Ms Yahaya
Member
- Apr 14, 2022
- 6
- 12
Simulizi; "NITAWATETEA"
Sehemu Ya Kwanza (01)
Mwandishi; MARIAM YAHAYA
Namba; +255744654969
*****************************
RORYA
Ni katika kijiji cha Nyanchabakenye, ilikua siku ya jumamosi tulivu sana ambayo ilipambwa na jua la alfajiri lisilokuwa na makali. Kwa mbali walisikika ndege wakiburudisha anga baada ya kuiona siku nyingine tena, huku ndege wafugwao yaani kuku nao walisikika wakinon’gona wakisubiri kufunguliwa lango la gereza lao.
Wazee nao walionekana wakipita pita wakiwa wanaelekea kwenye vijiwe vyao vya kahawa ambavyo walipendelea kukaa mida ya asubuhi na jioni ili kupanda hadithi za ukweli na uongo wakisindikizwa na kahawa pamoja na mziki mtulivu wa asili.
Zilikua ni pilika pilika za kuhakikisha ratiba na mipango ya siku hiyo mpya ziende sawia, wanawake wengi walionekana na vifaa vyao vya kuchotea maji wakielekea mtoni lakini viajana nao walibeba majembe kuelekea shambani.
‘’Hivi bado amelala tu …?, mwanamke mzima hana hata haya …’’ ni maneno yaliyomtoka mama mmoja baada ya kutoka nje na kukuta pakiwa pamepooza, uwanja uliozunguka nyumba hiyo ukiwa mchafu huku kuku wakijidonolea mabaki ya magimbi katika vyombo vilivyoegeshwa barazani. Haraka sana alipiga hatua kadhaa kuelekea chumbani wanakolala wanae.
‘’……hivi bhoke kweli na utu zima huo unataka nikukumbushe kuamka mapema na kufanya usafi hapa?... huoni kua umeshakua mtu mzima, eeh? Hivi ni kitu gani kinachokufanya ulale hadi mda huu?".
Mama huyo alisimama mlangoni huku akifunga vizuri kanga yake ambayo Ilionekana imechahakaa lakini haikupoteza maneno yake ambayo bila shaka mnunuzi aliinunua si kwa uzuri wa maua yake bali kwa maneno yale ‘’kisichoridhiki hakiliki’’ ni maandishi yaliyoipamba kanga hiyo.
‘’Lakini mama…’’ ‘’lakini nini?’’ mama huyo hakusubiri mwanae amalizie lalamiko lake, alimkatisha akiendelea kumfokea.
"Unataka kusemaje mwanahizaya wewe… eeeh! Hivi unadhani watu watanichukuliaje…? Kwamba mimi sijui kulea au...?"
"Mama kwanini huna huruma na mimi lakini?, Wiki nzima tangu jumatatu kuanzia jua linachomoza hadi linazama nimekunja mgongo tu, kwanini na mimi nisipumzike hata siku mbili hizi….’’ Neema alilalama kwa mama yake huku akijivutia kushuka kitandani. Lakini haikusaidia kitu, ni kama aliyoyaongea yalipita kama upepo karibu na sikio la mama huyo.
Mama Bhoke huku akisogea na kuketi kitandani hapo alisema na mwanaye kwa sauti ya upole “Mhh... Mwanangu kama unavyojua humu ndani wananwake tupo wawili tu, mimi na wewe…” mama huyu alisita kidogo ili kurusu mate yaliyojaa mdomoni kushuka.
"...haya nambie nani natakusaidia hizo kazi kwa siku hizi unazotaka kupumzika…? Au unataka mimi nikunje mgongo kukusidia kufagia na kuosha vyombo eti…. Mmh halafu nikupikie chai mtoto mzuri, nikutengee maji ya kuoga halafu nije hapa nikuamshe ule... Eeh au nikubebee kabisa chakula nikuletee humu chumbani si ndio mama eeeh?....” aliendelea kusema na mwanae Mama Bhoke, mishipa ya shinggo nayo haikuwa mbali kutoa ushahidi ni kwa kiasi gani mama huyo alivyokasirika.
Ghafla, Bhoke aliruka; ni wakati mama yake alipokua akimfinya, kisha kwa haraka, Mama Bhoke alishika maskio na kuyavuta kwa nguvu mithili ya nywele zivutwavyo wakati wa kusukwa.
"Mamaaaaaa…” ni ukunga uliomtoka Bhoke baada ya kuona hali si shwari kwani mama yake alikua amekasirishwa na alichokisema.
“Nyamaza mjinga, mbwa wewe….” Huku akiwa amekunja sura, nidhahiri kua mama huyu alichukia haswa siku hiyo. Lakini baada mda alitulia tena huku uso wake ukionesha manunguniko, alimkazia macho mwanae aliyekua amesimama mbele yake.
‘’Mwanangu kafanye hizo kazi kwanza kabla baba yako hajarudi, kisha tuongee… sawa mamaa?’’ mara hii mama bhoke aliongea kwa sauti ya upole iliyojaa simanzi na yenye kubembeleza huku akimwangalia mwanae kwa macho ya huruma. Ni kama alikua akiona namna mwanae anavyoteseka nyumbani kwao bila ya msaada wowote kutoka kwa wadogo zake.
Baada ya mzozano huo uliochukua dakika kadhaa, bhoke alivuta miguu yake kuelekea nje, huku akiwa amekaza shingo dhahiri kua maisha yale yalimchosha haswa.
Ni maisha ya kuamka asubuhi na kuanza kufanya kazi zote za nyumbani, kumuhudumia yeyote yule atakayekuwepo ndani kwa vyote walivyohitaji bila kusahahu kutumwa huku na kule siku nzima.
Sio kwamba Bhoke alikuwa mtoto wa pekeee, hapana. Walikuwepo wengine lakini kwakua ni watoto wakiume basi kazi yao ilikua ni moja tu, nayo si nyingine zaidi ya kuchanja kuni. Ndo kitu pekee walichofanya.
Bhoke ni mtoto wa tano kati ya watoto kumi na mbili wa mzee Wambura, kati ya watoto hao watoto nane ndio wa tumbo moja na bhoke, lakini wengine wanne walikua wa baba yake na wanawake wengine wa nje, na kila mtoto alikua na mama yake kama mjuavyo, eti mwanaume aridhike na chungu kimoja hahahah…! haiwezekani.
Familia yao waliishi kiafrika zaidi kwani ilijaa watu kweli kweli, alikuwepo babu yake mzaa baba, binamu, baba zake wadogo wawili, bila kusahau hao ndugu zake wengine amabao nao wote walikua jinsia ya kiume.
Katika familia hiyo wenye jinsia ya kike walikua wawili tu yaani mama bhoke na bhoke mwenyewe, na familia yao ni moja ya familia ambazo mtoto wa kike hubebeshwa majukumu makubwa sana ikiwa na pamoja na kufanya shughuli zote za ndani na hata nje kama shambani na kuchota maji.
Kwa watoto wakiume maisha yalikua rahisi sana, kwao ni kuchanja kuni na kula tu, mara chache wangeonekana shambani.
Na kwa bahati mbaya kati ya watoto saba wa mzee Wambura, hakuna mtoto hata mmoja aliyepata kuendelea na masomo baada ya kumaliza darasa la saba, isipokua Bhoke peke yake, bahati iliyoje.
Sasa watoto wakiume wangesoma ili wapate nini?, maana ufahari wao ilikua mashamba na mifugo kama ng'ombe na kondoo, na babu yao pamoja na baba yao walikua navyo vya kutosha, walijihakikishia umiliki wa vitu hivyo tu baada ya wazee hao kuwatoka.
.
Sehemu Ya Kwanza (01)
Mwandishi; MARIAM YAHAYA
Namba; +255744654969
*****************************
RORYA
Ni katika kijiji cha Nyanchabakenye, ilikua siku ya jumamosi tulivu sana ambayo ilipambwa na jua la alfajiri lisilokuwa na makali. Kwa mbali walisikika ndege wakiburudisha anga baada ya kuiona siku nyingine tena, huku ndege wafugwao yaani kuku nao walisikika wakinon’gona wakisubiri kufunguliwa lango la gereza lao.
Wazee nao walionekana wakipita pita wakiwa wanaelekea kwenye vijiwe vyao vya kahawa ambavyo walipendelea kukaa mida ya asubuhi na jioni ili kupanda hadithi za ukweli na uongo wakisindikizwa na kahawa pamoja na mziki mtulivu wa asili.
Zilikua ni pilika pilika za kuhakikisha ratiba na mipango ya siku hiyo mpya ziende sawia, wanawake wengi walionekana na vifaa vyao vya kuchotea maji wakielekea mtoni lakini viajana nao walibeba majembe kuelekea shambani.
‘’Hivi bado amelala tu …?, mwanamke mzima hana hata haya …’’ ni maneno yaliyomtoka mama mmoja baada ya kutoka nje na kukuta pakiwa pamepooza, uwanja uliozunguka nyumba hiyo ukiwa mchafu huku kuku wakijidonolea mabaki ya magimbi katika vyombo vilivyoegeshwa barazani. Haraka sana alipiga hatua kadhaa kuelekea chumbani wanakolala wanae.
‘’……hivi bhoke kweli na utu zima huo unataka nikukumbushe kuamka mapema na kufanya usafi hapa?... huoni kua umeshakua mtu mzima, eeh? Hivi ni kitu gani kinachokufanya ulale hadi mda huu?".
Mama huyo alisimama mlangoni huku akifunga vizuri kanga yake ambayo Ilionekana imechahakaa lakini haikupoteza maneno yake ambayo bila shaka mnunuzi aliinunua si kwa uzuri wa maua yake bali kwa maneno yale ‘’kisichoridhiki hakiliki’’ ni maandishi yaliyoipamba kanga hiyo.
‘’Lakini mama…’’ ‘’lakini nini?’’ mama huyo hakusubiri mwanae amalizie lalamiko lake, alimkatisha akiendelea kumfokea.
"Unataka kusemaje mwanahizaya wewe… eeeh! Hivi unadhani watu watanichukuliaje…? Kwamba mimi sijui kulea au...?"
"Mama kwanini huna huruma na mimi lakini?, Wiki nzima tangu jumatatu kuanzia jua linachomoza hadi linazama nimekunja mgongo tu, kwanini na mimi nisipumzike hata siku mbili hizi….’’ Neema alilalama kwa mama yake huku akijivutia kushuka kitandani. Lakini haikusaidia kitu, ni kama aliyoyaongea yalipita kama upepo karibu na sikio la mama huyo.
Mama Bhoke huku akisogea na kuketi kitandani hapo alisema na mwanaye kwa sauti ya upole “Mhh... Mwanangu kama unavyojua humu ndani wananwake tupo wawili tu, mimi na wewe…” mama huyu alisita kidogo ili kurusu mate yaliyojaa mdomoni kushuka.
"...haya nambie nani natakusaidia hizo kazi kwa siku hizi unazotaka kupumzika…? Au unataka mimi nikunje mgongo kukusidia kufagia na kuosha vyombo eti…. Mmh halafu nikupikie chai mtoto mzuri, nikutengee maji ya kuoga halafu nije hapa nikuamshe ule... Eeh au nikubebee kabisa chakula nikuletee humu chumbani si ndio mama eeeh?....” aliendelea kusema na mwanae Mama Bhoke, mishipa ya shinggo nayo haikuwa mbali kutoa ushahidi ni kwa kiasi gani mama huyo alivyokasirika.
Ghafla, Bhoke aliruka; ni wakati mama yake alipokua akimfinya, kisha kwa haraka, Mama Bhoke alishika maskio na kuyavuta kwa nguvu mithili ya nywele zivutwavyo wakati wa kusukwa.
"Mamaaaaaa…” ni ukunga uliomtoka Bhoke baada ya kuona hali si shwari kwani mama yake alikua amekasirishwa na alichokisema.
“Nyamaza mjinga, mbwa wewe….” Huku akiwa amekunja sura, nidhahiri kua mama huyu alichukia haswa siku hiyo. Lakini baada mda alitulia tena huku uso wake ukionesha manunguniko, alimkazia macho mwanae aliyekua amesimama mbele yake.
‘’Mwanangu kafanye hizo kazi kwanza kabla baba yako hajarudi, kisha tuongee… sawa mamaa?’’ mara hii mama bhoke aliongea kwa sauti ya upole iliyojaa simanzi na yenye kubembeleza huku akimwangalia mwanae kwa macho ya huruma. Ni kama alikua akiona namna mwanae anavyoteseka nyumbani kwao bila ya msaada wowote kutoka kwa wadogo zake.
Baada ya mzozano huo uliochukua dakika kadhaa, bhoke alivuta miguu yake kuelekea nje, huku akiwa amekaza shingo dhahiri kua maisha yale yalimchosha haswa.
Ni maisha ya kuamka asubuhi na kuanza kufanya kazi zote za nyumbani, kumuhudumia yeyote yule atakayekuwepo ndani kwa vyote walivyohitaji bila kusahahu kutumwa huku na kule siku nzima.
Sio kwamba Bhoke alikuwa mtoto wa pekeee, hapana. Walikuwepo wengine lakini kwakua ni watoto wakiume basi kazi yao ilikua ni moja tu, nayo si nyingine zaidi ya kuchanja kuni. Ndo kitu pekee walichofanya.
Bhoke ni mtoto wa tano kati ya watoto kumi na mbili wa mzee Wambura, kati ya watoto hao watoto nane ndio wa tumbo moja na bhoke, lakini wengine wanne walikua wa baba yake na wanawake wengine wa nje, na kila mtoto alikua na mama yake kama mjuavyo, eti mwanaume aridhike na chungu kimoja hahahah…! haiwezekani.
Familia yao waliishi kiafrika zaidi kwani ilijaa watu kweli kweli, alikuwepo babu yake mzaa baba, binamu, baba zake wadogo wawili, bila kusahau hao ndugu zake wengine amabao nao wote walikua jinsia ya kiume.
Katika familia hiyo wenye jinsia ya kike walikua wawili tu yaani mama bhoke na bhoke mwenyewe, na familia yao ni moja ya familia ambazo mtoto wa kike hubebeshwa majukumu makubwa sana ikiwa na pamoja na kufanya shughuli zote za ndani na hata nje kama shambani na kuchota maji.
Kwa watoto wakiume maisha yalikua rahisi sana, kwao ni kuchanja kuni na kula tu, mara chache wangeonekana shambani.
Na kwa bahati mbaya kati ya watoto saba wa mzee Wambura, hakuna mtoto hata mmoja aliyepata kuendelea na masomo baada ya kumaliza darasa la saba, isipokua Bhoke peke yake, bahati iliyoje.
Sasa watoto wakiume wangesoma ili wapate nini?, maana ufahari wao ilikua mashamba na mifugo kama ng'ombe na kondoo, na babu yao pamoja na baba yao walikua navyo vya kutosha, walijihakikishia umiliki wa vitu hivyo tu baada ya wazee hao kuwatoka.
.