Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #501
SEHEMU YA 394
Mara mdogo wake Dora alitoka kwenye chumba cha Sia na kusogea karibu kisha kumkumbatia Sia na kumwambia dada yake,
“Wewe ondoka zako tu maana mimi kwa Sia ndio nimefika”
Kisha akambusu Sia, haya mambo yote Tumaini aliyaona na kuyasikia kwakweli yalimstaajabisha sana.
Tumaini hakuamini kile kitu na kujihisi kama yupo ndotoni, aliamua kujitokeza katikati yao, kitendo kile cha Sia kumuona Tumaini mbele yao akamsukumiza Steve, kile kitu kilimsikitisha zaidi Tumaini na kusema,
“Sia hata usingemsukumiza huyo maana nimesikia kila kitu, ila mpaka muda huu nashindwa kuamini, hivi si ni wewe Sia uliyekunywa sumu kwaajili ya kaka yangu? Inamaana ulikuwa unaigiza kunywa sumu? Upendo uliousema unao dhidi ya kaka yangu uko wapi?”
Sia alianza kujitetea kwa kuomba msamaha
“Nisamehe Tumaini, mimi ni mwanamke mwenzio”
“Hebu nitolee ujinga mie, mwanmke mwenzangu kwenye mambo ya kijinga kama hivi! Nilikuwa nakuamini sana ila imani yangu umeipoteza.”
Dora alikuwa anaangalia tu na kushangaa aliyechukuliwa dawa alikuwa ni kaka wa Tumaini, sababu hakutaka umbea umpite akauliza,
“Huyo kaka yako ni nani Tumaini? Namfahamu?”
“Utakuwa unamfahamu ndio, anaitwa Erick”
“Kheee kumbe ni Yule Erick mpenzi wa Erica?”
“Ndio huyo huyo”
“Kheee kumbe Sia nilikubali kukupeleka kwa mganga ukamroge shemeji yangu jamani!”
Tumaini aliposikia kuwa Dora ndiye aliyempeleka Sia kwa mganga ndio akafunguka macho kabisa na kusema,
“Kumbe ni kweli alienda kwa mganga?”
“Ndio ni kweli, na bahati mbaya kakako hakula lile tunda ndio likaliwa na huyo mdogo wangu hapo ambaye hasikii kwasasa wala haoni anadai anampenda tu Sian a hakubali kuwa amerogwa”
Na kweli ingawa Steve alisukumiwa pembeni ila kusikia ile mada ya kurogwa alisogea karibu na Sian a kusema,
“Mimi sijarogwa, ni mapenzi yangu. Nampenda sana huyu mwanamke toka moyoni na ndio nitamuoa na atakuwa mke wangu daima”
Kwakweli Tumaini alizidi kushangaa sana yani alijikuta akimchukia Sia gafla maana hakutegemea kuwa Sia angeweza kwenda kwa mganga kwaajili ya kumroga Erick, kwahiyo kwa yale maneno ilikuwa kama ni uthibitisho. Alisikitika sana na kusema,
“Yani kwa ulichofanya leo Sia, sitaki tena kukuona kwetu. Sitaki tena urafiki na wewe”
“Wananisingizia Tumaini”
Tumaini hakutaka kumsikiliza Sia kwakweli maana alichokisikia hakupenda hata kidogo, moja kwa moja aliondoka. Na aliamua kwenda kwa mama yake ili amsimulie kidogo ndio aende kwao maana alihisi akili yake kutokuwa sawa kabisa.
Alifika na kumkuta mama yake, akamsalimia na kuanza kumsimulia yaliyotokea siku hiyo,
“Unaona sasa mwanangu, unagombana na kaka yako sababu ya mwanamke mshirikina. Huyo hakuwa anampenda kaka yako wala nini maana kama kumpenda asingemuendea kwa mganga maana kama mtu unampenda kweli hutotoka kumsumbua kwa madawa, utapenda akupende ule upendo halisia, na ule upendo halisia ni mzuri sana maana unajisikia kuwa unapendwa yani hata wewe unajihisi raha”
“Ila mama huyo msichana alikunywa hadi sumu sababu ya Erick”
“Hakumpenda Erick huyo mwanangu, na labda alikunywa sumu kuwapima imani tu, huyo kuna kitu alihitaji kwa Erick ndiomana kaweza kumwendea hadi kwa mganga, tena shukuru Mungu umegundua mapema kabla hajawa wifi yako maana ungejuta huyo, angefanya uone maisha machungu maana angemfanya kaka yako ndondocha yani kila ambacho ungemwambia asingekuelewa sababu yake. Mwanangu hakuna upendo mzuri kama upendo halisia, hakika hata mimi ningeangalia upendo halisia basi nisingezaa na baba yako ila hela zake zilinichanganya sana na kuhisi kuwa ananipenda na kuhisi nitaishi kama malkia kwenye himaya yake, kumbe hakuwa na upendo na mimi hata kidogo na nilimgundua baada ya kuzaa tu”
“Mmmh mama, hivi baba anampenda nani? Maana toka nikae nae sijawahi msikia akitaka kuoa wala akisema labda nimuoe mama yake Erick maana Yule mama nae anaishi mwenyewe”
“Yule baba yenu nadhani hajielewi, yupo yupo tu. Nilijua angenioa wapi, nimezaa ndio akanipiga teke kabisa, basi mama Erick nilijua atamuoa wapi, ndio kwanza amezaa nasikia hata hospitali hakwenda kumchukua yani Yule mwanamke kahudumiwa na mdogo wake mwanzo mwisho ndiomana anamthamini sana mdogo wake, Yule mzee ana wazimu Yule mpaka leo yupo yupo tu ila nasikia ana wanawake wengi balaa”
“Ila hajawahi kuwaleta nyumbani mama, baba yetu anajiheshimu”
“Angejiheshimu angeoa, pesa anayo, mali anayo, kitu gani kinamshinda asioe? Kaeni vizuri na baba yenu muulizeni vizuri kuwa kwanini haoi?”
“Sawa mama”
Tumaini aliongea ongea pale na mama yake kisha akajiandaa kurudi kwao tu maana siku hiyo alikuwa amechefuka haswaa na yale aliyoyaona kwa Sia.
Dora alimuangalia Sia bila kummaliza maana alijilaumu sana kumpeleka Sia kwa mganga kwanza kumbe ilikuwa ni kuharibu mahusiano ya rafiki yake na pia imepelekea kuharibu akili ya mdogo wake, kisha akaanza kumwambia,
“Hivi wewe Sia aliyekwambia kwamba penzi linatafutwa kwa dawa nani?”
“Na wewe hebu ukae kimya huko, kumbuka ni wewe mwenyewe ndio ulinipeleka kwa Yule mganga. Kama penzi halinunuliwi kwa mganga na wewe ulienda kufanya dawa upendwe ili iweje? Mimi bila kujua kama kuna dawa uliifanya ya kupendwa na wewe mwenyewe kunipa ushuhuda ningejuaje kama kwa mganga kuna dawa ya mapenzi? Unaponisema mimi nijiangalie na wewe kungwi”
“Sikatai ni kweli nilienda kwa mganga ila lengo langu na lako halifanani, niliamua kumfanyia James dawa sababu nilipanga kumkomesha na nilifanya vile sio sababu nilikuwa nampenda hapana, nilitaka kumchuna tu pesa zake. Sasa wewe shoga yangu kumfanyia dawa mwanaume ili akupende ni vipi hapo? Hivi unajisikiaje ukipendwa na mwanaume kwa upendo wa dawa? Inanoga kweli?”
“Bhana eeeh achana na mimi”
“Niachane na wewe kitu gani? Mdogo wangu akomboke huyu, uende kwenye maombi”
“Siendi popote, achana na mimi kwanza wewe ni mbaya sana ushanipotezea laki moja yangu jumlisha na zile hasara za nauli na chakula kwenda huko Bagamoyo ndani ndani, wala sijapenda kabisa, naomba tu uende”
“Siwezi kwenda na kumuacha mdogo wangu”
“Si umchukue, huyo hapo mchukue kama mtoto mdogo mbebe mgongoni”
Kiukweli Dora alichukia sana kama angeweza kupigana na huyu Sia kwa hakika angepigana nae ila uwezo wa kupigana na huyu Sia hakuwa nao kwani alionekana kuwa na nguvu kushinda yeye na ndiomana hata Tumaini hakuweza kumzaba vibao Sia maana amehisi kuwa pengine angepigwa yeye ndiomana alijiondokea tu.
Basi Dora akamwambia,
“Sia, subiri tu nione hivi hivi nilivyo ila hiko ulichomfanyia mdogo wangu utalipia nakwambia yani utalipia, nimeachana na mambo ya waganga ila naweza kurudi tena sababu yako kwaheri”
Dora aliondoka pale na hata mdogo wake hakujigusa kumuuliza kuwa mbona anaondoka akiwa amechukia vilke kwani yeye alijionea kawaida tu.
Dora akiwa njiani huku ananung’unika mwenyewe, kuna gari ilipaki karibu yake, kisha Yule wa kwenye gari alishusha kioo, basi Dora akamuangalia akakuta ni George akafurahi sana na kwenda kupanda kwenye gari ya George huku akimsalimia.
“Mmmh za siku George, inaonekana maisha yako mazuri siku hizi eeeh!”
“Kiasi chake kwakweli namshukuru Mungu, twende nikupeleke kwangu”
“Twende tu”
Kwa muda huo hata hakufikiria kuwa muda umeenda na anataka kurudi kwao ila aliondoka na George tu.
Mara mdogo wake Dora alitoka kwenye chumba cha Sia na kusogea karibu kisha kumkumbatia Sia na kumwambia dada yake,
“Wewe ondoka zako tu maana mimi kwa Sia ndio nimefika”
Kisha akambusu Sia, haya mambo yote Tumaini aliyaona na kuyasikia kwakweli yalimstaajabisha sana.
Tumaini hakuamini kile kitu na kujihisi kama yupo ndotoni, aliamua kujitokeza katikati yao, kitendo kile cha Sia kumuona Tumaini mbele yao akamsukumiza Steve, kile kitu kilimsikitisha zaidi Tumaini na kusema,
“Sia hata usingemsukumiza huyo maana nimesikia kila kitu, ila mpaka muda huu nashindwa kuamini, hivi si ni wewe Sia uliyekunywa sumu kwaajili ya kaka yangu? Inamaana ulikuwa unaigiza kunywa sumu? Upendo uliousema unao dhidi ya kaka yangu uko wapi?”
Sia alianza kujitetea kwa kuomba msamaha
“Nisamehe Tumaini, mimi ni mwanamke mwenzio”
“Hebu nitolee ujinga mie, mwanmke mwenzangu kwenye mambo ya kijinga kama hivi! Nilikuwa nakuamini sana ila imani yangu umeipoteza.”
Dora alikuwa anaangalia tu na kushangaa aliyechukuliwa dawa alikuwa ni kaka wa Tumaini, sababu hakutaka umbea umpite akauliza,
“Huyo kaka yako ni nani Tumaini? Namfahamu?”
“Utakuwa unamfahamu ndio, anaitwa Erick”
“Kheee kumbe ni Yule Erick mpenzi wa Erica?”
“Ndio huyo huyo”
“Kheee kumbe Sia nilikubali kukupeleka kwa mganga ukamroge shemeji yangu jamani!”
Tumaini aliposikia kuwa Dora ndiye aliyempeleka Sia kwa mganga ndio akafunguka macho kabisa na kusema,
“Kumbe ni kweli alienda kwa mganga?”
“Ndio ni kweli, na bahati mbaya kakako hakula lile tunda ndio likaliwa na huyo mdogo wangu hapo ambaye hasikii kwasasa wala haoni anadai anampenda tu Sian a hakubali kuwa amerogwa”
Na kweli ingawa Steve alisukumiwa pembeni ila kusikia ile mada ya kurogwa alisogea karibu na Sian a kusema,
“Mimi sijarogwa, ni mapenzi yangu. Nampenda sana huyu mwanamke toka moyoni na ndio nitamuoa na atakuwa mke wangu daima”
Kwakweli Tumaini alizidi kushangaa sana yani alijikuta akimchukia Sia gafla maana hakutegemea kuwa Sia angeweza kwenda kwa mganga kwaajili ya kumroga Erick, kwahiyo kwa yale maneno ilikuwa kama ni uthibitisho. Alisikitika sana na kusema,
“Yani kwa ulichofanya leo Sia, sitaki tena kukuona kwetu. Sitaki tena urafiki na wewe”
“Wananisingizia Tumaini”
Tumaini hakutaka kumsikiliza Sia kwakweli maana alichokisikia hakupenda hata kidogo, moja kwa moja aliondoka. Na aliamua kwenda kwa mama yake ili amsimulie kidogo ndio aende kwao maana alihisi akili yake kutokuwa sawa kabisa.
Alifika na kumkuta mama yake, akamsalimia na kuanza kumsimulia yaliyotokea siku hiyo,
“Unaona sasa mwanangu, unagombana na kaka yako sababu ya mwanamke mshirikina. Huyo hakuwa anampenda kaka yako wala nini maana kama kumpenda asingemuendea kwa mganga maana kama mtu unampenda kweli hutotoka kumsumbua kwa madawa, utapenda akupende ule upendo halisia, na ule upendo halisia ni mzuri sana maana unajisikia kuwa unapendwa yani hata wewe unajihisi raha”
“Ila mama huyo msichana alikunywa hadi sumu sababu ya Erick”
“Hakumpenda Erick huyo mwanangu, na labda alikunywa sumu kuwapima imani tu, huyo kuna kitu alihitaji kwa Erick ndiomana kaweza kumwendea hadi kwa mganga, tena shukuru Mungu umegundua mapema kabla hajawa wifi yako maana ungejuta huyo, angefanya uone maisha machungu maana angemfanya kaka yako ndondocha yani kila ambacho ungemwambia asingekuelewa sababu yake. Mwanangu hakuna upendo mzuri kama upendo halisia, hakika hata mimi ningeangalia upendo halisia basi nisingezaa na baba yako ila hela zake zilinichanganya sana na kuhisi kuwa ananipenda na kuhisi nitaishi kama malkia kwenye himaya yake, kumbe hakuwa na upendo na mimi hata kidogo na nilimgundua baada ya kuzaa tu”
“Mmmh mama, hivi baba anampenda nani? Maana toka nikae nae sijawahi msikia akitaka kuoa wala akisema labda nimuoe mama yake Erick maana Yule mama nae anaishi mwenyewe”
“Yule baba yenu nadhani hajielewi, yupo yupo tu. Nilijua angenioa wapi, nimezaa ndio akanipiga teke kabisa, basi mama Erick nilijua atamuoa wapi, ndio kwanza amezaa nasikia hata hospitali hakwenda kumchukua yani Yule mwanamke kahudumiwa na mdogo wake mwanzo mwisho ndiomana anamthamini sana mdogo wake, Yule mzee ana wazimu Yule mpaka leo yupo yupo tu ila nasikia ana wanawake wengi balaa”
“Ila hajawahi kuwaleta nyumbani mama, baba yetu anajiheshimu”
“Angejiheshimu angeoa, pesa anayo, mali anayo, kitu gani kinamshinda asioe? Kaeni vizuri na baba yenu muulizeni vizuri kuwa kwanini haoi?”
“Sawa mama”
Tumaini aliongea ongea pale na mama yake kisha akajiandaa kurudi kwao tu maana siku hiyo alikuwa amechefuka haswaa na yale aliyoyaona kwa Sia.
Dora alimuangalia Sia bila kummaliza maana alijilaumu sana kumpeleka Sia kwa mganga kwanza kumbe ilikuwa ni kuharibu mahusiano ya rafiki yake na pia imepelekea kuharibu akili ya mdogo wake, kisha akaanza kumwambia,
“Hivi wewe Sia aliyekwambia kwamba penzi linatafutwa kwa dawa nani?”
“Na wewe hebu ukae kimya huko, kumbuka ni wewe mwenyewe ndio ulinipeleka kwa Yule mganga. Kama penzi halinunuliwi kwa mganga na wewe ulienda kufanya dawa upendwe ili iweje? Mimi bila kujua kama kuna dawa uliifanya ya kupendwa na wewe mwenyewe kunipa ushuhuda ningejuaje kama kwa mganga kuna dawa ya mapenzi? Unaponisema mimi nijiangalie na wewe kungwi”
“Sikatai ni kweli nilienda kwa mganga ila lengo langu na lako halifanani, niliamua kumfanyia James dawa sababu nilipanga kumkomesha na nilifanya vile sio sababu nilikuwa nampenda hapana, nilitaka kumchuna tu pesa zake. Sasa wewe shoga yangu kumfanyia dawa mwanaume ili akupende ni vipi hapo? Hivi unajisikiaje ukipendwa na mwanaume kwa upendo wa dawa? Inanoga kweli?”
“Bhana eeeh achana na mimi”
“Niachane na wewe kitu gani? Mdogo wangu akomboke huyu, uende kwenye maombi”
“Siendi popote, achana na mimi kwanza wewe ni mbaya sana ushanipotezea laki moja yangu jumlisha na zile hasara za nauli na chakula kwenda huko Bagamoyo ndani ndani, wala sijapenda kabisa, naomba tu uende”
“Siwezi kwenda na kumuacha mdogo wangu”
“Si umchukue, huyo hapo mchukue kama mtoto mdogo mbebe mgongoni”
Kiukweli Dora alichukia sana kama angeweza kupigana na huyu Sia kwa hakika angepigana nae ila uwezo wa kupigana na huyu Sia hakuwa nao kwani alionekana kuwa na nguvu kushinda yeye na ndiomana hata Tumaini hakuweza kumzaba vibao Sia maana amehisi kuwa pengine angepigwa yeye ndiomana alijiondokea tu.
Basi Dora akamwambia,
“Sia, subiri tu nione hivi hivi nilivyo ila hiko ulichomfanyia mdogo wangu utalipia nakwambia yani utalipia, nimeachana na mambo ya waganga ila naweza kurudi tena sababu yako kwaheri”
Dora aliondoka pale na hata mdogo wake hakujigusa kumuuliza kuwa mbona anaondoka akiwa amechukia vilke kwani yeye alijionea kawaida tu.
Dora akiwa njiani huku ananung’unika mwenyewe, kuna gari ilipaki karibu yake, kisha Yule wa kwenye gari alishusha kioo, basi Dora akamuangalia akakuta ni George akafurahi sana na kwenda kupanda kwenye gari ya George huku akimsalimia.
“Mmmh za siku George, inaonekana maisha yako mazuri siku hizi eeeh!”
“Kiasi chake kwakweli namshukuru Mungu, twende nikupeleke kwangu”
“Twende tu”
Kwa muda huo hata hakufikiria kuwa muda umeenda na anataka kurudi kwao ila aliondoka na George tu.