Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #161
SEHEMU YA 135
Alipokuwa kwao alifikiria sana, na kuanza kuhisi huenda maneno aliyoyasema Fetty yana ukweli kuwa huenda Derick ndio amesambaza habari mbaya kuhusu yeye,
“Itakuwa ni Derick tu maana ndio aliyeshuhudia wale vijana waliotaka kunibaka, jamani kwanini ananifanyia hivi wakati ni ndugu yangu! Na habari kubwa anayotaka kueneza kuhusu mimi ni ipi?”
Akawaza sana na kusema,
“Mungu wangu, asije akaeneza kuwa nimetoa mimba, jamani nitaweka wapi sura yangu mimi Erica? Najuta kumfahamu huyu mtu, ni kwanini nimempata ndugu wa aina hii?”
Aliwaza sana, na kusema kuwa kesho yake ataenda kumtafuta Derick ili aongee nae na aache kumfanyia vitu vya ajabu kiasi hiko kama kumsambazia vitu vya uongo, kiukweli Erica hakuwa na raha kabisa na alijiona akikosa amani moyoni mwake kila siku maana ni kama liliibuka jipya kila siku, usiku ulifika na mama yake alimuuliza kuwa imekuwaje amerudi tena kutoka chuoni, alisema uongo wake wa kumkumbuka ila kiukweli chuo kile kilianza kumchosha kwa kipindi hiko.
Kesho yake alienda chuoni na alimtafuta Derick hewani ili aonane nae, na kweli Derick alikubali kuonana nae na kwenda kuongea nae,
“Derick kwanini lakini umeamua kunifanyia hivi? Kweli kabisa wewe ni wa kueleza habari mbaya kunihusu mimi?”
“Habari gani Erica?”
“Wewe umewaambia watu kuwa mimi nilibakwa na wanaume wane sijui, jamani Derick, unajua fika kuwa sikubakwa, kweli ni wa kunisambazia habari za hivyo?”
“Erica, kwani habari hizo ni za uongo”
“Ndio ni uongo, kwani wewe hukuona kama sikubakwa?”
“Kama hukubakwa mbona ulikubali twende kupima mimba na magonjwa ya zinaa? Erica, unaweza kumdanganya mtoto ila sio mimi, na kila leo unajiliza liza, hata hivyo habari hizo zilizagaa kipindi kile kile hata sijagundua kuwa wewe ni ndugu yangu”
“Sasa umepata faida gani kwa mfano kunisema hivyo? Unataka watu wanichukie eeh! Unajua wewe ni muuwaji?”
“Hivi uuwaji wangu mimi unaweza kufikia uuwaji wako wa kutoa mimba? Nyie kwenu ni wauaji ndiomana mamako hakunitaka”
“Hivi wewe Derick unaongea au unaropoka? Jamani siku ile da Mage si amesema maneno ambayo mimi na wewe hatukuyajua kabisa, kwanza kumbuka ulilala na mimi bila ridhaa yangu, halafu unataka nionekane malaya, hivi ukoje Derick, wewe ni mtoto wa baba kweli? Labda baba alisingiziwa tu”
Derick akacheka kwa kejeli na kusema,
“Mamako hajanipa haki zangu sababu naye akikazania kuwa mimi ni mtoto wa kusingiziwa, sikia nikwambie Erica, siku niliyogundua kuwa wewe ni ndugu yangu nimekuchukia balaa. Katika watoto wa baba nampenda dada Mage tu sababu amekuwa name bega kwa bega maisha yote, hivi wewe ulishindwa kuzaa hadi kwenda kutoa ile mimba kama sio mchezo wako? Hata kama nilifanya mapenzi nawe kwa bahati mbaya ila si ungezaa tu na tungeendelea kufanya iwe siri maana kama mapenzi tumefanya kweli”
“Basi yaishe, tushakuwa ndugu sasa naomba yaishe. Niheshimu kama dada yako”
“Nitaanza kukuheshimu pale tu nitakaposema kuwa ulitoa mimba na watu wote wajue rangi yako halisi, maana unaonekana binti mpole kumbe hakuna lolote”
Erica alihisi kuchanganyikiwa kabisa maana huyu ndugu yake hakumuelewa hata kidogo aliona akimchanganya tu akili hata akajiuliza kuwa baba yao alianzaje kuzaa nje mtoto wa aina ile asiyekuwa na akili ya utu hata kidogo.
“Hivi Derick, undugu wa wewe na mimi uko wapi? Hivi unajua kuwa mimi ni dada yako?”
“Tena nitasambaza kuwa huna aibu umelala na kaka yako hadi ukapata mimba na mimba hiyo ukaenda kutoa, yani Erica utapata sifa chafu sana kutoka kwangu. Unafikiri maisha niliyoishi mimi niliyafurahia? Mama yangu alipata shida sana sababu ya mama yako na tena alisema baba alikataa nisilelewe pale sababu mkewe alikuwa na mtoto mdogo, umefanya nikose upendo wa baba, halafu unajishauwa nini? Nataka upate uchungu nilioupata mimi wa kuishi bila upendo wa baba”
“Derick unadhani utapata faida gani kufanya hivyo? Au maisha uliyoishi wewe kutaka wengine wayaishi kutakufaidisha nini? Sasa mimi nahusika vipi na kuteseka kwako? Wakulaumiwa sio mimi ni baba”
“Sikia Erica, mimi nimeteseka sana sababu sijawahi kupata upendo wa baba, kila mwanaume aliyetaka kumuoa mama yangu haikuwezekana sababu mama ana mtoto ambaye ni mimi, baba amemfanya mama yangu asifurahie kama kuna kitu kinaitwa ndoa maishani mwake, nimeteseka sana mimi, na wewe ukaenda kutoa mimba kama ambavyo baba alitaka mimba yangu itolewe”
“Sasa ulitaka nizae mtoto wa laana, tena bora hata mimba yako ingetolewa tusingeletewa machizi kama wewe duniani”
“Mimi chizi eeeh! Subiri, uchizi wangu utauona vizuri, hiki chuo kitakuwa kichungu sana kwako”
Erica alimshangaa sana huyu Derick yani hakumuelewa kabisa, Yule Derick akaondoka zake kisha Erica nae akaondoka zake na kurudi hosteli huku akiwa na mawazo mengi sana maana akili yake alihisi ikiruka kabisa.
Alipokuwa kwao alifikiria sana, na kuanza kuhisi huenda maneno aliyoyasema Fetty yana ukweli kuwa huenda Derick ndio amesambaza habari mbaya kuhusu yeye,
“Itakuwa ni Derick tu maana ndio aliyeshuhudia wale vijana waliotaka kunibaka, jamani kwanini ananifanyia hivi wakati ni ndugu yangu! Na habari kubwa anayotaka kueneza kuhusu mimi ni ipi?”
Akawaza sana na kusema,
“Mungu wangu, asije akaeneza kuwa nimetoa mimba, jamani nitaweka wapi sura yangu mimi Erica? Najuta kumfahamu huyu mtu, ni kwanini nimempata ndugu wa aina hii?”
Aliwaza sana, na kusema kuwa kesho yake ataenda kumtafuta Derick ili aongee nae na aache kumfanyia vitu vya ajabu kiasi hiko kama kumsambazia vitu vya uongo, kiukweli Erica hakuwa na raha kabisa na alijiona akikosa amani moyoni mwake kila siku maana ni kama liliibuka jipya kila siku, usiku ulifika na mama yake alimuuliza kuwa imekuwaje amerudi tena kutoka chuoni, alisema uongo wake wa kumkumbuka ila kiukweli chuo kile kilianza kumchosha kwa kipindi hiko.
Kesho yake alienda chuoni na alimtafuta Derick hewani ili aonane nae, na kweli Derick alikubali kuonana nae na kwenda kuongea nae,
“Derick kwanini lakini umeamua kunifanyia hivi? Kweli kabisa wewe ni wa kueleza habari mbaya kunihusu mimi?”
“Habari gani Erica?”
“Wewe umewaambia watu kuwa mimi nilibakwa na wanaume wane sijui, jamani Derick, unajua fika kuwa sikubakwa, kweli ni wa kunisambazia habari za hivyo?”
“Erica, kwani habari hizo ni za uongo”
“Ndio ni uongo, kwani wewe hukuona kama sikubakwa?”
“Kama hukubakwa mbona ulikubali twende kupima mimba na magonjwa ya zinaa? Erica, unaweza kumdanganya mtoto ila sio mimi, na kila leo unajiliza liza, hata hivyo habari hizo zilizagaa kipindi kile kile hata sijagundua kuwa wewe ni ndugu yangu”
“Sasa umepata faida gani kwa mfano kunisema hivyo? Unataka watu wanichukie eeh! Unajua wewe ni muuwaji?”
“Hivi uuwaji wangu mimi unaweza kufikia uuwaji wako wa kutoa mimba? Nyie kwenu ni wauaji ndiomana mamako hakunitaka”
“Hivi wewe Derick unaongea au unaropoka? Jamani siku ile da Mage si amesema maneno ambayo mimi na wewe hatukuyajua kabisa, kwanza kumbuka ulilala na mimi bila ridhaa yangu, halafu unataka nionekane malaya, hivi ukoje Derick, wewe ni mtoto wa baba kweli? Labda baba alisingiziwa tu”
Derick akacheka kwa kejeli na kusema,
“Mamako hajanipa haki zangu sababu naye akikazania kuwa mimi ni mtoto wa kusingiziwa, sikia nikwambie Erica, siku niliyogundua kuwa wewe ni ndugu yangu nimekuchukia balaa. Katika watoto wa baba nampenda dada Mage tu sababu amekuwa name bega kwa bega maisha yote, hivi wewe ulishindwa kuzaa hadi kwenda kutoa ile mimba kama sio mchezo wako? Hata kama nilifanya mapenzi nawe kwa bahati mbaya ila si ungezaa tu na tungeendelea kufanya iwe siri maana kama mapenzi tumefanya kweli”
“Basi yaishe, tushakuwa ndugu sasa naomba yaishe. Niheshimu kama dada yako”
“Nitaanza kukuheshimu pale tu nitakaposema kuwa ulitoa mimba na watu wote wajue rangi yako halisi, maana unaonekana binti mpole kumbe hakuna lolote”
Erica alihisi kuchanganyikiwa kabisa maana huyu ndugu yake hakumuelewa hata kidogo aliona akimchanganya tu akili hata akajiuliza kuwa baba yao alianzaje kuzaa nje mtoto wa aina ile asiyekuwa na akili ya utu hata kidogo.
“Hivi Derick, undugu wa wewe na mimi uko wapi? Hivi unajua kuwa mimi ni dada yako?”
“Tena nitasambaza kuwa huna aibu umelala na kaka yako hadi ukapata mimba na mimba hiyo ukaenda kutoa, yani Erica utapata sifa chafu sana kutoka kwangu. Unafikiri maisha niliyoishi mimi niliyafurahia? Mama yangu alipata shida sana sababu ya mama yako na tena alisema baba alikataa nisilelewe pale sababu mkewe alikuwa na mtoto mdogo, umefanya nikose upendo wa baba, halafu unajishauwa nini? Nataka upate uchungu nilioupata mimi wa kuishi bila upendo wa baba”
“Derick unadhani utapata faida gani kufanya hivyo? Au maisha uliyoishi wewe kutaka wengine wayaishi kutakufaidisha nini? Sasa mimi nahusika vipi na kuteseka kwako? Wakulaumiwa sio mimi ni baba”
“Sikia Erica, mimi nimeteseka sana sababu sijawahi kupata upendo wa baba, kila mwanaume aliyetaka kumuoa mama yangu haikuwezekana sababu mama ana mtoto ambaye ni mimi, baba amemfanya mama yangu asifurahie kama kuna kitu kinaitwa ndoa maishani mwake, nimeteseka sana mimi, na wewe ukaenda kutoa mimba kama ambavyo baba alitaka mimba yangu itolewe”
“Sasa ulitaka nizae mtoto wa laana, tena bora hata mimba yako ingetolewa tusingeletewa machizi kama wewe duniani”
“Mimi chizi eeeh! Subiri, uchizi wangu utauona vizuri, hiki chuo kitakuwa kichungu sana kwako”
Erica alimshangaa sana huyu Derick yani hakumuelewa kabisa, Yule Derick akaondoka zake kisha Erica nae akaondoka zake na kurudi hosteli huku akiwa na mawazo mengi sana maana akili yake alihisi ikiruka kabisa.