Simulizi : Ukweli Wenye Kuuma (Painful Truth)

Simulizi : Ukweli Wenye Kuuma (Painful Truth)

SEHEMU YA 60

alikuwa ameandaliwa chakula cha usiku na mheshimiwa rais kama heshima ya kukitangaza chama kile kwa nguvu zote. Moyo wake ulikuwa katika presha kubwa, ni kweli kwamba alikuwa akifanya mawasiliano na rais mara kwa mara lakini siku hiyo kwake ilionekana kuwa siku tofauti na nyingine.
Kwanza kuitwa ndani ya Ikulu huku akiwa pamoja na mumewe, George kulionekana kumfurahisha kupita kiasi. Muda wote macho yake yalikuwa yakiangalia saa kubwa ya ukutani, kwake, aliuona mshale wa dakika ukienda taratibu sana tofauti na siku nyingine. Alitamani asimame na kuifuata saa ile na kisha kuusogeza mshale wa saa na kisha kuona dunia nzima ikienda kama vile ambavyo alikuwa akitaka iwe.
Kila alipokuwa akiyaandaa mafaili yakea alikuwa akimuita sekretari wake ambaye alikuwa akiyaweka katika sehemu ambayo yalikuwa yakitakiwa kuwa. Muda ulizidi kwenda mbele mpaka kufikia muda ambao alitakiwa kutoka ndani ya ofisi yake. Akayakusanya mafaili yote ambayo yalitakiwa kuandikwa mambo fulani katika kipindi ambacho angekuwa nyumbani na kisha kumpa sekretari wake.
Sekretari akayachukua na kisha kupewa ufunguo wa gari ambapo akaanza kuondoka kuelekea katika sehemu ambayo ilikuwa na gari la kifahari lililokuwa na rangi nyeusi, Range na kisha kuufungua mlango.
Annastazia bado alikuwa ofisini huku akiendelea kukusanya vitu vingine. Mara sauti kubwa ya mlipuko ikasikika, Annasatazia akashtuka kupita kawaida kiasi ambacho alitamani kutoka nje ya ofisi ile na kukimbia. Kutokana na presha kubwa aliyokuwa nayo, akajikuta akiingia chini ya meza na kujilaza chini.
Katika maisha yake yote, hakuwahi kuusikia mlio wowote wa mlipuko kiasi ambacho alipousikia mlipuko ule alijikuta akitetemeka kwa hofu kubwa. Moshi mwingi ukaanza kuonekana nje ya ofisi ile kwa dirishani huku sauti za wakinamama zikisikika.
Annastazia hakutoka, aliendelea kubaki ndani ya ofisi ile tena chini ya meza kwa muda wa dakika thelathini na ndipo hapo alipotoka nje ya ofisi ile. Watu walikuwa wamejazana katika korido huku wakiongea yao, Annastazia alipotokea, wote wakayaamishia macho kwake na kuanza kumwangalia.
Annastazia hakuyaelewa macho ya watu wale yalikuwa yakimaanisha nini mbele yake, alitamani kuuliza lakini akajikuta akikaa kimya. Bado moyoni mwake hakuwa akijisikia amani kabisa, alikuwa akipiiga hatua za haraka haraka kuelekea kule ambapo kulikuwa na gari lake.
Watu walikuwa wamejazana kule P2 ambapo alikuwa amelipaki gari lake. Kwanza hakuelewa sababu iliyowafanya watu wale wajazane namna ile,
 
SEHEMU YA 61

akaanza kusogea karibu zaidi. Kila mtu ambaye alikuwa amemuona mahali hapo alimshangaa kwani watu wote waliokuwa mahali pale walifikiri kwamba mtu ambaye alikuwa akionekana garini alikuwa yeye.
Annastazia akajikuta akilia kama mtoto mdogo mara ya kuona ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea. Hakulia kwa sababu ya thamani kubwa ya gari lake bali alikuwa akilia kwa sababu alikuwa amempoteza mtu ambaye alikuwa karibu nae kwa asilimia nyingi, Shannia, msichana ambaye alikuwa sekretari wake.
Annastazia hakuendelea kubaki mahali hapo, alichokifanya ni kuanza kupiga hatua kurudi ofisini mwake. Machozi yakaanza kumtoka na kilio kikaanza kusikika, Moyo wake ulikuwa unamuuma kupita kawaida, kumpoteza hannia kulionekana kumuumiza.
“Hawa watakuwa wapinzani wetu. Watakuwa viongozi wa vyama pinzani” Annastazia alijisemea huku akiwa hana habari kwamba kila kitu kilichokuwa kimetokea kilikuwa kimepangwa na Andy, mwanaume ambaye alikuwa amemsaliti miaka minne iliyopita.
****
Serikali ikaonekana kuchanganyikiwa mara baada ya kupata taarifa ya mlipuko ule ambao ulikuwa umetokea. Kila mtu alionekana kutokuelewa sababu ambayo ilimfanya mlipuaji kulilipua gari lile la mwanamke ambaye alionekana kuwa na nguvu sana katika mambo ya siasa nchini Tanzania, Annastazia Kapama.
Hakukuwa na sababu ya kupoteza muda, moja kwa moja uchunguzi ukaanza kufanyika kwa haraka sana. Tukio lile la kuripuliwa kwa gari la Annastazia Kapama likaonekana kuanza kuibua vita vya chama tawala na vyama pinzani kwa kuwaona kwamba walikuwa nyuma ya tukio lile.
Upelelezi ulikuwa ukifanyika chini chini lakini hakukuwa na mtu ambaye alipatikana kwa kulifanya tukio lile. Miezi ilienda zaidi na zaidi lakini hakukuwa na mtu yeyote ambaye alipatikana na hatia ya kufanya tukio lile.
Siku ziliendelea kukatika huku miezi nayo ikiendelea kukatika. Vuguvugu la uchaguzi likaanza kutokota nchini Tanzania. Wanachama mbalimbali wa vyama pinzani pamoja na wale wanachama wa chama tawala wakaanza kufanya kazi zao kama kawaida.
Kwa wale ambao walikuwa wakitumia khanga wakaanza kuzigawa kwa wanawake kama hatua mojawapo ya kuchaguliwa siku ya uchaguzi itakapofika. Wanaume nao wakaanza kupewa fulana pamoja na kofia kama harakati fulani za kuweza kuwateka na kuchukua kura zao.
Mwaka ukaisha na mwaka mwingine kuingia. Annastazia akaanza harakati zake za kusimama majukwaani na kuanza kuhutubia huku akiwaomba wananchi wa maeneo mbalimbali katika wilaya ya Kinondoni kumpigia kura katika uchaguzi mkuu ambao ulikuwa umebakia mwezi mmoja kabla ya kufanyika.
Kila mwananchi ambaye alikuwa akimsikiliza Annastazia alionekana
 
SEHEMU YA 62

kumkubali na kila mtu kuahidi kumpa kura yae mwanamke huyo ambaye alikuwa akitikisa sana jijini Dar es Salaam kwa wakati huo.
Annastazia alitembea maeneo mbalimbali wilayani Kinondoni huku akiendelea kuhutubia katika mikutano mbalimbali. Kila sehemu ambayo alikuwa akihutubia, watu walikuwa wakijaa kupita kawaida.
Kwa maneno ambayo alikuwa akiyaongea Annastazia, kila mtu alikuwa akimkubali kupita kawaida. Annastazia akaonekana kushinda uchaguzi hata kabla kura hazikuanza kupigwa. Watu zaidi ya asilimia sabini walikuwa wakimuunga mkono Annastazia ambaye alionekana kupania kuleta mabadiliko makubwa katika wilaya ya Kinondoni.
Kwa kuwa Annastazi alikuwa akikubalika huku amejikusanyia umaarufu mkubwa nchini Tanzania, wanasiasa wengine wakaanza kumtumia katika mikutano yao. Alionekana kukubalika kupita kiasi jambo ambalo kila aliposimama katika jukwaa lolote, alionekana kukubalika.
Katika kila mkutano ambao ulikuwa ukimhusu, mumewe, George alikuwa pembeni yake akimsikiliza. George alikuwa akijisikia amani na furaha moyoni, kuwa na mke kama Annastazia kulionekana kumfurahisha kupita kawaida.
Katika kila mkutano ambao alikuwa akiufanya, Annastazia alikuwa akimtambulisha mumewe, George kama mtu pekee ambaye alikuwa akimpenda na kumtia nguvu katika kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea katika maisha yake.
George alijisikia fahari, alijiona kuthaminiwa kupita kawaida, mapenzi juu ya mke wake yakaongezeka zaidi na zaidi. Waliishi kwa amani na upendo ndani ya ndoa yao, walithaminiana na kupeana mapenzi ya dhati.
Hatimae siku ambayo ilikuwa ikisubiriwa ikafikia, watu hawakutakiwa kuvaa aina yoyote ya nguo ambayo ilikuwa ikionekana kuwa ya chama fulani. Watu walitakiwa kuelekea katika sehemu maalumu ambazo zilikuwa zimetengwa kwa ajili ya kupiga kura na kumchagua kiongozi ambaye walimuona kufaa kuwawakilisha.
Saa tano asubuhi, Annastazia alikuwa akiingia katika viwanja vya shule ya Kambangwa kwa ajili ya kupiga kura huku akiwa ameongozana pamoja na mumewe, George. Watu wote ambao walikuwa wakimuona mahali hapo wakaanza kumshangilia huku wakianza kuimba nyimbo mbalimbali japokuwa walijua kufanya hivyo lilikuwa kosa kbwa sana hasa katika siku hiyo ya uchaguzi.
Annastazia na mumewe wakapiga kura na kisha kuanza kuongea na viongozi wengine ambao walikuwa mahali hapo na kisha kulifuata gari lao, wakaingia ndani na kuondoka katika uwanja wa shule hiyo.
Ingawa alikuwa na uhakika wa asilimia zote kushinda uchaguzi ule lakini moyo wake ulikuwa na wasiwasi mkubwa. Hali ya kujiamini ikaanza kuondoka moyoni mwake huku akianza kuamini kwamba kitu chochote kingeweza kutokea siku ya matokeo.
Aliwafahamu sana Watanzania ambao mara yingi walikuwa wakikukubali sana siku za kampeni lakini siku ya uchaguzi wakakugeuka. Alijiona kutakiwa kusubiria matokeo na kuona kama Watanzania walikuwa wamekifanya kile ambacho walikuwa wakimuonyeshea au walikuwa wamemgeuka.
“Nina wasiwasi mpenzi” Annastazia alimwambia mumewe, George.
“Hautakiwi kuwa na wasiwasi. Hebu jifikirie ni kwa jinsi gani unakubalika” George alimwambia Annastazia.
“Lakini si unawajua Watanzania walivyo?”
“Nawajua”
“Sasa kuna sababu itakayonifanya kujiamini mpenzi?”
“Wewe jiamini tu. Yaani kwa kura yangu na yako pekee zimekwishakupitisha hata kama wengine hawajapiga” George alimwambia Annastazia na kuanza kucheka.
 
SEHEMU YA 63

Siku ambayo matokeo yalitakiwa kutangazwa ikawadia. Annastazia pamoja na mumewe wakaanza kuelekea katika ofisi za makao makuu ya chama chao cha Republic na kisha kuingia ndani ya jengo hilo huku wakisikiliza kutangazwa kwa matokeao yale kupitia redio ya Taifa.
Kila mtu ndani ya ofisi ile alibaki kimya huku akionekana kuwa makini kusikiliza matokeo ambayo yalikuwa yakiendelea kutangazwa edioni mule. Wagombea wengi wa chama tawala walikuwa wameshinda viti vya Ubunge katika sehemu mbalimbali nchini Tanzania.
Ghafla kama mtu alieyekuwa ameshtushwa na mlipuko fulani mkubwa, Annastazia akaruka juu, mikono yake akainyoosha juu mara baada ya kutangazwa kwamba alikuwa ameshinda kiti cha Ubunge wa Kinondoni.
Watu wote ambao walikuwa wakaanza kushangilia, ushindi wa Annastazia wa kuwa mbunge wa Kinondoni ukaonekana kuwafurahisha kupita kawaida. Annastazia akashindwa kuvumilia, akaanza kumfuata mumewe, George na kisha kumkumbatia huku machozi yakiomtoka.
Tayari watu ambao walikuwa mitaani wakatoka na kuelekea katika ofisi ya chama cha Republic huku wakishanglia kwa kupiga ngoma. Annastazia hakuweza kuvumilia kubaki ndani, akajikuta akitoka nje huku akianza kupunga mikono yake hewani.
Watu zaidi ya mia saba walikuwa wamekusanyika nje ya ofisi ya chama kile huku kadri muda ulivyozidi kwenda mbele wakizidi kuongezeka zaidi na zaidi. Mpaka saa moja kupita, watu zaidi ya elfu mbili walikuwa wamekwishakusanyika nje ya uwanja wa ofisi ile huku wengi wao wakiwa wamevaa khanga, fulana na kofia za chama cha Republic.
Safari ya kutembea mitaani huku wakishangilia ikaanza kufanyika mahali hapo. Watu wakajikusanya wengi mitaani huku Annastazia, mumewe pamoja na viongozi wa chama kile wakiwa pamoja na wananchi ambao walikuwa wakioekana kuwa na furaha kupita kawaida.
Kushinda kwa Annastazia kulionekana kuwapa nguvu na kuona kwamba mwisho wa matatizo yao ulikuwa umefikia tamati. Walikuwa wakimuamini sana Annastazia kwamba alikuwa mtetezi wa maisha yao magumu ambayo walikuwa wakiishi.
Maisha kwao yalionekana kuwa magumu, barabara zilikuwa mbovu sana huku maji yakiwa shida kupatikana katika sehemu kubwa ya wilaya ya Kinondoni. Annastazia ndiye ambaye alionekana kuwa na nguvu ya kupambana na matatizo hayo ambayo yalionekana kuwa sugu katika wilaya hiyo.
“Sasa nitafanya mabadiliko makubwa” Annastazia alimwambia mumewe, George.
“Hicho ndicho ambacho kinatakiwa kufanyika. Nitakuwa pamoja nawe mke wangu” George alimwambia Annastazia.
 
SEHEMU YA 64

Utengezaji wa dawa ukaanza tena. Watu walikuwa wakizidi kuambukizwa huku wengine nao wakizidi kupatiwa tiba. Ugonjwa ule ulionekana kutisha kupita kawaida. Maambukizi yalikuwa makubwa kuliko hata magonjwa mengine.
Amani ikaonekana kutoweka duniani hasa nchini Marekani. Watu ambao walikuwa wakiondoka barani Marekani pamoja na Ulaya kuelekea Afrika ndio ambao waliufanya ugonjwa huo kuingia barani Afrika.
Dawa zilikuwa zimecheleweshwa kuletwa barani Afrika kiasi ambacho kiliwafanya watu wengi kupoteza maisha. Ugonjwa ule ulionekana kuwa na nguvu kubwa sana barani Afrika huku maambukizi yakiwa ya hali ya juu. Kila siku watu walikuwa wakifa na wengine wakizidi kuambukizwa.
Mpaka zile dawa zinaingia barani Afrika, zaidi ya watu milioni mbili walikuwa wamekufa na kuzikwa huku milioni kumi na mbili wakiwa wamekwishaambukizwa ugonjwa huo ambao ulionekana kuwa wa kihistoria.
Hapo ndipo wale watu ambao walikuwa hawamuabudu Mungu wakaanza kumuabudu Mungu kwani kwao waliona kuwa kama laana ambayo ilishushwa katika kizazi hiki ambcho kinaonekana kujawa na maovu mengi.
Ingawa Andy alikuwa akijitahidi kutengeneza dawa nyingi kwa siku lakini maambukizi yakaonekana kuwa makubwa hata zaidi ya utengenezaji wa dawa zile. Zaidi ya aslimia saba walikuwa wakiambukizwa ugonjwa ule kila mwezi.
Ingawa watu walikuwa wakitakiwa kutumia kinga lakini wengi wao hawakutaka kutumia kinga hizo kwa kuona kwamba zilikuwa zikiondoa ladha fulani hasa wakati wa kufanya tendo la ndoa na wapenzi wao au wake zao.
Bado kiasi kikubwa cha fedha kilikuwa kikiendelea kumiminika katika akaunti yake ikiwa sehemu ya malipo ambayo alikuwa akilipwa na Dawson. Utajiri wake ulikuwa ukizidi kuongezeka kila siku lakini kamwe hakutaka kuridhika.
Miezi iliendelea kukatika na hatimae kukutana na msichana ambaye moyo wake ukaanza kuangukia katika penzi zito, msichana huyu alikuwa Sofia aliyekuwa na asili ya Venezuela. Lengo lake kubwa kwa Sofia lilikuwa ni kuanzisha mahusiano ya mapenzi na hatimae kufunga ndoa hapo baadae.
Andy hakuwa radhi kumwambia Sofia ingawa mara kwa mara alikuwa akikutana nae hasa alipokuwa akielekea katika katika benki ya Atlantic. Sofia alikuwa akifanya kazi hapo kama mwanamahesabu katika benki hiyo.
Tayari moyo wake ulikuwa katika mapenzi mazito, ni kweli kwamba
 
SEHEMU YA 65

alikwishawahi kupenda sana kipindi cha nyuma lakini kwa sasa alikuwa akipenda zaidi ya mara ya kwanza. Alimhesabia Sofia kuwa sehemu katika maisha yake, alijiona kuanza kumthamini binti huyo hata kabla hajamwambia kitu chochote kuhusiana na mahusiano.
Mara kwa mara alikuwa akimtaka akutane nae katika mghahawa kwa ajili ya chakula cha usiku lakini kidogo Sofia hakuonekana kumuelewa kabisa. Alijifanya yuko bize sana na kazi mbalimbali za nyumbani.
Sofia alikwishajua kwamba Andy alikuwa akimpenda sana lakini kwake alijiona kutokuwa tayari kuanza mahusiano na mwanaume yeyote kwa kipindi hicho. Kumbukumbu za maisha yake ya nyuma ya kusalitiwa ndizo ambazo zilikuwa zimeuharibu kabisa moyo wake na kuuacha ukiwa na matundu matundu.
Ingawa alikuwa akiletewa mapozi lakini Andy hakukata tamaa, Sofia akakubali kutoka na Andy kwa ajili ya chakula cha usiku. Kila mmoja alionekana kuwa na furaha siku hiyo huku uhusiano wa kimapenzi ukianzia hapo mghahawani.
“Nitakupenda katika maisha yangu yote” Andy alimwambia Sofia.
“Usije kuumiza moyo wangu Andy. Nilikuwa nahofia sana kuwa na uhusiano na mtu maarufu au tajiri” Sofia alimwambia Andy.
“Naomba uniamini. Kamwe sitoweza kukuumiza” Andy alimwambia Sofia.
Hiyo ndio ilikuwa siku ya kwanza kuingia katika mahusiano tangu asalitiwe na Annastazia. Kwake hakumkumbuka kabisa Annastazia kwani alijua kwamba tayari katika kipindi hicho alikuwa marehemu mara baada ya kumlipua na bomu garini.
Andy hakutaka kupoteza muda, alichokifanya ni kwenda kumtambulisha Sofia nyumbani kwao. Bwana Wayne na mkewe, Happy walionekana kuwa na furaha, kumuona kijana wao akiwa katika mahusiano huku akijiandaa kuoa kuliwapa furaha sana.
“Nimeamua kusahau kila kitu” Andy aliwaambia wazazi wake.
“Umefanya jambo la maana sana” Bwana Wayne alimwambia Andy.
Baada ya miezi miwili, Andy akafunga ndoa na Sofia na kuanza maisha ya ndoa. Maisha yake yalikuwa yametawaliwa na furaha kubwa, Sofia ndiye alikuwa mtu wa karibu katika maisha yake lakini kamwe hakutaka kumuambia kitu chochote kuhusiana na virusi vya katapilar ambavyo alivitengeneza.
****
Hakukuwa na mtu ambaye aliamini kama Annastazia angeweza kushinda nafasi ya kuwa spika wa Bunge la Jamhuri wa Muuungano wa Tanzania. Umri wake ulikuwa mdogo sana lakini alionekana kukubalika kupita kawaida.
 
SEHEMU YA 66


Ndoto zake ambazo alikuwa amejiwekea miaka mingi iliyopita tayari zilikuwa zimekamilika. Kuchaguliwa kwake na kuwa Spika wa Bunge kulimuonyeshea ni kwa jinsi gani alikuwa akikubalika sana hata Bungeni.
Watanzania walishtuka kutokana na uchaguzi wa kumchagua kama spika wa Bunge lakini hakukuwa na mtu yeyote ambaye alilaumu. Kwao, Annastazi alionekana kustahili kuchukua nafasi yoyote ile hata kama ulikuwa uraisi wa nchi.
Alionekana kuwa mwanamke aliyekuwa na kiu kubwa ya maendeleo, alionekana kuwa mwanamke ambaye kamwe hakutaka kuwaona Watanzania wakiishi katika maisha ambayo walikuwa wakiishi, maisha yaliyojaa umasikini mkubwa.
Magazeti mbalimbali na vyombo vingine vya habari vilikuwa vikimwaga sifa mbalimbali kwa Annastazia. Kura amabazo zilikuwa zimempigia zilionekana kuwa nyingi sana hali iliyoonyesha kwamba hata baadhi ya wabunge wa vyama pinzani walikuwa wamempigia kura.
Siku ya kwanza bungeni, Annastazi hakuweza kuamini kama kweli alikuwa amevaa jozi kubwa ambalo lilikuwa likivaliwa na spika wa Bunge. Moyoni mwake alikuwa akijisikia furaha sana kiasi ambacho wakati mwingine alikuwa akilengwa na machozi ya furaha.
Hiyo ndio ilikuwa siku ya kwanza ambayo ilikuwa imebaki kuwa kama kumbukumbu katika maisha yake. Katika kila kitu ambacho kilikuwa kikitokea katika maisha yake, alikuwa akimshukuru Mungu pamoja na mume wake, George ambaye alionekana kuwa mfariji mkubwa katika maisha yake.
****
Maisha yake ya ndoa pamoja na mke wake yalikuwa yakiendelea kama kawaida, alimpenda Sofia kuliko msichana yeyote yule. Alimthamini na kumpa kila kitu ambacho alikuwa amekistahili kukipata kutoka kwake.
Miezi ikaatika na hatimae mwaka wa kwanza kupita, Sofia akawa mjauzito. Hiyo ilikuwa ni furaha kubwa kwa Andy ambaye alikuwa ameongeza mapenzi maradufu kwa mke wake. Miezi tisa ikapita na hatimae mtoto wa kiume kuzaliwa na kumpa jina la Brian.
Familia ikaonekana kuongezeka, mapenzi makubwa yakaongezeka maradufu katika maisha yao. Kwa sababu Andy alikuwa akijulikana sana nchini Marekani, taarifa ile ilikuwa ikitangazwa sana. Magazeti mbalimbali, majarida pamoja na vyombo vingine vya habari vilikuwa vikitangaza mambo mengi ambayo yalikuwa yakitokea katika familia hiyo.
Miezi iliendelea kukatika na mwaka mwingine kuingia. Andy alionekana kupatwa na mshtuko mkubwa. Sura ya mtu ambaye alikuwa akiiangalia katika
 
SEHEMU YA 67

kompyuta yake hakuwa akiamini hata mara moja, ilikuwa picha ya Annastazia ambaye alikuwa Spika wa Bunge la Tanzania.
Andy akaivuta vizuri laptop yake na kisha kuiangalia vizuri picha ile, alikuwa Annastazia. Kumbukumbu za maisha yake ya nyuma zikaanza kurudi tena, chuki ambayo alikuwa nayo juu ya msichana huyo ikarudi tena.
Hakuelewa ni kwa nini Annastazia hakuwa amekufa katika ule mlipuko ambao alikuwa amemlipua mwaka uliopia. Alichokifanya Andy ni kuichukua ile picha na kuihifadhi sehemu huku kila wakati akiwa akiiangalia.
Bado alikuwa na hasira na Annastazia, hakuona sababu yoyote ambayo ilimpelekea Annastazia kuendelea kuvuta pumzi ndani ya dunia hii, alikuwa akitaka kumuua kabisa na kumpoteza katika dunia hii.
Hapo ndipo alipopanga safari ya kurudi tena nchini Tanzania na kisha kumuua Annastazia. Wala hakutaka kuchelewa, alichokifanya ni kumuaga mke wake, Sofia na kisha safari ye kuelekea nchini Tanzania kuana huku akiwa na hasira kali na Annastazia.
Kwa sasa hivi hakutaka kumuua kwa kitu chochote zaidi ya kumchoma kisu tumboni mara kadhaa na ndipo amuache huku akimwangalia mpaka katika kipindi ambacho atakata roho. Baada ya siku mbili, Andy akaanza safari ya kuelekea nchini Tanzania huku akitumia ndege yake.
Kila wakati alikuwa akijifikiria ni kwa njia gani ambayo angeitumia kuonana na Anastazia na kisha kumuua kwa kumchoma kisu zaidi ya mara tano tumboni. Mawazo mbalimbali yalikuja kichwani mwake, hivyo akaona kwamba kazi haikuwa kubwa sana.
Nchini Tanzania, akaamua kuanza kufuatilia Annastazia alikuwa mbunge wa wapi. Wala hakupata shida ya kulifahamu hilo, akapata jibu kwamba alikuwa mbunge wa Kinondoni. Alichokifanya ni kuchukua ndevu za bandia ambazo alikuwa amekuja nazo na kisha kuzivaa.
Alichokifanya hapo ni kwenda katika ofisi ya mbunge huyo na kisha kuongea na wasaidizi wake ambao alikuwa amewakuta mapokezini. Akajiwekea lengo la kutaka kuisaidia wilaya ya Kinondoni kwa kuitengenezea barabara kadhaa ambazo zitahesabika kwamba Bi Annastazia ndiye ambaye alikuwa amefanya hilo.
Hiyo ilikuwa ni taaarifa ya furaha sana kwa upande wao, mfadhiri ambaye alikuwa amejitokeza kwa kutaka kuisaidia wilaya ya Kinondoni alionekana kuwa muhimu kwao. Walichokifanya ni kumpigia simu Annastazia na kisha kumwambia kuhusiana na mtu huyo ambaye alionekana kuwa mfadhiri ambaye alikuwa na fedha za kutosha.
“Anaitwa nani” Annastazia aliuliza huku akionekana kuwa na furaha.
“Ben Killerandy” Msaidizi wake alisema.
Japokuwa Annastazia alikuwa mkoani Dodoma ambapo Bunge lilikuwa likiendelea, akaamua kuanza safari ya kuja jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuonana na mfadhiri huyo ambaye alionekana kuja katika muda muafaka.
Alipofika ndani ya jiji la Dar es Salaam moja kwa moja akaanza kuelekea katika ofisi yake ambako huko akaanza kupata mambo mengi kuhusiana na
 
SEHEMU YA 68

mtu huyo ambaye alikuwa amejitolea kuitengeneza wilaya ya Kinondoni.
Annastazia akapewa namba ya simu na kisha kuanza kufanya nae mawasiliano. Sauti ya Andy ilikuwa imebadilika kabisa na isingewezekana hata kidogo kujulikana na Annastazia. Wakapanga sehemu ya kuonana na bila hiyana yoyote Andy akataka waonane nyumbani kwa Annastazia ambako huko ndipo angemuua.
Siku iliyofuata, Andy akajiandaa vilivyo huku akiziweka ndevu za bandia ambazo alikuwa amekuja nazo kutoka nchini Marekani na kisha kukodi teksi. Huku safari ikiwa inaendelea, Andy alikuwa na kiu ya kumuona Annastazia na kumuua kama ahadi ambayo alikuwa ameiweka katika maisha yake.
Gari likafunga breki nje ya geti la jumba kubwa la kifahari na kisha kuruhusiwa. Andy akateremka na kuanza kuingia ndani ya eneo la nyumba hiyo ambako alikaribishwa mpaka ndani. Macho yake yakatua kwa Annastazia ambaye alifika sebuleni hapo.
Mshipa wa hasira ukamsimama, chuki kubwa na hasira ikaanza kumpanda moyoni mwake. Alitamani kumrukia Annastazia na kisha kuvizamisha visu vile tumboni mwake. Uso wa Annastazi ulikuwa na tabasamu kubwa, ingawa Andy alikuwa akirudisha tabasamu lile lakini moyo wake ulikuwa umejawa na hasira kali.
“Karibu” Annastazia alimkaribisha.
“Asante”
Hapo ndipo mangezi yalipoanza. Andy alikuwa akimwambia mipango ambayo alikuwa ameipanga kuhusiana na kuboresha miundombinu mbalimbali nchini Tanzania hasa katika wilaya ya Kinondoni. Alichokifanya yeye kwa wakati huo ni kuzitoa karatasi kadhaa ambazo alikuwa amekuja nazo kutoka nchini Marekani na kisha kuanza kumuonyeshea. Ilionekana kuwa karatasi ambayo iliandikwa mipango mikubwa ya kuibadilisha kabisa wilaya ya Kindondoni ambako baada ya kila kitu kukamilika basi Annastazia ndiye ambaye angeonekana kwamba alikuwa amefanya yote hayo.
“Sawa” Ngoja nijiandae tuelekee ofisini kuonana na wenzangu ambao moja kwa moja kazi hiyo itafanyika” Annastazia alisema na kisha kuondoka kuelekea chumbani.
Andy hakutaka kubaki mahali hapo, alichokifanya ni kusimama na kisha kuanza kuelekea chumba mule. Lengo lake kubwa lilikuwa ni kumuua huko huko chumbani kwa kumchoma visu kadhaa. Huku akiendelea kujiandaa, ghafla Annastazia akashtukia mlango ukifunguliwa na Andy kuingia ndani.
Annastazia alionekana kushtuka sana, hakuamini kama mgeni huyo angeweza kuingia chumbani kwake kirahisi namna ile. Alibaki akimwangalia Andy huku macho yake yakionyesha mshtuko.
“Unafanya nini chumbani humu?” Annastazia alimuuliza Andy pasipo kumfahamu.
“Nimekuja kukuua tu” Andy alijibu huku hasira zikianza tena kumpanda.
“Nimekufanya nini Killerandy?” Annastazia aliuliza huku akionekana kuwa na wasiwasi.
Alichokifanya Andy ni kuzivua zile ndevu za bandia. Annastazia bado hakuwa amemfahamu Andy kwani ilikuwa imepita mika mingi sana bila kumtia machoni. Hata zile ndevu ziipotolewa, bado hakuweza kumfahamu.
“Nimekufanya nini?”
“Ulinisaliti. Uliuumiza sana moyo wangu” Andy alisema lakini bado Annastazia hakuonekana kuamini.
“Kukusaliti! Mbona sikufahamu na wala sikuwahi kukuona kabla!” Annastazia alisema huku akianza kutetemeka kwa woga.
“Ninaitwa nani?”
“Killerandy”
“Hayo ni majina mawili. Hebu yaweke yawe kwenye majina mawili ndio
 
SEHEMU YA 69

utatambua mimi ni nani” Andy alimwambia Annastazia.
“Mungu wangu!” Annastazia alisema kwa mshtuko.
“Najua umenifahamu mimi ni nani” Andy alimwambia Annastazia.
Alichokifanya Andy ni kukitoa kisu chake na kisha kuanza kumsogelea Annastazia. Alipotaka kupiga kelele tu, akashtukia akifunikwa mdomo wake na viganja vikubwa vya Andy. Akalazwa kitandani na kisha kufungwa mdomo kwa kanga zilizokuwa kitandani.
“Nitakuua baada ya kukubaka. Sikubaki kwa sababu nina tamaa ila ninakubaka kama hatua ya kukudhalilisha” Andy alimwambia Annastazia na kisha kuanza kumbaka.
Yalikuwa ni maumivu makali kwa Annastazia kwa kuwa Andy hakutaka kutumia uume wake tu, wakati mwingine alikuwa akitumia hadi mkono wake na mpini wa kisu chake. Annastazia alibaki akilia lakini sauti yake haikutoka kabisa.
Andy hakutaka kutoka kifuani kwa Annastazia, kadri alivyokuwa akifikiria namna ambavyo mwanamke yule alivyokuwa ameeuumiza moyo wake kipindi cha nyuma, alizidi kumbaka zaidi na zaidi. Kutoka na mpini wa kisu kile kuchunika chunika, sehemu ya ukeni ya Annastazia ikaanza kutoka damu.
“Ni lazima nikuue” Andy alimwambia Anastazia.
Machozi yalikuwa yakimtoka Andy, kadri alivyokuwa akimwangalia Annastazia na ndivyo ambavyo alikuwa na hasira zaidi na zaidi. Akanyanyua kisu juu na kisha kukizamisha kifuani mwa Annastazia. Anastazia akakipeleka kifua chake juu na kukileta chini, damu zikaanza kutapakaa kitandani. Andy hakuridhika, akakinyanyua kisu tena na kisha kukizamisha tena kifuani mwa Annastazia, alifanya hivyo mara sita, Annastazia akatulia kitandani, alikuwa amekwishakufa hapo hapo.
Andy hakutaka kubaki mahali hapo, alichokifanya ni kutoka chumbani mule na kuondoka zake. Hakukuwa na mtu yeyote ambaye alifahamu kitu chochote kilichokuwa kimetokea ndani, wakairuhusu ile teksi kuondoka.
“Nina amani sasa” Andy alijisemea.
“Unasemaje?” Dereva aliuliza.
“Hapana. Hakuna kitu”
“Sawa. Ila unatoka damu”
“Damu! Ziko wapi?”
“Shingoni” Dereva alimwambia Andy ambaye alionekana kuwa na wasiwasi mkubwa.
Andy akamtaka dereva asimamisha gari nje ya baa moja ambako akateremka na kuanza kuelekea chooni huku lengo lake likiwa ni kujifuta damu zile hata kabla hajashtukiwa na mtu yeyote yule. Akaingia chooni, maji yalikuwa mengi, alichokifanya ni kuzivua nguo zake na kisha kuanza kujifuta.
Alitumia muda wa dakika thelathini chooni na ndipo akatoka kuelekea katika sehemu ilipokuwa teksi ile. Andy akapigwa na mshtuko mara baada ya kuona gari la mapolisi likiwa limesimama pembeni ya teksi ile huku mapolisi wakiongea na dereva yule ambaye alionekana kuwa na wasiwasi mwingi.
Mara macho ya dereva yakagongana na macho yake, dereva akanyoosha mkono wake kumuelekezea yeye. Andy akaonekana kushtuka, hakujua ni kitu gani ambacho kilikuwa kinaendelea, akili yake ikamtuma kuona kwamba tayari hali ya amani ilikuwa imechafuka. Alichokifanya mahali hapo ni kukimbia na mapolisi wale waliokuwa na bunduki kuanza kumkimbiza huku wakipiga risasi hewani kama ishara ya kumtaka kusimama na kujisalimisha ila Andy hakufanya hivyo zaidi ya kuendelea kukimbia tena kwa kasi kubwa kama mwanariadha wa mbio fupi.
 
SEHEMU YA 70


Chakula kilikuwa kimekwishaiva na ni Annastazia ndiye ambaye alikuwa akihitajika kwenda katika sehemu ya kulia chakula na kula chakula hicho cha mchana. Kama kawaida yake mfanyakazi wake wa ndani, Glory akaanza kuugonga mlango wa chumbani kwa Annastazia lakini hakukuwa na dalili za mtu kwenda kuufungua mlango ule.
Glory hakuonekana kuwa na wasiwasi, alichokifanya ni kulekea sebuleni huku akidhani kwamba Annastazia alikuwa nje ya jengo lile akiongea na walinzi au wafanyakazi wengine wa nyumba hiyo. Annastazia hakuonekana mbele ya macho yake.
Ingawa alikuwa amekifunika vizuri chakula kile katika hotpot lakini bado alihitaji bosi wake ale katika muda muafaka na hata kama alikuwa amelala, kila siku alikuwa amemwambia amuamshe mara tu chakula kinapokuwa tayari.
Glory hakuonekana kuelewa kitu chochote kile, kwa jinsi alivyokuwa ameita nje ya chumba kile hakuwa na uhakika kwamba Annastazia hakuwa amemsikia hata kama alikuwa katika usingizi mzito namna gani. Alichokifanya kwa wakati huo baada ya kuita kwa muda mrefu ni kuufungua mlango ule.
Moyoni alikuwa akihofia kwani toka aanze kufanya kazi ndani ya nyumba ile hakuwahi hata kukiona chumba kile, si kwamba alikuwa akizuiliwa bali hakuwa amejiwekea mazoea ya kuingia ndani ya chumba kile.
Mlango haukuwa umefungwa, aliufungua na kisha kuingia ndani. Moyo wake ukamlipuka, damu mwilini mwake ikaanza kuzunguka kwa kasi kubwa huku hofu ikiwa imemwingia moyoni. Hakuamini kile ambacho alikuwa akikiangalia mbele yake, maiti ya Annastazia.
Glory akaanza kupiga uyowe ambao uliwafanya walinzi pamoja na wafanyakazi wengine kufika chumbani mule. Kila mtu ambaye alikuwa ameuona mwili wa Annastazia alibaki kuwa na mshtuko, hawauamini kile ambacho walichokuwa wakikiona kwa wakati ule.
“Msiuguse mwili huu” Mlinzi mmoja aliyekuwa na nguo za kiaskari aliwaambia na kisha kutoka nje ya chumba kile.
Moja kwa moja akaanza kuelekea mpaka katika kijumba kidogo ambacho kilikuwa kikitumiwa na mlinzi wa pale mlangoni na kisha kuchukua daftari lililokuwa mezani na kisha kuanza kulifungua kwa kasi ya ajabu.
Macho yake yakatua katika jina la Killerandy. Alichokifanya ni kuanza kuangalia namba za gari ambalo lilikuwa limeingia ndani ya eneo la nyumba ile. Kwa haraka haraka akaanza kuandika pembeni na kisha kuondoka mahali hapo.
Kitu cha kwanza ni kwenda katika kituo cha polisi ambacho wala hakikuwa mbali kutoka katika nyumba ile na kisha kuanza kuelekezea kile ambacho kilikuwa kimetoke. Kila polisi alionekana kuwa na mshtuko, walichokifanya ni kuingia katika defender yao na kisha kuondoka mahali hapo.
“Unasema namba za gari unazikumbuka?” Polisi aliuliza.
“Si kuzikumbuka tu, hadi kuzinadika nimeziandika. Hizi hapa”
“Hebu zitaje”
“T113 NYC”
“Na njia ambayo gari hiyo imeelekea unaifahamu?”
“Yeah! Tena wameelekea kule kunapokuwa na foleni kubwa”
Dereva alikuwa akiendesha gari kwa mwendo wa kasi sana kiasi ambaco watu
 
SEHEMU YA 71

wengi ambao walikuwa wakiliangalia gari lile walifikiri kwamba lilikuwa katika mashindano fulani. Mapolisi walikuwa wamejiandaa na bunduki zao kama walikuwa katika muvi fulani iliyotungwa na Ubunifu Wetu.
Foleni kubwa ilikuwa ikionekana mbele yao, magari ambayo mengi yao yalikuwa ya watu binafsi yalikuwa yakisogea taratibu sana kuingia katika barabara ya Ally Hassan Mwinyi. Walichokifanya ni kuanza kuvunja sheria kwa kupita katika njia ya watembea kwa miguu huku watu wakiwashangaa.
“Ilikuwa ni gari aina gani?” Polisi mmoja aliuliza.
“Teksi”
“Mstari wa rangi gani?”
“Njano”
“Sio ile iliyosimama nje ya ile bar?”
“Yeah! Ndio ile ile” Mlinzi yule alijibu hasa mara baada ya kuona namba za gari.
Mapolisi wale wakazidi kulisogelea gari lile huku wakiweka bunduki zao vizuri. Kila akaonekana kuwa na hamu ya kuingia kwa ajili ya mapambano tu, mikono yao ikaanza kuwasha, kiu ya kumpiga mtu makofi ikaanza kuwakamata.
Wakaruka kutoka garini na kisha kuanza kulifuata teksi ile. Dereva alikuwa akipiga mluzi huku sauti ya muziki ikisikika kwa mbali. Ghafla akashtukia mlango ukifunguliwa na kushikwa fulana na kutolewa nje bila kufahamu ni mtu gani alikuwa amemtoa nje ya gari kinguvu.
“Yuko wapi?”
“Nani?”
“Paaaaa” Alipigwa kibao cha nguvu shavuni.
“Yuko wapi?” Lilikuwa swali la pili kutoka kwa polisi, hata kabla hajatoa jibu lolote lile, Andy akatokea mahali hapo jambo lililomfanya kumnyooshea kidole na mapolisi wale kuanza kumfukuza huku wakijaribu kumfyatuulia risasi ambazo zilimkosa ila hawakuataka kumuacha.
****
Andy alikuwa akikimbia kwa kasi kuelekea katika upande ambao ulikuwa na fremu nyingi. Milio ya risasi bado ilikuwa ikisikika kutoka katika bunduki walizozishika maaskari wale ambao walionekana kutokuwa na shabaha kabisa.
Watu waliokuwa karibu na eneo lile walikuwa wakikimbia ovyo, milio ya risasi ambayo ilikuwa ikisikika ilikuwa ikiwatisha kupita kawaida. Andy hakutaka kusimama, kukamatwa kwa kusalimu amri kungemaanisha kwamba alikuwa ameshindwa kabisa kujinasua kutoka kwa mapolisi wale.
Aliendelea kukimbia mpaka kufika katika uwanja wa Don Bosco, hapo hakutaka kusimama, akaendelea kukimbia zaidi na zaidi kuelekea ilipokuwa barabara ya kuingilia Orysterbay. Alipoifikia barabara ile, hakutaka kuiingia, akaendelea kwenda mbele kule kulipokuwa na sheli iliyokuwa karibu na jengo la Mult Choice.
Watu bado walikuwa wakiendelea kukimbia kila milio ya risasi ilipokuwa ikiendelea kusikika. Andy alionekana kuwa kama mtu ambaye alikuwa amekimbia riadha kwa kipindi cha nyuma kutokana na kasi yake ilivyokuwa kubwa.
Mapolisi ambao walikuwa walinzi katika geti la kuingilia katika jengo la Multi Choice walionekana kutokuwa na ushirikiano na mapolisi wale ambao walikuwa wakimkimbiza Andy. Walimuona kabisa Andy akielekea katika upande ule waliokuwa lakini hawakufanya kitu chochote zaidi ya kupigwa na butwaa tu.
Andy hakuwa akifahamu sehemu yoyote ile, yeye alikuwa akikimbia huku lengo lake likiwa ni kuwapotea mapolisi tu. Bila kuangalia kama kulikuwa na
 
SEHEMU YA 72

magari yalikuwa yakipita, Andy akavuka barabara na kuelekea kule kulipokuwa kukitengenezwa masofa.
Wauza masofa wote walikuwa wamekwishakimbia kutokana na milio ya risasi ambayo ilikuwa ikiendelea kusikika mahali pale. Andy hakuonekana kuwa radhi kusimama, akaendelea kukimbia mpaka karibu na viwanja vya Leaders.
Milio ya risasi wala haikusikika tena hali iliyoonyesha kwamba bunduki zile za mapolisi zilikuwa zimeishiwa risasi. Andy akapandisha njia ya juu mpaka karibu na jengo la T.H.T na kulipita kwa kasi ya ajabu. Andy akayapeleka macho yake nyuma, mapolisi hawakuonekana kabisa hali iliyomuonyesha kwamba alikuwa amewaacha umbali mrefu.
Hakusimama, aliendelea kukimbia mpaka alipotokea katika shule ya Sekondari ya Kinondoni Muslim ambako hapo akachukua teksi na kumtaka dereva kuendesha kuelekea Posta. Mpaka teksi inaondoka mahali hapo, Andy hakuwa akiamini kama alikuwa amefanikiwa kuwatoka mapolisi wale ambao walionekana kuwa na uchu wa kumpiga japo risasi moja.
“Mbona hivyo?” Dereva alimuuliza Andy huku akionekana kumshangaa.
“Nimepigiwa simu ya dharura. Ofisi yetu inateketea kwa moto. Nawahi kwenda kuokoa mafaili yangu ya muhimu” Andy alijibu.
“Ofisi gani?”
“Ofisi yetu”
“Ipi?”
“Augh! Acha maswali bwana. Endelea kuendesha gari” Andy alimwambia dereva mara baada ya kuona maswali yakizidi kuongezeka.
Mpaka wanafika katika hoteli ya Serena, dakika theathini zilikuwa zimekatika. Andy akateremka na kisha kumgawia dereva kiasi cha fedha ambacho kilitakiwa na kisha kuanza kuelekea ndani ya hoteli ile.
Akaingia chumbani na kisha kujilaza kitandani. Moyo wake ulionekana kuwa na furaha kupita kawaida mara alipokumbuka kwamba kile kitu ambacho kilimfanya kuja nchini Tanzania kilikuwa kimekwishakamilika.
Alichokifanya kwa wakati huo ni kuinuka na kuanza kuelekea sehemu ilipokuwa televisheni na kisha kuiwasha. Hakutaka kuangalia vituo vya nje, akafungua kituo cha TBC na kisha kuanza kuangalia kuona kipi kilikuwa kimeendelea.
Macho yake yakatua katika picha ya Annastazia, taarifa za kifo chake zilikuwa zimekwishatangazwa. Moyo wake ukafarijika kupita kiasi, kumuua Annastazia kulionekana kumfurahisha kupita kiasi.
Akainuka na kwenda kuchukua kikopo cha Red Bull na kupiga pafu moja. Uso wake ulikuwa umejawa na tabasamu kila alipokuwa akiangalia televisheni na kukutana na picha ya Annastazia ambapo taarifa juu ya kifo chake zikiwa zinatangazwa.
“Hayo ndio malipo ya usaliti” Andy alisema huku akiichukua glasi yake ya soda na kuunyoosha mkono wake juu kama ishara ya ushindi.
Ghafla Andy akapigwa na mshtuko mara baada ya kuyarudisha macho yake katika kioo cha televisheni na kukutana na picha yake. Huku akionekana kuwa na mshtuko na macho yake yakionekana kutokuamini, akaanza kuiangalia vizuri picha yake.
Jina lake halisi lilikuwa likitangazwa hadharani huku picha yake ikionekana vizuri. Bado Andy alikuwa amepigwa na mshtuko mkubwa huku akionekana kutokuamini macho yake. Kwa haraka haraka, akabadilisha kituo cha televisheni na kuhamia katika vituo vya kimataifa hasa katika kituo cha CNN.
 
SEHEMU YA 73

Hapo ndipo wasiwasi ulipozidi kumkamata hasa mara baada ya kuona kwamba hata CNN walikuwa wamepata taarifa ile kutokana na mtandao wao kuwa mkubwa.
Walichokifanya CNN ni kuanza kuielezea historia fupi ya maisha yake huku baba yake akiwa mchungaji mkubwa wa Kimataifa huku akiwa mlemavu. Andy alionekana kuumia kupita kawaida kwani aliamini kwamba alikuwa amelichafua jina la baba yake kupita kawaida.
Akajikuta akipiga magoti chini, machozi yakaanza kumtoka na kuanza kulia kwa uchungu. Moyo wake ulikuwa katika maumivu makali kupita kawaida, kulichafua jina la baba yake kulionekana kumuumiza sana.
“Nisamehe baba” Andy alijisemea.
Hapo ndipo alipojiona kuanza kuishi maisha ya kujificha, hakuwa radhi kukamatwa kabisa, alihitaji kuanza kujificha mpaka atakapoanza safari ya kuelekea nchini Marekani kwa kutumia njia za panya, hasa meli kubwa za mizigo.
Tayari Andy hakujisikia kuwa na amani hata mara moja kama tu angeendelea kukaa katika hoteli hiyo. Alichokifanya ni kulala kitandani huku akisubiri usiku uingie na hivyo kuondoka hotelini hapo kwani kukaa hapo kwake kulimaanisha kwamba angkamatwa muda wowote ule.
Usingizi haukupatikana kabisa ila alikuja kushtuka kutoka katika lindi la mawazo ilipotimia saa moja na nusu usiku. Alichokifanya ni kuchukua kila kitu kilichokuwa chake na kisha kuanza kuelekea nje ya chumba kile.
Akaingia katika lifti ambayo ilimchukua mpaka chini na kuanza kuondoka huku akionekana kuwa na wasiwasi mkubwa. Lifti ilipofika chini, kwa haraka haraka akateremka na kuanza kuelekea sehemu ambayo ilikuwa na mlango wa kutokea katika eneo la hoteli ile huku saa yake ikimuonyesha kwama tayaari ilikuwa imetimia saa mbili kasoro.
Huku akiwa ametoka nje ya hoteli ile, ghafla akageuka nyuma, macho yake yakatua kwa wanaume watatu ambao nao walionekana kumfuatilia huku kadri muda ulivyozidi kwenda mbele walikuwa wakiongeza kasi.
Tayari Andy akaona kuwa kulikuwa na hatari na wala hakutaka kujiuliza wale walikuwa ni wakina nani, akaanza kukimbia kwa kasi. Nao wale wanaume watatu wakaanza kumkimbiza. Tayari swali lake ambal alikuwa nalo kichwani kuhusiana na wale watu alikuwa amekwishapata jibu, walikuwa askari kanzu.
Kama kawaida yake, kwa sababu yeye ndiye alikuwa kwenye hali ya hatari, aliweza kukimbia kwa mwendo wa kasi hata zaidi ya wale mapolisi ambao walikuwa wakimkimbiza. Akafika kwenye eneo lililokuwa na makaburi ya wahindi, akayapita na kuzidi kuelekea mbele zaidi huku akiifuata barabara ile ya Ally Hassan Mwinyi.
Alipofika mbele karibu na daraja la Sarender, akakata kona kushoto na kuanza kuifuata barabara ile. Andy akaanza kuchoka jambo ambalo hata kasi yake ikaonekana kuanza kupungua. Mapolisi wale walionekana kuwa kama walikunywa dawa za kuongeza nguvu, walizidi kumsogelea zaidi na zaidi.
Akakata kona nyingine na kutokea katika sehemu ambayo ilikuwa na baadhi ya watu ambao walikuwa wamelala chini, walikuwa watoto yatima. Kwa kuwa
 
Back
Top Bottom