Abou Shaymaa
JF-Expert Member
- Oct 19, 2022
- 1,479
- 3,229
- Thread starter
- #501
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA TISINI NA SABA
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA TISINI NA SITA:- Pale mapokezi hakuwaona kabisa wale jamaa wanne, wala jamaa wa mapokezi au meneja wa hotel, “wameenda wapi hawa jamaa” aliuliza Cheleji, akimuuliza mmoja wa askari aliekuwepo pale eneo la mapokezi, “wameelekea chumba cha kuongozea camera” alijibu yule askari huku akionyesha upande wenye chumba cha kuongozea camera za usalama wa jengo hilo…..….ENDELEA…
Cheleji alitoka haraka na kuelekea upande ule alio onyeshwa, yani kwenye chumba chenye camera za usalama za hotel nzima.********
Naam! sasa turudi mbezi mwisho, stendi ya malamba mawili mtaa bado umechangamka, wafanya biashara wadogo wadogo waliojaa pembezoni mwa barabara wanaendelea kuwahudumia wateja wao sauti za matangazo toka kwenye speeker zinasikika zikinadi bidhaa mbali, ikiwa ni pamoja na simu usajiri wa line za simu na bidhaa nyingine nyingi, sauti za music na kelele za watu toka kwenye bar za jirani zilisikika, magari boda boda na waenda kwa miguu nao walizidi kupilikisha mtaa.
Mita mia mbili toka lilipo jengo la Benk ya uhifadhi, BMW jeusi toleo la kisasa kabisa (kwa wakati huo) linaonekana likiwa limesimama, huku bado likiwa katika muungurumo, japo kama haukuwa makini usingesikia ngurumo hiyo hafifu ya gari hilo la kisasa, zaidi ungegundua kwa taa ambazo zilikuwa zinawaka kwa mwanga hafifu.
Ndani ya gari hilo la kisasa, yupo kijana Deus peke yake, ambae anatoa simu yake ndogo na kufungua, hapo anakutana na jumbe kadhaa za whatsap, ana bofya huku anatabasamu, nikama alijua mtumaji ni nani, hata anapofungua application ile ni kweli anakutana na jumbe kadhaa toka kwa pacha, “nita jibu baadae, ngoja kwanza ni mpigie baba” anajisemea Deus huku anaodoa ile sehemu ya whatsap na kupiga kwenda sehemu ya miito na kuipiga namba ya baba yake.
Simu inaita kwa sekunde chache kisha inapokelewa, “Deus, vipi tena usiku huu, kuna tatizo?” aliuliza mzee Frank akionekana wazi kuwa hakuwa na dalili yoyote ya mtu ambae ametoka usingizini, “usiku vipi baba wakati hujalala bado?” aliongea Deus, kwa sauti ya utani, “ok! tuyaache hayo kuna jipya gani huko dar?” aliuliza mzee Frank, “nikuhusu mzee James, yule tajiri, alietoroka #mbogo_land, mwaka 1992” alisema Deus, na kuanza kumsimulia mkasa wote ulivyokuwa.
Wakati Deus anasimulia mkasa wake na baba yake, sisi twendeni ndani ya jengo la benk, ambako tunaingia tukiongozana na vijana watatu wenye kuvaa makoti makubwa ya baridi na sox vichwani mwao, wanatembea kwa kwaharaka huku wamekumbatia mikono yao maeneo ya vifuani mwao kama vile wameshikilia vitu fulani, lakini sisi tunatangulia kuingia ndani kabla yao.
Ndani ya jengo lile kubwa kiasi, shughuli zinaendelea kama kawaida, watu wapo kwenye mistari ya kusubiria huduma, anaonekana mschana mmoja mrembo mwenye uso uliojaa wasi wasi akiwa amekaa kwenye kiti kimoja kati ya vingi vya kusubiria huduma, macho yake yakiwa yanazunguka kuwatazama wateja waliopo kwenye foleni ya kusubiria huduma, baadae macho yake yanakwama kwa kijana mmoja, aliebeba begi lenye ukubwa wa kipimo cha kati, aliekuwa kwenye ile foleni ya kusubiria huduma akiwa mtu wa saba toka dirishani.
Wakati huo huo wanaingia vijana watatu wenye makoti mazito ya baridi na kofia za sox vichwani mwao, kila mmoja anashtuka na kabla hawajafanya lolote, wanamuona kijana wa mwisho kuingia anasimama mlangoni na mwingine anakimbilia mwishoni mwa ukumbi ule mdogo na kusimama karibu na main switch, huku mmoja akisimama katikati ya ukumbi na wote kwa pamoja wakafungua zip za makoti yao na kutoa bunduki, kisha yule wakatikati akaelekeza juu na kuminya trigger.
Hapo ukasikika mlipuko mkubwa wa risasi, “wote lala chini” alipiga kelele mmoja na mwingine pia akadakia, “lala chini pumbavu” alisema mwingne na mwingine akadakia, huku watu wakihangaika kujilaza chini kwa uoga kama vile mwanadada Veronica alivyofanya, alilala chini kwa haraka, yeye na wenzake wakiwa wametawaliwa na uoga wa hali ya juu.
Naaaam Veronica akiwa amelala pale chini, pamoja na wengine, anaweza kumuaona mmoja kati ya wale vijana watatu waliokuwa wameshikilia mitutu ya bunduki akienda moja kwa moja mpaka kwa yule mtu mwenye begi la kipimo cha kati toka kwenye kampuni ya bwana Lumen Manyonyi na kuchukua lile begi, “wekeni sura zenu chini” alisema yule aliechukuwa begi lile huku anatembea kusogelea kule alikokuwepo Veronica na wakatia anamkaribia yule wa mlangoni akapiga kelele, “oya fanyeni haraka polisi wanakuja” sauti hiyo ya juu, iliambatana na tukio la ghafla la kuzimika kwa taa za mule ndani.
Giza lilitanda, kimya kilitawala, hofu zilizidi mioyoni mwa watu, ndio wakati ambao Veronica alihisi begi linawekwa karibu yake, kisha vikasikika vishindo ya watu kutoka nje ya jengo lile, huku vishindo vingine vikiingia ndani, “polisi tulieni hivyo hivyo” ilisikika sauti ya kikakamavu, toka kwa mmoja kati ya wale waliongia na sekunde chache taa zikawashwa.
Naam mwanga ukatanda mle ndani watu walianza kuonana wazi wazi, kila mmoja aliweza kuwaona polisi wanne waliovalia sale zao mpya za kipolisi, majambazi watatu hawakuwepo mule ndani, mateka wa muda mfupi walijiona sasa wapo salama nao wakaanza kuinuka, “bilion kumi, za boss” alipiga kelele mmoja kati ya wale wateja, huku akikaribia kuangua kilio huku ana nyayuka toka chini.
Veronica nae akanyanyuka na lile begi, hakuna aliekumbuka kulitazama, maana hakukuwa na hata mmoja aliewaza kuwa begi lile liliachwa mule ndani, “subiri utatoa maelezo yako kituoni, kwa sasa tokeni nje kupisha ukaguzi” alisema mmoja kati ya wale polisi na hapo watu wakaanza kutoka kwa fujo mule ndani, huku Veronica akijichanganya na watu hao akiwa na begi lake, hata polisi nao walitoka na watu wale, hakika mambo yalifanyika kwa muda mfupi sana.
Turudi mita mia mbili, liliposimama BMW S7, ndani yake kuna Deus Nyati, ambae licha ya kusikia mlipuko wa risasi ambao moja kwa moja alijua kuwa mteja wake anahusika, yeye aliendelea kuongea na simu, “kwa hiyo baba, unatakiwa kuwa makini sana, kama wameanza na mzee James, pengine wakaja kwako pia” alisema Deus huku anatazama saa kwenye dash board ya gari lile la kifahari, ilikuwa imeshatimia saa nne na dakika mbili, “sidhani kama wananihitaji mimi, lengo lao lilikuwa ni kuniuwa na sio kunitumia baadae” alijibu bwana Frank na wakati huo Deus analiona land rover puma, likipita pale alipo na kuondoka zake likitokomea upande wa barabara kuu ya morogoro, “ok! baba ninapaswa kuondoka sehemu hii muda wangu umeisha” alisema Deus, huku anakata simu, ambayo aliitazama kwa sekunde kadhaa kama vile anajiuliza au anajishauri kitu fulani, “nitamjibu nikifika home” alijisemea Deus huku anaweka simu kwenye dash board.
Naaam ile anakanyaga cruitch ili aingize gia namba moja mara akasikia mlango wa gari seat ya abiria unafunguliwa kisha akaingia mwanamke, mwanamke ambae kama tukisema mrembo sidhani kama inatosha, labda niseme ni mzuri kuliko wote ambao Deus aliwahi kuwaona kwa macho yake, japo aliweza kumuona mwanamke huyu akimtazama kwa macho ya uoga na wasiwasi, lakini haikusababisha kuondoa uzuri asilia wa mwanmke huyu aliekuwa na begi mkononi, “sheria namba nane imeshavunjwa, mume shindwa kwenda na muda” alisema Deus kwa sauti tulivu huku anatazama mbele na mikono yake akishika kiongoza gari, yani mshikanio, “sheria ngapi za nchi mumevunja mpaka unajali kuhusu muda?” aliuliza yule mwanamke kwa sauti ya chini kama vile anajaribu, maana wasi wasi mwingi ulionekana ndani yake, wakati huo anafunga mlango, “ni vyema ukaweka hilo begi lako set ya nyuma na ukafunga mkanda kuliko kuongea ukiwa hujui unacho ongea” alisema Deus.
Naaam Veronica anaweka begi seat ya nyuma, na kufunga mkanda huku anamtazama kijana huyu, wenye sura ya upole ya kupendeza yenye kushangza na umbo la kusisimua, ambalo kila mwanamke angependa kujilaza kifuani kwake nyakati za usiku, ambae sasa alikuwa anakanyaga crachi na kuingiza gia namba moja, kisha gari linaondoka taratibu kuingia barabarani.
Safari inanza kimya kimya, huku kila mmoja akiwaza la kwake moyoni mwake, “hivi demu mkali kama huyu anawezaje kuwa jambazi, yani amekosa kabisa mwanaume wa kumhudumia au tamaa za kutajirika haraka haraka?” alijiuliza Deus huku akijizuia kumtazama Veronica ambae pia alikuwa anawaza yake , “masikini kijna wa watu mzuriiii lakini jambazi, hivi ukikutana nae mchana akikutongoza si unaweza kusema umepata mwanaume?” alijiuliza Veronica huku akimtazama kijana huyu kwa jicho la wizi.
Naaam kila mmoja akiwa katika mawazo yake, mala ghafla wanasikia ving’ora vya magari ya polisi, wote wanashtuka na kushikwa na wasi wa..….ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
SEHEMU YA TISINI NA SABA
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA TISINI NA SITA:- Pale mapokezi hakuwaona kabisa wale jamaa wanne, wala jamaa wa mapokezi au meneja wa hotel, “wameenda wapi hawa jamaa” aliuliza Cheleji, akimuuliza mmoja wa askari aliekuwepo pale eneo la mapokezi, “wameelekea chumba cha kuongozea camera” alijibu yule askari huku akionyesha upande wenye chumba cha kuongozea camera za usalama wa jengo hilo…..….ENDELEA…
Cheleji alitoka haraka na kuelekea upande ule alio onyeshwa, yani kwenye chumba chenye camera za usalama za hotel nzima.********
Naam! sasa turudi mbezi mwisho, stendi ya malamba mawili mtaa bado umechangamka, wafanya biashara wadogo wadogo waliojaa pembezoni mwa barabara wanaendelea kuwahudumia wateja wao sauti za matangazo toka kwenye speeker zinasikika zikinadi bidhaa mbali, ikiwa ni pamoja na simu usajiri wa line za simu na bidhaa nyingine nyingi, sauti za music na kelele za watu toka kwenye bar za jirani zilisikika, magari boda boda na waenda kwa miguu nao walizidi kupilikisha mtaa.
Mita mia mbili toka lilipo jengo la Benk ya uhifadhi, BMW jeusi toleo la kisasa kabisa (kwa wakati huo) linaonekana likiwa limesimama, huku bado likiwa katika muungurumo, japo kama haukuwa makini usingesikia ngurumo hiyo hafifu ya gari hilo la kisasa, zaidi ungegundua kwa taa ambazo zilikuwa zinawaka kwa mwanga hafifu.
Ndani ya gari hilo la kisasa, yupo kijana Deus peke yake, ambae anatoa simu yake ndogo na kufungua, hapo anakutana na jumbe kadhaa za whatsap, ana bofya huku anatabasamu, nikama alijua mtumaji ni nani, hata anapofungua application ile ni kweli anakutana na jumbe kadhaa toka kwa pacha, “nita jibu baadae, ngoja kwanza ni mpigie baba” anajisemea Deus huku anaodoa ile sehemu ya whatsap na kupiga kwenda sehemu ya miito na kuipiga namba ya baba yake.
Simu inaita kwa sekunde chache kisha inapokelewa, “Deus, vipi tena usiku huu, kuna tatizo?” aliuliza mzee Frank akionekana wazi kuwa hakuwa na dalili yoyote ya mtu ambae ametoka usingizini, “usiku vipi baba wakati hujalala bado?” aliongea Deus, kwa sauti ya utani, “ok! tuyaache hayo kuna jipya gani huko dar?” aliuliza mzee Frank, “nikuhusu mzee James, yule tajiri, alietoroka #mbogo_land, mwaka 1992” alisema Deus, na kuanza kumsimulia mkasa wote ulivyokuwa.
Wakati Deus anasimulia mkasa wake na baba yake, sisi twendeni ndani ya jengo la benk, ambako tunaingia tukiongozana na vijana watatu wenye kuvaa makoti makubwa ya baridi na sox vichwani mwao, wanatembea kwa kwaharaka huku wamekumbatia mikono yao maeneo ya vifuani mwao kama vile wameshikilia vitu fulani, lakini sisi tunatangulia kuingia ndani kabla yao.
Ndani ya jengo lile kubwa kiasi, shughuli zinaendelea kama kawaida, watu wapo kwenye mistari ya kusubiria huduma, anaonekana mschana mmoja mrembo mwenye uso uliojaa wasi wasi akiwa amekaa kwenye kiti kimoja kati ya vingi vya kusubiria huduma, macho yake yakiwa yanazunguka kuwatazama wateja waliopo kwenye foleni ya kusubiria huduma, baadae macho yake yanakwama kwa kijana mmoja, aliebeba begi lenye ukubwa wa kipimo cha kati, aliekuwa kwenye ile foleni ya kusubiria huduma akiwa mtu wa saba toka dirishani.
Wakati huo huo wanaingia vijana watatu wenye makoti mazito ya baridi na kofia za sox vichwani mwao, kila mmoja anashtuka na kabla hawajafanya lolote, wanamuona kijana wa mwisho kuingia anasimama mlangoni na mwingine anakimbilia mwishoni mwa ukumbi ule mdogo na kusimama karibu na main switch, huku mmoja akisimama katikati ya ukumbi na wote kwa pamoja wakafungua zip za makoti yao na kutoa bunduki, kisha yule wakatikati akaelekeza juu na kuminya trigger.
Hapo ukasikika mlipuko mkubwa wa risasi, “wote lala chini” alipiga kelele mmoja na mwingine pia akadakia, “lala chini pumbavu” alisema mwingne na mwingine akadakia, huku watu wakihangaika kujilaza chini kwa uoga kama vile mwanadada Veronica alivyofanya, alilala chini kwa haraka, yeye na wenzake wakiwa wametawaliwa na uoga wa hali ya juu.
Naaaam Veronica akiwa amelala pale chini, pamoja na wengine, anaweza kumuaona mmoja kati ya wale vijana watatu waliokuwa wameshikilia mitutu ya bunduki akienda moja kwa moja mpaka kwa yule mtu mwenye begi la kipimo cha kati toka kwenye kampuni ya bwana Lumen Manyonyi na kuchukua lile begi, “wekeni sura zenu chini” alisema yule aliechukuwa begi lile huku anatembea kusogelea kule alikokuwepo Veronica na wakatia anamkaribia yule wa mlangoni akapiga kelele, “oya fanyeni haraka polisi wanakuja” sauti hiyo ya juu, iliambatana na tukio la ghafla la kuzimika kwa taa za mule ndani.
Giza lilitanda, kimya kilitawala, hofu zilizidi mioyoni mwa watu, ndio wakati ambao Veronica alihisi begi linawekwa karibu yake, kisha vikasikika vishindo ya watu kutoka nje ya jengo lile, huku vishindo vingine vikiingia ndani, “polisi tulieni hivyo hivyo” ilisikika sauti ya kikakamavu, toka kwa mmoja kati ya wale waliongia na sekunde chache taa zikawashwa.
Naam mwanga ukatanda mle ndani watu walianza kuonana wazi wazi, kila mmoja aliweza kuwaona polisi wanne waliovalia sale zao mpya za kipolisi, majambazi watatu hawakuwepo mule ndani, mateka wa muda mfupi walijiona sasa wapo salama nao wakaanza kuinuka, “bilion kumi, za boss” alipiga kelele mmoja kati ya wale wateja, huku akikaribia kuangua kilio huku ana nyayuka toka chini.
Veronica nae akanyanyuka na lile begi, hakuna aliekumbuka kulitazama, maana hakukuwa na hata mmoja aliewaza kuwa begi lile liliachwa mule ndani, “subiri utatoa maelezo yako kituoni, kwa sasa tokeni nje kupisha ukaguzi” alisema mmoja kati ya wale polisi na hapo watu wakaanza kutoka kwa fujo mule ndani, huku Veronica akijichanganya na watu hao akiwa na begi lake, hata polisi nao walitoka na watu wale, hakika mambo yalifanyika kwa muda mfupi sana.
Turudi mita mia mbili, liliposimama BMW S7, ndani yake kuna Deus Nyati, ambae licha ya kusikia mlipuko wa risasi ambao moja kwa moja alijua kuwa mteja wake anahusika, yeye aliendelea kuongea na simu, “kwa hiyo baba, unatakiwa kuwa makini sana, kama wameanza na mzee James, pengine wakaja kwako pia” alisema Deus huku anatazama saa kwenye dash board ya gari lile la kifahari, ilikuwa imeshatimia saa nne na dakika mbili, “sidhani kama wananihitaji mimi, lengo lao lilikuwa ni kuniuwa na sio kunitumia baadae” alijibu bwana Frank na wakati huo Deus analiona land rover puma, likipita pale alipo na kuondoka zake likitokomea upande wa barabara kuu ya morogoro, “ok! baba ninapaswa kuondoka sehemu hii muda wangu umeisha” alisema Deus, huku anakata simu, ambayo aliitazama kwa sekunde kadhaa kama vile anajiuliza au anajishauri kitu fulani, “nitamjibu nikifika home” alijisemea Deus huku anaweka simu kwenye dash board.
Naaam ile anakanyaga cruitch ili aingize gia namba moja mara akasikia mlango wa gari seat ya abiria unafunguliwa kisha akaingia mwanamke, mwanamke ambae kama tukisema mrembo sidhani kama inatosha, labda niseme ni mzuri kuliko wote ambao Deus aliwahi kuwaona kwa macho yake, japo aliweza kumuona mwanamke huyu akimtazama kwa macho ya uoga na wasiwasi, lakini haikusababisha kuondoa uzuri asilia wa mwanmke huyu aliekuwa na begi mkononi, “sheria namba nane imeshavunjwa, mume shindwa kwenda na muda” alisema Deus kwa sauti tulivu huku anatazama mbele na mikono yake akishika kiongoza gari, yani mshikanio, “sheria ngapi za nchi mumevunja mpaka unajali kuhusu muda?” aliuliza yule mwanamke kwa sauti ya chini kama vile anajaribu, maana wasi wasi mwingi ulionekana ndani yake, wakati huo anafunga mlango, “ni vyema ukaweka hilo begi lako set ya nyuma na ukafunga mkanda kuliko kuongea ukiwa hujui unacho ongea” alisema Deus.
Naaam Veronica anaweka begi seat ya nyuma, na kufunga mkanda huku anamtazama kijana huyu, wenye sura ya upole ya kupendeza yenye kushangza na umbo la kusisimua, ambalo kila mwanamke angependa kujilaza kifuani kwake nyakati za usiku, ambae sasa alikuwa anakanyaga crachi na kuingiza gia namba moja, kisha gari linaondoka taratibu kuingia barabarani.
Safari inanza kimya kimya, huku kila mmoja akiwaza la kwake moyoni mwake, “hivi demu mkali kama huyu anawezaje kuwa jambazi, yani amekosa kabisa mwanaume wa kumhudumia au tamaa za kutajirika haraka haraka?” alijiuliza Deus huku akijizuia kumtazama Veronica ambae pia alikuwa anawaza yake , “masikini kijna wa watu mzuriiii lakini jambazi, hivi ukikutana nae mchana akikutongoza si unaweza kusema umepata mwanaume?” alijiuliza Veronica huku akimtazama kijana huyu kwa jicho la wizi.
Naaam kila mmoja akiwa katika mawazo yake, mala ghafla wanasikia ving’ora vya magari ya polisi, wote wanashtuka na kushikwa na wasi wa..….ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums