Just Nana
JF-Expert Member
- Jul 27, 2023
- 500
- 1,038
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA SABA:
Mheshimiwa waziri katika serikali inayomaliza muda wake, mgombea katika nafasi ya uraisi ambae amekatwa jina lake dakika za mwisho kabisa alikua mzee wa totoz kwelikweli, tulimfuatilia na kufahamu ratiba zake kadhaa, lakini jamaa alikua kama ana kismart hivi maana tulikua tunapishana nae sana. Kupitia Inno tukafanikiwa kufahamu weakness ya jamaa, jamaa alikua ana mahusiano ya kudumu na mwanadada mrembo sana wa kuitwa Kidawa, Kidawa alikua Kidawa kweli kweli, slay queen wa kwenda.
Niliona si haba kama nitaanza na Kidawa na kupitia yeye atatupatia mheshimiwa. Shetani akawa upande wetu maana Kidawa alikua mjamzito na alikua na clinic yake maalumu pale aghakhan hospitali, ana shida gani Kidawa wa watu, acha afaidi pesa ya mheshimiwa. Niliegesha gari pembeni ya gari ya kidawa , nikasubiri kwa masaa kadhaa ili amalizane na daktari wake , baada ya muda nikamuona Kidawa akitoka ndani ya jengo la hospitali akiwa anajizoazoa, ujauzito ulimpendeza Kidawa, macho yalipata tulizo kwa picha nzuri niliyokua naitazama.
Kwa mwendo wa kivivu alifungua mlango wa gari lake na kuliondoa maeneo ya maegesho. Sikua na papara, nilijua tu kwa mda ule zaidi ya kupitia sehemu akapate chakula, hakuna mahala pengine ataelekea, lazma atahitaji mapumziko, nilichohitaji ni dakika chache za maongezi nae, na niliona si vyema kuongea na mjamzito akiwa na njaa , acha apate msosi kwanza. Nilimfata kwa tahadhari, Kama nilivyowaza ndivyo ilivyokua, Kidawa alipitia mgahawani kupata chakula, nilimsubiri hadi alipomaliza na safari yetu ya kurudi nyumbani ilianza.
Kwa tahadhari ileile niliendelea kumfuatilia hadi katika makazi yake upanga . Ile nyumba ilikua ni mfano wa nyumba ya kisasa, ilikua na kila kitu kinachohitajika kuwepo katika nyumba, kwa muonekano ule ulinipa taswira ya kua nipo sehemu sahihi kwani mheshimiwa alimpa thamani Kidawa kiasi cha kumpa maisha ya gharama namna ile. Nilisubiri geti lifunguliwe na nihakiki kua pale ndipo anapoishi mrembo yule wa mheshimiwa kisha nikapotea maeneo yale.
Nilihitaji kufahamu vitu vichache vya Kidawa, hakuna mrembo asie na siri, na sikuchelewa sana kuipata, jioni ya ile siku nikiwa katika ziara zangu zisizo rasmi niliona gari aina ya crown ya kijivu ilitoka ndani ya nyumba ya mheshimiwa, ndani ya gari alikuwepo Kidawa na kijana wa makamo mwenye muonekano wa kijana wa kisasa. Sikuchelewa nikaamua kuwaungia tela, msafara wetu uliishia club moja maarufu sana kwa kipindi kile.
Haikuhitaji kua na elimu ya shahada kujua kua ile mikao ya mama kijacho na kijana wa kisasa ilikua ni ya kimapenzi, niliwaacha wafurahie usiku wao, mimi ni nani wa kuzuia watu kufurahia maisha yao, nikajipa mahangaiko kidogo ya nafsi kutaka kujua ule mzigo wa mama kijacho utakua wa muheshimiwa kweli au wa kijana wa kisasa, nilijicheka mwenyewe, tangu lini nimeanza biashara ya udaku jamani.
Saa sita usiku ulinikuta katika sebule maridhawa ya bibie Kidawa, kijana wa kisasa waliachana na Kidawa pale club baada ya kumkodia usafiri wa kumfikisha nyumbani, na yeye akapotelea gizani, sikutaka kuhangaika nae, niliyemuhitaji ni Kidawa, hakukua na mlinzi kwa usiku ule, nadhani Kidawa hakutaka mashahidi kwa yale anayoyafanya na hivyo alilazimika kumpumzisha mlinzi, kwa tahadhari nikiwa nimeegesha gari yangu mita chache toka makazi ya kidawa , nilijongea geti la mrembo yule, kwa kutumia zana zangu maalum nilifanikiwa kufungua geti na kuingia hadi ndani.
Nilimkuta mrembo akiwa kajilaza kihasara pale sebuleni, chupa kadhaa za pombe zikiwa sakafuni kudhihirisha kua palikua na hekaheka si kitoto, nilikionea huruma kitoto kilichopo tumboni mwa mwanamke yule mrembo asiyejielewa. Nikachukua maji kwenye jokofu na kumuamsha mrembo wa mheshimiwa, Kidawa alikurupuka akawa anataka kukimbia, nikamuamuru atulie na akae chini.
Nilimueleza juu ya niliyoyashuhudia, nikamwambia kua kama anahitaji taarifa zake za ufuska na ulevi zisimfikie mheshimiwa aanze kuropoka anayoyajua kuhusu mheshimiwa. Nilihitaji kufahamu makazi ya kudumu ya mheshimiwa kwa pale dar, shule wanazosoma wanae, marafiki zake ni kina nani, mali anazomiliki kama anafahamu na aina ya magari anatumia.
Ndani ya dakika chache nikawa nimepata taarifa nyingi kuliko nilivyowaza na zaidi ya kua mheshimiwa amedhamiria kuingia Ikulu kwa heri au kwa shari, kwahiyo atahakikisha anagombea kupitia upinzani na ameshaanza kufanya taratibu za kuhama chama , ilikua imebaki siku ya kutangazwa rasmi .
Hio ilikua taarifa muhimu sana, ama kweli tulicheza karata muhimu sana, mheshimiwa anamthamini na kumuamini kimada kiasi cha kumuelezea mipango yake ya kisiasa. Kwa mwendo wa tahadhari niliiacha nyumba ya kimada wa mheshimiwa na kutokomea kusikojulikana.
Mheshimiwa waziri katika serikali inayomaliza muda wake, mgombea katika nafasi ya uraisi ambae amekatwa jina lake dakika za mwisho kabisa alikua mzee wa totoz kwelikweli, tulimfuatilia na kufahamu ratiba zake kadhaa, lakini jamaa alikua kama ana kismart hivi maana tulikua tunapishana nae sana. Kupitia Inno tukafanikiwa kufahamu weakness ya jamaa, jamaa alikua ana mahusiano ya kudumu na mwanadada mrembo sana wa kuitwa Kidawa, Kidawa alikua Kidawa kweli kweli, slay queen wa kwenda.
Niliona si haba kama nitaanza na Kidawa na kupitia yeye atatupatia mheshimiwa. Shetani akawa upande wetu maana Kidawa alikua mjamzito na alikua na clinic yake maalumu pale aghakhan hospitali, ana shida gani Kidawa wa watu, acha afaidi pesa ya mheshimiwa. Niliegesha gari pembeni ya gari ya kidawa , nikasubiri kwa masaa kadhaa ili amalizane na daktari wake , baada ya muda nikamuona Kidawa akitoka ndani ya jengo la hospitali akiwa anajizoazoa, ujauzito ulimpendeza Kidawa, macho yalipata tulizo kwa picha nzuri niliyokua naitazama.
Kwa mwendo wa kivivu alifungua mlango wa gari lake na kuliondoa maeneo ya maegesho. Sikua na papara, nilijua tu kwa mda ule zaidi ya kupitia sehemu akapate chakula, hakuna mahala pengine ataelekea, lazma atahitaji mapumziko, nilichohitaji ni dakika chache za maongezi nae, na niliona si vyema kuongea na mjamzito akiwa na njaa , acha apate msosi kwanza. Nilimfata kwa tahadhari, Kama nilivyowaza ndivyo ilivyokua, Kidawa alipitia mgahawani kupata chakula, nilimsubiri hadi alipomaliza na safari yetu ya kurudi nyumbani ilianza.
Kwa tahadhari ileile niliendelea kumfuatilia hadi katika makazi yake upanga . Ile nyumba ilikua ni mfano wa nyumba ya kisasa, ilikua na kila kitu kinachohitajika kuwepo katika nyumba, kwa muonekano ule ulinipa taswira ya kua nipo sehemu sahihi kwani mheshimiwa alimpa thamani Kidawa kiasi cha kumpa maisha ya gharama namna ile. Nilisubiri geti lifunguliwe na nihakiki kua pale ndipo anapoishi mrembo yule wa mheshimiwa kisha nikapotea maeneo yale.
Nilihitaji kufahamu vitu vichache vya Kidawa, hakuna mrembo asie na siri, na sikuchelewa sana kuipata, jioni ya ile siku nikiwa katika ziara zangu zisizo rasmi niliona gari aina ya crown ya kijivu ilitoka ndani ya nyumba ya mheshimiwa, ndani ya gari alikuwepo Kidawa na kijana wa makamo mwenye muonekano wa kijana wa kisasa. Sikuchelewa nikaamua kuwaungia tela, msafara wetu uliishia club moja maarufu sana kwa kipindi kile.
Haikuhitaji kua na elimu ya shahada kujua kua ile mikao ya mama kijacho na kijana wa kisasa ilikua ni ya kimapenzi, niliwaacha wafurahie usiku wao, mimi ni nani wa kuzuia watu kufurahia maisha yao, nikajipa mahangaiko kidogo ya nafsi kutaka kujua ule mzigo wa mama kijacho utakua wa muheshimiwa kweli au wa kijana wa kisasa, nilijicheka mwenyewe, tangu lini nimeanza biashara ya udaku jamani.
Saa sita usiku ulinikuta katika sebule maridhawa ya bibie Kidawa, kijana wa kisasa waliachana na Kidawa pale club baada ya kumkodia usafiri wa kumfikisha nyumbani, na yeye akapotelea gizani, sikutaka kuhangaika nae, niliyemuhitaji ni Kidawa, hakukua na mlinzi kwa usiku ule, nadhani Kidawa hakutaka mashahidi kwa yale anayoyafanya na hivyo alilazimika kumpumzisha mlinzi, kwa tahadhari nikiwa nimeegesha gari yangu mita chache toka makazi ya kidawa , nilijongea geti la mrembo yule, kwa kutumia zana zangu maalum nilifanikiwa kufungua geti na kuingia hadi ndani.
Nilimkuta mrembo akiwa kajilaza kihasara pale sebuleni, chupa kadhaa za pombe zikiwa sakafuni kudhihirisha kua palikua na hekaheka si kitoto, nilikionea huruma kitoto kilichopo tumboni mwa mwanamke yule mrembo asiyejielewa. Nikachukua maji kwenye jokofu na kumuamsha mrembo wa mheshimiwa, Kidawa alikurupuka akawa anataka kukimbia, nikamuamuru atulie na akae chini.
Nilimueleza juu ya niliyoyashuhudia, nikamwambia kua kama anahitaji taarifa zake za ufuska na ulevi zisimfikie mheshimiwa aanze kuropoka anayoyajua kuhusu mheshimiwa. Nilihitaji kufahamu makazi ya kudumu ya mheshimiwa kwa pale dar, shule wanazosoma wanae, marafiki zake ni kina nani, mali anazomiliki kama anafahamu na aina ya magari anatumia.
Ndani ya dakika chache nikawa nimepata taarifa nyingi kuliko nilivyowaza na zaidi ya kua mheshimiwa amedhamiria kuingia Ikulu kwa heri au kwa shari, kwahiyo atahakikisha anagombea kupitia upinzani na ameshaanza kufanya taratibu za kuhama chama , ilikua imebaki siku ya kutangazwa rasmi .
Hio ilikua taarifa muhimu sana, ama kweli tulicheza karata muhimu sana, mheshimiwa anamthamini na kumuamini kimada kiasi cha kumuelezea mipango yake ya kisiasa. Kwa mwendo wa tahadhari niliiacha nyumba ya kimada wa mheshimiwa na kutokomea kusikojulikana.