SIMULIZI: "The Godfather"

SEHEMU YA KUMI NA TATU:

Tuliingia jijini salama, general aliamuru Tolu ahakikishe kua Inno na 'package' wanafika salama Arusha, sikua na shaka na utendaji wa Tolu. Tulifanya utaratibu wa kuondoka dar kwa kutumia usafiri binafsi, ilitafutwa gari maalumu ya kubeba mizigo iliyokua na uwazi wa kutosha kulala mtu mzima katikati ya bodi ya nyuma na sehemu ya dereva ambayo huwezi kuiona kwa jicho la kawaida. Nyuma ya bodi ilipakiwa shehena ya magodoro, mzigo ulijaa ukashona, jamaa tulimuwekea mtungi wa hewa kwa ajili ya kupumua, ngoma ikalala hadi Arusha.

Nilijipa mapumziko ya siku mbili kabla ya kurudi rasmi kibaruani kwangu kwa mheshimiwa. Nilikua natoka matembezi ya hapa na pale, kwa mbali nikaona kuna pikipiki inanifungia mkia, sikua na hakika sana ikanibidi kufanya kitu. Nilikua kwenye foleni nikitokea kurasini kuelekea Mbezi, wakati nakaribia mataa ya Tazara nikafanya jaribio la pata potea, nilisubiri taa zikaruhusu nikakunja kulia kama naelekea mjini, nikaona jamaa wa pikipiki akijihakiniza kukunja kona kunifuata pia, nadhani alijua nitaendelea kutumia Mandera road. Nikanyoosha mbele kidogo na kuingia kulia nikaweka kambi zilipokuwepo ofisi za NHIF zamani.

Jamaa hakua smart, alinifata na kunipita na kwenda kuweka kambi kwa mbele, hadi hapo nikajua tu jamaa ananifatilia. Nilishuka kwenye gari na kuingia ndani ya zile ofisi za bima, ikawa bahati kwangu nikakuta watu kadhaa wapo kwenye utaratibu wa kupewa huduma, nikapoa kwa muda kwenye benchi nikisubiri kuona jamaa atafanya nini.

Baada ya kama dakika kumi nikaona Ile pikipiki inajongea mahala nimeegesha gari yangu kwa tahadhari , na kwa haraka akainama na kuweka kifaa na kupotea kwa kasi. Sikua na shaka ya kua atakua ametumwa kuniwekea kifaa cha kufuatilia mienendo yangu, ila nikajipa angalizo . Niliita bodaboda na kupotea mahala pale, nilipiga simu garage maarufu iliyopo Tabata na kuwaomba wakanichukulie gari langu kwa ajili ya marekebisho madogomadogo ili nimudu kulitumia safarini.

Nilisubiri hadi usiku wa saa nane na kuamua kua utakua muda muafaka wa kulifata gari langu, napenda utulivu na pia ulikua mda sahihi kuhangaishana na wanaotaka kuhangaika nami maana hapana foleni na pia itaepusha kudhuru raia wema wasio na hatia. Ile garage ilikua na mlinzi mzee sana, kwa mda nimefika alikua amelala hana habari, nikaona nisimsumbue bali nimuongezee masaa ya kulala kwa kumpulizia dawa ya usingizi, wazee sio watu wakusumbuliwa jamani, na kwanini wanaajiri walinzi wazee kulinda mali za mamilioni, sijawahi kufahamu.

Niliingia na kukagua kile kifaa kama bado kipo, nikakuta bado kipo na kinafanya kazi, gari yangu haikua imefanyiwa chochote hadi muda huo, nikaitoa na kuongoza uelekeo wa Kawe beach. Nikiwa maeneo ya Mwananchi nikaona kuna gari inakuja uelekeo wangu kwa kasi, nikanyoosha hadi Ubungo mataa jamaa bado wapo na mimi, nikaingia kulia kuitafuta Mwenge jamaa bado wanakomaa ,nikasema kumekucha....

Magari yalikua machache sana barabarani hivyo kufanya utulivu kiasi na kuonana kwa umakini, walijua kufata mchoro wangu na waliingia bila hodi, ilikua ni suala la muda kuawaambia karibu. Maeneo ya beach yalikua tulivu sana kwa muda huo wa saa nane, niliegesha gari yangu gizani mahala ambapo haliwezi kuonekana kwa urahisi sikuhitaji usumbufu na walinzi.

Jamaa waliweka kambi umbali wa kilometa moja toka nilipokuwepo, kwa tahadhari nikashuka na kurudishia mlango wa gari, nikajificha chini ya gari na kutulia. Dakika chache nikaona kivuli kikijongea mahala nilipokuwepo, kikifuatiwa na kingine, kwa msaada wa mbalamwezi nilihesabu vile vivuli na kuona idadi ya watu wanne. Niliwasubiri hadi wasogee karibu, mmoja wao akafungua mlango wa gari upande wa dereva, najua alihamaki kuona patupu, kabla hajafungua mdomo nilimvuta uvunguni , pigo moja la nguvu lilitosha kumnyamazisha.

Mwenzie alikuja kwa kunyata huku akiita jina la yule aliyetangulia, hakujua kua mwenzake alikua anawasaidia malaika kuchochea kuni ahera, maana kwa hizi mishe zetu pepo tutaisikia tu. Alikaribia gari lakini katika kusita , sikumchelewesha nikamchana na kisu mshipa unaounganisha unyayo na mguu, alipiga yowe na kuanguka kama zigo, nikamshindilia bisu la shingo na kumuacha akitapatapa na roho yake.

Waliobaki wakawa katika kuhaha, nilichomoka uvunguni mwa gari kwa kasi ya umeme, nikamuotea mmoja wa wale mabwana kwa risasi ya kifua, yowe ya uchungu lilimtoka, aliyebaki alijaribu kutimua mbio, sikumpa nafasi ya kupiga hatua, nilimuwahi na ngumi mbili matata zilizomfanya atepete , nikawasachi na zaidi ya simu na bunduki nne hawakua na chochote. Sikua na muda wa maziko maana kwa ile milio ya risasi nilijua itakua imewashtua walinzi, acha polisi wetu wapate cha kuwaweka bize kwa siku mbili tatu, niijua hawawezi pata chochote maana bunduki niliyotumia ilikua ya magendo,nikambeba majeruhi wangu na kupotea eneo hilo baada ya kuing'oa kile kifaa na kukiweka kwenye mfuko wa suruali wa mmoja wa zile maiti.

Nilimfikisha mgeni wangu Mbezi na kumfungia chumba maalumu, zile simu nilizizima kwa hofu ya kama zitakua zinasoma location. Nilirudisha gari na kumkuta babu yangu mlinzi akiendelea kukoroma, nilihakiki kama patakua na chochote cha kutia shaka kwenye gari nikaona amani asilimia mia. Nilimpulizia dawa nyingine babu ya kumuwezesha kupata ahueni ya usingizi baada ya lisaa lizima ambayo itamfanya akiamka zaidi ya kuhisi uchovu hakuna tofauti yoyote ataiona mwilini mwake. Nilipotea maeneo ya garage Kama sijawahi kuwepo, kwa usafiri wa pikipiki niliyoisimamisha njiani nilimudu kufika kwangu Mbezi mapema kabla hapajakucha.
 
SEHEMU YA KUMI NA NNE:

Sikua na papara na mgeni wangu, nilimuacha apate usingizi wa kutosha, nilifanya majukumu yangu ya asubuhi ikiwemo mazoezi, usafi binafsi na wa nyumba . Majira ya saa mbili kamili nikaingia chumba nilichomuhifadhi jamaa. Alikua kaamka anahangaika kujitoa kwenye kiti nilichomfunga, nikamwambia usijihangaishe ndugu, 'save your energy , you might need it'.

Jamaa aliniangalia kwa hofu, nadhani ile picha ya ufukweni bado alikua nayo kichwani, alikua anawaza nitakachomfanya au sijui alimkumbuka mwanamke wake kua hatomuona tena, mi hayanihusu hayo. Niliandaa zana zangu za kazi , na vifaa vya kumfanyia bianadamu usafi wa mwili. Nilimuinua jamaa na kiti chake akawa anaangalia dari, nilichukua kitambaa na kumfunika mdomo,nilichukua mafuta ya petrol kwenye dumu la lita tano na kumshindilia mdomoni.

Jamaa alitoa macho kama anakata roho, nilimpa dakika tatu za kuvuta hewa, kisha nikarudia zoezi kwa dakika moja na zaidi. Nilipomuachia na kuonesha dalili ya kutaka kurudia kwa mara ya tatu jamaa huku akipambana kupumua kwa kasi na akiwa ametoa jicho hadi sentimeta ya mwisho akanionesha ishara ya mkono kua niache kumtesa. Mimi ni nani nisiwe msikivu kwa kiumbe wa Mungu, nikavuta kiti nikamwambia tuanze maongezi yetu.

Nilimwambia jamaa sidhani kama itafaa kujitambulisha, hadi mnanifuatilia nadhani mnanifahamu, ila ingekua vyema kama ungejitambulisha. Akanambia kua wametumwa na bwana Juma ,mlinzi binafsi wa mgombea wa Uraisi, wametumwa kuniteka ili niwaambie wapi nilipokua wiki nzima. Nilijikuta nimecheka kwanza, niliona jicho la husda la bwana Juma tangu siku ya kwanza naenda kuongea na mheshimiwa hotelini, nilikua na mtafutano wa nafsi wa kufahamu iwapo bwana yule ananichunguza kwa matakwa yake binafsi au ya bosi wake?

Nilimwambia anieleze waliyoyafahamu kuhusu mimi hadi wakati huo, nilikua nimeshachunguza zile simu na kuzikagua kama zitakua na kifaa chochote cha kufuatilia mahala tulipo,sikuona chochote, baada ya kuona hazina madhara, niliziacha wazi ili nione kama naweza kung'amua chochote, hadi muda huo hakuna simu iliyoita katika zile simu, nikagundua kua zile zilikua simu maalumu kwa ajili ya ile kazi tu, jamaa alijipanga kupambana na mimi, ni vile tu hakua smart since day one.

Kupitia mateka wangu niligundua kua hawakua wamefika mbali katika upelelezi wao, na hata ile kuniotea mara ya kwanza ni kwa sababu jamaa anajua aina ya gari natumia na kwa kushirikiana na askari wa barabarani aliweza kuninasa kwenye rada zake. Kwa hilo nilimpongeza, ila nadhani angeokoa maisha ya vijana wake kama angetumia askari haohao wa barabarani kuniweka kizuizini na kunipata kirahisi, maana katika vitu nilikua najiepusha ni kuichokonoa serikali waziwazi. Ndio maana nachelea kusema jamaa hakua smart kabisa.

Niliwasiliana na jamaa yangu wa garage na kumwambia kua nahitaji kubadilisha rangi ya gari yangu. Jamaa hakua mtu wa maswali, niliifata gari jioni ya siku hiyo, nilikua na plate number za aina tatu tofauti pale nyumbani, nikabandika mojawapo na kuipa gari yangu muonekano mpya. Nilishaona nuksi za ile gari na hivyo nikaona ni wakati muafaka wa kuiiuza na kutafuta gari nyingine. Kwa msaada wa jamaa yangu wa garage niliuza ile gari na kununua gari nyingine aina ya Noah, niliona itanifaa kwa mishemishe zangu.

Akuanze mmalize, nilimalizana na mateka wangu na kwenda kumtupa bonde la mto msimbazi. Jioni yake ilinikuta Hongera bar, bar moja maarufu kwa kipindi kile pale Sinza. Kwa kiasi nilikua nimeifahamu ratiba ya mgombea uraisi ,alikua ni mtu wa ibada sana, siku ya ijumaa huitumia kwa ibada na kukutana na viongozi wa kidini pamoja na familia. Kwa vyovyote vile bwana Juma atakua anajipongeza kwa ratiba ngumu ya wiki nzima. Ijumaa ilikua mapumziko ya bwana Jumaa, ingawa alikua kijana wa kiislamu lakini kwake ijumaa ilitumika kufanya ufuska wa kutosha na kuwatambishia watu jinsi alivyotakata na kufahamiana na wakuu wa nchi.

Dada poa wa Sinza walijua kuitafuna pesa ya bwana Jumaa, nami niliona sio vibaya kuanzia hapo . Niliegesha gari katika garage bubu upande wa pili wa barabara , magari yalitapika utadhani sikukuu, watu walijazana kutumia pesa zao. Nilipata meza sehemu iliyojificha ambayo naweza kumuona kila anayeingia na kutoka na kumuomba muhudumu aniletee kinywaji, nilikipiga taratibu huku nikisindikizwa na mziki wa bolingo wakati huohuo nikitazama uumbaji wa Mungu, maana walipita kila aina ya warembo, kila mmoja akijaribu kunasa mawindo nami nilikua mawindoni.

Haikupita kitambo kabla sijamuona mtarajiwa wangu, alikua amezungukwa na warembo watatu, walikua wamelewa haina mfano. Niliwaacha wamelewa kwa kiasi cha kutojielewa, ilipofika saa nane usiku bwana Jumaa na warembo wake walinyanyuka kwa ajili ya kwenda kupumzika. Mtaa wa nyuma na pale bar palikua na gest bubu , nilimshangaa yule bwana kwa kuyaweka maisha yake rehani kwa kulala katika kagesti uchwara kama kile. Niliwaacha wakachukua chumba, nami nikachukua chumba kinachofuatia.

Ulevi haujawahi kumuacha mtu salama, yule bwana na wale dada poa watatu walichokumbuka ni kuingia chumbani , kurudishia mlango na kujitupa kitandani, hata mlango hawakukumbuka kufunga. Nilielewa sasa kwanini dada poa walimpenda bwana Jumaa, sasa mtu anakunywesha pombe za bure na michemsho ya kutosha na unalala mahala walau pana pangaboi na kunguni wa kuhesabu wasiokera, na hakuna anachokufanya hadi asubuhi, unaachaje kumshobokea jamani.

Niliingia mle chumbani na kumkokota bwana Juma hadi chumbani kwangu, sikutaka kuwasumbua dada zetu, majukumu yao mazito jamani. Nilimfunga bwana Juma kwenye kakiti cha mbao kalikokua mle chumbani, nilimsaidia kumvua viatu na soksi, nilimvua tisheti alilovaa na kumshindilia mdomoni, nilichukua plaizi na kuanza kung'oa kucha yake ya dolegumba , jamaa aliruka kama kang'atwa na siafu, na kutua chini kama furushi na kujikuta amevunja hadi kiti cha watu, bwana Jumaa muharibifu sana, si angeruka taratibu tuuu, ona kamtia hasara mwenye gesti sasa. Nikamsalimu yule bwana, 'Asalaam Aleykuuum bwana Jumaaa'
 
Hatari.

Sent from my SM-A115F using JamiiForums mobile app
 
Come on come NANA , STORI TAMU SANA GO ON GO ON
 
Nitaandika, sijapata utulivu, halafu sijawahi katisha story labda sio mfuatiliaji wa story zangu....tutamalizia siku si mingi, mepita tu kuwasalimu
 
Maua Yako nana yaan nasoma najiona mm ndio godfather kumbe pisi Kali tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…