Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #161
SEHEMU YA 138
Walipofika shuleni, moja kwa moja Erica alipelekwa kwenye usahili na kupewa mitihani ambayo aliifanya kwa umakini mkubwa sana kiasi kwamba walimu walipoichukua ile mitihani walifurahi sana na kumwambia baba Angel kuwa mtoto wake apelekwe tu kesho akaanze shule maana anaonekana yupo vizuri sana.
Basi wakapanda kwenye gari na kuanza safari ya kurudi nyumbani, wakiwa njiani Erica aliuliza,
“Sasa baba mbona hatuendi tena kule shuleni ili nikawaage rafiki zangu?”
“Tutaenda kesho, ngoja leo turudi tu nyumbani kwani nina mambo mengi sana ya kufanya”
Yani Erica kilichokuwa kikimuumiza moyo ni kuhusu habari ambayo Elly alimwambia kuwa atamwambia, basi alichukia sana ila hakutaka tu kumuonyesha baba yake kuwa amechukia.
Kuna mahali walikuwa wakikatisha na gari mara Erica alimuona mtu na kumshtua baba yake,
“Kheee baba, yule sio kaka Junior?”
Baba Angel alisimamisha gari na kuangalia vizuri ni kweli kabisa alimuona Junior akiingia kwenye nyumba ya kulala wageni tena akiwa ameongozana na mwanamke aliyemzidi sana kwa umri, kwakweli baba Angel alichukia sana hivyo alipaki gari lake vizuri na kushuka hadi kwenye ile nyumba ya kulala wageni.
Alifika pale na kumuulizia Junior, ila pale alikuwa ameandikisha jina lingine,
“Hakuna Junior hapa mzee wangu”
“Aaaah namtaka yule mtoto aliyeingia hapa muda huu, hivi mnajua kama yule ni mwanafunzi? Nitawafunga nyie”
Wale wahudumu wakaogopa hivyobasi wakamuonyesha baba Angel chumba ambacho Junior ameelekea na yule mwanamke, basi baba Angel akiwa na hasira sana alienda hadi kwenye kile chumba na kujaribu kufungua ila kilikuwa kimefungwa kwa ndani hivyo na kuamua kugonga ambapo mlango ulifunguliwa na Junior mwenyewe akijua ni muhudumu wa ile guest, kwakweli baba Angel alichukia sana na kumvuta kisha alimzaba vibao vya kutosha na kuondoka nae ambapo alimpakia kwenye gari lake na moja kwa moja kwenda nao nyumbani kwake.
Kwakweli mama Angel pia alisikitika sana baada ya kusikia habari za Junior, basi baba Angel alikaa nae chini na kujaribu kuzungumza nae,
“Hivi wewe Junior una tatizo gani lakini?”
“Sina tatizo mimi baba mdogo ila sina raha kabisa”
“Kwanini?”
“hakuna mtu anayenipenda”
“Hivi wewe mtoto una kichaa au nini? Familia yako yote tunakupenda, mama yako na sisi wote tunakupenda tena sana tu. Sasa kwanini useme hakuna anayekupenda?”
“Sijawahi kuishi na baba yangu mimi, muda wote mama hunitukana na kuniambia kuwa tabia zangu ni kama za baba yangu, hata akinituma nikimwambia nimechoka basi huwa anasema tabia zangu ni kama za baba yangu na mara nyingi huwa anasema anajuta kunizaa anasema angejua angetoa hata mimba yangu. Haya na baba ninayeishi nae pia, hataki hata kuniona ingawa mama analea watoto wa baba vizuri tu ila yule baba hanitaki mimi kabisa na hata hanipendi. Kwahiyo mimi sina furaha yoyote ya maisha zaidi ya hii, yani kuzunguka na wanawake ndio furaha yangu”
“Sasa Junior, hayi sio maisha ujue mwanangu, yani sio maisha kabisa. Naomba kwasasa uishi hapa nyumbani kwangu, nitaenda kukuchukulia nguo zako na kukuletea hapa, kwahiyo utakuwa ukienda shule na kurudi hapa, ila Junior sitaki ujinga hapa nyumbani kwangu, achana na habari kusema kuwa watu wote hawakupendi wakati tupo tunaokupenda sana tu, sawa!”
“Sawa, bamdogo nimekuelewa”
Basi baba Angel alipanga kwenda kesho yake kumchukulia Junior nguo zake ila kwa siku hiyo alimtaka ake hapo hapo na asiende popote pale.
Walipofika shuleni, moja kwa moja Erica alipelekwa kwenye usahili na kupewa mitihani ambayo aliifanya kwa umakini mkubwa sana kiasi kwamba walimu walipoichukua ile mitihani walifurahi sana na kumwambia baba Angel kuwa mtoto wake apelekwe tu kesho akaanze shule maana anaonekana yupo vizuri sana.
Basi wakapanda kwenye gari na kuanza safari ya kurudi nyumbani, wakiwa njiani Erica aliuliza,
“Sasa baba mbona hatuendi tena kule shuleni ili nikawaage rafiki zangu?”
“Tutaenda kesho, ngoja leo turudi tu nyumbani kwani nina mambo mengi sana ya kufanya”
Yani Erica kilichokuwa kikimuumiza moyo ni kuhusu habari ambayo Elly alimwambia kuwa atamwambia, basi alichukia sana ila hakutaka tu kumuonyesha baba yake kuwa amechukia.
Kuna mahali walikuwa wakikatisha na gari mara Erica alimuona mtu na kumshtua baba yake,
“Kheee baba, yule sio kaka Junior?”
Baba Angel alisimamisha gari na kuangalia vizuri ni kweli kabisa alimuona Junior akiingia kwenye nyumba ya kulala wageni tena akiwa ameongozana na mwanamke aliyemzidi sana kwa umri, kwakweli baba Angel alichukia sana hivyo alipaki gari lake vizuri na kushuka hadi kwenye ile nyumba ya kulala wageni.
Alifika pale na kumuulizia Junior, ila pale alikuwa ameandikisha jina lingine,
“Hakuna Junior hapa mzee wangu”
“Aaaah namtaka yule mtoto aliyeingia hapa muda huu, hivi mnajua kama yule ni mwanafunzi? Nitawafunga nyie”
Wale wahudumu wakaogopa hivyobasi wakamuonyesha baba Angel chumba ambacho Junior ameelekea na yule mwanamke, basi baba Angel akiwa na hasira sana alienda hadi kwenye kile chumba na kujaribu kufungua ila kilikuwa kimefungwa kwa ndani hivyo na kuamua kugonga ambapo mlango ulifunguliwa na Junior mwenyewe akijua ni muhudumu wa ile guest, kwakweli baba Angel alichukia sana na kumvuta kisha alimzaba vibao vya kutosha na kuondoka nae ambapo alimpakia kwenye gari lake na moja kwa moja kwenda nao nyumbani kwake.
Kwakweli mama Angel pia alisikitika sana baada ya kusikia habari za Junior, basi baba Angel alikaa nae chini na kujaribu kuzungumza nae,
“Hivi wewe Junior una tatizo gani lakini?”
“Sina tatizo mimi baba mdogo ila sina raha kabisa”
“Kwanini?”
“hakuna mtu anayenipenda”
“Hivi wewe mtoto una kichaa au nini? Familia yako yote tunakupenda, mama yako na sisi wote tunakupenda tena sana tu. Sasa kwanini useme hakuna anayekupenda?”
“Sijawahi kuishi na baba yangu mimi, muda wote mama hunitukana na kuniambia kuwa tabia zangu ni kama za baba yangu, hata akinituma nikimwambia nimechoka basi huwa anasema tabia zangu ni kama za baba yangu na mara nyingi huwa anasema anajuta kunizaa anasema angejua angetoa hata mimba yangu. Haya na baba ninayeishi nae pia, hataki hata kuniona ingawa mama analea watoto wa baba vizuri tu ila yule baba hanitaki mimi kabisa na hata hanipendi. Kwahiyo mimi sina furaha yoyote ya maisha zaidi ya hii, yani kuzunguka na wanawake ndio furaha yangu”
“Sasa Junior, hayi sio maisha ujue mwanangu, yani sio maisha kabisa. Naomba kwasasa uishi hapa nyumbani kwangu, nitaenda kukuchukulia nguo zako na kukuletea hapa, kwahiyo utakuwa ukienda shule na kurudi hapa, ila Junior sitaki ujinga hapa nyumbani kwangu, achana na habari kusema kuwa watu wote hawakupendi wakati tupo tunaokupenda sana tu, sawa!”
“Sawa, bamdogo nimekuelewa”
Basi baba Angel alipanga kwenda kesho yake kumchukulia Junior nguo zake ila kwa siku hiyo alimtaka ake hapo hapo na asiende popote pale.