Simulizi: Nini maana ya mapenzi

Simulizi: Nini maana ya mapenzi

SEHEMU YA 419

Erica alipeleka juisi sebleni ili Tumaini na Tony wanywe, halafu akawakaribisha, walipokuwa wakinywa ndipo Erica akauliza sasa,
"Eeeh kaka niambie, umefahamiana vipi na Tumaini?"
"Yani huwezi amini, Tumaini nilisoma nae shule ya msingi. Kipindi hiko alikuwa mwembamba ila nashangaa saivi kawa bonge"
Erica akacheka na kusema,
"Kipindi hicho ilikuwa utoto ila saivi ni ukubwa, ila huoni kuwa kapendeza"
"Ndio, amependeza sana yani leo nina furaha sana"
Erica akatania,
"Kwahiyo hadi umemsahau Doroth, na wewe na majina ya D sijui vipi!"
"Aaaah achana na hizo habari bhana, yule acha aende ila lengo la kuoa lipo kwenye akili yangu bado"
Erica akatania tena,
"Si umuoe Tumaini tu!"
Tumaini akacheka na kusema,
"Wewe Erica wewe sijui leo umekunywa nini jamani yani unaongea kama kitu gani vile! Sasa Tony anioe mimi kweli wakati ana mwanamke wake!"
"Lakini kumbuka huyo mwanamke wake hamtaki tena"
Tumaini akacheka tu, halafu Tony akaongezea
"Erica mambo ya Tumaini na mimi hebu yaache kwanza. Ila Tumaini ndio unaishi hapa?"
"Hapana hapa nimekuja tu kumtembelea Erica"
Ilibidi Tony amuulize vizuri dadake ambaye aliamua kumueleza ukweli tu,
"Kwahiyo Tumaini ni dada wa Erick?"
"Ndio, ni ndugu yake"
"Sasa Tumaini, hapa leo tutaondoka wote ili nikapafahamu kwenu au unasemaje?"
"Hakuna shida"
Na kweli pale waliongea weee na muda wa kuondoka ni Tumaini na Tony waliondoka pamoja.
Jioni ilipofika alirudi Erick ambapo alipopumzika kidogo tu Erica akaanza kumueleza yaliyotukia siku hiyo ila tu hakuweka ile sehemu ya kusema na Doroth, alieleza tu kuwa kakake alifika na kaonana na Tumaini na ilivyokuwa kwenye maongezi,
"Kheeee Tumaini alikuja hapa kumbe! Kweli dadangu kabadilika jamani!"
"Hadi nilishangaa ila sijaweza kuongea nae chochote maana ndio kaka yangu alifika"
"Kwahiyo inaonyesha wamepatana sana eeeh!"
"Ndio sana, yani sijui kama hawajatongozana wale maana macho yao tu yalionyesha wanatakana"
"Hahaha Erica bhana, muache dada yangu nae apate mpenzi maana sijui kama ana historia ya kupata mpenzi"
"Unadhani kwanini?"
"Nafikiri ni muonekano wake, yupo serious sana labda ndio sababu ya vijana kuogopa kumtongoza na hata hivyo nadhani wanaojaribu huwa anawajibu vibaya sana maana yule kajengewa dhana mbaya na mama yake kuwa wanaume ni viumbe wabaya, si unajua mamake alitendwa na baba ila kwa jinsi sisi tunavyopendana ndio na yeye ameona radha ya mapenzi, kwa maana hiyo kama huyo Tony atakuwa na lengo kweli basi atamkubali"
"Mmmh hivi itakuwaje, mimi na wewe halafu Tumaini na Tony!"
"Aaaah hizo habari tuziache Erica maana watajuana wenyewe, sisi tujali tunavyopendana tu"
Kisha Erick akamsogelea Erica na kumkumbatia, ambapo Angel nae alitoka chumbani na kukumbatiwa pamoja nao.
Kisha walienda kula, wakati wanakula simu ya Erica tena ikaita na mpigaji alikuwa ni mamake, Erica akawaza kuwa muda huo mamake anataka kusema kitu gani, akaacha kula na kuinuka kisha akapokea ile simu na kuongea nayo,
"Erica, nakupa wiki moja uwe umeleta hayo matendegu yako nyumbani, wewe mtoto usitake kunipanda kichwani. Narudia tena, nakupa wiki moja, siwezi kuendelea kuvumilia huo ujinga unaofanya"
"Lakini mama"
"Hakuna cha lakini, nishasema nimemaliza kwakweli maswala ya lakini sitaki kuyasikia, mwambie huyo huyo mjinga mwenzio lakini sio mimi. Nimemaliza"
Simu ikakatika ila Erick alikuwa nyuma ya Erica yani muda alivyoinuka kuipokea ile simu na Erick nae aliinuja na kusimama nyuma yake, alimkumbatia kwa nyuma kama kumbembeleza,
"Usijali Erica, usiwe na mawazo wala presha. Wala hiyo wiki haitafika kwani mimi nitahakikisha tunaenda kufanya taratibu zote kwenu"
"Na kwenu je watakubali?"
"Usijali kuhusu kwetu maana mama anakaribia kurudi, na nikimwambia swala la wewe kuwa mjamzito ni lazima ataomba mwenyewe kuwa akaongee na mama yako. Wakiongea wamama watupu najua kuna uelewa utakuwepo yani hata usihali mpenzi wangu"
Erica alijihisi raha sana kwavile alivyoambiwa na Erick, na jinsi alivyomshika ndio alijisikia furaha zaidi kisha wakaenda tena kula na walipomaliza walikaa kidogo na kwenda kulala.
Wakati wamelala kuna ujumbe uliingia kwenye simu ya Erick, ilikuwa ni usiku sana ila alichukua simu yake na kuangalia ule ujumbe akakuta umetoka kwa baba yake,
"Erick, siku hizi hurudi nyumbani unazamia kwa wanawake. Hao ni viumbe wa kupita tena hawana thamani kama wazazi yani unasahau mzazi sababu ya mwanamke? Sijapenda hilo swala kabisa, na umeishia wapi kuhusu swala la kuongea na Ester ili awe mama yenu Serious Erick usipofanya hivyo na mimi nitasahau kuhusu ubaba, yani hutomuoa huyo mdudu wako Erica"
Erick alisoma ule ujumbe wa babake mara mbili mbili ila aliona utamuumiza kichwa tu, hivyo alimsogelea vizuri Erica na kumkumbatia na kuendelea kulala.
 
SEHEMU YA 420


Kulipokucha Erick alijiandaa kwenda kwao ila hakuweza kuondoka mapema maana kuna mambo alikuwa akipanga na Erica, kwahiyo alipomalizana nae alipita kuyakamilisha kisha ndio akaenda kwao kutokana na ujumbe ambao baba yake alimtumia usiku kwani alijua kinachomsumbua babake pengine ni zile milioni tatu kwahiyo alitaka akaongee nae na amkabidhi pesa yake.
Alifika kwao na kumkuta dada yake, ingawa alienda kwenye mida ya saa tano asubuhi ila alimkuta dada yake yupo siku hiyo wala hakwenda dukani na alionyesha kuwa na furaha sana kupita siku zote, alimsalimia na kuanza kumuuliza
"Kwanza kabla ya yote, mbona unafuraha sana Tumaini"
"Aaah kawaida tu"
"Mmmh sio kawaida jamani, hilo tabasamu zito hivyo silionagi ujue. Kuna kitu lazima kimekufurahisha"
"Hakuna kitu Erick, ni kawaida tu"
"Basi ngoja nikwambie jambo lingine, huyu mzee yupo kwanza?"
"Awepo wapo saa hizi? Kaondoka muda tu"
Basi Erick alimuonyesha ule ujumbe ambao ulitumwa na babake usiku, Tumaini alishangaa sana ila akamwambia jambo kakake,
"Hivi Erick, kwanini tusiende kwa yule mama na tumueleze kila kitu kuhusu baba yani tusimfiche kitu. Yule mama ana busara sana, kwa hakika atatushauri vizuri"
Erick aliafikiana na dadake kuwa waende kwa yule mama wakaongee nae.
Basi Tumaini akaenda kujiandaa ili waende kwa huyo mama.
Wakiwa njiani Erick alimuuliza dada yake,
"Na mbona leo hujaenda dukani?"
"Sasa Erick ningeenda tungewezaje kwenda huko?"
Kabla Erick hajasema kingine walimuona Dora njiani na kusimamisha gari kumsalimia na kuongea nae, Tumaini akatania,
"Nakuona mama yetu mdogo"
Erick akamuangalia dada yake kwa kuchukia kitu kilichomfanya Tumaini acheke sana, basi Dora akawauliza kuwa wanaelekea wapi, Erick akamjibu,
"Tunaenda kwa yule mwanamaombi"
"Aaaah nikajua mnaenda kwa Sia"
"Kufanya nini?"
"Jana nilimkuta huko baba yenu akidai kuwa Sia ana mimba yako ila nilimwambia ukweli kuwa mimba ya Sia ni ya mdogo wangu Steve"
Hapo Erick alitabasamu ba kujikuta akifungua wallet yake akatoa laki moja na kumpa Dora kisha akamwambia,
"Vizuri sana Dora, kuna watu kama wewe Duniani kwa kazi maalum kabisa, nakupongeza sana maana baba yetu anajua ukweli kwasasa"
Dora alipokea ile hela huku akitabasamu na kuwaambia kuwa wamsalimie mama wa maombi. Kisha Erick na Tumaini wakaagana nae na kuondoka zao.

Walifika kwa mama wa maombi na kumkuta ameshika kitabu cha nyimbo, akiimba imba, walimsalimia na kuanza kuongea nae.
Tumaini alimueleza kila kitu huyo mama hadi kuhusu baba yao kumtaka Erica na kumfumania akiwa na Dora, yule mama alisikitika sana na kuwaambia,
"Baba yenu anatakiwa kuwa makini sana, kuwa na pesa sio kila kitu katika maisha kwani kwenye maisha kuna kitu kinaitwa furaha je baba yenu anahangaika na wanawake mbali mbali, swali ni je ana furaha? Furaha hana ila amejaa laana na machozi ya wanawake mbalimbali, mama zenu kawazalisha na kuwaacha unadhani ni kiasi gani wamelia kuhusu yeye? Ngoja nikwambie na wewe Erick, usiache chozi la mwanamke litoke sababu yako maana utajiona huna furaha kamwe sababu ya chozi la mwanamke, baba yenu sikumkubali toka enzi hizo sababu ya matendo yake, alijivuna kuwa kwao wanapesa nyingi, aliwadharau wengine na kusahau kuwa yale ni maisha tu na yanapita. Hiyo ni sababu kubwa ya mimi kutokuwa na baba yenu"
"Sasa katupa mtihani kuwa eti wewe ukubali kuwa nae halafu ndio atamruhusu Erick kuoa"
"Yani hata msipate shida wanangu, mwambieni baba yenu nimekubali halafu mwacheni aje niongee nae nahitaji kumfundisha. Asifanye makosa aliyoyafanya, kashamaliza wanawake wengi, achukue kati yao aoe sio anataka tena mwanamke mpya"
Tumaini akamuuliza huyu mama swali,
"Ila inaonyesha una uelewa mkubwa sana, hivi mapenzi ni nini?"
Erick alicheka sana maana alihisi kuwa dadake kuna mtu kashapendana nae ndiomana anaanza kuuliza kuhusu mapenzi,
"Sasa mkitaka niwafundishe vizuri hiyo mada mnifate kwa muda mwingine ila mapenzi ni mazuri sana mkipendana"
"Na unajuaje kama ndio mnapendana?"
Erick alimkatisha dada yake,
"Si amesema tuje siku nyingine dada! Nitakuleta usijali"
Basi wakamuaga akawafanyia maombi pale na kuondoka, walipokuwa kwenye gari Erick alimuuliza dada yake,
"Kuna mahali umependa nini dada?"
"Wewe nae hebu achana na hayo maswali (kuna mtu alimuona njiani na kumwambia Erick) Hebu simama, yule kijana namjua"
Erick alisimamisha gari na Tumaini kufungua kioo na kumuita,
"Derick"
Alikuwa ni Derick yule ndugu wa Erica ila alionekana kama hasikii vile, ikabidi Erick apige honi ndio akageuka kisha Tumaini akashuka na kuonana nae, walimsalimia na kumpa lifti ila Derick alionekana kutokuwa na furaha kabisa hata Tumaini alishangaa sana kuwa Derick aliyemzoea kapatwa na nini, ila hakuelewa kwakweli. Walifika mahali ambapo Derick alisema anashuka na kumshusha kisha Erick alimpeleka dadake nyumbani na kumshusha halafu yeye akarudi kule alipokuwa akiishi na Erica.
Alifika nyumbani na kumkuta Erica yupo nje anacheza cheza na Angel.
Basi akapaki gari yake na Erica alisogea karibu na kumsalimia kisha akamwambia,
"Bora umerudi mapema, hakuna mboga leo Erick?"
"Si ungenipigia tu simu"
"Simu yangu sijaweka salio"
"Basi tusiongee sana, twende tukanunue hiyo mboga"
Erica alisogea kwenye nyumba yao na kufunga milango kisha akaelekea na Angel kwenye gari ambapo alikaa naye mbele.
Walifika na kununua mboga wanayotaka kisha kuanza safari ya kurudi.
Wakati wanarudi Angel aling'ang'ania kukaa kile kiti cha nyuma ikabidi Erica amuweke kile kiti cha nyuma.
Walipofika nyumbani wakati wanashuka kuna karatasi Angel alikuwa amelishika, Erica alilichukua na kulisoma kisha akashangaa sana na kumpa Erick, naye alishangaa pia, kisha Erica akasema
"Hili jina ni la ndugu yangu Derick, inamaana ana ukimwi? Limefika vipi huku?"
Erick alimueleza Erica jinsi walivyokutana na Derick hadi kumpa lifti kwenye gari,
"Itakuwa ndiomana hakuwa na furaha, labda ndio alitoka kupima"
"Si unaona ni tarehe ya leo, mmmh makubwa"
"Erica mke wangu, ukimwi unasambaa kwa kasi sana naomba uwe muaminifu"
"Mimi ni muaminifu Erick, nakupenda kweli"
Erick alisogea na kumkumbatia Erica kwa furaha kisha kuingia nae ndani.
 
Mpaka hapa sina la ziada tukutane kesho...... tukizimalizia sehemu chache za simulizi hii.

Endelea kuweka utabiri, zikifika tabiri 5 tofauti , kutakuwa na bonus 5, pengine tukaimaliza hiyo kesho 😂😂😂
 
Simulizi Zinazorushwa na BURE SERIES

1. Simulizi: Kurudi Kwa Moza
Bonyeza hapa chini kusoma
Simulizi: Kurudi Kwa Moza

2. Riwaya: Kasri ya Mwinyi Fuad
Bonyeza hapa chini kusoma
Riwaya: Kasri ya Mwinyi Fuad

3.Simulizi: Nini maana ya mapenzi
Bonyeza hapa chini kusoma
Simulizi: Nini maana ya mapenzi


4. Simulizi : Nguvu Ya Mapenzi
Bonyeza hapa chini kusoma
Simulizi : Nguvu Ya Mapenzi

5. Mkuki Kwa Nguruwe (Kisa Cha Kweli)
Bonyeza hapa chini kusoma

Mkuki Kwa Nguruwe (Kisa Cha Kweli)

💥💥💥💥NEW 💥 💥 💥 💥

6. RIWAYA: Sauti Yake Masikioni Mwangu
Bonyeza hapa chini kusoma
RIWAYA: Sauti Yake Masikioni Mwangu

7. NDOA ILIVYOTETERESHA IMANI YANGU (Kisa Cha Kweli)
Bonyeza hapa chini kusoma
NDOA ILIVYOTETERESHA IMANI YANGU (Kisa Cha Kweli)
 
Mpaka hapa sina la ziada tukutane kesho...... tukizimalizia sehemu chache za simulizi hii.

Endelea kuweka utabiri, zikifika tabiri 5 tofauti , kutakuwa na bonus 5, pengine tukaimaliza hiyo kesho [emoji23][emoji23][emoji23]
Simulizi nzuri sana mkuu. Ila kesho imeshafika
 
SEHEMU YA 421


Kesho yake wakati Erica ametulia akicheza na Angel, akapokea simu kwa namba ngeni na kupokea.
"Mimi Doroth nahitaji kuja kuongea na wewe"
"Karibu"
"Nitakuja na ndugu yangu"
"Karibu"
Erica alijua wazi kuwa Doroth anataka kuomba msamaha, basi akamuacha afike nyumbani kwake na akajua wazi anaenda na ndugu yake ili amsaidie kuomba msamaha.
Basi muda kidogo Doroth alifika nyumbani kwa Erica na kugonga mlango, basi Erica akaenda kufungua ila alipomuona Doroth alihisi tena kuchefuka, ila alichefuka zaidi baada ya kumuona mtu ambaye aliongozana na Doroth maana alikuwa ni meneja wa ile hoteli ambayo walimpa adhabu ya kuosha vyombo, Erica aliwaangalia kwa chuki na kusema,
"Kumbe nyie ni ndugu na wote mna roho mbaya, jamani hakuna mnachoweza kuongea nikawaelewa. Kwaherini"
Erica alifunga mlango wake na moja kwa moja alimpigia simu kaka yake Tony,
"Kaka yule mwanamke Doroth hakufai kabisa, ni mbaya na ukoo wake wote"
"Erica, kwanza huyo mwanamke nishamsahau uwepo wake kwasasa, wifi yako mwingine yupo"
"Yuko wapi? Ni nani?"
"Tulia tu utamfahamu"
Erica alijikuta akiwa na hamu sana ya kumfahamu huyo wifi yake mpya ila kaka yake hakumtaja kabisa zaidi ya kumfanya Erica kuwa na hamu ya kumfamu huyo wifi yake mpya.
Basi simu ilikatika na Erica kuendelea na mambo mengine, alishangaa muda huo akipigiwa simu na Derick, alishangaa sana na kupokea,
"Niambie Derick"
"Nahitaji kuonana na wewe"
"Kwema huko?"
"Nimekwambia nahitaji kuonana na wewe"
Kwajinsi Derick alivyokuwa anaongea Erica alihisi tu kuwa hakuna jambo jema pale kwahiyo akaamua kumgelesha,
"Njoo nyumbani kwetu utanikuta"
"Sitaki kwenu, nahitaji kuonana nawe sehemu nyingine"
"Mmmh wapi?"
"Hotelini"
"Kufanya nini?"
"Wewe njoo tu utajua huku huku"
"Wewe huna nia nzuri, unataka kunibaka eeeh! Maana ni ndugu yangu ila kutwa kucha unanitamani, unataka umuambukize nani maukimwi yako"
Derick alikata ile simu baada ya ile kauli ya mwisho, Erica aliona kamjibu sawa maana Derick huwa haaminiki kabisa.

Ilifika siku hiyo ambayo Tony aliwapigia simu nyumbani kwao kuwa anaenda kumtambulisha mchumba wake rasmi, mama yake alimuuliza sana
"Sio kimeo huyo?"
"Sio mama, ni mtu anayejielewa"
"Kama kimeo nadhani unanitambua vizuri maana nitamtimua"
"Sio kimeo mama"
"Haya mlete"
Kwahiyo siku hiyo hadi Mage alienda ili kumuona huyo mchumba wa Tony.
Muda ulipofika Tony alifika na mchumba wake, kwakweli mama yao alikuwa wa kwanza kuhamaki,
"Yani Tony mchumba mwenyewe ndio umemleta huyu Tumaini?"
Dada zake nao walitoka kumuangalia.


Muda ulipofika Tony alifika na mchumba wake, kwakweli mama yao alikuwa wa kwanza kuhamaki,
"Yani Tony mchumba mwenyewe ndio umemleta huyu Tumaini?"
Dada zake nao walitoka kumuangalia.
Bite alishangaa pia na kusema,
"Huyu si ndio dadake Erick, watoto wa yule mzee!"
Mama yao akajibu,
"Ndio mwenyewe na licha ya hivyo ni hana adabu huyu binti hata kidogo, nishawahi kumkuta akimpiga Erica sio mara moja kisa tu hataki mahusiano ya Erica na kaka yake, sasa na yeye ndio kafanya nini hapa kama sio ujinga jamani? Wewe Tumaini nilijua huna mpango wa kuwa na mwanaume maana ungekuwa na mpango basi usingekuwa hivyo ulivyokuwa yani ungejua kabisa usimtendee mwenzio"
Mage nae akaingilia kati,
"Kumbe mtu mwenyewe ndio huyu loh hata mimi simtaki awe wifi yangu, Tony huyu meanamke hatumtaki"
"Jamani hii familia sasa hapana jamani, mimi umri umeenda nitamuoa nani? Wengine nimeona pengine siwafahamu vizuri ila huyu Tumaini namjua vizuri hadi kwa mamake napajua alikuwa ni mwalimu wetu halafu leo mnanikatalia kweli? Jamani huyu Tumaini na Erica mbona wanapatana"
"Kama wanapatana, mwambie aje hapa mguu wake, mguu wa Erica. Halafu Tony mdogo wangu yanu Erica awe na kaka mtu na wewe uwe na dada mtu uliwahi kuona wapi hiyo?"
"Sema wewe Bite, yani hawa watoto wananiletea laana tu jamani utafikiri kuna jambo baya nilitenda jamani, yani kweli kabisa Erica na Tony wa kunifanyia hivi mimi! Mnaenda kuniletea wachumba kwenye maukoo yaliyotengwa huko, maukoo yenye laana. Baba yao hawa ni ana laana mpaka unyayoni sasa bila aibu na wewe umeenda kulivaa hilo furushi jamani loh!"
Bite akasema tena,
"Kwanza mwanamke mwenyewe hata haendani na wewe, mwanamke bonge utafikiri anakunywa mafuta"
Ile hoja ilionekana kumchukiza Tumaini na kujikuta akikimbia mahali pale, alitoka nje ya geti la kina Erica na kujikuta akimwaga machozi tu, yani kitu ambacho hakukipenda ni mtu kumsema sababu ya ubonge, yani hali ya kuwa mnene ilimfanya ajione kuwa na kasoro kubwa sana. Ila Tony nae akatoka kwani hakutaka kuendelea kusikiliza nyumbani kwao, alimkuta Tumaini akilia na kuamua kuondoka nae tu.
Pale ndani waliona bora kaondoka, wakarudi ndani wakiongea ila mama yao akawasema,
"Ila Bite sio vizuri kumsema yule sababu ya ubonge wake"
"Ila mama, si unaona kaondoka mwenyewe, mabonge wengi hawapendi kusemwa?"
Wakacheka kwa pamoja, ila Mage nae akasema,
"Lakini kumkataa mtu sababu ya maumbile yake sio vizuri, tuchukue sababu nyingine tu"
"Wewe nae lazima utetee maana ulivyojifungua tu ukabongeka"
"Ila mama, mbona hata wewe sio mwembamba jamani!"
"Hujaona picha za usichana wangu, nilikuwa nadai mimi ila kuzaa nyie wote unafikiri mchezo na hata hivyo mimi nipo kawaida tofauti na yule Tumaini ila si vizuri kweli kumsema mtu sababu ya maumbile"
"Halafu tunampa mawazo Tony, alimleta Dora hapa yupo kawaida tu yani ni mwanamke aliyekamilika ila tukamkataa na sasa kamleta Tumaini naye tumemtaa sababu ya ubonge, nadhani haelewi kuwa sisi tunahitaji aoe mwanamke wa aina gani"
"Na wewe Mage hebu tulia, huyo Tumaini na Eeick nadhani humfahamu baba yao, ni katili huyo mzee balaa. Acha watoto wake waondoke maana ukoo wetu hauwataki"
Bite alihitimisha hivyo na wote wakacheka sana.
 
SEHEMU YA 422

Tony aliondoka na Tumaini hadi nyumbani kwakina Tumaini ila Tumaini hakuwa na raha kweli, Tony alimuomba msamaha,
"Nisamehe mimi Tumaini maana ndugu zangu hata mwenyewe sijapenda waseme vile"
"Kwahiyo ubonge wangu ndio tatizo"
"Ubonge wako sio tatizo Tumani na hujui tu jinsi gani nimeanza kukupenda tangia muda ila kwavile sikuhisi kama naweza kukutana na wewe ndiomana nikaonyesha nia ya kutaka kuoa wanawake wengine ila Tumaini upo moyoni na hujui tu ni jinsi gani nilivyokuona tena siku ile moyo wangu ulivyofurahi yani wewe ndio mke wangu hata waseme vipi"
"Wewe unasema tu, kwani nyie wanaume siwafahamu? Hakuna mwanaume anayependa mwanamke mnene, ndiomana sikutaka kujiingiza kwenye mahusiano"
"Basi Tumaini wewe ndio hujui, hakuna mwanaume asiyependa kuwa na mwanamke mnene sema ukiwasikia wanaongea utahisi hawapendi wanene ila wanawapenda balaa, wewe pita sehemu wamekaa wanaume wawili au watatu uone kama hawajageuka kukutazama wewe. Ila anaweza kupita mwanamke mwembamba na wasigeuke. Kiukweli Tumaini nakupenda sana na ninahitaji kuwa na wewe, nilipokwambia nahitaji uwe mke wangu nilikuwa namaanisha wala sijatania"
"Mimi sitaki tena kuolewa bora nikae hivi hivi mwenyewe"
"Tumaini jamani, hivi huoni raha ukitazama mapenzi ya Erica na Erick?"
"Wale wanapendana"
"Na sisi tunapendana Tumaini, nitafanya kila kitu ninachoweza uelewe ni jinsi gani nakupenda"
Tony alifanya kazi ya kumbembeleza Tumaini kwa muda huo kwani alihisi asipombembeleza basi atampoteza.
Alimbembeleza pale na mwisho wa siku Tumaini alikubali kwenda nae kwenye matembezi, hivyo waliondoka na kwenda kwenye matembezi.
Walifika kwenye hoteli moja wakiongea na kufurahi sana hadi Tumaini akaona ni vyema alivyokubali kwani aliweza kugundua ni jinsi gani Tony anampenda.
Muda ulivyoenda Tumaini akahitaji kurudi nyumbani, basi Tony akajiandaa kwaajili ya kumpeleka.
Wakati wanatoka pale hotelini wakakutana na Dora, waliangaliana nae ila Tony alitamani Dora asiongee chochote maana Tumaini ni mama kisirani, ila Dora kama kawaida yake kunyamaza haikuwezekana, aliwaambia
"Kheeee Tony upo na Tumaini kwasasa?"
Tony akawa kimya na kujiuliza kuwa Tumaini na Dora wamejuana vipi, ila Tumaini alielewa kuwa Dora amefahamiana na Tony sababu ni kaka wa Erica na yeye anaifahamu familia ya Erica kumbe aliwahi kuwa mchumba wake pia.
Tony akaona asimjibu Dora tu, hivyo akamshika mkono Tumaini na kuondoka nae.
Dora alicheka sana,
"Hata msiponijibu nimewabamba"
Akawaangalia na kuwaacha waondoke. Akasogea sehemu ya kukaa pale hotelini na kukaa kwani kuna mtu alikuwa akumsubiri ila kuna mawazo yalimjia kuwa ndugu wa Erica walimkataa kuwa asiolewe na Tony, vipi kuhusu Tumaini? Na pia akawaza kuwa lazima Erica hajui, akaamua kumpigia simu
"Erica, kuna umbea ninao na unaniwasha sana"
"Ushaanza na mambo yako Dora"
"Naomba unielekeze kwako nije kukupa huo umbea"
"Wewe nae huachi loh!"
Basi Erica akamuelekeza na kuagana nae.

Erick akiwa kwenye shughuli zake, akapigiwa simu na baba yake kuwa aende ofisini kwake, ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Erick kufika kwenye ofisi ya baba yake, yani alipoingia wengi mabinti wa pale walionyesha kuvutiwa nae, basi akaenda kuonana na baba yake.
"Unajua nilichokuitia hapa Erick?"
"Sijui baba"
"Kwanza kazi niliyowapa mmeishia nayo wapi?"
Erick alimueleza baba yake kuwa yule mama amekubali na anahitaji waende kuonana nae, mzee Jimmy alionekana kutabasamu tu kwa ujumbe aliopewa na mwanae, baada ya hapo alimruhusu kuondoka,
"Mmmh baba, kwahiyo hii ndio sababu pekee uliyoniitia?"
"Ndio hiyo hiyo, hakuna lingine"
Ila Erick alikuwq na mashaka sana kwani kwa kipindi hiko alikuwa hamuamini baba yake kabisa kabisa, sasa wakati anatoka pale kuna binti alimuita Erick basi Erick alienda kumsikiliza,
"Samahani, hapo nje kuna vijana wanaonyesha wapo kukufatilia maana nimeona wana picha yako"
Akili ya Erick ilicheza haraka haraka na kuhisi kuwa huenda baba yake amemuita hapo ili kumlaghai halafu watu wamfatilie na wajue anapoishi, basi akamshukuru yule dada na kutoka na wakati anaondoka alihisi kabisa kuna watu wanamfatilia akaamua muda huo aende moja kwa moja nyumbani kwao ili kuwapoteza uelekeo kabisa.
Alifika nyumbani kwao na moja kwa moja kwenda chumbani kwake, alipekua ile bahasha ambayo aliipata mlangoni kwakina Erica kwani alijua ndio posa inayomuumiza baba yake, akaenda chumbani kwa babake na kumuwekea kitandani ili akifika tu aione, kisha akarudi chumbani kwake kwani alijua angetoka muda huo basi wale watu wangeendelea kumfatilia.
Alipokaa kwao, kwenye mida ya saa moja na nisu usiku alifika dada yake alisikia kama amefika na mwanaume maana alisikia sauti ya kiume ila wakati anatoka huyo mwanaume alikuwa kaondoka, alimsalimia dadake na kumuuliza,
"Ulikuja na nani Tuma?"
"Mmmh mbona nimerudi mwenyewe tu"
"Ulienda dukani leo?"
"Hapana sijaenda ila walifungua duka"
"Vipi wewe mpaka muda huu upo nyumbani, na Erica umemuacha na nani?"
Erick alimueleza baba yao alivyomuita kazini kwake na kusema kuhusu watu wanaomfatilia,
"Mmmh au ndio ile gari nyeusi niliyoiona imesimama pembeni ya nyumba yetu?"
"Khaaaaa kumbe wapo mpaka muda huu, ndio hao hao wananifatilia"
"Erick, wewe ni mwanaume hebu achana na kuogopa"
"Usidhani naogopa bure, ila sitaki wale wapajue ninapoishi na Erica, wakienda kumbaka mke wangu je! Baba mwenyewe hana nia nzuri"
"Sasa na huu usiku umemuacha mwenyewe akiingiliwa je utamlaumu nani?"
"Kwahiyo unanishauri nini Tumaini?"
"Erick, kama hela unayo kwanini usiweke mlinzi nyumbani kwako? Tena mwambie Erica, sio amkaribishe kila mtu ndani, yani awe anauliza kwanza kabla ya kumkaribisha."
"Umenishauri jambo jema, ngoja nifanyie kazi swala hilo. Ila kwa leo inabidi nifanye njia ya kutoka bila hawa kutambua"
"Ngoja nikwambie kitu, nipe funguo ya gari yako halafu mimi nitoke na gari yako wanifatilie mimi niwapoteze wakati huo na wewe utoke na gari yangu uende nayo kwako maana hakuna namna zaidi ya hivyo"
Erick aliona ushauri wa dada yake ni mzuri sana, hivyo akaona aufanyie kazi muda huo huo sababu muda ulienda sana.
Kwahiyo muda huo Tumaini alienda kuoga na kubadili nguo kwanza kisha kufanya kile walichopanga na kaka yake.
 
SEHEMU YA 423

Erica alimsubiria Erick siku hiyo na kuanza kuhisi vitu vingine kuwa pengine Erick kaenda kwa wanawake, akajikuta akiumia sana moyo na kukumbuka maneno ya mama yake kuwa usimuamini sana mwanaume kwani anaweza kubadilika muda wowote, aliwaza sana
"Yani kweli Erick inawezekana kaenda kwa wanawake wengine kweli! Si huwa anasema ananipenda, huu ndio upendo kweli?"
Alikuwa akiangalia mida tu inavyoyoyoma na kuzidi kumkosesha raha kabisa, alipoona saa nne ndio akazidi kukosa raha yani siku hiyo hata chakula hakikupanda kabisa, kwahiyo hakula.
Kwenye mida ya saa tano, alijikuta akianza kulia kwa uchungu alioupata moyoni mwake, muda kidogo akisikia mlango ukigongwa akafuta machozi yake na kwenda kufungua, aliyeingia alikuwa ni Erick ila Erica hakumfurahia kama siku zote naye Erick alitambua hilo, akaenda kumfata alipokaa maana alimfungulia tu na kwenda kukaa, Erick alimuuliza
"Tatizo nini Erica? "
"Hakuna tatizo, usinifiche tafadhari mpenzi wangu, hebu niangalie kwanza"
Alipomtazama Erick alogundua kuwa Erica alikuwa akilia sana maana hata machozi bado yalimtoka, alimsogelea na kumuweka karibu yake huku akimwambia taratibu,
"Mpenzi nadhani unanifkkiria bibaya, ila sio kosa lako ni sababu unanipenda sana ila usifikirie kama naweza kukufanyia kitu kibaya kama hiko. Erica una mimba, ni mtoto wetu huyo tambua unapolia na mtoto nae analia yani unamsononesha mtoto. Ni kweli nilikuwa muhuni sana, nilihangaika na wanawake ila sababu nilikuwa nakuhitaji wewe, na sasa nimekupata nihangaike tena na wanawake wa kazi gani? Erica unanitosheleza, umenipatia mtoto mrembo Angel na sasa unaenda kuniletea mdogo wa Angel, nihangaike na wanawake wengine nataka nini? Nataka laana au kitu ganu? Erica nakupenda sana"
Yale maneno ya Erick yalimuingia akilini Erica na kuona hakupaswa kulia ila kumuuliza kuwa Erick amechelewa wapi, baada ya hapo Erick alimueleza Erica ilivyokuwa hadi kumfanya yeye kuchelewa.
"Basi siku nyingine uwe unanipigia simu kunipa taarifa?"
"Nisamehe kwa hilo mpenzi hata sijui nilipitiwa na kitu gani. Nisamehe tafadhali"
"Nimekusamehe usijali"
"Cheka basi Erica nione kweli umenisamehe"
Erick alianza kumtekenya tekenya Erica ili afurahi tu kama siku zote, Erica nae alianza kucheka na kusahau kila kitu.
Basi Erica na Erick wakafurahi pamoja yani walienda kulala wakati tofauti zao zimeisha.
Kulipokucha asubuhi kabisa, simu ya Erick ilianza kuita, alipoichukua kuangalia alikuta ni babake ndiye anampigia simu, basi akaipokea na kuanza kuongea nayo,
"Erick, wewe ndio uliingia chumbani kwangu?"
"Ndio baba"
"Kwahiyo Erica amekupa hii bahasha uniletee huoni kama ni udhalilishaji huo?"
"Baba, hiyo bahasha hajanipa Erica ila nilikuwa nayo mwenyewe niliipata mlangoni kwakina Erica"
"Sikuelewi, hebu leo uje ofisini kwangu tena"
Erick alimuitikia babake ila kiukweli hakuwa na mpango huo hata kidogo.
Basi akiamka na kujiandaa kutoka kwani kwa kipindi hiko kuna mambo aliyokuwa akiyafanya sababu aliona kashayaanza majukumu.

Leo Erica akiwa ametulia kwake alipigiwa simu na rafiki yake wa muda, alipigiwa simu na Fetty na ilionyesha kuwa Fetty anahitaji kuonana nae, ikabidi amuelekeze alipo ili afike na waonane na kuongea.
Na muda kidogo Fetty alifika maeneo yale, alimkaribisha na kuingia ndani huku wakiongea mambo mbalimbali, kisha Fetty akamueleza rafiki yake lengo la kuntafuta,
"Yani Erica, nimekutafuta ili nikwambie kuwa nimepata mchumba na ana lengo la kunioa"
"Hongera sana, na mbona umenitafuta mimi namfahamu?"
"Unamfahamu ndio, tumesoma nae chuo ni yule George aliluwa mwaka wa tatu wakati tupo mwaka wa kwanza"
Erica alishtuka kidogo kwani huyu George alitambua vilivyo ila hawezi kumwambia rafiki yake kuwa George amewahi kuwa nae, zaidi ya kumponheza tu
"Hongera Fetty, kwahiyo harusi lini?"
"Aaah bado kidogo tu ila nimegoma kukutana nae kimwili hadi tutakapooana"
Muda huo alifika Dora na kugonga kwahiyo Erica alimkatibibisha na Fetty alishangaa sana kuona kuwa Erica bado ana urafiki na Dora, baada ya salamu kumbe Dora alisikia pale mwishoni wakati Erica akiongea na Fetty na kuuliza,
"Jamani kabla hamjaendelea na mada yenu au kuiacha kabisa sababu yangu, nimesikia mkiongelea kidogo. Ngoja niwaulize, hivi ni mwanaume gani siku hizi anayevumilia mpaka ndoa ndio mfanye?"
Fetty alijibu kwa kujiamini kabisa,
"George wangu huyo ndio anaweza kuvumilia nadhani Unamfahamu"
"George yule yule tuliyesoma nae chuo, alikuwa sijui kiongozi wa nini wakati tupo mwaka wa kwanza alikuwa mwaka wa tatu? "
"Ndio huyo huyo"
"Hongera ila kwa George yule akuvumilie hadi ndoa hiyo haipo yani hata atakubaka"
"Mmmh jamani"
"Sikutishi ila kabla ya yote nenda mkapime mjue afya zenu, usibabaishwe na mwili wa mtu kuwa ni mzima. Ukimwi umekaa sehemu mbaya sana yani sehemu inahopendwa na wengi, nakuomba ukapime kwanza na George. Au hnamuamini sana?"
"Hamna ila sikuwa na wazo hilo la kupima, umenishauri vyema asante"
"Natakiwa nikushauri hivi maana yule George alikuwa anatafuta bikra, kwa mantiki hiyo unafikii kupitia wasichana wangapi? Au Erica hujamwambia mwenzio kuwa hadi wewe umepitiwa na George"
"Mmmh na wewe Dora maneno yako!"
"Erica ugomvi wangu ni wako ni kwamba sikukwambia ukweli kuwa George amewahi kutembea na mimi, halafu wewe hnataka kumficha Fetty. Shoga wee huyo George unaotuona hapa kashatupitia mwenzangu, kapime nae tu. Sijasema umuache ila nimekwambia ukapime nae."
Kwakweli kwa maelezo haya tu Fetty alijihisi vibaya haswaaa kuwa mwanaume anayejivunia nae kumbe kashapita kwa anaowafahamu ila Erica alijaribu pale kumpa moyo sema ilionyesha kuwa imemuuma sana kwani muda huo huo akaaga na kuondoka.
Walibaki Dora na Erica basi Erica akamsema Dora kuwa alichofanya sio kizuri,
"Sio kizuri nini, kwanza nimemuokoa huyo rafiki yako kwani George ana tamaa sio mwanaume wa kuishi nae. Hivi karibuni tu nimempitia tena sijamuachia virusi kweli!"
Erica alimshangaa Dora maana aliongea swala la virusi kama ni swala la kawaida sana.
Kisha Dora akamuelezea Erica lengo lake la kumpeleka pale kuhusu mahusiano ya Tony na Tumaini.
"Mmmh sitaki useme chochote, nimekuletea ujumbe tu. Naondoka, kwaheri"
Aliinuka na kumuaga Erica kwahiyo Erica alipata jibu kuwa kutoka kwa Doroth basi kaka yake amepata nafasi ya kuwa na Tumaini ila hakuchukia zaidi zaidi alitabasamu tu.

Rahim hakuweza kumwambia chochote mke wake ila aliona kuwa siku ya leo ni njema kama atampeleka mke wake matembezi kidogo ili mke wake afurahi pia na yeye asahau swala zima la kupimwa na kukutwa na ukimwi, kwahiyo alimuambia mke wake ajiandae watoke wakatembee, kwakweli Salma alifurahi sana yani ile ilikuwa kama ndoto katika maisha yake yani aliona mambo sasa yanakuwa mambo, basi Rahim alienda kusafisha gari wakati kamuacha mke wake akijiandaa, kwakwelo hakuacha kumpigia simu yule mama kumpa shukrani,
"Yani mama yangu sijui nikushukuru vipi, mume wangu hata mara moja hajawahi kusema kuwa tukatembee yani hata mara moja hajawahi ila leo nimeshangaa yani toka jana mume wangu ni mpole hataki tena kumtaja Zainabu na kaniambia leo twende tukatembee yani kama naota vile"
"Mwanangu endelea kufurahia ndoa ambayo ipo katika hali ya ukweli, hata usijali yani mimi ndio mwisho mwanangu hakuna aliyepitia kwangu akaachwa, yani mimi ndii kila kitu"
"Asante mama yangu, zawadi yako bado ipo nitakuletea mama maana umenifanya niwe mpya katika ndoa yangu"
Basi akaagana na huyu mama kisha akaendelea kuvaa na kumvalisha mtoto, Rahim aliporudi kitoka kuosha gari Salma alishangaa kuona Rahim karudi na kopo la maziwa, akamkabidhi mke wake na kumwambia amkorogee yale maziwa
"Nimkorogee ya nini mume wangu wakati tunaenda nae"
"Hapana tutamuacha kwa mama, nahitaji tukafurahi mke wangu bila ya kusumbuliwa na kitu chochote kile"
Ilibidi Salma akubali na kumkorogea mwanae maziwa na alipomaliza walienda kumuacha kwa mama yao kama walivyopanga kisha wao kuondoka.
Kwakweli leo Salma alishangaa sana maana Rahim alimpeleka mahali mbalimbali na mwisho wa siku alimpeleka hotelini ili wapate chakula cha jioni, huko aliongea nae mambo mengi sana
"Salma, nahitaji umuachishe mtoto ziwa"
"Mbona mapema sana, atakunywa nini?"
"Utaniambia maziwa yoyote mazuri ya kopo nimnunilie ila ziwa lako aache"
"Jamani kwanini Rahim wakati hii ni haki yake?"
"Salma, nahitaji maziwa yako niyamiliki mimi. Sasa nitatumiaje mimi na mtoto? Kama unahitaji apate maziwa yako basi nakununulia mashine ya kukamulia maziwa yani awe ananyonya maziwa ya kukamuliwa ila asinyonye hapo kutoka kwako"
Salma alihisi ni upendo umezidi kwa Rahim kiasi kwamba anaonekana kumuonea wivu mtoto kumbe mwenzie anajua kiwa atakuwa kashamuambukiza ukimwi kwahiyo anaangalia jinsi mtoto wao asipate ukimwi, Salma hakuelewa kabisa yani yeye alijua ni mapenzi tu.
 
SEHEMU YA 424

Leo Erick alimpata mlinzi aliyekuwa anamuhitaji na akaanza safari ya kurudi nae nyumbani, wakiwa kwenye gari yule mlinzi aliongea,
"Yani wanawake ni vuruga, mimi mapenzi yamenivuruga hadi nimezeeka hivi"
"Kwanini unasema hivyo?"
"Yani mwanamke ukimkuta kazaa ni shida haswaa"
"Kwanini?"
"Huwa wanawake hawawasahau wanaume waliozaa nao, unaweza kumpa kila kitu ika mawazo yake ni kwa mwanaume aliyezaa nae tu. Na wakikutana wanarudisha majeshi hapo unakuwa umeliwa"
"Yashawahi kukukuta nini?"
"Mpaka nimesema yamenikuta, yani mimi hadi niliishi na yule mwanamke ila siku niliyomshangaa ni aliponiambia anarudi kwa baba watoto wake dah niliumia sana, toka hapo mapenzi siyataki tena bora nilinde watu tu ila mapenzi hapana kwakweli"
Erick alifikiria kwa upande wake akaona hiyo haipo sababu Erica alisema wazi kuwa Rahim hakumpenda.
Basi aliwahi kurudi nyumbani, na yule mlinzi wa kuwalindia sehemu ile na kumwambia Erica,
"Nimekuja na mlinzi"
"Sasa mlinzi wa nini jamani Erick?"
"Kwasasa huoni umuhimu wake ila ipo siku utaona umuhimu wa kuwa na mlinzi mahali hapa, ninakujali, nakupenda na sipendi upatwe na jambo baya kwaajili yangu. Kwasasa atakuwepo mlinzi mahali hapa wakati nashughulikia mahali ambako patakuwa na usalama zaidi kwetu."
"Sawa nimekuelewa"
Kisha Erick alimuomba Erica kuwa siku hiyo waende kula hotelini, Erica alikubali na kwenda kujiandaa huku akimuandaa na mtoto pia, wakati huo Erick nae alioga na kubadili nguo ili waondoke wakiwa wasafi.
Waliondoka na kwenda kwenye hoteli ambayo haikuwa mbali sana na pale kwao, waliagiza chakula kisha Erick aliongea na Erica
"Unajua toka tupate matatizo basi muda wa kukaa chini na kupanga kuhusu maisha yetu umekuwa mdogo sana, mwanzoni ilikuwa najiona mwanaume ila sasa ndio nimekuwa mwanaume wa ukweli maana nimeyatambua majukumu ya mwanaume katika dunia hii"
Erica alicheka tu, chakula kilifika na walianza kula, wakati Erica anatazama meza ya pili akajikuta akiangusha hadi kijiko cha chakula kwani alionana na Rahim macho kwa macho, aliogopa ila muda huo Rahim na mke wake walikuwa wanainuka maana walimaliza kula pia kwahiyo alipomuona Erica akaona ni vyema kwenda kumsalimia.
Erick alikuwa akimshangaa Erica na kumuuliza,
"Nini tatizo, mbona umeshtuka hivyo?"
Erica alikuwa kimya tu na kumfanya Erick ageuke, akamuona Rahim akiwa ameongozana na mwanamke wakienda mahali pale, alijua ni kwanini Erica ameshtuka kwahiyo nae alijipanga pale ikiwa Rahim angeleta fujo, ila walishangaa Rahim akifika pale huku akiwa mpole kabisa na kuwasalimia kipole huku akisifia kuwa wamependeza kukaa na mtoto pale, alimsogelea Angel na kumwambia,
"Niamkie baba yako Angel"
"Taki"
Kisha Angel akainuka na kwenda mwilini mwa Erick, kitendo kile kilimuuma moyo sana Rahim ila hakusema jambo lingine la ziada zaidi ya kuwaaga tu na kuondoka, kwakweli walimshangaa sana na hawakuongelea habari zake kabisa hadi wanarudi nyumbani, ni Erica alianza kuuliza
"Mbona Rahim kawa mpole vile?"
Erick akasema,
"Sasa unamuuliza nani?"
"Basi samahani yaishe, nilikuwa najiuliza tu"
"Ndii jiulize mwenyewe si ndio unamjua yule! Pengine unaweza kujua ni kwanini amekuwa mpole vile"
Erica akaamua kunyamaza ili kuepusha shari kwani alimuona dhahiri Erick kuwa na chuki na Rahim, pengine sababu amezaa na Rahim maana Erick aliinekana kumchukia kweli tangu ameujua ukweli.
Ericq hakuongea tena jambo na kwenda kulala tu na mwanae, hali ile hakuipenda pia Erick ila alihisi huenda Erica ameanza kumkumbuka Rahim basi alimuacha tu alale bila kumsumbua ila moyoni mwake aliumia sana wakati huo huo Erica nae anaumia moyoni kuwa kwanini siku hiyo hajabembelezwa na Erick.
Kulipokucha kama kawaida, Erick alijiandaa na kutaka kuondoka ila akafikiria kuhusu Erica na kujisemea,
"Najua sasa ataanza kuniwaza mimi sababu kabeba pia mtoto wangu, ngoja niachane na mawazo ya yule mlinzi"
Basi alimsogelea na kumbusu ambapo Erica alishtuka ila alitabasamu kuona Erick amembusu, kisha akamwambia
"Natoka Erica, ila kumbuka nakupenda sana"
"Nakupenda pia Erick"
Basi Erick alimbusu tena na kumuaga, kwa wakati huu Erica alisahau kabisa kama usiku wote kalala akiwa na mawazo tele juu ya Erick kutokumbembeleza.

Kwenye mida ya mchana, Erica akiwa ametulia nyumbani alipigiwa simu na Dora na kuipokea ile simu,
"Erica, nikwambie kitu"
"Niambie"
"Kuna yule mwanaume wako alikuwa anakuganda sana kipindi upo chuo. Huwezi amini leo kanitongoza"
"Nani huyo?"
"Si huyu Bahati, yani hapa napanga nae mipango ya kuvunja amri maana anaonekana ana uchu balaa"
"Dora hapana usifanye hivyo"
"Nisifanye hivyo kwanini na ananitaka mwenyewe!"
"Jamani Dora, kwani wewe unajiuza kusema kila anayekutongoza umkubali? Namjua Bahati, yani kama kakutongoza ni bahati mbaya, tafadhali usifanye nae chochote"
"Huo wivu sasa, unamuonea wivu wa nini wakati upo na Erick?"
"Hapana si wivu ila naomba nije kuongea nae kwanza, uko wapi nae tafadhali nakuja"
Dora akamtajia sehemu waliyopo, yani Erica alijiandaa haraka haraka na kumbeba mwanae. Akatoka nje na kukodi bajaji maana gari yake hakuichukua kwao wakati anaondoka.
Alienda hadi eneo alilisema Dora, ni kweli alimkuta na Bahati tena muda huo walikuwa wamesimama kama wanataka kwenda mahali. Erica aliita,
"Bahati"
Bahati aligeuka, kile kitendo cha Bahati kumuona Erica ikawa kama akili yake imerudi kwani alimuacha Dora pale na kwenda kumkumbatia Erica, kumbe Erick nae alikuwa eneo lile anapita ni Angel alimuona akaita,
"Baba"
Erick akageuka na kumuona Erica akiwa amekumbatiwa na Bahati, aliingiwa na chuki ya gafla kwavile huwa hampendi Bahati.
 
SEHEMU YA 425

Bahati aligeuka, kile kitendo cha Bahati kumuona Erica ikawa kama akili yake imerudi kwani alimuacha Dora pale na kwenda kumkumbatia Erica, kumbe Erick nae alikuwa eneo lile anapita ni Angel alimuona akaita,
"Baba"
Erick akageuka na kumuona Erica akiwa amekumbatiwa na Bahati, aliingiwa na chuki ya gafla kwavile huwa hampendi Bahati.
Erick alisogea karibu na kumvuta Erica pembeni, alimuangalia kwa hasira sana kisha akamnyanyua Angel na kumvuta Erica mkono hadi kwenye gari yake, akawapandisha humo naye kupanda na kuondoka zao, hakumsikiliza hata Dora anasema kitu gani maana Dora aliita ila Erick hakuitika sababu alikuwa na hasira zake.
Bahati alisimama akishangaa maana kitendo alichokifanya Erick kilikuwa cha haraka sana, Dora akacheka na kumfata Bahati,
"Unajiachia tu kukumbatia wake za watu, siku moja umkute Erick kashika bastola wewe angekufyatua"
Ila bado Bahati alikuwa kama na bumbuwazi vile, Dora alimwambia tena,
"Eeeh si tulipanga tunaenda kulala, twende basi"
"Ulipanga na nani kwenda kulala?"
"Wewe hapo, unajisahaulisha eeeh! Sababu tu ulimuona Erica."
"Sijapanga na wewe kitu chochote"
"Kheee makubwa haya, kwahiyo Erica kakusahaulisha kila kitu"
"Cha kunisaidia naomba namba ya Erica"
Dora alimtajia Bahati namba ya simu ya Erica, kisha Bahati akamuomba pia Dora na namba yake ambapo Dora alimpa pia na baada ya hapo Bahati akaenda kupanda gari yake na kuondoka.

Walifika nyumbani na kuingia ndani, Erica alikaa sebleni ila Erick alifunga mlango wa sebleni na kuwasha katuni ili Angel aangalie na kweli alitulia akiangalia, kisha akamshika Erica mkono na kwenda nae chumbani na kumkalisha kitandani kisha akasema,
"Yani ningekuwa mtu wa kupiga basi leo ningekuchakaza maana ningekupiga hadi usahau jina lako, unajua ni kwajinsi gani namchukia yule mtu halafu wewe unatoroka nyumbani kwenda kukumbatiana nae"
Erica aliongea kwa uoga,
"Nisamehe Erick"
"Kitendo cha kuja nawe hadi nyumbani ni wazi nimekusamehe. Na nimekusamehe sababu moja tu, sababu wewe ni mke wangu. Mke hapigwi wala hasemwi hadharani ndiomana nikakuleta nyumbani tena chumbani ili niongee na wewe, kuna mambo Erica siyapendi. Unapokuwa na mimi kuna mambo unatakiwa kuacha, mfano urafiki na Dora siutaki yani sitaki kabisa Dora awe rafiki yako. Na watu kama yule Bahati sijui Rahim fanya kama hawajawahi kutokea katika maisha yako hata kama kuna vitu unahusika nao kwa ufupi ukaribu na watu wa ajabu sitaki"
"Nisamehe mpenzi"
"Huo wimbo nimechoka nataka wimbo mpya. Sasa ukinikosea unajua msamaha unatokaje?"
"Sijui"
"Erica, sikia licha ya kukupenda sana na najua wazi una mimba yangu ila bado niliheshimu msimamo wako kuwa tusikutane tena kimwili mpaka tuoane, leo navunja neno hilo Erica, labda ndio kitu kinafanya uwakumbuke wakina Bahati. Haya msamaha wangu unatoa kwa kunipa penzi"
Erica alijikuta akimuangalia kwa aibu sana Erick ila muda huo huo Erick alisogea na kuanza kumpapasa na mwisho wa siku kuangukia kwenye mapenzi.
Kisha usingizi mzito ukawapitia, walikuja kushtuka baada ya kusikia sauti ya Angel ikiwagongea mlango huku akiita mama, baba.
Erica aliinuka na kwenda kumfungulia mtoto ambapo ilibidi ampe chakula kisha akamuogeshe na Angel akalala.
Muda huo Erick alikuwa amekaa tu, Angel alipolala tu Erick akamwambia Erica
"Na mimi leo nataka uniogeshe"
Erica alitabasamu tu na kuamua kwenda kuoga na Erick kisha kwenda pamoja kula na baada ya hapo walikaa pamoja wakiangalia taarifa ya habari.
Mara simu ya Erica ikaanza kuita, Erick akasema,
"Nipe hiyo simu Erica, kwasasa tumekuwa mke na mume rasmi, tumejialalisha wenyewe kwahiyo tu mwili mmoja na mimi ndio kichwa cha familia, lazima nijue ni nani anayekupigia muda huu mke wangu na anataka nini"
Ile simu iliita wee hadi kukatika, ikaanza kuita tena ikabidi Erica amkabidhi ile simu Erick.
Akaiangalia namba ngeni ila akaipokea na kuongea nayo,
"Hallow, unataka nini kwa mke wangu."
"Kumbe Erica kaolewa kweli?"
"Wewe ni nani?"
"Mimi Bahati"
"Sikia usimsumbue mke wangu kwaheri"
Erick akakata simu, ila muda kidogo uliingia ujumbe kwenye simu ile, Erick akaufungua, ulitoka kwenye ile ile namba ya Bahati,
"Erica, unampa simu apokee mwanaume kweli! Hata hivyo bado nakupenda tena sana, hata kama kwenu umehama nitamwambia rafiki yako anilete"
Erick alimuangalia Erica na kumuuliza,
"Dora anapajua hapa?"
"Ndio anapajua"
"Yani katika watu wote ukamkaribisha Dora kweli Erica! Kesho tunahama, usiulize tunahamia wapi ila kesho tunahama. Haya twende tukalale"
Basi Erica aliinuka tu na kufatana na Erick kwenda chumbani kulala.

Bahati alirudi moja kwa moja kwa ndugu zake na kuwaeleza kuwa amekutana na Erica, kwakweli ndugu zake walifurahi sana kwani Bahati alionekana kuwa mzima kabisa kichwani kwa siku hiyo.
Hakutaka kurudi kwake na kuamua kulala kwao siku hiyo, ila aliona usiku kuwa mrefu sana yani alikosa raha na kuamua kupiga ile namba ya Erica na hata ambapo haikupokelewa aliipiga tena na mwishoe ikapokelewa na Erick, akaumia sana moyo wake na ilipokatika ndipo akatuma ule ujumbe.
Yani alikuwa anangoja pakuche tu maana moyo wake wote ulijaa na mawazo dhidi ya Erica.
Kulipokucha aliona ni vyema amtafute Dora kwanza ili pengine ampeleke anapoishi Erica, ala kabla hajafanya hivyo dada zake walienda kuongea nae,
"Kwakweli Bahati tumefurahi sana, kwakweli Erica katumwa na Mungu kuokoa maisha yako. Ulikuwa hutamaniki Bahati kabisa maana ulikuwa unafanya mambo ya ajabu tu"
"Ila sisi ndugu zako ndio chanzo cha yote maana kama tungekuwa makini basi tusingeruhusu ufanyiwe dawa. Kwakweli kwa kupitia wewe tumejifunza mambo mengi sana"
"Hivi kwa mambo hayo mnayoniambia, Erica atakubali tena kuwa wangu kweli? Erica akijua hizo ndio tabia zangu atakubali kweli?"
"Najua hawezi kukubali ila bado tunapaswa kumshukuru sana kwa kukuokoa"
"Mnajua ndugu zangu hakika mtalaaniwa yani mmefanya nimsahau Erica kiasi hiki kweli? Hivi mnajua mali zote nilizonazo ni sababu ya Erica, mnatambua hilo? Najua hamjui ila kila nilichonacho ni sababu ya Erica tu yani yeye ndio kafanya nimepata mali zote hizi ila mkafanya kitu cha ajabu nimsahau kweli!"
Yani ndugu wa Bahati ndio walishtuka hapa kuwa mali zote alizonazo Bahati ni sababu ya Erica maana ndio kasababisha Bahati kupata mali zile, waliishia tu kumuomba msamaha ndugu yao maana tayari walishafanya makosa.
Basi Bahati akawasiliana na Dora tu kwani nia yake ilikuwa ni kupelekwa anapoishi Erica ili aweze kuongea nae.

Yani asubuhi na mapema Erick alimwambia Erica ajiandae na wamuandae na Angel kwaajili ya kuondoka na walipomaliza, Erick alibeba mabegi ya nguo zao na kupakia pia kwenye gari na kumwambia Erica waondoke,
"Kheee ndio tunahama!"
"Ndio, unashangaa nini sasa?"
"Mbona gafla hivyo, na kodi tuliyotoa je?"
"Sijali kuhusu kodi kabisa, Erica wewe ni wa muhimu sana kwangu. Namshukuru Mungu akili zako nimezijua maana nisingezijua akili zako basi na mimi ningefanya ujinga. Sasa hapa tunahama, na tunapohamia sitaki kuona umekaribisha takataka yoyote sijui shoga yako, sitaki huo ujinga unakaribisha watu nyumbani na unajua wazi unabakiaga mwenyewe si kujiwekea makaa ya moto! Twende"
Basi Erica akawa hana jinsi zaidi ya kufatana tu na Erick kwenye gari kisha safari ikaanza.
Walifika kwenye nyumba hiyo ambayo bado ipo kwenye ujenzi, Erick akamwambia Erica,
"Siku zote nipo busy sababu ya hii nyumba, nilitaka nimalize kwanza nyumba yetu ndio tuhamie ila kwasasa acha tu tuishi na tutaimalizia tukiwa hapahapa pamoja kuliko kuendelea kupeana presha huko"
Erica hakutia neno, kwenye nyumba ile kulikuwa na chumba kimoja ndio kimekamilika kwahiyo Erick alimwambia Erica wataishi humo kwanza wakati nyumba inamaliziwa vitu vingine,
"Ila Erick nisamehe sana, naumia jamani"
"Unaumia na nini sasa?"
"Tumetupa kodi kule"
"Kuhusu kule usijali, nilishaongea na dalali anitafutie mteja kwahiyo nitapata tu kodi yangu hata usijali, ile hela wala haipotei bure. Yani usijali kuhusu hilo ila nimekuleta hapa ili tuishi kwa amani na upendo, halafu hiyo simu yako nipe"
Erica alimpa Erick ile simu yake, halafu akamuuliza
"Na mimi nitawasiliana na simu gani?"
"Nitakutafutia simu nyingine na hii ni mimi ndio nitawasiliana na ndugu zako, wale wa muhimu tutawapa namba zako ila sijui wakina Derick siwatambui kama ni nduguzo."
Erica hakubisha zaidi ni kukubaliana tu na Erick maana yeye ndio kasababisha yale yote mpaka Erick kawa vile.
Basi aliingia ndani na Angel kutulia nae kisha Erick akaenda kufanya kazi ya kuhamisha baadhi ya vitu ambavyo alinunua kule.
 
SEHEMU YA 426

Bahati aliwasiliana na Dora na kukutana nae, kisha wakakutana na kuanza kuongea,
"Yani Dora huwezi amini, jana nilipomuona Erica akili yangu iliruka kabisa"
"Kwani Erica alikupa nini wewe?"
"Hakuna ila mimi ndio nilikuwa mwanaume wa kwanza kwa Erica, nampenda sana na ninaamini hata yeye ananipenda sana"
"Aliyekudanganya kuwa ukiwa wa kwanza kwq mwanamke atakupenda sana nani? Umeniona mimi, hata mwanaume wangu wa kwanza simkumbuki kabisa yani hata jina lake silijui, kuwa wa kwanza sio kigezo cha kupendwa"
"Hata kama, naomba tu unipeleke kwakina Erica yani anapoishi kwasasa, nahitaji kuongea nae."
"Utanipa nini nikikupeleka?"
"Unataka nikupe pesa ngapi?"
"Nipe laki moja ndio nitakupeleka"
"Nitakupe laki na elfu hamsini"
"Wow kumbe umekuwa na hela hivyo, twende nikupeleke ila nipe changu kabisa"
Muda ule ule Bahati alifanya muamala na kumwambia Dora amtajie namba zake kisha akamrushia laki moja na elfu hamsini, basi Dora akachekelea na kumwambia kuwa waende.
Basi wakaondoka na kufika hadi anapoishi Erica, waligonga mlango bila kufunguliwa, muda kidogo alifika Fetty ambaye pia alikuwa na lengo la kuonana na Erica, akawasalimia pale na wakamwambia kuwa wamegonga ila hawajafunguliwa, wanahisi huenda Erica hayupo.
Ila kwa leo Fetty alimuangalia Dora na kuanza kumshukuru,
"Asante sana Dora"
"Asante ya nini tena?"
"Nilifata ule ushauri wako na kwenda kupima na George uwiii nimemkuta kaathirika"
Dora baada ya kusikitika alionekana akicheka sana hadi Fetty alimshangaa na kumwambia
"Mbona unacheka?"
"Nacheka ya George, katafuta bikra weeee mwisho wa siku kaibuka na gonjwa. Unapotafuta bikra, hakikisha na wewe umetulia lakini ukiwa macho juu juu basi utaukwaa tu"
Akaendelea kucheka sana, Fetty akamuangalia Bahati na kukumbuka kuwa kuna siku Bahati alipigana na George, ndio hapa akapata picha kuwa George alikuwa na mahusiano na Erica mpaka kupigana na huyo Bahati ila alimshangaa muda huo kwenda tena nyumbani kwa Erica, akamuuliza
"Na hapa umefata nini wewe? Si ulikuwa na mahusiano na Erica wewe!"
Dora akamjibia,
"Eti badi anamtaka Erica, huyu anacheza na Erick eeeh! Mwenzio Erick kashatembeza bakora kwa kila mwanamke unayemjua hadi katulia kwa Erica ujue kafika na atakufanyia kitu kibaya wewe. Kupenda gani huko?"
"Jamani hamjui tu, nampenda sana Erica"
"Huo wako sio upendo ni uchizi, ila Bahati nishakufikisha kwa Erica nadhani katoka na mume wake maana Erick anavyojua mahaba yule najua baada ya jana basi leo kaenda kumpeleka matembezi ili Erica asifikirie tena kuhusu nyie vinuka mkojo"
"Unasemaje Dora?"
"Sijasema kitu bhana, ila naondoka tutaonana siku nyingine. Kwa Erica ndio hapa, kwahiyo akili juu yako"
Basi Bahati nae akaamua kuondoka na Fetty pia akaondoka na wote kupata lifti kwenye gari ya Bahati.

Wakiwa kwenye gari ya Bahati, njiani Dora alishuka na kuwaaga basi Bahati alibaki akiwa na Fetty kwenye gari ila alikumbuka jambo na kumuuliza Fetty,
"Ulisema mlienda kupima ukimwi?"
"Ndio, tulienda kupima"
"Naomba nami nipeleke hiyo sehemu maana sina hakika na afya yangu"
"Kwani ni muhuni sana wewe?"
"Dah ni historia ndefu sana sijui nianzie wapi ila cha kunisaidia nipeleke tu huko nikapime"
Basi Fetty alikubali na kwenda nae kupima kwenye hiyo hospitali na majibu yalipotoka Bahati hakuamini kabisa maana alikutwa hajaathirika, kwakweli alifurahi sana na kumshukuru Fetty kwa kumpeleka sehemu hiyo kupima kisha akamuomba namba yake ya simu na kuagana nae.
Moja kwa moja Bahati alirudi kwao na kuwaonyesha dada zake kile cheti cha ukimwi,
"Yani siamini dada zangu, siamini kama nimepona kwakweli."
"Mungu mkubwa kaka, ila inabidi tumshukuru sana Erica"
"Nimeenda kwake aijamkuta"
"Labda karudi kwao"
"Inawezekana, kwahiyo tufanyeje sasa?"
"Naomba twendeni tena kwakina Erica, tukaombe msamaha tu maana hakuna namna jamani"
Wakakubaliana kuwa kesho yake waende tena kwakina Erica.

Erick alipeleka vitu pale kwake ambapo chumba kingine walimalizia haraka haraka na kuweka vyombo ambavyo vimetoka kule walipokuwa wamepanga.
Jioni hiyo alifika na simu na laini mpya na kumpa Erica,
"Kwasasa tutawasiliana kwa namba hii yani ukiwa na shida na mimi basi unatafute ukiwa na namba hii maana ile yako ya mwanzo nitatumia mimi. Halafu unajua kilichotokea wakati naenda kumalizia vyombo?"
"Kimetokea nini?"
"Kuna watu niliwaona pale nyumbani akiwepo Dora na yule jamaa yako, kwakweli Erica ukifahamisha tena hizi takataka zako huku tulipohamia sijui nitafanyaje, sikuahidi cha kufanya ila watu hawa siwataki tena. Nilishakwambia, mimi ndio rafiki yako na msiri wako, ukiwa na habari yoyote niambie mimi. Najua wanawake mnapenda sana umbea kwahiyo ikitokea kuna umbea wowote unatamani kuufanya basi fanya kwangu, yani huo umbea nieleze mimi nitaelewa kuliko kuzoa zia marafiki wasiokuwa na tija. Nadhani tumeelewana"
"Ndio, nimekuelewa"
Kisha Erica aliendelea kumuelekeza cha kufanya mahali hapo sababu ilikuwa ni nyumba ambayo bado haijaisha, Erica aliuliza tena
"Na kwetu wakitaka kuwasiliana na mimi je?"
"Hamna shida utawasiliana nao, kipindi hiki nipo huku karibia muda wote kwahiyo ikiita tu simu ya kwenu nitakupa uongee nayo, mama yangu anarudi wiki ijayo tu kwahiyo nitamueleza kila kitu na atakwenda kwenu na kila kitu kitakuwa sawa, najua mama hawezi tena kubishana au kukukataa akijua kuwa una mimba yangu, kwahiyo lazima kila kitu kitaenda sawa sawa kama tulivyopanga"
Basi Erica akafurahi pale, na muda ule ule simu ya Erica ilianza kuita tena, Erick akaitazama na kuona ni namba ya baba yake, kwahiyo hakupokea aliacha iite hadi ikatike, iliita mara kadhaa na kukatika, mara ikaingia namba ya Tumaini kwenye simu ya Erica ndipo Erick akapokea hiyo simu,
"Erica uko wapi? Nimekuja hapa sijamkuta mtu, uko wapi?"
Erick aliamua kujibu maana alipatwa na hisia kuwa kuna kitu hakipo sawa,
"Tumaini, ni mimi ndiyo nina simu ya Erica. Aliondoka leo asubuhi kurudi kwao maana kuna mambo yalitokea akachukizwa eti kwahiyo simu yake ndio nimekuja nayo mimi kwenye shughuli zangu"
"Aaaah sawa"
Ile simu ikakatika, kisha Erick akasema,
"Kuna kitu hakipo sawa hapa, simu ya baba imeeita kama mara mbili halafu inakuja simu ya Tumaini kuuliza ulipo? Mmmh naona sio sawa kwakweli."
"Au baba yenu kaenda pale tunapokaa?"
"Inawezekana ndiomana nikasema kuwa pale si salama kwasasa"
Basi wakafanya mambo mengine na kujiandaa kulala.
 
SEHEMU YA 427

Wakati wa usiku ndio wanalala, simu ya Erica iliita tena, Erick akaangalia na kuona ni Tony yani kaka yake na Erica, akampa ile simu Erica aongee nayo,
"Erica mama kakupigia simu?"
"Hapana kwani anasemaje?"
"Yani mimi kanipigia simu kasema niachane na mwanamke niliyempeleka"
"Kwani kaka ulimpeleka nani?"
"Eti sijui ana ugomvi na wewe, mimi nilimpeleka Tumaini tafadhali Erica usimkatae, nampenda sana. Niambie unamuonaje?"
Erica akamuangalia kwanza Erick kisha akamjibu kaka yake,
"Aaaah mbona yupo vizuri tu yule"
"Sasa nyumbani hawamtaki, ila kuna mpango nitafanya"
"Mpango gani?"
"Nitaondoka kama wewe nyumbani na kwenda kuishi na Tumaini"
"Na yeye atakubali?"
"Sasa hapo pagumu mmmh! Ila nampenda sana. Sasa basi nitakuja kwako huko ili tupange"
Erica akataka kumwambia kuwa wamehama ila Erick akamziba mdomo na kukata ile simu, kisha akamwambia
"Kwasasa sitaki yeyote ajue kuwa tumehama, mpaka mambo yakikamilika. Erica acha tuishi tu mafichoni lakini kwa usalama wetu, siku hata Angel wetu watamuiba kumbe sababu ya kukaribisha wageni hovyo"
Erica nae alianza kuelewa mipango ya Erick, kwani muda ule ule simu ya Erick iliita na mpigaji alikuwa ni Tumaini, basi Erick akapokea,
"Niambie dada"
"Yani Erick kama mtaweza hameni hapo mnapoishi, maana jioni baba alinibana hadi nikamleta yani muda ule napiga simu ya Erica nilikuwa na baba na alivyosikia Erica karudi kwao basi kasema anaenda kwakina Erica, yani baba yetu sijui ana tatizo gani"
"Kwahiyo hakwenda kwa yule mwanamke?"
"Hajaenda, nahisi kakutana na mtu kamshauri ujinga ndio baba yupo hivyo. Nisamehe Erick sikutaka kumleta baba ila ilibidi nimlete tu"
"Sawa nimekuelewa usijali"
Ila Erick hakuthubutu kumwambia dada yake kuwa wamehama maana mwenendo wa baba yao aliuona. Kisha yeye na Erica waliamua kulala tu muda huo.

Kulipokucha Erick alishangaa kupokea simu kutoka kwa mama yake,
"Kesho narudi Erick"
"Si ulisema wiki ijayo mama"
"Nimeghairi, narudi kesho"
"Sawa mama, niambie ni muda gani nije kukupokea?"
"Kwanza kabla ya yote, mkamwana wangu Sia hajambo"
"Mama, huyo sio mkweo. Yani mkweo ni Erica"
"Sitaki kusikia hilo jina, na wala sirudi kesho yani hata usijiandae kuja kunipokea"
"Jamani mama"
"Hakuna cha jamani"
Kwakweli Erick huwa haelewi kabisa kuwa ni kwanini mama yake hampendi Erica na wakati huo huo yeye akiwa hapendi kabisa na ndugu wa Erica yani hapo alishindwa kuelewa kwakweli. Na kubaki akijisemea mwenyewe,
"Yani mapenzi siyaelewi hapa tu jamani, ukipata mnayependana basi vikwazo kila kona, yani nashindwa kuelewa mapenzi ni nini jamani"
Kisha akaamua kuendelea na kazi zake za kusimamia ujenzi wa nyumba yake.
Akapokea ujumbe toka kwa babake,
"Umemficha wapi Erica?"
Kwakweli leo Erick aliona ni kumuondolea uvivu baba yake kwani muda ule ule akampigia simu na kuanza kuongea nae,
"Hivi baba huwa unaongelea nini?"
"Namuongelea Erica"
"Baba, unampenda Erica au Ester? Na ukiendelea hivi nitamueleza yule mama kila kitu yani kama alikukataa kidogo basi akukatae sana"
"Mmmh mwanangu yamekuwa hayo! Wewe ni mtoto wa kiume na mwanaume siku zote ni kustahimili mambo"
"Baba, wewe ni baba yangu ila kutwa kucha kumng'ang'ania mke wangu, hivi nikimuoa na kuja nae nyumbani si utambaka wewe"
"Kunikosea adabu huko Erick"
"Sio kukukosea adabu, unadhani unachofanya kipo sawa? Badala unipe baraka zako ila wewe ndio unakazana na mambo yasiyofaa. Hatujakataa kuoa kwako ila oa wanawake ulioruka nao sio hawa usiohusika nao. Kama hela si nilikuwekea, ile ni posa yako ambayo huwa unailalamikia. Naomba umuache Erica wangu, tafadhali baba"
Mzee Jimmy alikata simu yake kwani aliona leo Erick amepaniki haswaa.
Baada ya muda tu Erick alipokea tena ujumbe kutoka kwa baba yake,
"Erick mwanangu naomba yaishe, mimi ni baba yako na nitabaki kuwa baba yako"
Erick alisoma ule ujumbe ila hakuujibu wala nini na kuendelea na shughuli zake tu.

Mama Erica alikaa na Bite leo wakizungumzia tukio la jana yake la kufikiwa na mzee Jimmy
"Hivi mama, yule mzee akili zake zikoje jamani mbona yupo vile?"
Ilibidi amuelezee pia kilichowahi kutokea kati yake na mzee Jimmy na sababu ya yeye kuwachukia watoto wa mzee Jimmy.
"Mwanangu kama hivyo kweli yule mzee anastahili kusamehewa na mimi? Je nastahili kuchukua watoto wake kama wakwe zangu?"
"Ila mama, swala la Erica hatuna jinsi zaidi ya kukubali tu aolewe na Erick maana hiyo mimba tutaipeleka wapi? Kama aibu tayari ishaingia ndani ya nyumba, naomba tukubali tu"
"Huyo Erick ni kiburi mwanangu, hivi unaweza kuishi na mtoto wa mtu bila kutaarifu kwao?"
"Hiyo inafanya nihisi huenda Erick hampendi kweli Erica maana kama angempenda basi asingefanya vile na usikute hana hata nia ya kumuoa yani anampotezea muda tu ajifungue, na toto lako lilivyojinga limejikalisha kwa mwanaume yani lishafanywa mke kabisa"
"Na hata harusi yao ikija yani Erica nitamkomesha na hatosahau kamwe, watafunga ndoa ila atapata aibu sana"
"Utamfanyaje mama?"
"Subiri tu, ujinga aliofanya sijaupenda hata kidogo. Jitu tumelisomesha, sasa badala ya kutafuta kazi anafanya tu kazi ya kubeba mimba na kwenda kukaa kwa mwanaume. Yani Erica hapana kwakweli"
Wakati wanaongea wakasikia watu wakigonga mlango na Bite kwenda kufungua, kwakweli alishangaa sana kuwaona tena Bahati na ndugu zake, aliwauliza kwa mshangao,
"Kheeee mmekuja tena!"
Mama yake alitoka kuwaangalia, alipowaona alichukia sana na kuwatimua. Basi ndugu wa Bahati wakaondoka ila kama kawaida Bahati aligoma kuondoka na kukaa nje kwenye nyuma ya kina Erica.

Jioni ya siku hiyo, Mage alikuwa akienda kwao alishangaa sana kumkuta Bahati amekaa pale nje, alimuuliza tatizo,
"Nahitaji kumuona Erica"
"Pole sana, Erica alitoroshwa na mume wake kwahiho hadi leo hajarudi nyumbani"
Ila bado Bahati hakutaka kuondoka, ikabidi Mage agonge ndani na walipofungua pia walishangaa kumuona Bahati, mama yao alihamaki
"Yani hujaondoka hadi muda huu?"
Bahati alibaki akimuangalia tu. Kisha yule mama akasema tena
"Yani sijui Erica alikuokotea wapi Mungu wangu, pole sana kijana. Erica anakaribia kuolewa na kwasasa Erica ni mjamzito"
Bahati akashtuka sana,
"Erica ni mjamzito?"
"Ndio, sio unauliza mara kwa mara uniletee kifaduro hapa sijui degedege, wewe ondoka tu kaishi vyema na mkeo. Erica ni mjamzito na hapa nyumbani hayupo"
"Ila Erica ananipenda sana"
"Bwana weeee kama angekuwa anakupenda angezaa na wewe, ila kazaa na mwanaume mwingine na sasa kabeba mimba ya mwanaume mwingine halafu wewe bogozo unajifanya na mada yako ya kupendwa na Erica!"
"Mama, lakini mimi ndio mwanaume wa kwanza kwa Erica"
"Huo ujinga ndio siutaki maana hamkawii kuanza kueleza na staili mnazofanyaga mlipokutana na Erica. Kwaheri, ondoka sasa hivi kabla sijatenda dhambi"
Bahati alikuwa amesimama tu, ila kufumba na kufumbua mamake Erica alitoka na panga na kufanya Bahati akimbie na kuondoka.
Yule mama alirudi ndani huku akisema tu,
"Hawa vijana ni hovyo kabisa, yule wa siku ile nae kaja kujitapa hapa sijui mimi mwanaume wa kwanza wa Erica na huyu mgonjwa wa akili nae anakuja na mada zake zisizoeleweka. Jamani nina shida mimi, huyu Erica huyu loh!"
Mage alishangaa sana na kusema,
"Erica katoa wapi hai punguani wa kujisifu kuwa wa kwanza? Loh mbona makubwa"
Waliongea sana pale maana ilikuwa kama mada ya siku hiyo.
 
SEHEMU YA 430

Leo James aliamua kwenda tena kwa mke wake ili kujaribu kuongea tena kuona kama wataweza kumruhusu kuendelea kuishi na mke wake.
Alifika pale nankumkuta Bite na mama yake, alieleza azma yake ya kutaka kuishi tena na Bite, mama yao akamwambia,
"Yani leo nikajua umekuja kusema kuwa umempata mwanamke wa kuishi nae ambaye amekubaliana na maukimwi yako, yani uneng'eneke hukonupate gonjwa halafu uje kulitua kwa mwanangu, naomba ukome"
"Ila madaktari wameshauri kuwa naweza kuishi na mke wangu"
"Uishi nae wapi? Hao madaktari kama wanaona ni kazi rahisi basi kawaoe wao ndio uwe mume wao, mwanaume mchafu wewe yani happ ulipo unanuka zinaa halafu bila aibu ukaishi na mwanangu"
Kisha akamgeukia Bite na kumwambia,
“Na wewe nisikie huu ujinga kuwa umeamua kwenda kuishi na James sijui sababu ya kumpenda, umpende James kuliko mamako mzazi si uchizi wa Erica huo kumpenda mwanaume hadi kutoroka nyumbani"
James akadakia na kusema,
"Halafu huyo Erica nilimuona hotelini ila nilivyoenda kumshauri basi mwanae akanichoma na kisu"
Mama Erica alicheka sana na kusema,
"Unacheza na Angel eeeh! Siku nyingine atakutoboa macho, kwani sisi tumekwambia utusaidie kumrudisha Erica nyumbani? Kuna mahali tumeomba msaada wako? Hebu achana na mwanangu bhana"
James aliona thamani yake kwenye nyumba hii imeshuka sana kwahiyo ilibidi aendelee tu kubembeleza kurudiana na mkewe,
"Cha kukushauri James, nenda mahakamani ufanye harakati za kumpa mwanangu talaka kisha uende kumuoa Dora nimemaliza"
"Jamani mama"
"Mimi sina watoto wasiojielewa kama wewe, toka nyumbani kwangu nitakuitia mwizi sasa hivi"
Ilibidi James atoke na kuondoka zake.

Dada wa Bahati ndio waliofanya kazi ya kumkataza Bahati kurudi nyumbani kwake kwani walijua akirudi tu basi atatupiwa tena madawa na mwanamke yule, kwahiyo walifanya kila jitihada ili Bahati asirudi kwake, wakati huo huo Bahati hakutaka kwenda hata kwa Siwema kwani tangu amekuwa sawa basi familia ya Nasma hakuitaka kabisa.
Alichojibiwa usiku kwenye simu na Erica kilimsononesha sana na kumkosesha raha kabisa, alijiona hana thamani kwa kitendo cha kukataliwa na Erica, muda huo mchana aliamua kumpigia simu Fetty yule rafiki wa Erica ili pengine akae nae na amshauri. Akawasiliana na Fetty na kukubali kukutana, ni kweli Fetty alikutana nae na kufanya nae mazungumzo.
"Hivi ukaribu wako na Erica upo vipo?"
"Erica ni rafiki yangu sana, tumejikuta tukiambiana mambo mengi sana"
"Hajawahi kukwambia kuwa ananipenda sana?"
"Mmmmh hajawahi kwakweli, nakumbuka kila nilipokuwa nikikaa na kuongea na Erica alikuwa akimtaja mwanaume mmoja tu kuwa anampenda sana. Alisema anampenda sana Erick"
"Ila mbona mimi nampenda hivi Erica! Yani upendo wangu mimi sidhani kama huyo Erick anaufikia, yani katika dunia hii hakuna mtu anayempenda Erica kama mimi"
"Pole sana, hayo tunaita ni mapenzi ya sehemu moja yani unampenda ila yeye hakupendi. Mapenzi mazuri ni kupendana"
"Jamani nitafanyaje sasa mimi? Nampenda sana Erica"
"Pole ila kama unampenda kweli Erica basi unatakiwa kukubaliana na matakwa yake, Erica anampenda Erick na Erick anampenda Erica unachotakiwa kufanya ni kuwatakia kheri tu ili waishi salama. Na sio kubaki na msimamo wako huo kuwa unampenda sana utaumia"
"Nawezaje sasa? Mke niliyeoa nasikia ni madawa na simpendi hata kidogo jamani nifanyeje sasa?"
"Cha kufanya anza maisha upya, tafuta mke mwingine uoe"
"Duh una ushauri mzuri saba, nikwambie kitu Fetty"
"Niambie"
Kabla hajasema alitokea George kumbe alikuwa mitaa hiyo, na George alivyomuona Bahati alimshika sura kabisa kuwa ndiye alifanya fujo hosteli kwakina Erica na siku hiyo alimuacha ampige tu ila leo aliona ndio vyema na yeye kulipiza kisasi chake alichokuwa nacho kwa muda mrefu sana. Tena alimkuta kakaa na Fetty ndio kabisa alichukia, akichanganya na yale majibu ya vipimo alipata hasira sana, akamfata na kumkunja, sababu Bahati hakujiandaa alijikuta akipokea kipigo kizito sana kutoka kwa George halafu George aliondoka eneo lile huku Bahati akiwa abapepesuka tu.
Ingawa Fetty alienda kujificha wakati wanapigana, ila George alivyoondoka huruma ikamjia kwahiyo alienda kumsaidia Bahati mpaka kwenye gari ya Bahati kisha Fetty alianza kuendesha kumpeleka hospitali, uzuri aliweza kuendesha gari maana bila ya hivyo angeshindwa.
Walifika hospitali ambayo Bahati huwa anahudumiwa mara kwa mara, basi walimuhudumia bila kibali cha polisi, wakati wanatoka pale hospitali na Fetty, walikutana na Mrs.Peter ambaye alimsalimia Bahati na kumpa pole, kisha alivyomuona Fetty akamuuliza Bahati,
"Ndii huyo mke wako?"
Bahati akacheka tu kisha mrs.Peter akasema tena,
"Ila mmependezana sana, yani mnapendeza kwakweli. Hongereni"
Bahati alishukuru tu pale na kuagana na huyu mama maana hakutaka aulize kitu kingine.
Kisha alimuomba Fetty ampeleke nyumbani kwao maana aliona kuwa anaendesha vizuri.

Usiku wakati Erick yupo na Erica, mama yake alipiga simu na alijua tu kuwa mama yake anamwambia habari ya kurudi nyumbani. Basi Erick alipokea,
"Uko wapi? Mbona hujaja nyumbani?"
"Nimeshindwa mama"
"Kwanini umeshindwa?"
"Kesho nitakwambia vizuri mama"
"Hivi wewe Erick una matatizo gani eeeh! Usifikiri nimeibuka tu kukupigia simu na kukuuliza. Sijaibuka ila nimempigia kwanza dada yako Tumaini na kasema haupo nyumbani, tatizo nini? Kwa baba yako haupo na huku kwangu haupo, uko wapi?"
Erick akaona ampe mama yake kauli ya kumfurahisha ili asimuulize sana,
"Leo nimekuja kulala huku kwa Sia"
"Mwanangu unasema kweli? Nipe Sia niongee nae?"
"Kwahiyo huniamini mama"
"Basi nakuamini mwanangu, kesho uje ofisini tupange vizuri"
"Sawa mama"
Muda huo akaagana na mama yake na kukata simu, alipoangalia pembeni alimuona Erica akilia na kumfata karibu,
"Unalia nini sasa? Umechukia niliposema nipo kwa Sia? Nimesema vile ili mama asiongee sana, kwani kweli nipo kwa Sia jamani Erica!"
Erica alinyamaza kimya kisha akasema,
"Nyie wanaume ni waongo"
"Nakubali Erica kuwa wanaume ni waongo ila mwanaume mimi ni wa tofauti sana kwani napenda ukweli na sipendi kumchukiza mtu nimpendaye. Erica nimempooza mama tu, tena kesho nina mpango kabambe maana naenda na Dora ofisini kwa mama ili akamuhakikishie kuwa mimba ya Sia sio yangu"
Bado Erica hakuonekana kufurahi wala nini, basi Erick akajua kuwa ni mawazo ya kwao yanamsumbua
"Erica, nakuahidi kesho tukishaongea na mama nitakamilisha kila kitu. Yani nahakikisha mama yangu anaenda kwenu na tunapeleka mshenga na kuoana"
Erica akatabasamu sasa, Erick pia alitabasamu kwani alijua swala linalomchanganya Erica kwa muda huo ni mimba aliyobeba na kuhusu kuchelewa kwa harusi yao.
Baada ya hayo, kila Erick alipotaka kulala Erica alitaka waongee tu yani hata kama cha kuongea kimeisha, mpaka Erick alihisi kusinzia na kuwaza kuwa anajukumu la kuweka Tv yake sawa ili Erica asipojihisi usingizi basi azubalie kwenye Tv.
Mwishoe Erick alisinzia tu ndipo Erica nae akalala.
Kulipokucha, Erick alijiandaa haraka haraka maana siku hiyo alichelewa kuamka tofauti na siku zote, kwahiyo alijiandaa haraka haraka na kumuaga Erica.
Basi kama alivyopanga alikutana na Dora na kwenda nae ofisini kwa mamake.
Walipoingia ofisini, kile kitendo cha mamake Erick kumuona Dora kilionekana kumchukiza sana kwani alitoka kwenye kiti chake na kwenda kumnasa kibao Dora.


Basi kama alivyopanga alikutana na Dora na kwenda nae ofisini kwa mamake.
Walipoingia ofisini, kile kitendo cha mamake Erick kumuona Dora kilionekana kumchukiza sana kwani alitoka kwenye kiti chake na kwenda kumnasa kibao Dora.
Erick alimshangaa sana mama yake kufanya vile, Dora mwenyewe hakuelewa ni kwanini Yule mama kamnasa kibao alikuwa akijishika shavu tu huku akiugulia maumivu, Erick alimuuliza mama yake,
“Mama, nini tatizo?”
“Hivi kwanini umeniletea wasichana pumbavu kama huyu ofisini kwangu?”
Akataka tena kwenda kumnasa kibao Dora, ila muda huu Dora alienda nyuma ya Erick kwani naye alitaka kujua ni kwanini huyu mama kamchukia kiasi hiki, alitaka kujua kuwa ni kwanini anafanyiwa hivi na huyu mama, kwahiyo alimshikilia Erick kwa nyuma huku Erick akiendelea kumdadisi mama yake kuwa tatizo ni nini,
“Jana, wakati natoka kidogo hapa ofisini niliwakuta huyu msichana na George, muda huo George alikuwa anamlalamikia sijui kakutwa na ukimwi, huyu msichana akacheka na kumwambia nimekuambukiza mimi, tena kwa makusudi tu. Yani mjinga huyu kachanganya akili ya George tangia jana, maana alikimbia na bodaboda ila George hakuweza tena kuendelea kufanya kazi, na leo hajafika kazini”
Hapo Dora ndio kumbukumbu ya jana yake ikamjia vizuri kuwa alipoachana na Erick, alienda mitaa hiyo na kukutana na George ila hakumbuki kama kulikuwa na mtu anasikiliza maelekezo yake na George, nay ale mawazo ndio yaliyofanya George jana yake ampige sana Bahati maana alikuwa na hasira za kutosha.
Erick alimtazama sana Dora na kumuuliza,
“Inamaana umewahi kuwa na mahusiano na George? Inamaana una ukimwi Dora?”
Mama Erick akajibu,
“Isingekuwa kweli basi George asingechanganyikiwa, huyu msichana kamuambukiza George ukimwi kwa makusudi, na lazima alikuwa na mahusiano nae shetani hili”
Ila kile kitendo cha Erick kusikia kuwa Dora ana ukimwi na anamahusiano na George, wakati huo huo anatembea na baba yake alihisi kimemchanganya kiasi, akamuangalia kwa gadhabu na kumuuliza tena,
“Dora ni kweli una ukimwi?”
“Ila Erick mbona unabadilisha mada, nimekuja huku ili tuongelee habari zaa mimba ya Sia, sasa unanielezea habari za ukimwi mbona sikuelewi!”
“Ila ni kweli ulikuwa na mahusiano na George?”
“Kwani ni ajabu hiyo? Mimi ni mwanamke na George ni mwanaume sasa mahusiano kati yetu yatashindikanaje? Na hata hiyo, sio peke yangu kwani hata Erica amewahi kuwa na mahusiano na George”
Hapo Erick alihisi akili kutosoma kabisa kwani amemtaja mwanamke ampendaye, na huwa hampendi George, kwahiyo swala la kusikia kuwa Erica alikuwa na mahusiano na George akawaza vingi sana, akawaza kuwa pengine ni kipindi Erica aliposema amepata kazi na ilikuwa ni ofisini kwa mama yake, akakumbuka pia siku aliyokuwa anarudi na kukutana na George ambaye aliuliza maswali mengi sana, ambapo naye Erica aliuliza undugu wa George na Erick, kwa hapo tu alishindwa hata kuongea ila mama yake ndiye aliongea,
“Kheeee makubwa, kwahiyo wewe unamjua Erica, unamjua malaya mwenzio eeeh! Umeona Erick sasa, ndio umeniletea huyu nijue ukweli au wewe ndio uujue ukweli? Kwahiyo wewe binti ni nani kwa Erica?”
“Erica ni rafiki yangu”
Erick aliamua kumtimua Dora kwani aliona akisimama hapo basi ataongea mengi zaidi,
“Dora naomba uende tafadhali”
“Hutaki tena nimweleze mama yako ukweli?”
“Nimesema nenda”
Dora aliangalia sura ya Erick ambayo ilikuwa imebadilika haswaaa kwahiyo ilibidi aondoke tu.
Mama Erick alimwambia Erick sasa,
“Hii ndio aina ya marafiki wa Erica, unategemea nini kutoka kwake? Kama rafiki yake kaathirika je yeye anaponaje? Yani Erick mwanangu kwa Yule msichana ulipotea tena ulipotea kabisa, kale katoto kachawi mwanangu unaweza kuhisi unakapenda sana kumbe kamekufanyia dawa. Nakwambia kweli nilikakuta mimi kananuka dawa mwili mzima, sasa sijui utanishawishi kitu gani kuhusu huyo Erica. Ila kama umeamua kutulia na Sia, nakupa pongezi na harusi yenu nitaisimami”
Kwa mara ya kwanza leo Erick aliondoka huku mama yake akiendelea kuongea, yani hakumuaga kabisa ila aliondoka.
 
SEHEMU YA 431

Siku hiyo mapema kabisa mzee Jimmy aliamua kuacha kazi zake na kuamua kwenda nyumbani kwa Ester kwani ujumbe wa mwisho wa Erick ulimvutia sana kuwa Ester kakubali, basi alifika pale na kuanza kuazungumza nae, ila kabla hajasema yanayomsibu akapigiwa simu na Dora, alitaka asiipokee ila Yule mama alimwambia aipokee,
“Nina shida na wewe ya haraka sana”
“Kuna mahali nipo Dora labda badae”
“Hapana ni muda huu, nakuomba uje haraka”
Basi Yule mama al;imwambia mzee Jimmy kuwa akasikilize alichoitiwa kwani yeye anamazungumzo marefu sana naye.
Dora aliamua kumpigia simu mzee Jimmy kwani alijua kama Erick atapeleka ile habari kwa mzee Jimmy basi itakuwa tatizo kubwa sana.
Baada ya muda mfupi, mzeeJimmy alifika eneo ambalo aliitwa n Dora.
“Eeeh Dora nimefika, niambie nini tatizo?”
“Nilikuwa sijisikii vizuri, nikaamua kwenda hospitali ila dokta kanishauri nipime na ukimwi, akaniuliza kama nina mwenzi wangu basi niende nae kupima ndio nimeamua kukutafuta wewe tukapime”
“Hivi wewe Dora una akili kweli? Nani mwenzi wako sasa, mimi mwenzi wako tokea lini?”
“Kwahiyo siku zote tunazokuwa pamoja sio mwezi wangu wewe?”
“Hebu kuwa na adabu wewe binti, hivi mimi nitakutambulisha vipi kwa watu eti mwenzi wangu, inakuja hiyo kweli? Wewe Dora wewe uwe na akili mara nyingine”
“Kwani tatizo liko wapi?”
“Huoni tatizo wewe? Hujioni kuwa ni mdogo sana? Unadhani mimi na utu uzima huu nianze kuhangaika na mtoto mdogo kama wewe sina aibu?”
“Na ulivyokuwa unataka kuhangaika na Erica ni mkubwa mwenzio Yule? Unavyolala kifuani kwangu ni mkubwa mwenzio mie, tena usitake nikuongelee maneno ya shombo mtu mzima wewe usiyejielewa, wakati unalala na mimi hukutambua kama kuna watu wazima wenzio? Hukutambua kama unatakiwa kuwa nao zaidi yangu? Hebu nitolee balaa, kwanza unaogopa nini kupima mtu mzima wewe, utakuwa unajua fika kama unao, kwaheri”
Dora aliinuka na kuondoka, ila mzee Jimmy hakutaka kumuita Dora kwa muda huo kwani alihisi ataongea maneno ya kumdhalilisha tu.
Kakweli kwa yale maneno ya dora yalifanya siku hiyo mzee Jimmy ajihisi vibaya sana, akainuka na kuondoka ila hakuwa sawa akilini na hakuweza tena kurudi kwa Ester na badala yake akarudi nyumbani kwake.

Leo Tony alikuwa nyumbani kwakina Tumaini huku akiongea nae na kujaribu kupanga nae mambo mbali mbali,
“Tumaini kwanini sisi tusiamue kuishi kama Erica na Erick?”
“Hapana Tony, baba yangu hawezi kukukataa wala mama yangu hawezi kukukataa basi uje kwetu ujitambulishe na tufate sharia zote za ndoa. Unafikiri Erica na Erick maisha wanayoishi ni ya furaha? Hawana furaha wale ila wanajaribu kutuonyesha tu sisi tuone kuwa wanafurahia ila hawana furaha hata kidogo, nakupenda unanipenda ila kwenu hawanitaki na kwetu hawawezi kukukataa, naomba tufate taratibu zote tuishi kwa amani”
“Sawa, basi unipeleke kwa mamako ukanitambulishe”
“Hakuna tatizo, tena ngoja nikajiandae twende’
Tumaini alienda kujiandaa ili aondoke na Tony kwenda nae kwa mama yake.
Wakati Tumaini anajiandaa, mzee Jimmy alifika na kumkuta Tony sebleni, alimuangalia tu ila hata salamu ya Tony hakuiitikia na moja kwa moja alienda humbani kwake.
Tony alishangaa sana, na baada ya muda alitoka Tumaini akiwa kashajiandaa ili waondoke, alivyofika Tony alimsifia sana
“Wow, umependeza Tumaini”
Akatabasamu tu na kumwambia kuwa waondoke tu, ila kabla hawajatoka alitoka ndani mzee Jimmy tena na kumsimamisha Tumaini,
“Weee Tumaini subiri kwanza”
Tumaini akasimama ila alimshangaa babake kuwa mbona karudi mapema vile nyumbani maana haikuwa kawaida, kisha mzee Jimmy akasogea na kumuuliza,
“Huyu kijana asiye na adabu umemuokota wapi?”
“Baba jamani si ungesubiri nikutambulishe kwanza”
“Kabla hujanitambulisha ngoja niulize, kijana una gari?”
“Hapana sina”
Mzee Jimmy alitikisa kichwa, akamuuliza tena,
“Una nyumba?”
“Hapana sina”
“Kwahiyo unategemea mwanangu utaishi nae kwenye pango? Nilikuwa nakusikiliza tu unavyojifanya kumsifia Tumaini, je unajua gharama ya nguo alizovaa Tumaini au unasifia tu”
Tony alikaa kimya maana hakuwa na cha kumjibu, kisha mzee Jimmy akamwambia Tumaini,
“Sitaki kuiona hii takataka tena kwenye nyumba yangu, najivunia kuwa na mtoto wa kike ila sio aolewe na fukara umesikia?”
Tumaini alishindwa hata kumuitikia baba yake na kuamua kumshika mkono Tony na kutoka nae nje, na kupanda ile gari aliyoachiwa na Erick na kuondoka nayo.
Kiukweli Tony hakuwa na raha kabisa, kwani kitendo cha kudharauliwa hakukipenda kabisa.

Walipokuwa wanakaribia kufika kwa mama wa Tumaini, Tony alijihami na kuuliza,
“Kama kwa babako kwenyewe hali ndio ile hivi mama yako atanielewa kweli?”
“Atakuelewa tu hata usiwe na shaka, mama yangu ni muelewa”
“Dah yani watu wenye hali za kawaida tunadharaulika sana jamani dah!”
Basi walifika na kugonga mlango kisha ndugu wa Tumaini alifungua na kuwakaribisha ndani.
Waliingia na kumkuta mama yake Tumaini yupo ndani ambapo baada ya salamu tu, Tumaini alianza kumtambulisha Tony kwa mama yake, Yule mama alimkaribisha vizuri tu Tony ila alimuuliza Tumaini,
“Huyu kijana ulisoma nae chuo?”
“Hapana mama, nilisoma nae shule ya msingi”
“Aaah kumbe! Vipi kijana umesoma hadi kiwango kipi cha elimu?”
“Nimeishia kidato cha sita mama”
“Mmmmh!”
Tumaini aliamua kumuuliza mama yake,
“Mbona umeguna mama?”
“Hivi unaona ni kitu cha kawaida hiki Tumaini?”
“Kwanini mama?”
“Wewe una shahada halafu mwanaume kidato cha sita inakuja kweli? Mara nyingi mwanaume anatakiwa awe juu kielimu kushinda mwanamke, sasa wewe umemshinda elimu unadhani atakusaidia nini? Haya ngoja nikuulize kingine, unajishughulisha na nini?”
“Sana sana najishughulisha na kilimo na mifugo”
Mama Tumaini alicheka sana yani hakutegemea kujibiwa vile kabisa, kisha akasema,
“Yani Tumaini na elimu yako kabisa kabisa unaenda kuchukua mwanaume mkulima kweli?”
“Sasa mama, ni mwanaume gani ananifaa jamani!”
“Badala upate mwanaume mwenye kazi yake, mwanaume mwenye ofisi zake, kweli unaenda kumchukua mkulima mwanangu na zaidi zaidi umemzidi elimu kweli anakufaa huyu!!”
“Kwani mama mtu kutokusoma ndio nini? Kumbuka Erick kaishia kidato cha nne ila ana hela hadi mimi namtegemea yeye, je amesoma?”
“Kuhusu Erick sawa, haya na huyu ana hela gani?”
“Mama, kila kitu ni taratibu”
“Mahali milioni tano, atakuwa nayo huyu?”
“Kila kitu kinawezekana chini ya jua”
Tumaini huwa hapendi kusemwa wala kukosolewa kwahiyo muda huo alichukia sana, na kuamua kuinuka kisha akashika mkono Tony waondoke.
Walipofika nje, Tony alimuelekeza
“Haipaswi kuchukia hivyo mpenzi, hawa ni wazazi wetu yani inatakiwa kuwaelekeza tu, ili waelewe kuwa ni jinsi gani wanatuumiza na maneno yao.”
“Tuondoke bhana, siwezi kuvumilia maneno ya mama”
Basi wakapanda kwenye gari na kuondoka zao.
 
SEHEMU YA 432

Erick hakunywa pombe kwa siku nyingi ila siku hiyo alipitia kwanz kunywa pombe halafu ndio akaenda nyumbani kwake, na kumkuta Erica akicheza na Angel hakutaka kumuuliza mbele ya mtoto kwani aliona ni picha mbaya watamuonyesha Angel. Basi alienda chumbani moja kwa moja ila Erica aliona kuwa ile hali haikuwa ya kawaida kabisa, kwani Erick huwa akirudi basi lazima atamkumbatia na kumtania Tania ila siku hiyo haikywa sawa, alienda ndani kumfata, aligundua kuwa amekunywa alihisi kuwa huenda ile ndio sababu ya kukimbilia ndani moja kwa moja ili asionekane kama amekunywa. Basi aliendelea kumbembeleza Angel na alipolala alienda kumlaza, ila muda huu alimuona Erick amekaa tu kitandani, akamuuliza,
“Mbona leo hata kwenda kuoga hujaenda Erick, nini tatizo?”
“Niambie kwanza mahusiano yako na George ya ofisini kwa mama yangu?”
“Sitakuficha Erick, nitakwambia ukweli, wakati nipo chuo nimewahi kuwa na mahusiano na George na tena ni mwanaume aliyeniumiza sana, sababu kuna mahali aliniacha tena bila…..”
“Usiendelee, ila nilikueleza kuwa George ni nani yangu? Mbona hukuniambia hayo?”
“Erick, sikuona sababu ya mimi kuongelea mahusiano yaliyopita maana mimi na wewe tulianza maisha mapya”
“Unajua Erica mtu akikuangalia unaonekana ni binti uliyetulia sana, yani nashindwa kuamini kama ulishawahi kuwa na Yule fedhuli. Haya umewahi kuwa nae hivi karibuni?”
“Hapana toka nimeachana nae kipindi cha chuo sijawahi kuwa nae tena”
“Na vipi ulipokuwa unafanya kazi ofisini kwa mama yangu?”
“Muulize hata mama yako akwambie ukweli. Alikuwa akiniambia kila mara kuwa niwe na George anioe ila nilikataa, na hiyo ni sababu pia ya mimi kuacha kazi ofisini kwa mama yako”
“Je ni kweli Dora ameathirika?”
“Ndio Dora ameathirika, ni muda tu”
“Dah inamaana na baba yangu nae ameathirika?”
“Sijui”
“Sasa hujui nini?”
“Sijui tu, ila je hiyo ndio sababu ya wewe kuchukia Erick hadi kunywa pombe?”
“Erica, nadhani hujui ni jinsi gani mapenzi yanavyoumiza. Mapenzi yanaumiza sana Erica halafu uwe unatambua kuwa nakupenda sana ten asana, huwezi amini moyo wangu ulivyopasuka na wivu baada ya kusikia kuwa ulikuwa na mahusiano na George, simpendi Yule jamaa simpendi kabisa”
“Nisamehe Erick, ila ilikuwa kipindi hiko hata sipo na wewe na hakuna dalili ya kuwa pamoja kabisa, nisamehe mpenzi wangu’
Erica alimuona Erick ametulia tu ila kwavile alijua kuwa Erick anapenda sana mapenzi basi akaanza kumshawishi na mwisho wa siku wakajikuta wamelala wote.

Dora alipotoka pale kuongea na mzee Jimmy, akaenda sehemu na kuagiza pombe ili anywe maana alijihisi kuwa na mawazo mengi sana na aliamini kuwa pombe ndio njia pekee yay eye kuacha kuwaza sana. Kuna muda aliwaza kuwa hayupo sawa kwa yale anayoyafanya,
“Hivi mimi nitaendelea kuhangaika hivi hadi lini? Kwanini nipo hivi mimi, Yule mama wa watu alihangaika kuniombea masikini kumbe mtu mwenyewe sikio la kufa halisikii dawa. Kuna muda natamani na mimi niwe na familia yangu, mimi nifurahie mapenzi kama Erica anavyofurahi kwa Erick maana kwangu ni kuhangaika na mwanaume huyu mara Yule na hadi sasa nimekuwa mzoefu yani hakuna ninachofanya kizuri. Mwishowe nitachukiwa na watu wote mimi jamani, natakiwa kubadilika kwakweli, ila ngoja ninywe pombe kwanza nipunguze mawazo.”
Basi akazidi kuagiza pombe na kunywa, wakati akinywa pombe zile, mara akafika James eneo lile nae alienda kunywa pombe, kwahiyo alipomuona Dora aliamua kwenda kunywa nae pombe, na siku hiyo walikunywa sana hadi walilewa na kuanza kuongea kilevi tu na kufanya mambo ambayo ulevi unawatuma. James alimwambia Dora akiwa katika ile hali ya ulevi,
“Leo nataka twende Yule mwanamke ambaye alisababisha mimi na mke wangu tugombane mara ya kwanza, nataka twende kwa Yule msichana wangu wa kazi”
“Ndio twende James, na leo nitamuonyesha huyo mwanamke namna ya kuiba mume wa mtu, yeye si alikuiba wewe kutoka kwa mkeo na mimi nitakuiba leo kutoka kwake”
Wakacheka sana muda huo na kuingia kwenye gari ya James huku gari ikiendeshwa kilevi sana maana siku hiyo walilewa sana, yani Dora hata alishasahau kuwa pombe zimewahi kumtenda kitu gani ila alichojali muda huo ni kunywa na kufurahia maisha tu kwa ulevi.
Yule mwanamke alikuwa amelala muda huo akashangaa kusikia mtu akigonga kwa nguvu mlango wake, basi aliinuka na kwenda kufungua, alishangaa sana kumuona James akiingia na mwanamke tena wakiwa kwenye hali ya ulevi sana, alishindwa hata kuwaambia chochote maana walikuwa hawamuelewi wala nini na waliendelea kufanya mambo yao ya kilevi, Dora na James walienda kitandani kwa Yule mwanamke na kuanza kufanya mapenzi, kwakweli Yule mwanamke aliumizwa sana na kitendo kile, hakutegemea kama James anaweza kumfanyia akili mbovu kiasi kile alichomfanyia, kisha Dora na James wakalala kitandani kwa Yule mwanamke, na Yule mwanamke na mtoto wake walikaa kwenye kochi ambapo alimlaza mwanae kwenye kochi nay eye kulia tu.
Kulipokucha, Dora alishtuka pale akitandani alipolala na James na kumshtua James pia, James alikaa ila kumbukumbu zote za usiku zilimjia kichwani kuwa walichokuwa wanafanya na Dora hakikuwa sawa, basi akainuka pale na Dora na kuondoka ila walivyofika mlangoni walikuta mlango umefungwa kwa nje yani Yule mwanamke alitoka na kuwafungia mlango.

Fetty nae asubuhi na mapema alienda kumuona Bahati na alimkuta kwao akiwa tu nje akipunga upepo na kuangalizia majeraha yake ya kipigo alichopata kutoka kwa George, Dora alimpa pole tena, kisha alianza kuongea nae kilichomfanya amfate kwa wakati ule,
“Bahati, kilichonileta hapa ni kuwa kuna ndoto mbaya sana nimepata kuhusu wewe”
“Ndoto gani hizo?”
“Inaonekana kuna watu wanataka kukufanyia kitu kibaya sana, sasa nataka nikushauri kitu”
“Kitu gani?”
“Una Kuran ndani?”
“Ipo”
“Unasomaga?”
“hapana, sisomagi na sionagi cha kusoma”
“Wewe Bahati wewe, kwahiyo kitu gani mnategemea nyumbani kwenu hapa? Yani nini kinawalinda?”
“Nyumba hii imezindikwa bwana, yani nyumba hii tulichinja mbuzi na kichwa chake kilifukiwa hapo mlangoni ndio kinga yetu hiyo’
“Mnajidanganya Bahati, tunatakiwa tumtegemee Mungu ndio msaada pekee katika maisha yetu. Wakristo huwa wanasoma Biblia na sisi Waislamu tunatakiwa tuwe tunasoma Kuran”
“Sasa nisome nini?”
“Unatakiwa usome ili ujikinge na watu wabaya, wachawi na mikosi, ngoja nikutajie sura kadhaa za kusoma zitakusaidia sana. Zisome kila siku ujiepushe na vinavyotaka kukuvamia maana naona kabisa haupo salama Bahati”
“Niambie basi hizo sura za kusoma”
“Soma Kul-audhubi rabil-nas na Kul-audhubi rabil-falaq”
“Sawa Fetty, nitaanza sasa kusoma hivyo ulivyoniambia, kiukweli mimi sikujua kama kuna sura kwenye Kuran unaweza kusoma na ikakusaidia usifatwe na wachawi au watu wabaya au mikosi”
“Katika maisha ya sasa tunatakiwa kumtegemea Allah tu na si vinginevyo, achana na imani za kishirikina ndugu yangu utakuwa unaandamwa na mikosi kila siku, unatakiwa kumtegemea Allah tu”
“Asante sana Fetty”
“Na ukimaliza kusoma uwe unapiga dua”
“Sawa Fetty nimekuelewa”
Muda ule ule Fetty alimuaga Bahati na kuanza kuondoka zake, ila simu ya Bahati ilianza kuita alipoona ni mkewe anapiga basi alimuita Fetty apokee ile simu na upande wa pili uliposikia sauti ya mwanamke basi aliamua kukata ile simu halafu Fetty akaaga tena na kuondoka zake.
Bahati nae aliona ni vyema kuanza kusoma hiyo Kuran muda ule ule alioambiwa na Fetty kwani ni kweli alikuwa ameandamwa sana na watu wabaya, kwahiyo aliinuka pale nje na kwenda ndani na wakati anaanza kusoma aliamua kuzima simu ili isimsumbue.

Nasma alikuwa nyumbani akimgoja Bahati ila hakufika nyumbani kwa siku zote, aliumia sana moyo wake kuwa amepata ujuzi halafu mume wake hataki tena kurudi nyumbani yani hapo alijihisi vibaya kabisa.
Aliamua kumpigia simu Bahati ndio muda ule alipokea mwanamke, kwakweli aliumia sana moyo wake yani alijihisi vibaya haswaa, na alipokaa kaa na kujaribu tena kumpigia simu alikuta ile namba haipatikani kwahiyo aliumia zaidi, ila wakati amekaa akapokea simu kutoka kwa baba yake,
“Wewe ushafanya dawa nilizokupa?”
“Bahati hajarudi hadi leo baba”
“Hiyo ya mlangoni ulimwaga?”
“Sikumwaga baba”
“Mjinga wewe, ungemwaga hiyo kwanza imvute yani umekaa na dawa siku zote hizi itakuwa haina ile nguvu ya awali, mjinga kabisa wewe mtoto”
“Nisamehe baba”
“Umenipa kazi ya ziada yani hata sielewi nianzie na mimi, mi nitamuharibu kabisa huyo mume wako, wewe si umeshindwa?”
“Baba, naenda kuimwaga sasa ile dawa”
“Ndio imwage na mimi nafanya vitu vyangu huku halafu akifika kama nilivyosema, usikosee masharti sawa?”
“Sawa baba”
Nasma aliagana na baba baba yake na kwenda kuimwaga ile dawa mlangoni ili iweze kumvuta Bahati arudi pale na aweze kumfanyia dawa zingine ila shida yake ilikuwa ni kumfanyia yale ambayo amefundishwa na Yule kungwi.
Alivyomaliza kumwaga dawa, akampigia tena simu Salma ili kumuuliza maendeleo yake na mumewe,
“Hahahah shoga yangu mahaba yanajibu, yani hapa nilipo najihisi kimimba kimeshanasa”
“Jamani, mbona mtoto mdogo huyo?”
“Mdogo ndio ila mume wangu alisema tumpe maziwa ya kopo kwahiyo kubeba mimba nyingine kwasasa ni halali yangu Nasma. Vipi wewe na mumeo?”
“Mmmh mume wangu hajarudi nyumbani kabisa, yani nyumba imekuwa kituo cha polisi, hata sijui nifanye kitu gani?”
“Pole mwaya, ila vumilia tu. Mvumilivu hula mbivu kama mimi hapa, ngojea wiki ijayo nikapime vizuri kabisa ila nahisi tu ishanasa”
“Hongera sana”
Basi aliagana nae ila yeye alikuwa na masononeko sana kwani hakuweza kuonana na mumewe kabisa. Alivyokata ile simu, aliamua kujigelesha na kujaribu kupiga namba ya dada yake Bahati,
“Wifi habari”
“Koma, sina wifi mshirikina kama wewe”
“Jamani wifi ndio yamekuwa hayo? Mnasahau kuwa ni nyie ndio mlinishawishi mwanzoni na kumfanyia dawa Bahati ili anioe? Jamani umesahau kabisa wifi yangu!”
“Ni kweli nilikushawishi ila sikukushawishi umpe kaka yangu dawa awe kama jogoo, asante Mungu Bahati alibahatika kuonana na Erica na ile midawa yenu ikayeyuka ila mlimfanyia vibaya sana Bahati hata dada zake alikuwa akitutamani loh! Nyie ni wabaya sana, wewe Nasma na ukoo wako mzima hamfai hata kidogo”
Kisha dadake Bahati akakata simu ndipo Nasma akaelewa kuwa Bahati alipona baada ya kukutana na Erica, ingawa nay eye ile hali ilikuwa ikimsumbua sana ila hakutaka kuona kuwa Erica ndio sababu ya kupona kwa Bahati kwani alijiona akizidi kukosa sifa za kuwa mke wa Bahati.
Ila badae aliwaza kitu kuhusu mwanamke aliyepokea simu ya Bahati na kuhisi kuwa huenda ni mdogo wake Siwema, kwakweli hakupenda na aliapa akikutana na Siwema basi alipize kisasi.
 
SEHEMU YA 433

Tony leo alienda nyumbani kwao tena kuongea na mama yake, na alimkuta vizuri kabisa akamsalimia na kuanza kuongea nae,
“Hivi mama unajisikiaje kuona kuwa Erica hayupo nyumbani na hujui alipo, unajisikiaje?”
“Maswali gani hayo ya kijinga unaniuliza?”
“Unajua mama, kuna mambo kama mzazi unatakiwa kuyasawazisha. Sio jambo jema kwa sie watoto wako kukosa uelekeo kabisa, mfano hutaki niwe na Tumaini, ila sababu Tumaini hapatani na Erica wakati huo huo Erica humtaki nyumbani sasa utasemaje unampenda Erica kwa mtindo huo mama?”
“Umetumwa au? Aliyekutuma mwambie sijawakuta wenyewe”
“Ila mama kwanini upo hivyo lakini?”
“Ngoja nikuulize, unatakaje yani?”
“Niruhusu mimi nimuoe Tumaini na Erica aolewe na Erick”
“Halafu harusi yenu mtaifanya siku moja eeeh!”
“Ikiwezekana”
“Nilijua tu, huna lolote unataka mdebwedo tu unajua Erick ataandaa kila kitu halafu wewe utaandaa tumbo lako hilo ule ukajisaidie, ila kwavile umelazimisha mwenyewe nataka nikukubalie kwa sharti moja”
“Sharti gani hilo mama?”
“Nataka Tumaini aje akae hapa kwa siku moja tu yani atakuja na kuondoka kesho yake, nataka nimuone utendaji wake wa kazi. Sio unaoa mwanamke wa maonyesho tu, mwanamke hajui kupika, hajui kufua, hajui kuosha vyombo, hajui kudeki, hapana kwakweli hata kama umempenda siwezi kuruhusu uoe kibwengo cha aina hiyo. Unaona hapa nyumbani, ukimuangalia Erica huko nje utamuona kama binti mzembe ila ndani kwangu hakunaga mfanyakazi ni kukukuruka mwenyewe kama hataki ajue siku hiyo hali, mimi napenda kufanya kazi na watoto wangu nao napenda wanaojishughulisha. Narudia tena, mwanamke wa maonyesho simtaki nyumbani kwangu”
“Kama sharti lenyewe ndio hilo basi Tumaini wangu kafaulu mia ya mia, nitamleta mama. Nitamleta Jumamosi atashinda hapa na kuondoka Jumapili, na mtakula chakula cha Tumaini kwahiyo msijali kitu”
“Haya tutaona, Yule anaonekana mzembe kabisa, na kalelewa maisha ya kitajiri ataweza kazi kweli?”
“Ila mama, mbona Erica nae anaonekana mzembe lakini kazi anafanya?”
“Usimfananishe Erica na huo uchafu wako”
Tony hakutaka kubishana sana na mama yake ila alikubaliana na swala kuwa Tumaini aje hapo ila tu aliwaza Tumaini anaweza kukubali kuja hapo kwao ikiwa anaujua mdomo wa mama yake.

Dora na James walikaa mule mule ndani bila kuweza kutoka, kwakweli James aliona kapatikana siku hiyo maana hakutegemea kabisa kama Yule mwanamke angemfanyia vile, James alitafuta kila njia ya kuweza kufungua ule mlango, aliangalia mule ndani kuwa hata kuna kijiko au kisu ila hakuona chochote cha kuweza kukorokochoa ule mlango maana Yule mwanamke alitoa vyombo vyote inaonyesha alihisi pengine watatumia kisu kufungua mlango, James alijaribu kutafuta simu yake ila mfukoni hakuwa na chochote yani Yule mwanamke alichukua na simu zao zote hadi funguo ya gari alichukua maana si walilala kwa ulevi kwahiyo kuna muda hawakujitambua kabisa,
“Dah huyu mwanamke kanikomesha aiseee dah”
“Tutakula nini sasa?”
“Yani Dora unawaza kula badala ya kuwaza tutatokaje hapa jamani!”
“Sasa. Kutoka haiwezekani na kula je! Nina kiu, nina njaa, jamani James huyu mwanamke ulimuokota wapi?”
“Yani najuta kumfahamu huyu mwanamke, kazi zangu zote zimegoma leo. Mijinga Yule kachukua hadi funguo za nyumba yangu, sijui ataenda kufanya nini kule”
“Na hujaweka mlinzi nyumbani kwako?”
“Nilimtimua maana alikuwa ananifatilia sana na kumwambia mke wangu, hapa ndio najuta sijui nitafanyaje”
Yani waliona usiku ukiingia huku wakiwa bado ndani ya kile chumba, kwakweli Dora alikuwa na njaa sana na akaona kwa muda huo hakuna jinsi zaidi ya kujipa uchizi na kuanza kupiga kelele, basi Dora alianza kupiga kelele za yowe na kufanya watu wajae nje ya chumba kile, na baada ya kelele kuzidi ndipo raia walipojitolea kuvunja ule mlango, yani walitoka mule hawana chochote, si simu si funguo ya gari na hata gari haikuwepo na si hela yoyote maana Yule mwanamke alikomba hela zote, James aliamua kumuomba mmoja aliyewasaidia kutoka hela na kumuahidi kumrejeshea,
“Aaaah sikufahamu kaka utanirudishiaje?”
“Chukua kitanda cha humu ndani, naomba elfu ishirini tu”
Kwa kuambiwa vile, Yule mtu alitoa ile hela bila utata na kutoa kile kitanda ndani, ila James muda huo hakujali kuwa mlango haujafungwa mwala nini ila aliita bajaji kisha wakapanda na kuondoka na Dora.

Steve aliondoka ila alirudi tena kwa Sia maana hakuweza hata kukaa nyumbani kwao, alirudi na kumuomba sana Sia kuwa waishi tu na hatojaribu tena kumsemea neno baya.
“Basi siku hizi nataka mchana usishinde huku kabisa yani uje usiku tu, sawa?”
“Sawa mpenzi wangu”
Steve alifurahi sana kukubaliwa tena na Sia, kisha akakumbatiana nae kwa furaha. Sababu giza lilikuwa limeingia na Sia alitamani kupata upepo wan je, akatoa mkeka na mto na kwenda kukaa nao nje, muda huu alijilaza kwenye miguu ya Steve huku wakiongea ongea mambo mbalimbali.
Mamam Erick alipata jambo na aliona kuwa lile jambo asikawie nalo, aende kumwambia Sia hata kama muda umeenda ndipo alipoenda hapo nyumbani kwa Sia na kumkuta Sia yupo kwenye miguu ya Steva, akawashtua na kuwaambia,
“Wewe Sia si ulisema huyu ni kijana wako wa kazi? Hata hivyo si nilikwambia umuondoe wewe”
Sia akainama chini kwa aibu kwani hakuwa na cha kujieleza


Mama Erick alipata jambo na aliona kuwa lile jambo asikawie nalo, aende kumwambia Sia hata kama muda umeenda ndipo alipoenda hapo nyumbani kwa Sia na kumkuta Sia yupo kwenye miguu ya Steva, akawashtua na kuwaambia,
“Wewe Sia si ulisema huyu ni kijana wako wa kazi? Hata hivyo si nilikwambia umuondoe wewe”
Sia akainama chini kwa aibu kwani hakuwa na cha kujieleza.
Mama Erick aliendelea kuongea,
“Kataaa sasa kwa kinywa chako kuwa huyu si mwanaume wako, ni kijana wa kazi. Hivi kwa mtindo huu ukimwi utaisha kweli? Juzi tu ulikuwa na Erick huku na leo unajiachia na huyo kijana?”
Muda huu aliamua kujitetea,
“Erick hajawahi kuja kulala huku, na huyu kijana nimejinyoosha tu sio kwamba mtu wangu”
“Sia, mimi sio mtoto mwenzio ambaye ukiamua kumdanganya tu unamdanganya sawa? Mimi ni mtu mzima mwenye akili zangu timamu, ngoja niondoke zangu hapa nisije kutenda dhambi bure maana wengine hasira zetu zipo karibu”
Basi mama Erick aliondoka na kupanda gari lake kuelekea nyumbani kwake huku analalamika mwenyewe,
“Mapenzi bhana sijui ni kitu gani jamani, wanaume waongo, wanawake waongo jamani! Hivi hakuna hata abnayeweza kuwa mkweli angalau kwa uchache jamani! Dah”
Alifika nyumbani kwake na kuamua kuoga na kwenda kujipumzisha tu kwani hakuwa hata nay a kuongea kwa wakati huo.
Asubuhi na mapemz kama kawaida aliamka na kwenda zake kazini kwake kwenye kazi yake, ila muda ule ule wa asubuhi alipita mzee Jimmy ofisini kwake na kukumbuka kuwa jana kabla hajaenda kwa Sia alimpigia mtu huyo na kumwambia kuwa waonane kwaajili ya kuzungumza kuhusu mtoto wao,
“Eeeeh nimepokea wito”
“Yani, unajua kuna jambo nililifikiria kuhusu Erick, niliona kuliko mtoto kutangatanga na maisha na mwisho wa siku kuwa kama wazazi wake ambapo baba yake hajaoa mpaka leo na mama yake hajaolewa, mwishowe watu watasema mtoto karithi bure. Najua umri wa Erick sio mkubwa sana wa kusema ni lazima aoe kwa kipindi hiki ila baada ya kugundua kuna mwanamke mwenye mimba yake nikaona ni bora tufanye mipango waoane kuliko kuishi tu. Ila sasa nilichogundua kuhusu huyo mwanamke ndio kimenikata maini kabisa”
“Kwahiyo wewe hukumjua Erica eeeh! Umegundua nini?”
“Kwanza simuongelei Erica hapa, namuongelea Sia”
“Aaaah kumbe unamuongelea huyo mtoto asiyejielewa, yani hajielewi huyo binti sijui kama kichwa chake ni kizima, alinidanganya kuwa ana mimba ya Erick na hata mimi kufanya jitihada zote awe pamoja na Erick nakuja kugundua ana kajamaa kengine, binti hajielewi Yule”
“Kheeee kumbe ningekwambia mapema ningejua dah! Mimi ndio nimejua jana, nimemkuta kajiachia na huyo mwanaume, kwanza mvulana mwenyewe mdogo Yule atampa nini zaidi ya kumuongezea umasikini tu”
“Ndio hapo, na ile mimba si ya Erick maana Erick kaikataa kabisa”
“Basi ndio nilichokuitia hiko ila Erick hajakataa ile mimba kwangu, maana majuzi nilimwambia aje kulala nyumbani akasingizia kuwa amelala kwa Sia”
“Aaaah mwanao muongo tena muongo kabisa, kwanza siku hizi hakai nyumbani asije akakudanganya muda mwingine kuwa yupo nyumbani.”
“Kwahiyo anakaa wapi?”
“Mwanao sijui kapanga wapi huko na Erica ndio anaishi nae”
“Unasemaje! Erick anaishi na Erica?”
“Ndio hivyo, yani pika pakua wako wote. Erica katoroka kwao na Erick katoroka kwangu wanaishi wote”
“Mmmh hiyo habari imenichanganya zaidi ujue, yani nahisi kama kichwa kinazunguka hapa, kweli Erick dah! Halafu Yule binti ni mshirikina yani namuhurumia Erick jamani, nitamtafuta niongee nae, ndiomana anapokea simu kwa uoga sana kumbe kuna maovu ameyafanya. Dah nimesikitika sana”
Mzee Jimmy akainuka na kumuaga mama Erick na akajua sasa ameacha jambo la Erick kwenye mikono ya mama yake maana anamjua huyu mwanamke kama kitu haktaki ni hataki hata iweje, kwahiyo aliondoka na tabasamu pana sana kugundua kuwa hata mama Erick anapinga mahusiano ya Erick na Erica.
 
Back
Top Bottom