Tupio la XVII – Deliverence
Ilipoishia...
“Naomba maji ya kunywa…” Yalikuwa maneno ya kwanza kumtoka mama Mchungaji baada ya kuinuliwa…
“Mpeni kiti sasa akae na sisi sote turudi kwenye viti vyetu tukakae tumsikilie..” Aliongeza Zawadi baada ya kuona mama mchungaji ameshakunywa maji lakini pia waumini walijazana eneo la mbele kiasi cha kufanya kuwe na hewa nzito na nafasi finyu.
“Bwana Yesu apewe sifaaa!...” mama mchungaji alianza kufunguka…
Sasa endelea…
“Bwana Yesu apewe sifa!...”
“Bwana Yesu apewe sifa!...”
“Tumsifu Yesu Kristu…!
Alirudia rudia kusema maneno hayo huku kila aliporudia alikuwa akiongeza sauti… kisha akaendelea…
“Wapendwa katika Bwana, leo ni zamu yangu ya kuleta ushuhuda na kutubu…”
Waumini walikuwa kimyaaaa isipokuwa wale wachache ambao ni kundi mhemko likiongoza na dada mmoja asiye na simile katika kuyaendea mambo.
“Hakika leo nimeona utukufu wa Mungu wa Mbinguni, Mungu aliye umba mbingu nan chi, Mungu wa Isaka, Mungu ya Yakobo…”
“Nilifungwa katika maagano ya kishetani lakini leo namshukuru Mungu kwa kumleta yule binti…” akanyoosha mkono na kidole kumuelekezea Zawadi…
“Binti amakuja kuvunja maagano niliyokuwa nayo…”
“Nilikuwa namtumikia shetani…”
Mama mchungaji alikuwa anaongea kwa kukata kata maneno kama vile akipata tabu ya kuvuta pumzi, ingawaje alikuwa ameketi kwenye kiti lakini ile hali ya mhemo ilikuwa Dhahiri wa waumini wote…
“Mwaka Fulani (aliutaja) nilimaliza masomo katika chuo cha Biblia Mwanza na huko nikakutana na bwana mmoja ambaye ndiye alinishawishi baada ya kumaliza mafunzo yale tuende Nigeria kusoma zaidi ili tuwe na nguvu nyingi za kimiujiza ili kuwaaminisha waumini juu ya nguvu za Mungu…”
“Ilinichukuwa miezi kadhaa hadi kuandaa nauli pamoja na masurufu ya safri kwa ajili ya kwenda huko Logos ambako kwa maelekezo ya bwana yule tungepata nguvu za miujiza mingiii”
“Kweli siku ya siku tulifunga safari na tukakaa huko kwa miezi 18 tukipata mafundisho mbalimbali ya kiroho na kisha ndipo nilipojikuta nimetumbukia katika maagano ya nguvu za giza ambapi mimi nilpatiwa nyoka aina ya chatu pamoja na makolokolo mengine nikawa na uwezo wa kufanya miujiza mbele za watu na kuvutia watu wengi katika huduma yangu niliporudi nchini…”
“Huduma yangu kwanza ilikuwa ndani ya makanisa mengine, nikifanya miujiza kidogo basi watu wanaamini na kuanza kuniletea pesa kuniomba niwaombee mambo mbalimbali hadi mwaka juzi nilioamua kuanzisha kanisa langu hili…”
“Kwa kushirikiana na baadhi yenu, tumefanya udanganyifu mwingi wa kuleta ushuhuda wa uongo ili tu ninyi waumini muone nguvu nilizonazo, nimetoa mapepo ya uongo mengi tu na kuendelea kujineemesha kupitia sadaka zenu...”
“Lile kapu mlilokuwa mnaliona halikuwa kikapu, lilikuwa ni joka kubwa aina ya chatu ambalo ndilo lilikuwa likihifadhi zile hela na usiku likiniamuru kwa njia ya ndoto kufanya makafara mbalimbali ili nguvu zangu zisipotee…”
“Ni mabay mengi sana nimeyafanya, lakini leo hii nimefunguliwa, Haleluyaa!”
“Haleluya!” alirudia kusema neon hilo baada ya kuona uitikio ni hafifu kutoka kwa waumini.
“Binti yule sijui ametokea wapi, maana hata siku ile ya kwanza kumuona humu kanisani nilitamani anisaidie katika kuondosha hali hii niliyonayo lakini nilikuwa sina namna…”
“Leo hii namshukuru Mungu Baba kwa kupitia huyu binti, nimevuja lile agano na lile joka limekufa kwa maana wakati nakabidhiwa niliambiwa siku joka lile likifa ama kupotea basi nguvu zangu nazo zitakufa na ikitokea hivyo basi haraka niwahi kuwenda Logos kwa ajili ya ku-update maagano…”
Aliendelea kuongea pale weee akisimulia mengi aliyokuwa nayo, mengine ya hiyari maengine hakuwa na hiyari nayo na kuonesha kujuta kwa kitendo alichofanya…”
“Leo hii niko hapa mbele yenu, lakini sina zile nguvu tena za miujiza bali nina mafundisho sahihi kama tulivyofundishwa kule Nyakato chuo cha Biblia, na kwa heshima ninaomba binti huyu aniongoze sala ya toba ili nitubu mbele za Mungu na mbele zenu…”
Zawadi akasogea mbele kwa kupanda pale madhabahuni na kuanza kusema kwa sauti nyembamba kali huku mkono wake mmoja akiinua juu…
“Niwakaribisheni nyote kumpokea YYesu kama BBwana nna MMwokozi wa maisha yako…”
“Na kufanya mana hiyo unapokea upendo wa Mungu na kumiminwa ndani ya mioyo yetu kwa uwezo wa Roho mtakatifu…”
“Inawezekana umepoa, inawezekana upendo wako kwa Mungu umepoa, unaomba tu kwa sababu una tatizo ama shida fulani, lakini shida ama tatizo hilo likiisha utacha kuomba…”
“Warumi 5 tano inatuambia… ‘Tukiwa na tumaini hatuwezi kukata tamaa kwa sababu Mungu amekwisha kumimina upendo wake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ni zawadi tuliyopewa na Mungu’…”
“Basi na tutumie muda huu kufufua imani, turudishe tena ule moto kama alivyosema habakuki katika kitabu chake sura ya tatu mstari wa pili… ‘Ffufua kazi yako katikati ya miaka…’, sasa hebu fuata maneno haya, sema…”
“Eee Mungu Baba...,
Nimekuja mbele zako…,
Naomba unirehemu…,
Naomba unisamehe…,
Zambi zangu zote…,
Nilizokukosea…”
“EE Bwana Yesu…,
Nimefungua moyo wangu…,
Nakukaribisha sasa…,
Inhia ndani yangu…,
Kwa uweza wa roho wako…,
Uwe Bwana na mwakozi na kiongozi wa maisha yangu…,
Ee Bwana Yesu…,
Ingia kwa upya…,
Fufua upendo wako ndani yangu…,
Fufua kwa upya…,
Katika JJina la Yesu…”
“Asante kwa kunihesabia haki…,
Katika Jjina la Yesu…,
Unisaidie…,
Niingiapo na nitokapo…,
Katika Jina la Yesu…,
Dhambi zisinishinde, Majaribu yasinishinde…,
Shetani asinishinde…,
Nipe mabadiliko…,
Kutoka kwenye uzima wa milele…,
Unayoyataka kwangu…,
Na shughuli ninazozifanya…,
Katika jina la Yesu…, Amen”
Wakati Zawadi akiongoza sala ile ya toba, waumini wote walifuatisha, tena kwa sauti za kutetema na kujuta na kutoa machozi…
Zawadi aliendelea…
“Kama umefuatisha sala hii kwa dhati, basi Mungu amekusamehe, na nguvu za Mungu zimeingia ndani yako, roho wa Mungu ameingia ndani yako tangia sasa, pendo la Mungu limeingia ndani yako….”
“Sasa tumejenga msingi mpya wa Imani katika maisha yetu ya kiroho. Kwa heshima kubwa kabisa sasa nimkaribishe mchungaji aendelee…”
Wakati wote huo, mpiga kinanda wa kanisa alikuwa naye akichombeza kwa mirindimo ya sautu za kuhanikiza matukio yaliyokuwa yanaendelea…
Mama Mchungaji akasogea katikati ya madhabau na kumgeukia mpiga kinanda akimwashiria kama aanzishe kitu hivi mara…
Melodi za wimbo wa kusifu zikapigwa na kwa kuwa melodi ya wimbo ule ulikuwa unajulikana kanisa zima likaitikia kibwagizo wakiongonzwa na kwanya ya kanisa…
“Ninamjua…, aliye mwamba…., ameyeniokoa… ni Bwana Yesu…”
Waumini waliimba kwa furaha na kucheza…
Kabla wimbo haujaisha, Zawadi aliwaashiria akina Vai waondoke warudi kule nyuma kwenye siti zao, walipokaribia kwenye siti, Zawadai akawaambia twendeni nyumbani hivyo wakatoka mle ndani wakati bado watu wakiimba kwa furaha kumsifu Mungu.
Itaendelea...