Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #301
SEHEMU YA 258
Wakati baba Angel na Erick walipokuwa wakirudi nyumbani, basi baba Angel alimpa Erick hela kama ambavyo alikuwa ameahidi kufanya hivyo naye Erick alimshukuru sana baba yake kisha baba Angel alimuuliza.
“Utaenda kununua nini na hiyo hela?”
“Aaah zawadi baba ila nyingine naiweka kwanza”
“Oooh haya mwanangu, kwahiyo hiyo zawadi unaenda kununua lini?”
“Kesho baba’
“Je mama yako yupo kwenye watakaopata zawadi au ni za kwako mwenyewe? Au mama yako utampa zawadi ya pipi? Yani zawadi wewe unanunua kwaajili ya nani?”
Erick akacheka kwanza na kumwambia baba yake,
“Mama, nitamnunulia zawadi ila sina tatizo sana na mama sababu huwa anapata zawadi kutoka kwako, ila zawadi ninayopanga kununua napanga kumnunulia Erica”
“Wow, mwanangu ni vizuri sana kumpenda dada yako, kumbe huwa unamkumbuka eeeh! Oooh ni vizuri sana, nina uhakika Erica atafurahia sana zawadi utakayomnunulia”
Erick akatabasamu tu, kisha baba yake akasema,
“Unajua mwanzoni nilikuwa najiuliza kuwa unapanga kununua zawadi ya nani? Nimejiuliza sana, nakumbuka mimi jamani wakati nimeanza mahusiano na mama yenu basi katika swala la zawadi ni yeye tu aliyekuwa akinijia kichwani mwangu”
“Na kabla ya hapo baba?”
“Kabla ya hapo, sikuwa mzuri sana kwenye swala la zawadi ni mpaka mtu aniambie kuwa nataka zawadi, kama dada yangu alikuwa na mtindo wa kuniambia nataka zawadi, basi ndio naenda kumnunulia. Badae nilipoanza na mama yenu alinifundisha umuhimu wa zawadi basi hata mama yangu nikaanza kumpelekea zawadi, dada yangu nae na ndugu zangu wengine. Nafurahi mwanangu umejua umuhimu wa zawadi ukiwa mdogo hivi, kwakweli dada zako wamepata kaka wa kujivunia haswaa”
Baba Angel alionekana kumfurahia sana mtoto wake na waliongea mengi sana hadi wanaingia nyumbani.
Basi kutokana na uchovu uchovu wa siku hiyo walikula tu na kwenda moja kwa moja vyumbani maana hakuna aliyekaa kuongea na wengine zaidi ya kuoga na kulala tu.
Usiku wa leo, Junior alikuwa chumbani kwa Vaileth huku akijaribu kuweka sawa baadhi ya mambo,
“Ila kwanini Junior ulinidanganya mpenzi? Yani umesema mama yako anaumwa wakati haumwi jamani Junior!”
“Kwanza naomba unisamehe sana, yani hata sijui nisemaje. Unajua mama alinidanganya pia kuwa anaumwa kumbe shida yake ilikuwa kuniona tu, si unajua huwa siendi mara kwa mara! Halafu kitu kingine, hata mamdogo kanisema sana nilivyorudi, jamani kitoto Erica ni kimbea hadi kimeshindikana. Kweli kwa sauti ile jikoni ni ya kusikiwa jamani!”
Vaileth alicheka kwa muda na kusema,
“Hujamzoea tu Erica, ila kumbuka katufichia siri”
“Kwanza tujiandae wakati wowote ule litabumburuka, katoto kambea kale wala sio ka kukaamini sana”
“Je ikibumburuka itakuwaje?”
“Yani hapo ni kukataa tu hakuna namna”
“Mmmh unajua kuwa Erica ni mbea ila sio muongo ndiomana anaaminiwa sana! Hapa ni kuombea tu asije kusema ukweli”
“Ila sijapata kuona mtu mbea kama yule mtoto, yani akija kuolewa mumewe atapata shida, hao mawifi zake na mama mkwe wajipange maana kanauwezo wa kusambaratisha ukoo mzima kwa umbea wake, atatoka kwa mama mkwe na hili na kupeleka kwa wifi hili, katoto kambea hadi kameshindikana”
“Sasa karithi wapi?”
“Aaaah sijui kwakweli, ila Vaileth kwakweli nimekumiss sana mke wangu yani nilikuwa na mambo mengi ila mawazo yote ni juu yako”
Moyo wa Vaileth uliridhika sana kwa maneno yale ya Junior na kujikuta akitabasamu tu kisha wakalala kama kawaida yao.
Mama Junior akiendelea na kazi zake za hapa na pale, mara alipigiwa simu na rafiki yake daktari, basi alitabasamu na kupokea ile simu,
“Bite, habari. Jana ndugu yangu hata hatukuongea vizuri kwani ulikumbwa na nini rafiki yangu”
“Mmmmh nini tena!!”
“Unajua nilivyopokea ule ujumbe wako tu nikaamua kutuma muda ule ule na hata sikukuuliza ndugu yangu”
“Ujumbe gani tena!”
“Khee Bite, si wewe jana umenitumia ujumbe wa kuazima laki mbili!”
“Mmmh jamani Maimuna, mimi nimekutumia huo ujumbe!! Muda gani?”
“Ngoja nikutumie zile jumbe kwanza tulizokuwa tukiwasiliana”
Basi Daktari alikata ile simu na kumtumia mama Junior zile jumbe za jana, kwakweli mama Junior alikuwa akishangaa tu maana hakumbuki kabisa kuwasiliana na huyu daktari kuhusu maswala ya hela, kwahiyo alikuwa na mshangao, kisha daktari akampigia tena simu,
“Unajua nini Maimuna naomba unipe muda tafadhari, mimi na wewe hatuwezi kujivunjia heshima kwa vitu vidogo kama hivi. Ngoja tu nitapata ukweli”
“Duh! Ila inashangaza, au uliibiwa simu?”
“Hapana, simu ninayo mwenyewe muda wote, ngoja tu Maimuna nitakujibu”
Basi mama Junior alikata ile simu, kiukweli hakuelewa kabisa aliamua kujiandaa na kwenda moja kwa moja kwenye kwenye ofisi za mtandao wa simu ili apate taarifa za akaunti yake ya simu.
Alipopewa alistaajabu sana kuona kweli alitumiwa laki mbili na yule daktari tena sio laki mbili tupu ila ilikuwa laki mbili na elfu kumi, halafu akaona yote ilirushwa kweye namba ya Junior, kwakweli alichoka kabisa na kusema,
“Kheee tuzaege tu jamani, mambo yenyewe ndio kama haya loh! Huyu Junior angebaki tumboni kwangu si angenipatia uvimbe huyu jamani! Khaaa mtoto gani huyu!!”
Basi aliondoka zake kurudi nyumbani kwake ila alikuwa na hasira sana.
Baba Angel leo hakwenda ofisini ila alienda kwenye ujenzi wake kuangalia tu mwenyewe, na pale yule fundi wake mkuu alimwambia,
“Kwakweli hongera sana”
“Hongera ya nini tena?”
“Una kijana mwenye akili sana, yani mtoto wako ana mawazo ya kikubwa hatari tofauti na umri wake”
“Erick huyo!”
“Ndio, Erick yani akiwa hapa anasimamia utadhani ni mtu mkubwa sana yani anauelewa wa kila kitu, nakwambia karibia utaacha kutembelea kweye hizi saiti na kumuachia yeye tu afanye hivyo. Kwakweli una kijana mwerevu sana, hongera kwa hilo”
Baba Angel alifurahi sana na kujisifia zaidi,
“Yule ni mwanangu pekee wa kiume, na amechukua jina langu maana Erick ni jina langu”
“Aaaah kumbe! Yani nimemtamani hata awe ni mwanangu, jamani mtoto ana akili yule na yupo vizuri sana kichwani nina uhakika hata maendeleo yake shuleni ni mazuri. Yule mwingine sasa, na yeye ana akili sana ila asione mwanamke kapita uwiii macho juu juu mpaka namuhurumia kwakweli, ila Erick yupo makini sana”
Baba Angel alizidi kufurahi sana na kufanya upendo wake kwa Erick uwe maradufu kwani aliona fahari sana kwa kila aliyekutana nae halafu akamsifia Erick.
Basi siku hii hakukaa sana kule kwenye ujenzi na kuamua kuondoka tu sababu hakukuwa na mambo mengi sana wala nini.
Moja kwa moja baba Angel alirudi nyumbani kwake, na kumkuta mkewe akiwa chumbani muda huu akimlaza mtoto basi alisalimiana nae pale na kumuuliza,
“Erick yuko wapi?”
“Nilimuona anaenda bustanini kukaa, naona siku hizi anapenda sana lile eneo”
“Sawa, ngoja nikaongee nae”
Basi baba Angel aliondoka na kwenda bustanini ila muda huo huo mama Angel alipigiwa simu na mama Junior,
“Mdogo wangu unajua alichokifanya Junior?”
“Kafanya nini tena?”
“Ngoja tukionana nitakueleza vizuri, yani huyu mtoto ni pasua kichwa hatari”
“Ila kafanyaje dada?”
“Nitakuelezea tu hakuna tatizo”
Basi mama Junior alikata simu na kumfanya mama Angel kujiuliza kuwa tatizo ni nini ila hakupata jibu.
Wakati baba Angel na Erick walipokuwa wakirudi nyumbani, basi baba Angel alimpa Erick hela kama ambavyo alikuwa ameahidi kufanya hivyo naye Erick alimshukuru sana baba yake kisha baba Angel alimuuliza.
“Utaenda kununua nini na hiyo hela?”
“Aaah zawadi baba ila nyingine naiweka kwanza”
“Oooh haya mwanangu, kwahiyo hiyo zawadi unaenda kununua lini?”
“Kesho baba’
“Je mama yako yupo kwenye watakaopata zawadi au ni za kwako mwenyewe? Au mama yako utampa zawadi ya pipi? Yani zawadi wewe unanunua kwaajili ya nani?”
Erick akacheka kwanza na kumwambia baba yake,
“Mama, nitamnunulia zawadi ila sina tatizo sana na mama sababu huwa anapata zawadi kutoka kwako, ila zawadi ninayopanga kununua napanga kumnunulia Erica”
“Wow, mwanangu ni vizuri sana kumpenda dada yako, kumbe huwa unamkumbuka eeeh! Oooh ni vizuri sana, nina uhakika Erica atafurahia sana zawadi utakayomnunulia”
Erick akatabasamu tu, kisha baba yake akasema,
“Unajua mwanzoni nilikuwa najiuliza kuwa unapanga kununua zawadi ya nani? Nimejiuliza sana, nakumbuka mimi jamani wakati nimeanza mahusiano na mama yenu basi katika swala la zawadi ni yeye tu aliyekuwa akinijia kichwani mwangu”
“Na kabla ya hapo baba?”
“Kabla ya hapo, sikuwa mzuri sana kwenye swala la zawadi ni mpaka mtu aniambie kuwa nataka zawadi, kama dada yangu alikuwa na mtindo wa kuniambia nataka zawadi, basi ndio naenda kumnunulia. Badae nilipoanza na mama yenu alinifundisha umuhimu wa zawadi basi hata mama yangu nikaanza kumpelekea zawadi, dada yangu nae na ndugu zangu wengine. Nafurahi mwanangu umejua umuhimu wa zawadi ukiwa mdogo hivi, kwakweli dada zako wamepata kaka wa kujivunia haswaa”
Baba Angel alionekana kumfurahia sana mtoto wake na waliongea mengi sana hadi wanaingia nyumbani.
Basi kutokana na uchovu uchovu wa siku hiyo walikula tu na kwenda moja kwa moja vyumbani maana hakuna aliyekaa kuongea na wengine zaidi ya kuoga na kulala tu.
Usiku wa leo, Junior alikuwa chumbani kwa Vaileth huku akijaribu kuweka sawa baadhi ya mambo,
“Ila kwanini Junior ulinidanganya mpenzi? Yani umesema mama yako anaumwa wakati haumwi jamani Junior!”
“Kwanza naomba unisamehe sana, yani hata sijui nisemaje. Unajua mama alinidanganya pia kuwa anaumwa kumbe shida yake ilikuwa kuniona tu, si unajua huwa siendi mara kwa mara! Halafu kitu kingine, hata mamdogo kanisema sana nilivyorudi, jamani kitoto Erica ni kimbea hadi kimeshindikana. Kweli kwa sauti ile jikoni ni ya kusikiwa jamani!”
Vaileth alicheka kwa muda na kusema,
“Hujamzoea tu Erica, ila kumbuka katufichia siri”
“Kwanza tujiandae wakati wowote ule litabumburuka, katoto kambea kale wala sio ka kukaamini sana”
“Je ikibumburuka itakuwaje?”
“Yani hapo ni kukataa tu hakuna namna”
“Mmmh unajua kuwa Erica ni mbea ila sio muongo ndiomana anaaminiwa sana! Hapa ni kuombea tu asije kusema ukweli”
“Ila sijapata kuona mtu mbea kama yule mtoto, yani akija kuolewa mumewe atapata shida, hao mawifi zake na mama mkwe wajipange maana kanauwezo wa kusambaratisha ukoo mzima kwa umbea wake, atatoka kwa mama mkwe na hili na kupeleka kwa wifi hili, katoto kambea hadi kameshindikana”
“Sasa karithi wapi?”
“Aaaah sijui kwakweli, ila Vaileth kwakweli nimekumiss sana mke wangu yani nilikuwa na mambo mengi ila mawazo yote ni juu yako”
Moyo wa Vaileth uliridhika sana kwa maneno yale ya Junior na kujikuta akitabasamu tu kisha wakalala kama kawaida yao.
Mama Junior akiendelea na kazi zake za hapa na pale, mara alipigiwa simu na rafiki yake daktari, basi alitabasamu na kupokea ile simu,
“Bite, habari. Jana ndugu yangu hata hatukuongea vizuri kwani ulikumbwa na nini rafiki yangu”
“Mmmmh nini tena!!”
“Unajua nilivyopokea ule ujumbe wako tu nikaamua kutuma muda ule ule na hata sikukuuliza ndugu yangu”
“Ujumbe gani tena!”
“Khee Bite, si wewe jana umenitumia ujumbe wa kuazima laki mbili!”
“Mmmh jamani Maimuna, mimi nimekutumia huo ujumbe!! Muda gani?”
“Ngoja nikutumie zile jumbe kwanza tulizokuwa tukiwasiliana”
Basi Daktari alikata ile simu na kumtumia mama Junior zile jumbe za jana, kwakweli mama Junior alikuwa akishangaa tu maana hakumbuki kabisa kuwasiliana na huyu daktari kuhusu maswala ya hela, kwahiyo alikuwa na mshangao, kisha daktari akampigia tena simu,
“Unajua nini Maimuna naomba unipe muda tafadhari, mimi na wewe hatuwezi kujivunjia heshima kwa vitu vidogo kama hivi. Ngoja tu nitapata ukweli”
“Duh! Ila inashangaza, au uliibiwa simu?”
“Hapana, simu ninayo mwenyewe muda wote, ngoja tu Maimuna nitakujibu”
Basi mama Junior alikata ile simu, kiukweli hakuelewa kabisa aliamua kujiandaa na kwenda moja kwa moja kwenye kwenye ofisi za mtandao wa simu ili apate taarifa za akaunti yake ya simu.
Alipopewa alistaajabu sana kuona kweli alitumiwa laki mbili na yule daktari tena sio laki mbili tupu ila ilikuwa laki mbili na elfu kumi, halafu akaona yote ilirushwa kweye namba ya Junior, kwakweli alichoka kabisa na kusema,
“Kheee tuzaege tu jamani, mambo yenyewe ndio kama haya loh! Huyu Junior angebaki tumboni kwangu si angenipatia uvimbe huyu jamani! Khaaa mtoto gani huyu!!”
Basi aliondoka zake kurudi nyumbani kwake ila alikuwa na hasira sana.
Baba Angel leo hakwenda ofisini ila alienda kwenye ujenzi wake kuangalia tu mwenyewe, na pale yule fundi wake mkuu alimwambia,
“Kwakweli hongera sana”
“Hongera ya nini tena?”
“Una kijana mwenye akili sana, yani mtoto wako ana mawazo ya kikubwa hatari tofauti na umri wake”
“Erick huyo!”
“Ndio, Erick yani akiwa hapa anasimamia utadhani ni mtu mkubwa sana yani anauelewa wa kila kitu, nakwambia karibia utaacha kutembelea kweye hizi saiti na kumuachia yeye tu afanye hivyo. Kwakweli una kijana mwerevu sana, hongera kwa hilo”
Baba Angel alifurahi sana na kujisifia zaidi,
“Yule ni mwanangu pekee wa kiume, na amechukua jina langu maana Erick ni jina langu”
“Aaaah kumbe! Yani nimemtamani hata awe ni mwanangu, jamani mtoto ana akili yule na yupo vizuri sana kichwani nina uhakika hata maendeleo yake shuleni ni mazuri. Yule mwingine sasa, na yeye ana akili sana ila asione mwanamke kapita uwiii macho juu juu mpaka namuhurumia kwakweli, ila Erick yupo makini sana”
Baba Angel alizidi kufurahi sana na kufanya upendo wake kwa Erick uwe maradufu kwani aliona fahari sana kwa kila aliyekutana nae halafu akamsifia Erick.
Basi siku hii hakukaa sana kule kwenye ujenzi na kuamua kuondoka tu sababu hakukuwa na mambo mengi sana wala nini.
Moja kwa moja baba Angel alirudi nyumbani kwake, na kumkuta mkewe akiwa chumbani muda huu akimlaza mtoto basi alisalimiana nae pale na kumuuliza,
“Erick yuko wapi?”
“Nilimuona anaenda bustanini kukaa, naona siku hizi anapenda sana lile eneo”
“Sawa, ngoja nikaongee nae”
Basi baba Angel aliondoka na kwenda bustanini ila muda huo huo mama Angel alipigiwa simu na mama Junior,
“Mdogo wangu unajua alichokifanya Junior?”
“Kafanya nini tena?”
“Ngoja tukionana nitakueleza vizuri, yani huyu mtoto ni pasua kichwa hatari”
“Ila kafanyaje dada?”
“Nitakuelezea tu hakuna tatizo”
Basi mama Junior alikata simu na kumfanya mama Angel kujiuliza kuwa tatizo ni nini ila hakupata jibu.