Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 60
alikuwa ameandaliwa chakula cha usiku na mheshimiwa rais kama heshima ya kukitangaza chama kile kwa nguvu zote. Moyo wake ulikuwa katika presha kubwa, ni kweli kwamba alikuwa akifanya mawasiliano na rais mara kwa mara lakini siku hiyo kwake ilionekana kuwa siku tofauti na nyingine.
Kwanza kuitwa ndani ya Ikulu huku akiwa pamoja na mumewe, George kulionekana kumfurahisha kupita kiasi. Muda wote macho yake yalikuwa yakiangalia saa kubwa ya ukutani, kwake, aliuona mshale wa dakika ukienda taratibu sana tofauti na siku nyingine. Alitamani asimame na kuifuata saa ile na kisha kuusogeza mshale wa saa na kisha kuona dunia nzima ikienda kama vile ambavyo alikuwa akitaka iwe.
Kila alipokuwa akiyaandaa mafaili yakea alikuwa akimuita sekretari wake ambaye alikuwa akiyaweka katika sehemu ambayo yalikuwa yakitakiwa kuwa. Muda ulizidi kwenda mbele mpaka kufikia muda ambao alitakiwa kutoka ndani ya ofisi yake. Akayakusanya mafaili yote ambayo yalitakiwa kuandikwa mambo fulani katika kipindi ambacho angekuwa nyumbani na kisha kumpa sekretari wake.
Sekretari akayachukua na kisha kupewa ufunguo wa gari ambapo akaanza kuondoka kuelekea katika sehemu ambayo ilikuwa na gari la kifahari lililokuwa na rangi nyeusi, Range na kisha kuufungua mlango.
Annastazia bado alikuwa ofisini huku akiendelea kukusanya vitu vingine. Mara sauti kubwa ya mlipuko ikasikika, Annasatazia akashtuka kupita kawaida kiasi ambacho alitamani kutoka nje ya ofisi ile na kukimbia. Kutokana na presha kubwa aliyokuwa nayo, akajikuta akiingia chini ya meza na kujilaza chini.
Katika maisha yake yote, hakuwahi kuusikia mlio wowote wa mlipuko kiasi ambacho alipousikia mlipuko ule alijikuta akitetemeka kwa hofu kubwa. Moshi mwingi ukaanza kuonekana nje ya ofisi ile kwa dirishani huku sauti za wakinamama zikisikika.
Annastazia hakutoka, aliendelea kubaki ndani ya ofisi ile tena chini ya meza kwa muda wa dakika thelathini na ndipo hapo alipotoka nje ya ofisi ile. Watu walikuwa wamejazana katika korido huku wakiongea yao, Annastazia alipotokea, wote wakayaamishia macho kwake na kuanza kumwangalia.
Annastazia hakuyaelewa macho ya watu wale yalikuwa yakimaanisha nini mbele yake, alitamani kuuliza lakini akajikuta akikaa kimya. Bado moyoni mwake hakuwa akijisikia amani kabisa, alikuwa akipiiga hatua za haraka haraka kuelekea kule ambapo kulikuwa na gari lake.
Watu walikuwa wamejazana kule P2 ambapo alikuwa amelipaki gari lake. Kwanza hakuelewa sababu iliyowafanya watu wale wajazane namna ile,
alikuwa ameandaliwa chakula cha usiku na mheshimiwa rais kama heshima ya kukitangaza chama kile kwa nguvu zote. Moyo wake ulikuwa katika presha kubwa, ni kweli kwamba alikuwa akifanya mawasiliano na rais mara kwa mara lakini siku hiyo kwake ilionekana kuwa siku tofauti na nyingine.
Kwanza kuitwa ndani ya Ikulu huku akiwa pamoja na mumewe, George kulionekana kumfurahisha kupita kiasi. Muda wote macho yake yalikuwa yakiangalia saa kubwa ya ukutani, kwake, aliuona mshale wa dakika ukienda taratibu sana tofauti na siku nyingine. Alitamani asimame na kuifuata saa ile na kisha kuusogeza mshale wa saa na kisha kuona dunia nzima ikienda kama vile ambavyo alikuwa akitaka iwe.
Kila alipokuwa akiyaandaa mafaili yakea alikuwa akimuita sekretari wake ambaye alikuwa akiyaweka katika sehemu ambayo yalikuwa yakitakiwa kuwa. Muda ulizidi kwenda mbele mpaka kufikia muda ambao alitakiwa kutoka ndani ya ofisi yake. Akayakusanya mafaili yote ambayo yalitakiwa kuandikwa mambo fulani katika kipindi ambacho angekuwa nyumbani na kisha kumpa sekretari wake.
Sekretari akayachukua na kisha kupewa ufunguo wa gari ambapo akaanza kuondoka kuelekea katika sehemu ambayo ilikuwa na gari la kifahari lililokuwa na rangi nyeusi, Range na kisha kuufungua mlango.
Annastazia bado alikuwa ofisini huku akiendelea kukusanya vitu vingine. Mara sauti kubwa ya mlipuko ikasikika, Annasatazia akashtuka kupita kawaida kiasi ambacho alitamani kutoka nje ya ofisi ile na kukimbia. Kutokana na presha kubwa aliyokuwa nayo, akajikuta akiingia chini ya meza na kujilaza chini.
Katika maisha yake yote, hakuwahi kuusikia mlio wowote wa mlipuko kiasi ambacho alipousikia mlipuko ule alijikuta akitetemeka kwa hofu kubwa. Moshi mwingi ukaanza kuonekana nje ya ofisi ile kwa dirishani huku sauti za wakinamama zikisikika.
Annastazia hakutoka, aliendelea kubaki ndani ya ofisi ile tena chini ya meza kwa muda wa dakika thelathini na ndipo hapo alipotoka nje ya ofisi ile. Watu walikuwa wamejazana katika korido huku wakiongea yao, Annastazia alipotokea, wote wakayaamishia macho kwake na kuanza kumwangalia.
Annastazia hakuyaelewa macho ya watu wale yalikuwa yakimaanisha nini mbele yake, alitamani kuuliza lakini akajikuta akikaa kimya. Bado moyoni mwake hakuwa akijisikia amani kabisa, alikuwa akipiiga hatua za haraka haraka kuelekea kule ambapo kulikuwa na gari lake.
Watu walikuwa wamejazana kule P2 ambapo alikuwa amelipaki gari lake. Kwanza hakuelewa sababu iliyowafanya watu wale wajazane namna ile,