Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
Simulizi: NINI MAANA YA MAPENZI
Mwandishi: ATUGANILE MWAKALILE
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
SEHEMU YA 1
Alikuwa binti mpole ila muongeaji sana, aliyelelewa katika mazingira ya dini, nyumba yao ilijihusisha zaidi na maswala ya dini kiasi kwamba hakutaka kujihusisha na maswala ya mapenzi kwa umri mdogo kwani akiangalia dada zake wote walikuwa kwenye ndoa zako, kwahiyo ndoto yake yeye ilikuwa ni kumaliza shule, kuanza kazi kisha kupata mchumba na kuolewa. Ni mtoto wa mwisho kwenye familia ya watoto wanne, wakike watatu na wakiume mmoja tu.
Alikuwa na dada yake mmoja ambaye alipatana nae sana na kipindi hicho dadake huyo ndoa yake ilikuwa bado changa kwani ndio kwanza alitoka kuolewa, alikuwa akipenda kupiga nae stori na mara zote dadake alikuwa akimshauri kuwa makini sana na vijana,
“Erica mdogo wangu, nakupenda sana. Naomba uwe makini sana na vijana, ni wadanganyifu. Unatuona dada zako, tumejiheshimu hadi tumeolewa, ni fahari kwetu na heshima kwa familia. Alitangulia dada yetu Maria, nimefata mimi. Najua na wewe utaenda katika mtiririko unaofaa. Usikubali kushawishiwa kijinga na wanaume”
“Dada Bite najua unanijua vizuri mdogo wako, hayo mambo sina. Ndio kwanza nipo kidato cha pili”
“Ndio upo kidato cha pili, yani hiko kidato ndio asilimia kubwa huharibikia hapo kuwa makini sana”
“Usijali kuhusu mimi dada”
Walikuwa wakiongea vizuri sana kirafiki kama marafiki wa kawaida vile lakini ilikuwa ni mtu na dada yake. Beatrice alimrudisha mdogo wake nyumbani kwao baada ya kutoka kumsalimia kwani mama yao alikuwa anampenda sana binti yake huyo na alikuwa anamuona bado ni mdogo kutembea mwenyewe.
Mwandishi: ATUGANILE MWAKALILE
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
SEHEMU YA 1
Alikuwa binti mpole ila muongeaji sana, aliyelelewa katika mazingira ya dini, nyumba yao ilijihusisha zaidi na maswala ya dini kiasi kwamba hakutaka kujihusisha na maswala ya mapenzi kwa umri mdogo kwani akiangalia dada zake wote walikuwa kwenye ndoa zako, kwahiyo ndoto yake yeye ilikuwa ni kumaliza shule, kuanza kazi kisha kupata mchumba na kuolewa. Ni mtoto wa mwisho kwenye familia ya watoto wanne, wakike watatu na wakiume mmoja tu.
Alikuwa na dada yake mmoja ambaye alipatana nae sana na kipindi hicho dadake huyo ndoa yake ilikuwa bado changa kwani ndio kwanza alitoka kuolewa, alikuwa akipenda kupiga nae stori na mara zote dadake alikuwa akimshauri kuwa makini sana na vijana,
“Erica mdogo wangu, nakupenda sana. Naomba uwe makini sana na vijana, ni wadanganyifu. Unatuona dada zako, tumejiheshimu hadi tumeolewa, ni fahari kwetu na heshima kwa familia. Alitangulia dada yetu Maria, nimefata mimi. Najua na wewe utaenda katika mtiririko unaofaa. Usikubali kushawishiwa kijinga na wanaume”
“Dada Bite najua unanijua vizuri mdogo wako, hayo mambo sina. Ndio kwanza nipo kidato cha pili”
“Ndio upo kidato cha pili, yani hiko kidato ndio asilimia kubwa huharibikia hapo kuwa makini sana”
“Usijali kuhusu mimi dada”
Walikuwa wakiongea vizuri sana kirafiki kama marafiki wa kawaida vile lakini ilikuwa ni mtu na dada yake. Beatrice alimrudisha mdogo wake nyumbani kwao baada ya kutoka kumsalimia kwani mama yao alikuwa anampenda sana binti yake huyo na alikuwa anamuona bado ni mdogo kutembea mwenyewe.