Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #341
SEHEMU YA 296
Erica alikuwa anakaribia kutoka shule, alifika rafiki yake Samia na kumsisitiza kuhusu Junior kumpatia yeye pesa,
“Mmmh Junior nae, ana tamaa sana yule halafu muhuni sana”
“Namjua vizuri yule kaka yako halafu mimi simpendi wala nini, yani simpendi kabisa”
“Tena uwe unamshushua kabisa”
“Ila nina ujumbe wangu huu naomba ukamkabidhi Erick”
Samia alimpa Erica ule ujumbe ambapo ulikuwa ndani ya bahasha, na juu ya bahasha hiyo iliandikwa Erick, basi Erica alikubali kuwa barua hiyo ataifikisha,
“Nitafurahi sana ukimpatia ujumbe wangu huo, halafu mwambie kuwa nasubiria barua kesho toka kwake kwahiyo atakuagiza wewe”
“Sawa, hakuna tatizo”
Erica aliiweka ile barua ila kiukweli alitamani sana kujua ni kitu gani kilikuwa kimeandikwa kwenye ile barua, alitamani sana afike nyumbani mapema ili aangalie kuna ujumbe gani.
Erica alipofika nyumbani tu, cha kwanza alienda chumbani kwake na kabla hata hajavua zile sare za shule alifungua kwanza ile barua na kuanza kuisoma,
“Kwako Erick, najua utastaajabu sana kwa hii barua yangu fupi, inawezekana si kawaida kwako kuambiwa na mwanamke neno nakupenda, kwakweli nimevumilia sana ila nimeshindwa, nakupenda sana Erick, nahitaji uwe mpenzi wangu. Tafadhari naomba unijibu”
Basi Erica alisoma mara mbilimbili na kusema,
“Kheee hivi huyu Samia ana wazimu au kitu gani? Yani kabisa kaka chini na kuandika barua kama hii kwa Erick jamani!! Sasa ngoja nimjibu, mjinga kabisa huyu msichana”
Akachukua peni na karatasi na kuanza kuandika jibu kwa Samia, ila alijifikiria na kusema,
“Ila Samia atasema mbona muandiko sio wangu?”
“Ngoja nikampelekee Erick mwenyewe aamue mwenyewe, akikubali tu basi nauvunja undugu leo”
Akatoka chumbani kwake na moja kwa moja akaingia chumbani kwa Erick ambapo alikuwa akibadilisha nguo, yeye mwenyewe Erica alipoingia alishtuka na kumwambia
“Jifunike jamani Erick”
“Na wewe kwanini unapenda kuingia chumbani kwangu bila hodi!”
“Mmmh yani hadi mimi nigonge hodi jamani!! Sijazoea hayo”
Basi Erick alijifunga taulo na kukaa ili kusikiliza ujumbe ambao umeletwa na Erica,
“Samahani, Samia kanipa barua yako ila sijaweza kuvumilia nimeifungua na kuisoma ndio nimekuletea, naomba nisamehe”
“Ingekuwa siijui tabia yako ya umbea sawa, ila naijua fika tabia yako”
“Jamani Erick, ndio maneno gani hayo!!”
Erick alichukua ile barua na kusoma ule ujumbe, alisikitika sana na kumuangalia Erica kisha akamuuliza,
“Nishauri nimuandikie jibu gani?”
“Sina ushauri ila usirogwe kukubali maana leo nitavunja undugu baina yetu”
“Kwanini sasa?”
“Kwanini!! Inamaana umesahau ahadi yetu au!!”
“Ahadi yetu naikumbuka, ni kuwa nisiwe na rafiki wa kike na wewe usiwe na rafiki wa kiume, haya huyu sio rafiki anaomba kuwa mpenzi. Kwani wewe unaweza kuwa mpenzi wangu?”
Erica alichukia kwa swali hilo, aliinuka na kuondoka zake na kumfanya Erick ajue kuwa amemkera kwa swali alilomuuliza.
Baba Angel leo wakati anarudi nyumbani kwake, alimuona Derrick njiani, tena akiwa amesimama na mtu yani hapo akili ikamcheza kuwa Derrick anataka kumliza mtu huyo, basi akasimamisha gari, akashuka na kumfata karibu halafu akamuita yani Derrick alishtuka kama mtu aliyeshtuliwa toka usingizini kiasi kwamba hata hakuweza kuongea tena na yule mtu ila Erick alimvuta mkono pembeni na kuongea nae,
“Derrick, hiki unachokifanya sio kabisa na kitakupeleka pabaya”
“Najua ushasikia vingi kuhusu mimi, hata wewe unaweza kuwa mmoja kati ya watu wanaonichukia”
“Sikuchukii kabisa, na nikuchukie kwasababu ipi? Naomba twende mahali tuongee kidogo”
Basi wakapanda kwenye gari, na kweli walishuka mahali na kupata sehemu nzuri na kukaa kisha kuanza mazungumzo ya hapa na pale,
“Kwanza kabisa Derrick ni kitu gani kikubwa kinakusumbua?”
“Sijui nikuelezeje upate kunielewa, ni hivi katika dunia mimi ni kiumbe nisiyekuwa na bahati kabisa”
“Huna bahati kivipi?”
“Kwanza kabisa, mimi nimeanza kukataliwa toka nipo tumboni mwa mama yangu, nimezaliwa sijapata mapenzi ya baba kabisa, nimepelekwa nyumbani kwa baba nasikia tukatimuliwa, toka hapo ndugu wa baba hawanipendi ni wachache tu wanaonaoniona kama mmoja wa familia yao. Nimekazana nitoke kimaisha, mama yangu kapata tabu ya kunisomesha na kweli nimefika chuo, nimehangaika kupata kazi, nikapata kazi ila hiyo kazi nimefukuzwa, hivi ni maisha gani nitakayoishi mimi? Kwanini dunia inanifanya hivi!! Ndiomana nikaamua nichague aina nyingine ya maisha kwani hata mimi natamani nimuhudumie mama yangu, nae aishi vizuri na ashukuru kunizaa”
“Unajua Derrick umekata tamaa mapema sana, yani elimu yako hupendezi kabisa kufanya kazi ya kitapeli, hivi kweli umetafuta kazi kote imeshindikana? Kuna siku hata umewahi kuja kwangu na kusema shemeji nisaidie angalau nipate kazi?”
“Hivi nakuja vipi kwako ikiwa mkeo ambaye nina undugu nae, hataki hata kuniona. Yani mimi sijui ni gundu sijui ni kitu gani. Katika maisha yangu ni kweli nilikuwa muhuni sana ila hakuna kitu ambacho sikupenda kama kutoa mimba, ila kuna mwanamke aliivuruga akili yangu kwa kutoa mimba yangu, huyu alikuwa ni mwanamke wa kwanza kumpa mimba na alikuwa wa kwanza kuitoa mimba yangu, kiukweli aliivuruga sana akili yangu, toka hapo huwa nahisi akili ikiwehuka tu. Kuna mwanamke nimezaa nae, na siku zote najua mtoto ni wangu kumbe mtoto mwenyewe katupa mababa wawili, yani wanawake jamani dah!! Ameona sieleweki ndio anasema yule mtoto sio wako, nimeumia sana, ila najua yule ni mwanangu ila tu sababu wanawake wanaangalia sehemu yenye maslahi zaidi”
“Kwahiyo huyo mtoto yuko wapi?”
“Najua basi, yule mwanamke alihama na watoto wake, roho iliniuma sana kila siku naenda kumlilia mwanangu, nilimpa jina la mama yangu ila yeye kampa jina lake analolijua mwenyewe. Yote hii sababu sijapata maslahi tu”
“Toka uanze kutapeli hujapata maslahi tu!!”
“Sijui ni kitu gani, sijui ni laana sijui ni nini. Yani mimi huwa natapeli hela za maana ila hakuna kitu cha maana ninachofanya”
“Unapotea ndugu yangu, yani unapotea kabisa. Kiukweli Erica kanibadilisha mimi ila ilikuwa rahisi sababu na mimi niliona ile njia niliyokuwa napita haikuwa njia sahihi kwa mimi kuendelea nayo, unajua kuna vitu vingine badala vikuendeleze vinakutia umasikini tu, unapata pesa ya laana kwa uongo ila pesa hiyo hiyo unayopata unaenda kumalizia kwa wanawake, haya hayo maendeleo utayatoa wapi?”
“Ni kweli kabisa, ila hii laana imeletwa na yule mwanamke aliyetoa mimba yangu”
“Basi achana na hayo, kama upo tayari naomba kesho niache mambo yangu nikupeleke kwenye maombia. Upo tayari?”
“Mmmmh!!”
“Nini sasa Derrick?”
“Utanipeleka kwenye maombi, utanipa na kazi? Maana hata niombewe na wachungaji wote duniani, na mshekhe nao waungane wote, ila kama sina kazi mwendo utakuwa ni huu huu wa kutapeli tu”
“Dah!! Yani wewe jamani!! Nitakupatia na kazi, ila sasa huwezi kufanya kazi vizuri kama hujaamua kuacha kabisa haya unayoyafanya”
Basi wakakubaliana pale kuwa wataonana kesho yake ili kuweza kuzungumza na kwenda huko kwenye maombi.
Erica alikuwa anakaribia kutoka shule, alifika rafiki yake Samia na kumsisitiza kuhusu Junior kumpatia yeye pesa,
“Mmmh Junior nae, ana tamaa sana yule halafu muhuni sana”
“Namjua vizuri yule kaka yako halafu mimi simpendi wala nini, yani simpendi kabisa”
“Tena uwe unamshushua kabisa”
“Ila nina ujumbe wangu huu naomba ukamkabidhi Erick”
Samia alimpa Erica ule ujumbe ambapo ulikuwa ndani ya bahasha, na juu ya bahasha hiyo iliandikwa Erick, basi Erica alikubali kuwa barua hiyo ataifikisha,
“Nitafurahi sana ukimpatia ujumbe wangu huo, halafu mwambie kuwa nasubiria barua kesho toka kwake kwahiyo atakuagiza wewe”
“Sawa, hakuna tatizo”
Erica aliiweka ile barua ila kiukweli alitamani sana kujua ni kitu gani kilikuwa kimeandikwa kwenye ile barua, alitamani sana afike nyumbani mapema ili aangalie kuna ujumbe gani.
Erica alipofika nyumbani tu, cha kwanza alienda chumbani kwake na kabla hata hajavua zile sare za shule alifungua kwanza ile barua na kuanza kuisoma,
“Kwako Erick, najua utastaajabu sana kwa hii barua yangu fupi, inawezekana si kawaida kwako kuambiwa na mwanamke neno nakupenda, kwakweli nimevumilia sana ila nimeshindwa, nakupenda sana Erick, nahitaji uwe mpenzi wangu. Tafadhari naomba unijibu”
Basi Erica alisoma mara mbilimbili na kusema,
“Kheee hivi huyu Samia ana wazimu au kitu gani? Yani kabisa kaka chini na kuandika barua kama hii kwa Erick jamani!! Sasa ngoja nimjibu, mjinga kabisa huyu msichana”
Akachukua peni na karatasi na kuanza kuandika jibu kwa Samia, ila alijifikiria na kusema,
“Ila Samia atasema mbona muandiko sio wangu?”
“Ngoja nikampelekee Erick mwenyewe aamue mwenyewe, akikubali tu basi nauvunja undugu leo”
Akatoka chumbani kwake na moja kwa moja akaingia chumbani kwa Erick ambapo alikuwa akibadilisha nguo, yeye mwenyewe Erica alipoingia alishtuka na kumwambia
“Jifunike jamani Erick”
“Na wewe kwanini unapenda kuingia chumbani kwangu bila hodi!”
“Mmmh yani hadi mimi nigonge hodi jamani!! Sijazoea hayo”
Basi Erick alijifunga taulo na kukaa ili kusikiliza ujumbe ambao umeletwa na Erica,
“Samahani, Samia kanipa barua yako ila sijaweza kuvumilia nimeifungua na kuisoma ndio nimekuletea, naomba nisamehe”
“Ingekuwa siijui tabia yako ya umbea sawa, ila naijua fika tabia yako”
“Jamani Erick, ndio maneno gani hayo!!”
Erick alichukua ile barua na kusoma ule ujumbe, alisikitika sana na kumuangalia Erica kisha akamuuliza,
“Nishauri nimuandikie jibu gani?”
“Sina ushauri ila usirogwe kukubali maana leo nitavunja undugu baina yetu”
“Kwanini sasa?”
“Kwanini!! Inamaana umesahau ahadi yetu au!!”
“Ahadi yetu naikumbuka, ni kuwa nisiwe na rafiki wa kike na wewe usiwe na rafiki wa kiume, haya huyu sio rafiki anaomba kuwa mpenzi. Kwani wewe unaweza kuwa mpenzi wangu?”
Erica alichukia kwa swali hilo, aliinuka na kuondoka zake na kumfanya Erick ajue kuwa amemkera kwa swali alilomuuliza.
Baba Angel leo wakati anarudi nyumbani kwake, alimuona Derrick njiani, tena akiwa amesimama na mtu yani hapo akili ikamcheza kuwa Derrick anataka kumliza mtu huyo, basi akasimamisha gari, akashuka na kumfata karibu halafu akamuita yani Derrick alishtuka kama mtu aliyeshtuliwa toka usingizini kiasi kwamba hata hakuweza kuongea tena na yule mtu ila Erick alimvuta mkono pembeni na kuongea nae,
“Derrick, hiki unachokifanya sio kabisa na kitakupeleka pabaya”
“Najua ushasikia vingi kuhusu mimi, hata wewe unaweza kuwa mmoja kati ya watu wanaonichukia”
“Sikuchukii kabisa, na nikuchukie kwasababu ipi? Naomba twende mahali tuongee kidogo”
Basi wakapanda kwenye gari, na kweli walishuka mahali na kupata sehemu nzuri na kukaa kisha kuanza mazungumzo ya hapa na pale,
“Kwanza kabisa Derrick ni kitu gani kikubwa kinakusumbua?”
“Sijui nikuelezeje upate kunielewa, ni hivi katika dunia mimi ni kiumbe nisiyekuwa na bahati kabisa”
“Huna bahati kivipi?”
“Kwanza kabisa, mimi nimeanza kukataliwa toka nipo tumboni mwa mama yangu, nimezaliwa sijapata mapenzi ya baba kabisa, nimepelekwa nyumbani kwa baba nasikia tukatimuliwa, toka hapo ndugu wa baba hawanipendi ni wachache tu wanaonaoniona kama mmoja wa familia yao. Nimekazana nitoke kimaisha, mama yangu kapata tabu ya kunisomesha na kweli nimefika chuo, nimehangaika kupata kazi, nikapata kazi ila hiyo kazi nimefukuzwa, hivi ni maisha gani nitakayoishi mimi? Kwanini dunia inanifanya hivi!! Ndiomana nikaamua nichague aina nyingine ya maisha kwani hata mimi natamani nimuhudumie mama yangu, nae aishi vizuri na ashukuru kunizaa”
“Unajua Derrick umekata tamaa mapema sana, yani elimu yako hupendezi kabisa kufanya kazi ya kitapeli, hivi kweli umetafuta kazi kote imeshindikana? Kuna siku hata umewahi kuja kwangu na kusema shemeji nisaidie angalau nipate kazi?”
“Hivi nakuja vipi kwako ikiwa mkeo ambaye nina undugu nae, hataki hata kuniona. Yani mimi sijui ni gundu sijui ni kitu gani. Katika maisha yangu ni kweli nilikuwa muhuni sana ila hakuna kitu ambacho sikupenda kama kutoa mimba, ila kuna mwanamke aliivuruga akili yangu kwa kutoa mimba yangu, huyu alikuwa ni mwanamke wa kwanza kumpa mimba na alikuwa wa kwanza kuitoa mimba yangu, kiukweli aliivuruga sana akili yangu, toka hapo huwa nahisi akili ikiwehuka tu. Kuna mwanamke nimezaa nae, na siku zote najua mtoto ni wangu kumbe mtoto mwenyewe katupa mababa wawili, yani wanawake jamani dah!! Ameona sieleweki ndio anasema yule mtoto sio wako, nimeumia sana, ila najua yule ni mwanangu ila tu sababu wanawake wanaangalia sehemu yenye maslahi zaidi”
“Kwahiyo huyo mtoto yuko wapi?”
“Najua basi, yule mwanamke alihama na watoto wake, roho iliniuma sana kila siku naenda kumlilia mwanangu, nilimpa jina la mama yangu ila yeye kampa jina lake analolijua mwenyewe. Yote hii sababu sijapata maslahi tu”
“Toka uanze kutapeli hujapata maslahi tu!!”
“Sijui ni kitu gani, sijui ni laana sijui ni nini. Yani mimi huwa natapeli hela za maana ila hakuna kitu cha maana ninachofanya”
“Unapotea ndugu yangu, yani unapotea kabisa. Kiukweli Erica kanibadilisha mimi ila ilikuwa rahisi sababu na mimi niliona ile njia niliyokuwa napita haikuwa njia sahihi kwa mimi kuendelea nayo, unajua kuna vitu vingine badala vikuendeleze vinakutia umasikini tu, unapata pesa ya laana kwa uongo ila pesa hiyo hiyo unayopata unaenda kumalizia kwa wanawake, haya hayo maendeleo utayatoa wapi?”
“Ni kweli kabisa, ila hii laana imeletwa na yule mwanamke aliyetoa mimba yangu”
“Basi achana na hayo, kama upo tayari naomba kesho niache mambo yangu nikupeleke kwenye maombia. Upo tayari?”
“Mmmmh!!”
“Nini sasa Derrick?”
“Utanipeleka kwenye maombi, utanipa na kazi? Maana hata niombewe na wachungaji wote duniani, na mshekhe nao waungane wote, ila kama sina kazi mwendo utakuwa ni huu huu wa kutapeli tu”
“Dah!! Yani wewe jamani!! Nitakupatia na kazi, ila sasa huwezi kufanya kazi vizuri kama hujaamua kuacha kabisa haya unayoyafanya”
Basi wakakubaliana pale kuwa wataonana kesho yake ili kuweza kuzungumza na kwenda huko kwenye maombi.