Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #341
SEHEMU YA 261
Wakaingia ndani, Erica akaona kuna wababa watano, kisha kuna mmoja alikuwa amekaa kwenye kiti cha mbele ambapo Yule meneja alimwambia Erica kwa taratibu,
“Yule wa mbele ndio mkurugenzi mkuu”
Erica alipomuangalia vizuri, akagundua ndio Yule mzee Jimmy.
Alijikuta akiishiwa nguvu kabisa ila bado alisimama ili kujua hatma yake, alimsikia Yule meneja akimtambulisha Erica kwa wale wakurugenzi,
“Huyu anaitwa Erica, ndio mama wa Yule mtoto”
Kisha meneja akatambulisha majina ya wale wakurugenzi kwa Erica, ila alishangaa kuona mzee Jimmy hata hakushtuka wala hakujifanya kumfahamu zaidi zaidi walimuuliza baadhi ya maswali kisha Mzee Jimmy akasema,
“Binti, Jumamosi saa nne asubuhi umlete huyo mtoto wako tuje tumuangalie vizuri na tukusainishe mikataba yetu”
Erica alikubali, kisha wakamruhusu kuondoka. Kwakweli alivyotoka nje ya ile benki ndio aliweza kupumua sasa, huku akiliangalia lile jingo refu la ile benki. Alikuwa amekubali tu ila hakujua kwakweli kama itakuwa rahisi maana Yule mzee alishaonyesha kumtaka.
Erica alirudi ofisini akiwa hana raha kabisa, James alimuita na kumuuliza kuwa imekuwaje alipotoka maana alimdanganya kuwa anaenda hospitali,
“Mbona unaonekana huna furaha?”
“Hamna mbona nipo kawaida tu”
“Erica, nakufahamu wewe pengine kupita hata unavyojifahamu au umeanza tena kumuwaza Yule mwanaume wako?”
“Hapana”
Kisha Erica akaenda kuendelea na kazi zake ila muda huo ndio alianza kumfikiria Erick sasa, alitamani kujua Erick anaendeleaje, aliinuka na kutoka nje kisha kupiga ile namba aliyopewa usiku, ila alipopiga aliambiwa kuwa Erick aliruhusiwa kurudi nyumbani na aliendelea vizuri, muda huo Erica aliamua kupiga namba ya Erick, na kweli iliita na kumfanya afurahi sana kisha Erick akapokea simu,
“Unaendeleaje Erick?”
“Salama kabisa, unanijali hadi kunijulia hali!”
“Ndio nakujali Erick”
“Hivi kweli unanipenda Erica?”
“Ndio nakupenda sana Erick”
Muda huo kumbe James alikuwa nyuma ya Erica kwahiyo lile neno la mwisho alilosema Erica alilisikia vizuri sana, akamfokea Erica hadi akaangusha simu
“Yani unaacha kufanya kazi unaanza kuongea maswala ya mapenzi ofisini? Haya Erica, nifate ofisini kwangu”
Erica aliinama kuokota simu yake kisha akamfata nyuma James kuelekea ofisini kwake ila kwa mara ya kwanza aliweza kuona sura ya James ikichukia sana na kuonyesha hasira za waziwazi, Erica alipofika James alianza kuongea,
“Erica, kipi kimekufanya uwepo hapa ofisini?”
“Ni kazi bosi”
“Sasa kazi ya kuongea na simu na kumwambia mtu unampenda ndio iliyokuleta hapa ofisini?”
“Nisamehe bosi”
“Aaah umenikera sana, mimi napenda kazi, muda wa kazi fanya kazi, na muda wa madudu yako huko fanya madudu sikuzuii ila sio ofisini kwangu. Erica katika wafanyakazi wangu umekuwa namba moja kuomba udhuru mara leo sijui imekuwaje, mara nampeleka mtoto kliniki, mara naenda kumfungulia mtoto akaunti, mara tumbo linaniuma siji, mara naenda hospitali yani umefanya kama ofisi hii ni ofisi ya baba yako sasa yani unafanya unavyotaka wewe na sio anavyotaka mwenye ofisi. Ushemeji wa mimi na wewe unaishia nyumbani lakini sio ofisini, ndiomana watu huwa hawaajili ndugu zao sababu ya mambo kama haya yani kazi haziendi na ndugu akitoa taarifa lazima umsikilize hata kama hiyo taarifa ni uongo. Nimekuvumilia sana Erica, na sasa naomba nikwambie kuwa nimekusimamisha kazi”
“Jamani shemeji nihurumie”
“Nishakwambia, ushemeji ni nyumbani, ila nikiwa ofisini sina ushemeji na wewe. Yani uharibu kazi zangu kwa dhana ya ushemeji? Kuna umuhimu gani wa kumuajiri mtu asiyejielewa kama wewe? Yani huna akili hata kidogo, unabebwa ila hubebeki, unataka ufanyiwe nini ubebeke? Erica, nishafanya upande wangu hata Mungu mwenyewe anaona ila kwasasa nimechoka, na ninamaanisha kuwa nimekusimamisha kazi”
Erica akapiga magoti kwa shemeji yake huku akilia na kuzidi kuomba msamaha,
“Naomba unisamehe bosi, haitajirudia tena”
“Mwambie huyo uliyekuwa unamwambia kuwa unampenda sana akutafutie kazi ila kwangu umesimamishwa kwasasa, mpaka pale nitakapoamua mimi kukurudisha tena kazini”
Erica alikazana kuomba msamaha ila shemeji yake alishaamua kwani alichukizwa sana na ile simu ya Erica ya kusema ‘nakupenda sana Erick’ yani muda wote alijikuta hilo neno likiimba kwenye kichwa chake kama mziki, kwahiyo hakuweza tena kuendelea kumuona Erica hapo ofisini, kwahiyo Erica ilibidi ainuke na kwenda kuweka sawa kazi zake kisha kudhikabidhi na kuondoka.
Alikuwa na mawazo sana, alihisi kama kichwa chake kitavurugika tena maana hakujua kuwa amekosa kazi atafanya nini tena, maana lile swala la kwenda kazini tu lilikuwa likifariji moyo wake.
Akiwa kwenye daladala alichukua simu yake na kuiangalia, aliiona kioo hakitamaniki kabisa maana aliiangusha sana na kumfanya akose raha zaidi ila akaiwasha na ikawaka, akaona ni vyema imewaka ingawa imevunjika kioo ila swala la kuwaka lilikuwa ni bora kwake maana hakutaka kutumia hela yoyote ya mtoto wake kwaajili ya kununua simu ukizingatia kazi tena ndio ilikuwa basi, sasa akianza kujiendekeza kutumia hela za mtoto itakuwaje? Alishukuru tu vile simu inawaka.
Wakaingia ndani, Erica akaona kuna wababa watano, kisha kuna mmoja alikuwa amekaa kwenye kiti cha mbele ambapo Yule meneja alimwambia Erica kwa taratibu,
“Yule wa mbele ndio mkurugenzi mkuu”
Erica alipomuangalia vizuri, akagundua ndio Yule mzee Jimmy.
Alijikuta akiishiwa nguvu kabisa ila bado alisimama ili kujua hatma yake, alimsikia Yule meneja akimtambulisha Erica kwa wale wakurugenzi,
“Huyu anaitwa Erica, ndio mama wa Yule mtoto”
Kisha meneja akatambulisha majina ya wale wakurugenzi kwa Erica, ila alishangaa kuona mzee Jimmy hata hakushtuka wala hakujifanya kumfahamu zaidi zaidi walimuuliza baadhi ya maswali kisha Mzee Jimmy akasema,
“Binti, Jumamosi saa nne asubuhi umlete huyo mtoto wako tuje tumuangalie vizuri na tukusainishe mikataba yetu”
Erica alikubali, kisha wakamruhusu kuondoka. Kwakweli alivyotoka nje ya ile benki ndio aliweza kupumua sasa, huku akiliangalia lile jingo refu la ile benki. Alikuwa amekubali tu ila hakujua kwakweli kama itakuwa rahisi maana Yule mzee alishaonyesha kumtaka.
Erica alirudi ofisini akiwa hana raha kabisa, James alimuita na kumuuliza kuwa imekuwaje alipotoka maana alimdanganya kuwa anaenda hospitali,
“Mbona unaonekana huna furaha?”
“Hamna mbona nipo kawaida tu”
“Erica, nakufahamu wewe pengine kupita hata unavyojifahamu au umeanza tena kumuwaza Yule mwanaume wako?”
“Hapana”
Kisha Erica akaenda kuendelea na kazi zake ila muda huo ndio alianza kumfikiria Erick sasa, alitamani kujua Erick anaendeleaje, aliinuka na kutoka nje kisha kupiga ile namba aliyopewa usiku, ila alipopiga aliambiwa kuwa Erick aliruhusiwa kurudi nyumbani na aliendelea vizuri, muda huo Erica aliamua kupiga namba ya Erick, na kweli iliita na kumfanya afurahi sana kisha Erick akapokea simu,
“Unaendeleaje Erick?”
“Salama kabisa, unanijali hadi kunijulia hali!”
“Ndio nakujali Erick”
“Hivi kweli unanipenda Erica?”
“Ndio nakupenda sana Erick”
Muda huo kumbe James alikuwa nyuma ya Erica kwahiyo lile neno la mwisho alilosema Erica alilisikia vizuri sana, akamfokea Erica hadi akaangusha simu
“Yani unaacha kufanya kazi unaanza kuongea maswala ya mapenzi ofisini? Haya Erica, nifate ofisini kwangu”
Erica aliinama kuokota simu yake kisha akamfata nyuma James kuelekea ofisini kwake ila kwa mara ya kwanza aliweza kuona sura ya James ikichukia sana na kuonyesha hasira za waziwazi, Erica alipofika James alianza kuongea,
“Erica, kipi kimekufanya uwepo hapa ofisini?”
“Ni kazi bosi”
“Sasa kazi ya kuongea na simu na kumwambia mtu unampenda ndio iliyokuleta hapa ofisini?”
“Nisamehe bosi”
“Aaah umenikera sana, mimi napenda kazi, muda wa kazi fanya kazi, na muda wa madudu yako huko fanya madudu sikuzuii ila sio ofisini kwangu. Erica katika wafanyakazi wangu umekuwa namba moja kuomba udhuru mara leo sijui imekuwaje, mara nampeleka mtoto kliniki, mara naenda kumfungulia mtoto akaunti, mara tumbo linaniuma siji, mara naenda hospitali yani umefanya kama ofisi hii ni ofisi ya baba yako sasa yani unafanya unavyotaka wewe na sio anavyotaka mwenye ofisi. Ushemeji wa mimi na wewe unaishia nyumbani lakini sio ofisini, ndiomana watu huwa hawaajili ndugu zao sababu ya mambo kama haya yani kazi haziendi na ndugu akitoa taarifa lazima umsikilize hata kama hiyo taarifa ni uongo. Nimekuvumilia sana Erica, na sasa naomba nikwambie kuwa nimekusimamisha kazi”
“Jamani shemeji nihurumie”
“Nishakwambia, ushemeji ni nyumbani, ila nikiwa ofisini sina ushemeji na wewe. Yani uharibu kazi zangu kwa dhana ya ushemeji? Kuna umuhimu gani wa kumuajiri mtu asiyejielewa kama wewe? Yani huna akili hata kidogo, unabebwa ila hubebeki, unataka ufanyiwe nini ubebeke? Erica, nishafanya upande wangu hata Mungu mwenyewe anaona ila kwasasa nimechoka, na ninamaanisha kuwa nimekusimamisha kazi”
Erica akapiga magoti kwa shemeji yake huku akilia na kuzidi kuomba msamaha,
“Naomba unisamehe bosi, haitajirudia tena”
“Mwambie huyo uliyekuwa unamwambia kuwa unampenda sana akutafutie kazi ila kwangu umesimamishwa kwasasa, mpaka pale nitakapoamua mimi kukurudisha tena kazini”
Erica alikazana kuomba msamaha ila shemeji yake alishaamua kwani alichukizwa sana na ile simu ya Erica ya kusema ‘nakupenda sana Erick’ yani muda wote alijikuta hilo neno likiimba kwenye kichwa chake kama mziki, kwahiyo hakuweza tena kuendelea kumuona Erica hapo ofisini, kwahiyo Erica ilibidi ainuke na kwenda kuweka sawa kazi zake kisha kudhikabidhi na kuondoka.
Alikuwa na mawazo sana, alihisi kama kichwa chake kitavurugika tena maana hakujua kuwa amekosa kazi atafanya nini tena, maana lile swala la kwenda kazini tu lilikuwa likifariji moyo wake.
Akiwa kwenye daladala alichukua simu yake na kuiangalia, aliiona kioo hakitamaniki kabisa maana aliiangusha sana na kumfanya akose raha zaidi ila akaiwasha na ikawaka, akaona ni vyema imewaka ingawa imevunjika kioo ila swala la kuwaka lilikuwa ni bora kwake maana hakutaka kutumia hela yoyote ya mtoto wake kwaajili ya kununua simu ukizingatia kazi tena ndio ilikuwa basi, sasa akianza kujiendekeza kutumia hela za mtoto itakuwaje? Alishukuru tu vile simu inawaka.