Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #321
SEHEMU YA 276
Ila Erica alivyotoka chumbani kwa Vaileth moja kwa moja alienda bustanini maana alimuona Junior akielekea huko basi alimkuta na kuanza kuongea nae,
“Umemfanya nini dada Vai?”
“Kwanini?”
“Nimemkuta macho yamemvimba, kanidanganya kuwa macho yanamuuma ila anavyoonekana ni kuwa amelia sana”
“Mmmh mimi sijui kitu”
“Halafu kitu kingine, siku ile Samia amekuja amesema kuwa ulimpatia laki tano”
“Mmmh huyo Samia chizi eeeh!”
“Ndio kasema, pia kasema wewe hakupendi wala nini ila kuna mwanaume mwingine kwenye nyumba yetu ndio anampenda”
“Haya sasa umeona kama Samia ni chizi, anamaanisha kuwa anampenda Erick”
Hapo Erica akashtuka kidogo na kuuliza tena,
“Unasema?”
“Ndio hivyo anampenda Erick, sasa unashtuka nini? Samia ni msichana na Erick ni mvulana, tatizo liko wapi wakipendana? Hutaki wifi wewe? Ndio nyie ambao huwa mnagombana na mawifi zenu bila sababu”
“Kwani mimi nimesema jambo lolote”
“Hata kama ila nakuelewesha”
“Ila umebadili mada tu, umemuhonga Samia laki tano!!”
Vaileth akaenda kule bustanini pia maana alikuwa anataka kufagia kidogo na kuweka mazingira safi, kwahiyo alisikia haya maneno ya mwishoni na kumfanya aelewe zaidi kuwa kwanini Junior aling’ang’ania kumsindikiza Samia siku ile, kwahiyo Vaileth akazidi kupata ushahidi.
Basi alisogea pale na Junior alimsalimia ila hakumuitikia yani moyoni mwake alikuwa na kinyongo sana.
Kisha muda wa kwenda kanisani leo wote walijiandaa na kwenda Kanisani kama kawaida ya nyumba hii, na leo ni nyumba nzima waliondoka na kwenda Kanisani.
Huku nyumbani alifika Derrick ambaye alikaribishwa na mlinzi tu na kwenda kukaa kwenye kibaraza kwani familia nzima hii haitakuwepo kwa siku hiyo.
Basi alikaa pale kwenye kibaraza hadi akasinzia pale pale, ila wakati amesinzia akajiwa na ndoto na hiyo ndoto aliona watu wengi wamemzingira huku wakisema mwizi huyooo, mwizi huyooo piga pia, Derrick alishtuka sana huku akihema, akaamka na kujisemea,
“Ila mimi sio mwizi, mimi siibi na simpori yoyote ila wanatoa kwa hiari yao, nitakuwaje mwizi sasa?”
Akaona hapo hata hapamfai kuendelea kusinzia sababu alikuwa na mambo yake mengi tu ya kufanya basi aliinuka na kumuaga mlinzi na kuondoka zake.
Wakati anaondoka ndipo akakutana na Tumaini ambaye nae alikuwa akienda mahali hapo, ila alikuwa ameongozana na rafiki yake kwa muda huo basi akamuuliza Derrick,
“Kheee Derrick, leo ulikumbuka kuja kwa dada yako!”
“Ndio, nilitaka kumsalimia maana nimemkumbuka sana ila sijawakuta”
Huyu rafiki yake Tumaini alishtuka kidogo na kumuuliza Derrick,
“Kaka, hunikumbuki?”
“Nikukumbuke kwani tumesoma wote?”
“Hapana sio hivyo, mimi nakukumbuka vizuri ulinitapeli wewe”
“Kuwa na adabu mwanamke, hivi unavyoniona nina muonekano wa kitapeli? Kuwa na heshima”
Kisha akamuaga Tumaini na kuondoka zake, ambapo yule dada alimwambia Tumaini,
“Huyu kaka ni tapeli, yani alinitapeli mimi kila kitu nilichokuwa nacho”
“Lazima umemfananisha, unajua anafanya kazi gani huyu? Unajua elimu yake, hawezi kuwa tapeli hata kidogo”
“Namkumbuka vizuri dada, alinitapeli huyu”
“Haiwezekani nakwambia, wewe nawe ujue tunaenda nyumbani kwa dada yake kwenye ofisi yake anatafuta mtu wa kumsaidia ndio nakupeleka wewe unaanza kumuita kaka yake tapeli, hebu usije sema hivyo mbele yake kabisa”
Ila sasa hata na wao waliposogea kwa mlinzi waliambiwa vile vile kuwa wale watu bado wapo Kanisani na siku hiyo walichelewa sana kutoka Kanisani tofauti na siku zingine, waliwasubiri pia na kuchoka ikabidi waondoke zao tu.
Siku ya leo, walipotoka Kanisani baba Angel aliamua kuwapeleka wote kwenda kula hotelini, yani siku hiyo alikuwa na furaha sana ya kumaliza ujenzi wake wa kile kiwanda kidogo, kwahiyo alikaa na familia yake na kuagiza nao chakula ambapo walikuwa wakila huku wakifurahi, kasoro Vaileth ambaye muda mwingi alikuwa kimya kwani alikuwa akifikiria laki tano yake, ila walipomuuliza sababu ya kuwa kimya kiasi kile alisingizia kuwa siku hiyo hakuamka vizuri tu.
Basi walikuwa wanakula huku wakiongea mambo mbalimbali ndipo Junior alipoingizia swala la kumuona Derrick ufukweni,
“Halafu mamdogo, tulimuona mjomba Derrick mahali anacheza ile michezo ya kitapeli”
“Michezo gani?”
“Ule mchezo wa karata tatu”
Baba Angel alishtuka kidogo na kusema,
“Hivi ule mchezo bado upo!! Kwahiyo kuna watu wanapeliwa bado kwa ule mchezo, nakumbuka zamani sana utakuta mtu anatapeliwa hadi nguo”
“Hata hapo ilikuwa hivyo hivyo, unajua bamdogo mjini kila siku washamba wanaongezeka, yani kuna watu hawajui kama ile ni michezo ya kitapeli”
“Hivi mmesema Derrick, mna uhakika nyie mnamfahamu Derrick?”
“Tumemuita na kumuita, akasogea na kuuliza tunafanya nini halafu akaondoka”
Mama Angel alikaa kimya tu kwani alishawahi kuambiwa tabia ya kaka yake huyo kwa siku hizo kwahiyo akajikuta hana cha kusema, mumewe akamuangalia na kumuuliza,
“Kwahiyo unaamini haya maneno ya watoto?”
“Tutaongea zaidi tukirudi nyumbani ila sio muda huu”
Yani mama Angel alikatisha yale maneno ya kuhusu ndugu yake, mara kuna ujumbe uliingia kwenye simu yake basi akafungua na kusoma,
“NImekuja kwenu nimekaa sana hadi nimechoka, by Derrick”
Mama Angel akashtuka kidogo kwani kwa tabia ya utapeli aliyosimuliwa kuhusu Derrick akajikuta akihofia kuwa isikuwa Derrick kamtapeli hadi mlinzi wao ila akaona ni vyema asiwaze hayo sana sababu atashindwa kukaa vizuri mahali pale na kufurahi na familia yake.
Basi waliendelea tu na mazungumzo mengine hadi pale walipomaliza na kufurahi.
Sia akiwa katika harakati zake za biashara, anakutana na Dora na kumsimamisha kisha kuanza kuongea nae,
“Leo sijakusimamisha kwa ubaya Dora maana hapo ulipo tayari ushakunja sura jamani, pole sana”
“Kwani mimi nimesema kuwa umenifananisha kwa shari? Hata hivyo niambie ulichonisimamisha, kwanza upo kwenye biashara saa hizi hukwenda kwenye ibada leo?”
“Leo sijaenda, yani mimi kwenda kuna watoto wa Erick, wakiniona kanisani wanaona kama mzuka vile”
“Jamani! Mbona una mambo ya ajabu Sia, kwani wale watoto wanakufahamu?”
“Tuachane na habari hiyo, Kwa kifupi ni hivi, mdogo wako kapewa dawa na yule mwanamke”
“Kivipi?”
Sia alianza kumueleza toka yule madam Oliva alivyokuwa akimtaka Erick, na jinsi ambavyo alimpelekea Erick viatu halafu mama Angel akavipeleka kwa Steve,
“Kheee kumbe ndio ilivyokuwa!”
“Ndio hivyo”
“Jamani kwanini mdogo wangu mmemuonea hivi!! Hivi kweli haiwezekani kwa yeye kumpenda mwanamke anayemtaka mpaka mumkorogee madawa, kuna kipindi mtaharibu akili ya mdogo wangu”
“Mmmh usiniseme mimi, mseme huyo wifi yako mpya”
“Simtambui kama ni wifi yangu”
“Hata mimi hujawahi kunitambua ingawa nimezaa na kaka yako, yani wewe Dora una matatizo sana”
“Ila samahani, unapafahamu nyumbani kwa huyo mwanamke?”
“Napafamu ndio”
“Nakuomba basi unipeleke ili nikaongee nao mwenyewe”
Sia alikubali kumpeleka na aliweka vitu vyake vizuri kisha yeye na Dora waliondoka eneo lilena kwenda nyumbani kwa madam Oliva.
Walifika pale na kugonga geti ambapo mlinzi wa nyumba ile alienda kufungua mlango, ila macho ya Diora na yule mlinzi yalipokutana kila mmoja alionekana kupata mshangao dhidi ya mwenzie.
Sia alikubali kumpeleka na aliweka vitu vyake vizuri kisha yeye na Dora waliondoka eneo lilena kwenda nyumbani kwa madam Oliva.
Walifika pale na kugonga geti ambapo mlinzi wa nyumba ile alienda kufungua mlango, ila macho ya Dora na yule mlinzi yalipokutana kila mmoja alionekana kupata mshangao dhidi ya mwenzie.
Waliangaliana kwa makini sana, ila mwisho wa siku Dora alijihisi vibaya kwani huyu mlinzi wa madam Oliva alikuwa ni mtoto wa James ambaye alizaa na msichana wa kazi, maana alimuuliza,
“Unaitwa nani kijana?”
“Naitwa James”
“Imekuwaje hadi umekuwa mlinzi?”
“Unajua mimi naishi na mjomba, sasa kila kitu namtegemea mjomba, nikaona ni vyema nitafute kazi ila Mungu mwema ndio nikapata kazi mahali hapa”
Kwakweli Dora aliacha hadi kufikiria kilichompeleka mahali pale na kujikuta akimuangalia kwa makini sana huyu kijana kwani moyo ulikuwa ukimuuma sana, basi Sia alimuuliza,
“Inamaana huyu ni James, mtoto wa James!”
Dora aliitikia kwa kichwa tu kisha Sia akamwambia,
“Mimi nilishawahi kukwambia haya, nadhani leo umenielewa ni kitu gani nilichokuwa nazungumzia, unaishi kwenye nyumba nzuri, una maisha mazuri, unafanya utakacho ila watoto wa huyo mtu wanaishije? Je wanalalamikaje kwa Mungu. Haya kama wamefikia hatua ya kuwa walinzi ni mara ngapi wamelalamika kwa Mungu, na wakati wewe unaouwezo wa kuwasaidia?”
Basi Dora akamuangalia yule kijana na kumuandikia namba yake kwenye karatasi kisha akampatia na kumwambia,
“Naomba utanitafuta”
Halafu Dora akaondoka, ikabidi Sia nae aondoke zake maana aliyempeleka alikuwa ameondoka kwa muda huo.
Ila Erica alivyotoka chumbani kwa Vaileth moja kwa moja alienda bustanini maana alimuona Junior akielekea huko basi alimkuta na kuanza kuongea nae,
“Umemfanya nini dada Vai?”
“Kwanini?”
“Nimemkuta macho yamemvimba, kanidanganya kuwa macho yanamuuma ila anavyoonekana ni kuwa amelia sana”
“Mmmh mimi sijui kitu”
“Halafu kitu kingine, siku ile Samia amekuja amesema kuwa ulimpatia laki tano”
“Mmmh huyo Samia chizi eeeh!”
“Ndio kasema, pia kasema wewe hakupendi wala nini ila kuna mwanaume mwingine kwenye nyumba yetu ndio anampenda”
“Haya sasa umeona kama Samia ni chizi, anamaanisha kuwa anampenda Erick”
Hapo Erica akashtuka kidogo na kuuliza tena,
“Unasema?”
“Ndio hivyo anampenda Erick, sasa unashtuka nini? Samia ni msichana na Erick ni mvulana, tatizo liko wapi wakipendana? Hutaki wifi wewe? Ndio nyie ambao huwa mnagombana na mawifi zenu bila sababu”
“Kwani mimi nimesema jambo lolote”
“Hata kama ila nakuelewesha”
“Ila umebadili mada tu, umemuhonga Samia laki tano!!”
Vaileth akaenda kule bustanini pia maana alikuwa anataka kufagia kidogo na kuweka mazingira safi, kwahiyo alisikia haya maneno ya mwishoni na kumfanya aelewe zaidi kuwa kwanini Junior aling’ang’ania kumsindikiza Samia siku ile, kwahiyo Vaileth akazidi kupata ushahidi.
Basi alisogea pale na Junior alimsalimia ila hakumuitikia yani moyoni mwake alikuwa na kinyongo sana.
Kisha muda wa kwenda kanisani leo wote walijiandaa na kwenda Kanisani kama kawaida ya nyumba hii, na leo ni nyumba nzima waliondoka na kwenda Kanisani.
Huku nyumbani alifika Derrick ambaye alikaribishwa na mlinzi tu na kwenda kukaa kwenye kibaraza kwani familia nzima hii haitakuwepo kwa siku hiyo.
Basi alikaa pale kwenye kibaraza hadi akasinzia pale pale, ila wakati amesinzia akajiwa na ndoto na hiyo ndoto aliona watu wengi wamemzingira huku wakisema mwizi huyooo, mwizi huyooo piga pia, Derrick alishtuka sana huku akihema, akaamka na kujisemea,
“Ila mimi sio mwizi, mimi siibi na simpori yoyote ila wanatoa kwa hiari yao, nitakuwaje mwizi sasa?”
Akaona hapo hata hapamfai kuendelea kusinzia sababu alikuwa na mambo yake mengi tu ya kufanya basi aliinuka na kumuaga mlinzi na kuondoka zake.
Wakati anaondoka ndipo akakutana na Tumaini ambaye nae alikuwa akienda mahali hapo, ila alikuwa ameongozana na rafiki yake kwa muda huo basi akamuuliza Derrick,
“Kheee Derrick, leo ulikumbuka kuja kwa dada yako!”
“Ndio, nilitaka kumsalimia maana nimemkumbuka sana ila sijawakuta”
Huyu rafiki yake Tumaini alishtuka kidogo na kumuuliza Derrick,
“Kaka, hunikumbuki?”
“Nikukumbuke kwani tumesoma wote?”
“Hapana sio hivyo, mimi nakukumbuka vizuri ulinitapeli wewe”
“Kuwa na adabu mwanamke, hivi unavyoniona nina muonekano wa kitapeli? Kuwa na heshima”
Kisha akamuaga Tumaini na kuondoka zake, ambapo yule dada alimwambia Tumaini,
“Huyu kaka ni tapeli, yani alinitapeli mimi kila kitu nilichokuwa nacho”
“Lazima umemfananisha, unajua anafanya kazi gani huyu? Unajua elimu yake, hawezi kuwa tapeli hata kidogo”
“Namkumbuka vizuri dada, alinitapeli huyu”
“Haiwezekani nakwambia, wewe nawe ujue tunaenda nyumbani kwa dada yake kwenye ofisi yake anatafuta mtu wa kumsaidia ndio nakupeleka wewe unaanza kumuita kaka yake tapeli, hebu usije sema hivyo mbele yake kabisa”
Ila sasa hata na wao waliposogea kwa mlinzi waliambiwa vile vile kuwa wale watu bado wapo Kanisani na siku hiyo walichelewa sana kutoka Kanisani tofauti na siku zingine, waliwasubiri pia na kuchoka ikabidi waondoke zao tu.
Siku ya leo, walipotoka Kanisani baba Angel aliamua kuwapeleka wote kwenda kula hotelini, yani siku hiyo alikuwa na furaha sana ya kumaliza ujenzi wake wa kile kiwanda kidogo, kwahiyo alikaa na familia yake na kuagiza nao chakula ambapo walikuwa wakila huku wakifurahi, kasoro Vaileth ambaye muda mwingi alikuwa kimya kwani alikuwa akifikiria laki tano yake, ila walipomuuliza sababu ya kuwa kimya kiasi kile alisingizia kuwa siku hiyo hakuamka vizuri tu.
Basi walikuwa wanakula huku wakiongea mambo mbalimbali ndipo Junior alipoingizia swala la kumuona Derrick ufukweni,
“Halafu mamdogo, tulimuona mjomba Derrick mahali anacheza ile michezo ya kitapeli”
“Michezo gani?”
“Ule mchezo wa karata tatu”
Baba Angel alishtuka kidogo na kusema,
“Hivi ule mchezo bado upo!! Kwahiyo kuna watu wanapeliwa bado kwa ule mchezo, nakumbuka zamani sana utakuta mtu anatapeliwa hadi nguo”
“Hata hapo ilikuwa hivyo hivyo, unajua bamdogo mjini kila siku washamba wanaongezeka, yani kuna watu hawajui kama ile ni michezo ya kitapeli”
“Hivi mmesema Derrick, mna uhakika nyie mnamfahamu Derrick?”
“Tumemuita na kumuita, akasogea na kuuliza tunafanya nini halafu akaondoka”
Mama Angel alikaa kimya tu kwani alishawahi kuambiwa tabia ya kaka yake huyo kwa siku hizo kwahiyo akajikuta hana cha kusema, mumewe akamuangalia na kumuuliza,
“Kwahiyo unaamini haya maneno ya watoto?”
“Tutaongea zaidi tukirudi nyumbani ila sio muda huu”
Yani mama Angel alikatisha yale maneno ya kuhusu ndugu yake, mara kuna ujumbe uliingia kwenye simu yake basi akafungua na kusoma,
“NImekuja kwenu nimekaa sana hadi nimechoka, by Derrick”
Mama Angel akashtuka kidogo kwani kwa tabia ya utapeli aliyosimuliwa kuhusu Derrick akajikuta akihofia kuwa isikuwa Derrick kamtapeli hadi mlinzi wao ila akaona ni vyema asiwaze hayo sana sababu atashindwa kukaa vizuri mahali pale na kufurahi na familia yake.
Basi waliendelea tu na mazungumzo mengine hadi pale walipomaliza na kufurahi.
Sia akiwa katika harakati zake za biashara, anakutana na Dora na kumsimamisha kisha kuanza kuongea nae,
“Leo sijakusimamisha kwa ubaya Dora maana hapo ulipo tayari ushakunja sura jamani, pole sana”
“Kwani mimi nimesema kuwa umenifananisha kwa shari? Hata hivyo niambie ulichonisimamisha, kwanza upo kwenye biashara saa hizi hukwenda kwenye ibada leo?”
“Leo sijaenda, yani mimi kwenda kuna watoto wa Erick, wakiniona kanisani wanaona kama mzuka vile”
“Jamani! Mbona una mambo ya ajabu Sia, kwani wale watoto wanakufahamu?”
“Tuachane na habari hiyo, Kwa kifupi ni hivi, mdogo wako kapewa dawa na yule mwanamke”
“Kivipi?”
Sia alianza kumueleza toka yule madam Oliva alivyokuwa akimtaka Erick, na jinsi ambavyo alimpelekea Erick viatu halafu mama Angel akavipeleka kwa Steve,
“Kheee kumbe ndio ilivyokuwa!”
“Ndio hivyo”
“Jamani kwanini mdogo wangu mmemuonea hivi!! Hivi kweli haiwezekani kwa yeye kumpenda mwanamke anayemtaka mpaka mumkorogee madawa, kuna kipindi mtaharibu akili ya mdogo wangu”
“Mmmh usiniseme mimi, mseme huyo wifi yako mpya”
“Simtambui kama ni wifi yangu”
“Hata mimi hujawahi kunitambua ingawa nimezaa na kaka yako, yani wewe Dora una matatizo sana”
“Ila samahani, unapafahamu nyumbani kwa huyo mwanamke?”
“Napafamu ndio”
“Nakuomba basi unipeleke ili nikaongee nao mwenyewe”
Sia alikubali kumpeleka na aliweka vitu vyake vizuri kisha yeye na Dora waliondoka eneo lilena kwenda nyumbani kwa madam Oliva.
Walifika pale na kugonga geti ambapo mlinzi wa nyumba ile alienda kufungua mlango, ila macho ya Diora na yule mlinzi yalipokutana kila mmoja alionekana kupata mshangao dhidi ya mwenzie.
Sia alikubali kumpeleka na aliweka vitu vyake vizuri kisha yeye na Dora waliondoka eneo lilena kwenda nyumbani kwa madam Oliva.
Walifika pale na kugonga geti ambapo mlinzi wa nyumba ile alienda kufungua mlango, ila macho ya Dora na yule mlinzi yalipokutana kila mmoja alionekana kupata mshangao dhidi ya mwenzie.
Waliangaliana kwa makini sana, ila mwisho wa siku Dora alijihisi vibaya kwani huyu mlinzi wa madam Oliva alikuwa ni mtoto wa James ambaye alizaa na msichana wa kazi, maana alimuuliza,
“Unaitwa nani kijana?”
“Naitwa James”
“Imekuwaje hadi umekuwa mlinzi?”
“Unajua mimi naishi na mjomba, sasa kila kitu namtegemea mjomba, nikaona ni vyema nitafute kazi ila Mungu mwema ndio nikapata kazi mahali hapa”
Kwakweli Dora aliacha hadi kufikiria kilichompeleka mahali pale na kujikuta akimuangalia kwa makini sana huyu kijana kwani moyo ulikuwa ukimuuma sana, basi Sia alimuuliza,
“Inamaana huyu ni James, mtoto wa James!”
Dora aliitikia kwa kichwa tu kisha Sia akamwambia,
“Mimi nilishawahi kukwambia haya, nadhani leo umenielewa ni kitu gani nilichokuwa nazungumzia, unaishi kwenye nyumba nzuri, una maisha mazuri, unafanya utakacho ila watoto wa huyo mtu wanaishije? Je wanalalamikaje kwa Mungu. Haya kama wamefikia hatua ya kuwa walinzi ni mara ngapi wamelalamika kwa Mungu, na wakati wewe unaouwezo wa kuwasaidia?”
Basi Dora akamuangalia yule kijana na kumuandikia namba yake kwenye karatasi kisha akampatia na kumwambia,
“Naomba utanitafuta”
Halafu Dora akaondoka, ikabidi Sia nae aondoke zake maana aliyempeleka alikuwa ameondoka kwa muda huo.