Simulizi: Mimi na Mimi

Simulizi: Mimi na Mimi

IMG-20240604-WA0020.jpg


Inaanza...
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KWANZA

★★★★★★★★★★★★★★


Wiki nne zikawa zimepita baada ya mambo yale yote kutokea. Ndiyo. Mwezi mzima. Najua, najua... JC natakiwa nielezee yaliyotokea ndani ya huo muda wote, nimekoswa sana naambiwa, na kiukweli ni mengi mno yaliyokuwa yametokea mpaka kufikia sasa. Mengi yenye kuridhisha, na baadhi yenye kukwaza kwa kiasi fulani.

Tuanze na Joshua. Mwanaume huyo, baada ya kuwa amemfanyia binti Mariam vitendo vya kinyama kwa kujaribu kumuua zaidi ya mara moja na kutunga hila kibao ili tu aitaifishe mali ya binti, alikuwa amepelekwa mahakamani kwa kufunguliwa kesi ya makosa mbalimbali ya jinai.

Ndani ya huu mwezi ulioisha yaani, alifikishwa mahakamani zaidi ya mara tatu kujibu mashtaka ya hila za udhulumaji, au uporaji mali kwa kutumia hati bandia za kimahakama, vitendo vya kijeuri kama vile kupanga mauaji, na pia kuna mtu mwingine akawa ameongezea ishu ya kumkodisha gari jamaa na kuahidiwa malipo, lakini hakulipwa na badala yake gari lilirudishwa likiwa limeharibika.

Kesi zake mbili za kupanga mauaji na wizi hasa ndiyo ambazo zilikuwa nzito kwa huyu Joshua, ushahidi ukiwepo wa kuridhisha kabisa, naye akawa amepewa adhabu ya kwenda kutumikia kifungo cha miaka kumi jela. Siyo mchezo! Mvua ya miaka kumi!

Waliokuwepo sanasana kwenye mahudhurio ya kesi ya jamaa ilikuwa ni mimi mwenyewe, askari Ramadhan na mwandamani wake, Tesha, Khadija, Yohana wa Kleptomaniax, Bi Zawadi mara mbili, na Miryam pia mara moja; kwenye siku ambayo jamaa ndiyo alipewa hukumu. Ushahidi alioutoa huyo Khadija na Tesha kwenye suala la yeye Tesha kutekwa pamoja na mdogo wake ili wauawe, ulikuwa nyundo nzito sana ya kuupigilia ndani zaidi msumari wa hukumu ya haki aliyopewa jamaa. Huko ndiyo angeenda kulia na kusaga mipira yake vizuri!

Tulihakikisha haya yote hayamfikii binti Mariam kwa muda wote yalipoendelea mpaka kumalizika, na ilionekana kwamba familia yake iliridhishwa mno na hukumu aliyopewa huyo Joshua. Alistahili hata cha maisha kabisa, ila kuna vitu vitu tu vilipunguzwa, hadi nilishangaa kiasi kwamba Khadija hakula hata miaka miwili kwa sababu ya kusindikiza uhalifu ilhali wenzake wote, wale wakina Yohana wa Kleptomaniax, wote walikula mvua za miaka mitano mpaka saba jela kwa kusindikiza maovu ya Joshua. Hakukuwa na neno, la muhimu likawa kwamba mbaya wa amani ya familia yake Mariam alikuwa amewekwa mbali hatimaye.

Tukija upande wa madam Bertha sasa, mambo kweli yalikuwa 'underway' kama msemo wake. Yaani ndani ya hizi wiki tatu za mwisho zilizokuwa zimekata, tayari alikuwa ameshanionyesha sehemu ambayo biashara yake ya kutengenezea cocaine ingefanyikia, na kupitia mimi, tayari unga ulikuwa umeshaanza kutengenezwa, kuongezwa, na sasa ulikuwa kwenye harakati za kusambazwa.

Mwanzoni ilibidi kutoa kiasi fulani kama kionjo, kidogo-kidogo, kisambazwe hapa na kule ili watumiaji waelewe kulikuwa na zigo jipya jijini, na wanajeshi wake waliofanya kazi ya usambazaji wangetangaza pia bei mpya ya kuyapata madawa hayo yaliyokuwa yameanza kushika kasi mpya kwenye soko hilo jijini.

Kufikia wakati huu, tayari nilikuwa nimeshaona na kusoma njia zao kuu za kufanya usambazaji wa kisiri, na kiukweli zilikuwa njia ambazo sikutegemea mwanzoni, ila walikuwa wanatumia akili sana. Madawa yao yalipita sehemu na maeneo yenye hadhi za juu, mashuleni, vyuoni, mpaka kwenye makampuni, na haikuwa rahisi kwa yeyote ambaye hakuwa ndani ya hili game la uuzaji kujua jinsi ambavyo ishu hiyo iliendeshwa.

Kwa muda wote huo, nilikuwa nimejitahidi sana kumwonyesha madam Bertha kwamba nilikuwa makini na kazi aliyotaka tuifanye, na alinifurahia mno. Hadi wale wanaume ambao tulienda kukutana nao African Princess casino siku ile walisifia sana kazi yetu mpya, kwa hiyo kuna mara ambazo tungekutana, na wao kujiachia sana mbele ya ushirika wangu.

Lakini hawakujua kwamba kwa muda huo wote, mimi nilikuwa nafanya kazi na askari mpelelezi Ramadhan, na uamuzi wa kusubiria kwanza kabla ya kuchukua hatua dhidi ya watu hawa ulikuwa ni wake. Haikuwa tena juu ya suala la mauaji ya Joy tu, la. Sasa hivi kwa sababu mambo mengi yalikuwa yanaongezeka, ingebidi tuwe na kila kitu tulichohitaji ili yeye askari Ramadhan na wenzake wakipiga tu hatua kuwaweka chini ya ulinzi watu wote wa Bertha, iwe ni moja kwa moja. Yaani kusiwepo na njia ya kurudi nyuma tena.

Ila kama ni kitu kilichokuwa kikinifanya nikune kichwa changu bado ilikuwa ni kutojua nitumie njia ipi ili kumkamatisha na Festo pia. Aisee, yule jamaa sikumwelewa. Yaani, alikuwepo, lakini ilikuwa kama vile hayupo. Ningemwona tu alipotaka nimwone, lakini nisingeweza kujua alifanya mambo yake kwa njia zipi. Hawa wengine walikuwa wepesi kufunguka kwa mambo mengi na hivyo ilikuwa rahisi kuwa na vitu na sehemu za kuwakamatia, lakini Festo? Hapana.

Nilitakiwa kupata kitu cha kumnasia huyo jamaa, hasa kwa kuwa bado aliendelea kumfatilia bibie Miryam akimtaka kimapenzi. Mwanamke huyo hakuonyesha utayari wa kuwa ndani ya mahusiano ya kimapenzi kwa kipindi hiki kwa kuwa kweli fikira zake zote zilielekezwa kwa Mariam. Karibia mara zote ambazo nilienda pale kwake na kuwa pamoja na mdogo wake, Miryam alikuwepo, na alijitahidi sana kuniunga mkono kwa kila jambo nililofanya ili binti Mariam aweze kukaa sawa tena.

Wiki hizi nne za kuendelea kumsaidia Mariam zilihusisha lile suala la kumpeleka hospitali kwa ajili ya vipimo, na shukrani kwa Mola tukawa tumepata uhakika kuwa binti hakuingiwa vibaya kimwili, na hivyo alikuwa safi na salama kabisa. Hatukumwambia hilo, wala kuongelea waziwazi mbele yake mambo yaliyotokea usiku ule alipotekwa, na kadiri mazoezi ya kuuimarisha utimamu wake yalivyoendelea, ndiyo akawa anaendelea kufunguka kiutambuzi.

Mwezi mmoja tu ukatosha kumfanya Mariam aanze kuzungumza kama ilivyokuwa awali, hata nyakati nyingine angewaita watoto wa hapo mtaani ili acheze pamoja nao ndani ya geti la nyumba yao. Alionyesha tabia za kitoto bado, lakini haikuwa kwa jinsi niliyokuwa nimemkuta mwanzoni kabisa. Wote tulijitahidi sana kumfanya afurahie maisha yake, na kilichokuwa kimebaki ikawa ni kumjuza kutambua tena yeye ni nani, na angepaswa kuwa nani kwenye maisha yake kwa mapenzi na uchaguzi wowote alioutamani.

Chalii Gonga, mume halali wa madam Bertha, alikuwepo bado katika shughuli za biashara ambazo mke wake alimwachia, na mara kwa mara tungeonana pale Masai nyakati ambazo ningeenda na Tesha pamoja na Ankia. Mara hizo zote tulizokutana, hatukusemeshana, na alifanya iwe wazi kwamba hakutaka kunisogelea kabisa kwa sababu nafikiri kuna kitu ambacho Bertha alikuwa amefanya ili kuleta hali hiyo.

Sikuwahi kumuuliza tena mwanamke yule kama kuna jambo lolote lilitokea baina yake na Chalii hasa baada ya jamaa kunikuta kwenye chumba cha hoteli ya madam siku ile, maana ndani ya hizo wiki chache nilikuwa nimekutana kimwili na huyo mwanamke karibia mara tano, lakini hakutaka kumzungumzia mume wake kwa undani, na mimi nisingeweza kumsukuma.

Ila hali hii baina yangu na Chalii Gonga ilinionyesha wazi kwamba jamaa alikuwa amenyamazishwa. Lakini yote kwa yote, bado niliendelea kujitahidi kuwa makini sana mara zote ambazo ningemwona, kuepusha tu matatizo kwa upande wangu, yaani ya moja kwa moja, maana bado kuna hisia iliyokuwa ikiniambia kwamba mwanaume huyo alipanga kitu fulani. Kuwa chonjo ilikuwa lazima.

Na tukija upande wa familia yangu, haikuonekana kuwa na tatizo lolote tena upande wa mzee wangu, Mr. Frank Manyanza, tokea nilipokwenda kwenye ofisi yake kumwelezea vizuri kuhusiana na ishu ya Joshua kuihujumu familia yake ili aliuze shamba. Hakunitafuta kabisa kuongelea hilo suala tena mpaka Joshua amefungwa jela, na mimi nikachukulia kwamba mambo yalikwenda poa.

Nilikuwa nimeshafanya safari fupi ya kuwatembelea mama na dada yangu na kuwasalimia pia, na tuliweza kuongelea mambo mengi sana na mama kuhusiana na maisha yangu, nikimwambia tu kuna vitu vya huku ningekuja kushughulika navyo nikishatoka likizo, na nikamtia moyo Jasmine asonge mbele kutoka kwa mwanaume yule ambaye hakujali hali yake.

Mwanaume wake hakuwa mtu mwelewa, na alitoa maneno machafu sana hata alipokorofishana kidogo tu na Jasmine, na mimi nikawa nimemshauri tu dada yangu aachane na mtu ambaye hakumpa heshima, kwa kuwa bila hicho upendo ungetoka wapi sasa? Akawa ameniahidi kuwa angesonga mbele, na mimi nikamwahidi kuja kumjulia hali hapo kwetu kwa mara nyingine kabla ya wakati wake kujifungua kuwadia.

Kwa hiyo kwa ujumla ikawa ni kwamba kwenye suala la Joshua nilipata ushindi, masuala ya Mariam na Bertha ndiyo yakawa kwenye kalenda bado za kutarajia ushindi, lakini huyo Festo ndiyo bado akawa kikwazo. Ila nisingekata tamaa. Zamu hii sikutaka kumwambia bibie Miryam, oh kuna hiki, au kuna kile, hapana. Nilitaka nije nifichue kila kitu kwa vitendo tu. Na najua angekuja kushangaa mno baada ya kugundua rangi halisi ya yule mwanaume.

Nilikuwa nimewasihi watu wa familia yake Miryam wasije kuzungumza na watu wa nje kuhusiana na ishu yote ya Joshua, na waliafikiana na hilo, lakini lengo langu hasa lilikuwa kuhakikisha habari za mimi kushirikiana na polisi mpaka kumkamata Joshua hazifiki kwa Festo; maana ingemwashia taa nyekundu ya hatari na hivyo kumfanya aanze kunifatilia zaidi.

Ni huyu jamaa tu ndiyo aliyekuwa mwiba mgumu sana kwangu uliobaki kung'oa, na nilitaka kuhakikisha namwondoa pia maishani mwake Miryam kabla ya matatizo mengine kujitokeza....


★★★


Basi bwana, hivyo ndivyo mambo yalivyokuwa. Mpaka kufikia sasa bado nilikuwa kwa Ankia, tukiendeleza maisha yetu ya mama mwenye nyumba na mpangaji wake, na urafiki wetu ulizidi kukua. Hiyo hasa ilitokana na kujuana naye kwa mengi zaidi ya story na msosi wake mtamu tu, ikiwa unaelewa namaanisha nini. Kufikia sasa mwanamke huyu alikuwa amefungua biashara nzuri sana ya duka, alipouzia vijora, suruali za wanawake, pamoja na nguo za watoto wa kike, watoto wadogo yaani, hapo hapo Mzinga maeneo ya barabarani kwenye shughuli nyingi.

Kwa hiyo kutokana na kazi yake, tungeonana kwa mida iliyoachana-achana sana, hasa jioni, usiku, au asubuhi tu. Ratiba yangu ya kutoka kwenda kwenye ishu ya madam Bertha ilikuwa kwa siku za Jumatatu, Jumatano, na Ijumaa, kuanzia asubuhi mida ya saa nne mpaka jioni. Mwanzoni ilikuwa na ulazima sana kukaa huko mpaka jioni, lakini kwa wakati huu, ningeweza hata kuondoka mapema maana wengi wa vijana wake walielewa namna ya kuunda yale madini. Sema tu ndiyo niliwekwa kama msimamizi eti!

Hivyo, nilikuwa na muda na siku za kutosha kukaa na binti Mariam na kuendelea na tiba yake. Kwa kipindi hiki, Tesha alikuwa anahangaikia zaidi kupata kazi nzuri ambayo ingemfaa, lakini hakuwa amepata kwa hiyo aliendelea kutulia huku akipata michongo ya hapa na pale mara kwa mara iliyomwingizia pesa ya matumizi yake binafsi ama kusaidia familia pia akiwa kama mwanaume. Hali kwa familia yake ilikuwa tulivu zaidi kwa wakati huu, na nilitamani sana iendelee kubaki namna hiyo hiyo bila drama nyingi kama zile za wiki kadhaa nyuma kutokea.

Sasa, leo ilikuwa ni siku ya Alhamisi, asubuhi na mapema kabisa. Kulikuwa na ishu ya maana sana kwa mrembo wangu iliyonihitaji, cheupe mwenyewe Bi Zawadi. Mwanamke huyo alikuwa na mpango wa kwenda sehemu fulani iliyoitwa Chamgando, ukiwa unaelekea Kisemvule kule sijawahi hata kufika, akiwa na lengo la kumwona mtumishi fulani wa kanisa la kilokole huko kwa ajili ya maombi "spesho" ambayo husafisha mabalaa yake, na kwa niaba ya familia yake.

Ingekuwa kama kwenda kwa Mwamposa tu lakini alikuwa anamjua vizuri sana mtumishi wa huko Chamgando, akisema ni mzuri sana, ana maono, nakwambia yaani dah! Ndiyo nikawa nimepata na huo mwaliko sasa wa kumsindikiza, na mimi ningefanyaje? Nisingeweza kumkatalia mrembo wangu. Ni kitu ambacho alikuwa ameshakililia kwa wiki chache sasa lakini kutokana na mambo ya hapa na pale nikawa sijaweza kuambatana naye, sanasana alikuwa akienda na Tesha kwa nafasi za Jumapili, hivyo leo ningeenda pamoja naye. Ahadi ni deni kama ujuavyo.

Kwa hiyo nilikuwa nimeamka mapema sana, nikajiandaa vizuri na kuvalia T-shirt langu jeupe la mikono mifupi, suruali nyeusi ya jeans, na kiatu cheusi kinachong'aa chenye muundo wa kiatu cha ballet, hutu ambato wakorea walitufanya tukawa fashion kwa kuvalia bila soksi na suruali ya kitambaa ikiwa imevaliwa kama njiwa. Nilikuwa nimetununua wiki moja nyuma, na sasa ndiyo ikawa mara ya kwanza kuvitumia.

Hii ikiwa ni mida ya saa mbili asubuhi sasa, nikatoka zangu na kuagana na Ankia, akiwa ananiambia mwonekano wangu ndiyo ungefanya watu wafikiri mimi ni mchina kweli, akisema nimependeza, nami nikamshukuru na kumwambia tungeonana baadaye. Nikatoka ndani hapo na kuanza kuelekea nje.

Nikiwa usawa wa ukuta uliotenganisha nyumba hizi mbili, nikamwona bibie Miryam akiwa anapiga deki sehemu ya kibaraza chao kutokea kule ndani, ikiwa wazi hakuwa ameenda kazini bado, nami nikaelekea nje mpaka kufikia getini kwao. Mvua zilikuwa zikinyesha mara kwa mara hasa mwezi huu ulipoingia, na jana pia ilinyesha kwa hiyo ardhi ilikuwa mbichi.

Nikaufungua mlango mdogo wa geti la nyumba yao majirani zetu kwa kuvuta kikamba nilichokuwa nimemsaidia Tesha kuweka siku ile, na nafikiri leo ndiyo ningekuwa mgeni wa kwanza kufika hapo ingawa hawa watu walinichukulia kuwa kama mwenyeji wao tayari.

Ile tu ndiyo nimeingia, nikamwona Miryam akijinyanyua na kusimama kutoka kwenye kuinama kwake kupiga deki, na baada tu ya kuniona pia, akaachia tabasamu la furaha lililofanya sura yake ipendeze sana. Mimi pia nikatabasamu na kujikuta nimeendelea tu kumtazama kwa furaha pia.

Alikuwa amevaa T-shirt nyeusi ya mikono mifupi, huku kutokea kiunoni akijifunga kwa khanga safi lakini niliweza kuona kwamba ilificha suruali laini nyeusi, labda skinny, aliyokuwa amevaa kwa ndani na kuivuta juu kiasi miguuni. Nywele zake laini na ndefu alikuwa amezibana juu ya kichwa chake, na weupe wake uliomulikwa kwa jua la asubuhi ulimfanya aonekane kung'aa mikononi kutokana na umaji iliyokuwa nayo.

"Karibu."

Akaniambia hivyo kwa sauti yake tamu sana. Na ndiyo iliyokuwa moja ya sauti za kwanza nilizohitaji kusikia kwa asubuhi hii!

Nikasema, "Asante," kisha ndiyo nikarudishia mlango wa geti na kuanza kuelekea hapo kibarazani, nikilipita gari lake huku nalipiga-piga kidogo kwa kiganja.

Akawa ananitazama kwa yale macho ya 'nakuona,' kisha akasema, "Mzee wa kung'aa!"

Nikatabasamu kidogo na kuinua viganja vyangu huku nikijiangalia kwa majivuno, nami nikamwambia, "Kama kawaida yangu."

Akacheka kidogo kwa pumzi.

"Naona unapiga usafi," nikamwambia hivyo.

"Yeah. Kama kawaida yangu," akasema hivyo pia.

Nikatabasamu kidogo huku nikiangalia ulowani wake wa jasho uliofanya nywele zake zilainike.

"Mamu bado hajaamka," akaniambia.

"Ah, hamna shida... Mamu tutaonana baadaye. Nimekuja kumpitia cheupe wangu," nikamwambia hivyo.

"Ahaa... ee kweli ameniambia... unamsindikiza kwa mtumishi, si ndiyo?" akasema hivyo.

"Mm-hmm," nikakubali.

"Ahah... alivyo na hamu ya kwenda nawe! Kama vile mnaenda date," akatania.

"Ahahah... usipime! Ila nina hamu pia ya kwenda, maana... sikumbuki mara ya mwisho nimeenda kanisani ilikuwa lini. Ndo' nafasi ya kuanza kumrudia Mzee wa Siku physically hii," nikamwambia.

"Wewe pia unataka kuponywa?" akauliza.

"Eeh, kama itawezekana... fresh. Siyo kwamba naumwa au nini, ila... najua ibada ni muhimu haijalishi dini ni ipi. Biblia inasema pale ambapo kuna roho ya Mungu watu wake wanapaswa kukusanyika pia, kwa hiyo kuwa na sehemu za ibada ni lazima ili kuwakusanya watu wamwabudu na kumsifu... na kuwaombea wengine," nikamwambia hayo.

"Wacha! Kumbe na Biblia unasomaga?" akauliza.

"Huwa nasoma kila nikipata nafasi, nina app kwenye simu. Mistari miwili, mitano, natafakari, namshukuru Mungu. Angalau kale ka-touch na muumba kanakuwepo bado... ndiyo maana ananifanya nazidi kuwa handsome," nikamwambia hivyo.

Miryam akacheka na kuinamisha uso wake, yaani kile kicheko laini cha kutoka moyoni. Alionekana kufurahi sana.

"Hahah... au nadanganya?" nikamuuliza.

Akaniangalia na kusema, "Hamna... ahahah... ni kweli kabisa."

"Sa' mbona unanicheka?" nikamuuliza huku nikitabasamu kiasi.

"A-ah... ahahah... siyo hivyo, yaani... unaongea kama Tesha," akasema hivyo.

"Ahah... eeh, akili zetu zinafanana ndiyo maana tunapatana," nikasema hivyo.

"Kweli. Ila... naona kama we' umemzidi kidogo. Atakuwa anachukua madarasa kutoka kwako," akasema hivyo.

Nikacheka kwa furaha kiasi, naye akacheka pia, kisha kwa sekunde chache tukabaki kuangaliana machoni huku tukitabasamu. Ulikuwa utizami wa uliojaa upendezi mwingi sana, sote tukiwa tunafurahia hali hii mpya ya urafiki baina yetu, naye Miryam akaibana midomo yake kiasi na kutazama pembeni, kitu ambacho kikanifanya mimi pia niache kumwangalia usoni na kushusha macho yangu kuelekea chini.

Ndipo akaniangalia na kusema, "Karibu mwaya. Karibu ndani... ma' mkubwa atakuwa anamalizia kujiandaa."

Nikawa nimemwangalia na kusema, "Sawa. Inabidi nivue viatu ili nisikuchafulie...."

"Hamna shida, pita tu," akanikatisha kwa kusema hivyo.

"A-ah, hamna bwana. Kuvua viatu lazima," nikasema hivyo na kusogea pembeni huku nikianza kuvua kiatu.

Akawa anatabasamu na kusema, "Kumbe na we' unajali usafi eeh..."

"Uhakika. Hiyo ishu naielewa inavyochosha. Mama alipokuwaga akipiga deki halafu sisi tupite tu na miguu yetu, wee! Tungeinama kudeki nyumba yote," nikamwambia hivyo.

"Ahahah... hata kama hamjachafua kwingine?" akauliza.

"Yaani kote! Lilikuwa somo zuri ili tusirudie tena," nikamwambia nikiwa nimemaliza kuvua viatu vyote.

"Aliwapatia. Haya, ingia ndani. Me namalizia hapa," akasema hivyo.

"Sawa," nikamjibu.

Akainama tena na kushika dekio, nami nikawa namwangalia tu kwa utulivu, kisha ndiyo nikaingia ndani hapo na kurudishia mlango.

Nilijihisi vizuri sana kuwa na hako kawakati pamoja na huyo mwanamke, yaani ile hali nzuri ya kirafiki tuliyokuwa nayo sasa ilinipa amani sana na kujenga hamu ya kutaka kuendelea kuukuza na kuukuza tu huo urafiki. Ni mengi tuliyokuwa tumepitia na huyu dada mpaka kufikia hatua hii ambayo mwanzoni nilidhani isingekuwa rahisi kufikiwa, kwa hiyo niliithamini sana.

Hakukuwa na mtu hapo sebuleni, nami nikasogea mpaka sehemu ya dining na kumwona Bi Jamila akiwa anatengeneza chai pale jikoni kwao. Na ilikuwa mapema kweli, kwa hiyo nikawaza labda hata ilikuwa ni uji. Nikaelekea mpaka upande huo wa jikoni na kumsalimu, naye akaniitikia vizuri sana huku akinikaribisha kupika. Alikuwa akitengeneza dawa ya kuchemsha, kwa ajili yake mwenyewe, kisha ndiyo angeandaa na chai pia.

Kwa kuelewa kwamba nilikuja kumpitia mwenzake, akawa ameniambia ndiyo sasa hivi tu Bi Zawadi alikuwa ameingia chumbani ili kuvaa, na kweli nikasikia sauti ya mrembo cheupe wangu kutokea chumbani ikinisemesha, JC bwana karibu, sichelewi, natoka sasa hivi tunaenda. Nikamwambia atumie muda wote aliohitaji kumaliza kujiandaa, nami nikaendelea kusimama pembeni yake Bi Jamila na kuongelea dawa hiyo aliyokuwa akichemsha.

Baada ya dakika chache tu, Miryam akawa amerejea ndani kwa kilichoonekana kuwa amemaliza kupiga deki, naye akaelekea chumbani kwake huko. Nilikuwa nikitamani sana yaani katukio kokote kale kajiunde tu ili arudi huku na niweze kumsemesha tena, basi tu ilikuwa imeshajijenga ndani yangu kutaka kumwangalia kwa ukaribu au kunena naye mara kwa mara.

Sifichi kuwa upendezi wangu kumwelekea mwanamke huyo ulikuwa mkubwa zaidi kwa wakati huu, lakini najua nilitakiwa kuendelea kuheshimu uhusiano wetu wa udada na ukaka tuliokuwa tumejenga, na hivyo kunizuia kuvuka mipaka kimawazo kumwelekea. Kama unaelewa namaanisha nini.

Bi Zawadi akawa ametoka hatimaye, akipendezea kwa kuvaa nguo nzuri sana ya kitenge na kuzibana nywele zake za kusukwa kwa juu, huku akishikilia mkoba mdogo ambao alisema ulikuwa maalumu kwa ajili ya kuwekea Biblia. Nikamsifia kwa kudamshi, mwenyewe akipenda kweli kujua alionekana vizuri, nasi tukiwa tayari kuondoka sasa ndiyo Miryam akawa amerejea sehemu hii ya sebule. Akatuaga vizuri pia, na ilikuwa ni yeye na Bi Jamila pekee ndiyo waliokuwa macho kutuaga, Tesha na Mariam bado walikuwa wanavuta mashuka yao huko vitandani.

Kulikuwa na ishu ya kupangilia mambo yaliyohitajika kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya kuzaliwa ya Bi Zawadi, ambayo sasa ilikuwa karibu zaidi kufika, na ndiyo Miryam akamwambia mama yake mkubwa kwamba wangekuja kuongelea mambo yaliyohitaji kumaliziwa tukisharudi baadaye. Inaonekana bibie asingekwenda kazini leo, kwa hiyo hapo ndiyo tukaachana nao, kisha Bi Zawadi na mie kuingia mwendoni kulifata jumba la ibada.

★★

Tulichukua daladala za kwenda Kisemvule, tukapita maeneo kadhaa mpaka kufikia sehemu fulani ambayo tulishuka na kupanda daladala nyingine tena iliyoelekea Chamgando. Watu wengi walikuwa wakitutazama sana mimi na Bi Zawadi, na mwanamke huyu alikuwa mwenye story zenye ucheshi sana; akigusia mara nyingi sana suala hilo la mie kutazamwa mno.

Alitaka kujua ikiwa labda nilikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanamke mmoja ama ikiwa na mimi sikuwa nimetulia kama Tesha, nami nikamwambia sikuwa na mtu kabisa. Aliona kwamba nampiga fix tu kwa sababu alikisia labda hata nilikuwa nimeshatoka na wanawake kama Ankia na wengine ambao hakuwajua, na kauli zake zilinifanya nicheke sana lakini kweli nikampiga fix kwa kusema sikuwa wa namna hiyo. Nilitulia kabisa.

Akanipongeza na kusema natakiwa kujitahidi sana kubaki safi maana magonjwa yalikuwa mengi mno, na huku tulikokuwa tunaenda ndiyo ningepata kujua mengi kuhusu maisha yangu na jinsi ya kuyaendesha ili yafanikiwe zaidi. Aliifanya hali hii ionekane kama tulikuwa tunaenda kwa mganga yaani, na tulipofikia hilo eneo la Chamgando kweli ikaonekana kama vile tulikuwa tunaenda kwa mganga.

Ilikuwa ni sehemu ambayo haijaendelea kivile, yaani utafikiri tulikuwa tumekuja kijijini kabisa. Watu waliotuona walitusindikiza kwa macho toka tumeshuka garini mpaka kuingia kwenye kijia kilichoelekea ndani zaidi ya eneo lenye uoto mwingi wa asili na miti mingi ya minazi. Ndiyo tukawa tumeifikia nyumba ndogo iliyojengwa kwa mbao sanasana na kufunikwa na Maturubai na mapazia mekundu na ya zambarau, huku kukiwa michoro ya msalaba mweupe hapa na kule. Lilikuwa ni kanisa chipukizi.

Nikamuuliza Bi Zawadi alipajuaje huku kote, naye akaniambia mke wa mwenye hili kanisa aliwahi kuishi Mzinga, na walijuana hasa kipindi ambacho wazazi wao akina Miryam walipoteza maisha yao. Akasema kwamba mchungaji alikuwa mzuri sana na upako wake, lakini hapa tulikuwa tumekuja kuonana na mama mchungaji kwa kuwa ni yeye ndiye aliyekuwa na maono, na alitoa maneno ya ushauri na saha fulani hivi lakini kwa njia ya upako. Dah!

Nikasema haina noma, nasi tukaifikia nyumba hii takati... taka... takatifu ya ibada. Kulikuwa na mwanamke aliyebeba mtoto mgongoni hapo nje, akionekana kuwa mtunzaji wa kanisa sijui, naye akatufata na kutusalimu kwa heshima. Yaani sana, kiasi kwamba alipiga magoti mpaka chini alipokuwa ameushika mkono wangu, nami kiukweli nilijisikia uajabu kiasi. Lakini tukaingia ndani kwa pamoja baada ya mwanamke huyo kutuongoza mpaka kufikia viti vya plastiki, nasi tukakaa.

Mwanamke huyo akatuambia mama mchungaji alikuwa anakuja sasa hivi tu, uzuri Bi Zawadi alikuwa ameshawasiliana naye pia, na hakuishi mbali na kanisa. Kwa hiyo dakika chache za kumsubiria zikatumiwa vyema na Bi Zawadi kunielewesha mambo yalivyo kwa sehemu hii. Ilikuwa ni sehemu ya kawaida tu, ya mwanzo, hata sakafu ilikuwa ya michanga na kinara cha mbao iliyofunikwa kwa kitambaa chenye msalaba uliochorwa kwa chaki. Naelezea mengi ndiyo ili uone nilichokiona, yoh!

Basi, mama mchungaji akawa amefika hatimaye, akiwa ni mmama ambaye hakuwa mbali sana kiumri kumfikia hata mama yangu mzazi, arobaini ya mwishoni, naye akanikaribisha vizuri sana. Leo haikuwa siku ya ibada ya pamoja, bali kama tu maombi spesho ya mtu mmoja mmoja, na Bi Zawadi akawa amemwambia kwamba mimi ndiyo "yule kijana" aliyemsema ambaye alikuwa kama baraka kubwa sana kwenye maisha ya familia yake, na alinileta ili kunisaidia nitakasiwe maisha yangu maradufu zaidi na mwenyezi Mungu.

Mwanamke huyo, mama mchungaji yaani, aliniangalia kwa umakini sana kama vile ananisoma, nami nikawa nimebunda tu kama vile sielewi somo. Kisha akaanza ghafla tu kusema kwamba anayaona maisha yangu, anajua nimetoka kwenye mazingira magumu sana lakini ni kama vile maisha yangu yote yaliongozwa na bahati kunifanya nitoke sehemu mbaya mpaka kufikia sehemu nzuri, na bado ilikuwa kwa kupambana sana.

Akasema nina moyo mzuri mno, lakini kuna kitu fulani ambacho kilikuwa kinaihangaisha nafsi yangu na hivyo nilikuwa najaribu sana kukiepuka kwa kujifanya kama sijali, ila kutoka ndani ya moyo wangu nilikuwa najali sana.

Mh? Alinifanya nimwangalie kwa mkazo zaidi, kwa kuwa sikatai, kuna vitu kweli nilikuwa najitahidi sana kuviepuka maishani mwangu kwa sababu zangu mwenyewe, lakini sikudhani mwanamke huyu angeweza kujua ni mambo gani. Labda aliotea tu. Ndipo akasema niache kuwaza kwamba kuliepuka jambo hilo kutanifanya niridhike, badala yake ifike wakati nitambue kwamba hilo ndiyo litakuwa chanzo kikubwa sana cha furaha ya kweli ambayo ninaitafuta. Dah!

Sawa aliongea kimafumbo fulani hivi, ile kwamba ni yangu tu mimi kujua, na kiukweli alinifanya niguswe sana kwa kuwa maneno hayo yaligusa sehemu fulani kubwa sana ya maisha yangu ambayo nilikuwa nimeiweka pembeni mno. Mbali sana yaani. Na hapa akawa amenifanya niitafakari, kitu ambacho kikanikosesha amani kiasi.

Sijui ilikuwa ni upako kweli, ama huyu mwanamke alijua tu kusoma nyota? Kwa vyovyote vile, akanishauri nianze kuamini kwamba Mungu yupo pamoja nami, na angenipatia zawadi nzuri sana kwa mambo mengi mazuri niliyokuwa nayafanya, lakini hilo jambo aliloniambia naepuka ndiyo lingenikamilishia furaha niliyoihitaji.

Mi' bwana nikakubali, amen kama zote, kisha mama akaanza maombi. Tukasimama kabisa, mzee nikaombewa yaani, maneno yaliyosemwa yalinigusa sana mpaka nikajihisi kutaka kulia. Sikutegemea kabisa hali iwe namna hiyo, lakini nashukuru tu mabomu ya 'fire' yaliporushwa sikuanguka chini. Nilikuwa nimevaa T-shirt nyeupe. Akili yangu hii!

Tulipomaliza maombi ya zaidi ya nusu saa, tukaketi tena, nikianza kuulizwa najisikiaje, nami nikasema nilijihisi vizuri kiasi. Bi Zawadi alifurahi sana alipotambua kuwa niliguswa mno na hii kitu. Nisingeweza kusema mengi mno kwa kuwa kuna hisia zilivurugana ndani yangu, ila nilijikuta nimeipenda sana hii kitu, nami nikaomba kujua ratiba za ibada kwa wiki.

Wakati akiwa ameanza kuelezea, simu yangu ikaita, nami nikaitoa mfukoni ili kuiondolea sauti, lakini baada ya kuona mpigaji kuwa askari Ramadhan, nikawaomba wanawake hawa nipokee simu mara moja, nao wakakubali. Nikanyanyuka na kuelekea mpaka nje, kisha nikapokea ili nimsikilize jamaa. Sikuwa nimetegemea anitafute leo.

"Hallo..." nikasema hivyo.

"Yes, JC? Uko wapi?" Ramadhan akasikika.

"Nipo... maeneo siyo mbali sana na Mbagala. Vipi mkuu?" nikamuuliza.

"Uko na kazi, au?"

"Hapana, ni matembezi tu..."

"Naomba tukutane upesi. Nakutumia location kwa sms, ufike hapa mida ya saa sita hadi saa saba. Utaweza?" akauliza hivyo.

Nikatazama saa mkononi kukuta ni saa tano kasoro, nami nikamwambia, "Ndiyo, naweza. Ni muhimu sana?"

"Yes, ni muhimu. Na uwe cautious," akasema hivyo.

"Sawa. Nakuja," nikamwambia kwa uhakika.

Simu ikakatwa.

Nikatulia kidogo na kutafakari ni nini kilichokuwa kimezuka kwa upande wa askari huyu, ila kujua hilo ingenibidi niende huko haraka. Nikarejea pale ndani na kuwaambia wanawake wale kuwa nilipata dharura ndogo iliyonihitaji kuwahi, kwa hiyo nikaomba radhi ya kuhitaji kuondoka haraka.

Mama mchungaji akasema haina shida kabisa, naye Bi Zawadi akasimama pia na kuahidi kuja kwa ajili ya ibada Jumapili. Mimi pia nikatoa ahadi hiyo, kisha ndiyo mama mchungaji pamoja na yule mwanamke mwingine wakatusindikiza kwa pamoja mpaka kufikia sehemu ya kupandia daladala.

Ulikuwa ni wakati mzuri sana kuwa pamoja na Bi Zawadi huku, na nilitamani hata tupite sehemu pamoja naye ili tupate kitafunwa na nini, ila ukitegemea na muda niliokuwa nimepewa na yule askari ingetubidi tu tuchukue usafiri na kuondoka kurudi nyumbani. Kwa hiyo baada ya daladala kufika, tukaagana kwa mara ya mwisho na mama mchungaji na kupanda, haoo tukaishia.

★★

Mbinde za hapa na pale za usafiri zilisababisha tukawie kiasi, mpaka inaingia saa sita kabisa ndiyo tukawa tumeshukia Mzinga. Sasa kutokana na dirisha la wakati kuwa dogo kwa upande wangu, nikamwambia Bi Zawadi atangulie kwenda nyumbani ili mimi nipitilize mpaka huko nilikokuwa naenda, halafu tungekuja kuonana baadaye. Hakuwa na neno. Nikamwitia boda ili asisumbuke kutembea mpaka nyumbani, na baada ya yeye kupanda na kuondoka, mimi pia nikachukua boda na kuomba nipelekwa Rangi Tatu fasta.

Tayari askari Ramadhan alikuwa amenitumia ujumbe kwenye simu wa sehemu ambayo alitaka tukutane, na alitaka niwe makini sana ili nisije kufatiliwa maana sehemu hii ilikuwa ya kibinafsi mno. Nilihisi tu kungekuwa na vitu vya siri-siri kwenye huu mkutano wangu pamoja naye, kwa hiyo nikamwambia nimeelewa na niko njiani, nikaweka akilini hilo eneo na jengo alipotaka niende, kisha nikaifuta sms yake na kuzima simu pia. Mambo ya kuwa keyafuli hayo!

Nimekuja kufika kwenye eneo husika tayari saa saba ikiwa imeshaingia, lakini ya dakika za mapema, nami nikaelekea mpaka kwenye jengo nililoelekezwa. Nikaenda moja kwa moja kwenye chumba ambacho kilikuwa na namba hususa niliyopewa, kwa sababu kulikuwa na vyumba vingi vyenye namba pia kutokana na jengo hilo kuwa la upangishwaji, nami nikafungua mlango na kuingia.

Nikasimama usawa wa mlango ndani ya chumba hiki ambacho kilikuwa na hali ya ugiza sana kutokana na kutokuwa na madirisha makubwa isipokuwa sehemu nyembamba tu kwa juu zaidi za kupitishia hewa, na taa ndogo iliyomulika mwanga wa rangi ya chungwa ndiyo iliyokuwa katikati kutokea juu. Kilikuwa kipana lakini hakukuwa na vitu vingi ndani humo. Usawa wa sehemu hiyo katikati hapo sakafuni kulikuwa na meza moja tu, ambayo haikuzungukwa na viti, bali watu. Watatu.

Wawili sikuwafahamu, ila mmoja alikuwa ni askari Ramadhan. Ni yeye tu ndiye aliyekuwa amevalia kwa njia ya kawaida kama raia, lakini wenzake walivaa kwa mitindo fulani kama vile walikuwa majasusi. Na miili yao ilijengeka vyema sana, wakiwa na nyuso makini, mmoja mrefu kunifikia na mwingine mfupi kiasi, na kwenye hiyo meza kulikuwa na karatasi kubwa, pana mno, ambayo nadhani ilikuwa imeandikiwa mipango yao maalumu.

Hapa nikajua nilikuwa nimeingia sehemu yenye hali makini sana, na huu mchezo ulikuwa wa kiwango cha aina yake.

"Karibu JC. Ingia," askari Ramadhan akanisemesha namna hiyo baada ya kuniona.

Nikaelekea mpaka hapo walipokuwa na kusimama upande mmoja wa meza, nami nikawatikisia vichwa kisalamu wenzie Ramadhan, na jibu lao likawa kwa njia hiyo hiyo.

Ramadhan akasema, "Huyu ndiyo CI wangu wa kwanza niliyewaambia. Anaitwa JC. JC..."

"Naam..." nikaitika.

"Hawa ni maaskari wenzangu, special forces, wako nasi kwenye hii ishu. Huyu ni Richard, na huyu ni Mwitakabilamba," Ramadhan akawatambulisha wenzake.

Kudadeki! Ilikuwa karibu nimwombe arudie kulisema tena hilo jina la pili, lakini nikakaza tu na kutikisa kichwa utadhani nilikuwa nimelielewa. Yaani jina lilikuwa na "mwita," "kabila," na "lamba." Siyo poa!

"Tunajitahidi kufanya kila kitu kwa care sana, ndiyo maana tumekutana kama hivi. Una uhakika hamna mtu anakufatilia?" Ramadhan akaniuliza.

"Ndiyo, nina uhakika. Na simu nimezima," nikamwambia hivyo.

"Vizuri. Sasa... hawa hapa, ni vichwa wa vikosi maalumu ambavyo vitashughulika na round up yote ya hawa watu tunaowanyatia, na nimeona nikukutanishe nao ili wajue kwamba we' ni mmoja wetu, na part unayocheza kwenye hili game..." Ramadhan akasema hivyo.

"Sawa sawa," nikakubali.

"Tutakapowasomba watu wote wa huyo madam Bertha, itabidi iwe kwa mpigo mmoja, na hivyo hiki kikao kidogo ndiyo kitakuwa cha mwisho ili kuhakikisha kwamba tunajua kila kitu kiko sehemu husika... tukipiga tu hatua, iwe ni moja kwa moja. Si unaelewa?" Ramadhan akaniuliza tena.

"Ndiyo. Na unamaanisha kwamba hiyo round up iko karibu zaidi kufanywa?" nikamuuliza pia.

"Ndiyo. Karibu sana," Ramadhan akajibu.

"Kama lini?" nikauliza.

"Kwa upana wa sehemu zote za hiyo organization ya madawa ya kulevya, ndani ya wiki moja tu ndiyo tutapiga hatua ya kuwakusanya wote," akajibu hivyo yule mwenye jina gumu kama Ntibazokiza.

"Ila bado tunahitaji kujua ikiwa info zote za sehemu, procedure, na usambazaji, kufikia sasa... ikiwa zipo vile vile bado au kuna mabadiliko ambayo yanafanywa au yatafanywa kabla ya hiyo wiki kuisha," akasema hivyo yule Richard.

Nikamwangalia usoni askari Ramadhan.

"Anamaanisha anataka uelezee jinsi ambavyo mambo yalivyo. Kila kitu tunacho mezani, ila hawa wenzangu wanahitaji review kutoka kwako kabisa. Unaweza kuwaelezea," Ramadhan akaniambia hivyo.

Nikashusha pumzi kiasi na kuangalia mezani, nami nikaona ramani iliyokuzwa vizuri sana ya jiji la Dar es Salaam kwenye karatasi iliyokuwepo hapo. Kulikuwa na michoro-michoro ya kalamu pia, nami nikawaza bora kama kungekuwa na kifaa cha kielektroni kwa ajili ya kuonyeshana mipangilio ya mambo, lakini kwa sababu za kiusalama na uharaka nilielewa kwa nini waliamua kutumia pepa. Hakukuwa na shida.

Nikawaambia, "Okay. Hamna lolote lile lililobadilika, zaidi... ndiyo wanazidi tu kuimarisha mfumo wao mzima wa hii biashara. Iko hivi. Huyu madam Bertha na kundi lake wana vyumba maalumu kwenye majengo makubwa 21 hapa jijini, ambavyo anatumia kutunza mizigo mingi ya madawa ya kulevya. Kunakuwa na watu wake kwa hizi sehemu, na wamekaa kama watu wa kawaida tu; kama ni duka la nguo, au vitu vya rejareja, ama mashine ya kusaga nafaka... wanakuwa wanakaa kama wauzaji wa kawaida tu, lakini ikifika mida special kwa ajili ya kufanya delivery ya madawa hayo, wanaanza kuyatoa na kuyasambaza kwa kutumia system ya taka..."

Ramadhan, akiwa amekunjia mikono yake kifuani, akatabasamu na kutikisa kichwa chake, kisha akasema, "Nani angefikiria wangekuwa wanatumia njia ya kuondoa uchafu ili kusambaza uchafu wao?"

"Siyo rahisi. Kwa hiyo wanatumia system ya takataka?" Richard akaniuliza hivyo.

Nikasema, "Yeah. Bertha, na jamaa yake anaitwa Festus, wana ushirika na makampuni manne jijini yanayohusika na huduma ya kuondoa taka majumbani, maofisini, kwenye makampuni, vyuoni, everywhere yalipo available. Nafikiri mmeshayajua..."

"Yeah, tunayajua..." Mwitakabilamba akasema hivyo.

"Yes, kwa hiyo ikitegemea na pale ambapo order za hayo madawa zinatakiwa ziende, zinapelekwa kupitia hayo magari ya taka. Wanaweza feign kwamba wanaenda kupitia takataka hapa au kule, na hata kama unakuta gari linakuwa limejaa takataka halisi, kunakuwa na sehemu ya kificho kwa ndani ambayo ndiyo inakuwa imebeba mifuko yenye haya madawa. Kwa hiyo wanaoyapokea wanakuwa wanajua kabisa... ah, ikifika saa fulani, gari la taka litapita hapa. Kama kunakuwa na fuko la uchafu kwenye dustbin, wanaokuja kulitoa na kuli-empty wakimaliza, wanayatia madawa humo yakiwa kwenye mifuko safi na kurudisha fuko la kwenye kopo likiwa na hayo madawa. Kwa hiyo wanaoyategemea wanaenda upesi kuyachukua kwa njia hiyo, na malipo wanakuwa wameshafanya mapema. Njia za kuhakikisha kwamba hawaonwi tayari zimewekwa mahala pake, kwa hiyo unakuwa ni utaratibu usioshtua yeyote ambaye hahusiki," nikawaelezea.

"Na hiyo ni kwa sehemu zenye watu wenye nazo tu bila shaka," akasema hivyo Richard.

"Yes. Kinondoni, Kigamboni, Makumbusho, Kariakoo, Sinza, Mlimani, UDSM, sehemu nzuri za Mbezi, Kawe... yaani, nyingi sana kuzungukia jijini. Utaratibu wao wa malipo na delivery ni wa maana, gari liwe kubwa ama dogo, haijalishi. Wafanyakazi wapo wa kutosha, na wako fasta yaani kama tu system ya kumwita Uber... ila yao bora zaidi," nikawaambia hivyo huku nikiwaonyeshea kwenye ramani.

"Ni bora kwa uchafu zaidi. Wako smart lakini, hakuna traffic hata mmoja ambaye atasimamisha gari la takataka kuchunguza. Na wanaowasambazia lazima wawe wanalipwa vizuri ndiyo maana wanaongezeka, eh?" akaongea hivyo Richard.

"Ajira zenyewe safi mbinde. Nani atawalaumu? Pesa popote, watakwambia angalau hawafanyi ushoga," Ramadhan akasema hivyo.

"Ila ndiyo lazima huu upuuzi ukomeshwe. Shida siyo wanaonunua, ila ni wanaoyasambaza, haijalishi ni wakubwa au wadogo. Na vipi kwa walala hoi? Hivi vitu vinawafikia?" akauliza Mwitakabilamba.

"Zinafika, ila mfikishaji siyo Bertha. CI wangu mwingine anasema Bertha ni kama retailer kwa watu wakubwa, anapokea chake kikubwa, anawasambazia kipato wanajeshi wake waliohusika, na yeye anakula pesa ndefu... kama malkia vile," akasema hivyo Ramadhan.

Kauli yake Ramadhan ikanifanya nimtazame kimaswali kiasi. Alisema "CI" wake mwingine, yaani Confidential Informant, neno linalomaanisha mtu afanyaye kazi na maaskari kisiri ili kuwakamatisha wahalifu. Kwa hiyo alimaanisha kulikuwepo na mtu mwingine kwenye mtandao wa mishe zake Bertha ambaye alifanya kazi na maaskari hawa kisiri na kuwapa taarifa, kama vile mimi tu. Sikuwa najua hilo, kwa hiyo sikujua alikuwa amemwongelea nani.

"Okay sawa. Hivyo ndiyo network yao ya usambazaji inavyoenda. Vipi kuhusu ishu ya wewe kumtengenezea coke ili akuze soko lake?" Mwitakabilamba akaniuliza.

"Ndiyo, huu mwezi ulioisha ndiyo limekuwa suala la kipaumbele kwake, na wameshaanza kuyazagaza. Faida inaingia. Kwa ajili ya hiyo operation, Bertha alitafuta sehemu nzuri sana ya kuniweka mimi na watu wake ili tuyatengenezee huko bila kuvuta attention. Kwenye supermarket moja kubwa," nikamwambia.

"Ipo Riverside. Ubungo," akasema hivyo Richard.

"Yeah," nikakubali.

"Tumeshai-monitor pia, kama tu hayo majengo 21. Kilichopo hapa JC, ni kusubiri tu tuwe kwenye position nzuri ya umoja ili hiyo round up ikifanywa, iwe ni kwa siku moja ambayo Bertha, sijui Farao, Tito, Sudi, na nani... huyo Chalii... anayefanya uuzaji wa wanawake, yeah wote yaani... WOTE... tutawaweka ndani. Na itakuwa kwa siku ambayo hawatategemea," Ramadhan akaniambia hivyo.

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Kwa hiyo endelea kungoja kwa subira, uwe makini, mchezeshe Bertha karibu, ujue kabisa pale utakapotakiwa kuwepo hiyo siku ikifika. Si unaelewa?" Ramadhan akaniambia hivyo.

"Ndiyo, naelewa," nikamwambia.

"Vizuri sana, JC. Yote uliyosema yako in check. Kinachotakiwa sasa hivi tu ni kufuata mwongozo atakaokupa Rama, na hii wiki ikiisha huu mzigo utakuwa umeshautua," akaniambia hivyo Richard.

"Sawa sawa, ila...."

"Shika hii," Ramadhan akanikatisha kwa kusema hivyo.

Alikuwa ameninyooshea kifaa fulani kidogo sana cha kielektroni, nami nikakipokea na kumtazama.

"Kaa nayo muda wote, itunze vizuri. Wakati mwafaka ukifika, utajua jinsi ya kuitumia," akaniambia hivyo.

Nikatikisa kichwa na kuiweka mfukoni, nami nikamwambia, "Lakini... bado sina chochote juu ya yule jamaa, Festus. Ni fence aliye makini sana, namaanisha... anajua kujilinda, so, sijapata lolote la kumweka kwenye position ambayo wengine watakuwepo ili muwaangushe wote pamoja naye. Tutafanyaje kuhusu hilo?"

Maaskari hawa watatu wakaangaliana kwa pamoja, kisha Ramadhan akasema, "Usijali. Nitashughulika na hilo. Ni mjanja huyo jamaa, lakini atakamatika tu."

Nikatikisa kichwa kuonyesha nimemwelewa.

Ramadhan akatazama saa yake mkononi, kisha akasema, "Alright. Hii session imeisha. JC... unaweza kwenda. Be very careful. Umenielewa?"

"Ndiyo. Nakuelewa mkuu. Asante," nikamjibu hivyo.

Akanionyesha ishara kwa mkono kuwa niende sasa, na wenzake wakanitikisia vichwa vyao kama kuniaga.

Nikageuka zangu na kuanza kujiondokea sehemu hiyo, lakini kabla sijaufikia mlango nikawa nimekumbuka jambo fulani, nami nikawageukia na kusema, "Mkuu..."

Wote wakaniangalia, na Ramadhan akasema, "Ndiyo?"

"Umesema kwamba... kuna CI wako mwingine ndani ya network ya Bertha. Naweza kujua ni nani?" nikamuuliza kwa umakini.

Akatulia kidogo, kisha akaniambia, "Usiwaze kuhusu hilo. Na yeye yuko kama wewe tu, hajui kwamba uko pamoja nami, na sidhani kama anakujua."

Nikaendelea kumwangalia usoni tu.

"Ni muhimu msijuane kabisa ili mbaki kuwa salama mpaka hii yote iishe. Umeelewa?" Ramadhan akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kukubaliana na hilo, kisha ndiyo nikafungua mlango na kutoka ndani humo.

Mambo yalikuwa yanaelekea kupamba moto! Ah, yaani kuwa sehemu kama hiyo ilinifanya nijione kuwa mpelelezi fulani hivi, lakini yule mnafiki kinoma! Huo unafiki naoongelea ndiyo ambao ningetakiwa kuuendeleza kwa upande wa madam Bertha ili mambo haya nyuma ya pazia lake yashike hatamu haraka siku ambayo angetumbuliwa majipu yake ya maovu, yeye pamoja na kundi lake lote lililohusika.

Nilijihisi vizuri sana kuwa karibu zaidi na ushindi dhidi ya kile ambacho mwanamke huyo alikuwa amemfanyia Joy na watu wengi ambao sikuwafahamu pia. Kuangusha biashara zake zote ghafla yeye na watu wake waliohusika lingekuwa ni tukio zito sana ambalo lingemuumiza, kwa hiyo nilikuwa na hamu kubwa ya kuja kushuhudia hayo yote wiki moja mbeleni.

Lakini, bado nilikuwa namtafakari sana huyo "CI" mwingine wa askari Ramadhan. Bora kama ingekuwa najijua tu kuwa mwenyewe kama "snitch" kwa madam Bertha, lakini sasa kujua alikuwepo mwingine pia kulinipa hisia fulani za wasiwasi kiasi. Vipi ikiwa kama huyu mtu alinijua, au nilimjua, na tulijuana? Alikuwa ndani ya huu mchezo kwa muda gani mpaka na yeye awe ametoa taarifa zilezile nilizokuwa nimewapa maaskari hao? Vipi kama bila mimi kujua, huyu jamaa angekuwa "snitch" kwangu mimi pia kuelekea mipango ya maaskari na ya madam Bertha mbeleni? Angekuwa nani huyu mtu?




★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
Ci mwingine ni chalii Gonga ,, kwanini huyu jamaa

1) haiwezekani haiingii akili mtu anakucheat wazi wazi (bertha ) afu eti anavumilia bila kuleta fujo zozote

2) chalii gonga kashajua J. C ndiyo mbaya wake lakn wala hajapanic wala kuleta shida kwa jamaa ,, sababu anajua ni swala la muda j.c na madam Bertha wote wataenda lupango ,,, little did he knows j.c na yeye wote wanafanya kazi moja ...
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA PILI

★★★★★★★★★★★★★★


Nilikuwa namuwaza sana huyu CI mwingine kwa kuwa sikupenda tu hii hali ya kuwekwa gizani, ila kama tu askari Ramadhan alivyokuwa ameniambia, huenda sababu kuu na nzuri ilikuwa ni ili tuwe salama. Ni kweli kutojuana ingesaidia tuwe salama, ila ndiyo huwezi kuwa na uhakika sikuzote kwamba uko salama kwa sababu tu mwingine anadhani upo salama. Kuna kitu kilikuwa kikiniwasha sana kutaka kujua huyu mtu alikuwa nani, na ningejitahidi kuhakikisha namjua.

Baada ya kuondoka hiyo sehemu, nikaelekea mpaka eneo la kupanda daladala ili nirejee Mzinga kushughulika na mgonjwa wangu wa muhimu sana, Mariam. Akili ilikuwa imehamishwa sana kutoka kwenye upande mzuri wa kiroho kwa msaada wa Bi Zawadi ile asubuhi, na sasa ilikuwa kwenye ule mbaya kutokana na kuwaza mambo mengi ambayo yangefanyika hizi siku chache zijazo kwa upande wake madam Bertha.

Kulikuwa na ka hisia ka sintofahamu kalikozunguka sana ndani yangu, hali fulani ya kujihukumu kutokana na kujiingiza katika hayo yote tokea Joy alipouawa. Sawa, sehemu kubwa ya hiyo ishu ilikuwa ni ili kukomesha matendo yasiyo ya kiungwana ya Bertha na watu wake, ila huu mwezi mzima, kuwa naye karibia kila mara, yaani sikatai kwamba nilikuwa nimeshamzoea yule mwanamke kwa njia ambayo ndiyo ilisababisha sehemu fulani ya hisia zangu ihisi kujuta kiasi shauri ya kujua kile ambacho kingempata mbeleni akikomeshwa matendo yake.

Ila si ilikuwa kwa nia nzuri? Si nilifanya hivi ili akome kufanya vitu haramu na hivyo kumwangusha kama nilivyokuwa nimetazamia toka mwanzo? Kwa hiyo sikupaswa kabisa kuhisi hivi. Kazi ingepaswa kuendelea. Ndani ya wiki moja haya yote yangekuwa yamekwisha, na nikaombea tu yaishe kiwepesi kabisa.

Kuwaza vitu vingi vya namna hiyo kukawa kumeifanya akili yangu irudie jambo fulani ambalo mara nyingi nilikuwa naliweka pembeni sana, yaani dada yake Joy, Adelina. Mwanamke huyo mwenye kujali alikuwa na kawaida ya kunitumia jumbe za salamu mara kwa mara, na mimi kutokana na kuwa na mambo mengi nilishindwa kumjali hata mara moja. Yaani kwa huo mwezi mzima uliopita, alikuwa amenitumia jumbe kadhaa za salamu, lakini sikuwahi kujibu hata moja.

Sasa wakati huu nikiwa naelekea huko kwa Mariam ndiyo nikaona ingekuwa vyema nikimtafuta, kumsalimu tu na kuomba radhi kwa kutingwa na mambo mengi. Inawezekana hata familia yake ilidhani suala la kuwasaka wasababishi wa kifo cha Joy ndiyo lilikuwa limezikwa, maana muda ulikuwa ukienda upesi sana.

Nikawa nimeifikia Rangi Tatu kwenye mida ya saa nane ya saa tisa hivi, nami nikaingia Zakhem kupata msosi kabla sijatimkia Mzinga. Ilikuwa ni kwenye mgahawa ule mzuri wa Zakhem, sehemu ya nje kwenye uwazi uliojengewa mabenchi-meza mapana kwa ajili ya wateja, nami nikakaa na kuagiza msosi mzuri. Kutazamwa mno na baadhi ya watu ilikuwa kama kawaida, na mimi nikaendelea kula hamsini zangu tu.

Nilikuwa nimeshaboresha vizuri ratiba yangu ya ulaji, ila siku ya leo ilipaswa kunisamehe tu kwa kukosa mlo wa asubuhi kwa kweli. Mambo yaliingiliana. Nikiwa nasubiria msosi uletwe ndiyo nikaamua kumpigia Adelina sasa, naye hakukawia kupokea.

"Halloo..." sauti yake ikasikika upande wa pili.

"Hallo. Vipi dada?" nikamuuliza hivyo.

"Safi. Za masiku JC?"

"Ah, Mungu anasaidia. Nimeona nikujulie hali leo maana... kwa kweli mambo yamekuwa mengi, wakati mwingine mpaka nakosa kukujibu ukinijulia hali dada'angu..."

"Kweli aisee, mambo lazima yatakuwa mengi. Me nikafikiri labda hata ulipoteza simu ama hutaki tu kujibu..."

"Ahahah... hapana, na... nisamehe tu kwa hilo..."

"Haina shida. Mapumziko yako yanaendaje?"

"Namalizia-malizia siku za likizo then nitarudi kwetu. Bado si upo Mbezi toka umeondoka Nachingwea?" nikamwambia.

"Kinyerezi, ndiyo," akajibu.

"Yeah, Kinyerezi kweli. Vipi kazi?"

"Ah, sasa hivi nipo tu. Ile kazi niliiacha," akasema hivyo.

"Kumbe?"

"Eeeh, ilikuwa hailipi kivile, kwa hiyo nikaamua kuachana nayo. Ninatarajia kuanza nyingine pale airport..."

"International?"

"Eeeh."

"Ah, hongera sana. Unaenda kupaisha ndege?"

Akacheka kidogo kwa furaha, kicheko chake kizuri kikinifanya nitabasamu, naye akasema, "Ni uhudumu tu. Niliona nisomee haya masuala miaka miwili mitatu iliyopita bwana, sasa hivi ndiyo majibu ya sala za kupata hiyo kazi yamejibiwa. Nitapangiwa labda... kama ni nje au ndani ya ndege."

"Vyema sana Adelina. Utakuwa sehemu nzuri sana... na ndiyo inakufaa."

"Eti eeh?"

"Kabisa."

"Asante," akasema hivyo.

Ni hapa ndiyo msosi wangu nilioagiza ukawa umeletwa, nami nikaanza kula taratibu huku simu ikiwa sikioni bado.

"Mama mzima?" nikamuuliza Adelina.

"Hajambo. Anaendelea vizuri sasa hivi. Vipi na wewe? Mkeo hajambo?" akaniuliza pia.

"Ahah... yupo. Siku hizi na ye' amekuwa bize kweli..."

"Eeh, aliniambia amefungua duka, nitapanga nije kuliona siku moja."

"Itakuwa vizuri sana. Tena sasa hivi kwa sababu umetulia, kwa nini tu usije kututembelea? Ni kitambo hatujaonana..." nikamwambia hivyo.

"Kweli. Unataka tuonane tena?" akauliza.

"Ndiyo. Nimekukumbuka," nikamwambia hivyo.

"Hata mimi JC," akasema hivyo kwa njia fulani ya taratibu.

Nikatabasamu kiasi, kisha nikasema, "Unaweza kuja hata Jumamosi ikiwezekana."

"Mmm... Jumamosi hapana, ninaenda sehemu fulani kusaidia maandalizi ya harusi jioni hiyo hiyo. Labda kesho. Au... kesho una mipango mingine?"

Kesho ilikuwa ni Ijumaa, kwa hiyo ndiyo nilikuwa na mipango mingine, hivyo nikamwambia, "Eeh, kesho nitakuwa location nyingine. Vipi ukija Jumapili basi?"

"Ni sawa. Tutaangalia na Kariakoo Derby," akasema hivyo.

"Hahahah... kumbe na we' shabiki wa mpira?" nikamuuliza.

"Ndiyo, naangalia pia. Wewe Simba au Yanga?"

"Simba."

"Wow! Mimi pia," akasema hivyo kwa shauku.

"Safi sana. Uje sasa ili tumzomee vizuri Ankia Yanga ikitandikwa 10," nikaongea kiutani.

"Hahahahah... sawa nitafika," akasema hivyo.

"Haya bwana. Me ndo' naweka msosi mahala pake hapa. Karibu," nikamwambia hivyo.

"Asante, me mwenyewe ndo' napakua," akasema.

"Haya, tutachekiana mida eh?"

"Poa. Badae," akaniaga.

Nikakata simu baada ya kumaliza maongezi hayo na mwanamke huyo, nami nikawa nimejisikia vizuri kiasi. Inaonekana kufikia wakati huu Adelina alikuwa ameshaizoea ile hali ya kumpoteza mdogo wake, na nilikuwa nimetaka kuuliza lolote kuhusu upande wa suala la kifo cha Joy, ila nilighairi baada ya kuhisi namna ambavyo alitulia kihisia wakati huu. Kama ni kumwongelea Joy, basi tungemwongelea akifika huku hiyo Jumapili.

Na hakuwa amekosea aliposema kwamba Jumapili ilikuwa ni siku ya mechi ya watani wa jadi, almaarufu Kariakoo Derby. Kulikuwa na msisimko mkubwa kutoka pande zote za mashabiki kwa kuwa ni mechi iliyokuwa imesubiriwa kwa hamu kubwa sana, na nilitazamia pia kuitumia pindi hiyo kufurahia wakati mzuri zaidi pamoja na marafiki zangu wa huku; kujumuisha na ujio wa Adelina pia. Na sijui kwa nini tu, ila kuongea naye hivyo, kulinipa hisia fulani tamu sana. Ila sikutaka kupeleka mawazo mbali mno. Yajayo nisiyoyajua ndiyo yangefurahisha.

★★

Nikawa nimemaliza msosi baada ya dakika chache, kisha nikalipa na moja kwa moja nikaelekea kupanda daladala ili nifike Mzinga. Kama kawaida tu, haikuchukua dakika nyingi sana nami nikawa nimeshafika huko, kisha nikaelekea pale ambapo duka lake Ankia lilikuwa ili nimsalimie kwanza. Alifurahi kuniona, naye akasema alikuwa na mpango wa kwenda nyumbani mapema, kwa hiyo nikamwambia angenikuta kwao Mariam ikiwa asingenikuta kwake.

Basi, nikaendelea na safari yangu mpaka nilipofika kwao Mariam, nami nikaingia getini hapo na kumkuta Tesha akiwa amekaa pamoja na binti Mariam varandani. Alionekana kumwonyesha mdogo wake vitu fulani kwenye simu, na baada ya Mariam kuniona, akanyanyuka na kunifata huku akitabasamu kwa furaha. Akanikumbatia kwa nguvu kweli utadhani hakuwa ameniona miezi, nami nikatoa viashirio vya bandia kumwelekea Tesha kwamba ningekufa kutokana na jinsi nilivyobanwa na binti, naye akatabasamu kiasi na kusimama.

Mariam akaniachia na kunitazama machoni huku akitabasamu, naye akasema, "Shikamoo JC?"

Nikatabasamu pia na kusema, "Marahabaa. Aisee! Unalisema jina langu vizuri sana sasa hivi. Nikupe maua yako bwana..."

Nilipomwambia hivyo, nilikuwa nimenyanyua kiganja changu kwa upande wa juu, naye akaweka chake karibu na changu kwa upande wa chini, vidole vyetu vikiwa vimegusana kiasi, kisha tukavichezesha haraka-haraka kwa pamoja huku tukisema "Broooop," halafu ndiyo sote tukapiga vidole viwili kiganjani kwa njia iliyotoa sauti. Sijui kama hii taswira imeeleweka vizuri!

Huu ulikuwa mtindo mpya wa kisalamu ya kishkaji niliokuwa nimemfundisha binti, na alikuwa ameupenda sana zaidi ya ule wa "Hi-five" niliomzoesha kipindi kile, na hii mpya tuliitamka 'bruup.' Kwa hiyo nyakati zozote alipojisikia furaha kwa kufanya jambo zuri, ningetumia mtindo huu pamoja naye ili kuikuza zaidi furaha yake na hisia ya kujiamini, na yeye alipenda mno kusifiwa kwa kuendelea kujitahidi kuimarika zaidi kiutimamu.

Mariam alikuwa anafanya maendeleo upesi sana, yaani ni kama yale mabaya yote yaliyokuwa yametokea hayakutokea kabisa, na hilo lilikuwa jambo jema. Niliona wazi kwamba si muda mrefu sana huyu binti angeacha kuwa "binti" tu, na hatimaye angerudia hali yake ya kawaida ya kujitambua kuwa mwanadada aliyeelekea kuwa mwanamke kikamili.

Baada ya kupiga hiyo 'Broop,' Mariam akasema, "Nimechora na kuandika leo, JC. Nimeandika."

"Wow! Kweli? Umeandika nini?" nikamuuliza.

"Alph, alpha-beti..." akasema hivyo.

"Zote?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Safi. Enhe... na nini kingine?" nikamuuliza.

"Majina yetu wote," akasema hivyo.

"Wewee... kweli? Nani kakuelekeza?" nikauliza.

"Kaandika mwenyewe. Mama, Tesha, JC, Miryam... kaandika hayo yote mwenyewe," Tesha akaniambia hivyo baada ya kutufikia.

"Aisee! Safi sana Mamu. Vipi kusoma? Unasoma-soma?" nikamuuliza binti.

"Yes. I am... studying..." Mariam akasema hivyo.

Nikajikuta natabasamu kwa furaha sana baada ya binti kusema hivyo, nami nikamwekea kiganja ili tufanye 'Broop' tena. Eti na Tesha pia akataka kuweka kiganja chake kwenye vyetu aliunge, lakini Mariam akamsukuma kwa nguvu ili asituharibie, mpaka nikashangaa. Tesha akacheka na kunyanyua mikono juu kama kusema yaishe, kisha Mariam akarudi kwangu na kunipa 'Broooop' ndefu kwa raha zote.

"Tufanye mazoezi ya kinanda, eh?" Mariam akauliza.

"Kweli, nenda kakiandae tuje tupige zoezi," nikamwambia hivyo.

Mariam akaanza kuelekea kule ndani, huku akitazamana na kaka yake kwa njia ya chuki eti, naye Tesha akamfanyia ishara kwa vidole vyake viwili kuwa anamtazama kwa umakini.

Tesha akanisogelea tena, nasi tukagongesha viganja vyetu kirafiki, kisha akasema, "Nakuona mchungaji. Leo kitakatifu kweli, au siyo?"

"Ahahah... ma' mkubwa wako amenipeleka huko Chamgando aisee, nimepapenda!" nikamwambia.

"Katusimulia. Anasema umeguswaaa..."

"Kasema na nini kingine? Kwamba nimeanguka?"

"Hahah... labda siyo JC. Tena umevaa nyeupe kabisa, hata kama ungekuwa na mapepo usingeanguka ili tu kulinda nguo yako isichafuke..."

"Unanijua vizuri kumbe."

"Mbona ukamkimbia sa'? Ulienda wapi?"

"Niliitwa sehemu mara moja."

"Na demu?"

"Ahah... akili zako hizo..."

"Aa, we' sema tu. Huwa kuna tumambo-mambo unaficha sana, ila me huwa najua mbona..." akasema hivyo.

"Mambo kama yapi?"

"Kama wewe na Soraya," akaniambia hivyo.

Nikamkazia macho.

"Najua ulimla Tausi mwanangu, wala hamna noma," akasema hivyo.

"Umejuaje?"

"Mwezi mzima umetosha kunifanya nijue, we' unanionaje? Anakukubali mno, naonaga anakupigia wee... ila we' unamkaushia tu. Nikajua tayari ushakula na kutema..."

"Mbona unaongea kama vile imekuuma sana?"

"Ah, toka hapa! Kiniume nini, kwani me sina demu?"

Nikacheka kidogo kwa pumzi.

"Sema una mambo kubwa sana we' jamaa, unatoka-toka sana kwa mishe kali inaonekana. Ungenipa michongo basi na mimi," akasema hivyo.

"Siyo mambo kama hayo, ni... masuala tu ya kifamilia narekebisha," nikamwambia hivyo.

"Ahaa..."

"Eeh. Nani yupo huko ndani?" nikamuuliza hivyo huku tukianza kuelekea mlangoni.

"Mama hao... na Shadya. Wanapiga tu umbea kuhusu ishu ya Doris," akasema hivyo.

"Doris ndo' nani?" nikamuuliza.

"Ih! Hivi kumbe nilikuwa sijakwambia?" Tesha akasema hivyo.

"Kuniambia nini?" nikauliza.

"Kuna sherehe ya harusi, ya huyu dada anaitwa Doris. Ni ndugu yetu pia, sijafatilia kivile ila nadhani tunatakiwa kumwita binamu. Anaolewa," akasema hivyo.

"Ooh, sawa. Yeye anakaa wapi?"

"Kijitonyama. Si unamkumbuka nanilii... yule Dina... tuliyeendaga kwake kule Uhasibu?"

"Ee, namkumbuka..."

"Ee, Dina ni mdogo wake Doris sasa..."

"Okay... sawa. Ndo' maandalizi ya harusi yameanza..."

"Eee, wamewaweka da' Mimi na Shadya wanakamati... wanaanza na kitchen party kabisa... halafu..."

Kabla Tesha hajamaliza kuniambia kuhusu suala hilo, Mariam akatokezea mlangoni kwa kasi mpaka tukashtuka kiasi, naye akasema, "JC, njoo. Nimeshaweka kinanda."

Nikatabasamu na kumwambia sawa, kisha ndiyo kwa pamoja tukaingia ndani.

Mama wakubwa walikuwa hapo na Shadya wakipata mazungumzo yao wanawake, nasi tukasalimiana vizuri sana na Bi Zawadi akaanza kukumbushia jinsi mambo yalivyokuwa asubuhi tulipokuwa tumekwenda kwa mama mchungaji. Mariam akaniondoa sehemu ya warembo wangu upesi na kunipeleka dining, maana aliona kama vile anacheleweshwa sana, kwa hiyo nikakaa naye pamoja na Tesha ili kuendelea na utaratibu wetu kama kawaida.

★★

Nilitumia muda mrefu nikifanya michezo na mafunzo pamoja na Mariam, mpaka inafika mida ya saa mbili usiku, bado nilikuwa hapo kwao. Kufikia wakati huu Tesha alikuwa ameondoka kwenda kutembea sijui, na wakina Bi Zawadi na Shadya walikuwa wakisaidizana kupika.

Mapishi ni kitu kilichokuwa kikimvutia sana Mariam, alipenda hata kucheza nami kwa kujipikilisha kipindi cha nyuma, lakini kwa sasa kila mara alipoona wakubwa wanaandaa misosi, alijitahidi kuhusika kwa lolote ili kuwasaidia. Kwa hiyo alikuwa akienda jikoni na kurudi kwangu mara kwa mara, na mida hii nilikuwa sehemu ya sebuleni nikingojea Miryam arejee ili nimsalimu kabla ya kuwaaga wa hapa na kwenda kupumzika huko kwa Ankia.

Nilikuwa nikiwaburudisha mama wakubwa kwa story za hivi ama vile, huku na wenyewe wakiwa wamenipatia madokezo kuhusiana na sherehe ya huyo mwanamke aliyeitwa Doris iliyokuwa inakaribia. Kulikuwa na hamu kubwa kutoka kwa Bi Zawadi hasa kuelekea hafla hiyo kwa sababu alisema yeye na mama yake Doris walikuwa marafiki sana, na alimwona Doris wakati alipozaliwa pia. Huyo Doris hakuwa mbali sana kiumri kumfikia Miryam, akiwa kwenye thelathini ya mapema, na mama zao walikua pamoja kutokea udogoni.

Kwa hiyo hapa mbele kungekuwa na sherehe mbili; hiyo ya Doris, pamoja na sikukuu ya kuzaliwa ya Bi Zawadi, ambayo ingeitangulia harusi ya Doris. Mambo yaliyokuwa yakija kwa upande wa familia hii yalionekana kuwa mazuri, na wakaniomba nihusike pia kwenye lolote ili kupendezesha hafla hizo kwa mguso wangu waliouona kuwa baraka sikuzote. Nikawahakikishia kwamba hilo lingetimia kwa asilimia mia.

Basi, saa mbili ikiwa inaendelea kutembea, nikawa nimepigiwa simu na Ankia, na nilipopokea akaniambia alikuwa kwake muda mrefu tayari, na alinimiss, hivyo niende upesi maana alikuwa akiandaa msosi mtamu kwa ajili yetu; na sikupaswa kutoa kisingizio sijui Mamu, sijui nini, na yeye alikuwa wa muhimu. Dah! Nikaona nimkubalie tu, nami nikawaambia mama wakubwa pamoja na Shadya kuwa kuna ishu nilihitaji kufanya hapo kwa Ankia mara moja hivyo ningeondoka sasa ili kwenda kuiandaa.

Kama kawaida, malalamiko kutoka kwa Shadya na Bi Zawadi ya mimi kutaka kuondoka wakati tu msosi ulikuwa unaivishwa yakaanza, lakini nikawatuliza na kuwaahidi ningetenga muda mzuri wa kufurahia mlo pamoja nao; sema kwa wakati huu mambo yalikuwa mengi kidogo. Yaani nilikuwa napendwa na hawa watu hadi kujigawa ilikuwa tabu kiasi, lakini Ankia na yeye aliihitaji ushirika wangu kwa hiyo zamu hii ingekuwa yake.

Mama wakubwa na Shadya wakaridhia, nami nikamuaga na Mariam pia nikisema kesho kama nitawahi kutoka huko "mjini," basi nitakuja ili tucheze tena. Hakuwa na neno. Tukapiga 'Broop' kama kawaida, kisha nikawaambia wote wampe Miryam salamu zangu akirejea, nami ndiyo nikawaacha.

Nikaelekea upande wetu na kumkuta Ankia akiwa sebuleni, mwili wake ukiwa ndani ya nguo za unyumbani, kilemba kichwani, na akiwa anaangalia tamthilia runingani. Tukasalimiana vizuri, nami nikaelekea chumbani na kuvua T-shirt na suruali, nikavaa pensi nyepesi na kaushi tu, kisha nikarudi sebuleni kukaa pamoja naye sofani na kuanza story.

Ankia akaanza kunisimulia kuhusu jamaa fulani aliyekuwa anamsumbua sana kwa kwenda pale dukani kwake kumtongoza kila siku, nami nikaanza kumtania ile ya 'Ankia kapata mchuumba, Ankia kapata mchuumba.' Akacheka sana na kuniambia niache mambo yangu ya kipuuzi.

Kweli nilikuwa tu nina hamu ya kutaka kukaa na Ankia ndiyo maana hata kusema niendelee kuwa pale na mama wakubwa kumsubiria Miryam haikuwa kitu nilichowazia sana tena, kama kumwona bibie ningemwona tu tena, huu sasa ungekuwa ni muda wangu na Ankita. Alikuwa anatoa kero zake mwenyewe na mimi nikimpa ushauri kwa utani mwingi, huku mboga ya msosi mtamu uliolekea kuiva ikihisika vyema puani mwangu kutokea huko jikoni.

Katika zile pindi ambazo angenyanyuka kwenda kukoroga-koroga mapishi yake na kurudi kukaa tena, nilikuwa nikijibu jumbe tofauti-tofauti kwenye simu yangu na kuperuzi mitandao ya kijamii, hii ikiwa ni saa tatu, na wakati Ankia alipokuwa amenyanyuka kwa mara nyingine tena na kwenda jikoni, simu yangu ikaanza kuita.

Nilipoangalia mpigaji, nikakuta ni yule Dotto, kikaragosi mtiifu wa madam Bertha, ndiye aliyekuwa akinipigia. Kufikia kipindi hiki nilikuwa na namba zake pia, kwa sababu na yeye alikuwa na sehemu muhimu kwenye upande tofauti wa biashara za Bertha kama tu ilivyokuwa kwangu, kwa hiyo wakati mwingine tulikuwa tukifanya collabo na nini... hasa kutokana na yeye kuyapenda madawa niliyokuwa nawatengenezea.

Lakini haikuwa kawaida yake kunipigia ama mimi kumpigia, isipokuwa tu iwe ni jambo muhimu, sanasana madam Bertha akihusika; yaani sikuwa na kitu chochote na huyu jamaa ambacho kingefanya aonekane kama mshkaji wa karibu sana mbali na kujuana tu kwa sababu ya biashara zetu na madam. Hivyo kupiga kwake simu muda huu kukaniweka katika hali ya umakini, nami nikapokea nikiwa hapo hapo sofani na kumsikiliza.

"Halloo..." sauti yake ikasikika.

"Yeah, niaje?" nikasema hivyo.

"Poa. Upo kitaa?"

"Cha Masai, yeah. Vipi?"

"Njoo hapa Masai," akaniambia.

"Bar? Upo hapo?" nikamuuliza.

"Ee, njoo."

"Ishu gani? Maana ndo' msosi unawekwa mezani sa'hivi," nikamwambia hivyo.

"Achana na njaa wewe, njoo hapa sasa hivi kuna ishu ya muhimu. Fanya haraka," akasema hivyo kwa sauti makini.

Mh?

Nikamwambia, "Poa. Dakika tano basi."

"Zisipite," akasema hivyo, kisha akakata simu.

Nikatulia kidogo kutafakari ni nini ambacho kingekuwa kinaenda kutokea hapo Masai, na ni mawazo mawili yaliyoingia hasa kwenye fikira zangu.

Kwanza, inawezekana tu kwamba Bertha alikuwa amefika hapo na kutaka niende, ama hakuwa amefika hapo na ndiyo Dotto akawepo kusimama kwa ajili ya ishu niliyohitajiwa. Lakini cha pili, nikawaza vipi ikiwa labda kwa njia fulani yale mambo yangu ya pembeni na maaskari yalikuwa yamewafikia hawa watu? Je kama waliniona, ama kuhisi kuwa ninaelekea kuwa-snitch, na huu ungekuwa mwito wa kwenda kubainisha upande gani niliokuwa hasa, ama labda hata kuumizwa?

Ingenibidi niwe makini mno maana chochote kile kingeweza kutokea, na nikikumbukia vizuri kabisa kwamba askari Ramadhan alikuwa amenipa kifaa fulani maalumu cha kutumia wakati wa hali ya dharula, nikanyanyuka kutoka hapo na kwenda kuvaa suruali pamoja na kofia yangu, ile kama kibandiko ambayo Tesha alininunuliaga kipindi kile ndiyo nimejuana naye. Kifaa kile nikakitia mfukoni.

Baada ya kuvaa hivyo nikatoka na kumuaga Ankia kwa kusema naenda hapo Masai mara moja. Alifikiri nimeitwa labda kwenda kunywa na hivyo ningekimbia msosi aliokuwa akiandaa, lakini nikamwambia hapana, ningeenda tu kuongea na mtu mara moja kisha ningerudi kula. Kwa hilo hakuwa na neno, nami nikatoka na kuanza kuelekea huko Bar.

★★

Nikiwa ndiyo naikaribia Masai, pembezoni mwa geti la mbele kwenye mwingilio wa jengo hilo niliweza kuliona gari la madam Bertha, ile Harrier yake ya silver, likiwa limeegeshwa usawa huo na Dotto mwenyewe akionekana kusimama karibu nalo. Alikuwa amevaa tracksuit kubwa ya blue kama jezi ya klabu ya Chelsea, huku akiwa amesimama na wanaume wengine wawili wa mitaa hii hii akionekana kuongea nao vitu vya kihuni tu, nami nikakaribia sehemu hiyo na kusimama pembeni.

Aliponiona, akanisogelea na kugongesha tano pamoja nami, na wenzake vilevile, kisha akaniambia kwamba kuna sehemu natakiwa kwenda naye si mbali sana na hapa, kwa hiyo niingie kwenye gari ili anipeleke. Nikamuuliza wapi, lakini akasema twende kwenye gari ndiyo tutaongea vizuri, naye akawaaga wenzake na kwenda kuingia kwenye gari, huku akinionyeshea ishara kwa kichwa kuwa niwahishe.

Nilikuwa nimeshapandisha mashaka hata zaidi, lakini hakukuwa na nafasi ya kuwa mwoga hapa. Nilikuwa tayari kwa lolote, kwa hiyo nikaingia upande wa mbele pia pembeni yake, naye akatia gari moto na kuanza kulitembeza. Taratibu tu tukaiacha Masai, tukielekea lamini huko, nami nikaamua kuongea sasa maana jamaa alikuwa kimya tu.

"Mishe zinaendaje?" nikamsemesha.

"Ah, fresh. Fresh. Mambo ni wali nazi," akasema hivyo.

"Haujaja Masai muda. Kulikoni leo? Umewamiss wa huku?"

"Haamnaa. Nilikuwa nimekufata wewe tu," akaniambia hivyo.

"Kwa nini?" nikamuuliza.

"Si nimekwambia kuna sehemu nakupeleka?" akasema hivyo.

"Eeeh, ila hujasema ni wapi," nikamwambia hivyo.

"Tulia sasa. Ni surprise," akaongea namna hiyo.

Nikamtazama kwa umakini sana, kisha nikaangalia pembeni na kuuliza, "Madam anajua kuhusu hii... surprise?"

"Mhmhm... unataka sana niiharibu hiyo surprise, eti?"

"Oh, kumaanisha kwamba yeye ndiyo anafanya hii surprise, si ndiyo?"

"Tutajuaje? Inabidi kulifungua kwanza boksi ndiyo uione. Tulia. Boksi lako unaenda kulifungua muda si mrefu," akaniambia hivyo.

Nikamtazama usoni kisomi zaidi, naye akaniangalia na kutabasamu kiujeuri kiasi, na safari ikaendelea tu.

Tulikuwa tumeingia lami na kuelekea upande wa huko Rangi Tatu, lakini yaani bado ilikuwa ni hapo hapo Mzinga gari likawa limeingia kwenye barabara ya changarawe upande wa pili wa lami hiyo kutokea huko tulikotoka. Yaani, tukawa tumeivuka lami na kwenda upande wa pili wa Mzinga. Akaliendesha gari taratibu kupitia barabara ya changarawe kuelekea sehemu ya ndani zaidi ya mitaa hiyo ambayo sikuwahi kuwa na kawaida kabisa ya kuitembelea, mpaka alipolifikisha eneo lililokuwa na kumbi ya vinywaji na starehe kama tu Bar ya Masai.

Lakini huku palikuwa na hali ya ugiza sana, hapakuwa na watu wengi hapo. Sehemu alipoegeshea gari, kulikuwa na gari lingine aina ya Toyota Vanguard nyeusi, nasi tukashuka kwa pamoja nikiwa sijauliza kingine chochote mpaka wakati huu. Mambo mawili yakawa hakika. Moja, ni kwamba hakudanganya aliposema kuwa hatungeenda mbali, yaani hapa hata kwa mguu tu tulikuwa tunafika na kurudi tulipotoka upesi, na mbili, kilichokuwa kinanisubiri kama "surprise" ndiyo kilikuwa huko ndani.

Dotto akakutana nami mbele ya gari na kuniambia, "Karibu Facebook. Ushawahi kuja hapa?"

Nikatikisa kichwa kukanusha, nami nikamwambia, "Masai pamekuboa sana? Mpaka ukaamua kuja kunipea surprise yangu huku..."

Akacheka kidogo na kunishika begani huku akisema, "Masai kuna macho mengi mno. Huku ndo' pametulia. Twende."

"Subiri. Si uniambie tu kuna nini? Unanipa hali ya wasiwasi bro," nikamwambia hivyo.

"Ah, usiogope..."

"Siogopi..."

"Ee, ndo' twende sasa. Tumekaa pamoja mwezi mzima tunapiga mishe safi halafu huniamini bana? Come on," akanisisitizia huku akitangulia.

Nikafata nyuma yake.

Sehemu hii kimwonekano haikuwa na ule ubora wa kadiri kuifikia hata Masai; jengo lilishikiliwa na kupambwa na mbao nyingi, isipokuwa tu sehemu ya kaunta, na hata waliofika kulewa hapo hawakuwa wengi kivile. Yaani ilikuwa kama vile hamna umeme, taa pekee zikiwa zile za kuwaka-waka kwa mapambo, hapakuchangamka kabisa, lakini ni wazi Dotto hakuwa amenileta ili tujichangamshe hapo.

Tukaipita tu sehemu ya kaunta na kuelekea ndani zaidi mpaka kufikia mlango ambao nilikisia ndiyo ulikuwa wa chumba kama cha VIP kwa hapa Facebook, naye Dotto akafungua mlango na kuingia. Nikajitia ujasiri zaidi na kumfata pia, na kweli kilikuwa chumba kwa ajili ya maVIP, ingawa hakikuwa bora kwa lolote lile ambalo niliwahi kuona. Mwonekano wake ulikuwa wa kujitahidi, lakini sikukazia fikira zangu kwa vitu vilivyokuwa humo, bali watu niliowakuta.

Wanaume. Wawili. Na niliwafahamu vizuri sana. Wote walikuwa wameketi kwenye masofa ya humo, huku katikati kwenye meza kukiwa na sahani yenye kitimoto nyingi, pamoja na chupa chache za bia na K-vant; wakiwa wanatazama upande wangu kwa kuridhika. Ilikuwa ni Chalii Gonga, pamoja na mshirika wa kundi la Festo kutokea kule Red Room, yule jamaa aliyeitwa Sudi!

Mh? Sikutakiwa kuonekana kwamba nilishangaa, lakini nilishangaa. Sikuwa nimetarajia kabisa. Chalii Gonga alionekana makini akiwa ndani ya Manga pana nyeusi na suruali ya jeans, pamoja na buti za kaki miguuni, huku kichwani akivaa kofia kama alivyopendelea. Sudi yeye alikuwa amevaa T-shirt la mikono mifupi lenye rangi mchanganyiko pamoja na suruali ya kijani, nyepesi kwa michezo, huku kiatu cheupe kama vile ametoka sehemu fulani kufanya ukocha wa netiboli kikiificha miguu yake chini.

Nikasimama tu nikiwaangalia watatu hawa, namaanisha na Dotto, ambaye akaenda mpaka alipokaa Chalii Gonga na kuketi kwenye mkono wa sofa, kisha naye akawa ananitazama kwa utulivu kama wawili hao tu. Kofia yangu ilikuwa imeficha kiasi sehemu ya juu ya uso wangu, kwa hiyo kwa jinsi nilivyowaangalia kwa umakini na kuchanganywa kwa wakati mmoja, ilionekana kama nimekuja kigaidi zaidi.

Sudi akasema, "Karibu JC. Kaa hapo tuongee."

Huyu huyu jamaa ndiyo yule ambaye mara ya kwanza kabisa madam Bertha kunipeleka kule Red Room alikuwa ananitendea vibaya kwa chuki binafsi, lakini sasa akawa eti ananikaribisha kama vile tuna amani sana wakati hata sikuwahi kuwa na habari naye. Kumkuta hapa akiwa na Chalii kuliwasha taa nyekundu ya hatari kali kwenye hisia zangu, lakini zaidi ni kwa nini Dotto awe pamoja nao na kutumiwa kunileta kwao. Baada ya kukaribishwa hivyo, nikaendelea tu kusimama na kuwaangalia.

"Wewe ndiyo... kaa hapo tuongee," Chalii akaniambia hivyo.

Nikamtazama Dotto na kuuliza, "Nini kinaendelea?"

Chalii Gonga akatabasamu na kuvuta pombe yake, naye Dotto akasema, "Boksi ndiyo limefunguka. Surprise!"

Nikatabasamu kiasi na kusema, "So... uko kwenye Kahoot na hawa watu, ama labda ni mkutano wa wote na madam hajafika?"

Chalii akamwambia Sudi, "Ahah, si unaona? Yaani kashachizika mno kuwa kibenteni wa mke wangu, unafikiri ataambilika?"

"Zipo njia nyingi za kushawishi watu, lakini ana akili. Tumpe tu ukweli aji-adjust, mengine yatafata," Sudi akasema hivyo.

"Kaa chini dogo. Hakuna mabunduki humu, wala usijali," Dotto akaniambia hivyo.

"Niko sawa nikisimama. Semeni mlichoniitia," nikawaambia hivyo kwa ujasiri.

Sudi akaniangalia usoni kwa umakini, naye akasema, "Toa hiyo kofia."

Nikaishika kofia yangu na kuirekebisha vizuri zaidi kichwani, halafu nikaendelea kumwangalia.

Dotto akatabasamu na kutikisa kichwa chake kiasi.

"Hapa dharau hazitakusaidia kwa chochote mdogo wangu. Ungekuwa unajua ni namna gani unaweka maisha yako hatarini kuwa na Bertha, usingejifanya una kiburi sana," Sudi akaniambia hivyo.

"Yangu me na Bertha, ni yangu me na Bertha. Nimekujulia kwake, na sina ishu yoyote na wewe. Na pia yako wewe na yeye hayanihusu mimi. Sa' sijui unataka nini," nikamwambia hivyo

"Nataka utumie akili yako, na kipaji chako... vizuri. Bertha anakutumia tu, lakini ukiisha faida kwake atakutupa sehemu mbaya mno," Sudi akasema hivyo.

"Okay, kwa hiyo we' unataka nini? Ndo' unataka kusema kwamba unajali sana... utaumia mno nikitupwa, au?" nikamuuliza hivyo.

Chalii akasimama na kuja karibu nami huku akisema, "Acha kujifanya mjuaji dogo. Hivi unaelewa ni namna gani nimetamani sana kukushika na kukutufua-tufua, nikukatekate kila kiungo cha mwili wako kwa kufanya uhawala na mke wangu mimi... tena mpaka unanionyesha kabisa hilo waziwazi? Unataka kujifanya unajua sana dharau, kamwonyeshe mtu mwingine asiyejua nini maana ya kudharauliwa, na siyo mimi. Naijua dharau vizuri sana. Na una... una bahati tu JC. Una bahati tu kwamba ninakuona kama mimi, la sivyo usingekuwa unaivuta hiyo pumzi hata sasa hivi..."

Maneno yake yalieleweka katika kuyasikia, na domo lake likinuka pombe kiasi, lakini sikuelewa alikuwa anamaanisha nini kiujumla. Nikabaki nimemtazama usoni kwa umakini tu.

"Uko sehemu mbaya sana, hujui tu. Nilipokujuaga kipindi kile, nilikukubali sana, lakini ukaamua kuonyesha we' ni mbwa zaidi ya mbwa. Hapa... chukulia yaani ni kama vile tunataka kukusaidia, kwa sababu we' ni mbwa kipofu mwenye faida, na Bertha kakushika mkono akikudanganya kwamba anakuongoza, lakini ni yeye ndiyo unamwongoza pamoja na kwamba huoni. Advantage aliyonayo ni wewe, na akishafika anapotaka, anakuachia uangukie shimoni..." Chalii Gonga akasema hayo.

"Unataka nini Chalii? Unataka nikuombe msamaha? Mke wako ndiye aliyenitaka, muulize ukipenda. Me nilikwenda kwake kikazi, mengine yaliyotokea yalitokea tu... sa' sijui unaongea haya yote ili iweje," nikamwambia hivyo.

"Ahah... yaani bado haelewi tu," Chalii akamwambia Sudi hivyo.

"Well, labda uache kutumia methali nyingi ndiyo nitaelewa unachotaka. Sema mnataka nini," nikawaambia hivyo.

Sudi akasimama pia na kutusogelea, naye akasema, "Tunataka kumwangusha Bertha."

Kauli yake ya moja kwa moja ikanifanya niendelee kumtazama tu utadhani sikusikia alichokuwa amesema.

"Hicho ndiyo tunachotaka," Sudi akasema hivyo.

"Na mnaniambia mimi? Kwa nini?" nikamuuliza hivyo.

"Kwa sababu wewe ndiyo kitu ambacho kinampa nguvu zaidi sasa hivi, ilianza kama masihara tu... lakini siyo wewe tunayetaka kumwangusha. Ikiwa unaelewa nachomaanisha," Sudi akasema hivyo.

Nikawaangalia wote kimaswali kiasi, Dotto akiwa amekaa kule kule tu akitutazama kwa utulivu, nami nikauliza, "Unataka ni-flip? Unataka ni... nijiunge na nyie kumwangusha Bertha?"

Sudi akatikisa kichwa kukubali.

Nikacheka kidogo nikiwa nimeshangazwa kiasi na jambo hili, huku wao wakinitazama kwa umakini tu, kisha nikasema, "Samahani... ahah... nimeshangaa tu. Okay. Kwa hiyo, mnataka kumwangusha madam, halafu mnasema mimi ndiyo nguvu yake. Kwa nini tena mnafanya ionekane kama mnaniomba nijiunge nanyi? Kama me ndo' nguvu yake, si ni mimi ndiyo napaswa kuondolewa, au?"

"Hapana. Wewe utabaki kuwa na nguvu uliyonayo, na utaitumia ukiwa pamoja na sisi," Sudi akaniambia hivyo.

"Nguvu gani unaongelea?" nikamuuliza.

"Uwezo wako wa kutengeneza cocaine hii ambayo imeanza kuagizwa zaidi, ndiyo nguvu anayoongelea," Chalii Gonga akasema hivyo.

Nikamwangalia Sudi usoni.

"Bertha ametumia akili, kukutumia wewe, na watu wake wachache, kutengeneza hiyo kitu bila kutuhusisha sisi wengine; yaani ukiondoa Festus, mimi na wenzetu hatujui mnapozitengenezea, na delivery mnazotoa ni za maana... lakini najua haupati chochote unachostahili zaidi ya kuendelea kulamba tu tako lake kama Charles alivyokuwa akifanyiwa. Tunataka kumwondoa Bertha kwenye picha, ujiunge nami, na manufaa utakayopata yatakuwa mara mia zaidi ya huyo mwanamke anayokupa. Trust me, hautajuta," Sudi akasema hivyo.

Nikatazama chini kwa ufupi, kisha nikasema, "Kumbe ni hicho? Yaani... hofu yako ipo kwenye suala kwamba Bertha ameanza kuichukua market kwa kasi sana, si ndiyo? Unaogopa vile mnavyouza nyie vitapigwa chini muda siyo mrefu maana watu wengi watakuwa wanataka hizi cooking mpya, si ndiyo?"

"Siogopi chochote mimi," Sudi akaniambia hivyo.

"Sasa shida ni nini? Bertha si ni mwenzako? Mpo kundi moja, kwa muda mrefu, hata me sijui mmeanza lini hizi mambo mpaka nilipozikuta, kwa nini sa...."

"Acha kujitoa akili JC! Nisikilize. Mimi nimeshaona mengi nikiwa na yule mwanamke, najua jinsi anavyoweza kubadilika haraka, sasa hivi anakuchekeaa unajiona umefika, ila utakuja kujuta. Nakwambia utakuja kujuta usipoamua kusimama nasi mdogo wangu," Chalii Gonga akasema hayo.

"Huo muda wote ulikuwa wapi Chalii? Kwa nini sasa hivi ndiyo unaonyesha... ujasiri, wa kusimama dhidi ya Bertha?" nikamuuliza.

Sudi akasema, "Unajua kwamba Bertha ana nguvu..."

"Exactly! Ana nguvu, ndiyo maana nyie wote hapa mnamwogopa. Wewe Sudi unaonekana kuwa rebel, sijapinga, lakini hata zile stunt... kuninyooshea bastola ili nikuogope, ulikuwa tu unataka kujitutumua mbele ya wengine lakini unajua huwezi kumgusa. Halafu mnanifata eti mnataka ni-flip? We' Chalii umeshindwa huo muda wote, mimi ndiyo niweze? Na wewe Dotto unakubaliana na haya yote?" nikawaambia wote hivyo.

Wakaangaliana na kucheka kidogo, naye Sudi akasema, "Tumia akili dogo. Sisi, hatumwogopi Bertha... ila, ni aliyesimama mbele zaidi kumpa hiyo nguvu."

Nikatulia kidogo, kisha nikasema, "Festo."

"Mm-hmm. Na, uko sahihi, nina... me ni mjeuri. Sana. Festus ana control kubwa over what we do na tumeheshimu chain yake ya command kwa muda mrefu sana, ila inatakiwa ufike muda mwanaume ujue kwamba huwezi sikuzote kusimama nyuma ya mgongo wa mtu. Bertha... ni kikwazo. Ni... ni kunguni, anayehitaji kutumbuliwa haraka sana. Angekuwa anajali maslahi ya group zima, ange-share mipango yake kwa sisi wote, lakini anaifanya kwa siri zaidi, anaiba mpaka na wateja waliokuwa loyal kwetu, faida zetu sisi zinaporomoka kwa sababu ya ubinafsi wake. Nimeangalia hilo kwa wiki mbili zilizopita, na hasara aliyotupatia mimi, Tito na Farao ni kubwa; anaiba wateja wetu, tena hadi nilisikia wakati anafanya tangazo la biashara yake mpya na we' mbwa wake ulikuwa naye... lakini wengine hawana kifua cha kukoroma kwa madam kwa sababu tu anamfurahisha Festus. Well not me. Sitaruhusu ushindi wake umaanishe me nianguke, that's why inatakiwa yeye ndiyo aanguke haraka sana," Sudi akasema hayo yote kwa mkazo.

Nikawa nimeelewa vizuri shida yake, na sikupenda walivyokuwa wananiita mbwa, ila nikamuuliza, "Kwa hiyo... unataka nitoke upande wa madam Bertha, nije kwako, si ndiyo? Ili nikuongezee faida kama navyofanya kwake, ili tena na wewe iwe vile vile kama yeye, halafu Farao... au nani, aje kwangu tena baadaye kunishawishi nikusaliti na wewe?"

Sudi akacheka kidogo.

Chalii Gonga akasema, "Haitakuwa hivyo. Tukishamwondoa Bertha, kila kazi utakayofanya na sisi itakuwa kwa malipo unayostahili. No monkey business."

"Na kwa kusema 'kumwondoa,' unamaanisha?" nikamuuliza hivyo.

"Tutamuua," Dotto akaongea hivyo.

Nikamtazama kwa umakini sana, kisha nikasema, "Ni Dotto kabisa ndiyo amesema hivyo? Ahah... I can't believe this. Hii... coup imeanza lini kaka?"

"Dotto ni mdogo wangu. Usifikiri amefurahia sana kufanya kazi ndani ya kiganja cha yule mwanamke, na mambo mengi mabaya ambayo Bertha amenifanyia, Dotto ameona. Imetosha sasa," Chalii Gonga akasema hivyo.

"Mabaya? Chalii kaka, si umepewa na hoteli mbili kabisa?" nikamwambia hivyo.

"Acha usenge, malaya wewe! Ulikuwepo? Unajua ni kwa nini alinipa? Muda wote niliokaa nalipia makosa yake lakini kwa wengine inaonekana kama nafurahia maisha... unafikiri ninafurahia kweli? Kama alikwambia alinipa hizo hoteli na bar, alikwambia pia ni kwa nini? Alikwambia kwamba alisababisha mtoto wetu afe? Halafu mimi ndiyo nikalipia makosa yake mwenyewe kwa kulishwa nyama mbichi ya mtu? Eh?" Chalii akaongea kwa hisia.

Nikakaza uso kimaswali kiasi. Hadithi aliyoitoa ilikuwa tofauti kidogo na jinsi nilivyosimuliwa na Bertha, nami nikamuuliza, "Bertha alimuua mtoto wenu?"

"Alikuwa anataka kumnywesha juice yenye sumu mwanamke aliyefikiri ninatoka naye kimapenzi, lakini mtoto wetu akainywa kimakosa na kufariki. Huyo mwanamke nilikuwa hata sitoki naye! Halafu bado akanilaumu mimi kwa kifo cha mtoto wetu, ikawa ni masimango, vitisho, ujeuri... unafikiri ni mwanaume gani anaweza kukaa kuvumilia hayo yote kutoka kwa mwanamke, eh? Kisa tu amepewa kanguvu fulani na Festus na watu wao? Ndiyo nitetemeke forever?" Chalii akasema hivyo.

Mh?

Nikatazama tu chini huku nikitafakari mambo kwa kina.

"Bertha ana mpango mwingine, JC nakwambia. Huo mpango ukikamilika wewe ukiwa umeshamaliza kumsaidia kuutimiza, anakuua. Tena vibaya zaidi ya alivyomuua Joy, bila hata sababu. Hujaujua ulimwengu wake vizuri mdogo wangu, usijione umefika. Utakufa vibaya sana," Chalii akasema hivyo.

Nikatulia kidogo na kushusha pumzi taratibu, kisha nikawauliza, "Kwa hiyo mnachotaka ni nini? Nifanye nini yaani? Me ndo' nimuue Bertha, au?"

Sudi akasema, "Mbona unaenda mbali sana? Tulia. Hapa tunachotaka tu ni wewe kusema kama utajiunga nasi, au la. Mengine baadaye."

"Na kama jibu ni la?" nikamuuliza hivyo.

Wakaangaliana kwa ufupi.

"Ahah... kwamba ndiyo mtaniua? Ikiwa ni hivyo, hata msichelewe. Karibuni," nikawaambia hivyo.

"Nah, kukuua haitupi faida, zaidi ni hasara. Baada ya kukueleza hayo yote, we' ndo' unapaswa uamue. Kubali kuja upande wangu, utapata faida kubwa. Lakini ukiendelea kukaa kwa Bertha kisa anakupa titi unyonye, utaumia sana mwanangu. Hauko peke yako anayenyonyesha," Sudi akasema hivyo.

"Kwamba nini, unanijali sana?" nikamuuliza hivyo.

"Hapana. Najali biashara zangu tu, na nimeona wewe unaweza kuwa asset nzuri. Huko uliko, wanakufichia kile unachostahili, na we' unaendekeza ujinga kufikiri utakuwa mfalme wa malikia anayetaka kukaa kwenye kiti cha ufalme peke yake. Hiyo haipo. Ni muda wa kuamka. Na ni sasa," Sudi akaniambia hivyo.

"Ahah... hivi kweli! Dah, kwa hiyo... tuseme natoka hapa, naenda kumwambia Bertha kila kitu ambacho mmesema. Hapo itakuwaje?" nikawauliza.

"Bertha atakuua vibaya mno ukienda kumwambia haya!" Chalii Gonga akasema hivyo.

Nikamtazama kwa umakini.

"Anamwamini Dotto mara mia zaidi yako, wewe amekujua kwa miezi miwili tu. Ukisema ninajaribu kukufanya umgeuke nikiwa pamoja na Sudi, labda atakuamini. Lakini hatua yoyote atakayotaka kuchukua lazima itapita kwa Dotto, na anafikri Dotto hawezi kumsaliti hata kwa ajili ya kaka yake. Imagine ni namna gani hiyo itakuwa ni rollercoaster juu yako mwenyewe," Chalii akaniambia hivyo kwa uhakika.

Nikamwangalia Dotto kwa umakini, ambaye alikuwa akila tu nyama za kitimoto huku pia akinitazama kama vile siyo yeye aliyekuwa akiongelewa. Nikatabasamu kiasi na kutikisa kichwa kwa kutoamini haya yote.

"Every man's gotta think for himself. Utakaa nyuma ya mgongo wa Bertha mpaka lini wakati wewe ndiyo mwenye nguvu? Oh, usijali kuhusu yale tunayopanga kumfanya. Wewe jali zaidi juu ya ni wapi utasimama. Tumekuita ili uione picha kwa ukamili; we' ni mwanaume, tumia akili, utakachoamua baada ya hapo ni juu yako... na uamue kwa busara," Sudi akaniambia hivyo.

Nikaendelea kumtazama tu kwa utulivu.

Sudi akarudi pale alipokuwa ameketi, huku Chalii Gonga akiendelea kusimama karibu yangu na kuniangalia kwa umakini, na jamaa akachukua simu yake pamoja na kitu kama mkanda wa kuvaa kiunoni sijui, kisha akaja tena upande wangu na kusimama.

Akasema, "Usichukue muda mrefu kunipa jibu. Mambo yatabadilika kwa kasi. Umenielewa?"

Nikabaki tu kumtazama usoni, naye akanipita na kuelekea nje. Chalii Gonga naye akachukua chupa zake za bia pale mezani na kunipita pia, na hapo ndani nikawa nimebaki mimi na Dotto.

Nilimwangalia mwanaume huyo kwa utathmini wa hali ya juu sana, na kwa kweli hakuonekana kuwa na tatizo lolote na yale yote yaliyokuwa yamesemwa humo muda mfupi nyuma. Akatafuna kipande kimoja cha nyama, na kunionyeshea sahani eti na mimi nichukue, lakini nikaendelea tu kumwangalia usoni kwa umakini.

Akanyanyuka pamoja na hiyo sahani yenye kitimoto na kuja mpaka niliposimama, naye akasema, "Game on."

Kisha akanipita na kuelekea nje pia.

Kwa sekunde chache nikabaki nikiwa nawaza huu mchezo ungeelekea wapi zaidi baada ya haya yote, maana ni mengi sana yalikuwa yakiongezeka, na kwa kasi. Yaani kama ni kuwa snitch, basi ningetakiwa kuwa snitch kwa kila upande, mpaka nikaanza kuchanganyikiwa juu ya ni upande upi ambao nilistahili kusimama nao zaidi.

Watu wake Bertha mwenyewe walikuwa wameanza kuunda njama za kutaka kumuua, halafu wanichukue mimi kwa ajili ya mipango yao. Maelezo yote waliyotoa kuhusu kwa nini nisingeweza kumwambia madam kuhusiana na hili yalionekana kuwa utumbo tu kwangu, lakini najua nisingeweza kumwambia yule mwanamke kwa sababu nilielewa kuwa maaskari walikuwa kwenye nyendo za karibu mno kufanikisha zoezi la kuwakamata watu hawa WOTE; haijalishi ikiwa na wao walianza kutangaziana vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Hivyo uamuzi sahihi kwa wakati huu ungetakiwa kuwa kuendelea kutulia tu na kuona ni mkondo gani ambao mambo haya yangeelekea mpaka kufikia siku ambayo yote yangekomeshwa, na ningepaswa kujitahidi kuwa mwangalifu kutojikuta naumizwa vibaya mno na matokeo ambayo yangekuja.






★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TATU

★★★★★★★★★★★★★★


Nikatoka hapo walipopaita Facebook nikiwa nimeanza kuwaza mambo mengi, na baada ya kufika nje sikuyakuta yale magari mawili pale ambapo yalikuwa yameegeshwa, kuonyesha kwamba wale jamaa walikuwa wameshaondoka. Ingenibidi kurudi makwetu kwa kutembea, na haikuwa na tatizo. Kutembea mdogo mdogo mpaka huko kungenipa dakika chache za kutafakari vizuri yale ambayo hasa Chalii alikuwa ameyasema.

Kwenye hiki kisa haikujalisha nani alikuwa anasema ukweli na nani alikuwa anadanganya, lakini jamaa aliponiambia upande wake wa story kuhusu jinsi mtoto wake na Bertha alivyopoteza maisha, nilihisi kama hakuwa akidanganya. Wakati ule Bertha aliponisimulia kwa upande wake nilimwamini kabisa maana si unajua uchungu wa mama na nini, lakini inawezekana alikuwa ananidanganya.,

Hivyo nikaanza kutilia mashaka mambo yote aliyokuwa amesema kuhusu yeye kwenda jela, sijui akatoka, sijui akamuua nani, kwa sababu ndiyo vitu ambavyo vilikuwa hata vimenipa hali ya kumwona kuwa mtu aliyepitia mambo magumu mpaka kusababisha awe jinsi alivyo. Ikiwa alikuwa amedanganya tu kuhusu kifo cha mwanaye na kumtesa Chalii kwa makosa yake yeye mwenyewe, basi alikuwa wa daraja lingine la ubaya huyo mwanamke. Baya sana.

Na siyo kwamba nilikuwa nimepuuzia kila kitu ambacho Sudi na Chalii waliniambia kuhusiana na mwanamke yule kuniua akishafika pale anapotaka afike baada ya kunitumia, hicho kilikuwa ni kitu ambacho nilitakiwa kuchukua kwa tahadhari. Ningetulia kuona jinsi ambavyo mambo yangeenda, lakini mpaka kufikia siku ambayo askari Ramadhan na wenzake wangepiga hatua kuwakamata watu hawa, ningepaswa niwe chonjo sana. Yaani LOLOTE lingeweza kutokea, huenda hata ningeuliwa lakini bado nikawa hai kiroho kuendelea kusimulia hiki kisa!

Kesho ingekuwa Ijumaa, kwa hiyo najua ningeonana na Bertha tu. Hatukuwa tumeonana tokea Jumatano, zaidi tuliwasiliana tu kwa sms fupi na yeye kuonekana ana mambo mengi aliyokuwa anapika, kwa hiyo sikujifanya mbwa sana wa kunusanusa aliyofanya kila muda. Tulikuwa tunashiriki mapenzi, lakini hatukuwa wapenzi kabisa.

Mimi kuendelea kuigiza kwamba nampenda sana Bertha ilikuwa muhimu kwa faida yangu, na nilifurahi tu kwamba hakutaka ipitilize maana hata na mimi kiukweli sikutaka ipitilize. Ah, yaani nilikuwa naombea siku ya askari Ramadhan iwahi kufika! Na tena na hapo bado hata sikujua ingekuwa vipi kuhusu kiongozi Festo, jamaa mtata aliyekuwa akiogopwa na akina Sudi, sijui ikiwa na yeye angeshikwa? Ingebidi kuendelea kungoja tu.

Dakika kadhaa kupita na saa tano ikawa imeingia baada ya kuwa nimefika hapo kwa Ankia. Wakati nikija nilikutana na Bobo nje ya Masai Bar, tukaongea kidogo na akanitambulisha kwa mpenziwe hatimaye kwa mara ya kwanza kabisa. Alikuwa mdada mdogo tu tena kukaribiana rika na Mariam kabisa, lakini alionekana kuwa mjanja mno, na Bobo alipendelea wenye umri kama wa huyo demu wake.

Kwa hiyo ndiyo nikafika na kuingia hapo getini, na yule Fatuma wa dukani alikuwa ameshafunga. Wakati nilipotazama upande wa jirani zetu nikaliona gari la Miryam hapo nje, lakini ni uwepo wa mwanamke huyo nje hapo ndiyo ukafanya nisitishe hatua zangu na kuendelea kumwangalia kupitia vitundu vya ukuta wa uzio. Alikuwa ameketi kitini sehemu ya varanda lao pale, akiwa ametazama tu simu yake akionekana kusoma ama kuchat.

Nikasogea kwenye tundu la ukutani na kumchungulia vizuri, na kama kuotea tu, akanyanyua uso wake na kutazama sehemu hiyo hiyo, hivyo akawa ameniona. Nikatabasamu kiasi na kumpungia mkono, naye akatabasamu pia na kunipungia mkono pia. Nikatoa ishara kwa kiganja kumuuliza jambo fulani, lakini nafikiri kwa kutoelewa vizuri, akaamua kunionyesha ishara kuwa nimfate hapo ili tuweze kupeana salamu vyema zaidi.

Ikabidi nizunguke, moja kwa moja mpaka getini kwao na kuingia, nami nikaanza kukielekea kibaraza hapo alipokuwa. Alikuwa ndani ya kiblauzi chepesi cheupe, ambacho kilifunika kifua chake vizuri kabisa, na kinguo laini na kirefu kwa juu kilimsitiri vyema mikononi mpaka chini kama vile koti la kike, ila jepesi. Alikuwa amevalia na suruali pana ya kulalia pia, akiketi kwa kukunja nne, na nywele zake laini alikuwa ameziachia zimwagikie mgongoni kwake.

Nikafika karibu zaidi na hapo huku nikitabasamu kirafiki, naye akawa ananiangalia machoni kwa utulivu tu.

"Vipi?" nikamuuliza hivyo.

"Safi. Ndiyo umetoka mizunguko?" akaniuliza hivyo na kasauti kake katamu ambako walahi nisingewahi kuja kukakinai.

Nikamwambia, "Yeah, ila sikuwa mbali sana. Hapo tu Mzinga. Nilikuwepo hapa mpaka mida saa mbili kabla hujafika. Umeingia muda umeenda sana?"

"Saa tatu ndiyo nimefika. Sijachelewa sana," akasema hivyo.

"Wengine?"

"Wameshaingia kulala."

"Na Tesha amelala sasa hivi?"

"Hapana. Hayupo. Nimerudi sijamkuta. Ameniambia yupo njiani kutokea Tandika huko kwa rafiki yake... alikuwa amemwalika," akanijulisha.

"Ahaa... ningeshangaa," nikasema hivyo.

Akatabasamu kiasi na kusema, "Nyie wote mida hii ndiyo sahihi kwa mambo yenu kufanywa."

"Ahahah... me siyo sana..."

"Aa wapi..." akasema hivyo, nasi tukacheka kidogo kwa pamoja.

"Mbona hujaingia kulala bado? Au unakula upepo hapa shauri ya joto eh?" nikamuuliza.

"Ee joto pia. Ila huwa napenda kukaa nje mara moja moja... kufikiria vitu," akasema hivyo huku akiangalia pembeni.

Niliona kuwa kuna "vitu" ndiyo alikuwa anafikiria, nami nikataka nijue kama ningeweza kusaidia kwa njia yoyote.

"Umekula lakini?" nikamuuliza.

Akaniangalia na kutikisa kichwa kukubali, naye akasema, "Mapema tu wote tumekula, ndiyo hadi na Mamu akalala. Wewe je?"

"Mimi pia," nikasema hivyo ingawa bado sikuwa nimekula.

Akaonekana kutafakari kitu, kisha akasema, "Ngoja nikuletee kiti."

Sikuwa hata na mpango wa kutaka kukaa kabisa, na kabla hata sijasema lolote lile akawa amenyanyuka na kuelekea ndani. Baada ya sekunde chache akarejea akiwa amebeba kiti kimoja, nami nikamsaidia kukipokea na kukiweka chini, kisha sote tukakaa vitini kwa pamoja tukiwa tumeacha uwazi katikati yetu, na tukiwa tumetazama upande wa gari lake. Hali nzuri ya utulivu na kaupepo ka hapo nje vilifanya nipate hisia nzuri, nami nikamwangalia bibie.

"Ulikuwa umeenda kuzungukia wapi leo baada ya kuachana na ma' mkubwa?" akauliza hivyo.

"Kwenye ile ishu," nikamwambia hivyo.

"Mmefikia wapi sasa hivi?"

"Karibu sana. Yaani ni kesho, kesho-kutwa... hawa watu wanakamatwa," nikamwambia hivyo.

"Ni bora. Jitahidi sana kuwa mwangalifu, eti?" akaniambia hivyo.

"Ah, ondoa shaka. Kila kitu kinaenda kwa mpangilio," nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa na kuangalia pembeni.

Ni Miryam pekee ndiye aliyekuwa anajua kuhusiana na ishu ya mimi kushirikiana na maaskari kisiri ili kuwasaidia wawakamate wakina Bertha, kwa kuwa baada ya yale mambo yote kutokea ule mwezi uliopita, aliniuliza ikiwa nilimaanisha kile nilichosema kuhusu suala hilo siku ile aliponipiga kibao kwa kutoniamini, ndiyo nikakiri ukweli huo. Ila kuhusiana na Festo kuingiliana na haya mambo pia sikuwa nimemwambia, na inawezekana jamaa alikuwa bado akimfatilia huyu mwanamke lakini nilitumaini kuwa mwisho wake ungefika hivi karibuni, na Miryam angejionea mwenyewe.

Nikamtathmini kidogo baada ya yeye kuendelea kutazama pembeni tu, nami nikasema, "Vipi huko dukani? Wateja kama wote wanafurika eh?"

Akasema, "Eeh, angalau. Mungu anasaidia. Mambo yanaenda."

"Hivi... kabla haujaja huku, ulikuwa unafanya kazi wapi?" nikamuuliza hivyo.

"Dodoma. Nilikuwa mhasibu kwenye benki ya Exim kule Area D," akanifahamisha.

"Wow! Sikujua. Kumbe una expertise ya uhasibu?"

Akatabasamu na kusema, "Yeah."

"Kwa hiyo kama usingekuja huku... mpaka sasa hivi ungekuwa bado unafanya hiyo kazi ya uhasibu?"

"Labda. Sijui kwa kweli," akaniambia hivyo.

"Haukutafuta sehemu nyingine hata ulipofika Dar?"

"Hapana. Nilitaka tu ku-focus kwenye duka aliloniachia baba," akasema hivyo.

"Okay. Haujutii kuiacha kazi yako lakini? Haujawa-miss uliokuwa umefanya nao kazi, ama eneo ulilokuwa unaishi... marafiki wa huko?"

"Ah, kama ni marafiki, tunafanya mawasiliano. Nilipokatisha mkataba wangu kuja huku, waajiri na wafanyakazi wenzangu walielewa... so hatujaachana pabaya, kuna ambao nakutana nao mitandaoni, wananijulia hali, utani kidogo, basi. Ni miaka michache imepita hata hivyo... siwezi kusema sija-miss kazi niliyokuwa nayo, lakini sijuti kuiacha. Huku niko sawa pia," akasema hivyo.

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

"Kwa nini umeuliza?" akaniuliza hivyo.

"Oh... yaani, huwa nafikiria tu, kwa mambo yote ambayo umepitia toka umekuja kwa familia yako, ingekuwa mwingine angekata tamaa na kurudi alikokuwa kwa sababu labda ni pazuri zaidi. Lakini wewe uko imara sana... ni jambo zuri mno," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu kiasi na kusema, "Asante. Hata wewe pia."

Nikamwangalia usoni.

"Kuamua kujitoa ili kuwasaidia maaskari wawakamate hao watu wabaya, kuacha kwenda kufanya mambo yako ili ubaki kumsaidia mdogo wangu, tena kwa kupoteza gharama na muda wako... wewe ni imara pia," akaniambia hivyo.

"Ahah... asante. Lakini me gharama gani nimepoteza sasa? Mbona unatia chumvi?"

"Wakati wako wa mapumziko, na ujuzi wako ambao ni wa kulipwa unautumia kwa mdogo wangu bure kabisa... hiyo ni gharama. Unamsogeza Mamu sehemu nzuri sana yaani... sikufikiria kwamba ingeweza...."

"Imeshawezekana Miryam. Mdogo wako yuko imara kama wewe, kwa hiyo hata hilo atalishinda tu," nikamwambia hivyo kwa uhakikisho.

Akashusha pumzi na kuangalia pembeni.

"Kuna vitu kuhusu Mamu bado vinakuhangaisha, Miryam?" nikamuuliza kwa upole.

Bila kuniangalia, akasema, "Nawaza tu kuhusu ufahamu wake. Tunamwita mtoto, lakini Mariam ni msichana mkubwa tayari. Anaelekea kuwa mwanamke kamili. Nilikuwa nataka hali hii imwondoke mapema... arudi shule... a... asomee jambo fulani, yaani... sijui kama itawezekana..."

"Itawezekana, Miryam. Taratibu tu."

"Lakini hiyo taratibu itaisha lini? Najua nilikuomba ubaki, ila hautaendelea kuwa hapa sikuzote, na ukiondoka sijui ndiyo itakuwaje..."

"Haina shida Miryam. Hata kama nikiondoka, Mamu tayari ame-progress... kile ambacho nimefanya naye, hata kama ni Tesha anaweza kukifanya. Kikubwa tu ni kumbukumbu yake kuwa imara zaidi... basi. Hata akija kwenda shule tena, la muhimu linatakiwa kuwa tumeifanya kumbukumbu yake ikae vizuri sana. Akili anayo, na atafanikiwa," nikamtia moyo.

"Kwa hiyo kikubwa ni kuifanya kumbukumbu yake iwe imara... na ndiyo unachofanya sasa hivi?"

"Yes."

"Lakini... tutajuaje kwamba imetosha?"

"Haihitaji kutosha, ila kuanza tu kuonekana. Anatakiwa yeye mwenyewe aanze kuona kwamba kucheza rede na watoto, ni utoto. Anatakiwa aje akwambie 'dada, nataka kwenda kutembea huko Kigamboni,' yeye mwenyewe, siyo mpaka asindikizwe na mtu, kwa sababu anajua jinsi ya kujiongoza kwenda na kurudi. Zipo ishara tu zitajionyesha kwamba yuko tayari... tena... najua siku siyo nyingi zitaanza kujionyesha," nikamwambia hivyo.

"Eti eh?"

"Mmm," nikakubali.

"Sawa. Nimeelewa. Na... unaongea kama vile mwalimu wa falsafa, siyo wa biology," akatania.

Nikacheka kidogo na kusema, "Napenda kusoma vitu vingi, tia ndani falsafa pia."

"Kumbe?"

"Eeh. Unafikiri ilikuwaje sharobaro kama mimi akawa daktari?"

Akatabasamu na kusema, "Kwa kupenda kusoma sana."

"Ndiyo hivyo."

Akiwa ananiangalia kwa utulivu, akasema, "Haya nielezee jinsi unavyoiona kumbukumbu ya Mamu kwa sasa toka umeanza kumfundisha. Kifalsafa zaidi."

"Ahah... unapenda kusikiliza falsafa?" nikamuuliza.

Akatikisa nyusi kuonyesha "ndiyo" huku akitabasamu kwa mbali.

Nikasafisha koo kiasi, nami nikamwambia, " Well... naweza kusema yuko kwenye hatua nzuri, siyo kama mwanzo, ila... kifalsafa ya biology na sayansi yake zaidi, iko hivi..."

Akatabasamu zaidi huku akiniangalia kwa utulivu.

"Niliwahi kusoma makala fulani. Inaeleza jinsi kumbukumbu ilivyo complex sana, hasa kwa kuwa ubongo ni mtata, na inapotokea mtu anakuwa amepoteza kabisa kumbukumbu, kuirudisha kunakuwa na mitihani yake. Lakini kwa case kama ya Mamu, ikiwa amepatwa tu na usahaulifu shauri ya trauma, ama nini, ndiyo unakuta tunafanya hizi harakati sasa... kumsaidia... arejeshe... ahahah..."

Nikajikuta nacheka tu kutokana na jinsi Miryam alivyokuwa akinitazama kwa njia iliyoonyesha usikivu, naye akatabasamu na kusema, "Endelea."

Nikamwambia, "Unakuta pale ubongo unapokuwa unajaribu kuvuta kumbukumbu, zile kumbukumbu imara ndiyo zinakuwa zinaimarika zaidi, halafu zile dhaifu..."

"Zinafifia zaidi," akamalizia.

"Eeeh. Maana yake sasa mtu anapojipa challenge ya kuvuta kumbukumbu ya mambo aliyojifunza, iwe ni leo, jana, juzi... ndiyo inakuwa njia nzuri ya kuuondoa ule udhaifu ili kuupa ubongo nafasi nzuri ya kuboresha kumbukumbu. Mazoezi ninayofanya na Mamu ndiyo yana lengo hilo la mwanzo. Hatakumbuka kila kitu ambacho amewahi kuona au kujifunza, kama tu wewe huwezi kukumbuka kila sura uliyoiona ulipoenda mizunguko na kurudi nyumbani. Yale mambo ambayo yanaongezeka kwenye ubongo wake; vitu anavyojifunza, anavyoona, na kuhisi, iwe vipya au vya zamani, ndiyo vinakuwa kama gharama inayofunika yale ambayo aliyajali zamani, na kumbukumbu yake inaimarika zaidi kwa haya ambayo... inayapata sasa na kuendelea. Umeelewa?"

Akatikisa kichwa taratibu kukubali huku akinitazama kwa utulivu.

"Kumbukumbu ya Mamu imekuwa ikishindana yenyewe kwa yenyewe, na kwa sababu ilimtawala kwa muda mrefu akiwa namna hiyo, haikuwa rahisi kwa ubongo wake kuzingatia... au niseme... yaani kutilia maanani yeye ni nani, ikiwa itafaa arudishwe nyuma kiufahamu ama asonge mbele... ubongo wake ukaamua ah, ngoja tumrudishe huyu nyuma, halafu abaki hivyo hivyo. Kwa hiyo ili kumtoa huko, ingehitajika kuuchezesha ubongo wake kwa kumbukumbu za vitu vinavyodumu kupitia njia za kipekee... namaanisha vitendo, sauti, na hisia. Kumshikamanisha Mamu hasa na vitu vinavyoteka hisia zake, kwa njia nzuri, ndiyo kutamfanya akumbuke mambo mengi vyema zaidi, popote pale atakapoenda. Haimhitaji JC peke yake kwa ajili ya hilo. Ni nyie wote," nikamwambia hivyo kwa sauti tulivu.

Miryam alikuwa ameganda kunitazama usoni tu na macho yake mazuri, naye akaachia tabasamu hafifu lililoonyesha upendezi.

Nikabana midomo yangu nikitabasamu pia, hapo nikijiona kama mwambaaa, kisha nikasema, "Ndiyo falsafa ya daktari hiyo."

Akafumba macho yake taratibu na kuyafumbua tena huku akiangalia pembeni, naye akaniambia, "Una akili... na maneno mengi."

Nikiwa nimejisikia vizuri baada ya kusifiwa, nikamwambia, "Ndiyo Jayden huyo."

Akarudia kunitazama machoni huku akitabasamu kiasi, nami pia nikamwangalia usoni.

Tulikuwa tunaangaliana kama vile tumegandishwa, na aisee hisia ya hapo niliipenda sana. Ilikuwa kama vile mwanamke alitaka niendelee kuongea, lakini mimi nikawa nimekosa cha kuendelea kumpa, hivyo ni macho yetu tu ndiyo yakabaki kuambiana kitu fulani kwa lugha ambayo sidhani kama sisi kwa pamoja tuliielewa. Ndipo akawa amekatisha utizami huo na kujiweka sawa zaidi kwa jinsi alivyokuwa ameketi, nami nikaacha kumwangalia pia.

"Sawa. Nashukuru kwa company. Falsafa imeeleweka vizuri. Asante pia," akasema hivyo huku akizilaza nywele zake kwa kiganja.

Nikasimama, naye pia akasimama, kisha nikamwambia, "Nina kausingizi kananivuta, nataka nikakawahi hahah..." nikaongea kwa kujishaua.

"Hata me nausikia. Kesho mapema kazini," akasema hivyo.

"Yeah... mimi pia. Namaanisha... nitawahi kuamka, nije kumcheki Mamu," nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa kukubali hilo huku akiniangalia kwa macho yenye subira fulani hivi, sijui nini tu.

Nikamwambia, "Sawa. U-usiku mwema. Ngoja nikusaidie kupeleka kiti ndani..."

Mwanamke hakuwa na neno, naye akageuka na kukibeba kiti chake, mimi pia nikibeba nilichokuwa nimekalia, nasi tukaviingiza ndani pamoja mpaka sehemu ya dining. Nikawa nimemuaga kwa mara nyingine tena, nami huyoo nikaelekea mpaka kwa Ankia nikimwacha bibie anafunga geti la nje.

Nilimkuta Ankia akiwa sebuleni bado, anatazama tamthilia za Azam Two, na eti alikuwa amenuna shauri ya mimi kuchelewa kurudi. Nikaanza kumtekenya baada ya kukaa naye ili mood yake nzuri irudi, naye akaacha kununa na kudeka kwake nilipomwambia nimejitahidi kuwahi ili nile msosi wake mtamu. Eti hakuwa amekula bado, akinisubiri mpaka nirudi, na kwa kweli alikuwa akitaka tu tule pamoja maana aliandaa pilau na nyama vizuri sana utafikiri ilikuwa sikukuu.

Kwa hiyo mwenye nyumba wangu akapakua, nasi tukala na kushiba na kusaza. Story mbili tatu zikafata mpaka mida ya saa sita usiku, ndiyo sote tukaanza harakati za kwenda kujipumzisha vyumbani kwa amani; kuoga kidogo kwanza, kuhakikisha milango na mageti yamefungwa, kisha ndiyo tukaagana na kwenda kujitupia vitandani.

Bado mawazo yaliyohusiana na mkutano wangu pamoja na Sudi, Chalii Gonga, na Dotto yalikuwa yakizunguka kichwani, lakini nikajitahidi kuulazimisha usingizi unibebe upesi ili mambo mengine yafuate siku ikishakucha.


★★★


Na hatimaye ikakucha. Hii ikiwa ni Ijumaa, asubuhi na mapema tu nikajiandaa vizuri kwa ajili ya kutoka, Ankia akiwa ameshaandaa chai na kuweka mambo mezani ili tukamue na kiporo cha moto cha pilau na nyama aliyotengeneza jana. Nikavaa T-shirt langu jipya la mikono mifupi lenye rangi ya maroon (napenda sana hii rangi), pamoja na suruali ya jeans nyeusi, na kiatu cheupe miguuni kikakamilisha mwonekano wangu wa daktari sharobaro. Nikanywa chai pamoja na Ankia na kuagana naye ikiwa inakaribia kufika saa nne, nami nikaelekea kwao Mariam upesi.

Nikiwa tu ndiyo nimefika getini kwao na kuingia, hapo hapo simu yangu ikaanza kuita; Bertha. Nikapokea. Mwanamke akawa anauliza nilikuwa wapi, kwa nini nilichelewa mno kufika kule Riverside Ubungo kwa ajili ya mishe yetu, nami nikamwambia ndiyo nilikuwa njiani lakini nilikuja kwa uangalifu maana nilihisi kuna watu wangekuwa wananifatilia. Kauli hiyo ikamfanya aniulize kwa nini nilidhani hivyo, ila nikamtuliza kwa kusema asiwe na wasiwasi, ilikuwa ni hisia tu na nilijitahidi kuwa makini.

Dakika hiyo hiyo, kutokea mlango wa pale ndani akawa ametoka Tesha, bila shaka akiwa amesikia geti lilipofunguliwa, naye akanitikisia kichwa kisalamu na mimi kumrudishia pia. Nikamwambia madam Bertha kwenye simu kuwa ningemtafuta baadaye nikishafika kule, lakini akanibadilishia mpango.

Akasema niende moja kwa moja kule hotelini kwake, yaani nisiende Ubungo, na mimi kuona Tesha anaanza kuja upande wangu kukanifanya tu nimkubalie madam haraka-haraka, kisha ndiyo nikamuaga na kukata simu. Sababu za yeye kunibadilishia mkondo wa safari ningezijua huko huko.

Tesha akawa amenifikia karibu zaidi na kusema, "Demu... na najua sijakosea!"

Nikacheka kidogo na kumwambia, "Zamu hii sitakataa."

Akacheka pia na kugongesha tano pamoja nami, kisha akasema, "Umeng'aa mwanangu. Wapi hiyo?"

"Naingia Vunja Bei mara moja..."

"Unaenda kumnunulia manzi kijora, nini?"

"Aa wee... hiyo haipo. Ni business za maana naenda kufanya, nipate ya kutosha kwa ajili ya mechi Jumapili."

"Aa, hapo umeongea! Kariakoo Derby bonge moja la dude Jumapili. Katafute mwanangu tuje tunywe haswa!"

"Ahahahah... tafuta ya kwako, fala wewe! Me namtengenezea mambo Adelina," nikamwambia hivyo.

"Adelina? Yule sista'ake Joy?"

"Eeh, atakuja huku kuangalia Derby."

"Ahaa... kumbe ushaanza kutoka naye?"

"Hamna, rafiki yangu tu. Nimemwalika. Tutakaa naye Jumapili, labda tutaenda Masai, au siyo?"

"Uhakika. Na sisi kesho nanilii, Doris... anakuja hapa kututembelea," akasema hivyo.

"Ahaa, Doris anayeolewa?"

"Eeh. Halafu atakuja na Dina."

"Okay. Afu' Dina kitambo! Yuko poa?" nikamuuliza hivyo.

"Ah, kwanza we' mwana si unafanya mambo siyo fresh," akaniambia hivyo.

"Nimefanyaje tena?"

"Mpaka leo mwanangu hujaenda kumwona Dina... wakati ulimpaga promise kabisa, mwenzio akaiweka moyoni..."

"Ah, ahahahah... dah!" nikajikuta nachoka.

"Ananicheki sana kaka, kila mara lazima JC uuliziwe. Sema, huwa tu nasahau, inabidi nikupe namba yake ili ndo' upate motisha zaidi. Unamtesa mtoto wa watu," akasema hivyo.

"Ah, basi unadhani shida ni namba Tesha?"

"Ee, ni namba. Hauchukulii serious maana huna contact zake kabisa... mpaka mwezi umepita."

"Hamna bro, hiyo siyo shida. Shida ni muda. Mambo yanakuwa mengi. Hivi... unamkumbuka yule mwanamke mwislamu ambaye... tulikutana naye kwenye daladala ile siku tunaenda Kigamboni, alikuwa na kale kadem keupe ulikokuwa unataka namba yake?" nikamuuliza.

"Eeh, afu' kweli, dah! Kitambo! Ulizipata?"

"Hamna, lakini si nilizichukua za yule mama yake?"

"Ee. Mnawasiliana? Ushapiga?"

"Ndo' hicho nachotaka kukwambia. Toka hiyo siku tunawasiliana, ananielewa, anataka show... lakini mpaka sasa hivi hatujawahi kukutana tena. Kwo' ishu siyo mawasiliano, ni muda tu," nikamwambia hivyo.

"Ah, mwanangu una raha wewe! Kumbe maza mtu akakukubali?"

Nikacheka kidogo.

"Afu' dili si lilikuwa umpate kisha uniletee namba za mtoto wake yule? Ulizipata sasa?"

"Aa wapi, we' mwenyewe si ulikuwa umeshasahau? Ndo' imeisha hiyo..."

"Unazingua. Kwani shi'ngapi kukutana tena Kigamboni na huyo maza? Kwanza uliwahi kumwona uso wake kabisa?"

"Tunaongeaga video call, anavua zile mask zao."

"Anaitwa nani?"

"Ibtisam."

"Mzuri?"

"Mzuri ee. Mwarabu."

"Dah, sa' unafeli wapi?"

"Yaani wewe Tesha wewe... ahah. Wewe umetoka tu sasa hivi kuniambia simtendei Dina haki, halafu kidogo tu na Ibtisam ushaanza kumwakilisha. Kwa nini hauna msimamo?" nikamuuliza.

Akacheka na kusema, "Ndo' nilivyo. Kama raha za UKIMWI zinakutaka wewe tu, lazima nikusapoti ili ulazwe pema peponi, kamanda! Mapema..."

"Ahahahah... endelea kuota. Au ndo' kusema Dina anao sasa?"

"Hamna. Dina yuko clean kama sahani nyeupee..."

"Unajuaje?"

"Najua tu. We' ngoja nikupe namba yake, umtafute tu ajisikie vizuri... ile kwamba wewe ndiyo umemtafuta yeye. Atafurahi sana. Tena na kesho akija mkaonana, fresh zaidi," akasema hivyo.

"Haya, nipe. Sifagilii wenye umri mdogo, ila ilete," nikasema hivyo.

"We' si unapenda mashangazi tu, badala utafute viembe bado vibichii unakalia hayo madude yaliyoiva mpaka yanatepeta byeee..." akaniambia hivyo, nasi kwa pamoja tukacheka kidogo.

Akanipatia namba za huyo Dina, nami nikazitunza na kumwambia ningemtafuta baadaye.

Ikawa ni kwenda huko ndani kuwasalimu wakina Bi Jamila na Bi Zawadi baada ya kuongea hivyo kidogo na Tesha, pamoja na Mariam pia ambaye ndiyo alikuwa ametoka tu kuamka kama binti ya mfalme. Nikawaaga pia dakika chache zilipopita za maongezi mafupi kuhusiana na sherehe ya bibi harusi mtarajiwa Doris, ambaye alikuwa ameanza kunijengea hamu ya kutaka kumwona bila hata ya mimi kuelewa sababu kihalisi, na baada ya hapo ndiyo nikaondoka kuelekea kwa madam Bertha.

★★

Safari ya kunipeleka huko ilichukua muda wa kama saa moja hivi kutokana na msongamano wa magari mara kwa mara, na hatimaye nikafika hoteli ya Royal Village. Huku nikiwa nakumbukia ishu yote ya jana usiku pamoja na yule Dotto, nikaelekea hadi chumbani kwa madam nikiwa nimehakikisha sikuwa na mkia wowote nyuma yangu, yaani sikufatiliwa.

Hii haikuwa kama sinema ya wamarekani ambao muda wote hutembea na bastola kiunoni ili kujilinda, hapa palikuwa Bongo, kwa hiyo ni macho pekee ndiyo yaliyotumika kuangaza huku na kule kujihakikishia usalama maana kwa sasa sikujua nani angekuwa akiniangalia zaidi. Hata ulinzi ambao ningeahidiwa na maaskari najua haukutosha kwa asilimia zote, nilipaswa kuwa na macho makali ya utambuzi wa kilichonizunguka na kujua hatua za kuchukua kuepuka mabalaa mapema.

Baada ya kufika kwenye chumba hicho, madam Bertha akawa anenifungulia mlango. Nilimwangalia kwa njia ya kawaida tu usoni, lakini yeye alikuwa akinitazama kwa upendezi na tabasamu hafifu midomoni mwake. Wakati huu alikuwa amebadilisha mwonekano wake kichwani kwa kusukia nywele za rasta nene na nyekundu, ambazo zilitengenezwa kwa njia fulani kama minyororo mirefu iliyofikia mpaka usawa wa hips zake. Na hapa alikuwa amevaa T-shirt la mikono mirefu kama sweta, lenye rangi ya kijivu, refu mno mpaka kufikia magotini, na zaidi ya hilo hakuwa amevaa kingine.

Nikamtikisia nyusi moja kiuchokozi kiasi, naye akanyoosha mikono yake yote kunielekea kama kuniita niende kumkumbatia. Nikaingia na kumkumbatia kweli, nikiwa makini kutokana na mawazo yaliyokuwa yakizunguka akilini, naye akaniachia mgongoni na kuendelea kuyashika mabega yangu huku akiniangalia usoni kwa macho yenye raha, na mie nikiendelea kukishika kiuno chake.

"Nimekumiss," akaniambia hivyo.

"Mimi, wewe?" nikamuuliza hivyo kiutani.

"Mhm... mdogo wako anaendelea vizuri?"

"Ee, anasukuma-sukuma angalau."

Bertha akanisogelea karibu zaidi usoni na kunibusu mdomoni mara mbili, kisha akaniangalia na kusema, "Mbona uko serious hivyo?"

"Hamna, kawaida tu," nikamwambia hivyo.

Akiwa anasugua-sugua mabega yangu kwa viganja vyake vyenye makucha marefu, akasema, "Hujapenda nilipokubadilishia safari ghafla eh?"

"Hapana, nimefurahi. Nilifikiri ningekuja kukuona jioni... ila now ndo' ntakuwa nawe mpaka jioni," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu kidogo na kunibusu mdomoni tena, kisha akaniachia na kusema, "Haya, funga mlango. Njoo tuongee."

Akaanza kulielekea sofa, nami nikaurudishia mlango na kumfata pia. Alikuwa akifanya utafiti fulani mtandaoni inaonekana kwenye laptop yake iliyokuwa kwenye meza hapo pembeni, nami nilipofika karibu naye, akakaa kwenye sofa huku akiuvuta mkono wangu ili nikae pamoja naye. Ikawa hivyo. Akawa amenitazama usoni sawia huku akiegamiza mwili wake kwenye egemeo la sofa, nami nikawa namwangalia kwa utulivu.

"Ulikuwa umefika wapi nilipokupigia?" akaniuliza hivyo.

"Nilikuwa... maeneo ya Kariakoo. Ndiyo nilikuwa nataka tu kupanda mwendokasi," nikamdanganya.

"Nini kilifanya ukafikiri kuna mtu alikuwa anakufatilia?"

"Sijasema hivyo, yaani... nilikuwa tu najitahidi kuwa mwangalifu..."

"Na ndo' ungefanyaje hivyo?"

"Nisingeenda Ubungo moja kwa moja. Ningepitiliza kabisa mpaka mbele huko, niangalie mazingira, halafu ndo' niende kwa spot yetu hata kwa boda... precaution tu," nikamwambia.

Akatikisa kichwa na kusema, "Sawa."

Nikaiangalia laptop yake na kumuuliza, "Ulikuwa unatafuta kitu fulani hapo?"

Akaitazama na kisha kuifunika huku akisema, "Yeah, nimemaliza. Achana nayo."

"Kwa hiyo supermarket leo sitaenda, eti? Au nitaenda baadaye?"

"Achana na ishu za kazi, HB. Nimekuita hapa tuongee... mimi na wewe," akasema hivyo.

Nikajiweka kiumakini zaidi na kushika nywele zake, kisha nikasema, "Niambie."

"Kwa hizi wiki zilizopita... umefanya kazi nzuri sana kunionyesha kwamba kweli uko serious na mimi, na najua bado sijakupa tuzo yako unayostahili," akaniambia hivyo.

Nikamwangalia kwa njia ya ufikirio.

Akasema, "Usipandishe mzuka, simaanishi nitaanza kukupa mpalange!"

"Ahahahah... huwa unawaza vitu vya ajabu madam!" nikamwambia hivyo.

"Well, great minds think alike. Hata wewe una akili ya ajabu sana. Yaani tumeanza kuuza coke yako muda mfupi tu lakini neema kubwa imeanza kushuka mikononi mwetu..." akaniambia hivyo.

"Unajiongelea wewe na nani?"

"Sisi wote. Festus hasa. Na hivi ndiyo nilivyokuwa nataka HB wangu. Umeni-impress kweli kama ulivyoahidi," akaongea kwa njia yenye hisia sana.

Nikalazimisha tabasamu na kusema, "Usiwaze. Nilikwambia chochote kwa ajili yako."

"Kweli eh?"

"Kabisa. Kila kitu nilichofanya... ni kwa sababu yako. Na kila kitu nitakachofanya, ni kwa sababu yako wewe tu," nikamwambia hivyo kwa njia ya fumbo.

Akatabasamu na kunishika usawa wa sikio, naye akasema, "Unataka niwe wako peke yako, ndiyo maana umefanya kila uwezacho mpaka kuwa hapa. Unataka nifungue moyo wangu kwako na kukuweka ndani zaidi, si ndiyo? Huu ndiyo wakati wako sasa."

Maneno hayo yalisemwa kwa njia ya hisia za kweli kabisa, yaani Bertha hakuwa akijaribu kunitania wala nini, niliona wazi kwamba alimaanisha kile ambacho alikisema. Nikaendelea kumwangalia usoni kwa umakini, huku fikira zangu zikiendelea kupingana kwelikweli na hisia zangu.

"Sidanganyi kwamba tayari nilikuwa nimeshakuelewa pia, ila ndo' sitaki tu yale yale ya Chaz yanipate tena maana nawaelewa nyinyi vizuri mno..." akasema hivyo.

"Mimi siyo..."

"Wewe siyo Charles, najua. Ndiyo maana nimeweza kufungua tena milango ya moyo wangu kwa ajili yako. Nimekukubali kwa asilimia zote JC," akasema hivyo.

Dah! Alikuwa akiongea kwa hisia yaani, sikutegemea. Haya yote yalikuwa yanatokea wapi?

"Nataka tu nikuombe... msamaha. Nisamehe kwa jinsi nilivyokuwa nakutendea mwanzoni mpaka sasa, nilikuwa sijagundua tu thamani yako. Ila sasa hivi nimeijua, sitaki inipotee kabisa. Nakuhitaji sana... uendelee kuwa upande wangu... siyo kwa sababu ya kazi tu, yaani... kama hivi... ni... najua unaelewa..."

Aliongea kwa kubabaika kiasi, akionyesha kuwa na udhaifu wa wazi mbele yangu, na tayari nilikuwa nimeshaelewa alichokuwa anajaribu kuniambia.

Nikaangalia pembeni kwanza na kusema, "Ndiyo... nimekuelewa."

"Umeelewa nini?" akauliza.

Nikamwangalia na kusema, "Kuna neno unataka kusema, lakini unashindwa kulisema."

"Ahahah... haujakosea," akaniambia hivyo.

Nikiwa makini, nikamuuliza, "Kinachokufanya ushindwe ni nini?"

"I guess... siyo mtu wa tamthilia-tamthilia mimi, hayo maneno nayaona kuwa ya kipuuzi..."

"Lakini si ndiyo ukweli wa kile unachohisi?"

"La muhimu ni kwamba umenielewa, kwa hiyo siyo lazima niyaseme."

"Sawa. Haina shida," nikamwambia hivyo.

"Haina shida? Yaani nimeongea hayo yote halafu unasema haina shida?" akauliza.

"Ee, si nimekwambia nimeelewa? Kwa hiyo poa. Haina shida. Nimekuelewa," nikamwambia hivyo.

Akanikazia macho yake.

"Ahah... mbona unaniangalia hivyo sa'?" nikamuuliza.

"Hata dakika mbili hazijaisha tayari umeshaanza kunionyesha dharau kisa tu nimekwambia...."

"Umeniambia nini?" nikamkatisha.

Akanikazia macho yake tena, naye akasema, "Kwa hiyo kumbe ni mpaka niseme?"

Nikatabasamu na kusema, "Haujasema. Mpaka useme."

Akashindwa kujizuia kutabasamu kwa hisia, naye akaniangalia kwa macho yaliyojaa upendezi na kusema, "Nakupenda."

Mh?

Nikabaki nikimwangalia kwa njia ya kawaida, kwa sababu kihalisi mwenzake hapa nilikuwa naigiza, lakini yeye alionekana kuwa mahali palipompoteza kabisa kihisia. Yaani alionyesha ile ya kufa na kuoza kabisa, na mimi hapo nikawa natafakari mambo mengi kinoma.

Kila kitu ambacho niliambiwa jana na wale wanaume kilikuwa kikizunguka kichwani, hasa vitu alivyosema Chalii. Kwa hiyo hapa asilimia kubwa ya kile ambacho akili yangu iliniambia ilikuwa kwamba mwanamke huyu alikuwa akinidanganya tu ili niendelee kulainika zaidi kwake, nimpe mafanikio zaidi, halafu mwisho wa siku ndiyo aje kuniangamiza. Tena bila sababu.

Nikashindwa hata kutoa itikio lolote la maigizo na kuendelea kumwangalia usoni kwa umakini sana, kwa sababu akili yangu ilikuwa ikinishawishi kuweka kigingi cha kutoamini kabisa maneno hayo, lakini tena ikawa kama hisia zangu zinaniambia aliyamaanisha. Na yaani ilikuwa ni kwa nini wakati huu huu tu ambao mambo yangeenda kumharibikia eti ndiyo akaanza kuleta swaga za 'nakupenda sana?'

Alipoona nimeishia kumtazama tu, akasema, "Nini wewe? Si ndiyo ulichotaka nikiseme, au? Out loud. Nimekisema."

Nikatazama pembeni tu na kushusha pumzi kama mtu aliyeishiwa raha.

"HB... vipi? Haujafurahi?" akaniuliza hivyo.

Nikamwangalia na kusema, "No, siyo hivyo. Sikutegemea tu..."

"Kwa nini? Kutokana na jinsi ulivyonizoea, yaani hauwezi kuamini kabisa eti?"

"Siyo... ahah... siyo kabisa, yaani... ni ngumu tu kidogo. Nilikuwa hadi nimeshaanza kuzoea kuwa toy wako tu," nikamwambia hivyo.

Akanishika shingoni na kuniambia, "Usiseme hivyo bwana, namaanisha nayokwambia. Umeshaniteka kihisia, mbali tu na kuwa mzuri kitandani..."

Nikatabasamu na kutikisa kichwa kiasi.

"Ona, kuanzia sasa hivi... nataka tuwe serious. Umenipigania kwa vingi, na umeshinda. Nataka nikupe unachostahili sasa. Labda ndiyo itakuwa njia nzuri ya kukuthibitishia kwamba nimekupenda pia..." akasema hivyo.

"Na ni nini hicho kitakachonithibitishia?" nikamuuliza.

Akatabasamu na kusema, "Nataka kuzaa na wewe."

Nikamtazama kimaswali kiasi, na kwa sauti ya chini nikasema, "Nini?"

"Yes. Nataka kukuzalia JC. Niko tayari kuwa mama wa mtoto wako," akaniambia hivyo.

Raa!

Nikabaki nikimtazama machoni kwa umakini sana utadhani alikuwa amenipiga kwa kitu kizito kupita uzito wenyewe. Nilishindwa kuelewa ikiwa mpaka kufikia hapa mwanamke huyu bado alikuwa akicheza na mimi, ama ilikuwa vipi. Huyu alikuwa Bertha, ama nilikuwa naota?




★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TATU

★★★★★★★★★★★★★★


Nikatoka hapo walipopaita Facebook nikiwa nimeanza kuwaza mambo mengi, na baada ya kufika nje sikuyakuta yale magari mawili pale ambapo yalikuwa yameegeshwa, kuonyesha kwamba wale jamaa walikuwa wameshaondoka. Ingenibidi kurudi makwetu kwa kutembea, na haikuwa na tatizo. Kutembea mdogo mdogo mpaka huko kungenipa dakika chache za kutafakari vizuri yale ambayo hasa Chalii alikuwa ameyasema.

Kwenye hiki kisa haikujalisha nani alikuwa anasema ukweli na nani alikuwa anadanganya, lakini jamaa aliponiambia upande wake wa story kuhusu jinsi mtoto wake na Bertha alivyopoteza maisha, nilihisi kama hakuwa akidanganya. Wakati ule Bertha aliponisimulia kwa upande wake nilimwamini kabisa maana si unajua uchungu wa mama na nini, lakini inawezekana alikuwa ananidanganya.,

Hivyo nikaanza kutilia mashaka mambo yote aliyokuwa amesema kuhusu yeye kwenda jela, sijui akatoka, sijui akamuua nani, kwa sababu ndiyo vitu ambavyo vilikuwa hata vimenipa hali ya kumwona kuwa mtu aliyepitia mambo magumu mpaka kusababisha awe jinsi alivyo. Ikiwa alikuwa amedanganya tu kuhusu kifo cha mwanaye na kumtesa Chalii kwa makosa yake yeye mwenyewe, basi alikuwa wa daraja lingine la ubaya huyo mwanamke. Baya sana.

Na siyo kwamba nilikuwa nimepuuzia kila kitu ambacho Sudi na Chalii waliniambia kuhusiana na mwanamke yule kuniua akishafika pale anapotaka afike baada ya kunitumia, hicho kilikuwa ni kitu ambacho nilitakiwa kuchukua kwa tahadhari. Ningetulia kuona jinsi ambavyo mambo yangeenda, lakini mpaka kufikia siku ambayo askari Ramadhan na wenzake wangepiga hatua kuwakamata watu hawa, ningepaswa niwe chonjo sana. Yaani LOLOTE lingeweza kutokea, huenda hata ningeuliwa lakini bado nikawa hai kiroho kuendelea kusimulia hiki kisa!

Kesho ingekuwa Ijumaa, kwa hiyo najua ningeonana na Bertha tu. Hatukuwa tumeonana tokea Jumatano, zaidi tuliwasiliana tu kwa sms fupi na yeye kuonekana ana mambo mengi aliyokuwa anapika, kwa hiyo sikujifanya mbwa sana wa kunusanusa aliyofanya kila muda. Tulikuwa tunashiriki mapenzi, lakini hatukuwa wapenzi kabisa.

Mimi kuendelea kuigiza kwamba nampenda sana Bertha ilikuwa muhimu kwa faida yangu, na nilifurahi tu kwamba hakutaka ipitilize maana hata na mimi kiukweli sikutaka ipitilize. Ah, yaani nilikuwa naombea siku ya askari Ramadhan iwahi kufika! Na tena na hapo bado hata sikujua ingekuwa vipi kuhusu kiongozi Festo, jamaa mtata aliyekuwa akiogopwa na akina Sudi, sijui ikiwa na yeye angeshikwa? Ingebidi kuendelea kungoja tu.

Dakika kadhaa kupita na saa tano ikawa imeingia baada ya kuwa nimefika hapo kwa Ankia. Wakati nikija nilikutana na Bobo nje ya Masai Bar, tukaongea kidogo na akanitambulisha kwa mpenziwe hatimaye kwa mara ya kwanza kabisa. Alikuwa mdada mdogo tu tena kukaribiana rika na Mariam kabisa, lakini alionekana kuwa mjanja mno, na Bobo alipendelea wenye umri kama wa huyo demu wake.

Kwa hiyo ndiyo nikafika na kuingia hapo getini, na yule Fatuma wa dukani alikuwa ameshafunga. Wakati nilipotazama upande wa jirani zetu nikaliona gari la Miryam hapo nje, lakini ni uwepo wa mwanamke huyo nje hapo ndiyo ukafanya nisitishe hatua zangu na kuendelea kumwangalia kupitia vitundu vya ukuta wa uzio. Alikuwa ameketi kitini sehemu ya varanda lao pale, akiwa ametazama tu simu yake akionekana kusoma ama kuchat.

Nikasogea kwenye tundu la ukutani na kumchungulia vizuri, na kama kuotea tu, akanyanyua uso wake na kutazama sehemu hiyo hiyo, hivyo akawa ameniona. Nikatabasamu kiasi na kumpungia mkono, naye akatabasamu pia na kunipungia mkono pia. Nikatoa ishara kwa kiganja kumuuliza jambo fulani, lakini nafikiri kwa kutoelewa vizuri, akaamua kunionyesha ishara kuwa nimfate hapo ili tuweze kupeana salamu vyema zaidi.

Ikabidi nizunguke, moja kwa moja mpaka getini kwao na kuingia, nami nikaanza kukielekea kibaraza hapo alipokuwa. Alikuwa ndani ya kiblauzi chepesi cheupe, ambacho kilifunika kifua chake vizuri kabisa, na kinguo laini na kirefu kwa juu kilimsitiri vyema mikononi mpaka chini kama vile koti la kike, ila jepesi. Alikuwa amevalia na suruali pana ya kulalia pia, akiketi kwa kukunja nne, na nywele zake laini alikuwa ameziachia zimwagikie mgongoni kwake.

Nikafika karibu zaidi na hapo huku nikitabasamu kirafiki, naye akawa ananiangalia machoni kwa utulivu tu.

"Vipi?" nikamuuliza hivyo.

"Safi. Ndiyo umetoka mizunguko?" akaniuliza hivyo na kasauti kake katamu ambako walahi nisingewahi kuja kukakinai.

Nikamwambia, "Yeah, ila sikuwa mbali sana. Hapo tu Mzinga. Nilikuwepo hapa mpaka mida saa mbili kabla hujafika. Umeingia muda umeenda sana?"

"Saa tatu ndiyo nimefika. Sijachelewa sana," akasema hivyo.

"Wengine?"

"Wameshaingia kulala."

"Na Tesha amelala sasa hivi?"

"Hapana. Hayupo. Nimerudi sijamkuta. Ameniambia yupo njiani kutokea Tandika huko kwa rafiki yake... alikuwa amemwalika," akanijulisha.

"Ahaa... ningeshangaa," nikasema hivyo.

Akatabasamu kiasi na kusema, "Nyie wote mida hii ndiyo sahihi kwa mambo yenu kufanywa."

"Ahahah... me siyo sana..."

"Aa wapi..." akasema hivyo, nasi tukacheka kidogo kwa pamoja.

"Mbona hujaingia kulala bado? Au unakula upepo hapa shauri ya joto eh?" nikamuuliza.

"Ee joto pia. Ila huwa napenda kukaa nje mara moja moja... kufikiria vitu," akasema hivyo huku akiangalia pembeni.

Niliona kuwa kuna "vitu" ndiyo alikuwa anafikiria, nami nikataka nijue kama ningeweza kusaidia kwa njia yoyote.

"Umekula lakini?" nikamuuliza.

Akaniangalia na kutikisa kichwa kukubali, naye akasema, "Mapema tu wote tumekula, ndiyo hadi na Mamu akalala. Wewe je?"

"Mimi pia," nikasema hivyo ingawa bado sikuwa nimekula.

Akaonekana kutafakari kitu, kisha akasema, "Ngoja nikuletee kiti."

Sikuwa hata na mpango wa kutaka kukaa kabisa, na kabla hata sijasema lolote lile akawa amenyanyuka na kuelekea ndani. Baada ya sekunde chache akarejea akiwa amebeba kiti kimoja, nami nikamsaidia kukipokea na kukiweka chini, kisha sote tukakaa vitini kwa pamoja tukiwa tumeacha uwazi katikati yetu, na tukiwa tumetazama upande wa gari lake. Hali nzuri ya utulivu na kaupepo ka hapo nje vilifanya nipate hisia nzuri, nami nikamwangalia bibie.

"Ulikuwa umeenda kuzungukia wapi leo baada ya kuachana na ma' mkubwa?" akauliza hivyo.

"Kwenye ile ishu," nikamwambia hivyo.

"Mmefikia wapi sasa hivi?"

"Karibu sana. Yaani ni kesho, kesho-kutwa... hawa watu wanakamatwa," nikamwambia hivyo.

"Ni bora. Jitahidi sana kuwa mwangalifu, eti?" akaniambia hivyo.

"Ah, ondoa shaka. Kila kitu kinaenda kwa mpangilio," nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa na kuangalia pembeni.

Ni Miryam pekee ndiye aliyekuwa anajua kuhusiana na ishu ya mimi kushirikiana na maaskari kisiri ili kuwasaidia wawakamate wakina Bertha, kwa kuwa baada ya yale mambo yote kutokea ule mwezi uliopita, aliniuliza ikiwa nilimaanisha kile nilichosema kuhusu suala hilo siku ile aliponipiga kibao kwa kutoniamini, ndiyo nikakiri ukweli huo. Ila kuhusiana na Festo kuingiliana na haya mambo pia sikuwa nimemwambia, na inawezekana jamaa alikuwa bado akimfatilia huyu mwanamke lakini nilitumaini kuwa mwisho wake ungefika hivi karibuni, na Miryam angejionea mwenyewe.

Nikamtathmini kidogo baada ya yeye kuendelea kutazama pembeni tu, nami nikasema, "Vipi huko dukani? Wateja kama wote wanafurika eh?"

Akasema, "Eeh, angalau. Mungu anasaidia. Mambo yanaenda."

"Hivi... kabla haujaja huku, ulikuwa unafanya kazi wapi?" nikamuuliza hivyo.

"Dodoma. Nilikuwa mhasibu kwenye benki ya Exim kule Area D," akanifahamisha.

"Wow! Sikujua. Kumbe una expertise ya uhasibu?"

Akatabasamu na kusema, "Yeah."

"Kwa hiyo kama usingekuja huku... mpaka sasa hivi ungekuwa bado unafanya hiyo kazi ya uhasibu?"

"Labda. Sijui kwa kweli," akaniambia hivyo.

"Haukutafuta sehemu nyingine hata ulipofika Dar?"

"Hapana. Nilitaka tu ku-focus kwenye duka aliloniachia baba," akasema hivyo.

"Okay. Haujutii kuiacha kazi yako lakini? Haujawa-miss uliokuwa umefanya nao kazi, ama eneo ulilokuwa unaishi... marafiki wa huko?"

"Ah, kama ni marafiki, tunafanya mawasiliano. Nilipokatisha mkataba wangu kuja huku, waajiri na wafanyakazi wenzangu walielewa... so hatujaachana pabaya, kuna ambao nakutana nao mitandaoni, wananijulia hali, utani kidogo, basi. Ni miaka michache imepita hata hivyo... siwezi kusema sija-miss kazi niliyokuwa nayo, lakini sijuti kuiacha. Huku niko sawa pia," akasema hivyo.

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

"Kwa nini umeuliza?" akaniuliza hivyo.

"Oh... yaani, huwa nafikiria tu, kwa mambo yote ambayo umepitia toka umekuja kwa familia yako, ingekuwa mwingine angekata tamaa na kurudi alikokuwa kwa sababu labda ni pazuri zaidi. Lakini wewe uko imara sana... ni jambo zuri mno," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu kiasi na kusema, "Asante. Hata wewe pia."

Nikamwangalia usoni.

"Kuamua kujitoa ili kuwasaidia maaskari wawakamate hao watu wabaya, kuacha kwenda kufanya mambo yako ili ubaki kumsaidia mdogo wangu, tena kwa kupoteza gharama na muda wako... wewe ni imara pia," akaniambia hivyo.

"Ahah... asante. Lakini me gharama gani nimepoteza sasa? Mbona unatia chumvi?"

"Wakati wako wa mapumziko, na ujuzi wako ambao ni wa kulipwa unautumia kwa mdogo wangu bure kabisa... hiyo ni gharama. Unamsogeza Mamu sehemu nzuri sana yaani... sikufikiria kwamba ingeweza...."

"Imeshawezekana Miryam. Mdogo wako yuko imara kama wewe, kwa hiyo hata hilo atalishinda tu," nikamwambia hivyo kwa uhakikisho.

Akashusha pumzi na kuangalia pembeni.

"Kuna vitu kuhusu Mamu bado vinakuhangaisha, Miryam?" nikamuuliza kwa upole.

Bila kuniangalia, akasema, "Nawaza tu kuhusu ufahamu wake. Tunamwita mtoto, lakini Mariam ni msichana mkubwa tayari. Anaelekea kuwa mwanamke kamili. Nilikuwa nataka hali hii imwondoke mapema... arudi shule... a... asomee jambo fulani, yaani... sijui kama itawezekana..."

"Itawezekana, Miryam. Taratibu tu."

"Lakini hiyo taratibu itaisha lini? Najua nilikuomba ubaki, ila hautaendelea kuwa hapa sikuzote, na ukiondoka sijui ndiyo itakuwaje..."

"Haina shida Miryam. Hata kama nikiondoka, Mamu tayari ame-progress... kile ambacho nimefanya naye, hata kama ni Tesha anaweza kukifanya. Kikubwa tu ni kumbukumbu yake kuwa imara zaidi... basi. Hata akija kwenda shule tena, la muhimu linatakiwa kuwa tumeifanya kumbukumbu yake ikae vizuri sana. Akili anayo, na atafanikiwa," nikamtia moyo.

"Kwa hiyo kikubwa ni kuifanya kumbukumbu yake iwe imara... na ndiyo unachofanya sasa hivi?"

"Yes."

"Lakini... tutajuaje kwamba imetosha?"

"Haihitaji kutosha, ila kuanza tu kuonekana. Anatakiwa yeye mwenyewe aanze kuona kwamba kucheza rede na watoto, ni utoto. Anatakiwa aje akwambie 'dada, nataka kwenda kutembea huko Kigamboni,' yeye mwenyewe, siyo mpaka asindikizwe na mtu, kwa sababu anajua jinsi ya kujiongoza kwenda na kurudi. Zipo ishara tu zitajionyesha kwamba yuko tayari... tena... najua siku siyo nyingi zitaanza kujionyesha," nikamwambia hivyo.

"Eti eh?"

"Mmm," nikakubali.

"Sawa. Nimeelewa. Na... unaongea kama vile mwalimu wa falsafa, siyo wa biology," akatania.

Nikacheka kidogo na kusema, "Napenda kusoma vitu vingi, tia ndani falsafa pia."

"Kumbe?"

"Eeh. Unafikiri ilikuwaje sharobaro kama mimi akawa daktari?"

Akatabasamu na kusema, "Kwa kupenda kusoma sana."

"Ndiyo hivyo."

Akiwa ananiangalia kwa utulivu, akasema, "Haya nielezee jinsi unavyoiona kumbukumbu ya Mamu kwa sasa toka umeanza kumfundisha. Kifalsafa zaidi."

"Ahah... unapenda kusikiliza falsafa?" nikamuuliza.

Akatikisa nyusi kuonyesha "ndiyo" huku akitabasamu kwa mbali.

Nikasafisha koo kiasi, nami nikamwambia, " Well... naweza kusema yuko kwenye hatua nzuri, siyo kama mwanzo, ila... kifalsafa ya biology na sayansi yake zaidi, iko hivi..."

Akatabasamu zaidi huku akiniangalia kwa utulivu.

"Niliwahi kusoma makala fulani. Inaeleza jinsi kumbukumbu ilivyo complex sana, hasa kwa kuwa ubongo ni mtata, na inapotokea mtu anakuwa amepoteza kabisa kumbukumbu, kuirudisha kunakuwa na mitihani yake. Lakini kwa case kama ya Mamu, ikiwa amepatwa tu na usahaulifu shauri ya trauma, ama nini, ndiyo unakuta tunafanya hizi harakati sasa... kumsaidia... arejeshe... ahahah..."

Nikajikuta nacheka tu kutokana na jinsi Miryam alivyokuwa akinitazama kwa njia iliyoonyesha usikivu, naye akatabasamu na kusema, "Endelea."

Nikamwambia, "Unakuta pale ubongo unapokuwa unajaribu kuvuta kumbukumbu, zile kumbukumbu imara ndiyo zinakuwa zinaimarika zaidi, halafu zile dhaifu..."

"Zinafifia zaidi," akamalizia.

"Eeeh. Maana yake sasa mtu anapojipa challenge ya kuvuta kumbukumbu ya mambo aliyojifunza, iwe ni leo, jana, juzi... ndiyo inakuwa njia nzuri ya kuuondoa ule udhaifu ili kuupa ubongo nafasi nzuri ya kuboresha kumbukumbu. Mazoezi ninayofanya na Mamu ndiyo yana lengo hilo la mwanzo. Hatakumbuka kila kitu ambacho amewahi kuona au kujifunza, kama tu wewe huwezi kukumbuka kila sura uliyoiona ulipoenda mizunguko na kurudi nyumbani. Yale mambo ambayo yanaongezeka kwenye ubongo wake; vitu anavyojifunza, anavyoona, na kuhisi, iwe vipya au vya zamani, ndiyo vinakuwa kama gharama inayofunika yale ambayo aliyajali zamani, na kumbukumbu yake inaimarika zaidi kwa haya ambayo... inayapata sasa na kuendelea. Umeelewa?"

Akatikisa kichwa taratibu kukubali huku akinitazama kwa utulivu.

"Kumbukumbu ya Mamu imekuwa ikishindana yenyewe kwa yenyewe, na kwa sababu ilimtawala kwa muda mrefu akiwa namna hiyo, haikuwa rahisi kwa ubongo wake kuzingatia... au niseme... yaani kutilia maanani yeye ni nani, ikiwa itafaa arudishwe nyuma kiufahamu ama asonge mbele... ubongo wake ukaamua ah, ngoja tumrudishe huyu nyuma, halafu abaki hivyo hivyo. Kwa hiyo ili kumtoa huko, ingehitajika kuuchezesha ubongo wake kwa kumbukumbu za vitu vinavyodumu kupitia njia za kipekee... namaanisha vitendo, sauti, na hisia. Kumshikamanisha Mamu hasa na vitu vinavyoteka hisia zake, kwa njia nzuri, ndiyo kutamfanya akumbuke mambo mengi vyema zaidi, popote pale atakapoenda. Haimhitaji JC peke yake kwa ajili ya hilo. Ni nyie wote," nikamwambia hivyo kwa sauti tulivu.

Miryam alikuwa ameganda kunitazama usoni tu na macho yake mazuri, naye akaachia tabasamu hafifu lililoonyesha upendezi.

Nikabana midomo yangu nikitabasamu pia, hapo nikijiona kama mwambaaa, kisha nikasema, "Ndiyo falsafa ya daktari hiyo."

Akafumba macho yake taratibu na kuyafumbua tena huku akiangalia pembeni, naye akaniambia, "Una akili... na maneno mengi."

Nikiwa nimejisikia vizuri baada ya kusifiwa, nikamwambia, "Ndiyo Jayden huyo."

Akarudia kunitazama machoni huku akitabasamu kiasi, nami pia nikamwangalia usoni.

Tulikuwa tunaangaliana kama vile tumegandishwa, na aisee hisia ya hapo niliipenda sana. Ilikuwa kama vile mwanamke alitaka niendelee kuongea, lakini mimi nikawa nimekosa cha kuendelea kumpa, hivyo ni macho yetu tu ndiyo yakabaki kuambiana kitu fulani kwa lugha ambayo sidhani kama sisi kwa pamoja tuliielewa. Ndipo akawa amekatisha utizami huo na kujiweka sawa zaidi kwa jinsi alivyokuwa ameketi, nami nikaacha kumwangalia pia.

"Sawa. Nashukuru kwa company. Falsafa imeeleweka vizuri. Asante pia," akasema hivyo huku akizilaza nywele zake kwa kiganja.

Nikasimama, naye pia akasimama, kisha nikamwambia, "Nina kausingizi kananivuta, nataka nikakawahi hahah..." nikaongea kwa kujishaua.

"Hata me nausikia. Kesho mapema kazini," akasema hivyo.

"Yeah... mimi pia. Namaanisha... nitawahi kuamka, nije kumcheki Mamu," nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa kukubali hilo huku akiniangalia kwa macho yenye subira fulani hivi, sijui nini tu.

Nikamwambia, "Sawa. U-usiku mwema. Ngoja nikusaidie kupeleka kiti ndani..."

Mwanamke hakuwa na neno, naye akageuka na kukibeba kiti chake, mimi pia nikibeba nilichokuwa nimekalia, nasi tukaviingiza ndani pamoja mpaka sehemu ya dining. Nikawa nimemuaga kwa mara nyingine tena, nami huyoo nikaelekea mpaka kwa Ankia nikimwacha bibie anafunga geti la nje.

Nilimkuta Ankia akiwa sebuleni bado, anatazama tamthilia za Azam Two, na eti alikuwa amenuna shauri ya mimi kuchelewa kurudi. Nikaanza kumtekenya baada ya kukaa naye ili mood yake nzuri irudi, naye akaacha kununa na kudeka kwake nilipomwambia nimejitahidi kuwahi ili nile msosi wake mtamu. Eti hakuwa amekula bado, akinisubiri mpaka nirudi, na kwa kweli alikuwa akitaka tu tule pamoja maana aliandaa pilau na nyama vizuri sana utafikiri ilikuwa sikukuu.

Kwa hiyo mwenye nyumba wangu akapakua, nasi tukala na kushiba na kusaza. Story mbili tatu zikafata mpaka mida ya saa sita usiku, ndiyo sote tukaanza harakati za kwenda kujipumzisha vyumbani kwa amani; kuoga kidogo kwanza, kuhakikisha milango na mageti yamefungwa, kisha ndiyo tukaagana na kwenda kujitupia vitandani.

Bado mawazo yaliyohusiana na mkutano wangu pamoja na Sudi, Chalii Gonga, na Dotto yalikuwa yakizunguka kichwani, lakini nikajitahidi kuulazimisha usingizi unibebe upesi ili mambo mengine yafuate siku ikishakucha.


★★★


Na hatimaye ikakucha. Hii ikiwa ni Ijumaa, asubuhi na mapema tu nikajiandaa vizuri kwa ajili ya kutoka, Ankia akiwa ameshaandaa chai na kuweka mambo mezani ili tukamue na kiporo cha moto cha pilau na nyama aliyotengeneza jana. Nikavaa T-shirt langu jipya la mikono mifupi lenye rangi ya maroon (napenda sana hii rangi), pamoja na suruali ya jeans nyeusi, na kiatu cheupe miguuni kikakamilisha mwonekano wangu wa daktari sharobaro. Nikanywa chai pamoja na Ankia na kuagana naye ikiwa inakaribia kufika saa nne, nami nikaelekea kwao Mariam upesi.

Nikiwa tu ndiyo nimefika getini kwao na kuingia, hapo hapo simu yangu ikaanza kuita; Bertha. Nikapokea. Mwanamke akawa anauliza nilikuwa wapi, kwa nini nilichelewa mno kufika kule Riverside Ubungo kwa ajili ya mishe yetu, nami nikamwambia ndiyo nilikuwa njiani lakini nilikuja kwa uangalifu maana nilihisi kuna watu wangekuwa wananifatilia. Kauli hiyo ikamfanya aniulize kwa nini nilidhani hivyo, ila nikamtuliza kwa kusema asiwe na wasiwasi, ilikuwa ni hisia tu na nilijitahidi kuwa makini.

Dakika hiyo hiyo, kutokea mlango wa pale ndani akawa ametoka Tesha, bila shaka akiwa amesikia geti lilipofunguliwa, naye akanitikisia kichwa kisalamu na mimi kumrudishia pia. Nikamwambia madam Bertha kwenye simu kuwa ningemtafuta baadaye nikishafika kule, lakini akanibadilishia mpango.

Akasema niende moja kwa moja kule hotelini kwake, yaani nisiende Ubungo, na mimi kuona Tesha anaanza kuja upande wangu kukanifanya tu nimkubalie madam haraka-haraka, kisha ndiyo nikamuaga na kukata simu. Sababu za yeye kunibadilishia mkondo wa safari ningezijua huko huko.

Tesha akawa amenifikia karibu zaidi na kusema, "Demu... na najua sijakosea!"

Nikacheka kidogo na kumwambia, "Zamu hii sitakataa."

Akacheka pia na kugongesha tano pamoja nami, kisha akasema, "Umeng'aa mwanangu. Wapi hiyo?"

"Naingia Vunja Bei mara moja..."

"Unaenda kumnunulia manzi kijora, nini?"

"Aa wee... hiyo haipo. Ni business za maana naenda kufanya, nipate ya kutosha kwa ajili ya mechi Jumapili."

"Aa, hapo umeongea! Kariakoo Derby bonge moja la dude Jumapili. Katafute mwanangu tuje tunywe haswa!"

"Ahahahah... tafuta ya kwako, fala wewe! Me namtengenezea mambo Adelina," nikamwambia hivyo.

"Adelina? Yule sista'ake Joy?"

"Eeh, atakuja huku kuangalia Derby."

"Ahaa... kumbe ushaanza kutoka naye?"

"Hamna, rafiki yangu tu. Nimemwalika. Tutakaa naye Jumapili, labda tutaenda Masai, au siyo?"

"Uhakika. Na sisi kesho nanilii, Doris... anakuja hapa kututembelea," akasema hivyo.

"Ahaa, Doris anayeolewa?"

"Eeh. Halafu atakuja na Dina."

"Okay. Afu' Dina kitambo! Yuko poa?" nikamuuliza hivyo.

"Ah, kwanza we' mwana si unafanya mambo siyo fresh," akaniambia hivyo.

"Nimefanyaje tena?"

"Mpaka leo mwanangu hujaenda kumwona Dina... wakati ulimpaga promise kabisa, mwenzio akaiweka moyoni..."

"Ah, ahahahah... dah!" nikajikuta nachoka.

"Ananicheki sana kaka, kila mara lazima JC uuliziwe. Sema, huwa tu nasahau, inabidi nikupe namba yake ili ndo' upate motisha zaidi. Unamtesa mtoto wa watu," akasema hivyo.

"Ah, basi unadhani shida ni namba Tesha?"

"Ee, ni namba. Hauchukulii serious maana huna contact zake kabisa... mpaka mwezi umepita."

"Hamna bro, hiyo siyo shida. Shida ni muda. Mambo yanakuwa mengi. Hivi... unamkumbuka yule mwanamke mwislamu ambaye... tulikutana naye kwenye daladala ile siku tunaenda Kigamboni, alikuwa na kale kadem keupe ulikokuwa unataka namba yake?" nikamuuliza.

"Eeh, afu' kweli, dah! Kitambo! Ulizipata?"

"Hamna, lakini si nilizichukua za yule mama yake?"

"Ee. Mnawasiliana? Ushapiga?"

"Ndo' hicho nachotaka kukwambia. Toka hiyo siku tunawasiliana, ananielewa, anataka show... lakini mpaka sasa hivi hatujawahi kukutana tena. Kwo' ishu siyo mawasiliano, ni muda tu," nikamwambia hivyo.

"Ah, mwanangu una raha wewe! Kumbe maza mtu akakukubali?"

Nikacheka kidogo.

"Afu' dili si lilikuwa umpate kisha uniletee namba za mtoto wake yule? Ulizipata sasa?"

"Aa wapi, we' mwenyewe si ulikuwa umeshasahau? Ndo' imeisha hiyo..."

"Unazingua. Kwani shi'ngapi kukutana tena Kigamboni na huyo maza? Kwanza uliwahi kumwona uso wake kabisa?"

"Tunaongeaga video call, anavua zile mask zao."

"Anaitwa nani?"

"Ibtisam."

"Mzuri?"

"Mzuri ee. Mwarabu."

"Dah, sa' unafeli wapi?"

"Yaani wewe Tesha wewe... ahah. Wewe umetoka tu sasa hivi kuniambia simtendei Dina haki, halafu kidogo tu na Ibtisam ushaanza kumwakilisha. Kwa nini hauna msimamo?" nikamuuliza.

Akacheka na kusema, "Ndo' nilivyo. Kama raha za UKIMWI zinakutaka wewe tu, lazima nikusapoti ili ulazwe pema peponi, kamanda! Mapema..."

"Ahahahah... endelea kuota. Au ndo' kusema Dina anao sasa?"

"Hamna. Dina yuko clean kama sahani nyeupee..."

"Unajuaje?"

"Najua tu. We' ngoja nikupe namba yake, umtafute tu ajisikie vizuri... ile kwamba wewe ndiyo umemtafuta yeye. Atafurahi sana. Tena na kesho akija mkaonana, fresh zaidi," akasema hivyo.

"Haya, nipe. Sifagilii wenye umri mdogo, ila ilete," nikasema hivyo.

"We' si unapenda mashangazi tu, badala utafute viembe bado vibichii unakalia hayo madude yaliyoiva mpaka yanatepeta byeee..." akaniambia hivyo, nasi kwa pamoja tukacheka kidogo.

Akanipatia namba za huyo Dina, nami nikazitunza na kumwambia ningemtafuta baadaye.

Ikawa ni kwenda huko ndani kuwasalimu wakina Bi Jamila na Bi Zawadi baada ya kuongea hivyo kidogo na Tesha, pamoja na Mariam pia ambaye ndiyo alikuwa ametoka tu kuamka kama binti ya mfalme. Nikawaaga pia dakika chache zilipopita za maongezi mafupi kuhusiana na sherehe ya bibi harusi mtarajiwa Doris, ambaye alikuwa ameanza kunijengea hamu ya kutaka kumwona bila hata ya mimi kuelewa sababu kihalisi, na baada ya hapo ndiyo nikaondoka kuelekea kwa madam Bertha.

★★

Safari ya kunipeleka huko ilichukua muda wa kama saa moja hivi kutokana na msongamano wa magari mara kwa mara, na hatimaye nikafika hoteli ya Royal Village. Huku nikiwa nakumbukia ishu yote ya jana usiku pamoja na yule Dotto, nikaelekea hadi chumbani kwa madam nikiwa nimehakikisha sikuwa na mkia wowote nyuma yangu, yaani sikufatiliwa.

Hii haikuwa kama sinema ya wamarekani ambao muda wote hutembea na bastola kiunoni ili kujilinda, hapa palikuwa Bongo, kwa hiyo ni macho pekee ndiyo yaliyotumika kuangaza huku na kule kujihakikishia usalama maana kwa sasa sikujua nani angekuwa akiniangalia zaidi. Hata ulinzi ambao ningeahidiwa na maaskari najua haukutosha kwa asilimia zote, nilipaswa kuwa na macho makali ya utambuzi wa kilichonizunguka na kujua hatua za kuchukua kuepuka mabalaa mapema.

Baada ya kufika kwenye chumba hicho, madam Bertha akawa anenifungulia mlango. Nilimwangalia kwa njia ya kawaida tu usoni, lakini yeye alikuwa akinitazama kwa upendezi na tabasamu hafifu midomoni mwake. Wakati huu alikuwa amebadilisha mwonekano wake kichwani kwa kusukia nywele za rasta nene na nyekundu, ambazo zilitengenezwa kwa njia fulani kama minyororo mirefu iliyofikia mpaka usawa wa hips zake. Na hapa alikuwa amevaa T-shirt la mikono mirefu kama sweta, lenye rangi ya kijivu, refu mno mpaka kufikia magotini, na zaidi ya hilo hakuwa amevaa kingine.

Nikamtikisia nyusi moja kiuchokozi kiasi, naye akanyoosha mikono yake yote kunielekea kama kuniita niende kumkumbatia. Nikaingia na kumkumbatia kweli, nikiwa makini kutokana na mawazo yaliyokuwa yakizunguka akilini, naye akaniachia mgongoni na kuendelea kuyashika mabega yangu huku akiniangalia usoni kwa macho yenye raha, na mie nikiendelea kukishika kiuno chake.

"Nimekumiss," akaniambia hivyo.

"Mimi, wewe?" nikamuuliza hivyo kiutani.

"Mhm... mdogo wako anaendelea vizuri?"

"Ee, anasukuma-sukuma angalau."

Bertha akanisogelea karibu zaidi usoni na kunibusu mdomoni mara mbili, kisha akaniangalia na kusema, "Mbona uko serious hivyo?"

"Hamna, kawaida tu," nikamwambia hivyo.

Akiwa anasugua-sugua mabega yangu kwa viganja vyake vyenye makucha marefu, akasema, "Hujapenda nilipokubadilishia safari ghafla eh?"

"Hapana, nimefurahi. Nilifikiri ningekuja kukuona jioni... ila now ndo' ntakuwa nawe mpaka jioni," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu kidogo na kunibusu mdomoni tena, kisha akaniachia na kusema, "Haya, funga mlango. Njoo tuongee."

Akaanza kulielekea sofa, nami nikaurudishia mlango na kumfata pia. Alikuwa akifanya utafiti fulani mtandaoni inaonekana kwenye laptop yake iliyokuwa kwenye meza hapo pembeni, nami nilipofika karibu naye, akakaa kwenye sofa huku akiuvuta mkono wangu ili nikae pamoja naye. Ikawa hivyo. Akawa amenitazama usoni sawia huku akiegamiza mwili wake kwenye egemeo la sofa, nami nikawa namwangalia kwa utulivu.

"Ulikuwa umefika wapi nilipokupigia?" akaniuliza hivyo.

"Nilikuwa... maeneo ya Kariakoo. Ndiyo nilikuwa nataka tu kupanda mwendokasi," nikamdanganya.

"Nini kilifanya ukafikiri kuna mtu alikuwa anakufatilia?"

"Sijasema hivyo, yaani... nilikuwa tu najitahidi kuwa mwangalifu..."

"Na ndo' ungefanyaje hivyo?"

"Nisingeenda Ubungo moja kwa moja. Ningepitiliza kabisa mpaka mbele huko, niangalie mazingira, halafu ndo' niende kwa spot yetu hata kwa boda... precaution tu," nikamwambia.

Akatikisa kichwa na kusema, "Sawa."

Nikaiangalia laptop yake na kumuuliza, "Ulikuwa unatafuta kitu fulani hapo?"

Akaitazama na kisha kuifunika huku akisema, "Yeah, nimemaliza. Achana nayo."

"Kwa hiyo supermarket leo sitaenda, eti? Au nitaenda baadaye?"

"Achana na ishu za kazi, HB. Nimekuita hapa tuongee... mimi na wewe," akasema hivyo.

Nikajiweka kiumakini zaidi na kushika nywele zake, kisha nikasema, "Niambie."

"Kwa hizi wiki zilizopita... umefanya kazi nzuri sana kunionyesha kwamba kweli uko serious na mimi, na najua bado sijakupa tuzo yako unayostahili," akaniambia hivyo.

Nikamwangalia kwa njia ya ufikirio.

Akasema, "Usipandishe mzuka, simaanishi nitaanza kukupa mpalange!"

"Ahahahah... huwa unawaza vitu vya ajabu madam!" nikamwambia hivyo.

"Well, great minds think alike. Hata wewe una akili ya ajabu sana. Yaani tumeanza kuuza coke yako muda mfupi tu lakini neema kubwa imeanza kushuka mikononi mwetu..." akaniambia hivyo.

"Unajiongelea wewe na nani?"

"Sisi wote. Festus hasa. Na hivi ndiyo nilivyokuwa nataka HB wangu. Umeni-impress kweli kama ulivyoahidi," akaongea kwa njia yenye hisia sana.

Nikalazimisha tabasamu na kusema, "Usiwaze. Nilikwambia chochote kwa ajili yako."

"Kweli eh?"

"Kabisa. Kila kitu nilichofanya... ni kwa sababu yako. Na kila kitu nitakachofanya, ni kwa sababu yako wewe tu," nikamwambia hivyo kwa njia ya fumbo.

Akatabasamu na kunishika usawa wa sikio, naye akasema, "Unataka niwe wako peke yako, ndiyo maana umefanya kila uwezacho mpaka kuwa hapa. Unataka nifungue moyo wangu kwako na kukuweka ndani zaidi, si ndiyo? Huu ndiyo wakati wako sasa."

Maneno hayo yalisemwa kwa njia ya hisia za kweli kabisa, yaani Bertha hakuwa akijaribu kunitania wala nini, niliona wazi kwamba alimaanisha kile ambacho alikisema. Nikaendelea kumwangalia usoni kwa umakini, huku fikira zangu zikiendelea kupingana kwelikweli na hisia zangu.

"Sidanganyi kwamba tayari nilikuwa nimeshakuelewa pia, ila ndo' sitaki tu yale yale ya Chaz yanipate tena maana nawaelewa nyinyi vizuri mno..." akasema hivyo.

"Mimi siyo..."

"Wewe siyo Charles, najua. Ndiyo maana nimeweza kufungua tena milango ya moyo wangu kwa ajili yako. Nimekukubali kwa asilimia zote JC," akasema hivyo.

Dah! Alikuwa akiongea kwa hisia yaani, sikutegemea. Haya yote yalikuwa yanatokea wapi?

"Nataka tu nikuombe... msamaha. Nisamehe kwa jinsi nilivyokuwa nakutendea mwanzoni mpaka sasa, nilikuwa sijagundua tu thamani yako. Ila sasa hivi nimeijua, sitaki inipotee kabisa. Nakuhitaji sana... uendelee kuwa upande wangu... siyo kwa sababu ya kazi tu, yaani... kama hivi... ni... najua unaelewa..."

Aliongea kwa kubabaika kiasi, akionyesha kuwa na udhaifu wa wazi mbele yangu, na tayari nilikuwa nimeshaelewa alichokuwa anajaribu kuniambia.

Nikaangalia pembeni kwanza na kusema, "Ndiyo... nimekuelewa."

"Umeelewa nini?" akauliza.

Nikamwangalia na kusema, "Kuna neno unataka kusema, lakini unashindwa kulisema."

"Ahahah... haujakosea," akaniambia hivyo.

Nikiwa makini, nikamuuliza, "Kinachokufanya ushindwe ni nini?"

"I guess... siyo mtu wa tamthilia-tamthilia mimi, hayo maneno nayaona kuwa ya kipuuzi..."

"Lakini si ndiyo ukweli wa kile unachohisi?"

"La muhimu ni kwamba umenielewa, kwa hiyo siyo lazima niyaseme."

"Sawa. Haina shida," nikamwambia hivyo.

"Haina shida? Yaani nimeongea hayo yote halafu unasema haina shida?" akauliza.

"Ee, si nimekwambia nimeelewa? Kwa hiyo poa. Haina shida. Nimekuelewa," nikamwambia hivyo.

Akanikazia macho yake.

"Ahah... mbona unaniangalia hivyo sa'?" nikamuuliza.

"Hata dakika mbili hazijaisha tayari umeshaanza kunionyesha dharau kisa tu nimekwambia...."

"Umeniambia nini?" nikamkatisha.

Akanikazia macho yake tena, naye akasema, "Kwa hiyo kumbe ni mpaka niseme?"

Nikatabasamu na kusema, "Haujasema. Mpaka useme."

Akashindwa kujizuia kutabasamu kwa hisia, naye akaniangalia kwa macho yaliyojaa upendezi na kusema, "Nakupenda."

Mh?

Nikabaki nikimwangalia kwa njia ya kawaida, kwa sababu kihalisi mwenzake hapa nilikuwa naigiza, lakini yeye alionekana kuwa mahali palipompoteza kabisa kihisia. Yaani alionyesha ile ya kufa na kuoza kabisa, na mimi hapo nikawa natafakari mambo mengi kinoma.

Kila kitu ambacho niliambiwa jana na wale wanaume kilikuwa kikizunguka kichwani, hasa vitu alivyosema Chalii. Kwa hiyo hapa asilimia kubwa ya kile ambacho akili yangu iliniambia ilikuwa kwamba mwanamke huyu alikuwa akinidanganya tu ili niendelee kulainika zaidi kwake, nimpe mafanikio zaidi, halafu mwisho wa siku ndiyo aje kuniangamiza. Tena bila sababu.

Nikashindwa hata kutoa itikio lolote la maigizo na kuendelea kumwangalia usoni kwa umakini sana, kwa sababu akili yangu ilikuwa ikinishawishi kuweka kigingi cha kutoamini kabisa maneno hayo, lakini tena ikawa kama hisia zangu zinaniambia aliyamaanisha. Na yaani ilikuwa ni kwa nini wakati huu huu tu ambao mambo yangeenda kumharibikia eti ndiyo akaanza kuleta swaga za 'nakupenda sana?'

Alipoona nimeishia kumtazama tu, akasema, "Nini wewe? Si ndiyo ulichotaka nikiseme, au? Out loud. Nimekisema."

Nikatazama pembeni tu na kushusha pumzi kama mtu aliyeishiwa raha.

"HB... vipi? Haujafurahi?" akaniuliza hivyo.

Nikamwangalia na kusema, "No, siyo hivyo. Sikutegemea tu..."

"Kwa nini? Kutokana na jinsi ulivyonizoea, yaani hauwezi kuamini kabisa eti?"

"Siyo... ahah... siyo kabisa, yaani... ni ngumu tu kidogo. Nilikuwa hadi nimeshaanza kuzoea kuwa toy wako tu," nikamwambia hivyo.

Akanishika shingoni na kuniambia, "Usiseme hivyo bwana, namaanisha nayokwambia. Umeshaniteka kihisia, mbali tu na kuwa mzuri kitandani..."

Nikatabasamu na kutikisa kichwa kiasi.

"Ona, kuanzia sasa hivi... nataka tuwe serious. Umenipigania kwa vingi, na umeshinda. Nataka nikupe unachostahili sasa. Labda ndiyo itakuwa njia nzuri ya kukuthibitishia kwamba nimekupenda pia..." akasema hivyo.

"Na ni nini hicho kitakachonithibitishia?" nikamuuliza.

Akatabasamu na kusema, "Nataka kuzaa na wewe."

Nikamtazama kimaswali kiasi, na kwa sauti ya chini nikasema, "Nini?"

"Yes. Nataka kukuzalia JC. Niko tayari kuwa mama wa mtoto wako," akaniambia hivyo.

Raa!

Nikabaki nikimtazama machoni kwa umakini sana utadhani alikuwa amenipiga kwa kitu kizito kupita uzito wenyewe. Nilishindwa kuelewa ikiwa mpaka kufikia hapa mwanamke huyu bado alikuwa akicheza na mimi, ama ilikuwa vipi. Huyu alikuwa Bertha, ama nilikuwa naota?




★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
Good
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KWANZA

★★★★★★★★★★★★★★


Wiki nne zikawa zimepita baada ya mambo yale yote kutokea. Ndiyo. Mwezi mzima. Najua, najua... JC natakiwa nielezee yaliyotokea ndani ya huo muda wote, nimekoswa sana naambiwa, na kiukweli ni mengi mno yaliyokuwa yametokea mpaka kufikia sasa. Mengi yenye kuridhisha, na baadhi yenye kukwaza kwa kiasi fulani.

Tuanze na Joshua. Mwanaume huyo, baada ya kuwa amemfanyia binti Mariam vitendo vya kinyama kwa kujaribu kumuua zaidi ya mara moja na kutunga hila kibao ili tu aitaifishe mali ya binti, alikuwa amepelekwa mahakamani kwa kufunguliwa kesi ya makosa mbalimbali ya jinai.

Ndani ya huu mwezi ulioisha yaani, alifikishwa mahakamani zaidi ya mara tatu kujibu mashtaka ya hila za udhulumaji, au uporaji mali kwa kutumia hati bandia za kimahakama, vitendo vya kijeuri kama vile kupanga mauaji, na pia kuna mtu mwingine akawa ameongezea ishu ya kumkodisha gari jamaa na kuahidiwa malipo, lakini hakulipwa na badala yake gari lilirudishwa likiwa limeharibika.

Kesi zake mbili za kupanga mauaji na wizi hasa ndiyo ambazo zilikuwa nzito kwa huyu Joshua, ushahidi ukiwepo wa kuridhisha kabisa, naye akawa amepewa adhabu ya kwenda kutumikia kifungo cha miaka kumi jela. Siyo mchezo! Mvua ya miaka kumi!

Waliokuwepo sanasana kwenye mahudhurio ya kesi ya jamaa ilikuwa ni mimi mwenyewe, askari Ramadhan na mwandamani wake, Tesha, Khadija, Yohana wa Kleptomaniax, Bi Zawadi mara mbili, na Miryam pia mara moja; kwenye siku ambayo jamaa ndiyo alipewa hukumu. Ushahidi alioutoa huyo Khadija na Tesha kwenye suala la yeye Tesha kutekwa pamoja na mdogo wake ili wauawe, ulikuwa nyundo nzito sana ya kuupigilia ndani zaidi msumari wa hukumu ya haki aliyopewa jamaa. Huko ndiyo angeenda kulia na kusaga mipira yake vizuri!

Tulihakikisha haya yote hayamfikii binti Mariam kwa muda wote yalipoendelea mpaka kumalizika, na ilionekana kwamba familia yake iliridhishwa mno na hukumu aliyopewa huyo Joshua. Alistahili hata cha maisha kabisa, ila kuna vitu vitu tu vilipunguzwa, hadi nilishangaa kiasi kwamba Khadija hakula hata miaka miwili kwa sababu ya kusindikiza uhalifu ilhali wenzake wote, wale wakina Yohana wa Kleptomaniax, wote walikula mvua za miaka mitano mpaka saba jela kwa kusindikiza maovu ya Joshua. Hakukuwa na neno, la muhimu likawa kwamba mbaya wa amani ya familia yake Mariam alikuwa amewekwa mbali hatimaye.

Tukija upande wa madam Bertha sasa, mambo kweli yalikuwa 'underway' kama msemo wake. Yaani ndani ya hizi wiki tatu za mwisho zilizokuwa zimekata, tayari alikuwa ameshanionyesha sehemu ambayo biashara yake ya kutengenezea cocaine ingefanyikia, na kupitia mimi, tayari unga ulikuwa umeshaanza kutengenezwa, kuongezwa, na sasa ulikuwa kwenye harakati za kusambazwa.

Mwanzoni ilibidi kutoa kiasi fulani kama kionjo, kidogo-kidogo, kisambazwe hapa na kule ili watumiaji waelewe kulikuwa na zigo jipya jijini, na wanajeshi wake waliofanya kazi ya usambazaji wangetangaza pia bei mpya ya kuyapata madawa hayo yaliyokuwa yameanza kushika kasi mpya kwenye soko hilo jijini.

Kufikia wakati huu, tayari nilikuwa nimeshaona na kusoma njia zao kuu za kufanya usambazaji wa kisiri, na kiukweli zilikuwa njia ambazo sikutegemea mwanzoni, ila walikuwa wanatumia akili sana. Madawa yao yalipita sehemu na maeneo yenye hadhi za juu, mashuleni, vyuoni, mpaka kwenye makampuni, na haikuwa rahisi kwa yeyote ambaye hakuwa ndani ya hili game la uuzaji kujua jinsi ambavyo ishu hiyo iliendeshwa.

Kwa muda wote huo, nilikuwa nimejitahidi sana kumwonyesha madam Bertha kwamba nilikuwa makini na kazi aliyotaka tuifanye, na alinifurahia mno. Hadi wale wanaume ambao tulienda kukutana nao African Princess casino siku ile walisifia sana kazi yetu mpya, kwa hiyo kuna mara ambazo tungekutana, na wao kujiachia sana mbele ya ushirika wangu.

Lakini hawakujua kwamba kwa muda huo wote, mimi nilikuwa nafanya kazi na askari mpelelezi Ramadhan, na uamuzi wa kusubiria kwanza kabla ya kuchukua hatua dhidi ya watu hawa ulikuwa ni wake. Haikuwa tena juu ya suala la mauaji ya Joy tu, la. Sasa hivi kwa sababu mambo mengi yalikuwa yanaongezeka, ingebidi tuwe na kila kitu tulichohitaji ili yeye askari Ramadhan na wenzake wakipiga tu hatua kuwaweka chini ya ulinzi watu wote wa Bertha, iwe ni moja kwa moja. Yaani kusiwepo na njia ya kurudi nyuma tena.

Ila kama ni kitu kilichokuwa kikinifanya nikune kichwa changu bado ilikuwa ni kutojua nitumie njia ipi ili kumkamatisha na Festo pia. Aisee, yule jamaa sikumwelewa. Yaani, alikuwepo, lakini ilikuwa kama vile hayupo. Ningemwona tu alipotaka nimwone, lakini nisingeweza kujua alifanya mambo yake kwa njia zipi. Hawa wengine walikuwa wepesi kufunguka kwa mambo mengi na hivyo ilikuwa rahisi kuwa na vitu na sehemu za kuwakamatia, lakini Festo? Hapana.

Nilitakiwa kupata kitu cha kumnasia huyo jamaa, hasa kwa kuwa bado aliendelea kumfatilia bibie Miryam akimtaka kimapenzi. Mwanamke huyo hakuonyesha utayari wa kuwa ndani ya mahusiano ya kimapenzi kwa kipindi hiki kwa kuwa kweli fikira zake zote zilielekezwa kwa Mariam. Karibia mara zote ambazo nilienda pale kwake na kuwa pamoja na mdogo wake, Miryam alikuwepo, na alijitahidi sana kuniunga mkono kwa kila jambo nililofanya ili binti Mariam aweze kukaa sawa tena.

Wiki hizi nne za kuendelea kumsaidia Mariam zilihusisha lile suala la kumpeleka hospitali kwa ajili ya vipimo, na shukrani kwa Mola tukawa tumepata uhakika kuwa binti hakuingiwa vibaya kimwili, na hivyo alikuwa safi na salama kabisa. Hatukumwambia hilo, wala kuongelea waziwazi mbele yake mambo yaliyotokea usiku ule alipotekwa, na kadiri mazoezi ya kuuimarisha utimamu wake yalivyoendelea, ndiyo akawa anaendelea kufunguka kiutambuzi.

Mwezi mmoja tu ukatosha kumfanya Mariam aanze kuzungumza kama ilivyokuwa awali, hata nyakati nyingine angewaita watoto wa hapo mtaani ili acheze pamoja nao ndani ya geti la nyumba yao. Alionyesha tabia za kitoto bado, lakini haikuwa kwa jinsi niliyokuwa nimemkuta mwanzoni kabisa. Wote tulijitahidi sana kumfanya afurahie maisha yake, na kilichokuwa kimebaki ikawa ni kumjuza kutambua tena yeye ni nani, na angepaswa kuwa nani kwenye maisha yake kwa mapenzi na uchaguzi wowote alioutamani.

Chalii Gonga, mume halali wa madam Bertha, alikuwepo bado katika shughuli za biashara ambazo mke wake alimwachia, na mara kwa mara tungeonana pale Masai nyakati ambazo ningeenda na Tesha pamoja na Ankia. Mara hizo zote tulizokutana, hatukusemeshana, na alifanya iwe wazi kwamba hakutaka kunisogelea kabisa kwa sababu nafikiri kuna kitu ambacho Bertha alikuwa amefanya ili kuleta hali hiyo.

Sikuwahi kumuuliza tena mwanamke yule kama kuna jambo lolote lilitokea baina yake na Chalii hasa baada ya jamaa kunikuta kwenye chumba cha hoteli ya madam siku ile, maana ndani ya hizo wiki chache nilikuwa nimekutana kimwili na huyo mwanamke karibia mara tano, lakini hakutaka kumzungumzia mume wake kwa undani, na mimi nisingeweza kumsukuma.

Ila hali hii baina yangu na Chalii Gonga ilinionyesha wazi kwamba jamaa alikuwa amenyamazishwa. Lakini yote kwa yote, bado niliendelea kujitahidi kuwa makini sana mara zote ambazo ningemwona, kuepusha tu matatizo kwa upande wangu, yaani ya moja kwa moja, maana bado kuna hisia iliyokuwa ikiniambia kwamba mwanaume huyo alipanga kitu fulani. Kuwa chonjo ilikuwa lazima.

Na tukija upande wa familia yangu, haikuonekana kuwa na tatizo lolote tena upande wa mzee wangu, Mr. Frank Manyanza, tokea nilipokwenda kwenye ofisi yake kumwelezea vizuri kuhusiana na ishu ya Joshua kuihujumu familia yake ili aliuze shamba. Hakunitafuta kabisa kuongelea hilo suala tena mpaka Joshua amefungwa jela, na mimi nikachukulia kwamba mambo yalikwenda poa.

Nilikuwa nimeshafanya safari fupi ya kuwatembelea mama na dada yangu na kuwasalimia pia, na tuliweza kuongelea mambo mengi sana na mama kuhusiana na maisha yangu, nikimwambia tu kuna vitu vya huku ningekuja kushughulika navyo nikishatoka likizo, na nikamtia moyo Jasmine asonge mbele kutoka kwa mwanaume yule ambaye hakujali hali yake.

Mwanaume wake hakuwa mtu mwelewa, na alitoa maneno machafu sana hata alipokorofishana kidogo tu na Jasmine, na mimi nikawa nimemshauri tu dada yangu aachane na mtu ambaye hakumpa heshima, kwa kuwa bila hicho upendo ungetoka wapi sasa? Akawa ameniahidi kuwa angesonga mbele, na mimi nikamwahidi kuja kumjulia hali hapo kwetu kwa mara nyingine kabla ya wakati wake kujifungua kuwadia.

Kwa hiyo kwa ujumla ikawa ni kwamba kwenye suala la Joshua nilipata ushindi, masuala ya Mariam na Bertha ndiyo yakawa kwenye kalenda bado za kutarajia ushindi, lakini huyo Festo ndiyo bado akawa kikwazo. Ila nisingekata tamaa. Zamu hii sikutaka kumwambia bibie Miryam, oh kuna hiki, au kuna kile, hapana. Nilitaka nije nifichue kila kitu kwa vitendo tu. Na najua angekuja kushangaa mno baada ya kugundua rangi halisi ya yule mwanaume.

Nilikuwa nimewasihi watu wa familia yake Miryam wasije kuzungumza na watu wa nje kuhusiana na ishu yote ya Joshua, na waliafikiana na hilo, lakini lengo langu hasa lilikuwa kuhakikisha habari za mimi kushirikiana na polisi mpaka kumkamata Joshua hazifiki kwa Festo; maana ingemwashia taa nyekundu ya hatari na hivyo kumfanya aanze kunifatilia zaidi.

Ni huyu jamaa tu ndiyo aliyekuwa mwiba mgumu sana kwangu uliobaki kung'oa, na nilitaka kuhakikisha namwondoa pia maishani mwake Miryam kabla ya matatizo mengine kujitokeza....


★★★


Basi bwana, hivyo ndivyo mambo yalivyokuwa. Mpaka kufikia sasa bado nilikuwa kwa Ankia, tukiendeleza maisha yetu ya mama mwenye nyumba na mpangaji wake, na urafiki wetu ulizidi kukua. Hiyo hasa ilitokana na kujuana naye kwa mengi zaidi ya story na msosi wake mtamu tu, ikiwa unaelewa namaanisha nini. Kufikia sasa mwanamke huyu alikuwa amefungua biashara nzuri sana ya duka, alipouzia vijora, suruali za wanawake, pamoja na nguo za watoto wa kike, watoto wadogo yaani, hapo hapo Mzinga maeneo ya barabarani kwenye shughuli nyingi.

Kwa hiyo kutokana na kazi yake, tungeonana kwa mida iliyoachana-achana sana, hasa jioni, usiku, au asubuhi tu. Ratiba yangu ya kutoka kwenda kwenye ishu ya madam Bertha ilikuwa kwa siku za Jumatatu, Jumatano, na Ijumaa, kuanzia asubuhi mida ya saa nne mpaka jioni. Mwanzoni ilikuwa na ulazima sana kukaa huko mpaka jioni, lakini kwa wakati huu, ningeweza hata kuondoka mapema maana wengi wa vijana wake walielewa namna ya kuunda yale madini. Sema tu ndiyo niliwekwa kama msimamizi eti!

Hivyo, nilikuwa na muda na siku za kutosha kukaa na binti Mariam na kuendelea na tiba yake. Kwa kipindi hiki, Tesha alikuwa anahangaikia zaidi kupata kazi nzuri ambayo ingemfaa, lakini hakuwa amepata kwa hiyo aliendelea kutulia huku akipata michongo ya hapa na pale mara kwa mara iliyomwingizia pesa ya matumizi yake binafsi ama kusaidia familia pia akiwa kama mwanaume. Hali kwa familia yake ilikuwa tulivu zaidi kwa wakati huu, na nilitamani sana iendelee kubaki namna hiyo hiyo bila drama nyingi kama zile za wiki kadhaa nyuma kutokea.

Sasa, leo ilikuwa ni siku ya Alhamisi, asubuhi na mapema kabisa. Kulikuwa na ishu ya maana sana kwa mrembo wangu iliyonihitaji, cheupe mwenyewe Bi Zawadi. Mwanamke huyo alikuwa na mpango wa kwenda sehemu fulani iliyoitwa Chamgando, ukiwa unaelekea Kisemvule kule sijawahi hata kufika, akiwa na lengo la kumwona mtumishi fulani wa kanisa la kilokole huko kwa ajili ya maombi "spesho" ambayo husafisha mabalaa yake, na kwa niaba ya familia yake.

Ingekuwa kama kwenda kwa Mwamposa tu lakini alikuwa anamjua vizuri sana mtumishi wa huko Chamgando, akisema ni mzuri sana, ana maono, nakwambia yaani dah! Ndiyo nikawa nimepata na huo mwaliko sasa wa kumsindikiza, na mimi ningefanyaje? Nisingeweza kumkatalia mrembo wangu. Ni kitu ambacho alikuwa ameshakililia kwa wiki chache sasa lakini kutokana na mambo ya hapa na pale nikawa sijaweza kuambatana naye, sanasana alikuwa akienda na Tesha kwa nafasi za Jumapili, hivyo leo ningeenda pamoja naye. Ahadi ni deni kama ujuavyo.

Kwa hiyo nilikuwa nimeamka mapema sana, nikajiandaa vizuri na kuvalia T-shirt langu jeupe la mikono mifupi, suruali nyeusi ya jeans, na kiatu cheusi kinachong'aa chenye muundo wa kiatu cha ballet, hutu ambato wakorea walitufanya tukawa fashion kwa kuvalia bila soksi na suruali ya kitambaa ikiwa imevaliwa kama njiwa. Nilikuwa nimetununua wiki moja nyuma, na sasa ndiyo ikawa mara ya kwanza kuvitumia.

Hii ikiwa ni mida ya saa mbili asubuhi sasa, nikatoka zangu na kuagana na Ankia, akiwa ananiambia mwonekano wangu ndiyo ungefanya watu wafikiri mimi ni mchina kweli, akisema nimependeza, nami nikamshukuru na kumwambia tungeonana baadaye. Nikatoka ndani hapo na kuanza kuelekea nje.

Nikiwa usawa wa ukuta uliotenganisha nyumba hizi mbili, nikamwona bibie Miryam akiwa anapiga deki sehemu ya kibaraza chao kutokea kule ndani, ikiwa wazi hakuwa ameenda kazini bado, nami nikaelekea nje mpaka kufikia getini kwao. Mvua zilikuwa zikinyesha mara kwa mara hasa mwezi huu ulipoingia, na jana pia ilinyesha kwa hiyo ardhi ilikuwa mbichi.

Nikaufungua mlango mdogo wa geti la nyumba yao majirani zetu kwa kuvuta kikamba nilichokuwa nimemsaidia Tesha kuweka siku ile, na nafikiri leo ndiyo ningekuwa mgeni wa kwanza kufika hapo ingawa hawa watu walinichukulia kuwa kama mwenyeji wao tayari.

Ile tu ndiyo nimeingia, nikamwona Miryam akijinyanyua na kusimama kutoka kwenye kuinama kwake kupiga deki, na baada tu ya kuniona pia, akaachia tabasamu la furaha lililofanya sura yake ipendeze sana. Mimi pia nikatabasamu na kujikuta nimeendelea tu kumtazama kwa furaha pia.

Alikuwa amevaa T-shirt nyeusi ya mikono mifupi, huku kutokea kiunoni akijifunga kwa khanga safi lakini niliweza kuona kwamba ilificha suruali laini nyeusi, labda skinny, aliyokuwa amevaa kwa ndani na kuivuta juu kiasi miguuni. Nywele zake laini na ndefu alikuwa amezibana juu ya kichwa chake, na weupe wake uliomulikwa kwa jua la asubuhi ulimfanya aonekane kung'aa mikononi kutokana na umaji iliyokuwa nayo.

"Karibu."

Akaniambia hivyo kwa sauti yake tamu sana. Na ndiyo iliyokuwa moja ya sauti za kwanza nilizohitaji kusikia kwa asubuhi hii!

Nikasema, "Asante," kisha ndiyo nikarudishia mlango wa geti na kuanza kuelekea hapo kibarazani, nikilipita gari lake huku nalipiga-piga kidogo kwa kiganja.

Akawa ananitazama kwa yale macho ya 'nakuona,' kisha akasema, "Mzee wa kung'aa!"

Nikatabasamu kidogo na kuinua viganja vyangu huku nikijiangalia kwa majivuno, nami nikamwambia, "Kama kawaida yangu."

Akacheka kidogo kwa pumzi.

"Naona unapiga usafi," nikamwambia hivyo.

"Yeah. Kama kawaida yangu," akasema hivyo pia.

Nikatabasamu kidogo huku nikiangalia ulowani wake wa jasho uliofanya nywele zake zilainike.

"Mamu bado hajaamka," akaniambia.

"Ah, hamna shida... Mamu tutaonana baadaye. Nimekuja kumpitia cheupe wangu," nikamwambia hivyo.

"Ahaa... ee kweli ameniambia... unamsindikiza kwa mtumishi, si ndiyo?" akasema hivyo.

"Mm-hmm," nikakubali.

"Ahah... alivyo na hamu ya kwenda nawe! Kama vile mnaenda date," akatania.

"Ahahah... usipime! Ila nina hamu pia ya kwenda, maana... sikumbuki mara ya mwisho nimeenda kanisani ilikuwa lini. Ndo' nafasi ya kuanza kumrudia Mzee wa Siku physically hii," nikamwambia.

"Wewe pia unataka kuponywa?" akauliza.

"Eeh, kama itawezekana... fresh. Siyo kwamba naumwa au nini, ila... najua ibada ni muhimu haijalishi dini ni ipi. Biblia inasema pale ambapo kuna roho ya Mungu watu wake wanapaswa kukusanyika pia, kwa hiyo kuwa na sehemu za ibada ni lazima ili kuwakusanya watu wamwabudu na kumsifu... na kuwaombea wengine," nikamwambia hayo.

"Wacha! Kumbe na Biblia unasomaga?" akauliza.

"Huwa nasoma kila nikipata nafasi, nina app kwenye simu. Mistari miwili, mitano, natafakari, namshukuru Mungu. Angalau kale ka-touch na muumba kanakuwepo bado... ndiyo maana ananifanya nazidi kuwa handsome," nikamwambia hivyo.

Miryam akacheka na kuinamisha uso wake, yaani kile kicheko laini cha kutoka moyoni. Alionekana kufurahi sana.

"Hahah... au nadanganya?" nikamuuliza.

Akaniangalia na kusema, "Hamna... ahahah... ni kweli kabisa."

"Sa' mbona unanicheka?" nikamuuliza huku nikitabasamu kiasi.

"A-ah... ahahah... siyo hivyo, yaani... unaongea kama Tesha," akasema hivyo.

"Ahah... eeh, akili zetu zinafanana ndiyo maana tunapatana," nikasema hivyo.

"Kweli. Ila... naona kama we' umemzidi kidogo. Atakuwa anachukua madarasa kutoka kwako," akasema hivyo.

Nikacheka kwa furaha kiasi, naye akacheka pia, kisha kwa sekunde chache tukabaki kuangaliana machoni huku tukitabasamu. Ulikuwa utizami wa uliojaa upendezi mwingi sana, sote tukiwa tunafurahia hali hii mpya ya urafiki baina yetu, naye Miryam akaibana midomo yake kiasi na kutazama pembeni, kitu ambacho kikanifanya mimi pia niache kumwangalia usoni na kushusha macho yangu kuelekea chini.

Ndipo akaniangalia na kusema, "Karibu mwaya. Karibu ndani... ma' mkubwa atakuwa anamalizia kujiandaa."

Nikawa nimemwangalia na kusema, "Sawa. Inabidi nivue viatu ili nisikuchafulie...."

"Hamna shida, pita tu," akanikatisha kwa kusema hivyo.

"A-ah, hamna bwana. Kuvua viatu lazima," nikasema hivyo na kusogea pembeni huku nikianza kuvua kiatu.

Akawa anatabasamu na kusema, "Kumbe na we' unajali usafi eeh..."

"Uhakika. Hiyo ishu naielewa inavyochosha. Mama alipokuwaga akipiga deki halafu sisi tupite tu na miguu yetu, wee! Tungeinama kudeki nyumba yote," nikamwambia hivyo.

"Ahahah... hata kama hamjachafua kwingine?" akauliza.

"Yaani kote! Lilikuwa somo zuri ili tusirudie tena," nikamwambia nikiwa nimemaliza kuvua viatu vyote.

"Aliwapatia. Haya, ingia ndani. Me namalizia hapa," akasema hivyo.

"Sawa," nikamjibu.

Akainama tena na kushika dekio, nami nikawa namwangalia tu kwa utulivu, kisha ndiyo nikaingia ndani hapo na kurudishia mlango.

Nilijihisi vizuri sana kuwa na hako kawakati pamoja na huyo mwanamke, yaani ile hali nzuri ya kirafiki tuliyokuwa nayo sasa ilinipa amani sana na kujenga hamu ya kutaka kuendelea kuukuza na kuukuza tu huo urafiki. Ni mengi tuliyokuwa tumepitia na huyu dada mpaka kufikia hatua hii ambayo mwanzoni nilidhani isingekuwa rahisi kufikiwa, kwa hiyo niliithamini sana.

Hakukuwa na mtu hapo sebuleni, nami nikasogea mpaka sehemu ya dining na kumwona Bi Jamila akiwa anatengeneza chai pale jikoni kwao. Na ilikuwa mapema kweli, kwa hiyo nikawaza labda hata ilikuwa ni uji. Nikaelekea mpaka upande huo wa jikoni na kumsalimu, naye akaniitikia vizuri sana huku akinikaribisha kupika. Alikuwa akitengeneza dawa ya kuchemsha, kwa ajili yake mwenyewe, kisha ndiyo angeandaa na chai pia.

Kwa kuelewa kwamba nilikuja kumpitia mwenzake, akawa ameniambia ndiyo sasa hivi tu Bi Zawadi alikuwa ameingia chumbani ili kuvaa, na kweli nikasikia sauti ya mrembo cheupe wangu kutokea chumbani ikinisemesha, JC bwana karibu, sichelewi, natoka sasa hivi tunaenda. Nikamwambia atumie muda wote aliohitaji kumaliza kujiandaa, nami nikaendelea kusimama pembeni yake Bi Jamila na kuongelea dawa hiyo aliyokuwa akichemsha.

Baada ya dakika chache tu, Miryam akawa amerejea ndani kwa kilichoonekana kuwa amemaliza kupiga deki, naye akaelekea chumbani kwake huko. Nilikuwa nikitamani sana yaani katukio kokote kale kajiunde tu ili arudi huku na niweze kumsemesha tena, basi tu ilikuwa imeshajijenga ndani yangu kutaka kumwangalia kwa ukaribu au kunena naye mara kwa mara.

Sifichi kuwa upendezi wangu kumwelekea mwanamke huyo ulikuwa mkubwa zaidi kwa wakati huu, lakini najua nilitakiwa kuendelea kuheshimu uhusiano wetu wa udada na ukaka tuliokuwa tumejenga, na hivyo kunizuia kuvuka mipaka kimawazo kumwelekea. Kama unaelewa namaanisha nini.

Bi Zawadi akawa ametoka hatimaye, akipendezea kwa kuvaa nguo nzuri sana ya kitenge na kuzibana nywele zake za kusukwa kwa juu, huku akishikilia mkoba mdogo ambao alisema ulikuwa maalumu kwa ajili ya kuwekea Biblia. Nikamsifia kwa kudamshi, mwenyewe akipenda kweli kujua alionekana vizuri, nasi tukiwa tayari kuondoka sasa ndiyo Miryam akawa amerejea sehemu hii ya sebule. Akatuaga vizuri pia, na ilikuwa ni yeye na Bi Jamila pekee ndiyo waliokuwa macho kutuaga, Tesha na Mariam bado walikuwa wanavuta mashuka yao huko vitandani.

Kulikuwa na ishu ya kupangilia mambo yaliyohitajika kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya kuzaliwa ya Bi Zawadi, ambayo sasa ilikuwa karibu zaidi kufika, na ndiyo Miryam akamwambia mama yake mkubwa kwamba wangekuja kuongelea mambo yaliyohitaji kumaliziwa tukisharudi baadaye. Inaonekana bibie asingekwenda kazini leo, kwa hiyo hapo ndiyo tukaachana nao, kisha Bi Zawadi na mie kuingia mwendoni kulifata jumba la ibada.

★★

Tulichukua daladala za kwenda Kisemvule, tukapita maeneo kadhaa mpaka kufikia sehemu fulani ambayo tulishuka na kupanda daladala nyingine tena iliyoelekea Chamgando. Watu wengi walikuwa wakitutazama sana mimi na Bi Zawadi, na mwanamke huyu alikuwa mwenye story zenye ucheshi sana; akigusia mara nyingi sana suala hilo la mie kutazamwa mno.

Alitaka kujua ikiwa labda nilikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanamke mmoja ama ikiwa na mimi sikuwa nimetulia kama Tesha, nami nikamwambia sikuwa na mtu kabisa. Aliona kwamba nampiga fix tu kwa sababu alikisia labda hata nilikuwa nimeshatoka na wanawake kama Ankia na wengine ambao hakuwajua, na kauli zake zilinifanya nicheke sana lakini kweli nikampiga fix kwa kusema sikuwa wa namna hiyo. Nilitulia kabisa.

Akanipongeza na kusema natakiwa kujitahidi sana kubaki safi maana magonjwa yalikuwa mengi mno, na huku tulikokuwa tunaenda ndiyo ningepata kujua mengi kuhusu maisha yangu na jinsi ya kuyaendesha ili yafanikiwe zaidi. Aliifanya hali hii ionekane kama tulikuwa tunaenda kwa mganga yaani, na tulipofikia hilo eneo la Chamgando kweli ikaonekana kama vile tulikuwa tunaenda kwa mganga.

Ilikuwa ni sehemu ambayo haijaendelea kivile, yaani utafikiri tulikuwa tumekuja kijijini kabisa. Watu waliotuona walitusindikiza kwa macho toka tumeshuka garini mpaka kuingia kwenye kijia kilichoelekea ndani zaidi ya eneo lenye uoto mwingi wa asili na miti mingi ya minazi. Ndiyo tukawa tumeifikia nyumba ndogo iliyojengwa kwa mbao sanasana na kufunikwa na Maturubai na mapazia mekundu na ya zambarau, huku kukiwa michoro ya msalaba mweupe hapa na kule. Lilikuwa ni kanisa chipukizi.

Nikamuuliza Bi Zawadi alipajuaje huku kote, naye akaniambia mke wa mwenye hili kanisa aliwahi kuishi Mzinga, na walijuana hasa kipindi ambacho wazazi wao akina Miryam walipoteza maisha yao. Akasema kwamba mchungaji alikuwa mzuri sana na upako wake, lakini hapa tulikuwa tumekuja kuonana na mama mchungaji kwa kuwa ni yeye ndiye aliyekuwa na maono, na alitoa maneno ya ushauri na saha fulani hivi lakini kwa njia ya upako. Dah!

Nikasema haina noma, nasi tukaifikia nyumba hii takati... taka... takatifu ya ibada. Kulikuwa na mwanamke aliyebeba mtoto mgongoni hapo nje, akionekana kuwa mtunzaji wa kanisa sijui, naye akatufata na kutusalimu kwa heshima. Yaani sana, kiasi kwamba alipiga magoti mpaka chini alipokuwa ameushika mkono wangu, nami kiukweli nilijisikia uajabu kiasi. Lakini tukaingia ndani kwa pamoja baada ya mwanamke huyo kutuongoza mpaka kufikia viti vya plastiki, nasi tukakaa.

Mwanamke huyo akatuambia mama mchungaji alikuwa anakuja sasa hivi tu, uzuri Bi Zawadi alikuwa ameshawasiliana naye pia, na hakuishi mbali na kanisa. Kwa hiyo dakika chache za kumsubiria zikatumiwa vyema na Bi Zawadi kunielewesha mambo yalivyo kwa sehemu hii. Ilikuwa ni sehemu ya kawaida tu, ya mwanzo, hata sakafu ilikuwa ya michanga na kinara cha mbao iliyofunikwa kwa kitambaa chenye msalaba uliochorwa kwa chaki. Naelezea mengi ndiyo ili uone nilichokiona, yoh!

Basi, mama mchungaji akawa amefika hatimaye, akiwa ni mmama ambaye hakuwa mbali sana kiumri kumfikia hata mama yangu mzazi, arobaini ya mwishoni, naye akanikaribisha vizuri sana. Leo haikuwa siku ya ibada ya pamoja, bali kama tu maombi spesho ya mtu mmoja mmoja, na Bi Zawadi akawa amemwambia kwamba mimi ndiyo "yule kijana" aliyemsema ambaye alikuwa kama baraka kubwa sana kwenye maisha ya familia yake, na alinileta ili kunisaidia nitakasiwe maisha yangu maradufu zaidi na mwenyezi Mungu.

Mwanamke huyo, mama mchungaji yaani, aliniangalia kwa umakini sana kama vile ananisoma, nami nikawa nimebunda tu kama vile sielewi somo. Kisha akaanza ghafla tu kusema kwamba anayaona maisha yangu, anajua nimetoka kwenye mazingira magumu sana lakini ni kama vile maisha yangu yote yaliongozwa na bahati kunifanya nitoke sehemu mbaya mpaka kufikia sehemu nzuri, na bado ilikuwa kwa kupambana sana.

Akasema nina moyo mzuri mno, lakini kuna kitu fulani ambacho kilikuwa kinaihangaisha nafsi yangu na hivyo nilikuwa najaribu sana kukiepuka kwa kujifanya kama sijali, ila kutoka ndani ya moyo wangu nilikuwa najali sana.

Mh? Alinifanya nimwangalie kwa mkazo zaidi, kwa kuwa sikatai, kuna vitu kweli nilikuwa najitahidi sana kuviepuka maishani mwangu kwa sababu zangu mwenyewe, lakini sikudhani mwanamke huyu angeweza kujua ni mambo gani. Labda aliotea tu. Ndipo akasema niache kuwaza kwamba kuliepuka jambo hilo kutanifanya niridhike, badala yake ifike wakati nitambue kwamba hilo ndiyo litakuwa chanzo kikubwa sana cha furaha ya kweli ambayo ninaitafuta. Dah!

Sawa aliongea kimafumbo fulani hivi, ile kwamba ni yangu tu mimi kujua, na kiukweli alinifanya niguswe sana kwa kuwa maneno hayo yaligusa sehemu fulani kubwa sana ya maisha yangu ambayo nilikuwa nimeiweka pembeni mno. Mbali sana yaani. Na hapa akawa amenifanya niitafakari, kitu ambacho kikanikosesha amani kiasi.

Sijui ilikuwa ni upako kweli, ama huyu mwanamke alijua tu kusoma nyota? Kwa vyovyote vile, akanishauri nianze kuamini kwamba Mungu yupo pamoja nami, na angenipatia zawadi nzuri sana kwa mambo mengi mazuri niliyokuwa nayafanya, lakini hilo jambo aliloniambia naepuka ndiyo lingenikamilishia furaha niliyoihitaji.

Mi' bwana nikakubali, amen kama zote, kisha mama akaanza maombi. Tukasimama kabisa, mzee nikaombewa yaani, maneno yaliyosemwa yalinigusa sana mpaka nikajihisi kutaka kulia. Sikutegemea kabisa hali iwe namna hiyo, lakini nashukuru tu mabomu ya 'fire' yaliporushwa sikuanguka chini. Nilikuwa nimevaa T-shirt nyeupe. Akili yangu hii!

Tulipomaliza maombi ya zaidi ya nusu saa, tukaketi tena, nikianza kuulizwa najisikiaje, nami nikasema nilijihisi vizuri kiasi. Bi Zawadi alifurahi sana alipotambua kuwa niliguswa mno na hii kitu. Nisingeweza kusema mengi mno kwa kuwa kuna hisia zilivurugana ndani yangu, ila nilijikuta nimeipenda sana hii kitu, nami nikaomba kujua ratiba za ibada kwa wiki.

Wakati akiwa ameanza kuelezea, simu yangu ikaita, nami nikaitoa mfukoni ili kuiondolea sauti, lakini baada ya kuona mpigaji kuwa askari Ramadhan, nikawaomba wanawake hawa nipokee simu mara moja, nao wakakubali. Nikanyanyuka na kuelekea mpaka nje, kisha nikapokea ili nimsikilize jamaa. Sikuwa nimetegemea anitafute leo.

"Hallo..." nikasema hivyo.

"Yes, JC? Uko wapi?" Ramadhan akasikika.

"Nipo... maeneo siyo mbali sana na Mbagala. Vipi mkuu?" nikamuuliza.

"Uko na kazi, au?"

"Hapana, ni matembezi tu..."

"Naomba tukutane upesi. Nakutumia location kwa sms, ufike hapa mida ya saa sita hadi saa saba. Utaweza?" akauliza hivyo.

Nikatazama saa mkononi kukuta ni saa tano kasoro, nami nikamwambia, "Ndiyo, naweza. Ni muhimu sana?"

"Yes, ni muhimu. Na uwe cautious," akasema hivyo.

"Sawa. Nakuja," nikamwambia kwa uhakika.

Simu ikakatwa.

Nikatulia kidogo na kutafakari ni nini kilichokuwa kimezuka kwa upande wa askari huyu, ila kujua hilo ingenibidi niende huko haraka. Nikarejea pale ndani na kuwaambia wanawake wale kuwa nilipata dharura ndogo iliyonihitaji kuwahi, kwa hiyo nikaomba radhi ya kuhitaji kuondoka haraka.

Mama mchungaji akasema haina shida kabisa, naye Bi Zawadi akasimama pia na kuahidi kuja kwa ajili ya ibada Jumapili. Mimi pia nikatoa ahadi hiyo, kisha ndiyo mama mchungaji pamoja na yule mwanamke mwingine wakatusindikiza kwa pamoja mpaka kufikia sehemu ya kupandia daladala.

Ulikuwa ni wakati mzuri sana kuwa pamoja na Bi Zawadi huku, na nilitamani hata tupite sehemu pamoja naye ili tupate kitafunwa na nini, ila ukitegemea na muda niliokuwa nimepewa na yule askari ingetubidi tu tuchukue usafiri na kuondoka kurudi nyumbani. Kwa hiyo baada ya daladala kufika, tukaagana kwa mara ya mwisho na mama mchungaji na kupanda, haoo tukaishia.

★★

Mbinde za hapa na pale za usafiri zilisababisha tukawie kiasi, mpaka inaingia saa sita kabisa ndiyo tukawa tumeshukia Mzinga. Sasa kutokana na dirisha la wakati kuwa dogo kwa upande wangu, nikamwambia Bi Zawadi atangulie kwenda nyumbani ili mimi nipitilize mpaka huko nilikokuwa naenda, halafu tungekuja kuonana baadaye. Hakuwa na neno. Nikamwitia boda ili asisumbuke kutembea mpaka nyumbani, na baada ya yeye kupanda na kuondoka, mimi pia nikachukua boda na kuomba nipelekwa Rangi Tatu fasta.

Tayari askari Ramadhan alikuwa amenitumia ujumbe kwenye simu wa sehemu ambayo alitaka tukutane, na alitaka niwe makini sana ili nisije kufatiliwa maana sehemu hii ilikuwa ya kibinafsi mno. Nilihisi tu kungekuwa na vitu vya siri-siri kwenye huu mkutano wangu pamoja naye, kwa hiyo nikamwambia nimeelewa na niko njiani, nikaweka akilini hilo eneo na jengo alipotaka niende, kisha nikaifuta sms yake na kuzima simu pia. Mambo ya kuwa keyafuli hayo!

Nimekuja kufika kwenye eneo husika tayari saa saba ikiwa imeshaingia, lakini ya dakika za mapema, nami nikaelekea mpaka kwenye jengo nililoelekezwa. Nikaenda moja kwa moja kwenye chumba ambacho kilikuwa na namba hususa niliyopewa, kwa sababu kulikuwa na vyumba vingi vyenye namba pia kutokana na jengo hilo kuwa la upangishwaji, nami nikafungua mlango na kuingia.

Nikasimama usawa wa mlango ndani ya chumba hiki ambacho kilikuwa na hali ya ugiza sana kutokana na kutokuwa na madirisha makubwa isipokuwa sehemu nyembamba tu kwa juu zaidi za kupitishia hewa, na taa ndogo iliyomulika mwanga wa rangi ya chungwa ndiyo iliyokuwa katikati kutokea juu. Kilikuwa kipana lakini hakukuwa na vitu vingi ndani humo. Usawa wa sehemu hiyo katikati hapo sakafuni kulikuwa na meza moja tu, ambayo haikuzungukwa na viti, bali watu. Watatu.

Wawili sikuwafahamu, ila mmoja alikuwa ni askari Ramadhan. Ni yeye tu ndiye aliyekuwa amevalia kwa njia ya kawaida kama raia, lakini wenzake walivaa kwa mitindo fulani kama vile walikuwa majasusi. Na miili yao ilijengeka vyema sana, wakiwa na nyuso makini, mmoja mrefu kunifikia na mwingine mfupi kiasi, na kwenye hiyo meza kulikuwa na karatasi kubwa, pana mno, ambayo nadhani ilikuwa imeandikiwa mipango yao maalumu.

Hapa nikajua nilikuwa nimeingia sehemu yenye hali makini sana, na huu mchezo ulikuwa wa kiwango cha aina yake.

"Karibu JC. Ingia," askari Ramadhan akanisemesha namna hiyo baada ya kuniona.

Nikaelekea mpaka hapo walipokuwa na kusimama upande mmoja wa meza, nami nikawatikisia vichwa kisalamu wenzie Ramadhan, na jibu lao likawa kwa njia hiyo hiyo.

Ramadhan akasema, "Huyu ndiyo CI wangu wa kwanza niliyewaambia. Anaitwa JC. JC..."

"Naam..." nikaitika.

"Hawa ni maaskari wenzangu, special forces, wako nasi kwenye hii ishu. Huyu ni Richard, na huyu ni Mwitakabilamba," Ramadhan akawatambulisha wenzake.

Kudadeki! Ilikuwa karibu nimwombe arudie kulisema tena hilo jina la pili, lakini nikakaza tu na kutikisa kichwa utadhani nilikuwa nimelielewa. Yaani jina lilikuwa na "mwita," "kabila," na "lamba." Siyo poa!

"Tunajitahidi kufanya kila kitu kwa care sana, ndiyo maana tumekutana kama hivi. Una uhakika hamna mtu anakufatilia?" Ramadhan akaniuliza.

"Ndiyo, nina uhakika. Na simu nimezima," nikamwambia hivyo.

"Vizuri. Sasa... hawa hapa, ni vichwa wa vikosi maalumu ambavyo vitashughulika na round up yote ya hawa watu tunaowanyatia, na nimeona nikukutanishe nao ili wajue kwamba we' ni mmoja wetu, na part unayocheza kwenye hili game..." Ramadhan akasema hivyo.

"Sawa sawa," nikakubali.

"Tutakapowasomba watu wote wa huyo madam Bertha, itabidi iwe kwa mpigo mmoja, na hivyo hiki kikao kidogo ndiyo kitakuwa cha mwisho ili kuhakikisha kwamba tunajua kila kitu kiko sehemu husika... tukipiga tu hatua, iwe ni moja kwa moja. Si unaelewa?" Ramadhan akaniuliza tena.

"Ndiyo. Na unamaanisha kwamba hiyo round up iko karibu zaidi kufanywa?" nikamuuliza pia.

"Ndiyo. Karibu sana," Ramadhan akajibu.

"Kama lini?" nikauliza.

"Kwa upana wa sehemu zote za hiyo organization ya madawa ya kulevya, ndani ya wiki moja tu ndiyo tutapiga hatua ya kuwakusanya wote," akajibu hivyo yule mwenye jina gumu kama Ntibazokiza.

"Ila bado tunahitaji kujua ikiwa info zote za sehemu, procedure, na usambazaji, kufikia sasa... ikiwa zipo vile vile bado au kuna mabadiliko ambayo yanafanywa au yatafanywa kabla ya hiyo wiki kuisha," akasema hivyo yule Richard.

Nikamwangalia usoni askari Ramadhan.

"Anamaanisha anataka uelezee jinsi ambavyo mambo yalivyo. Kila kitu tunacho mezani, ila hawa wenzangu wanahitaji review kutoka kwako kabisa. Unaweza kuwaelezea," Ramadhan akaniambia hivyo.

Nikashusha pumzi kiasi na kuangalia mezani, nami nikaona ramani iliyokuzwa vizuri sana ya jiji la Dar es Salaam kwenye karatasi iliyokuwepo hapo. Kulikuwa na michoro-michoro ya kalamu pia, nami nikawaza bora kama kungekuwa na kifaa cha kielektroni kwa ajili ya kuonyeshana mipangilio ya mambo, lakini kwa sababu za kiusalama na uharaka nilielewa kwa nini waliamua kutumia pepa. Hakukuwa na shida.

Nikawaambia, "Okay. Hamna lolote lile lililobadilika, zaidi... ndiyo wanazidi tu kuimarisha mfumo wao mzima wa hii biashara. Iko hivi. Huyu madam Bertha na kundi lake wana vyumba maalumu kwenye majengo makubwa 21 hapa jijini, ambavyo anatumia kutunza mizigo mingi ya madawa ya kulevya. Kunakuwa na watu wake kwa hizi sehemu, na wamekaa kama watu wa kawaida tu; kama ni duka la nguo, au vitu vya rejareja, ama mashine ya kusaga nafaka... wanakuwa wanakaa kama wauzaji wa kawaida tu, lakini ikifika mida special kwa ajili ya kufanya delivery ya madawa hayo, wanaanza kuyatoa na kuyasambaza kwa kutumia system ya taka..."

Ramadhan, akiwa amekunjia mikono yake kifuani, akatabasamu na kutikisa kichwa chake, kisha akasema, "Nani angefikiria wangekuwa wanatumia njia ya kuondoa uchafu ili kusambaza uchafu wao?"

"Siyo rahisi. Kwa hiyo wanatumia system ya takataka?" Richard akaniuliza hivyo.

Nikasema, "Yeah. Bertha, na jamaa yake anaitwa Festus, wana ushirika na makampuni manne jijini yanayohusika na huduma ya kuondoa taka majumbani, maofisini, kwenye makampuni, vyuoni, everywhere yalipo available. Nafikiri mmeshayajua..."

"Yeah, tunayajua..." Mwitakabilamba akasema hivyo.

"Yes, kwa hiyo ikitegemea na pale ambapo order za hayo madawa zinatakiwa ziende, zinapelekwa kupitia hayo magari ya taka. Wanaweza feign kwamba wanaenda kupitia takataka hapa au kule, na hata kama unakuta gari linakuwa limejaa takataka halisi, kunakuwa na sehemu ya kificho kwa ndani ambayo ndiyo inakuwa imebeba mifuko yenye haya madawa. Kwa hiyo wanaoyapokea wanakuwa wanajua kabisa... ah, ikifika saa fulani, gari la taka litapita hapa. Kama kunakuwa na fuko la uchafu kwenye dustbin, wanaokuja kulitoa na kuli-empty wakimaliza, wanayatia madawa humo yakiwa kwenye mifuko safi na kurudisha fuko la kwenye kopo likiwa na hayo madawa. Kwa hiyo wanaoyategemea wanaenda upesi kuyachukua kwa njia hiyo, na malipo wanakuwa wameshafanya mapema. Njia za kuhakikisha kwamba hawaonwi tayari zimewekwa mahala pake, kwa hiyo unakuwa ni utaratibu usioshtua yeyote ambaye hahusiki," nikawaelezea.

"Na hiyo ni kwa sehemu zenye watu wenye nazo tu bila shaka," akasema hivyo Richard.

"Yes. Kinondoni, Kigamboni, Makumbusho, Kariakoo, Sinza, Mlimani, UDSM, sehemu nzuri za Mbezi, Kawe... yaani, nyingi sana kuzungukia jijini. Utaratibu wao wa malipo na delivery ni wa maana, gari liwe kubwa ama dogo, haijalishi. Wafanyakazi wapo wa kutosha, na wako fasta yaani kama tu system ya kumwita Uber... ila yao bora zaidi," nikawaambia hivyo huku nikiwaonyeshea kwenye ramani.

"Ni bora kwa uchafu zaidi. Wako smart lakini, hakuna traffic hata mmoja ambaye atasimamisha gari la takataka kuchunguza. Na wanaowasambazia lazima wawe wanalipwa vizuri ndiyo maana wanaongezeka, eh?" akaongea hivyo Richard.

"Ajira zenyewe safi mbinde. Nani atawalaumu? Pesa popote, watakwambia angalau hawafanyi ushoga," Ramadhan akasema hivyo.

"Ila ndiyo lazima huu upuuzi ukomeshwe. Shida siyo wanaonunua, ila ni wanaoyasambaza, haijalishi ni wakubwa au wadogo. Na vipi kwa walala hoi? Hivi vitu vinawafikia?" akauliza Mwitakabilamba.

"Zinafika, ila mfikishaji siyo Bertha. CI wangu mwingine anasema Bertha ni kama retailer kwa watu wakubwa, anapokea chake kikubwa, anawasambazia kipato wanajeshi wake waliohusika, na yeye anakula pesa ndefu... kama malkia vile," akasema hivyo Ramadhan.

Kauli yake Ramadhan ikanifanya nimtazame kimaswali kiasi. Alisema "CI" wake mwingine, yaani Confidential Informant, neno linalomaanisha mtu afanyaye kazi na maaskari kisiri ili kuwakamatisha wahalifu. Kwa hiyo alimaanisha kulikuwepo na mtu mwingine kwenye mtandao wa mishe zake Bertha ambaye alifanya kazi na maaskari hawa kisiri na kuwapa taarifa, kama vile mimi tu. Sikuwa najua hilo, kwa hiyo sikujua alikuwa amemwongelea nani.

"Okay sawa. Hivyo ndiyo network yao ya usambazaji inavyoenda. Vipi kuhusu ishu ya wewe kumtengenezea coke ili akuze soko lake?" Mwitakabilamba akaniuliza.

"Ndiyo, huu mwezi ulioisha ndiyo limekuwa suala la kipaumbele kwake, na wameshaanza kuyazagaza. Faida inaingia. Kwa ajili ya hiyo operation, Bertha alitafuta sehemu nzuri sana ya kuniweka mimi na watu wake ili tuyatengenezee huko bila kuvuta attention. Kwenye supermarket moja kubwa," nikamwambia.

"Ipo Riverside. Ubungo," akasema hivyo Richard.

"Yeah," nikakubali.

"Tumeshai-monitor pia, kama tu hayo majengo 21. Kilichopo hapa JC, ni kusubiri tu tuwe kwenye position nzuri ya umoja ili hiyo round up ikifanywa, iwe ni kwa siku moja ambayo Bertha, sijui Farao, Tito, Sudi, na nani... huyo Chalii... anayefanya uuzaji wa wanawake, yeah wote yaani... WOTE... tutawaweka ndani. Na itakuwa kwa siku ambayo hawatategemea," Ramadhan akaniambia hivyo.

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Kwa hiyo endelea kungoja kwa subira, uwe makini, mchezeshe Bertha karibu, ujue kabisa pale utakapotakiwa kuwepo hiyo siku ikifika. Si unaelewa?" Ramadhan akaniambia hivyo.

"Ndiyo, naelewa," nikamwambia.

"Vizuri sana, JC. Yote uliyosema yako in check. Kinachotakiwa sasa hivi tu ni kufuata mwongozo atakaokupa Rama, na hii wiki ikiisha huu mzigo utakuwa umeshautua," akaniambia hivyo Richard.

"Sawa sawa, ila...."

"Shika hii," Ramadhan akanikatisha kwa kusema hivyo.

Alikuwa ameninyooshea kifaa fulani kidogo sana cha kielektroni, nami nikakipokea na kumtazama.

"Kaa nayo muda wote, itunze vizuri. Wakati mwafaka ukifika, utajua jinsi ya kuitumia," akaniambia hivyo.

Nikatikisa kichwa na kuiweka mfukoni, nami nikamwambia, "Lakini... bado sina chochote juu ya yule jamaa, Festus. Ni fence aliye makini sana, namaanisha... anajua kujilinda, so, sijapata lolote la kumweka kwenye position ambayo wengine watakuwepo ili muwaangushe wote pamoja naye. Tutafanyaje kuhusu hilo?"

Maaskari hawa watatu wakaangaliana kwa pamoja, kisha Ramadhan akasema, "Usijali. Nitashughulika na hilo. Ni mjanja huyo jamaa, lakini atakamatika tu."

Nikatikisa kichwa kuonyesha nimemwelewa.

Ramadhan akatazama saa yake mkononi, kisha akasema, "Alright. Hii session imeisha. JC... unaweza kwenda. Be very careful. Umenielewa?"

"Ndiyo. Nakuelewa mkuu. Asante," nikamjibu hivyo.

Akanionyesha ishara kwa mkono kuwa niende sasa, na wenzake wakanitikisia vichwa vyao kama kuniaga.

Nikageuka zangu na kuanza kujiondokea sehemu hiyo, lakini kabla sijaufikia mlango nikawa nimekumbuka jambo fulani, nami nikawageukia na kusema, "Mkuu..."

Wote wakaniangalia, na Ramadhan akasema, "Ndiyo?"

"Umesema kwamba... kuna CI wako mwingine ndani ya network ya Bertha. Naweza kujua ni nani?" nikamuuliza kwa umakini.

Akatulia kidogo, kisha akaniambia, "Usiwaze kuhusu hilo. Na yeye yuko kama wewe tu, hajui kwamba uko pamoja nami, na sidhani kama anakujua."

Nikaendelea kumwangalia usoni tu.

"Ni muhimu msijuane kabisa ili mbaki kuwa salama mpaka hii yote iishe. Umeelewa?" Ramadhan akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kukubaliana na hilo, kisha ndiyo nikafungua mlango na kutoka ndani humo.

Mambo yalikuwa yanaelekea kupamba moto! Ah, yaani kuwa sehemu kama hiyo ilinifanya nijione kuwa mpelelezi fulani hivi, lakini yule mnafiki kinoma! Huo unafiki naoongelea ndiyo ambao ningetakiwa kuuendeleza kwa upande wa madam Bertha ili mambo haya nyuma ya pazia lake yashike hatamu haraka siku ambayo angetumbuliwa majipu yake ya maovu, yeye pamoja na kundi lake lote lililohusika.

Nilijihisi vizuri sana kuwa karibu zaidi na ushindi dhidi ya kile ambacho mwanamke huyo alikuwa amemfanyia Joy na watu wengi ambao sikuwafahamu pia. Kuangusha biashara zake zote ghafla yeye na watu wake waliohusika lingekuwa ni tukio zito sana ambalo lingemuumiza, kwa hiyo nilikuwa na hamu kubwa ya kuja kushuhudia hayo yote wiki moja mbeleni.

Lakini, bado nilikuwa namtafakari sana huyo "CI" mwingine wa askari Ramadhan. Bora kama ingekuwa najijua tu kuwa mwenyewe kama "snitch" kwa madam Bertha, lakini sasa kujua alikuwepo mwingine pia kulinipa hisia fulani za wasiwasi kiasi. Vipi ikiwa kama huyu mtu alinijua, au nilimjua, na tulijuana? Alikuwa ndani ya huu mchezo kwa muda gani mpaka na yeye awe ametoa taarifa zilezile nilizokuwa nimewapa maaskari hao? Vipi kama bila mimi kujua, huyu jamaa angekuwa "snitch" kwangu mimi pia kuelekea mipango ya maaskari na ya madam Bertha mbeleni? Angekuwa nani huyu mtu?




★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
Shukhran🙏🙏
 
Back
Top Bottom