamoja na wadada wengine, nafikiri kuweka mambo ya msosi sawa zaidi.
Nikamwangalia Miryam. Alikuwa amesimama pembeni tu, akiwatazama Bi Zawadi na Mariam kwa hisia sana, nami nikasogea upande wake na kusimama karibu naye bila yeye kutambua kwamba nilikuwa nyuma yake. Doris, Dina, na wageni wengine walikuwepo hapo sebuleni pia, na niliona umakini wao ukielekea kwangu mara kwa mara, lakini sikuwajali sana wakati huu.
Nikamwambia Miryam kutokea pembeni, "Hiyo hapo."
Akageuza shingo yake kuelekea upande wangu, lakini hakunitazama kabisa.
Nikasema, "Unakumbuka tulivyoongea siku ile? Kuhusu Mamu?"
Akionekana makini zaidi sasa, akamtazama tena mdogo wake.
"Nilikwambia kuna ishara zingejionyesha Mamu akianza kuwa imara zaidi kiufahamu. Hiyo hapo moja, Miryam. Kumbukumbu yake inazidi kuwa imara. ASD inaondoka hivyo," nikamwambia.
Akaniangalia machoni kwa hisia makini.
Nikampa tabasamu hafifu la uhakikisho, naye akaacha kuniangalia na kumtazama Mariam tena, kisha akashusha pumzi na kunipita kuelekea jikoni bila kusema asante wala nini. Lakini najua kutoka ndani ya moyo wake kwamba alikuwa amefurahi sana kusikia hivyo, ni basi tu eti hakutaka nione hilo moja kwa moja.
Nikajisogeza tu pembeni tena baada ya hapo, na Mariam alipomaliza kupiga kinanda chake, Tesha kama MC akasema, "Haya, umefika wakati wa kuhalalisha rasmi kabisa umri wa bibi wetu mrembo. Mko tayari?"
Wanawake na watoto wakasema 'ndiyoo' bila hata ya kuelewa alichomaanisha, na Tesha aliponiangalia, tukajikuta tunacheka kidogo kwa kuwa ni mimi na yeye tu ndiyo tuliokuwa tunaelewa kilichokuwa karibu kutokea. Miryam akawa amerejea tena. Tesha akaomba kiti ili aweze kupanda usawa huo hapo katikati, na baada ya kufanya hivyo, akayafikia maputo huko juu na kuichukua kwa uangalifu ile kamba iliyobaki mwishoni, kisha ndiyo akashuka. Halafu akamvuta Bi Zawadi usawa wake na kusimama karibu yake.
"Hii ni zawadi nyingine kwa mrembo wetu Zawadi. Makofi kwake na vilegelege kwa kutimiza miaka 62!" Tesha akaongea hivyo kwa shauku.
Watu wakacheka na wakina mama Chande kupiga hivyo "vilegelege," halafu Tesha akaniangalia huku akijikaza asicheke. Nikamtikisia kichwa kama kumwambia aache tu, naye Miryam akaniangalia kwa macho yaliyoonyesha alikuwa ameshashtukia dili. Tesha akaivuta hiyo kamba na kumkimbia mama mkubwa wake ghafla, na yale maputo hapo juu yakaanza kupasuka moja baada ya lingine. Kila moja lililopasuka lilitoa vikaratasi vingi vidogo-vidogo vilivyomeremeta, halafu maputo mawili ya mwisho yakamwaga maji!
Miryam akafunika mdomo wake kwa kiganja. Bi Zawadi alikuwa bado amesimama hapo kati, kwa hiyo hivyo vikaratasi na maji yakawa yamemwagikia. Wakati maputo yalipokuwa yanapasuka na kutoa hivyo vikaratasi, watu walikuwa wanashabikia eeeeh, lakini maji yalipommwagikia Bi Zawadi, wengine wakaonekana kushangaa na kubaki kimya. Tesha akaanza kucheka, Mariam pia, huku Bi Zawadi akiwa amefumba macho, kisha naye akaanza kucheka.
Watu wengine wakaanza kucheka pia, Bi Jamila ndiyo alikufa mbavu yaani, naye Tesha akasema, "Maji ya baraka ya sikukuu ya kuzaliwa! Ulifikiri tungekuacha salama ma' mkubwa?"
Bi Zawadi akasonya kidogo na kusema, "Shenzi wewe!"
Wengine ndiyo wakazidisha vicheko, na maongezi kuhusu hicho kitendo yaanza hapa na pale. Nilikuwa nikijizuia nisicheke, lakini nilipomwona Miryam anatabasamu huku akitikisa kichwa chake, nikashindwa kujizuia tena. Ankia akaja karibu na kunilalia begani huku akicheka, na Doris akawa amemsogelea Miryam kumnon'goneza jambo fulani lililofanya kwa pamoja wacheke kwa furaha sana.
Bi Zawadi alipouliza nani aliweka hayo maputo yenye maji huko juu, mimi na Tesha tukanyoosheana vidole kama kulaumiana, naye Bi Zawadi akatikisa tu kichwa na kuanza kuelekea chumbani ili akajikaushe. Miryam akanikata jicho kali kweli eti kama vile hakupenda, maana alijua ni mimi ndiye niliyekuwa nimeyafunga maputo huko juu, nami nikabana tu tabasamu langu na kuamua kwenda uani kwanza kabla hajanitafuna. Lakini naelewa alikuwa ameburudika sana. Ilikuwa wakati wenye kiburudisha kwa kweli!
DJ Bobo pale varandani akawasha muziki tena. Tukawa tumemwomba Bi Zawadi samahani ya kummwagia maji bila kumwandaa baada ya yeye kurudi tena sebuleni, na alituvuta masikio mimi na Tesha, lakini akasema alikuwa ameburudika sana leo kwa kweli.
Akatushukuru sisi wote kwa kuifanya siku hii iwe murua mno kwake, na akaombea uzima wetu sote ili tuendelee kuwa pamoja kwa mazuri na magumu yote ya maisha. Na alimshukuru mno Miryam kwa kuwatunza wote vizuri kwa upendo, akimwombea mafanikio zaidi kwenye maisha yake. Na huyu mama alikuwa na maneno mazuri sana yaliyogusa hisia, mpaka nikajikuta nampigia makofi na wengine kufanya hivyo pia.
Baada ya hayo ndiyo wanawake wakaanza kusambaza upendo wa misosi kwetu sisi wote. Kwa watoto waliokuwepo, waliketi sehemu ya chini pale dining na kuwekewa kwenye masinia, wanawake wakila pamoja hapo sebuleni, na sisi wanaume tukawa kwa huku varandani tukila na kunywa pia taratibu. Wakina Bobo na Tesha walipiga bia mbili tatu, lakini mie sikunywa hata kidogo. Tesha ndiyo akawa ameniambia kuwa yule mpenzi wake, Happy, alibanwa na kazi hata kwa siku hii, ndiyo maana hakuweza kuja kujiunga nasi leo.
Kwa hiyo muda ukaendelea kusonga tu. Hakukuwa na nafasi ya fujo hapo, kila kitu kilikwenda kwa utulivu na utaratibu mzuri kabisa mpaka sote tulipomaliza kula na kunywa, kisha tukamalizia muda wa masaa machache kwa kuoiga story na nini, na watu wengi waliokuwepo wakawa wanaaga na kurudi makwao.
★★
Ikiwa imeshaingia mida ya saa tano, umati ukawa umepungua, hapo kwa Miryam tukabaki siye tu tuliokuwa na ukaribu zaidi na familia hii, yaani hata wanaume tuliokuwepo ilikuwa mimi, Tesha, Bobo, na jamaa wengine wawili waliokuwa na ukaribu na Tesha. Basi. Kule ndani walikuwepo wanawake, Doris na familia yake wangelala hapa leo, na ili wapate nafasi ya kutoshea ya vyumba, Tesha angekuja kulala pamoja nami pale kwa Ankia, na hata Shadya angelala pamoja na Ankia huku kwake. Haikuwa na noma.
Wakati huu nikawa tu hapa varandani pamoja na Bobo na hao jamaa wawili, muziki ukiwa umeshushwa sauti, na Bobo tayari alikuwa ameshaniambia kwamba alimtokea Ankia kimapenzi, na mwanamke huyo alimkubalia lakini alitaka jambo lao liwe la chini-chini kwanza; wengine wasijue. Zilikuwa ni taarifa nzuri, kujua kwamba Ankia alipata mtu wa kumpenda aliyetaka kutulia naye, nami nikampa pongezi Bobo na kuahidi kutunza siri yake.
Tesha alikuwa ameenda huko ndani ili arudi pamoja na chupa zingine za bia, na hata wakina Doris na Dina hapo sebuleni walikuwa wakinywa huku wanapiga story na Miryam, Bi Zawadi, Ankia na mama Chande. Inaonekana Bi Jamila na Mariam walikuwa vyumbani, na hata mama yake Doris na yule mwanamke waliyekuja naye hawakuwepo sebuleni pia.
Nikiwa nimeegamia tu ukuta huku nakula story za kuchorwa tattoo na nini kutoka kwa hawa wasela, Miryam akawa ametoka ndani na kuja hapo varandani pia, nami nikamwangalia kwa umakini. Akasemeshana na Bobo kiurafiki na kisha kuvaa ndala na kutupita sote kuelekea ule upande wa nyuma ya nyumba uliokuwa na stoo. Inaonekana alitaka kwenda kuchukua kitu fulani huko. Kwa hiyo kwa kuzuga, nikajivuta-vuta tu na kuelekea upande huo pia ili nikajaribu kumchokoza kidogo.
Uzuri hakukuwa na watu wakati huu ambao wangekuja kwa huku maana na sherehe ilikuwa inaelekea kuzimika hapo mbele, na nilipofika huko kwenye chumba cha stoo, nikamkuta bibie akiwa ndiyo anatoka humo na kutaka kurudi tena huku tulikotoka. Lakini akasitisha hatua zake baada ya kuniona nimefika mbele yake, naye akanishusha na kunipandisha kwa mtazamo wa kawaida tu. Ile 'na huyu naye vipi?'
Hakuonekana kuwa amechukua chombo wala kitu chochote kutokea humo stoo, kwa hiyo kwa sauti ya chini nikamuuliza, "Ulikuwa unatafuta nini?"
Akaendelea tu kuniangalia kimkazo kiasi.
Nikatabasamu na kusema kimchezo, "Hakuna kilichokuleta kuchukua, eti? Ulikuwa tu unataka nikufate..."
Bila kunijibu, akageuka tu na kuanza kuelekea huko nyuma zaidi, nadhani ili akapitie kwenye mlango wa huko nyuma ili kuniepuka. Nikatabasamu zaidi na kumwahi ili nimsimamishe kwanza.
"Miryam, sikia... usikimbi...."
Nilikuwa nimeanza kumfata huku nikisema hivyo kwa sauti ya chini sana, na yeye kusimama ghafla ndiyo kukafanya maneno yangu yakatike. Alikuwa amefikia kwenye kile kikona chenye nafasi nyembamba, pale pale ambapo nilimnyuka Dina siku ile, na kutokana na yeye kusimama ghafla yaani ikawa imefanya nikaribie kabisa kumgusa kutokea nyuma, na kabla sijajirudisha, nikatambua upesi kwa nini alisitisha kuelekea mbele zaidi.
"Kumbe?"
"Eeh, zilikuwaga za nondo, sa'hivi naona wameweka na chupa-chupa. Ni vizuri, hapa wezi hawaruki ukuta. Nimekuja sana hapa kipindi cha nyuma..."
Nikasikia sauti mbili za wanawake zikisema maneno hayo kutokea huko nyuma, na upesi nikatambua kwamba moja ilikuwa ni ya mama yake Doris pamoja na yule rafiki yake aliyekuja naye, ndiyo waliokuwa wakiongea hivyo. Inaonekana walikuwa wamekuja kwa huku nyuma ili kupaona, na labda kuzungumza kidogo.
Miryam akageuka na kutaka kurudi tena kwa upande wangu, sijui ili awaepuke, lakini nilikuwa karibu zaidi na yeye kwa hiyo akaishia kuniangalia usoni kwa kutotarajia niwe karibu naye namna hiyo. Kisha ndiyo akaashiria kutaka kunipita kwa kulazimisha mwili wake upite kwa kujibana sana hapo ukutani, na mimi nikajikuta natulia tu na kumwangalia alivyokuwa anahangaika kutaka kupita kwa lazima.
Hii ikafanya nyuso zetu ziwe karibu zaidi, na kwa makusudi nikakaza mwili wangu ili kuzuia yeye asisonge mbele zaidi, yaani abaki hapo hapo. Miryam akanitazama usoni kwa ile njia yake ya kuudhika, akiwa anajua nimemfanyia makusudi kabisa, nami nikajitahidi kubana tabasamu langu na kuamua kulegeza mwili ili apite, mwishowe angenimeza kweli!
Maongezi ya wanawake wale yakaendelea.
"Hivi ni kweli kabisa ulivyosema kuhusu huyo dada?"
"Nikudanganye kwa lipi sasa?"
"Hmm... basi ana lake jambo..."
"Siyo siri, me nakwambia. Na tena... hiyo siyo tangu Maimuna alipofariki tu, wala kwa sababu ya vurugu za Joshua na nini hapo juzi... ni tokea muda sana, mpaka me huwa nashangaa...."
Sauti ya mama yake Doris akisema hivyo ikasikika vizuri sana kwetu, na mkazo uliokuwepo usoni mwake Miryam ukafifia baada ya jambo hilo lililosemwa kuonekana kuteka zaidi umakini wake, na hakuacha kunitazama usoni. Mimi pia nikaendelea kumwangalia Miryam usoni kwa utulivu, nikiwa nimeweka umakini wangu kwake kwa sababu ya jambo hilo.
"Kwani tayari alikuwa ameshakuja huku?"
"A-aah, huku amekuja wazazi wake walipofariki... Maimuna alipofariki nimekwambia," mama Doris akasema hivyo.
"Ahaa, sawa. Eh! Mbona sasa anachelewa jamani? Mwanamke mwenyewe mzuri kweli, shida itakuwa wapi?"
"Ndo' maana nakwambia nashangaa. Tumeshamshauri sana, mimi na Shadya tumeshamtafutia wachumba wenye hela, lakini wote kawakataa. Mwanamke heshima ndoa, kuzaa, uwe na kwako na familia yako... yeye mpaka anataka kuzeeka ndo' aje kushtuka eti! Yaani sijui amekuwaje jamani..." mama Doris akaongea hivyo kwa sauti ya chini.
Ilieleweka kwamba wanawake hao walikuwa wanamwongelea Miryam, naye bibie akashusha macho yake kutazama chini huku akionekana kuanza kuhuzunishwa na jambo hilo. Kwa mara ya kwanza leo nikawa nimetambua kuwa marehemu mama yake na Miryam aliitwa Maimuna, na mama Doris kumsema hivyo bila shaka kulimtia simanzi kuu Miryam. Nikawa namtazama kwa hisia.
"Hakuwaga hivyo? Alikuwa na wanaume?"
"Ndiyo, alikuwaga tena anatoka na mtu wa maana nakwambia. Eti akaachana naye, kisa nini sijui. Sasa hivi amekuwa mfungwa kwa hii familia, Doris ni mdogo kwake lakini anatangulia kuolewa.... nakwambia ataendelea kukaa hivyo hivyo hadi huyu mdogo wake wa kike ataolewa ye' anakodoa tu. Sijui anafikiri atakuja kuazima ndoa ya mtu? Labda kwa sababu tu ya huo uzuri?" mama Doris akasema hivyo.
Miryam akafumba macho yake na kutikisa kichwa taratibu, akionekana kutoamini.
"Usiseme hivyo ila, tusimwombee mabaya. Ni vizuri ametulia, labda uje tu ujaribu tena kuongea naye. Atakusikiliza," rafiki akaongea hivyo.
"Ah, me nilishachoka. Ameshakuwa mtu mzima, tumemjali mno, imetosha. Sa'hivi tunajali hawa makinda waliobaki. Yeye kama kaamua kujilaani eti kisa ameachiwa familia ya kutunza... ni yeye. Atakapokuja kujuta baadaye lakini, atakuwa ameshachelewa. Na amechelewa mno. Yaani hataolewa huyu. Ndoa isimame kabisa? Haipo. Me nakwambia, atabaki kudandia ndoa za watu kama siyo kutumiwa na wanaume ambao watamwacha na mamichango tu..." mama Doris akasema hayo.
Aisee!
Rafiki yake akasikika akisema, "Basi turudi ndani, tukikutwa hapa tunapiga umbea!"
"Ahahahah... siongei kwa ubaya, ni ukweli tu. Tushamshindwa. Loh! Twende tukale tu keki tena..." mama Doris akaongea hivyo.
Inaonekana wanawake hao wakawa wamerudi ndani tena, bila kujua kuwa sehemu ndogo ya maongezi yao kumhusu mwanamke mwenzao ilikuwa imemwachia hisia mbaya na nzito sana maana aliwasikia. Najua Miryam aliumizwa na maneno ya mama yake Doris. Yaani mtu aliyemwona kama mama mdogo ama shangazi yake, ndiye aliyekuwa akimsema namna hiyo kabisa, tena hapa hapa nyumbani kwake? Lazima iliuma.
Miryam akawa bado ameinamisha uso wake kiasi, akionekana kuhuzunishwa na utambuzi wa jambo hilo, nami nikapatwa na hisia ya simanzi kumwona namna hii. Nikaweka tu kiganja changu kimoja usawa wa shavu lake na kuligusa, kisha nikalishika lote kwa njia yenye kumpatia faraja ya bila maneno. Akapandisha macho yake na kunitazama usoni kwa macho yaliyojaa hisia zilizovurigika kiasi, na najua aliweza kuiona hisia yangu ya uelewa wa hali yake ndani ya macho yangu kwa jinsi nilivyomtazama pia.
Nikataka nimwambie kitu chenye kufariji ili asiwazie sana kuhusu maneno ya mama yake Doris, nami nikasema, "Miryam... hayo yote siyo kweli. Sawa? Haujajilaani popote. Hawa hawakujui, hawawezi kuelewa kwa nini una...."
Akaacha kuniangalia na kuweka kiganja chake kwenye kifua changu kama kunizuia nisiendelee, kisha taratibu akautoa mkono wangu kutoka usoni kwake na kuondoka hapo; akielekea kule mbele tulikowaacha wakina Bobo. Nikajihisi vibaya kweli.
Sasa ndiyo ikaeleweka vizuri zaidi kwangu kwa nini mama yake Doris alimtendea Miryam kwa njia fulani ya masengenyo. Lilikuwa tu ni suala la mwanamke huyu kukataa wanaume wengi waliokuwa wametafutwa kwa ajili yake ili aolewe, yaani ile tu kwamba aliwapiga chini ndugu zake katika harakati zao za kujaribu kumshurutisha aolewe. Walikuwa wanataka kumpeleka sana, lakini yeye kuendelea kuwa na msimamo ndiyo kitu kilichowafanya wakerwe naye mno. Si wanaukoo ndiyo huwa wako hivyo?
Kwa sekunde chache nikabaki tu sehemu hiyo nikimfikiria kidogo, maana ilikuwa wazi kwamba alibeba mambo mengi mazito moyoni yaliyomsumbua mno kihisia. Ilikuwa ni vita kwake akiwa kama mwanamke kupambana na jinsi jamii ilivyomchukulia, ingawa najua haikuwa lazima kujali hilo, lakini matokeo ya maamuzi yake yaliathiri kwa njia nzuri au mbaya jinsi ambavyo alionwa na jamii nzima mpaka kufikia kwenye familia yake, na watu aliowajali.
Katika hilo pia, ningetakiwa kumsaidia. Najua nisingeweza kubadili jinsi ambavyo watu walimfikiria, lakini ningeweza kufanya jambo fulani ili kubadili jinsi mambo yalivyokuwa kwake yeye. Hapo mbele naelewa kungekuwa na mengi magumu kwenye uhusiano wangu pamoja naye kuendana na yote yaliyokuwa yakimzunguka, lakini ningehakikisha anaipata heshima aliyokuwa akiistahili kutoka kwa watu wote waliokuwa wameishusha. Na huyo mama yake Doris angeisoma!
★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★
Full Story WhatsApp or inbox
Whatsapp +255 678 017 280