Abou Shaymaa
JF-Expert Member
- Oct 19, 2022
- 1,479
- 3,229
- Thread starter
- #341
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA SABINI NA MOJA
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA SABINI: mschana aliempa habari za watu wanaopanga kumpora mali zake, walitembea kwa haraka kuelekea upande wa barabarani, huku bwana Simba mwenyewe akiwa ametawaliwa na hofu kubwa sana, “hivi hapa ninaweza kupata usafiri wa ufika Moshi usiku huu?” aliuliza mzee Simba ambae sauti yake ilikuwa imetawaliwa na kitetemeshi, “usafiri mwingi sana ila kuwa makini, maana inaonyesha yule kaka anawenzake na wapo njiani wanakuja” alisema yule mwanamke, huku wakiwa wanakaribia mwisho wa jengo lile la hotel ambako palionekana kuwa na mwanga, ..…….ENDELEA…
Naaam mara walipofika mwisho wa ile chochoro, yule mwanamke akasimama, akifuatiwa na mzee Simba ambae pia alisimama nyuma ya yule mwanamke, “sasa babangu, nadhani nimesha kusaidia vya kutosha, mimi naishia hapa cha kufanya wewe kimbilia hapo mbele ukivuka tu kona ya hapo mbele utatokea stendi, kuna magari na boda boda mimi nakushauri chukuwa boda boda mpaka mianzini ukapande gari, ila kama una ishirini na tano au thelathini boda boda anakupeleka mpaka moshi” alisema yule mwanamke huku akimtazama mzee Simba, ambae kiukweli hakuwahi kutegemea kama leo angekutana na dhahama kama hii, “asante sana dada yangu, wacha niwahi kabla hao wenzake hawajafika, nikija siku nyingine nitakutafuta, kwaajili ya shukrani zaidi” alisema mzee Simba huku anachungulia na kutazama kushoto na kulia, kuangalia kama sehemu ile ina usalama, “usiwe na shaka babaa hapa nipo kama nyumbani kwangu utanikuta tu” alisema yule mwanamke ambae bado alikuwa pale kizimbani.
Ukweli mzee Simba aliona eneo lile la mbele ya hotel kuwa ni salama kabisa, yani hapa kuwa na mtu wa kumtilia mshaka yoyote zaidi ya kuwaona watu waliokuwa wanaingia na kutoka pale hotelini, hapo akashika mkoba wake vyema na kuanza kutembea kwa haraka kutoka kwenye ile chochoro akiibukia eneo la mbele la hotel ile maarufu mjini Arusha, akikifuata kichochoro cha mbele yake ambacho kingempeleka mpaka barabara kuu ya Monduri ambako kuna stendi ndogo.*******
Yap! wakati huo huo Kijana Deus akiwa anakaribia njia panda ya kuelekea stendi kuu ameshikilia simu yake mkononi ana taka kubofya kiwashio, ndipo ghafla mbele yake likaingia gari dogo aina ya Toyota Altezza lililo kuwa katika speed ya ajabu, ambalo liliingia na kukamata uelekeo wa kule anakoelekea yeye na kujikuta akakinyaga brake za ghafla ili asiligonge lile gari, ambalo aliweza kuliona linamuacha kwa mwendo ule ule wa kasi ya ajabu, “hii ndiyo Arusha” alijisemea Deus huku anaachia brake na kukanyaga mafuta kidogo kuendelea na safari yake, “dah! angeligonga gari langu sidhani kama ningemuacha” aliwaza Deus, ambae kwa kuona kilichotokea alijuwa kuwa kama asipokuwa makini anaweza kujikuta akisababishiwa ajali, hivyo ni vyema angeachana na simu na kuiwasha baadae atakapo kuwa amesha jipumzisha kwenye hotel, ambayo kwa mujibu wa GPS yake ilikuwa mita chache toka pale alipokuwepo, kwa ushauri huo aliojipa Deus akaiweka simu kwenye seat ya pembeni.
Deus aliendesha gari lake kwa tahadhari na uangalifu mkubwa akihofia kusababishiwa ajali, na wakati huo akiliona kwa mbali lile gari dogo, linapunguza mwendo na kuingia upande wa kushoto wa barabara kwenye njia ambayo kwa mujibu wa GPS ambao ni mpangilio maalumu wa kuonyesha sehemu, walioanzisha hiyo wanaitwa Global Positioning System, ilimuonyesha kuwa na yeye alikuwa anatakiwa upande huo huo.
Deus akaongeza mwendo kuifuata ile barabara, ambayo ilikuwa mita chache mbele yake, barabara ambayo aliifikia sekunde chache sana baadae, alipoifikia akakata kushoto ambapo mita chache mbele yake aliweza kuona jengo kubwa lililoandikwa Mrina Hotel, siyo hivyo tu aliweza kuliona pia lile gari lililompita wakati ule nakutaka kumsababishia ajali, gari ambalo lilionekana kuwa limeingia muda mfupi uliopita, maana sasa aliweza kuona milango yote minne ya gari lile inafunguliwa na wanashuka watu wanne huku wawili kati yao wakitupa vipisi vya sigara na kisha kuanza kutembea kuelekea kwenye lango la hotel “mh! ni sehemu sahihi kweli hii” alijiuliza Deus, huku anaendesha gari lake taratibu akipishana na watu mbali mbali waliokuwa wanaingia na kutoka pamoja na magari.
Deus akiwa anaendesha gari lake taratibu, huku anatafuta sehemu ya kuegesha mara akawaona wale vijana wanne waliokuwa wanaelekea kwenye jengo la hotel, wakisimama ghafla kumtazama mwanaume mmoja mtu mzima, aliebeba sanduku dogo jeusi, ambae alikuwa anatembe kwa kasi kuja upande wa pili wa jengo la hotel, akipita usawa wa gari lake lilikuwa linatembea taratibu.
Deus ambae mwanzo hakuwajali watu wale, akawaona wanaanza kumfuata yule mwanaume mtu mzima, ambae pia nikama aliwaona watu wale na kuanza kuongeza mwendo, kuja usawa wa gari, kitu ambacho kilimlazimu Deus kusimama kabisa ilikuepuka kusababisha ajali ya kugonga mtu.
Hapo sasa Deus akaweza kushuhudia juhudi za yule mwanaume mtu mzima ambae ni mzee Simba, ziligonga mwamba maana aliweza kuwaona wale jamaa wa nne wakianza kumkimbiza yule mtu mzima, ambae pia hakutaka kuzubaa, nae akatoka mbio dhaifu.
Hakika mazoezi binafsi ni kitu muhimu sana, maana huyu mwanaume mtu mzima hakuweza hata kulivuka gari la Deus, tayari alijikuta mikononi mwa wale jamaa wanne, “we! boya unadhani unaweza kutukimbia sisi” alisema mmoja wao huku akimnyang’anya lile sanduku, yule mzee alionekana kuwa na wasi wasi na uoga mkubwa huku sura ya kinyonge na kukata tamaa ikimtawala,
Kitendo kile kilimuumiza sana Deus, ambae hakutaka kujiingiza kwenye jambo lile ambalo aliliona kama vile halikumhusu, “hii ndiyo R chuga wewe hatuishi kizembe” alisema mwingine huku akimsukuma kwa nguvu yule mzee, ambae alienda kujibamiza kwenye BMW S7, “khaaa! imezidi sasa” alisema Deus, huku anaweka gia katika sehemu ya kuegesha wakati huo anamuona yule aliemsukuma yule mzee, akimfuata pale kwenye gari na kumkwida yule mzee akimkandamiza kwenye gari, “sikia we fala, funga mdomo wako na utulie hivyo hivyo, “alisema yule mmoja huku anaingiza mkono wake wakulia kwenye mfuko wa suruali wa yule mtu mzima na kuibuka na kitita cha fedha akakiweka kwenye mfuko wake.
Deus alifungua mkanda seat na kufungua mlango wakati huo yule mkabaji akizamisha tena mkono kwenye mfuko mwingine wa suruali ya mtu mzima na kuinuka na simu, “we boya rudi ndani ya gari faster” alisema mmoja kati ya wale wanne, huku anamsogelea Deus kwa haraka huku ameinua mkono kwa lengo la kutandika ngumi kijana huyu ambae umoja wa maaifa wameliweka jina lake kwenye orodha yao.
Ukweli kijana huyu, hakuwa na bahati maana kabla hata hajarusha ngumi yake, tayari alisha kutana na kitu kizito kilichotuwa usawa wa mgongo wa pua na kumtupa hatua kadhaa nyuma, huku wenzake wakigeuka kumtazama kwa mshtuko kubwa wasiamini kama amepigwa au amegongwa na boda boda, kisha kwa macho yaliyojaa hasira na mshangao wakamtazama Deus, “ase we fala unaleta maniaje tena, hivi unatujuwa sisi” alisema yule aliemshika yule mzee, huku anamuachia mzee mtu mzima na kuingiza mkono wake usawa wa kiuno, ambap aliibuka na kisu kirefu maarufu kama sime, kilichokuwa kinang’ara kwa makali yake na wenzake wawili, ukiacha yule alieshika sanduku, nao wakatoa visu vinavyo fanana na kile cha mwenzao, ambae ni Mduma, huku Deus akiwa anawatazama tu.
“sikilizeni wakubwa, sina ugomvi na nyie, ila nilitaka niwaambie msiguse gari langu” alisema Deus, kwa sauti ya upole yenye utaratibu wa kidaktari, ambayo haikuwashtua wakina Mduma, “oyaaa, acha kuongea ujinga babake, kama vipi weka mazaga yote juu ya boneti kisha tambaa zako” alisema Mduma huku anamsogelea Deus, ni wazi aliamini kuwa Deus amekuwa mpole kwaajili ya vile visu walivyoshika, “sikia bro, sijapenda kuumiza mtu mwingine zaidi, ni vyema mukakaa mbali na gari langu, ila mukini lazimisha nitafanya” alisema Deus, wakati huo bwana Simba akiwa amesimama pembeni anawatazama kwa macho ya uoga mfano wa paka anae subiria chakula kianguke toka mezani.
Neno la Deus nikama lilikuwa dharau kwa Mduma, ambae aliinua mkono juu akivuta lile nusu panga na kulishusha kuelekea begani kwa Deus, “hebu kaa chini we kim…” kabla hata mduma hajamaliza kuongea alichokusudia kuongea, aliweza kushuhudia yule jamaa akivuta hatua moja mbele kumkaribia zaidi na kuudaka mkono wake ambao aliuzungusha kwa nguvu na kwa ghafla, kitendo kilicho sababisha mduma mwenyewe zunguke kwa nguvu na kabla hajakaa sawa alihisi kitu kizito kikitua usawa wa kifua chake, huku mlio kama wa kuvunjika kwa mbao au kijiti kikavu ukisikika na yeye kwenda chini kama kiroba akinyimwa kupiga kelele ya aina yoyote kwa mkandamizo wa mguu, uliokita shingoni kwake huku akinyang’anywa lile panga lake, ambalo ndilo lililo tumika kuwageuza bucha wenzake.
Yani ndani ya muda mfupi watu waliokuwepo eneo la mbele la hotel pamja na mzee Simba walikuwa wameshuhudia tukio ambalo kama kuna aliewahi kuliona basi ni kwenye filamu za kikorea japan au china au hata ile ya sara dini part 3, kilikuwa ni kipigo kizito kipigo cha paka jizi, kipigo ambacho kilitumia muda mfupi sana, kipigo ambacho kilimfanya mzee Simba abakie anamtazama Deus kwa mshangao, nikama alikuwa anajiuliza kama Deus nae alikuwa anafuata sanduku lake ama sivyo, na kama ndiyo hivyo basi hatima yake ni mbaya zaidi kuliko ile ya mwanzo, maana sio kwa kipigo kile ambacho alikiona kwa macho yake, ambacho hata mimi sijaona kama itakuwa vyema kukielezea, kwa kunusuru wale mwana JF mwenye ugonjwa wa moyo.
Naam tayari watu walikuwa wanaanza kusogelea kwenye tukio huku kelele za chini chini zikianza kusikika, “ameuwa, kauwa” hawa kuwa watu waliokuwepo pale nje pekee, wapo pia waliotokea nani, “ni vyema kama utaacha kunitazama na ukachukuwa kila kilichochako, kisha ukaondoka eneo hili” alisema Deus, huku anatazama gari lake kama vile analikagua kuhakiksiha halijaumia sehemu, liwe tayari kwa safari mpya, ukweli asingeweza kukaa tena pale Arusha japo n ikama tukio lile lilichukuliwa kawaida na wenyeji, wakidhania kuwa ulikuwa ni ugomvi wa walevi.
Wakati huo mzee Simba, akiwa analiokota sanduku lake na kisha akamfuata Mduma, ambae sasa alikuwa amelala chini, huku anatokwa na damu puani na mdomoni, akampekuwa na kuchukuwa fedha yake na simu yake, kama vile alikuwa anafanya juhudi ya kumuwahi Deus, alie kuwa anaingia kwenye gari ili waondoke pamoja.
Ni kweli ile fumba na kufumbua tayari mzee Simba alishafungua mlango wa seat ya abiria wa mbele, na kufunga mlango, “kijana naomba unipeleke Dar es salaam, nitagharamia kuanzia mafuta na gharama nyingine zozote zitakazojitkeza wakati wote wa safari” alisema yule mtu mzima kwa sauti ya kuomboleza, akonyesha wazi kuwa anaamini kuwa Deus ndie mtu pekee anaeza kumfikisha Dar es salaam.
Hapo Deus akahisi kama vile kazi ya usafirishaji, inaenda kuwa kazi yake mpya, “unadhani mzigo wako na thamani yako inaweza kuwa sawa na lita mia moja za petrol?” aliuliza Deus kwa sauti tulivu huku anafunga mkanda wa kwenye kiti, “kijana taja gharama kiasi cha fedha unachohitaji” alisema mzee Simba, akionyesha kuhitaji sana usafiri wenye usalama wa kijana huyu,msomaji wangu nakukumbusha tena kuwa simulizi yetu bado haijaanza, huu ni utangulizi tu wa bwana Deusi Frank Nyati ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
SEHEMU YA SABINI NA MOJA
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA SABINI: mschana aliempa habari za watu wanaopanga kumpora mali zake, walitembea kwa haraka kuelekea upande wa barabarani, huku bwana Simba mwenyewe akiwa ametawaliwa na hofu kubwa sana, “hivi hapa ninaweza kupata usafiri wa ufika Moshi usiku huu?” aliuliza mzee Simba ambae sauti yake ilikuwa imetawaliwa na kitetemeshi, “usafiri mwingi sana ila kuwa makini, maana inaonyesha yule kaka anawenzake na wapo njiani wanakuja” alisema yule mwanamke, huku wakiwa wanakaribia mwisho wa jengo lile la hotel ambako palionekana kuwa na mwanga, ..…….ENDELEA…
Naaam mara walipofika mwisho wa ile chochoro, yule mwanamke akasimama, akifuatiwa na mzee Simba ambae pia alisimama nyuma ya yule mwanamke, “sasa babangu, nadhani nimesha kusaidia vya kutosha, mimi naishia hapa cha kufanya wewe kimbilia hapo mbele ukivuka tu kona ya hapo mbele utatokea stendi, kuna magari na boda boda mimi nakushauri chukuwa boda boda mpaka mianzini ukapande gari, ila kama una ishirini na tano au thelathini boda boda anakupeleka mpaka moshi” alisema yule mwanamke huku akimtazama mzee Simba, ambae kiukweli hakuwahi kutegemea kama leo angekutana na dhahama kama hii, “asante sana dada yangu, wacha niwahi kabla hao wenzake hawajafika, nikija siku nyingine nitakutafuta, kwaajili ya shukrani zaidi” alisema mzee Simba huku anachungulia na kutazama kushoto na kulia, kuangalia kama sehemu ile ina usalama, “usiwe na shaka babaa hapa nipo kama nyumbani kwangu utanikuta tu” alisema yule mwanamke ambae bado alikuwa pale kizimbani.
Ukweli mzee Simba aliona eneo lile la mbele ya hotel kuwa ni salama kabisa, yani hapa kuwa na mtu wa kumtilia mshaka yoyote zaidi ya kuwaona watu waliokuwa wanaingia na kutoka pale hotelini, hapo akashika mkoba wake vyema na kuanza kutembea kwa haraka kutoka kwenye ile chochoro akiibukia eneo la mbele la hotel ile maarufu mjini Arusha, akikifuata kichochoro cha mbele yake ambacho kingempeleka mpaka barabara kuu ya Monduri ambako kuna stendi ndogo.*******
Yap! wakati huo huo Kijana Deus akiwa anakaribia njia panda ya kuelekea stendi kuu ameshikilia simu yake mkononi ana taka kubofya kiwashio, ndipo ghafla mbele yake likaingia gari dogo aina ya Toyota Altezza lililo kuwa katika speed ya ajabu, ambalo liliingia na kukamata uelekeo wa kule anakoelekea yeye na kujikuta akakinyaga brake za ghafla ili asiligonge lile gari, ambalo aliweza kuliona linamuacha kwa mwendo ule ule wa kasi ya ajabu, “hii ndiyo Arusha” alijisemea Deus huku anaachia brake na kukanyaga mafuta kidogo kuendelea na safari yake, “dah! angeligonga gari langu sidhani kama ningemuacha” aliwaza Deus, ambae kwa kuona kilichotokea alijuwa kuwa kama asipokuwa makini anaweza kujikuta akisababishiwa ajali, hivyo ni vyema angeachana na simu na kuiwasha baadae atakapo kuwa amesha jipumzisha kwenye hotel, ambayo kwa mujibu wa GPS yake ilikuwa mita chache toka pale alipokuwepo, kwa ushauri huo aliojipa Deus akaiweka simu kwenye seat ya pembeni.
Deus aliendesha gari lake kwa tahadhari na uangalifu mkubwa akihofia kusababishiwa ajali, na wakati huo akiliona kwa mbali lile gari dogo, linapunguza mwendo na kuingia upande wa kushoto wa barabara kwenye njia ambayo kwa mujibu wa GPS ambao ni mpangilio maalumu wa kuonyesha sehemu, walioanzisha hiyo wanaitwa Global Positioning System, ilimuonyesha kuwa na yeye alikuwa anatakiwa upande huo huo.
Deus akaongeza mwendo kuifuata ile barabara, ambayo ilikuwa mita chache mbele yake, barabara ambayo aliifikia sekunde chache sana baadae, alipoifikia akakata kushoto ambapo mita chache mbele yake aliweza kuona jengo kubwa lililoandikwa Mrina Hotel, siyo hivyo tu aliweza kuliona pia lile gari lililompita wakati ule nakutaka kumsababishia ajali, gari ambalo lilionekana kuwa limeingia muda mfupi uliopita, maana sasa aliweza kuona milango yote minne ya gari lile inafunguliwa na wanashuka watu wanne huku wawili kati yao wakitupa vipisi vya sigara na kisha kuanza kutembea kuelekea kwenye lango la hotel “mh! ni sehemu sahihi kweli hii” alijiuliza Deus, huku anaendesha gari lake taratibu akipishana na watu mbali mbali waliokuwa wanaingia na kutoka pamoja na magari.
Deus akiwa anaendesha gari lake taratibu, huku anatafuta sehemu ya kuegesha mara akawaona wale vijana wanne waliokuwa wanaelekea kwenye jengo la hotel, wakisimama ghafla kumtazama mwanaume mmoja mtu mzima, aliebeba sanduku dogo jeusi, ambae alikuwa anatembe kwa kasi kuja upande wa pili wa jengo la hotel, akipita usawa wa gari lake lilikuwa linatembea taratibu.
Deus ambae mwanzo hakuwajali watu wale, akawaona wanaanza kumfuata yule mwanaume mtu mzima, ambae pia nikama aliwaona watu wale na kuanza kuongeza mwendo, kuja usawa wa gari, kitu ambacho kilimlazimu Deus kusimama kabisa ilikuepuka kusababisha ajali ya kugonga mtu.
Hapo sasa Deus akaweza kushuhudia juhudi za yule mwanaume mtu mzima ambae ni mzee Simba, ziligonga mwamba maana aliweza kuwaona wale jamaa wa nne wakianza kumkimbiza yule mtu mzima, ambae pia hakutaka kuzubaa, nae akatoka mbio dhaifu.
Hakika mazoezi binafsi ni kitu muhimu sana, maana huyu mwanaume mtu mzima hakuweza hata kulivuka gari la Deus, tayari alijikuta mikononi mwa wale jamaa wanne, “we! boya unadhani unaweza kutukimbia sisi” alisema mmoja wao huku akimnyang’anya lile sanduku, yule mzee alionekana kuwa na wasi wasi na uoga mkubwa huku sura ya kinyonge na kukata tamaa ikimtawala,
Kitendo kile kilimuumiza sana Deus, ambae hakutaka kujiingiza kwenye jambo lile ambalo aliliona kama vile halikumhusu, “hii ndiyo R chuga wewe hatuishi kizembe” alisema mwingine huku akimsukuma kwa nguvu yule mzee, ambae alienda kujibamiza kwenye BMW S7, “khaaa! imezidi sasa” alisema Deus, huku anaweka gia katika sehemu ya kuegesha wakati huo anamuona yule aliemsukuma yule mzee, akimfuata pale kwenye gari na kumkwida yule mzee akimkandamiza kwenye gari, “sikia we fala, funga mdomo wako na utulie hivyo hivyo, “alisema yule mmoja huku anaingiza mkono wake wakulia kwenye mfuko wa suruali wa yule mtu mzima na kuibuka na kitita cha fedha akakiweka kwenye mfuko wake.
Deus alifungua mkanda seat na kufungua mlango wakati huo yule mkabaji akizamisha tena mkono kwenye mfuko mwingine wa suruali ya mtu mzima na kuinuka na simu, “we boya rudi ndani ya gari faster” alisema mmoja kati ya wale wanne, huku anamsogelea Deus kwa haraka huku ameinua mkono kwa lengo la kutandika ngumi kijana huyu ambae umoja wa maaifa wameliweka jina lake kwenye orodha yao.
Ukweli kijana huyu, hakuwa na bahati maana kabla hata hajarusha ngumi yake, tayari alisha kutana na kitu kizito kilichotuwa usawa wa mgongo wa pua na kumtupa hatua kadhaa nyuma, huku wenzake wakigeuka kumtazama kwa mshtuko kubwa wasiamini kama amepigwa au amegongwa na boda boda, kisha kwa macho yaliyojaa hasira na mshangao wakamtazama Deus, “ase we fala unaleta maniaje tena, hivi unatujuwa sisi” alisema yule aliemshika yule mzee, huku anamuachia mzee mtu mzima na kuingiza mkono wake usawa wa kiuno, ambap aliibuka na kisu kirefu maarufu kama sime, kilichokuwa kinang’ara kwa makali yake na wenzake wawili, ukiacha yule alieshika sanduku, nao wakatoa visu vinavyo fanana na kile cha mwenzao, ambae ni Mduma, huku Deus akiwa anawatazama tu.
“sikilizeni wakubwa, sina ugomvi na nyie, ila nilitaka niwaambie msiguse gari langu” alisema Deus, kwa sauti ya upole yenye utaratibu wa kidaktari, ambayo haikuwashtua wakina Mduma, “oyaaa, acha kuongea ujinga babake, kama vipi weka mazaga yote juu ya boneti kisha tambaa zako” alisema Mduma huku anamsogelea Deus, ni wazi aliamini kuwa Deus amekuwa mpole kwaajili ya vile visu walivyoshika, “sikia bro, sijapenda kuumiza mtu mwingine zaidi, ni vyema mukakaa mbali na gari langu, ila mukini lazimisha nitafanya” alisema Deus, wakati huo bwana Simba akiwa amesimama pembeni anawatazama kwa macho ya uoga mfano wa paka anae subiria chakula kianguke toka mezani.
Neno la Deus nikama lilikuwa dharau kwa Mduma, ambae aliinua mkono juu akivuta lile nusu panga na kulishusha kuelekea begani kwa Deus, “hebu kaa chini we kim…” kabla hata mduma hajamaliza kuongea alichokusudia kuongea, aliweza kushuhudia yule jamaa akivuta hatua moja mbele kumkaribia zaidi na kuudaka mkono wake ambao aliuzungusha kwa nguvu na kwa ghafla, kitendo kilicho sababisha mduma mwenyewe zunguke kwa nguvu na kabla hajakaa sawa alihisi kitu kizito kikitua usawa wa kifua chake, huku mlio kama wa kuvunjika kwa mbao au kijiti kikavu ukisikika na yeye kwenda chini kama kiroba akinyimwa kupiga kelele ya aina yoyote kwa mkandamizo wa mguu, uliokita shingoni kwake huku akinyang’anywa lile panga lake, ambalo ndilo lililo tumika kuwageuza bucha wenzake.
Yani ndani ya muda mfupi watu waliokuwepo eneo la mbele la hotel pamja na mzee Simba walikuwa wameshuhudia tukio ambalo kama kuna aliewahi kuliona basi ni kwenye filamu za kikorea japan au china au hata ile ya sara dini part 3, kilikuwa ni kipigo kizito kipigo cha paka jizi, kipigo ambacho kilitumia muda mfupi sana, kipigo ambacho kilimfanya mzee Simba abakie anamtazama Deus kwa mshangao, nikama alikuwa anajiuliza kama Deus nae alikuwa anafuata sanduku lake ama sivyo, na kama ndiyo hivyo basi hatima yake ni mbaya zaidi kuliko ile ya mwanzo, maana sio kwa kipigo kile ambacho alikiona kwa macho yake, ambacho hata mimi sijaona kama itakuwa vyema kukielezea, kwa kunusuru wale mwana JF mwenye ugonjwa wa moyo.
Naam tayari watu walikuwa wanaanza kusogelea kwenye tukio huku kelele za chini chini zikianza kusikika, “ameuwa, kauwa” hawa kuwa watu waliokuwepo pale nje pekee, wapo pia waliotokea nani, “ni vyema kama utaacha kunitazama na ukachukuwa kila kilichochako, kisha ukaondoka eneo hili” alisema Deus, huku anatazama gari lake kama vile analikagua kuhakiksiha halijaumia sehemu, liwe tayari kwa safari mpya, ukweli asingeweza kukaa tena pale Arusha japo n ikama tukio lile lilichukuliwa kawaida na wenyeji, wakidhania kuwa ulikuwa ni ugomvi wa walevi.
Wakati huo mzee Simba, akiwa analiokota sanduku lake na kisha akamfuata Mduma, ambae sasa alikuwa amelala chini, huku anatokwa na damu puani na mdomoni, akampekuwa na kuchukuwa fedha yake na simu yake, kama vile alikuwa anafanya juhudi ya kumuwahi Deus, alie kuwa anaingia kwenye gari ili waondoke pamoja.
Ni kweli ile fumba na kufumbua tayari mzee Simba alishafungua mlango wa seat ya abiria wa mbele, na kufunga mlango, “kijana naomba unipeleke Dar es salaam, nitagharamia kuanzia mafuta na gharama nyingine zozote zitakazojitkeza wakati wote wa safari” alisema yule mtu mzima kwa sauti ya kuomboleza, akonyesha wazi kuwa anaamini kuwa Deus ndie mtu pekee anaeza kumfikisha Dar es salaam.
Hapo Deus akahisi kama vile kazi ya usafirishaji, inaenda kuwa kazi yake mpya, “unadhani mzigo wako na thamani yako inaweza kuwa sawa na lita mia moja za petrol?” aliuliza Deus kwa sauti tulivu huku anafunga mkanda wa kwenye kiti, “kijana taja gharama kiasi cha fedha unachohitaji” alisema mzee Simba, akionyesha kuhitaji sana usafiri wenye usalama wa kijana huyu,msomaji wangu nakukumbusha tena kuwa simulizi yetu bado haijaanza, huu ni utangulizi tu wa bwana Deusi Frank Nyati ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums