mbuzi wa mshenga
Senior Member
- Oct 28, 2016
- 160
- 173
Mkuu usingiz hauji
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tuvute subira huenda katekwa na askari wa UMD.Watito wa mjini wanasema bro kala bunda toka juzi😀😀
Mkuu kwema hukooo.😅😅 Team songoro wapo wapi maana zamu yao sasa
UMD cyo watu wazuri wale,Tuvute subira huenda katekwa na askari wa UMD.
Kwamba "Kamanda" ni mzembe kiasi Cha kutekwa na kundi la Sangolo!!!Kikosi cha songoro kimeondoka na Abou Shaymaa 🤣🤣🤣🤣
Wahi ukamfariji maana dr kashachojolewa kule hadi baba simu azipokelewi 😀😀😀Kwamba "Kamanda" ni mzembe kiasi Cha kutekwa na kundi la Sangolo!!!
Basi UMD ninaenda kumteka Carolina🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃😂🤣😂😂😂😂🤣😂
Mkuu, tutegemee lini Tena kuupata mwendelezo wa matukio ya "UMD"NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA MIA MOJA NA ISHILINI NA NANE
MTUNZI: Mbogo EDGAR
WHATSAPP: 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA MIA MOJA NA ISHILINI NA SABA:- Hapo King Elvis, mteja wa zamani wa bagia za kunde, aliinua uso wake huku akitabasamu, ni wazi alikuwa amepata wazo zuri sana, “ujue mke wangu katika vitu ambavyo nimefanikiwa katika Maisha yangu, ni nokuwa na mke kama wewe, yani unawaza kwa haraka sana, utadhania umepitia mafunzo ya kijeshi kwa ngazi za juu” alisema Elvis, akimalizia kwa kuweka mdomo wake kwenye paji la uso la mke wake, nakupiga busu zito kisha akachukua simu yake ambayo ile kuchukua tu nayo inaanza kuita, na mpigaji alikuwa ni Waziri wa mambo ya ndani, yani Mheshimiwa Dickson Chitopelah, hakika ilimshtua sana Elvis, ambae alimtazama mke wake, ambae pia alishaona jina la Chitopela, nao wakatazamana, “vipi mume wangu, mbona kama umeshtuka sana” aliuliza Malikia Vaselisa huku anamtazama mume wake, “unadhani hii simu itakuwa na Habari gani, mbona kama inanipa wasi wasi” alisema Elvis kabla hajaipokea na kuweka sauti ya wazi…..ENDELEA….
Na hapo ikasikika sauti iliyojaa nidhamu na heshima toka upende wa pili wa simu “salaaam ewe mfalme wa Mbogo Land” huyo alikuwa ni Waziri Chitopelah, “salaam Waziri chitopelah” aliitikia mfalme Elvis, huku anatazamana na mke wake, “asante mtukufu mfalme kwa kupokea simu yangu kwaajili ya usalama wa taifa letu” ilisikika sauti iliyojaa utiifu ya bwana Chitopelah, “ni Habari gani ambazo umekusudia kunipatia bwana Chitopelah?” aliuliza Elvis, alie onekana kuwa katika hali ya mstuko, “mtukufu kuna habari mbili, moja ikiwa mbaya kwa usalama wetu na nyingine ikiwa njema kwa usalama wetu, naomba nianze na hii mbaya” alisikika Chitopelah, na hapo mfalme na mke wake Vaselisa wakatega masikio kwa umakini.
Chitopelah akaanza kueleza, “mtukufu, imebainika kuwa, kuna uwepo wa mamluki ndani ya serikali yako tukufu, ambao wanatusaliti na kusaidia upangaji wa mapinduzi wakisaidiana na UMD” alisikika Chitopelah, na kumfanya Elvis na mke wake watazamane kwa macho ya mshangao, huku kila mmoja akiwaza sawa na mwenzie, “yanajirudia mambo ya mwaka 92” wakati wanawaza hayo, Chitopelah, alikuwa kimya akisikilizia matokeo ya taarifa ile, “unasema, yani Pamoja na usalama wote tulionao lakini bado UMD wamejipenyeza ndani ya Serikali?” aliuliza king Elvis akionyesha mstuko wa hali ya juu.
Naam pengine hapo ndipo Chtopela alipokuwa anapahitaji, “mtukufu, ukweli ni kwamba ni rahisi sana kwa mamluki kuingia serikalini yaani kwenye vyombo vya ulinzi na usalama, kwasababu wahusika ni viongozi wakubwa na watu muhimu walio aminiwa na serikali yako tukufu” maneno ya Chitopelah yalionyesha wazi kumvuruga Elvis, ambae alimtazama tena mke wake lakini akashangaa kumuona mwanamke huyu mrembo, akiwa anatabasamu na kutikisa kichwa kwa masikitiko, ilimshangaza Elvis, “kuna mmoja aliefahamika Chitopelah?” aliuliza Elvis, ambae mpaka sasa, alionyesha mshtuko wa wazi kabisa, “mtukufu hilo ndilo lililonifanya nikupigie simu, ikiwa ni habari njema kwamba, nahitaji kibali cha kuunda kikundi kidogo, ambacho kitachunguza na kuwakamata wote wanaohusika, kwasababu hatuwezi kutoa taarifa ambazo hazijafanyiwa uchunguzi” alisema Chitopeah kwa sauti yenye kujaa utiifu, “sawa kibali kimetolewa, fanya hivyo haraka iwezekanavyo, nahitaji majibu” alisema king Elvis, kabla ya kukata simu.
Hapo mke wake akacheka kwa nguvu kiasi cha Elvis kushangaa, “unacheka nini Vaselisa, unajua kuwa nchi ipo katika wakati mgumu wa kiusalama?” aliuliza Elvis kwa sauti yenye kuonyesha kutokumuelewa mke wake, “hivi unashindwa kufahamu kuwa kinataka kujirudia kilichotokea mwaka 92?” aliuliza malikia Vaselisa, huku akimtazama mume wake kama vile anataka kuhakikisha anamuelewa anachoongea.
Nikweli kabisa alicho kiongea Vaselisa, kwamba kuna kitu kinataka kujirudia katika utawala wake kama kile kilichowahi kutokea miaka ishirini iliyopita, lakini ni kitu gani kinamchekesha mke wake, “ndiyo inajirudia, lakini kinacho kuchekesha ni kitu gani?” aliuliza Elvis, ambae licha ya kumwamini mke wake, lakini kwa hili ni wazi hakumuelewa mke wake, zaidi alimuona kuwa analeta utani kwenye jambo muhimu, “mume wangu, huwezi kuona kuwa hii njama ya pili kuondoa watu muhimu katika serikali na kuuchafua utawala wako kama ilivyokuwa kwa babu Eugen” alisema Malkia Vaselisa, lakini Elvis hakuonekana kukubaliana nae moja kwa moja.
Maana mfalme huyu alitulia kwa sekunde kadhaa, kabla hajaongea neno, “hata kama ilitokea mwaka 92, lakini haiwezi kuwa sawa na hii, hasa katika kipindi kama hiki ambacho serikali inatilia mashaka msako ule wa mwanzo, ni wazi sasa tunahitaji kuwapata watu waliopo ndani ya serikali wanao shirikiana na waasi” alisisitiza king Elvis, na kumfanya mke wake atikise kichwa kwa masikitiko, “mume wangu, unapaswa kutuliza akili katika kipindi kigumu, wewe ni sawa na mgonjwa ambae hajapata tiba sahihi ya ugonjwa wake, mgonjwa ambae anapokea kila ushauri na kuutumia katika kujitibu pasipo kujua kuwa wasio mpenda nao wanatumia nafasi hiyo hiyo kumuangamiza” alisema Vaselisa kwa sauti tulivu yenye kubembeleza, “una maana gani Vaselisa, unadhani nimechanganyikiwa kiasi hicho?” aliuliza Elvis, ambae ni kama alianza kukasilika.
Ni kama mke wake alishaliona hilo, akaachia tabasamu laini huku anamtazama mume wake, tabasamu ambalo halijawahi kumuacha salama king Elvis toka alipo kutana na Vaselisa kwa mara ya kwanza wakiwa wanamiaka mitano, mpaka leo hajawahi kulizoea na kuliona la kawaida, “mume wangu si unajua huwa sipendi ukasirike?” aliuliza Vaselisa huku anapitisha mkono wake taratibu, juu ya kifua cha mume wake huyu ambae ni mfalme pekee mwenye umri mdogo kwa wakati huo, “najua, lakini nashangaa leo” alisema Elvis, huku sauti yake ikiwa imepoa kabisa, “basi sasa ndio ujue kuwa lengo langu sio kukukasirisha, ila nikukusaidia, kama inavyokuwa siku zote” alisema Vaselisa, ambae ukimuona hapa kitandani unaweza kusema anajiandaa kwenda kwenye mualiko mkubwa na wakipekee, yani alikuwa amependeza vibaya sana, na kitu cha kuvutia zaidi ambacho msomaji utakiwa ukifahamu ni kwambanmalkia Vaselisa, alikuwa amejipaka mafuta nazi pekee, ndiyo mafuta ambayo uyatumia wakati wakulala, lakini ungesema ametumia vipozi zaidi kumi na unga wa mapambo wa rangi saba tofauti, na ile midomo yake milaini ungesema amejipaka king’arisho cha midomo, wao wanaita “lip shine”*********
Naaaam wakati huo kilomita kama arobaini, magharibi mwa TT City, yani Treanch Town City, nje ya kitongozji maarufu cha Komwe la Mwanamtama, kutokana na urefu wa jina la kitongoji hicho chenye jina la mwanamke maarufu Mwanamtama aliepata kuishi miaka mingi iliyopita aliejaaliwa kuwa na kipanda uso kikubwa kuliko mwanamke yoyote aliewahi kutokea #mbogo_land, walifupisha na kuita Komwe.
Usiku huu, kitongoji kilikuwa tulivu sana ni wazi watu walikuwa wamelala, maana usiku ulikuwa mkubwa sana, hapa kuonekana mtu wala magari yaliyokuwa yakizurula usiku ule, achana na Kijiji, twende magharibi zaidi, ambako ukiachilia mapori mkubwa na misitu ya kati, tunakutana na mashamba makubwa makubwa ya ngano na mahindi, ambayo pia katikati au pembeni ya shamba ungeona Nyumba kubwa yenye kupembeziwa na mabanda ya mifugo, “kupembeziwa ni neno ambalo linatumika kuwakirisha kile kilicho shikizwa pembeni ya kitu kingine.
Lakini tofauti na mashamba hayo makubwa, pia pembezoni mwa mto bhumbu (korodani) la Chifu Kwala, ni mto mkubwa kiasi, uliopewa jina hilo la Korodani za Chief Kwala, mwishoni mwa karne ya 18, miaka michache kabla ya uvaamizi wa wadachi katika nchi zinazoizunguka Mbogo land ni baada ya Chiefu huyo wa kiyao, aliekuwa anasafiri toka magharibi mwa Tanzania, kabla hata haijaitwa Dueustche ost – afrika ambayo baada ya kuchukuliwana waingeleza ikaitwa Tanganyika, jina lililotokana na ziwa Tanganyika, na baadae kuitwa Tanzania baada ya muungano, akielekea wilayani tunduru, akikwepa majeshi ya kingoni yaliyokuwa yamechukua eneo la kaskazini mwa milima ya matogoro.
Sehemu hii ambayo ilikuwa na wenyeji wapole na wastaarabu, wenye ukarimu na wapenda amani, ndiyo ilikuwa sehemu pekee ambayo wasafiri wengi waliweza kupumzika na kupata chakula, sasa siku hiyo Chiefu kwala, au Ache Kwala, kama unavyoweza kumwita, aliamua kuoga kidogo ndani ya mto huo, na kwa habati mbaya wakati anaoga baadhi ya wasaidi wake wakike walienda kuchota maji muda huo na kuona korodani za Chief, toka siku hiyo mto ukaitwa jina hilo, bhumbu za Kwala.
Hapo mtoni kuna shamba moja lenye mazao yaliyostawi vyema, japo mkazi au wakazi wa nyumba hii ndogo hafifu iliyo jengwa kwa Udongo na kuezekwa kwa makuti ya minazi, walionekana kujihusisha na uvuvi, kwasababu kulikuwa na nyavu pale nje, ila hapakuwa na mtu yoyote zaidi alie onekana pale nje kama ilivyo kule kitongojini, ni wazi kuwa wenyeji walikuwa wamelala, hapo ghafla tunaona askari wa MLA waliovalia sale nyeusi, wakiibuka toka vichakani kushoto kulia na mbele ya nyumba hii, huku wakiizuka na kujipanga kwa ulinzi na bunduki zao aina ya Uzi gun ya mwaka 2008.
Kitendo cha haraka, askari wanatembea kwa kunyata wakipeana majukumu na maeneo ya ulinzi kwa kutumia ishara za kivita, vilivyo husisha vidole vya mikono, ishara zilizo wagawa askari hawa, na kila mmoja akikaa kwenye sehemu yake, kila kona ya nyumba ile, huku askari wanne wakiusogelea mlango ambao walipoaribu kuufungua taratibu nao ukafunguka, na askari wakaingia kwa kunyata huku tochi zao zikiwa zimetangulia mbele na kuangazia mule ndani, “hamkuwa na haja ya kunyatia, nilikuwa najua ipo siku mutanifikia ndio maana sikukimbia nilipo hisi ujio wenu” ilisikika sauti toka upande wa kulia wa chumba kile, wote wanageuka upande ule, ambapo wanamuona mwanaume mmoja mtu mzima akiwa amesimama kwenye kizingiti cha mlango kilichokuwa kimezibwa kwa kipande cha shuka chakavu.
Makamanda wa kikundi maalumu cha uchunguzi wa kivita, kila mmoja akashangaa moyoni mwake, huku wote bila kupepesa wakiwa bado wameelekeza bunduki zao kwa mwanaume huyo, unatakiwa kutulia hivyo hivyo, usijiguse sehemu yeyote” alisistiza mmoja kati ya wale askari wanne waliongingia ndani, huku bunduki imemkodolea yule mzee aliekuwa anawatazama kwa macho ya kukata tamaa, “chochote mutakacho nifanya naomba musiidhuru familia yangu” alisema yule mwanaume mtu mzima kwa sauti ya kukata tamaa, “staff sajent Ashraf Kibwana, sisi hatupo hapa kukudhuru ila tunahitaji ujisalimishe na hii itasaidia familia yako kuwa salama” alisema mmoja kati ya wale askari walioingia ndani, “inamaana hamtonifanya kama mulivyo wafanya wengine?” aliuliza mzee yule kwa sauti yenye mashaka, “tunahitaji kuondoka na wewe kwaajili ya mahojiano, ili kujuwa kilicho tokea mwaka 92 pamoja na kujua kilicho watokea askari wenzio walioshiriki katika operation ya kuondoa waasi, hii ni siri na kwa faida ya taifa” alisema yule askari wa MLA, “nyie mmetumwa na nani, serikali yenyewe au Waziri Chitopelah?” aliuliza bwana Ashraff kwa sauti yenye mashaka, “hili ni agizo toka kwa mfalme Elvis, hivyo unatakiwa kuongozana na sisi” alisema yule askari.
Nivkama kauli hiyo iliibua matumaini kwa mzee huyu, ambae kwa mara ya kwanza aliachia tabasamu, kama ni kweli nipo tayari, lakini naomba munihakikishie usalama wangu na familia yangu” alisema yule mzee, kwa sauti yenye kuchangamka kdogo, “bila shaka, tutaondoka na familia yako, lakini kumbuka kuwa usijaribu kuleta ujanja wowote” alisema yule askari.*********
Yaaaap! Magari Matano yaliyopo katika msafara wa makamanda wa ngazi za juu wa jeshi la polisi kanda maalumu ya kipolisi ya dar es salaam, yalionekana yakikatika mapori ya misegese, maeneo ya relini, huku katika gari manne yaliyokuwepo katikati ya magari matatu ya walinzi yaliyojipanga kwa mtindo wa moja mbele mawili nyuma, gari la nne katikati lilikuwa ni gari la RPC ilala, bwana Robart Ulenje, ambae muda wote alikuwa anaongea na simu kutoa maelekezo kwa watu ambao kwa namna moja au nyingine, ni washirika wake nje ya taratibu za kiuongozi wa jeshi la polisi.
Naaaam, ukiachilia kuongea na simu mara kwa mara, pia Ulenje alikuwa anafikiria sana kuhusu uwepo wa kundi dogo la bwana Uled Songoro, katika maeneo haya ya msitu wa misegese, akimsaka kijana shupavu na mjuzi wa vita Deus Nyati, “huyu mjinga hajui anamsaka nani, lazima kitamkuta kitu ambacho kitamfanya akimbilie msaada wa polisi, ambao watamuweka chini ya ulinzi na kunisababishia matatizo” aliwaza Ulenje huku anabofya namba ya Songoro na kuipiga.
Bahati nzuri simu iliita na kupokelewa mara moja, “niambie Ulenje, kuna jipya” aliuliza Songoro kwa shauku kubwa, “Songoro upo wapi sasa hivi?” aliuliza Ulenje, “nipo kichakani nimejibanza, nasubiri kwanza magari ya polisi yapite, vipi kuna inshu?” aliuliza Songoro, “Songoro nataka kujuwa sehemu mulipo” alisema Ulenje, ambae alionyesha kuto kuhitaji maongezi mengi, “nipo ndani kidogo kutoka barabarani, karibu na reli” alisema Songoro, na hapo Ulenje akashusha pumzi kidogo, kama vile ana jambo fulani muhimu anataka kumueleza Songoro.
“sikia Songoro, ni vyema kama utaondoka eneo hili, kwasababu jeshi la polisi lote la dar es salaam lipo huku, hebu subirini sisi tupite, kisha nyie muondoke, vinginevyo kitawakuta kitu ambacho sitokuwa na msaada kwenu” alisisitiza Ulenje wakati anaongea na simu, “hivi Ulenje unanichukuliaje wewe, nyie watafuteni hao wapuuzi wenu, mimi namsaka yule mjinga, mpaka nimtie mkononi” ilisikika sauti ya upande wa pili wa simu iliyojaa majisifu na kujitia umwamba, “Songoro hebu nikuulize kitu, hapo unavijana wangapi?” aliiuliza Ulenje, “hapa nina watu kama tisa na mimi mwenyewe wa kumi” alijibu Songoro upande wapili wa simu, “wanamafunzo gani ya kijeshi?” aliuliza Ulenje, na hapo kikafuata kicheko kikali cha dharau, “inamaana Ulenje ndio umenidharau kiasi hicho, kwamba watu wangu hawawezi kupambana na huyu mtoto?” aliuliza Songoro, ambae alionekana wazi kuwa kile kicheko chake, kilikuwa cha hasira, “sikia Songoro, sio kwamba nakudharau, ila ukweli ni kwamba, hao vijana ulio nao hawawezi kupambana na Dereva, cha kufanya wewe rudi mjini hii kazi niachie mimi” alisema Ulenje, kwa sauti iliyojaa maombi.
Lakini ilikuwa ni kama kupigia mbuzi gitaa, Sogoro hakuonyesha dalili yoyote ya kukubariana na Ulenje, “Ulenje, wewe shida yako nini, mimi najua ninachofanya, wewe endelea na mipango yako na mimi napambana kivyangu” alisema Songoro, kwa sauti yenye ubabe ndani yake, mpaka hapo ACP Ulenje, aliona wazi kuwa anaenda kuharibikiwa kabla jua ailijachomoza, hivyo nilazima achukue maamuzi magumu, “sawa bwana Songoro, pengine umejipanga, ila itabidi nikuongezee nguvu ya askari na silaha” alisema Ulenje, kwa sauti tulivu mfano wa mtu alie kubaliana na msimamo wa Songoro, “hapo sasa ndio umeongea point, sasa nakutana nao wapi hao askari?” aliuliza Songoro, akionyesha kufurahia mpango wa Ulenje, akujuwa kuwa kilichopangwa na Ulenje ni zaidi ya mipango yake ya kikatiri aliyowai kuifanya……..……. ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums