Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #461
SEHEMU YA 409
Walipofika mlango wa kuingia ndani, Samir alikuwa kafungua mlango akitoka basi bibi Angel alishtuka sana kumuona Samir na kumuuliza baba Angel kwa mshangao,
“Ni nani huyu!?”
Baba Angel alimshangaa pia mama yake na kumuuliza,
“Kwani unamfahamu mama?”
“Hapana, ila ni nani?”
“Aaaah historia ndefu mama, nitakwambia tu karibu ndani”
Bibi Angel aliingia ndani ila jicho lake halikuganduka kwa Samir kwani alijikuta akimuangalia sana na kabla ya yote alitaka kutambulishwa kwa Samir kwanza kuwa ni nani, ikabidi baba Angel amuulize mama yake kuwa anafikiria ni kitu gani.
“Kwani mama unafikiria ni nani maana uleshtuka sana na bado unamuangalia?”
Bibi Angel alikuwa akiongea kiutaratibu na mwanae sasa,
“Weee mbona huyu kijana kafanana sana na baba yako! Yani kipindi cha ujana wao ndio alikuwa hivi hivi, yani huyu ni mzee Jimmy mtupu”
“Mmmmh mama!”
“Ndio, hamjawahi kuona picha za baba yenu za ujana wake? Alikuwa hivi hivi, yani kila kitu khaaa, hebu niambie ni nani?”
Baba Angel alipumua kidogo, akakumbuka mambo ya mtoto wa Jack, akakumbuka jinsi Rahim alivyosema huenda yeye na Rahim wana undugu, basi akafikiria kidogo na kusema, hapana kisha akamuuliza mama yake,
“Mama,kwani mzee Jimmy alikuwa na mtoto mwingine?”
“Mmmh yule baba yenu alikuwa na matatizo ya kizazi haswaaa, awe na mtoto mdogo hivyo!! Mimi nilijua huenda ukasema kuwa huyo ni mtoto wako, ulizaa huko nje maana nyie watoto wa kiume mna mambo sana, mwanamke akiolewa ajue tu kuna siku mambo yataripuka yani muda wote awe tayari kwa chochote. Kwahiyo huyo kijana ni mtoto wa nani?”
“Ni mtoto wa rafiki yangu mama”
Bibi Angel akaomba kutoka nje kidogo na baba Angel, kisha alienda nae moja kwa moja kwenye bustani ambapo bibi Angel alimuuliza baba Angel,
“Hebu niambie ukweli mwanangu, huyu mtoto sio damu yako kweli?”
“Mmmh sijui mama”
“Naomba kamuulize vizuri mama wa huyu mtoto, hamfahamiani kweli?”
“Aaaah mama, huyo mamake niliwahi kuwa na mahusiano nae zamani”
“Inawezekana ikawa ni damu yako ila alikuficha maana sisi wanawake tunamatatizo sana ikiwa mwanaume kakuudhi, mara nyingi unaamua kumfanya mtoto ni wako peke yako sababu baba yake alikuumiza sana. Hebu muulize vizuri ila nina uhakika asilimia mia moja kuwa hii ni damu yako, ingekuwa mzee Jimmy alikuwa na uwezo wa kuzaa tena baada ya wewe basi ningesema huyu ni mtoto wake ila mzee Jimmy alipata matatizo ya kizazi, halafu usifikirie ni mtloto wa mdogo wake mzee Jimmy labda ndio kamzaa huyo mtoto hapana, mzee Jimmy kwao alizaliwa peke yake ndiomana alikuwa na mali nyingi sana kwani ukoo mzima walikuwa wakimthamini yeye, na babu yao alikuwa ni mwenye pesa nyingi kwenye kijiji chao, kwahiyo alimtoa mjukuu wake kule na kumpa mali nyingi sana. Kwahiyo, nina uhakika asilimia mia moja kuwa hii ni damu yako”
Yani baba Angel alipumua ila alijiona kuwa na mawazo zaidi, maana kama Samir ni damu yake, je ataweza vipi kuliweka sawa swala hilo? Na je ni kivipi ikiwa yeye na mamake Samir waliachana sababu ya yeye kumsababishia yule mwanamke mimba itoke!! Alijikuta akikaa kimya kwa muda huku akimtazama mama yake ambaye alimwambia tena,
“Ukoo wenu sio mkubwa, kusanya vitoto vyako, bile mwenyewe katika mstari. Kwangu upo peke yako, kwa baba yako mpo wawili tu, kusanya hao ndio ndugu zenu wa badae. Nimemaliza, ila yule ni mjukuu wangu”
Kisha bibi Angel akauliza alipo Angel ili akamsalimie, yani baba Angel alimpeleka mama yake huku akiwa na mawazo sana juu ya kile ambacho mama yake amekiongea kwake kwa muda huo.
Basi baba Angel alirudi sebleni huku akimuangalia sana Samir, yani kwa muda huu alimuangalia sana hakuweza hata kummaliza, alijiuliza maswali mengi sana kuwa kama kweli Samir ni mtoto wake ila hakupata jibu la moja kwa moja.
Basi bibi Angel alipotoka alimtaka mwanae amsindikize kidogo, ingawa alikuwa na gari ila alitaka mwanae amwendeshe kidogo ambapo baba Angel alitoka kumsindikiza mama yake.
Wakiwa kwenye gari, bibi Angel alirudia tena yale maneno yake,
“Wakati wa kutoka tena nimemuangalia sana yule kijana, aaaah yule ni mwanao lazima ni mwanao Erick”
“Mmmh ila mama, siku ya kwanza nakutana na yule kijana nilimfananisha sana na jamaa fulani hivi”
“Acha kujidanganya Erick, labda kama unajifananisha nae mwenyewe, yule mtoto ni damu yako.”
Baba Angel alikaa kimya ila mama yake aliendelea kuongea,
“Jumamosi nitakuuliza kama tayari ushaongea na mama wa mtoto, akigoma nenda kapime damu na mtoto yule maana ni damu yako”
Yani baba Angel alishindwa kuongea kwakweli na kukaa kimya tu, mpaka pale mama yake aliporidhika basi yeye alishuka na kurudi nyumbani kwake ambapo tayari ilikuwa ni usiku.
Mama Angel alimuuliza mumewe kitu ambacho mama yake alishangaa kumuona Samir,
“Alishangaa sana halafu alikuwa kama anakunong’oneza kitu, mara ukatoka nae nje ni kitu gani hiko”
“Aaaah mama alikuwa kiuliza ugonjwa wa Angel, mbona alishaacha kumshangaa Samir yani yeye alichokuwa akishangaa ni kuwa yule kijana anafanya nini hapa nyumbani kwetu. Nilipomwambia ni mtoto wa rafiki yangu akaridhika”
“Aaaah kumbe!! Eeeeh umemwambia Angel alikuwa akiumwa nini?”
“Hivi mama Angel, mwanzoni kabisa nilipomuona Samir nilikwambia namfananisha na nani?”
“Mmmmh hata hukuniambia ila ulisema kuwa kuna mtu anafanana nae tena ulisema mtu huyo namfahamu ila hukuniambia hadi leo kuhusu huyo mtu”
“Aaaah nilifikiri nilimtaja?”
“Hapana, ni nani uliyekuwa ukimfananisha na Samir?”
“Aaaah ni Rahim”
“Rahim wapi? Yule mtoto hata hafanani na Rahim sijui na yeye kachomekewa”
Halafu mama Angel alianza kucheka ambapo baba Angel akamuuliza,
“Kama wewe ulivyonichomekea Angel?”
“Mmmh jamani yamekuwa hayo tena!! Wewe si ulimkubali Angel ilihali unafahamu kila kitu!! Tuachane na hayo mume wangu, tujadili maswala ya watoto”
“Eeeeh Angel anaendeleaje”
“Hajambo kabisa, anaendelea vizuri”
Baba Angel hakutaka kuongea sana kwa muda huo kwani aliona akili yake kama imevurugika hivi, kwahiyo aliamua tu kulala.
Leo baba Angel alimuita Samir mapema kabisa kwenye bustani yao na kuanza kuongea nae,
“Eti Samir, huwa baba yako unamuonaje yule?”
“Sijawahi kumuelewa tangu nilipokuwa mtoto, sijui kama ni baba yangu yule”
“Kwa mfano mama yako akakutambulisha baba yako mwingine utafanyaje?”
“Nitafurahi tu, maana yule baba hata huwa simuelewi”
“Jiandae, kuna mahali nataka kwenda na wewe”
Basi Samir alijiandaa kisha alitoka na baba Angel na moja kwa moja baba Angel alienda na Samir nyumbani kwa Tumaini, wakati huo alikuwa amemtumia ujumbe Tumaini kuwa amuangalie sana huyu kijana ambaye anaenda nae nyumbani kwake.
Walipofika ni kweli Tumaini nae aliguna na kuwasalimia pale kisha alimvuta nje kaka yake na kumuuliza,
“Erick, ndio matunda yako yameanza kuonekana nini?”
“Kivipi?”
“Unafikiri mchezo!! Wale wanawake wote uliokuwa ukiwapa mimba kipindi kile na kuwatoa, wapo ambao walitunza”
“Kwanini unasema hivyo?”
“Hii damu yetu hii, umekuja kunionyesha shangazi yangu eeeh!!”
“Aaaah sio hivyo, unaona kafanana na nani huyo mtoto?”
“Kuna picha za baba akiwa mvulana mdogo yani hivyo hivyo kama huyo kijana. Siku nikienda kule nyumbani nitaenda kuzipekua, Erick kwakweli una damu kali mdogo wangu”
“Hivi hujawahi kumuona huyu kijana eeeh!!”
“Sijui kama nimewahi kumuona, nahisi sijawahi kumuona ila nimefurahi kumjua. Kumbe tuna kijana mkubwa hivi, nilijua Erick ndio mkubwa pekee”
“Aaaah Tumaini acha zako bhana”
“Halafu sikukwambia, jana kuna maeneo nilikuwepo halafu akapita Erick nikasikia wanasema duh yule kijana ni hatari sana, mwengine akasema anacheza kungfuu huyo, duh sikusema kitu maana hawakujua kama wanayemuongelea ni damu yangu”
“Mmmh dada, mambo ya Erick yaache kwanza. Nilimleta huyu kijana umuone basi”
“Nimemuona na nimemkubali kuwa ni wa kwetu”
Hapo baba Angel hakuwa na usemi zaidi basi walirudi ndani ambapo Tumaini alienda kuwaandalia chakula ili waweze kula pale nyumbani kwake.
Walipoanza kula tu, simu ya baba Angel iliita ikabidi atoke nje na kuipokea maana aliyekuwa akipiga ni Jack,
“Samahani Erick, naona kila siku hatuelewani. Ni hivi, mtoto huyu kuna binti alimpa mimba, yule binti kajifungua leo, ile familia wanahitaji twende kujitambulisha. Ndiomana siku zote hizi nilikuwa nakukazania ili ujue kuwa mtoto wako anahitaji kutambua kwamba ana baba yake”
Baba Angel akapumua kidogo na kusema,
“Nimekuelewa Jack, mmepanga kwenda lini?”
“Wiki ijayo”
“Sawa hakuna tatizo, tutaenda wote. Nishtue tu siku ikifika”
Basi baba Angel alikata ile simu na kurudi ndani kuendelea kula, na baada ya muda waliondoka zao.
Jioni ya leo, Angel alitoka na kwenda kukaa kwenye bustani yao ambapo Erica nae alienda kukaa nae karibu na kuongea nae,
“Unaendeleaje dada?”
“Sarah yuko wapi?”
“Amelala, ila nimekuuliza unaendeleaje?”
“Kwani nilikuwa naumwa?”
“Ndio, si ulikuwa na mimba wewe imetoka!”
“Mama amekwambia?”
“Hapana”
“Ila umepata wapi hiyo habari?”
“Nimeota”
“Umeanza mambo yako ya ndoto, haya hiyo mimba ni ya nani ilikuwa?”
“Nimeota kuwa ulipata mimba ya Samir, siku ile mliyosababisha moto. Halafu baada ya kugundua, baba na mama wakakukimbizia kwa bibi ambapo kuna siku hukula na ukikuwa ukilia sana, ukahisi kizunguzungu na kuanguka hakuna aliyejua, ulizinduka ukiwa mwenyewe chumbani, bibi akakuuliza ukasema uitiwe baba ndio baba akaitwa ukapelekwa hospitali na kukuta mimba imetoka”
“Kheee nimekuvulia kofia wewe mtoto jamani, hebu niambie kwenye ndoto zako unaona mimi nitaolewa na nani?”
“Niliwahi kuota kuwa wewe unaolewa na huyo huyo Samir ila kuna utata mkubwa sana ulitokea maana kila mtu alikuwa akipinga kuoana kwenu na wakidai kuwa nyie ni kama ndugu”
“Ni kama!! Kwahiyo sisi sio ndugu?”
“Sijui kitu, nakueleza vile nilivyoota”
“Wewe Erica, unapata wapi uwezo wa kuota vitu vyote hivyo?”
“Hata mimi sijui, kuna ndoto zingine hata kusema huwa naogopa maana zinakuwa na makubwa ndani yake”
“Kama ndoto gani?”
“Kama ndoto ya kuhusu mimi na Erick”
“Eeeeh wewe na Erick mmefanyaje?”
“Ipo siku nitakwambia ila sio leo. Sema pole sana dada yangu, haya ni mapito tu, kuna muda utazoea na kusahau kama kuna kitu cha namna hii kimepita katika maisha yako”
“Wewe bado mdogo ila mara nyingine una maneno ya busara sana. Yani Sarah ndio mvivu kama mimi jamani, hebu kamuamshe”
Basi Erica alienda ndani kumuamsha Sarah ambaye aliamka na kutoka na Erica hadi kwenye bustani, halafu Angel alimwambia Sarah
“Yani wewe unapenda kulala jamani, utapata wapi muda wa uwaza maendeleo? Muda wa kuwaza mahali pa kupatia pesa?”
“Kwanini niwaze vyote hivyo dada?”
“Kwanini?”
“Mimi kwetu ni mtoto wa pekee, baba yangu aliniachia mali nyingi sana, hapa unavyoniona nina nyumba tatu, nina mashamba makubwa matatu, nina ile shule kubwa sana. Baba yangu alikuwa akinipenda sana, na hakutaka nipate shida duniani, namshukuru mama kwa kunitafutia baba kama yule”
“Mama yako akiviuza je?”
“Angeviuza wakati nipo mdogo ila sio kwasasa hivi nikiwa mkubwa hivi, mama hana kiburi cha kufanya chochote bila ridhaa yangu. Ila kwa jinsi ninavyowapenda Erick na Erica basi najitolea kugawana nao mashamba yangu yani kila mmoja atachukua moja moja”
“Kheee na mimi je dada mkubwa?”
“Wewe nitakupa nyumba”
Walicheka pale, walijua ni maongezi tu ya kumaliza siku yani hakuna aliyetilia maanani yale yote yaliyokuwa yakizungumzwa mahali pale.
Walipofika mlango wa kuingia ndani, Samir alikuwa kafungua mlango akitoka basi bibi Angel alishtuka sana kumuona Samir na kumuuliza baba Angel kwa mshangao,
“Ni nani huyu!?”
Baba Angel alimshangaa pia mama yake na kumuuliza,
“Kwani unamfahamu mama?”
“Hapana, ila ni nani?”
“Aaaah historia ndefu mama, nitakwambia tu karibu ndani”
Bibi Angel aliingia ndani ila jicho lake halikuganduka kwa Samir kwani alijikuta akimuangalia sana na kabla ya yote alitaka kutambulishwa kwa Samir kwanza kuwa ni nani, ikabidi baba Angel amuulize mama yake kuwa anafikiria ni kitu gani.
“Kwani mama unafikiria ni nani maana uleshtuka sana na bado unamuangalia?”
Bibi Angel alikuwa akiongea kiutaratibu na mwanae sasa,
“Weee mbona huyu kijana kafanana sana na baba yako! Yani kipindi cha ujana wao ndio alikuwa hivi hivi, yani huyu ni mzee Jimmy mtupu”
“Mmmmh mama!”
“Ndio, hamjawahi kuona picha za baba yenu za ujana wake? Alikuwa hivi hivi, yani kila kitu khaaa, hebu niambie ni nani?”
Baba Angel alipumua kidogo, akakumbuka mambo ya mtoto wa Jack, akakumbuka jinsi Rahim alivyosema huenda yeye na Rahim wana undugu, basi akafikiria kidogo na kusema, hapana kisha akamuuliza mama yake,
“Mama,kwani mzee Jimmy alikuwa na mtoto mwingine?”
“Mmmh yule baba yenu alikuwa na matatizo ya kizazi haswaaa, awe na mtoto mdogo hivyo!! Mimi nilijua huenda ukasema kuwa huyo ni mtoto wako, ulizaa huko nje maana nyie watoto wa kiume mna mambo sana, mwanamke akiolewa ajue tu kuna siku mambo yataripuka yani muda wote awe tayari kwa chochote. Kwahiyo huyo kijana ni mtoto wa nani?”
“Ni mtoto wa rafiki yangu mama”
Bibi Angel akaomba kutoka nje kidogo na baba Angel, kisha alienda nae moja kwa moja kwenye bustani ambapo bibi Angel alimuuliza baba Angel,
“Hebu niambie ukweli mwanangu, huyu mtoto sio damu yako kweli?”
“Mmmh sijui mama”
“Naomba kamuulize vizuri mama wa huyu mtoto, hamfahamiani kweli?”
“Aaaah mama, huyo mamake niliwahi kuwa na mahusiano nae zamani”
“Inawezekana ikawa ni damu yako ila alikuficha maana sisi wanawake tunamatatizo sana ikiwa mwanaume kakuudhi, mara nyingi unaamua kumfanya mtoto ni wako peke yako sababu baba yake alikuumiza sana. Hebu muulize vizuri ila nina uhakika asilimia mia moja kuwa hii ni damu yako, ingekuwa mzee Jimmy alikuwa na uwezo wa kuzaa tena baada ya wewe basi ningesema huyu ni mtoto wake ila mzee Jimmy alipata matatizo ya kizazi, halafu usifikirie ni mtloto wa mdogo wake mzee Jimmy labda ndio kamzaa huyo mtoto hapana, mzee Jimmy kwao alizaliwa peke yake ndiomana alikuwa na mali nyingi sana kwani ukoo mzima walikuwa wakimthamini yeye, na babu yao alikuwa ni mwenye pesa nyingi kwenye kijiji chao, kwahiyo alimtoa mjukuu wake kule na kumpa mali nyingi sana. Kwahiyo, nina uhakika asilimia mia moja kuwa hii ni damu yako”
Yani baba Angel alipumua ila alijiona kuwa na mawazo zaidi, maana kama Samir ni damu yake, je ataweza vipi kuliweka sawa swala hilo? Na je ni kivipi ikiwa yeye na mamake Samir waliachana sababu ya yeye kumsababishia yule mwanamke mimba itoke!! Alijikuta akikaa kimya kwa muda huku akimtazama mama yake ambaye alimwambia tena,
“Ukoo wenu sio mkubwa, kusanya vitoto vyako, bile mwenyewe katika mstari. Kwangu upo peke yako, kwa baba yako mpo wawili tu, kusanya hao ndio ndugu zenu wa badae. Nimemaliza, ila yule ni mjukuu wangu”
Kisha bibi Angel akauliza alipo Angel ili akamsalimie, yani baba Angel alimpeleka mama yake huku akiwa na mawazo sana juu ya kile ambacho mama yake amekiongea kwake kwa muda huo.
Basi baba Angel alirudi sebleni huku akimuangalia sana Samir, yani kwa muda huu alimuangalia sana hakuweza hata kummaliza, alijiuliza maswali mengi sana kuwa kama kweli Samir ni mtoto wake ila hakupata jibu la moja kwa moja.
Basi bibi Angel alipotoka alimtaka mwanae amsindikize kidogo, ingawa alikuwa na gari ila alitaka mwanae amwendeshe kidogo ambapo baba Angel alitoka kumsindikiza mama yake.
Wakiwa kwenye gari, bibi Angel alirudia tena yale maneno yake,
“Wakati wa kutoka tena nimemuangalia sana yule kijana, aaaah yule ni mwanao lazima ni mwanao Erick”
“Mmmh ila mama, siku ya kwanza nakutana na yule kijana nilimfananisha sana na jamaa fulani hivi”
“Acha kujidanganya Erick, labda kama unajifananisha nae mwenyewe, yule mtoto ni damu yako.”
Baba Angel alikaa kimya ila mama yake aliendelea kuongea,
“Jumamosi nitakuuliza kama tayari ushaongea na mama wa mtoto, akigoma nenda kapime damu na mtoto yule maana ni damu yako”
Yani baba Angel alishindwa kuongea kwakweli na kukaa kimya tu, mpaka pale mama yake aliporidhika basi yeye alishuka na kurudi nyumbani kwake ambapo tayari ilikuwa ni usiku.
Mama Angel alimuuliza mumewe kitu ambacho mama yake alishangaa kumuona Samir,
“Alishangaa sana halafu alikuwa kama anakunong’oneza kitu, mara ukatoka nae nje ni kitu gani hiko”
“Aaaah mama alikuwa kiuliza ugonjwa wa Angel, mbona alishaacha kumshangaa Samir yani yeye alichokuwa akishangaa ni kuwa yule kijana anafanya nini hapa nyumbani kwetu. Nilipomwambia ni mtoto wa rafiki yangu akaridhika”
“Aaaah kumbe!! Eeeeh umemwambia Angel alikuwa akiumwa nini?”
“Hivi mama Angel, mwanzoni kabisa nilipomuona Samir nilikwambia namfananisha na nani?”
“Mmmmh hata hukuniambia ila ulisema kuwa kuna mtu anafanana nae tena ulisema mtu huyo namfahamu ila hukuniambia hadi leo kuhusu huyo mtu”
“Aaaah nilifikiri nilimtaja?”
“Hapana, ni nani uliyekuwa ukimfananisha na Samir?”
“Aaaah ni Rahim”
“Rahim wapi? Yule mtoto hata hafanani na Rahim sijui na yeye kachomekewa”
Halafu mama Angel alianza kucheka ambapo baba Angel akamuuliza,
“Kama wewe ulivyonichomekea Angel?”
“Mmmh jamani yamekuwa hayo tena!! Wewe si ulimkubali Angel ilihali unafahamu kila kitu!! Tuachane na hayo mume wangu, tujadili maswala ya watoto”
“Eeeeh Angel anaendeleaje”
“Hajambo kabisa, anaendelea vizuri”
Baba Angel hakutaka kuongea sana kwa muda huo kwani aliona akili yake kama imevurugika hivi, kwahiyo aliamua tu kulala.
Leo baba Angel alimuita Samir mapema kabisa kwenye bustani yao na kuanza kuongea nae,
“Eti Samir, huwa baba yako unamuonaje yule?”
“Sijawahi kumuelewa tangu nilipokuwa mtoto, sijui kama ni baba yangu yule”
“Kwa mfano mama yako akakutambulisha baba yako mwingine utafanyaje?”
“Nitafurahi tu, maana yule baba hata huwa simuelewi”
“Jiandae, kuna mahali nataka kwenda na wewe”
Basi Samir alijiandaa kisha alitoka na baba Angel na moja kwa moja baba Angel alienda na Samir nyumbani kwa Tumaini, wakati huo alikuwa amemtumia ujumbe Tumaini kuwa amuangalie sana huyu kijana ambaye anaenda nae nyumbani kwake.
Walipofika ni kweli Tumaini nae aliguna na kuwasalimia pale kisha alimvuta nje kaka yake na kumuuliza,
“Erick, ndio matunda yako yameanza kuonekana nini?”
“Kivipi?”
“Unafikiri mchezo!! Wale wanawake wote uliokuwa ukiwapa mimba kipindi kile na kuwatoa, wapo ambao walitunza”
“Kwanini unasema hivyo?”
“Hii damu yetu hii, umekuja kunionyesha shangazi yangu eeeh!!”
“Aaaah sio hivyo, unaona kafanana na nani huyo mtoto?”
“Kuna picha za baba akiwa mvulana mdogo yani hivyo hivyo kama huyo kijana. Siku nikienda kule nyumbani nitaenda kuzipekua, Erick kwakweli una damu kali mdogo wangu”
“Hivi hujawahi kumuona huyu kijana eeeh!!”
“Sijui kama nimewahi kumuona, nahisi sijawahi kumuona ila nimefurahi kumjua. Kumbe tuna kijana mkubwa hivi, nilijua Erick ndio mkubwa pekee”
“Aaaah Tumaini acha zako bhana”
“Halafu sikukwambia, jana kuna maeneo nilikuwepo halafu akapita Erick nikasikia wanasema duh yule kijana ni hatari sana, mwengine akasema anacheza kungfuu huyo, duh sikusema kitu maana hawakujua kama wanayemuongelea ni damu yangu”
“Mmmh dada, mambo ya Erick yaache kwanza. Nilimleta huyu kijana umuone basi”
“Nimemuona na nimemkubali kuwa ni wa kwetu”
Hapo baba Angel hakuwa na usemi zaidi basi walirudi ndani ambapo Tumaini alienda kuwaandalia chakula ili waweze kula pale nyumbani kwake.
Walipoanza kula tu, simu ya baba Angel iliita ikabidi atoke nje na kuipokea maana aliyekuwa akipiga ni Jack,
“Samahani Erick, naona kila siku hatuelewani. Ni hivi, mtoto huyu kuna binti alimpa mimba, yule binti kajifungua leo, ile familia wanahitaji twende kujitambulisha. Ndiomana siku zote hizi nilikuwa nakukazania ili ujue kuwa mtoto wako anahitaji kutambua kwamba ana baba yake”
Baba Angel akapumua kidogo na kusema,
“Nimekuelewa Jack, mmepanga kwenda lini?”
“Wiki ijayo”
“Sawa hakuna tatizo, tutaenda wote. Nishtue tu siku ikifika”
Basi baba Angel alikata ile simu na kurudi ndani kuendelea kula, na baada ya muda waliondoka zao.
Jioni ya leo, Angel alitoka na kwenda kukaa kwenye bustani yao ambapo Erica nae alienda kukaa nae karibu na kuongea nae,
“Unaendeleaje dada?”
“Sarah yuko wapi?”
“Amelala, ila nimekuuliza unaendeleaje?”
“Kwani nilikuwa naumwa?”
“Ndio, si ulikuwa na mimba wewe imetoka!”
“Mama amekwambia?”
“Hapana”
“Ila umepata wapi hiyo habari?”
“Nimeota”
“Umeanza mambo yako ya ndoto, haya hiyo mimba ni ya nani ilikuwa?”
“Nimeota kuwa ulipata mimba ya Samir, siku ile mliyosababisha moto. Halafu baada ya kugundua, baba na mama wakakukimbizia kwa bibi ambapo kuna siku hukula na ukikuwa ukilia sana, ukahisi kizunguzungu na kuanguka hakuna aliyejua, ulizinduka ukiwa mwenyewe chumbani, bibi akakuuliza ukasema uitiwe baba ndio baba akaitwa ukapelekwa hospitali na kukuta mimba imetoka”
“Kheee nimekuvulia kofia wewe mtoto jamani, hebu niambie kwenye ndoto zako unaona mimi nitaolewa na nani?”
“Niliwahi kuota kuwa wewe unaolewa na huyo huyo Samir ila kuna utata mkubwa sana ulitokea maana kila mtu alikuwa akipinga kuoana kwenu na wakidai kuwa nyie ni kama ndugu”
“Ni kama!! Kwahiyo sisi sio ndugu?”
“Sijui kitu, nakueleza vile nilivyoota”
“Wewe Erica, unapata wapi uwezo wa kuota vitu vyote hivyo?”
“Hata mimi sijui, kuna ndoto zingine hata kusema huwa naogopa maana zinakuwa na makubwa ndani yake”
“Kama ndoto gani?”
“Kama ndoto ya kuhusu mimi na Erick”
“Eeeeh wewe na Erick mmefanyaje?”
“Ipo siku nitakwambia ila sio leo. Sema pole sana dada yangu, haya ni mapito tu, kuna muda utazoea na kusahau kama kuna kitu cha namna hii kimepita katika maisha yako”
“Wewe bado mdogo ila mara nyingine una maneno ya busara sana. Yani Sarah ndio mvivu kama mimi jamani, hebu kamuamshe”
Basi Erica alienda ndani kumuamsha Sarah ambaye aliamka na kutoka na Erica hadi kwenye bustani, halafu Angel alimwambia Sarah
“Yani wewe unapenda kulala jamani, utapata wapi muda wa uwaza maendeleo? Muda wa kuwaza mahali pa kupatia pesa?”
“Kwanini niwaze vyote hivyo dada?”
“Kwanini?”
“Mimi kwetu ni mtoto wa pekee, baba yangu aliniachia mali nyingi sana, hapa unavyoniona nina nyumba tatu, nina mashamba makubwa matatu, nina ile shule kubwa sana. Baba yangu alikuwa akinipenda sana, na hakutaka nipate shida duniani, namshukuru mama kwa kunitafutia baba kama yule”
“Mama yako akiviuza je?”
“Angeviuza wakati nipo mdogo ila sio kwasasa hivi nikiwa mkubwa hivi, mama hana kiburi cha kufanya chochote bila ridhaa yangu. Ila kwa jinsi ninavyowapenda Erick na Erica basi najitolea kugawana nao mashamba yangu yani kila mmoja atachukua moja moja”
“Kheee na mimi je dada mkubwa?”
“Wewe nitakupa nyumba”
Walicheka pale, walijua ni maongezi tu ya kumaliza siku yani hakuna aliyetilia maanani yale yote yaliyokuwa yakizungumzwa mahali pale.