Simulizi: Nyuma ya mlango wa adui

Simulizi: Nyuma ya mlango wa adui

NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA MIA MOJA NA KUMI NA SABA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
WHATSAPP: 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA MIA MOJA NA KUMI NA SITA:- “hallow!! Vero, upo wapi mwanangu?” ilisikika sauti ya mama Vero toka upande wa pili wa simu ikifuatiwa na saut ya mzee James, “upo salama Vero, hebu tuambie upo wapi tuwalete polisi waje kukuchukua” hapo Veronica alie shindwa kujibu anamtazama Dereva aliekuwa anaendesha gari kimya kimya, “dada mbona huongei jamani, ni kweli upo na Deus Nyati?” hilo lilikuwa swali toka kwa Carloline na ndilo swali lililo mfungua mdomo mwana dada Veronica, “Deus Nyati ndio nani huyo?” aliuliza Veronica kwa sauti iliyojawa na mshangao…..ENDELEA…..

Hapo Deus alishtuka kidogo, sio kwa sababu ya kujulikana kwa Veronica yupo na yeye, hilo alilijua wazi kuwa tayari kuna baadhi ya polisi,l wanafahamu kuwa Veronica yupo ndani ya BMW S7, tatizo ni wamejuaje kuwa dereva wa BMW anaitwa Deus Nyati, simjui huyo Deus Nyati” alisema Veronica, “sasa kama haupo na huyo upo wapi na upo na nani?” aliuliza mzee James, hapo Veronica akamtazama Deus ambae alimuona amekaa kwa utulivu kwenye kiti cha dereva anaendesha gari taratibu kuisogelea nyumba moja ambayo niwazi haikumaliza ujenzi, japo mazingira yake kwa nje ilionyesha wazi kuna mkulima anaishi ndani yake, “kuna kaka mmoja amenisaidia, nachotaka mujue ni kwamba JJ ni jambazi yeye na wenzake waliniteka, akalazimisha niende nikachukue hela benk, halafu alitaka anibake lakini huyu kaka akanisaidia” alisema Veronica kwa sauti yenye deko na lalamiko ndani yake, “tutaongea baadae Vero, kwa sasa tuambie upo wapi na huyo kijana ni nani?” alisema mama Vero na hapo Vero akamtazama tena dereva ambae alikuwa ameelekeza macho mbele kwa utulivu mkubwa, alionyesha wazi kuwa maongezi yale hayakuwa yakimhusu.

Kitu ambacho Veronca hakukijuwa ni kwamba, dereva wake alikuwa anawaza na kuwazua, ambavyo ameweza kubainika kuwa yeye ndie dereva wa BMW s7, japo alipanga kazi hii ilikuwa ya mwisho, yani ya kumchukuwa Veronica benk na kwamba angeachana na biashara hii, lakini sio kwa mtindo huu, “mama nyie tambueni hivyo kuwa nipo salama, mengine tutaongea baadae kwa sasa siwezi kuwaambia kwasababu hamuwezi kuwatumia polisi, baadhi yao wanasaidiana na majambazi, msinipige mpaka niwapigie mimi” alisema Veronica na kukata simu, huku anatazama mbele ambako gari lilikuwa linaingia kwenye kibanda cha gari kwenye ile nyumba isiyo malizika.

Veronica anashangaa wasi wasi unaongezeka, maana niwazi hapa porini kwenye nyumba hii chakavu ndio mwisho wa safari yao, anashindwa kuuliza maana hakuwa na chaguzi, ukichukulia hapa alipo asingeweza kuondoka mwenyewe, maana sio tu kwaajili ya msitu uliopo, ila pia asingeweza kujua aeleeke wapi ili afike nyumbani kwao, na kilicho mtisha zaidi tabia ya upole ya kijana huyu.

Naam wakati anaendelea kujiuliza mara doctor Veronica anashangaa kuona gari linaanza kuzama ardhini taratib mfano wa watu waliopo kwenye lift, lakini kila walipozama ndipo alipoanza kuona mwanga kama vile wanashukia kwenye jengo la kisasa lenye umeme, na hata wanapofika chini anaweza kuona gari dogo aina ya Suzuki la kubebea mzigo likiwa katika maegesho ya kisasa kabisa, “bibie usiku huu utapumzika hapa wakati tunaangalia namna ya kukufika nyumbani kwenu, maana sio wewe wala sio mimi ambae atasalimika endapo tutakutana na wale polisi wanao wasaidia adui zetu” alisema Deus huku anatoa mkanda wa kiti gari likiwa bado lina unguruma.******

Naam! Sasa twendeni dar es salaam airport, ambapo wanaonekana maafisa kadhaa wa jeshi, wamesimama eneo zinaposimama ndege za VIP, mita kadhaa nyuma yao yanaonekana magari manne aina ya Toyota V8 meusi yenye namba za ubalozi wa mbogo land sambamba na magari mengine mawili ya jeshi la ulinzi yanye rangi za kijani na fito nyeupe lenye maandishi mekundu yakiwa katika herufi mbili tu, MP huku askari wacheche ambao ni wazi kabisa kuwa ni polisi wa jeshi, ambao pamoja na wakuu wao walikuwa wanaitazama ndege moja ndogo ya shirika la ndege la nchini #mbogo_land, ambayo hutumiwa na mabalozi wa nchi hiyo waliopo nchi Tanzania, wafanyakazi na familia zao, ikiwa inamesimama sehemu ya VIP upande wa jeshi la ulinzi la Tanzania linalohusika na mambo ya anga, ndege ambayo ndiyo kwanza ilikuwa inazima engine.

Yap! mlango wa ndege unafunguliwa, mlango ambao ndiyo ngazi moja kwa moja ikifuatiwa na kuonekana kwa vijana kumi na sita waliobeba mabegi yao wakishuka toka kwenye ndege hiyo ya kisasa na moja kwa moja kuelekea waliposimama maafisa wa jeshi la ulinzi wanapo wafikia, yule wa mbele ambae ni captain Amos Makey anasalimia kijeshi, ni baada ya kuona kati ya wenyeji wake watatu, ukiachana na mteule daraja la pili na luten, pia palikuwa na major, ambae ni mkubwa kwa cheo ukilinganisha na cheo cha captain cha Amos.

Kwa kifupi ni kwamba, jeshi dunia nzima ni moja, hata kama akiwa ni komandoo wa marekani, mwenye cheo cha private, atapokea amri ya toka kwa koplo wa msumbiji au Tanzania, endapo watakutana katika majukumu ya kijeshi na aendapo atakataa kutekeleza jukumu, basi atashitakiwa kwa sheria za kijeshi, “jambo captain Makey, habari ya #mbogo_land” aliitikia yule Major, ikiwa ni haki yake kabisa kupokea salut hii ya captain wa MLA, “huko tumeacha salama, matatizo ni haya ambayo yametuleta huku na tunajitahidi kuyadhibiti” alisema captain Amos Makey huku wanapeana mikono na wale makamanda wenzao.

Naam baada ya kupokelewa na kusalimiana wakina makey wakaingia kwenye magari aina ya Toyota V8, na safari ikaanza kuelekea kinyerezi, huku mbele ikiongoza land rover 110, la MP na jingine kama hilo likiwa nyuma huku askari wa jeshi hili imara la Tanzania, wakiwa wananing’inia na silaha zao mikononi. ******

Naam! Wakati kikundi cha Amoured Rece Troop, yaani ART, wakiwa wanaingia Tanzania, mfalme Elvis akiwa nyumbani kwake chumbani kitandani na malikia Vaselisa, wanajadiri hili na lile, mara akapigiwa simu toka kwa mkurugenzi wa idara ya habari na mawasiliano ya ikulu ya Golden House, nae akiwa na mke wake wakajua lazima kutakuwa na jambo jipya limetokea, “vipi kuna jambo gani tena?” aliuliza mfalme akisahau hata kutoa salamu ya kifalme, “mtukufu mfalme, kuna habari toka kwenye ile kurasa ya uchochezi na proper ganda iliyotuma habari za James kuwa mfadhiri wa UMD, ni vyema kama ukiiona” alisema msemaji huyo wa ikulu, “hawa watu bwana, wamekuja na jambo gani tena?” aliuliza Elvis huku anainuka toka kitandani na kusogelea sehemu ambayo wanaweka simu, hasa nyakati za usiku, “mtukufu mfalme, kuna habari tatu lakini kiukweli hazina ukweli wowote” alisikika mkurugenzi wa habari, wakati huo king Elvis, alikuwa anachukua simu mezani, huku mke wake akiwa anainuka na kumfuata mume wake.

Naam Vaselisa alimfikia mume wake na kumkuta anabofya simu yake kubwa kuingia kwenye mtandao aliotajiwa, mtandao ambao mara zote umekuwa ukitoa habari sizopendeza za serikali ya #MBOGO_LAND, yani habari zenye kuichafua nchi hiyo, nyingi zikiwa ni uvumi na uongo, “nadhani wanajaribu kuichonganisha serikari na raia” alisikika mkurugenzi wa habari, "vipi mliwahi kuangalia chanzo cha habari hii kinapatikana wapi?" aliuliza king Elvis, huku mke wake akichukua simu toka kwa mfalme huyo kijana na kupekuwa kurasa ambayo mume wake alikusudia kuipekuwa, "mtuku mfalme, hilo tulilifanya siku za nyuma sana, tukagundua kuwa kurasa hii ilisajiliwa na mtu ambae alikuwa tanzania, lakini muhusika aliesajiri kurasa hii licha ya kutumia utambulisho bandia, lakini pia aliwahi kuitumia kurasa hii akiwa sehemu mbali mbali, ikiwa pamoja na hapa nchini, ila mara nyingi tanzania, hata hizi post za leo amezipost akiwa tanzania" alisema kurugenzi na hapo wakaongea mawili matatu kabla ya hawajakata simu na mfalme kuungana na mke wake kusoma zile habari za kuchochezi, huku mara kwa mara akipokea simu toka kwa wasaidizi wake, yani mawaziri na wakurugenzi, pamoja na wazee wa baraza waliokuwa wakimpatia habari za makala ya kichochezi iliyopostiwa usiku huu mtandaoni.**********

Yaap! Veronica anashuka toka kwenye gari na kumfuata mweji wake aliekuwa anatembea, kueleka kwenye mlango uliokuwa mbele yao upande wa kushoto, Veronica alitembea nyuma ya mwenyeji wake huku amekumbatia mkoba wake, begi la fedha wakiwa wameliacha kwenye gari.

Veronica anamuona dereva kijana mwenye sura ya upole akiwa anaufikia mlango na kuufungua, wote wanaingia ndani ambapo wanaibukia ndani ya sebule moja nzuri ya kifahari yenye ukumbi wa chakula na jiko, bar ndogo na kila kinachohitajika, "hoooo! plan nzuri, unaishi na nani hapa?" anauliza Veronica huku anakaa kwenye kochi, wakati mwenyeji wake anasimama mbele ya friji na kukinga maji ya kunywa, "nipo peke yangu, na zaidi yangu hapa tanzania ni wewe tu ndie unae pajua hapa" alisema Deus huku anamaliza kukinga maji na kuyagugumia, kisha anamgeukia mgeni wake na kwa msaada wa mwanga wa taa za pale sebuleni, wote wawili wanapata nafasi ya kutazamana na kuonana vyema, ikiwa ni baada ya kukaa kwenye mwanga hafifu toka wamekutana. …..…. ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
 
Du!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭

Mkuuu tumekusubiri takribani masaa 48.
Jaribu kuiongezea mkuu🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔
 
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA MIA MOJA NA KUMI NA SABA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
WHATSAPP: 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA MIA MOJA NA KUMI NA SITA:- “hallow!! Vero, upo wapi mwanangu?” ilisikika sauti ya mama Vero toka upande wa pili wa simu ikifuatiwa na saut ya mzee James, “upo salama Vero, hebu tuambie upo wapi tuwalete polisi waje kukuchukua” hapo Veronica alie shindwa kujibu anamtazama Dereva aliekuwa anaendesha gari kimya kimya, “dada mbona huongei jamani, ni kweli upo na Deus Nyati?” hilo lilikuwa swali toka kwa Carloline na ndilo swali lililo mfungua mdomo mwana dada Veronica, “Deus Nyati ndio nani huyo?” aliuliza Veronica kwa sauti iliyojawa na mshangao…..ENDELEA…..

Hapo Deus alishtuka kidogo, sio kwa sababu ya kujulikana kwa Veronica yupo na yeye, hilo alilijua wazi kuwa tayari kuna baadhi ya polisi,l wanafahamu kuwa Veronica yupo ndani ya BMW S7, tatizo ni wamejuaje kuwa dereva wa BMW anaitwa Deus Nyati, simjui huyo Deus Nyati” alisema Veronica, “sasa kama haupo na huyo upo wapi na upo na nani?” aliuliza mzee James, hapo Veronica akamtazama Deus ambae alimuona amekaa kwa utulivu kwenye kiti cha dereva anaendesha gari taratibu kuisogelea nyumba moja ambayo niwazi haikumaliza ujenzi, japo mazingira yake kwa nje ilionyesha wazi kuna mkulima anaishi ndani yake, “kuna kaka mmoja amenisaidia, nachotaka mujue ni kwamba JJ ni jambazi yeye na wenzake waliniteka, akalazimisha niende nikachukue hela benk, halafu alitaka anibake lakini huyu kaka akanisaidia” alisema Veronica kwa sauti yenye deko na lalamiko ndani yake, “tutaongea baadae Vero, kwa sasa tuambie upo wapi na huyo kijana ni nani?” alisema mama Vero na hapo Vero akamtazama tena dereva ambae alikuwa ameelekeza macho mbele kwa utulivu mkubwa, alionyesha wazi kuwa maongezi yale hayakuwa yakimhusu.

Kitu ambacho Veronca hakukijuwa ni kwamba, dereva wake alikuwa anawaza na kuwazua, ambavyo ameweza kubainika kuwa yeye ndie dereva wa BMW s7, japo alipanga kazi hii ilikuwa ya mwisho, yani ya kumchukuwa Veronica benk na kwamba angeachana na biashara hii, lakini sio kwa mtindo huu, “mama nyie tambueni hivyo kuwa nipo salama, mengine tutaongea baadae kwa sasa siwezi kuwaambia kwasababu hamuwezi kuwatumia polisi, baadhi yao wanasaidiana na majambazi, msinipige mpaka niwapigie mimi” alisema Veronica na kukata simu, huku anatazama mbele ambako gari lilikuwa linaingia kwenye kibanda cha gari kwenye ile nyumba isiyo malizika.

Veronica anashangaa wasi wasi unaongezeka, maana niwazi hapa porini kwenye nyumba hii chakavu ndio mwisho wa safari yao, anashindwa kuuliza maana hakuwa na chaguzi, ukichukulia hapa alipo asingeweza kuondoka mwenyewe, maana sio tu kwaajili ya msitu uliopo, ila pia asingeweza kujua aeleeke wapi ili afike nyumbani kwao, na kilicho mtisha zaidi tabia ya upole ya kijana huyu.

Naam wakati anaendelea kujiuliza mara doctor Veronica anashangaa kuona gari linaanza kuzama ardhini taratib mfano wa watu waliopo kwenye lift, lakini kila walipozama ndipo alipoanza kuona mwanga kama vile wanashukia kwenye jengo la kisasa lenye umeme, na hata wanapofika chini anaweza kuona gari dogo aina ya Suzuki la kubebea mzigo likiwa katika maegesho ya kisasa kabisa, “bibie usiku huu utapumzika hapa wakati tunaangalia namna ya kukufika nyumbani kwenu, maana sio wewe wala sio mimi ambae atasalimika endapo tutakutana na wale polisi wanao wasaidia adui zetu” alisema Deus huku anatoa mkanda wa kiti gari likiwa bado lina unguruma.******

Naam! Sasa twendeni dar es salaam airport, ambapo wanaonekana maafisa kadhaa wa jeshi, wamesimama eneo zinaposimama ndege za VIP, mita kadhaa nyuma yao yanaonekana magari manne aina ya Toyota V8 meusi yenye namba za ubalozi wa mbogo land sambamba na magari mengine mawili ya jeshi la ulinzi yanye rangi za kijani na fito nyeupe lenye maandishi mekundu yakiwa katika herufi mbili tu, MP huku askari wacheche ambao ni wazi kabisa kuwa ni polisi wa jeshi, ambao pamoja na wakuu wao walikuwa wanaitazama ndege moja ndogo ya shirika la ndege la nchini #mbogo_land, ambayo hutumiwa na mabalozi wa nchi hiyo waliopo nchi Tanzania, wafanyakazi na familia zao, ikiwa inamesimama sehemu ya VIP upande wa jeshi la ulinzi la Tanzania linalohusika na mambo ya anga, ndege ambayo ndiyo kwanza ilikuwa inazima engine.

Yap! mlango wa ndege unafunguliwa, mlango ambao ndiyo ngazi moja kwa moja ikifuatiwa na kuonekana kwa vijana kumi na sita waliobeba mabegi yao wakishuka toka kwenye ndege hiyo ya kisasa na moja kwa moja kuelekea waliposimama maafisa wa jeshi la ulinzi wanapo wafikia, yule wa mbele ambae ni captain Amos Makey anasalimia kijeshi, ni baada ya kuona kati ya wenyeji wake watatu, ukiachana na mteule daraja la pili na luten, pia palikuwa na major, ambae ni mkubwa kwa cheo ukilinganisha na cheo cha captain cha Amos.

Kwa kifupi ni kwamba, jeshi dunia nzima ni moja, hata kama akiwa ni komandoo wa marekani, mwenye cheo cha private, atapokea amri ya toka kwa koplo wa msumbiji au Tanzania, endapo watakutana katika majukumu ya kijeshi na aendapo atakataa kutekeleza jukumu, basi atashitakiwa kwa sheria za kijeshi, “jambo captain Makey, habari ya #mbogo_land” aliitikia yule Major, ikiwa ni haki yake kabisa kupokea salut hii ya captain wa MLA, “huko tumeacha salama, matatizo ni haya ambayo yametuleta huku na tunajitahidi kuyadhibiti” alisema captain Amos Makey huku wanapeana mikono na wale makamanda wenzao.

Naam baada ya kupokelewa na kusalimiana wakina makey wakaingia kwenye magari aina ya Toyota V8, na safari ikaanza kuelekea kinyerezi, huku mbele ikiongoza land rover 110, la MP na jingine kama hilo likiwa nyuma huku askari wa jeshi hili imara la Tanzania, wakiwa wananing’inia na silaha zao mikononi. ******

Naam! Wakati kikundi cha Amoured Rece Troop, yaani ART, wakiwa wanaingia Tanzania, mfalme Elvis akiwa nyumbani kwake chumbani kitandani na malikia Vaselisa, wanajadiri hili na lile, mara akapigiwa simu toka kwa mkurugenzi wa idara ya habari na mawasiliano ya ikulu ya Golden House, nae akiwa na mke wake wakajua lazima kutakuwa na jambo jipya limetokea, “vipi kuna jambo gani tena?” aliuliza mfalme akisahau hata kutoa salamu ya kifalme, “mtukufu mfalme, kuna habari toka kwenye ile kurasa ya uchochezi na proper ganda iliyotuma habari za James kuwa mfadhiri wa UMD, ni vyema kama ukiiona” alisema msemaji huyo wa ikulu, “hawa watu bwana, wamekuja na jambo gani tena?” aliuliza Elvis huku anainuka toka kitandani na kusogelea sehemu ambayo wanaweka simu, hasa nyakati za usiku, “mtukufu mfalme, kuna habari tatu lakini kiukweli hazina ukweli wowote” alisikika mkurugenzi wa habari, wakati huo king Elvis, alikuwa anachukua simu mezani, huku mke wake akiwa anainuka na kumfuata mume wake.

Naam Vaselisa alimfikia mume wake na kumkuta anabofya simu yake kubwa kuingia kwenye mtandao aliotajiwa, mtandao ambao mara zote umekuwa ukitoa habari sizopendeza za serikali ya #MBOGO_LAND, yani habari zenye kuichafua nchi hiyo, nyingi zikiwa ni uvumi na uongo, “nadhani wanajaribu kuichonganisha serikari na raia” alisikika mkurugenzi wa habari, "vipi mliwahi kuangalia chanzo cha habari hii kinapatikana wapi?" aliuliza king Elvis, huku mke wake akichukua simu toka kwa mfalme huyo kijana na kupekuwa kurasa ambayo mume wake alikusudia kuipekuwa, "mtuku mfalme, hilo tulilifanya siku za nyuma sana, tukagundua kuwa kurasa hii ilisajiliwa na mtu ambae alikuwa tanzania, lakini muhusika aliesajiri kurasa hii licha ya kutumia utambulisho bandia, lakini pia aliwahi kuitumia kurasa hii akiwa sehemu mbali mbali, ikiwa pamoja na hapa nchini, ila mara nyingi tanzania, hata hizi post za leo amezipost akiwa tanzania" alisema kurugenzi na hapo wakaongea mawili matatu kabla ya hawajakata simu na mfalme kuungana na mke wake kusoma zile habari za kuchochezi, huku mara kwa mara akipokea simu toka kwa wasaidizi wake, yani mawaziri na wakurugenzi, pamoja na wazee wa baraza waliokuwa wakimpatia habari za makala ya kichochezi iliyopostiwa usiku huu mtandaoni.**********

Yaap! Veronica anashuka toka kwenye gari na kumfuata mweji wake aliekuwa anatembea, kueleka kwenye mlango uliokuwa mbele yao upande wa kushoto, Veronica alitembea nyuma ya mwenyeji wake huku amekumbatia mkoba wake, begi la fedha wakiwa wameliacha kwenye gari.

Veronica anamuona dereva kijana mwenye sura ya upole akiwa anaufikia mlango na kuufungua, wote wanaingia ndani ambapo wanaibukia ndani ya sebule moja nzuri ya kifahari yenye ukumbi wa chakula na jiko, bar ndogo na kila kinachohitajika, "hoooo! plan nzuri, unaishi na nani hapa?" anauliza Veronica huku anakaa kwenye kochi, wakati mwenyeji wake anasimama mbele ya friji na kukinga maji ya kunywa, "nipo peke yangu, na zaidi yangu hapa tanzania ni wewe tu ndie unae pajua hapa" alisema Deus huku anamaliza kukinga maji na kuyagugumia, kisha anamgeukia mgeni wake na kwa msaada wa mwanga wa taa za pale sebuleni, wote wawili wanapata nafasi ya kutazamana na kuonana vyema, ikiwa ni baada ya kukaa kwenye mwanga hafifu toka wamekutana. …..…. ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
🤔🤔😭🤔🤔🤔😭😭😭😭🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔🤔😭😭😭🤔😭🤔🤔🤔🤔 Abuou shaymaaaaaaaa
Jaribu kulitafakhari ombi la wadauuuuuuúuu.
 
Yaan mkuu hicho kipande cha deus na dokta malizia kabisa maana hiyo arosto ni mbaya bora shada.
 
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA MIA MOJA NA KUMI NA NANE
MTUNZI: Mbogo EDGAR
WHATSAPP: 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA MIA MOJA NA KUMI NA SABA:- Veronica anamuona dereva kijana mwenye sura ya upole akiwa anaufikia mlango na kuufungua, wote wanaingia ndani ambapo wanaibukia ndani ya sebule moja nzuri ya kifahari yenye ukumbi wa chakura na jiko, bar ndogo na kila kinachohitajika, "hoooo! plan nzuri, unaishi na nani hapa?" anauliza Veronica huku anakaa kwenye kochi, wakati mwenyeji wake anasimama mbele ya friji na kukinga maji ya kunywa, "nipo peke yangu, na zaiidi yangu hapa tanzania ni wewe tu ndie unae pajua hapa" alisema Deus, huku anamaliza kukinga maji na kuyagugumia, kisha ana mgeukia mgeni wake na kwa msaada wa mwanga wa taa za pale sebuleni wote wawili wanapata nafasi ya kutazamana na kuonana vyema, ikiwa ni baada ya kukaa kwenye mwanga hafifu toka wamekutana. …..…. ENDELEA…


Kila mmoja anatuliza macho kwa mwenzie, ni kama walishangaana, kila mmoja alishangaa uzuri wa mwenzie nakuonekana kuvutiwa na muonekano wa mwenzi, maana ukiachilia Deus ambae ni lazima angemshangaa na kuvutika kwa uzuri wa mwanadada Veronica, ambae kiukweli ni zaidi ya waschana wote aliowahi kuwa nao karibu, hata doctor Neela asingeweza kumfikia mwanadada huyo mzuri na mrembo, ila kwa upande wa Veronica ambae licha ya kumuona kijana huyu aliechafuka damu mikononi na kwenye nguo zake, hakutegemea kuona sura nzuri kama hii ikiwa kwa kijana muuwaji kama huyu, japo uuwaji wake ni wenye kutetea wanyonge.


Sekunde arobaini ndio muda ambao, walitumia kutazamana, kabla hawaja tabasamuliana na kukwepesha macho yao, "hongera sana nyumba nzuri" alisema Veronica wakiendelea kutabasamuliana, "kawaida tu" alisema Deus kwa sauti yake ya upole huku anatoa simu yaketoka mfukoni na kuanza kuandika ujumbe, huku anatembea kuelekea upande wa chumbani, akimuacha Veronica anatoa simu yake na kubofya simu yake, ambapo alikutana na jumbe nyingi sana zilizo tumwa kwake ziimtakia pole kwakile kinachoendelea mitandaoni kwake na kwa baba yake.


Veronica kwa kuzingatia ushauri wa dereva, ana acha kujibu jumbe zile, lakini kabla haja weka simu pembeni, ujumbe ukaingia kwenye simu yake, alipotazama jina la mtumaji wa ujumbe huo, akajikuta anatabasamu, "mwanaume una roho ngumu wewe, yaani muda wote huu hata kunitafuta kujua ninashida gani" alijisemea Veronica huku anabofya kufungua ujumbe ule uliotumwa na mtu mwenye jina la Mchoraji, kisha anatupa macho ujumbe wa wa kwanza, "sorry pacha, nilikuwa na mambo mengi sana usiku wa leo" ndivyo ulivyo someka ujumbe huo, ambao kiukweli ulimsisimua Veronica na kujikuta akifurahi moyoni mwake na kumuona mchoraji wake ni mtu wa pekee kwake, japo hakuwahi kumuona uso kwa uso.


Lakini kabla haja jibu ujumbe ule wa mchoraji wake, kijana mjasiriamali mara ujumbe mwingine unaingia, nao unatoka kwa kijana huyo huyo mchoraji wake, anaufungua haraka japo wakati anaanza kuusoma anaona ujumbe mwingine unaingia toka kwa huyo huyo mchoraji, "najua una hamu ya kunipa taarifa ya kilichotokea huko kwa mpenzi wako, wacha nioge halafu unieleze upuuzi wako" ndivyo ulivyosema ujumbe, ukiungwa na ule wa mwisho, "lakini usinifiche alichokufanyia" Veronica alijikuta anacheka mwenyewe, "kumbuka usimueleze mtu juu ya huku uliko, ni kwaajili ya usalama wako" Veronica alishtuliwa na sauti ya dereva, akainua uso wake haraka na kumtazama dereva, anamuona akiwa ameshika nguo mkononi mwake, hakujua ni nguo za aina gani, ila alihisi kuwa ni suruali ya truck suit na tishert jeupe, "nachati na rafiki yangu, tena nadhani hajui lolote juu ya kilichotokea" alisema Veronica huku anamtazama kijana yule, ambae alikuwa anamsogelea pale alipokuwepo, "utabadili nguo hizi hapa, chumba kile pale kuna bafu na choo, ukiwa tayari karibu kwa chakula" alisema dereva kwa sauti yake ile ile ya upole, huku Veronica akamtazama usoni na kushindwa kulinganisha kuwa kama kweli huyu kijana mbele yake ndie yule ambae alikuwa anatoboa vichwa vya watu kwa risasi kule makabe, anamuona kijana huyu anageuka na kuelekea chumbani kwake.


Veronica alimsindikiza kwa macho mpaka alipopotelea chumbani kwake huku akishangazwa na ukarimu wa kijana huyu mwenye moyo wa upendo na matendo magumu kwa adui zake, alipomuona ameingia chumbani na kufunga mlango akaweka sawa simu yake kuandika ujumbe kwenda kwa mchoraji wake, "poa wacha na mimi nioge, halafu nitakushtua, maana ndio naingia home mida hii" kisha akatuma na yeye akainuka toka kwenye kochi, nakuchukua simu mkoba na zile nguo kisha akatembea kuelekea kwenye kile chumba alicho elekezwa na dereva wake, yani kijana mwenye sura ya upole.*******


Naam bwana Frank ambae sasa alikuwa ameshapata habari nzima na kwamba tayari kijana wake ameingia kwenye kisa ambacho kilianzia miaka mingi iliyopita, ni baada ya kumtoa bwana James mikononi mwa UMD pasipo yeye kujua kuwa analiokoa taifa kutoka katika uasi mkubwa wa UMD, kwahiyo mzee Frank akaona kuna kila sababu ya kumtahadharisha kijana wake kuwa makini na UMD ambao ni wajanja sana.


Pia mzee Frank ambae mida hii alikuwa juu kitanda anaperuzi mtandao kuona kilichokuwa kinaendelea juu ya matukio yaliyoanza kutokea usiku wa leo hii, huku akisikiliza mikoromo mwepesi wa mke wake, "hawa jamaa wajinga sana, yani wananchi wameshaingia kwenye mtego wa UMD" alijisemea Frank, baada ya kuona ile makala kwenye mtandao ambayo ilikuwa inasema wanachi kuandamana kwa kupinga uongozi wa kifalme, uongozi ambao utendaji wake umekuwa ukitamaniwa na wananchi wa nchi nyingi duniani, maana mahitaji muhimu yote walikuwa wanapata bure, "lazima hawa watu wametumia watu fulani kushawishi wananchi" alijisemea mzee Frank ambae kiukweli alisha toa onyo kwa mfalme wa zamani wa mbogo land, lakini mfalme hakusikia na baada yake yeye anaishi uhamishoni kama mkimbizi, isitoshe alijua wazi kuwa asingeweza kueleweka pale ambapo angeamua kueleza anacho kishuku juu ya Chitopela, ambae sasa ni waziri, kwamba anahusika na UMD, maana mara ya mwisho alimuona akiwa na Kadumya usiku ule alipokuwa amevamiwa na MLA.


Mwisho mzee huyu akaona itakuwa vyema kama atampigia kijana wake na kumueleza hali halisi na ujio wa MLA nchini tanzania, na sasa wapo njiani wanaenda dar es salaam kwaajili ya kumlinda mzee James, ambae yeye ametoka kumuokoa muda mfupi uliopita, mzee Frank anapiga simu na kuiweka sikioni, nayo inaanza kuita mara moja, nae anainuka toka kitandani na kuelekea sebuleni.


Bahati nzuri kwake bwana Frank, simu inapokelewa na kijana wake, "baba hujalala mpaka saa hizi?" anauliza Deus kwa sauti ile ile ya upole, lakini inaonyesha kushangaa, "nitalala vipi wakati najua upo kwenye mkasa mzito, na kitu ambacho unatakiwa ukijue ni kwamba, huo mkasa unanihusu moja kwa moja" alisema mzee Frank kwa sauti ndogo ya chini, "inakuhusu kivipi, kwasababu walimteka mzee James na wewe unadhani watakuteka" aliuliza Deus huku anacheka kidogo, inamshangaza mzee Frank kwamba kijana wake mpaka sasa hajajua yupo katika hatari kiasi gani, lakini kabla hajauliza au kuongea chochote, akasikia Deus akiongea upuuzi wake, "wenzio wamemfwata mzee James kwasababu ana fedha nyingi maana kuna wengine pia walimteka mtoto wake na wakamtumia kuiba fedha benk, bahati yake nilimtoa pale" alisema Deus na kumshangaza kidogo mzee Frank, "eti, mtoto wa James nae alitekwa, nao wanajua kuwa wewe ndie uliemuokoa?" aliuliza mzee Frank kwa sauti yenye mshangao, "bado hawajua, na bado hajafika kwao, natafuta njia sahihi ya kumpeleka kwa wazazi wake pamoja na hizi fedha ambazo baba yake atazipeleka sehemu husika, kwasababu sasa hivi watu hawaaminiki, kuna polisi wametushambulia tukiwa njiani" alisema Deus, na hapo baba yake akaanza kumpa kisa kamili na jinsi ulivyokuwa mpango wa UMD, kuomba ufadhili wa bwana James, ili waweze kuingiza silaha nchini mbogo land.


Pia mzee Frank akaeleza kuhusu ujio wa ART, kikundi toka MLA, na kwamba kwasasa, kikundi hicho cha watu 16, kipo safarini Dar es salaam, kwaajili ya kutoa ulinzi kwa bwana James na familia yake, "kwahiyo hayo yote ni mpango wa muda mrefu ambao ulipangwa na hawa UMD, ilikufanikisha mapinduzi yao haramu" alisema mzee Frank, ambae alikuwa sebuleni peke yake. ******


Yap! nyumbani kwa mzee James, mambo yalikuwa tofauti kidogo, licha ya kusikia kuwa binti yao alikuwa saama kabisa na akiwasisitiza kuwa alisha toka mikononi mwa UMD, kitu ambacho hata wao waliona wazi kuwa binti yao anaongea akiwa katika hali ya kawaida, huku akisisitiza kuwa ameokolewa na kijana mmoja, ambae sio Deus kama walivyofikiria, na kilicho wachanganya zaidi ni kitendo cha kwamba, kijana walie mtambua kuwa ni mpenzi wa binti yao, ndie alieongoza utekwaji wa binti yao Veronica, "kwahiyo JJ alikuwa ni jambazi pia?" aliuliza Carlolina kwa sauti ya mshangao huku anatazama picha ya kwenye simu yake, "inashangaza kwa kweli, ndio maana yule kijana alikuwa haeleweki, yani hakuna cha ndugu wala rafiki wa karibu" alisema mama Veronica, huku na yeye anachungulia kwenye simu ya binti yake na kuiona picha ya kijana John Joseph Daud, ambae alitambuliwa kama mkwe wa familia hii ya mfanya biashara tajiri afrika, "kitu ambacho inabidi tufahamu ni kwamba, UMD ni wajanja sana, na walianza kutufuatilia muda mrefu na kupanga mipango yao ya kuniingiza kwenye mtego, hata uchumba wa Veronica huyo mshenzi, nao ulikuwa ni mtego pia" alisema mzee James., muda huo huo mlango ukafunguliwa, wote wanatazama upande wa mlango, wanamuona yule luteni wa jeshi la ulinzi, ambae ni mkuu wa ulinzi wa nyumba ya bwana James, ambae aliingia ndani na kusimama pembeni ya mlango.


Naam wanamuona yule luten akipiga saluti ikifuatia na kuingia kwa afisa wa jeshi mwenye cheo cha major, akifuatia na askari wawili wenye vyeo tofauti, afisa mwenye cheo cha luten na mwingine askari mwenye cheo cha afisa mteule daraja la pili, ambae nyuma yake waliifuatia vijana kumi na sita waliovalia nguo za kiraia.


Familia wakiwa wanawatazama wageni wao, ndipo yule askari mwenye cho cha major akasalimia, "habari za jioni hii bwana James" alisaimia major, "nzuri afande karibu sana" aliitikia bwana James, japo kwa asilimia kubwa, macho yake yalikuwa upande waliosimama wale wageni waliovalia kiraia na kubeba mabegi makubwa, "asante bwana James, pasipokupoteza muda, tumewafikisha wageni wako hapa, nashani tayari unayo taarifa ya ujio wao, hawa ART askari toka #mbogo_land, ambao wapo hapa kukupa ulinzi na kukuongoza kufika mbogo land ukaonane na mfalme" alisema yule Major na hapo familia nzima ikawageukia wageni na kuwatazama wale wageni.


Naam wale wageni wakainamisha vichwa vyao na kusalimia, "salaam bwana James na familia yako" walisalimia wote kwa pamoja, na bwana James na mke wake nao wakainamisha vichwa na kusalimia, huku binti yao ambae hakuwa anafahamu ile salam akiwaigiza wazazi wake kusalimia kwa mtindo ule, "salaam watumishi toka mbogo land" alieitikia alikuwa ni mzee James peke yake.


Baada ya salam wale wengine wakaondoka na kuwaacha askari kumi na tano na kiongozi wao , ambae ni luten Amos Makey, nao wakamueleza James majukumu ya kikundi chake ya kumlinda na kumpeleka nchini kwao, na pia mzee James akasimulia kile ambacho kimemtokea na pia kutekwa kwa binti yake, japo kwa sasa binti yake anasema yupo salama ila hawezikujitokeza, kwasababu mpaka sasa ni hatari kwake, kusogea mitaa ya nyumbani kwao maana wametoka kushambuliwa na polisi ambao sio waaminifu, wanaoshirikiana na UMD, "lakini siwezi kuondoka tanzania pasipo kumpata binti yangu" alisema mzee James, ambae pia alieleza juu ya muhusika mwingine aliejifanya mchumba wa binti yao, huku akiwaonyesha picha ya kijana John Joseph Daud, "huyu anaitwa luten Enoc Kafulu, ambae ameacha jeshi mwaka mmoja uliopita" alieleza luten Amos, ambae anamfahamu Kafulu, kwasababu ni askari walioingia jeshi pamoja.


Baada ya majadiliano na maoongezi yaliyodumu kwa dakika kumi, makamanda hawa wanatoa tamko la makubaliano, "imekubaliwa, tutakuwa na wewe mpaka Veronica apatikane, kisha tutaondoka kuelekea nchini kama alivyoagiza mfalme" alisema Amos, kabla hajaomba sehemu ya kubadiri nguo wajiweke tayari kwa kazi, na pia yeye kupata nafasi ya kutoa taarifa kwa luten general Sixmund kumueleza kuwa wamefika salama na pia kumueleza uwepo wa luten mtoro MLA kafulu.********


Naam mambo yalizidi kupamba moto ndani ya usiku huu, polisi waliendelea kusambaa mtaani wakimsaka dereva wa BMW jeusi ambae sasa inasemekana ndie aliemteka mwanadada Veronica, wakishirikiana na askari wa marine specia force waliohitaji kumfikisha Deus Nyati makao makuu ya jeshi.


Lakini wakati polisi, TSA na MFS, wakiwa hawana uhakika wa kupata japo lepe moja tu la usingizi usiku wa leo, wakati huo mschana Veronica doctor wa hospital ya mkoa wa pwani, alikuwa bafuni anamalizia kuoga huku kichwani mwake akiwa anawaza juu ya mambo yaliyotokea, Veronica anajifuta maji mwilini, huku anavuta picha ya kwamb endapo angebakwa na JJ, na kuondoa uschana wake ingekuwaje, ni machungu kiasi gani angekuwa nayo, lakini katikati ya mawazo hayo, inaibuka sura ya kijana huyu mpole, mwenye sura na sauti ya upole, ambae alimuokoa toka kwa mbakaji huyo, aliechukulia kama mwanaume sahihi kwake, "ila ni mzuri sijui anakaa hapa na mke wake?" alijuliza Veronica huku anachagua baadhi mafuta kwenye mkoba wake, maana alibeba kwaajili ya kuyatumia, akioga baada ya kumaliza kufanya kile ambacho walikuwa wamepanga kukifanya kile walicho taka kukifanya na JJ.


Veronica akiwa kama alivyozaliwa, anajipaka mafuta taraibu huku anaukagua mwili wake, ambao ni mtetemo wa mioyo ya wanaume huko mtaani, lakini kiukweli alishangaa kuona kijana huyu kama vile hakuwa muumini wa jambo hilo, pangine anatamani kimoyo moyo" alijisemea Veronica, huku ana chukua nguo ya ndani kwenye mkoba wake na kuivaa, halafu anatazama nguo zilizokuwa kitandani, ni zile ambazo alikuwa amepewa na dereva, "mh! leo navaa nguo za mwanaume" alijisemea Veronica huku anajichekesha na kuchukua ile ya chini anaivaa, kisha anajitazama imekaa kweli kweli, kama sio kuvutika kama mpira, tungesema imem'bana, ni kutokana na udogo wake, lakini sasa iliweza kuonyesha vyema umbo la mwana dada huyu, ambae hata yeye alijikuta anajisemea peke yake, "mh! sijui kama hatotoa mate kwa matamanio, maana sio kwa muonekano huu" alijisemea Veronica huku anachukua tishet jeupe juu ya kitanda na kulivaa.


Hiyo ilikuwa ni hatari zaidi, maana kikawaida ni kwamba, Deus hupenda tishet zinazo mkaa mwilini, yani za kubana, hivyo basi, hata hii aliyopewa Veronica ilikuwa ni tishert iliyomkaa kisawa sawa na kusababisha kila kitu kujichora juu ya tishert lile, achana na chuchu juu ya kichuguu cha mazwa yake, sasa basi hata vile vijipele vilivyozunguka chuchu za mwana dada huyu zilionekana wazi wazi, "shauri zake itabidi avumilie tu, maana yeye mwenyewe ndie kanipa nguo hizi" alijisemea Veronica huku anachukua simu yake na kufungua upande wa kuandika ujumbe wa whatsapp, kisha anaanza kuandika ujumbe kwenda kwa mchoraji, "vipi mchoraji wangu umesha maliza kuoga?" aliuliza Veronica na kutuma ujumbe ule kwenda kwa mchoraji na ujumbe ukajiweka alama mbili nyeusi kwamba umepokelewa lakini haujasomwa, "anaoga muda mrefu sana, lakini sawa kutembea kutwa nzima kwenye jua na mizigo sio mchezo" alijisemea Veronica huku anatazama kitanda kidogo kilicho kuwa mbele yake, kimetandikwa vizuri, lakini hakukuwa na dalili ya kwamba kuna mtu alikuwa anakitumia kwa sasa.... ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI
Hapa Hapa JamiiForums Twende Pamoja Mdau Usisahau Kuacha Commeti Na Like Kama Sapoti Yako.


NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA MIA MOJA NA KUMI NA TISA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
WHATSAPP: 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA MIA MOJA NA KUMI NA NANE:- alijisemea Veronica, huku anachukua simu yake na kufungua upande wa kuandika ujumbe wa whatsapp, kisha anaanza kuandika ujumbe kwenda kwa mchoraji, "vipi mchoraji wangu, umesha maliza kuoga?" aliuliza Veronica na kutuma ujumbe ule, kwenda kwa mchoraji na ujumbe ukajiweka alama mbili nyeusi kwamba umepokelewa lakini haujasomwa, "anaoga muda mrefu sana, lakini sawa kutembea kutwa nzima kwenye jua na mizigo sio mchezo" alijisemea Veronica huku anatazama kitanda kidogo kilicho kuwa mbele yake kimetandikwa vizuri, lakini hakukuwa na dalili ya kwamba kuna mtu alikuwa anakitumia kwasasa. ENDELEA…


Veronica ana achana na kitanda kisha anatembea taratibu akiufuata mlango, kisha anaufungua, na hapo anakutana na harufu nzuri ya chakula, "kwahiyo baba, kumbe huo ni mpango wa muda mrefu?" Veronica alimsikia dereva akiongea kwa sauti yenye mshangao, Veronica akatazama upande wa meza ya chakula iliyo unganishwa na jiko la kisasa, akamuona dereva akiwa amesimama mbele ya meza yenye majiko kadhaa ya aina tofauti, akiwa anaendelea na mapishi huku simu ameibana kwa bega lake la kushoto, lakini Veronica hakusikia sauti ya upande wa pili, lakini akamsikia dereva akiongea tena, "naamini kila kitu kinaenda kuisha, basi wacha mimi nipumzike ila kama kuna lolote nijulishe" alisema Dereva, kisha akakata simu na kuangalia.


Veronica akamsogelea kwa lengo la kumsaidia kuandaa chakula, lakini hilo sio lengo kusudiwa, lengo halisi lilikuwa ni kujaribu kuzoeana na kijana huyu, ikiwezekana aonyeshe urafikinna yeye kujihakikishia usalama wake, "unapika chakula kinanukia vizuri, kaka yangu we ni hatari kwenye mapishi" alisema Veronica huku anamtazama dereva, aliekuwa ameelekeza mawazo yake kwenye simu, niwazi alikuwa anasoma ujumbe fulani, " akaonekana kama vile kuna ujumbe anausoma na kuujibu, "Veronica ambae alikuwa anaufuatilia uso wa kijana huyu, kwamba aliona dalili ya tabasamu wakati anajibu ujumbe kwenye simu yake, nae akatabasamu, huku anasogelea meza ya jiko, "ni mapishi ya kawaida tu, ni vyema ukachukua kinywaji na kutulia mezani katika siku yako ya kwanza hapa nyumbani kwangu" alisema Deus, huku anaweka simu mfukoni.


Kabla Veronica hajasema chochote mara akahisi ujumbe umeingia kwenye simu yake, hivyo akatoa simu yake huku anatembea kufuata sehemu ya vinywaji, wakati huo anatazama ujumbe kwenye simu, "nipo tayari kusikia story" ndivyo ulivyosema ujumbe toka kwa mchoraji, ambae kumbu kumbu pekee kwa Veronica ni vile alivyo muambia kuwa, kitu wanachoenda kufanya hakiwezekani, na niwazi kuwa huko wanakoenda lazima kuna kitu kitokee.


Veronica hakujibu chochote, zaidi anapiga hatua kadhaa kuelekea kwenye kabati la vinywaji, kuna kitu anahisi, hapo anageuka nyuma haraka, anakutana uso kwa macho na Deus, aliekuwa anamtazama, wote wanatabasamuliana kwa macho ya aibu, kisha wanakwepesha macho yao, "pole kaka yangu, naomba mungu akupe uvumilivu" Veronica anajisemea moyoni huku anafika kwenye kabati la vinywaji na kuchagua aina ya kinywaji anachoweza kutumia akaona ni vyema kama atapata juice ya matunda, ambayo aliichukua pamoja na grass, kisha akaelekea mezani na kukaa kwenye kochi, kisha akaanza kujibu ujumbe, mambo sio mazuri mchoraji wangu, kweli wewe uliniambia ukweli" kisha akatuma kwenda kwa mchoraji wake, wakati huo tayari Deus alikuwa anaweka vyakula kwenye sahani na kuzipeleka mezani, huku mara moja moja akitazama simu yake na kujibu ujumbe, "pole sana, vipi alipitiliza au ulishtuka" ulisema ujumbe, kwenye simu ya Veronica toka kwa mchoraji na kabla hajajibu ukaingia mwingine, "lakini najuwa huwezi kuniambia, na usikute bado upo nae hapo" ujumbe huo ulimfanya Veronica ajihisi kidogo.


Veronica akamtazama Dereva, ambae sasa alikuwa anakaa kwenye kochi amesha maliza kuandaa chakula, nakumfanya Veronica aweze kuona sahani kadhaa zenye vyakula vya aina mbali mbali vya kupendeza na kuleta hamu ya kula, pia tayari dereva alikuwa na chupa ya wine nyekundu na grass yake, karibu chakula" alisema Deus, huku ana fungua wine na kumimina kwenye grass yake na mara kwa mara akitazama simu yake, "Asante sana, tena nilikuwa njaa" alisema Veronica huku anachukua uma na kuchapua mnofu wa samaki alielala kwenye sahani, kisha anaiweka mdomoni na kumtafuna kidogo, "hongera kaka Dereva chakula ni kitamu" alisema Veronica huku anamazaliza kuandika ujumbe kwenye simu yake, "hakuna lolote, kumbe mtu mwenyewe ni mshenzi tu" kisha akautuma kwenda kwa mchoraji wake, na hapo hapo akaanza kuandika ujymbe mwingine, wakati huo anamuona dereva akiwa anachukua simu yake mezani, ni wazi kuna ujumbe uliingia, maana alimuona anausoma, yeye hakujali akaendelea kuandika ujumbe wake wa pili, "karibu tule" ndivyo ulivyosema ujumbe wa Veronica kwenda kwa mchoraji.


Veronica anapoutuma ujumbe ule nachukua uma, na kudunga kiazi mviringo cha kuchemsha, na kuweka mdomoni, huku anamtazama dereva wake ambae alikuwa anamaliza kusoma ujumbe kwenye simu yake na kuandika mwingine, huku muda wote anatabasamu na kufanya uso wa kijana huyu uzidi kuonekana vizuri zaidi kiasi Veronica akajikuta anatabasamu.


Ni kama dereva alijishtukia kitu fulani, maana baada ya kumaliza kutuma ujumbe aliinua uso wake na kumtazama mgeni wake ambae alijitambulisha mwenyewe kwa jina la doctor Veronica, akamuona anamtazama kwa macho ya tabasamu, "samahani dada yangu, kuna mtu nawasiliana nae hapa" alisema dereva, huku anaweka simu mezani na kuanza kula, "nimeona, inaonekana ni rafiki yako mkubwa sana" alisema Veronica huku na yeye anachukua simu yake na kusoma ujumbe uliokuwa umeingia, ulikuwa unatoka kwa mchoraji, akaufungua na kuusoma, "hooo kumbe hata mimi nipo mezani napata chakula, kweli wewe ni pacha wangu" ndivyo ulivyo sema ujumbe huo, Veronica anatabasamu kidogo, huku anainua uso kumtazama dereva ambae bado alikuwa hajampatia jibu la mtu anae chati nae, nikama deus aligundua hilo, "yah! sio rafiki mkubwa, ila naweza kusema ni wapekee" alijibu Deus kwa sauti iliyobeba hisia toka moyoni.


Veronica anajikuta anasisimkwa kwa hisia alizo onyesha dereva na kushindwa kuamini kama mtu kama huyu anaweza kuwa na hisia kiasi hiki, "ni wifi yangu au?" aliuliza Veronica huku anaandika ujumbe kwenda kwa mchoraji, "unakula nini?" alipomaliza akautuma, wakati huo dereva alikuwa anamjibu swali lake, "hapana sio mpenzi wangu, ila ametokea kuwa rafiki yangu mkubwa sana" alijibu deus huku anachukua simu yake ambayo ilikuwa imeingia ujumbe, ulikuwa unatoka kwa pacha, akaufungua na kuusoma, kisha akajibu na kutuma kwenda kwa pacha wake.


Veronica anauona ujumbe unaingia kwenye simu yake, "mh! wanaume ndio mlivyo, usikute umesha mkana mpenzi wako kwa kuona mrembo yupo mbele yako" hivyo Veronica alijisema moyoni, huku anausoma ujumbe kwenye simu yake, "ni kawaida tu, samaki viazi na vitu vidogo vidogo" ndivyo ulivyosema ujumbe huo, ambao unamshtua Veronica, na kumfanya ainue uso wake kumtazama Deus, ambae ndio kwanza alikuwa anabugia chakula chake huku anashushia wine, "mbona kama kila kitu kina fanana" anajiuliza Veronica, huku anakumbuka mwanzo, wakati dereva anaenda kuoga, mchoraji akasema na yeye anaenda kuoga, hata sasa mambo mengi yanaonekana kufanana, pia kila yeye akituma ujumbe dereva nae anapokea ujumbe.


Lakini Veronica anaachana na dereva na kuandika ujumbe, "mh! kweli leo tume kuwa mapacha, kwani wewe amekupikia nani?" aliandika Veronica ikiwa ni swali la mwisho ambalo lingempa mwanga wa kugundua kuwa dereva ndie mchoraji, alipomaliza kuandika, akaituma na kuendelea kula huku anashusha maswali kwa mwenyeji wake, "kwanini huyoo mtu amekuwa rafiki yako wa pekee?" aliuliza Veonica huku anainamia chakula chake.


Naam ile Veronica anainua uso, anamuona kijana huyu anachukua simu mezani, ikionyesha kuwa ilikuwa imeingia ujumbe, "kwasababu ndie rafiki yangu peke yake, sina rafiki mwingine, na yeye yupo mbali kidogo" alijibu dereva huku anasoma ujumbe na kuujibu, kisha anautuma na kuweka simu mezani, "hooo, kwahiyo kaka hauna mke hauna rafiki hauna mtoto?" aliuliza Veronica, huku akimtazama Deus kwa macho ya mashaka, sio mashaka juu ya upweke wake, ila ni kuhisi kuwa pengine yeye ndie anae mtumia ujumbe.


Lakini hakuwa na uwezo wa kumuuliza, hivyo akatulia kimya kusubiri ujumbe uingie athibitishe mashaka yake, "ni sawa na wewe tu, haukuwa na mpenzi zaidi ya tapeli ambae alitaka kukutumia tu, hauna mume wala mtoto, pengine umenizidi marafiki" alisema dereva kwa sauti tulivu, ambayo safari hii haikuwa na utani, Veronica anakili moyoni mwake kuwa maneno ya dereva ni ya ukweli, anajikuta anatabasamu peke yake, huku anafungua ujumbe ulioingia kwenye simu yake, "nipo kwa mama ntilie nakula, namatumaini kama ungekuwepo ungenipikia" ndivyo ulivyosema ujumbe ule, nae akajikuta amepata jibu ambalo lilimthibitishia kuwa alichodhania kilikuwa tofauti.


Veronica anapata wazo la kumaliza kuchati na mchoraji ili waweze kuongea na kijana huyu, wakati huu wanakula ili ajue kesho mwisho wake ni nini, hivyo akamtazama Deus akamuona na yeye anamtazama usawa wa kifua, nadhani kaka aliona vile vichuchu, Veronica anatabasamu kwa aibu huku anaweka mkono kifuani kuzuia chuchu zake zisiendelee kuwa burudani machoni pa dereva, hata dereva nae alijihisi aibu kiasi fulani, "sorry macho yamekosea" alisema Deus na wote wakatabasamu.


Kimya kikatawala, kila mmoja akiwaza la kwake, kabla Veronica hajaamua kuwakilisha ombi lake, "samahani kaka, naweza kupiga simu moja tu kwa rafiki yangu" aliuliza Veronica huku ana anajaribu kumtazama Deus, lakini anashindwa, "nani huyo ni huyo uliekuwa unachati nae?" alizungumza Deus pasipo kumtazama Veronica, "ndiyo nataka kuagana nae" alisema Veronica, huku anachukua simu yake toka mezani, "mh! unawezaje kuagana na mtu ambae upo nae, au nimekosea kwamba Unataka kumpgia mchoraji?" aliuliza Deus na kumfanya Veronica atoe macho ya mshangao kwa kuthibitisha kuwa huyu mbele yake ndie mchoraji aliekuwa anachati nae wakati wote, ni rafiki yake wa muda mrefu ambae ambae hawakuwahi kuonana toka wamekuwa marafiki, "mchoraji umenijuaje" aliuliza Veronica huku anamtazama Deus kwa macho ya mshangao, wakati huo deusi alikuwa anaendelea kula bila kumtazama Veronica..... ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao Kujia hapa hapa JamiiForums
 
Nimejikuta nafurahi mwenyewe, story imekaa kimtego saana, nimejikuta nimeshakuwa mhusika yaani mjeda wa UMD. Tehtehteh🤣🤣🤣😅😅😅😂🤣😅😅😅. Hongera saaana mtunzi. 👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍
 
UMD tupo siriaz, ishu ni mkubwa Chitopela namuonaga ni kama vile Hana akili nzuri🥰🥰🥰
 
Back
Top Bottom