Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 17
Siku hiyo usiku watoto wa familia hii waliambiwa kuwa wawahi kulala ili kesho yake wawahi ibadani, basi mama yao akawaambia kuwa kesho wawahi kuamka kwaajili ya kwenda Kanisani basi kila mmoja alienda kulala ambapo Angel alilala hoi kabisa ila Erica alijihisi kutokuwa na usingizi kabisa kwa wakati huo basi alikaa tu chumbani kwake mara Erick nae akaenda chumbani kwa dadake na kuanza kuongea nae,
“Yani mama katufukuza mapema sana kulala, mimi sina hata usingizi”
“Hata mimi sina usingizi jamani”
“Sasa tufanye nini?”
“Tucheze karata”
“Kheee karata umezipata wapi?”
“Usiulize, ngoja nizitoe tucheze”
Basi Erica akatoa karata kisha yeye na kaka yake wakaanza kucheza karata yani walicheza karata hadi usiku sana bila kugundua ni usiku sana, mara mama yao alienda chumbani na kuwashtua,
“Yani nimepita hapa na kushangaa taa inawaka, nikajiuliza huyu Erica hajalala au kasahau kuzima taa au anaogopa, kumbe mnacheza karata nyie wajinga, mnajua saa ngapi saa hizi?”
“Tusamehe mama”
“Tusamehe mama ndio nini, haya Erick inuka nenda chumbani kwako na ulale nakuja kukuangalia muda sio mrefu na wewe Erica lala muda huu sitaki ujinga wa kucheza karata usiku’
Wote walifanya vile ambavyo mama yao alisema kisha mama yao akazima taa na yeye kwenda chumbani kwake kulala huku akilalamika tu.
Siku hiyo usiku watoto wa familia hii waliambiwa kuwa wawahi kulala ili kesho yake wawahi ibadani, basi mama yao akawaambia kuwa kesho wawahi kuamka kwaajili ya kwenda Kanisani basi kila mmoja alienda kulala ambapo Angel alilala hoi kabisa ila Erica alijihisi kutokuwa na usingizi kabisa kwa wakati huo basi alikaa tu chumbani kwake mara Erick nae akaenda chumbani kwa dadake na kuanza kuongea nae,
“Yani mama katufukuza mapema sana kulala, mimi sina hata usingizi”
“Hata mimi sina usingizi jamani”
“Sasa tufanye nini?”
“Tucheze karata”
“Kheee karata umezipata wapi?”
“Usiulize, ngoja nizitoe tucheze”
Basi Erica akatoa karata kisha yeye na kaka yake wakaanza kucheza karata yani walicheza karata hadi usiku sana bila kugundua ni usiku sana, mara mama yao alienda chumbani na kuwashtua,
“Yani nimepita hapa na kushangaa taa inawaka, nikajiuliza huyu Erica hajalala au kasahau kuzima taa au anaogopa, kumbe mnacheza karata nyie wajinga, mnajua saa ngapi saa hizi?”
“Tusamehe mama”
“Tusamehe mama ndio nini, haya Erick inuka nenda chumbani kwako na ulale nakuja kukuangalia muda sio mrefu na wewe Erica lala muda huu sitaki ujinga wa kucheza karata usiku’
Wote walifanya vile ambavyo mama yao alisema kisha mama yao akazima taa na yeye kwenda chumbani kwake kulala huku akilalamika tu.