Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 21
Mama Erica alirudi nyumbani akiwa na hasira sana kwanza kwa kile alichoambiwa mwanae kakifanya na pia kuhusu swala la mwanae kumkimbia shuleni. Aliingia ndani na kumkuta Erica sebleni akijiliza, kwakweli mama Erica alimshika Erica na kuanza kumpiga sana,
“Umenitia aibu sana wewe mtoto, nitaiweka wapi sura yangu hii. Yani siku zote najivunia wanangu wametulia ni wasomi halafu wewe unataka kuharibu sifa ya familia kweli? Sijapenda ulichokifanya Erica, na umesimamishwa masomo mjinga wewe, sijui utafanyaje na kuna mtihani wa kidato cha pili”
Erica alilia sana hadi alikosa raha kabisa kwa kulia, akaenda kujifungia chumbani kwake akilia, yani siku hiyo hakutoka tena nje ukizingatia alionekana ni msichana mstaarabu halafu gafla kaonekana ni msichana asiye na maadili kabisa, alijikuta akiyachukia mapenzi na kukosa raha kabisa.
Mama Erica, alipiga simu kwa Bite ili washauriane kuhusu Erica, naye Bite aliamua kwenda ili akajue imekuwaje.
Baada ya mazungumzo na mama yao aliamua kwenda kuzungumza na mdogo wake,
“Pole mdogo wangu Erica”
“Nisameheni dada ila sijafanya chochote kibaya”
“Naelewa ila niambie ukweli jinsi ilivyokuwa ili nijue jinsi ya kukusaidia”
Erica aliamua kumueleza kitendo cha yeye kwenda nyuma ya ofisi ili kusikiliza alichokuwa anaambiwa mzazi wa Erick na jinsi Erick alivyokuja nyuma yake na kumbusu kisha mwalimu kuwakuta,
“Dada sijafanya chochote kibaya, hata mimi nilikuwa nikimshangaa tu kunibusu ila nimeshangaa walimu kuchukua maamuzi mazito sana kwangu”
“Sawa mdogo wangu nimekuelewa basi usiwe na mawazo sana”
“Mawazo lazima dada, nipo kidato cha pili natakiwa kufanya mtihani”
“Si bado namba za mitihani hamjaandikisha?”
“Ndio ila nitafanyaje?”
“Usijali nitakufanyia mpango haraka iwezekanavyo na tutaenda kuishi wote kule kwangu hadi umalize kidato cha nne na kumaliza masomo yoko yote vizuri ila niahidi tu kuwa hutoniangusha. Yani maswala ya mapenzi hayatakuwepo kwenye akili yako”
“Dada nataka kusoma, sitaki habari za mapenzi kabisa nataka kusoma”
“Basi usijali, ngoja niongee na mama. Tutaondoka leoleo maana mama inaonyesha amechukizwa sana asije akafanya kitu kibaya bure, ngoja twende ili mama nae apunguze mawazo”
“Sawa dada nimekuelewa”
Basi Bite aliamua kwenda kuongea na mama yao ili kuangalia namna ya kumsaidia mdogo wake huyu.
Mama Erica alirudi nyumbani akiwa na hasira sana kwanza kwa kile alichoambiwa mwanae kakifanya na pia kuhusu swala la mwanae kumkimbia shuleni. Aliingia ndani na kumkuta Erica sebleni akijiliza, kwakweli mama Erica alimshika Erica na kuanza kumpiga sana,
“Umenitia aibu sana wewe mtoto, nitaiweka wapi sura yangu hii. Yani siku zote najivunia wanangu wametulia ni wasomi halafu wewe unataka kuharibu sifa ya familia kweli? Sijapenda ulichokifanya Erica, na umesimamishwa masomo mjinga wewe, sijui utafanyaje na kuna mtihani wa kidato cha pili”
Erica alilia sana hadi alikosa raha kabisa kwa kulia, akaenda kujifungia chumbani kwake akilia, yani siku hiyo hakutoka tena nje ukizingatia alionekana ni msichana mstaarabu halafu gafla kaonekana ni msichana asiye na maadili kabisa, alijikuta akiyachukia mapenzi na kukosa raha kabisa.
Mama Erica, alipiga simu kwa Bite ili washauriane kuhusu Erica, naye Bite aliamua kwenda ili akajue imekuwaje.
Baada ya mazungumzo na mama yao aliamua kwenda kuzungumza na mdogo wake,
“Pole mdogo wangu Erica”
“Nisameheni dada ila sijafanya chochote kibaya”
“Naelewa ila niambie ukweli jinsi ilivyokuwa ili nijue jinsi ya kukusaidia”
Erica aliamua kumueleza kitendo cha yeye kwenda nyuma ya ofisi ili kusikiliza alichokuwa anaambiwa mzazi wa Erick na jinsi Erick alivyokuja nyuma yake na kumbusu kisha mwalimu kuwakuta,
“Dada sijafanya chochote kibaya, hata mimi nilikuwa nikimshangaa tu kunibusu ila nimeshangaa walimu kuchukua maamuzi mazito sana kwangu”
“Sawa mdogo wangu nimekuelewa basi usiwe na mawazo sana”
“Mawazo lazima dada, nipo kidato cha pili natakiwa kufanya mtihani”
“Si bado namba za mitihani hamjaandikisha?”
“Ndio ila nitafanyaje?”
“Usijali nitakufanyia mpango haraka iwezekanavyo na tutaenda kuishi wote kule kwangu hadi umalize kidato cha nne na kumaliza masomo yoko yote vizuri ila niahidi tu kuwa hutoniangusha. Yani maswala ya mapenzi hayatakuwepo kwenye akili yako”
“Dada nataka kusoma, sitaki habari za mapenzi kabisa nataka kusoma”
“Basi usijali, ngoja niongee na mama. Tutaondoka leoleo maana mama inaonyesha amechukizwa sana asije akafanya kitu kibaya bure, ngoja twende ili mama nae apunguze mawazo”
“Sawa dada nimekuelewa”
Basi Bite aliamua kwenda kuongea na mama yao ili kuangalia namna ya kumsaidia mdogo wake huyu.