Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #541
SEHEMU YA 419
Erica alipeleka juisi sebleni ili Tumaini na Tony wanywe, halafu akawakaribisha, walipokuwa wakinywa ndipo Erica akauliza sasa,
"Eeeh kaka niambie, umefahamiana vipi na Tumaini?"
"Yani huwezi amini, Tumaini nilisoma nae shule ya msingi. Kipindi hiko alikuwa mwembamba ila nashangaa saivi kawa bonge"
Erica akacheka na kusema,
"Kipindi hicho ilikuwa utoto ila saivi ni ukubwa, ila huoni kuwa kapendeza"
"Ndio, amependeza sana yani leo nina furaha sana"
Erica akatania,
"Kwahiyo hadi umemsahau Doroth, na wewe na majina ya D sijui vipi!"
"Aaaah achana na hizo habari bhana, yule acha aende ila lengo la kuoa lipo kwenye akili yangu bado"
Erica akatania tena,
"Si umuoe Tumaini tu!"
Tumaini akacheka na kusema,
"Wewe Erica wewe sijui leo umekunywa nini jamani yani unaongea kama kitu gani vile! Sasa Tony anioe mimi kweli wakati ana mwanamke wake!"
"Lakini kumbuka huyo mwanamke wake hamtaki tena"
Tumaini akacheka tu, halafu Tony akaongezea
"Erica mambo ya Tumaini na mimi hebu yaache kwanza. Ila Tumaini ndio unaishi hapa?"
"Hapana hapa nimekuja tu kumtembelea Erica"
Ilibidi Tony amuulize vizuri dadake ambaye aliamua kumueleza ukweli tu,
"Kwahiyo Tumaini ni dada wa Erick?"
"Ndio, ni ndugu yake"
"Sasa Tumaini, hapa leo tutaondoka wote ili nikapafahamu kwenu au unasemaje?"
"Hakuna shida"
Na kweli pale waliongea weee na muda wa kuondoka ni Tumaini na Tony waliondoka pamoja.
Jioni ilipofika alirudi Erick ambapo alipopumzika kidogo tu Erica akaanza kumueleza yaliyotukia siku hiyo ila tu hakuweka ile sehemu ya kusema na Doroth, alieleza tu kuwa kakake alifika na kaonana na Tumaini na ilivyokuwa kwenye maongezi,
"Kheeee Tumaini alikuja hapa kumbe! Kweli dadangu kabadilika jamani!"
"Hadi nilishangaa ila sijaweza kuongea nae chochote maana ndio kaka yangu alifika"
"Kwahiyo inaonyesha wamepatana sana eeeh!"
"Ndio sana, yani sijui kama hawajatongozana wale maana macho yao tu yalionyesha wanatakana"
"Hahaha Erica bhana, muache dada yangu nae apate mpenzi maana sijui kama ana historia ya kupata mpenzi"
"Unadhani kwanini?"
"Nafikiri ni muonekano wake, yupo serious sana labda ndio sababu ya vijana kuogopa kumtongoza na hata hivyo nadhani wanaojaribu huwa anawajibu vibaya sana maana yule kajengewa dhana mbaya na mama yake kuwa wanaume ni viumbe wabaya, si unajua mamake alitendwa na baba ila kwa jinsi sisi tunavyopendana ndio na yeye ameona radha ya mapenzi, kwa maana hiyo kama huyo Tony atakuwa na lengo kweli basi atamkubali"
"Mmmh hivi itakuwaje, mimi na wewe halafu Tumaini na Tony!"
"Aaaah hizo habari tuziache Erica maana watajuana wenyewe, sisi tujali tunavyopendana tu"
Kisha Erick akamsogelea Erica na kumkumbatia, ambapo Angel nae alitoka chumbani na kukumbatiwa pamoja nao.
Kisha walienda kula, wakati wanakula simu ya Erica tena ikaita na mpigaji alikuwa ni mamake, Erica akawaza kuwa muda huo mamake anataka kusema kitu gani, akaacha kula na kuinuka kisha akapokea ile simu na kuongea nayo,
"Erica, nakupa wiki moja uwe umeleta hayo matendegu yako nyumbani, wewe mtoto usitake kunipanda kichwani. Narudia tena, nakupa wiki moja, siwezi kuendelea kuvumilia huo ujinga unaofanya"
"Lakini mama"
"Hakuna cha lakini, nishasema nimemaliza kwakweli maswala ya lakini sitaki kuyasikia, mwambie huyo huyo mjinga mwenzio lakini sio mimi. Nimemaliza"
Simu ikakatika ila Erick alikuwa nyuma ya Erica yani muda alivyoinuka kuipokea ile simu na Erick nae aliinuja na kusimama nyuma yake, alimkumbatia kwa nyuma kama kumbembeleza,
"Usijali Erica, usiwe na mawazo wala presha. Wala hiyo wiki haitafika kwani mimi nitahakikisha tunaenda kufanya taratibu zote kwenu"
"Na kwenu je watakubali?"
"Usijali kuhusu kwetu maana mama anakaribia kurudi, na nikimwambia swala la wewe kuwa mjamzito ni lazima ataomba mwenyewe kuwa akaongee na mama yako. Wakiongea wamama watupu najua kuna uelewa utakuwepo yani hata usihali mpenzi wangu"
Erica alijihisi raha sana kwavile alivyoambiwa na Erick, na jinsi alivyomshika ndio alijisikia furaha zaidi kisha wakaenda tena kula na walipomaliza walikaa kidogo na kwenda kulala.
Wakati wamelala kuna ujumbe uliingia kwenye simu ya Erick, ilikuwa ni usiku sana ila alichukua simu yake na kuangalia ule ujumbe akakuta umetoka kwa baba yake,
"Erick, siku hizi hurudi nyumbani unazamia kwa wanawake. Hao ni viumbe wa kupita tena hawana thamani kama wazazi yani unasahau mzazi sababu ya mwanamke? Sijapenda hilo swala kabisa, na umeishia wapi kuhusu swala la kuongea na Ester ili awe mama yenu Serious Erick usipofanya hivyo na mimi nitasahau kuhusu ubaba, yani hutomuoa huyo mdudu wako Erica"
Erick alisoma ule ujumbe wa babake mara mbili mbili ila aliona utamuumiza kichwa tu, hivyo alimsogelea vizuri Erica na kumkumbatia na kuendelea kulala.
Erica alipeleka juisi sebleni ili Tumaini na Tony wanywe, halafu akawakaribisha, walipokuwa wakinywa ndipo Erica akauliza sasa,
"Eeeh kaka niambie, umefahamiana vipi na Tumaini?"
"Yani huwezi amini, Tumaini nilisoma nae shule ya msingi. Kipindi hiko alikuwa mwembamba ila nashangaa saivi kawa bonge"
Erica akacheka na kusema,
"Kipindi hicho ilikuwa utoto ila saivi ni ukubwa, ila huoni kuwa kapendeza"
"Ndio, amependeza sana yani leo nina furaha sana"
Erica akatania,
"Kwahiyo hadi umemsahau Doroth, na wewe na majina ya D sijui vipi!"
"Aaaah achana na hizo habari bhana, yule acha aende ila lengo la kuoa lipo kwenye akili yangu bado"
Erica akatania tena,
"Si umuoe Tumaini tu!"
Tumaini akacheka na kusema,
"Wewe Erica wewe sijui leo umekunywa nini jamani yani unaongea kama kitu gani vile! Sasa Tony anioe mimi kweli wakati ana mwanamke wake!"
"Lakini kumbuka huyo mwanamke wake hamtaki tena"
Tumaini akacheka tu, halafu Tony akaongezea
"Erica mambo ya Tumaini na mimi hebu yaache kwanza. Ila Tumaini ndio unaishi hapa?"
"Hapana hapa nimekuja tu kumtembelea Erica"
Ilibidi Tony amuulize vizuri dadake ambaye aliamua kumueleza ukweli tu,
"Kwahiyo Tumaini ni dada wa Erick?"
"Ndio, ni ndugu yake"
"Sasa Tumaini, hapa leo tutaondoka wote ili nikapafahamu kwenu au unasemaje?"
"Hakuna shida"
Na kweli pale waliongea weee na muda wa kuondoka ni Tumaini na Tony waliondoka pamoja.
Jioni ilipofika alirudi Erick ambapo alipopumzika kidogo tu Erica akaanza kumueleza yaliyotukia siku hiyo ila tu hakuweka ile sehemu ya kusema na Doroth, alieleza tu kuwa kakake alifika na kaonana na Tumaini na ilivyokuwa kwenye maongezi,
"Kheeee Tumaini alikuja hapa kumbe! Kweli dadangu kabadilika jamani!"
"Hadi nilishangaa ila sijaweza kuongea nae chochote maana ndio kaka yangu alifika"
"Kwahiyo inaonyesha wamepatana sana eeeh!"
"Ndio sana, yani sijui kama hawajatongozana wale maana macho yao tu yalionyesha wanatakana"
"Hahaha Erica bhana, muache dada yangu nae apate mpenzi maana sijui kama ana historia ya kupata mpenzi"
"Unadhani kwanini?"
"Nafikiri ni muonekano wake, yupo serious sana labda ndio sababu ya vijana kuogopa kumtongoza na hata hivyo nadhani wanaojaribu huwa anawajibu vibaya sana maana yule kajengewa dhana mbaya na mama yake kuwa wanaume ni viumbe wabaya, si unajua mamake alitendwa na baba ila kwa jinsi sisi tunavyopendana ndio na yeye ameona radha ya mapenzi, kwa maana hiyo kama huyo Tony atakuwa na lengo kweli basi atamkubali"
"Mmmh hivi itakuwaje, mimi na wewe halafu Tumaini na Tony!"
"Aaaah hizo habari tuziache Erica maana watajuana wenyewe, sisi tujali tunavyopendana tu"
Kisha Erick akamsogelea Erica na kumkumbatia, ambapo Angel nae alitoka chumbani na kukumbatiwa pamoja nao.
Kisha walienda kula, wakati wanakula simu ya Erica tena ikaita na mpigaji alikuwa ni mamake, Erica akawaza kuwa muda huo mamake anataka kusema kitu gani, akaacha kula na kuinuka kisha akapokea ile simu na kuongea nayo,
"Erica, nakupa wiki moja uwe umeleta hayo matendegu yako nyumbani, wewe mtoto usitake kunipanda kichwani. Narudia tena, nakupa wiki moja, siwezi kuendelea kuvumilia huo ujinga unaofanya"
"Lakini mama"
"Hakuna cha lakini, nishasema nimemaliza kwakweli maswala ya lakini sitaki kuyasikia, mwambie huyo huyo mjinga mwenzio lakini sio mimi. Nimemaliza"
Simu ikakatika ila Erick alikuwa nyuma ya Erica yani muda alivyoinuka kuipokea ile simu na Erick nae aliinuja na kusimama nyuma yake, alimkumbatia kwa nyuma kama kumbembeleza,
"Usijali Erica, usiwe na mawazo wala presha. Wala hiyo wiki haitafika kwani mimi nitahakikisha tunaenda kufanya taratibu zote kwenu"
"Na kwenu je watakubali?"
"Usijali kuhusu kwetu maana mama anakaribia kurudi, na nikimwambia swala la wewe kuwa mjamzito ni lazima ataomba mwenyewe kuwa akaongee na mama yako. Wakiongea wamama watupu najua kuna uelewa utakuwepo yani hata usihali mpenzi wangu"
Erica alijihisi raha sana kwavile alivyoambiwa na Erick, na jinsi alivyomshika ndio alijisikia furaha zaidi kisha wakaenda tena kula na walipomaliza walikaa kidogo na kwenda kulala.
Wakati wamelala kuna ujumbe uliingia kwenye simu ya Erick, ilikuwa ni usiku sana ila alichukua simu yake na kuangalia ule ujumbe akakuta umetoka kwa baba yake,
"Erick, siku hizi hurudi nyumbani unazamia kwa wanawake. Hao ni viumbe wa kupita tena hawana thamani kama wazazi yani unasahau mzazi sababu ya mwanamke? Sijapenda hilo swala kabisa, na umeishia wapi kuhusu swala la kuongea na Ester ili awe mama yenu Serious Erick usipofanya hivyo na mimi nitasahau kuhusu ubaba, yani hutomuoa huyo mdudu wako Erica"
Erick alisoma ule ujumbe wa babake mara mbili mbili ila aliona utamuumiza kichwa tu, hivyo alimsogelea vizuri Erica na kumkumbatia na kuendelea kulala.