Simulizi: Mimi na Mimi

Simulizi: Mimi na Mimi

Elton Tonny unajua sana Kaka, yaani uandishi wako kama unatazama sinema. Sema kwenye scene ya Miry na JC umeua mnoo 🤣🤣🤣
Kipaji sana Mkuu.
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA THELATHINI NA TISA

★★★★★★★★★★★★★★★★★★★


Salumu alinisindikiza mpaka barabarani nilipopanda daladala kuelekea stendi ya Makumbusho, na baada tu ya kuingia humo na kukaa, nikachukua simu na kumpigia Adelina upesi. Nilikuwa nimeweka mambo haya pembeni kidogo kwa ajili ya kutumia muda zaidi na Miryam kutokea jana, lakini siyo kwamba nilisahau kabisa ile ishu niliyokuwa nimemwomba Adelina anisaidie kufatilia. Na yeye inawezekana alikuwa na mambo mengi ya kikazi ndiyo sababu hakunitafuta, hivyo sasa ukawa ndiyo muda mzuri wa kuhakikisha baada ya taarifa ya kifo cha Bertha kunifikia.

Mwanamke huyo akapokea simu yangu hatimaye, na baada ya salamu, nikaenda moja kwa moja kwenye pointi ili nisimkengeushe kutoka kwenye kazi zake. Nilimuuliza ikiwa aliangalia safari ya ndege ya jamaa mwenye jina Festus Yakubu, naye ndiyo akasema 'oooh kweli,' alisahau kunitumia jibu ingawa alilifanyia suala hilo utafiti. Akaniambia ni uhakika, mwanaume mwenye jina hilo alisafiri kwa ndege kuelekea Nairobi hiyo wiki iliyopita, jina lake lilikuwepo kwenye orodha ya abiria waliopanda kuelekea huko Kenya. Ahaa? Nikamwambia sawa, nikamshukuru kwa jitihada na kumwomba samahani kumsumbua kwa wakati huu, naye akasema haikuwa na shida kabisa, ndiyo tukaagana kwa ahadi za kuja kuwasiliana baadaye.

Nikawa nimehakikisha sasa kwamba kweli Festo alikuwa ameondoka nchini, na labda hata safari yake haingeishia Nairobi tu, huenda angekwenda sehemu zingine. Hivyo, kwa kiwango kikubwa sidhani kama na yeye angekuwa na mkono ndani ya ishu ya ajali iliyompata Bertha, ikiwa kama kweli hiyo ilikuwa ajali ya kupangwa. Umakini wangu wote sasa hivi kuelekea hilo suala ungepaswa kuwa kwa huyo Beatha, yaani ningehakikisha Ramadhani anamchimba kokote alikokuwa na kumchunguza vyema ili kumdaka na lolote lile haramu, na hivyo amweke pembeni haraka sana.

Kila hisi ndani yangu iliniambia kwamba hiyo haikuwa ajali, na ni baada ya muda mfupi tu ingefahamika zaidi. Ikiwa ingegundulika hako kadada ndiyo kaleta shida kapya kwa kipindi hiki, ningetakiwa kuhakikisha usalama wa familia yangu yote kwa ujumla, na familia ya Miryam pia, halafu nihakikishe hakaji kutusumbua tena hata kama kasingetaka kufanya hivyo. Tahadhari kabla ya hatari. Nikaendelea tu na safari mpaka Makumbusho stendi hapo, kisha ndiyo nikapanda gari ili nielekee Mbagala na Mzinga.

★★

Nimekuja kufika Mzinga kwenye mida ya saa moja usiku, shauri ya msongamano wa magari ulionikawiza kweli tulipofikia barabara iliyoelekea maeneo hayo. Nilifika kwa Ankia na kumkuta mwanamke huyo akiwa anapika, na alinipokea vizuri sana kama mgeni vile, akifurahi kuniona nimerejea. Alikuwa ananiambia eti alijihisi upweke kuwa hapo mwenyewe, nami nikamwambia acha zako wewe, yaani uko na Bobo unakuwaje mpweke? Akacheka sana na kusema ni kweli, Bobo ndiye aliyekuwa akimwondolea upweke na alijitahidi kweli kumpa raha zote alizohitaji. Eti akawa ananidolishia!

Alipomaliza kunidolishia Bobo wake ndiyo akaanza kuuliza mambo yangu na Miryam yalikuwaje huko tulikoenda huku akiangalia mizigo yangu na nini, nami nikampatia zawadi yake ya nguo niliyokuwa nimemnunulia bila kuongelea mengi sana ambayo nilifanya na Miryam. Sikuwa wa aina ya kudolishia mimi. Ila si akawa anataka kujua kama nilimtembezea bibie kichapo? Nikamwambia hiyo ni siri yetu, na kwa hapo tu akawa ameelewa kuwa ndiyo, Miryam nilikuwa nimeshammiliki rasmi kimwili baada ya kumteka kihisia.

Akanipa hongera ya bata niliyokula na kuniambia alikuwa anatayarisha msosi wa nguvu ili tule pamoja wakati huu, na Bobo mume wake angekuja ili atulishe sisi pamoja. Eti mume wake! Alikuwa ameshaanza kumwita hivyo nakwambia, nami nikasema sawa, wacha niende kuwasalimu wapendwa wangu hapo jirani na kuwapatia zawadi zao, kisha ndiyo ningerejea ili kupumzika.

Nikavua tu viatu na kubeba mfuko mmoja, na wakati nikiwa naelekea hapo kwake Miryam ndiyo nikatambua kwamba bibie hakuwa amerejea bado baada ya kumtumia ujumbe kuuliza ikiwa alikuwepo ndani, na yeye akajibu kusema hakuwa ameondoka Kijichi. Hivyo, nikaenda mpaka getini, na kama kawaida kimlango kidogo cha geti kingehitaji kuvutwa kwa kamba huku kwa nje ili kufunguka lakini nikakuta hicho kikamba kimetoka. Sijui nani alikitoa kwa huku nje, ila ikanibidi nigonge tu geti sasa maana kimlango kilifungwa kwa ndani. Nikasikia sauti za hatua zikija kutokea hapo ndani ya geti, nami nikatulia na kusubiri.

Hicho kimlango kilipofunguka, ikawa ni Mariam ndiye aliyekuwa amesimama hapo mbele yangu, na sasa hivi nisingemwita "binti Mariam" tena, alikuwa Mariam kamili sasa. Alinitazama kwa njia ya kawaida tu, akiwa ndani ya blauzi nyeupe yenye tiki ya Nike kifuani, pamoja na skinny jeans laini, na mtindo wa nywele zake ulikuwa vile vile wa rasta nene isipokuwa sasa alifunga ule urefu wa mapembe-rasta kwa pande za kichwa chake kama mabutu mawili makubwa. Hakuniamkia, wala kutabasamu, akaachia tu uwazi zaidi kwenye hicho kimlango na kuanza kurudi huko ndani.

Nikaingia na kumwita, "Mamu..."

Akasimama na kunigeukia.

Nikamsogelea, nami nikamwambia, "Haujambo?"

Akatikisa kichwa mara moja kukubali.

Nikarudishia mlango wa geti na kumuuliza, "Nani yuko ndani?"

"Wakina mama. Na Tesha," akasema hivyo.

Nikatoa mfuko mdogo kutoka kwenye mfuko mkubwa niliobeba, nami nikampa huku nikisema, "Nimekuletea zawadi."

Akaupokea na kuukunjia tu usawa wa kifua chake, naye akasema, "Asante JC."

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Mamu... nataka kujua ikiwa me na we' tuko poa. Yaani, sitaki kuwe na hali ya utengano baina yangu me na wewe... baada ya kilichotokea juzi. Nataka sana tuendelee kuwa marafiki."

Akabana midomo yake kiasi huku akiangalia pembeni, lakini hakutoa jibu.

Nikamuuliza, "Ama ndiyo umenichukia?"

Akaniangalia usoni upesi na kuweka macho yenye kujali, naye akasema, "A-ah. Siwezi kufanya hivyo JC..."

"Kweli?"

"Ndiyo. Sikuchukii... siwezi," akaniambia hivyo.

"Mbona unakuwa serious sasa kama vile...."

"Hapana, haimaanishi nakuchukia. Bado tu ninazoea hii hali... siyo rahisi ku... kubadilisha tu hisia. Bado ninakupenda," akaniambia hivyo.

Nikaendelea kumtazama usoni kwa kujali.

"Lakini kama tutaendelea kuwa marafiki tu, napaswa ku.... itachukua muda kuzoea, maana bado nikikuona...." akaishia hapo na kuangalia pembeni tena.

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa, nami nikamwambia, "Sawa. Nisamehe tu lakini Mamu. Siyo nia yangu kukuumiza kama hivyo."

Akaniangalia na kusema, "Usijali. Ni muda tu, ninahitaji muda tu. Nitazoea."

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Nitakusaidia ili uzoee haraka. Si unajua me Superman ikija kwenye suala la kukusaidia na nini?"

Akajitahidi kutabasamu kiasi na kuniambia, "Superman wapi? Huwezi hata kunyanyua hili gari."

Nikacheka kidogo na kusema, "Asa' hilo tu! Hii nyumba yote nabeba kwa haka kakidole!"

"Haa! Umdanganye mtoto," akasema hivyo na kutabasamu zaidi.

"Aahhahah... Nitakuja kukuonyesha..."

"Na ukishindwa?" akauliza.

"Basi nitakununulia kitu chochote unachotaka yaani," nikamwambia hivyo.

"Sawa. Tupinge," akasema hivyo na kuniwekea kidole chake kidogo kwenye kiganja changu.

Nikamwekea changu pia, naye akakivuta kwa nguvu kama kutia muhuri.

"Tena siyo nyumba, haka kagari tu. Ukishindwa kunyanyua, unaninunulia chochote kile nachotaka. Sawa?" akaongea hivyo kwa shauku kiasi.

Nikajikuta nimebaki kumtazama tu kwa hisia.

"Sawa?" akasisitiza swali.

Nikaondoa mzubao na kusema, "Poa. Si tumeshapinga? Kesho tu. Utaona."

"Haya," akasema hivyo.

Nikiwa natabasamu, nikamwekea kiganja changu kimoja karibu naye, na yeye akaniangalia na kutabasamu kiasi, kisha akaweka cha kwake hapo na kwa pamoja tukasema, "Brooop!"

Tukacheka kidogo tukiwa tumeanza kujenga kale kahali ka amani kazuri angalau, na ilinifariji, kisha baada ya hapo ndiyo tukaelekea huko ndani pamoja.

Warembo wangu, Bi Jamila na Bi Zawadi walinipokea kwa furaha sana, wakisema walikuwa wamenikosa kweli jana. Yaani tena Bi Zawadi akasema ikiwa sikumletea zawadi basi angeninunia, na ni kama nilikuwa nimeotea tu kumletea. Nikawapatia na wenyewe zawadi zao, nguo nzuri za wamama yaani, zenye vilemba na vitenge spesho vya kuweka begani, na ilikuwa imeniponyoka pesa nyingi kwa ajili ya hizo ila furaha yao ilipita gharama yote iliyotumika. Tesha akaja, eti na yeye akitaka zawadi, nami nikamwambia tungeenda kutafuta udongo mfinyanzi ili nimtengenezee gari zuri sana la kumpatia.

Ikawa ni pindi yenye kufurahisha sana, Mariam akaenda chumbani kujaribishia nguo yake niliyomletea na kuja kutuonyesha, na alikuwa amependeza kweli yaani. Ndiyo mama zake wakubwa wakasema wangevaa nguo hizi ikifika kesho, wakati wa kwenda kwake Doris. Sikujua kama walikuwa na huu mpango, nami nilipouliza, ndiyo wakanifahamisha kwamba Doris aliwaalika wote kwenda kumtembelea kwake mapema ya kesho, yaani familia yote iende kupaona huko kwake na mume wake maeneo ya Chanika. Kwa hiyo bila shaka Miryam angewapeleka, na walikuwa na hamu ya kuvaa vizuri tena kwenda kwenye hayo matembezi, kwa hiyo hapa nikawa nimewaletea ukombozi.

Basi, nimekaa-kaa hapo mpaka kwenye mida ya saa mbili usiku ndiyo nikawaambia ningeondoka sasa na kwenda huko gym, maana nilitakiwa kuendeleza ratiba ya kupiga mazoezi yangu ya mwili. Hawakuwa na shida kwa hilo na kuniambia kama nikipata nafasi basi nije tena hapa kwao, nami nikakubaliana nao. Tesha akaamua tuondoke pamoja ili akajiunge nami huko gym, na bibie Miryam hakuwa amerejea bado, kwa hiyo tukawaacha wanafamilia wake, nikaenda kwa Ankia kuvaa nguo nyepesi, halafu ndiyo tukaelekea gym.

Ilikuwa ni kwa uratibu wa kawaida tu kutokea hapo, yaani tukaelekea gym na Tesha kupiga tizi mpaka saa nne kasoro, kisha tukarudi nyumbani. Miryam tayari alikuwa amefika, na sikwenda kwake tena, ila tukawasiliana na mambo kuonekana kuwa poa hapo kwao. Akanijulisha kuhusiana na matembezi ya familia yake kwenda kwa Doris kesho na kusema labda tungekuja kukutana jioni ya kesho, na hilo halikuwa na neno. Tukaagana vizuri sana baada ya kuchat kwa video call hadi kwenye mida ya saa saba bibie alipoomba alale. Nikaanza kutafuta usingizi pia muda huo huo, kwa kuwa nilipanga kuamkia kwenye safari fupi siku ya kesho pia.

Jumatano ikapita.


★★★


Alhamisi asubuhi ilipofika, nikajikuta naamka ikiwa imeshaingia mida ya saa nne. Yaani nililala! Nafikiri shauri ya hiyo jana kuamka mapema mno na kugoma kurudi kulala tena, mechi zote tamu tulizocheza na Miryam wangu pia zikiwa zimeuleta huo uchovu nadhani. Ila kwa sasa nikaamka nikiwa najihisi vizuri sana mwilini, na kwa kuwa masaa yalikuwa yameenda, cha kwanza ikawa kuangalia nani ambaye angekuwa amenitafuta kwa asubuhi hii. Nikakuta ujumbe kutoka kwa Tesha akiniambia kwamba aliwaendesha ndugu zake kwenda kwa Doris hii leo asubuhi, na nikiwa huru nimcheki ili aniambie jambo fulani.

Ilikuwa ni Tesha pekee ndiye aliyenitumia ujumbe, huku Miryam, Soraya, askari Ramadhan, pamoja na yule Kevin bwana wake na Jasmine wakiwa wamenipigia. Cha kwanza ikawa ni kumpigia Miryam upesi, lakini hakupokea mara zote tatu nilizojaribu. Bila shaka wangekuwa wameshafika huko kwa Doris labda alikuwa na mambo ya kufanya, kwa hiyo nikamtumia ujumbe nikisema akiwa huru anicheki pia. Nikamjibu na Tesha, halafu nikaamua kumpigia na askari Ramadhan. Soraya nikampiga chini kabisa kwanza.

Jamaa alipopokea ndiyo akaniambia sasa yaani huko alikokuwa ameenda kuangalia miili ya wale wafungwa, mpaka alichoka. Ilikuwa imeungua vibaya kinoma, wote wakiwa kama wamekaangwa yaani mpaka sehemu za mafuvu kuonekana, isingekuwa rahisi kutambua nani ni nani. Lakini waliipima yote kuchunguza DNA, na kweli kabisa mmoja wao ulikuwa ni mwili wa Bertha. Dah! Ndiyo ikawa imeenda hiyo, Bertha hakuwepo tena. Ramadhan akaniambia alikuwa amenipigia ili tuongee kuhusu ishu niliyosema ningemwambia, ila kwa sasa alikuwa akishughulika na mambo fulani, hivyo angenitafuta akiwa na uhuru. Yaani kila mtu alihitaji uhuru kwa hii siku!

Tukawa tumeachiana hapo, nikiwa nahisi huzuni kiasi kwa kilichompata "madam," nami nikaamua kwenda kupiga usafi wa mwili kisha ndiyo niondoke kuelekea kwenye ishu niliyotaka kufanya leo. Na ilikuwa kwa ajili ya bibie wangu. Ankia alikuwa ameshaenda kazini kwake, akiacha chai na mkate alionunua asubuhi zaidi nadhani, nami nikaoga na kuvaa vizuri kabla ya kunywa chai upesi, kisha nikatoka hapo kwake ikiwa imeshaingia mida ya saa sita. Moja kwa moja mpaka Mzinga, na nikapita eneo la dukani kwake Ankia na kumpungia mkono wa 'tutaonana baadaye,' kisha nikaenda kuchukua usafiri.

Wakati nimekaa tayari ndani ya daladala na yenyewe kuanzisha mwendo, Miryam akanipigia, nami nikapokea kumsikiliza. Akaniambia kitu ambacho sikuwa nimetarajia. Yaani kumbe alikuwepo pale kwake, hakuondoka pamoja na wengine shauri ya kujisikia vibaya sehemu ya tumbo lake kwa chini alipoamka mapema leo. Ih! Nikamwambia yaani ndiyo nimeondoka sasa hivi kwa Ankia, kama angekuwa amenitafuta dakika moja nyuma mapema zaidi ningegeuka kurudi kwake, lakini akaniambia haina tatizo; niende nilipokuwa naenda na tungekuja kuonana baadaye.

Nikamuuliza shida ya tumbo ilikuwa nini, naye akaniambia hiyo asubuhi alijitahidi kwenda maabara kupima akidhani ana tatizo kubwa, ila akaambiwa haikuwa shida, bali ni mwili wake tu uliitikia jambo jipya ulilojihusisha nalo hivi karibuni ambalo hakuwa amelifanya kwa muda mrefu. Nikawa nimeelewa. Alipokea dawa za kutuliza maumivu kiasi, na akashauriwa awe na kawaida ya kushiriki tendo la kimahaba na mwenzi wake ili hiyo hali isimpate tena, maana kuna sehemu humo ndani-ndani zilikuwa zimedhoofika ila sasa ndiyo zingekuwa imara zaidi. Ndiyo mwili wake tu ulivyokuwa.

Ahaa? Nikamwambia anisubiri sasa niwahi kurudi, ningekuja na dawa nzuri zaidi. Akasema acha ujinga, niende nilipokuwa naenda na niishie huko huko. Tukaachana nikiwa nahisi furaha kweli, licha ya kwamba bado kuna mengi yenye utata yaliyokuwa yananizunguka, nami nikatulia tu kusubiri safari inifikishe nilipodhamiria kwenda na nirudi haraka kwa mpenzi wangu.

★★

Nimekuja kumaliza mipango yangu yote iliyokuwa imenipeleka maeneo ya huko Morocco kwenye mida ya saa nane, na nikaamua kurudi Mbagala upesi sana kwa kuchukua bodaboda kutokea huko moja kwa moja. Nilitaka kuwahi kwa Miryam kabla familia yake haijarejea, maana nilikuwa nimeshawasiliana na Tesha pia na yeye kuniambia angewaleta wote jioni. Kwa hiyo haikuchukua muda mrefu sana, yaani saa tisa tu nikawa nimeshafika Mbagala. Huyu boda angenila hela nyingi sana kama ningesema anishushe mpaka Mzinga, kwa hiyo nikampa chake hapo Rangi Tatu, kisha nikaamua kupanda bajaji ya jero.

Wakati bajaji ikiwa mwendoni, nikampigia Miryam kumjulisha kwamba nilikuwa njiani, kimasihara nikimwambia "jiandaee." Kama kawaida yake akaweka pingamizi, lakini akawa ameniomba nipite kwenye duka wanalouza samaki wale wabichi ili nimchukulie sato wakubwa kilo mbili, halafu eti angenilipa hela yangu nikimfikishia mboga hiyo aliyotaka kuandaa kwa ajili ya familia yake, ili kufikia muda ambao wangerudi wapate mlo mzuri. Na alitia ndani viungo na mboga za majani, nami kiutani nikamwambia haina shida, chochote kwa ajili yake ningefanya. Akanishukuru kwa utayari wangu kumtimizia ombi lake.

Basi, baada ya kushuka hapo Mzinga, nikaingia sokoni kulitafuta duka wanalouza hao samaki, lakini kwanza ikanibidi nitafute mifuko miwili ili nibebee vitu ambavyo ningechukua. Nikiwa kwenye duka moja kuchukua mifuko hiyo, nikaona kwamba palikuwa na bidhaa za ice cream, zile nzuri za kwenye makopo ambazo ni tamu sana na huwa na tuvijiko twa kutumia. Nikawaza ingekuwa poa sana kama ningemchukulia Miryam kopo moja, baridi la ice cream lingeenda kumsaidia kupoza-poza na hilo tumbo lake, hivyo nikanunua ya shilingi elfu saba, vanilla flavor, kisha ndiyo nikaelekea kufata samaki na viungo kwa ajili ya mapishi ya mpenzi wangu.

Mwendo mdogo mdogo mpaka nikawa nimefika kwake Miryam, na wakati huu sikupita kwa Ankia, nami nilipofika getini kwao nikapita moja kwa moja hadi ndani na kuingia sebuleni. Kile kikamba getini kilikuwa kimesharudishwa. Hapo sebuleni palikuwa na hali ya utupu shauri ya wanafamilia wake kuondoka, nami nikavipeleka jikoni vitu alivyoniagiza bibie huku nikimwita kumjulisha kwamba nilikuwa nimefika. Akaitikia kutokea chumbani, lakini sauti yake ilisikika kwa umbali kiasi utadhani ilizibwa, nami nikaona nizipeleke samaki kwenye friji ili ziendelee kupigwa na ubaridi.

Nikiwa usawa huo ndiyo nikaanza kusikia sasa sauti ya maji kumwagika kutokea huko chumbani kwake Miryam, nami nikakisia kwamba alikuwa akioga. Nikatabasamu kiasi kwa kuwaza ni namna gani angefanana akiwa anadondokewa na maji sehemu za mwili wake, nami nikaitoa ice cream niliyokuwa nimemletea na kusogea sehemu ya korido lililoelekea chumbani kwake.

"Mimi... nimekuletea zawadi," nikamwambia hivyo kwa sauti.

"Zawadi wapi? Sema tu umetumia shilingi ngapi, nitoke nikulipe kabisa. Usiniongezee madeni..." akaongea kimasihara.

"Ahahah... hivi we' unanionaje?"

"Kama ulivyo. Na hao samaki inabidi nije kuwakagua ndiyo ulipwe sasa."

"Ahaa? Kwa hiyo itategemea na matokeo ya ukaguzi wako ndiyo utaamua nalipwa vizuri ama vibaya?"

"Sijasema hivyo. Ila nikikuta umeleta wabaya, na malipo yanashuka..."

"Thubutu! Yaani hapa unarudisha mkopo na riba," nikamtania namna hiyo.

Nikasikia maji yakiwa yameacha kumwagika, na hakutoa itikio lolote baada ya mimi kusema hivyo.

"La sivyo we' ndo' nitakushukia. Unataka nikushukie?" nikamuuliza kiutani tena.

Hakujibu, badala yake nikasikia tu sauti kama ya mlango ukiwa unafungwa, nami nikahisi ndiyo alikuwa akitoka bafuni mule mule chumbani kwake. Nikawa nataka nimsemeshe tena, ila kukaingia mawazo mengine ndani ya kichwa changu yaliyofanya nisisimke kiasi. Hapa, tulikuwa tumebaki wawili tu mimi na mwanamke aliyekuwa mpenzi wangu, halafu ndiyo alitoka kuoga. Nini kingine kingekuwa bora zaidi kama siyo kujionea jinsi ambavyo alifanana kwa wakati huu? Na tena isingekuwa kuona tu, nilitaka nicheze naye kabisa ikiwezekana, maana hata maabara ilihalalisha mimi kuwa dawa ya tatizo lake la tumbo. Ningempa dawa!

Kwa hiyo nikaamua kuelekea upande wa chumba chake taratibu tu, huku kopo la ice cream niliyomletea likiwa kiganjani. Nilipofikia hapo mlangoni nilikuwa nachekelea kichini-chini kama mtu mwenye hila fulani hivi, kisha taratibu nikakizungusha kimkono cha kitasa na kuusukuma mlango uingie ndani. Mlango haukutoa sauti mwanzoni mpaka nikawa nimeweza kumwona Miryam sasa. Aisee! Yaani ilikuwa kama vile nazidi kuona kitu kipya tu kutoka kwake kila mara.

Alikuwa usawa wa kitanda chake, mwilini akijifunga kwa taulo nyeupe kutokea kifuani mpaka usawa wa mapaja yake, huku akitumia nyingine kukausha maji kutoka kwenye nywele zake laini. Alikuwa amenipa mgongo, hivyo niliweza kutalii vyema namna ambavyo kalio lake lenye kutamanisha kwelikweli lilivyotikisika alipokanyaga hapa na hapo kadiri alivyoendelea kujikausha maji, na jinsi ngozi yake nyeupe na nyororo sana ilivyopendeza kuanzia juu mpaka chini, ikiwa haina doa hata chembe yaani utadhani alivaalisha yote ngozi ya plastiki. Bado nilikuwa naendelea kuusukuma mlango taratibu, ndipo ukatoa sauti ndogo ya kukwaruza.

Miryam akageuka na kuniona sasa hatimaye, nami nikawa namtazama kwa hisia sana machoni.

Akakunja sura kimaswali kiasi na kusema, "Jayden..."

Nikatabasamu kiasi na kuuachia mlango sasa.

"Ah, umenishtua. Nakuja, subiria nivae," akasema hivyo na kasauti kake.

Nikaendelea kumwangalia usoni kwa upendo.

Akaendelea kujifuta-futa nywele na kusema, "Jayden nenda bana, nataka kuja kupika. Acha kuniangalia hivyo... nenda huko. Pisha nivae."

Nikaanza kupiga hatua kumwelekea.

Akaacha kujifuta nywele na kusema, "Sijakwambia uingie, rudi huko. Nimesema rudi huko nivae."

Alikuwa anatabasamu kiasi, nami nikamuuliza, "Kwani kuna shida yoyote ukivaa na mimi niko humu?"

"Ahah... ee ipo. Hiyo hapo imeshasimama," akasema hivyo na kunionyesha kwa ishara ya macho kuelekea suruali yangu.

Nikajiangalia na kucheka kidogo kwa pumzi, kisha nikamwambia, "Hapo mbona haijasimama? Inajaribu tu kuchungulia. Wala siyo shida. Tena ni dawa yako hii."

"Jayden hebu acha mambo yako. Rudi bwana sebuleni nivae," akaongea kwa kumaanisha.

"Mbona unaekti kama vile itakuwa mara ya kwanza kukuona?"

"Haijalishi. We' nakujua, ukibaki humu itanichukua zaidi ya masaa mawili kuvaa," akasema hivyo.

Kauli yake ikanifanya nicheke kidogo, kisha nikamwambia, "Kweli, unanijua vizuri."

"Nenda bwanaa..." akasema hivyo huku akinisukuma kiasi.

"Sawaa. Nilikuwa tu nimekuletea zawadi hii hapa, e?" nikamwonyeshea kopo la ice cream.

Akaliangalia na kutabasamu kwa kukunja midomo yake, kisha akalipokea na kuliweka kwenye dressing table yake karibu na ukuta uliojengewa makabati ya nguo.

"Asante. Haya nenda sasa," akasema hivyo huku amenishikia kiuno.

Nikatabasamu na kumtazama mwilini kimchezo. Akakaza macho yake kuonyesha hatanii. Nikamwonyeshea ishara kwa kidole kwamba anibusu mdomoni kisha ndiyo niondoke, naye akaonekana kuudhika sasa.

"Jayden lakini, mbona unakuwa hauko... nenda bwana, muda una... ah..." akaongea kwa njia ya kulalamika.

"We' ni-kiss, kwani saa ngapi?" nikamwambia hivyo.

"Jayden!" akatumia sauti yake kuonyesha mkazo.

"We' ndo' unajichelewesha. Ungekuwa umeshavaa tayari, kiss moja tu ingemwondoa JC hapa," nikamwambia hivyo.

Akashusha pumzi eti kwa njia ya kukerwa, kisha akanifata mdomoni na kugusisha wake mara moja, kisha akasogea nyuma tena. Khh!

Nikamuuliza, "Ndiyo nini sasa?"

"Busu yako hiyo moja..."

"Ahaa... ndo' busu hiyo?"

"Eeeh..."

"Haka kaujeuri unakatoa-toa wapi?"

"Bafuni, kwa sababu nahitaji kupaka mafuta yangu, nilainishe ngozi, lakini wewe na bichwa lako umekuja na kusababisha nimekauka kabisa sasa!"

"Me na bichwa langu? Sss... ni kweli ila, hili bichwa huku chini limekaza balaa... sina tiba ya kuilainisha ngozi yako zaidi ya ilivyo laini, lakini bichwa langu linaweza kukulainishia zaidi sehemu fulani nzuri zaidi ya ngozi yako tu, maana leo umetoka kuambiwa ni dawa. Ungependa ikulainishie?" nikaongea haraka-haraka kimchezo.

Akazuia kicheko na kusema, "Sitaki lolote, me nataka kuvaa. Nenda bwana me ni...."

Nikakishika kiuno chake ghafla na kumvuta kwangu mpaka miili yetu ilipogandana, naye akaonyesha sura ya taharuki akiwa karibu zaidi na uso wangu.

"Jayden, ni nini lakini?" akauliza hivyo huku akijaribu kujinasua.

"Busu moja tu..." nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

"Si meshakupa? Ah..." eti akawa anadengua.

Nikapandisha mkono wangu mmoja mpaka nyuma ya kichwa chake, nikiishika shingo yake taratibu, naye akaniangalia usoni kwa njia tulivu zaidi. Nilikuwa namtazama kwa hisia sana.

"Jayden... tunaweza kukutwa..." akaendelea tu kulalamika.

"Na nani? Wote wameondoka," nikamwambia hivyo.

"A-ah, hata kama. Hii siyo sehe...."

Nikanyamazisha maneno yake kwa kufata mdomo wake na kuanza kumbusu kwa mahaba ya hali ya juu sana. Na hakuwa amekosea, nilisimama dede kwa nguvu zote hasa baada ya kuanza kumdendesha namna hiyo, naye akawa anazipokea busu zangu kwa hamu pia. Nilikuwa nimeshajua namna ya kumlegeza huyu mwanamke, yaani kumbusu tu tayari akawa kama anataka kuanguka. Ni jana tu asubuhi tulipiga hii mambo, lakini nikawa nimeshamhamu vibaya mno. Piga denda moja ya ajabu, na hivi alikuwa na midomo laini!

Nikaendelea kunyonya midomo yake na ulimi wake mtamu kwa njonjo kama zote, huku mkono wangu uliomkamata kiunoni nikiutumia kupandisha taulo yake taratibu kutokea pajani, naye akaushika na kuutoa. Akawa anajaribu kuikwepa busu yetu kwa kuupeleka mwili wake huku na huku, lakini nikaukamata huo mkono wake na kuubana mgongoni kwake huku nikijikandamiza zaidi mwilini mwake, kisha nikaushusha mkono mwingine na kuupitisha katikati ya miili yetu kwa chini mpaka kufikia katikati ya mapaja yake manono.

"Jayden..."

Akaita hivyo katikati ya busu yetu, nami nikakiweka kiganja changu usawa wa kibofu chake na kuanza kusugua sehemu hiyo ya juu kwa vidole. Yaani palikuwa panateleza kama vile pamemwagiwa mafuta lainii, naye akaanza kutoa miguno yake myembamba ndani ya mdomo wangu. Nilikuwa nimeanza kumpeleka mbali, na sikutaka safari ikome. Nikiwa nakisugua kitoweo chake kwa juu, akapitisha mkono wake mmoja mpaka juu ya kichwa changu na kunikamata nywele kwa nguvu, kama kawaida yake, naye hatimaye akawa anaiendeleza denda yetu kwa kupenda.

Nikaona ameanza kunogewa, hivyo nikauachia mkono wake nilioubana mgongoni kwake, naye akauleta mpaka kichwani kwangu kuuunganisha na mwingine kukishika kichwa changu, denda ikiwa pale pale. Nikayakamata makalio yake kwa pamoja na kuanza kuyafinya kwa nguvu kiasi ndani ya taulo yake, naye akajitoa mdomoni mwangu na kuanza kuhemea juu-juu. Nikaanza kuibusu shingo yake, huku nikitembeza mikono yangu kwenye mwili wake na kuonyesha kutaka kumtolea taulo, lakini akaikaza usawa wa kifua chake kwa mkono mmoja. Dah, yaani Miryam!

Nikaona isiwe shida. Nikaanza kumsukuma polepole kukielekea kitanda, na kwa sababu ya kutotarajia kukifikia haraka akawa amekaa kwa kishindo kama vile kajitupia. Uso wake ukawa usawa wa sehemu yangu ya suruali iliyotuna haswa, naye akaniangalia usoni kwa macho legevu. Nafikiri alidhani nataka anifanyie usafi wa eneo, lakini hapana. Mimi ndiyo nikapiga magoti chini karibu kabisa na mapaja yake, kisha nikayaachanisha na kujiweka katikati huku nikiufuata mdomo wake tena, kwa kuwa nyuso zetu zililingana.

"Jayden, we shouldn't be doing this here...."

Nikanyamazisha kimombo chake cha kulalamika tena kwa kuanza kumbusu mdomoni, na alikuwa hajambo katika kuupokea vyema sana ulimi wangu. Busu zetu zilitoa sauti tamu sana za mifyonzo kama tuko kwenye movie ya kizungu yaani, kisha ndiyo nikaanza kushuka taratibu kuelekea mapaja yake. Eti bado akawa ameikazia taulo kifuani, nami nikatabasamu kiasi na kufikisha uso wangu karibu na uanamke wake. Ah!

Maelezo ya hii kitu nilishayatoa kwa hiyo unaweza tu kuelewa kwamba niliikubali kinoma yaani. Halafu sasa kwangu mimi haikuchelewaga kujilowanisha, yaani mimi hapa ndiyo nilikuwa furaha yake. Safi, lainii... mzee nikazamisha ulimi! Nyonya, nyonya, nyonya, nyo-nya, nami nikawa namwangalia Miryam na kuona jinsi alivyopumua kwa kulegea na kupeleka kichwa chake huku na huko taratibu. Nikaendelea kumnyonya tu na kucheza na titi lake moja baada ya kuingiza kiganja changu ndani ya taulo yake, naye akaweka kiganja chake kwenye nywele zangu na kuanza kuzivuta.

Nadhani wote tuliweza kusikia pale simu yake ilipoanza kuita, lakini kwa pamoja tukaipuuzia kama vile haikusikika. Utamu ndiyo ulikuwa umeanza kumkolea bibie. Nikaendelea kumnyonya kitoweo kwa ufundi, mara nyingine akishtuka na kukisukuma kichwa changu, lakini ningeendelea tu kumpa ladha ya ulimi mpaka akaanza kuzungusha kiuno chake taratibu usoni kwangu.

Nikaacha kunyonya kwa ufupi na kumsemesha kidogo, "You like it baby?"

Akatikisa kichwa kukubali, kisha akasema, "Yes... sss... I like it..."

Nikaendelea kumnyonya kitoweo chake taratibu.

"Mmmhh... Jayden...."

"Naam..."

"Hapo hapohh..."

"Yes baby..."

"Ahhh... usiniite baby..."

"Ahahah... yes ma'am. Hapo vipi?"

"Hhh... hapo sawa..."

Alikuwa na masharti kweli, yaani dah! Ila ndiyo aliifanya hii kitu inoge sana, basi tu hakujua.

Nikakatisha unyonyaji hatimaye baada ya dakika kama kumi kabisa kuonekana kupita, na kweli nilipenda kuinyonya hii kitu aisee. Akalegea zaidi na kulalia mgongo wake huku akipumua kichovu fulani hivi, nami nikaona nitoe nguo zangu zote fasta wakati alipokuwa hanitazami.

"Basi, inatosha Jayd...."

Alipofumbua macho na kukuta sina nguo hata moja, akakodoa macho yake na kuegemia kiwiko huku akinitazama kwa kushangaa.

"Ja.... mbona ume...."

"Achana na maswali ambayo unajua majibu yake Mimi..." nikamwambia hivyo.

"Lakini Jayden...."

Nikajirusha kitandani na kuanza kumvuta, naye akawa anaweka mgomo.

"No, ach.... Jayden hapa siyo..."

Nikaendelea kulazimisha kumvuta, nikijiweka katika hali ya kulala chali ili niuvute mwili wake uje juu yangu. Na pamoja na usumbufu wake lakini nikafanikiwa kumburuza mpaka tukawa tumepandana katikati ya kitanda. Akawa anagoma kuiachia taulo yake, huku akinikalia usawa wa kiuno changu, kalio lake likiisukuma mashine yangu kwa nyuma. Nikaendelea kuishikilia mikono yake pande za viwiko.

Akiwa amekunja sura, akasema, "Jayden, no please... jaman.... nimetoka kuoga..."

Akanifanya nicheke kidogo, kisha nikamwambia, "Acha nikupe dawa kidogo tu... bafu si lipo?"

"Mm-mm..." akatikisa na kichwa kukataa.

Nikaukamata mgongo wake ili kuulazimisha mwili wake unilalile zaidi na kumwambia, "Hauoni nilivyowamba? Inabidi unitulize. Ukiniacha tu hivi hivi nikaenda kuiweka kwa mwingine?"

"Ah, we' nenda tu..." akaongea kwa kudeka.

Nywele zake laini zilikuwa karibu na uso wangu kwa hiyo zilinitekenya kiasi, nami nikalipiga kalio lake kofi kidogo na kulitikisa kwa kiganja.

"Jayden mbona husikii? Niachie..." akaongea kwa kudeka.

"Haya," nikamwambia hivyo.

Kweli nikamwachia, na ile ameanza kujinyanyua kwa kuutoa mguu wake mmoja, mimi nikaishika mashine yangu kwa mbele na kisha kuukandamiza mwili wake tena ili asiutoe upesi, na nafasi ndogo iliyoachia ikaniruhusu nikiweke kichwa cha msuli wangu usawa wa kitoweo chake. Akaweka mkono wake mmoja kifuani kwangu na kunikandamiza huku akiachama na kujikaza kimwili, nami nikatumia nafasi hiyo ya kuganda kwake kuanza kuuingiza mtalimbo ndani. Ai, hilo joto! Yaani kama alikuwa ananipasha mwili mzima.

Nikaendelea kuiingiza mashine, yeye bado akiwa ameuinua mguu wake mmoja kiasi, kisha akaurudisha katika mtindo wa kupiga magoti akiwa ananikalia sasa. Taratibu. Akainyoosha shingo yake kuelekea juu kidogo na kuweka mikono yake yote kifuani kwangu, kisha akanitazama kwa macho yenye uzito. Ah, nilijihisi vizuri sana! Joto lake lilikuwa tamu balaa!

Taulo yake ikataka kuachia, lakini akaweka mkono wake mmoja hapo kuziba, sijui huu mtindo ulikuwa wa makusudi tu ama labda kuna kitu alikuwa anaficha? Ila sikujali hapo sana, nikawa tu nasikilizia raha yenyewe kule mbele-kati baada ya yeye mwenyewe kuanza kupeleka kiuno chake mbele-nyuma taratibu.

"Ohh yes... sss... Jesus... Jaydenhh..." akaongea kwa hisia.

"Ahah... ushaanza kuniita hadi Jesus?" nikamwambia hivyo kiutani.

Akatoa tabasamu lililojaa hisia za kimahaba, naye akaelekeza uso wake juu tena na kuendelea kujisugua taratibu. Nikawa nayapapasa mapaja yake mpaka kalioni, kisha nikaikanyagisha miguu kitandani ili sasa niile bata vizuri baada ya yeye kuzoea mazingira. Nafikiri hakuwa ametarajia hili, kwa sababu nilipopandisha tu kiuno juu ghafla, akashtuka kiasi na kuniangalia usoni kama anashangaa, nami nikaanza kukuna.

Panda, shuka, panda, shuka, akawa ananesa tu huku akiguna, akijing'ata mdomo wake, na kurembua macho yake. Bado mkono wake mmoja aliuweka kifuani kwangu na mwingine kushikilia taulo yake kuficha sijui nini, nami nikaendelea kuchezesha kiuno juu-chini ili ni-enjoy zaidi utamu wake. Na utamu wake wote ulisikika vyema kwa jinsi alivyoguna kwa mideko na kuzidi kulegea tu.

Nikaanza kuongeza spidi kiasi, naye akakunja sura zaidi na kuiachia taulo yake. Akainamisha kifua chake kunielekea akiwa anasikilizia raha aliyopata bila kuacha kutoa miguno, na hapo akawa amenisogezea matiti yake mazuri sana usoni. Baraka! Nikayashika mashavu ya kalio lake na kuendelea kumkuna tu huku nikinyonya titi hili na lile kwa hamu kubwa, na kiuno chake kikawa kinatetemeka kadiri nilivyoendelea.

Dakika chache za kumpa raha namna hiyo zikanifanya nitulie kwanza ili kupumua kidogo, naye akaweka tena mikono yake kifuani kwangu na kuanza kukatikia hapo katikati. Jinsi kitoweo chake kilivyokuwa na utelezi na kuibana mashine yangu ndani kwa ndani, kujumuisha na mauno yake, yaani alinipeleka mbali sana huko juu kwenye hisia. Usipime! Kiuno chake kilikuwa laini, angekizungusha na kuanza kushuka na kupanda yeye mwenyewe, kisha nami ningeendelea kupampu ili kukutana na mapigo yake. Nilimpenda sana huyu mwanamke!

Dakika kadhaa zikawa zimepita tukipeana raha kwa mtindo huu huu, kwa sababu Miryam hakutaka nimgeuze. Yaani, alionekana kusikia raha sana iliyokuja kutokana na yeye kutetemeka miguu mara kwa mara, na nadhani mtindo huu ndiyo ulifanya hiyo itokee sana. Ndipo ikafika hatua akajikaza zaidi na kuanza kutetema huku sauti yake ikifuata huo mtetemo wake, naye akajitoa kutoka kwenye mashine yangu.

Akaniangukia mwilini, kichwa chake kikiwa kimekipita cha kwangu kwa hiyo uso wangu ulikuwa kifuani kwake, nasi tukawa tunapumua kwa uzito kiasi huku tukipapasana taratibu. Nikawa nambusu kifuani na shingoni, huku yeye akionekana kuisikilizia raha aliyokuwa ameipata kwa wakati huu. Nikatabasamu kiasi kwa kiburi maana nilikubali sana hii ishu ya kumtetemesha kama hivyo, nilijiona ngangali la hatari!

"You good?" nikamuuliza kwa sauti ya chini.

Akanyanyua uso wake na kunitazama machoni, kisha akasema, "Yes."

"Hamna maumivu?" nikamuuliza.

"Hamna. That was amazing," akajibu kwa hisia.

"Tamu eh? Haujuti sikurudi sebuleni?" nikamuuliza kimchezo.

Akatabasamu kwa hisia na kunilalia kifuani.

"Hhh... hadi raha. Sometimes hadi nakuwa naona ni kama ndoto kuwa nawe hivi," nikamwambia hivyo huku nikizichezea nywele zake.

"Na ndiyo nataka nikuje kukuwasha kofi ili uamke kutoka kwenye hiyo ndoto," akasema hivyo.

"Ahahah... kwa kosa gani tena?"

"Kunilazimu nihitaji kuoga mara ya pili."

"Oooh, lakini si ni baada ya ku-enjoy? Hilo kofi halitakuwa fair. Na kwanza sitaki hata kuamka..."

"Mhm... kwa nini?"

"Sijawahi kuwa kwenye ndoto nzuri kama hii. Sitaki kuamka kwa sababu nitakuwa na wewe muda wote wa kuiota..."

"Mmm?"

"Mm-hmm. Maisha halisi yamejaa maumivu tu, na hatuna jinsi ila kuyaishi. Ila kama ningeweza, ningechagua kuwa ndani ya ndoto hii kwa maisha yangu yote, kwa sababu wewe ndiyo ungekuwa kitu pekee ndani yake ambacho kingeifanya ndoto isiwe ndoto tena... bali uhalisia," nikamwambia hivyo kwa hisia.

"Unayatoaga wapi hayo maneno?" akauliza.

"Moyoni, Miryam. Moyoni," nikamwambia hivyo.

Akanyanyua uso wake taratibu na kuutazamisha karibu zaidi na wangu, naye akazirudisha nywele zake nyuma ya sikio na kuanza kunibusu mdomoni taratibu sana, akiuvuta mdomo wangu wa chini huku ananiangalia kwa upendo machoni, halafu akachezesha pande za mdomo wake wa juu kunielekea kwa njia fulani kama vile mnyama mkali anayeng'ata afanyavyo, akitishia kuning'ata kiutundu yaani, nami nikatabasamu na yeye akacheka kidogo na kulaza kichwa chake kifuani kwangu tena.

"Ushageuka kuwa mtundu hivi?" nikamuuliza hivyo huku nikilaza nywele zake taratibu.

Akacheka kwa pumzi na kusema, "Naona raha, Jayden. Unanipa furaha kubwa sana yaani, hata kwa wakati ambao sitarajii..."

"I'm glad," nikamwambia hivyo kwa kuridhika.

"Halafu Jayden, nakuomba... punguza kuwa unanunua-nunua au kuleta vitu vingi sana hapa," akasema hivyo.

"Nini tena? Hauitaki ice cream?"

"A-ah, namaanisha si kama hivyo jana nimekuta umewanunulia wakina mama nguo, na Mariam... usipende kufanya hivyo..."

"Kwa nini? Ni vibaya?"

"Siyo vibaya, ila... sitaki uwazoeshe hayo mambo. Sioni kama italeta picha nzuri mbeleni," akasema hivyo.

"Sawa Mimi. Nimekuelewa. Moja ya njia ambazo kwetu huwa tunaonyesha kuwajali wengine ni kuwanunulia vitu na nini... nilifikiri si mbaya nikifanya hivyo na kwa familia yako," nikamwambia kwa upole.

Akashusha pumzi kiasi na kusema, "Naelewa pia. Sema... kwa sasa bado, sisemi ni vibaya, ila uwe na limit tu baba. Utawanunulia chochote unachotaka ukishaniweka ndani."

Nikacheka kidogo na kumpiga kofi laini kwenye kalio lake.

Akasema, "Inabidi ninyanyuke. Sijui hata tumekaa hapa kwa muda gani..."

"Masaa mawili kabisa..."

"Ahahah... sikukosea eh? Busu moja uliyotaka imezaa masaa mawili."

"Hahah... huwezi kunilaumu. Mpenzi wangu we' wa moto sana..." nikamwambia hivyo huku nikisugua mkono wake taratibu.

"Mhm... eti wa moto! Unanifanya nalegea mno we' kaka, yaani sijui itakuwa sahihi zaidi tukisema unatumia dawa kuni...."

Kabla Miryam hajamaliza maneno yake, sote tukashtushwa na sauti ya mlango kufunguliwa kutokea pale sebueni, nasi tukaangalia upande wa mlango wa chumba hiki. Ih! Kumbe sikuwa nimeufunga mlango wa chumbani kwake Miryam wakati nimeingia muda ule mpaka tumemaliza mambo yetu? Si ndiyo kuuangalia sasa tukakuta bado uko wazi!

Lakini ishu ikawa juu ya ni nani aliyekuwa ameingia kule sebuleni, maana kama ni familia yake Miryam, wote walikuwa wameenda kule kwa Doris. Miryam akajinyanyua kutoka juu yangu na kuivuta taulo yake, huku mimi pia nikikaa.

"Ni nani huyo?" nikamuuliza kwa sauti ya kunong'oneza.

"Sijui. Eh, ngoja nifunge mlango kwanza..." Miryam akasema hivyo upesi.

Akaifunga taulo yake mwilini ili aende kurudishia mlango wa hapa chumbani kwanza, nami nikavuta boksa yangu na kuanza kuivaa. Sijui ni nani alikuwa ameingia huko, ila... alikuwa ametuchanganyia habari kabisa. Miryam akauelekea mlango wake na kuanza kuuvuta ili aufunge, pale ghafla tu kutokea nje ya chumba alipotokezea Shadya!

Nilishtuka. Miryam akaishia kuushikilia tu mlango akiwa ameusitiri mwili wake kwa taulo fupi, bila shaka akimwangalia mwanamke huyo kwa mshangao, huku mimi hapo kitandani nikiwa ndani ya boksa tu! Nilipomtazama Shadya kwa umakini, niliona namna ambavyo alimtazama Miryam pamoja na mimi kwa kutoamini, naye Miryam akanigeukia na kunitazama kwa wasiwasi.

"Mungu wangu! Mimi!" Shadya akasema hivyo.

Ikanibidi nianze kuvaa nguo zangu shuta, nikiwa najilaani moyoni kwa kutokuwa makini mpaka kusababisha hali hii mbaya sana itokee. Kwa jinsi Shadya alivyokuwa, yaani najua mambo yangeharibika upesi.

"Mimi... nini hiki unafanya?" Shadya akauliza.

"Shangazi... ona... njoo, ingia nikuelezee..." Miryam akasema hivyo.

Nikawa nimemaliza kuvaa suruali na T-shirt langu, nami nikaona Shadya aliposogea ndani zaidi na kusimama karibu yake Miryam, huku akitutazama kwa mshangao bado.

Miryam akasema, "Shangazi, usifikirie vibaya. Usi... haiko kama inavyoonekana, yaani...."

"Ila ikoje?" Shadya akamkatisha.

Nikawa nimetulia tu nikiwaangalia kwa umakini, naye Shadya akanitazama.

"JC... mambo gani haya? Yaani, unaacha kwenda kufanya mambo yako unakuja kumvua nguo huyu mwanamke mtu... kwa nini umekuja kumfedhehesha namna hii?" Shadya akanisemesha namna hiyo.

"Shangazi..." Miryam akaita kwa huzuni.

"Na wewe Miryam! Kweli, yaani wewe?! Nilikuwa nakupigia simu kukwambia mambo ya muhimu, hupokei, kumbe uko unafanya haya maujinga? Tumekutafutia wachumba wangapi mama? Wachumba wa maana, wote umewakataa... unadai hauko tayari kuwa na mwanaume yeyote lakini kumbe unataka kutoka na watoto wadogo? Ai jamani, sikutegemea Miryam. Kweli ni wewe?" Shadya akasema hivyo.

"Shadya... usifikirie hivyo. Miryam na mim...."

"Kaa kimya, JC. Kaa kimya. Huoni aibu? Me nilikuona kuwa kijana mstaarabu lakini kumbe... umekuja tu kumharibia maisha huyu dada, si ndiyo? Kwa hiyo kumbe umefanya kila kitu kumsaidia Mamu, Tesha, sijui nani, na sasa hivi Miryam ndiyo anakulipa kwa kukuvulia nguo, eh?" akanisemesha namna hiyo.

Nikaingiwa na hasira kiasi, nami nikasema, "Maneno unayoongea siyo ya kweli. Kwa nini usimsikilize... kwa nini usitulie uelezewe vizuri badala ya kusema maneno makali namna hiyo?"

"Maneno makali?! Unayajua maneno makali wewe? Unajua hiki chumba walikuwa wanalala wakina nani? Yaani... umekichafua chumba ambacho marehemu wazazi wa Miryam walikuwaga wanakitumia, na Miryam anakitumia ili kuwaenzi...."

"Shangazi..." Miryam akaita kwa hisia.

"... halafu unakuja kuingia na kumrubuni afanye upuuzi pamoja nawe? We' Miryam... unafikiri mama zako wakija wakajua unafanya haya mambo na huyu mtoto watakuonaje? Eh? Amekufanyaje huyu kijana mpaka akili yako imehama? Unawaachia wengine waende kwa Doris ubaki peke yako kisa eti unasema unaumwa, kumbe ni ili ubaki kufanya huu ujinga? Kweli kabisa?" Shadya akaendelea kulalama.

Miryam alikuwa amebaki kimya tu huku akiangalia pembeni kwa huzuni, nami nilikuwa nataka hata kumwambia aache kuwa mnyonge namna hiyo na kuongea ukweli wa hisia zake kwangu ili ifahamike kwamba jambo letu lilikuwa na maana zaidi ya ujinga.

Shadya akapiga viganja vyake na kusema, "Heee... haki ya Mungu! Hii ya leo kali. Umemkataa mpaka na Festo, mkaka mzuri sana, ana vitu vingi vya...."

"Shangazi, basi!" Miryam akasema hivyo kwa uthabiti.

Shadya akatulia na kuendelea kumwangalia.

"Ninakuheshimu, lakini usinisemeshe kama vile me ni mtoto. Mimi ni mtu mzima, nina maamuzi yangu juu ya maisha nayotaka kuishi. Naomba unionyeshe heshima, maana sasa naona ni kama unataka kunipanda. Unataka kuniamulia mwanaume ambaye nitampenda? Ni maisha yangu au yako?" Miryam akamwambia hivyo.

Nikatabasamu kiasi kwa mbali kwa kuridhishwa na maoni hayo. Hivyo ndivyo ilivyotakiwa!

Shadya akasema, "Ahaa? Kumbe ndiyo iko hivyo? Sawa. Haya mama, endelea. Endelea tu, uone kama hii itakufikisha popote."

Miryan akaangalia pembeni na kutikisa kichwa kwa kusikitika.

Shadya akamwambia, "Kila mtu anakuheshimu Miryam, kila mtu anakupenda, lakini wakijua hii ndiyo tabia yako unadhani kuna hata mmoja atataka kuwa na urafiki na wewe? Utasemwa sana mtaani na sifa zako nzuri zitaharibika. Tena sifa ya familia nzima. Mimi nimeona mengi, na sawa sina undugu wa damu na nyie, lakini ninajua mengi sana na ninakupenda kama mwanangu. Maimuna, mama yako, kama angekuwepo sasa hivi, asingekubaliana na hivi vitendo vya kimalaya na watoto wadogo unavyofanya... maana vinaharibu taswira nzuri ya familia yake aliyoiacha... na nakwambia Mimi, umeshaanza kuiharibu. Ngoja tuje kusikia mama zako watasema nini kuhusu haya. Endeleeni na mambo yenu..."

Baada ya mwanamke huyo kusema hayo, akaelekea sebuleni tena, akituacha tukiwa tumesimama hapo kwa kuvurugiwa amani yote tuliyokuwa nayo. Nikawa namtazama Miryam na kuona jinsi ambavyo aliumia sana, yaani aliangalia pembeni tu kwa huzuni kuu, nami nikamsogelea mpaka karibu na kumshika mkononi. Akaniangalia usoni.

"I'm sorry," nikamwambia hivyo kwa hisia.

Akaweka kiganja chake mdomoni kiasi na kutikisa kichwa kukubali pole yangu huku akitazama chini.

"Tunahitaji kumwamb...."

"No Jayden, we'.... nenda tu. Tutaongea baadaye," akaniambia hivyo kwa upole.

"Lakini vipi kuhusu...."

Kabla sijamaliza kuongea, akaniangalia usoni kwa njia yenye msisitizo kuwa nimwache tu kwanza, nami nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

Nikakinyanyua kiganja chake na kukibusu mara mbili, kisha nikamshika shingoni kwa wororo, lakini hakuniangalia kabisa na kubaki ametazama pembeni kwa kufadhaika. Nikaona nimpite tu na kuondoka. Dah, yaani jamani! Wakati wetu mzuri ukawa umevurugwa vibaya sana, sijui hata ni kwa nini huyo Shadya alikuwa ameamua kuja wakati huu! Na alivyokuwa mbea sasa, hapo kama angeondoka yaani ndiyo angesambaza maneno hata kwa watu ambao hawakutufahamu.

Lakini sikujali. Najua kwa njia moja ama nyingine wenye kuongea wangeongea tu kuhusu uhusiano wangu na Miryam, hasa ukitegemea na aina yao tu ya maisha. Ila hakukuwa na chochote cha ajabu, ni basi tu ndiyo tungepaswa kuonyesha kwamba mahusiano yetu hayakuwa ya mtindo wa kuridhishana tu, bali yalikuwa ya malengo. Na nilikuwa tayari kwa lolote ambalo lingefuata baada ya hapo ili nithibitishe upendo wangu kwa mwanamke huyo kwa kila mtu ambaye angejifanya anajua sana kujaji. Hiyo ingetia ndani na mama wakubwa endapo kama na wao wangeleta dukuduku kama la Shadya.

Nilipofika sebuleni, nikamkuta Shadya akiwa amekaa sofani huku akichat, nafikiri kusambaza ubuyu sasa, yaani hakuchelewesha, nami nikampita tu na kuuelekea mlango huku nikiona alivyokuwa ananiangalia kwa macho yenye kisirani. Mzee nikatoka zangu tu hapo na kuelekea kwa Ankia, mpaka chumbani, nami nikajilaza kitandani kwa kutazama juu, nikiwa namtafakari sana Miryam wangu.








★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Pata Full Story WhatsApp au inbox

Whatsapp +255 678 017 280

Karibuni sana
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA THELATHINI NA TISA

★★★★★★★★★★★★★★★★★★★


Salumu alinisindikiza mpaka barabarani nilipopanda daladala kuelekea stendi ya Makumbusho, na baada tu ya kuingia humo na kukaa, nikachukua simu na kumpigia Adelina upesi. Nilikuwa nimeweka mambo haya pembeni kidogo kwa ajili ya kutumia muda zaidi na Miryam kutokea jana, lakini siyo kwamba nilisahau kabisa ile ishu niliyokuwa nimemwomba Adelina anisaidie kufatilia. Na yeye inawezekana alikuwa na mambo mengi ya kikazi ndiyo sababu hakunitafuta, hivyo sasa ukawa ndiyo muda mzuri wa kuhakikisha baada ya taarifa ya kifo cha Bertha kunifikia.

Mwanamke huyo akapokea simu yangu hatimaye, na baada ya salamu, nikaenda moja kwa moja kwenye pointi ili nisimkengeushe kutoka kwenye kazi zake. Nilimuuliza ikiwa aliangalia safari ya ndege ya jamaa mwenye jina Festus Yakubu, naye ndiyo akasema 'oooh kweli,' alisahau kunitumia jibu ingawa alilifanyia suala hilo utafiti. Akaniambia ni uhakika, mwanaume mwenye jina hilo alisafiri kwa ndege kuelekea Nairobi hiyo wiki iliyopita, jina lake lilikuwepo kwenye orodha ya abiria waliopanda kuelekea huko Kenya. Ahaa? Nikamwambia sawa, nikamshukuru kwa jitihada na kumwomba samahani kumsumbua kwa wakati huu, naye akasema haikuwa na shida kabisa, ndiyo tukaagana kwa ahadi za kuja kuwasiliana baadaye.

Nikawa nimehakikisha sasa kwamba kweli Festo alikuwa ameondoka nchini, na labda hata safari yake haingeishia Nairobi tu, huenda angekwenda sehemu zingine. Hivyo, kwa kiwango kikubwa sidhani kama na yeye angekuwa na mkono ndani ya ishu ya ajali iliyompata Bertha, ikiwa kama kweli hiyo ilikuwa ajali ya kupangwa. Umakini wangu wote sasa hivi kuelekea hilo suala ungepaswa kuwa kwa huyo Beatha, yaani ningehakikisha Ramadhani anamchimba kokote alikokuwa na kumchunguza vyema ili kumdaka na lolote lile haramu, na hivyo amweke pembeni haraka sana.

Kila hisi ndani yangu iliniambia kwamba hiyo haikuwa ajali, na ni baada ya muda mfupi tu ingefahamika zaidi. Ikiwa ingegundulika hako kadada ndiyo kaleta shida kapya kwa kipindi hiki, ningetakiwa kuhakikisha usalama wa familia yangu yote kwa ujumla, na familia ya Miryam pia, halafu nihakikishe hakaji kutusumbua tena hata kama kasingetaka kufanya hivyo. Tahadhari kabla ya hatari. Nikaendelea tu na safari mpaka Makumbusho stendi hapo, kisha ndiyo nikapanda gari ili nielekee Mbagala na Mzinga.

★★

Nimekuja kufika Mzinga kwenye mida ya saa moja usiku, shauri ya msongamano wa magari ulionikawiza kweli tulipofikia barabara iliyoelekea maeneo hayo. Nilifika kwa Ankia na kumkuta mwanamke huyo akiwa anapika, na alinipokea vizuri sana kama mgeni vile, akifurahi kuniona nimerejea. Alikuwa ananiambia eti alijihisi upweke kuwa hapo mwenyewe, nami nikamwambia acha zako wewe, yaani uko na Bobo unakuwaje mpweke? Akacheka sana na kusema ni kweli, Bobo ndiye aliyekuwa akimwondolea upweke na alijitahidi kweli kumpa raha zote alizohitaji. Eti akawa ananidolishia!

Alipomaliza kunidolishia Bobo wake ndiyo akaanza kuuliza mambo yangu na Miryam yalikuwaje huko tulikoenda huku akiangalia mizigo yangu na nini, nami nikampatia zawadi yake ya nguo niliyokuwa nimemnunulia bila kuongelea mengi sana ambayo nilifanya na Miryam. Sikuwa wa aina ya kudolishia mimi. Ila si akawa anataka kujua kama nilimtembezea bibie kichapo? Nikamwambia hiyo ni siri yetu, na kwa hapo tu akawa ameelewa kuwa ndiyo, Miryam nilikuwa nimeshammiliki rasmi kimwili baada ya kumteka kihisia.

Akanipa hongera ya bata niliyokula na kuniambia alikuwa anatayarisha msosi wa nguvu ili tule pamoja wakati huu, na Bobo mume wake angekuja ili atulishe sisi pamoja. Eti mume wake! Alikuwa ameshaanza kumwita hivyo nakwambia, nami nikasema sawa, wacha niende kuwasalimu wapendwa wangu hapo jirani na kuwapatia zawadi zao, kisha ndiyo ningerejea ili kupumzika.

Nikavua tu viatu na kubeba mfuko mmoja, na wakati nikiwa naelekea hapo kwake Miryam ndiyo nikatambua kwamba bibie hakuwa amerejea bado baada ya kumtumia ujumbe kuuliza ikiwa alikuwepo ndani, na yeye akajibu kusema hakuwa ameondoka Kijichi. Hivyo, nikaenda mpaka getini, na kama kawaida kimlango kidogo cha geti kingehitaji kuvutwa kwa kamba huku kwa nje ili kufunguka lakini nikakuta hicho kikamba kimetoka. Sijui nani alikitoa kwa huku nje, ila ikanibidi nigonge tu geti sasa maana kimlango kilifungwa kwa ndani. Nikasikia sauti za hatua zikija kutokea hapo ndani ya geti, nami nikatulia na kusubiri.

Hicho kimlango kilipofunguka, ikawa ni Mariam ndiye aliyekuwa amesimama hapo mbele yangu, na sasa hivi nisingemwita "binti Mariam" tena, alikuwa Mariam kamili sasa. Alinitazama kwa njia ya kawaida tu, akiwa ndani ya blauzi nyeupe yenye tiki ya Nike kifuani, pamoja na skinny jeans laini, na mtindo wa nywele zake ulikuwa vile vile wa rasta nene isipokuwa sasa alifunga ule urefu wa mapembe-rasta kwa pande za kichwa chake kama mabutu mawili makubwa. Hakuniamkia, wala kutabasamu, akaachia tu uwazi zaidi kwenye hicho kimlango na kuanza kurudi huko ndani.

Nikaingia na kumwita, "Mamu..."

Akasimama na kunigeukia.

Nikamsogelea, nami nikamwambia, "Haujambo?"

Akatikisa kichwa mara moja kukubali.

Nikarudishia mlango wa geti na kumuuliza, "Nani yuko ndani?"

"Wakina mama. Na Tesha," akasema hivyo.

Nikatoa mfuko mdogo kutoka kwenye mfuko mkubwa niliobeba, nami nikampa huku nikisema, "Nimekuletea zawadi."

Akaupokea na kuukunjia tu usawa wa kifua chake, naye akasema, "Asante JC."

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Mamu... nataka kujua ikiwa me na we' tuko poa. Yaani, sitaki kuwe na hali ya utengano baina yangu me na wewe... baada ya kilichotokea juzi. Nataka sana tuendelee kuwa marafiki."

Akabana midomo yake kiasi huku akiangalia pembeni, lakini hakutoa jibu.

Nikamuuliza, "Ama ndiyo umenichukia?"

Akaniangalia usoni upesi na kuweka macho yenye kujali, naye akasema, "A-ah. Siwezi kufanya hivyo JC..."

"Kweli?"

"Ndiyo. Sikuchukii... siwezi," akaniambia hivyo.

"Mbona unakuwa serious sasa kama vile...."

"Hapana, haimaanishi nakuchukia. Bado tu ninazoea hii hali... siyo rahisi ku... kubadilisha tu hisia. Bado ninakupenda," akaniambia hivyo.

Nikaendelea kumtazama usoni kwa kujali.

"Lakini kama tutaendelea kuwa marafiki tu, napaswa ku.... itachukua muda kuzoea, maana bado nikikuona...." akaishia hapo na kuangalia pembeni tena.

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa, nami nikamwambia, "Sawa. Nisamehe tu lakini Mamu. Siyo nia yangu kukuumiza kama hivyo."

Akaniangalia na kusema, "Usijali. Ni muda tu, ninahitaji muda tu. Nitazoea."

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Nitakusaidia ili uzoee haraka. Si unajua me Superman ikija kwenye suala la kukusaidia na nini?"

Akajitahidi kutabasamu kiasi na kuniambia, "Superman wapi? Huwezi hata kunyanyua hili gari."

Nikacheka kidogo na kusema, "Asa' hilo tu! Hii nyumba yote nabeba kwa haka kakidole!"

"Haa! Umdanganye mtoto," akasema hivyo na kutabasamu zaidi.

"Aahhahah... Nitakuja kukuonyesha..."

"Na ukishindwa?" akauliza.

"Basi nitakununulia kitu chochote unachotaka yaani," nikamwambia hivyo.

"Sawa. Tupinge," akasema hivyo na kuniwekea kidole chake kidogo kwenye kiganja changu.

Nikamwekea changu pia, naye akakivuta kwa nguvu kama kutia muhuri.

"Tena siyo nyumba, haka kagari tu. Ukishindwa kunyanyua, unaninunulia chochote kile nachotaka. Sawa?" akaongea hivyo kwa shauku kiasi.

Nikajikuta nimebaki kumtazama tu kwa hisia.

"Sawa?" akasisitiza swali.

Nikaondoa mzubao na kusema, "Poa. Si tumeshapinga? Kesho tu. Utaona."

"Haya," akasema hivyo.

Nikiwa natabasamu, nikamwekea kiganja changu kimoja karibu naye, na yeye akaniangalia na kutabasamu kiasi, kisha akaweka cha kwake hapo na kwa pamoja tukasema, "Brooop!"

Tukacheka kidogo tukiwa tumeanza kujenga kale kahali ka amani kazuri angalau, na ilinifariji, kisha baada ya hapo ndiyo tukaelekea huko ndani pamoja.

Warembo wangu, Bi Jamila na Bi Zawadi walinipokea kwa furaha sana, wakisema walikuwa wamenikosa kweli jana. Yaani tena Bi Zawadi akasema ikiwa sikumletea zawadi basi angeninunia, na ni kama nilikuwa nimeotea tu kumletea. Nikawapatia na wenyewe zawadi zao, nguo nzuri za wamama yaani, zenye vilemba na vitenge spesho vya kuweka begani, na ilikuwa imeniponyoka pesa nyingi kwa ajili ya hizo ila furaha yao ilipita gharama yote iliyotumika. Tesha akaja, eti na yeye akitaka zawadi, nami nikamwambia tungeenda kutafuta udongo mfinyanzi ili nimtengenezee gari zuri sana la kumpatia.

Ikawa ni pindi yenye kufurahisha sana, Mariam akaenda chumbani kujaribishia nguo yake niliyomletea na kuja kutuonyesha, na alikuwa amependeza kweli yaani. Ndiyo mama zake wakubwa wakasema wangevaa nguo hizi ikifika kesho, wakati wa kwenda kwake Doris. Sikujua kama walikuwa na huu mpango, nami nilipouliza, ndiyo wakanifahamisha kwamba Doris aliwaalika wote kwenda kumtembelea kwake mapema ya kesho, yaani familia yote iende kupaona huko kwake na mume wake maeneo ya Chanika. Kwa hiyo bila shaka Miryam angewapeleka, na walikuwa na hamu ya kuvaa vizuri tena kwenda kwenye hayo matembezi, kwa hiyo hapa nikawa nimewaletea ukombozi.

Basi, nimekaa-kaa hapo mpaka kwenye mida ya saa mbili usiku ndiyo nikawaambia ningeondoka sasa na kwenda huko gym, maana nilitakiwa kuendeleza ratiba ya kupiga mazoezi yangu ya mwili. Hawakuwa na shida kwa hilo na kuniambia kama nikipata nafasi basi nije tena hapa kwao, nami nikakubaliana nao. Tesha akaamua tuondoke pamoja ili akajiunge nami huko gym, na bibie Miryam hakuwa amerejea bado, kwa hiyo tukawaacha wanafamilia wake, nikaenda kwa Ankia kuvaa nguo nyepesi, halafu ndiyo tukaelekea gym.

Ilikuwa ni kwa uratibu wa kawaida tu kutokea hapo, yaani tukaelekea gym na Tesha kupiga tizi mpaka saa nne kasoro, kisha tukarudi nyumbani. Miryam tayari alikuwa amefika, na sikwenda kwake tena, ila tukawasiliana na mambo kuonekana kuwa poa hapo kwao. Akanijulisha kuhusiana na matembezi ya familia yake kwenda kwa Doris kesho na kusema labda tungekuja kukutana jioni ya kesho, na hilo halikuwa na neno. Tukaagana vizuri sana baada ya kuchat kwa video call hadi kwenye mida ya saa saba bibie alipoomba alale. Nikaanza kutafuta usingizi pia muda huo huo, kwa kuwa nilipanga kuamkia kwenye safari fupi siku ya kesho pia.

Jumatano ikapita.


★★★


Alhamisi asubuhi ilipofika, nikajikuta naamka ikiwa imeshaingia mida ya saa nne. Yaani nililala! Nafikiri shauri ya hiyo jana kuamka mapema mno na kugoma kurudi kulala tena, mechi zote tamu tulizocheza na Miryam wangu pia zikiwa zimeuleta huo uchovu nadhani. Ila kwa sasa nikaamka nikiwa najihisi vizuri sana mwilini, na kwa kuwa masaa yalikuwa yameenda, cha kwanza ikawa kuangalia nani ambaye angekuwa amenitafuta kwa asubuhi hii. Nikakuta ujumbe kutoka kwa Tesha akiniambia kwamba aliwaendesha ndugu zake kwenda kwa Doris hii leo asubuhi, na nikiwa huru nimcheki ili aniambie jambo fulani.

Ilikuwa ni Tesha pekee ndiye aliyenitumia ujumbe, huku Miryam, Soraya, askari Ramadhan, pamoja na yule Kevin bwana wake na Jasmine wakiwa wamenipigia. Cha kwanza ikawa ni kumpigia Miryam upesi, lakini hakupokea mara zote tatu nilizojaribu. Bila shaka wangekuwa wameshafika huko kwa Doris labda alikuwa na mambo ya kufanya, kwa hiyo nikamtumia ujumbe nikisema akiwa huru anicheki pia. Nikamjibu na Tesha, halafu nikaamua kumpigia na askari Ramadhan. Soraya nikampiga chini kabisa kwanza.

Jamaa alipopokea ndiyo akaniambia sasa yaani huko alikokuwa ameenda kuangalia miili ya wale wafungwa, mpaka alichoka. Ilikuwa imeungua vibaya kinoma, wote wakiwa kama wamekaangwa yaani mpaka sehemu za mafuvu kuonekana, isingekuwa rahisi kutambua nani ni nani. Lakini waliipima yote kuchunguza DNA, na kweli kabisa mmoja wao ulikuwa ni mwili wa Bertha. Dah! Ndiyo ikawa imeenda hiyo, Bertha hakuwepo tena. Ramadhan akaniambia alikuwa amenipigia ili tuongee kuhusu ishu niliyosema ningemwambia, ila kwa sasa alikuwa akishughulika na mambo fulani, hivyo angenitafuta akiwa na uhuru. Yaani kila mtu alihitaji uhuru kwa hii siku!

Tukawa tumeachiana hapo, nikiwa nahisi huzuni kiasi kwa kilichompata "madam," nami nikaamua kwenda kupiga usafi wa mwili kisha ndiyo niondoke kuelekea kwenye ishu niliyotaka kufanya leo. Na ilikuwa kwa ajili ya bibie wangu. Ankia alikuwa ameshaenda kazini kwake, akiacha chai na mkate alionunua asubuhi zaidi nadhani, nami nikaoga na kuvaa vizuri kabla ya kunywa chai upesi, kisha nikatoka hapo kwake ikiwa imeshaingia mida ya saa sita. Moja kwa moja mpaka Mzinga, na nikapita eneo la dukani kwake Ankia na kumpungia mkono wa 'tutaonana baadaye,' kisha nikaenda kuchukua usafiri.

Wakati nimekaa tayari ndani ya daladala na yenyewe kuanzisha mwendo, Miryam akanipigia, nami nikapokea kumsikiliza. Akaniambia kitu ambacho sikuwa nimetarajia. Yaani kumbe alikuwepo pale kwake, hakuondoka pamoja na wengine shauri ya kujisikia vibaya sehemu ya tumbo lake kwa chini alipoamka mapema leo. Ih! Nikamwambia yaani ndiyo nimeondoka sasa hivi kwa Ankia, kama angekuwa amenitafuta dakika moja nyuma mapema zaidi ningegeuka kurudi kwake, lakini akaniambia haina tatizo; niende nilipokuwa naenda na tungekuja kuonana baadaye.

Nikamuuliza shida ya tumbo ilikuwa nini, naye akaniambia hiyo asubuhi alijitahidi kwenda maabara kupima akidhani ana tatizo kubwa, ila akaambiwa haikuwa shida, bali ni mwili wake tu uliitikia jambo jipya ulilojihusisha nalo hivi karibuni ambalo hakuwa amelifanya kwa muda mrefu. Nikawa nimeelewa. Alipokea dawa za kutuliza maumivu kiasi, na akashauriwa awe na kawaida ya kushiriki tendo la kimahaba na mwenzi wake ili hiyo hali isimpate tena, maana kuna sehemu humo ndani-ndani zilikuwa zimedhoofika ila sasa ndiyo zingekuwa imara zaidi. Ndiyo mwili wake tu ulivyokuwa.

Ahaa? Nikamwambia anisubiri sasa niwahi kurudi, ningekuja na dawa nzuri zaidi. Akasema acha ujinga, niende nilipokuwa naenda na niishie huko huko. Tukaachana nikiwa nahisi furaha kweli, licha ya kwamba bado kuna mengi yenye utata yaliyokuwa yananizunguka, nami nikatulia tu kusubiri safari inifikishe nilipodhamiria kwenda na nirudi haraka kwa mpenzi wangu.

★★

Nimekuja kumaliza mipango yangu yote iliyokuwa imenipeleka maeneo ya huko Morocco kwenye mida ya saa nane, na nikaamua kurudi Mbagala upesi sana kwa kuchukua bodaboda kutokea huko moja kwa moja. Nilitaka kuwahi kwa Miryam kabla familia yake haijarejea, maana nilikuwa nimeshawasiliana na Tesha pia na yeye kuniambia angewaleta wote jioni. Kwa hiyo haikuchukua muda mrefu sana, yaani saa tisa tu nikawa nimeshafika Mbagala. Huyu boda angenila hela nyingi sana kama ningesema anishushe mpaka Mzinga, kwa hiyo nikampa chake hapo Rangi Tatu, kisha nikaamua kupanda bajaji ya jero.

Wakati bajaji ikiwa mwendoni, nikampigia Miryam kumjulisha kwamba nilikuwa njiani, kimasihara nikimwambia "jiandaee." Kama kawaida yake akaweka pingamizi, lakini akawa ameniomba nipite kwenye duka wanalouza samaki wale wabichi ili nimchukulie sato wakubwa kilo mbili, halafu eti angenilipa hela yangu nikimfikishia mboga hiyo aliyotaka kuandaa kwa ajili ya familia yake, ili kufikia muda ambao wangerudi wapate mlo mzuri. Na alitia ndani viungo na mboga za majani, nami kiutani nikamwambia haina shida, chochote kwa ajili yake ningefanya. Akanishukuru kwa utayari wangu kumtimizia ombi lake.

Basi, baada ya kushuka hapo Mzinga, nikaingia sokoni kulitafuta duka wanalouza hao samaki, lakini kwanza ikanibidi nitafute mifuko miwili ili nibebee vitu ambavyo ningechukua. Nikiwa kwenye duka moja kuchukua mifuko hiyo, nikaona kwamba palikuwa na bidhaa za ice cream, zile nzuri za kwenye makopo ambazo ni tamu sana na huwa na tuvijiko twa kutumia. Nikawaza ingekuwa poa sana kama ningemchukulia Miryam kopo moja, baridi la ice cream lingeenda kumsaidia kupoza-poza na hilo tumbo lake, hivyo nikanunua ya shilingi elfu saba, vanilla flavor, kisha ndiyo nikaelekea kufata samaki na viungo kwa ajili ya mapishi ya mpenzi wangu.

Mwendo mdogo mdogo mpaka nikawa nimefika kwake Miryam, na wakati huu sikupita kwa Ankia, nami nilipofika getini kwao nikapita moja kwa moja hadi ndani na kuingia sebuleni. Kile kikamba getini kilikuwa kimesharudishwa. Hapo sebuleni palikuwa na hali ya utupu shauri ya wanafamilia wake kuondoka, nami nikavipeleka jikoni vitu alivyoniagiza bibie huku nikimwita kumjulisha kwamba nilikuwa nimefika. Akaitikia kutokea chumbani, lakini sauti yake ilisikika kwa umbali kiasi utadhani ilizibwa, nami nikaona nizipeleke samaki kwenye friji ili ziendelee kupigwa na ubaridi.

Nikiwa usawa huo ndiyo nikaanza kusikia sasa sauti ya maji kumwagika kutokea huko chumbani kwake Miryam, nami nikakisia kwamba alikuwa akioga. Nikatabasamu kiasi kwa kuwaza ni namna gani angefanana akiwa anadondokewa na maji sehemu za mwili wake, nami nikaitoa ice cream niliyokuwa nimemletea na kusogea sehemu ya korido lililoelekea chumbani kwake.

"Mimi... nimekuletea zawadi," nikamwambia hivyo kwa sauti.

"Zawadi wapi? Sema tu umetumia shilingi ngapi, nitoke nikulipe kabisa. Usiniongezee madeni..." akaongea kimasihara.

"Ahahah... hivi we' unanionaje?"

"Kama ulivyo. Na hao samaki inabidi nije kuwakagua ndiyo ulipwe sasa."

"Ahaa? Kwa hiyo itategemea na matokeo ya ukaguzi wako ndiyo utaamua nalipwa vizuri ama vibaya?"

"Sijasema hivyo. Ila nikikuta umeleta wabaya, na malipo yanashuka..."

"Thubutu! Yaani hapa unarudisha mkopo na riba," nikamtania namna hiyo.

Nikasikia maji yakiwa yameacha kumwagika, na hakutoa itikio lolote baada ya mimi kusema hivyo.

"La sivyo we' ndo' nitakushukia. Unataka nikushukie?" nikamuuliza kiutani tena.

Hakujibu, badala yake nikasikia tu sauti kama ya mlango ukiwa unafungwa, nami nikahisi ndiyo alikuwa akitoka bafuni mule mule chumbani kwake. Nikawa nataka nimsemeshe tena, ila kukaingia mawazo mengine ndani ya kichwa changu yaliyofanya nisisimke kiasi. Hapa, tulikuwa tumebaki wawili tu mimi na mwanamke aliyekuwa mpenzi wangu, halafu ndiyo alitoka kuoga. Nini kingine kingekuwa bora zaidi kama siyo kujionea jinsi ambavyo alifanana kwa wakati huu? Na tena isingekuwa kuona tu, nilitaka nicheze naye kabisa ikiwezekana, maana hata maabara ilihalalisha mimi kuwa dawa ya tatizo lake la tumbo. Ningempa dawa!

Kwa hiyo nikaamua kuelekea upande wa chumba chake taratibu tu, huku kopo la ice cream niliyomletea likiwa kiganjani. Nilipofikia hapo mlangoni nilikuwa nachekelea kichini-chini kama mtu mwenye hila fulani hivi, kisha taratibu nikakizungusha kimkono cha kitasa na kuusukuma mlango uingie ndani. Mlango haukutoa sauti mwanzoni mpaka nikawa nimeweza kumwona Miryam sasa. Aisee! Yaani ilikuwa kama vile nazidi kuona kitu kipya tu kutoka kwake kila mara.

Alikuwa usawa wa kitanda chake, mwilini akijifunga kwa taulo nyeupe kutokea kifuani mpaka usawa wa mapaja yake, huku akitumia nyingine kukausha maji kutoka kwenye nywele zake laini. Alikuwa amenipa mgongo, hivyo niliweza kutalii vyema namna ambavyo kalio lake lenye kutamanisha kwelikweli lilivyotikisika alipokanyaga hapa na hapo kadiri alivyoendelea kujikausha maji, na jinsi ngozi yake nyeupe na nyororo sana ilivyopendeza kuanzia juu mpaka chini, ikiwa haina doa hata chembe yaani utadhani alivaalisha yote ngozi ya plastiki. Bado nilikuwa naendelea kuusukuma mlango taratibu, ndipo ukatoa sauti ndogo ya kukwaruza.

Miryam akageuka na kuniona sasa hatimaye, nami nikawa namtazama kwa hisia sana machoni.

Akakunja sura kimaswali kiasi na kusema, "Jayden..."

Nikatabasamu kiasi na kuuachia mlango sasa.

"Ah, umenishtua. Nakuja, subiria nivae," akasema hivyo na kasauti kake.

Nikaendelea kumwangalia usoni kwa upendo.

Akaendelea kujifuta-futa nywele na kusema, "Jayden nenda bana, nataka kuja kupika. Acha kuniangalia hivyo... nenda huko. Pisha nivae."

Nikaanza kupiga hatua kumwelekea.

Akaacha kujifuta nywele na kusema, "Sijakwambia uingie, rudi huko. Nimesema rudi huko nivae."

Alikuwa anatabasamu kiasi, nami nikamuuliza, "Kwani kuna shida yoyote ukivaa na mimi niko humu?"

"Ahah... ee ipo. Hiyo hapo imeshasimama," akasema hivyo na kunionyesha kwa ishara ya macho kuelekea suruali yangu.

Nikajiangalia na kucheka kidogo kwa pumzi, kisha nikamwambia, "Hapo mbona haijasimama? Inajaribu tu kuchungulia. Wala siyo shida. Tena ni dawa yako hii."

"Jayden hebu acha mambo yako. Rudi bwana sebuleni nivae," akaongea kwa kumaanisha.

"Mbona unaekti kama vile itakuwa mara ya kwanza kukuona?"

"Haijalishi. We' nakujua, ukibaki humu itanichukua zaidi ya masaa mawili kuvaa," akasema hivyo.

Kauli yake ikanifanya nicheke kidogo, kisha nikamwambia, "Kweli, unanijua vizuri."

"Nenda bwanaa..." akasema hivyo huku akinisukuma kiasi.

"Sawaa. Nilikuwa tu nimekuletea zawadi hii hapa, e?" nikamwonyeshea kopo la ice cream.

Akaliangalia na kutabasamu kwa kukunja midomo yake, kisha akalipokea na kuliweka kwenye dressing table yake karibu na ukuta uliojengewa makabati ya nguo.

"Asante. Haya nenda sasa," akasema hivyo huku amenishikia kiuno.

Nikatabasamu na kumtazama mwilini kimchezo. Akakaza macho yake kuonyesha hatanii. Nikamwonyeshea ishara kwa kidole kwamba anibusu mdomoni kisha ndiyo niondoke, naye akaonekana kuudhika sasa.

"Jayden lakini, mbona unakuwa hauko... nenda bwana, muda una... ah..." akaongea kwa njia ya kulalamika.

"We' ni-kiss, kwani saa ngapi?" nikamwambia hivyo.

"Jayden!" akatumia sauti yake kuonyesha mkazo.

"We' ndo' unajichelewesha. Ungekuwa umeshavaa tayari, kiss moja tu ingemwondoa JC hapa," nikamwambia hivyo.

Akashusha pumzi eti kwa njia ya kukerwa, kisha akanifata mdomoni na kugusisha wake mara moja, kisha akasogea nyuma tena. Khh!

Nikamuuliza, "Ndiyo nini sasa?"

"Busu yako hiyo moja..."

"Ahaa... ndo' busu hiyo?"

"Eeeh..."

"Haka kaujeuri unakatoa-toa wapi?"

"Bafuni, kwa sababu nahitaji kupaka mafuta yangu, nilainishe ngozi, lakini wewe na bichwa lako umekuja na kusababisha nimekauka kabisa sasa!"

"Me na bichwa langu? Sss... ni kweli ila, hili bichwa huku chini limekaza balaa... sina tiba ya kuilainisha ngozi yako zaidi ya ilivyo laini, lakini bichwa langu linaweza kukulainishia zaidi sehemu fulani nzuri zaidi ya ngozi yako tu, maana leo umetoka kuambiwa ni dawa. Ungependa ikulainishie?" nikaongea haraka-haraka kimchezo.

Akazuia kicheko na kusema, "Sitaki lolote, me nataka kuvaa. Nenda bwana me ni...."

Nikakishika kiuno chake ghafla na kumvuta kwangu mpaka miili yetu ilipogandana, naye akaonyesha sura ya taharuki akiwa karibu zaidi na uso wangu.

"Jayden, ni nini lakini?" akauliza hivyo huku akijaribu kujinasua.

"Busu moja tu..." nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

"Si meshakupa? Ah..." eti akawa anadengua.

Nikapandisha mkono wangu mmoja mpaka nyuma ya kichwa chake, nikiishika shingo yake taratibu, naye akaniangalia usoni kwa njia tulivu zaidi. Nilikuwa namtazama kwa hisia sana.

"Jayden... tunaweza kukutwa..." akaendelea tu kulalamika.

"Na nani? Wote wameondoka," nikamwambia hivyo.

"A-ah, hata kama. Hii siyo sehe...."

Nikanyamazisha maneno yake kwa kufata mdomo wake na kuanza kumbusu kwa mahaba ya hali ya juu sana. Na hakuwa amekosea, nilisimama dede kwa nguvu zote hasa baada ya kuanza kumdendesha namna hiyo, naye akawa anazipokea busu zangu kwa hamu pia. Nilikuwa nimeshajua namna ya kumlegeza huyu mwanamke, yaani kumbusu tu tayari akawa kama anataka kuanguka. Ni jana tu asubuhi tulipiga hii mambo, lakini nikawa nimeshamhamu vibaya mno. Piga denda moja ya ajabu, na hivi alikuwa na midomo laini!

Nikaendelea kunyonya midomo yake na ulimi wake mtamu kwa njonjo kama zote, huku mkono wangu uliomkamata kiunoni nikiutumia kupandisha taulo yake taratibu kutokea pajani, naye akaushika na kuutoa. Akawa anajaribu kuikwepa busu yetu kwa kuupeleka mwili wake huku na huku, lakini nikaukamata huo mkono wake na kuubana mgongoni kwake huku nikijikandamiza zaidi mwilini mwake, kisha nikaushusha mkono mwingine na kuupitisha katikati ya miili yetu kwa chini mpaka kufikia katikati ya mapaja yake manono.

"Jayden..."

Akaita hivyo katikati ya busu yetu, nami nikakiweka kiganja changu usawa wa kibofu chake na kuanza kusugua sehemu hiyo ya juu kwa vidole. Yaani palikuwa panateleza kama vile pamemwagiwa mafuta lainii, naye akaanza kutoa miguno yake myembamba ndani ya mdomo wangu. Nilikuwa nimeanza kumpeleka mbali, na sikutaka safari ikome. Nikiwa nakisugua kitoweo chake kwa juu, akapitisha mkono wake mmoja mpaka juu ya kichwa changu na kunikamata nywele kwa nguvu, kama kawaida yake, naye hatimaye akawa anaiendeleza denda yetu kwa kupenda.

Nikaona ameanza kunogewa, hivyo nikauachia mkono wake nilioubana mgongoni kwake, naye akauleta mpaka kichwani kwangu kuuunganisha na mwingine kukishika kichwa changu, denda ikiwa pale pale. Nikayakamata makalio yake kwa pamoja na kuanza kuyafinya kwa nguvu kiasi ndani ya taulo yake, naye akajitoa mdomoni mwangu na kuanza kuhemea juu-juu. Nikaanza kuibusu shingo yake, huku nikitembeza mikono yangu kwenye mwili wake na kuonyesha kutaka kumtolea taulo, lakini akaikaza usawa wa kifua chake kwa mkono mmoja. Dah, yaani Miryam!

Nikaona isiwe shida. Nikaanza kumsukuma polepole kukielekea kitanda, na kwa sababu ya kutotarajia kukifikia haraka akawa amekaa kwa kishindo kama vile kajitupia. Uso wake ukawa usawa wa sehemu yangu ya suruali iliyotuna haswa, naye akaniangalia usoni kwa macho legevu. Nafikiri alidhani nataka anifanyie usafi wa eneo, lakini hapana. Mimi ndiyo nikapiga magoti chini karibu kabisa na mapaja yake, kisha nikayaachanisha na kujiweka katikati huku nikiufuata mdomo wake tena, kwa kuwa nyuso zetu zililingana.

"Jayden, we shouldn't be doing this here...."

Nikanyamazisha kimombo chake cha kulalamika tena kwa kuanza kumbusu mdomoni, na alikuwa hajambo katika kuupokea vyema sana ulimi wangu. Busu zetu zilitoa sauti tamu sana za mifyonzo kama tuko kwenye movie ya kizungu yaani, kisha ndiyo nikaanza kushuka taratibu kuelekea mapaja yake. Eti bado akawa ameikazia taulo kifuani, nami nikatabasamu kiasi na kufikisha uso wangu karibu na uanamke wake. Ah!

Maelezo ya hii kitu nilishayatoa kwa hiyo unaweza tu kuelewa kwamba niliikubali kinoma yaani. Halafu sasa kwangu mimi haikuchelewaga kujilowanisha, yaani mimi hapa ndiyo nilikuwa furaha yake. Safi, lainii... mzee nikazamisha ulimi! Nyonya, nyonya, nyonya, nyo-nya, nami nikawa namwangalia Miryam na kuona jinsi alivyopumua kwa kulegea na kupeleka kichwa chake huku na huko taratibu. Nikaendelea kumnyonya tu na kucheza na titi lake moja baada ya kuingiza kiganja changu ndani ya taulo yake, naye akaweka kiganja chake kwenye nywele zangu na kuanza kuzivuta.

Nadhani wote tuliweza kusikia pale simu yake ilipoanza kuita, lakini kwa pamoja tukaipuuzia kama vile haikusikika. Utamu ndiyo ulikuwa umeanza kumkolea bibie. Nikaendelea kumnyonya kitoweo kwa ufundi, mara nyingine akishtuka na kukisukuma kichwa changu, lakini ningeendelea tu kumpa ladha ya ulimi mpaka akaanza kuzungusha kiuno chake taratibu usoni kwangu.

Nikaacha kunyonya kwa ufupi na kumsemesha kidogo, "You like it baby?"

Akatikisa kichwa kukubali, kisha akasema, "Yes... sss... I like it..."

Nikaendelea kumnyonya kitoweo chake taratibu.

"Mmmhh... Jayden...."

"Naam..."

"Hapo hapohh..."

"Yes baby..."

"Ahhh... usiniite baby..."

"Ahahah... yes ma'am. Hapo vipi?"

"Hhh... hapo sawa..."

Alikuwa na masharti kweli, yaani dah! Ila ndiyo aliifanya hii kitu inoge sana, basi tu hakujua.

Nikakatisha unyonyaji hatimaye baada ya dakika kama kumi kabisa kuonekana kupita, na kweli nilipenda kuinyonya hii kitu aisee. Akalegea zaidi na kulalia mgongo wake huku akipumua kichovu fulani hivi, nami nikaona nitoe nguo zangu zote fasta wakati alipokuwa hanitazami.

"Basi, inatosha Jayd...."

Alipofumbua macho na kukuta sina nguo hata moja, akakodoa macho yake na kuegemia kiwiko huku akinitazama kwa kushangaa.

"Ja.... mbona ume...."

"Achana na maswali ambayo unajua majibu yake Mimi..." nikamwambia hivyo.

"Lakini Jayden...."

Nikajirusha kitandani na kuanza kumvuta, naye akawa anaweka mgomo.

"No, ach.... Jayden hapa siyo..."

Nikaendelea kulazimisha kumvuta, nikijiweka katika hali ya kulala chali ili niuvute mwili wake uje juu yangu. Na pamoja na usumbufu wake lakini nikafanikiwa kumburuza mpaka tukawa tumepandana katikati ya kitanda. Akawa anagoma kuiachia taulo yake, huku akinikalia usawa wa kiuno changu, kalio lake likiisukuma mashine yangu kwa nyuma. Nikaendelea kuishikilia mikono yake pande za viwiko.

Akiwa amekunja sura, akasema, "Jayden, no please... jaman.... nimetoka kuoga..."

Akanifanya nicheke kidogo, kisha nikamwambia, "Acha nikupe dawa kidogo tu... bafu si lipo?"

"Mm-mm..." akatikisa na kichwa kukataa.

Nikaukamata mgongo wake ili kuulazimisha mwili wake unilalile zaidi na kumwambia, "Hauoni nilivyowamba? Inabidi unitulize. Ukiniacha tu hivi hivi nikaenda kuiweka kwa mwingine?"

"Ah, we' nenda tu..." akaongea kwa kudeka.

Nywele zake laini zilikuwa karibu na uso wangu kwa hiyo zilinitekenya kiasi, nami nikalipiga kalio lake kofi kidogo na kulitikisa kwa kiganja.

"Jayden mbona husikii? Niachie..." akaongea kwa kudeka.

"Haya," nikamwambia hivyo.

Kweli nikamwachia, na ile ameanza kujinyanyua kwa kuutoa mguu wake mmoja, mimi nikaishika mashine yangu kwa mbele na kisha kuukandamiza mwili wake tena ili asiutoe upesi, na nafasi ndogo iliyoachia ikaniruhusu nikiweke kichwa cha msuli wangu usawa wa kitoweo chake. Akaweka mkono wake mmoja kifuani kwangu na kunikandamiza huku akiachama na kujikaza kimwili, nami nikatumia nafasi hiyo ya kuganda kwake kuanza kuuingiza mtalimbo ndani. Ai, hilo joto! Yaani kama alikuwa ananipasha mwili mzima.

Nikaendelea kuiingiza mashine, yeye bado akiwa ameuinua mguu wake mmoja kiasi, kisha akaurudisha katika mtindo wa kupiga magoti akiwa ananikalia sasa. Taratibu. Akainyoosha shingo yake kuelekea juu kidogo na kuweka mikono yake yote kifuani kwangu, kisha akanitazama kwa macho yenye uzito. Ah, nilijihisi vizuri sana! Joto lake lilikuwa tamu balaa!

Taulo yake ikataka kuachia, lakini akaweka mkono wake mmoja hapo kuziba, sijui huu mtindo ulikuwa wa makusudi tu ama labda kuna kitu alikuwa anaficha? Ila sikujali hapo sana, nikawa tu nasikilizia raha yenyewe kule mbele-kati baada ya yeye mwenyewe kuanza kupeleka kiuno chake mbele-nyuma taratibu.

"Ohh yes... sss... Jesus... Jaydenhh..." akaongea kwa hisia.

"Ahah... ushaanza kuniita hadi Jesus?" nikamwambia hivyo kiutani.

Akatoa tabasamu lililojaa hisia za kimahaba, naye akaelekeza uso wake juu tena na kuendelea kujisugua taratibu. Nikawa nayapapasa mapaja yake mpaka kalioni, kisha nikaikanyagisha miguu kitandani ili sasa niile bata vizuri baada ya yeye kuzoea mazingira. Nafikiri hakuwa ametarajia hili, kwa sababu nilipopandisha tu kiuno juu ghafla, akashtuka kiasi na kuniangalia usoni kama anashangaa, nami nikaanza kukuna.

Panda, shuka, panda, shuka, akawa ananesa tu huku akiguna, akijing'ata mdomo wake, na kurembua macho yake. Bado mkono wake mmoja aliuweka kifuani kwangu na mwingine kushikilia taulo yake kuficha sijui nini, nami nikaendelea kuchezesha kiuno juu-chini ili ni-enjoy zaidi utamu wake. Na utamu wake wote ulisikika vyema kwa jinsi alivyoguna kwa mideko na kuzidi kulegea tu.

Nikaanza kuongeza spidi kiasi, naye akakunja sura zaidi na kuiachia taulo yake. Akainamisha kifua chake kunielekea akiwa anasikilizia raha aliyopata bila kuacha kutoa miguno, na hapo akawa amenisogezea matiti yake mazuri sana usoni. Baraka! Nikayashika mashavu ya kalio lake na kuendelea kumkuna tu huku nikinyonya titi hili na lile kwa hamu kubwa, na kiuno chake kikawa kinatetemeka kadiri nilivyoendelea.

Dakika chache za kumpa raha namna hiyo zikanifanya nitulie kwanza ili kupumua kidogo, naye akaweka tena mikono yake kifuani kwangu na kuanza kukatikia hapo katikati. Jinsi kitoweo chake kilivyokuwa na utelezi na kuibana mashine yangu ndani kwa ndani, kujumuisha na mauno yake, yaani alinipeleka mbali sana huko juu kwenye hisia. Usipime! Kiuno chake kilikuwa laini, angekizungusha na kuanza kushuka na kupanda yeye mwenyewe, kisha nami ningeendelea kupampu ili kukutana na mapigo yake. Nilimpenda sana huyu mwanamke!

Dakika kadhaa zikawa zimepita tukipeana raha kwa mtindo huu huu, kwa sababu Miryam hakutaka nimgeuze. Yaani, alionekana kusikia raha sana iliyokuja kutokana na yeye kutetemeka miguu mara kwa mara, na nadhani mtindo huu ndiyo ulifanya hiyo itokee sana. Ndipo ikafika hatua akajikaza zaidi na kuanza kutetema huku sauti yake ikifuata huo mtetemo wake, naye akajitoa kutoka kwenye mashine yangu.

Akaniangukia mwilini, kichwa chake kikiwa kimekipita cha kwangu kwa hiyo uso wangu ulikuwa kifuani kwake, nasi tukawa tunapumua kwa uzito kiasi huku tukipapasana taratibu. Nikawa nambusu kifuani na shingoni, huku yeye akionekana kuisikilizia raha aliyokuwa ameipata kwa wakati huu. Nikatabasamu kiasi kwa kiburi maana nilikubali sana hii ishu ya kumtetemesha kama hivyo, nilijiona ngangali la hatari!

"You good?" nikamuuliza kwa sauti ya chini.

Akanyanyua uso wake na kunitazama machoni, kisha akasema, "Yes."

"Hamna maumivu?" nikamuuliza.

"Hamna. That was amazing," akajibu kwa hisia.

"Tamu eh? Haujuti sikurudi sebuleni?" nikamuuliza kimchezo.

Akatabasamu kwa hisia na kunilalia kifuani.

"Hhh... hadi raha. Sometimes hadi nakuwa naona ni kama ndoto kuwa nawe hivi," nikamwambia hivyo huku nikizichezea nywele zake.

"Na ndiyo nataka nikuje kukuwasha kofi ili uamke kutoka kwenye hiyo ndoto," akasema hivyo.

"Ahahah... kwa kosa gani tena?"

"Kunilazimu nihitaji kuoga mara ya pili."

"Oooh, lakini si ni baada ya ku-enjoy? Hilo kofi halitakuwa fair. Na kwanza sitaki hata kuamka..."

"Mhm... kwa nini?"

"Sijawahi kuwa kwenye ndoto nzuri kama hii. Sitaki kuamka kwa sababu nitakuwa na wewe muda wote wa kuiota..."

"Mmm?"

"Mm-hmm. Maisha halisi yamejaa maumivu tu, na hatuna jinsi ila kuyaishi. Ila kama ningeweza, ningechagua kuwa ndani ya ndoto hii kwa maisha yangu yote, kwa sababu wewe ndiyo ungekuwa kitu pekee ndani yake ambacho kingeifanya ndoto isiwe ndoto tena... bali uhalisia," nikamwambia hivyo kwa hisia.

"Unayatoaga wapi hayo maneno?" akauliza.

"Moyoni, Miryam. Moyoni," nikamwambia hivyo.

Akanyanyua uso wake taratibu na kuutazamisha karibu zaidi na wangu, naye akazirudisha nywele zake nyuma ya sikio na kuanza kunibusu mdomoni taratibu sana, akiuvuta mdomo wangu wa chini huku ananiangalia kwa upendo machoni, halafu akachezesha pande za mdomo wake wa juu kunielekea kwa njia fulani kama vile mnyama mkali anayeng'ata afanyavyo, akitishia kuning'ata kiutundu yaani, nami nikatabasamu na yeye akacheka kidogo na kulaza kichwa chake kifuani kwangu tena.

"Ushageuka kuwa mtundu hivi?" nikamuuliza hivyo huku nikilaza nywele zake taratibu.

Akacheka kwa pumzi na kusema, "Naona raha, Jayden. Unanipa furaha kubwa sana yaani, hata kwa wakati ambao sitarajii..."

"I'm glad," nikamwambia hivyo kwa kuridhika.

"Halafu Jayden, nakuomba... punguza kuwa unanunua-nunua au kuleta vitu vingi sana hapa," akasema hivyo.

"Nini tena? Hauitaki ice cream?"

"A-ah, namaanisha si kama hivyo jana nimekuta umewanunulia wakina mama nguo, na Mariam... usipende kufanya hivyo..."

"Kwa nini? Ni vibaya?"

"Siyo vibaya, ila... sitaki uwazoeshe hayo mambo. Sioni kama italeta picha nzuri mbeleni," akasema hivyo.

"Sawa Mimi. Nimekuelewa. Moja ya njia ambazo kwetu huwa tunaonyesha kuwajali wengine ni kuwanunulia vitu na nini... nilifikiri si mbaya nikifanya hivyo na kwa familia yako," nikamwambia kwa upole.

Akashusha pumzi kiasi na kusema, "Naelewa pia. Sema... kwa sasa bado, sisemi ni vibaya, ila uwe na limit tu baba. Utawanunulia chochote unachotaka ukishaniweka ndani."

Nikacheka kidogo na kumpiga kofi laini kwenye kalio lake.

Akasema, "Inabidi ninyanyuke. Sijui hata tumekaa hapa kwa muda gani..."

"Masaa mawili kabisa..."

"Ahahah... sikukosea eh? Busu moja uliyotaka imezaa masaa mawili."

"Hahah... huwezi kunilaumu. Mpenzi wangu we' wa moto sana..." nikamwambia hivyo huku nikisugua mkono wake taratibu.

"Mhm... eti wa moto! Unanifanya nalegea mno we' kaka, yaani sijui itakuwa sahihi zaidi tukisema unatumia dawa kuni...."

Kabla Miryam hajamaliza maneno yake, sote tukashtushwa na sauti ya mlango kufunguliwa kutokea pale sebueni, nasi tukaangalia upande wa mlango wa chumba hiki. Ih! Kumbe sikuwa nimeufunga mlango wa chumbani kwake Miryam wakati nimeingia muda ule mpaka tumemaliza mambo yetu? Si ndiyo kuuangalia sasa tukakuta bado uko wazi!

Lakini ishu ikawa juu ya ni nani aliyekuwa ameingia kule sebuleni, maana kama ni familia yake Miryam, wote walikuwa wameenda kule kwa Doris. Miryam akajinyanyua kutoka juu yangu na kuivuta taulo yake, huku mimi pia nikikaa.

"Ni nani huyo?" nikamuuliza kwa sauti ya kunong'oneza.

"Sijui. Eh, ngoja nifunge mlango kwanza..." Miryam akasema hivyo upesi.

Akaifunga taulo yake mwilini ili aende kurudishia mlango wa hapa chumbani kwanza, nami nikavuta boksa yangu na kuanza kuivaa. Sijui ni nani alikuwa ameingia huko, ila... alikuwa ametuchanganyia habari kabisa. Miryam akauelekea mlango wake na kuanza kuuvuta ili aufunge, pale ghafla tu kutokea nje ya chumba alipotokezea Shadya!

Nilishtuka. Miryam akaishia kuushikilia tu mlango akiwa ameusitiri mwili wake kwa taulo fupi, bila shaka akimwangalia mwanamke huyo kwa mshangao, huku mimi hapo kitandani nikiwa ndani ya boksa tu! Nilipomtazama Shadya kwa umakini, niliona namna ambavyo alimtazama Miryam pamoja na mimi kwa kutoamini, naye Miryam akanigeukia na kunitazama kwa wasiwasi.

"Mungu wangu! Mimi!" Shadya akasema hivyo.

Ikanibidi nianze kuvaa nguo zangu shuta, nikiwa najilaani moyoni kwa kutokuwa makini mpaka kusababisha hali hii mbaya sana itokee. Kwa jinsi Shadya alivyokuwa, yaani najua mambo yangeharibika upesi.

"Mimi... nini hiki unafanya?" Shadya akauliza.

"Shangazi... ona... njoo, ingia nikuelezee..." Miryam akasema hivyo.

Nikawa nimemaliza kuvaa suruali na T-shirt langu, nami nikaona Shadya aliposogea ndani zaidi na kusimama karibu yake Miryam, huku akitutazama kwa mshangao bado.

Miryam akasema, "Shangazi, usifikirie vibaya. Usi... haiko kama inavyoonekana, yaani...."

"Ila ikoje?" Shadya akamkatisha.

Nikawa nimetulia tu nikiwaangalia kwa umakini, naye Shadya akanitazama.

"JC... mambo gani haya? Yaani, unaacha kwenda kufanya mambo yako unakuja kumvua nguo huyu mwanamke mtu... kwa nini umekuja kumfedhehesha namna hii?" Shadya akanisemesha namna hiyo.

"Shangazi..." Miryam akaita kwa huzuni.

"Na wewe Miryam! Kweli, yaani wewe?! Nilikuwa nakupigia simu kukwambia mambo ya muhimu, hupokei, kumbe uko unafanya haya maujinga? Tumekutafutia wachumba wangapi mama? Wachumba wa maana, wote umewakataa... unadai hauko tayari kuwa na mwanaume yeyote lakini kumbe unataka kutoka na watoto wadogo? Ai jamani, sikutegemea Miryam. Kweli ni wewe?" Shadya akasema hivyo.

"Shadya... usifikirie hivyo. Miryam na mim...."

"Kaa kimya, JC. Kaa kimya. Huoni aibu? Me nilikuona kuwa kijana mstaarabu lakini kumbe... umekuja tu kumharibia maisha huyu dada, si ndiyo? Kwa hiyo kumbe umefanya kila kitu kumsaidia Mamu, Tesha, sijui nani, na sasa hivi Miryam ndiyo anakulipa kwa kukuvulia nguo, eh?" akanisemesha namna hiyo.

Nikaingiwa na hasira kiasi, nami nikasema, "Maneno unayoongea siyo ya kweli. Kwa nini usimsikilize... kwa nini usitulie uelezewe vizuri badala ya kusema maneno makali namna hiyo?"

"Maneno makali?! Unayajua maneno makali wewe? Unajua hiki chumba walikuwa wanalala wakina nani? Yaani... umekichafua chumba ambacho marehemu wazazi wa Miryam walikuwaga wanakitumia, na Miryam anakitumia ili kuwaenzi...."

"Shangazi..." Miryam akaita kwa hisia.

"... halafu unakuja kuingia na kumrubuni afanye upuuzi pamoja nawe? We' Miryam... unafikiri mama zako wakija wakajua unafanya haya mambo na huyu mtoto watakuonaje? Eh? Amekufanyaje huyu kijana mpaka akili yako imehama? Unawaachia wengine waende kwa Doris ubaki peke yako kisa eti unasema unaumwa, kumbe ni ili ubaki kufanya huu ujinga? Kweli kabisa?" Shadya akaendelea kulalama.

Miryam alikuwa amebaki kimya tu huku akiangalia pembeni kwa huzuni, nami nilikuwa nataka hata kumwambia aache kuwa mnyonge namna hiyo na kuongea ukweli wa hisia zake kwangu ili ifahamike kwamba jambo letu lilikuwa na maana zaidi ya ujinga.

Shadya akapiga viganja vyake na kusema, "Heee... haki ya Mungu! Hii ya leo kali. Umemkataa mpaka na Festo, mkaka mzuri sana, ana vitu vingi vya...."

"Shangazi, basi!" Miryam akasema hivyo kwa uthabiti.

Shadya akatulia na kuendelea kumwangalia.

"Ninakuheshimu, lakini usinisemeshe kama vile me ni mtoto. Mimi ni mtu mzima, nina maamuzi yangu juu ya maisha nayotaka kuishi. Naomba unionyeshe heshima, maana sasa naona ni kama unataka kunipanda. Unataka kuniamulia mwanaume ambaye nitampenda? Ni maisha yangu au yako?" Miryam akamwambia hivyo.

Nikatabasamu kiasi kwa mbali kwa kuridhishwa na maoni hayo. Hivyo ndivyo ilivyotakiwa!

Shadya akasema, "Ahaa? Kumbe ndiyo iko hivyo? Sawa. Haya mama, endelea. Endelea tu, uone kama hii itakufikisha popote."

Miryan akaangalia pembeni na kutikisa kichwa kwa kusikitika.

Shadya akamwambia, "Kila mtu anakuheshimu Miryam, kila mtu anakupenda, lakini wakijua hii ndiyo tabia yako unadhani kuna hata mmoja atataka kuwa na urafiki na wewe? Utasemwa sana mtaani na sifa zako nzuri zitaharibika. Tena sifa ya familia nzima. Mimi nimeona mengi, na sawa sina undugu wa damu na nyie, lakini ninajua mengi sana na ninakupenda kama mwanangu. Maimuna, mama yako, kama angekuwepo sasa hivi, asingekubaliana na hivi vitendo vya kimalaya na watoto wadogo unavyofanya... maana vinaharibu taswira nzuri ya familia yake aliyoiacha... na nakwambia Mimi, umeshaanza kuiharibu. Ngoja tuje kusikia mama zako watasema nini kuhusu haya. Endeleeni na mambo yenu..."

Baada ya mwanamke huyo kusema hayo, akaelekea sebuleni tena, akituacha tukiwa tumesimama hapo kwa kuvurugiwa amani yote tuliyokuwa nayo. Nikawa namtazama Miryam na kuona jinsi ambavyo aliumia sana, yaani aliangalia pembeni tu kwa huzuni kuu, nami nikamsogelea mpaka karibu na kumshika mkononi. Akaniangalia usoni.

"I'm sorry," nikamwambia hivyo kwa hisia.

Akaweka kiganja chake mdomoni kiasi na kutikisa kichwa kukubali pole yangu huku akitazama chini.

"Tunahitaji kumwamb...."

"No Jayden, we'.... nenda tu. Tutaongea baadaye," akaniambia hivyo kwa upole.

"Lakini vipi kuhusu...."

Kabla sijamaliza kuongea, akaniangalia usoni kwa njia yenye msisitizo kuwa nimwache tu kwanza, nami nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

Nikakinyanyua kiganja chake na kukibusu mara mbili, kisha nikamshika shingoni kwa wororo, lakini hakuniangalia kabisa na kubaki ametazama pembeni kwa kufadhaika. Nikaona nimpite tu na kuondoka. Dah, yaani jamani! Wakati wetu mzuri ukawa umevurugwa vibaya sana, sijui hata ni kwa nini huyo Shadya alikuwa ameamua kuja wakati huu! Na alivyokuwa mbea sasa, hapo kama angeondoka yaani ndiyo angesambaza maneno hata kwa watu ambao hawakutufahamu.

Lakini sikujali. Najua kwa njia moja ama nyingine wenye kuongea wangeongea tu kuhusu uhusiano wangu na Miryam, hasa ukitegemea na aina yao tu ya maisha. Ila hakukuwa na chochote cha ajabu, ni basi tu ndiyo tungepaswa kuonyesha kwamba mahusiano yetu hayakuwa ya mtindo wa kuridhishana tu, bali yalikuwa ya malengo. Na nilikuwa tayari kwa lolote ambalo lingefuata baada ya hapo ili nithibitishe upendo wangu kwa mwanamke huyo kwa kila mtu ambaye angejifanya anajua sana kujaji. Hiyo ingetia ndani na mama wakubwa endapo kama na wao wangeleta dukuduku kama la Shadya.

Nilipofika sebuleni, nikamkuta Shadya akiwa amekaa sofani huku akichat, nafikiri kusambaza ubuyu sasa, yaani hakuchelewesha, nami nikampita tu na kuuelekea mlango huku nikiona alivyokuwa ananiangalia kwa macho yenye kisirani. Mzee nikatoka zangu tu hapo na kuelekea kwa Ankia, mpaka chumbani, nami nikajilaza kitandani kwa kutazama juu, nikiwa namtafakari sana Miryam wangu.








★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Pata Full Story WhatsApp au inbox

Whatsapp +255 678 017 280

Karibuni sana
Kimeumana 😂😂
Sasa Ile scene ambayo Maryam alikuwa haitaki imefika 😂
Ujiandae kutambulishwa tu
 
Back
Top Bottom