Simulizi: Mimi na Mimi

Simulizi: Mimi na Mimi

Sahivi na imekaa vizuri siyo kama msimu uliopita,kujisifia kulikuwa kwingi mpaka mtu ukifika kwenye aya za namna hiyo una-skip,endelea hivihivi Elton Tonny
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA NNE

★★★★★★★★★★★★★★


Bertha akaona kwamba jambo hilo lilikuwa limenichanganya kiasi, naye akasema, "Unawaza challenge za kuwa baba zitakuwaje eh?"

Nikaangalia pembeni kwanza.

"Ahah... me mwenyewe ninawaza sana. Ni muda umepita toka Giselle alipofariki... sikuwaza kuwa mama tena, yaani... mambo yalikuwa mengi. Nataka kuipata hiyo furaha ya kuwa mzazi tena... na ninataka nikuzalie wewe," akaniambia hivyo.

Nikamwangalia usoni kwa umakini.

"Vipi? Ungependa tulete ka kike au ka kiume?" akauliza.

Nikaangalia chini tu.

"Au hutaki mtoto?" akaniuliza hivyo hatimaye.

Nikamwangalia na kusema, "Nafikiria hali zilizopo, Bertha. Mambo yanayotuzunguka. Kweli litakuwa wazo zuri kupata mtoto sasa hivi?"

"Unataka iwe lini?" akauliza.

Nikashindwa hata kutoa jibu.

"Unajua nina miaka mingapi?" akaniuliza.

"Thelathini na saba," nikamwambia.

"Right. Chumvi imeenda sana. Unataka nizae nikiwa na miaka mingapi sasa? Arobaini? Ili mwanangu akifikisha miaka 20 aanze kuniita bibi?"

"Sijamaanisha hivyo Bertha, najua unanielewa..."

"Sikuelewi. Niambie kama hutaki nikuzalie," akasema hivyo.

Nikashusha pumzi kiasi na kumuuliza, "Uko serious kabisa?"

"Kuhusu?"

"Kuzaa na mimi?"

"Ni kipi kinachofanya ufikiri kwamba natania?"

Nikatulia tu na kuendelea kumwangalia kwa umakini.

"Hivi unanipenda kweli?" akauliza.

"Ah, hilo swali likianzaga kutumiwa kama silaha huwa inaboa..."

"Kwa hiyo kumbe nakuboa?"

"Unataka niseme nini Bertha?"

"Nataka uniambie, utazaa na mimi, au hautazaa na mimi?" akauliza hivyo kwa mkazo.

"Me... muda bado Bertha..." nikamwambia hivyo.

Akaniachia na kutazama pembeni huku akisema, "Ah, fuckit..."

"Nisikilize. Bertha... sawa najua ume-miss kuwa mama, lakini... unaonaje ukifikiria kuzaa wakati ambao mazingira yote kwa ujumla yatakuwa salama kwa ajili ya mtoto?" nikamwambia hivyo.

"Usalama upi? Pesa si ipo?"

"Namaanisha... kila kitu kwa ujumla Bertha. Maisha uliyonayo sasa hivi, unayapata kupitia njia... harmful. Hiyo inaweza ikamwathiri na mtoto pia ikiwa bado utakuwa ndani ya hayo maisha...." nikajikuta nimeenda mbali kiasi katika kuongea.

Akaniangalia usoni kwa umakini sana, naye akauliza, "Unataka kusema nini?"

Nikafumba macho kwa ufupi, kisha nikamwambia, "Najua na wewe unatafuta nafasi ya kupata furaha, kama wanawake wote. Ila kama ni mtoto... labda ufikirie njia nyingine... salama... ya maisha, baada ya kumalizana na haya tuliyonayo sasa hivi..."

Akaendelea tu kuniangalia kwa umakini.

"Kama tu nilivyokwambia siku ile... labda kwa jambo hilo, vipi ukiamua tu kuachana na madawa halafu ukajenga kitu kingine clean kabisa, ujitoe yaani... uchukue mkondo mwingine ambao... a-ambao utakuwa salama kwa ajili yako wewe na mtoto utakayezaa? Eh?" nikamwambia hivyo.

Akaangalia tu pembeni na kucheka kidogo kwa pumzi, na kiukweli najua alikuwa akiniona kama mpuuzi fulani hivi, ila na mimi mwenyewe sijui tu ni kwa nini nilikuwa kama vile najitahidi sana kumfanya ageukie mbali kutoka kwenye biashara zake haramu na kumpa kama ukombozi. Yaani... ilikuwa ni kama vile namwonea huruma eti kwa sababu ya kutambua mambo yaliyokuwa yakija. Sijui nilikuwaje tu!

Akasimama ghafla na kisha kusema, "Unaweza kwenda sasa."

Nikasimama pia na kumwambia, "Bertha, ona... sina maana mbaya, ila ukikaa ukafikiria...."

"Sihitaji kufikiria chochote. Nimekwambia nenda. Jibu langu nimeshalipata," akanikatisha kwa kusema hivyo.

"Bertha, come on..." nikamsemesha kwa upole.

"Nenda Ubungo, sasa hivi. That's an order," akaniambia hivyo kwa uthabiti.

Nikatulia kidogo nikimtazama usoni kwa utulivu, kisha nikageuka na kwenda nje ya chumba chake. Nikajikuta nasimama tu pembezoni mwa mlango wa chumba hicho, nikiwa nafikiria lipi ni hasi na lipi ni chanya. Aloo! Hapo ndiyo nilikuwa nimejikoroga bila kujitambua.

Kweli kuchanganya mafuta na maji halafu ukategemea yaunganikane ni kitu ambacho kingefanya yeyote akuone kuwa mpuuzi, na mimi kusema kweli nilikuwa nimeanza kuonyesha huo upuuzi kwa kujikuta nachanganya vitu vilivyohusisha hisia tofauti na uhalisia tofauti sehemu moja, na kwa matokeo yenye kuvunja moyo havikuunganikana.

Hakukutakiwa kuwa na hisia yoyote ile ndani yangu ambayo ingenilazimu nimwonee mwanamke huyo huruma mpaka kujaribu kumshawishi afanye mambo mengine tofauti na uhalisia wa maisha aliyokuwa ameamua kuwa nayo, lakini hisia hiyo ilikuwepo. Ni kwamba tu labda kukaa naye huo muda wote kulikuwa kumenifanya nione uwezekano wa yeye kuacha matendo yake na kuishi maisha mengine, ila ni wazi kuwa hakutaka hilo.

Ni wazi pia kwamba hata kama kweli alikuwa akitaka kuzaa na mimi, ilikuwa ni kwa sababu za kibinafsi, si kwamba alitaka kuunda familia salama na kijana mdogo kama mimi. Lakini bado tu nilikuwa navutwa na kitu fulani kutaka kumkingia kifua, yaani... sijui tu kwa nini. Siyo kwamba nilimpenda, hapana. Labda tu ilikuwa ni suala la kumzoea, kiasi kwamba mpaka ningeweza kumsamehe kwa vitendo vyake vingi vya dharau alivyonionyesha wakati wa nyuma, lakini bado akilini nilielewa ni lazima angetakiwa kwenda chini.

Ila kwa kufikiria hasa ni namna gani watu kama wakina Sudi walitaka mwanamke huyu aende chini ndilo suala lililoupa ubongo wangu kizungumkuti ukuti kuhusu uamuzi wa mimi kuchukua. Aisee, mawazo yalikuwa mengi mno kichwani mpaka nikashindwa kuelewa niyapange vipi, hivyo nikaamua tu kuondoka hotelini hapo upesi kabla kichwa hakijapasuka.

★★

Basi, nikaondoka hayo maeneo ya Vunja Bei na kufanikiwa kupata mwendokasi ambayo ilinipeleka mpaka Ubungo, nami nikashukia huko Riverside na kupanda bajaji iliyonipeleka hadi kwenye supermarket fulani kubwa eneo hilo. Hii ndiyo ilikuwa sehemu kuu ya kazi yetu bwana, kazi ya kupikia madawa ya kulevya ya cocaine kwa njia ya kificho. Palikuwa hivi.

Supermarket kama supermarket yoyote ile, huwa zinakuwa na mpangilio wa shelfu ndefu zenye bidhaa mbalimbali, na huwekwa kwa utaratibu mzuri sana kuwafaa wateja wanaofika kujichagulia bidhaa wanazohitaji, kisha kwenda sehemu ya malipo kulipia. Kunakuwa na chumba cha ziada ndani humo ambacho kinatunza bidhaa zingine zaidi, ili baadhi zilizo kwenye manunuzi zikiisha ama kupungua kwenye shelfu, basi zinaongezwa.

Ni kwenye hicho chumba ndiyo kulipokuwa na chumba kingine kidogo, ambacho kilijengewa ndani humo humo na kufichwa mlango kwa shelfu la kutunzia maboksi ya bidhaa. Yaani kama mtu angeingia, isingekuwa rahisi kudhani kuna chumba kingine, lakini kwa sisi tuliohusika nacho, ilitupaswa tuyasogeze maboksi hayo kwa uangalifu ili kuachia njia, na kuyarudishia vile vile tena ili kuziba njia tulipoingia na kutoka. Humo ndiyo madawa yalitengenezewa sasa.

Mwenye supermarket hiyo alikuwa ameshanunuliwa na Bertha, kwa hiyo hata wauzaji na wafanyakazi wa hapo ambao hawakujihusisha na haya madawa walijulishwa kuhusu chumba hicho kuwa na biashara za watu wengine zisizowahusu, hivyo hakuna aliyetakiwa kujifanya mpekenyuzi. Oh, iliwahi kutokea mmoja wao akanusanusa yaliyokuwa yanaendelea, Bertha akamtembezea upendo wake. Ikiwa unaelewa. Kwa hiyo hata kwa wengine, ilikuwa wazi kwamba biashara hiyo ilikuwa na uhatari, na ili kutopoteza kazi na mambo mengi, walifanya iwe kama vile chumba hicho hakikuwepo kabisa.

Isipokuwa tu kwa sisi ambao tulihusika. Madam Bertha alikuwa na kawaida ya kuja hapo kila Jumatatu ya wiki, nadhani kumlipa jamaa mwenye supermarket hiyo, ambaye alikuwa mwarabu, kwa makubaliano yao waliyojua wenyewe. Zaidi yake, ni mimi tu pamoja na wanaume wengine wawili wa madam ambao ndiyo tuliruhusiwa kwenda huko nyuma, na ni sisi tu ndiyo tuliopika hayo madawa. Walikuwa wanaume wa kazi kwelikweli, hakuna mchezo yaani, ni kazi, matokeo, malipo. Na walikuwa watiifu kwa madam kwelikweli.

Kwa hiyo yalikuwa yakitengenezwa, hayo madawa, halafu yanapimwa kwa gramu ama kilo kadhaa na kutunzwa kwenye mifuko, halafu ingewekwa kwenye mapakiti makubwa ya maboksi ya vitu kama biskuti, ama sabufa, ama blenda, yaani maboksi ya vitu vilivyoonekana kuwa bidhaa safi za mauzo, kisha yangetolewa na kuanza kusambazwa kwenye kila moja ya yale majengo 21 ambayo madam alikuwa ameshasimamishia hii biashara pamoja na wenzake, ili madawa haya yaweze kurefushwa hata zaidi (yaani yaongezwe wingi), halafu baada ya hapo ndiyo usambazaji kupitia magari ya takataka ungeanza kufanywa.

Yaani lilikuwa ni shirika kubwa hili, na walienda kwa mtindo wa maana. Sudi kunifata hiyo jana usiku na kusema ishu ya madam inaharibu soko lake, ilikuwa hasa shauri ya hii supermarket. Bertha alichanganya hii ishu yake mpya na ambazo wenzake walikuwa wameshasimamisha pia kabla ya mimi kuja, na ndiyo maana haya madawa mapya yalipoanza kukolea ikabidi yaanze kurefushiwa na kwenye hayo majengo pia. Hivyo yale ambayo yalikuwa yameshazoewa yalianza kushuka kiwango cha uagizwaji, ununuzi, vyovyote vile, kwa kuwa hii mpya ndiyo iliyopendwa zaidi.

Bertha hakuwa amewaonyesha wenzake sehemu hususa ambayo madawa haya mapya yalitengenezewa, ndiyo sababu Sudi, labda na wengine pia, walikuwa wameanza kutetemeka mno kwa kuhisi soko lote lingegeukia haya madawa mapya zaidi na kuwasababishia hasara. Ndiyo maana nikafatwa. Madam alijua kuwatetemesha.

Nilikuwa sitaki ikawie mno kwa maaskari kuwamaliza hawa watu mwanzo na mwisho, kwa sababu tayari madawa hayo yalikuwa yameanza kushika kasi kubwa mno hapo jijini, na nilihofia yangetoka nje haraka. Bertha alikuwa ameshaanza kung'ara yaani, na kiukweli mwezi huo mmoja kupita ulikuwa mrefu sana kwa sababu nguvu yake na huyo Festo ilikuwa inazidi kukua; hao mapolisi wangehitaji kumaliza haya yote upesi kabla hiyo cocaine haijamaliza watu. Ooh!

Huwezi kunilaumu bwana, sasa mimi ningejua vipi kama maaskari wangehitaji huo muda wote kunyoosha haya mambo? Ni kwamba tu ushirika wote wa Bertha ulikuwa ni mkubwa sana, kwa hiyo kweli muda ulihitajika. Ila kwa kuwa isingechukua muda mrefu mno kutokea hapa mpaka muda ambao maaskari wangetoka vichakani, suala la kufanya lingetakiwa kuwa kuendelea kuigiza tu, na kutulia mpaka wakati mwafaka wa haya yote kukoma.

Mwana baada ya kufika hapo, nikashusha pumzi tu kujipa utulivu wa kiakili, kisha ndiyo nikaelekea huko ndani ya supermarket ili kuendeleza kazi ya kuliharibu taifa.

★★

Tumekuja kumaliza kazi zilizohitajika kwa siku ya leo kwenye mida ya saa kumi jioni, na ndiyo kwa pamoja, mimi na hao vijakazi wawili wa madam tukawa tumeondoka kutoka kwenye supermarket hiyo. Na tulikuwa tukifanya vitu kwa umakini, yaani hata kutoka tu tulifanya ionekane kama vile sisi ni wateja wa kawaida waliokuwa dukani, na tuliondoka kila mtu kivyake kama hatujuani. Hizo ndiyo zilikuwa "code" za madam Bertha, na tulizifata kuhakikisha usalama wa biashara zake unaendelea.

Kwa hiyo mimi nikajiondokea zangu na kwenda kutafuta mgahawa mzuri ili nipate msosi kwanza, kisha ndiyo ningerudi kule Mbagala. Na huu ulikuwa ni utaratibu kwa hizi siku za Jumatatu, Jumatano, na Ijumaa nilipokuja huku Ubungo kufanya haya mambo, lakini nilitakiwa kubadilisha sehemu na maeneo kwa ajili ya mlo kabla ya kwenda nyumbani ili kuepuka kukaririwa sehemu moja tu. Hivyo sasa nikaelekea kwenye mgahawa mmoja eneo waliloliita Fire, na hapo ndiyo nikaagiza msosi wangu na kufungua simu.

Nilikuwa nataka kuona ikiwa Bertha alinitafuta ama vipi, lakini haikuwa hivyo. Nikaamua tu kuzama Facebook kuangalia mambo mapya na nini, ndiyo nikakutana na pendekezo la urafiki kwa mwanadada Dina. Nikakumbuka kweli leo Tesha alikuwa amenipa namba yake, hivyo nikaamua kum-text mtoto. Muda si mrefu akanijibu, nasi tukaanza kuchat hatimaye baada ya utambulisho na nini, na maongezi yakahamia WhatsApp.

Inaonekana mrembo alifurahia sana mimi kumtafuta, kwa hiyo mpaka namaliza msosi bado nilikuwa nachat naye tu, maana kila mara nilipokuwa nakaribia kumuaga yeye angeanzisha mada nyingine tena iliyofanya tuendelee tu kuwasiliana namna hiyo. Kwa hiyo nikatoka hapo mgahawani baada ya kushiba ikiwa imeshaingia saa kumi na moja, na nikawaza nitembee tu kutokea hapo mpaka pale ambapo ningechukulia daladala kwa kuwa kufika huko Kariakoo stendi kuu ya mwendokasi haikuwa mbali sana kutokea Fire.

Nilikuwa nikitembea huku naendelea kuchat na Dina, utani mwingi ukiwa umeshaanza kugeukia kwenye masuala ya 'nani mchumba wako, mimi sina mtu, aah we' mwongo,' ndipo simu yangu ikaanza kuita ghafla. Aliyekuwa akinipigia ni mtu ambaye sikuwa nimetarajia kabisa anipigie, kwa sababu tulifahamiana lakini pamoja na kuwa na namba zake za mawasiliano, hatukuwa na ukawaida wa kuwasiliana kabisa. Na hasa zaidi kwa wakati huu kuna sababu mbaya iliyokuwa imesababisha hilo.

Lakini nikaona nipokee tu ili kusikiliza alichokuwa anataka kusema, na hiyo ni baada ya kumtumia Dina ujumbe mfupi kuwa nitamcheki baadaye, na sauti ya mpigaji ikasikika kutokea upande wa pili akisema, "Hallo... JC?"

"Naam..." nikaitika kama vile sitaki.

"Vipi bro, za siku?" akauliza hivyo.

"Fresh. Nani?" nikauliza hivyo kwa makusudi.

"Dah! Naona hadi na namba yangu ulikuwa umeshafuta..."

"Huwa sifuti namba nazo-save. Labda sikuku-save kwa jina."

"Aaa... haya bwana. Ni Kevin hapa," akasema hivyo.

"Kevin gani?"

"Acha hizo mdogo wangu... ni mimi Kevin, mume wa Jasmine."

"Bado unajiita mume wa dada yangu wakati umemwacha akiwa na ujauzito?" nikamuuliza hivyo.

"Ishu haiko hivyo JC, wote mmeelewa vibaya..."

"Ila ikoje?"

"Ah, kaka we' mwenyewe unajua kabisa kwamba Jas ana mood swing kali mno, hata kwa mambo madogo alikuwa anakuja juu sana... na ujauzito ndiyo ulikuwa unaongeza hilo..." Kevin akaongea kwa upole.

"Ndiyo maana ukaanza kum-cheat, si ndiyo?" nikamuuliza.

"Una uhakika gani na hilo? Kwa sababu tu yeye ndiyo amesema hivyo?"

"Hawezi akakusingizia tu, Kevin. Ni lazima kuwe na ukweli kwenye hilo..."

Akasema, "Nisikilize JC. Nilikuwa nimekutana na sonara mmoja hivi, mwanamke, kumwomba anitafutie mkufu special sana kwa ajili ya Jasmine. Kumbe wakati huo kuna rafiki yake Jasmine alikuwa kwenye mazingira hayo, akatuona, halafu akatupiga picha akamtumia mke wangu. Nimefika home nakuta Jas kavimba, nikijaribu kumwelezea haelewi, na tena nilikuwa nimetoka kunywa kidogo na wakina Banza ndiyo maana ugomvi ukawa mkubwa sana... mpaka nikaamua tu kuondoka ili nisije kusababisha hali yake iwe mbaya..."

"Na ilikuwa mbaya! Unajua kwamba mimba ilikuwa karibu kutoka?" nikamuuliza hivyo.

"Ndiyo, nilisikia, nikaenda hospitali kumwona, lakini alinifukuza kwa kunilaumu kwamba yote ni makosa yangu. Me JC sikupenda kumwacha Jas kwa... njia ya kufanya ionekane kama labda tumeachana kabisa, nilikuwa nataka tu kumpa space atulie kwanza, maana kama unavyojua mambo ya mimba na nini...."

"Nisikie Kevin. Me ni mwanaume, najua mambo mengi ambayo huwa tunafanya, kwa hiyo hata ujiteteeje... najua hayo yote uliyosema siyo kweli. Wewe kiri tu kwamba ulikuwa na mwanamke mwingine, then tafuta utaratibu wa kufanya amani na...."

"No, JC I swear to God... sikudanganyi. Kama unataka kuthibitisha...."

"Mimi nithibitishe ili iweje? Nimekuwa Jasmine? Kwanza kwa nini unanipigia mimi kuniambia haya mambo wakati ni ya wewe na mke wako ku-solve?" nikamuuliza hivyo kistaarabu tu.

Akaniambia, "Unafikiri sijafanya hivyo? Tokea Jasmine aliponifukuza hospitalini, kila nikimpigia simpati, namtumia sms kibunda, hajibu. Nikimtafuta na mama, call zote zinaenda voicemail, najua hata na yeye ana hasira na mimi japo hatukuwahi kuzungumzia haya. Na Mr. Frank... yaani, sijui hata kama naweza kuongea naye, ndiyo maana nikakutafuta wewe mdogo wangu ili nipate njia ya kusema na Jas tena... nimem-miss sana JC... hayupo nyumbani kwangu zaidi ya mwezi sasa hivi, na najua atakuwa kwa mama mkwe huko... natamani hata kwenda, lakini...."

Wakati nikiendelea kusikiliza maombi ya mume huyu wa dada yangu, bado nilikuwa natembea hapo hapo Kariakoo, nikipishana na watu wengi sana, lakini jicho langu likawa limeweza kukamata uwepo wa mtu fulani ambaye ilionekana kama alikuwa akinifuatilia. Sikuweza kuuona uso wake vizuri, ila alikuwa upande wa pili wa barabara, na kwa muda fulani sasa tokea nilipokuwa nimepokea simu ya Kevin, alionekana tu kutembea sambamba na mimi akijifanya kama mpita njia wa kawaida tu.

Alikuwa ni mwanaume, mwenye mwili mkubwa uliolelekea kuwa wa ubonge, akiwa amevalia sweta jepesi jeusi pamoja na suruali ya jeans nyeusi, na sandals za kahawia miguuni. Kofia yake nyekundu kichwani ilisogezwa mbele sana usoni kuuziba vizuri, na kilichofanya nisiuone vyema ni hasa kutokana na umbali, watu, na pia mimi mwenyewe kujitahidi kujifanya kama vile sikuwa nimemtilia maanani mwanaume huyo.

Baada ya Kevin kumaliza kutoa kilio chake kilichoonekana kuwa kilitoka moyoni, nikamuuliza, "Umem-miss eh? Sawa. Nimekuelewa. Kwa hiyo... wewe unachotaka sasa hivi ni nini?"

"Nataka kurudiana na dada yako mapema, JC. Space kwa huu mwezi mzima imetosha, siwezi kusema niendelee kukaa kimya tu halafu aje kujifungua me hata sipo, hiyo italeta picha gani mbele ya wazazi? Hatujafunga ndoa kihalali bado, sawa, lakini moyoni mwangu yule tayari ni mke wangu. Nakuomba ujaribu kunisaidia niongee naye tena," Kevin akasema hivyo.

Huku nikiwa naendelea kuibia kwa jicho langu kumwona jamaa aliyekuwa sambamba nami, nikamuuliza Kevin, "Uko wapi kwani sasa hivi?"

"Nipo kwangu, nimesharudi..."

"Sa' si ungetulia tu mpaka Jasmine ajifungue?"

"Hata hilo nitakubaliana nalo, ila me nachotaka ni kwamba tuwe kwenye mstari mzuri mpaka kufikia siku atakayojifungua. Eh? Haina shida hata akiendelea kukaa na mama huko, la muhimu tu uhusiano wetu uwe sehemu nzuri kwanza, pamoja na wazazi pia... lakini bado simpati yaani... najisikia vibaya..."

Kevin alipokuwa ananiambia hayo, nilikuwa nimeamua kuachana na barabara na kuingia ndani ndani kwenye majengo na sehemu zenye shughuli nyingi, nikitembea kawaida tu, ili nione kama kweli yule jamaa angeendelea kusonga na mimi. Sikukosea. Alikuwa ananifatilia, kwa sababu ningejifanya kugeuza shingo huku na huku kuangalia hiki na kile, na yeye angeonekana kuja nyuma yangu taratibu. Hapo nikaelewa kulikuwa na hatari.

"JC? JC vipi, bado upo?"

Kevin akauliza hivyo baada ya kuona nipo kimya, na kiukweli nilikuwa sijasikiliza mengi zaidi aliyokuwa amesema kwa sekunde chache za mwisho, hivyo nikamwambia, "Yeah, nimekusikia. Nimekuelewa Kevin. Ona... niko... Kariakoo sasa hivi, vurugu, kelele, nitakutafuta bro. Sawa?"

"Nataka unifanyie mpango JC... Jasmine..." Kevin akaongea kwa msisitizo.

"Yeah, nimekuelewa. Tutaongea vizuri baadaye," nikasema hivyo kiuharakishi.

"Haya poa. Nashukuru br..."

Nikakata simu kabla hajamaliza kuongea, nami nikaiweka mfukoni upesi.

Bado mfatiliaji wangu alikuwa akija taratibu tu, na mimi nikaelewa wazi kwamba huyo alikuwa ametumwa kwa mambo mawili; aidha anifatilie tu na kuona ningekwenda wapi mpaka wapi, ama anifatilie mpaka kufikia sehemu ambayo ingekuwa rahisi zaidi kunidhuru. Sikufikiria mtu mwingine yeyote ambaye kwa wakati huu angekuwa na nia ya kutaka lolote baina ya hayo mambo mawili isipokuwa Sudi.

Huenda machale yangu ya kukisia kwamba ningeanza kufatiliwa na watu wake kwa kipindi hiki ndiyo yalikuwa yameanza kuzaa matunda yake, lakini kama siyo hivyo, basi hapa ningekuwa nikishughulika na adui mwingine ambaye sikufahamu wazi alikuwa nani. Kwa vyovyote vile, ningepaswa kumwepuka haraka sana, hivyo nikaamua kuanza chenga.

Kwa mwendo wa kawaida tu, nikaanza kupita huku na kule na kuibukia sehemu ambazo hata sikuwa na ujuzi kuzihusu kufahamu nilikuwa wapi, na bado katika hizo zote huyo jamaa aliendelea kuwa mkia wangu. Nilijitahidi sana kuhakikisha sifanyi agundue kwamba nilitaka kumwepuka, lakini najua wazi kwamba angetambua muda siyo mrefu kuwa nilimpiga chenga kwa makusudi.

Hivyo nikawa nimefikia sehemu fulani ya ndani zaidi iliyokuwa na soko la vyakula na mbogamboga, pakiwa na ardhi yenye matope mazito na uchafu mwingi, watu wakipishana kwa shida, nami nikaona sehemu ndogo sana iliyokuwa na uwazi uliotenganisha milingoti ya miti minene, iliyoshikilia maturubai ya wafanyabiashara. Nikafanya kuingia hapo na kujibananiza huku nikiigiza kuweka simu sikioni na kuficha uso wangu kiasi, na baada ya sekunde chache, nikamwona jamaa akitokea upande niliotokea pia, naye akapitiliza zaidi kwa kufikiri niliendelea kwenda huko mbele.

Hapo hapo nikatoka upesi sana na kuanza kurudi haraka kule nilikotoka, na ingawa hizi kona na chocho za Kariakoo zilichanganya, nikafanikiwa kufika mpaka eneo lililoegeshewa daladala, lakini siyo kule nilikokuwa nadhamiria kwenda kuchukua daladala za kuelekea Mbagala, na sikuwa nimemwona yule jamaa tena.

Haraka mno nikapanda gari ambalo lilikuwa linaelekea sehemu ambayo hata sikuangalia na kujali, yaani nikapanda tu na kukaa. Likaendelea kusimama hapo hapo kwa dakika kadhaa hata baada ya kujaza abiria, na kupitia kioo cha dirisha nikawa nimemwona yule jamaa akiwa anakuja upande huu.

Bila hata ya kuwa nimeuona uso wake, ikanibidi nijifiche zaidi kwa kuinamisha uso wangu, na mpaka kufikia dakika ambayo daladala ilianza kuondoka hapo, ningemwona mwanaume yule pale nje akiwa amesimama pembezoni mwa duka fulani kubwa, akiangaza huku na kule bila shaka kunitafuta, lakini bado sikuweza kuuchora uso wake vizuri sana, ingawa sasa nilitambua kwamba alikuwa na ndevu nyingi kwenye mashavu mpaka kidevuni. Aloo! Siyo poa.

Nikakaa vizuri zaidi baada ya gari kuondoka eneo hilo, huku nikiwaza ni nini hasa ambacho niliponea chupuchupu kwa muda huo. Huu mchezo ulikuwa umeanza kuwa hatari zaidi kwangu, na kama nisingekuwa mwangalifu, basi ningejikuta najipoteza mapema mno. Kuna maamuzi fulani magumu ambayo ningehitaji kuchukua haraka kabla mambo hayajaniharibikia kwa sababu ya kukaa kusubiri tu, nami nikaamua kuvuta simu yangu na kumpigia mtu ambaye sikufikiri ningekuja kuwahi kutaka kumpigia mimi mwenyewe, naye akawa amepokea.

"Hallo..." sauti yake ikasikika.

"Yes, hallo..." nikaitikia hivyo.

"JC. Habari gani?" akauliza.

Nikamwambia, "Ninaomba kuonana na wewe tafadhali... Festo."





★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TANO

★★★★★★★★★★★★★★


Gari nililokuwa nimepanda lilifanya safari ya kuelekea Kigamboni huko, nami niliamua kutoshuka kabisa mpaka mwisho ambapo lingesimama. Ilikuwa kama tu siku ile ambayo nilitoka na Tesha kuja kutembelea huku, yaani likaelekea mpaka pale ambapo mimi na jamaa tulipanda daladala iliyotupeleka hadi Kariakoo, kwa hiyo na hili la sasa hivi lilikuwa la utaratibu huo.

Hivyo niliposhuka, wazo likawa kwenda "kukata tiketi" ya kupanda meli ndogo ya abiria kwenye kivuko cha bahari, kisha nikifika upande wa pili ndiyo nipande daladala ya kunirudisha mpaka Mzinga. Sikujali nani wala nini yaani; nikapanga foleni hadi ilipofika zamu yangu kupata kadi, nikaipata na kupanda meli, tukavushwa salama mpaka upande wa pili, na moja kwa moja nikaelekea stendi ya magari ambapo ningechukua daladala. Nikapanda tu moja ambayo nilikuwa na uhakika ingenifikisha Kongowe huko, na kwa utulivu tu nikaendelea kusubiri hadi pale lilipoondoka hatimaye.

Bado nilikuwa nikiwaza kuhusiana na haya mambo yote, lakini zaidi ni uamuzi wangu wa kumpigia Festo na kumwomba tuonane. Kuna vitu nilikuwa nataka kuhakikisha navipata zaidi, na jamaa alikuwa na hiyo nguvu ya kunihakikishia. Alikuwa amekubali kukutana na mimi, lakini hakusema ni wakati gani zaidi tu ya kwamba angenitafuta na kunipangia pa kukutana hivi karibuni, kwa kuwa mambo yake yalikuwa mengi mno, ratiba ilimbana. Sikuwa na namna ila kumkubalia tu, kwa hiyo kuusubiri mkutano huo na jamaa lingekuwa jambo la lazima.

Lakini hiyo haikumaanisha kwamba kwa kila jambo ambalo lilikuwa limetokea kuanzia hiyo jana nilikuwa nikitegemea Festo ndiyo awe kama suluhisho langu, hapana. Huyu alikuwa kama njia tu ya kunifikisha mahala fulani, katika sehemu fulani ya haya yote, na baada ya hapo ndiyo mengine yangefuata. Ila hata kama ingetokea kwamba jaribio langu kwake lingeshindikana, basi ningetafuta njia nyingine tu ya kutatua vikwazo nilivyokuwa naona vikija; mimi kama mimi. Kama nilivyokuwa nimeshasema, huu ulikuwa ndiyo wakati wa kuwa tayari kuchukua maamuzi mazito, na nilikuwa tayari.

Nimekuja kufika Kongowe ikiwa imeshaingia saa moja, na kutokea hapo mpaka Mzinga nikaamua kutembea tu taratibu. Kumbukumbu kadhaa zilirejea kichwani kwangu baada ya kuipita ile hospitali ambayo tulimpeleka Mariam usiku ule wa matukio mabaya kumpata yeye pamoja na Tesha, nami nikatumia muda huo kuwapigia simu akina Bi Zawadi ili kuwasalimu. Waliendelea vizuri, na Mariam akapewa simu anisalimie pia, huku nikiwaambia ningechelewa kurudi leo hivyo kuja kuonana ingekuwa mpaka kesho, nao wakaonekana kuridhia.

Sikuwa hata nimechelewa kivile, ila ni basi tu kwa muda huu sikuwa na ile amani iliyotosha kuniruhusu hata kwenda kuwatembelea wapendwa wangu hao nikishafika huko. Amani iliyokuwa imevurugwa hasa na kujikuta nafatiliwa na mtu aliyeonekana kuwa na nia mbaya kunielekea. Nilihitaji zaidi kukaa tu kivyangu, pale kwa Ankia, nipige-pige mahesabu kifikira na nini, kisha nipumzishe mwili na akili kwa ajili ya mambo mengine ambayo yangefuata.

Sijui kwa nini tu yaani ila nilikuwa nimeshaanza kuhisi kama vile kuna kitu kikubwa sana kilikuwa kinakaribia kutokea kwenye maisha yangu. Tena kibaya. Na haya yote niliyokuwa nimejiingiza kufanya ndiyo yangekuwa sababu ya kitu hicho kutokea. Kwa hiyo hisia hii ilinivuta chini mno kwa sababu kwa wakati huu ndiyo ilikuwa na nguvu zaidi, hivyo kweli ningehitaji kutuliza hisia na akili kwanza, na kwa muda uliotosha.

★★

Nimekuja kufika kwa Ankia ikiwa imeshaingia saa mbili usiku, nami nikamkuta mwanamke huyo akiwa ndani tayari pamoja na marafiki zake wale wavaa pini puani na mama Chande pia, wakitengenezeana urembo wa Yna kwa kuzichorea mikononi. Ankia pia alikuwa amechorwa, na baada tu ya kusalimiana nao nikaelekea zangu chumbani kubadili mavazi, kisha nikatoka na kwenda kujimwagia kwanza. Nikarudi ndani tena na kutulia tu chumbani baada ya kuvaa nguo nyepesi.

Aliyekuwa ananipa company zaidi kwa muda huu ilikuwa ni Dina, ambaye alinitafuta ili tuendelee na maongezi yetu yaliyokatishwa ile jioni baada ya Kevin kunipigia. Nilikuwa sijisikii hata kuchat naye lakini nikawa mpole tu kwake na kuendelea kutumiana naye jumbe fupi za kirafiki, na hatimaye akawa amefunguka kuvutiwa sana na mimi.

Dina alikuwa mwanadada mwenye akili iliyofunguka, kama tu Ankia, yaani ingawa alijua ningeweza kuwa natoka na mtu mwingine kimapenzi, alikuwa tayari kujiweka karibu nami bila kujali hilo kabisa. Ili kutofikishana mbali sana, nikamwambia ndiyo, nilikuwa na mpenzi, na isingekuwa vizuri nikimsaliti kwa kufanya uhusiano na mtu mwingine, lakini Dina akaendelea kuonyesha msisitizo wa hisia zake kwangu, japo hakuwa wa ile aina ya kulazimisha mahusiano. Alitaka tu mambo huyo!

Nikiwa nimejilaza tu kitandani kwa kuegamia mto huku nachat naye, Ankia akawa amekuja chumbani hapo, naye akasogea mpaka kitandani na kukaa usawa wa ubavu wangu huku akinionyeshea jinsi viganja vyake vilivyopendezeshwa ya michoro ya Yna.

"Imeshakauka?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kukubali huku akitabasamu.

"Umechora tattoo za waislam Ankia, hata Eid bado?" nikamsemesha kizembe.

Akaigiza kuudhika na kusema, "Si uniambie tu kama nimependeza na we' naye..."

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Ni nzuri. Inaonekana unapenda sana uislamu."

"Kwa nini?"

"Kuanzia harufu, mashosti zako, mpaka haya mambo... mbona iko wazi?"

"Wala, me mroma mroma. Siwezi kujifungia huko mie mpenda pombe," akasema hivyo.

Nikatabasamu kivivu na kutazama simu tu.

"JC, vipi? Unaumwa?" Ankia akaniuliza hivyo.

Nikamwangalia na kusema, "Hamna, niko kawaida. Mbona uulize hivyo?"

"Nimeona umeingia kama vile huna raha..."

"Nimechoka tu," nikamwambia hivyo kiupole.

"Unachoshwa na nini?" akauliza.

Nikabaki kimya wakati nikijibu jumbe ya Dina kwenye simu.

"Ndo' unachat na demu wako mpya?" Ankia akaniuliza.

"Hamna. Huyu ni rafiki yangu," nikamwambia.

"Ndiyo anayefanya kila ukiondoka unachelewa kurudi, na ukirudi unakuwa umechoka sana, si ndiyo? Huyo rafiki yako huyo?" akaongea kwa njia ya utani.

"Unaniuliza hivyo we' kama nani?" nikamsemesha kiujeuri, lakini kwa utani.

"Mimi kama mama watoto wako," akajibu.

"Unataka kipigo sasa hivi, eti? Em' nenda kawatawaze kwanza hao watoto huko..."

Ankia akacheka kidogo na kunipiga mkononi kidogo, naye akasema, "Chakula kimeiva baba. Njoo ule."

"Nitakula baadaye. Napumzika kidogo," nikamwambia.

"Mmm..."

"Nini sasa?"

"Sema tu kama umetoka umeshiba huko..."

"Yeah, nimekula saa kumi, so... bado sina njaa kivile," nikamwambia.

"Haya. Leo kweli unaonekana kuchoka, sijui hata ulikuwa unamfanya nani..."

"Halafu we' Ankia wewe, inaonekana umeni-miss tu wewe. Unawashwa-washwa sana siku hizi. Unataka nikutandike, eti?"

"Thubutu! We' mwenyewe ndiyo ulikuja na swaga za 'ooh... sasa hivi tuwe marafiki tu, hakuna kunyanduana...' hiyo ya kunitandika itoke wapi? Ndiyo imeisha hiyo mpangaji wangu. Hugusi hili sambwanda tena," akaniambia hivyo.

"Ahahahah... naona mama Chande anakulisha bangi zake," nikamwambia.

"Kwa nini?" akauliza huku akitabasamu.

"Umeanza kuongea kama yeye, kwa hiyo naona akili zenu zitafanana tu. Hilo 'sambwanda' kama halijabantalala ndani ya wiki moja tu, basi ndo' nitajua haujatembezwa naye kwenda kulipigisha makofi," nikamwambia hivyo kiutani.

Ankia akacheka kwa sauti kubwa na kugonga kiganja chake kwenye changu, naye akasema, "Eti 'bantalala!' Me siyo wa hivyo, utasubiri sana."

"Mhm... sawa."

"Haya, sisi tunaenda kula. Halafu... Adelina ameniambia mliongea," akasema hivyo.

"Alikupigia?"

"Eeeh, tumeongea leo, akasema atakuja Jumapili... ulimwalika tuje kuangalia mechi?"

"Yeah. Ni sawa akija na kulala hapa?"

"Eeh! Kwa nini isiwe sawa? Acha mambo yako bwana. Ila ndo' utunze ya kutosha. Yanga itashinda, na utaninunulia bia zote nazotaka," akaniambia hivyo.

"Ahahah... endelea kuota..." nikamwambia hivyo huku nikiendelea kuchat.

"Hahahah... haya baba, tutaona. Yaani Aziz Ki lazima afanye yake," akaniambia.

"Na limdomo lake..." nikasema hivyo kiutani.

Akanyanyuka huku akiendelea kuongea kuhusiana na mechi ya watani wa jadi ili aamshe maneno na kwa kina mama Chande huko, na mimi nikaendelea tu kuchat na Dina mpaka kufikia saa nne usiku kabisa. Ndiyo nikaamua kwenda kupakua chakula kwa muda huo, rafiki zake na Ankia bado wakiwepo, nasi tukajumuika pamoja kimaongezi japo sikuzungumza nao kwa wingi; sanasana Ankia tu na mama Chande.

Haikuchukua muda mrefu nikawa nimerejea chumbani tena, na aisee Dina hakutaka kuniacha. Mtoto alinielewa, alikuwa ameni-miss japo aliniona kwa siku moja tu, na akaelezea hamu yake kubwa ya kuniona siku ya kesho wakati ambao angekuja pamoja na dada yake, Doris, kuwatembelea wakina Miryam. Tumekuja kuagana usiku wa saa saba kabisa nikiwa nimetosha kuchat na mwanadada huyo, nami ndiyo nikaanza kuutafuta usingizi wangu.

Ijumaa ikawa imepita.


★★★


Nimekuja kuamka asubuhi kwenye mida ya saa tatu hivi, ikiwa ni Jumamosi sasa, na kama kawaida, ratiba yangu ingeanza kwa usafi wa mwili kwanza. Nilikuwa najihisi ahueni kiasi baada ya kupumzika, na nilitaka kwa leo nimezwe na mambo mengine tofauti kabisa na yale yaliyowahusu wabaya wangu, kwa hiyo ningetumia muda mwingi pamoja na Ankia na familia yake Miryam. Na nilitaka kumwona huyo Doris pamoja na Dina leo.

Kwa hiyo ikawa ni kunywa chai pamoja na Ankia hapo kwake, tukakaa kupiga story za hapa na pale huku tukiangalia TV hadi mida ya saa sita mchana, kwa kuwa leo Ankia asingekwenda dukani kwake kwa sababu alizojua mwenyewe. Hata kwa asubuhi hii, Dina alikuwa ameamka na mimi kwa kutuma jumbe za salamu, nami nikawa nikichat naye mara kwa mara mpaka aliposema kuwa yeye na dada yake tayari walikuwa njiani kuja huku Mzinga.

Nilikuwa nimejaribu kumpigia madam Bertha na kumtumia ujumbe pia, lakini hakurudisha majibu. Inaonekana bado nilikuwa nimemkwaza sana, na sijui hiyo ingeniacha wapi lakini kwa kweli ilipokuja kwenye suala la kuwa na "mtoto," tena pamoja na Bertha, kilikuwa siyo kitu cha kuchukulia juu juu. Angeendelea tu kuvimba na mimi ningeendelea kujifanya najaribu kumbembeleza, lakini nisingekubaliana naye kwa suala hilo kabisa kwa kujua mambo yaliyokuwa yakija.

Nikaamua tu kuendelea kutulia, na ilipotimia mida ya saa nane bado nilikuwa ndani tu na Ankia, wakati huu akiwa anapika ugali na samaki huko, ndiyo nikatumiwa ujumbe na Tesha. Tesha bana akaniambia kwamba Dina alikuwa ndiyo amefika, kwa hiyo niende, lakini nikamwambia 'tulia wewe.' Kujipeleka kisa wageni wamefika ingekuwa ni michoro ya hali ya juu, kwa hiyo nikamwambia ningeenda baadaye kabisa na si sasa.

Misisitizo zaidi ikaja baada ya Dina na yeye kuanza kunitumia sms kuwa niende anione, lakini nikaendelea kukaza tu. Mpaka Ankia amepakua, tukala, tukamaliza, Dina na Tesha bado walikuwa wananisumbua tu niende, niende, niende, na ilipofika mida ya saa kumi hivi jioni, ndiyo nikawa nimepigiwa simu na Bi Zawadi. Cheupe wangu. Hii ndiyo ingekuwa 'sina jinsi' yangu niliyohitaji zaidi, maana kwa mwito mmoja wa mama huyo kwenda hapo kwao kuwatembelea, jibu la moja kwa moja lilikuwa 'yes!'

Bi Zawadi alinitaka niende hasa ili anitambulishe kwa huyo Doris, ile tu kujuana mimi ni nani kwenye hiyo familia na nini, kwa hiyo mwana nikaingia chumbani kuvaa suruali na T-shirt, nikatengeneza nywele vizuri, kisha ndiyo nikatoka na kwenda mpaka hapo kwao. Nilikuwa nimemwacha Ankia akiwa ameingia chumbani kwake kulala kidogo, na nilipoingia hapo getini nikakuta gari la bibie Miryam likiwepo. Inawezekana bibie alikuwa amewahi kurudi kwa ajili ya wageni ama leo hakwenda kazini kwake, hivyo nikasogea mpaka mlangoni na kuomba kuingia kwa kusema 'hodi.'

Aliyesema 'karibu' alikuwa ni binti Mariam, na ile nimeingia tu, nikapokelewa kwa shangwe sana na binti huyu, akinikumbatia kwa nguvu kama kawaida yake. Mariam alivaa moja ya madera yake ya kawaida, na bado kunikumbatia kwake mbele ya ndugu zake namna hiyo kulinifanya nijihisi uajabu kiasi, lakini nikajitahidi kuonyesha utulivu. Ilikuwa kama vile sebule ilijaa, maana walikuwepo mama wakubwa, Mariam mwenyewe, Shadya, Tesha, Miryam, Dina, pamoja na mwanamke mwingine rika la bibie Miryam, ambaye bila shaka ndiye aliyekuwa Doris.

Nikasalimiana na wa hapo vizuri sana, nikawasalimia na wageni vizuri pia, kisha nikaenda kuketi sofani pamoja na Mariam baada ya Tesha kutuachia nafasi. Hapo sasa ndiyo Bi Zawadi na Shadya wakaanza kunitambulisha kwa wageni kwa mapambo ya hali ya juu, na mimi nikajitahidi sana kumsemesha Doris kirafiki na kumpa hongera yake ya kuelekea kuwa jiko rasmi. Alikuwa mwanamke mzuri, mweusi wa maji ya kunde kama Dina tu, akiwa si mnene sana wala mwembamba, na alikuwa na shepu ya ukweli hata kwa kumwangalia tu alipokuwa ameketi.

Wakati huu alikuwa amevalia T-shirt la mikono mifupi la kijivu lililoficha kifua chake kilichobeba maboga haswa, pamoja na suruali nyeusi iliyombana kiasi cha kuonekana kama skinny. Nywele zake alikuwa amesukia rasta nyembamba na fupi, zilizomwagika kuzungukia kichwa kama vile tambi, akiwa na macho makubwa na midomo minene iliyopakwa lipstick yenye kung'arisha. Saa yake mkononi na pete, hereni, bangili, mkufu, vilionyesha alikuwa mwanamke aliyependa vitu vizuri vyenye gharama na kupendezesha, lakini alitaka kuonekana 'simple' tu kwa watu wengine.

Baada ya kuongea kidogo mambo ya hapa na pale nikatambua alikuwa msomi, na alifanya kazi kwenye kitengo fulani maalumu huko TRA. Alikuwa na ka aina fulani ka uzungu, na niliona akikakoleza zaidi ili ile hali ya yeye kuwa 'msomi' ionekane wazi. Lakini hapa akili yangu ilikuwa imekengeushwa zaidi na Dina, kwa sababu mwanadada huyo alikuwa ananitazama utadhani nilikuwa chakula cha jioni.

Yeye alivalia shati pana kweli kupita umbo lake dogo-dogo, jeupe lenye mistari-mistari, ambalo kwa njia ya mtindo alikuwa amelifungia mbele ya tumbo lake kama fundo. Uwazi mdogo wa tumbo lake ulionekana, na yeye alikuwa amevalia suruali ya jeans ya blue iliyokoza na kurembwa na rangi nyeupe hapa na pale. Alikuwa amesuka rasta ndefu za kahawia alizoziachia mpaka huko mgongoni kwake, akisindikiza maongezi yenye kufurahisha hasa kutoka kwa Tesha na kuendelea kunitazama mara nyingi sana; nafikiri akiwa anasubiri ishara.

Bibie Miryam alikuwa akishughulika zaidi na suala la msosi, kwa kuwa alikwenda jikoni na kurudi kujumuika nasi, na yeye alikuwa amevaa kinyumbani kwa kutia T-shirt nyeusi ya mikono mifupi pamoja na khanga ngumu iliyomfunika kutokea kiunoni. Nilipenda sana jinsi ambavyo alikuwa amepaka rangi nyeusi kwenye kucha za vidole vyake vya kiganja cha kushoto, na kila mara ambayo tungeangaliana usoni, angenipa tabasamu la kirafiki, nami ningejihisi amani sana na kumrudishia pia.

Ikawa ni muda ulioneemeka sana wa kufurahia ushirika wa maongezi pamoja na familia hii ulionifanya nijihisi vizuri zaidi ya ilivyokuwa kwa siku ya jana, nami nikaendelea kuwa hapo pamoja nao hadi giza lilipoingia kuuelekea usiku.

★★

Ikiwa imekwishaingia mida ya saa moja kuelekea saa mbili, bado nilikuwa ndani hapo nikipiga story mbili tatu pamoja na Bi Jamila, Bi Zawadi, Shadya, na Doris. Hawa ndiyo waliokuwa wamenikamata zaidi kwa wakati huu, na Doris alikuwa ameshanizoea haraka. Alikuwa mcheshi pia, kwa hiyo tuliwaburudisha sana hawa wenyeji utadhani sisi ndiyo tulikuwa wazawa wa hapo. Bibie Miryam alikuwa huko nje akifanya nini sijui, halafu Tesha, Mariam, na Dina walikuwa chumbani kwa jamaa wakifanya mambo ya vijana na nini, si unajua? Ile kupatana zaidi.

Tesha alikuwa ameshanitumia jumbe kadhaa kuniambia niende huko chumbani pia nikajaribu hata kumtekenya Dina, angefanya hata kumwondoa Mariam kabisa, lakini najua alijua hiyo haingekuwa kitu yangu kukubaliana naye kabisa. Hata Dina alikuwa akinitumia sms pia kusema amefurahi mno kuniona, anatamani tuongee, lakini mimi nikaendelea kukazia fikira zangu zaidi kwa warembo hawa wengine sebuleni.

Katikati ya maongezi yangu na wanawake hawa, simu yangu ikaanza kuita, nami nikaona mpigaji kuwa mama. Nikawaomba waniekskyuzi kidogo ili nikapokee simu, kisha nikaenda mpaka pale nje varandani na kupokea. Hapo nje nikawa nimemkuta bibie Miryam, akiwa mbele zaidi kuukaribia ukuta wa uzio, na akionekana kutumia simu yake kwa ishu zake, hivyo nikaendelea kuongea na mama yangu huku nikimwangalia bibie.

Mama alikuwa ananisalimu tu, na mimi pia nikamwambia ningekuja kwenda nyumbani kabisa ili kumwona ndani ya hizi siku chache mbeleni, nasi ndiyo tukaagana baada ya hayo na umakini wangu ukarudi kwa bibie pale. Alionekana kuwa makini sana kuchat na nani sijui, nami nikaamua kumfata ili nimsemeshe kidogo. Tayari alikuwa ameniona, kwa hiyo nadhani alipoona navaa ndala zangu akafikiri ninataka kuondoka.

Akasema, "Unaenda, Jayden?"

"Hamna, nipo. Sisepi mpaka nile msosi wako," nikamwambia hivyo kiutani.

"Ahaa, sawa. Nilikuwa nafikiri unataka kuondoka, maana una katabia tukishaivisha tu ndiyo unanyanyuka kukimbia..."

"Ahahahah... Shadya atakuwa ameshanisema sana."

"Na ni kweli..." akasema hivyo huku umakini wake ukirudia simu.

Nikasogea mpaka pembeni yake na kuuegamia ukuta, nami nikasema, "Hiyo taa ya... imeungua eh..."

Nilikuwa nikimwonyesha taa ya upande ule uliolekea kwenye bomba la maji kuzungukia mpaka huko nyuma ya nyumba yao, ambayo haikuwa ikiwaka kama ya hapa mbele, naye akaangalia huko mara moja na kusema, "Eeeh, itakuwa imeungua. Tesha atakuja kubadilisha."

"Okay. Ndugu zako ni watu wazuri sana," nikamwambia hivyo, nikijitahidi kutengeneza mazungumzo zaidi.

"Nani, Doris? Eeh. Yuko vizuri," akasema hivyo.

"Ni mabinamu, si ndiyo? Na ni upande wa baba au mama?" nikamuuliza hivyo.

"Aaa... ni... ukoo wa baba sanasana..." akajibu hivyo huku akiwa bize na simu.

"Ahah... sorry, inaonekana uko bize, nakuvuruga tu hapa. Ngoja ni...."

"Oh no, haunivurugi wala. Nilikuwa tu na... natuma email hapa... nimemaliza," akasema hivyo na kuniangalia.

Nikatoa tabasamu hafifu.

"Na wewe? Ulikuwa unaongea na nani kwenye simu? Baby?" akaniuliza hivyo kiutani.

"Aa wee... ahahahah..." akanifanya nicheke kidogo.

Yeye pia akacheka kidogo.

"Sinaga habari hizo mimi..." nikamwambia.

"Mmm, sawa," akafanya hivyo kikejeli.

"Ilikuwa ni mama bwana. Alikuwa ananisalimia," nikasema hivyo.

"Aaa, kumbe ndiyo maana. Nimesikia unaongea kwa sauti ya kudeka, nikafikiri ni baby," akanitania.

"Ahahah... hapana. Me niko single," nikaongea kwa kujitutumua.

"Mmmm..." akafanya hivyo.

"Nini sasa, hutaki?" nikamuuliza hivyo nikiwa najihisi raha sana kuongea naye namna hii.

"Mhm... haya bwana. Mama hajambo?" akabadili mada.

"Eeh, yuko poa. Wako tu sa'hivi wanasubiria dada yangu ajifungue."

"Ooh, kumbe dada yako mjamzito?"

"Ndiyo. Sikuwahi kukwambia?"

"Hapana, ulishasema tu kwamba una dada, sikujua kama anakaribia kujifungua," akasema hivyo.

"Well, yupo karibu sana kujifungua. Kama siyo mwezi huu, basi ujao mwanzoni," nikamjulisha.

"Okay. Hongera kwake. Na yupo na mama na baba yenu?"

"Yeah."

"Sawa. Uliwahi kusema nyie mme... tokea Mwanza eh? Familia nzima yaani?"

"Aaa... ni mimi, dada yangu Jasmine, na mama sanasana. Dar es Salaam tumekuja hasa baada ya mama kufunga ndoa na huyu mzee wetu miaka kadhaa iliyopita..." nikamweka wazi.

"Ahaa..."

"Eeeh. Mume wake na mama yangu ndiyo... aliyefanya mama na dada wakaja Dar, ila me tayari nilikuwa nimeshakuja huku na wao walipofika pia," nikamwambia hivyo.

"Sawa. Ni vizuri. Na huyo mzee wako yuko poa eh?" akauliza hivyo.

"Sana. Yuko peace mno. Amenisaidia kwa vitu vingi, mpaka hapa nilipo amechangia kwa mengi sana," nikamwambia hivyo.

"Je... baba yako mzazi kabisa?"

Nikaangalia pembeni kwanza na kusema, "Simfahamu."

"Kwa nini?" akauliza hivyo.

"Sikuwahi kumwona. Alinitelekeza mimi na Jasimine tukiwa wadogo mno, yaani... alimwacha tu mama... akaenda wapi sijui... ndiyo hivyo, mpaka leo," nikamwambia.

"Pole kwa hilo," akasema hivyo.

"Hamna tabu wala," nikamwambia.

"Kwa hiyo mlilelewa na mama yenu peke yake? Hujawahi kumtafuta baba yako?" akaniuliza.

"Wa kazi gani sasa?" nikamuuliza pia kwa sauti tulivu.

Akabaki kimya na kuendelea kunitazama kwa utulivu.

"Jasmine alikuwa na miaka miwili sijui, na mimi bado hata nilikuwa sijaanza kusimama, jamaa akakimbia. Maisha hayakuwa rahisi kwa mama kutulea akiwa peke yake, na hakuwahi kumtafuta, sijui... msaada? Hapana. Alipambana, na Mola akamsaidia, tukakua, tukafika sehemu... na yeye sasa hivi yupo sehemu yake ametulia. Ya nini tena kuanza kusumbuka kutafuta watu wasiojali kutuhusu?" nikamwambia hivyo.

Akaonekana kutafakari maneno yangu kwa ufupi, naye akasema, "Kwenye maisha hata mie nimeshajifunza kupokea na kuthamini zaidi kile nachopata kwa kuwa nakihitaji, siyo kukitaka. Hata me sikumpata baba niliyemtaka, ila nikapewa baba niliyemhitaji, na kwa hilo nikaridhika. La muhimu tu ni kuridhika, na naona ndivyo ilivyo kwako. Kama inakupa amani zaidi usipohangaika kumtafuta, basi hiyo ni sawa," Miryam akasema hivyo.

Kauli yake ilieleweka, lakini sikuelewa vizuri sana alimaanisha nini aliposema hivyo kumhusu baba yake yeye, nami nikataka kuulizia upana wa maana ya maneno hayo.

Nikasema, "Ndiyo, ni kweli unavyosema. La muhimu ndo' hilo, sionagi faida kuangalia hayo mambo, nimeridhika na jinsi maisha yanaenda kwa uweza na baraka za Mola..."

Akatikisa kichwa chake taratibu kukubaliana na hilo.

Nikaanza kumuuliza, "Ila, Miryam... umemaanisha nini uliposema kwamb..."

"Mimiii..."

Sauti ya Bi Zawadi kutokea ndani ikasikika ikimwita bibie namna hiyo, naye akaitika.

"Bee... ngoja nione ikiwa wageni wanahitaji kitu fulani, na... ninapakua muda si mrefu, usikimbie," Miryam akasema hivyo na kuanza kuondoka.

Nikamtikisia kichwa kukubali hilo huku nikitabasamu, naye akaelekea ndani kwao.

Nikaendelea kusimama hapo nikiwa nimeegamia ukuta, tafakari za mambo mengi yaliyohusiana na maongezi yangu na bibie Miryam zikiwa zinazunguka kichwani, kisha nikatoa simu kuangalia muda na kukuta ni saa mbili kasoro robo hivi. Nikawaza labda tu nielekee hapo ndani pia, sijui walikuwa wamemwita Miryam kwa masuala ya kuivisha, lakini jambo fulani likavuta umakini wangu.

Kutokea upande ambao ulielekea kwenye bomba la maji nje ya nyumba hii, jicho langu likaanza kuona kama mwanga fulani uliokuwa ukishtua-shtua, nami nikatazama huko na kutambua kwamba ilikuwa ni mwanga wa tochi ya simu uliozimwa na kuwashwa kwa makusudio ya kuvuta uangalifu wangu. Kwa sababu taa ya upande huo ilikuwa imeungua na kutobadilishwa bado, isingekuwa rahisi kumwona usoni aliyekuwa akinifanyia hivyo, lakini nikamtambua. Ilikuwa ni Dina.

Alikuwa ameegamia ukuta wa nyumba uliokaribiana na ukuta wa uzio kuelekea nyuma kabisa ya nyumba hii, na kwa kuwa yeye angeweza kuniona mimi hapo nilipokuwa nimesimama, nikamtolea ishara kwa mkono kuwa aje, lakini yeye ndiyo akatoa ishara kuwa nimfate. Yale mambo ya 'kumchum kumchum,' yaani nyatia nyatia.

Nikaona isiwe shida, nikaenda hadi hapo, naye akasogea mpaka usawa wa sehemu ambayo kulikuwa na chumba cha nje ambacho ndiyo kilitumiwa kutunzia vifaa vingi vya nyumbani, stoo yaani, na kijengo chake kidogo kiilifanya njia ya kuzungukia mpaka huko nyuma ya ukuta wa uzio iwe nyembamba, na yeye ndiyo akasimama hapo. Inaonekana alikuwa ameniita kwa yale madhumuni ya 'sisi wawili tu,' na kulielewa hilo kukanifanya nimkaribie zaidi na kumsemesha kwa sauti ya kunong'oneza.

"Vipi Dina?"

Alikuwa ameukunjia mguu wake mmoja mbele huku mikono akiiegamiza ukutani, naye akajibu kwa kunong'oneza, "Ndiyo nimepata nafasi kuja nje... nikakuona."

"Umepitia mlango wa huku nyuma?" nikamuuliza.

"Eeh..."

"Nani kakufungulia? Tesha?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Dah! Mbona unataka kunitia majaribuni afu' tuko kwa watu?"

Akatabasamu na kuuliza, "Majaribu yapi tena?"

"Kwani we' umeniita gizani ili iweje?"

"Si ili nikuone?"

"Kwenye mwanga ulikuwa hunioni?"

Akacheka kidogo na kuuziba mdomo wake eti kwa madoido.

"Wanafanya nini ndani sa'hivi?" nikamuuliza.

"Wamemwita aunty Miryam ili waongee kidogo, halafu wapakue sijui... me ndiyo nikachomoka," akasema.

"We' chautundu kumbe? Halafu unajifanya malaika..." nikamtania kidogo.

Niliweza kuona Dina akitabasamu kiasi na kung'ata mdomo wake wa chini, kisha akashika T-shirt langu kwa kidole kimoja sehemu yenye uwazi shingoni na kuanza kulivuta kumwelekea. Ilikuwa wazi kwamba alitaka nimfate mdomoni ili tupige busu, nami nikaona isingekuwa mbaya kuionja midomo yake kwa mara ya kwanza.

Nikaifata na kuanza kunyonyana naye midomo, ulimi, meno yakigongana, huku nikiwa nimekishika kiuno chake, naye akajisogeza karibu yangu zaidi na kuizungushia mikono yake mgongoni kwangu. Kwa sababu alikuwa mfupi ilinihitaji kuinama kiasi ili asinyanyue miguu yake, na tayari hamu ilikuwa imenipanda mno kufanya msuli wangu ukaze ile mbaya, na ukikandamiza tumbo lake kwa nguvu.

Hatimaye nikaivunja busu hiyo na kugeuka nyuma kuangalia usalama, kisha nikamtazama na kusema, "Aisee... Dina! Umeniwashia balaa."

"Mhm... unataka nilipoze?" akasema hivyo na kuishika mashine yangu ikiwa ndani ya suruali, kisha akawa anasugua-sugua hapo.

Nikamwambia, "Hapa jau. Tutapanga siku nyingine."

"Me naitaka hiyo jau sasa hivi..." akasema hivyo.

"Dina!" nikashangaa.

"Kidogo tu..."

"Dina, mazingira. Tutakutana siku nyingine..."

"Kidogo tu JC..." akawa ananibembeleza kama vile anataka kulia.

"Tuko kwa watu Dina, umekuja kama mgeni... kwanza ndo' wanapakua. Wakikutafuta wakatukuta? Halafu kwanza me nimebanwa kukojoa..."

"Nikojolee tu mimi..."

"Wewe!" nikamshangaa.

Akaendelea tu kupasugua pale pagum-gum.

Nikamuuliza, "Kwa hiyo utarudi ndani unanuka mikojo? Mbona umekuwa hivi?"

Akasema, "Nina hamu sana na wewe, JC. Na ni muda mrefu..."

Masikini! Mpaka nikamwonea huruma. Mwanadada alionyesha kuwa na hamu kali kwelikweli, na mimi ningekuwa nani kumnyima msaada? Eti?

Pamoja na kuwazia usalama wetu kutokana na mazingira, nikaamua nimpe utamu angalau kidogo. Nyakati kama hizi ndiyo mwanaume unatakiwa uchukue maamuzi ya haraka kwa kutumia akili, na ujanja unahusika pia. Hapo nilikuwa sijambo.

Nikaona nimsogeze Dina nyuma zaidi ili tujibananize kwenye kile kinjia cha kuelekea nyuma, na nikamfikisha kwenye sehemu ambayo ukuta ndiyo ulikunja kona. Kwa hiyo, mimi nikawa nimesimama upande huu ambao tulikuwa, huku mwili wake ukiwa kwa upande ule wa nyuma, kwa hivyo ingekuwa rahisi kuona kama mtu angekuwa anakuja upande wangu au upande wake.

Dina alikuwa ameshaanza kuhangaika na zipu ya suruali yangu, lakini mimi nikaishika mikono yake na kuugeuza mwili wake ili anipe mgongo, halafu yeye akajiongeza na kuanza kuishusha suruali yake na kinguo chekundu alichovalia kwa ndani. Alikuwa na mwili mweusi, na upande huu wa nyuma taa ilikuwa ikiangaza, lakini ukuta ulituficha vizuri. Nilikuwa nahisi msuli wangu umekaza ile mbaya, si unajua mara ya kwanza na mtu mwingine inavyokuwa? Maua!

Mtoto akauegamia ukuta huku akinibinulia kalio lake lisilo kubwa sana, nami nikafungua suruali yangu pia na kuishusha, nikiiachia mashine itambe. Hapa shida kubwa ingekuwa mbu, walipiga kelele yaani utafikiri kulikuwa na sherehe, lakini siye hatukuwajali hata kama wangeng'ata vipi.

Dina akapandisha mshati wake juu vizuri huku akijaribu kunigeukia ili aniangalie, nami nikaanza kuichokonoa mambo kutokea nyuma kwa vidole vyangu, na ilikuwa imelowana haswa. Nikapakaa kidogo ute huo kwenye msuli wangu, kisha nikakiingiza kichwa kidogo ndani yake na kumshika mgongoni kwa mkono mmoja kama namkandamiza ainame chini zaidi. Hakuwa mbishi. Nikaanza kuingiza mtambo ndani zaidi na kukuna taratibu tu, kisha nikakishika kiuno chake kwa mikono yote na kuanza kukoleza raha.

(..........).

(..........).

(..........).

Yeye mwenyewe alionekana kufurahia za taratibu, na mimi nilikuwa makini kuangalia huko mbele na huku nyuma kuhakikisha usalama, na show ikaendelea kwa dakika kama tano hivi, kisha nikaichomoa mashine. Bado ilikuwa imewamba, lakini nilitaka kumwambia Dina tuishie hapo. Sasa sijui shauri ya mazoea?

Kabla hata sijamsemesha, mwanadada akanigeukia na kuchuchumaa, naye akaishika mashine na kuitumbukiza mdomoni mwake. Ai kudadeki! Maneno yakapotea.

(..........).

(..........).

Pamoja na umbo lake lisilo kubwa lakini mtambo wangu mrefu ulikuwa unazama wote, na inaonekana aliufurahia zaidi ulipofika kwenye mabandama huko. Akalishika T-shirt langu na kuling'ang'ania kwa nguvu huku akijitahidi kunigeukia na kuniangalia, na macho yake yalikuwa yamelegea haswa.

Niliridhika tu kwamba hakutoa sauti ya juu sana maana kule ndani walitulia, na utamu kolea, utamu kolea, changu cha kwanza chenye kiherehere kikaja upesi ndani ya dakika saba tu. Nilikuwa natamani nijiachie ndani yake yaani, ila... hapana. Sikuwa na uhakika kuhusu faida na hasara za jambo hilo kwa huyu dada. Nikamwonya tu kuwa mi' nakaribia, naye akafanya kitu ambacho sikuwa nimetarajia.

Akajichomoa na kunigeukia tena, kisha akachuchumaa na kuishika mashine hiyo, halafu akaanza kuinyonya na kuichua haraka-haraka sana. Dah! Alitaka nishushe mzigo, na alitaka niushushie mdomoni mwake. Alikuwa ameshaangalia ujinga mwingi wa wazungu huyu mtoto kama siyo kuufanya!

(.........). Kumwangalia Dina, nikakuta akiwa analamba mashine yangu huku ikionekana kila kitu alikuwa amekunywa. Kila kilichotoka! Aisee, kweli hiyo ndiyo ilikuwa hamu. Na siyo mbaya, mtoto akawa ameongeza glucose mwilini.

Baada ya hiyo pindi yenye kusisimua, nikavuta suruali yangu, naye pia akasimama na kujiweka sawa zaidi. Nikamtazama usoni na kuona jinsi ambavyo aliniangalia kwa njia iliyoonyesha furaha, ile ya kimahaba, nami nikamfuta mate kidogo pande za mdomo wake.

"Nenda ndani sa'. Umeridhika?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa mara moja kukubali.

"Au unataka tuendelee?" nikamuuliza tena.

Akatikisa nyusi kukubali.

"Oh no... imetosha kwa leo. Tukikutana siku nyingine haitakuwa quickie, sawa? Utafurahia zaidi, kwa hiyo andaa namna ya kumkimbia bwana'ako," nikamwambia hivyo.

Akacheka kwa pumzi fulani ndefu, huku akikileta kichwa chake mpaka kifuani na kukilaza hapo kwa njia ya aibu na kudeka eti. Ih!

Nikamshika na kusema, "We', usisinzie hapa, nenda ndani. Pita hapo, me napitia huku... uende unawe huo mdomo, afu' utulie kama vile hatujuani. Usilegeze hayo macho mbele ya ndugu zako..."

Akacheka kidogo kwa furaha, naye akasema, "Sawa daddy. Nimeelewa."

Alikuwa ananiangalia kwa kurembua, naughty, nami nikamwambia, "Em' nenda huko... eti daddy..."

Yanakuwaga kama mazezeta yakishapagawa!

Akageuka na kuuelekea mlango wa nyuma ya nyumba hii hapo mbele yetu, nami nikataka kurudi kupitia huku gizani mpaka pale pale nilipokuwa nimesimama muda ule na Miryam, na ile nimeanza tu kupiga hatua na kutazama mbele, nikashtuka kiasi moyoni na kusimama ghafla baada ya kukutana na mtu mwingine ambaye alikuwa amesimama hapo. Nilihisi mtetemo uliopita mwilini shauri ya kutotarajia kabisa kumwona, na ilikuwa ni binti Mariam!





★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TANO

★★★★★★★★★★★★★★


Gari nililokuwa nimepanda lilifanya safari ya kuelekea Kigamboni huko, nami niliamua kutoshuka kabisa mpaka mwisho ambapo lingesimama. Ilikuwa kama tu siku ile ambayo nilitoka na Tesha kuja kutembelea huku, yaani likaelekea mpaka pale ambapo mimi na jamaa tulipanda daladala iliyotupeleka hadi Kariakoo, kwa hiyo na hili la sasa hivi lilikuwa la utaratibu huo.

Hivyo niliposhuka, wazo likawa kwenda "kukata tiketi" ya kupanda meli ndogo ya abiria kwenye kivuko cha bahari, kisha nikifika upande wa pili ndiyo nipande daladala ya kunirudisha mpaka Mzinga. Sikujali nani wala nini yaani; nikapanga foleni hadi ilipofika zamu yangu kupata kadi, nikaipata na kupanda meli, tukavushwa salama mpaka upande wa pili, na moja kwa moja nikaelekea stendi ya magari ambapo ningechukua daladala. Nikapanda tu moja ambayo nilikuwa na uhakika ingenifikisha Kongowe huko, na kwa utulivu tu nikaendelea kusubiri hadi pale lilipoondoka hatimaye.

Bado nilikuwa nikiwaza kuhusiana na haya mambo yote, lakini zaidi ni uamuzi wangu wa kumpigia Festo na kumwomba tuonane. Kuna vitu nilikuwa nataka kuhakikisha navipata zaidi, na jamaa alikuwa na hiyo nguvu ya kunihakikishia. Alikuwa amekubali kukutana na mimi, lakini hakusema ni wakati gani zaidi tu ya kwamba angenitafuta na kunipangia pa kukutana hivi karibuni, kwa kuwa mambo yake yalikuwa mengi mno, ratiba ilimbana. Sikuwa na namna ila kumkubalia tu, kwa hiyo kuusubiri mkutano huo na jamaa lingekuwa jambo la lazima.

Lakini hiyo haikumaanisha kwamba kwa kila jambo ambalo lilikuwa limetokea kuanzia hiyo jana nilikuwa nikitegemea Festo ndiyo awe kama suluhisho langu, hapana. Huyu alikuwa kama njia tu ya kunifikisha mahala fulani, katika sehemu fulani ya haya yote, na baada ya hapo ndiyo mengine yangefuata. Ila hata kama ingetokea kwamba jaribio langu kwake lingeshindikana, basi ningetafuta njia nyingine tu ya kutatua vikwazo nilivyokuwa naona vikija; mimi kama mimi. Kama nilivyokuwa nimeshasema, huu ulikuwa ndiyo wakati wa kuwa tayari kuchukua maamuzi mazito, na nilikuwa tayari.

Nimekuja kufika Kongowe ikiwa imeshaingia saa moja, na kutokea hapo mpaka Mzinga nikaamua kutembea tu taratibu. Kumbukumbu kadhaa zilirejea kichwani kwangu baada ya kuipita ile hospitali ambayo tulimpeleka Mariam usiku ule wa matukio mabaya kumpata yeye pamoja na Tesha, nami nikatumia muda huo kuwapigia simu akina Bi Zawadi ili kuwasalimu. Waliendelea vizuri, na Mariam akapewa simu anisalimie pia, huku nikiwaambia ningechelewa kurudi leo hivyo kuja kuonana ingekuwa mpaka kesho, nao wakaonekana kuridhia.

Sikuwa hata nimechelewa kivile, ila ni basi tu kwa muda huu sikuwa na ile amani iliyotosha kuniruhusu hata kwenda kuwatembelea wapendwa wangu hao nikishafika huko. Amani iliyokuwa imevurugwa hasa na kujikuta nafatiliwa na mtu aliyeonekana kuwa na nia mbaya kunielekea. Nilihitaji zaidi kukaa tu kivyangu, pale kwa Ankia, nipige-pige mahesabu kifikira na nini, kisha nipumzishe mwili na akili kwa ajili ya mambo mengine ambayo yangefuata.

Sijui kwa nini tu yaani ila nilikuwa nimeshaanza kuhisi kama vile kuna kitu kikubwa sana kilikuwa kinakaribia kutokea kwenye maisha yangu. Tena kibaya. Na haya yote niliyokuwa nimejiingiza kufanya ndiyo yangekuwa sababu ya kitu hicho kutokea. Kwa hiyo hisia hii ilinivuta chini mno kwa sababu kwa wakati huu ndiyo ilikuwa na nguvu zaidi, hivyo kweli ningehitaji kutuliza hisia na akili kwanza, na kwa muda uliotosha.

★★

Nimekuja kufika kwa Ankia ikiwa imeshaingia saa mbili usiku, nami nikamkuta mwanamke huyo akiwa ndani tayari pamoja na marafiki zake wale wavaa pini puani na mama Chande pia, wakitengenezeana urembo wa Yna kwa kuzichorea mikononi. Ankia pia alikuwa amechorwa, na baada tu ya kusalimiana nao nikaelekea zangu chumbani kubadili mavazi, kisha nikatoka na kwenda kujimwagia kwanza. Nikarudi ndani tena na kutulia tu chumbani baada ya kuvaa nguo nyepesi.

Aliyekuwa ananipa company zaidi kwa muda huu ilikuwa ni Dina, ambaye alinitafuta ili tuendelee na maongezi yetu yaliyokatishwa ile jioni baada ya Kevin kunipigia. Nilikuwa sijisikii hata kuchat naye lakini nikawa mpole tu kwake na kuendelea kutumiana naye jumbe fupi za kirafiki, na hatimaye akawa amefunguka kuvutiwa sana na mimi.

Dina alikuwa mwanadada mwenye akili iliyofunguka, kama tu Ankia, yaani ingawa alijua ningeweza kuwa natoka na mtu mwingine kimapenzi, alikuwa tayari kujiweka karibu nami bila kujali hilo kabisa. Ili kutofikishana mbali sana, nikamwambia ndiyo, nilikuwa na mpenzi, na isingekuwa vizuri nikimsaliti kwa kufanya uhusiano na mtu mwingine, lakini Dina akaendelea kuonyesha msisitizo wa hisia zake kwangu, japo hakuwa wa ile aina ya kulazimisha mahusiano. Alitaka tu mambo huyo!

Nikiwa nimejilaza tu kitandani kwa kuegamia mto huku nachat naye, Ankia akawa amekuja chumbani hapo, naye akasogea mpaka kitandani na kukaa usawa wa ubavu wangu huku akinionyeshea jinsi viganja vyake vilivyopendezeshwa ya michoro ya Yna.

"Imeshakauka?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kukubali huku akitabasamu.

"Umechora tattoo za waislam Ankia, hata Eid bado?" nikamsemesha kizembe.

Akaigiza kuudhika na kusema, "Si uniambie tu kama nimependeza na we' naye..."

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Ni nzuri. Inaonekana unapenda sana uislamu."

"Kwa nini?"

"Kuanzia harufu, mashosti zako, mpaka haya mambo... mbona iko wazi?"

"Wala, me mroma mroma. Siwezi kujifungia huko mie mpenda pombe," akasema hivyo.

Nikatabasamu kivivu na kutazama simu tu.

"JC, vipi? Unaumwa?" Ankia akaniuliza hivyo.

Nikamwangalia na kusema, "Hamna, niko kawaida. Mbona uulize hivyo?"

"Nimeona umeingia kama vile huna raha..."

"Nimechoka tu," nikamwambia hivyo kiupole.

"Unachoshwa na nini?" akauliza.

Nikabaki kimya wakati nikijibu jumbe ya Dina kwenye simu.

"Ndo' unachat na demu wako mpya?" Ankia akaniuliza.

"Hamna. Huyu ni rafiki yangu," nikamwambia.

"Ndiyo anayefanya kila ukiondoka unachelewa kurudi, na ukirudi unakuwa umechoka sana, si ndiyo? Huyo rafiki yako huyo?" akaongea kwa njia ya utani.

"Unaniuliza hivyo we' kama nani?" nikamsemesha kiujeuri, lakini kwa utani.

"Mimi kama mama watoto wako," akajibu.

"Unataka kipigo sasa hivi, eti? Em' nenda kawatawaze kwanza hao watoto huko..."

Ankia akacheka kidogo na kunipiga mkononi kidogo, naye akasema, "Chakula kimeiva baba. Njoo ule."

"Nitakula baadaye. Napumzika kidogo," nikamwambia.

"Mmm..."

"Nini sasa?"

"Sema tu kama umetoka umeshiba huko..."

"Yeah, nimekula saa kumi, so... bado sina njaa kivile," nikamwambia.

"Haya. Leo kweli unaonekana kuchoka, sijui hata ulikuwa unamfanya nani..."

"Halafu we' Ankia wewe, inaonekana umeni-miss tu wewe. Unawashwa-washwa sana siku hizi. Unataka nikutandike, eti?"

"Thubutu! We' mwenyewe ndiyo ulikuja na swaga za 'ooh... sasa hivi tuwe marafiki tu, hakuna kunyanduana...' hiyo ya kunitandika itoke wapi? Ndiyo imeisha hiyo mpangaji wangu. Hugusi hili sambwanda tena," akaniambia hivyo.

"Ahahahah... naona mama Chande anakulisha bangi zake," nikamwambia.

"Kwa nini?" akauliza huku akitabasamu.

"Umeanza kuongea kama yeye, kwa hiyo naona akili zenu zitafanana tu. Hilo 'sambwanda' kama halijabantalala ndani ya wiki moja tu, basi ndo' nitajua haujatembezwa naye kwenda kulipigisha makofi," nikamwambia hivyo kiutani.

Ankia akacheka kwa sauti kubwa na kugonga kiganja chake kwenye changu, naye akasema, "Eti 'bantalala!' Me siyo wa hivyo, utasubiri sana."

"Mhm... sawa."

"Haya, sisi tunaenda kula. Halafu... Adelina ameniambia mliongea," akasema hivyo.

"Alikupigia?"

"Eeeh, tumeongea leo, akasema atakuja Jumapili... ulimwalika tuje kuangalia mechi?"

"Yeah. Ni sawa akija na kulala hapa?"

"Eeh! Kwa nini isiwe sawa? Acha mambo yako bwana. Ila ndo' utunze ya kutosha. Yanga itashinda, na utaninunulia bia zote nazotaka," akaniambia hivyo.

"Ahahah... endelea kuota..." nikamwambia hivyo huku nikiendelea kuchat.

"Hahahah... haya baba, tutaona. Yaani Aziz Ki lazima afanye yake," akaniambia.

"Na limdomo lake..." nikasema hivyo kiutani.

Akanyanyuka huku akiendelea kuongea kuhusiana na mechi ya watani wa jadi ili aamshe maneno na kwa kina mama Chande huko, na mimi nikaendelea tu kuchat na Dina mpaka kufikia saa nne usiku kabisa. Ndiyo nikaamua kwenda kupakua chakula kwa muda huo, rafiki zake na Ankia bado wakiwepo, nasi tukajumuika pamoja kimaongezi japo sikuzungumza nao kwa wingi; sanasana Ankia tu na mama Chande.

Haikuchukua muda mrefu nikawa nimerejea chumbani tena, na aisee Dina hakutaka kuniacha. Mtoto alinielewa, alikuwa ameni-miss japo aliniona kwa siku moja tu, na akaelezea hamu yake kubwa ya kuniona siku ya kesho wakati ambao angekuja pamoja na dada yake, Doris, kuwatembelea wakina Miryam. Tumekuja kuagana usiku wa saa saba kabisa nikiwa nimetosha kuchat na mwanadada huyo, nami ndiyo nikaanza kuutafuta usingizi wangu.

Ijumaa ikawa imepita.


★★★


Nimekuja kuamka asubuhi kwenye mida ya saa tatu hivi, ikiwa ni Jumamosi sasa, na kama kawaida, ratiba yangu ingeanza kwa usafi wa mwili kwanza. Nilikuwa najihisi ahueni kiasi baada ya kupumzika, na nilitaka kwa leo nimezwe na mambo mengine tofauti kabisa na yale yaliyowahusu wabaya wangu, kwa hiyo ningetumia muda mwingi pamoja na Ankia na familia yake Miryam. Na nilitaka kumwona huyo Doris pamoja na Dina leo.

Kwa hiyo ikawa ni kunywa chai pamoja na Ankia hapo kwake, tukakaa kupiga story za hapa na pale huku tukiangalia TV hadi mida ya saa sita mchana, kwa kuwa leo Ankia asingekwenda dukani kwake kwa sababu alizojua mwenyewe. Hata kwa asubuhi hii, Dina alikuwa ameamka na mimi kwa kutuma jumbe za salamu, nami nikawa nikichat naye mara kwa mara mpaka aliposema kuwa yeye na dada yake tayari walikuwa njiani kuja huku Mzinga.

Nilikuwa nimejaribu kumpigia madam Bertha na kumtumia ujumbe pia, lakini hakurudisha majibu. Inaonekana bado nilikuwa nimemkwaza sana, na sijui hiyo ingeniacha wapi lakini kwa kweli ilipokuja kwenye suala la kuwa na "mtoto," tena pamoja na Bertha, kilikuwa siyo kitu cha kuchukulia juu juu. Angeendelea tu kuvimba na mimi ningeendelea kujifanya najaribu kumbembeleza, lakini nisingekubaliana naye kwa suala hilo kabisa kwa kujua mambo yaliyokuwa yakija.

Nikaamua tu kuendelea kutulia, na ilipotimia mida ya saa nane bado nilikuwa ndani tu na Ankia, wakati huu akiwa anapika ugali na samaki huko, ndiyo nikatumiwa ujumbe na Tesha. Tesha bana akaniambia kwamba Dina alikuwa ndiyo amefika, kwa hiyo niende, lakini nikamwambia 'tulia wewe.' Kujipeleka kisa wageni wamefika ingekuwa ni michoro ya hali ya juu, kwa hiyo nikamwambia ningeenda baadaye kabisa na si sasa.

Misisitizo zaidi ikaja baada ya Dina na yeye kuanza kunitumia sms kuwa niende anione, lakini nikaendelea kukaza tu. Mpaka Ankia amepakua, tukala, tukamaliza, Dina na Tesha bado walikuwa wananisumbua tu niende, niende, niende, na ilipofika mida ya saa kumi hivi jioni, ndiyo nikawa nimepigiwa simu na Bi Zawadi. Cheupe wangu. Hii ndiyo ingekuwa 'sina jinsi' yangu niliyohitaji zaidi, maana kwa mwito mmoja wa mama huyo kwenda hapo kwao kuwatembelea, jibu la moja kwa moja lilikuwa 'yes!'

Bi Zawadi alinitaka niende hasa ili anitambulishe kwa huyo Doris, ile tu kujuana mimi ni nani kwenye hiyo familia na nini, kwa hiyo mwana nikaingia chumbani kuvaa suruali na T-shirt, nikatengeneza nywele vizuri, kisha ndiyo nikatoka na kwenda mpaka hapo kwao. Nilikuwa nimemwacha Ankia akiwa ameingia chumbani kwake kulala kidogo, na nilipoingia hapo getini nikakuta gari la bibie Miryam likiwepo. Inawezekana bibie alikuwa amewahi kurudi kwa ajili ya wageni ama leo hakwenda kazini kwake, hivyo nikasogea mpaka mlangoni na kuomba kuingia kwa kusema 'hodi.'

Aliyesema 'karibu' alikuwa ni binti Mariam, na ile nimeingia tu, nikapokelewa kwa shangwe sana na binti huyu, akinikumbatia kwa nguvu kama kawaida yake. Mariam alivaa moja ya madera yake ya kawaida, na bado kunikumbatia kwake mbele ya ndugu zake namna hiyo kulinifanya nijihisi uajabu kiasi, lakini nikajitahidi kuonyesha utulivu. Ilikuwa kama vile sebule ilijaa, maana walikuwepo mama wakubwa, Mariam mwenyewe, Shadya, Tesha, Miryam, Dina, pamoja na mwanamke mwingine rika la bibie Miryam, ambaye bila shaka ndiye aliyekuwa Doris.

Nikasalimiana na wa hapo vizuri sana, nikawasalimia na wageni vizuri pia, kisha nikaenda kuketi sofani pamoja na Mariam baada ya Tesha kutuachia nafasi. Hapo sasa ndiyo Bi Zawadi na Shadya wakaanza kunitambulisha kwa wageni kwa mapambo ya hali ya juu, na mimi nikajitahidi sana kumsemesha Doris kirafiki na kumpa hongera yake ya kuelekea kuwa jiko rasmi. Alikuwa mwanamke mzuri, mweusi wa maji ya kunde kama Dina tu, akiwa si mnene sana wala mwembamba, na alikuwa na shepu ya ukweli hata kwa kumwangalia tu alipokuwa ameketi.

Wakati huu alikuwa amevalia T-shirt la mikono mifupi la kijivu lililoficha kifua chake kilichobeba maboga haswa, pamoja na suruali nyeusi iliyombana kiasi cha kuonekana kama skinny. Nywele zake alikuwa amesukia rasta nyembamba na fupi, zilizomwagika kuzungukia kichwa kama vile tambi, akiwa na macho makubwa na midomo minene iliyopakwa lipstick yenye kung'arisha. Saa yake mkononi na pete, hereni, bangili, mkufu, vilionyesha alikuwa mwanamke aliyependa vitu vizuri vyenye gharama na kupendezesha, lakini alitaka kuonekana 'simple' tu kwa watu wengine.

Baada ya kuongea kidogo mambo ya hapa na pale nikatambua alikuwa msomi, na alifanya kazi kwenye kitengo fulani maalumu huko TRA. Alikuwa na ka aina fulani ka uzungu, na niliona akikakoleza zaidi ili ile hali ya yeye kuwa 'msomi' ionekane wazi. Lakini hapa akili yangu ilikuwa imekengeushwa zaidi na Dina, kwa sababu mwanadada huyo alikuwa ananitazama utadhani nilikuwa chakula cha jioni.

Yeye alivalia shati pana kweli kupita umbo lake dogo-dogo, jeupe lenye mistari-mistari, ambalo kwa njia ya mtindo alikuwa amelifungia mbele ya tumbo lake kama fundo. Uwazi mdogo wa tumbo lake ulionekana, na yeye alikuwa amevalia suruali ya jeans ya blue iliyokoza na kurembwa na rangi nyeupe hapa na pale. Alikuwa amesuka rasta ndefu za kahawia alizoziachia mpaka huko mgongoni kwake, akisindikiza maongezi yenye kufurahisha hasa kutoka kwa Tesha na kuendelea kunitazama mara nyingi sana; nafikiri akiwa anasubiri ishara.

Bibie Miryam alikuwa akishughulika zaidi na suala la msosi, kwa kuwa alikwenda jikoni na kurudi kujumuika nasi, na yeye alikuwa amevaa kinyumbani kwa kutia T-shirt nyeusi ya mikono mifupi pamoja na khanga ngumu iliyomfunika kutokea kiunoni. Nilipenda sana jinsi ambavyo alikuwa amepaka rangi nyeusi kwenye kucha za vidole vyake vya kiganja cha kushoto, na kila mara ambayo tungeangaliana usoni, angenipa tabasamu la kirafiki, nami ningejihisi amani sana na kumrudishia pia.

Ikawa ni muda ulioneemeka sana wa kufurahia ushirika wa maongezi pamoja na familia hii ulionifanya nijihisi vizuri zaidi ya ilivyokuwa kwa siku ya jana, nami nikaendelea kuwa hapo pamoja nao hadi giza lilipoingia kuuelekea usiku.

★★

Ikiwa imekwishaingia mida ya saa moja kuelekea saa mbili, bado nilikuwa ndani hapo nikipiga story mbili tatu pamoja na Bi Jamila, Bi Zawadi, Shadya, na Doris. Hawa ndiyo waliokuwa wamenikamata zaidi kwa wakati huu, na Doris alikuwa ameshanizoea haraka. Alikuwa mcheshi pia, kwa hiyo tuliwaburudisha sana hawa wenyeji utadhani sisi ndiyo tulikuwa wazawa wa hapo. Bibie Miryam alikuwa huko nje akifanya nini sijui, halafu Tesha, Mariam, na Dina walikuwa chumbani kwa jamaa wakifanya mambo ya vijana na nini, si unajua? Ile kupatana zaidi.

Tesha alikuwa ameshanitumia jumbe kadhaa kuniambia niende huko chumbani pia nikajaribu hata kumtekenya Dina, angefanya hata kumwondoa Mariam kabisa, lakini najua alijua hiyo haingekuwa kitu yangu kukubaliana naye kabisa. Hata Dina alikuwa akinitumia sms pia kusema amefurahi mno kuniona, anatamani tuongee, lakini mimi nikaendelea kukazia fikira zangu zaidi kwa warembo hawa wengine sebuleni.

Katikati ya maongezi yangu na wanawake hawa, simu yangu ikaanza kuita, nami nikaona mpigaji kuwa mama. Nikawaomba waniekskyuzi kidogo ili nikapokee simu, kisha nikaenda mpaka pale nje varandani na kupokea. Hapo nje nikawa nimemkuta bibie Miryam, akiwa mbele zaidi kuukaribia ukuta wa uzio, na akionekana kutumia simu yake kwa ishu zake, hivyo nikaendelea kuongea na mama yangu huku nikimwangalia bibie.

Mama alikuwa ananisalimu tu, na mimi pia nikamwambia ningekuja kwenda nyumbani kabisa ili kumwona ndani ya hizi siku chache mbeleni, nasi ndiyo tukaagana baada ya hayo na umakini wangu ukarudi kwa bibie pale. Alionekana kuwa makini sana kuchat na nani sijui, nami nikaamua kumfata ili nimsemeshe kidogo. Tayari alikuwa ameniona, kwa hiyo nadhani alipoona navaa ndala zangu akafikiri ninataka kuondoka.

Akasema, "Unaenda, Jayden?"

"Hamna, nipo. Sisepi mpaka nile msosi wako," nikamwambia hivyo kiutani.

"Ahaa, sawa. Nilikuwa nafikiri unataka kuondoka, maana una katabia tukishaivisha tu ndiyo unanyanyuka kukimbia..."

"Ahahahah... Shadya atakuwa ameshanisema sana."

"Na ni kweli..." akasema hivyo huku umakini wake ukirudia simu.

Nikasogea mpaka pembeni yake na kuuegamia ukuta, nami nikasema, "Hiyo taa ya... imeungua eh..."

Nilikuwa nikimwonyesha taa ya upande ule uliolekea kwenye bomba la maji kuzungukia mpaka huko nyuma ya nyumba yao, ambayo haikuwa ikiwaka kama ya hapa mbele, naye akaangalia huko mara moja na kusema, "Eeeh, itakuwa imeungua. Tesha atakuja kubadilisha."

"Okay. Ndugu zako ni watu wazuri sana," nikamwambia hivyo, nikijitahidi kutengeneza mazungumzo zaidi.

"Nani, Doris? Eeh. Yuko vizuri," akasema hivyo.

"Ni mabinamu, si ndiyo? Na ni upande wa baba au mama?" nikamuuliza hivyo.

"Aaa... ni... ukoo wa baba sanasana..." akajibu hivyo huku akiwa bize na simu.

"Ahah... sorry, inaonekana uko bize, nakuvuruga tu hapa. Ngoja ni...."

"Oh no, haunivurugi wala. Nilikuwa tu na... natuma email hapa... nimemaliza," akasema hivyo na kuniangalia.

Nikatoa tabasamu hafifu.

"Na wewe? Ulikuwa unaongea na nani kwenye simu? Baby?" akaniuliza hivyo kiutani.

"Aa wee... ahahahah..." akanifanya nicheke kidogo.

Yeye pia akacheka kidogo.

"Sinaga habari hizo mimi..." nikamwambia.

"Mmm, sawa," akafanya hivyo kikejeli.

"Ilikuwa ni mama bwana. Alikuwa ananisalimia," nikasema hivyo.

"Aaa, kumbe ndiyo maana. Nimesikia unaongea kwa sauti ya kudeka, nikafikiri ni baby," akanitania.

"Ahahah... hapana. Me niko single," nikaongea kwa kujitutumua.

"Mmmm..." akafanya hivyo.

"Nini sasa, hutaki?" nikamuuliza hivyo nikiwa najihisi raha sana kuongea naye namna hii.

"Mhm... haya bwana. Mama hajambo?" akabadili mada.

"Eeh, yuko poa. Wako tu sa'hivi wanasubiria dada yangu ajifungue."

"Ooh, kumbe dada yako mjamzito?"

"Ndiyo. Sikuwahi kukwambia?"

"Hapana, ulishasema tu kwamba una dada, sikujua kama anakaribia kujifungua," akasema hivyo.

"Well, yupo karibu sana kujifungua. Kama siyo mwezi huu, basi ujao mwanzoni," nikamjulisha.

"Okay. Hongera kwake. Na yupo na mama na baba yenu?"

"Yeah."

"Sawa. Uliwahi kusema nyie mme... tokea Mwanza eh? Familia nzima yaani?"

"Aaa... ni mimi, dada yangu Jasmine, na mama sanasana. Dar es Salaam tumekuja hasa baada ya mama kufunga ndoa na huyu mzee wetu miaka kadhaa iliyopita..." nikamweka wazi.

"Ahaa..."

"Eeeh. Mume wake na mama yangu ndiyo... aliyefanya mama na dada wakaja Dar, ila me tayari nilikuwa nimeshakuja huku na wao walipofika pia," nikamwambia hivyo.

"Sawa. Ni vizuri. Na huyo mzee wako yuko poa eh?" akauliza hivyo.

"Sana. Yuko peace mno. Amenisaidia kwa vitu vingi, mpaka hapa nilipo amechangia kwa mengi sana," nikamwambia hivyo.

"Je... baba yako mzazi kabisa?"

Nikaangalia pembeni kwanza na kusema, "Simfahamu."

"Kwa nini?" akauliza hivyo.

"Sikuwahi kumwona. Alinitelekeza mimi na Jasimine tukiwa wadogo mno, yaani... alimwacha tu mama... akaenda wapi sijui... ndiyo hivyo, mpaka leo," nikamwambia.

"Pole kwa hilo," akasema hivyo.

"Hamna tabu wala," nikamwambia.

"Kwa hiyo mlilelewa na mama yenu peke yake? Hujawahi kumtafuta baba yako?" akaniuliza.

"Wa kazi gani sasa?" nikamuuliza pia kwa sauti tulivu.

Akabaki kimya na kuendelea kunitazama kwa utulivu.

"Jasmine alikuwa na miaka miwili sijui, na mimi bado hata nilikuwa sijaanza kusimama, jamaa akakimbia. Maisha hayakuwa rahisi kwa mama kutulea akiwa peke yake, na hakuwahi kumtafuta, sijui... msaada? Hapana. Alipambana, na Mola akamsaidia, tukakua, tukafika sehemu... na yeye sasa hivi yupo sehemu yake ametulia. Ya nini tena kuanza kusumbuka kutafuta watu wasiojali kutuhusu?" nikamwambia hivyo.

Akaonekana kutafakari maneno yangu kwa ufupi, naye akasema, "Kwenye maisha hata mie nimeshajifunza kupokea na kuthamini zaidi kile nachopata kwa kuwa nakihitaji, siyo kukitaka. Hata me sikumpata baba niliyemtaka, ila nikapewa baba niliyemhitaji, na kwa hilo nikaridhika. La muhimu tu ni kuridhika, na naona ndivyo ilivyo kwako. Kama inakupa amani zaidi usipohangaika kumtafuta, basi hiyo ni sawa," Miryam akasema hivyo.

Kauli yake ilieleweka, lakini sikuelewa vizuri sana alimaanisha nini aliposema hivyo kumhusu baba yake yeye, nami nikataka kuulizia upana wa maana ya maneno hayo.

Nikasema, "Ndiyo, ni kweli unavyosema. La muhimu ndo' hilo, sionagi faida kuangalia hayo mambo, nimeridhika na jinsi maisha yanaenda kwa uweza na baraka za Mola..."

Akatikisa kichwa chake taratibu kukubaliana na hilo.

Nikaanza kumuuliza, "Ila, Miryam... umemaanisha nini uliposema kwamb..."

"Mimiii..."

Sauti ya Bi Zawadi kutokea ndani ikasikika ikimwita bibie namna hiyo, naye akaitika.

"Bee... ngoja nione ikiwa wageni wanahitaji kitu fulani, na... ninapakua muda si mrefu, usikimbie," Miryam akasema hivyo na kuanza kuondoka.

Nikamtikisia kichwa kukubali hilo huku nikitabasamu, naye akaelekea ndani kwao.

Nikaendelea kusimama hapo nikiwa nimeegamia ukuta, tafakari za mambo mengi yaliyohusiana na maongezi yangu na bibie Miryam zikiwa zinazunguka kichwani, kisha nikatoa simu kuangalia muda na kukuta ni saa mbili kasoro robo hivi. Nikawaza labda tu nielekee hapo ndani pia, sijui walikuwa wamemwita Miryam kwa masuala ya kuivisha, lakini jambo fulani likavuta umakini wangu.

Kutokea upande ambao ulielekea kwenye bomba la maji nje ya nyumba hii, jicho langu likaanza kuona kama mwanga fulani uliokuwa ukishtua-shtua, nami nikatazama huko na kutambua kwamba ilikuwa ni mwanga wa tochi ya simu uliozimwa na kuwashwa kwa makusudio ya kuvuta uangalifu wangu. Kwa sababu taa ya upande huo ilikuwa imeungua na kutobadilishwa bado, isingekuwa rahisi kumwona usoni aliyekuwa akinifanyia hivyo, lakini nikamtambua. Ilikuwa ni Dina.

Alikuwa ameegamia ukuta wa nyumba uliokaribiana na ukuta wa uzio kuelekea nyuma kabisa ya nyumba hii, na kwa kuwa yeye angeweza kuniona mimi hapo nilipokuwa nimesimama, nikamtolea ishara kwa mkono kuwa aje, lakini yeye ndiyo akatoa ishara kuwa nimfate. Yale mambo ya 'kumchum kumchum,' yaani nyatia nyatia.

Nikaona isiwe shida, nikaenda hadi hapo, naye akasogea mpaka usawa wa sehemu ambayo kulikuwa na chumba cha nje ambacho ndiyo kilitumiwa kutunzia vifaa vingi vya nyumbani, stoo yaani, na kijengo chake kidogo kiilifanya njia ya kuzungukia mpaka huko nyuma ya ukuta wa uzio iwe nyembamba, na yeye ndiyo akasimama hapo. Inaonekana alikuwa ameniita kwa yale madhumuni ya 'sisi wawili tu,' na kulielewa hilo kukanifanya nimkaribie zaidi na kumsemesha kwa sauti ya kunong'oneza.

"Vipi Dina?"

Alikuwa ameukunjia mguu wake mmoja mbele huku mikono akiiegamiza ukutani, naye akajibu kwa kunong'oneza, "Ndiyo nimepata nafasi kuja nje... nikakuona."

"Umepitia mlango wa huku nyuma?" nikamuuliza.

"Eeh..."

"Nani kakufungulia? Tesha?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Dah! Mbona unataka kunitia majaribuni afu' tuko kwa watu?"

Akatabasamu na kuuliza, "Majaribu yapi tena?"

"Kwani we' umeniita gizani ili iweje?"

"Si ili nikuone?"

"Kwenye mwanga ulikuwa hunioni?"

Akacheka kidogo na kuuziba mdomo wake eti kwa madoido.

"Wanafanya nini ndani sa'hivi?" nikamuuliza.

"Wamemwita aunty Miryam ili waongee kidogo, halafu wapakue sijui... me ndiyo nikachomoka," akasema.

"We' chautundu kumbe? Halafu unajifanya malaika..." nikamtania kidogo.

Niliweza kuona Dina akitabasamu kiasi na kung'ata mdomo wake wa chini, kisha akashika T-shirt langu kwa kidole kimoja sehemu yenye uwazi shingoni na kuanza kulivuta kumwelekea. Ilikuwa wazi kwamba alitaka nimfate mdomoni ili tupige busu, nami nikaona isingekuwa mbaya kuionja midomo yake kwa mara ya kwanza.

Nikaifata na kuanza kunyonyana naye midomo, ulimi, meno yakigongana, huku nikiwa nimekishika kiuno chake, naye akajisogeza karibu yangu zaidi na kuizungushia mikono yake mgongoni kwangu. Kwa sababu alikuwa mfupi ilinihitaji kuinama kiasi ili asinyanyue miguu yake, na tayari hamu ilikuwa imenipanda mno kufanya msuli wangu ukaze ile mbaya, na ukikandamiza tumbo lake kwa nguvu.

Hatimaye nikaivunja busu hiyo na kugeuka nyuma kuangalia usalama, kisha nikamtazama na kusema, "Aisee... Dina! Umeniwashia balaa."

"Mhm... unataka nilipoze?" akasema hivyo na kuishika mashine yangu ikiwa ndani ya suruali, kisha akawa anasugua-sugua hapo.

Nikamwambia, "Hapa jau. Tutapanga siku nyingine."

"Me naitaka hiyo jau sasa hivi..." akasema hivyo.

"Dina!" nikashangaa.

"Kidogo tu..."

"Dina, mazingira. Tutakutana siku nyingine..."

"Kidogo tu JC..." akawa ananibembeleza kama vile anataka kulia.

"Tuko kwa watu Dina, umekuja kama mgeni... kwanza ndo' wanapakua. Wakikutafuta wakatukuta? Halafu kwanza me nimebanwa kukojoa..."

"Nikojolee tu mimi..."

"Wewe!" nikamshangaa.

Akaendelea tu kupasugua pale pagum-gum.

Nikamuuliza, "Kwa hiyo utarudi ndani unanuka mikojo? Mbona umekuwa hivi?"

Akasema, "Nina hamu sana na wewe, JC. Na ni muda mrefu..."

Masikini! Mpaka nikamwonea huruma. Mwanadada alionyesha kuwa na hamu kali kwelikweli, na mimi ningekuwa nani kumnyima msaada? Eti?

Pamoja na kuwazia usalama wetu kutokana na mazingira, nikaamua nimpe utamu angalau kidogo. Nyakati kama hizi ndiyo mwanaume unatakiwa uchukue maamuzi ya haraka kwa kutumia akili, na ujanja unahusika pia. Hapo nilikuwa sijambo.

Nikaona nimsogeze Dina nyuma zaidi ili tujibananize kwenye kile kinjia cha kuelekea nyuma, na nikamfikisha kwenye sehemu ambayo ukuta ndiyo ulikunja kona. Kwa hiyo, mimi nikawa nimesimama upande huu ambao tulikuwa, huku mwili wake ukiwa kwa upande ule wa nyuma, kwa hivyo ingekuwa rahisi kuona kama mtu angekuwa anakuja upande wangu au upande wake.

Dina alikuwa ameshaanza kuhangaika na zipu ya suruali yangu, lakini mimi nikaishika mikono yake na kuugeuza mwili wake ili anipe mgongo, halafu yeye akajiongeza na kuanza kuishusha suruali yake na kinguo chekundu alichovalia kwa ndani. Alikuwa na mwili mweusi, na upande huu wa nyuma taa ilikuwa ikiangaza, lakini ukuta ulituficha vizuri. Nilikuwa nahisi msuli wangu umekaza ile mbaya, si unajua mara ya kwanza na mtu mwingine inavyokuwa? Maua!

Mtoto akauegamia ukuta huku akinibinulia kalio lake lisilo kubwa sana, nami nikafungua suruali yangu pia na kuishusha, nikiiachia mashine itambe. Hapa shida kubwa ingekuwa mbu, walipiga kelele yaani utafikiri kulikuwa na sherehe, lakini siye hatukuwajali hata kama wangeng'ata vipi.

Dina akapandisha mshati wake juu vizuri huku akijaribu kunigeukia ili aniangalie, nami nikaanza kuichokonoa mambo kutokea nyuma kwa vidole vyangu, na ilikuwa imelowana haswa. Nikapakaa kidogo ute huo kwenye msuli wangu, kisha nikakiingiza kichwa kidogo ndani yake na kumshika mgongoni kwa mkono mmoja kama namkandamiza ainame chini zaidi. Hakuwa mbishi. Nikaanza kuingiza mtambo ndani zaidi na kukuna taratibu tu, kisha nikakishika kiuno chake kwa mikono yote na kuanza kukoleza raha.

(..........).

(..........).

(..........).

Yeye mwenyewe alionekana kufurahia za taratibu, na mimi nilikuwa makini kuangalia huko mbele na huku nyuma kuhakikisha usalama, na show ikaendelea kwa dakika kama tano hivi, kisha nikaichomoa mashine. Bado ilikuwa imewamba, lakini nilitaka kumwambia Dina tuishie hapo. Sasa sijui shauri ya mazoea?

Kabla hata sijamsemesha, mwanadada akanigeukia na kuchuchumaa, naye akaishika mashine na kuitumbukiza mdomoni mwake. Ai kudadeki! Maneno yakapotea.

(..........).

(..........).

Pamoja na umbo lake lisilo kubwa lakini mtambo wangu mrefu ulikuwa unazama wote, na inaonekana aliufurahia zaidi ulipofika kwenye mabandama huko. Akalishika T-shirt langu na kuling'ang'ania kwa nguvu huku akijitahidi kunigeukia na kuniangalia, na macho yake yalikuwa yamelegea haswa.

Niliridhika tu kwamba hakutoa sauti ya juu sana maana kule ndani walitulia, na utamu kolea, utamu kolea, changu cha kwanza chenye kiherehere kikaja upesi ndani ya dakika saba tu. Nilikuwa natamani nijiachie ndani yake yaani, ila... hapana. Sikuwa na uhakika kuhusu faida na hasara za jambo hilo kwa huyu dada. Nikamwonya tu kuwa mi' nakaribia, naye akafanya kitu ambacho sikuwa nimetarajia.

Akajichomoa na kunigeukia tena, kisha akachuchumaa na kuishika mashine hiyo, halafu akaanza kuinyonya na kuichua haraka-haraka sana. Dah! Alitaka nishushe mzigo, na alitaka niushushie mdomoni mwake. Alikuwa ameshaangalia ujinga mwingi wa wazungu huyu mtoto kama siyo kuufanya!

(.........). Kumwangalia Dina, nikakuta akiwa analamba mashine yangu huku ikionekana kila kitu alikuwa amekunywa. Kila kilichotoka! Aisee, kweli hiyo ndiyo ilikuwa hamu. Na siyo mbaya, mtoto akawa ameongeza glucose mwilini.

Baada ya hiyo pindi yenye kusisimua, nikavuta suruali yangu, naye pia akasimama na kujiweka sawa zaidi. Nikamtazama usoni na kuona jinsi ambavyo aliniangalia kwa njia iliyoonyesha furaha, ile ya kimahaba, nami nikamfuta mate kidogo pande za mdomo wake.

"Nenda ndani sa'. Umeridhika?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa mara moja kukubali.

"Au unataka tuendelee?" nikamuuliza tena.

Akatikisa nyusi kukubali.

"Oh no... imetosha kwa leo. Tukikutana siku nyingine haitakuwa quickie, sawa? Utafurahia zaidi, kwa hiyo andaa namna ya kumkimbia bwana'ako," nikamwambia hivyo.

Akacheka kwa pumzi fulani ndefu, huku akikileta kichwa chake mpaka kifuani na kukilaza hapo kwa njia ya aibu na kudeka eti. Ih!

Nikamshika na kusema, "We', usisinzie hapa, nenda ndani. Pita hapo, me napitia huku... uende unawe huo mdomo, afu' utulie kama vile hatujuani. Usilegeze hayo macho mbele ya ndugu zako..."

Akacheka kidogo kwa furaha, naye akasema, "Sawa daddy. Nimeelewa."

Alikuwa ananiangalia kwa kurembua, naughty, nami nikamwambia, "Em' nenda huko... eti daddy..."

Yanakuwaga kama mazezeta yakishapagawa!

Akageuka na kuuelekea mlango wa nyuma ya nyumba hii hapo mbele yetu, nami nikataka kurudi kupitia huku gizani mpaka pale pale nilipokuwa nimesimama muda ule na Miryam, na ile nimeanza tu kupiga hatua na kutazama mbele, nikashtuka kiasi moyoni na kusimama ghafla baada ya kukutana na mtu mwingine ambaye alikuwa amesimama hapo. Nilihisi mtetemo uliopita mwilini shauri ya kutotarajia kabisa kumwona, na ilikuwa ni binti Mariam!





★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
Mariam kashuhudia show au inakuaje?😳😳
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Siri, Tamaa, Hila, Usaliti, Ukatili, Mauaji, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA SITA

★★★★★★★★★★★★★★


Hee! Mariam alikuwa amefika hapo saa ngapi? Dakika chache za kutoangalia upande huu zilikuwa zimetosha kumweka hapo, na sikuwa na uhakika alikuwa ameona ama kusikia nini. Yaani kujua tu kwamba angeweza kuwa ameona ama kusikia niliyokuwa nimetoka kufanya, kukanipa hisia mbaya moyoni. Na alikuwa akinitazama usoni kwa umakini kiasi.

Lakini nikajitia usabuni na kusema, "Mamu? Mbona umekuja hapa? Vipi?"

Akiwa ananiangalia kwa njia ya kawaida sasa, akasema, "Nilikuja... kukuita, tukale."

"Aaaa... sawa. Umekuja hapa zamani? Mbona hujaniita sasa?" nikajitoa akili kuuliza hivyo.

Akaangalia chini huku akianza kuvifikicha-fikicha vidole vyake, kama vile anaona aibu. Duh!

"Eti? Mbona hujaniita sasa?" nikamuuliza tena.

Akasema, "Niliogopa."

Nikamuuliza, "Unaogopa nini Mamu?"

"Nim... nilikuwa... nasubiri... umalize... kojoa..." akasema hivyo.

Ahueni ikiwa imeingia ndani yangu kiasi, nikamwambia, "Aaa... sawa. Haina shida, usi... usiogope wala."

Akaniangalia usoni kwa macho yenye ugeni fulani hivi.

"Kwa hiyo ulikuwa tu unasubiria nimalize kukojoa ndiyo uniite, eh?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kukubali.

"Sawa. Nimemaliza. Ila... usimwambie dada na mama mkubwa kama umekuta nakojoa huku, eti? Watanichapa," nikamwambia hivyo kwa ule ushawishi wa kitoto.

Akatikisa kichwa kukubali, nami nikamshika begani na kumwambia tuelekee ndani ili kupata chakula sasa.

Inaonekana nilikuwa nimeponea chupuchupu, ila sikuwa na uhakika sana. Ikiwa Mariam angekuwa amesikia ama kuelewa yaliyofanyika baina yangu na Dina, basi ningekuwa nimeiingizia akili yake jambo fulani ambalo halikutakiwa kabisa kumwingia kwa wakati huu, yaani ingemvuruga. Lakini nilitumaini kuwa haikuwa hivyo, maana binti hakuwa mwongo, kwa hiyo tukaenda ndani kujiunga na wengine kwa ajili ya msosi. Ikawa kama vile hakuna chochote kilichokuwa kimetokea baina yangu na mwanadada Dina.

★★

Kwa hiyo sote kwa pamoja tukapata msosi mtamu kabisa kutoka kwa mpishi maridadi, bibie Miryam, na wageni walifurahia sana na kumsifu Miryam kwa ubunifu wake katika mapishi. Katika mazungumzo, Bi Zawadi akawa ameniambia kuwa kesho angekwenda tena kule Chamgando kuhudhuria ibada kanisani, na kama nilivyokuwa nimemwahidi mama mchungaji, basi na mimi ningepaswa kwenda naye. Na nilikuwa nimesahau, lakini baada ya kukumbushwa hivi, nikamwambia tungekwenda pamoja bila shaka. Ndiyo akawa ameniambia kwamba hata Mariam angekwenda pamoja nasi kesho.

Kulikuwa na kitu kilichoniambia kwamba suala langu na Dina pale nje lilikuwa limechafua hali ya hewa kwa wengine kiasi, maana nilihisi kama vile Mariam alijua, ila ni kama tena hakujua, yaani alikuwa ameanza kunitendea kwa njia fulani ya woga woga hivi; siyo ule woga wa kukuta tu mtu anakojoa nyuma ya nyumba yao. Ikiwa alijua nilichokuwa nimefanya na Dina, basi angeanza kunichukulia kwa mtazamo tofauti kabisa, na sikujua hiyo ingeathiri vipi ufahamu wake kiujumla.

Mpaka tunamaliza kula na kurudi kukaa tena masofani, Doris pamoja na Dina wakaendelea kuwa hapo kumalizia matembezi yao kwa story chache zilizohusiana na kitchen party ya mwanamke huyo, na pia alikuwa ameshaalikwa kuhudhuria birthday party ya Bi Zawadi hapa nyumbani na kukubali kuja pamoja na watu wengine wa familia yake. Niliendelea pia kuwa hapo mpaka mida ya saa tatu na nusu hivi, ndiyo wageni wakaaga hatimaye.

Tukanyanyuka kwa pamoja ili kuwasindikiza kuelekea nje, na inaonekana Shadya angelala hapa leo, kwa hiyo baada ya Doris na Dina kuwaaga wote kwa upendo, Miryam, Tesha na mimi tukawatoa nje na kutembea nao mdogo mdogo kuelekea huko barabarani ili wakapande daladala.

Tesha alikuwa anajua kuhusu ishu yangu na Dina, maana yeye ndiye aliyekuwa mtengeneza mitambo, lakini ingawa nilitembea kwa ukaribu na wawili hawa sikuonyesha hulka yoyote ile kumwelekea Dina, ambaye naye alitulia kama vile haikuwa yeye aliyekuwa amekunywa glucose zangu. Nilipendezwa zaidi kuwasikiliza Miryam na Doris walipokuwa wakizungumza kirafiki sana. Sanasana Miryam. Yaani alijiachia kiasi, nikaanza kuona utu wake mwingine uliojaa uchangamfu alipotaniana kidogo na mwenzake na jinsi alivyofurahia sana ushirika wake.

Nilipenda mno yaani kumwona akifurahi, mara kwa mara nikimtazama kwa kuibia ili niendelee kuhisi raha niliyokuwa nahisi kwa kumwangalia tu, na kiukweli mpaka nikajishangaa. Yaani, nilikuwa tu nimeanza kujihisi kuwa mtu mwingine kabisa pindi zote ambazo ningekuwa karibu na mwanamke huyo, na ni kitu nilichokuwa najaribu kupotezea sana lakini, hakikuwa mbali na mimi kabisa; hasa kwa pindi kama hii.

Tulipowafikisha barabarani na kuwaacha wakivuka kwenda kuchukua usafiri, sisi watatu tukaanza kurudi nyuma. Tukiwa njiani, Tesha akawa akizungumzia hasa kuhusiana na mechi ya kesho.

"Dah, kaka! Nina hamu kubwa kinyama ya kuitazama hiyo mechi pamoja nanyi wote, yaani naona kama kesho haifiki," Tesha akasema hivyo.

"Itafika tu. Me mwenyewe nina hamu kweli," nikamwambia hivyo.

"Tena na hivi Adelina wako anakuja? Bia kama zote tukishashinda. Najua umejiandaa," Tesha akaniambia.

Nikacheka kidogo kwa pumzi na kutikisa kichwa.

"Adelina ndiyo nani?" Miryam akawa ameuliza.

"Ni dada yake na yule Joy," nikamwambia.

"Ahaa... sawa," bibie akasema hivyo.

"Haumjui na yeye?" Tesha akamuuliza.

Miryam akatikisa kichwa kukubali.

"Umeshawahi kumwona," nikamwambia hivyo Miryam.

"Wapi?" akaniuliza.

"Aliwahi kuja kwa Ankia. Siku ile tumeacha funguo na Tesha kwa Ankia, ulipokuja kuzichukua uka..."

"Oooh, sawa. Yule dada mrefu mrefu?" Miryam akaonyesha kukumbuka.

"Yeah," nikamjibu.

"Ndiyo dada yake na Joy kumbe?" akauliza.

"Eeeh, ndiyo dada yake. Kesho anakuja. Anamwelewaga kweli JC, lakini jamaa hamtaki," Tesha akasema hivyo.

Nikamwona Miryam anatabasamu kiasi na kutikisa kichwa chake, nami nikamsukuma Tesha begani kidogo na kumwambia, "Acha mambo yako wewe. Yule dada ni rafiki yangu tu. Me sinaga hizo habari kabisa."

Niliposema hivyo, Miryam akanitazama usoni kwa ile njia ya kuhukumu huku akitabasamu, nasi kwa pamoja tukacheka kidogo.

Tesha akasema, "Ila vibe kama lote akija, na yeye apunguze stress na nini, si unajua? Halafu da' Mimi..."

"Mm..." Miryam akaitika.

"Si na wewe tu uje na sisi kuangalia mechi kesho?" Tesha akasema hivyo.

Nikamwangalia bibie. Hilo lilikuwa wazo zuri!

Miryam akasema, "Sidhani kama nitakuwa na muda..."

"Aaaa, kesho si Jumapili? Tena mechi saa moja jioni... unaenda wapi kwani?" Tesha akasisitiza.

"Siwezi kujua nitakuwa wapi, siwezi kujua. Na... mnaenda kwenye klabu kuangalia mechi, si ndiyo? Me siwezi kwenda huko," Miryam akasema hivyo.

Mimi na Tesha tukacheka kidogo, nami nikamwambia, "Ni Masai tu hapo Miryam. Siyo klabu. Itakuwa fresh ukijiunga nasi, usikilize falsafa za mpira na nini..."

Miryam akanitazama usoni na kutabasamu kiasi. Alikuwa ameelewa upana wa maana ya maneno yangu, nami pia nikatabasamu kidogo.

"Eeh Mimi... uje tu. Na we' dada unahitaji kutuliza stress, eh? Nimemiss sana kipindi kile ulipokuwaga unakuja na sisi Masai kunywa kidogo, unatetemesha macho ya watu, safi," Tesha akasema hivyo.

Miryam akatabasamu zaidi. Nilipenda sana kumwona namna hiyo.

Tesha akasema, "Baada ya huo upuuzi wote wa Joshua, dada unahitaji kutuliza akili na wewe from time to time, au siyo? Kesho ndo' nafasi nzuri sana..."

Nikaona Miryam akiweka uso wa kuishiwa pozi kiasi, na najua hilo lilisababishwa na mdogo wake kumsema Joshua. Nikamfinya Tesha mkononi kwa nguvu, naye akanitazama kimaswali na mimi nikamkunjia sura kama kumwambia ameenda mbali mno.

"Sawa, nitakuja kesho," Miryam akasema hivyo.

Sote mimi na Tesha tukafurahi sana baada ya kusikia hivyo.

"Ila mie sinywi bia, nakunywa wine. Kwa hiyo mjipange," Miryam akatania.

"Ah, ondoa shaka Mimi. JC yupo... na yupo tayari," Tesha akasema hivyo.

Nikamkata jicho kali kimasihara, naye Miryam akatabasamu kwa hisia.

Alifanya nihisi furaha sana baada ya yeye kusema angejiunga nasi kesho, na Tesha ndiyo akaanza kuniambia kuwa dada yake ni mpenzi wa Yanga kama Ankia lakini aliachana na ushabiki wa mpira kitambo tu, hivyo tungehitaji kujua kesho angekuwa upande upi. Akasema ingawa hakufatilia mipira sana, bado aliipenda Yanga, kwa hiyo kesho angekuwa mtani na adui yetu sisi wanasimba.

Tukawa tumefikishana makwetu hatimaye, nami nikaagana na wawili hawa na kwenda huko kwa Ankia kupumzika nikiwa nahisi furaha sana moyoni. Furaha ambayo ilikuwa inazidi kukua tu kwa kutambua jambo fulani jipya lililokuwa limetokea ndani yangu mimi mwenyewe, lakini bado uhakika wa ikiwa ningetakiwa kuendelea kuifurahia hiyo furaha ndiyo sikuwa nao. Nikatumia muda mfupi tu kupeana ushirika na Ankia, kisha ndiyo nikaelekea kulala.


★★★


Jumapili ikakucha. Nilijitahidi kuamka mapema hasa kwa kuwa nilijitahidi kulala mapema pia, na baada ya kumaliza usafi wa mwili, nikatia viwalo vya ukweli mwilini, Tshirt jeupe la mikono mirefu na suruali nyeusi ya jeans, saa yangu kali mkononi pamoja na kiatu changu cheupe miguuni, nami nikakaribishwa chai kavu ya mapema na mwenye nyumba wangu ambaye kama kawaida yake alikuwa ameshaamka na kuanza kuandaa mambo. Ilinibidi ninywe kavu tu kwa sababu hakukuwa na kitafunwa, na hata alipotaka kunifatia mkate nikamwambia asiwaze.

Hii ikiwa ni saa mbili na nusu asubuhi, nikachukua simu yangu baada ya kumaliza kupasha tumbo ili niende sasa kuwapitia wakina Bi Zawadi, na sikukuta simu wala jumbe yoyote ile kutoka kwa madam Bertha, ikionekana bado kanuna, hivyo nikamrushia sms fupi ya salamu nikimwambia nimem-miss.

Waliokuwa wamenitafuta tayari asubuhi hii ilikuwa ni yule Kevin, Dina, Bi Zawadi, pamoja na Soraya, na aisee Soraya nilikuwa nimemtenga sana. Ila hata sasa nikaamua kuachana na hao wengine na kumpigia Bi Zawadi kumwambia ninakuja sasa hivi, kisha ndiyo nikamuaga Ankia na kuondoka hapo.

Kabla sijalifikia geti, Adelina akawa amenipigia, nami nikatabasamu kiasi na kupokea. Alianza kwa salamu na kusema sasa hivi alikuwa anaenda ibadani, nami nikamwambia vilevile na mimi pia nilikuwa naelekea kwenye ibada. Akagusia kuhusu suala la kuja huku baadaye kwa ajili ya kujiunga nasi, akisema sanasana jioni, nami nikamwambia angetukuta tunamsubiri kwa hamu, kisha tukaagana vizuri kwa utani kidogo.

Nilipofika getini kwa majirani zetu, nikakuta bado kimlango cha geti kikiwa kimefungwa kwa ndani, kwa hiyo nikagonga na kusubiri. Aliyekuja kunifungulia alikuwa Tesha, na mwonekano wake uliniambia kwamba yeye pia alitaka kutoka. Alivaa vizuri yaani, na kiatu mguuni, nami nikauliza ikiwa na yeye angekwenda kanisani ama alikuwa amejiandaa ili aende kwa Happy huko Tandika.

Ndiyo akaniambia kwamba wote tulikuwa tunaenda kanisani leo, ukitoa tu Bi Jamila na Shadya, kuanzia mimi, yeye Tesha, Mariam, Bi Zawadi, pamoja na Miryam, tungekwenda huko kanisani. Lilikuwa jambo zuri sana kuwaza kuwa ningepata nafasi zaidi ya kuwa karibu na Miryam kwa leo, basi tu yaani nilipenda. Nikamwambia jamaa hiyo ilikuwa poa sana, na ilieleweka kwa nini Bi Jamila angebaki, pamoja na Shadya ambaye angemsaidia kwa mambo ya hapa na pale mpaka wakati ambao tungerejea.

Walikuwa wameshakunywa chai tayari, yaani Tesha akaniambia Miryam alikuwa ameshughulika na mambo mengi upesi sana kwa asubuhi hii mpaka wote kukamilisha maandalizi, kwa hiyo nilikuwa nikisubiriwa mimi tu ili twende. Na kweli kabla hata sijaenda ndani, binti Mariam akawa ametoka, akipendeza kwa kuvalia gauni refu jekundu na kilemba kichwani kama mwanamke yaani, nasi tukasalimiana vizuri na yale ya jana kuonekana kuwa yamesahaulika kwake.

Wakafata na wengine pia, Bi Zawadi akipendeza kwa gauni la kitenge lenye rangi mchanganyiko za mimea, na bibie Miryam akiwa amevaa gauni refu la samawati lililokuwa laini na lenye mtindo wa kufunika bega moja, na lingine wazi. Aliziachia nywele zake laini mpaka mgongoni, akiwa amezilainisha zaidi kwa mafuta nafikiri, nami nikajikuta nimebaki kumtazama tu kwa upendezi wa hali ya juu mno.

Miryam alikuwa mrembo jamani! Halafu wala, yaani ni kama hata alikuwa hana habari na hilo. Kukamata mpaka hisia za mwanaume hatari kama Festo, sidhani ikiwa huyu mwanamke alielewa ama kujali ni namna gani alivyokuwa na mvuto mkubwa sana wa kumfanya amiliki ama kuwa katika sehemu za gharama ya hali ya juu. Yaani, alikuwa wa gharama, lakini alipenda kuwa simple. Familia yake kwanza, na hilo ndiyo lililomwongezea mvuto si kwenye urembo wa sura yake tu, bali na utu wake pia.

Nikasitisha kumwazia sana baada ya Shadya kututaka tupige picha za pamoja kwanza kabla ya kuondoka, na Miryam alikuwa hataki lakini Mariam akamlazimisha. Tukapiga picha kwa pamoja usawa wa gari la bibie, na ndiyo lingetumiwa kutupeleka mpaka Chamgando, hivyo tulipomaliza tukapanda na Miryam akaliondoa hapo. Nikawa nimeketi siti za nyuma pamoja na Tesha na Mariam, tukipiga story na Bi Zawadi aliyekuwa ameketi mbele na bibie Miryam, na safari ya kwenda kanisani ikaendelea.

Siku ya leo ilionekana kuelekea pazuri mno, nilihisi hivyo. Matarajio mengi niliyokuwa nayo baada ya mikasa yote mibaya ya pembeni kuisha, yalikuwa niwe na pindi zenye kuburudisha na kujenga kama hii tu ya sasa, na kwenda kumwomba Mungu abarikie hilo kwa leo ndiyo ingekuwa jambo kuu.

★★

Basi, tukawa tumefika huko Chamgando kwenye mida ya saa nne, tukiwa tumekawizwa kiasi barabarani kutokana na msongamano wa dakika kadhaa. Tulifika kanisani na kukuta mchungaji akiwa ameshaanza maombi yake, ibada ile ya kutoa hotuba, na yaani ujio wetu hapo ulifanya wadau watutazame mno kutokana na kuonekana kuwa kama familia moja ya wanajamii wa hali ya juu. Watu walikuwa wengi kiasi kwa hii Jumapili tofauti na ile Alhamisi nilipokuja hapa na Bi Zawadi, na mama huyu alikuwa na furaha sana sisi wote kuwa pamoja naye sehemu hiyo.

Tukaachiwa nafasi za kukaa, mimi nikiwa katikati ya Bi Zawadi na Mariam, kisha Miryam na Tesha pembeni zaidi, naye mchungaji akaona akatishe hotuba yake kwa ufupi ili kutupa nafasi ya kujitambulisha kwa waabudu wengine. Najua wengi walikuwa na hamu ya kutusikia wageni tukijitambulisha, na kwa sababu nilijua Mariam angehisi uzito kiasi wa kutojua ya kusema, nikaona nisimame kwanza huku nikimshika mkono, kwa hiyo na yeye akasimama pamoja nami.

Nikasema jina langu, mahali tunakoishi pamoja na huyu mdogo wangu, na shukrani kwa mchungaji kutukaribisha hapa kwa ajili ya ibada, nao waamini wakanipigia makofi kwa shangwe. Nikamnong'oneza Mariam kuwa aseme jina lake, naye akajitahidi kusema 'ninaitwa Mariam' kwa sauti iliyosikika vyema, na Tesha akaanzisha kupiga makofi yaliyofanya wengine pia wajiunge naye.

Tukakaa huku nikimwekea Mariam kiganja changu karibu naye kwa chini, naye akaweka chake kwangu huku akitikisa vidole na kunionyesha ishara kwa mdomo wake 'broop,' kitu ambacho kikafanya nitabasamu kwa furaha. Wengine pia wakafata kujitambulisha, nafikiri sauti ya Miryam alipokuwa akiongea ikiwafanya waumini wa hapo wajiulize ikiwa alikuwa anashindia mayai mabichi ya kienyeji kila siku, na baada ya hapo ibada ikaendelea.

Ilikuwa ni kusikiliza hotuba, kutoa sadaka, kufanyiwa maombi ya hapa na pale, na sisi pia tulinyanyuka kwenda kuombewa. Kwa kuwa sakafu lilikuwa la michanga, waliweka mikeka chini kwa wale ambao wangelala kabisa, lakini mimi na Tesha tukakaza, hakuna kwenda chini. Vile ambavyo wachungaji husukuma kichwa taratibu huku wakiombea mtu ilifanya Mariam, Bi Zawadi, na hata Miryam waelekee chini, kwa hiyo mimi na Tesha tukasaidia kuhakikisha hawaanguki ama kuchafua nguo zao.

Aisee! Kuna wadada wawili baada ya sisi kuwa tumerudi kukaa waliokuwa wamepagawa na mapepo. Walipiga kelele huku wakiwa wamelala chini na kugaagaa mchungaji alipokuwa anashusha zile 'toka katika jina la Yesu!' Mariam mpaka akaogopa na kunishikilia kwa nguvu mkononi, kwa sababu mmoja wao alikuwa akija upande wangu, yaani ni kama vile pepo lilikuwa linataka kumtoka halafu liingie kwangu sijui?!

Basi nikageuka kumwangalia Tesha na kukuta amenikazia macho huku akibana tabasamu, nami nikashindwa kujizuia na kutazama pembeni huku nikijitahidi kubana kicheko kilichokuwa karibu kunipasukia mbele za watu wote. Ingepaswa kuwa pindi yenye kugusa sana, lakini kila mara jicho langu lilipokutana na la Tesha, ilikuwa ngumu ku-focus, ila nikajitahidi kujidhibiti. Akili zetu hizi zilijuana zenyewe tu.

Kwa hiyo ibada ikaendelea mpaka kufikia mida ya saa saba na nusu hivi, ndiyo ikafikia hitimisho. Na tulilazimika kutoa sadaka kwa mara ya pili ili kuchangia maendeleo ya kanisa, kisha ndiyo sote tukatoka hapo ndani na kuelekea nje. Baadhi ya waumini walitusalimu kwa heshima sana, na wengine wakionekana kutuogopa sijui, nasi tukawa tumeletewa viti na kuambiwa tukakae kivulini ili kumsubiri mchungaji na mama mchungaji kwa ajili ya maongezi machache.

Tukaletewa na soda kabisa baada ya kukaa, nasi tukaendelea kusubiri huku tukipiga story pamoja na Bi Zawadi hapo kuhusu jinsi gani tulijisikia baada ya ibada kuisha. Aliyeanza kuja ilikuwa ni mama mchungaji, naye akaketi pamoja nasi baada ya kutusalimia vizuri sana na kuanza kujuana na wengine tuliokuja nao leo mmoja baada ya mwingine. Mchungaji bado alikuwa akihudumia watu fulani kule ndani kwa hiyo naye angekuja baada ya muda mfupi.

Mama mchungaji akaongea na Tesha, akajaribu pia kumsemesha Mariam na kuambiwa kuhusu changamoto zake. Alikuwa amemtia moyo Tesha kwamba angekuja kupata kazi nzuri sana na kuoa mapema mno, ndoa yaani, na alimwambia Mariam kwamba ndani ya kipindi kifupi tu kila jambo baya ambalo limewahi kumpata lingebaki kuwa historia ambayo hakuna mtu angekuja kuikumbukia, kwa sababu na yeye angefika sehemu nzuri sana maishani.

Akaongea na Miryam pia. Kama kawaida ya mwanamke huyu, hakusema mengi sana zaidi tu ya yeye kuwa nani na upendo wake kwa familia yake yote, lakini inaonekana mama mchungaji na maono yake alikuwa ameshaona vitu vingi. Miryam alifanya ionekane kwamba alikuwa poa kabisa, lakini mama mchungaji akasema kitu ambacho kilizunguka mno hata kichwani kwangu.

Akamwambia, "Una nguvu, na moyo mzuri sana binti yangu. Lakini bado kuna sehemu ndani ya hatma ya maisha yako imefichwa ndani sana ya gamba gumu kama la kobe, na wewe unaogopa kwamba ikitoka nje... utaumia. Kwa Mungu hakuna kuogopa. Na ninaona Mwenyezi Mungu akikuandalia njia itakayokusaidia ili uwe huru zaidi, hatma hiyo isijifiche tena. Wewe uko sawa kabisa Miryam. Hauna tatizo la kimwili au kiroho. Lakini, hakuna mwanadamu aliye kamili kwa kila jambo, ndiyo maana tumeumbwa wawili-wawili ili kuweza kusaidiana, kukamilishiana yale mambo ambayo hatuwezi kukamilisha sisi kama sisi. Mungu amekuandalia njia iliyo kama zawadi ya kukukamilishia, na hatma hiyo kufunguliwa. Amini kwamba utaipata, na maisha yako yatajaa amani na furaha ukishaitambua zawadi hiyo kutoka Kwake."

Baada ya maneno hayo yaliyokuwa yamejaa fumbo fulani, Miryam akasema tu 'amen,' vilevile na Bi Zawadi, halafu mama mchungaji akatabasamu kiasi na kunitazama machoni kwa umakini. Mimi pia nilikuwa namwangalia, na sijui ni kwa nini tu lakini ni kama vile alikuwa akijaribu kuwasilisha kitu fulani kwangu ambacho sikuelewa, nami nikamtazama Miryam kwa utafakari.

Sijui maneno ya huyo mama yalinihusisha na mimi? Nilijikuta nikitaka kuhusika yaani, maana aliongea kama mganga, au mtabiri fulani hivi au nabii, na kiukweli sikuwaga mtu wa kuamini sana hivi vitu lakini kwa wakati huu, vilinisisimua sana. Mawazo mengi yalikuwa yanapita akilini. Mengi mno. Bila matarajio yoyote kabisa, simu yangu ikaanza kuita, na baada ya kutazama aliyekuwa akipiga, nikakuta ni Festo.

Ikanibidi ninyanyuke na kwenda pembeni kwanza, kisha nikapokea. Jamaa aliongea kifupi tu, akisema amepata nafasi ya kukutana na mimi, na alitaka niende kule kule kwake walikonipeleka watu wake kipindi kile; ndiyo tungekutana huko. Sikujua ikiwa ningepakumbuka vizuri, lakini nilijua ilikuwa huko Kawe, hivyo nikamwambia 'sawa, ninakuja.' Akasema isipite saa kumi jioni sijafika huko, maana alikuwa na ratiba zingine, kisha ndiyo akakata. Doh!

Hapa ningehitaji kuwakimbia hawa marafiki zangu maana tayari ilikuwa saa nane, na kutoka huku mpaka huko Kawe ingekuwa ni mwendo mrefu mno. Lakini nikawafata tu wote na kuwaambia kuwa kuna dharula ilikuwa imetokea na nilihitajika mahala fulani mara moja, kwa hiyo ningetangulia kuondoka. Bi Zawadi alionelea ingekuwa vizuri kumsubiria mchungaji kwanza, lakini nilipomwangalia Miryam usoni kwa njia ya kumaanisha jambo fulani, nafikiri akaelewa ni mambo yaliyohusiana na ishu yangu na maaskari.

Kwa hiyo bibie akanisaidia kwa kumwambia tu mama mkubwa wake kwamba inaonekana ni dharula ya wagonjwa na nini, hivyo ningetakiwa kuwahi ili kuokoa uhai. Bi Zawadi aliporidhia, nikawaaga wote vizuri na kuomba samahani kwa mama mchungaji kwa sababu ya kutakiwa kukimbia kwa mara nyingine tena leo, naye akasema haikuwa na shida. Tesha akanikumbusha kutochelewa sana ili jioni wasinikose kwenye kujumuika pamoja, nami nikakubali na kutimka upesi.

★★

Yaani ilikuwa ni kutimka upesi kwelikweli, tena kwenda kwa mtu niliyemwona kuwa adui. Ilinibidi nipande bodaboda kutokea Chamgando mpaka barabara kuu, kisha nikapanda tena bodaboda mpaka Mbagala. Kutokea Mbagala tena, nikapanda bodaboda kwa kumlipa jamaa elfu kumi anikimbize mpaka Kawe, na nikafanikiwa kufika huko ikiwa imeingia saa tisa alasiri.

Nikamwongezea kiasi kingine ili anisogeze maeneo ya ndani zaidi, nikijitahidi kukumbuka njia ya kupita, na hatimaye nikafanikiwa kuiona nyumba ya Festo kwa umbali mfupi shauri ya ukubwa na ughorofa wake. Nikamwambia boda asimame tu, nikashuka, kisha akarudi alikokuwa ametoka. Nilitaka kuhakikisha hakuna ufatiliwaji na yeyote yule mpaka huku, kwa hiyo nikatembea taratibu na kwa uangalifu kuelekea upande wa nyumba hiyo.

Nikawa nimefika nje ya geti hatimaye, na nyumba ilionekana kuwa kubwa na nzuri zaidi ya mara ya kwanza kabisa nilipoletwa hapo. Nikampigia simu Festo kumjulisha kwamba nilikuwa getini, naye akasema sawa na kukata. Mazingira ya eneo hilo yalikuwa na miti na barabara nzuri sana ya lami, kukiwa na majengo mengine mazuri lakini si kwa umaridadi wa hali ya juu kama hili. Na hakukuonekana kuwa na wapita njia wengi, zaidi ni magari tu ndiyo yaliyofanya mizunguko mara moja moja.

Sekunde chache baada ya Festo kukata simu, geti la hapo nje likafunguliwa na yule yule mlinzi wa siku ile, nami nikaingia taratibu huku nikisikia kelele za mibweko ya mbwa kutokea sehemu aliyokuwa amefungiwa, na magari manne ya kifahari yakipumzika maegeshoni. Mlinzi akaniambia niende tu mpaka huko ndani, nami nikatii.

Mdogo mdogo tu, nikiwa nakumbuka vizuri pa kwenda hadi kuifikia sebule ile maridadi ya jamaa, nami nikawa nimeifikia. Halafu milango ya kuingilia hapo ilikuwa inafunguka kama vile milango ya lifti ifanyavyo, na muundo ulikuwa wa aina hiyo hiyo kabisa; chuma. Festo kweli alijua kujilinda, yaani kufika huku ndani ilikuwa ni kama nimetokea eneo tofauti kabisa na hii nyumba hapo hapo nje. Kwa hiyo nikabonyeza kitufe cha kengele na kusubiri, halafu milango hiyo ikafunguka, kisha ndiyo nikapenya ndani.

Mwonekano mzuri wa sebule pana ya hapo bado ulikuwa vile vile kabisa, isipokuwa wakati huu nikakuta kitu kimoja tu ndiyo kimebadilika; yule mpishi aliyekaa sehemu ya jikoni. Nilimkumbuka vizuri mpishi yule niliyemkuta kipindi kile, Shefu Saidi, ambaye hadi tulipeana namba za mawasiliano na kuna nyakati ndani ya huo mwezi mmoja tulikuwa tumewasiliana kupeana salamu na nini, lakini wakati huu haikuwa yeye niliyemkuta hapo.

Wakati huu alikuwepo jamaa mwingine, mweupe, mwenye mwonekano usiotoa ujumbe wowote kwamba alikuwa mpishi wa kawaida tu. Yaani alijazia, jinsi ambavyo aliniangalia ilikuwa kama vile ana njaa ya kutaka kunichinja, na alikuwa ameshikilia visu viwili akivinoa-noa tayari kukata-kata nyama iliyokuwa kwenye ubao mdogo juu ya sinki. Nikashindwa hata kumsalimia na kusimama tu kwa utulivu huku nikimtazama kwa umakini, na yeye akinikazia macho yake kikatili fulani hivi.

"JC..."

Nikageuka baada ya kusikia sauti ya Festo akiniita hivyo na kumwona akiwa anashuka kutoka juu ya ngazi zilizoelekea ghorofani. Mwamba alikuwa amevalia kwa njia iliyoonyesha kuwa alitoka kupiga tizi, labda kwenye gym ndogo hapa hapa kwake iliyokuwa huko juu, kwa sababu alikuwa ametia nguo za mazoezi mwilini zilizolowana kiasi, na zilizokuwa na rangi ya kijivu. Alikuwa pia amevaa glovu mikononi, na alishuka ngazi huku akizivua na kufungua bandeji zilizofungwa viganjani.

"Festus..." nikaita hivyo pia, kama kurudisha ile 'nimekuona.'

"Niite tu Festo. Festus ina-sound kama mtu fulani hivi ambaye simpendi," akasema hivyo kiutani.

Nikatabasamu kiasi na kumwambia, "Basi inawezekana hauko peke yako."

Akatabasamu kiasi pia na kunifikia, naye akanipiga ngumi kidogo begani kwa njia ya kirafiki na kunipita, akielekea kule kwa mpishi. Nikaendelea kumwangalia tu mpaka huyo mpishi alipompatia chupa ndogo ya maji kutoka kwenye friji, naye Festo akaanza kunywa.

Alipotosheka, akaishusha na kusema, "Unajua kukariri maeneo, nilifikiri ungepotea."

"Niko makini na kila kitu kinachonizunguka," nikamwambia hivyo.

Akaniangalia na kusema taratibu, "Is... that... right?"

"Ahah... well, I try," nikamwambia.

"Unajitahidi. Kazi zako zote na Bertha mpaka sasa, very impressive..."

"Asante."

Akaanza kunifata huku akisema, "Na nina-suppose kilichokuleta hapa ni ili uongelee ishu inayom-concern... mwanamke wako?"

"Ni... vitu vingi, ila..."

"Make it quick, friend. Nataka ku-bounce," akanikatisha kwa kusema hivyo.

"Ooh, kuna sehemu unaenda?" nikamuuliza.

"Yeah, so niambie. Unahitaji nini ambacho hungeweza kusema kwenye simu tu mpaka unione?" akauliza huku akianza kunywa maji tena.

Nikamwambia, "Nime... nilifikiria maneno ambayo uliniambia siku ile... na... nataka unisaidie."

"Maneno gani?" akauliza baada ya kumaliza kunywa maji.

"Uliniambia nikiwa kwenye hili game, sipaswi kuwa mtu vulnerable. Natakiwa niwe na means... njia yaani, za kujilinda ili nisiwe mtu rahisi kurukiwa," nikamwambia hivyo.

"Hmm... na hiyo ni baada ya mwezi mzima kupita? Nini kimekupa motisha ya kutaka kuwa na hiyo... means?" akaniuliza.

"Game lenyewe tu, Festo. Huwezi kuwa mwangalifu sikuzote," nikamwambia.

"No, no... nataka uniambie. Niambie ikiwa unahisi kuna mtu, au watu... wanataka kukurukia," akaongea kwa msisitizo.

"Siwezi kusema ni mtu fulani kwa uhakika, ila ndo' point yenyewe. Kutojua tu ni nani anaweza akanirukia ni sababu tosha ya kujua kwamba naweza nikarukiwa na yeyote. That's why nahitaji kujilinda mimi mwenyewe badala ya...."

"Kutegemea Bertha ndo' akulinde?" akanikatisha kwa kuuliza hivyo.

Nikaangalia pembeni.

"Ikiwa unataka hiyo means kutoka kwangu moja kwa moja, inamaanisha Bertha hajui kwamba uko hapa, si ndiyo? Na kwa sababu fulani, hautaki ajue," Festo akasema hivyo.

Nikamtazama tu usoni kwa umakini.

"Napata hisia kwamba kuna kitu unanificha, JC. Na unajua, huwa sipendi... kufichwa vitu, ama vitu kufanywa nyuma ya mgongo wangu na watu ambao ni wangu. So kama kuna chochote unajua napaswa kujua ila unahofia kuniambia, ni bora useme sasa hivi... la sivyo nikijua mimi mwenyewe, haitakuwa nzuri kwako mbeleni," akaniambia hivyo.

Nikatulia kidogo, kisha nikamwambia, "No. Hakuna kitu chochote kikubwa namna hiyo. Nataka tu kujilinda. Mimi kama mimi. Basi."

Akiwa amenikazia macho, akauliza, "Are you sure?"

"I'm sure," nikamwambia kwa uhakika.

Akasema, "Okay. So unataka nikupe piece moja?"

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Utaweza kutumia?" akauliza.

Nikatikisa kichwa tena kukubali.

Akaangalia pembeni kiufupi na kusema, "Xave..."

"Boss..." yule mpishi akaitika.

"Niletee taurus moja. 9mm," Festo akasema hivyo.

Nikamwangalia huyo "mpishi" alipotoka sehemu ya jikoni na kuja upande wetu huku akiniangalia kwa macho makini, naye akatupita na kuelekea upande wa vyumba vingine huko mbele; siyo ghorofani yaani.

"Bado uko Mbagala?" Festo akaniuliza hivyo.

"Ndiyo. Kwani haujui hilo?" nikamuuliza pia.

"Najua."

"Ooh, unamaanisha... pale kwa Miryam na nini?"

"Yeah. Anaendeleaje?" Festo akaniuliza hivyo kwa sauti ya chini.

"Yuko poa. Si bado mnawasiliana?" nikachimba.

Akavuta pumzi na kuangalia pembeni, naye akasema, "Bado, JC. Bado ananigomea, yaani... nafanya mengi, ila anayasukuma mbali, sijui kwa nini tu."

"Labda... unaweza ukakuta ana mtu wake..." nikaona nimchokoze.

"Ungekuwa umeshasikia msiba," akaniambia hivyo kwa hisia kali.

Nikashindwa kujizuia kucheka kidogo kwa pumzi, nami nikajidhibiti zaidi na kusema, "Kwa hiyo una uhakika hana mtu? Basi. Komaa tu."

"Unajua nini...."

Kabla Festo hajamaliza kuongea, mpishi Xave akawa amerejea na kutufikia karibu, naye akampatia Festo bastola yenye mwonekano mpya wa chuma yenye rangi ya shaba kwa juu na nyeusi kwenye kishikio na kisha kuondoka. We! Kitu chenyewe yaani, chuma chuma, kikiwa kifupi kiasi kutoshea vizuri kuficha kiunoni ama mfukoni mwa suruali kabisa, naye Festo akainyanyua hewani akiielekeza juu, huku akinitazama kwa utulivu.

"Subira huwa ni kitu muhimu maishani. Siyo wote wenye vitu kama vyangu wanavipata baada ya kuzaliwa tu, wengine tunahangaika mno mpaka kufika tunapofika... ndoto zetu kutimiza. Iwe unataka kujilinda, au kupata pesa, au kupata gari, au kufika sehemu fulani na kitu chochote unachokipenda, unahitaji subira, na ku-time vizuri mambo yote ili ufanikiwe kutimiza ndoto yako... na isikuponyoke kamwe," akaniambia hivyo.

Nikiwa namtazama kwa umakini, nikamwambia, "Na hiyo inamaanisha kwa mtu nayempenda pia. Bertha, na wewe Miryam vilevile."

"Yeah. Kama ni msemo naopenda zaidi maishani mwangu, ni kwamba maamuzi magumu sikuzote huwa yanatuhitaji tuwe na nia zenye nguvu sana ili kuyachukua, na ukiyafanya ukafanikiwa kupata unachotaka... hautakuwa mtu wa kupoteza lolote. Never," akaniambia hivyo huku akinikabidhi bastola kiganjani.

Nikaipokea bastola hiyo na kuishikilia kwa uangalifu, nikiwa natafakari maneno yake. Kwa njia fulani niliona kwamba alikuwa akizungumzia jambo lingine kabisa, jambo fulani zito, na ilipofika kwenye suala la maamuzi, alikuwa sahihi. Ni kama vile tu ambavyo mimi nilikuwa nimeamua kuchukua uamuzi huu wa kuwa daktari-mtembea-na-bastola kuanzia sasa, kitu ambacho sikuwahi kudhani kabisa kwamba kingekuja kuingia akilini.

Maisha yangu yalikuwa yananibadilisha kwa kasi sana, ndani ya kipindi kifupi tu yaani nilikuwa nimejikuta ndani ya mambo mengi yenye kutatanisha, lakini haya ndiyo yalikuwa maamuzi magumu kweli yaliyoonyesha nina nia yenye nguvu ya kuyachukua. Kwamba hata kama ingehitajika kuua, basi nilikuwa ndiyo najiandaa kwa ajili ya hilo. Aloo! Siyo mchezo.

Nikiwa nimeishikilia bastola hiyo kwa viganja vyangu, Festo akauliza, "Umeshawahi kutumia hii kitu, JC?"

Najua alikuwa anataka kuhakikisha ikiwa naelewa kile ambacho nilikuwa nimejiingiza kufanya, nami nikamwambia, "Sijawahi kuitumia kuumiza mtu, ila najua kutumia."

"Wewe ni daktari, my boy. Umeundwa kutibu majeraha, siyo kuyasababisha. Ikitokea ukahitaji kuitumia kuumiza mtu... utaweza?" akaniuliza.

Nikamwangalia usoni kwa umakini, nami nikaikoki bastola hiyo kwa makusudi, kisha nikasema, "Asilimia mia."

Akaachia tabasamu la pembeni na kisha kusema, "Uwe care, usije kuitumia kifala kabisa. Chuma zangu zote siyo traceable, kwa hiyo ikitokea ukatia mtu yeyote risasi, la muhimu ni wewe kutogundulika. Ukigundulika hata kwa kutembea nayo tu ndiyo imekula kwako. Do you understand?"

Nikamwangalia usoni kwa umakini kiasi, nami nikamwambia, "Ndiyo naelewa. Asante. Pistol nzuri sana. Una... unanisaidia, yaani... unanipa bure... kama... vile nahisi yaani, kama unataka kuhakikisha niko care sana pia...."

"Don't get it twisted, mimi siyo rafiki yako, nakupa hii kwa sababu umeniomba. Ungemwomba hata Bertha, lakini umeona uje kwangu ili asijue, si ndiyo?" akaniambia hivyo.

Nikaangalia chini na kusema, "Yeah. Sorry. Natumaini tu itabaki kuwa hivyo lakini... Bertha kutojua."

Akasema, "Unajua... group langu lote, nimeligawanyishia himaya zao hapa jijini mpaka mikoani, na Bertha ndiyo mwenye territory kubwa... and thanks to you, ananipa faida kubwa mno kwa sababu umeifanya biashara yake imekua zaidi. So that means... wewe ni muhimu. Hatutataka lolote likuhatarishe, and to be honest... najua kuna watu wanaweza wakataka kukumaliza, ila ndiyo sijui wa kumnyooshea kidole kwa uhakika. Sipendi kusingizia. Ikiwa unahisi kuna shida ndani ya network yangu me mwenyewe, niambie. Singependa uje uchukue maamuzi mabaya kwa mikono yako bila utambuzi wangu, ndiyo maana nakwambia kama kuna shida sehemu, iseme. Ukifikiri utaweza kuhandle kila kitu peke yako kwa sababu una kipisi mkononi... then bado hujaelewa jinsi hili game linavyofanya kazi mdogo wangu. Sikwambii haya kwa sababu nakujali, ila kwa sababu sitaki kazi zangu zichafuke. Nina nguvu yote ya kukusaidia ukitaka, ila usipotaka hilo... halafu mambo yangu yakaharibika, ujue kwamba mimi ndiyo nitakuharibu wewe. Umenipata?"

Alikuwa ameongea kwa ile njia ya kutikisa yaani, nami nikatikisa kichwa kwelikweli kuonyesha uelewa.

"Haya nenda. Ikiwa ni hayo tu..." akaniambia hivyo.

Nikaichomeka bastola mbele ya kiuno changu na kusema, "Sawa. Asante. Sijui sana kuhusu shift za hapa, ila utamfikishia na Saidi salamu zangu..."

"Saidi ndiyo nani?" Festo akaniuliza hivyo.

Nilikuwa nimeshaanza kuondoka, lakini nikasimama kwanza na kusema, "Saidi... yule chef mwingine. Nilikuwa namaanisha, akija kwenye shift yake labda...."

Festo akatabasamu kiasi na kumwangalia yule mpishi wake kule jikoni, ambaye alikuwa anakatakata nyama huku ananitazama kwa umakini.

"Au aliacha kazi?" nikamuuliza hivyo Festo.

Festo akaanza kuelekea kule ngazini huku akisema, "Hakuna mtu anaitwa Saidi amewahi kufika hapa. Utakuwa umekosea..."

Eh!

Nikabaki nikimtazama jamaa mpaka alipokuwa ameanza kuzipanda ngazi, nami nikamgeukia yule mpishi Xave pale jikoni, ambaye akafanya kuninyooshea kisu kuuelekea mlango; kwamba niondoke. Maneno ya Festo yalikuwa yameiingizia akili yangu taarifa fulani ambayo haikuwa nzuri hata kidogo, na kiukweli nilihitaji kuthibitisha kama nilichofikiria alikimaanisha ndiyo kile alichokuwa amemaanisha.

Nikajaribu kumpigia Shefu Saidi mara tatu, lakini simu yake ikawa haipatikani. Nikaendelea tu kwenda mpaka nje, na wakati nikielekea getini na mlinzi, nikawaza labda nichimbe kitu kutoka kwake.

Nikajisemesha hivi, "Nyumba nzuri kweli bro. Sisi tunatamani tu hivi vitu, wenzetu ndo' wanavipata."

Mlinzi, akiwa anafungua geti, akasema, "Ndo' maisha. Ila na wewe si ni... mvulana wa boss?"

"Ee, ndo' nimeanza-anza. Mara ya kwanza nililetwa nimefungwa macho kabisa," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu kiasi na kusema, "Nakumbuka. Mtu mkubwa ana mambo makubwa, ndiyo hayo sasa. Shukuru tu haukufa."

Nikajichekesha kidogo na kutoka sehemu hiyo ya getini, nami nikamuuliza, "Halafu, unamkumbuka yule mpishi mwingine niliyemkutaga hapa?"

"Nani? Wako wanabadilishana. Au unamwongelea Saidi?" akauliza hivyo.

"Eeh... Saidi, sijamkuta. Ila inaonekana hajakuwepo hapa muda. Aliacha kazi?" nikamuuliza pia.

Akageuka kuangalia upande wa nyumba hiyo, kisha akaniangalia tena na kutoa ishara kwa kiganja chake, akikipitisha mara moja usawa wa shingo yake huku akinitazama kwa umakini.

Nikiwa nimeelewa alichomaanisha, nikaingiwa na hisia mbaya sana, nami nikamuuliza, "Ilikuwaje?"

"Sijui. Inaonekana alim-diss boss... akapotea," akasema hivyo.

Nikaangalia chini kwa huzuni kiasi.

Akaanza kufunga geti huku akiniambia, "Jitahidi usivuke mistari usiyopaswa kuvuka mdogo wangu, kama mimi tu. Itakusaidia usipotee mapema. Sawa?"

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa, naye ndiyo akamaliza kufunga geti hilo.

Dah! Kwa hiyo kumbe Shefu Saidi alikuwa ameuawa, sijui hata alimfanya nini Festo baba wa watu masikini wakati alikuwa mpole na mwenye heshima sana. Jambo hili likawa limeigeuza siku yangu niliyodhani ingekwenda vizuri kuanza kuonekana kuwa mbaya, kwa sababu ya kuwaza ni namna gani Festo alivyokuwa hatari sana.

Namaanisha kuna watu hatari sawa, ila hatari nayoongelea ilikuwa ile ambayo angekuwa nayo kwa familia nzima ya Miryam kwa sababu ya yeye kumtaka mwanamke huyo. Festo alionekana kuwa mwanaume mwenye subira sana, lakini ikiwa ungefika wakati ambao subira yake ingechoka, angefanya lolote lile ili kupata alichokitaka, na najua hilo lilikuwa karibu kutokea kwa upande wa Miryam pia.

Haingefaa hata kidogo, kwa njia yoyote ile, mwanaume huyo awe pamoja na Miryam kimahusiano wakati nilijua alikuwa mtu wa aina gani, na Miryam kumwekea kigingi bado ndiyo jambo ambalo najua mwisho wa siku lingeweza kufanya Festo achukue maamuzi mabaya ili tu apate faida ya kulazimisha mapenzi pamoja naye. Nisingekaa kutazama tu hilo litokee. Hata kama jamaa alikuwa na nguvu nyingi kiasi gani, kwa hali na mali yoyote ile, ningehakikisha namlinda Miryam dhidi yake.





★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
jc wewe ndiyo uliyesababisha shefu said Àuwawe,,,, kwann???,,, siku umefika pale ulianza kuleta ukaribu na yule bwana ukuishia hapo na namba za simu mkabadilishana mbaya zaidi yote haya mliyafanyia ndani ya nyumba ya Festo ,,,

Sasa sijui hukufikiria ,,, kuwa festo siyo mjinga aamini walinzi tu peke yake ,,, bwana huyu lazima atakuwa kafunga Camera zakutosha nje na ndani ya hilo jumba lake ,,, sasa ikiwa niwazavyo ni sahihi,,, maongezi yako weww na shefu zaidi siku ile aliyaona na kuyasikia ,,, lakini pia kitendo cha weww kukaa na mpishi yule mkala chakula pamoja pia kilimuongezea matatizo ..

Sheria zilikuwa wazi ,,, kazi ya shefu said ilikuwa ni kupika tu na kuondoka zake,,, siyo kuanza kula na kuongea na wageni wasio muhusu ,, na kwenda mbali zaidi hata kuchukua namba zao kwa mawasiliano huu ulikuwa ni ukiukwaji mkubwa sana wa sheria na usaliti wa kiwango cha juu hivyo kama ulivyo sema festo ni mtu makini ,,, hivyo ilikuwa lazima ampoteze huyu bwana...
 
jc wewe ndiyo uliyesababisha shefu said Àuwawe,,,, kwann???,,, siku umefika pale ulianza kuleta ukaribu na yule bwana ukuishia hapo na namba za simu mkabadilishana mbaya zaidi yote haya mliyafanyia ndani ya nyumba ya Festo ,,,

Sasa sijui hukufikiria ,,, kuwa festo siyo mjinga aamini walinzi tu peke yake ,,, bwana huyu lazima atakuwa kafunga Camera zakutosha nje na ndani ya hilo jumba lake ,,, sasa ikiwa niwazavyo ni sahihi,,, maongezi yako weww na shefu zaidi siku ile aliyaona na kuyasikia ,,, lakini pia kitendo cha weww kukaa na mpishi yule mkala chakula pamoja pia kilimuongezea matatizo ..

Sheria zilikuwa wazi ,,, kazi ya shefu said ilikuwa ni kupika tu na kuondoka zake,,, siyo kuanza kula na kuongea na wageni wasio muhusu ,, na kwenda mbali zaidi hata kuchukua namba zao kwa mawasiliano huu ulikuwa ni ukiukwaji mkubwa sana wa sheria na usaliti wa kiwango cha juu hivyo kama ulivyo sema festo ni mtu makini ,,, hivyo ilikuwa lazima ampoteze huyu bwana...
Awesome observation! Inapendeza kuona ishu inaeleweka kabla haijaelezewa, napenda msomaji makini. Kudos brother 👊
 
jc wewe ndiyo uliyesababisha shefu said Àuwawe,,,, kwann???,,, siku umefika pale ulianza kuleta ukaribu na yule bwana ukuishia hapo na namba za simu mkabadilishana mbaya zaidi yote haya mliyafanyia ndani ya nyumba ya Festo ,,,

Sasa sijui hukufikiria ,,, kuwa festo siyo mjinga aamini walinzi tu peke yake ,,, bwana huyu lazima atakuwa kafunga Camera zakutosha nje na ndani ya hilo jumba lake ,,, sasa ikiwa niwazavyo ni sahihi,,, maongezi yako weww na shefu zaidi siku ile aliyaona na kuyasikia ,,, lakini pia kitendo cha weww kukaa na mpishi yule mkala chakula pamoja pia kilimuongezea matatizo ..

Sheria zilikuwa wazi ,,, kazi ya shefu said ilikuwa ni kupika tu na kuondoka zake,,, siyo kuanza kula na kuongea na wageni wasio muhusu ,, na kwenda mbali zaidi hata kuchukua namba zao kwa mawasiliano huu ulikuwa ni ukiukwaji mkubwa sana wa sheria na usaliti wa kiwango cha juu hivyo kama ulivyo sema festo ni mtu makini ,,, hivyo ilikuwa lazima ampoteze huyu bwana...
Mulemule🔐🔐
 
Back
Top Bottom