Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #381
SEHEMU YA 333
Kwakweli siku hii mama Angel alichoka sana, hakushinda na mwanae, alishinda kwenye biashara tu, basi alienda kuoga na kula chakula, kisha muda huo Erick alienda kuongea na mama yao,
“Mama, ulienda kiwandani leo?”
“Ndio nilienda mwanangu, nimechokaje jamani maana nilikuwa nafanya mahesabu na yule Yuda”
“Uligundua upotevu wa laki mbili?”
“Kheee kumbe na wewe ulijua? Mbona hukusema sasa?”
“Sikusema ndio ila niligundua muda tu, tatizo wale huwa wananiona mimi mtoto sana ndiomana sikuwauliza”
“Ila mwanangu unatakiwa ujiamini maana ile ni mali ya baba yenu, mkishindwa kuisimamia ni nani ambaye angeisimamia?”
“Ndiomaana zile laki tatu niliamua kuondoka nazo mama”
“Nimekuelewa mwanangu, ila unatakiwa kutetea mali ya baba yako kwa nguvu zako zote, watapoteza laki mbili, kesho milioni, kesho kutwa mtaji mzima na kiwanda kitafungwa, inatakiwa kuwa makini sana”
“Sawa mama”
Basi mama Angel alifurahi kwa kuona kuwa mwanae ana akili sana, muda huu aliinuka na kwenda chumbani huko aliamua kumpigia simu Tumaini ili kumpa taarifa kuhusu kuumwa kwa Derrick,
“Jamani, nini kimempata tena?”
“Nasikia kapigwa sana, kuna watu kakutana nao wamempiga sana”
“Au aliwafanyia kama alivyonifanyia mimi?”
“Mmmh sijui ila kapigwa sana na kwasasa yupo hoi hospitali”
“Dah! Itabidi kesho nijitahidi niende kumuona”
“Hata mimi kesho nitaenda tena, ila ndio hivyo Derrick hana hali nzuri kabisa”
Tumaini alishukuru kwa taarifa, na kwa muda huo mama Angel aliamua tu kulala kwani alikuwa amechoka kwa kiasi Fulani.
Kulipokucha tu, mama Angel alipokea simu kutoka kwa dada yake Mage,
“Ila Erica una tabia mbaya wewe, jana jioni umeahidi kwenda kumuona mgonjwa ila hujaenda”
“Ni majukumu dada yalinibana”
“Basi jitahidi leo, na jitahidi umuandalie mgonjwa chakula atakachokula usiku, muandalie tu mtori au chakula chochote kilaini”
“Sawa dada nimekuelewa”
Mama Angel alikata ile simu, ila kiukweli leo alikuwa amechoka na alitaka kutumia muda kidogo kuwa na mtoto wake kwahiyo aliona ni vyema asienda kiwandani kwa siku hii, anajua tu kule sababu hawajui lazima wajishughulishe kwani watahisi muda wowote ule ataenda.
Basi akaona ni vyema kwenda kutafuta vya kupika kwaajili ya kumpelekea mgonjwa jioni hospitali.
Kwenye mida ya saa tatu asubuhi, mama Angel aliondoka nyumbani kwake na kwenda sokoni, alipomaliza tu kununua mahitaji yake akakutana na Sia,
“Kheee kumbe na wewe huwa unakuja sokoni!”
“Jamani, kwani mimi nina nini cha kufanya nisije sokoni?”
“Aaah nimekuuliza tu, vipi mume amesharudi?”
“Bado”
“Huna wasiwasi? Unaibiwa huko, shauri yako nakwambia, wanaume wenyewe hata hawaaminiki hawa haswaa kwa mwanaume kama Erick unamuamini vipi? Yani kama hujaletewa binti mwenye mimba nyumbani kwako sijui”
“Nitolee balaa mie”
Mama Angel aliondoka zake na moja kwa moja kuelekea nyumbani kwake.
Muda huu Tumaini alikuwa anatoka nyumbani kwake, ila alifika mgeni pale nyumbani na mgeni huyo alikuwa ni mama Sarah,
“Kheee mama Sarah, karibu ila mimi nilikuwa natoka”
“Jamani, nilikuwa nina maongezi na wewe. Unaenda wapi kwani?”
“Mmmh kuna kijana nilisoma nae, sasa nasikia kapigwa sana na amelazwa hospitali, ndio naenda kumuona, yani nasikia yupo kwenye hali mbaya sana”
“Kheee, basi twende wote”
“Hakuna tatizo”
Basi Tumaini aliondoka na mama Sarah na moja kwa moja walienda hospitali huko, kisha walienda kwenye wodi aliyolazwa Derrick, hadi pale kitandani ilikuwa ni wodi ya mgonjwa mmoja mmoja, kwahiyo kwa muda huo alikuwepo Derrick na mama yake ambaye naye alifika kumuona mwanae, basi wakafika na kumpa pole ila mama Sarah alishtuka kidogo na kuuliza,
“Jamani huyu sio Derrick huyu!!”
“Ndio mwenyewe, kumbe unamfahamu?”
Mara mama Angel nae alifika pale kumuona mgonjwa, ila mama Sarah alishtuka na kumuangalia mama Angel kisha akamuuliza,
“Erica!! Inamaana unamfahamu huyu Derrick?”
“Ndio, ni kaka yangu wa damu”
Mara mama Angel nae alifika pale kumuona mgonjwa, ila mama Sarah alishtuka na kumuangalia mama Angel kisha akamuuliza,
“Erica!! Inamaana unamfahamu huyu Derrick?”
“Ndio, ni kaka yangu wa damu”
Mara mama Sarah akaonekana kama mtu aliye na kizunguzungu na kutaka kama kuanguka ni Tumaini ndio alimdaka kwa haraka.
Wote walimshangaa kuwa ana matatizo gani, mama Angel alimshika mkono na kutoka naye nje akamuuliza,
“Tatizo nini Manka?”
Mama Sarah alipumua kisha akasema,
“Acha tu kama ilivyo, utamwambia mama Leah nimeondoka. Kwaheri”
Kisha mama Sarah aliondoka zake, kwakweli mama Angel alimshangaa sana na kurudi wodini ambapo Tumaini alimuuliza vizuri,
“Kwani imekuwaje?”
“hata sijui, kaniaga tu na kuondoka”
Mama Derrick akasema kuwa,
“Au na yeye katapeliwa na mwanangu jamani, yani huyu Derrick dah!!”
“Usiwaze hayo mama, kwasasa tusifikirie utapeli wa Derrick ila tufikirie namna ya kupona kwa Derrick.”
Waliongea kidogo pale kisha waliaga ambapo walipotoka nje, Tumaini alimuuliza mama Angel,
“Inamaana Derrick ni tapeli!! Inamaana siku ile alinitapeli eeeh! Ndiomana nilihisi hivyo”
“Ni kweli ni tapeli ila nadhani anatumia dawa maana sio hali ya kawaida, utashangaa anakuazima tu hela ndogo na ukimpatia utakuta amekomba hela zote za kwenye mkoba wako”
“Aaaah kumbe, halafu kitu kingine hebu tuongee kikubwa, yule shoga yule yani mama Sarah nakumbuka aliwahi kuniambia kuwa anafahamiana na wewe, sema namba yake ndio akaichukua Derrick. Ila leo nimeshangaa sijui mlishaonana? Halafu kuna nini kinaendelea kati yake na Derrick?”
“Mmmh hata sijui”
“Hajakwambia chochote kwani ulivyotoka nae nje?”
“Si nilikwambia pale, hakuna alichoniambia zaidi ya kuniaga tu”
“Oooh nilijua unanificha sababu ya mama yake Derrick pale, au Derrick ndio baba mzazi wa Sarah?”
“Mmmh! Kwani unamfahamu vizuri yule mwanamke?”
“Namfahamu kiasi tu sio kivile, ila huwa haongei habari za kuwa na mume wala baba yake Sarah, ndiomana nimehisi hivi, labda hakutegemea kukutana nae, hebu fatilia usikute Sarah ni shangazi yako!!”
Halafu Tumaini akaagana na mama Angel ambapo muda huu mama Angel moja kwa moja aliondoka na kurudi nyumbani kwake, na yeye alikuwa akijiuliza tu bila ya kupata jibu.
Mama Angel aliwakuta wanae muda huu wanakula, basi na yeye alienda kujimwagia na kujumuika nao, kisha akawaambia hali ya mgonjwa,
“Jamani wanangu sikuwaambia ni hivi, mjomba wenu Derrick kalazwa, hospitali kumbe siku ile tulipomuona akapatwa majanga pale, nasikia walimpiga sana. Nimetoka kumuona leo hospitali anaendelea vizuri”
“Oooh masikini jamani, ndiomana nilikuwa nasema tukamsaidie ila wewe mama na Erick mlikataa na kusema kuwa tusimsaidie atatutapeli, niliona yale mazingira sio rafiki kwake. Ila bora anaendelea vizuri, Mungu amsaidie apone”
“Mmmh leo Erica naona una huruma sana”
“Ndio mama, yule ni mjomba wetu, lazima niwe na huruma naye”
Muda huu Erick hakuongea jambo lolote lile, walimaliza kula na kila mmoja alienda chumbani kwake, ila Erica moja kwa moja alienda chumbani kwa Erick na kuanza kuongea nae,
“Mbona hujasema chochote kuhusu mjomba kulazwa”
“Sasa ulitaka niseme nini jamani!”
“Hata utoe pole kwa mama , kwani yule ni kaka yake mama”
“Ila katutapeli laki tatu”
“Kumbuka kuna watu kawatapeli hela nyingi kuliko hizo, ila kapatwa na matatizo unatakiwa kuwa na huruma naye”
“Mimi sina huruma naye labda mpaka atakapoacha utapeli wake”
“Mmmh wewe nawe, halafu ngoja nikuulize, hivi siku ile alivyokuja Sarah na mama yake ulimuelewa mama yake Sarah na mama?”
“Sikuwaelewa ila inaonyesha kuwa ni watu wanaofahamiana ndiomana mama anasema kuwa Sarah ni ndugu yetu”
“Ila habari ya Sarah kuwa ndugu yetu nimeipenda sana”
“Kwanini?”
“Sababu ataacha kukusumbua wewe, toka lini ndugu wakawa wapenzi? Hakuna mila za kihivyo, mimi sitaki Sarah awe mpenzi wako, kwahiyo kama ni ndugu yetu ni afadhali sana yani”
Erick alikaa kimya tu, kisha Erica alimuuliza,
“Kwani hujapenda kwa Sarah kuwa ndugu yetu?”
“Vyote kwangu sawa tu, awe ni ndugu yetu, au asiwe ndugu yetu ila bado mimi siwezi kuwa na mahusiano naye”
“Kwahiyo utakuwa na mahusiano na nani? Au utamkubali Samia?”
“Hakuna, kwani umesahau kiapo chetu Erica hadi unaniuliza maswali kama hayo? Leo nimechoka halafu nina usingizi sana, muda sio mrefu nalala”
Erica ilibidi amuage kaka yake na kuondoka zake kuelekea chumbani kwake kulala.
Mama Angel alijikuta akiwaza kuhusu mama Sarah, alijiuliza maswali mengi sana bila ya majibu,
“Kwanini ashtuke vile na kutaka kuzimia? Je Derrick ni nani katika maisha yake au alikuwa na mahusiano na Derrick? Je Sarah ni mtoto wa nani? Wa mzee Jimmy, wa Erick au Derrick? Ila hawezi kuwa wa Erick bhana, hilo nakataa maana angeniambia mapema tu. Ila ni wa nani? Au ndio mtoto ambaye Derrick huwa anamsema? Sielewi jamani, kuna nini kati ya Manka na Derrick, au kipindi anampenda sana Erick akakutana na Derrick akamdanganya kama alivyonidanganya mimi? Mmmmh!!”
Mama Angel aliwaza sana bila hata ya jibu lolote na kuamua kulala, ila alishtuliwa na simu kutoka kwa mume wake na kuamua kupokea ile simu,
“Kumbe Derrick kalazwa? Ndio Tumaini kanipigia simu kuniambia leo, mke wangu umeshindwa kuniambia kweli?”
“Nisamehe mume wangu jamani, sijui hata nimeghafilika vipi ila ndio hivyo kalazwa”
“Una mawazo gani Erica? Sio hali ya kawaida, kwanza jana kutwa nzima hatujawasiliana na leo nisingekutafuta basi inamaana ingepita bila ya sisi kuwasiliana, tatizo ni nini mke wangu?”
“Hakuna tatizo”
“Nimekwambia kuwa habari za wakina Manka, sijui wakina nani zisikupe presha mke wangu, yote nikirudi tutazungumza kwakina, nakuomba usiwe na mawazo kwasababu hiyo”
“Sina mawazo yoyote hata usijali kuhusu mimi mume wangu”
Basi wakaongea mengi kwa usiku ule, kisha kuagana na mama Angel kuamua kulala sasa kwa uzuri zaidi.
Leo Erick alivyoenda shuleni tu alifatwa na Sarah ambaye alianza kuongea nae,
“Erick, mbona unaonekana kunikwepa sana?”
“Sikukwepi, ila Sarah hivi unajua kama sisi ni ndugu?”
“Hilo nishalikataa kabisa, siwezi kuwa na undugu na wewe Erick, ninachojua ni kimoja tu kuwa nakupenda sana”
“Duh!”
Muda wa kipindi ulianza kwahiyo ikabidi Sarah aende darasani, kwahiyo Erick alibaki huku akishangaa tu maana hakumuelewa Sarah kwakweli.
Basi waliendelea na masomo kama kawaida, ila siku hiyo mchana Erick alifatwa darasani kuwa anaitwa halafu alitoka na moja kwa moja kwenda ofisini kwa walimu na kukuta ni Sia yuko pale ambapo Sia aliwaomba walimu nafasi kidogo aweze kuzungumza na Erick maana alijitambulisha yeye kama mama mdogo wa Erick, kwanza kabisa Erick aliulizwa,
“Je unamfahamu huyu? Ni mamako mdogo?”
Erick aliitikia tu maana angekataa basi siku hii angemfanya Sia aumbuke sana, basi akatoka nae nje na kwenda kuzungumza nae,
“Kwanza kabisa asante Erick, nilijua utanikana”
“Hapana, nazijua akili zako ndiomana nimekubali, ushindwi kuangua kilio ofisini”
Leo Sia alicheka kiasi na kumwambia Erick,
“Kilichonileta hapa ni kitu kimoja, nimeona bora nije shule nikwambie hili, ni hivi nasikia kuna mwanaume anaitwa Juma anapenda sana kukufatilia. Tafadhari Erick kaa mbali na mtu huyu maana si mtu mzuri kwako”
“Kivipi?”
“Ipo siku nitakaa na wewe na kuongea nawe vizuri zaidi ila yule mtu si mtu mzuri kwako”
“Kwahiyo kwasasa hujaja na hoja kusema kuwa wewe ni mama yangu?”
“Siku zote uongo hujitenga na ukweli, na kitu kama ni ukweli basis i kulazimisha maana kuna kipindi kitajidhihirisha chenyewe. Kuna upendo ambao watu wanaita ni upendo wa asili, je huna upendo huo juu yangu? Kama unao basi mimi ni mama yako, ila kama huna huo upendo juu yangu basi mimi si mama yako, ila hata kama mimi si mama yako bado ninajukumu la kukulinda na kukutunza, nakuomba uwe mbali kabisa na Juma. Sikujua mapema kuwa anakufatilia ila sasa imejua”
“Umejuaje?”
“Yule Juma ana mke wake, na yule mke wake ni rafiki yangu mkubwa na ni rafiki wa mama yako pia. Nimejikuta nikimpenda na kuongea nae mambo mengi sana, kwahiyo kuwa makini sana na Juma, jiepushe nae na ikiwezekana ukimuona mkimbie kabisa. Yangu ni hayo tu, sina mengine wala sina la ziada, kwaheri”
Sia alienda ofisini na kuwashukuru walimu kwa kumruhusu kuongea na Erick halafu aliondoka zake, kwakweli Erick alikuwa akishangaa tu kwanza alishangaa jinsi huyu Sia alivyoongea kiustaarabu siku ya leo, basi alikuwa akienda darasani huku akisema,
“Ingawa kaongea na mimi kiustaarabu ila hiki kimama sikipendi jamani, yani sikipendi kabisa”
Akaenda zake darasani na kuendelea na masomo yake kama kawaida.
Mama Angel akiwa kiwandani leo, bado alitaka maelezo ya ile laki mbili, basi Yuda aliileta ile laki mbili na kumkabidhi huku akisema kuwa yule mtu amemlipa, haikuwa kweli ila Yuda alikopa ile hela mahali ili aweze kumlipa huyu mama na kuepuka lawama,
“Oooh kumbe wameleta, basin i vizuri kumbe ni waaminifu”
“Halafu Erick mtoto atakuja lini tena kiwandani?”
“Atakuja tu ila mwanangu nimeona bora akazanie masomo kwanza kwani ndio ya muhimu kuliko vitu vyote”
“Unaonekana unapenda shule eeeh!”
“Ndio napenda sana, napenda watoto wangu wawe wasomi wa kimataifa”
Waliendelea kufanya kazi huku mama Angel akipita kukagua kagua eneo lake, muda kidogo wakati anajiandaa kutoka, mule ofisini alifika mgeni na mgeni huyo alikuwa ni Juma kwani alijua kuwa siku hiyo angemkuta humo ofisini, ila alimkuta mama Angel, ikabidi tu akae na kuanza kuzungumza nae,
“Halafu sikutegemea kama ningekukuta wewe”
“Ndio umenikuta sasa, karibu”
“Asante, ila si una mtoto mdogo wewe huoni kama ukija huku unamkosesha mtoto haki yake?”
“Yani uzuri ni kuwa mtoto wangu amezoea kila kitu, kwahiyo anakunywa maziwa analala, na sio msumbufu hadi wakati narudi”
“Hata kama ila mtoto anahitaji jasho la mama kwa ukaribu sana”
“Aaaah hayo mambo ilikuwa zamani, ila kwasasa wanawake tumeamka”
“Sawa, sikupingi. Yuko wapi Erick?”
“Yupo shule, unadhani atakuwa wapi?”
“Yani alikopigwa hadi akazimia bado umemrudisha tena! Nina mashaka na wewe, ni mzazi wa aina gani usiye na huruma na mtoto wako?”
“Sikuelewi”
“Hivi umeshindwa kufikiria kweli, ni bora hata ungemuahamisha shule, kuliko kumrudisha shule hiyo hiyo. Hata hivyo hiki sio kilichonileta”
“Haya sema kilichokuleta”
“Ni hivi, nilipanga na Erick kuwa Jumamosi ningekuja kumchukua ili twende mahali ila nilishindwa, basi namuomba Jumamosi hii, tena ni vizuri nimekukuta na wewe mama yake, naomba ruhusa kwako”
“Haiwezekani, siwezi kumrudusu mwanangu kwenda sehemu nisiyoijua”
“Kumbe tatizo ni wewe kutokupajua tu!! Basi naomba twende wote siku hiyo, tafadhari nakuomba. Natumaini utatendea kazi ombi langu, kwaheri”
Juma aliinuka na kuondoka yani hakutaka hata kusikia jibu la mama Angel kama kakubali au kakataa ila yeye alihakikisha tu kuwa ameshamwambia na kama anataka na yeye aongozane nao.
Mama Angel alirudi nyumbani kwake muda huu akiwa amejichokea kiasi Fulani, baada ya kuoga na kula alienda kuongea na Erick kuhusu Juma,
“Nakuomba mwanangu jambo moja, najua nilikwambia ila narudia tena naomba mwanangu usiwe karibu na Juma, hata akufate wapi mkwepe, naona sio mtu mzuri kweko”
“Halafu leo mama, alikuja yule mwanamke nisiyempendaga shuleni”
“Nani huyo? Sia?”
“Ndio huyo huyo”
Mama Angel akachukia hapo na kuuliza kwa makini kuwa ni kitu gani Sia alimwambia mtoto wake, ila Erick alimwambia vile ambavyo alizungumza na Sia mpaka mama Angel alishangaa na kusema,
“Yani Sia ndio kaja kukwambia hayo maneno! Huo urafiki wa Sia na mke wa Juma umeanza lini hadi waambiane kila kitu jamani! Mmmmh unajua mtu unaweza kuzungukwa hapa hapa bila hata kujijua wala kutambua kuwa ni kitu gani kinachokusumbua kumbe ni mtu wako wa karibu. Haya mwanangu hata kama huwa unamchukia ila hilo alilokwambia ni bora zaidi, tafadhali kaa mbali na Juma”
Kisha akamuaga mwanae na moja kwa moja kwenda chumbani kwake, na huko alimpigia simu mumewe na kumwambia tu habari za Juma, ila hakumwambia kuwa alienda kiwandani kwani hakutaka mumewe ajue kuwa huwa anaenda kiwandani,
Huyu Juma ana wazimu eeeh! Kwahiyo alikuja tena hapo nyumbani?”
“Ndio alikuja”
“Sijui kaingiliwa na nini jamani na huyo Juma, anaacha kufatilia watoto wake anakazana kufatilia watoto wa wenzake”
“Tuachane na hayo, jamani mume wangu unarudi lini? Nimekukumbuka sana ujue”
“Nitarudi tu mke wangu usijali ila siku ya kurudi sitakwambia maana nataka nikushtukize tu”
“Ushaniambia tayari maana mshtukizo hata mtu haambiwi kabisa, huwa inatokea tu”
Baba Angel akacheka, na kuongea zaidi kidogo na mke wake kisha waliagana na kulala huku mama Angel anawaza kukikucha tu aende kwanza kiwandani maana alitakuwa kwasasa anataka kujua kila kitu.
Basi kulivyokucha, alijiandaa kwaajili ya kutoka ila muda ule ule alifika mama Junior, na kumfanya mama Angel ashangae maana ni asubuhi sana, basi alienda kukaa nae kwenye sebule yao nyingine na kuongea nae maana pale ndio kwanza Vaileth alikuwa akifanya usafi,
“Kheee dada mbona asubuhi asubuhi?”
“kwani na wewe hii asubuhi yote unaenda wapi?”
“Naenda kazini dada”
“Kivipi? Hebu nieleweshe vizuri”
Mama Angel alimwambia kuwa huwa anaenda kiwandani kuangalia jinsi kiwanda kinavyofanya kazi, na kufatilia wafanyakazi wa pale, na hata alimuelezea toka kaanza kufatilia ni makosa mangapi kayagundua,
“Ni vizuri sana sio vibaya ila huwa unaondoka muda gani na kurudi muda gani?”
“Asubuhi halafu narudi jioni”
“Aaaah Erica hebu wacha ujinga, una mtoto mdogo wewe ujue!! Sikia, unachofanya sio kibaya ila panga muda wako vizuri uwe unawahi kurudi kumnyonyesha mtoto na kukaa nae karibu, jamani unafanya kama wale wanawake ambao hawana waume kwahiyo wanapambana wenyewe ili watoto wale, ndio huwa wanafanya kazi muda wote hata muda wa kulea watoto haupo, unadhani Erick akisikia hili atafurahi? Hawezi kufurahi hata kidogo, amehangaika, ameteseka ili mke wake na watoto mtulie, amehitaji mtoto ili utulie nyumbani kulea mtoto ila wewe ndio kama biashara umeanza leo jamani Erica eeeh! Usiwe hivyo jamani mdogo wangu”
“Haya nimekuelewa, asubuhi yote hii ya nini?”
“Jana bhana, kuna binti kaja kunililia usiku mwenzangu ana mimba ya Junior”
Mama Angel alishtuka sana na kumuangalia dada yake,
“Kheee sasa umeamua nini?”
“Niamue nini zaidi ya kumshauri akatoe”
“Hapana dada usifanye hivyo, unajua kutoa mimba ni sawa na dhambi ya kuua tu. Muache azae mtoto wake”
“Unakumbuka kipindi chako nini?”
“Nakumbuka ndio, muacheni azae, wala hata usimtoe hiyo mimba. Kwanza wewe mwenyewe una kitoto kimoja tu halafu ndio uanze kutoa mimba za wakwe zako kweli? Muache azae tu”
“Haya, ila kuna mengine”
“Yapi hayo?”
“Kuhusu shemeji yako jamani, si kuna kimwanamke alikipata huko sijui wapi ndio kikawa kinamsumbua akili, hadi nilikuja siku ile ili nikueleze dukuduku langu, ila sasa akili ikacheza, siku hiyo kachelewa kurudi nikamuanzishia kilio kama cha msiba, yani nilikumbuka msiba wa baba kabisa, kwani amerudia tena kuwasiliana na yule mwanamke mbele yangu! Kwani kachelewa tena kurudi!!”
“Mmmh dada, kwa kilio tu au kuna mengine ulimfanyia?”
“Ukiona mumeo anakusumbua niambie nikueleze, ila ndio hivyo Deo saibvi katulia ila sitaki tena kukaa nyumbani, nataka kuanza kazi kwakweli nimechoka kukaa nyumbani, kwahiyo natafuta kazi”
“Hilo la kutafuta kazi ni wazo zuri dada, tena kuna rafiki yake baba Angel nitakuunganisha nae, hukusema tu mapema ila kwasasa usijali mambo ni moto. Ila bado hujaniambia mbona umekuja asubuhi sana?”
“Nilijua sitokukuta, maana mara nyingi tu napoiga simu naambiwa kuwa umeondoka”
“Huwa unapiga ya mezani wewe, ila hata hivyo Derrick kalazwa, sijui umepata habari au dada Mage alisahau kukwambia?”
Mama Junior alishangaa kidogo, na kusema kuwa siku hiyo itabidi waende wote kumuona Derrick maana hata wafanyeje bado ni ndugu yao tu.
Tumaini akiwa anaelekea katika shughuli zake, akakutana njiani na Dora na kuanza kuongea nae na kumpa taarifa kuhusu kulazwa kwa Derrick,
“Jamani masikini, kafanyaje tena?”
“Kumbe hujui? Derrick alikuwa ni tapeli ila dada yake yani Erica alikuwa akimfichia siri”
“Ila unajua kuna kitu huwa sielewi”
“Kitu gani?”
“Ni kuhusu Derrick na Erica, kwahiyo wale ni ndugu kabisa?”
“Ndio ndugu, baba mmoja wale”
“Unajua nini?”
“Nini?”
“Kipindi tupo chuo, kuna kipindi Fulani Erica alikuwa anatembea na Derrick, si unajua Erica alikuwa ni rafiki yangu sana ila tukaja kugombana badae kwa mambo madogo tu, basi Erica alikuwa anatembea na Derrick”
“Mmmh kwahiyo alikuwa ni mpenzi wake kabisa?”
“Ndio, alikuwa nae sasa nashangaa kusikia kuwa ni ndugu”
“Ila Erica anaonekana kuwa mpole sana, sidhani kama alitembea nae”
“Weeee ana upole gani yule! Niulize mimi listi ya wanaume aliotembea nao, ninaowajua tu ni wengi hatari, kuna kijamaa kilikuwa kinaitwa Babuu katembea nacho, kilikuwa kimasikini hatari ila Erica ndio alikufa alioza, mwenzio Erica katembea na George na aliachwa na George sababu hakuwa bikra”
“Mmmh unajua George na Erick ni ndugu kwa upande wa mama yake Erick huko!”
“Kheee basi hekaheka za Erica sio za nchi hii, kuna kipindi alijikuta kagonganisha ndugu watatu yule na wote katembea nao, huyo Derrick unayesema ni ndugu yake katembea nae, halafu kuna jamaa nadhani unamjua siku ya harusi ya Erick na Erica aliongea maneno mengi kiasi, yule jamaa anaitwa Bahati, kwasasa anaishi na Fetty basi yule Erica katembea nae, usimuone vile huwa kuna mambo namtetea tu. Ni kweli ni mpole ila kwenye swala la uhuni na yeye alikuwa muhuni”
“Kumbe!! Ndiomana alipatana na wewe, nikamshangaa msichana mpole vile kuwa na urafiki na wewe! Bora hata Fetty kidogo hakuwa na makuu chuoni ila wewe mmmh nilishangaa sana”
“Siku zote mwizi anatembea na mwizi mwenzie, ila kwasasa nimeokoka hayo mambo nimeacha jamani hata umbea huu sikutakiwa kukwambia, eeeh Mungu nisamehe”
Tumaini alicheka sana na kumuuliza,
“Ila hiyo listi ya wanaume wa Erica uliijuaje?”
“Mmmh unajua mimi nina dhambi nyingi jamani, namshukuru Mungu ni mwaminifu na anasamehe, la sivyo mimi nisengesamehewa jamani. Unajua nilikuwa namuonea sana huruma Erica akilia kuhusu mapenzi halafu hivi vidume vikijidai vyenyewe kwa kuumiza moyo wa Erica, yani siku niliyogundua nimeatirika basi nilimfata mmoja baada ya mwingine na kutembea nae, yani kila aliyemuumiza Erica nami nilihakikisha namuumiza na ukimwi”
“Ndiomana ukaamua kumuambukiza na baba yangu! Mwanamke mbaya wewe hata hufai”
“Mmmh tuachane na habari hizo Tumaini ila baba yako ndio aliniambukiza mimi. Nisamehe kwa hilo”
“Mbaya wewe na sidhani kama dhambi zote umesamehewa, hata huo ulokole wako nina mashaka nao. Kajinga kweli wewe”
Dora akaona yataanza marumbano pale bure, kwahiyo akaamua kuagana na Tumaini tu ila aliahidi kuwa ataenda kumsalimia Derrick pia.
Baada ya Dora kuondoka, kwakweli Tumaini alijiuliza sana,
“Kumbe watu wanatoka mbali eeeh! Ndiomana Erica alipata yule mtoto wa kiarabu kumbe na yeye alikuwa na mambo sana”
Basi akachukua simu yake na kumtumia mdogo wake ujumbe,
“Habari Erick, nasikia Erica kabla ya kukutana na wewe alishatembea na wanaume zaidi ya watano”
Muda kidogo akapokea ujumbe kwa Erick,
“Hata angetembea na dunia nzima bado ningempenda tu tena sana.”
Kisha akapiga simu ambapo Tumaini akapokea,
“Ila dada yangu kwani una matatizo gani? Ulisikia kuwa mwanamke akiwa ametembea na wanaume wengi haolewi wapi? Si ilimradi apate anayependana nae tu”
“Kheee yameisha basi, mimi nilikuwa nasema tu”
“Unajua kuna muda huwa sikuelewi, unampenda Erica ila unaniambia maneno kama haya, unataka niachane nae au ni kitu gani? Dada yangu nakuomba umuheshimu mke wangu, nampenda sana na unalijua hilo, mimi Erica nampenda hata niambiwe wale watoto wote sio wangu kazaa na wanaume wengine huko bado nitampenda na watoto nitawapenda yani usijisumbue kupata habari huko na kuniambia”
“Basi yameisha wala sitokwambia tena mambo kama haya”
“Halafu hizo tabia za umbea sijui umezitoa wapi? Utakuwa unaongea sana na Sia wewe ndiomana, naomba usiniletee tena umbea wa kuhusu mke wangu, nampenda jinsi alivyo na huwezi jua nimempendea nini”
“Nimekuelewa Erick, hata mimi nampenda Erica yani hata sijui naanzaje kukuletea umbea wa aina hii, naomba unisamehe”
“Kila siku na mke wangu tunajiuliza Erica mdogo katoa wapi umbea kumbe katoa kwako, naomba usiniambie tena habari za hivi, tuwe tunaongea mambo mengine tu”
“Nisamehe, nimekuelewa”
Tumaini alikata simu na kupumua kiasi kisha akasema,
“Kweli mapenzi ya kweli yapo, kuna muda hadi nahisi Erick karogwa jamani, si kwa kupenda huku mmmh! Ila hata mimi mume wangu ananipenda jamani, niache wivu loh!”
Akaendelea na safari yake ya kwenda kwenye shughuli zake.
Mama Angel alimuomba dada yake wapiti kwanza kiwandani halafu ndio waende hospitali maana hakutaka siku hiyo aipitishe bila kwenda kuangalia shughuli za kiwanda zimekwendaje.
Basi walienda hadi kiwandani, kwa mara ya kwanza mama Junior aliweza kuona kile kiwanda kilivyo,
“Jamani mdogo wangu, mmejitahidi sana”
“Asante”
Basi mama Junior alikuwa akitembelea tembelea maeneo baadhi ya kile kiwanda, kisha akatoka nje na kuanza kutembelea maeneo ya nje ya kile kiwanda, ila mara alipita mmama wa makamo
na kumsimamisha mama Junior kisha akamuuliza,
“Wewe si mama yake na Junior?”
“Ndio ni mimi”
Yule mama akamnasa kibao mama Junior, ila mama Junior nae huwa hapendi kuonewa kwahiyo alimnasa pia kibao yule mama.
Kwakweli siku hii mama Angel alichoka sana, hakushinda na mwanae, alishinda kwenye biashara tu, basi alienda kuoga na kula chakula, kisha muda huo Erick alienda kuongea na mama yao,
“Mama, ulienda kiwandani leo?”
“Ndio nilienda mwanangu, nimechokaje jamani maana nilikuwa nafanya mahesabu na yule Yuda”
“Uligundua upotevu wa laki mbili?”
“Kheee kumbe na wewe ulijua? Mbona hukusema sasa?”
“Sikusema ndio ila niligundua muda tu, tatizo wale huwa wananiona mimi mtoto sana ndiomana sikuwauliza”
“Ila mwanangu unatakiwa ujiamini maana ile ni mali ya baba yenu, mkishindwa kuisimamia ni nani ambaye angeisimamia?”
“Ndiomaana zile laki tatu niliamua kuondoka nazo mama”
“Nimekuelewa mwanangu, ila unatakiwa kutetea mali ya baba yako kwa nguvu zako zote, watapoteza laki mbili, kesho milioni, kesho kutwa mtaji mzima na kiwanda kitafungwa, inatakiwa kuwa makini sana”
“Sawa mama”
Basi mama Angel alifurahi kwa kuona kuwa mwanae ana akili sana, muda huu aliinuka na kwenda chumbani huko aliamua kumpigia simu Tumaini ili kumpa taarifa kuhusu kuumwa kwa Derrick,
“Jamani, nini kimempata tena?”
“Nasikia kapigwa sana, kuna watu kakutana nao wamempiga sana”
“Au aliwafanyia kama alivyonifanyia mimi?”
“Mmmh sijui ila kapigwa sana na kwasasa yupo hoi hospitali”
“Dah! Itabidi kesho nijitahidi niende kumuona”
“Hata mimi kesho nitaenda tena, ila ndio hivyo Derrick hana hali nzuri kabisa”
Tumaini alishukuru kwa taarifa, na kwa muda huo mama Angel aliamua tu kulala kwani alikuwa amechoka kwa kiasi Fulani.
Kulipokucha tu, mama Angel alipokea simu kutoka kwa dada yake Mage,
“Ila Erica una tabia mbaya wewe, jana jioni umeahidi kwenda kumuona mgonjwa ila hujaenda”
“Ni majukumu dada yalinibana”
“Basi jitahidi leo, na jitahidi umuandalie mgonjwa chakula atakachokula usiku, muandalie tu mtori au chakula chochote kilaini”
“Sawa dada nimekuelewa”
Mama Angel alikata ile simu, ila kiukweli leo alikuwa amechoka na alitaka kutumia muda kidogo kuwa na mtoto wake kwahiyo aliona ni vyema asienda kiwandani kwa siku hii, anajua tu kule sababu hawajui lazima wajishughulishe kwani watahisi muda wowote ule ataenda.
Basi akaona ni vyema kwenda kutafuta vya kupika kwaajili ya kumpelekea mgonjwa jioni hospitali.
Kwenye mida ya saa tatu asubuhi, mama Angel aliondoka nyumbani kwake na kwenda sokoni, alipomaliza tu kununua mahitaji yake akakutana na Sia,
“Kheee kumbe na wewe huwa unakuja sokoni!”
“Jamani, kwani mimi nina nini cha kufanya nisije sokoni?”
“Aaah nimekuuliza tu, vipi mume amesharudi?”
“Bado”
“Huna wasiwasi? Unaibiwa huko, shauri yako nakwambia, wanaume wenyewe hata hawaaminiki hawa haswaa kwa mwanaume kama Erick unamuamini vipi? Yani kama hujaletewa binti mwenye mimba nyumbani kwako sijui”
“Nitolee balaa mie”
Mama Angel aliondoka zake na moja kwa moja kuelekea nyumbani kwake.
Muda huu Tumaini alikuwa anatoka nyumbani kwake, ila alifika mgeni pale nyumbani na mgeni huyo alikuwa ni mama Sarah,
“Kheee mama Sarah, karibu ila mimi nilikuwa natoka”
“Jamani, nilikuwa nina maongezi na wewe. Unaenda wapi kwani?”
“Mmmh kuna kijana nilisoma nae, sasa nasikia kapigwa sana na amelazwa hospitali, ndio naenda kumuona, yani nasikia yupo kwenye hali mbaya sana”
“Kheee, basi twende wote”
“Hakuna tatizo”
Basi Tumaini aliondoka na mama Sarah na moja kwa moja walienda hospitali huko, kisha walienda kwenye wodi aliyolazwa Derrick, hadi pale kitandani ilikuwa ni wodi ya mgonjwa mmoja mmoja, kwahiyo kwa muda huo alikuwepo Derrick na mama yake ambaye naye alifika kumuona mwanae, basi wakafika na kumpa pole ila mama Sarah alishtuka kidogo na kuuliza,
“Jamani huyu sio Derrick huyu!!”
“Ndio mwenyewe, kumbe unamfahamu?”
Mara mama Angel nae alifika pale kumuona mgonjwa, ila mama Sarah alishtuka na kumuangalia mama Angel kisha akamuuliza,
“Erica!! Inamaana unamfahamu huyu Derrick?”
“Ndio, ni kaka yangu wa damu”
Mara mama Angel nae alifika pale kumuona mgonjwa, ila mama Sarah alishtuka na kumuangalia mama Angel kisha akamuuliza,
“Erica!! Inamaana unamfahamu huyu Derrick?”
“Ndio, ni kaka yangu wa damu”
Mara mama Sarah akaonekana kama mtu aliye na kizunguzungu na kutaka kama kuanguka ni Tumaini ndio alimdaka kwa haraka.
Wote walimshangaa kuwa ana matatizo gani, mama Angel alimshika mkono na kutoka naye nje akamuuliza,
“Tatizo nini Manka?”
Mama Sarah alipumua kisha akasema,
“Acha tu kama ilivyo, utamwambia mama Leah nimeondoka. Kwaheri”
Kisha mama Sarah aliondoka zake, kwakweli mama Angel alimshangaa sana na kurudi wodini ambapo Tumaini alimuuliza vizuri,
“Kwani imekuwaje?”
“hata sijui, kaniaga tu na kuondoka”
Mama Derrick akasema kuwa,
“Au na yeye katapeliwa na mwanangu jamani, yani huyu Derrick dah!!”
“Usiwaze hayo mama, kwasasa tusifikirie utapeli wa Derrick ila tufikirie namna ya kupona kwa Derrick.”
Waliongea kidogo pale kisha waliaga ambapo walipotoka nje, Tumaini alimuuliza mama Angel,
“Inamaana Derrick ni tapeli!! Inamaana siku ile alinitapeli eeeh! Ndiomana nilihisi hivyo”
“Ni kweli ni tapeli ila nadhani anatumia dawa maana sio hali ya kawaida, utashangaa anakuazima tu hela ndogo na ukimpatia utakuta amekomba hela zote za kwenye mkoba wako”
“Aaaah kumbe, halafu kitu kingine hebu tuongee kikubwa, yule shoga yule yani mama Sarah nakumbuka aliwahi kuniambia kuwa anafahamiana na wewe, sema namba yake ndio akaichukua Derrick. Ila leo nimeshangaa sijui mlishaonana? Halafu kuna nini kinaendelea kati yake na Derrick?”
“Mmmh hata sijui”
“Hajakwambia chochote kwani ulivyotoka nae nje?”
“Si nilikwambia pale, hakuna alichoniambia zaidi ya kuniaga tu”
“Oooh nilijua unanificha sababu ya mama yake Derrick pale, au Derrick ndio baba mzazi wa Sarah?”
“Mmmh! Kwani unamfahamu vizuri yule mwanamke?”
“Namfahamu kiasi tu sio kivile, ila huwa haongei habari za kuwa na mume wala baba yake Sarah, ndiomana nimehisi hivi, labda hakutegemea kukutana nae, hebu fatilia usikute Sarah ni shangazi yako!!”
Halafu Tumaini akaagana na mama Angel ambapo muda huu mama Angel moja kwa moja aliondoka na kurudi nyumbani kwake, na yeye alikuwa akijiuliza tu bila ya kupata jibu.
Mama Angel aliwakuta wanae muda huu wanakula, basi na yeye alienda kujimwagia na kujumuika nao, kisha akawaambia hali ya mgonjwa,
“Jamani wanangu sikuwaambia ni hivi, mjomba wenu Derrick kalazwa, hospitali kumbe siku ile tulipomuona akapatwa majanga pale, nasikia walimpiga sana. Nimetoka kumuona leo hospitali anaendelea vizuri”
“Oooh masikini jamani, ndiomana nilikuwa nasema tukamsaidie ila wewe mama na Erick mlikataa na kusema kuwa tusimsaidie atatutapeli, niliona yale mazingira sio rafiki kwake. Ila bora anaendelea vizuri, Mungu amsaidie apone”
“Mmmh leo Erica naona una huruma sana”
“Ndio mama, yule ni mjomba wetu, lazima niwe na huruma naye”
Muda huu Erick hakuongea jambo lolote lile, walimaliza kula na kila mmoja alienda chumbani kwake, ila Erica moja kwa moja alienda chumbani kwa Erick na kuanza kuongea nae,
“Mbona hujasema chochote kuhusu mjomba kulazwa”
“Sasa ulitaka niseme nini jamani!”
“Hata utoe pole kwa mama , kwani yule ni kaka yake mama”
“Ila katutapeli laki tatu”
“Kumbuka kuna watu kawatapeli hela nyingi kuliko hizo, ila kapatwa na matatizo unatakiwa kuwa na huruma naye”
“Mimi sina huruma naye labda mpaka atakapoacha utapeli wake”
“Mmmh wewe nawe, halafu ngoja nikuulize, hivi siku ile alivyokuja Sarah na mama yake ulimuelewa mama yake Sarah na mama?”
“Sikuwaelewa ila inaonyesha kuwa ni watu wanaofahamiana ndiomana mama anasema kuwa Sarah ni ndugu yetu”
“Ila habari ya Sarah kuwa ndugu yetu nimeipenda sana”
“Kwanini?”
“Sababu ataacha kukusumbua wewe, toka lini ndugu wakawa wapenzi? Hakuna mila za kihivyo, mimi sitaki Sarah awe mpenzi wako, kwahiyo kama ni ndugu yetu ni afadhali sana yani”
Erick alikaa kimya tu, kisha Erica alimuuliza,
“Kwani hujapenda kwa Sarah kuwa ndugu yetu?”
“Vyote kwangu sawa tu, awe ni ndugu yetu, au asiwe ndugu yetu ila bado mimi siwezi kuwa na mahusiano naye”
“Kwahiyo utakuwa na mahusiano na nani? Au utamkubali Samia?”
“Hakuna, kwani umesahau kiapo chetu Erica hadi unaniuliza maswali kama hayo? Leo nimechoka halafu nina usingizi sana, muda sio mrefu nalala”
Erica ilibidi amuage kaka yake na kuondoka zake kuelekea chumbani kwake kulala.
Mama Angel alijikuta akiwaza kuhusu mama Sarah, alijiuliza maswali mengi sana bila ya majibu,
“Kwanini ashtuke vile na kutaka kuzimia? Je Derrick ni nani katika maisha yake au alikuwa na mahusiano na Derrick? Je Sarah ni mtoto wa nani? Wa mzee Jimmy, wa Erick au Derrick? Ila hawezi kuwa wa Erick bhana, hilo nakataa maana angeniambia mapema tu. Ila ni wa nani? Au ndio mtoto ambaye Derrick huwa anamsema? Sielewi jamani, kuna nini kati ya Manka na Derrick, au kipindi anampenda sana Erick akakutana na Derrick akamdanganya kama alivyonidanganya mimi? Mmmmh!!”
Mama Angel aliwaza sana bila hata ya jibu lolote na kuamua kulala, ila alishtuliwa na simu kutoka kwa mume wake na kuamua kupokea ile simu,
“Kumbe Derrick kalazwa? Ndio Tumaini kanipigia simu kuniambia leo, mke wangu umeshindwa kuniambia kweli?”
“Nisamehe mume wangu jamani, sijui hata nimeghafilika vipi ila ndio hivyo kalazwa”
“Una mawazo gani Erica? Sio hali ya kawaida, kwanza jana kutwa nzima hatujawasiliana na leo nisingekutafuta basi inamaana ingepita bila ya sisi kuwasiliana, tatizo ni nini mke wangu?”
“Hakuna tatizo”
“Nimekwambia kuwa habari za wakina Manka, sijui wakina nani zisikupe presha mke wangu, yote nikirudi tutazungumza kwakina, nakuomba usiwe na mawazo kwasababu hiyo”
“Sina mawazo yoyote hata usijali kuhusu mimi mume wangu”
Basi wakaongea mengi kwa usiku ule, kisha kuagana na mama Angel kuamua kulala sasa kwa uzuri zaidi.
Leo Erick alivyoenda shuleni tu alifatwa na Sarah ambaye alianza kuongea nae,
“Erick, mbona unaonekana kunikwepa sana?”
“Sikukwepi, ila Sarah hivi unajua kama sisi ni ndugu?”
“Hilo nishalikataa kabisa, siwezi kuwa na undugu na wewe Erick, ninachojua ni kimoja tu kuwa nakupenda sana”
“Duh!”
Muda wa kipindi ulianza kwahiyo ikabidi Sarah aende darasani, kwahiyo Erick alibaki huku akishangaa tu maana hakumuelewa Sarah kwakweli.
Basi waliendelea na masomo kama kawaida, ila siku hiyo mchana Erick alifatwa darasani kuwa anaitwa halafu alitoka na moja kwa moja kwenda ofisini kwa walimu na kukuta ni Sia yuko pale ambapo Sia aliwaomba walimu nafasi kidogo aweze kuzungumza na Erick maana alijitambulisha yeye kama mama mdogo wa Erick, kwanza kabisa Erick aliulizwa,
“Je unamfahamu huyu? Ni mamako mdogo?”
Erick aliitikia tu maana angekataa basi siku hii angemfanya Sia aumbuke sana, basi akatoka nae nje na kwenda kuzungumza nae,
“Kwanza kabisa asante Erick, nilijua utanikana”
“Hapana, nazijua akili zako ndiomana nimekubali, ushindwi kuangua kilio ofisini”
Leo Sia alicheka kiasi na kumwambia Erick,
“Kilichonileta hapa ni kitu kimoja, nimeona bora nije shule nikwambie hili, ni hivi nasikia kuna mwanaume anaitwa Juma anapenda sana kukufatilia. Tafadhari Erick kaa mbali na mtu huyu maana si mtu mzuri kwako”
“Kivipi?”
“Ipo siku nitakaa na wewe na kuongea nawe vizuri zaidi ila yule mtu si mtu mzuri kwako”
“Kwahiyo kwasasa hujaja na hoja kusema kuwa wewe ni mama yangu?”
“Siku zote uongo hujitenga na ukweli, na kitu kama ni ukweli basis i kulazimisha maana kuna kipindi kitajidhihirisha chenyewe. Kuna upendo ambao watu wanaita ni upendo wa asili, je huna upendo huo juu yangu? Kama unao basi mimi ni mama yako, ila kama huna huo upendo juu yangu basi mimi si mama yako, ila hata kama mimi si mama yako bado ninajukumu la kukulinda na kukutunza, nakuomba uwe mbali kabisa na Juma. Sikujua mapema kuwa anakufatilia ila sasa imejua”
“Umejuaje?”
“Yule Juma ana mke wake, na yule mke wake ni rafiki yangu mkubwa na ni rafiki wa mama yako pia. Nimejikuta nikimpenda na kuongea nae mambo mengi sana, kwahiyo kuwa makini sana na Juma, jiepushe nae na ikiwezekana ukimuona mkimbie kabisa. Yangu ni hayo tu, sina mengine wala sina la ziada, kwaheri”
Sia alienda ofisini na kuwashukuru walimu kwa kumruhusu kuongea na Erick halafu aliondoka zake, kwakweli Erick alikuwa akishangaa tu kwanza alishangaa jinsi huyu Sia alivyoongea kiustaarabu siku ya leo, basi alikuwa akienda darasani huku akisema,
“Ingawa kaongea na mimi kiustaarabu ila hiki kimama sikipendi jamani, yani sikipendi kabisa”
Akaenda zake darasani na kuendelea na masomo yake kama kawaida.
Mama Angel akiwa kiwandani leo, bado alitaka maelezo ya ile laki mbili, basi Yuda aliileta ile laki mbili na kumkabidhi huku akisema kuwa yule mtu amemlipa, haikuwa kweli ila Yuda alikopa ile hela mahali ili aweze kumlipa huyu mama na kuepuka lawama,
“Oooh kumbe wameleta, basin i vizuri kumbe ni waaminifu”
“Halafu Erick mtoto atakuja lini tena kiwandani?”
“Atakuja tu ila mwanangu nimeona bora akazanie masomo kwanza kwani ndio ya muhimu kuliko vitu vyote”
“Unaonekana unapenda shule eeeh!”
“Ndio napenda sana, napenda watoto wangu wawe wasomi wa kimataifa”
Waliendelea kufanya kazi huku mama Angel akipita kukagua kagua eneo lake, muda kidogo wakati anajiandaa kutoka, mule ofisini alifika mgeni na mgeni huyo alikuwa ni Juma kwani alijua kuwa siku hiyo angemkuta humo ofisini, ila alimkuta mama Angel, ikabidi tu akae na kuanza kuzungumza nae,
“Halafu sikutegemea kama ningekukuta wewe”
“Ndio umenikuta sasa, karibu”
“Asante, ila si una mtoto mdogo wewe huoni kama ukija huku unamkosesha mtoto haki yake?”
“Yani uzuri ni kuwa mtoto wangu amezoea kila kitu, kwahiyo anakunywa maziwa analala, na sio msumbufu hadi wakati narudi”
“Hata kama ila mtoto anahitaji jasho la mama kwa ukaribu sana”
“Aaaah hayo mambo ilikuwa zamani, ila kwasasa wanawake tumeamka”
“Sawa, sikupingi. Yuko wapi Erick?”
“Yupo shule, unadhani atakuwa wapi?”
“Yani alikopigwa hadi akazimia bado umemrudisha tena! Nina mashaka na wewe, ni mzazi wa aina gani usiye na huruma na mtoto wako?”
“Sikuelewi”
“Hivi umeshindwa kufikiria kweli, ni bora hata ungemuahamisha shule, kuliko kumrudisha shule hiyo hiyo. Hata hivyo hiki sio kilichonileta”
“Haya sema kilichokuleta”
“Ni hivi, nilipanga na Erick kuwa Jumamosi ningekuja kumchukua ili twende mahali ila nilishindwa, basi namuomba Jumamosi hii, tena ni vizuri nimekukuta na wewe mama yake, naomba ruhusa kwako”
“Haiwezekani, siwezi kumrudusu mwanangu kwenda sehemu nisiyoijua”
“Kumbe tatizo ni wewe kutokupajua tu!! Basi naomba twende wote siku hiyo, tafadhari nakuomba. Natumaini utatendea kazi ombi langu, kwaheri”
Juma aliinuka na kuondoka yani hakutaka hata kusikia jibu la mama Angel kama kakubali au kakataa ila yeye alihakikisha tu kuwa ameshamwambia na kama anataka na yeye aongozane nao.
Mama Angel alirudi nyumbani kwake muda huu akiwa amejichokea kiasi Fulani, baada ya kuoga na kula alienda kuongea na Erick kuhusu Juma,
“Nakuomba mwanangu jambo moja, najua nilikwambia ila narudia tena naomba mwanangu usiwe karibu na Juma, hata akufate wapi mkwepe, naona sio mtu mzuri kweko”
“Halafu leo mama, alikuja yule mwanamke nisiyempendaga shuleni”
“Nani huyo? Sia?”
“Ndio huyo huyo”
Mama Angel akachukia hapo na kuuliza kwa makini kuwa ni kitu gani Sia alimwambia mtoto wake, ila Erick alimwambia vile ambavyo alizungumza na Sia mpaka mama Angel alishangaa na kusema,
“Yani Sia ndio kaja kukwambia hayo maneno! Huo urafiki wa Sia na mke wa Juma umeanza lini hadi waambiane kila kitu jamani! Mmmmh unajua mtu unaweza kuzungukwa hapa hapa bila hata kujijua wala kutambua kuwa ni kitu gani kinachokusumbua kumbe ni mtu wako wa karibu. Haya mwanangu hata kama huwa unamchukia ila hilo alilokwambia ni bora zaidi, tafadhali kaa mbali na Juma”
Kisha akamuaga mwanae na moja kwa moja kwenda chumbani kwake, na huko alimpigia simu mumewe na kumwambia tu habari za Juma, ila hakumwambia kuwa alienda kiwandani kwani hakutaka mumewe ajue kuwa huwa anaenda kiwandani,
Huyu Juma ana wazimu eeeh! Kwahiyo alikuja tena hapo nyumbani?”
“Ndio alikuja”
“Sijui kaingiliwa na nini jamani na huyo Juma, anaacha kufatilia watoto wake anakazana kufatilia watoto wa wenzake”
“Tuachane na hayo, jamani mume wangu unarudi lini? Nimekukumbuka sana ujue”
“Nitarudi tu mke wangu usijali ila siku ya kurudi sitakwambia maana nataka nikushtukize tu”
“Ushaniambia tayari maana mshtukizo hata mtu haambiwi kabisa, huwa inatokea tu”
Baba Angel akacheka, na kuongea zaidi kidogo na mke wake kisha waliagana na kulala huku mama Angel anawaza kukikucha tu aende kwanza kiwandani maana alitakuwa kwasasa anataka kujua kila kitu.
Basi kulivyokucha, alijiandaa kwaajili ya kutoka ila muda ule ule alifika mama Junior, na kumfanya mama Angel ashangae maana ni asubuhi sana, basi alienda kukaa nae kwenye sebule yao nyingine na kuongea nae maana pale ndio kwanza Vaileth alikuwa akifanya usafi,
“Kheee dada mbona asubuhi asubuhi?”
“kwani na wewe hii asubuhi yote unaenda wapi?”
“Naenda kazini dada”
“Kivipi? Hebu nieleweshe vizuri”
Mama Angel alimwambia kuwa huwa anaenda kiwandani kuangalia jinsi kiwanda kinavyofanya kazi, na kufatilia wafanyakazi wa pale, na hata alimuelezea toka kaanza kufatilia ni makosa mangapi kayagundua,
“Ni vizuri sana sio vibaya ila huwa unaondoka muda gani na kurudi muda gani?”
“Asubuhi halafu narudi jioni”
“Aaaah Erica hebu wacha ujinga, una mtoto mdogo wewe ujue!! Sikia, unachofanya sio kibaya ila panga muda wako vizuri uwe unawahi kurudi kumnyonyesha mtoto na kukaa nae karibu, jamani unafanya kama wale wanawake ambao hawana waume kwahiyo wanapambana wenyewe ili watoto wale, ndio huwa wanafanya kazi muda wote hata muda wa kulea watoto haupo, unadhani Erick akisikia hili atafurahi? Hawezi kufurahi hata kidogo, amehangaika, ameteseka ili mke wake na watoto mtulie, amehitaji mtoto ili utulie nyumbani kulea mtoto ila wewe ndio kama biashara umeanza leo jamani Erica eeeh! Usiwe hivyo jamani mdogo wangu”
“Haya nimekuelewa, asubuhi yote hii ya nini?”
“Jana bhana, kuna binti kaja kunililia usiku mwenzangu ana mimba ya Junior”
Mama Angel alishtuka sana na kumuangalia dada yake,
“Kheee sasa umeamua nini?”
“Niamue nini zaidi ya kumshauri akatoe”
“Hapana dada usifanye hivyo, unajua kutoa mimba ni sawa na dhambi ya kuua tu. Muache azae mtoto wake”
“Unakumbuka kipindi chako nini?”
“Nakumbuka ndio, muacheni azae, wala hata usimtoe hiyo mimba. Kwanza wewe mwenyewe una kitoto kimoja tu halafu ndio uanze kutoa mimba za wakwe zako kweli? Muache azae tu”
“Haya, ila kuna mengine”
“Yapi hayo?”
“Kuhusu shemeji yako jamani, si kuna kimwanamke alikipata huko sijui wapi ndio kikawa kinamsumbua akili, hadi nilikuja siku ile ili nikueleze dukuduku langu, ila sasa akili ikacheza, siku hiyo kachelewa kurudi nikamuanzishia kilio kama cha msiba, yani nilikumbuka msiba wa baba kabisa, kwani amerudia tena kuwasiliana na yule mwanamke mbele yangu! Kwani kachelewa tena kurudi!!”
“Mmmh dada, kwa kilio tu au kuna mengine ulimfanyia?”
“Ukiona mumeo anakusumbua niambie nikueleze, ila ndio hivyo Deo saibvi katulia ila sitaki tena kukaa nyumbani, nataka kuanza kazi kwakweli nimechoka kukaa nyumbani, kwahiyo natafuta kazi”
“Hilo la kutafuta kazi ni wazo zuri dada, tena kuna rafiki yake baba Angel nitakuunganisha nae, hukusema tu mapema ila kwasasa usijali mambo ni moto. Ila bado hujaniambia mbona umekuja asubuhi sana?”
“Nilijua sitokukuta, maana mara nyingi tu napoiga simu naambiwa kuwa umeondoka”
“Huwa unapiga ya mezani wewe, ila hata hivyo Derrick kalazwa, sijui umepata habari au dada Mage alisahau kukwambia?”
Mama Junior alishangaa kidogo, na kusema kuwa siku hiyo itabidi waende wote kumuona Derrick maana hata wafanyeje bado ni ndugu yao tu.
Tumaini akiwa anaelekea katika shughuli zake, akakutana njiani na Dora na kuanza kuongea nae na kumpa taarifa kuhusu kulazwa kwa Derrick,
“Jamani masikini, kafanyaje tena?”
“Kumbe hujui? Derrick alikuwa ni tapeli ila dada yake yani Erica alikuwa akimfichia siri”
“Ila unajua kuna kitu huwa sielewi”
“Kitu gani?”
“Ni kuhusu Derrick na Erica, kwahiyo wale ni ndugu kabisa?”
“Ndio ndugu, baba mmoja wale”
“Unajua nini?”
“Nini?”
“Kipindi tupo chuo, kuna kipindi Fulani Erica alikuwa anatembea na Derrick, si unajua Erica alikuwa ni rafiki yangu sana ila tukaja kugombana badae kwa mambo madogo tu, basi Erica alikuwa anatembea na Derrick”
“Mmmh kwahiyo alikuwa ni mpenzi wake kabisa?”
“Ndio, alikuwa nae sasa nashangaa kusikia kuwa ni ndugu”
“Ila Erica anaonekana kuwa mpole sana, sidhani kama alitembea nae”
“Weeee ana upole gani yule! Niulize mimi listi ya wanaume aliotembea nao, ninaowajua tu ni wengi hatari, kuna kijamaa kilikuwa kinaitwa Babuu katembea nacho, kilikuwa kimasikini hatari ila Erica ndio alikufa alioza, mwenzio Erica katembea na George na aliachwa na George sababu hakuwa bikra”
“Mmmh unajua George na Erick ni ndugu kwa upande wa mama yake Erick huko!”
“Kheee basi hekaheka za Erica sio za nchi hii, kuna kipindi alijikuta kagonganisha ndugu watatu yule na wote katembea nao, huyo Derrick unayesema ni ndugu yake katembea nae, halafu kuna jamaa nadhani unamjua siku ya harusi ya Erick na Erica aliongea maneno mengi kiasi, yule jamaa anaitwa Bahati, kwasasa anaishi na Fetty basi yule Erica katembea nae, usimuone vile huwa kuna mambo namtetea tu. Ni kweli ni mpole ila kwenye swala la uhuni na yeye alikuwa muhuni”
“Kumbe!! Ndiomana alipatana na wewe, nikamshangaa msichana mpole vile kuwa na urafiki na wewe! Bora hata Fetty kidogo hakuwa na makuu chuoni ila wewe mmmh nilishangaa sana”
“Siku zote mwizi anatembea na mwizi mwenzie, ila kwasasa nimeokoka hayo mambo nimeacha jamani hata umbea huu sikutakiwa kukwambia, eeeh Mungu nisamehe”
Tumaini alicheka sana na kumuuliza,
“Ila hiyo listi ya wanaume wa Erica uliijuaje?”
“Mmmh unajua mimi nina dhambi nyingi jamani, namshukuru Mungu ni mwaminifu na anasamehe, la sivyo mimi nisengesamehewa jamani. Unajua nilikuwa namuonea sana huruma Erica akilia kuhusu mapenzi halafu hivi vidume vikijidai vyenyewe kwa kuumiza moyo wa Erica, yani siku niliyogundua nimeatirika basi nilimfata mmoja baada ya mwingine na kutembea nae, yani kila aliyemuumiza Erica nami nilihakikisha namuumiza na ukimwi”
“Ndiomana ukaamua kumuambukiza na baba yangu! Mwanamke mbaya wewe hata hufai”
“Mmmh tuachane na habari hizo Tumaini ila baba yako ndio aliniambukiza mimi. Nisamehe kwa hilo”
“Mbaya wewe na sidhani kama dhambi zote umesamehewa, hata huo ulokole wako nina mashaka nao. Kajinga kweli wewe”
Dora akaona yataanza marumbano pale bure, kwahiyo akaamua kuagana na Tumaini tu ila aliahidi kuwa ataenda kumsalimia Derrick pia.
Baada ya Dora kuondoka, kwakweli Tumaini alijiuliza sana,
“Kumbe watu wanatoka mbali eeeh! Ndiomana Erica alipata yule mtoto wa kiarabu kumbe na yeye alikuwa na mambo sana”
Basi akachukua simu yake na kumtumia mdogo wake ujumbe,
“Habari Erick, nasikia Erica kabla ya kukutana na wewe alishatembea na wanaume zaidi ya watano”
Muda kidogo akapokea ujumbe kwa Erick,
“Hata angetembea na dunia nzima bado ningempenda tu tena sana.”
Kisha akapiga simu ambapo Tumaini akapokea,
“Ila dada yangu kwani una matatizo gani? Ulisikia kuwa mwanamke akiwa ametembea na wanaume wengi haolewi wapi? Si ilimradi apate anayependana nae tu”
“Kheee yameisha basi, mimi nilikuwa nasema tu”
“Unajua kuna muda huwa sikuelewi, unampenda Erica ila unaniambia maneno kama haya, unataka niachane nae au ni kitu gani? Dada yangu nakuomba umuheshimu mke wangu, nampenda sana na unalijua hilo, mimi Erica nampenda hata niambiwe wale watoto wote sio wangu kazaa na wanaume wengine huko bado nitampenda na watoto nitawapenda yani usijisumbue kupata habari huko na kuniambia”
“Basi yameisha wala sitokwambia tena mambo kama haya”
“Halafu hizo tabia za umbea sijui umezitoa wapi? Utakuwa unaongea sana na Sia wewe ndiomana, naomba usiniletee tena umbea wa kuhusu mke wangu, nampenda jinsi alivyo na huwezi jua nimempendea nini”
“Nimekuelewa Erick, hata mimi nampenda Erica yani hata sijui naanzaje kukuletea umbea wa aina hii, naomba unisamehe”
“Kila siku na mke wangu tunajiuliza Erica mdogo katoa wapi umbea kumbe katoa kwako, naomba usiniambie tena habari za hivi, tuwe tunaongea mambo mengine tu”
“Nisamehe, nimekuelewa”
Tumaini alikata simu na kupumua kiasi kisha akasema,
“Kweli mapenzi ya kweli yapo, kuna muda hadi nahisi Erick karogwa jamani, si kwa kupenda huku mmmh! Ila hata mimi mume wangu ananipenda jamani, niache wivu loh!”
Akaendelea na safari yake ya kwenda kwenye shughuli zake.
Mama Angel alimuomba dada yake wapiti kwanza kiwandani halafu ndio waende hospitali maana hakutaka siku hiyo aipitishe bila kwenda kuangalia shughuli za kiwanda zimekwendaje.
Basi walienda hadi kiwandani, kwa mara ya kwanza mama Junior aliweza kuona kile kiwanda kilivyo,
“Jamani mdogo wangu, mmejitahidi sana”
“Asante”
Basi mama Junior alikuwa akitembelea tembelea maeneo baadhi ya kile kiwanda, kisha akatoka nje na kuanza kutembelea maeneo ya nje ya kile kiwanda, ila mara alipita mmama wa makamo
na kumsimamisha mama Junior kisha akamuuliza,
“Wewe si mama yake na Junior?”
“Ndio ni mimi”
Yule mama akamnasa kibao mama Junior, ila mama Junior nae huwa hapendi kuonewa kwahiyo alimnasa pia kibao yule mama.